Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.


FOR YOU

Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa

Rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SABA

★★★★★★★★★★★★★


Baada ya kuwaacha Isiminzile na Sophia, Xander alielekea mpaka walipokuwa Lucas na Bernard na kuwakuta wanapata msosi kwenye mgahawa mmoja maeneo hayo. Wakamkaribisha na kumwambia na yeye achukue chakula, lakini Xander akakataa na kumwambia Lucas akimaliza aichukue pikipiki yake kwa muda fulani, kisha baadae ataipeleka nyumbani kwao. Lucas akauliza kwani yeye alikuwa anaenda wapi, naye Xander akasema ni sehemu ambayo hangehitaji pikipiki, hivyo atumie kwa muda kisha baadae aipeleke kwao; kwa kuwa alipajua. Akampatia funguo, naye akawaacha wawili hao wakiendelea na makamuzi.

Kutoka maeneo hayo ya chuo, Xander alichukua usafiri na kuelekea maeneo ya kati zaidi ya jiji, na hapo akaingia kwenye mgahawa fulani wa starehe na kuagiza kinywaji kimoja tu. Kisha akamtumia ujumbe Valentina kumwambia alikuwa sehemu gani, hivyo akitoka tu huko chuoni ampitie hapo ili wote waende kwake "kuichukua boxer." Alikuwa anajichekea mwenyewe tu huku akiwa na hamu sana ya kutaka kufanya jambo lingine kubwa siku hii. Baada ya kama dakika 10 hivi, Valentina akajibu ujumbe huo akisema sawa; alikuwa anamalizia mambo fulani kisha ndiyo angempitia.

Xander akahisi raha sana kwa kuwa ilionekana ni kama wanapanga kutoka "out" kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Alijiambia akilini mwake kwamba huyu mwanamke anataka muziki mnene, na yeye angempatia mpaka besi ya mwisho leo. Aliendelea kukaa hapo kwa dakika kadhaa, kisha simu yake ikaita. Mpigaji alikuwa ni Valentina, naye akamtaarifu kwamba alifika nje hapo, hivyo aende upesi. Xander akaachia tabasamu la kiburi na kuelekea nje, na baada ya kuliona gari la madam, akalifuata na kuingia upande wa mbele pembeni ya mwanamke huyu.

Valentina alikuwa anamwangalia kama vile anasubiri Xander aseme jambo fulani, lakini Xander akaonyesha kama anataka kutabasamu ila akajikaza na kuangalia mbele tu. Madam akaanzisha mwendo tena kuanza kuelekea nyumbani sasa. Baada ya kama dakika mbili za ukimya, Xander akaona amsemeshe.

"Hivi ile nyama ya jana bado ipo?" akauliza.

"Nyama gani?" Valentina akauliza pia.

"Niliacha... jana nilinunua nyama, nikakuachia nyum..."

"Ipo. Utaikuta kama na yenyewe unataka kuichukua," Valentina akamkatisha.

Xander akajitahidi kubana tabasamu lake, kwa kuwa aliona Valentina alikuwa anajifanya amekaza. Valentina akamwangalia na kukuta anamtazama kwa njia ya tabasamu.

"Nini?" akamuuliza.

"Nothing," Xander akajibu.

"Funguo yangu unayo?"

"Yep."

"Iweke hapo."

Xander akaiweka huku anacheka.

"Unacheka nini?"

"Nothing."

"Unaniona kama kituko eti?"

"Never. Nakuona kama mtu special sana kwangu."

"Kama girlfriend wako?"

"Ahahah... anakufanya uone wivu?"

"Nini?"

"Niambie kama anakukera. Tutasaidiana kuchimba shimo. Hatasikika tena," Xander akatania.

Valentina akacheka kidogo.

"Mimi siyo mtu wa kuona wivu," Valentina akasema.

"Mmmm kweli?"

"Sasa mimi nimwonee wivu Ramla msichana mdogo kweli nitakuwa na akili?"

"Inawezekana. Sikumbuki kukuambia jina la girlfriend wangu, na hata kama ulituona pamoja, sikuwahi kukwambia huyo ndiyo girlfriend wangu... ikimaanisha umefanya utafiti..."

"Hakuna haja ya utafiti, nyie ni... wanafunzi wa darasa ninalofundisha, kwa nini nisimjue? Na... kila mtu anajua hilo... kuhusu wewe na yeye..."

