FOR YOU
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
Rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA TANO
★★★★★★★★★★★★★
Xander anaanza kurejea nyumbani kwenye mida ya saa 2 usiku baada ya kutoka kujifurahisha na rafiki zake. Angalau kufikia wakati huu alikuwa amechangamka zaidi na kutomwaza Ramla hata kidogo baada ya kitendo alichokuwa amemfanyia mchana huo. Mpaka wakati huu, bado mwanadada huyo hakuwa amemtafuta, naye Xander ndiyo kwanza hakuwa na habari naye.
Wakati alipofika maeneo ya mgahawa ule wa kifahari ambao alimpeleka Ramla siku chache nyuma, aliweza kuliona gari aina ya IST yenye rangi ya silver hapo nje, na upesi akafikiria kwamba huenda lilikuwa ni la madam Valentina. Alijua mwalimu wake huyo alipenda kuja hapo, hivyo akaona ahakikishe kama gari lilikuwa ni lenyewe ili ikiwezekana akamsalimu huko ndani. Hawakuzungumza kabisa leo chuoni kwa kuwa ilionekana ni kama madam bado hakujisikia vizuri kuhusu jambo alilomfanyia kwenye kazi ile; hata kama alipata A.
Baada ya kufika na pikipiki nyuma ya IST hiyo, akawa amehakiki kuwa ndiyo yenyewe kwa kuangalia namba za usajili, kisha akaiegesha pikipiki yake karibu na hapo pia, naye akaelekea kule ndani. Kama kawaida, alimkuta madam Valentina akiwa kwenye meza yake ile ile ambayo alikuwa amekaa siku ile. Alikuwa mwenyewe tu hapo, huku sehemu zingine zikiwa na watu mbalimbali waliofurahia milo na vinywaji. Akaelekea mpaka hapo na kumshika begani akiwa nyuma yake.
Valentina akageuka na kuachia tabasamu hafifu la kirafiki. Hii ikamfanya Xander ajihisi ahueni kwa sababu sasa haikuonekana kama madam wake ana kinyongo naye.
"Alexander... unafanya nini hapa?" akamuuliza.
"Nilikuwa napita nikakuona... nikaona nije nikusalimie," Xander akajibu.
"Ooh... nilifikiri ulikuja na girlfriend wako," Valentina akasema.
"Hapana. Mh? Kumbe siku ile ulimwona?" Xander akauliza.
"Siku gani?"
"Kwani ni nini kimekufanya uniulize hivyo?"
"Aam... nimekuona leo pamoja naye. Mlikuwa kama mnagombana sijui au vipi... kwa hiyo' nikafikiri umemleta hapa..."
"Aaaa... ulikuwa wapi wakati huo?"
"Pembeni tu..." Valentina akasema kimkato, kisha akanywa 'wine' yake kwenye glass.
Xander akamtazama kwa sekunde kadhaa, kisha akauliza, "Naweza kukaa na wewe?"
"Ndiyo. Karibu. Lakini ni lazima uagize kitu ule," Valentina akasema.
"Sawa. Niagizie," Xander akasema huku akiketi.
"Huwa unapenda nini?"
"Nyama."
"Mhm... haya," Valentina akasema na kuita mhudumu.
Xander alikuwa anamwangalia tu kwa umakini sana. Valentina akamwagizia nyama nusu ya kukaangwa na kinywaji, kisha mhudumu akaondoka.
"Ulikuwa unatokea wapi?" Valentina akauliza.
"Beach."
"Aaaa... okay."
"Na wewe... ulikuwa unatokea wapi?" Xander akauliza.
"Sina sehemu maalumu nayokuwa. Mimi ni mvivu kupika. Kwa hiyo hii sehemu ndiyo jikoni kwangu napokuja kupata msosi..."
"Ahahah... sawa. Nimekorofishana na girlfriend wangu leo kwa hiyo nahitaji kujifurahisha angalau. Sipendi stress," Xander akamwambia.
"Kupata stress inamaanisha unampenda sana..."
"Ah! Siyo kivilee. Ana miosho na swaga ambazo mara nyingi huwa zinanikera, lakini ananielewa sana ndiyo maana bado niko naye. Ila... hata kama angesema azingue uzi wetu, ningeichomoa sindano fasta," Xander akasema kiutani, naye Valentina akacheka.
"Una maneno wewe! Kama tu kwenye uandishi wako," Valentina akamwambia.
"Asante. Nilikuwa nahofia labda bado ulikasirishwa, sorry... hukupendezwa saana na kazi ile... kupita maelezo yaani..."
"Hapana wala usiwaze. Nilipenda. Ilinigusa. Ilikuwa ni kama ulitegesha camera ndani ya maisha yangu yote," Valentina akamwambia.
