MIMI NA MIMI
A Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU
★★★★★★★★★★★★★★★★★
Mkono wangu bado ulikuwa kiunoni kwa Bertha, nami nikautoa taratibu na kukaa kwa njia tulivu tu, huku nikimtazama jamaa bila hisia yoyote usoni. Kitambo eh? Ndiyo nilikuwa namwona leo sasa, akiwa ndani ya T-shirt jeupe la Manga na suruali ya jeans iliyopauka, huku kofia ikificha nywele zake kichwani.
Akasogea mpaka usawa wa meza ya mwanzo huku akitutazama kwa umakini, naye Bertha akaweka glasi yake pembeni.
"Vipi?" Bertha akamuuliza hivyo.
"Kwa hiyo dogo... ukaona haitoshi kumchokonoa Joy sasa hivi umehamia kwa mke wangu, si ndiyo?" Gonga akaniambia hivyo kwa sauti yenye uzito.
"E-eeh honey, tuliza bass. Mimi siko kama wewe, unanielewa?" Bertha akamwambia hivyo.
"Nakuuliza JC. Umekosa wanawake wengine mpaka umfate MKE WANGU?!" akaongea kwa kufoka.
Nikamwangalia kwa hisia kali.
"Ahaa... kumbe una kiburi?" jamaa akaniambia hivyo.
Kilichofuata ikawa ni yeye kurudisha mkono wake nyuma na kuchomoa bastola, naye akawa ananiangalia kama vile anataka kupasuka. Eti ana uchungu sana! Sijui hata alikuwa ametokea wapi ghafla namna hiyo.
Bertha akaanza kucheka kwa dharau, naye akasimama kabisa na kuyumba kidogo. Nikamwahi na kumshika mkono, mimi pia nikiwa nimesimama sasa, naye akatabasamu na kunipiga kifuani mara mbili kwa kiganja chake.
Akaanza kuelekea pale ambapo Chalii Gonga alikuwa amesimama na kumfikia karibu zaidi, naye akajishika kiuno chake huku akimwangalia kibabe.
"Unafikiri hicho kimguu kinamwogopesha mtu yeyote humu ndani? Mhm... una panick attack Chaz. Tena unajikosha kifala sana. Hata haikupendezi. Unataka kushoot mtu? Anza na mimi," Bertha akamsemesha hivyo bila woga.
Ukimya wa Chalii Gonga kumwelekea mke wake ulifanya ionekene wazi kwamba mwanamke ndiye aliyekuwa na sauti, na undani wa haya maigizo yaliyomleta Chalii mpaka hapa na kutaka kuhamisha hasira zake kwangu ulikuwa ni mpana. Nikaendelea tu kusimama na kuwaangalia.
"Umepata kimjusi cha kuku(.....) unaona sifai sa'hivi, si ndiyo?" Chalii akamuuliza hivyo mke wake.
"Acha ungese Chaz. Kwa kipi ambacho kinakupa wewe hadhi ya kufaa labda? Huo unafiki wako haukusaidii lolote. Kwamba nini, unafikiri ndiyo nitaanza kurukaruka 'eeh mume wangu ananipenda jamani!' Ahahahah... Chaz... stop it. Mimi ni mke wako, siyo kama malaya zako, na japo unaendelea kuchafua mambo mengi, bado ni mimi ndiye nayekusafishia kwa sababu tu ya kuenzi kule tulikotoka. Lakini we' si umeshapasahau? Ndiyo maana unafikiri leo ukinitolea bunduki nitaogopa..." Bertha akasema hayo.
"Siyo hivyo. Yaani... kwanza, haifai kuongea haya yote mbele ya huyu pakashumi. Unataka kusema unamwamini sana kuliko Mimi? Amekupa nini mama G?" Chalii akamuuliza hivyo.
"Usiniite hivyo!"
Sauti ya Bertha iligeuka kuwa na uzito aliposema hivyo, na aliongea taratibu tu lakini ilikuwa kwa ukali ule wa kutoka moyoni. Chalii Gonga akaangalia pembeni.
"Huyu ana fungu lake hapa. Hakuhusu. Mbona hata wewe mwanzoni ulitaka kumchukua kabla ya malaya wako kuuliwa? Acha unafiki Chaz... wewe ndiyo pakashumi," Bertha akamwambia hivyo.
