Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

FOR YOU

Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa

Rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TATU

★★★★★★★★★★★★★


MWANZA


Tukio fulani lenye kushtua sana linatokea katikati ya jiji hili. Kikundi cha watu wanaojiita "Demba Group" wanavamia jengo kubwa la ofisi za PPF wakiwa na silaha nzito za mikononi aina ya AK-47, nao wanawafyatua risasi watumishi wa serikali pamoja na walinzi wa jengo hilo. Eneo zima linalozunguka hapo linapatwa na msukosuko mkubwa kwa kuwa watu wengi wanaanza kukimbia ovyo ovyo na shughuli nyingi zinaachwa ili kuokoa maisha yao.

Washiriki wa kikundi hiki wanaharibu vitu vingi hapo, na hakuna yeyote anayeweza kuwatambua kwa sura kwa sababu wanavaa viziba uso vinavyofunika mpaka vichwa vyao na kuacha macho na mdomo wazi kidogo. Hawaibi chochote, bali wanafanya tu vurugu hizo na kuua watu kadhaa hapo, kisha wanatokomea kusikojulikana. Mapolisi kama kawaida wanafika hapo kwa kuchelewa na kuingia jengoni, wakitaka kuhakikisha usalama, lakini bomu linalipuka kutokea ndani ya jengo hilo na kusababisha vifo vya mapolisi wote waliokuwa ndani.

Hali ya hewa inachafuka sana katikati ya jiji hili kwa kuwa sasa ni wazi kwamba hakuna usalama. Hii inakuwa mara ya pili kwa kundi hili kujitokeza na kufanya vurugu namna hii. Mara ya kwanza ilikuwa ni kule Kigoma kwenye shule ya sekondari. Waliua walimu na wanafunzi wachache tu na kufanya vurugu, lakini hii ya Mwanza ndiyo ikawa mbaya zaidi kuliko ile ya huko. Eneo likabaki bila mtu hata mmoja aliyethubutu kusogea, maana walihofia kuna bomu lingine lingelipuka.

Baada ya tukio lile la kwanza kule Kigoma, serikali, kupitia jeshi la polisi, ilikuwa imeahidi kwamba watu hao wangetafutwa na kukamatwa, lakini ahadi hiyo ikawa deni kubwa sasa lisiloweza kulipwa. Haya yaliyotokea jijini Mwanza yalitokea mchana kweupe, lakini hamna hata mtu mmoja wa kundi hilo aliyenaswa.

Muda fulani baadaye, vyombo vya usalama vya serikali vilifika hapo na "kupiga kambi" ya muda. Maaskari wengi kutokea idara mbalimbali walifika na kuzuia shughuli yoyote ile isiendelee upande huo. Waandishi wa habari kutoka vituo mbalimbali vya runinga walifika pia, na baadhi wakaweza kuongea na Kamanda wa Polisi wa mkoa kuhusiana na matukio haya. Akaeleza ni wazi sasa kuwa kundi hili ni hatari sana, nao wangefanya kila njia kuhakikisha kwamba wale wote wanaohusika wanakamatwa na kuadhibiwa, hivyo kokote walipo, wajiandae.

Jiji likawa kwenye tafaruku kubwa kwa kupoteza watu 38 siku hiyo; 16 wakiwa mapolisi. Lakini jambo lingine likatokea. Kuna video ikaanza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikiwaonyesha watu kadhaa, wakiwa wamefunika sura zao kabisa huku wameshikilia bunduki mikononi. Mmoja wao alikuwa anasema kwamba yeye ndiyo kiongozi wa Demba Group, na nia yao ni kupindua utawala wa Raisi kwa sababu anaongoza nchi kimabavu. Akatoa kiapo kwamba mambo haya yote mabaya hayataacha kutokea mpaka Raisi ajiondoe kutoka madarakani.