"Ila najua nilienda mbali sana. Kiukweli, nilikuwa najaribu kukufanya uone kwamba ninajua vitu vingi... lakini sasa hivi natambua hiyo haikuwa adabu wala heshima. Sikutakiwa kufanya vile. Samahani kwa hilo..." Xander akamwambia kwa hisia.
"Ahah... sawa. Haina shida. Unajua... labda ni kweli. Labda nilikasirika. Ila unajua ni kwa nini? Ni kwa sababu katika mambo yote ambayo uliandika... kuna jambo fulani hukuliweka. Ulifanya hivyo makusudi si ndiyo?" Valentina akauliza.
"Madam V..."
"Nataka uniambie. Niambie sasa hivi..."
"M..madam V sidhani kama..."
"Please... tell me. Please..."
Xander akaangalia chini kihuzuni kidogo, kisha akashusha pumzi kidogo.
"Ulikuwa... ulikuwa na mtoto. Alikufa siku hiyo hiyo uliyojifungua," Xander akamwambia bila kumtazama.
Valentina akanywa wine yote ya kwenye glasi kwa kishindo. Alikuwa akijikaza asitoe machozi.
"Hivi ulifanya nini mpaka ukajua mambo haya yote?" akamuuliza kwa sauti ya chini.
Xander akamwangalia. "Nilitafuta kupitia kwenye website zenye bio za faculty member wa chuo kwa somo lako, social media pia... nikapata taarifa nyingi kuhusu maisha yako ya zamani na marafiki, umri wako, unakoishi..."
"Hadi tattoo yangu," Valentina akamkatisha.
Xander akatazama pembeni.
"Lakini ukaacha kuandika kuhusu hili lingine. Kwa nini? Ulifikiri kwamba nitaumia sana? Au kwamba nilikuwa najaribu kusahau kila kitu kibaya kilichonipata maishani? Kwamba unaweza kuyaandika maisha yangu kwa njia ambayo WEWE unataka yawe?" Valentina akasema kwa hisia.
"Siyo hivyo. Madam V... nilikuwa tu najaribu ku..."
Xander akakatishwa na mhudumu aliyefika hapo akiwa na sahani liyojaa nyama na kinywaji kwa ajili ya Xander. Xander aliweza kumwona Valentina akijifuta chozi kwa uharaka, naye akamwonea huruma sana. Kisha ghafla Valentina akanyanyuka na kubeba mkoba wake. Akamwambia Xander kwamba yeye angeondoka sasa, hivyo kijana abaki kufurahia msosi wake. Lakini alipotaka kupiga hatua kuondoka, akayumba nusu kuanguka, ila mhudumu pamoja Xander wakawahi kumshika mwili wake.
"Madam V uko sawa?" Xander akamuuliza kwa kujali.
"Ndiyo niko sawa. Rudi ukae..." akajibu huku akijisawazisha.
Xander akatambua kwamba ile wine aliyokunywa kwa kishindo ilimgonga kichwani vibaya. Valentina akaanza kuondoka hapo taratibu, akitembea kwa umakini ili asianguke. Xander alijua kuwa hapo lazima shida ingetokea kwa sababu Valentina alihitaji kuendesha gari, na hali hii aliyokuwa nayo haikufaa. Akamwambia mhudumu amfungie mboga yake vizuri ili aondoke nayo, naye akampatia pesa bila kujali chenji. Alimwomba aharakishe ili aweze kumwahi Valentina, na mhudumu huyu akafanya upesi.
Baada ya kuchukua chakula chake akatoka haraka na kufika mpaka sehemu ambayo Valentina aliegesha gari lake. Akamkuta akiwa amesimama kando ya mlango akitaka kuufungua. Akamwahi na kumshika mkono.
"Madam V... huwezi kuendesha. Nafikiri wine imekuingia vibaya..." akamwambia.
"Niko sawa Alexander. Usiku mwema," Valentina akasema na kuanza kuweka funguo sehemu ya kufungulia mlango.
Xander akaona jinsi alivyohangaika kuiingiza kiusahihi, na ni wazi alikuwa anaona vitu mara mbili-mbili.
"Madam V... utaanguka. Huwezi kuendesha. Na mimi siwezi kukuruhusu," Xander akamwambia.
"Wewe kama nani?" Valentina akamuuliza.
Xander akabaki kumwangalia tu jinsi alivyomtazama kwa mkazo. Aliona sasa mwanamke huyu alikuwa na hisia nyingi sana zilizovurugika. Lakini pamoja na hayo yote, asingeweza kumwacha tu afanye jambo hili ambalo huenda lingemsababishia matatizo. Valentina akafanikiwa kuufungua mlango, lakini Xander akazikwapua funguo kutoka kiganjani mwake na kuanza kumvuta mkono kuelekea upande wa pili wa gari. Valentina alikuwa anajivuta na kumfokea kuwa amwachie, lakini Xander alimzidi nguvu na kufungua mlango wa pembeni wa mbele, kisha akamwingiza kwa lazima akae.
