Lengley,Virginia CIA HQ, 2021 FEBRUARY 0800Am
Ilianza kama siku tulivu ndani ya makao makuu haya , ambayo yalikuwa na pilika pilika za kiusalama, kwani kila mfanyakazi alionekana kuwa bize kuhakikisha kila mtu anatimiza majukumu yake , kama ilivyokuwa moja ya falsafa kwa wazungu “muda ni mali” basi kwa pilika pilika hizo waliendana na falsafa yao hio .
Basi asubuhi hio ndani ya ofisi ya DCI`s(Director of the Intelligence Agency) alionekana bwana George crispian mkuu wa kitengo cha Directorate of science and Technology akiwa ameambatana na Jane Smith mkuu wa kiitengo cha Directorate of Intelligence , wote asubuhi hio walionekana kuwa na jambo la muhimu la kuripoti kwa mkuu huyo wa CIA bwana Luis Tenet .
Jambo walilokuwa wanazungumzia asubuhi hio ilikuwa ni juu ya misheni iliopewa jina la Dragon X Trail , misheni ambayo ilikuwa ikienda kufanyika nchini Tanzania.
Mbele ya meza hio kubwa iliokuwa imezungukwa na watu wa tatu juu yake kulikuwa na fomu ama bahasha tatu ambapo kila bahasha ilikuwa na taarifa iliokuwa jumuishi juu ya misheni Dragon X ,bahasha namba moja ilikuwa na taarifa kutoka NSA , fomu hii au bahasha ilikuwa imebeba taarifa ya picha , hapa nazungumzia picha kama picha , na picha hizo zilikuwa zikizionyesha ubongo wa binadamu , lakini pia zilikuwa zikionyesha pia Screenshot ya jumbe za meseji kupitia mtandao wa Watsapp , jumbe hizo zilikuwa zikitoka kwa Profesa au daktari ndani ya hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwenda kwa mkuu (CEO) wa kampuni ya kitehama ifahamikayo kwa jina la EARTH TECH INC , kampuni iliokuwa na makazi yake ndani ya Taifa la Tanzania mkoani Arusha ..
Fomju ya pili ambayo hii sasa haikutoka NSA bali ilikuwa imetoka ndani ya CIA na ilikuwa imewasilishwa kwa DCI na mkuu wa kitengo cha Directorate of intelligence yaani Bi Jane Smith , Fomu hii ilikuwa imejaa nyaraka zenye taarifa kutoka kwa Undercover Agent(wakala) kutoka Tanzania(jina halikutajwa).
Fomu ya tatu hii ilikuwa ipo kwenye meza ya mkuu wa CIA ndani ya fomu hii juu kabisa ya ukurasa wa kwanza kulikuwa na maandishi ya DRAGON X TRAIL MISSION APPROVAL ikiambatana na neno Confidential , fomu hii ilikuwa imetoka kwa Raisi wa USA kupitia ofisi ya DNI kwenda kwa CIA.
Sasa basi ndani ya ofisi watu hao walionekana kujadili jambo , lakini baada ya kama nusu saa hivi , waliongezeka watu wawili watu hawa walikuwa ni wakuu wa vitengo viwili yaanni Directorate of support pamoja na ile ndogo kabisa ya Directorate of clandestine .
Walikuwa wote ni wanaume na baada ya kuungana , walionekana kuwa katika kikao na mwisho wa kikao walionekana walikuwa wakijadili mtu ambae anakwenda kuiongoza misheni hio ya DRAGON X TRAIL.
Lakini kati ya wale watu wawili walioingia ndani ya ofisi hio kwa kuchelewa mmoja alionekana kutoa faili na juu ya hilo faili likuwa na nembo kubwa ya alama ya UMOJA NAMBA TISINI NA SABA yaani U-97 na faili hilo lenyewe likiambatana na neno CONFIDENTIAL
Hii misheni ni nini haswa , kwanini ifanyiwe ndani ya Taifa laTanzania , jibu la jambo hilo linakuja kupitia tukio ambalo ndani ya Taifa lilionekana ni tukio la kawaida kabisa kutokea katika jamiii , lakini kumbe ni jambo ambalo lilikuwa limebeba athari kubwa kwa jamii ..
Tukio hilo linakwenda kwa jina la MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU ni tukio la kusisimua lililotengeneza sababu ya kuundwa kwa misheni iliofahamika kwa jina la DRAGON X TRAIL.
Lakini ni tukio ambalo lilipelekea kufichuka kwa siri kuu ya UMOJA NAMBA
TISINI NA SABA siri ya kitabu cha BOOK OF ALL NAMES
Huo ni utangulizi wa kitabu changu kinacho enda kwa jina la MASAA
MAWILI YA KUMBUKUMBU
Sasa kwa wewe ambae ushakwisha kusoma UMOJA NAMBA TISINI NA SABA (waraka wa raisi kabla ya kifo ) basi nakuomba usome na tukio
lililotokea katika kitabu cha MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU ili
upate maana halisi ya ya code name U-97 je ni nini maana halisi ya hilo neno , je kuna umoja huo kwenye jamii au duniani kwa ujumla wake basi usisite kusoma.
Mambo makuu mawili utakayo yapata kuyajua katika kitabu hiki ni pamoja na jinsi gani mashirika makubwa ya kimitandao yanavyokagua mawasiliano ya wateja wao wote dunia nzima .
Utapata kujua nini nini kiligunduliwa katika BLUE BOOK project, pia utakuja kugudnua namna projekti hio ilivyo changia uundwaji wa project ya TOP ON FILE project iliokuwa ipo chini ya STAR LABS pamoja na IBM .
Je unataka kujua ni nini kilichonyuma ya DRAGON X TRAIL MISSION hakikisha haukosi kusoma .
Hii simulizi imerudi rasmi na itakuwa inaendelea hapa kila siku kipande kimoja mpaka mwisho
Comments