Chalii Gonga akaniangalia na kusema, "Dogo leo unasikia natukanwa na mke wangu kwa sababu yako. Haki ya Mungu utalipia!"
"Ahiii... Charles!" Bertha akasema hivyo kwa mkazo.
Nikawa nimetulia tu, kila kitu nikikisoma fresh.
"Charles! Nije kusikia umemgusa huyu kijana, ndiyo utajua kwa nini huwa wananiita madam! Tena unajua. Unanijua. Ole wako! Aisee, nitakachokufanya zamu hii? Utatamani hata ujute lakini hautaweza," Bertha akamwambia hivyo.
Nikatazama pembeni na kuachia tabasamu la kiburi kiasi. Huyu mwanamke ndiye mtu ambaye umakini wangu wote wa kumporomosha ulikuwa kwake, lakini kwa wakati huu yeye ndiyo akawa amesimama kama malaika wangu. Ha! Wazungu husema twists in turns, yaani hali zisizotazamiwa ndani ya mizunguko ile ile, ndiyo kitu ambacho kilikuwa kinatokea hapa.
Sikuwa hata nimefanya mengi lakini tayari nikawa nimeshaanza, ama labda kuendelea kuwavuruga wanandoa hawa walioonekana kuwa na uhusiano wa kimaslahi tu. Na sasa nikawa nimetengeneza uadui wa wazi kabisa na mume, huku mke mwenye sauti akiwa ndiyo mlezi wangu. Na kumsikia Bertha akisema "zamu hii" ilimaanisha kwamba tayari alikuwa ameshawahi kumfundisha adabu Chalii Gonga huko nyuma, kwa hiyo ni kweli huyu mwanamke angepaswa kuwa kuchunga.
Chalii Gonga akaniangalia kwa macho yenye chuki kali, kama kusema "sisi si milima, tutakutana," kisha akaiweka bastola yake kiunoni na kuondoka hapo hatimaye. Bertha akaachia msonyo mrefu kweli na kunigeukia, naye akaninyooshea mkono wake kama kuniita nimfate. Nikaenda mpaka alipokuwa na kukishika kiganja chake.
"Usimwogope huyo, hawezi kukugusa, sawa?" akaniambia hivyo.
"Najua. Nikiwa na wewe, siogopi hata nyoka," nikamtania.
Akatabasamu na kukitoa kiganja chake kwenye changu, naye akasema, "We' nenda sasa. Nimwambie Dotto akusindikize?"
Kwa haraka nilitambua kwamba Dotto ndiyo yule baunsa wake, na ilishangaza kiasi kwamba tokea jamaa alipoondoka mpaka Chalii Gonga kuingia ndani humu, hakuwa amerudi kabisa.
Nikamwambia Bertha, "Hakuna shida, home hapo tu. Tutaonana kesho. Niombee ili Chalii asiturushie bomu."
"Si umesema hauogopi?"
"Ndiyo siogopi. Ila kuna raha gani nikifa mapema?"
Akaachia tabasamu hafifu na kuangalia pembeni, naye akasema, "Nenda. Usisahau kesho."
"Uhakika," nikamwambia.
"Hiyo kitu iache," akasema hivyo, akiwa amemaanisha yale madawa.
Nikatikisa kichwa kukubali, kisha nikampita na kutoka.
Nikashusha pumzi na kufumba macho kwanza, nikiwa najitahidi sana kutuliza hasira niliyokuwa nahisi. Kiukweli nilikuwa nimejawa na chuki kali sana moyoni kuwaelekea hawa watu wawili, na haijalishi hali ilikuwa vipi wakati tuko humo ndani, yaani kuwaona hivyo kwa pamoja kulikuwa kumenifanya nitamani hata kuwa na bastola ya kuwaangamiza!
Kuna kitu kilichokuwa kinaniambia kwamba suala zima la kumuua Joy halikutokana na kitu kama wivu wa mapenzi tu, na hii hasa ni baada ya kuona namna ambavyo huyo mwanamke alimwendesha mume wake.
