Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

FOR YOU

Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

 SEHEMU YA KWANZA

★★★★★★★★★★★★★


"Kulikuwa na demu mmoja aliyekuwa anasumbua kitaa fulani hivi, yaani kwa uzuri, shepu na maringo hakukamatika. Alikuwa wa kishua, mdingi wake alikuwa hataki aguswe na yeyote yule. Nyumba yao ilikuwa na ghorofa tatu; ya chini alikaa mshua wake, ya pili maza wa demu, af' ya tatu ndo' dodo alikuwa anakaa, yaani yale maisha ya usiniguse, usinitachi, salamu iwe kwa miguu. Basi wasela nini kitaa wakawa wanajikuta wanaweka mipango eti kumnasa, lakini hamna yeyote aliyefanikiwa. Ndo jamaa mmoja akajitoa akili na kuwaambia ndani ya siku 7 tu angekuwa ashakula huyo demu..."

"Ahahahah... enhe..." akasema Ramla.

"Wakambishia na kumwambia hangeweza na kwamba anajidanganya tu, kwo' mshkaji akasema angerekodi na video kabisa awaonyeshe. Basi siku iliyofuata jamaa akajipeleka kwa ile nyumba na kuomba kazi kama house boy... akaongea maneno mazuri mpaka mshua yule akamkubali. Alipomuuliza jina, jamaa akasema 'mimi kwa jina naitwa b(..).' Dah! Mshua akacheka sana na kumwambia apande juu ili aongee na mke wake. Alipofika kwa maza, akamwambia 'mimi kwa jina naitwa k(...). Huyo maza akacheka kifala na kumwambia apande juu kwa binti kisura ili akajitambulishe na huko..."

"Dah! Na wenyewe wanakubali majina ya matusi kabisa, si muhuni huyo! Hapo msela kashaweza mishe, an atateleza kiulainiii..." akasema Mecky.

"Tulia sasa story bado haijaisha..."

"Eti! Yaani Mecky naye! Em' endelea Xander..." akasema Ramla.

"Alipofika kwa mtoto akakubali sana maana kweli demu alivutia. Lakini alikuwa na nyodo nyingi mno. Alipouliza jina lake, jamaa akasema anaitwa 'kiazi na mchuzi.' Mtoto akafurahia sana na kuanza kuongea naye zaidi, na hapo ndo' akaona jamaa alikuwa mcheshi. Akaongea kwa sauti ya juu kuwaambia wazazi wake wamuajiri maana alimpenda. Basi siku mbili tatu jamaa akaendelea kazi. Alionyesha kujituma kinoma, lengo lake akiwa hajasahau lakini..."

"Enhe..." akasema Ramla.

"Ndo' siku ya siku akaandaa msosi ili kumpelekea demu. Sikuzote kabla ya kupeleka chakula juu ilikuwa lazima kipite kwa maza kwanza, kwo' alipokiangalia akashangaa kidogo. Jamaa alikuwa ametengeneza kiazi na mchuzi wa nyama, na mazeli alijua binti yake asingekula. Lakini jamaa akasisitiza akisema atavipenda, kwo' akamwachia ampelekee. Alipofika chumbani kwa mrembo, akaviweka pembeni af' akamfata kitandani pale alikuwa amejilaza huku ana-chat. Akapanda juu yake af' akaanza kumtekenya. Demu akaanza 'kiazi na mchuzi me sitaki buana... kiazi na mchuzi sitakiii.' Sa' si maza'ake akasikia, akapayuka, 'kama hutaki kiazi na mchuzi mpe K(...) ale!"

Marafiki wa kijana huyu waliokuwa wanamsikiliza wakacheka sana.

"Dah! Jamaa akamwambia mtoto, 'umesikia mama alichosema? Unipe nini nile?' Mh! Mtoto akatulia kwanza, af' akamuuliza maza'ake kwa sauti 'nimpe nini...?' Maza akajibu, 'mpe K(...) ale!' Msela akaanza kushughulika fasta! Ilibidi demu atulie tu... jamaa akapiga show ya kibabe huku anachukua mkanda mzima..."

"Ahahah... ahahahah... hizo fujo zote wazazi wake hawakuzisikia?" Ramla akauliza.

