Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

FOR YOU

Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa 

Rated 18+


★★★★★★★★★★★★★

 SEHEMU YA NNE

★★★★★★★★★★★★★


Raymond akalala pembeni ya mpenzi wake akiwa bado anajiuliza alipatwa na nini. Sikuzote Alexandra alipenda kupewa mapenzi kwa njia ya kistaarabu, kwa hiyo jambo hilo lililotokea lilikuwa jipya kwake. Akashika tumbo lake taratibu, naye Sandra akashtuka kidogo na kumtazama usoni. Raymond akawa anamwangalia kwa kujali sana, naye Sandra akamsogelea mdomoni na kumbusu kidogo. Kisha akajilaza kifuani kwake na kutembeza kiganja chake kwenye mwili wa Raymond, naye jamaa akawa anafanya hivyo hivyo pia.

"My... uko sawa?" Raymond akauliza kwa sauti ya chini.

"Yeah. Asante Ray," akasema Sandra.

"Unajua... nahisi labda nisingefata ulivyoniambia..."

"Kwa nini?"

"Nilikuwa nahofia nakuumiza, lakini wewe ukataka niendelee tu..."

"Hapana haujaniumiza..."

"Usinidanganye Alexandra. Najua ulikuwa unaumia. Lakini... nahitaji uniambie ni kwa nini ulikuwa unataka kuumia..." akasema Raymond.

Sandra akabaki kimya.

"Kuna tatizo. I know you. Pamoja na kwamba una umri mdogo lakini mambo mengi huwa unayafanya kwa njia mature sana. Sikuzote. Ila leo, umenifanya nihisi ni kama vile ulihitaji nikuadhibu... na sijui sababu ni nini. Tafadhali niambie..." Raymond akamwomba.

Sandra akaanza kulia kwa sauti ya chini. Raymond akawa anamfuta machozi kwa upendo.

"Shida ni nini mpenzi wangu?" Raymond akauliza.

"I'm sorry. Nimekuwa... nimekuwa tu na wakati mgumu kihisia," akasema Sandra.

"Nini kimetokea? You know unaweza kuniambia lolote..."

"Hakuna kitu wala. Labda... labda ni mimi ndiyo najiendekeza tu..."

"Kwa nini unafikiri hivyo?"

"Kwa muda mrefu sasa... nimejitahidi sana kuonyesha kwamba namwelewa baba yangu. Hata nimemtetea mara kwa mara kwa wengine... hasa Xander. Ila sasa hivi sijui tu Ray yaani... nahisi kama vile... ndani yangu... kuna sehemu inayotaka kunisukuma...." akaishia hapo.

"Kumchukia?" Raymond akauliza.

"Haionekani kuwa fair. I mean... kuna watoto wengine wengi ambao hawapati kuwa hata na wazazi wote kama sisi, kwa hiyo ninapaswa kuwa na shukrani, si ndiyo? Yaani, kwa nini baba kuwa mbali inanifanya.... yaani aah..."

"Basi Alexandra... basi," Raymond akambembeleza.

"Aisee! Yaani ni kama sijitambui tena, huwa siko hivi. Ila zamu hii suala hili limekuwa zito sana kwangu. Nimejitahidi kuonyesha niko sawa lakini kiukweli naumia sana," akasema Sandra huku akilia.

"Pole Alexandra. Najua siyo rahisi, hasa kwa sababu hata mimi ninaweza kuelewa inavyokuwa kwa kuwa baba yangu alinitelekeza nikiwa mdogo. Siujui sana upendo wa baba, ila kwa sababu wewe umeujua... naweza kusema anawaonea kwa kadiri kubwa..." Raymond akamwambia.

"Umeona eeh?" Sandra akaongezea.

"Ndiyo. Hafanyi vizuri kukaa mbali kisa kazi..."

"Huwa natamani sana kufanya kitu kubadili haya yote lakini nashindwa. Baba anafanya ionekane kama hatujali, lakini najua anatupenda. Sasa tatizo sisi kwa jinsi tulivyolelewa... inakuwa ngumu sana kuacha kufikiria ni mambo gani yanayomzuia kuwa pamoja na sisi... mwisho wa siku... aah am sorry Ray... nisamehe..."

"No usijali. Naelewa..."

"Hapana... hii ilitakiwa kuwa siku nzuri kwetu, hatujaonana kwa muda sasa, halafu mimi nimeharibu..."

"Ahahahah... umeharibu kwa kunipa penzi la kibabe ambalo sijawahi kupewa maishani mwangu?

Sandra akacheka kidogo.

"Hapana Alexandra, nakuelewa. Nimesema kwamba baba yenu hawafanyii fair... hilo ni kweli. Ila... nafikiri najua kwa nini anashindwa ku-rectify mambo haraka..." Raymond akasema.

"Why?"

"Nafikiri baba yako anaogopa. Anaogopa kwamba... atakuja, mtafurahi, then atapaswa kuondoka tena. Anatafuta njia ya kurudi kwa mtindo utakaoonekana kuwa wa moja kwa moja, lakini anaikosa. Na inaonekana anaipenda kazi yake pia, sasa... ukichanganya na upendo alionao kwenu na majukumu yake... hiyo njia haiwi rahisi kuonekana..." Raymond akasema kwa busara.

Sandra akayatilia maanani maneno yake.

"Kwa hiyo usijichukie kwa mambo yaliyo nje ya uwezo wako. Yeye ni mtu mzima, anapaswa kujua lililo sahihi kufanya au kuacha, na kuchukua hatua anayoona itafaa. Wewe tu... mpende. Mwonyeshe kwamba mnampenda sana. I think kila kitu kitajipa..." Raymond akasema.

"Asante Ray. Nilihitaji sana maneno yako mazuri. Unajua kunifanya nihisi vizuri. Sijui hata nilikutoa wapi..." akasema Sandra.

"Ahahah... me mwenyewe huwa nikikaa nawazaga hivi nilifanyaje kweli mpaka nikabarikiwa kukupata..." 

Sandra akaulalia mwili wa Raymond kwa juu na kumbusu mdomoni. Wakaendelea na denda hii, kisha Raymond akauliza, "Vipi kuhusu hiyo dinner?"

"Achana nayo. Me nataka tuendelee na hii tamu zaidi..." akajibu Sandra.

"Hapo umeongea!" Raymond akasema kwa furaha.

Wawili hawa wakaanzisha tena penzi lao hapo kitandani, na zamu hii Sandra akajitahidi kuongoza mambo vizuri zaidi. Baada ya muda, kasi na ufundi kutoka kwao wote vikaongezwa, na mahaba yao yakaendelea mpaka usiku ulipoingia.


★★


Ilifika mida ya saa mbili usiku; siku hiyo hiyo. Xander alikuwa ametoka kwenye mechi muda mfupi nyuma, akiwa na furaha baada ya upande aliochezea, yaani timu yao ya chuo, kufunga magoli manne kwa sifuri dhidi ya timu pinzani. Alichangia goli moja pia kwenye mchezo huu, na sasa alikuwa pamoja na Ramla baada ya kujisafisha vizuri na kuondoka kutoka huko uwanjani. Ramla alikuwa amemsisitizia amtoe "out" ili ajisikie vizuri kwa sababu alihitaji sana kuwa karibu naye. 

