Mikasa ya ajabu nilioishuhudia kwa macho yangu
Mikasa ya ajabu nilioishuhudia kwa macho yangu

Kwanza kabisa nianze kwa kusema ninayo mikasa miwili ambayo nimewahi kuishuhudia kwa macho yangu na kuifanya kwa mikono yangu mwenyewe,mkasa wa kwanza ulituhusu mimi na ndugu zangu ambapo wakati huo nikiwa nina miaka 14 - 15 mwaka 2000 - 2001 huko mkoani Mara,wilaya ya Tarime,nchini Tanzania.
Mkasa wa pili unanihusu mimi mwenyewe pia,huu mkasa niliufanya wakati ambapo nishakuwa mtu mzima,hii ilikuwa kuanzia mwaka 2012 - 2018,mkasa huu unahusu maisha ya kitajiri yaliyohusisha nguvu za giza.
Kuna nyuzi kadhaa humu nimekuwa nikizisoma za watu mbalimbali kusimulia visa na mikasa ya maisha yao au jamaa zao ambayo waliwahi pitia. Hivyo nami nikaona sasa ni muda muafaka wa kuleta simulizi nilizo pitia maishani ili kuwafundisha na kuwaonya vijana wenzangu wote wenye tamaa ya kutafuta mali kwa njia niliyoifanya mimi waache mara moja kwani Mwisho wake unaweza kuwa kifo mikononi mwa shetani,ingawa mimi niliponea chupuchupu.

8
0

CH

ongoing
Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa
Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

Naitwa Rojaz na nimezaliwa kwa wazazi ambao baba na mama matamanio yao ni kuona watoto wao tunasoma kwa bidii ili kuweza kufikia malengo yetu na ndoto ambazo wao kama wazazi wanaziota juu yetu,natumaini ni ndoto ya kila mzazi kwa mtoto wake,hakuna mzazi anayesomesha mtoto na asitamani kuona anapata mafanikio katika masomo yake,kiufupi mimi nilikuwa ni mmoja kati ya watoto 6 katika familia yetu nikiwa ni mtoto wa tatu kuzaliwa.

Na nimejaaliwa kusoma mpaka kidato cha nne na sikufanikiwa kufanya vizuri katika matokeo yangu ya mwisho, ukiniuliza sababu ya matokeo yangu kuwa mabaya kiukweli sikuwa na jibu la moja kwa moja ila kiukweli hakukuwa na ugumu huo ila naweza kusema ni mimi mwenyewe kwa uzembe wangu na uzembe wa wanafunzi baadhi mnapokuwepo shuleni kutotambua nini kilichowaleta pale. Kuna wengine ambao wanatilia mkazo masomo yao matunda yake waliyaona na wale wakina wenzangu mie akili tunaielekeza katika michezo isiyo na tija, naeleza haya usidhani nilidharau elimu kwakuwa labda nilitokea katika familia bora, familia yetu ina uwezo wa kiuchumi la hasha kwani hata elimu yangu tokea kidato cha kwanza ni harambee ndio ilikuwa inatawala katika upatikanaji wa ada yangu, mara kachangia shangazi, mara mamdogo au mwana familia yoyote anayeonekana ana nafuu ya kipato kwa wakati huo. Kiufupi nilikulia katika familia duni.