"Mama'ake alikuwa anasikia binti yake anasema, 'kiazi na mchuzi, tamu! Tamu jamani!' Akasema kwa sauti na yeye, 'sasa ulikuwa unalalamika nini kama ni vitamu?' Bila kujua mtoto wake analiwa!"

Wote wakacheka.

"Kwo' ikawaje?" akauliza Benjamin.

"Si ndo' maza'ake akaanza kuhisi kama na miguno inatoka huko juu. Ajabu! Akapanda kwenda kuona utamu wa hivyo viazi na mchuzi, kukuta mtoto wake anabenjuliwa kiaina..."

"Jamani... endelea..." akasema Ramla.

"Huyo maza akapiga kelele eti 'pervert! pervert!' jamaa akasanuka fasta na kuvaa bukta yake, af' alivyo mkuda akamgonga denda ya kumuaga mtoto... hapo dodo limeshalegea kinyama! Akatoka nduki mpaka kule chini, ma-bodyguard wakawa wanamkimbiza. Sa' si mzee akawa anawaambia 'kamateni b(..)! kamateni b(..)!' wakashindwa kuelewa wafanye nini, kwa hiyo wakasimama na kuyashika madude yao eti! Aheheheh... ai kudadeki!"

Marafiki wa kijana huyu walimpenda sana kwa kuwa alikuwa na vituko kupita maelezo. Wote walicheka sana baada ya yeye kuwa amewasimulia hadithi hii ya kubuni, na kuanza kuizungumzia utafikiri kilikuwa kisa cha kweli. Kijana huyu aliitwa Alexander, au kama wengi walivyomfahamu na kumwita, Xander. Hapa alikuwa chuoni, pamoja na rafiki zake watatu aliopenda kuwa nao mara nyingi, yaani Mecky, Benjamin, na binti mrembo aliyeitwa Ramla, ijapokuwa alikuwa na marafiki wengi. Ramla pia alikuwa na uhusiano wa kimapenzi pamoja na Xander.

Pamoja na ujanja wake mwingi hasa kwenye maneno lakini Xander alikuwa kijana mwerevu sana. Alifahamika kuwa mchezaji mahiri wa timu kuu ya mpira wa miguu ya chuo hiki walichosomea kwa kuwa tegemeo la ufungaji, naye alikuwa na umri wa miaka 21 tu. Pamoja na umri wake kuwa mdogo lakini kimwili alikuwa ngangali haswa, na sura yake ilikuwa nzuri pia na kufanya Ramla awe mwenye ushindani na wasichana wengine chuoni walioitaka nafasi yake; na ndiyo sababu aliringa sana.

Hapa alikuwa na rafiki zake hao baada ya kutoka kwenye kipindi cha somo fulani na kuketi nao sehemu ya nje ya uzio wa jengo la chuo hiki, wakifurahia maongezi ya hapa na pale. Walikuwa wamekaa chini ya mti mfupi wenye kivuli, uliozungukwa na nyasi zilizokatwa vizuri chini na kufanya eneo hilo lipendeze; kukiwa na baadhi ya wanachuo sehemu za pembeni pia. Xander alikuwa amelalia mgongo wake huku kichwa chake akikilaza kwenye mapaja ya Ramla, kama wapendanao wafanyavyo.

"Uliitolea wapi hiyo story?" Benjamin akamuuliza Xander.

"Alinisimuliaga mshkaji wangu mmoja hivi anaitwa Ishmael... nimemkumbuka sana..." Xander akajibu.

"Wa wapi?" akauliza Ramla.

"Kigoma. Nilikutanaga naye sekondari Mwanza, alikuwa poa sana..."

"Eeh afu' nyie mmesikia kuhusu lile kundi la majambazi, sijui majambazi, waliovamia ile shule ya kule Kigoma?" akauliza Benjamin.

"Eeh Ujiji. Nimeona kwenye habari eti wanajikuta magaidi na wenyewe wanajiita Demba Group sijui... Lakini hamna hata mmoja aliyekamatwa na waliwaumiza walimu na wanafunzi wengi," akasema Ramla.

