Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

FOR YOU

Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa

Rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA NANE

★★★★★★★★★★★★★


"Sandra... uko ndani ya mwili wangu?" Xander akauliza.

"Na wewe uko ndani ya wa kwangu! Eh Mungu, nina besi!" Sandra akasema kwa kustaajabisha.

"Sandra... nini kimetokea?"

"Sijui. Sijui. Si... sijui. Nimekuja jana humu... umenifanya nini Xander?"

"Sijakufanya chochote Sandra..."

"Oh God... hii haiwezekani. Ooooh my God!"

"Nini?"

"Hili dude lako limevimba!"

"Sandra usijali hiyo ni kawaida tu. Itaisha baada ya muda..."

"Hapana hii haiwezekani. Nini kimetokea Xander? Nini, nini... nini..."

Xander, akiwa ndani ya mwili wa Sandra, akamshika Sandra mabegani, akiwa ndani ya mwili "wake."

"Sandra calm down..."

"Calm down?"

"Nisikilize mdoli..."

"Unawezaje kuniita mdoli wakati nina lisura lako hapa!"

"Tunafanana bwana! Tulia. Shit... nina sauti ya kike! Kuna vitu huku chini vinaniwasha-washa hata sielewi ni nini... kwa hiyo siyo wewe tu ambaye umeshtushwa na hili. Lakini tunahitaji kutulia ili kujua tunalitatuaje... tafadhali Sandra..." Xander akamwambia.

"Sandra" akaanza kutulia.

"Okay. Niko calm. Now what?" Sandra akauliza.

"Okay aam... jana umekuja hapa usiku... mvua kubwa ilikuwa inanyesha. Ukalala nyuma yangu... nini baada ya hapo?"

"Sijui! Ndiyo unaniamsha sasa hivi najikuta hivi. Xander tunafanyaje?"

"Usijali. Tutajua tu. Tutatafuta njia. Labda... labda tutaonana na daktari... au... sijui ikiwa itakuwa sawa kuwaambia mama na baba..."

"Watashangaa!"

"Na sijui kama hata watatuamini..."

"Kuna mtu ametufanyia uchawi Xander. Hii kitu hai-make sense!"

"Ni lazima tujue shida ni nini. Labda hatukutakiwa kulala pamoja..."

"Xander mara ngapi tumelala pamoja na hii haijawahi kutokea?"

Xander akashusha pumzi.

"Tunafanyaje? Mama na wengine hawataelewa maana hata na sisi hatuelewi. Kwa hiyo... sasa hivi nitapaswa tu kuwa wewe?" Sandra akauliza.

"Ndiyo..." Xander akajibu kiupole.

"Nini?!" Sandra akashangaa.

"Ndiyo. Itapaswa kuwa hivyo Sandra. Aisee! Sasa hivi nitapaswa kuwa nakuita Xander..."

"Eeh Mungu!"

"Usijali. We'll figure this out. Nahitaji umakini wako," akasema Xander.

"Sawa. Niambie."

"Okay. Kwa hiyo... nataka tu-test vitu fulani... kama nguvu... kumbukumbu na mambo mengine..."

"Kwa nguvu... mimi sasa hivi nina mwili wako kwa hiyo... nakubonda si ndiyo?" akasema Sandra.

"Ahahah... yeah. Na mimi sa'hivi najua kuchamba eeh?" Xander akamwambia kimaringo.

"Ahah... mimi sifanyagi hayo bwana. Lakini Xander, vipi kuhusu hiki kitu... nafanyaje... sitakiwi kuona dude lako wala kuligusa... yuck!" Sandra akasema.

Xander akacheka kidogo, kisha akamwambia, "Haina jinsi. We jisikie huru tu maana utapaswa kuoga nalo."

Sandra, akiwa ndani ya mwili huu wa kaka yake akaivuta kaptura nyepesi aliyovaa na kujiangalia.

"Eh Mungu! Ndiyo likubwa hivyo?"

"Ahahahah... asante. Hiyo hapo dada ni sifa kwangu..."

"Kwa hiyo... naenda kuoga... nafanya kila kitu nikiwa na mwili wako... na wewe je?" Sandra akauliza.

"Na mimi vice versa. Eheh... naenda chumbani kwako kuucheki mwili wangu mpya... heheheee!" Xander akasema kimasihara.

"Xander nakuonya! Usifanye jambo lolote lile la kipumbavu kwenye mwili wangu! Ukioga fumba macho, ukitaka kuvaa fumba macho, usijiangalie kwenye kioo, usishike nguo zangu za ndani, na ole wako... ooole wako umpe mjinga yoyote almasi yangu!" Sandra akamwonya.

Xander akabaki anamshangaa tu.