41
2

CH

complete
IDAIWE MAITI YANGU
IDAIWE MAITI YANGU
GAVIN LUCA NDILO JINA AMBALO LIMEISHIKILIA IDAIWE MAITI YANGU. LILIKUWA NI JINA LA MWANAUME MMOJA AMBAYE ANATUSAFIRISHA MPAKA KENYA NDANI YA MSITU WA MAU AMBAKO NDIKO MAMBO YOTE YANAANZIA. MWANZONI KABISA ANAONEKANA MWANAUME HUYO AKIWA AMETEKWA NA MAKOMANDO WA JESHI LA TANZANIA. ALITESWA SANA KISHA AKAUAWA KWA KUPIGWA RISASI BAADA YA KUCHOMWA MOTO LAKINI MUDA MFUPI BAADAE LILITOKEA JAMBO LA AJABU BAADA YA ENEO HILO KUINGIA MTU MWINGINE NA KUUA MAKOMANDO WOTE AKAPONA MWANAMKE MMOJA TU WA KUITWA SARAH MARTIN. MWANAMKE HUYO ALISHANGAZWA SANA KUMUONA HUYO MWANAUME KWA SABABU NDIYE YULE AMBAYE WALITOKA KUMUUA DAKIKA CHACHE NYUMA. SASA ILIWEZEKANAJE? IDAIWE MAITI YANGU ITATUPATIA MAJIBU SAHIHI GAVIN LUCA ALIKUWA ANATAFUTWA NA MAMLAKA ZA USALAMA KWA MIAKA MINGI MPAKA ALIPOKUJA KUTOKEA HADHARANI. KUTOKEA KWAKE KULILETA MAAFA MAKUBWA NDANI YA AFRIKA YAKIWEPO YA MAUAJI YA MARAISI ZAIDI YA WAWILI. MWANAUME HUYO FAMILIA YAKE ILIKUWA NA HISTORIA YA KUTISHA NA YENYE UTATA AMBAPO ALIKUJA KUWA KIUMBE CHA AJABU SANA KWENYE DUNIA YA WATU WENYE MABAVU. GAVIN LUCA PIA ALIAMINIKA KWAMBA ALIKUWA NA NGUVU ZA AJABU NDANI YAKE AMBAZO ALIZIPATIA HUKO CHINA. NA KUONEKANA KWAKE ULIKUWA MWANZO WA UTAWALA WA FAMILIA YAKE NDANI YA AFRIKA NZIMA. SASA GAVIN LUCA NI NAN? ALITOKEA WAPI? ALIKUWA ANATAFUTWA SANA KWA SABABU ZIPI? ALIKUWA NA NGUVU ZA NAMNA GANI? KWANINI ALIONEKANA HAI WAKATI WAHUSIKA WALIMUUA? NI MWANZO KABISA WA SIMULIZI MOJA BORA SANA KUWAHI KUANDIKWA HAPA TANZANIA. TWENDE SAWA TUKAZIFUNUE KURASA ZA HUYU KIUMBE. NB USISAHAU SIMULIZI HII NI YA KUTUNGA TU, HAINA UHALISIA WA MAISHA YA MAPENZI, UJASUSI, SIASA, USALITI, UZANDIKI, WATU, MAUAJI, NGUVU ZA AJABU NA YOTE AMBAYO YAMEANDIKWA HUMO NDANI.
108
60

CH

ongoing
JUMBA JEUSI
JUMBA JEUSI
JUMBA JEUSI...... SIASA NI KAMARI....Je NANI HUIBUKA MSHINDI? JUMBA JEUSI ni andiko ambalo linaangazia siasa kwa ujumla wake.... Inaangazia namna viongozi duniani wanavyo yatumia madaraka kuhadaa watu lakini pia kufanya mambo ya kutisha... JUMBA JEUSI ni sanaa ya siasa ndani ya maandishi....utajifunza namna wananchi wanavyo danganywa na wanasiasa, namna wanasiasa wanavyo yafanya mambo ya kutisha nje ya macho ya kawaida ... Je wananchi wanapaswa kufanya nini kuhakikisha wanaikimbia hiyo hali na kuyapigania maslahi ya mataifa yao? Kumbuka tu kwenye kundi la wajinga wengi ambao wanadanganywa na wanasiasa huwa wanaibuka watu werevu, sasa watu hao huwa hawataki kwenda na ule ubaradhuli wa wanasiasa na mambo huwa yanaanza kubadilika hapo kwa sababu wanasiasa huwa hawawapendi watu wa namna hiyo..... Unahisi inakuaje kwenye mtanange wa namna hiyo baina ya watu werevu ambao wanaamua kuyatoa maisha yao kwa ajili ya kuwapigania wengi na mataifa yao? NI WAKATI SAHIHI WA WEWE KUYAPATA MAJIBU KWA KULISOMA ANDIKO HILI. KWA LEO NAKULETEA SEHEMU YAKE YA KWANZA Bux the storyteller CIAO
82
22