"Kumbe? Kwa hiyo... unasema kwamba kwa kuwa nina girlfriend, siwezi kukuona wewe kuwa special?"

"Ah me sijui bwana. Naomba tusiongelee hayo..."

"Lakini we si ndiyo umeanza kumtaja..."

"Mimi ni mtu mzima Alexander. Nina experience na mambo mengi, hivi siyo vitu vya kunichanganya. Na nilikuweka wazi kwamba kilichotokea kati yetu ilikuwa kimakosa. Nilikuwa nimelewa. Full stop. Tunaenda so ukachukue nguo yako, then... uende nyumbani," Valentina akasema bila kumwangalia.

"Kumbe... kumbe una experience na mambo mengi eeh?" Xander akamwambia kiutani.

Valentina akamtazama kimaswali.

"Yaani katika yote niliyokwambia, umesikia hilo tu?"

"Ahahah... ndiyo la muhimu kwangu. Nataka nijionee hayo mambo mengi," Xander akasema kiutongozi.

"No. Haiwezekani..."

"Kwa nini?"

"Kwa sababu Alexander, wewe ni... mimi... yaani hata sijui ni kwa nini nataka kujielezea kwako!"

"Kwa sababu unataka... full stop."

Valentina akamwangalia machoni sana, naye Xander akatabasamu kwa mbali. Kisha madam akaangalia mbele tu na kubaki kimya.

"Ninakuelewa sana madam V. Najua hatujayaanza mambo haya sehemu nzuri, lakini nataka mwisho wake uwe. Umenivutia sana madam... kila time nakuwaza tu... it's such a good feeling..."

"Alexander acha... acha tafadhali..."

"Kwa nini? Nakufanya ujihisi dhaifu? Nakufanya... uhisi raha ambayo umekuwa ukijaribu kuikimbia kwa muda mrefu eti? Hakuna haja ya kuikimbia madam V... nifungulie mlango wako niingie..."

"Ahah... unafaa kuwa mtunga mashairi. Hizo swagger hazitanikamata lakini..."

"Siyo swagger... ni ukweli. Ulikuwa umeufunga mlango wako wa kihisia kwa sababu... unaogopa kuumia. Lakini madam V... maumivu ni sehemu ya maisha, na maisha siyo fair kwa kila mtu. Kwa hiyo usijizuie kupenda kwa sababu unaogopa... la sivyo unaweza hata kulipuka..."

"Kulipuka na nini?"

"Si hivyo unavyoyafungia mahisia ndani? Yakijaa sana mwisho wa siku puuf! Watu wanakuja kuokota vipisi vipisi... ila me ntakimendea kimoja tu... kile kipisi..."

Valentina akajikaza asitabasamu kwa kuwa Xander alimtania kiuchokozi sana. Sasa hakuweza kujizuia kufurahishwa na kijana huyu, lakini bado akaona asimwachie sana acheze na akili yake.

Wakawa wamefika nje ya nyumba yake hatimaye. Bila kuambiwa, Xander akachukua ile funguo na kushuka, akielekea getini kufungua. Akalifungua lote na kuanza kumwonyesha Valentina ishara kwa kiganja chake kuwa aliingize gari ndani polepole; kama anamwita. Valentina akatabasamu kidogo huku anatikisa kichwa chake kwa kufurahishwa na vituko hivi, naye akaliingiza gari ndani.

Baada ya Xander kulifunga geti, akaelekea usawa wa gari na kusimama, lakini akashangaa kwa kuwa Valentina hakushuka. Akaona achungulie kupitia kioo na kumwona akiwa ameweka simu sikioni, hivyo akajua alikuwa anaongea na mtu. Wazo la kwamba huenda alikuwa labda anazungumza na askari aje kumkamata likamwingia, naye akatabasamu kwa sababu aliliona kuwa wazo la kipuuzi. Lakini akaufungua mlango wa gari na kuketi ndani yake tena, ili amwangalie madam wake akiongea.

"... na ni sawa kwa sababu itakuwa Jumamosi, mipango yote imekamilika tunasubiria tu tamko la TUSA... ndiyo... eeh ndiyo, bado ila.. wako tayari kwa hiyo we piga tiki tu... Asante sana kwa msaada wako Millie, unastahili lunch ya nguvu kutoka kwangu mpenzi... ahahahah...."