"Mimi sijakupa hayo masheria yote, mbona wewe unaniandama hivyo? Me sitaakiii..." Xander akaongea kwa deko eti kama mtoto wa kike kweli.

"Alexander..." Sandra akamwonyesha yuko 'serious.'

"Okay, okay usijali. Nitaulinda mwili wako. Ila kufanya hayo yote kwa njia hiyo ni ngumu. Hatuna jinsi dada yangu. Itabidi tu uniamini kama mimi navyokuamini. Usisahau... for me... for you," Xander akasema.

Sandra akabaki kumtazama tu. Xander akamshika kiganja.

"Come on say it..." akambembeleza.

Sandra akashusha pumzi, kisha akasema, "For me... for you..."

Xander sasa akiwa ndani ya mwili wa dada yake, akanyanyuka na kusimama chini. Akawa anajicheka jinsi alivyoonekana, huku Sandra naye akijiangalia pale kitandani. Kisha Xander akageuka na kuanza kutembea kimadoido kama mwanamitindo mpaka mlangoni, na alipoufikia akamgeukia "dada yake" kukuta anatikisa kichwa chake kwa kusikitika. Akaona atoke tu ndani ya chumba "chake" hiki na kuelekea kwenye chumba "chake" cha sasa. Ilikuwa ni hali moja ambayo ilifaa kupewa jina la kizungumkuti.

Xander alipofika kwenye chumba cha Sandra, akaelekea mpaka kwenye kioo na kujiangalia. Sura ya dada yake ilifanana na yake, lakini aliiona kuwa nzuri zaidi. Akatabasamu, kisha akavua T-shirt alilokuwa nalo mwilini. Kwa mara ya kwanza akayaona matiti ya dada yake, nayo yalikuwa yametuna vyema. Akaanza kuyashika na kuyavutavuta huku akicheka, lakini kadiri alivyoendelea alianza kupata hisi fulani mwilini "mwake," na kukawa na hisia kama za mtetemo fulani wenye kusisimua zilizoelekea kwenye almasi "yake."

Ijapokuwa hisia hizi zilikuwa mpya na zenye uajabu kwake, zilimfanya ajihisi vizuri sana. Akashusha kiganja chake kuelekea chini ili ajishike, lakini akili ikamrudia kukumbuka kwamba huu ulikuwa mwili wa dada yake, naye alipaswa kuuheshimu kama tu alivyomwahidi. Akajisahaulisha mambo hayo yote na kuamua kwenda kuoga haraka ili aanze kuuandaa mwili wake mpya kwa ajili ya chuo.

Kwa upande wake Sandra, aliona mambo kuwa magumu sana kuwa ndani ya mwili wa mwanaume. Hakuzoea kabisa kuwa na vinyweleo kwapani! Alipojitazama kwenye kioo, aliweza kuona jinsi mwili wa kaka yake ulivyokuwa imara, na aliweza kuhisi jinsi misuli ilivyokuwa na nguvu. Kufikia wakati huu, mashine "yake" ilikuwa imepungua, naye bado hakutaka kuiangalia hata kidogo kwa sababu aliona isingefaa. Ila kama kaka yake alivyomwambia, hakukuwa na jinsi. Kwa hiyo naye akaamua tu kwenda kuoga ili aanze kuuandaa mwili wake mpya kwa ajili ya chuo.

★★

Ilikuwa imefika saa 1 kamili asubuhi sasa. Salome ndiye aliyekuwa akifanya shughuli za ndani baada ya kumwamsha Azra ili ajiandae na shule wakati mapacha wakiwa wanajiandaa vyumbani, naye Alice alikuwa akivuta shuka bado. Baada ya Xander kumaliza kuuandaa mwili wa Sandra vizuri, akaenda kwenye chumba "chake" alikokuwa "dada yake." Aliingia tu na kumkuta akiwa anavaa T-shirt nyeupe na chini suruali ya jeans. Akatabasamu na kumwita, naye Sandra akamwangalia.

"Vipi? Nimependeza?" Xander akamuuliza huku akiweka pozi.

"Xander ndiyo umevaaje hiyo nguo?" Sandra akamshangaa.

Alikuwa amevaa kigauni chekundu kilichombana na kuishia magotini, lakini alikuwa amegeuza.

"Kwani vipi?" Xander akauliza.

"Umeigeuza hiyo nguo..."

"Nimei... aagh... yaani nguo zenu zinachanganya kweli..."

"Kwa hiyo kama nisingekuona ungeenda chuo hivyo hivyo?"

"Ahahah... ningeweka historia leo. Lakini ingekuwa ni WEWE..."

"Acha masihara Xander, em' vua uvae nyingine..."

"Nyingine? Si naweza tu kuigeuza hii?"

"Leo nilikuwa nataka kuvaa suruali..."

"Kwani hapo umevaa sketi?"

