
SHAMBA LA HELA
Katika maisha yake ya kawaida ya kila siku ya utafutaji.
Kijana Feruzi anajikuta akikosea kona na kuangukia pua dhidi ya watu hatari...
Watu ambao wanailinda siri kubwa...siri nyeusi. Siri ya shamba kubwa la hela.
Kulikoni?!
Karibu tuzifunue pamoja kurasa za riwaya hii.
Riwaya bora kutoka katika mkono wa kaka Godlove Kabati.
178
28
CH
complete

KIKAO CHA HAKI
Haujawahi kuwa mchezo salama kabisa.
Ni mchezo ambao kama ukiucheza na hujui kanuni zake...basi utapata majuto na maumivu.
Wengi wameutungia nyimbo na mashairi. Tukayaimba
Wengine wameuandikia hadithi na riwaya, kwa lugha nzuri za kifasihi na sarufi.
Tukazisoma.
Hawa wengine wameuigizia tamthilia na filamu. Tukazitazama.
Lakini bado hatukupata maana halisi na jibu la huu mchezo.
Ni kama fumbo gumu ambalo halijawahi kuwa rahisi kufumbua.
Ni kitendawili kigumu ambacho hata ukipewa mji uende na hurudi na majibu yake bado ungeshindwa tu.
Ni mchezo wa mapenzi.
Yaliyowakuta hawa wapendanao wawili.
Kila mmoja ana hadithi yake ya kusikilizwa.
Kilifanyika kikao..
Hatutamlaumu mwanamke baada ya kuisikia hadithi ya upande mmoja tu wa mwanaume.
Tutataka pia kuisikiliza hadithi ya mwanamke..
Hii ndio haki!
Hii ni simulizi fupi ya mapenzi, ambayo hakika haitakuacha mtupu baada ya kuisoma.
Utaburudika, utaelimika na zaidi utapata hekima kubwa kuhusu mahusiano.
Karibu tukisikilize kwa pamoja KIKAO CHA HAKI!
188
5
CH
complete

NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
NAFSI ZILIZO TELEKEZWA!!!!! â
NINI SIRI YA NAFSI ZILIZO TELEKEZWA?
Inahusu nini, inamhusu nani, kipi kipo nyuma yake?
Mwaka 1991, ni mwaka ambao umoja wa nchi za Kisovieti ulidondoka baada ya kushindwa kwenye vita baridi dhidi ya watu wa Magharibi hususani Marekani. Baada ya vita hiyo kuisha kulikuwa na sababu nyingi sana zilizo wafanya washindwe ikiwemo utaifa na mchango wa nchi za magharibi.
Kwa madhara makubwa ambayo yalipatikana, nchi ya Urusi ilikaa chini kufanya tathmini ili kujua ni wapi walifanya makosa mpaka jambo hilo likatokea nchini mwao. Moja kati ya sababu kubwa ambazo walizipata ni kufeli kwa shirika lao la kijasusi la KGB kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kiusalama kwa asilimia miamoja, waliamini kwamba huenda kama shirika hilo lingekuwa imara mapema na kutekeleza majukumu yake kwa usahihi basi wangeishinda vita hiyo.
Sasa mjadala ukawekwa mezani, walishindwaje? Ndipo ikanukia harufu ya usaliti ndani yao, iligundulika kwamba ndani ya shirika lao kuna watu ambao walikuwa wasaliti na usaliti wao ndio ambao ulifanya shirika hilo kuyumba na kufeli. Sasa wasaliti walikuwa nani na nani? Jina ambalo lilitokezea kwenye makablasha yao ni jina la mwanamke wa miaka ishirini na mitano (IRINA ESPANOVICH). Sasa IRINA ni nani na alitokea vipi kwenye hiyo orodha ya wasaliti?
IRINA ESPANOVICH alikuwa ni jasusi mbobevu ndani ya shirika hilo, Moja kati ya wapelelezi ambao waliaminika mno kiasi kwamba akapata bahati ya kuolewa na moja kati ya maafisa wakubwa ndani ya shirika hilo la KGB. Kuolewa kwake na kiongozi mkubwa wa shirika hilo ikawa nafasi ya yeye kupata taarifa nyingi na za siri za shirika hilo kwa njia ya kawaida ama kuziiba kwa sababu huyo mwanaume alikuwa akiishi naye nyumba moja. Sasa kwenye ule mchakato wa kuwatafuta wasaliti, waligundua kwamba kuna akaunti ndani ya Urusi ilipokea mabilioni ya fedha kutoka ndani ya nchi ya Marekani na walipo jaribu kuichunguza akaunti hiyo ili wajue sababu ya msingi ya pesa nyingi kiasi hicho kutumwa kwa mtu ambaye taifa lake lilikuwa vitani na nchi hiyo ni ipi! Ndipo wakagundua kwamba akaunti hiyo ilikuwa inamilikiwa kwa siri na mwanamke huyo IRINA ESPANOVICH.
Baada ya kuunganisha doti, wakagundua kwamba hizo pesa zilitoka ndani ya shirika la kijasusi la Marekani CIA ambalo wengi huwa wanaamini kwamba ndilo shirika namba Moja kwa ubora zaidi duniani kutokana na kuwa na bajeti kubwa ya uendeshwaji wake. IRINA alipokea pesa nyingi ambazo hata angefanya kazi miaka mia-moja asingeweza kuzipata, CIA wamtumie pesa kama nani? Ikahitimishwa kwamba huyo ndiye msaliti ambaye alikuwa akiwauza kwa CIA ndiyo maana walifeli hivyo ikatolewa amri kwamba asakwe popote alipo, akamatwe, ateswe kisha auawe mrembo huyo.
Bahati ikawa upande wake, mlinzi mkuu wa mumewe akampatia taarifa kwa simu kwamba Maam you are to be killed (unatakiwa kuuawa) hawa watu wanajua kila kitu hivyo KIMBIA (RUN). Alikuwa hatarini hivyo hakuwa na muda wa kupoteza akapotea haraka, KGB hawakumpata mwanamke huyo hivyo ukaanza msako wa kimya kimya kwa sababu waliogopa kuziweka taarifa hizo wazi kwani zingewavua nguo kwa kuonekana ni wazembe mpaka yote hayo yanatokea na hawana taarifa! Hawakutaka aibu wakaamua kuifanya siri kumtafuta huyo DOUBLE AGENT IRINA ESPANOVICH.
Kupotea kwake Urusi mikononi mwa KGB ambao walimpachika jina la LUNATIC GIRL, ukawa mwanzo wake wa kuingia ndani ya nchi ya Tanzania.
Kwanini iwe Tanzania? IRINA alipiga hesabu zake akagundua kwamba kama angeenda nchi kubwa hususani ambazo zina usambaaji wa taarifa haraka wangekuja kumpata tu siku moja hivyo alihitaji kuishi sehemu ambayo hata KGB wenyewe wasingeidhania kwamba anaweza kuwepo na ile amani ambayo imetawala Tanzania ikamvutia kuishi hapa kwani ingekuwa ni ngumu kuja kujulikana kwamba yupo hapa. Yes, mpango ulikuwa sahihi sasa Tanzania angeishije na angeweza vipi kujilinda? Ukawa mwanzo wa kuanzisha jamii ya Siri ambayo aliiita LUNATIC SOCIETY, jina ambalo alipewa na KGB kwa usaliti wake. Kumbuka alikuwa mgeni hivyo asingeweza kuianzisha jamii hiyo mwenyewe ikamlazimu kumtafuta mtu.
Macho yake yakadondokea kwa Novack Nyangasa, mdogo wa raisi wa Tanzania ambaye aliamini angekuwa na nguvu ya kumpeleka anapo pataka yeye. Alimshawishi mwanaume huyo kwa urembo wake na kumpa mpango mzima juu ya utajiri ambao wangeenda kuutengeza, Novack akatokwa na mate ya uchu, akakubali. Jamii hiyo ikaanzishwa kwa nguvu ya mdogo wa raisi ambapo waliwasajili watu wakubwa; wanasiasa wakubwa, maprofesa, wanafalsafa, madaktari bingwa, wafanya biashara wakubwa na kila ambaye walimuona anafaa. Baadae raisi akazipata habari, akachukia sana na kumuita mdogo wake IKULU.
Akamtaka aifute jamii hiyo kwa mwezi mmoja tu pekee, huo mwezi ukatumika kummaliza yeye, raisi akawekwa kati akatakiwa kufa ili jamii hiyo iwepo. Moja kati ya mipango mikakati ambayo waliiweka ili kujilinda ni kuanzisha chuo cha kuwatengeneza vijana hatari kwa ajili ya ulinzi na kufanya kazi yao kwa nguvu pale ambapo ingebidi, zoezi hilo likatua mikononi mwa jasusi wa zamani wa Tanzania ambaye aliachana na kazi hiyo baada ya kuhusika na mauaji ya watu wengi sana, NIKOLAI GIBSON. Mwanaume huyo kwenye moja ya mazao yake alifanikiwa kumtengeneza kijana wa kuitwa YOHANI MAWENGE, bwana mdogo ambaye alimuokota Tandale kwa Tumbo akililia mapenzi na kutaka kujiua kisa uchi wa mwanamke.
Alimfunza namna ya kuwa mwanaume akampa begi la pesa akale maisha kwa mwezi mzima, alale na wanawake warembo ambao aliishia kuwaona kwenye runinga ili ushamba umtoke kisha baada ya hapo alikuwa na kazi naye. Alitengenezwa kikawa kiumbe cha kutisha na Kazi yake ya kwanza ikawa kwenda kumuua mcheza KAMARI mmoja huko BAMBALI Senegal na alitakiwa kurudi na bilioni 30 zilizokuwa mkononi mwa bwana huyo..... Huyu tuna mengi ya kuyasoma kwake ni mhimu sana.
Ukawa mwanzo wa mwanamke huyo wa KGB kuitawala Tanzania kwa miaka takribani thelathini. Lakini baadae Moja kati ya makosa makubwa ambayo waliyafanya ni kumuua mwanasayansi aliyedaiwa kuwa binadamu mwenye akili zaidi nchini.
NAFSI ZILIZO TELEKEZWA ni zipi na za nani?
Kulikuwa na utata wa maisha ya mwanaume Edison, bwana ambaye hakuwa na kumbukumbu na kwenye mfuko wake alikuwa anatembea na picha ambayo walidai ni ya mkewe, bwana huyu alikuwa akishangaa kwa sababu yeye binafsi hakuwa na kumbukumbu yeyote kama aliwahi kuwa na mke au familia. Kitu cha kushangaza kwa EDISON ni kwamba alikuwa anatafutwa ili auawe kuliko hata pesa inavyo tafutwa na maskini mpaka yeye mwenyewe akawa anashangaa.
Hali hiyo ilimlazimu kwenda kuishi maisha ya chini sana huko Kigogo Mwisho ili awe salama kwani hakuna ambaye angempata kirahisi akiwa kwenye maisha ya kifukara huko lakini usiku mmoja mvua ikiwa inanyesha akiwa ndani ya kijumba kibovu kwenye mkeka, akapokea simu ambayo ilimtaka atoweke eneo hilo kwa dakika kumi na tano vinginevyo angekufa. Aliduwaa ila hakuwa na namna aliondoka haraka ila kabla hajafika mbali akavamiwa na wanaume wa kutisha ambapo alimuua mmoja akafanikiwa kutoroka.
Safari yake ikawa ni kwenda kwa mlezi wake ambaye ndiye alimpa taarifa hiyo na ndiye alimtaka akaishi huko Kigogo mapaka mambo yakae sawa ili akampe ukweli wa kwanini anatafutwa sana? Kufika kwa huyo mlezi wake ambaye alikuwa ni mchungaji wa KKKT pale Mabibo Mwisho karibu na hosteli za wanafunzi wa NIT, alimkuta mtu huyo yupo kwenye hatua za mwisho za uhai wake. Hakumwambia kitu zaidi ya kumtaka aende nyumbani kwake kwenye banda la mbwa akachukue kitabu ambacho kingemfunulia ukweli kwamba yeye ni nani, kwanini hana kumbukumbu, maisha yake kabla yalikuwaje na kwanini anatafutwa sana na watu ambao yeye alidai hawajui!
EDISON alishangaa baada ya kuambiwa kwamba anatafutwa kwa kuhusika na mauaji ya makomando TISA wa kikosi maamulu cha KOM (KILL ON MISSION).akabaki ameduwaaaa!!!!!!!
Ilishawahi kukukuta kwenye maisha yako ukatakiwa kumuua mama yako mzazi kwa mkono wako mwenyewe? Hilo ni jambo baya na gumu lakini Yes, kuna mwanaume alitakiwa kumuua mama yake aliye mzaa ili nchi iwe salama. Je huyu naye hatima yake ilikuwaje?
Kuna uhusiano gani kati ya hizo NAFSI ZILIZO TELEKEZWA, IRINA ESPANOVICH na EDISON?
Unataka kumjua zaidi IRINA ESPANOVICH? Unataka kuijua kiundani LUNATIC SOCIETY? Unataka kujua uhalisia wa maisha ya EDISON kabla na baada ya hapo? Hizo nafsi ZILIZO TELEKEZWA ndizo hizo za makomando TISA (9) ambao alidaiwa kuwaua au kuna mengine nyuma ya mlango wa siri? Ungana nami kwenye simulizi yangu bora zaidi kuwahi kuiandika kwa mkono wangu....
1. Storyline yake ni kali sana
2. Dialogue (majibizano) yake ni kali sana.
3.Haitabiriki kabisa (huwezi kutabiri kinacho tokea baadae)
4.Lakini pia ina actions kali mno.
Mwandishi ni Mimi FEBIANI BABUYA
KARIBU UWEZE KUZIGUSA KURASA HIZI HAPA HAPA KWA KUTUMIA Coin.
127
12
CH
ongoing