CH

complete
Chanzo Ni Yeye
Chanzo Ni Yeye
Simulizi ya kubuni ya kijana wa mtaani aitwaye Ayubu ambaye kwa sababu zisizojulikana anajikuta akiwa na maadui wengi bila kuwatambua....kuna chanzo cha yote tafadhali ungana na mimi mwandishi wako Machokulenga TZ
104
4

CH

ongoing
Gereza la Hazwa
Gereza la Hazwa
Mvua ilimwagika kwa nguvu, upepo mkali ukiparaganya miti na radi zikilipuka mithili ya mapigo ya ngoma ya kuzimu. Huu si msitu wa kawaida—ni Elnino, kichaka kinachomeza roho za wasiotarajia, hata mchana ukiwa na giza lisilo na mwisho. Lakini usiku huu, kivuli kilikuwa kinakimbia kwa kasi ya kutisha, miguu yake ikizama kwenye tope zito. Uso wake ulikuwa umefunikwa na nywele chafu na ndevu ndefu, macho yake yakiangaza hofu isiyoelezeka. Alikuwa akitoroka—lakini kutoka kwa nani? Nyuma yake, wanaume sita walimsakama. Wanne wamevaa mavazi ya kininja, wakipotea na kurejea kwenye giza kama manyoya yanayorushwa na upepo, huku wawili wakiwa wamevalia magwanda ya kijeshi. Hakukuwa na huruma katika macho yao, ni mauti tu. Kisu kikubwa kiliruka kwa kasi kuelekea shingo yake, kikapita kwa milimita chache tu. Punde hakuonekana tena. Mmoja wa wawinda wake alisimama, akisikiliza kwa makini—lakini upepo ulisambaza sauti kila upande, ukivuruga hisia zake. Waliashiriana kimyakimya: “Muaue.” Lakini ghafla… tone la jasho likamdondokea mmoja wao. Akakoki bastola, akaiinua juu, akifyatua bila kusita. Hakuna kilichompata mtu huyo wa kutisha, aliyejirusha kutoka juu ya mti kwa kasi isiyoelezeka. Mikono yao ilikutana kwa sekunde chache, mapambano ya mwili kwa mwili yakaanza juu ya mti. Risasi sita zilifyatuka—hakuna hata moja iliyompata. Mlio wa mifupa ukasikika. Shingo ya askari mmoja ilikatika kwa sekunde chache tu. Mwili wake ukaanguka huku damu ikimwagika kwa kasi. Mwanaume huyo mchafu hakuwa na muda wa kusherehekea ushindi. Kisu kikubwa kilikuwa kimetua mgongoni mwake, kikamdhoofisha—lakini hakuwa tayari kufa. Mbele yake kulikuwa na maporomoko makubwa yasiyo na mwisho. Nyuma yake, waninja wanne na askari mmoja wamesimama, wakitazama kwa macho baridi. Hakuhangaika kugeuka… alijirusha kwenye giza la maporomoko. "He is not human, he’s completely a devil." "But no survive, he is no more there." "Let's go and take Donald’s body." wakiamini kuwa msako wao umeisha. Lakini walikosea… Mwanaume huyu alikuwa mfungwa wa miaka 10 katika gereza ambalo hakuna aliyewahi kutoroka kwa miaka 200. Gereza ambalo hakuna mfungwa anayejua lilipo. Lakini leo, mtu mmoja yuko nje. Nani huyu? Ni kwa nini wanamtaka afe? Na je, kweli ameangamia kwenye maporomoko hayo...?
368
65

CH

complete
Mapenzi na kisasi
Mapenzi na kisasi
Simulizi inaelezea nguvu ya mapenzi na kisasi kwa mtu anayetaka kuondoa furaha yako ya mapenzi
281
6