Mambo haya yote yalimuudhi sana Valentina kwa sababu aliona ni kama kijana huyu anavuka mipaka. Xander akaufunga mlango na kuzunguka mpaka upande wa usukani na kuingia hapo, kisha akai-lock milango yote baada ya kuwasha gari bila hata kumwangalia madam wake usoni. Valentina alikuwa anamtazama kwa ukali, naye akamwambia alizime haraka sana la sivyo angemshtaki. Lakini kijana akaweka wazi kuwa hiyo ingekuwa hasara kwake kwa sababu ni yeye ndiye aliyetaka kuendesha gari huku akiwa amelewa.
"Sijalewa!" Valentina akakanusha.
"Okay... umelewa-lewa kwa mbali," Xander akamwambia.
"Unanipeleka wapi? Kwangu unapajua?"
"Ndiyo. Baada ya ile research yote, najua hadi namba yako ya nyumba..."
"Acha upuuzi Alexander, nitakuja kusema kuhusu huu ujinga kwa wazazi wako!" Valentina akamtishia.
Xander akamwangalia na kusema, "Sawa tu. Tutawaambia nilikuteka."
Valentina akakunja uso wake kimshangao.
Xander akaligeuza gari kutoka hapo na kuingia barabarani, akiwa ameiacha pikipiki yake nje ya eneo lile la mgahawa.
★★★
Mida hiyo hiyo, Meja Casmir, akiwa sehemu yake ya kupumzikia, anapigiwa simu na Kanali Jacob Rweyemamu, ambaye anamtaarifu kuwa anapaswa kwenda kwenye jengo la ofisi za kijeshi siku ya kesho; yeye pamoja na Kapteni Kendrick. Jambo hili linamshangaza kiasi, naye anauliza kuna jambo gani huko, lakini Kanali anamwambia tu Meja kwamba anapaswa kufika kesho pamoja na Kapteni, yote watayajua huko huko.
Casmir akaonyesha heshima na kutii agizo hilo. Kanali Jacob akamwambia kwamba amtaarifu Kapteni Kendrick mapema ili kesho kufikia mida ya mchana wawe wamefika huko. Casmir akamtafuta Kendrick kwa simu na kumwambia kuhusu hilo. Hata na yeye pia alishangaa kwa sababu walitakiwa kuacha sehemu zao za kazi ghafla tu na kwenda huko. Lakini akamwambia haikuwa na shida, naye angeanza matayarisho mapema ili kesho asubuhi waweze kuondoka mapema kwa pamoja.
★★★
Xander alimwendesha Valentina na kumfikisha mpaka nje ya nyumba yake. Tokea walipoondoka kule, hawakusemeshana lolote lile ndani ya gari hili. Xander akamtazama usoni madam wake, akiwa anataka kumuuliza ikiwa itakuwa sawa kwenda kumfungulia geti lake na kuingiza gari ndani. Lakini akahisi hilo lingekuwa swali la kipuuzi, maana hakuhitaji ruhusa kumlazimisha kuja pamoja naye. Ni kwamba alikuwa tu anataka kumsemesha lakini akakosa la kusema.
Hivyo, akauchukua mkoba wa madam wake na kuupekua, akitafuta funguo zingine. Alipata tano zilizounganishwa sehemu moja, naye akatoka na kuelekea getini. Valentina alikuwa anamtazama kwa makini sana, akiwa ameudhika pia, lakini akamwacha tu kwa kuwa Xander alijiona kuwa mjuaji sana. Xander akafanikiwa kufungua mlango mdogo wa geti na kuingia kwa ndani, kisha akalifungua geti lote pia. Akarejea kwenye gari na kuliingiza mpaka ndani, na baada ya kushuka akarudi kulifunga geti tena.
Nyumba aliyoishi Valentina ilikuwa ya kupanga, yaani nyumba yote aliilipia ili aishi hapo. Ilikuwa kubwa na pana kiasi, iliyozungushiwa uzio uliokaribiana na kuta za nyumba yenyewe. Ndani ya uzio wa nyumba, kulikuwa na sehemu ndogo ya kuegeshea gari lake kabla ya kuingia kule ndani kabisa. Ndani kabisa, kulikuwa na mpangilio maridadi wa vitu; mlango wa kuingilia kwenye sebule pana kiasi iliyokuwa na meza kubwa nyeusi katikati, huku pembeni kukiwa na masofa marefu ya aina moja yaliyozunguka kona zote za sehemu hiyo, na ukutani TV kubwa ya flat screen. Sehemu ya jikoni iliyotunza vyombo pia ilikuwa kwa mbele, na korido fupi upande mwingine lililoelekea kwenye vyumba vitano; chake, viwili kwa ajili ya wageni, kimoja kilichogawanywa kuwa bafu kubwa na choo, na kingine alichotumia kama ofisi yake ndogo iliyojaa vitabu na vifaa vyake vingi. Sakafu lote lilikuwa la vigae, na palikuwa pasafi sana. Alikuwa akiishi na msichana wake wa kazi hapo kipindi fulani nyuma, lakini baadae akamwachia aondoke kwa kuwa alitaka kubaki peke yake tu.