DOSARI
Mwanamke mmoja kijana asiye na maisha yenye uwezo wa hali ya juu anajikuta ndani ya changamoto nzito zaidi kwenye maisha yake baada ya mzazi wake kuugua na kukosa njia ya haraka kuweza kumsaidia. Akiwa peke yake na kuishiwa na namna ya kuleta suluhu, anatafuta msaada mahali ambapo panamwingiza matatani zaidi ya matarajio anayojipa ya kuleta suluhisho.
Upande mwingine wa kisa hicho, mwanaume tajiri mwenye familia nzuri na maisha yaliyotulia anakutana na masaibu mazito ghafla sana yanayovuruga amani yote aliyokuwa nayo moyoni. Ni mikazo kutoka kwenye matatizo hayo inayomfanya ashindwe kujua ni jambo gani sahihi analotakiwa kufanya ili asonge mbele na kuyafanya yaliyomkuta kuwa mapito, lakini inamwia ugumu sana kufanikisha jambo hilo, na maamuzi anayochukua yanabadili kabisa mpangilio wote wa maisha aliotaka kuwa nao mwanzoni.
Katikati ya hayo yote, kuna visa na mikasa yenye kusisimua sana inayozileta hatma za wawili hao pamoja, na kutokea hapo maisha yao yanaelekea kwenye mkondo usionyooka kutokana na mambo mengi yanayowazunguka kuyatia maisha yao vikwazo na dosari nyingi. Fuatilia kisa hiki chenye kusisimua na kujenga sana.
DOSARI...
251
8
CH
ongoing

SIKU ZA MWISHO- (THE DARKNESS OF AN ANGEL)
SIKU ZA MWISHO!!!!!
Je wewe ni mdau wa IDAIWE MAITI YANGU? Je wewe ni mdau wa SAFARI YA GAVIN LUCA? Kama jibu ni ndiyo kwanini usiisome SEHEMU YA MWISHO ya mtiririko wa simulizi hizi iitwayo SIKU ZA MWISHO - GIZA LA MALAIKA (THE DARKNESS OF AN ANGEL?)........
Hii simulizi ni sehemu ya mwisho au season 3 ya IDAIWE MAITI YANGU ambazo zimetoka kwa collection kama ifuatavyo
1. IDAIWE MAITI YANGU
2. SAFARI YA GAVIN LUCA - LIONELA (THE ODYSSEY OF GAVIN LUCA)
3. SIKU ZA MWISHO - GIZA LA MALAIKA kwa kiingereza THE DARKNESS OF AN ANGEL
Collection hii inaihusu familia ya GAVIN LUCA na mwanae wa pekee LIONELA GAVIN LUCA. Hivyo kama uliisoma IDAIWE MAITI YANGU ukapata maswali ambayo yalijibiwa kwenye SAFARI YA GAVIN LUCA kisha đ
SAFARI YA GAVIN LUCA ikatuachia maswali mengi ambayo yanajibiwa ndani ya SIKU ZA MWISHO. Hivyo hakikisha unaisoma hii collection nzima ili uweze kuipata hatima nzima ya maisha ya familia Moja kubwa sana na ya Kitajiri barani Afrika, familia ya GAVIN LUCA.
SIKU ZA MWISHO (GIZA LA MALAIKA)- THE DARKNESS OF AN ANGEL.....
Ni sehemu ya tatu na ya mwisho ya mwendelezo wa IDAIWE MAITI YANGU na SAFARI YA GAVIN LUCA (THE ODYSSEY OF GAVIN LUCA)....
Humu utajua hatima ya familia ya GAVIN LUCA na mwanae wa pekee LIONELA na hatima ya zile nguvu zao.
Kwenye SAFARI YA GAVIN LUCA uliona JABARI akionekana msaliti, hivyo kama unataka kujua sababu nyuma yake kwamba kwanini alimsaliti mkewe wa ndoa? Basi hii ndiyo sehemu sahihi ya kupata majibu yako.
JABARI alituacha wote mdomo wazi baada ya kumuoa LIONELA kisha akaanza kuua familia ya LIONELA Lakini mkurugenzi wa shirika la kijasusi la Kenya (NIS) alikuwa na ajenda gani hatari kwa Tanzania na familia ya GAVIN ?
KAA NA MIMI TWENDE SAWA MUDA HUU UANZE KULISOMA MOJA YA ANDIKO BORA SANA KUWAHI KUTOKEA TANZANIA.
FEBIANI BABUYA
360
122
CH
complete