"Namaanisha kwenye mwili wangu!"

"Ahahahah..."

"Unazingua Xander. Nenda kabadilishe."

Xander akamsogelea.

"Una mwili mzuri Sandra. Lakini kiukweli, nakuwa napata shida nikiuangalia. Ni ajabu yaani. Ni mwili 'wangu,' lakini ni 'wako.' Wewe ndiyo mmiliki halisi na haipaswi kuwa hivi..." Xander akawa anamwambia kiustaarabu.

"Ninaelewa unavyohisi. Hata mimi siko comfortable kwa kweli. Kukojoa nimesimama ni ngumu mno," akasema Sandra.

"Ahah... jaribu kuchuchumaa ndo' utaona!" Xander akasema.

"Yaani sijui itakuwaje. Wengine hapa nyumbani, wanachuo wenzetu na marafiki... walimu..."

"Inaonekana ni ubongo... akili zetu ndiyo zime-switch kwenye miili yetu... lakini kumbukumbu zetu bado zipo. Hatuna njia nyingine ila kufekisha tu tabia. Me nijifanye ndiyo wewe, na wewe ujifanye ndiyo..."

"Najua. Lakini Xander haitakuwa rahisi. Kuna vitu hatutaweza ku-control. Marafiki zangu sa'hivi watapaswa kuwa wako. Unajua vitu wanavyopenda kufanya? Hujui! Na mimi ndiyo hivyo hivyo. Sitaelewa lugha ya 'washkaji' zako wakianza kunisemesha. Halafu... eh Mungu wangu!" Sandra akasema akiziba mdomo.

"Nini?"

"Mashindano ya kuogelea! Xander mashindano ya kuogelea! Oh God what am I going to do?"

"Sandra relax. Nitaogelea, kwani shida ni nini?"

"Usifikiri ni rahisi tu au huwa ni ovyo ovyo tu. Kuna technique tunatumia. Kujua wakati wa kuruka, wakati wa kujigeuza, wakati wa kunyoosha mikono... wewe haujajifunza hayo na hauna faida ya misuli unayotumiaga kujua jinsi mwili wangu unavyofanya ka... oh my God! Jamani nilikuwa nimeji... wenzangu wananitegemea..."

Sandra, akiwa kwenye mwili wa kaka yake akawa anaongea hivyo huku analia. Xander alimwonea huruma, lakini mambo haya yote yalimshangaza. Akamsogelea karibu na kumshika mabegani.

"Sandra, kama nilivyokwambia, tutajua la kufanya. Kwanza kabisa, itabidi tutatue hili kabla ya siku ya competition. Na pili... usiwe unalialia ukiwa ndani ya mwili wangu. Watu watakuwa wanakushangaa maana watafikiri ni mimi..." Xander akamwambia.

"Sawa. Samahani," Sandra akafuta machozi.

"Ngoja tu tupitishe siku ya leo chuoni kwa njia hii. Muda wote tutapaswa kuwa pamoja... ili kuepuka zari za kushtukiza. Tukirudi tujipange vizuri zaidi," Xander akamwambia.

Sandra akatikisa kichwa kuonyesha ameelewa.

Hali hii bado ilikuwa inampa shida sana Sandra, ambaye sasa alikuwa dume. Xander akavua kigauni hicho alichovaa na kukigeuza ili akivae vizuri. Akamtania kwamba mwili wake ulikuwa unauangalia wa dada yake ukivua nguo, lakini kihalisi alikuwa anajiangalia yeye mwenyewe. Mambo yalikuwa yanachanganya sana. Baada ya kumaliza kujitengeneza vyema, mapacha wakatoka pamoja kuelekea chini ili kuondoka.

Walipofika sebuleni walimkuta Salome akiwa anasafisha meza ya chakula sehemu ya 'dining,' nao wakamsalimu.

"Azra ameshaondoka?" Sandra, akiwa kwenye mwili wa Xander, akamuuliza Salome.

"Ndiyo ameshaenda. Mama bado amelala," Salome akajibu.

"Aaaa sawa..." Sandra akasema.

"Mvua ya jana haijaangusha miti huko nje kweli?" Xander, akiwa kwenye mwili wa Sandra, akauliza.

"Mh! Kale kamvua ndiyo kakuangusha mti?" Salome akauliza pia.

"Kamvua? Ilikuwa dhoruba! Niliogopa sana jana!" Sandra akasema akionekana kama Xander.

"Ahahah... hakukuwa na mvua jana bwana. Ilinyesha kidogo tu na hata baadae usiku nilipoamka sikuisikia tena," Salome akawaambia.

Mapacha wakatazamana kimaswali. Wakahisi labda Salome alikuwa amelala fofofo mno, hivyo labda hakuisikia dhoruba ya jana. Wakaona wamuage tu, kisha wakatoka nje.