Chalii Gonga alimwogopa Bertha kwa sababu fulani, sababu ambayo huenda ndiyo ilifanya mwanamke huyo akasirike sana mume wake alipomwita "Mama G." Ningehitaji kuendelea kujiweka karibu zaidi na huyo boss lady, na kuwa chonjo zaidi na mume wake kuanzia sasa.
Nikapitia geti la nyuma na kuanza kuelekea upande tofauti na nyumbani, nikiwa makini sana kuona ikiwa nilifatiliwa. Si unajua haingekuwa poa endapo kama mtu angetaka kuniua halafu niende moja kwa moja kwa Ankia na kumpelekea shida zisizomhusu dada wa watu? Ingawa nilielewa kwamba Chalii Gonga aligongwa marufuku, bado nilitaka tu kuwa makini, nami nikafanikiwa kuzungukia njia nyingine mpaka kufikia pale tulipoishi bila kutatiliwa. Dah! Likizo yangu ilikuwa imeanza kujaa visa!
Nikalipita duka la Fatuma na kwenda mpaka ndani ya geti, nami nikasimama karibu na ukuta; sehemu ile ile niliyotulia ule usiku na kumsikia Joshua akiongea maovu yake. Nikaona kupitia matundu ya ukuta gari la bibie Miryam hapo nje, nami nikaelewa kwamba walikuwa wamerudi kutoka kwa huyo mpuuzi.
Nikawa nimeingiwa na hamu ya kutaka kwenda kumwona Mariam, nijue anaendelea vipi, lakini tena nikakumbuka kwamba Adelina alikuwa hapo kwa Ankia; na nilimwahidi kuwahi kurudi ili angalau tupatane kidogo. Ikiwa ningeenda kumwona Mariam najua ningehitaji kukaa tena hapo kwa muda zaidi. Aigh! Ningejigawaje, maana na akili yangu tayari ilikuwa imevurugwa na maadui zangu?
Nikaona nimpigie kwanza Tesha kumuuliza ikiwa alikuwa amesharudi... aaah kweli, nikakumbuka simu yake ilikuwa imeibiwa, hivyo nisingeweza kumpata. Nikaachana naye na kuamua niende tu kwa mgeni wetu, nami nikavaa sura ya kondoo na kwenda mpaka ndani.
Nikakuta Adelina akiwa amekaa pale pale sofani huku akiwa bize na simu yake, na baada ya kuniona akaachia tabasamu hafifu tu. Ankia hakuwepo hapo, nami kwa wakati huu ndiyo nikaweza kumchora vyema zaidi Adelina tofauti na nilivyokuja mara ya kwanza nikiwa na haraka.
Alivaa T-shirt la mikono mifupi, lenye rangi mchanganyiko wa nyeupe, zambarau, na pink, kwa mtindo wa mistari minene kama ngozi ya pundamilia, na miguuni ilikuwa ni suruali ya jeans iliyobana vyema umbo lake kuniruhusu kuona kwamba alikuwa na shepu nzuri sana. Yaani alikuwa na miguu mirefu, halafu paja lilikuwa nono na hips kujaa, na kwa jinsi alivyochomekea hiyo T-shirt kwenye suruali na kuivuta suruali mpaka kufikia tumboni, nilijua huko nyuma kwake kungenifanya nije kumwangalia kwa macho yenye dhambi!
Alikuwa black beauty, msafi, na wakati huu niliona msuko wake kichwani kuwa wa zile rasta ndefu zenye rangi ya kahawia, zikiwa zimemwagikia mgongoni kwake. Mkufu mzuri shingoni, mabangili mkononi, saa, yaani kama huyu mwanamke hakuwa na kazi ya maana hapa jijini, basi ni lazima kuna njemba iliyokuwa inagharamika mno hapo. Alionekana kujipenda kama tu Joy alivyokuwa.
"Adelina... nilifikiri ningekuta umeshasepa," nikamwambia hivyo baada ya kufunga mlango.
"Hamna, nipo. Vipi mishe?" akasema hivyo.
"Fresh. Ankia?"
"Yuko chumbani, ameingia sasa hivi tu," Adelina akanijibu.
"Ahaa, sawa," nikasema hivyo na kukaa kwenye sofa hilo hilo karibu naye.