THE IMMORTAL BOND (Kifungo Cha Milele)
The Immortal Bond ni riwaya ya mapenzi ya kiajabu inayomfuata Yolanda Mekkanan, mchawi mwenye nguvu ambaye aliishi kwa karne nyingi, na Michael Nsebo, mwanaume aliyetokea kumpenda kwa dhati kupita Kiasi.
Mwaka 1622, wakati wa kilele cha majaribio ya wachawi wa Salem, Yolanda anatuhumiwa kwa uongo kutumia uchawi kuleta tauni ya mafua kwa watu zaidi ya maelfu na kuhukumiwa kifo. Ingawa hukumu yake ya kifo inapitishwa, roho yake inafungwa duniani kwa uchawi wa kale, ikimpa kutokufa (immortality). Akilazimika kuishi kupitia nyakati mbalimbali, akitazama wale anaowapenda wakiwa wazee na kufa, bila kuweza kupata amani ya kweli.
Karne baadaye, Yolanda anakutana na Michael Nsebo, mwanaume ambaye anahisi kuwa naye na mahusiano yasioeleweka. Anapomfahamu zaidi, anatambua kwamba Michael ni mfululizo mpya wa mapenzi yake ya kwanza na pekee, mwanaume ambaye hapo awali alipigana kumwokoa kutoka kwenye hukumu ya kifo.
Lakini Michael, asiyejua chochote kuhusu maisha yake ya hapo awali, anajitahidi kuuelewa mvuto wake mkubwa kwa Yolanda na kumbukumbu za ajabu zinazojitokeza kila wanapokuwa pamoja.
Yolanda na Michael wanapotafuta njia katika uhusiano wao mpya, adui wao was zamani anajitokeza ambaye amekuwa akimfatilia Yolanda kupitia Nyakati tofauti tofauti(different time zones), akitafuta kisasi. Riwaya hii inaunganisha pamoja mada za hatima ya wapendanao(themes of fate), kuzaliwa upya(reincarnation), na mapambano kati ya wema na uovu wakati Yolanda anapopigania kujinasua kutoka kwenye mzunguko wa hasara na hatimaye kudai upendo ambao umekuwa ukimkwepa kwa karne nyingi.
Kwa mchanganyiko wake wa mazingira ya kihistoria na ya kisasa, The Immortal Bond ni hadithi pana ya upendo unaovuka wakati, ukithibitisha kwamba upendo wa kweli ni wa milele.
239
9
CH
ongoing

FOR YOU
Vijana wawili mapacha kutoka katika familia ya Meja wa kijeshi, wanajikuta ndani ya sintofahamu baada ya jambo lisilotazamiwa kusababisha miili yao iingiliane. Na katikati ya hayo yote, kuna kisa Cha usaliti ndani ya Serikali ya nchi yao kinachopelekea familia yao kubomoka na umwagaji mwingi wa damu isiyo na hatia kwa sababu ya tamaa na migogoro inayoletwa na watu wenye pupa. Lakini ili kutimiza ahadi aliyoweka kwa ajili ya pacha wake, pacha mmoja anafanya kila lililo ndani ya uwezo wake akiwa na mkono unaomsaidia kupambana na maadui wao wote ili kukomesha matendo maovu yanayosababisha maumivu kwa wengi. Safari yake kutimiza hilo inakuwa na vikwazo vingi hasa kwa kuwa anakutana na mkazo wa kufanya yaliyo sawa ingawa kwa njia zinazoacha maumivu kwenye pande zingine muhimu kwa maisha yake.
Yote hayo na mengine mengi ni ndani ya hadithi hii tamu na yenye kusisimua sana; FOR YOU. Ahadi ni damu.
115
18
CH
ongoing

JIJI LA KAMARI
JIJI LA KAMARI ( GAMBLING CITY)
INTRO...........
Usiku wa kiza kinene ambacho kilikuwa kinasindikizwa na mvua ambazo hazikuwa na mpaka wa kuweza kuzielezea vyema, alionekana mwanaume mmoja akiwa ndani ya nguo zake nyeusi tii na begi jeusi usiku huo huku mwili wake ukiwa umefunikwa na koti kubwa jeusi pia ambalo lilikuwa refu kiasi kwamba lilivuka mpaka magotini.
Mikono yake ilifunikwa na gloves nzito nyeusi pia ambapo mkono wake wa kulia ndio ambao alikuwa ameutumia kuweza kushika begi lake mkononi akiwa anatembea kwa mwendo wa haraka haraka huku akiwa makini mno kuonyesha wazi kwamba alikuwa anatakiwa kulifikisha begi hilo salama kabisa sehemu ambapo lilikuwa linahitajika kuweza kufika.
Akiwa kwenye mwendo wake huo wa haraka, wakati amefika katikati ya barabara ndogo ambayo ilikuwa imezungukwa na majengo marefu na pembeni yake kukiwa na vichochoro vingi, alihisi kwamba eneo hilo ni kama lilikuwa na mtu au watu wengine ukiacha yeye hivyo alizidisha hali ya umakini kwa hapo ambapo alikuwa amesimama.
Masikio yake yalimtekenya vizuri mithili ya funguo zinapokuwa zinazamishwa kwenye kufuli na kumpa taarifa hiyo, alikuwa ni mtu wa kuutumia mlango wake wa sita wa fahamu huo wa hisia kwa umakini mkubwa hivyo alikuwa na uhakika kwamba hisia zake zisingeweza kumsaliti kamwe kwani alikuwa akijiamini kwenye jambo hilo akawa na uhakika kwamba kulikuwa na ugeni ndani ya hilo eneo.
Alisimama na kutulia ili kuweza kujua kwamba huyo mgeni alikuwa anatokea upande upi huku akiwa ameyafumba macho yake kuweza kujipa hali ya utulivu zaidi kwenye masikio yake. Akiwa bado amesimama hapo alihisi kama kuna kitu kilikuwa kinakuja kwa kasi sehemu ambayo alikuwa amesimama hivyo aliinama kwa kasi mithili ya radi ya mvua.
Wakati anainama alipishana na shoka ambalo lilienda kukita kwenye ukuta mmoja wa jengo la pembeni. Aligeuka haraka ila wakati anageuka alitumia muda mrefu ambao ulimpa nafasi mtu ambaye alikuwa ameingia hapo kufanya kile ambacho alikuwa anakitaka.
Alihisi kifua kinamuwasha mithili ya mtu aliye tafuna pilipili kichaa maana spidi ambayo mvamizi aliitumia kumkita hapo kifuani haikuwa ya binadamu mwenye mifupa ya kawaida bali alikuwa ni mashine haswa kama namna umeme unavyo safiri kwenye zile njia zake. Alipokea mishindo ya haraka na mabuti makali hali iliyofanya begi kumtoka mkononi huku ikionekana wazi kwamba mabuti hayo yalitokea kwa mtu ambaye alidhamiria kabisa kumuua ndiyo maana hakumpa hata nafasi ya kuweza kumtazama maana mvamizi huyo uso wake ulifunikwa kwa kitambaa cheusi na hata mvamiwaji hakupata hiyo nafasi ya kumtazama kwa ukaribu.
Mwanaume huyo licha ya kurushwa mbali na mabuti hayo hali ambayo ingemfanya auvunje mgongo wake kwa kujibamiza kwenye kuta za mawe mazito za majengo ambayo yalikuwa pembeni, hakuwa fala kufa kijinga namna hiyo. Mkono wake ndio ambao aliutumia kukita kwenye kuta hizo na sio mgongo ambao ulitua ukutani kwa nguvu kubwa.
Kasi ambayo alitua nayo kwa mkono wake ililifanya koti lake kujivuta kidogo na kwenye mkono wake ikaonekana alama ya tatoo (tatuu) ambayo ilisomeka kama 001. Baada ya kujichomoa hapo ndipo aligeuka na kumuangalia mtu ambaye alionekana alihitaji kumuua, mtu huyo alikuwa kwenye mavazi meusi kama yeye na koti kama lake, yaani kiufupi wote walikuwa wamevaa sawa ila utofauti wao ni kwamba mvamiwaji alivaa kofia aina ya pama kichwani ila mvamiaji alikuwa amejifunika tu kitambaa kwenye uso wake hivyo sura yake haikuwa ikionekana kabisa.
Baada ya hapo ulipigwa mkono wa hatari mpaka umeme ulipo katika ghafla ndipo mvamiwaji alitulia akiwa makini maana hakuwa akimuona mtu ambaye alitakiwa kumshambulia huku akiwa amepigwa vibaya na umeme huo kukatika alishukuru japo ilikuwa ni hatari maana angeweza kuuawa bila kujua mhusika yuko wapi ila aliamini kwamba angepata dakika chache za kupumzika maana bila hivyo ni lazima angekufa.
Akiwa anaangaza kwa umakini huku na huko umeme ulirudi tena ghafla na ndipo alipo gundua kwamba ndani ya eneo hilo hapakuwa na mtu mwingine zaidi yake, mvamizi alikuwa ameondoka muda mrefu ila chini palikuwa na karatasi nyeupe ambayo ilikuwa imesainiwa kwa damu huku ikiendelea kunyeshewa na mvua.
Aligeuka na kuangalia pale ambapo begi lilikuwa limedondokea ili kujua usalama wake ila kwa bahati mbaya begi halikuwepo kabisa eneo hilo, alishtuka sana akionyesha hofu ya wazi moyoni na kwenye uso wake hivyo hakuwa na namna zaidi ya kuisogelea ile karatasi ili aweze kusoma kile ambacho kilikuwa kimeandikwa.
âKAMARI YANGU YA MWISHO, NDIYO KAMARI YAKO YA KWANZAâ hayo ndiyo maneno ambayo yalikuwa yameandikwa hapo.
Aliogopa sana baada ya kuisoma huku akionekana wazi kwamba mikono yake ilikuwa inatetemeka wakati huo. Hiyo ilikuwa ni kauli ambayo alikuwa anaitumia mwanaume mmoja ambaye alimuua yeye mwenyewe kwa mkono wake miaka kadhaa ambayo ilikuwa imepita huko nyuma, huku begi ambalo lilionekana kuwa na nyaraka mhimu mno likiwa limepotea kizembe.
Inawezekanaje mwanaume ambaye alimuua kwa mkono wake mwenyewe bado awe hai? Hilo begi lina nini mpaka mtu ambaye alisemekana kwamba alikufa aweze kupotea nalo? Nini maana halisi ya JIJI LA KAMARI na jiji hilo lina mambo yapi na siri zipi labda?
Unategemea kukutana na nini humu ndani? Mimi nashika kalamu yangu sasa nakaa mezani, kazi yako wewe ni kuhakikisha unaenda nayo nukta kwa nukta ili uweze kuifunua kila kurasa kuweza kuzisoma serikali tatu kwa wakati mmoja ndani ya JIJI LA KAMARI.
Kalamu ni yangu mwenyewe;
FEBIANI BABUYA.
215
88
CH
ongoing