Akiwa ameanza kurudi alipoegeshea gari, akakuta Valentina akiwa ndiyo anatoka ili aelekee ndani. Xander akamwambia kwamba yeye angerudi tu nyumbani sasa, lakini hakujibiwa. Valentina akaelekea mpaka kwenye mlango wa kuingilia ndani ya nyumba na kuufungua, na ni hapa Xander akakumbuka nyama ile aliyotoka nayo kule mgahawani. Akaiwahi kwenye gari na kuitoa, kisha akamfata na kumwambia aichukue. Lakini Valentina akawa kama hamsikii vile, naye akaingia tu ndani bila kumjali kijana huyu.
Xander akahisi hatia kiasi kwa sababu alikuwa ametoka kumwomba samahani usiku huo huo kwa sababu ya kutenda bila adabu kumwelekea, lakini tena sasa ikaonekana ni kama amerudia yale yale. Ijapokuwa hakukosea sana zamu hii, alijua Valentina alikuwa tu amevurugika, hivyo lolote ambalo kijana angefanya lingekuwa baya tu machoni pa mwanamke huyu.
Kutoka hapo aliposimama baada ya Valentina kuingia ndani sekunde chache tu, Xander akasikia sauti kama ya kilio, na kwa haraka akatambua ilikuwa ni Valentina. Akakimbia ndani upesi na kumkuta sehemu ya korido lile fupi, akiwa kama amekaa chini kwa kupiga magoti, huku akijishika mguuni. Usiku huu alikuwa amevalia gauni nyeupe na nyepesi tu ya maua-maua, na chini vilikuwa viatu virefu. Xander akatambua kwamba alikuwa ameanguka, naye akawahi hapo chini kumsaidia.
Valentina alikuwa amekunja sura kiasi kwa kuwa mguu wake uliteguka kidogo baada ya kiatu alichovaa kusababisha aanguke, lakini hasa kwa sababu alihisi kizunguzungu kwa mbali. Xander akamsadia kunyanyuka na kumpeleka sehemu ile ya sebule, kisha akamkalisha kwenye sofa na kuanza kuinyoosha sehemu ya mguu wake iliyoteguka. Mwanzoni Valentina alikuwa akitoa sauti za maumivu, lakini baada ya muda fulani akaacha kwa sababu Xander alimpa "massage" nzuri sana.
"Bado unauma sana? Tutumie dawa ya kuchua. Una dawa ya kuchua humu ndani?"
Xander akauliza hivyo bila kumtazama huku akiendelea kuugeuza-geuza mguu taratibu. Valentina hakumjibu, bali akawa anamtazama tu kwa umakini. Xander aliponyanyua uso wake kumwangalia na kukuta anatazamwa namna hiyo, naye akabaki kumwangalia tu machoni mwanamke huyu mwenye sura ya kuvutia. Utizami ambao Valentina alimpa Xander, ulimfanya kijana huyu apoteze mawazo mengine yote na kukaza akili yake yote kwa mwanamke huyu tu.
Bila hata kutambua haraka aliingiliwa na nini, Xander akajinyanyua taratibu na kuketi karibu naye kwenye sofa, na sasa wakawa wanaangaliana kwa ukaribu sana. Kwenye akili ya Valentina, alijua moja kwa moja jambo hilo lilikuwa linaelekea wapi, lakini ni kama akaamua kuacha aone ikiwa lingefika huko.
Xander alikuwa amepandwa na hisia kali sana kumwelekea mwanamke huyu, naye akamshika usoni kwa kiganja chake, wakiwa wanatazamana kwa njia fulani kama vile ni watu ambao hawajuani, kisha akaifata midomo ya madam bila kusita na kuibusu kwa juu. Ilimchukua ujasiri fulani kufanya hivyo, kwa sababu kichwani kwake alikuwa ameshajiwekea wazo la kwamba huenda madam angemzingua, lakini bado akafanya hivyo.
Busu yake ya kwanza kwa mwanamke huyu ilikuwa kavu tu, kisha akambusu tena mara mbili huku madam Valentina akiwa kama anajirudisha nyuma. Lakini Xander akaendelea kulazimisha tu, na sasa Valentina akailegeza midomo yake kidogo na kuruhusu Xander aanze kumbusu kimahaba sana. Pumzi za Valentina zilikuwa nzito na miguno ya mbali ikaanza kusikika, lakini akawa kama amerudiwa na ufahamu na kumsukuma Xander kidogo.
