Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

FOR YOU

Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa

Rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SITA

★★★★★★★★★★★★★


Meja Casmir pamoja na Kapteni Kendrick walipotoka ofisini humo, Kendrick alikumbuka kwamba kidogo kwenye maongezi yao mule ndani ni kama Casmir alikwepesha mambo kuhusiana na silaha zile kuibiwa. Akaona amuulize ni kwa nini hakumwambia Kanali yale aliyoyafikiria jana.

"Sikuona umuhimu tena. Labda nilifikiria mambo mengi kupita kiasi," akasema Casmir.

"Hapana bwana, ile ilikuwa ni discovery muhimu sana. Hatuwezi kuupuuza uwezekano wa yale yote kuwa kweli. Vipi kama kuna mtu jeshini anawasaidia hawa nyoko group kupata silaha? Tunapaswa kumwambia Kanali kuhusu hilo," akasema Kendrick.

"Lakini ndiyo hivyo Captain, hatujui ni nani hata kama ingekuwa kweli. Vipi kama ni Kanali mwenyewe halafu unamwambia hayo?" Casmir akasema.

"Aaaaa Meja..."

"Nime-assume tu. Namaanisha hatuwezi kuwa na uhakika sana, ndiyo maana inabidi tuchimbe zaidi..."

"Okay nimekuelewa. Lakini najua umerukaruka kwa furaha moyoni kwa sababu sasa unaweza kwenda nyumbani tena... kwa uhakika zaidi..."

"Ahahahah... yeah. Unajua... hii yote bado inanishangaza. Jenerali Pingu huwa... habadiliki-badiliki namna hii. Halafu... Kanali amejuaje kuhusu birthday ya mke wangu?" Casmir akaanza kudadisi.

"Umeona sasa? Umeshaanza kuwaza mbali kama kawaida yako. Hapo utaacha kuwafatilia nyoko group ili ujue ikiwa Kanali anamnyemelea Alice," Kendrick akamtania.

"Ahahahah... siyo hivyo bwana. Imenishangaza, that's all. Yaani..."

"Umefurahi sana, I get that. Kwa hiyo utamficha Alice kuhusu wewe kuwa huku mpaka birthday kama Kanali alivyo-suggest?"

"Hapana. Hapana Kendrick yaani, siwezi kusubiri. Nahitaji kumwambia mke wangu aisee..."

"Ila ngoja. Unajua ukimwambia kwamba uko huku tayari anaweza akakulazimisha uache masuala ya huku ili uende kuonana naye kwanza. Na najua jinsi anavyokuwaga akidekadeka, lazima utasahau na mission ili tu ukale tunda ohooo..."

"Ahahahah... dah! Kiukweli nimemiss sana hizo deko zake. Uko sahihi lakini. Nahitaji kuchagua wakati mzuri."

"Yeah. Mimi pia nitakuwepo. Natamani Margaret angekuja pia," akasema Kendrick.

"Iih! Hivi kumbe bado... huwa unawasiliana na huyo mwanamke wa Ghana? Si uliniambia uliachana na habari zake?" Casmir akauliza.

"Ndiyo, mwanzoni ilikuwa kama hit and run..."

Casmir akacheka.

"Lakini baadae akaja kuniambia kwamba alinipenda sana. Sema... mimi na mambo yangu mengi, na umbali pia kutoka huko aliko toka alivyoondoka... lakini huwa ananiambia hajanisahau na anatamani sana tuwe pamoja... akanifanya nianze kuwaza labda yeye ndiyo ananifaa zaidi, kama wewe na Alice... nikafikiria..."

"Basi, basi... inatosha. Nimeelewa. Umempenda, lakini wewe bado ni Playboy," Casmir akasema.

"Mimi siyo Playboy!" Kendrick akakanusha.

"Ahahahah... sawa. Ila... mambo mengine pembeni kwanza... tunahitaji kwenda kuendelea na mission. Wacha tuone layer zetu mpya hapa..." Casmir akasema.

Kendrick akakubali, kisha wote wakaelekea sehemu ambayo wangepata mtu wa kuwaelekeza mpaka kwenye vyumba vya ofisi zao mpya.