Niliemdhania kahaba kumbe bikra
Roma mbeba mizigo ndani ya soko la Mbagala Rangi Tatu anamdhania Edna Kama mwanamke anaejiuza ,baada ya mwanadada huyu kuwekewa dawa ya usingizi kwenye kinywaji na maadui zake katika ulimwengu wa Biashara akiwa ndani ya hoteli na Roma anambeba Edna na kumpeleka Geto kwake na afanya nae mapenzi.
Edna kwa Mara ya kwanza analala na Roma pasipokujitambua na kupoteza usichana wake ,baada ya tukio Hilo anaamua kuolewa na Roma kwa mkataba wa Miezi sita ili kuepuka kuolewa na mwanaume asiempenda ,baada ya Roma kufunga ndoa na Edna anakuja kugundua kuwa mke wake anamiliki kampuni kubwa Nchini huku akiwa na utajiri wa kutisha.
Edna anamuona Roma kama mtu asiyekuwa seriasi na maisha kutokana na aina ya mfumo wa maisha yake ,maisha ya kuwa na wanawake wengi swala linalomkasirisha Edna.
Edna anajitahidi kuweka ukaribu na Roma ili kujua sababu ya mume wake macho yake kubadilika Rangi anapokuwa na hasira na kuwa ya kijani huku akiwa na roho ya ukatili mno
Idara na mamlaka za kiusalama Nchini zinashangazwa na uwezo wa Roma wa kuzungumza Lugha zaidi ya ishirini na mbili na wanaanza kutafuta taarifa zinazomuhusu Roma lakini licha ya kupata taarifa inayoonyesha Roma kusomea ndani ya chuo kikubwa Duniani Cha Harvard wanakosa taarifa zingine zinazomuhusu Roma na kuishia kujiuliza Roma ni Nani haswa
222
29
CH
ongoing

MIMI NA MIMI
Simulizi yenye kusisimua kuhusu maisha halisi ya mwanaume kijana wa kitanzania anayekwenda likizo kutafuta wakati mzuri. Huko anakutana na watu, visa, na mikasa inayomfanya abomoe na kujenga aina ya utu unaofaa mbali na ulealiokuwa nao mwanzo. Na anapotafuta furaha anayoitaka, anakuja kuipata mahali ambapo hakutarajia kabisa, ingawa kwa magumu na mabaya mengi anayohitaji kupitia ili kuweza kuistahili furaha hiyo.
Yote ni ndani ya MIMI NA MIMI.
390
109
CH
ongoing

CHANGE (BADILIKO)
Ni hadirhi inayohusu wanawake wawili wanasheria walio marafiki wa damu, wanapokutana na mwanaume aliye na maisha yaliyojaa siri nzito sana zinazokuja kuingiliana na maisha yao pia mpaka kupelekea hali zenye utata mwingi kuwazunguka. Wakiwa na utayari kukumbana na changamoto zinazoletwa na mikasa mingi yenye kutatanisha, je wataweza kufaana na mabadiliko yatakayoletwa na matokeo ya visa hivyo?
Yote ni ndani ya CHANGE... BADILIKO.
110
17
CH
ongoing

INVISIBLE
Ni hadithi yenye kusismua inayomhusu mwanaume kijana anayejitahidi kuishi maisha rahisi na yenye usawaziko, lakini yanampa mkondo tofauti kabisa kwa kumwingiza katika hali yenye utata inayofanya maisha yake yote yabadilike. Na anakutana na changamoto nyingi zinazomhitaji atende kwa njia ambazo hakuwahi kuwazia kabla, lakini ndiyo zinamwongoza kuifikia tamati yenye kuridhisha kutokana na yanayomzunguka kumjenga zaidi kimtazamo, na kiutu.
INVISIBLE.
268
36
CH
ongoing

BADO NINAISHI
BADO NINAISHI.
Inamhusu mwanaume mmoja ambaye alikuwa ni kiongozi wa genge la kihalifu ambalo lilikuwa linaitwa SARAFU KUMI NA TANO.
Mwanaume huyo alikuwa anasakamwa na mamlaka za usalama ndani ya taifa la TANZANIA kwa miaka kumi bila mafanikio. Ndipo alitumika mwanamke mrembo ANELIA BATON ambaye alimwingiza mwanaume huyo kwenye HONEY TRAP kwa kupitia kikosi hatari kutoka ndani ya shirika la kijasusi kiitwacho HOLY TRINITY, walifanikiwa kumpata mwanaume huyo.
Alihukumiwa kifungo cha miaka sitini gerezani na baada ya hapo angenyongwa. Alipelekwa ndani ya gereza hatari la DOMINIC, huko alikutana na tajiri mmoja ambaye alikuwa amejificha ili kuyalinda maisha ya mwanae ambaye alitekwa.
Tajiri huyo alikutana na mwanaume huyo aliye itwa REMMY CLAUDE na kumuomba akamuokoe mwanae yeye anyemsaidia kumtorosha gerezani. Walifikia makubaliano mwanaume akatoroshwa gerezani.
Huko uraiani alienda kumtafuta mtoto wa kiongozi huyo lakini wakati anafanikisha hilo tajiri huyo alikuja kupata habari kwamba mfungwa huyo aliye Mtorosha gerezani hakufungwa kwa bahati mbaya bali ilikuwa ni mipango yake yeye ili akutane na tajiri huyo.
Alishangaa sana ilikuwaje mtu ajitoe kafara kufungwa gerezani kwa sababu yake? Ndipo akaja kugundua kwamba Remmy alikuwa anautafuta umoja wa watu ambao hawakuwa wakifahamika na tajiri huyo ndiye mtu pekee ambaye angemsaidia kuwajua wote ndani ya umoja huo.
Anakuja kushtuka akiwa amechelewa, mwanaume huyo alikuwa amempata mwanae tayari na kupotea naye hali ambayo ilileta maafa makubwa sana na kulilazimu shirika la kijasusi kuanza na moja kumtafuta.
SARAFU KUMI NA TANO halikuwa pambo bali ilikuwa idadi ya wanafamilia ambao waliuawa kikatili takribani miaka ishirini iliyokuwa imepita ila kwa bahati mbaya mtu mmoja alifanikiwa kuishi.
Sitaki nikumalizie uhondo. Unataka kujua huyo Remy ni nani? Kwanini alijitoa sadaka kwenda gerezani? Huo umoja una nini hasa ndani yake na unaongozwa na nani?
Nini hatima ya maisha ya Remy Claude?
Hili ni moja kati ya andiko ambalo litakufanya ujivunie sana kuyasoma maandishi.
SIMULIZI HII INAPATIKANA HAPA HAPA HIVYO TWENDE SAWA PAMOJA ILI UWEZE KUYAGUSA MAISHA YA BWANA REMMY CLAUDE TUPATE KUMJUA NI NANI HASWA NA ANAHUSIANA VIPI NA TITLE YA BADO NINAISHI AU ASHRAFU NDILO JINA LANGU âď¸đĽ
304
100
CH
complete