Ilikuwa ni video fupi tu yenye dakika moja na nusu. Ilisambaa kwa uharaka sana mpaka kwenye kampuni za vyombo vya habari, lakini vikapigwa marufuku kuionyesha kwenye runinga zao. Hilo halikuwazuia watu kuiona kwa kuwa wengi tayari waliipata kwa njia ya simu, hivyo hofu iliyoanza kujengwa na kundi hili ikazidi kuongezeka. Midomoni mwa watu wengi siku hii mada ilikuwa ni hiyo. Siyo kwamba wote nchini walipata kujua upesi, ila habari hazingechelewa kuwafikia.


★★★


JENGO LA KITUO CHA USALAMA WA TAIFA


Mkutano wa dharura uliitishwa haraka isivyo kawaida. Walifika baadhi ya viongozi wa vikosi vya ulinzi nchini ili kujadili matukio haya mawili yaliyotokea ndani ya wiki moja tu bila kupatiwa suluhisho la haraka. Aliyeitisha mkutano huu alikuwa ni Jenerali (General) mkuu wa jeshi la nchi (wanajeshi), ambaye aliitwa Jenerali Pingu Senganya. Waliokuwepo walikuwa na vyeo vilivyofuata kutoka kwake; Luteni Jenerali (Liutenant General) aliyeitwa Geneya Oyayu, Brigedia Jenerali (Brigadier General) aliyeitwa Sebastian Tambwe, Kanali (Colonel) aliyeitwa Jacob Rweyemamu, na Luteni Kanali (Lieutenant Colonel) aliyeitwa Oswald Deule.

Hao walikuwa ni baadhi ya viongozi wa jeshi la nchi. Pia, Inspekta Jenerali wa jeshi la polisi (IGP) Donald Ngassa na Kamishna wa jeshi la polisi (CP) Osman Hamisi walifika upesi, na aliyekuwa msimamizi msaidizi wa kitengo cha huduma za ulinzi nchini (Ministry of Defence), mwanamama shupavu Emiliana Ngoyi, alikuwepo pia. Jenerali Pingu alitaka kuwataarifu IGP Donald Ngasa na CP Osman Hamisi kwamba hali hii ilianza kuwa mbaya kupita maelezo, na hivyo angefanya mpango wa kuingiza wanajeshi kwenye msako wa kuwakamata Demba Group.

"Inawezekanaje... inawezekanaje watu 7 wanaingia kwenye jengo lenye ulinzi na kufanya mambo kama vile ni kwao na kuondoka tu? Askari wanakufa, watu wanakufa, halafu wanapotea tu? Halafu wanapost na video kabisa inayosambaa bila sisi kujua chanzo kimetokea wapi, watu wa tech wanafanya nini? Wiki nzima imeisha na sasa ya pili bado hatujawakamata, kwa nini?" Jenerali Pingu akaongea kwa mkazo sana.

"General, hili suala wangetupatia sisi ili tushughulike nalo, maana wanafanya nchi inaonekana ya kizembe," akasema Brigedia Sebastian, akimaanisha wanajeshi waingizwe badala ya mapolisi.

"Tunajua mambo yamekuwa magumu, lakini General, tunafanya kila kitu na wakati huu hawataweza ...." IGP Donald Ngasa akawa anajaribu kutoa maoni.

"Vitendo, matokeo. Ndiyo tunachotaka. Wiki nzima imeisha mmetoa ahadi ambayo imevunjwa na tukio la leo. Hawa watu wanataka kuipindua serikali, na wanaua ovyo tu kama kuwaonyesha wanaweza na hamtawafanya lolote. Tukio la leo linathibitisha kwamba hamjui mnachokifanya, wote ni ubweche tu!" Jenerali Pingu akafoka.

"Mheshimiwa, sisi hatuko chini ya jeshi, na tunaheshimu sehemu yenu kubwa hapa nchini. Ila hili suala tumepewa tushughulike nalo, na ninajua ndani ya siku chache watu hao watakamatwa. Kuna vitu tumeshaanza kufuatilia, na tuna uhakika tutawapata. Jeshi likiingia watu wengi wataumia, kwa sababu brute force mnayotumia huwa ni...."