"Vipi wa Kigamboni wanasemaje?" akaniuliza.
"Ah, unafikiri hata tumezungukia huko sana? Tumepita kivuko tu, mvua ikaanza kunyesha, kwo' ikatubidi tutimkie Kariakoo na kuzungukia sehemu zingine."
"Aaa... pole lakini. Mwenzako je?"
"Tuliachana pale Uhasibu, ye' akaelekea kwingine. Umefika zamani?"
"Hamna... ni kwenye saa kumi na moja..."
"Asa' si hata ungenitumia ujumbe kuniambia, labda hata ningewahi," nikamwambia hivyo.
"Aa, hamna. We' ulipaswa kumaliza mizunguko yako, me hapa ungenikuta tu," akaniambia hivyo.
"Au siyo?" nikamuuliza hivyo.
Akacheka kidogo kwa pumzi.
"Mbona huyu naye kakuacha peke yako tena?" nikamuuliza.
"Ameenda kuongea na simu," akaniambia hivyo.
"Ahaa, sirini eti? Watu na wapenzi wao..."
"Ahahahah... inawezekana," akasema hivyo.
Alikuwa na kicheko kizuri sana, nami nikiwa nataka kuendeleza story ndiyo ile "kwechee" ya mlango wa chumba cha Ankia ikasikika. Sote tukaangalia upande huo na kumwona Ankia anatoka, lakini bado alikuwa anamalizia kuufungua mlango wake taratibu huku macho yake yakiwa kwenye simu kiganjani, na huo mlango ukawa unamalizia kelele zake kama vile unacheka. Eee-he-he-e-e-e-e-e-e...!
Nikacheka kidogo na kusema, "Unausikia huo mlango lakini?"
Adelina akacheka kidogo, naye Ankia akaja upande wetu na kusema, "Hiyo sauti me mwenyewe inanikera!"
"Ni kukukera tu eeh, sijui shauri ya umaskini? Hadi mlango unakucheka kwa sababu umeuacha uzeeke," nikamtania hivyo Ankia.
Adelina akacheka tena, na mimi nilikuwa nataka tu nisikie kicheko chake, naye Ankia akacheka pia na kusema, "Kichwa chako."
Mwanamke huyo alikuwa amevaa kawaida yake ya nyumbani na kilemba, huku leo tena ndiyo nikimwona na pini puani kwa mara nyingine tokea mara ya kwanza nimefika hapa.
"Wakina Bi Zawadi wamefika zamani sana?" nikamuuliza Ankia.
"Siyo sana. Muda ule umerudi na kuondoka tena, ndiyo Miryam akaja kuchukua funguo zao. Tesha umemwacha wapi?" Ankia akauliza.
"Yupo Uhasibu, atakuja baadaye," nikamwambia.
"Ahaa sawa. Kwa hiyo unaenda kuwaona warembo wako?" Ankia akauliza hivyo.
"Nitawapigia simu baadaye kumsalimia Mamu pia maana... ishakuwa usiku kwenda kabisa," nikamwambia hivyo.
"Na unavyompenda Mamu! Mhm..." Ankia akasema.
"Ni mgonjwa wake, kumpenda lazima," Adelina akasema.
"Umeona? Kana wivu haka!" nikamwambia hivyo Adelina, naye akatabasamu.
"Haya bwana. Zawadi yangu iko wapi?" Ankia akauliza.
"Ah... nimesahau, mambo mengi. Kesho basi," nikamwambia hivyo.
"A-aah... me sitaki. Nipe zawadi yangu, uliniahidi. Tena... unapaswa kumpa na mgeni," akaniambia hivyo.
"Ila Ankia! Nitatoa wapi sasa na msimu wa Krismasi bado?" nikamuuliza pia.
"Ahahah... ameanza kudeka sasa," Adelina akasema.
"Nipe bwana hata nimfatie mgeni K-Vant," Ankia akaendelea kulazimisha.
"Ankia mbona una king'anganizi hivyo? Na mimi sitaki hiyo K-Vant usimpe presha mwenzako bwana," Adelina akamwambia hivyo.
"Unatumiaga K-Vant?" nikamuuliza Adelina.