CH

ongoing
Niliemdhania kahaba kumbe bikra
Niliemdhania kahaba kumbe bikra
Roma mbeba mizigo ndani ya soko la Mbagala Rangi Tatu anamdhania Edna Kama mwanamke anaejiuza ,baada ya mwanadada huyu kuwekewa dawa ya usingizi kwenye kinywaji na maadui zake katika ulimwengu wa Biashara akiwa ndani ya hoteli na Roma anambeba Edna na kumpeleka Geto kwake na afanya nae mapenzi. Edna kwa Mara ya kwanza analala na Roma pasipokujitambua na kupoteza usichana wake ,baada ya tukio Hilo anaamua kuolewa na Roma kwa mkataba wa Miezi sita ili kuepuka kuolewa na mwanaume asiempenda ,baada ya Roma kufunga ndoa na Edna anakuja kugundua kuwa mke wake anamiliki kampuni kubwa Nchini huku akiwa na utajiri wa kutisha. Edna anamuona Roma kama mtu asiyekuwa seriasi na maisha kutokana na aina ya mfumo wa maisha yake ,maisha ya kuwa na wanawake wengi swala linalomkasirisha Edna. Edna anajitahidi kuweka ukaribu na Roma ili kujua sababu ya mume wake macho yake kubadilika Rangi anapokuwa na hasira na kuwa ya kijani huku akiwa na roho ya ukatili mno Idara na mamlaka za kiusalama Nchini zinashangazwa na uwezo wa Roma wa kuzungumza Lugha zaidi ya ishirini na mbili na wanaanza kutafuta taarifa zinazomuhusu Roma lakini licha ya kupata taarifa inayoonyesha Roma kusomea ndani ya chuo kikubwa Duniani Cha Harvard wanakosa taarifa zingine zinazomuhusu Roma na kuishia kujiuliza Roma ni Nani haswa
443
9

CH

complete
Damiani
Damiani
Damiani mhitimu wa chuo kikuu cha uhasibu , anahitimu masomo yake na kurudi kijijini kwao kwa ajili ya kusubiria upepo wa ajira lakini katika hali ya kutokutegemea mama yake kipenzi anapigwa risasi mbili za kifuani na kufa hapo hapo na hio inatokana na kumpatia msaada mwanaume ambae hamfahamu mwenye asili ya ulaya (mzungu ) ambae na yeye alikuwa kwenye hatua ya mwisho ya kupoteza uhai wake kwani alikuwa na jeraha la risasi tumboni ,lakini mzungu huyo kabla ya kupoteza maisha anamkabidhi damiani nyaraka bila kumpa maelekezo ya aina yoyote ile . Damiani anajikuta anajenga chuki na kisasi kwa watu waliohusika na mauaji ya mama yake , anajiapiza kuwatafuta mahali popote pale na kulipiza kisasi , katika harakati za kuwatafuta wabaya wake anajikuta akifahamu siri nzito iliokuwa nyuma ya kifo cha ghafla cha raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania , anapata waraka ulioachwa na raisi huyo uliopewa jina la KAULI YA MWISHO YA RAIS KABLA YA KIFO CHAKE . JE UNAFIKIRI ATAFANIKIWA KULIPIZA KISASI CHAKE ? JE NI KAULI GANI YA MWISHO ALIO ACHA MHESHIMIWA RAISII KABLA YA KIFO CHAKE ?. simulizi hii imekamilika , mwandishi ataiweka hapa hivi punde .
354
1