IGP Donald alipokuwa anasema hayo, akakatishwa na Kanali Jacob Rweyemamu, aliyenyanyua kidole chake juu kumzuia asiendelee kuongea.

"Kwa hiyo ni bora zaidi kuwaacha nyie mwendelee kusinzia, hawa washenzi waendelee kujitawaza mbele ya chakula chetu, halafu tukae tu kuwaangalia? Unajua kwamba sisi hatuko chini ya yeyote ila Raisi, kwa hiyo tunaweza kufanya LOLOTE lile tunalotaka. Hatujali ikiwa kuna mtu yeyote ataumia mpaka tuhakikishe wanatoweka. Mnahesabu kwamba wako 7, kwa sababu mnataka kuonyesha wako 7 tu, lakini hawa wapuuzi wanaweza kuwa nchi nzima. Tumia akili IGP kutambua kwamba wanapotokeza tukio moja sehemu fulani, tukio la pili wanalifanya kwa njia itakayohakikisha wale waliokuwa kwenye lile la kwanza wanatoka huko kirahisi. Ndani ya siku mbili utasikia ni Arusha, Lindi, Nzega, na labda hata nyumbani kwako," Kanali Jacob akasema kwa uzito sana.

"Raisi atatoa tamko kuhusiana na tukio la leo litakalorushwa moja kwa moja kwenye Televisheni. Baada ya video hiyo kusambaa kwenye mitandao, imekuwa wazi kwamba hawa watu siyo wahuni tu. Wana lengo, na mipango yao inafanikiwa kwa njia ambayo inaonyesha wako makini. Bomu la leo liliwalenga mapolisi. Walikuwa wameshaondoka, kwa hiyo inamaanisha walipiga mahesabu kujua mapolisi wangeingia pale muda gani, na kwa utaratibu gani, ili watege muda gani kwenye bomu hilo. Ni wazi wana mafunzo. Kwa hiyo, kwa heshima yote General, ninahitaji kujua nini kitafanywa ili Raisi atoe kibali kwenu," akasema Secretary Emiliana Ngoyi.

"Hakuna cha kufikiria. Raisi ahidhinishe tu ruksa kwetu kuingiza vijana wetu na hili suala halitasikika tena. Kila kitu tutamaliza sisi. Watu hao, tunaowaona kuwa wachache sasa hivi, watasababisha vita. Ni muhimu tuwakalishe kabla hawajaianzisha," akasema Luteni Jenerali Geneya Oyayu.

"Na jeshi la polisi?" akauliza CP Osman Hamisi.

"Nyie fanyeni yenu. Tambeni kwenye vyombo vya habari. Imbeni, imbeni, imbeni... watu wote wasikie kwamba mtawashughulikia. Ndiyo mnachowezea hicho," akasema Jenerali Pingu.

"Lakini General, huu siyo aina ya ushirikiano..."

"Ushirikiano? Tuliwasumbua lini sisi tokea tukio la kwanza? Si mlisema mngewakamata? Raisi anafanya mengi kwa ajili ya hii nchi halafu sasa hivi, out of nowhere kunguni fulani waanze kumsumbua huku nyie mkiwa mmesinzia? Wewe unaweza ukawa na motivation lakini watu wenu wengi wamesinzia mno. Hatutaki mchezo na nchi yetu. Kapigeni domo, kazi tuachieni sisi," Jenerali Pingu akasema.

"Askari 16 wamekufa leo. Next watafata 30, 40, 50. Hatukai kuangalia hiyo pumba aisee," akasema Brigedia Sebastian.

"Tekeleza unayohitaji kufanya," Jenerali Pingu akamwambia Emiliana.

Secretary Emiliana Ngoyi akanyanyuka na kuwaaga wote kwa heshima, kisha akaondoka. IGP Donald Ngasa na CP Osman Hamisi pia wakanyanyuka na kupiga saluti, kisha nao wakaondoka zao.