Xander alikuwa anamtazama tu kwa kuvutiwa na sura yake alipocheka. Akaamua kutumia nafasi hii kumchokoza ili aone angeitikia vipi. Valentina akiwa bado anaongea na "Millie," Xander akatumia kiganja chake kuanza kuzichezea nywele za kichwa cha madam. Kisha akaanza kutembeza vidole vyake kutokea begani mpaka katikati ya mkono wake, huku akimwangalia. Valentina hakumtazama, lakini Xander aliona wazi kwamba alihisi vyema kile alichofanya, ila akakaza tu, akionyesha kama hajali.

Baada ya kukata simu, Valentina akataka kufungua mlango wa gari ili atoke, lakini Xander akauzuia kwa kuurudisha ufunge haraka. Hii ilifanya ainamie kumwelekea Valentina alipounyoosha mkono ili kufanya hivyo, kwa hiyo akawa amemkaribia zaidi usoni. Valentina hakumtazama, ila akaweka uso ulioonyesha dhahiri kwamba alikerwa na jambo hilo.

"Unafanya nini?" Valentina akauliza bila kumwangalia.

"Taking a moment to mesmerize your beauty (nachukua muda mfupi kuutathmini uzuri wako)," Xander akamwambia kwa sauti ya chini.

"Umemaliza?" Valentina akauliza.

"Bado," Xander akamwambia.

Kisha akaisogelea sehemu ya shingo yake na kuibusu kidogo. Valentina akamwangalia kwa njia iliyoonyesha kama hakupendezwa na hilo. Sasa midomo yao ikawa karibu zaidi, naye Xander akatabasamu kwa mbali.

"Unataka kunichezea Alexander?" Valentina akauliza kwa hisia.

Xander akawa makini kidogo.

"Hapana madam V. Hapana. Ninavutiwa nawe ukweli. Sina... sina mambo mengi... au vitu vingi navyojua kama wewe... lakini hii ndiyo njia yangu ya kukuonyesha jinsi navyoku-feel... Siwezi kukuchezea... siwezi," Xander akamwambia kwa kubembeleza.

Valentina akatazama mbele na kusema, "Hivyo ndivyo nyie husema. Lakini mkishapata mnachotaka... ni kama tu inavyokuwa kwa Ramla, si ndiyo?"

"Achana na habari za Ramla madam V. Niangalie mimi... sisi," akasema Xander.

Valentina akatoa tabasamu la kuguna, kisha akataka kufungua tena mlango, lakini Xander akauzuia kwa mara nyingine, kisha akaanza kuibusu shingo yake. Valentina akawa kama anamsukuma huku akisema aache, lakini Xander akaendelea. Akajaribu kumzuia kwa nguvu lakini kijana akamshinda na kumbananiza kwenye sehemu hiyo ya mlango, akiibusu kimahaba sana shingo yake. Valentina sasa akawa akipumua kwa nguvu sana.

"...Alexander... acha... stop... don't... ohh God..."

"Don't fight it... don't fight it... let yourself go... let it go..." Xander akamwambia kwa kunong'oneza.

Aliendelea kumbusu sehemu hiyo ya shingo huku amembana kwa kutumia nguvu kiasi, kisha akapandisha mpaka mdomoni mwake na kuanza kuibusu. Valentina hakuweza kujizuia kurudisha busu hii pia kwa sababu hisia kali kumwelekea kijana huyu zilikuwa zimempanda, na ni kama alifurahia sana njia hii ya kupatiwa mapenzi.

Xander alitoka mdomoni kwa madam wake na kushuka tena shingoni, naye taratibu akaanza kumpatia mwanamke huyu mapenzi ndani ya gari lake. Kijana akaisawazisha miili yao vizuri ili Valentina apitishe mguu wake mmoja upande mwingine wa siti, yaani awe katikati ya jamaa. Mambo haya yote Valentina aliyaruhusu kabisa, ikionyesha ni kitu alichokuwa anataka kama Xander alivyomwambia.

Wawili hawa wakaendelea kuonyeshana upendo wao kwa dakika kadhaa ndani ya gari hilo. Valentina akamshangaza Xander kiasi baada ya yeye kuonyesha alitaka mchezo huu uendelee. Tabasamu la furaha likaonekana mdomoni mwa Xander, naye akaendelea kumpa raha mwanamke wake.