Xander akawa anamwangalia kwa hamu sana huku wote wakitoa pumzi zenye presha kubwa. Valentina alikuwa anamwangalia kwa njia iliyoonyesha kama hakupendezwa na hilo.
"Alexander... nafikiri itakuwa vyema ukiondoka..." akamwambia.
"Lakini... madam V..."
"No! Tafadhali ondoka..." Valentina akasema kwa uthabiti.
Kisha akanyanyuka na kuanza kutembea akichechemea kuuelekea mlango. Xander hakutaka kukubali kwamba huu ndiyo ungekuwa mwisho, kwa sababu kuna vitu aliweza kuhisi wakati anambusu mwanamke huyu. Alihisi uhitaji wake mkubwa wa kupewa kitulizo, lakini alikuwa anajaribu kujizuia. Akanyanyuka haraka na kumwahi pale tu Valentina alipokuwa ameufikia mlango na kushika sehemu ya kuuvutia. Akafika nyuma yake, karibu sana, kisha akaushika mkono huo kama kumzuia.
Valentina akashtuka kidogo. Akamhisi vyema Xander nyuma yake, jinsi alivyoigusanisha miili yao.
"Alexander... unafanya nini?" akauliza kwa wasiwasi.
"Shhhh... relax madam V. Just... relax," Xander akasema kwa sauti ya kunong'oneza.
Hapo hapo Valentina akahisi shingo yake ikipewa busu laini kwa midomo ya Xander. Akasisimka sana na kutaka kugeuka kwa nguvu, lakini Xander akamdhibiti.
"Alex... Alexander sst... stoop... no..."
Valentina akawa anaendelea kukataa huku Xander akiendelea kumbusu shingoni mwake. Xander alitumia mkono wake mmoja kuubana vyema mwili wa Valentina kwake, huku mwingine akiutembeza kuanzia tumboni kuelekea mpaka usoni kwa mwanamke huyu. Valentina alianza kupata hisia za juu sana, na pumzi zake zikawa zikitoka kwa njia iliyothibitisha hilo.
Mambo yakazidi kupamba moto pale Xander alipoanza kushika sehemu zenye kukoleza hisia hizo hata zaidi kwenye mwili wa mwanamke huyu. Vizuizi alivyokuwa ameanza kutoa vikapungua, na sasa akawa amefumba macho tu akimwacha Xander amtawale, akitoa miguno ya juu juu ya pumzi. Kisha Xander akapeleka mchezo huu hatua nyingine wakiwa bado mlangoni hapo. Alipenda sana jinsi madam alivyoonyesha kufurahia kile alichopata, naye akaona aongeze manjonjo hata zaidi.
Akaanza kutembea kuelekea kwenye masofa akiwa amembeba, kisha akaendelea kumpatia penzi kisawasawa mwanamke huyu. Valentina alikuwa amenyanyua miguu hewani kama mbuzi aliyetoka kuchinjwa, akitoa vilio vya raha huku ameubana mgongo wa Xander kwa nguvu sana. Madam akalegea kupita maelezo, akawa anaongea maneno yasiyoeleweka na hata kumpiga vibao Xander kwa nguvu, lakini kijana akakazana tu. Kisha baada ya dakika kadhaa wote wakawa wameridhishana na kutulia kwenye sofa hilo.
Hiki ni kitu ambacho Xander alikuwa akihitaji sana leo, na alifikiri angekipata kwa Ramla, lakini akamzingua. Ila hakutegemea kama angeweza kukipata kwa mwanamke huyu, aliyemzidi umri, na ambaye hakujua ikiwa angeweza kuja kurudia naye jambo hilo tena kwa sababu mambo yote yaliyotokea hapa yalifanikishwa na msaada kidogo wa wine aliyokunywa madam. Akabaki akipumua kiuchovu kiasi, huku madam Valentina akiwa amefumba macho na kupumua kilegevu pia.
Xander akashindwa afanye nini. Alibaki kumtazama tu, kisha akajinyanyua na kuchukua boxer yake pale chini, naye akaitumia kumfuta Valentina. Alipomtazama tena, akatambua kwamba Valentina alikuwa amesinzia. Akawaza huenda alihisi uchovu sana; jumuisha na wine aliyokunywa. Akasogea mpaka karibu na uso wake, kisha akambusu kidogo mdomoni. Akamnyanyua kwa nguvu na kumbeba mikononi mwake, kisha akatoka sebuleni hapo kuelekea vyumbani; akitafuta kimoja ambacho angetambua ni cha kwake.
Hii ilikuwa ngumu kidogo kwa sababu Valentina alikuwa na uzito kiasi ijapokuwa hakuwa mnene, na kuzunguka naye mikononi kulichosha, lakini kijana akajikaza. Baada ya kuingia kwenye chumba cha madam, akamlaza kitandani, kisha akamfunika kwa shuka na kuondoka. Alikuwa bado hajavaa suruali kwa chini, hivyo akarudi sebuleni kule na kuivaa bila boxer, na baada ya kuangalia simu yake, akakuta missed call kadhaa kutoka kwa mama yake.