"Mafala tu hao. Siku mbili utasikia wameshakamatwa wote... sijui huwa wanajipelekaga kwa mapolisi?" akasema Xander.

"Ahahah... ni shida," akasema Ramla.

"Dah! Communication sasa hivi, tuwahi class maana patajaa sitaki kuhangaika kutafuta viti," akasema Mecky huku ananyanyuka.

Wote wakanyanyuka na kuanza kuelekea ndani ili kuwahi kipindi. Xander sikuzote alivalia kwa njia yenye mpangilio mzuri sana; yaani ni kama alitaka kujionyesha lakini kihalisi haikuwa hivyo. Alitupia pamba kali mara nyingi na alinukia vizuri sana. Nywele zake alizitengeneza kwa mtindo wa kiduku, nazo zilikuwa laini zenye kuviringika kutokana na yeye kuwa na asili ya uarabu fulani hivi; ijapokuwa hakuonekana hivyo usoni. Yaani alikuwa mwenye sura na ngozi nyeupe, lakini haikupita kiasi sana kama wazungu, na macho yake hayakuwa makubwa.

Ramla alikuwa msichana kutokea Tanga, mwenye miaka 22, naye alikuwa na asili ya uarabu pia (shombe shombe) ijapokuwa hakuwa mweupe sana. Alikuwa mfupi kiasi kumfikia Xander begani, na alibeba hips nene kiasi zilizotokeza kalio lake kwa nyuma vizuri. Alijivunia mwonekano wake, na hasa kuwa mtu wa Xander pia. Mara nyingi alipokuwa naye alipenda kutembea karibu yake au akiwa amemshika mikono, ili kuonyesha wadada wengine kwamba chake kilikuwa chake hivyo wachote vyao kwingine.


★★★


"Kwa hiyo Sandra una mpango gani?"

"Kuhusu?"

"Kuhusu Danny..."

"Sophia... mimi na Danny hatuendani. Sijui nikwambie mara ngapi uelewe..."

"Mpe nafasi tu jamani... mimi sioni ikiwa wewe na Raymond mko vizuri. Kwanza anakuzingua-zingua tu, mara yupo, mara hayupo... kwa nini usiangalie mtu anayeku-feel kama Danny, eh? Mzuri, ana hela..."

"Best, kama hela ingekuwa inanunua kila kitu basi trust me... ningekuwa na mabwana kumi na tano sasa hivi!"

"Sijamaanisha kwamba anataka kukununua. Danny anakupenda sana Sandra... yaani huwa ananieleza jinsi anavyoumia sana kutoweza kuwa nawe. Kwa nini umemng'ang'ania tu Raymond wakati hana hata...."

"Nini? Pesa? Ndiyo unachojali tu hicho maishani mwako Sophie?"

"Sasa siku hizi baby bila pesa unafikiri itakuwaje? Unataka wewe ndo' uje uwe unamlisha?"

"Ahahah... sikia. Mimi siangalii pesa. Kama pesa ninayo, kwa hiyo naangalia vitu zaidi ya pesa. Danny simjui vizuri, lakini ninaweza tu kukisia anachokitaka kutoka kwangu kama ilivyo kwa wasichana wengine. Na kiukweli Sophia mimi sipendi anavyokutumia wewe rafiki yangu kuniandama namna hii. Nilishamkataa. Naomba umwambie aelewe hilo... na aliheshimu. Vinginevyo, atakuwa anatafuta matatizo."

"Utafanyaje... utamwambia baba'ako?"

"Ahahahah... sikufikiria hilo ila ikifikia hatua hiyo atajuta..."

"Mh... haya bwana. Kaka wa watu anaumia sana... Fikiria tena maana siku hizi huwezi kujua mara paap majambazi wakaja kukuteka halafu yeye ndo' akakuokoa!"

"Ahahaaa... kama Demba Group? Ajibebe tu kwa kweli, me hapana... Twende tuwahi class ni Communication sa'hivi..."