★★★


CHUONI


Ikiwa ni mida ya saa 7 mchana, ukawa ni wakati wa Xander pamoja na rafiki zake kusubiri kipindi kingine cha somo ambalo lingefuata mida ya saa 8. Akiwa ameketi kwenye mabenchi yale pamoja nao kama kawaida, akamwona Isiminzile akiwa amesimama chini ya kivuli cha mti mwembamba tu wa ua fulani pembezoni mwa kuta za uzio wa kuzunguka jengo la chuo. Alikuwa peke yake, akiwatazama yeye na rafiki zake hapo. Benjamin akamtania Mecky kwamba "dogo" bado anam-mind, hivyo ajiandae maana muziki wake angeusikilizia puani. Mecky akasema "dogo" hana lolote huyo na huwa anamkera sana, hivyo kama ni kumwalika hapo ili aje amkarabati vizuri, basi wamwite.

Xander akanyoosha mkono wake kumwelekea Isiminzile na kumwonyesha kwa ishara kuwa aende hapo. Mwanzoni, kijana huyo alionekana kutoamini kwamba Xander alimwita yeye, lakini baada ya Xander kusisitiza, akaanza kwenda walipokuwa. Mecky akamuuliza alikuwa na maana gani kufanya hivyo, naye akamwambia ndiyo alikuwa anamwita ili aone kama atampiga kweli. Akamwonya kuhusu kumtendea kijana wa watu bila heshima, naye Isiminzile akawa amefika.

Bernard, Benjamin, Hussein, Lucas, na Xander, wote walimsalimu kirafiki kijana huyu, naye akawasalimu pia. Xander akamwambia aketi pamoja nao ili wajuane vizuri. Isiminzile alijihisi utofauti sana kwa sababu hiki ni kitu ambacho hakuwa ametarajia kabisa. Marafiki wa Xander wakawa wanamuuliza maswali na kumfanya azungumzie kuhusu mambo aliyojua, nao wakatambua kwamba alikuwa na ujuzi sana.

"Yaani uko course ya Human Resources lakini masuala ya magari na mapikipiki ndo' unajua hivyo?" akauliza Lucas.

"Ndiyo. Ninapenda kusoma mambo mengi kuhusiana na magari... motor vehicles yaani..." akajibu Isiminzile.

"Si ungesomea uinjinia wa magari?" akauliza Benjamin.

"Nilitamani sana ila... haikuwezekana..." akajibu huku anaangalia chini.

Xander akaona abadili mada.

"Okay. Tuambie hapa chuoni ni demu gani unayemkubali kuliko wote," akasema Xander.

Wenzake wakacheka huku wakimwambia Isiminzile aseme. Mwanzoni alikuwa akiona aibu, ila baada ya kusisitizwa sana akafunguka.

"Yupo hivi... mweupe... mrefu mfupi kiasi, ila siyo sana... huwa ni mwislamu anavaaga ushungi..." akawa anawaambia.

"Anaitwa nani?" Hussein akamuuliza.

"Ramla Jabir..." akajibu.

Wote wakaanza kucheka, kasoro Isiminzile. Alikuwa anashangaa kwa nini wanacheka.

"Oya, oya, kaa ukijua starehe gharama..." Mecky akaanza kutania.

"Ahahah... mtoto Ramla? Unamkubali kinoma eeh?" Bernard akamuuliza Isiminzile.

Isiminzile akaangalia chini tu.

"Dah mwanangu competition hii hapa... kazi kwako..." Lucas akamwambia Xander.

"Ahahah... unampenda Ramla? Si mko wote Human Resources?" Xander akamuuliza Isiminzile.

"Ndiyo... ila yule dada hawezi kutoka na mtu kama mimi..." Isiminzile akasema.

"Kwa nini asitoke na wewe?" Hussein akamuuliza.

"Kwanza ananizidi umri, na... anaonekana wa pesa sana, halafu..."

"Mmmm wewe... nani kasema? Yule demu anaweza kutoka na yeyote yule. Haangaliagi pesa, demu wa hivyo anaangalia kama unajua show vizuri na swagger... basi. Hupaswi kuwa mnyonge hivyo, yule unakula mbona!" Lucas akamwambia.

"Kweli?" Isiminzile akauliza.

"Kabisaaa!" Bernard akapigia mstari.

Xander alikuwa kimya tu anawaangalia rafiki zake walivyomfanya kijana wa watu aonekane kama mjinga.

"Sasa sikia. Huyo demu atakuja hapa muda siyo mrefu. Akifika tu tunakuunganisha kwake, sawa?" Lucas akamwambia.