"Lieutenant Colonel..." Jenerali Pingu akaita.

"Ndiyo..." Luteni Kanali Oswald Deule akaitika.

"Tuma taarifa kwa Meja mpakani kuhusiana na hili. Nataka Meja achague vijana finest walio makini zaidi ili order ikitoka waanze kutembea," Jenerali Pingu akamwambia.

"Sawa mkuu," Luteni Kanali Oswald Deule akakubali.

"Samahani General, naomba hiyo kazi uniachie mimi. Ninajua vijana wazoefu zaidi hasa kwa sababu niko juu ya Meja. Na..."

"Hapana," Jenerali Pingu akamkatisha Kanali Jacob.

Wote wakamtazama.

"Nataka Meja ndiyo achague na yeye ndiyo atawapanga. Anajua tactic nyingi vizuri na anawafunza vizuri vijana wake. Hatutakuwa na shida sana upande wetu akilishughulikia hili. Naamini atalipatia ufumbuzi haraka sana. Deule, zifike haraka," Jenerali Pingu akatoa amri.

Wote wakanyanyuka na kupiga saluti, kisha wakatoka ndani ya chumba cha ofisi hiyo.

Luteni Kanali Oswald akafanya kama alivyoagizwa. Akamtafuta upesi Meja (Major) wa jeshi la nchi, ambaye hakuwa mwingine ila Casmir Eliakim Sona. Ndiyo. Huyu ndiyo baba wa mapacha wale, Alexander na Alexandra. Luteni Kanali akampatia ujumbe wa muhimu kutoka kwa Jenerali Pingu, na bila kusita Meja Casmir akamhakikishia kuwa mambo yote waliyotaka angeanza kuyafanyia kazi haraka sana na hivyo ambacho angesubiri ni amri tu.


★★★


"Kwa nini umekubali?"

"Ningefanyaje sasa, ningekataa?" akauliza Meja Casmir.

"Lakini hili suala si angeshugulika nalo Kanali, kwa nini wakupe wewe?"

"Sijui Kendrick, lakini ni amri kutoka kwa Jenerali Pingu. Ni lazima nitekeleze," akasema Casmir.

Haya yalikuwa maongezi baina ya Meja Casmir Sona na Kapteni (Captain) Kendrick Jabari wa jeshi pia. Kapteni Kendrick alikuwa akimfuata Meja Casmir kwa cheo, lakini wawili hawa walikuwa marafiki wa karibu sana. Walishirikiana kwa mambo mengi sana tokea walipokutana mara ya kwanza kwenye kambi ya mafunzo ya jeshi na kutumikia pamoja kwa muda mrefu mpaka kufikia vyeo hivi. Hapa walikuwa kwenye ofisi zao ndogo za mpakani, wakiwa pamoja wakati Luteni Kanali Oswald alipompa Casmir taarifa ya Jenerali Pingu.

"Vipi kuhusu birthday ya Alice sasa? Na hii utaikosa tena," Kapteni Kendrick akamwambia.

"Ah... yaani sijui. Na nilikuwa nimemwahidi ningekuwepo," akasema Casmir kwa huzuni kiasi.

"Unajua siyo watu wengi wanaopata mwanamke kama wako Casmir. Ni muda mrefu sana unapita haumwonyeshi hata sura yako..."

"Kila siku nampigia video call..."

"Kwa hiyo unafikiri hiyo inatosha?"

"Najua haitoshi..."

"Kwa hiyo?"

"Lakini nitafanyaje? Jambo kama hili ni dharura... sikutegemea..."

"Sizungumzii kuhusu leo tu Casmir..."

"Dah, kaka na wewe umeanza kusound kama mama yangu..."

"Nakwambia ukweli. Wewe ni Meja kaka. Una mke na watoto wazuri... perfect. Wape time. Likizo zote au wakati wa kupumzika wewe unautumia kukaza misuli ya nchi. Maisha ni mafupi, usisahau hilo," Kendrick akamwambia.