Haya yalikuwa ni maongezi baina ya marafiki wa karibu sana; Sophia, na Alexandra. Ni ndani ya chuo hiki hiki, na hapa wawili hawa walikuwa wakijiandaa kuelekea kwenye kipindi cha somo la Communication walipoanza kuongelea mambo hayo. Sophia alikuwa akijaribu kwa siku kadhaa sasa kumshawishi Alexandra amkubali mwanaume fulani aliyeitwa Daniel, ambaye alikuwa ndiye mkuu ndani ya chuo hiki (principal). Pamoja na kwamba Sophia alikuwa mwenye uvutano wenye nguvu sana kwa Alexandra, lilipokuja kwenye suala hilo, binti alikataa katakata kuafikiana nalo.

Alexandra alikuwa binti mrembo sana. Chuoni hapo alikuwa anafahamika kama Waziri wa Afya, kwa sababu ya cheo chake kwenye masuala ya kuongoza na kushughulika na mambo yaliyohusiana na afya za wanachuo. Hii ilikuwa kawaida kwa wanachuo fulani pekee kupewa vyeo vya uongozi wa masuala mbalimbali kwenye chuo hiki, kukiwa na raisi, makamu wake, mawaziri mbalimbali, na wengine kwenye vitengo tofauti. Yaani mambo yaliendeshwa kwa njia fulani rasmi kama ilivyo serikalini. Lakini pia Alexandra na Sophia walikuwa kwenye timu ya mchezo wa kuogelea ya chuo hiki, na hilo lilifanya wajulikane na wengi hasa kwa kuwa wote walikuwa wenye ustadi sana kwenye mchezo huu.

Principal Daniel alikuwa amejaribu kumfanya Alexandra awe ndiyo raisi wa wanachuo eti ili awe juu. Lakini binti alielewa hiyo ilikuwa ni moja ya njia za kutaka kumlaghai ili awe pamoja naye kwa sababu kuna vifaida ambavyo angepata kutokana na cheo hicho. Alichaguliwa kuwa Waziri wa Afya na wanachuo wengine walioona anastahili hilo, na hiyo kwake ilitosha; hakutaka kupewa vitu ili naye arudishe vitu fulani vya faida kwa yeyote.

Alexandra alikuwa msichana mwenye miaka 21. Alikuwa mweupe sana, mwenye sura yenye kuvutia iliyomfanya aonekane kama mwanamitindo, mrefu kiasi, na mwenye umbo la wastani; siyo mwembamba, siyo mnene. Hips zake zilijichora vyema lakini hakuwa na kalio kubwa mno; la wastani lililotokeza kwa kadiri kwa kuwa alikuwa mtu wa mazoezi pia. Nywele zake nyeusi na laini zilikuwa ndefu kufikia mabegani, naye alipendelea sana kuvaa suruali za jeans zilizochanikia magotini na hata mapajani kiasi. Alikuwa binti mwerevu na aliyependa sana masomo yake.

Alexandra alikuwa na mpenzi wake aliyeitwa Raymond, ambaye alikuwa kijana mstaarabu aliyefahamiana naye tokea sekondari. Walikuwa marafiki tu zamani, lakini walipokuja kukutana tena chuoni hapo walianzisha uhusiano. Alimpenda kwa sababu alikuwa kijana mpole asiye na makuu kabisa. Lakini ni watu wachache mno waliojua kuhusu uhusiano wao kwa sababu hawakujionyesha kwa watu.

Raymond alimpenda sana Alexandra pia, naye ijapokuwa aliishi maisha ya familia isiyokuwa na uwezo mkubwa kifedha lakini alinwonyesha binti huyu upendo kwa njia zozote zile alizoweza hata kama kwa wengine ingeonekana ni kidogo. Mama yake alikuwa kwenye mkoa mwingine toka yeye alipofika kwenye huu ili kuanza chuo. Alikuwa na ndugu wengi wa kiukoo ambao hawakumjali sana mama yake wala yeye, hivyo walisaidizana tu kutegemezana kimaisha huku akiendelea kusoma. Naye pia alisoma kwa bidii.

Kufikia hapa ni rahisi kukisia kuwa hadithi hii inawahusu hasa vijana hawa wawili; Alexander, na Alexandra.