"Te amo, cariño..." Xander akanong'oneza sikioni kwa madam.

Dakika chache baadae Xander akajiachia kwa kuhisi mridhiko wa mwanzo. Valentina alikuwa amemshikilia kwa njia ya kumkumbatia huku akipumua kilegevu, kisha taratibu akajivuta na kumtazama usoni. Xander alikuwa anamwangalia kwa hisia sana, kisha akalishika shavu lake na kuanza kuchezea nywele nyuma ya shingo yake.

"Nina-note hili. Zamu hii haujalewa," Xander akasema kiutani.

"Hivi ninafanya nini?" Valentina akauliza kwa sauti ya chini.

"Unanipa utamu," Xander akamwambia.

Valentina akacheka kwa sauti ya chini na kulaza paji lake la uso shingoni kwa Xander. Xander akatabasamu kwa furaha pia.

"Sijui ni kwa nini unanifanya naishiwa nguvu," akasema Valentina kwa sauti yenye deko.

"Na bado. Nataka nikumalize nguvu zote kabisa," akasema Xander.

Valentina akanyanyua uso wake na kumwangalia machoni.

"Unapenda kujisifu sana," akamwambia.

"Hiyo ni lazima. Inafurahisha sana mwanaume akijua mwanamke wake anafurahia kile anachopewa," Xander akasema.

"Mhm... mwanamke wako? Vipi kuhusu Ramla?"

"Ramla... nitaongea naye. Nimekuwa nikijitahidi ku-keep up na mambo yake mengi yenye kukwaza, lakini, sa'hivi itabidi ni..."

"Alexander sisemi umwache... kwa sababu yangu. Haujui ni jinsi gani ataumia," Valentina akamwambia.

"Oh no! Sisemi kwamba ni kwa sababu hii tu. Kwa muda mrefu nimekuwa nikitaka kufanya hivyo ila basi tu kwa sababu nilitaka kutulia na mtu mmoja. Lakini kwa alichokifanya juzi..."

"Kwani alifanya nini?"

"Alinizingua. Alidai nina-cheat na rafiki ya dada yangu kwa kuwa aliniona naye tu kwenye pikipiki. Wivu kwenye mahusiano ni kawaida lakini yeye anaenda mbali sana kwenye kulalamika... hataki kusikiliza sababu, anajali anachofikiria yeye tu. Hii siyo mara ya kwanza ananitendea kwa njia ya dharau, anafanya iwe kama nimemuoa kumbe ni girlfriend tu," Xander akaeleza.

"Anaonyesha anakupenda sana..."

"Hata kama. Tume-date karibia miaka miwili, anapaswa kukua, siyo kila kitu abembelezwe, anyenyekewe... nimejitahidi sana ila sasa hivi I can't... nataka kuwa na wewe tu," Xander akamwambia huku anapapasa kiuno chake.

"Na mimi najua utafika huo wakati kama ilivyo kwa..."

"Usiwaze hayo madam V, furahia tu wakati huu. Hatujui kesho itakuwaje," Xander akamwambia na kuliminya kalio lake.

Valentina akavuta pumzi na kusema, "Alexander..."

"No. Mimi kwako siyo Alexander tena. Niite Xander mpenzi..." Xander akasema huku akimkonyeza.

Valentina akatabasamu na kuuliza, "Yale maneno... uliyoniambia... yarudie tena..."

"Te amo, cariño," Xander akasema.

"Maana yake?"

"I love you, darling," Xander akajibu.

Valentina akatabasamu, kisha Xander akaanza kumnyonya ulimi kimahaba kwa mara nyingine tena. Wakati huu Valentina pia alimwonyesha kwamba alijua kutoa penzi la mdomo kwa kuirudisha denda hii vyema.

"Vipi tukienda ndani?" Valentina akauliza katikati ya busu yao.

"Wazo zuri," Xander akajibu.

Wakapeana busu fupi, kisha wakaanza kujisawazisha ili watoke nje ya gari. Xander alipandisha suruali yake, naye Valentina akalivaa vizuri gauni lake kisha wote wakatoka na kuanza kuelekea ndani. Walikuwa wakitazamana kihisia sana, naye Xander akaubana mwili wa mwanamke huyu kwake huku wakitembea pamoja. Giza lilikuwa linaanza kuingia kwa mbali, saa moja ikikaribia.