Sandra alishukuru kwamba Xander aliwahi kumfundisha kuendesha pikipiki, la sivyo asingeweza kuiendesha akiwa kwenye mwili wa kaka yake. Wakapanda pamoja, Xander akiwa kwa nyuma na kufanya kama amemkumbatia dada yake ndani ya mwili "wake" kiutundu, kisha wakaondoka ili kuelekea chuoni.


★★★


NYUMBANI KWAO ISIMINZILE


Asubuhi hii Isiminzile aliamka mapema kama kawaida na kumaliza kujiandaa kwa ajili ya chuo. Ni wakati alipokuwa anatoka ili aondoke, pale alipovutwa mkono kwa nguvu. Alipomwangalia aliyemvuta akatambua ilikuwa ni bibi yake, naye akamzungusha mpaka nyuma ya nyumba yao ili waongee. Bibi yake alikuwa anamtazama kwa njia ya kimaswali, huku yeye Isiminzile akionyesha hofu.

"Wewe kichwa chako kina nini? Eeh?" bibi yake akauliza.

"Sh'kamoo bibi..."

"Sihitaji salamu yako. Juzi umekuja hujasema lolote. Jana ukanipita tu tena, halafu na leo unataka kunikwepa. Ndiyo makubaliano yetu yalivyokuwa?"

"Hapana bibi... nisamehe..."

"A-aagh... nataka uniambie kilichotokea. Kwa nini sijaona mabadiliko yoyote? Kwa nini unanikwepa? Huendi chuo mpaka useme la sivyo utanitambua!"

Isiminzile akawa anaangalia mara chini, mara juu, mara huku na kule, kwa wasiwasi tu. Hakujua aanze vipi kumwambia bibi yake jambo hili.

"Kwa hiyo? Naongea na bubu?" bibi akamshurutisha.

"Bibi... nisamehe sana... nisamehe bibi..."

"Kwa nini nikusamehe? Umefanyaje?"

"Sikufanikiwa..." akasema Isiminzile huku ameangalia chini.

"Hukufanikiwa? Kwa hiyo bado hujampa? Unaogopa? Basi kama ni hivyo nirudishie kitu yangu, sitaki ujinga mimi," bibi akamwambia.

"Hapana bibi. Nilijaribu... nilifanya vile ila... mambo yakaharibika!"

"NINI?!" bibi akashangaa.

Isiminzile akabaki tu kimya huku mapigo yake ya moyo yakikimbia sana.

"Yameharibikaje? Sema!" bibi akasema kiukali, lakini kwa sauti ya chini.

"Hakuinywa yule... walikunywa wengine!" Isiminzile akasema.

"Toba!" bibi akashangaa.

"Nisamehe bibi... mimi siku..."

Bibi yake akamtandika kofi la kichwani kwa nguvu. Isiminzile akajishika kichwa akihisi maumivu na hofu kubwa.

"Una akili wewe? Hivi una... una akili wewe?!" bibi akasema kwa hisia kali.

"Sikutarajia bibi..."

"Naomba useme nilikwambia nini, na wewe ukafanya nini. Sema..." bibi akamwambia.

"Uliniambia... ulinipa hiyo dawa ukasema niiweke kwenye soda moja..."

"Enhe..."

"... halafu niigawanyishe kwenye vikombe viwili, nimpe kwa mkono wa kushoto... akishakunywa tu, na mimi ninywe..."

"Ndiyo. Wewe ulifanya nini?"

"Nilifanya hivyo bibi. Alikunywa ila nilivyotaka tu kunywa yangu... pacha wake akaichukua na kuinywa yeye! Sikutegemea yaani...."

"Pacha wake? Huyo mkaka ana pacha?" bibi akauliza.

Isiminzile akabaki kumtazama tu.

"Huyo nanilii... Meki sijui... si ni wa pale juu? Toka lini ana pacha?!" bibi akauliza tena.

Isiminzile akabaki tu kimya.

"Niambie mshenzi wewe! Mimi nimekupa dawa umpe huyo mjinga uliyesema anakusumbua, wewe ukampa nani?" bibi akasema kwa mkazo.

"Ni... Alexander..." Isiminzile akasema kwa sauti ya chini.

"Ndiyo nani?"

"Ni mkaka mwingine wa hapo hapo chuo..."

"Aiyayayai! We mtoto una matatizo gani? Mm? Yaani... mbona hueleweki? Wewe si tulikubaliana unaenda kumpa... niambie nilichokwambia ufanye..."

"Bibi..."

"Sema mpumbavu wewe!"