Alexander ni Alexandra, na Alexandra ni Alexander. Vijana hawa ni mapacha, na ijapokuwa ni mapacha wa jinsia tofauti, wanafanana sana. Wote wanachukua kozi za masomo yanayohusiana na Tehama (technology), nao wanapenda sana kozi hii na kutazamia kuja kufanya kazi zinazohusiana nayo. Huu ni mwaka wao wa tatu wakiwa kwenye chuo hiki tokea walipojiunga nacho wakiwa na miaka 19. Wamebakiza mwaka mmoja kumaliza diploma, na wanatazamia kuendelea mbele zaidi hata kufikia masters; ijapokuwa hilo ni jambo ambalo ni wazazi wao ndiyo wamewapangia.

Alexandra ni mtaratibu sana, mwelewa, na mwenye msimamo imara. Kwa wengi anafahamika kama Sandra. Yeye hufanya mambo mengi kwa kutumia busara, na ndiyo sababu akapewa cheo cha Waziri wa Afya hasa kutokana na kiwango chake cha juu cha usafi. Lakini Alexander ni mwongeaji, jasiri, na mtukutu kupita kiasi. Anapendwa hasa kwa sababu sikuzote ana njia fulani kwenye maneno inayowapendeza wengi. Pamoja na ujanja wake lakini anampenda sana dada yake. Yaani kwa mambo mengi anaweza kutenda kijeuri na kwa kuongozwa na hisia badala ya hekima, lakini inapokuja kwenye suala la dada yake sikuzote huwa anaonyesha kumjali sana.

★★

Wote wakawa wameingia kwenye darasa moja pamoja na wanachuo wengine, wakimsubiria mwalimu wa somo la Communication Skills. Wanachuo wa kozi mbalimbali husoma somo hilo pia, hivyo mara nyingi darasa hujaa sana. Alexander kama kawaida aliketi upande walioketi wanaume zaidi, naye Alexandra upande waliojaa wasichana. Baada ya mwalimu kuingia, utulivu ukaanza kutawala maana walikuwa wakipiga makelele mno.

Sikuzote mwalimu huyu alipoingia, ukimya ulitawala haraka hasa kwa sababu alipendwa na kuheshimiwa na wengi. Jina lake lilikuwa ni Valentina, na wengi walizoea kumwita madam V. Alikuwa mwanamke anayevutia, mwenye urefu wa wastani. Alipenda kusuka nywele ndefu za rasta na mitindo mingine tofauti-tofauti. Leo alikuwa amesuka mtindo wa nywele nyingi zilizokuwa kama mawimbi-mawimbi na kuziachia zimwagikie mpaka mabegani. Hakuwa mweusi tii, bali kama watu wanavyosema, rangi ya maji ya kunde. Mwili wake ulikuwa mwembamba kiasi lakini kutokea kwenye kiuno chake chembamba kufikia mapajani alikuwa amenawiri vyema kuwaonyesha wengine kwamba 'hips' zake zilinona kwa kadiri fulani. Siku hii alikuwa amevalia T-shirt nyeusi yenye mikono mifupi iliyobana, na sketi ya rangi ya maziwa (cream) iliyobana pia na kuishia magotini mwake.

Umbo lake pia lilichangiwa na yeye kuwa mtu wa mazoezi. Alifundisha somo hili, lakini pia alikuwa ndiye kama mwalimu na kocha wa timu ile ya kuogelea ya wasichana ambayo Alexandra na Sophia walishiriki pia. Ijapokuwa alikuwa mkubwa kiumri, bado mwonekano wake ulimfanya awe kama binti mdogo. Alikuwa mstaarabu sana pia, na maisha yake ya ndani sikuzote hakuwa na kawaida ya kuyaweka wazi kwa yeyote; isipokuwa labda iwe ni kwa mtu aliyemwamini sana. Kwa hiyo wengi hawakuwa wanafahamu maisha yake binafsi yalikuwa vipi.