Akamtumia ujumbe mfupi mama yake kumjulisha kwamba alikuwa njiani kurudi nyumbani, hivyo akaharakisha kuondoka hapo ikiwa ni saa 6 usiku sasa. Aliamua kuchukua funguo ya ziada ya geti la nyumba hii ili aufunge mlango mdogo wa geti kwa nje, naye akaacha ujumbe kwenye simu ya madam Valentina kumwambia kwamba amefanya hivyo, kwa hiyo yeye angetumia funguo nyingine akitaka kuondoka asubuhi (Valentina), halafu kesho Xander angempatia hii huko chuoni.
★★
Ilimchukua kama nusu saa kufika kwao, kwa sababu alipotoka kwa madam Valentina alihangaika sana kutafuta usafiri, na baada ya kuupata akaenda mpaka kwenye sehemu ile aliyoacha pikipiki yake na kuikuta bado iko pale, kisha ndiyo akaenda nyumbani. Alimkuta mama yake akiwa bado hajalala, naye alimuuliza sana sababu ya yeye kutomwambia alipokuwa mpaka usiku hivyo. Haingekuwa na tatizo kutoka hata kama angeenda kulala na rafiki zake, lakini sikuzote Alice alipenda kupewa taarifa.
Xander akamwomba samahani na kumwahidi kwamba haitajitokeza tena, sema kwa siku hii alijisahau. Baada ya Alice kumwambia waliweke suala hili pembeni, Xander akamuuliza maandalizi ya sherehe yake ya siku ya kuzaliwa yalikwendaje, naye Alice akasema mambo yalikuwa yanakwenda vizuri.
Xander akasema alihisi uchovu sana, hivyo Alice akamwacha aende kupumzika, naye angeenda kulala baadae.
Xander alifika chumbani kwake na kujitupia kitandani, akianza kuyarudia kichwani mambo yaliyotokea nyumbani kwa Valentina. Alianza kuikumbukia sura yake, mwili wake, miguno yake, jinsi alivyomng'ang'ania sana wakati alipokuwa akimpa penzi murua, naye hakuweza kujizuia kutabasamu kwa kuhisi raha sana.
Muda haukupita mwingi sana na usingizi ukamjia hapo hapo.
★★★
Asubuhi na mapema sana, Meja Casmir pamoja na Kapteni Kendrick waliondoka kutoka sehemu zao za kikazi kwa kuelekea kwenye jengo la ofisi za kijeshi kwenye kambi yao baada ya kupewa mwito huo wa ghafla na Kanali Jacob Rweyemamu. Ofisi hizo zilikuwa kwenye jiji lile lile ambalo familia ya Casmir na Kendrick zilikuwa pia, hivyo Kendrick aligusia uwezekano wa wawili hawa kwenda kwa familia zao kutoa salamu pia. Lakini Casmir akamwambia walipaswa kwanza kujua walichoitiwa ni nini, ndiyo mambo mengine yangefuata.
Walikuja kufika jijini hapo kwenye mida ya saa 6 mchana na moja kwa moja kuelekea kwenye kambi ile yenye jengo la ofisi za wanajeshi. Nyumbani kwa Casmir kulikuwa upande tofauti na maeneo hayo kwa umbali mrefu kiasi. Walikuwa wamekuja pamoja kwa kutumia gari la Casmir, wakiwa wamefikiri kwamba wangerudi kule walikotoka pamoja tena.
Baada ya kufika nje ya kuta zilizozunguka jengo lile kubwa na pana, walikaribishwa na baadhi ya wanajeshi wenye vyeo vya chini yao kwa heshima kubwa, kisha wakaambiwa kwamba Kanali Jacob Rweyemamu alikuwa akiwasubiri ndani ya ofisi yake kuu. Bila kukawia wakaanza kuelekea huko huku wakiangalia na mazingira ya eneo hilo. Kulikuwa na uwanja mpana eneo la nje lenye sehemu mbalimbali ambazo walitambua zilitumiwa kwa ajili ya mazoezi. Pia kulikuwa na majengo madogo madogo kwa ajili ya wanajeshi waliokuwa hapo, na sehemu za pembeni za kuta zilizozungukia majengo haya kulikuwa na wanajeshi wenye silaha wakilinda.
Ndani ya jengo baada ya kuwa wamefika, waliweza kuona jinsi lilivyopangiliwa vizuri kwa kuta imara na vyumba kadhaa ambavyo bila shaka vilikuwa na matumizi maalumu hapo ya kiofisi; yaliyoshughulika na masuala ya usalama wa taifa. Walifika mpaka kwenye mlango wa ofisi ya Kanali, na baada ya Kanali Jacob kutaarifiwa kwa simu kuwa wamefika, akaomba waingie upesi. Wawili hawa wakaingia kwenye ofisi yake na kukuta akiwa ameketi kwenye kiti chake mbele ya meza yenye makablasha kadhaa, nao wakatoa heshima kwa kupiga saluti.