"Nikiwa tu nataka kulewa, na sasa hivi sijisikii," akanijibu.
"Basi hata Dompo tu jamani," Ankia akasema hivyo.
Niliweza kuona kwa jicho la pembeni kwamba Adelina alikuwa anajaribu kumzuia Ankia kwa ishara ya kichwa asiombe hayo mambo, nami nikatabasamu na kutoa wallet yangu. Nikachomoa shilingi elfu kumi na kumpa Ankia, naye akaipokea kwa furaha huku aking'ata mdomo wake.
"Ngoja nikafate Dompo," Ankia akasema hivyo kwa madoido.
"Masai?" nikamuuliza.
"Hamna, kuna grocery tu hapo pembeni. Nakuja sasa hivi," akasema hivyo na kuondoka upesi.
Inaonekana alikuwa na hamu sana na kileo!
Nikamtazama Adelina machoni, naye akaniangalia pia, kisha nikauliza, "Ulijuaje kwamba Mariam ni mgonjwa wangu? Unamjua?"
Akasema, "Hapana. Ankia ndiyo kaniambia. Kasema wewe ni daktari kabisa na unamsaidia huyo msichana. Nimemwona na dada yake leo alipokuja kuchukua funguo."
"Ahaa, sawa. Haukufahamiana na hiyo familia eti?"
"Ndiyo, siwafahamu. Zaidi... Ankia alishawahi tu kuniambia kuhusu huyo Miryam, walisaidianaga zamani sana. Wanaheshimiana yaani, na huyo dada anaonekana mstaarabu."
"Ndiyo, wote ni watu wazuri. Vipi wewe... nyumbani, hali ikoje?"
"Panatulia kadiri siku zinavyoenda. Jumamosi wanaanza mchakato wa kujenga kaburi la Joy kule Nachingwea," akaniambia.
"Ahaa, kumbe bado walikuwa hawajajenga?"
"Eeh. Nitakwenda huko ikifika Ijumaa. Kama ukiwa na nafasi, nilikuwa nataka nikwambie... nikuombe unisindikize," akasema hivyo.
Nikaangalia pembeni kwa ufikirio.
"Au... kama utakuwa na... mambo mengi... haina shida, nitapata tu...."
Nikakishika kiganja chake na kuanza kukisugua ili kumtuliza kiasi, naye akaniangalia kwa utulivu. "Usijali. Tutaenda pamoja. Utafika kwa... itakuwa nyumbani kabisa, si ndiyo?"
Akatikisa kichwa kukubali, naye akasema, "Asante. Nimemwalika na Ankia pia, kwa hiyo... asante kwa kukubali kuja, ingawa nimekushtukiza."
"Haina shida kabisa rafiki yangu. Tuko pamoja," nikamhakikishia hilo.
Akabaki kuniangalia tu kwa umakini, nami nikajikuta naendelea tu kumtazama. Huyu mwanamke hakuwa wa namna ya kupindisha maana, yaani niliona wazi kabisa kwamba alikuwa jasiri na aliyejua aliyoyataka, kwa sababu hakukwepesha macho yake wala kuonyesha shau yoyote ile kunielekea.
Alikuwa mwanamke ambaye unaweza kusema ni mkomavu, asiyeona uajabu wa hali zozote zile ambazo kikawaida zinakuwa za kawaida, kama hivyo nilivyomshika kiganja, na hilo nililiheshimu. Angekuwa mwingine hapo angeanza kujichekesha kimashauzi kisa tumebaki wawili, lakini huyu ndiyo moja ya wale wanaothibitisha kwamba siyo wote wako namna hiyo. Wengine wanajielewa.
Nikakiachia kiganja chake na kumuuliza, "Vipi... ishu ya Joy... mapolisi wameshawaambia lolote?"
Akatikisa kichwa kukanusha, naye akasema, "Hakuna lolote la maana kabisa. Japo... juzi hapo yule mpelelezi alinipigia akasema... hajasahau kuhusu mauaji ya mdogo wangu kwa hiyo niendelee... mimi na familia yetu yaani, tuendelee kungoja tu, na muda siyo mrefu sana watawakamata waliofanya yale mambo. Sijui hata kama naweza kuwaamini hawa mapolisi maana... ni chenga tu ndiyo zitakazofata mpaka litasahaulika."