"Uliniambia nikifanya hivyo... mambo yote ambayo nilikuwa natamani kutoka kwake Mecky yangekuwa yangu. Kila kitu kizuri kilichomfanya apendwe kingekuwa... watu wangekiona kwangu, na hata msichana wake angemwacha na kuja kwangu. Ningekuwa na nguvu zake... na yeye angenyong'onyea na kuonewa kama alivyokuwa ananifanyia..." Isiminzile akasema.

"Vizuri. Sasa nataka uniambie ni mdudu gani aliyekuingia kichwani kwako mpaka ukafanya mambo kinyume..."

"Bibi nisamehe. Ningempa Mecky ndiyo lakini... Xander ndiyo huwa anapendwa zaidi. Ana hela, ana kipaji, anaongea vizuri yaani kila mtu anampenda... hata msichana ninayemtaka anampenda yeye. Kwa hiyo... nikaamua kubadilishana bahati na yeye, siyo Mecky..." Isiminzile akasema.

"Mwana huyu mupuva sana! (Litoto lijinga sana hili!)" bibi yake akasema kwa kikabila huku anazunguka sehemu hiyo.

"Bibi nisamehe... nilikuwa naogopa kukwambia tu. Nisamehe sana..." Isiminzile akasema kwa huzuni.

"Unatenda kama litoto la darasa la pili, nami nilikuona mwerevu kumbe matope tu ndiyo yamejaa kichwani kwako. Haina shida. Maji yakishamwagika hayazoleki. Nenda chuo," bibi akamwambia huku akianza kuondoka.

"Lakini bibi... vipi kuhusu Xander na pacha wake?"

"Vipi kuhusu nyoko na pacha wake! Unaniuliza mimi hivyo nilikutuma umpe huyo mwingine? Utajua mwenyewe. Alaa! Mimi nimekupa msaada ili usiwe mnyonge mnyonge sana wewe ukauchezea! Na tena hata sikutakiwa kukuonyesha njia zetu za haya mambo ila nikakuonea sana huruma... halafu wewe unajikuta mjuaji zaidi. Kwenda huko chuoni na usiniambie matatizo yako tena..." bibi akasema kwa hasira na kusonya, kisha akarudi kwenye nyumba.

Isiminzile akaachwa njia panda. Kwa woga aliokuwa nao alianza hadi kulia. Ni yeye ndiye aliyekuwa chanzo cha hitilafu ile iliyowapata mapacha kupitia kwa bibi yake. Hakujua ni matatizo gani ambayo yangewapata mapacha wale kwa sababu ya ubinafsi wake, akiwaza labda hata wangekufa, na hakujua pia angeshughulika na suala hili namna gani hasa baada ya kumfanya bibi yake amkasirikie sana.

Akavuta tu mkanda wa begi lake mgongoni na kuanza kuondoka, akiwaza mengi mno kichwani kwake.


★★★


Wakiwa bado njiani kuelekea chuoni, mapacha waliongelea kuhusu mahusiano yao kwa wapenzi wao. Sandra alimweka wazi Xander kuhusu Raymond, na kwamba ameshafanya mapenzi pamoja naye mara tatu tokea walipoanza ku-date, naye Xander akamwambia ameshafanya mapenzi mara 394 na Ramla. Sandra akacheka sana, akijua ni jinsi gani mdada yule alivyo na mchecheto, lakini pia kwamba Xander anamtania tu. Kwa kuwa hawakujua hali hii ingeisha lini, wakakubaliana kwamba hawakutakiwa kuifanyisha miili yao mapenzi na yeyote, hata kama waliwaomba kufanya hivyo.

Sandra ndiye aliyesisitiza sana kuhusu hilo kwa sababu alijua Xander ni mkorofi, lakini kaka yake akamhakikishia kuwa mwili wa dada yake kipenzi ungekuwa salama. Katika mazungumzo yao hayo, Xander alisahau kumwambia dada yake kuhusu jambo moja; madam Valentina. Hakumwambia kuhusu kilichoendelea baina yake na mwalimu wao huyo, hivyo akawa hajamweka tayari kwa lolote ambalo lingetokea baina "yake" na madam Valentina.


★★


Walipofika chuoni, wakaegesha pikipiki ndani ya uzio wa jengo sehemu ya kuegeshea, kisha Xander akashuka kutoka kwenye pikipiki (akiwa kwenye mwili wa Sandra), naye akawa eti anajitengeneza-tengeneza na kurembua-rembua kimakusudi tu ili aonekane mrembo sana. Sandra alikuwa mrembo, lakini Xander alizidisha chumvi sana na kuanza kuutembeza mwili wa dada yake kimadoido mno. Sandra akiwa ndani ya mwili wa kaka yake akamwahi na kumshika mkono.

"Xander unafanya nini?" akamuuliza.

"Si ndo' nakuwa wewe au?" akamjibu huku anarembua.

"Naomba usinifanye nikaonekana kituko! Mimi siyo Joti..."