Ramla aliishi kwenye mabweni (hostel) ya chuo, na walikuwa na sheria iliyowapaswa wanachuo walioishi hostel kuwa ndani kabla ya mida ya saa 4 kamili usiku, la sivyo geti lingefungwa nao wangepewa aina fulani za adhabu kwa sababu ingeonwa kuwa ni utovu wa nidhamu. Kwa hiyo Xander akaamua kumridhisha mtoto. 

Kihalisi Ramla alikuwa anataka sana kupeana mahaba na Xander siku hii, lakini jamaa akamwambia muda uligoma kwa kuwa Ramla alihitaji kufika hostel mapema. Hii ilikuwa ni kwa sababu alijua kama angefanya naye mapenzi basi angetumia muda mwingi sana, na hivyo angemchelewesha binti. Kwa hiyo kumtoa out ikawa suluhusho kwa leo, halafu hilo lingine akamwahidi kumpa kesho. Alimpeleka kwenye sehemu nzuri sana ya starehe, kama mgahawa, nao wakapata chakula kizuri hapo kama wapendanao wafanyavyo. Binti alipenda sana mambo haya hasa kwa kuwa alijua pesa kwa Xander haikuwa changamoto.

Wakawa wanafurahia na maongezi huku wanashushia na vinywaji. Baada ya dakika kadhaa, Alice akampigia simu Xander kumuuliza alikuwa wapi, naye akamjulisha kwamba alitoka na rafiki kujipongeza baada ya kumaliza mechi kwa ushindi. Akamwambia mama yake wasimsubiri kwa ajili ya chakula, kwa kuwa yeye angefika nyumbani akiwa ameshiba. Alice alizoea kula na wanae wote mara nyingi, ndiyo maana alitaka kujua ikiwa angewahi au kuchelewa. Wakaagana, kisha Xander akamwambia Ramla ajiweke tayari ili amrudishe chuoni.

Baada ya kunyanyuka ili waelekee nje, Xander alitazama upande mwingine wa sehemu hiyo na kumwona madam Valentina akiwa ameketi, kwenye meza moja akiwa peke yake, na kwa haraka akakumbuka alichokifanya kuhusiana na kazi aliyompatia. Akatabasamu kidogo, na ndipo hapo Ramla akamshika mkono ili waondoke. Yeye Ramla hakuwa amemwona, lakini Xander kumwona kulimfanya akumbuke mambo aliyoandika kumhusu, na ukweli wa kwamba ni kama leo hakumwona kabisa chuoni.

Walipanda kwenye pikipiki na mpenzi wake, kisha akaanza kumrejesha chuoni. Alisimulia story za kumchekesha sana Ramla, mpaka wanafika kule, binti alikuwa amechangamka mno. Wakati akishuka na kumuaga mpenzi wake, Ramla akampa denda nzuri sana kumwonyesha jinsi alivyompenda, kisha akaelekea kule ndani. Xander alimfurahia Ramla, na alithamini jinsi ambavyo binti alionyesha upendo mwingi kwake ijapokuwa mara kwa mara na yeye alikuwa mwenye kuudhi. Akageuza pikipiki yake na kuanza kuelekea nyumbani.

Alipokuwa bado barabarani kuelekea huko, aliipita tena sehemu ile waliyotoka na Ramla muda mfupi uliopita, naye akakumbuka kwamba alimwona madam wake akiwa hapo. Akaingiwa na hisia fulani ya kutaka kumwona na hata kuongea naye kuhusiana na kazi aliyoifanya, ili ajue alihisije. Hakuwa mwoga hata kidogo kwenye mambo kama haya. Akaiegesha pikipiki nje na kurudi tena pale ndani, akifurahi kuona kwamba bado madam alikuwepo. 

Alifika usawa wa meza yake na kusimama hapo, akikuta kuna glass ya wine mezani na nyama choma zilizotengenezwa vizuri sana kwa kuwekewa "roast" pia. Akajifanya kama anakohoa ili auteke umakini wa mwanamke huyu, ambaye alikuwa amezama kusoma jambo fulani kwenye simu yake, naye akanyanyua uso wake na kumtazama mkohoaji.

"Hey... madam Valentina... niaje?" Xander akamsalimu.

"Safi," Valentina akajibu kibaridi.

"Naweza kujiunga nawe? Au kuna mtu unamsubiri?" Xander akauliza.

"Hapana. Hakuna mtu namsubiri. Nilifikiri labda unajua hilo tayari maana unafahamu mengi kuhusu maisha ya watu," Valentina akasema bila kumwangalia.

"Ohohooo... there it is. Nilitarajia bango. Bila shaka umenizungushia yai la adabu kwenye paper..."

Valentina akamwangalia na kutabasamu kidogo, kisha akasema, "Hapana. Umeistahili A wakati huu."

"Kweli?"

"Yeah."

"Okay... asante kwa A. Sasa hivi kweli umenitendea haki," akasema Xander.

"Sawa. Hongera. Unaandika vizuri sana," akasema Valentina na kunywa wine yake.

Xander akatambua kwamba hakuwa sawa.

"Una hasira na mimi?" akamuuliza.

"Kwa nini niwe na hasira na wewe?"

"Well... haujasema lolote kuhusu nilichoandika. Na hapa umekaa unaniambia tu hongera huku unapiga booze... sihitaji kuhofia kujikuta mtoni bila nguo asubuhi?" Xander akasema kiutani.

Valentina akashindwa kujizuia kucheka.

"Hapana sijakukasirikia. Kazi yako ilinishangaza, lakini nimekuwekea A kwa sababu umeiandika vizuri na kwa usahihi..."

"Lakini..."

"Lakini sijapendezwa nayo kwa kweli. Ilinifanya nihisi kama vile nachokonolewa sehemu nisiyotaka ichokonolewe," Valentina akafunguka.

"Sehemu gani hiyo?" Xander akasema kwa sauti ya chini kimasihara.

"Nini?"

"Namaanisha... samahani kwa kukufanya uhisi hivyo. Ila ulisema niandike kitu kwa passion kubwa. Mimi ndiyo nilichokifanya," Xander akamwambia.

"Tokea lini ulianza kuwa passionate kwangu mimi Xander?"

"Tokea... nilipoona jinsi unavyopendeza ukitabasamu," Xander akaongea kwa sauti yenye hisia.

Valentina akamwangalia kidogo, kisha akapiga ulimi wake kwa njia ya kusikitika na kutikisa kichwa. 

"Ulitolea wapi mambo yale yote?" Valentina akauliza.

"Mimi ni mwana-IT... tuna njia zetu," Xander akasema.

"Kwa hiyo unataka kuniambia vitu vyote kuhusu maisha yangu vipo kwenye intaneti?"

"Ahahah... hapana. Kiukweli mimi nina njia yangu tu ya ku-hack kwenye maisha ya mtu nikiamua. Ni kipaji tokea udogoni."

"Kuna watu hawapendi, na wanaweza hata wakakuchukulia hatua ukijulikana..."

"Najua. Lakini si unaona bado niko hapa? Sijachukuliwa hatua. Hiyo ni kwa sababu sifanyagi hivyo ovyo ovyo, na niko makini..."

Valentina akanywa kinywaji chake kidogo tena.

"Usi-mind sana madam. Nitajitahidi kuandika kilicho bora zaidi wakati mwingine, ili nistahili marks za juu zaidi," Xander akasema.

"Alama za juu kuipita A? Ni zipi hizo?"