CH

complete
Shetani rudisha akili zetu
Shetani rudisha akili zetu
Saa saba mchana Frida alionekana akiingiza gari ndani ya hospitali na taasisi ya kitafiti ya Neuroscience inayopatikana Kibaha , kilomita kadhaa kutoka ilipo hospitali ya Tumbi. Ilikuwa ni hospitali kubwa mno na ya kisasa yenye jengo moja lililoenda hewani kwa ghorofa kumi kumi na nane hivi na kufanya kuwa jengo refu zaidi ndani ya mkoa wote wa Pwani. Hospitali hio ilijengwa kwa msaada wa watu wa Marekani kupitia shirika la taasisi isiokuwa ya kiserikali ifahamikayo kama Haliz Neuroscience Foundation(HNF). Taasisi ya Haliz ilisifika dunia nzima kwa kujikita zaidi katika kuutafiti ubongo na maswala ya neva kwa ujumla wake, sera ya taasisi hio ilikuwa ni kuwezesha mataifa mengi kujifunza namna mfumo wa ubongo na neva unavyofanya kazi na hii imechangia sana kufungua matawi yake mengi karibia nchi nyingi duniani. Mashirika ya Afya ya umoja wa kimataifa yalikuwa yakiunga mkono kazi kubwa ambayo ilikuwa ikifanywa na taasisi hii kubwa ya kimarekanni isiokuwa ya faida(Non-profit organisation). Katika miaka ya hivi karibuni maendeleo ya sayansi ya neva na ubongo yalikuwa yamepiga hatua kubwa sana , wale wagonjwa ambao walikuwa wamepoteza kumbukumbu ilikuwa rahisi kurejeshewa kumbukummbu zao ndani ya muda mfupi tu chini ya taasisi hii ya Haliz. Haikuwa wagonjwa waliopoteza kumbukummbu tu , watu wengi ambao walionekana kusahau mambo muhimu katika maisha yao , iwe ni kubukumbu za utotini au za ukubwani taasisi ya Haliz ilikuwa na teknolojia ya tiba ya kurahisisha hayo yote. Licha ya taasisi hio kufanikiwa lakini bado utafiti wa kuujua ubongo wa binadamu ulikuwa ukiendelea zaidi , kwani wanasayansi wanaamini ubongo uwezo wake ni mkubwa kuliko ile ambavyo inadhaniwa , hivyo wanaamini kuuwezesha ubongo kufikia uwezo wake kamili kimatumizi italeta maendeleo makubwa. Frida alitembea kwa kujiamini kabisa ndani ya hospitali hio huku akipokelewa na harufu ya taasisi hio yenye kuzoeleka katika pua zake, kwa namna baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hio walivyokuwa wakimsalimia kwa kutingisha vichwa ilionekana alikuwa ni mfanyakazi mwenye cheo. Aliishia kutoa tabasamu huku akitingisha kichwa kwa kuonyesha tabasamu kwa baadhi ya watu aliopishana nao ndani na ndani ya dakika kadhaa aliweza kuzifikia lift na kuingia ndani, lakini kabla hata ya mlango wa lift haujajifunga mwanaume mzungu wa makamo alievalia koti la kimaabara aliweza kuzuia lift hio na kuingia ndani. Alikuwa ni mtanashati kweli aliependezeshwa na miwani ya macho , huku akiwa amepambwa na tabasamu. “Well!. Fancy meeting you here, Frida”Aliongea yule mzungu na kumfanya Frida kutoa tabasamu. “Una ajenda gani kukimbilia lift Blake, huu si muda wako wa kufanya Demostrations na wanafunzi?”Aliuliza Frida na kumfana Blake kutoa kicheko kama anakohoa. “Ndio nimemaliza, kulikuwa na mabadilishano na Dr John , Vipi wewe ndio umekuja kutubariki na utaalamu wako?,nilidhani upo likizo?” “Nipo likizo ndio , lakini haimaanishi sipaswi kufika hapa , nina biashara katika floor ya kumi na saba” “Wow!, Wow! , Floor ya wabobevu, sina neno la kuongezea, See you Frida”Aliongea Dr Blake na ni muda uleule Lift ilisimama katika floor ya kumi na bwana huyo mzungu alitoka akimuacha Frida kuendelea na safari