Walifika ndani ya nyumba na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha madam na kuendelea na penzi lao. Wakati Xander alipokuwa akiendelea na kazi yake, alihisi mjio wake ukitoka, naye alipokuwa ameanza kujivuta ili ajitoe kwa Valentina, Valentina akamng'ang'ania ili kuzuia hilo. Ikiwa imekuja kwa njia ya sintofahamu, Xander akajiachia ndani ya Valentina.

Xander akatulia kidogo na kuendelea kumlalia kwa juu, huku Valentina akipumua kichovu na kupapasa mgongo wa mpenzi wake mpya.

"Madam V... nafikiri nime... nime...." Xander akawa anaongelea shingoni kwa Valentina.

"Usijali. Kuna dawa nitakunywa," Valentina akamtuliza.

"Ahah... wewe ni mtamu sana madam V..."

"Mhm... wewe pia..."

"Ahahah... asante kwa kuniruhusu kuwa sehemu ya maisha yako..."

"No. Mimi ndo' nikushukuru. Sijataka kuwa na mwanaume kwa sababu... kama ulivyosema... niliogopa. Ila sasa ngoja nijionee safari yetu itakavyokuwa..."

"Asante madam V..."

"Karibu. Na mimi kwako kuanzia sasa siyo madam V tena... niite Valentina..."

Xander akatabasamu na kumbusu mdomoni, kisha shingoni, halafu akabusu na kifua chake kiutundu. Valentina akacheka kidogo.

"Nahisi njaa..." Xander akamwambia.

"Oh... hukula?"

Xander akatikisa kichwa kukanusha.

"Basi wacha nika-fix kitu, sawa?" Valentina akasema.

"Sawa... Valentina," Xander akamwambia.

Wakapiga busu laini tena, kisha Valentina akaingia bafuni kujimwagia maji kidogo. Baada ya kutoka akaelekea jikoni akimwambia Xander amfuate baada ya yeye kujimwagia pia.

Usiku ukawa umeingia sasa kufikia mida ya saa 2, na mvua ndogo ikaanza kunyesha. Xander na Valentina walikula pamoja huku wakiongea mambo yenye kufurahisha. Xander akamwelezea pia kuhusu maisha yake; kazi za mama na baba yake, ukaribu wake na Sandra, mdogo wake wa kike Azra, na hali walizopitia kama familia. Alimwambia jinsi alivyovunjwa moyo na baba yake, lakini hakumchukia, bali alitaka tu kuwa pamoja naye zaidi kama ilivyokuwa zamani. Valentina akamtia moyo kwamba bila shaka mambo yangekuwa sawa siku moja kuhusiana na hilo.

★★

Kwenye mida ya saa 3 baada ya wawili hawa kutumia muda kula na kuongea, Valentina akamwambia Xander kwamba angempeleka kwao. Xander akasema alitaka kulala hapo hapo siku hiyo ili wafurahie kuwa pamoja zaidi, lakini Valentina akakanusha na kusema wangepanga kuwa pamoja wakati mwingine mzuri; hasa kwa kuwa hakutaka mama yake amzingue. Ijapokuwa Xander alimshawishi kuwa mama yake hakuwa na tatizo hata akilala kwa rafiki, bado Valentina akasisitiza kumrudisha kwao kwa leo. Xander hakuwa na kipingamizi tena, hasa kwa sababu kwa leo mwanamke huyu alimridhisha. Hivyo baada ya kukubaliana, wakatoka pamoja na kuondoka kwa kutumia gari la madam.

Mvua bado ilinyesha kwa kuongezeka na kupungua, kukiwa na mianga ya radi pia, mpaka Valentina alipomfikisha Xander kwao kwa mara ya kwanza. Kijana akamwambia kuwa angefurahi sana kama mpenzi wake huyu angekuja kwenye sherehe ya mama yake, naye Valentina akasema wangeangalia na jinsi mambo yangekuwa.

Wakapeana busu fupi ya kuagana, kisha Xander akaelekea getini kwao akijaribu kuwahi ili asilowane sana. Valentina akabaki kumwangalia tu huku anatabasamu, kisha akaligeuza gari na kuanza kurejea nyumbani kwake.

Baada ya kufika ndani....