Isiminzile akaanza kusema hapana maana alimwogopa.

"Wewe tulia, yule ni rafiki yetu. Tena rafiki wa Xander. Atakuunganisha kwake. Au siyo jembe?" Lucas akazidisha chumvi.

"Haya, mchumba kafika..." Mecky akasema.

Wote wakatazama pembeni na kumwona Ramla akiwa anakuja na rafiki zake wengine wanne. Wawili walikuwa ni wapenzi wa Benjamin na Hussein pia. Xander alihisi kama kuishiwa pozi kwa kuwa bado alikumbuka jinsi Ramla alivyomrushia maneno bila kuwa na uhakika wa madai yake siku ya jana. Lakini bado mtoto alimwelewa sana jamaa, naye hakutaka kumpoteza hata kama angehitaji kumpigia magoti mbele ya wengine. Na hapa alikuwa amekuja kuthibitisha kwamba bado alimpenda sana.

"Ramla huyooo..." Lucas akamsifia alipofika.

Wadada hawa wakasalimiana na washkaji kisha story zikaanza.

"Mnamwona huyu? Huyu ndiyo pedeshee mpya hapa... mpeni respect!" akasema Lucas kwa mabinti.

"Eeh jamani Isiminzile... vipi?" mmoja akamsalimu.

"Safi," Isiminzile akajibu kwa haya.

"Nampendaga huyu kaka, mpole kweli," akasema dada mwingine huku akimshika Isiminzile begani.

"Unaona unavyopendwa?" Lucas akamwambia Isiminzile.

Ramla alikuwa anampa jicho la wiziwizi Xander ili kuona kama bado alikuwa na hasira naye. Alitarajia hata angemwangalia na kutabasamu lakini hakufanya hivyo. Kisha....

"Ramla mtoto mzuri, tuna jambo letu dogo hapa... hapana, ni kubwa sana tunataka kukuambia," akasema Bernard.

"Ropoka," Ramla akasema.

"Tumepata pedeshee mwingine zaidi ya yule mwenye sura ya mbuzi anayekukubali kinoma sana," Lucas akamwambia.

Xander akachekea kwa chini.

"Nani tena?" akauliza Ramla.

Isiminzile alikuwa anataka kukimbia kwa kuwa aliogopa sana, lakini akajitahidi kuzuia hisia zake na kujikakamaza hapo hapo alipokaa.

"Ila mshenga aliyetumwa ni Xander, kwa hiyo yeye ndo' atakwambia kuhusu pedeshee wetu," akasema Benjamin.

Ramla tayari aliweza kukisia maongezi haya yangeelekezwa kwa Isiminzile, lakini hakujali kumhusu; yeye alitaka kuona ikiwa Xander angemsemesha. Tokea walipogombana hawakutumiana ujumbe hata mara moja.

"Xander, mwambie..." Benjamin akasema.

Xander akamwangalia Ramla kwa ufupi, kisha akazungushia mkono wake begani kwa Isiminzile na kusema, "Isiminzile anakupenda sana Ramla. Toka alipojiunga na darasa lenu, hakuna mwanamke yeyote ambaye ametaka kuwa naye ila wewe. Mpe moyo wako."

Rafiki zake wote wakacheka sana. Isiminzile bado hakuelewa kilichowachekesha hasa kilikuwa ni nini, lakini Ramla hangechelewesha kumpatia jibu. Akatoka alipokuwa amesimama na kwenda mpaka alipoketi Xander, kisha akamkalia na kumpiga denda bila aibu yoyote. Wenzake wakaanza kuguna, huku Isiminzile akishangaa sana.

"Mmmm jamani... siyo vizuri hivyo Ramla," akasema rafiki yake.

"Nimeshanasa hii sehemu, sing'oki. Dogo akapambane na hali yake," Ramla akawaambia huku akiwa bado amemshika Xander.

Isiminzile akakaa kwa kutulia tu, akiigiza kwamba hilo lilikuwa ni kawaida. Wengine wakaendelea kuwatania Xander na Ramla kwamba waliyafanya mapenzi yao kuwa ya hadharani sana mpaka ilikera. Kihalisi Xander hakufurahishwa na kitendo ambacho Ramla alifanya, hasa kwa sababu ni kama hamu yote kumwelekea ilimwishia, lakini aliona afanye tu ustaarabu wa kutomwaibisha mbele ya rafiki zake. Benjamin akamweka wazi sasa Isiminzile kuwa Ramla alikuwa mpenzi wa Xander, hivyo walikuwa wakimtania tu, na alipaswa kumwona kama rafiki yake pia.