"Uuuh... madam nilifikiri wine imekukolea, kumbe kichwa chako bado kizima!"

"Sijakasirika Xander. Nime... niliaibika tu kusema kweli. Sikufikiria kuna mtu angewahi kuyaandika maisha yangu namna hiyo," akasema Valentina kwa hisia.

Xander akamsogelea karibu zaidi. Valentina akamwangalia kimshangao kiasi.

"Usione aibu. Story yako inagusa sana. Ni inspiration kubwa kwangu, hilo sitakudanganya. Any time ukijihisi kuwa down, just remember kuna kijana mmoja anayekukubali sana... na huyo ni Xander," akamwambia kwa ustaarabu.

Nyuso zao zilikuwa zimekaribiana sana, naye Valentina akawa anaona ni kama anaongea na mtu fulani aliyezijua hisia zake vizuri sana. Akatambua kuwa Xander alikuwa kijana jasiri na aliyejua kujieleza sana. Akashindwa hata aseme nini na kubaki amemwangalia tu, kisha Xander akarudi nyuma kidogo na kumwambia angeondoka sasa, hivyo wangeonana kesho yake. Akamwacha madam wake akifikiria kuhusu alichomwambia, naye akaingia barabarani kurudi nyumbani.


★★


Sandra anafika kwao kwenye mida ya saa tatu na nusu usiku baada ya kutumia muda pamoja na mpenzi wake kule hotelini. Anawakuta mama yake, Azra, pamoja na Salome wakiwa pamoja wanaangalia TV. Anawasalimu na kuelekea chumbani kwake kubadili mavazi, kwa kuwa alioga pamoja na Raymond kule kule hotelini, hivyo hahitaji kurudia hilo tena. Akatoka chumbani kwake baada ya muda mfupi ili kwenda kukaa na wengine huko chini.

Mama yao hakuwa na shida yoyote ile watoto wake hawa kuja nyumbani usiku, isipokuwa kama hawakutoa taarifa. Sandra alikuwa ameshamwambia mapema mama yake kuwa angeenda kutembea na rafiki, hivyo uwezekano wa kuchelewa ulikuwepo. Na tena siyo kwamba labda saa tatu ni kuchelewa sana, sema kwa familia hii iliyokuwa na baba mjeshi, sheria-sheria nyingi zilikuwepo, ijapokuwa hazikuwabana sana. Wengine walikuwa wakitazama kipindi cha kiingereza chenye kuchekesha kwenye chaneli pendwa ya Azra; Nickelodeon.

"Ulienda kutembelea wapi?" Alice akamuuliza Sandra.

"Town tu. Nimeenda na rafiki yangu CBD," akasema Sandra.

"CBD? Mlienda kufanya nini kwenye hiyo hoteli?" Alice akamuuliza kiudadisi.

"Kujifurahisha tu," akajibu.

"Gharama ya hapo najua ni kubwa..." Alice akasema.

"Yeah. Rafiki yangu ana tuhela-hela kwa hiyo haikuwa na noma," akasema Sandra kwa njia ya kificho.

"Huyo rafiki yako ni nani?" Alice akamuuliza.

"Nitakuja naye siku moja umwone," Sandra akasema huku anaibana midomo yake kiutundu.

Alice akamtazama kwa macho ya kudadisi, naye Sandra akachekea kwa chini.

"Azra... nani huyo?" akauliza Sandra.

"Yupi?" Azra akauliza.

"Huy... huyo... mwenye nywele nyeupe," akamwonyesha.

"Anaitwa Kendall. Hao wengine ni marafiki zake... wanaimbaga naye," akasema Azra.

"Aaaa... sawa," akasema Sandra.

"Azra anawapenda! Yaani lazima awaangalie kila siku," akasema Salome.

Ni wakati huu wote wakasikia geti la nje likifunguliwa, na pikipiki ikaonekana inaingia.

"Xander huyo," akasema Azra.

"Mbona umemuuliza Azra huyo ni nani?" Alice akamuuliza Sandra.

"Nimemuona siku fulani nyuma kwenye mtandao... sijui kwenye simu ya mtu... kama vile ameimba na Snoop Dogg..." Sandra akataarifu.

"Eee wameimba wote! Wote yeye na kundi lake hawa Big Time Rush wameimba na Snoop Dogg... remix wimbo wa Boyfriend," Azra akasema kwa shauku.

"Hee! Unawajua hivyo?" Alice akamuuliza.

"Wote! Huyo hapo James... Kendall... Logan... na Carlos. Nampenda zaidi James..." Azra akasema.

"Kwa sababu ni handsome kuliko wote kama sikosei?" akasema Sandra.

"Man of my dreams!" Azra akasema akijishika moyoni.

Wote wakacheka kidogo.

"Siyo hata mzuri sana," akasema Salome.

"Eeeh kwanza pua yake imekaaje sijui... ki-flamingo flamingo yaani..." Sandra akawa anatania.

"Acheni wivu nyie. Hata mseme nini nimeshakufa na kuoza," Azra akasema kwa uhakika.

Wanawake wote wakacheka kwa sauti sana. Xander akawa ameingia hapo na kuwafuata wote. Azra akanyanyuka na kumkimbilia ili amkumbatie.

"Xander!" akasema kwa shauku.

"Azra... naona mnaangalia BTR," Xander akasema.

"Umeniletea?" Azra akamuuliza kwa njia ya deko.

"Pff... nisahau tena? Chukua mtoto mzuri," akasema Xander huku anampatia boksi la chocolate.

Azra akafurahi na kumshukuru, kisha akarudi kukaa kwenye sofa ili aanze kula.

"Za mechi dork?" Sandra akamuuliza.

"Nne mtungi! Dadeki! Achana na sisi kabisa," Xander akajisifu.

"Mbona haunuki jasho, nani amekuogesha?" Sandra akamuuliza kiutani.

"Bomba la mvua," akajibu Xander.

Sandra akatabasamu.

"Nafurahi kujua kwamba leo mlitoka kujifurahisha ila mnapaswa kuwa makini sana sasa hivi. Matukio mengi yanayotokea ni mabaya, anytime, anyplace..." Alice akawaambia mapacha.

"Unaongelea kuhusu Demba Group?" Sandra akauliza.

"Ndiyo," akasema Alice.

"Heee! Hao jamaa ni hatari. Wanapiga watu risasi ovyo. Yaani eti watu 28 wamekufa leo. Watu hao siyo kuku!" akasema Azra.

"Oh, nakuhakikishia mdogo wangu, walikuwa 60. Ila taarifa za habari kwa kufinya mambo hazijambo," Xander akasema kimasihara.

"Mm... hamna bwana..." Azra na Salome wakakataa.

"Anatania tu. Mmeiona ile video?" Sandra akauliza.

"Nimeiona. Hawamtaki Raisi eti. Hawa watu wanatoka hapa, wanakwenda pale, muda wowote, sehemu yoyote... ni hatari sana," Alice akasema.

"Lakini Raisi ametangaza kwenye habari kwamba watawakamata ndani ya siku chache. Ameyasema yote kwa uhakika kweli, kwa hiyo ngoja tuone," akasema Salome.

"Ndiyo... tutaona," akasema Alice.

"Itakuwa vizuri wakitangaza vyuo kufungwa tupumzike kidogo," akasema Xander.

"Hiyo haitasaidia. Inabidi tu wawakamate haraka maana tumeshaanza kuingiwa na wasiwasi na hofu kubwa mno," Alice akasema kwa uzito.