"Mbona uliitelekeza pikipiki? Kaileta rafiki yako, wewe ulikuwa wapi?" Alice akamuuliza kwa njia ya kawaida.

"Aam... pikipiki ilipatwa na shida kwo'... nikaiacha kwa fundi. Baadaye nilikuwa na marafiki zangu, kwa hiyo nikamwambia Lucas aipitie maana niliona uvivu kuifata," Xander akadanganya.

"Si ungeniambia mapema?"

"Sikuona haja. Me kwanza nilikaa kusubiri maana fundi aliniambia ingetengemaa mapema lakini akawa anazungusha tu... kwo' mvua ilipoanza nikaona tu niiache..."

"Yaani liongo hili! Unachanganya story nyuma-mbele," akasema Sandra, aliyekuwa pembeni.

"Ulikuwepo?" Xander akamuuliza.

"Tunakujua we huna lolote, ulikuwa na mtu wako tu huko mmechelewa kutoka kufanya yenu ndiyo ukatunga hiki kisingizio," Sandra akasema.

"Ila Sandra..." Xander akasema kwa hofu kiasi huku akimtazama mama yake.

Alice akatikisa kichwa chake, kisha akauliza, "Umekula?"

"Yeah..." Xander akajibu.

"Sasa je, si nilikwambia? Anapikiwa huko... hahaaa..." Sandra akasema kiutani.

"Nenda sasa ukabadilishe nguo," Alice akamwambia Xander.

Xander akaanza kuondoka huku akitabasamu kwa njia iliyomfanya aonekane mwema, ila alipomgeukia Sandra, akamwonyesha ishara ya kumcheka na kumzomea kimya kimya, naye Sandra akamwonyesha kidole chake cha kati bila mama yao kuwaona. Baada ya kujikausha maji na kuvaa nguo zingine, Xander akarejea tena sehemu ya sebuleni kuketi pamoja na Sandra na mama yao. Salome na Azra walikuwa wameshakwenda kulala.

Watatu hawa wakakaa hapo kwa kama saa zima wakipiga story za hapa na pale, kisha baadae kila mmoja akaondoka kwenda kwenye vyumba vyao vya kupumzika.

★★

Mvua bado iliendelea kunyesha familia nzima ilipoingia kujipumzisha. Hali ilizidi kuwa mbaya kwa sababu iligeuka na kuwa kama dhoruba kadiri muda ulivyokwenda. Mapazia yalipeperushwa kwa nguvu ijapokuwa madirisha yalifungwa vyema, na mianga ya radi ilimulika mara nyingi sana na kufanya paonekane kama vile mchana. Ngurumo za radi ziliendelea kutawala, na hii ilimsumbua sana Alexandra ambaye alipata shida kusinzia kutokana na kuhofishwa na hali hii. Alijiona ni kama vile yuko ndani ya filamu yenye kutisha aliyowahi kutazama kipindi cha nyuma, na haikuonekana kama ingepita ndani ya muda mfupi.

Baada ya kufikiria kwa kina, akaona anyanyuke tu na kuchukua simu yake, naye akaona ilikuwa ni saa 6 na nusu usiku sasa. Akavaa kikaptura chepesi chini ya T-shirt lake refu alilokuwa amevaa na nguo ya ndani pekee, kisha akatoka chumbani kwake na kuelekea kwenye chumba cha pacha wake. Akaugonga mlango taratibu, kisha akausukuma kidogo na kuchungulia ndani. Sikuzote waliheshimiana hivyo ilikuwa ni lazima kugonga mlango kabla ya kuingia kwenye chumba cha mmoja na mwenzake ili kuepuka kukutana na hali zisizotazamiwa. Lakini kwa kuwa mvua ilikuwa kubwa, Alexandra akaona tu atumie zaidi sauti yake.

"Xander... Xander uko macho?" akauliza kwa sauti iliyosikika vizuri.

"Sandra? Ndiyo niko macho. Vipi?" Xander akajibu.

Sandra akasita kidogo, lakini akasema, "Naogopa."

"Unaogopa mvua? Ni kubwa kweli... siyo rahisi kulala..."

"Ndiyo. Naweza kulala huku? Kule nahisi kama vile kuna kitu nyuma ya shuka kinanivuta..."

"Ahahahah... Nsyuka eti?"

"Acha basi Xander!"