"Usimkalie muda mrefu, Oprah akija hapa... ehee..." rafiki yake Ramla akamwambia, akimaanisha mwalimu wa nidhamu.

Ramla akasimama tena, zamu hii akiwa nyuma ya Xander huku ameweka mikono yake begani kwa jamaa. Alifanya ionekane ni kama hawakuwa na tatizo lolote kabisa. Isiminzile alijisikia vibaya sana. Wengine wakaendelea na story, lakini yeye akawa kimya tu kwa sababu hawakujua kihalisi kwamba jambo hilo lilimuumiza. Wenyewe walichukulia kuwa limeshasahaulika, ila kichwani kwake Isiminzile likaendelea kuzunguka.

Wakiwa bado wanaendelea na maongezi ya hapa na pale, akafika binti mwingine ambaye alifahamiana nao.

"Xander... teacher wa Com anakuita," akamwambia na hapo hapo kuanza kuondoka.

"Aaaa sasa mbona haraka hivyo... hujaachiwa matumizi nini? Njoo me nikupe," Lucas akawa anamtania huku binti huyo akiondoka.

"Basi Xander kupiga A plus nafikiri ndo' atakuwa CR wa madam V sa'hivi," akasema Benjamin.

"Ngoja nikamsikilize," Xander akasema na kunyanyuka.

Ramla alikuwa anamwangalia kwa matumaini kwamba angemwambia hata jambo fulani dogo, lakini jamaa akaondoka tu kuelekea ofisi za chuo. Wengine hawakujua kuhusu tatizo lao, labda rafiki zake Ramla tu kwa kuwa aliwaambia, hivyo hawakuweza kuhisi kwamba walizinguana. Isiminzile akaendelea kukaa hapo na "rafiki" zake wapya, akijitahidi kuchangia maongezi pia mara kwa mara. Ramla aliketi sehemu ambayo Xander alikuwa hivyo Isiminzile alimwangalia kwa ukaribu, akivutiwa sana na uzuri wake, lakini pia akisikitika moyoni kwamba haingekuwa rahisi kumpata.

★★

Xander hakujua atarajie nini kwenye mwito huu na madam Valentina, ila mapigo yake ya moyo yalikimbia kwa kasi kutokana na kuwa na hamu ya kutaka kujua alichoitiwa. Alijua kilichotokea nyumbani kwa mwanamke huyu usiku wa jana kilimfanya apambane na akili yake mwenyewe na labda kuhisi yuko ndani ya wakati mgumu, hasa kwa sababu kijana alisukuma sana mpaka mambo yote yaliyotokea kutokea. Hivyo alitaka kuona sasa haya yote yangeishia wapi, na kuitwa kwake kukawa mwanzo mzuri kwa kuwa toka alipofika chuoni siku hii hakuwa ameonana naye.

Alipofika ofisini kwa madam Valentina, Xander alikuta mlango ukiwa wazi kiasi na kumwona madam akiwa amesimama usawa wa kabati lenye mafaili; akionekana kuangalia jambo fulani. Akaugonga mlango kidogo, naye Valentina akageuka na kumwona akiwa anachungulia. Akamwambia aingie na kuufunga mlango, naye Xander akatii. Ofisi yake ilikuwa pana kiasi yenye madirisha makubwa yaliyowekwa mapazia marefu sana, nayo ilipendeza kwa mwonekano safi na mpangilio mzuri wa vitu.

Siku ya leo Valentina alivalia gauni ya rangi ya samawati (blue) iliyoishia magotini, ambayo iliubana mwili wake kiasi. Nywele zake za mawimbi-mawimbi alikuwa amezibana kwa nyuma, naye Xander alipenda jinsi mkufu wa Valentina ulivyong'aa na kuipendezesha shingo yake. Aliposogea karibu na alipokuwa amesimama, akatambua kwamba Valentina hakuwa amevaa sidiria ndani, kwa kuwa sehemu za kifua chake zilijichora kwa mbali juu ya nguo aliyovaa.