Siku hii alikuwa akifundisha kuhusu jinsi mawasiliano yanavyoweza kutumika vizuri sehemu kadha wa kadha. Alikuwa akiwaelezea wanafunzi wake kuwa ili waweze kuboresha njia za kuwasiliana vizuri na watu wa maeneo na hali mbalimbali, wanahitaji kujua jinsi ya kujielezea vizuri kuanzia kwenye maongezi mpaka kwenye uandishi. Akaandika pointi kadhaa kwa ufupi huku akizielezea, kisha akaomba waulize maswali kuhusiana na mada hii. Wengi, hasa wanaume vijana humo, walipenda sana kumuuliza maswali kwa kuwa angewapa majibu kwa njia nzuri sana, na pia ili wamfanye aendelee tu kuwepo darasani kwa muda mrefu zaidi.

"...na ijapokuwa mawasiliano ya namna hii wakati mwingine yanaweza kuwa yenye challenge, hasa ikitegemea na sehemu tuseme labda... kwenye vyumba vya wagonjwa, njia ya therapy ya kuwasiliana nao ndiyo inakuwa yenye faida zaidi kwao, na hata kwa familia zao pia..." akaendelea kuelezea.

"Kwa hiyo kumbe njia hiyo hata ICU inaweza kutumika?" akauliza mwanachuo mmoja.

"Ndiyo, tena hasa wagonjwa wa ICU. Kwenye vyumba vya ICU kwa mfano, communication ambayo itategemea huruma ya kutoka moyoni na... experience nzuri ya muuguzi, au mtu wa karibu na mgonjwa, ni jambo la muhimu linalowasaidia sana wagonjwa waweze hata kuona mambo wanayopitia kwa njia positive, badala ya kupoteza matumaini kabisa..." akaeleza madam Valentina.

"Dah, mwanangu huyu ticha anaongeaga vizuri! Yaani kila neno analotamka ni maua tu..." Mecky akamsemesha Xander kwa sauti ya chini.

Xander akatikisa kichwa na kutazama simu yake. Alikuwa ametumiwa ujumbe na Ramla kuwa baadae amtoe "lunch."

"Kuna swali lingine?" madam Valentina akauliza.

Ilionekana hakukuwa mtu mwingine aliyetaka kuuliza swali, na kwa kuwa Mecky hakutaka madam aondoke haraka, akaona tu aulize chochote.

"Okay, kuna kazi hapa nataka... ndiyo una swali?" madam Valentina akasitisha alichokuwa anataka kusema baada ya kumwona Mecky amenyoosha mkono.

"Aaaa... eti kirefu cha ICU ni nini?" Mecky akauliza.

Minong'ono ikaanza kusikika hapo. Watu walikuwa wanajiuliza alikuwa anafikiria nini kuuliza swali hilo.

Valentina akatabasamu kwa mbali, kisha akasema, "Msaidieni. Eti kirefu cha ICU ni nini?"

"Ingia Chumbani Ufe!" Xander akajibu kiutani bila kutazama mbele.

Wanachuo wenzake wakacheka kwa sauti sana, hasa wasichana.

"Ni Intensive Care Unit bwana," akasema Sandra.

"Eeeh? Waziri wa Afya huyo!" Xander akamwambia dada yake na kumwonyesha ishara ya vidole kumpiga kwa bastola.

"Asante. Alexander, ulipojibu vile ulikuwa ukitania siyo?" Valentina akamuuliza Xander.

"Ndiyo ni joke kutoka FB," akajibu Xander.

"Kwa nini unaingiza utani?" Valentina akamuuliza tena.

"Nilifikiri ungetambua kiurahisi nia ya Mecky kukuuliza hilo swali lakini kwa sababu umeuliza... ni ili nifurahishe watu, maana wameboeka," Xander akamjibu hivyo.

Valentina akatabasamu kidogo, kisha akamwambia, "Simama."

Darasa likatulia. Hali ilikuwa imegeuka kuwa nzito ghafla. Xander akasimama na kumtazama "madam" kwa umakini.

"Somo la Communication Skills ni required kwa wote mlio humu. Wengine huwa wanaliona kama la kupoteza muda tu, lakini ni somo la muhimu sana. Hii semester nataka kila mmoja wenu anionyeshe kwamba anaweza kuandika vizuri, na itakuwa inaburudisha sana ikiwa hamtaona kwamba inachosha..." Valentina akasema.

"Nahisi kama inachosha kusimama, nikae?" Xander akasema kwa kejeli.