"Yeah. Hawa Demba Group wakinisababishia nikakosa event za mke na binti yangu, nawanyoa vipara makalioni," akasema Casmir.

"Tako ni kipara," Kendrick akamwambia kiutani.

Wote wakacheka kidogo.

"Unamwonea sana Alice. Utamwambia kuhusu hili?" Kendrick akamuuliza.

"Ngoja kwanza tuone itakavyokuwa..."

"Birthday yake iko kwenye kona tu hapo..."

"Najua. Lakini sitaki kumvunja moyo. Najua pia nisipomwambia halafu... ikafika tu ndiyo niseme ataumia hata zaidi. Na Sandra, Azra..."

"Bila kumsahau mzee wa fujo," akasema Kendrick, akimaanisha Xander.

"Yaani! Uko sahihi sana Ken. Nimeionea familia yangu kwa kipindi kirefu," akasema Casmir kwa hisia.

"Haina haja ya kuvunjika namna hiyo. Unakumbuka wakati ule tumejikuta chini ya shida? Ilionekana kama mimi na wewe hatungeokoka lakini mara puuf! Mungu akatuonyesha handaki lile lililookoa uhai wetu. Nachotaka kusema ni kwamba, usikate tamaa. Lazima itakuja njia tu. Lakini jambo la muhimu kwa Alice siyo birthday moja tu... ni wewe Casmir. Anahitaji uwepo wako karibu naye. Tafakari. Kuna mambo ni ya muhimu kutanguliza kwanza hata kama una wajibu mwingine. Familia Casmir. Familia kwanza. Hizi vita zipo tu. Kumbuka umesoma siasa na vita ili wanao wapate uhuru wa kusoma hesabu na falsafa," Kendrick akatoa ushauri.

"Dah, kaka inabidi huo upuuzi wa John Adams uuweke pembeni!" Casmir akasema, nao wote wakacheka.

"Ahheheheh... jamaa alikuwa anajua anachokiongea bwana. Ila sikwambii hivi kwa kuwa labda nataka ukiache cheo chako..."

"Ahahahah... usijali naelewa. Nina mambo mengi sana ya kufanya," Casmir akasema.

"Niko pamoja nawe kamanda," Kendrick akamwambia.

Kisha wakaunganisha viganja vyao kwa nguvu kwa njia ya kirafiki, naye Kendrick akatoka hapo.

Casmir alikuwa mwanaume mtu mzima, mwenye miaka 50, mrefu na mwenye mwili mpana wa mazoezi. Alikuwa mwenye utu wa kujali na mkarimu, lakini thabiti sana aliyefuata viwango vya juu vya maadili. Alimpenda sana mke wake na watoto, na kwa kipindi kirefu alijichukia sana kwa kuwanyima muda wake mwingi kwa sababu aliutumia kuimarisha ulinzi wa mipaka ya taifa. Sasa alitakiwa kufikiria kwa kina angefanya nini ili kuirudia familia yake tena na kuepuka kuwavunja moyo.

Kendrick alikuwa mwanaume mwenye nguvu pia, mkali, imara, na mwenye akili sana. Yeye ndiye aliwapa mafunzo na kuwaongoza wanajeshi wengi katika mazoezi ya kila siku ili kuwaimarisha, na hata mara nyingine kuhakikisha vifaa vya kivita vinakuwa sehemu maalumu kwa ajili ya matumizi. Yeye pia alijuana na familia ya Casmir, akiwaona mapacha wale walipozaliwa mpaka wanakua na kucheza nao. Watoto wa Casmir walizoea kumwita "Uncle Kendrick," kwa sababu ukaribu wake kwa baba yao ulifanya ionekane kama ni ndugu yake.