"Mambo yamezidi kuchacha. Lakini kama ni njia ya kuweka kisingizio kipya cha kukosa mambo ya muhimu... hii itakuwa happy hour kwake," Xander akasema.

Kisha akaondoka na kuelekea chumbani kwake. 

Alice na Sandra waliangaliana kwa sekunde kadhaa, wakiwa wameelewa alichosema Xander kwa njia ya fumbo. Alikuwa anamaanisha baba yake. Kwamba kwa sababu ya matukio haya yenye kushtua yaliyokuwa yameanza kutokea, ingekuwa ni sababu nyingine mpya ya kisingizio kwa Casmir kutoweza kujiunga nao kama familia; hasa kwa pindi muhimu za sherehe ya Alice na shindano la kuogelea la Alexandra. 

Wanawake hawa wawili hawakuweza kuzizuia hisia za kuvunjwa moyo kwa sababu walijua kuna ukweli kwenye maneno ya Alexander. Lakini wakajitahidi tu kuliweka hilo pembeni na kuendelea kuwa na imani.


★★★


Siku iliyofuata, mapacha wakawa wamefika chuoni kama kawaida. Sasa ilikuwa ni asubuhi ya saa 3  kwenye kipindi cha somo la Communication. CR wa madam Valentina alikuwa akizigawa karatasi za kazi aliyokuwa amewapatia kufanya juzi. Madam Valentina alikuwepo pia, akiwaelezea kwamba wengi walijitahidi na walihitaji kuongeza bidii katika suala hilo la uandishi mzuri. Alisifia zaidi kazi ya Benjamin, dada mwingine aliyeitwa Salima, na Alexandra pia, akisema waliandika kwa mtiririko mzuri sana unaostahili pongezi kubwa.

Xander alikuwa akimtazama kwa makini madam Valentina karibia muda wote. Mwalimu huyu hakuweza kujizuia kumwangalia Xander mara kwa mara na kukuta akimtazama sana, naye angekwepesha macho yake na kukazana kuwafundisha wanachuo humo darasani. Njia ya Valentina ya kumwangalia Xander ilikuwa yenye mkazo sana, kama hakutaka masihara kabisa, naye Xander alijua hiyo ni kutokana na yeye kuandika vitu vya maisha ya mwalimu huyo bila idhini yake.

Baada ya kipindi kumalizika, wanachuo wakatawanyika kila mtu kwenda mahali alikojua yeye mpaka wakati mwingine wa vipindi siku hiyo. Ramla akamwambia Xander kupitia ujumbe kuwa alihitaji sana kuwa naye leo ili wapeane mapenzi motomoto. Alikuwa anasisitiza waondoke hapo haraka kwenda hoteli yoyote ile maadamu tu alipate penzi la Xander haraka, kwa kuwa hamu ilimzidia na ilikuwa inakaribia kuisha wiki nzima tokea walipofanya mara ya mwisho. 

Xander akamwambia alipaswa kuwa na subira kidogo kwa kuwa bado alihitajika chuoni, lakini Ramla akawa analazimisha waondoke la sivyo angejisikia vibaya. Jamaa akajitahidi kueleza kwamba pindi tu ambapo vipindi vingekwisha ndiyo angekwenda pamoja naye, tena sehemu nzuri sana, lakini Ramla akaacha kutuma tena sms kwa kuudhika. Yeye pia alikuwa na hamu ya kutoka na Ramla, lakini alijua kuna mambo mengine yalihitajika kufanywa kwanza, hivyo akambembeleza (kupitia ujumbe) kuwa angempa raha nyingi leo baada ya kutoka hapo chuo.


★★


Basi, baada ya hapo Xander akawa pamoja na rafiki zake sehemu fulani za nje ya chuo wakipiga story zenye kufurahisha. Alikuwa na rafiki yake mwingine aliyeitwa Lucas, naye akiwa pamoja nao. Lucas alitambua kwamba yule "dogo," yaani Isiminzile, alikuwa amekaa sehemu fulani peke yake huku akiwaangalia sana. Akamtania Mecky kwamba dogo alikuwa anataka kuziruka naye bado kama njia ya kisasi, lakini Mecky akampuuzia tu na kuendelea na mambo yao hapo. Hazikupita dakika nyingi nao wadada wazuri Alexandra na Sophia wakawa wamefika sehemu hiyo.

Kama kawaida ya vijana wa kiume, walianza kuwasifia sana, lakini Xander akatambua kwamba kuna jambo halikuwa sawa. Sophia alionekana kama alikuwa analia, lakini akasema tu kuwa macho yalimuuma tokea alipoamka. Sandra akamwomba Xander waende pembeni ili waongee kidogo, naye akakubali upesi na kwenda pamoja nao mpaka usawa wa mti fulani mkubwa. Sophia akawa kama anamzuia Sandra asimwambie Xander jambo fulani, lakini Sandra akamwambia asijali kwa kuwa angeweza kumwamini Xander. Xander naye bila hata kujua shida ilikuwa nini, akasisitiza wamwambie tu ili aweze kusaidia.

Sandra akamwomba Xander amsaidie Sophia kwa kiasi fulani cha pesa kwa kuwa mama yake aliumwa sana kule mkoani kwao Singida, na alilazwa hospitalini tokea jana. Sophia alikuwa amepokea taarifa hizo muda mfupi nyuma, na zilikuwa taarifa nzito kwa sababu mama yake alihitaji tiba fulani haraka sana la sivyo... angekufa. Muda haungekuwa rafiki kwao, na kiwango cha pesa kilikuwa kikubwa sana. Baadhi ya ndugu zake waliokuwa huko walikuwa wanajichanga, lakini Sophia pia alihitaji kusaidia ijapokuwa hakuwa akifanya kazi.

Sandra yeye alikuwa ametumia sehemu kubwa ya pesa zake wiki chache nyuma, na mama yao hakuwa bado amemwekea kwenye akaunti yake. Kiasi alichoweza kutoa haraka wakati huu kilikuwa ni shilingi laki moja na nusu, lakini alihitaji Xander asaidie pia ili kiongezeke. 

Xander akamuuliza gharama yote ya matibabu ya mama yake ilikuwa shilingi ngapi, naye Sophia akasema kwenye laki nne. Hapo Xander akamwambia asiwaze kwa kusema kiutani kuwa alikuwa amebakiza chenji ambayo ingetosha. Lakini angehitaji kwenda kutoa kiasi cha laki tatu ATM, hivyo amsubiri hapo ili yeye aende maeneo ya mjini kumtolea na kumletea. Lakini Sandra akafikiria hivi; kwa nini wasiende pamoja huko ili aweze kuunganisha na laki moja aliyompa Sophia na kuituma pesa yote moja kwa moja? Akamwambia Sophia awataarifu ndugu zake kwamba angetuma pesa hiyo, hivyo wajiandae kuipokea na kuanza taratibu za kumtibu mama yake.

Lilikuwa ni wazo zuri, na kwa kuwa bado walikuwa na kama saa moja hivi kabla ya kipindi kingine kufuata, Xander akamwambia Sophia waondoke haraka kwenye pikipiki yake ili kwenda kukamilisha zoezi hilo. Sophia akawashukuru sana mapacha hawa kwa ukarimu wao na hata kuahidi angewalipa, naye Xander akamtania kwa kusema ole wake aache. Sophia akawa anatoa machozi ya furaha, naye Sandra akamkumbatia. 