Wenzake wakacheka.

"Nawapa assignment. Nataka mwandike essay, plain nne. Elezeeni kitu fulani mlichoona nyie wenyewe kipindi fulani cha nyuma. Mnatakiwa kuelezea vizuri sana na kwa ufasaha ili kunifanya mimi kama msomaji niweze kuona mambo jinsi nyie mlivyoyaona. Onyesheni mlichohisi kuwa sehemu hiyo, na jinsi ilivyowaathiri kwa ujumla. Kesho CR kusanya kazi saa 5. Marks mnajua ni za muhimu so get to work. Na wewe..." Valentina akahamishia umakini wake kwa Xander baada ya kumaliza kuwaambia wengine hayo.

Xander akabaki kumwangalia tu. Valentina akaanza kumfata mpaka aliposimama na kumtazama machoni kwa ukaribu.

"Wewe assignment yako ni hiyo hiyo, lakini nataka uiandike leo leo na umpe CR aniletee ofisini kabla ya muda wa kuondoka," Valentina akasema.

"Leo?" Xander akashangaa.

"Leo," Valentina akajibu.

"Kwa hiyo nisiende lunch?" akamuuliza.

"Ndiyo maana yake," Valentina akajibu.

"Kwo' unanipa adhabu kwa sababu..."

"Ndiyo," Valentina akamkatisha na kurudi mbele.

Watu hapo wakaanza kumcheka Xander. Akaishiwa pozi kabisa.

Baada ya madam Valentina kuondoka, wengi wakamfata Xander na kumtania kuwa madam kweli leo alimweza. Ijapokuwa ilimkera kiasi lakini alijua ikiwa angeacha kuifanya hiyo kazi basi kungekuwa na shida, hivyo akaamua angeondoka kuelekea kufata karatasi nne nyeupe ili aanze kuandika haraka.

"Una kiherehere mno, shavu limekushuka," Sandra akapita karibu yake na kumwambia hivyo, kisha akamsukuma kichwa kwa kidole na kuondoka huku anacheka.

"Kwa hiyo hatuwezi kwenda lunch wote baby?" Ramla akamuuliza Xander.

"Hapana. Nenda tu na wengine, me naenda library kuandikia huko," Xander akajibu.

"Haya poa baadae," Ramla akamwambia.

Binti akaenda upande mwingine na kumwacha Xander anaelekea maktaba. Hakuona sababu muhimu iliyofanya mpaka madam Valentina achukue hatua hiyo kwa sababu alikuwa akitania tu. Akawaza labda yeye kusema kwamba madam hakujua nia ya Mecky kumuuliza swali lile ndiyo kulimuudhi, lakini akaona huo ni kama utoto. Kwa vyovyote vile hakuwa na jinsi ila kwenda kuianza tu kazi ili amalize haraka.

Xander akaandika kuhusu wakati fulani alipokuwa na miaka tisa. Yeye, mama yake, pamoja na dada yake walikuwa sehemu fulani ya kujistarehesha wakati wa matembezi siku za likizo. Wakati walipokuwa wamekaa kuzunguka swimming pool, aliona mvulana fulani wa miaka minne au mitano hivi akiwa ndani ya maji hayo. Mvulana huyo alianza kutapatapa, akipiga-piga mikono yake na miguu juu chini ndani ya maji, akiwa anajitahidi kuelea vizuri kwa juu. Mwanzoni watu walifikiri labda alikuwa anatania tu, lakini vilio vyake vilipoanza kuzibwa na maji, msichana fulani wa kama miaka kumi na kitu akaingia upesi ndani ya maji na kumwokoa mtoto huyo. Ni kitu ambacho Xander pia angefanya kama msichana huyo asingemwahi mapema.

Xander alikiandika kisa hiki vizuri na kwa ubunifu sana, naye akampelekea CR (Class Representative) ili aifikishe kazi yake kwa Valentina. Baada ya Valentina kuipokea, akaipitia kwa umakini sana, kisha akaiwekea alama alizoona zinafaa.