Yeye Kendrick hakuwa na familia yake mwenyewe wakati huu. Kipindi cha nyuma alioa mwanamke fulani lakini akapatwa na ugonjwa uliosababisha kifo chake, hivyo Kendrick aliamua kujiunga tu na jeshi na kutojihusisha na mahusiano kwa muda mrefu sana kwa sababu alisikitishwa mno na kifo cha mke wake. Mara kwa mara ingetokea mahusiano ya "gusa nikuache" na wanawake kadhaa aliokutana nao, lakini hakuweka umakini wake wote kwa yeyote kati ya hao kwa sababu hakutaka kupenda tena kupitiliza. Labda kama ni mwanamke mmoja aliyeitwa Margaret, ndiye aliyempenda sana Kendrick kipindi fulani cha nyuma. Lakini aliondoka nchini kwenda kufanyia kazi Ghana.

Kendrick alikuwa na nyumba moja kwenye jiji lile lile ilipokuwepo familia ya Casmir pia, na hapo walikuwepo mama yake mzazi, pamoja na wadada wengine wawili ambao walikuwa ni ndugu wa kiukoo. Kwa kuwa umri wa mama yake ulikuwa umesonga, wanawake hao walikuwa pale kumsaidia wakati ambao Kendrick aliutumia kazini. Alimpenda na kumheshimu sana Casmir. Alimsikiliza kwa vitu vingi, na hata yeye pia alimshauri kwa mambo mengi kama alivyofanya wakati huu. Kendrick alikuwa na miaka 49.

Bila kuchelewa, Meja Casmir akaanza kujipanga kwa mambo ambayo angehitaji kufanya kwa ajili ya kazi mpya aliyopewa. Alianza kuangalia ni wanajeshi gani wangefaa kwa ajili ya kazi iliyohitajika kufanywa, na ni mbinu zipi wangetumia upesi ili kuhakikisha wanafanikiwa kuwafatilia na kuwakamata waasi wale. Hakuweza kujizuia kutulia kidogo na kuitafakari familia yake na yale Kendrick aliyomwambia, lakini akaendelea tu kufanya mipango ya mambo hayo aliyokabidhiwa.


★★★


UPANDE WA MAPACHA (SIKU HIYO HIYO)


Alexandra, au Sandra, alikuwa ameondoka nyumbani kwao mida ya saa 10 jioni ili kwenda kuonana na mpenzi wake, Raymond. Xander alikuwa ameondoka kabla yake kuelekea uwanjani kwa ajili ya mechi baada ya kumfikisha kwao kutokea chuoni muda mfupi nyuma. Ijapokuwa Sandra alivaa kwa njia ya kawaida tu, alipendezea sana. Alivaa T-shirt nyeupe na suruali ya jeans yenye kubana kiasi, iliyochanikia magotini kama kawaida. Kuwa mtoto wa kishua hakukumfanya ajidodeke mavitu mengi sana mwilini yasiyo na ulazima, kwa kuwa mwonekano wa kawaida ndiyo ulikuwa mtindo wake sikuzote.

Raymond aliishi mtaa mwingine jijini hapo, akiwa amepanga chumba kwenye nyumba ya kulipia. Alikuwa msafi na nadhifu sana, naye alijitahidi kuishi na wapangaji wengi wa pale kwa amani. Leo yeye ndiye alimwambia Sandra kwamba angemtoa "out" kwenye sehemu nzuri sana, hivyo binti alikuwa na hamu kubwa kwa kuwa hakuonana naye kwa siku chache za nyuma kutokana na yeye kuondoka jijini hapo. Alikuwa ndiyo amerejea sasa, na kitu cha kwanza alichotaka ilikuwa ni kumwona mpenzi wake.

Sandra alikwenda mpaka maeneo fulani ya jiji kwa kutumia usafiri. Alimkuta Raymond anasubiri sehemu waliyotumia mara nyingi kukutana, nao wakakumbatiana kwa furaha. Raymond alimzidi urefu kidogo, naye alikuwa mweusi kiasi, mwenye mwili imara wa mazoezi uliofanya T-shirt nyingi alizovalia zimbane na kuchoresha kifua chake vizuri. Hakuwa mtu mwenye makuu kabisa. Alikuwa mwelewa, mstaarabu, na mwenye heshima sana. Kipindi fulani cha nyuma kabla hajakutana tena na Sandra, aliumwa sana kwa muda mrefu, hivyo alihitaji uangalizi wa hali ya juu na mazoezi yaliyomjenga kimwili kufikia namna hii wakati huu.