"Ahahah... sorry. Haina shida. Njoo ulale hapa. Usisahau... anything for you..."

Sandra akatabasamu kwa kuhisi ahueni, kisha akaingia na kuufunga mlango. Kulikuwa na giza lakini bado mianga ya radi ilifanya sehemu kubwa ya chumba ionekane. Sandra akatembea mpaka kitandani na kupanda, kisha akajilaza karibu kabisa na mwili wa pacha wake. Xander akalala kwa kumpa mgongo, hivyo Sandra akajibana nyuma yake na kupitisha mkono wake mmoja ubavuni kwa pacha wake; kama amemkumbatia kwa nyuma. Xander hakuwa amevaa kitu juu, ila chini alikuwa amevaa kaptura nyepesi ya ndani. Wakalivuta shuka na kuifunika miili yao vizuri.

Hii haikuwa mara ya kwanza kwa mapacha hawa kulala pamoja namna hii, lakini ni muda mrefu ulikuwa umepita. Binti akajibana vizuri kwenye mwili wa kaka yake, huku kichwa chake kikiwa nyuma ya shingo ya Xander, na hali hiyo ikamtuliza kwa kumfanya ajihisi salama sana, na pole kwa pole usingizi ukawajia wote wawili.

Dhoruba hii kali iliendelea, na ilionekana ni kama iliiandama nyumba hii ya Meja Casmir tu. Baada ya muda fulani, ilipiga radi kubwa sana, na mwanga mkali kupita maelezo ukakitawala chumba walicholala mapacha hawa. Lakini walikuwa mbali sana kiusingizi kuweza kusikia, kisha hali ikaanza kutulia. Haukupita muda mrefu na sehemu hii ikatulia kabisa. Dhoruba ikapita.


★★★


Asubuhi Ikafika. Xander ndiye aliyekuwa wa kwanza kuamka. Kulikuwa na mwanga wa mbali wa jua, na angalau sasa chumba kiliangazwa. Akajigeuza kivivuvivu na kujinyoosha akiwa amefumba macho yake bado. Lakini akaanza kujihisi utofauti fulani hivi. Kwanza kabisa, sikuzote alizoea kuamka na kuhisi msuli wake ukiwa mgumu haswa, lakini leo hakuhisi hilo. Ajabu. Akajinyanyua na kujiangalia kifuani.

'Nilivaa T-shirt saa ngapi?' akawaza. 'Subiri. Mbona kama upande niliolala siyo... What the hell?!' akajishangaa.

Alihisi ni kama labda alikuwa anaota. Kwa nini? Alikuwa na matiti kama mwanamke! Akatikisa kichwa chake kwa nguvu, lakini haikuonekana kuwa ndoto. Akajishika kwa chini, mashine haipo. Nini kinaendelea? Akatazama pembeni yake kwenye kitanda na kukuta amelala na mwanaume. Mwanaume huyo alikuwa ni yeye mwenyewe! Akatoa macho kwa mshangao.

Akamtikisa mtu huyo na kumwambia kwa sauti, "Wewe amka!"

Mh! Mbona sauti ya kike? Alishindwa kuelewa.

Mtu huyo akanyanyuka huku akisema, "Xander nini? Mbona una..."

Kabla hajamaliza kuongea, akatoa macho pia kwa mshangao. Lakini Xander alikuwa anamwona mtu huyu kuwa ni yeye akiuliza 'Xander nini?' Aliyeuliza hivyo akataka kupiga kelele, lakini Xander akamwahi na kumziba mdomo.

"Usipige kelele. Mama atazingua!" akamwambia.

Xander alikuwa ameuziba mdomo "wake" mwenyewe huku uso "wake" huo ukimwangalia kwa hofu sana. Kisha akaushusha taratibu mkono wake.

"Nini kinaendelea? Mbona mwili wangu... mbona nauona uko huko?" mwili wa Xander ukauliza.

"Sijui. Kwani ninafanana na..."

"Mimi! Sura yangu! Mwili wangu!"

Xander akatafakari kidogo, kisha akauliza kwa sauti ya chini, "Sandra?"

"Nnn..diyo..."

Xander akabaki mdomo wazi akishangaa sana. Alikuwa ametambua sasa kwamba mwili wake na wa dada yake ilikuwa imebadilishana. Ni nini kilikuwa kimetokea?


★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Previoua Next