"Madam V... nimekuja," Xander akasema.

Valentina alikuwa anamwangalia sana machoni, kisha akashusha pumzi kama mtu aliyevunjika moyo.

"Alexander..."

"Niite tu Xander," akamkatisha.

"Sawa," Valentina akajibu na kuangalia chini.

"Vipi mguu?" Xander akauliza.

"Niko sawa," Valentina akajibu.

"Umependeza..."

"Asante."

"Huo mkufu ni dhahabu?" Xander akauliza.

"Ndiyo."

"Ni mzuri, umekupendezea..."

Valentina akaona ni kama Xander alikuwa hataki asikie kile alichomwitia, hivyo akaona akatishe maongezi hayo ambayo hayakuwa na mwelekeo wowote mzuri.

"Okay, inatosha. Nashukuru. Nimekuita ili tuongee kuhusiana na jambo la muhimu. Wewe Xander... ni kijana mzuri na... una akili, ni mwerevu, una kipaji kizuri cha kuandika..."

"Na ni handsome... ila nilikuwa tu nakazia maana tayari ulisema me mzuri," Xander akatania.

"Ni sawa. Jana... kilichotokea kati yetu... ni kitu ambacho kimeniweka kwenye wakati mgumu sana. Mambo hayakupaswa kuwa vile..."

"Lakini ulifurahia sana..."

"Nisikilize, usinikatishe."

Xander akatulia baada ya kuona jinsi Valentina alivyokuwa "serious."

"Kuna mipaka. Mipaka ambayo haipaswi kuvukwa. Jana ilikuwa too much. Mimi na wewe hatuna connection yoyote zaidi tu ya uhusiano wetu kama mwalimu na mwanafunzi. Nataka ibaki kuwa hivyo... kwa sababu singependa uingie kwenye shida yoyote kisa mimi. Unanielewa?" Valentina akasema.

"Ndiyo..." Xander akajibu kiupole.

"Ni vizuri. Hii siyo rahisi kwangu. Kitu tulichofanya... mambo yote... hata kama ni wazazi... au girlfriend wako akijua hangefurahi. Na pia mimi ni mkubwa sana kwako... nataka tu..."

Xander akamkatisha kwa kumsogelea karibu zaidi. Valentina akabaki kumwangalia kimshangao.

"Hata mimi siyo rahisi kwangu. Lakini nitafanyaje? I can't help it. I'm into you..." akasema kwa sauti yenye kubembeleza.

"Xander!" Valentina akashangaa.

"Ni kweli madam. Nimekuelewa sana yaani. Haitakuwa rahisi kwangu kusahau kila kitu; macho yako, pumzi zako, miguno yako, ngozi yako laini... kila mguso wako usiku wa jana... busu zako..."

Xander alikuwa anaongea maneno haya yenye kuamsha hisia huku akitembeza vidole vyake kwenye viganja vya Valentina. Ni kama yote ambayo mwanamke huyu aliyasema hakuwa ameyasikia kabisa. Valentina alisisimka sana, huku Xander akimsogelea mdomoni.

"Xander unafanya nini? Hapa ni ofisi... chuoni," Valentina akasema kwa sauti ya chini.

"Najua ulifurahia sana jana. Nataka sana kukuona ukifurahia vile tena... mbali na stress zako zote..." Xander akamwambia.

Valentina akarudi nyuma kidogo, lakini Xander akamsogelea tena na kuvishika viganja vyake.

"Nataka nikufanye uzisahau. Mimi ni mdogo ndiyo, lakini kukupa unachostahili ninaweza..." Xander akasema kwa kujiamini.

Alianza kupandisha viganja vyake mpaka juu ya mikono ya Valentina, huku mwanamke huyu akimwangalia tu, kisha akaifata midomo yake na kumbusu. Valentina aliangalia usawa wa mlango kwa uharaka, akihofia kuna mtu angeweza kuingia, lakini Xander akataka kumsahaulisha hilo na kuushika uso wake ili ampe denda kiusahihi. Sasa mwanamke huyu akalegea zaidi baada ya Xander kuanza kumbusu kimahaba. Ilikuwa busu nzito iliyomfanya afumbe mpaka na macho, akisahau kabisa yote aliyokuwa amemwambia muda mfupi nyuma.