"Meja... Kapteniii! Aah... ni muda sana hatujaonana!" Kanali Jacob akasema kwa shauku kubwa.
Wawili hao wakashusha mikono yao kutoka kichwani na kumtazama pia. Kendrick alikuwa anatabasamu kwa furaha baada ya kumwona Kanali amewaonyesha shauku ya urafiki, ikimaanisha hakukuwa na shida; naye Casmir akawa anamtazama kwa njia ya kawaida tu.
"Kanali Jacob... ni kitambo," akasema Kapteni Kendrick.
"Ah sana! Naona sasa hivi hadi una kitambi!" Kanali Jacob akamwambia Kendrick.
"Ahahahah... siyo kama chako," Kendrick akasema.
"Hahahah... and look at you... Major Casmir! Ah, jina lina nguvu sana hilo," Kanali akamsifia.
Casmir akatoa tabasamu hafifu na kusema, "Asante Kanali."
"Bila shaka mnajiuliza ni kwa nini nimewaita ghafla. Kuna jambo ninataka kuongea nanyi vijana wangu," akasema Kanali.
"Kanali, niite tu mimi kijana. Nywele nyeusi za Meja zisikudanganye ameficha mvi kwa chini," Kendrick akatania.
Kanali Jacob akacheka na kuuliza, "Kwa hiyo hastahili kuitwa kijana?"
"Haswaa!" Kendrick akasema.
Casmir akatabasamu na kumwangalia Kendrick huku akitikisa kichwa.
"Sawa sawa. Nina... nafahamu mmepewa mission ku-deal na Demba Group muda si mrefu sana," Kanali akasema.
Wote wakasema ndiyo.
"Na bila shaka mmeshaanza kusaka mambo mengi kuwahusu, kwa kuwa najua vizuri Meja ni mtekelezaji wa mambo kama haya discretely sana. Nilikuwa nahitaji kujua mmefikia wapi wakati huu," Kanali akawaambia.
Kendrick akamtazama Casmir, naye Casmir akamwangalia pia.
"Kuna jambo lolote zito linaendelea?" Kanali akawauliza.
"Aam... kwa heshima yote mkuu, ni kwamba nilipatiwa kazi hii moja kwa moja kutoka kwa Jenerali...."
"Jenerali Pingu. Ndiyo najua. Na najua unachotaka kusema ni kwamba taarifa unatakiwa kumpatia yeye kupitia njia aliyokuagizia utumie. Well, hiyo ndiyo sababu nimewaita hapa. Ni kuwataarifu kwamba kuanzia sasa mimi ndiyo nitakuwa nampatia taarifa hizo Jenerali, kwa hiyo mambo yote ambayo mnayapata yanapaswa kupita kwangu ili niyawasilishe kwake," Kanali Jacob akawaambia.
Wawili hawa wakatazamana kwa kifupi, kisha wakamwangalia tena Kanali.
"Kwa hiyo mambo tuliyoyapata tunatakiwa kukuambia kwanza si ndiyo?" Kendrick akauliza.
"Ndiyo," Kanali Jacob akajibu.
"Mbona mambo yamebadilika haraka? Taarifa tungetakiwa kumpa Luteni Kanali, halafu azifikishe kwa..."
"Ndiyo, lakini sasa hivi zitakuwa zikipita kwangu. Oswald amepata mgawo mpya, hiyo ndiyo sababu," Kanali akaeleza.
"Aaaa..." Kendrick akaonyesha kuelewa.
"Yeah. Kwa hiyo, mmefikia wapi?" Kanali Jacob akauliza kwa mara nyingine tena.
"Well... Meja ameongoza operesheni ya kuanza kuwasaka kisiri watu hao, na mpaka sasa tumepata vigezo kadhaa ambavyo vinaweza kutuongoza kuwatambua haraka. Tunajua bado amri haikuwa imetolewa lakini... tuliona ni bora kuanza mapema," akasema Kendrick.
"Haina shida. Ni kwenye mikoa gani?" Kanali akauliza.
"Hatuna uhakika sana, lakini macho yetu hasa yako mikoa ya Arusha, Singida na Dodoma. Ila tunajitahidi kuongeza force na maeneo mengine," akajibu tena Kendrick.
Kanali Jacob akatikisa kichwa kuonyesha ameelewa, naye Casmir akawa anamtazama kwa makini sana. Akili yake aliijua yeye mwenyewe.
"Okay sawa. Hakuna jambo lingine lolote ambalo nahitaji kujua?" Kanali akauliza.