"Ahahaaa... unaloo..."

"Acha... mambo hayo nimekwambia sifanyagi. Kuwa kawaida tu. Ila usiwe 'wewe' sana... na penyewe utaharibu..."

"Nafurahi kuona sasa hivi wewe ndiyo unanipa ushauri, ikimaanisha utanitendea na mimi haki. Just relax... twende tuwahi kipindi..."

"Subiri. Tunahitaji kubadilishana simu," Sandra akamwambia.

"Kwa nini?"

"Kwa sababu tumebadilishwa miili mjinga wewe!"

"Ahahahah mdoli bhana... uko intense kweli badala ufurahie sa'hivi utakuwa unagonga watu..." Xander akamwambia huku anatoa simu kutoka kwenye pochi "yake."

Wakabadilishana simu zao na kuanza kuyaelekea majengo yenye madarasa pamoja. Walitembea kwa ukaribu sana. Xander alikuwa anasalimiana na kila mtu aliyepishana naye huku akijitahidi kuigiza kawaida ya dada yake ya kutembea, naye Sandra alikuwa kimya tu akitembea kawaida. Kipindi cha kwanza ambacho wangeenda kilikuwa ni cha somo la masuala ya tovuti (Web Technology). Kwa kuwa iliwabidi wabadilishane hadi madaftari, ingehitajika waandikiane na mambo muhimu pia waliyojifunza.

Marafiki zao wachache waliokuwepo hapo kabla ya mwalimu kufika, waliwachangamkia kama kawaida. Sophia, rafiki wa karibu zaidi wa Sandra, alipiga naye story nyingi bila kujua anayeongea naye ni Xander. Xander alimchekesha mno kwa maneno mengi yaliyomfanya mpaka Sophia aone ni kama "rafiki" yake amebadilika. Sophia pia alisomea kozi hii waliyosomea mapacha, kutia ndani Lucas, Bernard, Mecky na Hussein. Rafiki za Xander waliona akiwa kimya tu karibia muda wote, asichangie maongezi yao ya kishkaji kabisa. Lakini Sandra akiwa kwa ndani pia alijitahidi kuigiza kama yuko poa tu, kwa hiyo hakukuwa na shida iliyotokea, nao wakaendelea kumsubiri mwalimu.

(Note: Nitawaelezea mapacha hawa waliobadilishwa miili kwa njia hii fupi: Nikiandika "Xander (Sandra)" hiyo inamaanisha kwamba ni mwili wa Xander, lakini aliye ndani ni Sandra. Na "Sandra (Xander)" inamaanisha ni mwili wa Sandra lakini aliye ndani ni Xander. Hii itakuwa hasa kwenye sehemu ambazo wanakuwa pamoja na watu wengine au nikiwaelezea, lakini wakiwa peke yao nitatumia majina yao kawaida).

Baada ya mwalimu kuwa amefika, wakaingia darasani na kuanza kujifunza. Mwalimu huyu, mwanaume aliyekuwa mnene kiasi, alipendwa nao kwa sababu yeye pia alikuwa mstaarabu, na alijua kufundisha. Aliwaelezea mambo vizuri sana kila alipoulizwa maswali, na jina lake lilikuwa Paul Ruta; au Sir Paul kama walivyozoea kumwita. Baada ya kuwafundisha jambo fulani siku hiyo, akawaomba wamuulize maswali, lakini hakuna hata mmoja aliyeuliza. Hivyo yeye akaona awaulize swali rahisi ili kuona kama wameshika vitu fulani kichwani.

"Haya ngoja mimi niwaulize... chemshabongo. WebKit huwa inatumika kwenye nini?"

Wote wakaendelea kumwangalia tu bila yeyote kunyoosha mkono. Kisha, Xander (Sandra) akanyoosha kiganja chake juu ili atoe jibu. Alikuwa ameketi kiti cha nyuma yake Sandra (Xander).

Sir Paul akasema, "Alexander..."

Xander, akiwa kwenye mwili wa Sandra, alikuwa ameangalia chini kwenye simu yake, lakini aliposikia jina lake likiitwa, akajisahau na kunyanyua uso.

"Naam..." Sandra (Xander) akaitika.

"Huwa inatumika kwenye browser kama Chrome na Safari," akajibu Xander (Sandra).

Jibu lilikuwa sahihi, lakini hii hali ikamchanganya kiasi mwalimu, na hata Sophia pia.

"Ndiyo ni kweli, asante. Alexandra ulikuwa unataka kusema nini?" Sir Paul akamuuliza aliyemwona kama Sandra.

"Hamna kitu," akajibu Sandra, akiwa ndani ya mwili wa Xander, kwa kujisahau pia.

Mh! Mwalimu Paul akashindwa kuelewa kwa nini amemuuliza Sandra swali lakini akajibu Xander.