yake. Frida aliishia kutoa tabasamu tu huku akiangalia namna ambavyo Blake anapotelea kwenye macho yake wakati lift ikijifunga. Haikuwa kama ambavyo amesema Frida kwani mara baada ya lift kufika katika foor ya kumi na saba alitoka katika lift na kuingia katika floor hio ambayo ilikuwa na utulivu wa hali ya juu , ilikuwa ni ubaridi tu na harufu ya kuvutia , huku rangi ya taa zisizokuwa na mwanga mkali zikipendezesha eneo hilo. Frida hakuingia ndani ya Foor hio bali alizunguka upande wa kushoto kwake na kuanza kupandisha ngazi kuelekea juu na ndani ya dakika chache tu aliweza kutokezea juu kabisa ya jengo hilo. Licha ya kwamba alionekana kutembea kwa haraka, lakini kwa namna ambavyo alikuwa na spidi hakuonyesha hata kuchoka, alionekana kama aina ya wanawake ambao walikuwa na mazoezi makali. Baada ya kutoka katika paa kabisa ya jengo hilo refu na kumfanya kuona mazingira ya mji wa Kibaha na baadhi ya maeneo ya Dar es salaam na Bagamoyo alivuta pumzi na kisha aliendelea kupiga hatua kusogea mbele. Hali ya hewa haikuwa ya jua kali ,ilikuwa ni kama vile mvua ingenyesha muda wowote. Mbele yake Frida alikuwa amesimama mwanaume alievalia suti ya rangi ya bluu akiangalia upande wa maeneo ya Dar es salaam kwa umakini mkubwa kana kwamba kuna kitu alichokuwa akitafuta. Alikuwa ni mzungu kwa muonekao wa nywele tu na kadri Frida ambavyo alikuwa akitembea hatua zake zilionyesha hali ya kuwa dhaifu kiasi. Kama ilivyo mwanaume yule alivyosimama ndio namna ambavyo Frida alienda kusimama katika ukingo wa jengo hilo na kuendela kuangalia upande wa mbele yake, ilikuwa ni kama vile anamwigizia yule mtu , na upande wa yule mtu hakugeuka kabisa ni kama alijua nani amefika hapo na kusimama pembeni yake. “Any progress on KF-Target?”Aliongea yule mzungu kwa sauti nzito. “We are almost there, I’ve initiated a plan to bring him closer to me, his curiosity will ensure our swift entry into the next phase”Aliongea akimaanisha kwamba anakaribia kumaliza , na ameanzisha mpango wa kumuweka karibu , anasema shauku yake itawafanya waingie hatua inayofuata kwa haraka” “Elezea”Aliongea. “Nimemfanya anifanyie Delivery ya Viungo vya akili kutoka Binamu , uhakika ni kwamba atauliza maswali juu ya malipo makubwa yanayolipwa kwa ajili ya chungu kimoja kama njia ya usafirishaji, kwa kile nilichoona amevutiwa” “A risky move” “Calculated Risky Sir”Aliongea Frida kwa kingereza na jibu lake lilimridhisha. “Vipi kuhusu wale wengine , namaanisha wanaoangalia kutoka mafichoni?” “We are keeping eye on them , once we have what we need, they ‘ll be nothing more than loose ends” “Endelea na kazi kwa umakini , hatuwezi kuruhusu kosa lolote” “Umeeleweka” “Sinagogi wanataka hii misheni kumalizika kwa haraka , siku zijazo utashughulikia na zaidi ya mtu mmoja katika tafiti yako , mategemeo makubwa yamewekwa juu ya hii sayansi mpya Frida ,natumaini kila kitu kitaenda sawa,Hatuwezi kuruhusu washindani wetu kupiga hatua kabla yetu” “Ili mradi malengo yanakuwa wazi , kila kitu kitaenda sawa , natumaini utakuwa vizuri kwenye kuwatoa wasiwasi” “Kama ni hivyo tutaonana tena katika hatua inayofuata kujua maendeleo”Aliongea yule mwanaume na ilitokea kitu kama upepo tu kwani alipotea palepale na wala hali ile isimuogofye Frida ikionyesha ni jambo ambalo amezoea.
2931
272