★★

Wakati fulani wakiwa wamemaliza vipindi vyao, Xander akafatwa na CR, aliyemwambia kwamba madam Valentina alitaka kumwona ofisini kwake. Xander akaanza kujitapa kwa marafiki zake kuwa alikuwa ameua hiyo kazi na hapo bila shaka madam alikuwa anamwita kumpongeza. Wakampa sifa kama jinsi ambavyo vijana wahuni hufanya, naye akaondoka na kuelekea mpaka ofisini kwa Valentina, na baada ya kuingia akamkuta akiwa ameketi kwenye kiti upande wa pili wa meza yake kutokea aliposimama Xander.

"Vipi Alexander, uko poa?" Valentina akamsalimu.

"Kama kawa," Xander akajibu kwa kujiamini.

"Sawa. Nilikuwa nataka tuongee. Nikuulize kitu fulani?"

"Uliza tu."

"Unalionaje somo la Communication Skills?"

"Nalipenda."

"Unalipenda? Hivyo tu? Tafadhali elezea zaidi hiyo kauli."

"Napenda nywele zako pia. Nakwambia kwa kuwa unastahili kujua," Xander akatania.

Midomo ya Valentina ikaonyesha tabasamu hafifu, kisha akasema, "Asante. Lakini nilikuwa namaanisha uelezee kile unachofikiria kuhusu hili somo."

"Ndiyo... kiukweli... ni darasa zuri. Tokea nilipoanza kusoma hivi vitu kwangu havijawahi kuwa vigumu sana... ijapokuwa siyo mara zote najua jinsi mambo yatakavyokuwa. Unafundisha vizuri sana tokea tulipoanza kusoma. Angalau wewe ni mwalimu unayejali kwamba siyo wanafunzi wote watakuelewa ukitumia English mwanzo mwisho kila unapofundisha," Xander akaeleza.

Valentina akacheka kidogo.

"Sawa. Hii hapa kazi yako," akampatia karatasi zake.

"Kwa hiyo ulikuwa unataka nikueleze... 2? Nimepata 2 ya 5?!!" Xander akashangaa.

"Ndiyo. Umeandika vizuri, na unajua kujieleza, lakini hukueleza jinsi ambavyo kisa hicho kiliku-affect WEWE. Nataka nione ni nini kilichokuchochea zaidi kutokana na yote uliyoona, yaani... Passion," Valentina akaeleza.

"Aisee!" Xander akaonyesha kuvunjika moyo.

"Najua inaonekana kuwa unfair..."

"Sana!"

"Ahahah... okay. Vipi nikikupa assignment nyingine?"

"Kwa nini unafanya hivi madam V?" Xander akauliza.

"Sitakuficha. Unaandika vizuri sana. Nataka tu uzame zaidi kwenye core muhimu za uandishi ili uone jinsi inavyoburudisha, na hivyo hautakuwa unaboeka sana class," akajibu.

"Kwa hiyo unakiri kwamba hujanitendea haki?" Xander akauliza.

Valentina akashindwa kujizuia kucheka. Kwa sababu fulani, Xander alipenda sana kuona jinsi mwalimu wake huyu alivyopendeza sana alipocheka. Akabaki kumwangalia kwa makini.

"Fanya hii assignment uni-impress, ndiyo utaona haki ikitendeka," Valentina akamwambia kiurafiki.

"Nambie..."

"Kaandike essay ya biography, ya mtu yeyote halisi unayempenda au unayemkubali sana. Elezea vitu vinavyokufurahisha au kukukwaza kumhusu kwa utaratibu mzuri sana. Plain tatu tu zinatosha... au ni nyingi?"

Xander alikuwa anamwangalia sana mwanamke huyu, kama anamtathmini kupita kiasi, mpaka Valentina akajishtukia.

"Alexander? Vipi?"

"Oh... fresh. Nita... nitaishughulikia. Unaitaka lini?"

"Kesho."

"Ai... nahisi nitapasua kichwa leo."

Valentina akatabasamu tena, kisha akamruhusu kijana huyu aondoke.

Xander alitoka nje akitafakari jambo fulani kwa kina, na baada ya akili yake kulisawazisha vyema, akaachia tabasamu la hila akipanga kufanya kitu ambacho alijua kingemkomesha mwalimu huyo.

★★★★★★★★★

 ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Next