"Well... jana kuna jambo fulani lilitokea..."
"Siyo muhimu sana," Casmir akamkatisha Kendrick.
Wote wakamtazama.
"Nimetoka kusema kwamba natakiwa kujua kila kitu. Kwa hiyo MIMI ndiyo nitaamua kama ni muhimu au siyo muhimu sana. Kendrick... sema," Kanali akaongea kwa mkazo.
"Jana kuna silaha hazikukutwa kwenye sanduku moja kati ya mengi wakati zinaelekea Arusha, na zilikuwemo bunduki na mabomu yaliyofanana na zile ambazo Demba Group walitumia. Tulifikiri tu ni ajabu kidogo..." akasema Kendrick.
"Mmmm. Wewe Meja unalionaje hili?" Kanali akauliza.
Casmir akatulia kidogo, kisha akasema, "Kama nilivyosema, siyo muhimu sana kwa sababu inawezekana tu hilo sanduku walisahau kuliwekea silaha."
Kendrick akamtazama Casmir kimaswali kidogo.
"Kwa hiyo hakuna jambo lolote mnalohisi haliko sawa na tukio hilo?" Kanali akawauliza.
Casmir akawa wa kwanza kukanusha, naye Kendrick akaona akanushe pia.
"Basi sawa. Hiyo haina haja ya kufika popote kwa kuwa kama ulivyosema, siyo muhimu. Ninawahamishia post zenu sasa. Mtakuwa huku badala ya kule kwa wiki nzima," Kanali Jacob akasema.
Wote wakashangaa.
"Unamaanisha nini Kanali?" Kendrick akauliza.
"Ohoo usijali Kapteni. Namaanisha nawapatia ofisi maalumu hapa kwa wakati huu ambao ni wa muhimu kwa Meja Casmir. Kwa hiyo mnaweza kuendelea kufanyia utafiti wenu mkiwa hapa na kutuma maagizo mnakohitaji," akasema Kanali Jacob.
"Wakati wa muhimu? Sijaelewa kikamili Kanali," akasema Casmir.
"Ninafanya hivi kwa ajili yako Meja. Ninafahamu kutakuwa na birthday ya mke wako wiki hii, tena siku mbili tu zimebaki. Naelewa haujawa na muda mwingi ku-spend na familia yako, na baada ya kuona ni jinsi gani hii mission ingekubana, nikaamua nikusogeze huku ili uweze kuhudhuria. Hakutakuwa na haja ya kuhamahama... wewe na Kapteni mtakuwa na ofisi zenu hapa, then baadae mwaweza rudi kule... kama mtachagua kufanya hivyo. Au mnaonaje?" Kanali Jacob akawaambia.
Kendrick alimtazama Casmir akiwa anatabasamu kwa furaha, naye Casmir alikuwa akishangaa na kutabasamu kwa wakati ule ule.
"Lakini... lakini..." Casmir akashindwa kuendelea.
"Kanali, hilo pigia mstari. Tuko tayari kuhamia huku. Nashukuru sana kwa ufikirio huu," akasema Kendrick.
"Haina shida. Ni muhimu kujali hali za ma-comrade wenzangu. Lakini nina ushauri kwako Casmir..." akasema Kanali Jacob.
"Ndiyo Kanali..." akajibu Casmir.
"Vipi uki...fanya kama surprise? Bila shaka mke wako atafurahi sana. Usimwambie kwamba upo huku tayari, ili ufike tu siku hiyo paap! Atarukaruka eeh..." akasema Kanali.
Wote wakacheka kwa pamoja, huku Casmir akihisi furaha mpya moyoni mwake.
"Sijui niseme nini Kanali..." Casmir akanena.
"Asante tu itatosha," Kanali Jacob akasema.
"Ahah... asante sana. Ninakuahidi nitakupatia Demba Group kama zawadi," akasema Casmir huku akipiga saluti.
Kendrick pia akapiga saluti.
"Sawa kabisa. Kumbukeni, mambo yote tunayafanya kisiri ili kuwapata hawa jamaa kabla hawajaufikisha mwiba mbali sana kwenye koo zetu. Nina imani tutashinda," Kanali akasema.
"Ndiyo Kanali. Tutashinda," akajibu Kendrick.
"Okay. Sasa mnaweza kwenda. Mtaonyeshwa ofisi zenu ambazo ziko tayari. Karibuni sana," Kanali akawaambia na kuwapigia saluti huku akiwa ameketi.
Wawili hawa wakapiga saluti pia kwa mara nyingine tena, kisha wakatoka kwenye ofisi hiyo.
Kanali Jacob Rweyemamu, akiwa ameweka sura yenye umakini sana baada ya wawili hawa kuondoka, akachukua simu yake na kupigia namba fulani, kisha akaanza kwa kusema, "Hallo... ndiyo... mnaweza kuendelea..."
★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★
Comments