"Sawa. Asante Alexander," Sir Paul akasema.

Xander, akionekana kuwa Sandra, akanyanyua uso wake tena na kusema, "Karibu sana."

Mwalimu Paul akakunja uso kimaswali. Haikuwachukua sekunde nyingi mapacha hawa kutambua kuwa walikuwa wamejisahau sana. Mwalimu akageukia ubaoni akiwa bado anajiuliza nini walikuwa wanamfanyia, naye Sandra (Xander) akamgeukia Xander (Sandra) na kumwangalia kwa yale macho ya 'tumeshaharibu.' Mwalimu Paul akawaangalia tena mapacha hawa, huku wengine darasani wakiwatazama pia.

"Okay. Alexander amesema Webkit ni kwenye Chrome na Safari. Nikumbusheni kazi yake ni nini," akawauliza.

Sophia akanyoosha mkono na kuchaguliwa. "Inaziwekea browser HTML code na CSS. Ili kui-apply, tunapaswa kuandika -webkit pamoja na CSS kwenye code za HTML," akajibu.

"Safi sana. Vizuri sana. Nani anaweza kuniambia ni tool engine gani ambazo husaidia kuweka code hizo kwenye Opera, Firefox, na Internet Explorer?" Sir Paul akawauliza tena.

Alikuwa amefanya kusisitiza maswali ili aone itikio lingine kutoka kwa mapacha, naye akalipata. Wakati huu, aliyenyoosha mkono alikuwa ni Xander ndani ya mwili wa Sandra, naye akamchagua.

"Alexandra..." Sir Paul akaita.

"Opera wenyewe ni Presto, Internet Explorer ni Microsoft Edge, halafu Mozilla Firefox ni...." Sandra (Xander) akaishia hivyo.

'Ni Gecko,' Sandra akajisemea kichwani kwake kama anamwambia Xander.

Cha kushangaza ni kwamba, Xander akamsikia!

"...ni Gecko," Sandra (Xander) akasema kwa sauti bila kuwa na uhakika sana.

Mwalimu Paul akatabasamu tu na kumpongeza kwa kutoa majibu sahihi. Zamu hii hakuona jambo lolote lililotia wasiwasi, hivyo akaona aachane nalo tu na kuanza kujiandaa kutoka. Lakini Xander alibaki akitafakari kuhusu sauti ya dada yake aliyoisikia kichwani. Xander akamgeukia Sandra.

"Hey mdoli, ulinisemesha?" akamuuliza kwa sauti ya chini.

"Saa ngapi?" Sandra akauliza.

"Wakati natoa jibu..."

"Hamna. Sikiliza. Mazoezi ya kuogelea saa 5. Kaa karibu na Sophia ili uone atakavyofanya mambo na wewe uige. Ah yaani sijui itakuwaje..."

"Usihofu. Me nitafurahia sana kuwaona watoto ndani ya swimsuit... vinanilii vikiwa vimevimba-vimba siunajua... hwehwehwe..." Xander akatania.

Mwalimu Paul akatoka darasani.

"Acha sifa. Sitaki u..."

"Sandra, twende zetu kwa Lava," Sophia akawakatisha.

Lava lilikuwa ni jina la kijana aliyefanya kazi ya upishi kantini. Mara nyingi watu waliposema twende kwa Lava walimaanisha kwenda kula chips mayai au kavu, kwa kuwa yeye ndiyo alikaanga.

"Mh! Kwa Lava mapema hii yote kufanya nini?" Sandra (Xander) akamuuliza.

"Si kuhusu ile ishu... au umesahau?" Sophia akamuuliza.

Sandra (Xander) akamtazama Xander (Sandra), naye akampa ishara ya haraka kwamba akubali.

"Aaaa... sawa. Twende zetu best... shostito," Sandra (Xander) akamwambia Sophia.

"Mhm... sijui umekuaje leo," Sophia akasema na kuanza kuelekea nje.

"Xander, mnaenda kwa Lava ili kupokea ujumbe kutoka kwa Tobias. Anapaswa akupe wewe, na usimwonyeshe yeyote labda Sophia tu..." Sandra akamnong'oneza haraka.

"Unahusu nini?" Xander akamuuliza.

"Ukishasoma tu utauelewa halafu ujiigilizishe vizuri. Mimi..."

"Jamani twende basi!" Sophia akasema kutokea mlangoni.

Sandra (Xander) akaanza kunyanyuka, akimwambia Xander (Sandra) kwa utani kwamba anatumaini haitakuwa madawa ya kulevya. Yeye na Sophia wakaondoka pamoja kuelekea kule. Lucas na wenzake wakamfata Xander (Sandra) na kuanza kuongea naye. Wakati wakiwa bado kwenye chumba hicho hicho, akapata ujumbe wa simu kutoka kwa madam Valentina. Jina alilokuwa ametunza Xander ni "madamV" hivyo ilikuwa rahisi kwa Sandra kujua ni yeye.