Wawili hawa wakaendelea kudendeshana huku mikono yake Xander ikimbana zaidi madam wake kwenye mwili wake. Valentina aliweza kuhisi jinsi Xander alivyopandisha hisia, na ijapokuwa alitaka kumwambia waache, hamu ikamzidia nguvu na kumruhusu kijana huyu aendelee kumpa busu hiyo; wakisahau kabisa kuwa wako ofisini. Kisha mara ghafla Xander akajitoa kwenye mdomo wa Valentina na upesi kuyapiga mafaili yaliyokuwa mezani kwa mkono wake, kitu kilichofanya yaangukie chini na kuzagaa.

Xander akainama kuanza kuyaokota. Valentina alishangazwa na jambo hilo, na hapo hapo mlango wa kuingilia ofisini kwake ukafunguliwa. Akashtuka kiasi kwa kutokutarajia hilo, na aliyeingia hakuwa mwingine ila mkuu wa chuo mwenyewe, Mr. Daniel. Akamtazama Valentina kimaswali na kumwangalia Xander akiwa anaokota makaratasi hapo chini, bila kumtambua kwa sababu alimpa mgongo.

"Valentina vipi?" Daniel akamsalimu.

"Aa... safi tu. Nambie..." Valentina akaficha wasiwasi wake.

"Huyu vipi? Wewe unafanya nini?" Daniel akauliza.

Mpaka kufikia sasa Xander hakuwa amemgeukia kwa sababu alificha mwonekano wa suruali yake kwa mbele iliyokuwa imetuna haswa na kujichora. Hivyo, akageuza shingo na kumwangalia mkuu machoni.

"Ah... Alexander kumbe! Umefanyaje?" Daniel akauliza.

"Nimemwangushia madam mafaili ndo' nayaokota hapa," Xander akajibu.

Daniel akaingia mpaka ndani na kusimama karibu na Valentina. Akaanza kuongea naye kuhusu masuala fulani ya kitaaluma, huku Xander akiendelea kujiokotelesha makaratasi taratibu ili msuli wake usinyae. Daniel akamaliza kuongea na Valentina na kuwaacha humo. Alimjua vizuri Xander hasa kwa kuwa kijana alichezea timu yao ya chuo, na pia Daniel alikuwa anamfukuzia pacha wake. Hivyo hakuwa na noma naye hata kidogo. Baada ya kutoka, Xander akawa amemaliza kuyakusanya makaratasi na kusimama.

"Sorry! Nilifanya hivi ili..."

"Usijali, nimeelewa. Yaweke tu hapo," Valentina akamkatisha.

Xander akayaweka mezani, kisha alipomgeukia akamshika kiunoni na moja kwa moja kumpiga busu mdomoni.

"Xander..." Valentina akajitoa kwenye mikono yake.

"Hiyo ilikuwa tamu madam V. Nitaipata tena..." Xander akamwambia kichokozi.

"Lakini wewe!" Valentina akasema.

Xander akachekea tu kwa chini na kuanza kuelekea mlangoni. Kisha akamgeukia alipokuwa anataka kutoka nje na kumwonyesha kwa ishara ya vidole kuwa angemtafuta kwa simu, na baada ya hapo akatoka. Valentina akabaki hapo akimtafakari kijana wake huyo machachari. Hakuweza kujizuia kupendezwa sana na jinsi Xander alivyomwonyesha ujasiri wa mapenzi na kumfanya aonekane kama mtu aliyemzidi umri. Lakini bado kuna sehemu fulani ya moyo wake ambayo ilimwambia hakupaswa kujiachia sana kwake; ijapokuwa tayari alionyesha kushindwa dakika chache nyuma.

Xander yeye akatoka hapo akijihisi kama mshindi mkubwa mno. Alijisifu sana moyoni na kujiahidi kuwa ni lazima angemlegeza zaidi madam wake mpaka anyong'onyee kwenye penzi lake ambalo alijua alilipenda na alilitaka tena. Hakutaka fikira za Ramla wala nini zimwondolee uhondo huu mpya ambao aliufurahia sana moyoni. Akaelekea zake darasani ili kusubiri kipindi.