Kisha Xander na Sophia wakaondoka ili kuifata pikipiki ya jamaa. Xander alimshika mkono wake na kutembea naye kwa ukaribu kama kumpa kitulizo cha kirafiki, huku akijaribu kumwambia mambo yenye kumfurahisha. Wakaifikia pikipiki na kupanda, Sophia akiwa nyuma ya jamaa huku amezungushia mikono yake kiunoni kwake, kisha Xander akaiondoa pikipiki hapo kuelekea katikati ya jiji. 

Hawakuwa wametambua kwamba kuanzia walipoanza kutembea pamoja mpaka kupanda pikipiki na kuondoka, Ramla alikuwa akiwatazama.


★★


Xander na Sophia walikamilisha kutuma kiasi cha laki nne na nusu kwa familia ya binti. Xander alimpatia Sophia laki moja ya matumizi yake mwenyewe, huku dada huyo akishangaa alikuwa akitoa wapi pesa zote wakati hakufanya kazi. Ndiyo hapo Xander alimwelezea kwamba wazazi wake yeye na Sandra walikuwa na kawaida ya kuwawekea pesa kwenye akaunti zao kila mwezi; hasa mama yao. 

Jambo hili la kuwekewa pesa lilianza zamani sana tokea wakiwa sekondari, hivyo mara nyingi walikuwa wanakuta pesa zimeshaongezwa tu bila kuambiwa lolote. Lakini Xander hakuwa na matumizi mengi sana ya pesa, kwa hiyo kwenye akaunti yake zilikuwemo nyingi. Sophia akaweka wazi kwamba alipenda sana aina yao ya maisha na kutamani angewahi kuishi namna hiyo, hivyo Xander akamtania kwamba asiwaze kwa sababu angemwoa wakimaliza chuo.

Kabla ya kurudi naye chuo baada ya kutoka benki, Xander akaamua kumpitisha Sophia kwenye mgahawa mzuri ili wapate chai nzuri ya haraka. Alitaka sana kumfanya rafiki ya dada yake ajisikie vizuri, na mambo haya yalimtia sana moyo Sophia. Akapendezwa hata zaidi na Xander sasa kuliko ilivyokuwa mwanzoni, kwa sababu kipindi cha nyuma alimwona kama mtu asiyejali sana. Walipomaliza mlo wao mfupi, wakarudi chuoni hatimaye.


★★


Vipindi vichache vilivyofuata viliisha saa 9 alasiri. Marafiki wa Xander walikuwa wanamshawishi kwenda pamoja naye sehemu fulani yenye fukwe ya starehe (beach) ili kujifurahisha, lakini yeye akasema alikuwa na mipango mingine kwa siku hiyo, hivyo angejiunga nao wakati mwingine. Mipango aliyosemea ilikuwa ni kumtoa "out" Ramla ili baada ya hapo atimize ahadi yake ya kupeana naye mahaba aliyokuwa anayalilia sana. Lakini kwa sababu asizozijua, Ramla hakuwa akijibu SMS wala kupokea simu yake alipompigia.

Xander akawaza labda bado alikuwa amenuna, na alijua njia rahisi ya kusuluhisha hili ilikuwa ni kumbembeleza kwa maneno mazuri, hivyo hakukata tamaa kumtafuta. Akajaribu kumuulizia kwa rafiki zake kwenye simu, na mmoja wao akamwambia kwamba Ramla alikuwa kwenye mgahawa fulani siyo mbali sana na chuo akipata chakula. Hivyo Xander akaona aelekee huko ili kuongea naye. Alizoea Ramla kuwa aina ya msichana mwenye kutaka sana "attention," hivyo kumpatia haikuwa jambo gumu sana kwake hata kama iliboa.

Baada ya kufika pale, alimkuta Ramla pamoja na rafiki yake mmoja wakiwa ndiyo wamemaliza kula ugali nyama. Huyo rafiki aliyekuwa amekaa naye, Xander alikuwa amempigia muda ule pia kumuuliza Ramla alipo, lakini akasema hajui. Sasa kuwakuta wote hapa ilimaanisha alimdanganya, lakini akaliweka hilo pembeni kwanza. Akaenda walipokaa na kuketi karibu na Ramla, kisha akazungushia mkono wake begani kwa binti.

"Mbona umenunaaa...." Xander akaigiliza wimbo fulani wa taarabu kiutani.

Ramla hata hakumwangalia, hakuonyesha itikio lolote, akautoa mkono wake begani kwake na kuanza kunyanyuka ili aondoke na rafiki yake bila kusema lolote.

"Aaaa... ndo' nini sasa? Eti jamani mama Ashura, ndo' nini?" Xander akasema huku akiongea na mama mmoja aliyefanya kazi hapo.

"Inaonekana umemuudhi," mama Ashura akasema.

"Ana mambo mengi ya kufanya. Mimi wa kazi gani?" Ramla akamwambia mama Ashura kwa kukerwa na kuanza kuondoka.

Xander akatabasamu na kumfuata nje. 

"Ramla subiri..." akamwita na kumshika mkono.

Lakini Ramla akautoa mkono wake kwa nguvu sana, kitu kilichomshangaza Xander kiasi.

"Ramla usiwe hivyo. Nimekuja sasa. Ndiyo nataka nikutoe..." akamwambia kwa kubembeleza.

"Sihitaji," Ramla akasema na kuanza kuondoka tena.

Xander akakerwa kidogo. Akamfata na kusimama mbele yake.

"Mbona unakuwa hivyo? Kwani kungekuwa na utofauti gani hata kama tungetoka muda ule na siyo sasa hivi?" Xander akamuuliza.

"Sijui," Ramla akajibu kwa njia ya kejeli.

"Badala ufurahi utapata mambo mengi kwa muda mrefu, we..."

"Kwani uliyatunza wiki nzima kwa ajili yangu au huyo malaya wako?" Ramla akamkatisha.

"What?" Xander akashangaa.

"Ukikaa eti ooh... subiri kwanza, utachelewa kurudi hostel, kuna vipindi, visa visa tu vya uwongo kumbe unakisugua hicho kimlingoti kingine!" Ramla akasema kwa ukali.

"Unaongelea nini?" Xander akawa haelewi.

"Acha kujishaua Xander. Tumekuona unaondoka na yule rafiki ya dada yako," akasema rafiki ya Ramla.

"Sophia? Ahahahah... kwa hiyo mkafanya team up ya kunizingua kwa sababu mmeniona naondoka naye? Unajua nilikuwa nampeleka wapi?" Xander akamuuliza Ramla.

"Utajua mwenyewe," Ramla akasema na kutaka kuondoka, lakini Xander akamzuia.

"Ramla sikia, tuache utoto..."

"Mtoto mwenyewe!" Ramla akasema.

"Kwa hiyo mimi kuondoka na Sophia ndiyo kumekukasirisha? Kuna jambo la muhimu nilikuwa nimeenda..."

"Si ndiyo ulikuwa umeenda naye maana yeye ni wa muhimu sana! Mimi nilipokwambia mapema tuondoke, ukasingizia vipindi. Lakini nusu saa baadae vipindi vikawa siyo vya muhimu tena, except kwa mtu mwingine ambaye alikubana kiunoni vizuri sana wakati mmepanda pikipiki," Ramla akatoa madai yake.