THE REVENGE SEASON 1 (DERICK)
Kijana mdogo Derrick anaapa kulipa kisasi Kwa watu wote walio husika na mauaji ya wazazi wake pamoja na mdogo wake wa kike, anapambana kadili ya uwezo wake na anafanikiwa kuwatambua watu hao na kuanza kumuangamiza mmoja baada ya mwengine
131
10
CH
ongoing

Safari ya Kweka â Kutoka Umasikini hadi Uongozi wa KGC
UTANGULIZI
Katika kijiji cha Mwika, kilichopo mlimani Kilimanjaro, alizaliwa kijana mmoja aliyepewa jina Joseph Kweka. Alikuwa mtoto wa pekee wa Mzee Petro Kweka na Mama Anna Kweka, wakulima wa kawaida waliotegemea kahawa na ndizi kuendesha maisha yao. Tangu utotoni, Joseph alikuwa tofauti. Alikuwa na udadisi usio wa kawaida kuhusu vitu vya kielektroniki, na mara nyingi alionekana akichunguza redio ya baba yake, akijaribu kuelewa jinsi inavyofanya kazi.
Katika mazingira yenye changamoto, ambako shule za kata zilikuwa na uhaba wa walimu na vifaa, Joseph alijitahidi sana katika masomo yake, akiamini kuwa elimu ilikuwa tiketi yake ya kutoka kwenye maisha ya kawaida na kuelekea ndoto kubwa. Alikuwa na ndoto ya siku moja kuwa mjasiriamali mkubwa katika sekta ya teknolojia, ingawa wengi waliona mawazo yake kama ndoto zisizowezekana.
Baada ya safari ndefu ya masomo, aliingia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusomea Teknolojia ya Habari (IT). Huko, alikutana na changamoto mpyaâmaisha ya jiji, ushindani wa wanafunzi wengine, na ugumu wa kifedha. Lakini, kila changamoto ilikuwa fursa kwake. Alianza kutengeneza programu ndogo ndogo za biashara, akijifunza mbinu za ujasiriamali kwa vitendo.
Baada ya kuhitimu, Joseph alifanya maamuzi magumuâbadala ya kutafuta kazi kwenye kampuni kubwa, aliamua kujenga biashara yake mwenyewe. Akiwa na mtaji mdogo, akaanzisha Kweka Group of Companies (KGC), kampuni iliyolenga kutoa suluhisho za kidigitali kwa biashara ndogo na kubwa. Njia yake haikuwa rahisi: alikumbana na vikwazo vya kifedha, usaliti wa washirika wa biashara, na changamoto za kibinafsi.
Katika safari yake, alihusiana na watu waliompa msaada na wengine waliomvunja moyo. Alipitia mapenzi ya ujana yaliyojaa matumaini na huzuni. Mahusiano yake na wazazi wake nayo yalipitia majaribu, hasa pale walipoona akipambana na biashara badala ya kazi ya ofisini yenye uhakika.
Hii ni hadithi ya kujitoa, maono, na ushindi dhidi ya vikwazo. Ni safari ya kijana wa kawaida aliyethubutu kuwa tofautiâaliyepigana kutoka kijiji cha Mwika hadi kuwa mfanyabiashara maarufu wa teknolojia nchini Tanzania na Afrika Mashariki.
Karibu kwenye safari ya Joseph Kweka, safari ya mafanikio iliyojaa mafunzo, vikwazo, na ushindi.
128
9
CH
ongoing

I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
I WANT TO DIE JUDGE ni hadithi ya kijana mmoja aliyeitwa Jamal, ambaye alishuhudia tukio la kutisha ambapo familia yake yote iliuawa kwa ukatili na wanaume wawili. Jamal aliona mwanaume mmoja akikata kichwa cha baba yake na kuondoka nacho mbele yake.
Kilicho msaidia Jamal kubaki hai ni msaada kutoka kwa mtu ambaye hakujua alitokea wapi. Baadaye aligundua kuwa huyo mtu alikuwa jasusi kutoka idara ya usalama wa taifa.
Jamal alipelekwa wilayani Kyela, jiji la Mbeya, ambapo aliishi kwa miaka saba pembeni mwa mlima Livingstone akifanya mazoezi makali ambayo hakuelewa kwa nini yalifanywa.
Baada ya miaka saba, alikabidhiwa mkufu ambao aliambiwa ulinde kwa maisha yake yote, hata kama inahitajika afe ili kulinda mkufu huo (mkufu ndio chanzo cha kila kitu kilichotokea baadaye). Hapo ndipo safari ya kurudi mjini ilipoanza.
Jamal alikuzwa na kuwa kamanda mkubwa ndani ya jeshi la Tanzania chini ya usimamizi wa mkuu wa majeshi. Lakini alikumbana na matatizo makubwa alipoanza kufuatilia kundi moja lililojulikana kama M96 OWNER'Z, ambalo lilihusishwa na mauaji ya familia yake.
Baadaye, Jamal alishitakiwa kwa kuua makamu wa rais wa Tanzania, ingawa ukweli ulidhihirika baadaye kwamba makamu huyo alikuwa hai. Ilikubaliwa kuwa Jamal alifungwa gerezani kwa kosa la kumwua makamu huyo ambaye alikuwa bado yupo hai.
Jamal alipata nafasi ya kutoka gerezani kwa kushirikiana na serikali, lakini aliambiwa atakubaliana na suala la kumrudisha mwanasheria mkuu wa Tanzania, ambaye alikuwa ametekwa huko MedellĂn, Colombia. Mwanasheria huyo alikuwa ndiye aliyesababisha Jamal afungwe gerezani.
Jamal alikubali kumleta mwanasheria huyo, lakini baada ya kumaliza kazi hiyo, alijikuta akitekwa na kupangwa kuuawa kwa sababu alikuwa anajua siri nyingi za serikali na viongozi wa juu waligopa kuwa angeweza kuwaumbua.
Jamal alipigwa risasi zaidi ya kumi na mwili wake kutupwa baharini. Baada ya mwaka mmoja, kiumbe cha kutisha kilichoingia mjini kilianza kuwashambulia wale wote waliotekeleza unyama dhidi ya Jamal.
Katika ulimwengu wa watu wenye nguvu, alitokea mwanamke aitwaye Catherine, ambaye alidaiwa kuwa mtoto wa mkuu wa kambi ya MAKOMANDO nchini Cuba. Mwanamke huyu alikuwa na nguvu kubwa, na dunia iliamini kuwa hakuna aliyeweza kusimama mbele yake.
Jinsi Catherine alivyovuka mipaka ya nchi na kuingia kwenye maeneo ya hatari? Hii ni hadithi ya kutishaâunataka kujua nini kilijificha nyuma ya mauaji ya makamu wa rais na kifo chake kilichosemekana?
MASWALI YANAYOHITAJI MAJIBU
Kuna nini ndani ya kundi la M96 OWNER'Z?
Je, ni nini kilichofichwa nyuma ya mauaji ya makamu wa rais na yeye kuwa hai, ikiwa ulimwengu wote ulijua kuwa amekufa?
Mwanasheria mkuu ni nani na kwanini alitekwa MedellĂn, Colombia?
Vipi Jamal alionekana kuwa muuaji wa makamu wa rais na madaktari walithibitisha kifo chake hadharani?
Mkuu wa majeshi ni nani na kwanini hakumtetea kijana wake?
Jamal alikufa baharini baada ya kupigwa risasi kumiâni kweli?
KUMBUKA
Yule aliyeondoka na kichwa cha baba yake, Jamal, ndiye mwanaume aliyeingia Ikulu, akamwua Rais na kuondoka akiwa amepigwa risasi moja tu. Na ndiye huyohuyo ambaye alimpiga mwanaume mwingine aliyetaka kumwokoa, kisha akamkata sehemu zake za siri na kuwarushia mbwa wale.
Hadithi hii ni ya kutisha. Ikiwa ulikuwa unawaza maisha yako kuwa ya huzuni, hakikisha unapata nafasi ya kuisoma hadithi hii bora ambayo haijawahi kuandikwa hapo awali.
Tuliza akili zako, achana na kila kitu kwa muda huu, kwani ikiwa utachanganya mambo mengi, hautaelewa, na utaishi kwa mashaka. Hii ni hadithi bora na ya ajabu ya Bux the Story Teller.
Magic fingers, kalamu ni yangu mwenyewe;
Bux the Story Teller.
Jina langu naitwa FEBIANI BABUYA.
296
100
CH
complete

Solo King: Ancient legacy
Hapo zamani, kabla ya historia kuandikwa, aliishi mtu mmoja ambaye alivuka mipaka ya asili. Alikuwa mchawi mwenye nguvu zaidi kuwahi kutokea duniani, aliyefikia upeo wa juu lakini jina lake lilisahaulika, na urithi wake ulipotea kwa muda mrefu.
Kitu kimoja kilichobaki ni kitabu cha kale, kilichoandikwa kwa lugha zilizozungumzwa zamani, lugha ambazo sasa ni za kihistoria. Kitabu hicho kilijulikana kama FORBIDDEN GRIMOIRE, na kilikuwa na masalia ya maarifa yake pamoja na nguvu zisizo za kawaida.
Karne zilipita, falme zilikuja na kupita, dunia ilibadilika, na uchawi ukawa ni hadithi tu za kusadikika.
Lakini hatima haikupotea. Kijana mmoja aitwaye Jimmy anakuja kubeba hatima yake bila kujua.
Usikose simulizi hii ya kusisimua, yenye matukio ya ajabu na mabadiliko ya nguvu. Inamhusu kijana machachari aitwaye Jimmy, anavyopitia changamoto na majira, na jinsi anavyotoka kuwa dhaifu hadi kuwa mwenye nguvu kubwa.
1163
27
CH
ongoing