CH

ongoing
Masaa mawili ya kumbukumbu
Masaa mawili ya kumbukumbu
Kijana Masumbuko ambae anaonekana kuwa na uwezo usiowa kawaida , uwezo wa kumfanya mtu kufanya kile anachokitaka yeye kwa kumkonyeza machoni huku akishidnwa kujua uwezo wake unatokana na nini , anaianza safari kutokea mkoani Tanga kuelekea mkoani Dar es salaam kwa ajili ya kutafuta maisha kama ilivyo kwa vijana wengi ambao wanaamini kuishi ndani ya jiji la Dar es salaam ndio njia rahisi ya kutoboa kimaisha. Kama ilivyokuwa jina lake hakuwa na maisha mazuri wala pesa yoyote mfukoni ya kumuwezesha kufika jijini Dar es salaam, kitu pekee ambacho alikuwa nacho na kujiamini anaweza kukamilisha safari yake hio ni uwezo wake wa kumpumbaza mtu kwa kumwangalia usoni kwa kile ambacho yeye anakiita kwamba ni masaa mawili ya kumbukumbu zake. Hatimae kwa uwezo wake huo wa ajabu anafanikiwa kula na kushiba na kupanda basi ambalo linamfikisha jijini Dar es salaam burea kabisa. Ndani ya jiji la Dar es salaam anakutana na Peter kijana msomi wa chuo kikuu cha Dar es salaam , kutokana na namna ambavyo wamekutana wanajikuta wanakuwa marafiki wa kubwa na Peter anamxchkua Masumbuko na kwenda kuishi nae. Peter ni mtoto wa Irene mwanadada ambae kazi yake ni uchangunduo kazi ya kuuza mwili wake kwa kufanya mapenzi na wanaume tofauti tofauti na kujipatia hela. Irene miaka mingi nyuma akiwa katika harakati za kazi hio , anajikuta anapata mteja tajiri afahamikae kwa jina la Samir, katika hali ya kushangaza tofauti na siku zote ambazo amefanya kazi Samiri anampatia Mimba Irene. Irene anagoma kutoa ujauzito kwa hofu ya kukosa kizazi baadae , hivyo anafanya maamuzi magumu na kulea ujauzito huo na licha ya kujua Samniri hawezi kukubali ujauzito wake anachukua maamuzi ya kijasiri na kwenda kumwambia kama amepata ujauzito wake na hawezi kuutoa kwasababu yta kuogopa kukosa mtoto baadae. Samiri anamfukuza Irene nyumbani kwake na kumwambia hatambui ujauzito huo , lakini licha ya hivyo mke wake Samiri afahamikae kwa jina la Shani anagundua juu ya swala la Irene kubeba ujauzito wa Samiri na jambo hilo linamchukiza sana na kuogopa kwa kudhania kwamba licha ya Samiri kukataa ujauzito huo mbeleni anaweza akamtafuta mtoto wa Irene na kumrisha mali za familia. Kutokana na hilo anaandaa mpango na kukodi mtu wa kumfatilia Irene kila siku na kumpa taarifa zake , miaka kadhaa mbele Peter anazaliwa na anafafikisha umri wa miaka saba na Shani anamtengenezea Irene ajali na anapoteza maisha. Peter anampoteza mama yake bila ya kujua wazazi wake na maisha yanaanza upya anafauafuru vizuri kwenda kidatoi cha kwanza ana anapata ufadhili kwa kampuni ya misaada ya F and R foundation , kampuni ambayo inaongozwa na baba yake Samiri na Peter anafanikiwa kutetea ndoto zake kama ilivyo kwa watoto wengi wenye uwezo na anafdika chuo. Siku moja akitoka kufana ununuzi wa simu katika mall za Mlimani City anajikuta kushangazwa na urembo wa binti mmoja ambae alikuwa akiingia katika maduka hayo kwa jili ya kufanya ununuzi, kitendo cha kushangaa anajikuta simu yake inakwapuiliwa na vibaka na kutokana na tukio hilo linamkiutanisha na Masumbuko ambae anamwahidi Peter anao uwezo wa kwenda kumrudishia simu yake kama tu atamslipa kiasi cha hela. Peter anashangazwa na masumbuko lakini mwisho wa siku anakubaliana na Masumbuko kwseli anafaikiwa kumrudishia Peter simu yake
484
3

CH

ongoing