"Ndiyo unahitaji kunisikiliza kwanza. Usikurupuke bwana. Sophia..."

"Hajakurupuka, anakwambia ukweli," rafiki yake Ramla akamkatisha.

"Aisee, we demu nitakuzingua. Hayakuhusu haya, kwo' ondoka hapa," Xander akamwambia kwa hisia kali akiwa amemnyooshea kidole.

"Hamna haja ya jazba baba. Ukweli sikuzote unauma," rafiki huyu akamwambia hivyo Xander.

"Unasemaje? Nitakukata kofi sasa hivi na hayo ma-make up yako kama mavi ya bata usoni! Toka hapa!" Xander akamfokea.

Kakaendelea kujisimamisha kwa kiburi. Ramla sasa akaona Xander alikuwa amekasirika, na sikuzote alijua akikasirika hilo halingekuwa jambo zuri. Lakini akaendelea kujifanya yuko sahihi sana.

"Umpige kwa nini? Kama unataka kupiga mtu nipige mimi," Ramla akasema.

Mama Ashura pamoja na wengine kutoka mgahawani kwake wakawa wamesogea hapo kujua nini kiliendelea.

"Xander kijana wangu, nini tatizo?" mama Ashura akauliza.

"Hakuna tatizo wala," rafiki ya Ramla akajibu.

"Nimekuuliza wewe?" mama Ashura akamwambia.

"Samahani mama. Hakuna shida kubwa. Kazi njema," Xander akamwambia mama Ashura na kuanza kuondoka akiwa ameudhika.

Ramla kuona hivyo, akaanza kumkimbilia na kumsimamisha.

"Kwa hiyo unaenda wapi? Unarudi kwa mtu wako siyo?" Ramla akaendelea kumkasirisha tu.

"Unataka kuamini unachoamini, amini hicho hicho. I don't care anymore," Xander akamwambia na kuanza kuondoka.

"Xander... Xander!" Ramla akaita kwa sauti, lakini jamaa hakugeuka hata mara moja.

Sasa binti akabaki tu kujiuliza nini kingefuata. Kihalisi alikuwa anajaribu kuonyesha umuhimu wake kwa mwanaume aliyempenda, lakini njia hii ikawa imemponza. Alishindwa kuelewa kama ni Xander ndiyo mwenye makosa au ni yeye. Lakini bado alimpenda na hangetaka waachane kabisa, kwa hiyo kwa kiasi kikubwa akaanza kujilaumu moyoni.

Xander aliudhika kwelikweli. Alirudi mpaka pikipiki yake ilipokuwa na kuondoka chuoni hapo upesi sana. Alikuwa anawaza jinsi huyo msichana alivyomtendea kwa dharau, naye hakupenda hata kidogo. Tatizo la wanawake kama yeye ni kwamba wanajali zaidi maoni yao kuliko kusikiliza maoni ya wengine, na ndiyo maana wanapoelewa jambo kwa njia tofauti na ukweli halisi, inakuwa ngumu kuwaelewesha kwa sababu HAWASIKILIZI. Akapata wazo la kuwapigia rafiki zake kuwauliza ikiwa walikuwa wameshakwenda kule "beach," hivyo akasimama sehemu na kumpigia Lucas.

Baada ya rafiki yake huyo kumwambia walikuwa ndiyo wanaelekea huko, Xander pia akasema angefika huko muda si mrefu, kwa kuwa alitaka kwenda nyumbani kwanza kubadili mavazi. Akarudi mwendoni tena baada ya kumaliza kuongea na Lucas.


★★


Sandra alikuwa ameshafika nyumbani kwao kutokea chuo muda fulani nyuma. Alikuwa ameamua kurudi na kukaa tu nyumbani kwa leo, kwa sababu alihisi uchovu baada ya kutumia muda fulani kufanya mazoezi ya kuogelea kule chuoni. Sasa alikuwa sebuleni ameketi huku ana-chat na Raymond. Ndani alikuwepo Salome tu, kwa kuwa Azra alibaki shuleni kwa ajili ya masomo ya ziada mpaka saa 11 (kama tuition), na mama yao alikuwa kazini bado.

Baada ya muda mfupi akaona geti likifunguliwa na pikipiki ya Xander ikiingia. Akaendelea kuchat na mpenzi wake, akimsubiri kaka yake afike ndani. Baada ya Xander kufika, Sandra akamwomba aende mpaka alipo ili waongee.

"Nambie Sandra, sina muda mrefu... naingia beach," Xander akamwambia.

"Unaenda na nani?" Sandra akauliza.

"Na washkaji..."

"Kupekenyua bikini za wake wa watu au siyo?"

"Ebwana ndiyo..."

"Ahahahah... haya sawa. Nilikuwa nataka kukushukuru tena kwa kumsaidia Sophia leo," Sandra akamwambia.

"Si mmeshanishukuru, inatosha..."

"Hapana Xander, niko serious. Ulichokifanya leo... kimenigusa moyo sana. Nashukuru kwa kumsaidia rafiki yangu. Nimeona ni kama umenisaidia mimi..." Sandra akasema kwa hisia.

"Usijali sister. Nimefurahi kusaidia pia," Xander akamwambia.

Sandra akatabasamu. Xander akashusha pumzi kwa njia iliyomwambia Sandra kwamba kuna tatizo.

"What's wrong?" akamuuliza.

"Aagh... nahitaji ku-clear kichwa changu kidogo. Huu mchana haukwenda vizuri kama nilivyotarajia," akasema Xander.

"Kwa nini? Nani amemzingua my baby brother?" Sandra akasema kiutani.

"Ahahah... ni Ramla. Ameniudhi sana..."

"Kisa?"

"Sophia..."

"Nini? Sophia amemfanyaje?"

"Hmm... muda ule... tulivyoondoka alituona. Anafikiri ninatoka naye eti..."

"Ish! Girlfriend wako ana matatizo gani?"

"Yaani hata sielewi. Af' njia aliyotumia kuongea na mimi sikuipenda yaani imenifanya nihisi kama vile ananidharau kweli. Na kale karafiki kake kanajifanya kana nyodo! Amenikata deep sana leo..." Xander akasema.

"Ulimwambia kilichokufanya uende Benki na Sophie?"

"Mwanzoni nilikuwa kidogo nimwambie, ila baadae sikuona haja maana alinidis sana. Halafu sidhani kama ingekuwa sahihi kuongelea maisha ya Sophia na kila mtu, kwa hiyo nafurahi sikumwambia..."

"Pole mwaya..."

"Usiwaze..."

"Kwa hiyo... ndiyo mmezinguana kabisaaa?"

"Agh yaani hata sielewi. Nataka nipotezee hilo kabisa leo..."

"Mh... hmmm. Ramla anajua sana kukera. Anyway najua mtayanyoosha tu mambo yenu. Asante sana kwa leo Xander," Sandra akarudia kutoa shukrani kwa mara nyingine.

"Ondoa shaka Sandirito..."

"Ahahah... Sandi-nini? Unaharibu jina langu bwana..."

"Ahahahah... kama Condorito!"

"Sitaki uniite hivyo tena... ever!"

"Ahahahah... bado huwa najiuliza ilikuwaje kifupi cha jina lako kuwa Sandra badala ya Xandra... ili iendane na Xander," Xander akamwambia.