Safari ya Gavin Luca- Lionela
Idaiwe Maiti Yangu Season 2 â
Gavin Luca
Katika Idaiwe Maiti Yangu, tulimfahamu Gavin Luca, lakini alibaki kuwa na hali ya kutatanisha. Hatukujua kama alikufa au alifanikiwa kuishi. Zaidi ya hayo, hatukuweza kugundua hatima ya nguvu zake wala mustakabali wa mtoto wake katika zile nguvu.
The Odyssey of Gavin Luca inakuja kutoa majibu ya maswali haya yote. Tutajua kilichotokea wakati ule, nini kilitokea kwa Gavin Luca, na ni nini kinatarajiwa kutokea siku zijazo.
Lionela, mtoto pekee wa Gavin Luca, anakuja kuwa kiumbe mwenye nguvu nyingi duniani, akitambua ukweli kwamba baba yake alikuwa mfu. Lakini je, ni kweli alikufa? Hatujapata uthibitisho wa kifo chake, na hakuna ishara ya uwepo wake.
Kama alikufa, kwa nini hakukuwa na dalili yoyote ya upanga wake au alama nyingine za uwepo wake? Kama alifanikiwa kuishi, alifanikiwaje kutoka kwenye hali hiyo? Alipo wapi sasa, na ni nini hatima yake?
Nini Kinaendelea Kuikumba Familia Hiyo Maarufu na Tajiri?
Je, kuna mtu alisahaulika katika The Immortals, au kuna siri nyingine nyuma ya pazia?
Nakaribisha kutazama hii simulizi inayofuata! Hautakiwi kuikosa simulizi hii kwa gharama yoyote ile.
Kabla ya kuisoma hii, hakikisha umesoma Idaiwe Maiti Yangu, kwani ni sehemu ya kwanza ya hadithi hii.
Idaiwe Maiti Yangu inapatikana hapa Fasihinet, ikiwa imekamilika kabisa. Kazi Kwako âď¸
Twende Sawa â
WhatsApp: +255621567672
Wao wananiita Bux the Storyteller.
Jina langu ni Febiani Babuya.
Wasalaam.
650
121
CH
complete

Mikasa ya ajabu nilioishuhudia kwa macho yangu
Kwanza kabisa, nianze kwa kusema kuwa nina mikasa miwili ya kipekee ambayo nimewahi kuishuhudia kwa macho yangu na kuifanya kwa mikono yangu mwenyewe.
Mkasa wa kwanza unahusu mimi na ndugu zangu, ulitokea nikiwa na miaka 14 - 15, mwaka 2000 - 2001, huko mkoani Mara, wilaya ya Tarime, Tanzania.
Mkasa wa pili unanihusu mimi pia, na ulitokea nikiwa mtu mzima, kuanzia mwaka 2012 hadi 2018. Huu ni mkasa wa maisha ya kitajiri, uliohusisha nguvu za giza.
Kuna nyuzi kadhaa ambazo nimekuwa nikizisoma za watu mbalimbali wakisimulia visa na mikasa ya maisha yao au ya jamaa zao, ambayo waliwahi kupitia. Hivyo, nikajiona kuwa sasa ni wakati muafaka wa kuleta simulizi za maisha yangu ili kuwafundisha na kuwaonya vijana wenzangu, hasa wale wenye tamaa ya kupata mali kwa njia niliyoifanya mimi.
Naomba wale vijana waache mara moja, kwa sababu mwisho wake unaweza kuwa kifo mikononi mwa shetani. Ingawa mimi niliponea chupuchupu.
124
0
CH
ongoing

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa
Naitwa Rojaz, nikiwa mtoto wa tatu kati ya watoto sita katika familia yetu. Nimezaliwa kwa wazazi ambao walikuwa na ndoto ya kuona watoto wao wanapata elimu bora na kufikia malengo yao. Hii ni ndoto ya kila mzazi, kwani hakuna mzazi anayewalea watoto wake bila kutamani kuona wanapata mafanikio katika masomo yao.
Nimeweza kufika kidato cha nne, lakini matokeo yangu hayakuwa mazuri. Nilijikuta nikikosa majibu ya moja kwa moja kuhusu sababu ya kushindwa kwangu. Hata hivyo, najua kuwa uzembe wangu na uzembe wa wenzangu shuleni ulifanya niwe na matokeo duni. Wakati wengine walijitahidi na kuzingatia masomo yao, mimi niliwekeza muda wangu kwenye michezo isiyo na tija. Hii haimaanishi kuwa nilidhihaki elimu, bali mazingira yangu na familia yangu ya kipato cha chini yalichangia katika changamoto nilizokutana nazo. Elimu yangu, kuanzia kidato cha kwanza, ilitegemea michango ya familia, marafiki, na misaada kutoka kwa shangazi au mamdogo.
Kwa kifupi, nilikulia katika familia duni, lakini hiyo haikunizuia kutoka kwa juhudi yangu ya kuboresha maisha yangu.
198
2
CH
ongoing

IDAIWE MAITI YANGU
GAVIN LUCA
Ndilo jina ambalo limeishikilia Idaiwe Maiti Yangu.
Hili ni jina la mwanamume mmoja ambaye anatusafirisha mpaka Kenya, ndani ya msitu wa Mau, ambako ndiko kila kitu kinapoanzia. Mwanzo wa simulizi hii unaanza na mwanaume huyo akiwa ametekwa na makomando wa Jeshi la Tanzania.
Aliteswa vikali, kisha akauawa kwa kupigwa risasi baada ya kuchomwa moto. Lakini muda mfupi baadaye, jambo la ajabu lilitokea. Mtu mwingine aliingia katika eneo hilo na kuwaua makomando wote, isipokuwa mwanamke mmoja tu aliyenusurika, aitwaye Sarah Martin.
Sarah alishangazwa sana kumwona mwanamume huyo, kwani alikuwa ndiye yuleyule waliyemuua dakika chache zilizopita. Inawezekanaje? Idaiwe Maiti Yangu itatupatia majibu sahihi.
Gavin Luca alikuwa akitafutwa na mamlaka za usalama kwa miaka mingi, mpaka alipokuja kujitokeza hadharani.
Kutokea kwake kulisababisha maafa makubwa ndani ya Afrika, yakiwemo mauaji ya zaidi ya marais wawili.
Mwanaume huyu anatoka katika familia yenye historia ya kutisha na utata mkubwa. Hatimaye, akawa kiumbe wa ajabu kabisa kwenye dunia ya watu wenye mabavu.
Gavin Luca pia aliaminika kuwa na nguvu zisizo za kawaida, ambazo alipata huko China. Kurejea kwake kulianza enzi mpya ya utawala wa familia yake ndani ya Afrika nzima.
Sasa Gavin Luca ni nani? Alitokea wapi? Kwa nini alitafutwa kwa miaka mingi? Ni nguvu za aina gani alizokuwa nazo? Na kwa nini alionekana akiwa hai baada ya kuuawa?
Hii ni simulizi moja bora sana kuwahi kuandikwa hapa Tanzania. Twendeni sawa, tukazifunuue kurasa za kiumbe huyu wa ajabu.
NB: Simulizi hii ni ya kutunga tu. Haina uhalisia wa maisha ya mapenzi, ujasusi, siasa, usaliti, uzandiki, watu, mauaji, nguvu za ajabu, na yote yaliyoandikwa humu ndani.
484
105
CH
complete

JUMBA JEUSI
JUMBA JEUSI......
SIASA NI KAMARI....Je NANI HUIBUKA MSHINDI?
JUMBA JEUSI ni andiko ambalo linaangazia siasa kwa ujumla wake....
Inaangazia namna viongozi duniani wanavyo yatumia madaraka kuhadaa watu lakini pia kufanya mambo ya kutisha...
JUMBA JEUSI ni sanaa ya siasa ndani ya maandishi....utajifunza namna wananchi wanavyo danganywa na wanasiasa, namna wanasiasa wanavyo yafanya mambo ya kutisha nje ya macho ya kawaida ...
Je wananchi wanapaswa kufanya nini kuhakikisha wanaikimbia hiyo hali na kuyapigania maslahi ya mataifa yao?
Kumbuka tu kwenye kundi la wajinga wengi ambao wanadanganywa na wanasiasa huwa wanaibuka watu werevu, sasa watu hao huwa hawataki kwenda na ule ubaradhuli wa wanasiasa na mambo huwa yanaanza kubadilika hapo kwa sababu wanasiasa huwa hawawapendi watu wa namna hiyo.....
Unahisi inakuaje kwenye mtanange wa namna hiyo baina ya watu werevu ambao wanaamua kuyatoa maisha yao kwa ajili ya kuwapigania wengi na mataifa yao? NI WAKATI SAHIHI WA WEWE KUYAPATA MAJIBU KWA KULISOMA ANDIKO HILI.
KWA LEO NAKULETEA SEHEMU YAKE YA KWANZA
Bux the storyteller
CIAO
450
101
CH
complete