★★


Baada ya kipindi kumalizika, Xander akatoka darasani pamoja na Lucas na Bernard na kwenda usawa wa kingo za chuma zilizozungukia ghorofa ya juu waliyokuwepo. Wawili hawa wakamwambia walitaka kwenda kupata msosi pamoja kwa kuwa rafiki zao wengine walitangulia, lakini Xander akasema waende tu kwa kuwa yeye hakuhisi njaa bado. Wakamshangaa kiasi kwa sababu hakuwa amekula kutokea asubuhi, na baada ya utani utani kidogo, wakawa wamemwacha peke yake.

Akawa anaangalia kwenye simu yake mambo kadhaa, zikiwemo jumbe za Ramla za kuomba samahani kwa jinsi alivyomfanyia jana. Lakini Xander hakujibu hata moja, naye akaamua kumtumia ujumbe madam Valentina. Alimuuliza kama alikuwa ameshakula, na kwa kushangaza, Valentina akajibu kwa kusema bado. Alitarajia labda hata asingejibiwa, hivyo jambo hilo likamfurahisha. Akaanza kuingiza maneno mafupi ya hapa na pale, na muda si muda, wawili hawa wakawa wana-chat.

Xander alifurahi sana, naye alijitahidi kumtumia meseji ambazo alitumaini zingemfanya Valentina atabasamu. Jambo hili lilianza kuonekana kuwa zuri sana kati yao ijapokuwa mwanamke alionyesha kama hataki mwanzoni, naye Xander akataka lisonge mbele hata zaidi. Wakati akiwa anasubiri SMS yake moja ijibiwe, akafika Isiminzile hapo na kumsalimu Xander. Alikuwa ameshikilia glasi mbili mikononi mwake.

"Bado mna vipindi?" Xander akamuuliza.

"Hapana. Wengi wa HR wameshaondoka," akasema Isiminzile.

"Na wewe?"

"Ah... me nilibaki kunywa soda kidogo. Nimekuona hapa nikaona nikuletee na wewe kidogo," akasema Isiminzile.

Akampatia glasi moja, iliyokuwa na soda kidogo ya Fanta Orange. Xander akatabasamu na kuipokea, akijua ni jinsi gani kijana huyu alivyokuwa mwenye kujishusha na kuhitaji marafiki.

"Asante," akasema Xander na kuinywa kidogo.

"Unamsubiri nani?" Isiminzile akamuuliza.

"Simsubiri mtu. Nilikuwa nazingua tu hapa," Xander akajibu huku akituma ujumbe kwa Valentina.

"Kwa hiyo... ngoja niulize... hivi... Ramla huwa anapenda mambo gani?" Isiminzile akauliza.

Lakini Xander hakumtilia maanani sana. Alikuwa ametoka kutuma ujumbe kwa Valentina akimwambia kwamba alisahau kitu fulani muhimu sana kwake usiku wa jana, hivyo alitaka kukichukua. Valentina akawa ameuliza ni nini ili amletee kesho, lakini Xander akasema ni boxer yake; kiuchokozi tu ijapokuwa ilikuwa kweli. Valentina akajibu kwamba kwa kitu kama hicho, angepaswa kukifata yeye mwenyewe, na jambo hili likamfanya Xander afurahi sana. Hakujua ni kwa nini lakini ilionekana ni kama Valentina alikuwa anampa mwaliko usio wa moja kwa moja. Akabaki anatabasamu tu.

"Eti Xander... Ramla huwa anapenda mambo gani? Kama movie labda... muziki... au mkiwaga wote huwa... huwa..." Isiminzile akawa anaendelea kumsemesha.

"Kwa nini? Uliongea naye muda ule? Mmepanga date?" Xander akauliza bila kumtazama.

"Aa... hapana... nilikuwa tu..."

Kabla Isiminzile hajamaliza kuongea, Xander akaachia tabasamu pana sana huku akiwa anaangalia simu yake. Valentina alikuwa amemwambia kwamba, muda siyo mrefu angeondoka, hivyo kama alitaka kwenda akaichukue boxer yake, basi aambatane naye kwenye gari lake. Hii ilikuwa ni sehemu ya ushindi kwa Xander ambao haukuwa umekamilika bado. Alianza kuona ni kama madam Valentina amemwelewa pia, na furaha aliyohisi ikapitiliza sana.

Kwa kuingiwa na hamu kubwa, akainywa soda yote haraka na kuiweka glasi pembeni, kisha akamwangalia Isiminzile.

"Oy... pole mwanangu sitaweza kuongea, kuna sehemu nawahi mara moja. Asante kwa..."