"Watu walizoea tu hivyo I guess. Kwanza Xandra isingependeza. Me nilikuwa napenda sana mnifupishie jina langu kuwa Lexi, lakini mazoea yameshawapa tabu," Sandra akasema.

"Lexi wa TVD eeh?" Xander akauliza.

"Nampenda huyo dada!" Sandra akasema.

"Ahahahah... haya bwana. Ngoja me niende. Ushanipotezea nusu saa nzima," Xander akasema na kupanda kuelekea juu.

Sandra alibaki kwenye sofa akicheza na simu yake viganjani mpaka Xander alipotoka huko na kumuaga kuwa anaelekea beach. Akasema ikiwa mama yao angefika kabla hajarudi, basi amwambie kwa niaba yake alikokuwa. Sandra hakuwa na kipingamizi na kumwacha pacha mtu aende kujifurahisha.


★★


UPANDE WAKE CASMIR


Meja Casmir Eliakim Sona, baba ya mapacha hao wawili, alikuwa amezama kwenye tafiti mbalimbali kuhusiana na mambo yaliyotokea Mwanza na Kigoma kwa kusababishwa na kundi la Demba Group. Alikuwa akisoma njia walizotumia kutoroka kwa umakini sana, na kuna jambo likaonekana kama haliko sawa. Kila jambo walilofanya watu wa kundi hili halikuwa sawa, lakini kilichomsumbua ni JINSI walivyoyafanya. 

Kwa kusaidiana na Kapteni Kendrick, rafiki yake wa karibu, walifikia mkataa kwamba kundi hili lilikuwa na watu wenye mafunzo ya hali ya juu, kwa sababu walijua vizuri jinsi ya kuingia sehemu, jinsi ya kutoka, njia za kutumia, muda waliopaswa kutumia, na hata kuwachengua maaskari na kuwafanya waonekane duni sana. Kwa hiyo kama walikuwa wanatakiwa kuwakamata watu hawa, walipaswa kwenda na njia bora zaidi ya kuwachengua vizuri na wao, siyo kichwa kichwa kwa sababu tu walikuwa wanajeshi.

Walipangilia mbinu mbalimbali za kuweza kuwasaidia kufanikisha hili, kisha wakachagua wanajeshi wenye ustadi wa hali ya juu kuweza kufanya kama upelelezi wa ndani zaidi kwenye baadhi ya maeneo waliyoona huenda yangepatwa na janga lingine kama Mwanza na Kigoma. Kwa kuwa bado hawakuwa wameambiwa kuanza kazi moja kwa moja, walifanya hivi kisiri ili kutosubiri amri ambayo huenda ingechelewa, na hili ndilo lililomfanya Casmir awe mahiri sana kwa sababu alichukua hatua za muhimu kuhakikisha mipango inafanikiwa hata kama hakupewa amri za moja kwa moja.

★★

Baada ya muda fulani, wawili hawa wakapokea taarifa kuhusu magari sita ya kijeshi yenye masanduku ya silaha, zilizokuwa zinaelekea kwa wanajeshi mkoani Arusha. Kapteni Kendrick ndiye ambaye sikuzote alitoa kama kibali kuruhusu yapite kwenye sehemu ambazo yangesimamishwa ili kuangalia kila kitu kiko sawa. Wakati akitaka kutoa ruhusa, kuna jambo likaingia kwenye akili ya Casmir. Akamzuia kwanza Kendrick, kisha akarudi kuangalia aina za risasi ambazo zilitumiwa na kundi la Demba Group kuwaua maaskari na watu wale wengine kule Mwanza.  

Baada ya kuthibitisha, akamwomba Kendrick waongozane pamoja kuelekea huko ili aangalie jambo fulani. Hii ilimshangaza Kapteni Kendrick kidogo kwa sababu hakujua nia ya Meja wake kufanya hivi ilikuwa ni nini, lakini akatii na kutuma ujumbe kuwa magari hayo yasimamishwe kwanza ili yeye afike kwanza hapo. Kwa kuwa hawakuwa mbali sana na eneo hilo, ingewachukua kama dakika 30 za kuendesha gari upesi ili kufika.

Wakiwa njiani, Kendrick alimuuliza Casmir alikuwa anataka kuangalia nini, naye akajibu kwamba kuna kitu fulani aliwaza ambacho hakuwa na uhakika nacho sana, na huko wanakoenda ni kwenda kuhakiki. 

★★

Walipofika maeneo hayo, waliyakuta magari hayo makubwa yakiwa yameegeshwa kwa kufuatana pembeni ya barabara kwenye kiwanja kidogo kisichokuwa na makazi. Mbele ya magari hayo kulikuwa na gari nyingine ya kijeshi, na hapo palikuwa na wanajeshi wengine 9; wakionekana kusubiria wakuu hawa wafike. Baada ya Kendrick na Casmir kuegesha gari lao sehemu hiyo, wakashuka pamoja na kusalimiwa kwa saluti za heshima na wanaume hao; walioonekana kuwa makini ndani ya sare zao za kijeshi.

Watatu kati ya hao 9 ndiyo walikuwa wakiongoza msafara huu wa silaha, hivyo wakawaambia Meja na Kapteni kuwa kila jambo lilikuwa sawa kabisa, na haikutokea shida yoyote. Meja Casmir akasema kwamba alitaka kuangalia masanduku ya silaha hizo, hivyo wakamwongoza kuelekea nyuma ya gari moja na kufungua sanduku kubwa lililotengenezwa kwa mbao nzito. Casmir aliweza kuona bunduki za kivita na mabomu ya kurusha humo, na mjeshi mmoja aliyeongoza msafara huu akamwambia kwamba kwenye kila sanduku kulikuwa na silaha nyingi tofauti-tofauti zilizopangwa vizuri kama hivyo.

Casmir akaulizia kama aina ya bunduki ambazo zilibeba risasi za aina ile waliyouliwa wale watu zilikuwepo, lakini bila kuwaambia moja kwa moja kuhusiana na jambo hilo. Wakamwambia kuwa zipo; kwenye gari la mwisho. Akawaomba waende kumwonyesha, nao wakatii. Lakini wakati walipokuwa wanalielekea, gari nyingine ambayo waliweza kuitambua kwa urahisi kuwa ya kijeshi ikafika hapo pia na kuegeshwa. Wakaiangalia kwa umakini sana, kisha akashuka mwanaume mtu mzima ambaye hakuwa mgeni machoni mwao.

Huyu alikuwa ni Luteni Weisiko (Lieutenant). Mwanaume mwenye mwili mkubwa wa mazoezi, mwenye sura isiyotaka mchezo hata kidogo. Cheo chake kilifata cha Kapteni Kendrick; yaani kwa vyeo vikubwa kutoka kwa Jenerali mpaka kwa Luteni Kanali, alifata Meja, Kapteni, halafu ndiyo huyu Luteni. Wote hawakuwa wameutarajia ujio wake hapo, hivyo wakabaki kumtazama alipoanza kuwaelekea pamoja na wanajeshi wengine wawili waliokuwa pamoja naye.

Wale wanajeshi wa msafara wakamsalimu Luteni Weisiko kwa saluti, naye pia akawasalimu kwa saluti ya heshima, hasa kuwaelekea Meja Casmir na Kapteni Kendrick. 

"Luteni... habari za muda?" Casmir akamuuliza.

"Ni nzuri Meja," Luteni Weisiko akajibu kirafiki.