Chanzo Ni Yeye
Simulizi ya kubuni ya kijana wa mtaani aitwaye Ayubu ambaye kwa sababu zisizojulikana anajikuta akiwa na maadui wengi bila kuwatambua....kuna chanzo cha yote tafadhali ungana na mimi mwandishi wako Machokulenga TZ
270
7
CH
ongoing

Gereza la Hazwa
Mvua ilimwagika kwa nguvu, upepo mkali ukiparaganya miti na radi zikilipuka mithili ya mapigo ya ngoma za kuzimu. Huu si msitu wa kawaidaâni Elnino, kichaka kinachokomeza roho za wasiotarajia, hata mchana ukiwa na giza lisilo na mwisho.
Lakini usiku huu, kivuli kilikuwa kinakimbia kwa kasi isiyoelezeka, miguu yake ikizama kwenye tope zito. Uso wake ulikuwa umefunikwa na nywele chafu na ndevu ndefu, macho yake yakiangaza hofu isiyoelezeka. Alikuwa akitorokaâlakini kutoka kwa nani?
Nyuma yake, wanaume sita walimsakama. Wanne walikuwa wamevaa mavazi ya kininja, wakipotea na kurejea kwenye giza kama manyoya yanayorushwa na upepo, huku wawili wakiwa wamevalia magwanda ya kijeshi. Hakukuwa na huruma katika macho yaoâmauti pekee ndiyo aliyoyajua.
Kisu kikubwa kiliruka kwa kasi kuelekea shingo yake, kikapita kwa milimita chache tu. Punde, alikata mwelekeo na hakuwapo tena. Mmoja wa wawinda wake alisimama, akisikiliza kwa makiniâlakini upepo ulisambaza sauti kila upande, ukivuruga hisia zake. Walielekezana kimyakimya: "Muaue."
Lakini ghafla⌠tone la jasho likamdondokea mmoja wao. Akakoki bastola, akaiinua juu, akifyatua bila kusita. Hakuna kilichompata mtu huyo wa kutisha, aliyejirusha kutoka juu ya mti kwa kasi isiyoelezeka. Mikono yao ilikutana kwa sekunde chache, mapambano ya mwili kwa mwili yakaanza juu ya mti. Risasi sita zilifyatukaâhakuna hata moja iliyompata.
Mlio wa mifupa ukasikika. Shingo ya askari mmoja ilikatika kwa sekunde chache tu. Mwili wake ukaanguka huku damu ikimwagika kwa kasi. Mwanaume huyo mchafu hakuwa na muda wa kusherehekea ushindi. Kisu kikubwa kilikuwa kimetua mgongoni mwake, kikamdhoofishaâlakini hakuwa tayari kufa.
Mbele yake kulikuwa na maporomoko makubwa yasiyo na mwisho. Nyuma yake, waninja wanne na askari mmoja wamesimama, wakimtazama kwa macho baridi. Hakuhangaika kugeuka⌠alijirusha kwenye giza la maporomoko.
"He is not human, heâs completely a devil."
"But no survive, he is no more there."
"Let's go and take Donaldâs body."
Walidhani kuwa msako wao umeisha. Lakini walikoseaâŚ
Mwanaume huyu alikuwa mfungwa wa miaka 10 katika gereza ambalo hakuna aliyewahi kutoroka kwa miaka 200. Gereza ambalo hakuna mfungwa anayejua lilipo. Lakini leo, mtu mmoja yuko nje.
Nani huyu? Ni kwa nini wanamtaka afe? Na je, kweli ameangamia kwenye maporomoko hayo...?
1000
116
CH
complete

Mapenzi na kisasi
Simulizi inaelezea nguvu ya mapenzi na kisasi kwa mtu anayetaka kuondoa furaha yako ya mapenzi
497
16
CH
complete

Damiani
Damiani mhitimu wa chuo kikuu cha uhasibu , anahitimu masomo yake na kurudi kijijini kwao kwa ajili ya kusubiria upepo wa ajira lakini katika hali ya kutokutegemea mama yake kipenzi anapigwa risasi mbili za kifuani na kufa hapo hapo na hio inatokana na kumpatia msaada mwanaume ambae hamfahamu mwenye asili ya ulaya (mzungu ) ambae na yeye alikuwa kwenye hatua ya mwisho ya kupoteza uhai wake kwani alikuwa na jeraha la risasi tumboni ,lakini mzungu huyo kabla ya kupoteza maisha anamkabidhi damiani nyaraka bila kumpa maelekezo ya aina yoyote ile .
Damiani anajikuta anajenga chuki na kisasi kwa watu waliohusika na mauaji ya mama yake , anajiapiza kuwatafuta mahali popote pale na kulipiza kisasi , katika harakati za kuwatafuta wabaya wake anajikuta akifahamu siri nzito iliokuwa nyuma ya kifo cha ghafla cha raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania , anapata waraka ulioachwa na raisi huyo uliopewa jina la KAULI YA MWISHO YA RAIS KABLA YA KIFO CHAKE .
JE UNAFIKIRI ATAFANIKIWA KULIPIZA KISASI CHAKE ?
JE NI KAULI GANI YA MWISHO ALIO ACHA MHESHIMIWA RAISII KABLA YA KIFO CHAKE ?.
simulizi hii imekamilika , mwandishi ataiweka hapa hivi punde
.
674
3
CH
ongoing