Wawili hawa wakafanya matembezi kidogo huku wakifurahia maongezi, na baada ya dakika kadhaa Raymond akamwomba Sandra waelekee kule alipokuwa ameandaa "kiburudisho" chao. Baada ya kufika, Sandra akashangaa kujua kwamba ilikuwa ni kwenye hoteli moja kubwa sana na ya kifahari jijini hapo. Raymond alimwambia alitaka kumfanya ashangae namna hiyo, lakini uhondo haukuishia hapo. Uhondo ulikuwa kule ndani. Wakaelekea ndani ya hoteli hiyo mpaka kwenye chumba kimoja juu kwenye ghorofa ya 7, ambacho Raymond alikuwa ameshalipia.

Walipoingia, Sandra aliachia tabasamu baada ya kukuta meza iliyowekewa viti viwili kwa pande zake, huku katikati kukiwa na vyakula na vileo (wine) kwenye glasi. Chumba kilikuwa kipana, chenye masofa, kitanda kikubwa upande wa pili, choo na bafu la kisasa, vifaa vya kuwekea vinywaji na kuingiza hewa safi chumbani, na TV kubwa ukutani. Alistaajabu sana kwa kuwa alijua gharama ya hapa ilikuwa ni kubwa sana. Alijua pia kwa Raymond haingekuwa rahisi kugharamia sehemu hii, labda kama angekuwa ameanza kazi au amekopa pesa sehemu. Mara zote walizotoka kipindi cha nyuma, ilikuwa ni kufanya mambo yenye kufurahisha kwenye sehemu za kawaida tu, na alipenda sana mambo "simple." Hivyo jambo hili kutoka kwa Raymond lilikuwa jipya kwake.

Akamgeukia na kumuuliza, "What is all this?"

"Ni... zawadi ndogo tu... yaani... outing ndogo nilipanga nikufanyie. Umeipenda?" Raymond akasema.

"Lakini Raymond, nilishakwambia kwamba mimi sijali sana vitu fancy. Nafurahia zaidi unapokuwa unanitendea kwa njia yako... kawaida tu," akasema Sandra.

"Ndiyo najua. Lakini leo nilitaka kujaribu hivi pia. Wewe ni malkia kwo' lazima utendewe kama malkia kweli," Raymond akasema.

"Ray..."

"Nmekumiss sana yaani. Nikafikiria niweke na njonjo kidogo kwa leo. Ila kama hujapenda hii, basi..."

"No, siyo kama sijapenda. Nimeshangaa tu. Umemfungia nani ndiyo ukamwibia chumba chake?"

"Ahahahah... najijua me masikini sana kwa hiyo sehemu kama hizi hautegemei nitakupeleka..."

"Ahahah... sijamaanisha hivyo..."

"I know love... natania tu. Nime... nimeachiwa sehemu fulani ya urithi na babu yangu," akasema Raymond.

"Babu yako? Si ndiyo huyo uliyekuwa umeenda kumwona?"

"Ndiyo. Amekufa hiyo juzi..."

"Ooh, pole sana Ray. Pole."

"Usiwaze..."

"Ila, si alikuwa mzima... ndiyo ulienda kumsalimu?"

"Ndiyo. Alituita mimi na mama yangu kwa sababu alikuwa anaumwa sana. Ndiyo zilikuwa dakika za mwisho..."

"Jamani Raymond, mbona hata hukuniambia?"

"Naah, mzee mwenyewe hakutaka wengi wajue kwamba alikuwa anakwenda..."

"Acha utani huo Raymond..."