"Ulikuwa unaelekea wapi?" Kendrick akamuuliza.

"Oh... nowhere in particular. Nimewaona tu hapa ikanibidi nisogee kusalimu," Weisiko akasema.

"Naona bado kimombo unapenda kukitwanga vizuri," Kendrick akasema kiutani.

Yeye na Weisiko wakacheka kidogo. Lakini Casmir alikuwa anamtazama kiudadisi.

"Aam... kwa ajili ya batalioni hizo eeh? Zinaelekea wapi?" Weisiko akauliza.

"Ni masanduku tu yanaingia Arusha, hakuna mizinga hahah... Tumeona kuja na sisi kuwasalimu vijana hawa mara moja," Kendrick akamwambia.

"Aaa inspection kidogo," Weisiko akatamka.

"Yeah, kidogo," Kendrick akamjibu.

"Bila shaka vijana wamehakikisha kila kitu kiko poa. Au kuna shida boys?" Weisiko akauliza wanajeshi wa msafara wa silaha.

"Hapana mkuu. Kila kitu kiko sawa," akajibu mmoja.

"Inaonekana hakuna haja ya ku-check. Me pia nilihakikisha mambo yote yanakuwa swadakta. Vipi mkijiunga na sisi? Tulikuwa tunaelekea kupata nyama choma. Kapteni nakumbuka unapenda mbuzi nyama choma. Nakununulia nzima upige yote," Weisiko akasema.

"Ahahahah... ni muda mrefu umepita kijana wangu. Itakuwa jambo zuri sana," Kendrick akamwambia.

"Meja... unaonaje?" Weisiko akamuuliza Casmir.

"Ni sawa. Lakini ngoja kwanza," Casmir akasema.

Kisha akageuka na kutoa ishara kwa mwanajeshi wa msafara kuwa afungue moja ya masanduku yale aliyosema kuna aina zile za bunduki. Baada ya mwanaume huyo kulifungua sanduku hilo kubwa, wote wakashangaa sana baada ya kukuta sanduku hilo liko tupu! Mwanajeshi huyo alionekana kuchanganyikiwa, naye akaanza kuwauliza wenzake silaha zilizokuwa humo zimekwenda wapi. Wenzake wakaanza kupekua na masanduku mengine, lakini yote yalikuwa na silaha ndani yake. 

Kapteni Kendrick aliwauliza kwa ukali silaha hizo zilikuwa wapi, nao wakasema labda kuna tatizo lilitokea kwenye upakiaji huko nyuma, kwa hiyo huenda sanduku hilo lilikuwa tupu tokea mwanzo nalo likachanganywa pamoja na mengine pia. Wakaomba radhi kwa hitilafu hiyo na kuahidi kuwa makini zaidi, naye Kapteni Kendrick akawaamuru waondoke eneo hilo haraka sana.

"Ah... yaani vijana hawa! Wanakosa kuwa makini kwa vitu vya namna hii halafu wanajiona wako juu kweli. Samahani sana Meja kwa hilo," Kendrick akamwambia Casmir.

"Hapana usijali. Kama walivyosema... inaonekana ilikuwa hitilafu," Casmir akaongea hivyo na kumwangalia Luteni Weisiko.

"Okay wakuu. Kwa hiyo... mtajiunga nasi?" Luteni Weisiko akawauliza tena.

"Hapana. Kuna sehemu tunaelekea kwanza. Na... jitahidi kutotumia muda mwingi kwenye starehe Luteni. Hatari ziko nyingi... popote pale," Casmir akamwambia.

Luteni Weisiko akamtazama kwa sekunde kadhaa, kisha akapiga saluti ya heshima pamoja na wenzake wawili, nao wakaaga na kuondoka hapo. Sasa wakawa wamebaki Casmir na Kendrick peke yao.

"Cas, kuna tatizo gani? Nimetambua ulikuwa serious sana, na... hatuna mpango wa kwenda popote. Unafikiria nini?" Kendrick akamuuliza.

"Kuna kitu fulani chenye utata kinaendelea Ken. Aina ya silaha walizotumia Demba Group kuua watu Kigoma na Mwanza ndiyo aina ya silaha ambazo hazikuwepo kwenye hilo sanduku. Hizo tu," Casmir akasema.

"Kwa hiyo... unataka kusema kwamba Demba Group wameziiba hizo silaha? Hiyo hai-make sense. Wangeiba masanduku mengi, siyo moja tu," Kendrick akasema.

"Ndiyo hai-make sense. Lakini umeshawaza kuwa labda... wamepewa?" Casmir akauliza.

"Nini? Na nani?" 

"Nitajuaje Ken? Siku chache baadaye utasikia tena watu Arusha au Singida au kokote wameuliwa na hawa watu, na kama sikosei, silaha zitakuwa ni za aina hiyo hiyo. Sisemi kwamba nina uhakika kuna mtu anawapa, ila..."

"Ni jambo linalo-make sense," Kendrick akamalizia.

"Yeah."

"Kwa hiyo inawezekana kuna mtu kutoka jeshini anashirikiana nao. Na kuchagua aina moja ya silaha ambazo watatumia... wanakuwa makini sana. Kila mara mzunguko wa silaha ukifanywa, wanapokea silaha hizo ambazo zinafikiriwa kuwa hazikuwekwa. Meja... wanatengeneza kikundi cha kivita!" Kendrick akamwambia kwa hisia za mshtuko.

"Ken, Ken, tulia... hatuna uhakika. Ni assumption tu ambayo..."

"Inaweza kuwa ya kweli! Vipi kama ni mmoja wa hao wanajeshi tuliowaacha waondoke sasa hivi?" Kendrick akauliza.

"Hapana Ken. Siyo wenyewe. Walikuwa tayari kutuonyesha bila kusita kabisa. Lakini..."

"Lakini?"

"Luteni Weisiko..."

"Nini kuhusu Weisiko?"

"Ametokea tu out of nowhere, all of a sudden anataka tukale nyama choma. Sijui sana, lakini... sijapenda hiyo hali," Casmir akasema ukweli.

"Lakini kijana ni mwaminifu sana huyo. Namjua kwa sababu na mimi nilisaidia kumkocha... unafikiri anaweza kuwa anahusika na hili?"

"Sina uhakika Kendrick. Kama nilivyokwambia ni assumption tu. Kufika kwake hapa ghafla kumewasha taa nyekundu kichwani kwangu. Fikiria alivyojikanyaga kwa kuuliza msafara unaenda wapi, halafu tena akasema amehakikisha mambo yamekwenda swadakta. Ni kama alikuwa hataki nilifungue hilo sanduku," Casmir akasema kwa mkazo.

Kendrick akabaki kimya akitafakari mambo hayo.

"Hii ishu ya Demba Group iko deep. Tunahitaji kuwa werevu sana juu ya hili," Casmir akasema.

"Unafikiria tumwambie General Pingu?" Kendrick akauliza.

"Hapana, bado kwanza. Tuchunguze mambo haya kisiri zaidi ili tuthibitishe. Then tujajua ikiwa kweli Demba Group ni kundi la waasi washenzi, au waasi wenye akili... na aliye nyuma yao ni nani," Casmir akasema kwa uzito.

Wawili hawa wakarejea kwenye gari lao na kuanza safari ya kurudi kule walikotoka baada ya mambo hayo yaliyotokea.

★★★★★★★★★

 ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Previoua Next