Shetani rudisha akili zetu
Saa saba mchana Frida alionekana akiingiza gari ndani ya hospitali na taasisi ya kitafiti ya Neuroscience inayopatikana Kibaha , kilomita kadhaa kutoka ilipo hospitali ya Tumbi.
Ilikuwa ni hospitali kubwa mno na ya kisasa yenye jengo moja lililoenda hewani kwa ghorofa kumi kumi na nane hivi na kufanya kuwa jengo refu zaidi ndani ya mkoa wote wa Pwani.
Hospitali hio ilijengwa kwa msaada wa watu wa Marekani kupitia shirika la taasisi isiokuwa ya kiserikali ifahamikayo kama Haliz Neuroscience Foundation(HNF).
Taasisi ya Haliz ilisifika dunia nzima kwa kujikita zaidi katika kuutafiti ubongo na maswala ya neva kwa ujumla wake, sera ya taasisi hio ilikuwa ni kuwezesha mataifa mengi kujifunza namna mfumo wa ubongo na neva unavyofanya kazi na hii imechangia sana kufungua matawi yake mengi karibia nchi nyingi duniani.
Mashirika ya Afya ya umoja wa kimataifa yalikuwa yakiunga mkono kazi kubwa ambayo ilikuwa ikifanywa na taasisi hii kubwa ya kimarekanni isiokuwa ya faida(Non-profit organisation).
Katika miaka ya hivi karibuni maendeleo ya sayansi ya neva na ubongo yalikuwa yamepiga hatua kubwa sana , wale wagonjwa ambao walikuwa wamepoteza kumbukumbu ilikuwa rahisi kurejeshewa kumbukummbu zao ndani ya muda mfupi tu chini ya taasisi hii ya Haliz.
Haikuwa wagonjwa waliopoteza kumbukummbu tu , watu wengi ambao walionekana kusahau mambo muhimu katika maisha yao , iwe ni kubukumbu za utotini au za ukubwani taasisi ya Haliz ilikuwa na teknolojia ya tiba ya kurahisisha hayo yote.
Licha ya taasisi hio kufanikiwa lakini bado utafiti wa kuujua ubongo wa binadamu ulikuwa ukiendelea zaidi , kwani wanasayansi wanaamini ubongo uwezo wake ni mkubwa kuliko ile ambavyo inadhaniwa , hivyo wanaamini kuuwezesha ubongo kufikia uwezo wake kamili kimatumizi italeta maendeleo makubwa.
Frida alitembea kwa kujiamini kabisa ndani ya hospitali hio huku akipokelewa na harufu ya taasisi hio yenye kuzoeleka katika pua zake, kwa namna baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hio walivyokuwa wakimsalimia kwa kutingisha vichwa ilionekana alikuwa ni mfanyakazi mwenye cheo.
Aliishia kutoa tabasamu huku akitingisha kichwa kwa kuonyesha tabasamu kwa baadhi ya watu aliopishana nao ndani na ndani ya dakika kadhaa aliweza kuzifikia lift na kuingia ndani, lakini kabla hata ya mlango wa lift haujajifunga mwanaume mzungu wa makamo alievalia koti la kimaabara aliweza kuzuia lift hio na kuingia ndani.
Alikuwa ni mtanashati kweli aliependezeshwa na miwani ya macho , huku akiwa amepambwa na tabasamu.
âWell!. Fancy meeting you here, FridaâAliongea yule mzungu na kumfanya Frida kutoa tabasamu.
âUna ajenda gani kukimbilia lift Blake, huu si muda wako wa kufanya Demostrations na wanafunzi?âAliuliza Frida na kumfana Blake kutoa kicheko kama anakohoa.
âNdio nimemaliza, kulikuwa na mabadilishano na Dr John , Vipi wewe ndio umekuja kutubariki na utaalamu wako?,nilidhani upo likizo?â
âNipo likizo ndio , lakini haimaanishi sipaswi kufika hapa , nina biashara katika floor ya kumi na sabaâ
âWow!, Wow! , Floor ya wabobevu, sina neno la kuongezea, See you FridaâAliongea Dr Blake na ni muda uleule Lift ilisimama katika floor ya kumi na bwana huyo mzungu alitoka akimuacha Frida kuendelea na safari yake.
Frida aliishia kutoa tabasamu tu huku akiangalia namna ambavyo Blake anapotelea kwenye macho yake wakati lift ikijifunga.
Haikuwa kama ambavyo amesema Frida kwani mara baada ya lift kufika katika foor ya kumi na saba alitoka katika lift na kuingia katika floor hio ambayo ilikuwa na utulivu wa hali ya juu , ilikuwa ni ubaridi tu na harufu ya kuvutia , huku rangi ya taa zisizokuwa na mwanga mkali zikipendezesha eneo hilo.
Frida hakuingia ndani ya Foor hio bali alizunguka upande wa kushoto kwake na kuanza kupandisha ngazi kuelekea juu na ndani ya dakika chache tu aliweza kutokezea juu kabisa ya jengo hilo.
Licha ya kwamba alionekana kutembea kwa haraka, lakini kwa namna ambavyo alikuwa na spidi hakuonyesha hata kuchoka, alionekana kama aina ya wanawake ambao walikuwa na mazoezi makali.
Baada ya kutoka katika paa kabisa ya jengo hilo refu na kumfanya kuona mazingira ya mji wa Kibaha na baadhi ya maeneo ya Dar es salaam na Bagamoyo alivuta pumzi na kisha aliendelea kupiga hatua kusogea mbele.
Hali ya hewa haikuwa ya jua kali ,ilikuwa ni kama vile mvua ingenyesha muda wowote.
Mbele yake Frida alikuwa amesimama mwanaume alievalia suti ya rangi ya bluu akiangalia upande wa maeneo ya Dar es salaam kwa umakini mkubwa kana kwamba kuna kitu alichokuwa akitafuta.
Alikuwa ni mzungu kwa muonekao wa nywele tu na kadri Frida ambavyo alikuwa akitembea hatua zake zilionyesha hali ya kuwa dhaifu kiasi.
Kama ilivyo mwanaume yule alivyosimama ndio namna ambavyo Frida alienda kusimama katika ukingo wa jengo hilo na kuendela kuangalia upande wa mbele yake, ilikuwa ni kama vile anamwigizia yule mtu , na upande wa yule mtu hakugeuka kabisa ni kama alijua nani amefika hapo na kusimama pembeni yake.
âAny progress on KF-Target?âAliongea yule mzungu kwa sauti nzito.
âWe are almost there, Iâve initiated a plan to bring him closer to me, his curiosity will ensure our swift entry into the next phaseâAliongea akimaanisha kwamba anakaribia kumaliza , na ameanzisha mpango wa kumuweka karibu , anasema shauku yake itawafanya waingie hatua inayofuata kwa harakaâ
âElezeaâAliongea.
âNimemfanya anifanyie Delivery ya Viungo vya akili kutoka Binamu , uhakika ni kwamba atauliza maswali juu ya malipo makubwa yanayolipwa kwa ajili ya chungu kimoja kama njia ya usafirishaji, kwa kile nilichoona amevutiwaâ
âA risky moveâ
âCalculated Risky SirâAliongea Frida kwa kingereza na jibu lake lilimridhisha.
âVipi kuhusu wale wengine , namaanisha wanaoangalia kutoka mafichoni?â
âWe are keeping eye on them , once we have what we need, they âll be nothing more than loose endsâ
âEndelea na kazi kwa umakini , hatuwezi kuruhusu kosa loloteâ
âUmeelewekaâ
âSinagogi wanataka hii misheni kumalizika kwa haraka , siku zijazo utashughulikia na zaidi ya mtu mmoja katika tafiti yako , mategemeo makubwa yamewekwa juu ya hii sayansi mpya Frida ,natumaini kila kitu kitaenda sawa,Hatuwezi kuruhusu washindani wetu kupiga hatua kabla yetuâ
âIli mradi malengo yanakuwa wazi , kila kitu kitaenda sawa , natumaini utakuwa vizuri kwenye kuwatoa wasiwasiâ
âKama ni hivyo tutaonana tena katika hatua inayofuata kujua maendeleoâAliongea yule mwanaume na ilitokea kitu kama upepo tu kwani alipotea palepale na wala hali ile isimuogofye Frida ikionyesha ni jambo ambalo amezoea.
6058
308
CH
ongoing

Masaa mawili ya kumbukumbu
Kijana Masumbuko ambae anaonekana kuwa na uwezo usiowa kawaida , uwezo wa kumfanya mtu kufanya kile anachokitaka yeye kwa kumkonyeza machoni huku akishidnwa kujua uwezo wake unatokana na nini , anaianza safari kutokea mkoani Tanga kuelekea mkoani Dar es salaam kwa ajili ya kutafuta maisha kama ilivyo kwa vijana wengi ambao wanaamini kuishi ndani ya jiji la Dar es salaam ndio njia rahisi ya kutoboa kimaisha.
Kama ilivyokuwa jina lake hakuwa na maisha mazuri wala pesa yoyote mfukoni ya kumuwezesha kufika jijini Dar es salaam, kitu pekee ambacho alikuwa nacho na kujiamini anaweza kukamilisha safari yake hio ni uwezo wake wa kumpumbaza mtu kwa kumwangalia usoni kwa kile ambacho yeye anakiita kwamba ni masaa mawili ya kumbukumbu zake.
Hatimae kwa uwezo wake huo wa ajabu anafanikiwa kula na kushiba na kupanda basi ambalo linamfikisha jijini Dar es salaam burea kabisa.
Ndani ya jiji la Dar es salaam anakutana na Peter kijana msomi wa chuo kikuu cha Dar es salaam , kutokana na namna ambavyo wamekutana wanajikuta wanakuwa marafiki wa kubwa na Peter anamxchkua Masumbuko na kwenda kuishi nae.
Peter ni mtoto wa Irene mwanadada ambae kazi yake ni uchangunduo kazi ya kuuza mwili wake kwa kufanya mapenzi na wanaume tofauti tofauti na kujipatia hela.
Irene miaka mingi nyuma akiwa katika harakati za kazi hio , anajikuta anapata mteja tajiri afahamikae kwa jina la Samir, katika hali ya kushangaza tofauti na siku zote ambazo amefanya kazi Samiri anampatia Mimba Irene.
Irene anagoma kutoa ujauzito kwa hofu ya kukosa kizazi baadae , hivyo anafanya maamuzi magumu na kulea ujauzito huo na licha ya kujua Samniri hawezi kukubali ujauzito wake anachukua maamuzi ya kijasiri na kwenda kumwambia kama amepata ujauzito wake na hawezi kuutoa kwasababu yta kuogopa kukosa mtoto baadae.
Samiri anamfukuza Irene nyumbani kwake na kumwambia hatambui ujauzito huo , lakini licha ya hivyo mke wake Samiri afahamikae kwa jina la Shani anagundua juu ya swala la Irene kubeba ujauzito wa Samiri na jambo hilo linamchukiza sana na kuogopa kwa kudhania kwamba licha ya Samiri kukataa ujauzito huo mbeleni anaweza akamtafuta mtoto wa Irene na kumrisha mali za familia.
Kutokana na hilo anaandaa mpango na kukodi mtu wa kumfatilia Irene kila siku na kumpa taarifa zake , miaka kadhaa mbele Peter anazaliwa na anafafikisha umri wa miaka saba na Shani anamtengenezea Irene ajali na anapoteza maisha.
Peter anampoteza mama yake bila ya kujua wazazi wake na maisha yanaanza upya anafauafuru vizuri kwenda kidatoi cha kwanza ana anapata ufadhili kwa kampuni ya misaada ya F and R foundation , kampuni ambayo inaongozwa na baba yake Samiri na Peter anafanikiwa kutetea ndoto zake kama ilivyo kwa watoto wengi wenye uwezo na anafdika chuo.
Siku moja akitoka kufana ununuzi wa simu katika mall za Mlimani City anajikuta kushangazwa na urembo wa binti mmoja ambae alikuwa akiingia katika maduka hayo kwa jili ya kufanya ununuzi, kitendo cha kushangaa anajikuta simu yake inakwapuiliwa na vibaka na kutokana na tukio hilo linamkiutanisha na Masumbuko ambae anamwahidi Peter anao uwezo wa kwenda kumrudishia simu yake kama tu atamslipa kiasi cha hela.
Peter anashangazwa na masumbuko lakini mwisho wa siku anakubaliana na Masumbuko kwseli anafaikiwa kumrudishia Peter simu yake
970
3
CH
ongoing