"Ahah... well, sisi wenyewe hatukutarajia. Hakuwahi kuweka ukaribu wowote na sisi, lakini mwishoni ndiyo akaweka wazi kwamba anampenda sana mama na mimi. Mali zake amejitahidi kuzigawa kwa wanae wengi na mama, na mimi pia akanipa chenji kidogo. Ndiyo maana unaona nimekuja na mng'ao mpya," Raymond akasema.

"Ahahahah... samahani, sidhani kama ni sahihi kucheka kwa hilo..." Sandra akamwambia.

"Usihofu. I want us to enjoy this moment," Raymond akamwambia huku akiweka mikono yake kiunoni kwa Sandra.

"Me too. I really missed you," Sandra akamwambia huku naye akizungushia mikono yake kichwani kwa Raymond.

Wawili hawa wakaanza kupeana busu ya upendo. Sikuzote kilichomfurahisha Alexandra kuhusu Raymond ni kwamba alikuwa na mapenzi yasiyotaka papara. Alipeleka mambo taratibu na kistaarabu, hivyo alimpa binti muda mwingi wa kufurahia kile alichompatia. Busu hii ikawa denda kadiri walivyoendelea, na sasa mifyonzo ya midomo yao ikawa inasikika vyema. Kisha, taratibu Raymond akajitoa mdomoni mwake. Sandra akawa anamwangalia kwa hamu.

"Plan A ilikuwa... tuje, niwashe muziki wa soul kidogo, tukae kwenye hiyo romantic dinner table; kuna msosi wa ukweli hapo..."

Raymond akawa anasema na kumfanya Sandra acheke kidogo.

"Lakini kufikia hapa nadhani tukianza na plan B ndiyo itafaa zaidi, au siyo?" Raymond akauliza.

"Na hiyo plan B ndiyo ipi?" Sandra akauliza huku anatabasamu.

"Wacha nikuonyeshe..."

Raymond akasema hivyo na kuirudia midomo ya binti tena. Walipiga busu kwa huba nzito sana, huku Raymond akitembea taratibu pamoja naye kuelekea upande uliokuwa na kitanda. Jinsi Raymond alivyotembeza viganja vyake kwenye mwili wa Sandra, ilimpa binti hisia nyingi nzuri ajabu. Alihisi ni kama mtikisiko mkubwa wa ardhi unautetemesha mwili wake kwa jinsi alivyosisimka, kwa kuwa Raymond alifanya mambo kwa njia yenye ufundi sana; hapo bado hajamvua nguo. Na hili ndiyo lililompa mrembo hamu ya kutaka mengi zaidi.

Wakiendelea na mahaba yao ya kuvuruga kitanda, ilifikia hatua Sandra akawa anamwomba jamaa aongeze kasi na nguvu zaidi. Raymond akatii na kuushika mkono wake mmoja. Sandra alihisi kama anataka kupasuka, huku mara kwa mara Raymond akiuliza ikiwa alitakiwa kuacha, lakini binti akaomba aendelee tu kwa mtindo huo huo. Alikunwa kwa nguvu mpaka alipoanza kuhisi kitu ndani yake kikimtetemesha kwa nguvu ndani ya mwili wake wote, naye akapiga kelele zaidi na kuanza kutetemeka mapaja kwa nguvu.

Raymond akajitoa kwa binti na kumshikilia Sandra tumboni alipokuwa anaendelea kushtuka-shtuka kwa nguvu sana. Akawa anatoa miguno iliyoenda sambamba na kila mshtuko uliotokea kiunoni kwake, huku akiwa amekilaza kichwa chake kitandani kilegevu. Jasho lilimjaa Raymond mwilini, huku jasho la mwili wa Sandra likionekana kiasi na kufanya kama kuing'arisha ngozi yake.

Kisha binti akajilegeza na kujilaza chali kitandani, akiwa amefumba macho huku ameweka mkono wake mmoja juu ya kichwa. Raymond alimwangalia kimaswali sana. Hakujua ni nini kilikuwa kimempata mpenzi wake ghafla.


★★★★★★★★★

 ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Previoua Next