Kabla hajamaliza kuongea, akashtushwa na sauti ya Sandra ikimwita.

"Alexander!"

Yeye pamoja na Isiminzile wakatazama upande wa nyuma yake na kumwona Sandra akiwa pamoja na Sophia, huku akija kwa njia iliyoonyesha amekasirika. Xander akiwa anajua vizuri alichokifanya, akaigiza kujificha nyuma ya Isiminzile ili dada yake asimpige. Sophia alikuwa anacheka tu. Sandra akafika hapo akiwa amekunja sura na kutaka kumshika Xander, lakini jamaa akawa anamkwepa kwa kuizungusha miili yake yeye na Isiminzile.

"Umefanya ujinga gani huu?" Sandra akamwambia.

"Mdoli sikiliza..." Xander akawa anasema huku akicheka.

"Nilikwambia usiniite tena lile jina... Xander nitakukaanga uwe mweusi!" Sandra akalalamika.

"Kwani amefanyaje jamani?" Sophia akauliza.

"Me mwenyewe nashangaa!" Xander akasema.

"Kapost... amepost picha yetu ya wakati tuna miaka 10. Kaipost FB, hii hapa... eti limeandika Throw back nikiwa na cute baby Sandirito!" Sandra akalalamika.

Sophia akacheka.

"Ahahahah... sasa shida iko wapi? Kukuita cute baby ni vibaya?" Xander akauliza.

"Nitakutafuna Xander, ifute! Nimekwambia usiniite hilo lijina tena. Yaani sijui ukoje!" Sandra akasema kwa kuudhika.

"Sandirito!" Sophia akasema.

"Na we usiniite hivyo!" Sandra akasema na kufanya wote wacheke.

"Haya punguza kuni basi, moto mkali mno. Ntaifuta, sawa?" Xander akamwambia.

"Ole wako uache. Nakupa saa moja, la sivyo nami nita... nitajua la kufanya," Sandra akasema.

Kisha kwa jazba, akaichukua glasi ya soda aliyoshikilia Isiminzile na kuinywa yote kwa kishindo, halafu akamrudishia Isiminzile glasi kwa nguvu.

"Iiiih jamani! Sasa soda ya mwenzio imekukosea nini?" Xander akasema.

Sandra akasonya kidogo na kuondoka hapo upesi. Sophia na Xander wakabaki wanacheka.

"Hilo jina umelitoa wapi?" Sophia akauliza.

"Ahahahah... kuna animation fulani inaitwa Condorito, inachekesha sana. Ndiyo nika-mend jina lake kama hivyo. Sasa... hapendi kwa sababu Condorito ni kituko kwo' anaona ni kama namharibia jina..." Xander akaeleza baada ya kumwachia Isiminzile.

"Mh... haya bwana. Nyie wawili mnafurahisha sana," Sophia akasema.

"Vipi mama?" Xander akauliza.

"Anaendelea vizuri Xander. Wameshaanza matibabu na habari ni nzuri," Sophia akasema kwa furaha.

"Sasa je, nilikwambia, she's a survivor. Utamwambia namsalimia," Xander akamwambia.

"Ahahah... asante mwaya. Unaenda home sa'hivi?" Sophia akauliza.

"Hapana, kuna sehemu napita kwanza. Halafu... nahitaji kuwahi. Wewe wapi?"

"Me naingia bweni kulala. Sandra atakuwa ameshaondoka hivyo maana hatuna zoezi leo."

"Okay. Baadae eti?"

"Poa."

"Oa... Simi, asante. Kesho," Xander akamwambia.

Isiminzile hakutoa jibu bali akawa amemtazama tu. Xander akaondoka upesi na kuwaacha wawili hawa hapo.

"Simi? Unaitwa Simi?" Sophia akamuuliza.

Lakini Isiminzile akawa anamtazama tu kama vile mtu aliyepigwa na bumbuazi. Sophia akamwona kama mtu wa ajabu-ajabu tu na kuamua kujiondokea hapo. Isiminzile akabaki amesimama, huku akiwa ameshikilia glasi yake mkononi, naye akawa anapumua kwa njia iliyoonyesha hofu kubwa.


JE, UNADHANI NI NINI AMBACHO ISIMINZILE AMEFANYA?


★★★★★★★★★

 ITAENDELEA 

★★★★★★★★★

Previoua Next