'Njoo ofisini.'

Ulisomeka hivyo. Rahisi sana kuelewa. Lakini Sandra akaanza kuwaza ni nini ambacho madam wao huyo angetaka kutoka kwa Xander mpaka amwite ofisini kwake. Kwa haraka akafikia mkataa kwamba huenda kulikuwa na kazi ameiacha huko, au Xander alikuwa amemfanyia ukorofi. Akawaaga rafiki "zake" akisema yeye anakwenda ofisini mara moja, nao wote wakatoka pamoja naye kisha walipofika kule nje wakamwacha aelekee huko.

Sandra, akiwa mwilini mwa kaka yake, akafika nje ya mlango wa ofisi aliyojua ilimhusu Valentina. Akagonga mlango kidogo, naye akasikia sauti ya madam ikimwambia apite ndani. Akaingia na kuuacha mlango ukiwa wazi kidogo na kwenda taratibu kumwelekea madam Valentina. Alikuwa ameketi kwenye kiti chake huku akimwangalia "Xander" kwa tabasamu hafifu usoni. Sandra akajitahidi kuonyesha heshima na kumsalimu kwanza.

"Madam V... sh'kamoo..." akamwamkia.

Valentina akacheka kidogo huku anatikisa kichwa chake. Yeye alifikiri huu ni utani mwingine wa Xander, akimwacha Sandra anashangaa kwa nini amecheka.

"Huishiwagi vituko eti?" Valentina akasema.

Sandra, akiwa anatambua kwamba anayesemeshwa ni Xander, akatabasamu kwa njia ya kujiamini kama kaka yake tu.

"Mbona hujani-check leo?" Valentina akauliza.

"Aam... ndiyo nimetoka kwenye kipindi nika... nikaona meseji yako. Kuna jambo fulani unataka kuniambia madam?" Xander (Sandra) akauliza.

"Ndiyo mwanafunzi wangu," Valentina akasema huku anatabasamu.

Kisha akanyanyuka na kumpita ''Xander" aliposimama mpaka mlangoni, naye akaufunga na kurudi kwake. Sandra alikuwa anashangazwa na haya yote, akikisia-kisia kichwani kwamba huenda madam Valentina alikuwa anamtaka Xander, lakini hakuwa na uhakika mwingi. Ni mpaka Valentina alipomkaribia na kupitisha mikono yake kiunoni kwake ndipo akatambua kuwa wawili hawa walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

"Nimekumiss... ijapokuwa ilikuwa jana tu," Valentina akasema kwa sauti yenye kudeka fulani hivi.

Sandra aliona hii kuwa ajabu, kwa sababu kihalisi huyu alikuwa ni mwanamke mwenzake akimwambia maneno ya kimapenzi. Lakini akaitikia haraka kwa kumshika mabegani na kutabasamu kiajabu-ajabu tu.

"Mimi pia," akasema bila kuelewa kilichomaanishwa hasa.

Valentina akamsogelea mdomoni na kumpiga busu laini iliyojaa upendo mwingi. Sandra akabaki kukodoa macho yake tu, akishindwa kuijibu busu hii kiusahihi. Mwili wake wa kiume ukaanza kupatwa na hisia za kimahaba ambazo zilimsisimua na kumchanganya kwa wakati mmoja. Akawa kama anamsukuma Valentina nyuma kidogo, naye madam akaivunja busu taratibu na kumwangalia kimaswali.

"Vipi?" Valentina akamuuliza.

"Aa... hamna kitu. Hapa ni ofisini kwa hiyo... niliogopa," Xander (Sandra) akajitetea.

"Ahah... toka lini umeanza kuogopa kwa sababu tuko ofisini? We ndiyo umenizoesha hivi. Au nimeshaanza kukuboa tayari?" Valentina akauliza.

"No, no, no... pfff... nani akuchoke? Siwezi. Aam... sijisikii vizuri sana leo... tuta...."

"Xander vipi, mbona hivyo?" Valentina akauliza kimashaka.

"I'm sorry. Nitakwambia lakini... nahitaji kwenda... I'm so sorry madam," Xander (Sandra) akasema.

Akaitoa mikono ya madam Valentina kiunoni kwake na kuanza kuondoka hapo haraka, bila kugeuka nyuma hata mara moja kumwangalia mpaka alipoondoka ofisini humo. Valentina alibaki kushangaa kwa kuwa hakuelewa mpenzi wake mpya alikuwa na tatizo gani. Huyu hakuwa Xander aliyemzoea kabisa, na kitendo hiki kikamkosesha raha sana.


★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Previoua Next