"Hapana, usiseme hivyo. Kuwa na imani tu. Hata mimi najua Joy atapata haki ya kifo chake," nikamtia moyo.
"Ngoja tuone. Hao watu wakikamatwa kweli... labda ndiyo tutapumua maana mpaka sasa hivi mama yetu hatoki ndani kwa kuhofia watu wa nje... amekuwa kama mgonjwa yaani," Adelina akasema hivyo na kupiga ulimi mdomoni kwa njia ya masikitiko.
Ilinifanya nimwonee huruma, lakini bado nikawa najizuia nisimwambie kuhusiana na mambo niliyokuwa nikifanya pamoja na huyo huyo mpelelezi aliyemsemea ili kuwakamata wasababishi wa kifo cha mdogo wake.
Ankia akawa amerejea, nami nikabadili mada upesi ili hali ya uchangamfu irudi. Alikuwa amepata chupa kubwa ya wine ya Dompo, naye akafata glass za vioo ili aje kutuwekea tushushe taratibu. Alikuwa ameshapika kabisa lakini tungekunywa kwanza ili kuchangamsha miili kisha ndiyo msosi tungepiga baadaye.
Joto nililokuwa nahisi lingehitaji kuondolewa kwa kwenda kujimwagia, lakini nikaamua kuendelea tu kukaa na marafiki hawa na maji ningekuja kupiga baadaye.
★★
Kwa hiyo tukanywa taratibu tu na kuendelea na maongezi mpaka nikasahau kupiga simu kwa Bi Zawadi ili kuwasalimia. Ankia akatufanyia wepesi wa kupakua vyakula ili tule pamoja na kinywaji taratibu, nami nikahisi kushiba na kuridhika kwa ushirika wa kirafiki pamoja na marafiki hawa. Hata nikasahau kabisa kuhusu vitisho vya Chalii Gonga masaa machache yaliyopita vilivyokuwa vimeniharibia amani kiasi.
Imeingia mida ya saa tano ndiyo Adelina akasema anahisi usingizi na alihitaji kulala mapema ili kesho awahi kuamka kwa ajili ya kwenda Mbezi; alihitajika kuwahi kazini. Wakati huu nilikuwa nimeshafahamishwa kwamba mwanamke huyu alifanya kazi ya kutengeneza mabatiki kwenye duka moja kubwa huko Mbezi, na alikuwa amepanga vyumba maeneo ya Kinyerezi kusiko mbali sana na alipofanyia kazi.
Kwa hiyo Ankia akawa ameenda pamoja naye chumbani kwake ili wakapangane sijui, na ndiyo nikawa nimetumia nafasi hiyo kumpigia Bi Zawadi. Akapokea, nasi tukasalimiana vizuri sana, na baada ya kumuuliza mambo yalikwendaje kwenye matembezi yao leo, akaniambia kwamba yalikuwa mazuri sana tofauti na matarajio yake.
Akasema kwamba huyo Joshua aliwaonyesha mabadiliko makubwa aliyokuwa ameanza kuyaweka maishani mwake, kwamba alimtendea mke wake vizuri sana kama mwanamke anavyostahili kutendewa, na aliwatendea kwa fadhili na heshima; wote kwa ujumla kama familia. Akaniambia kesho niende hapo kwao mapema maana Mariam alikuwa amenimiss sana leo, nami nikakubali na kumtakia heri ya usiku mwema.
Nikashusha simu na kutikisa kichwa kidogo kwa kusikitika. Jinsi sauti ya Bi Zawadi ilivyoonyesha imani mpya kuelekea suala la huyo Joshua, ilinifanya nimwonee huruma sana, familia hiyo yote kwa ujumla, kwa sababu mioyo yao mizuri ilikuwa ikichezewa vibaya na huyo mwanaume kwa mara nyingine tena bila wao kujua. Lazima tu kuna vitu ambavyo Joshua alikuwa anafanya kuwaaminisha kwamba amebadilika kiasi cha kumfanya hadi Bi Zawadi asifie nyendo mpya za jamaa.
Aisee, ningehitaji kuongea na Miryam. Alikuwa anapenda kutafuta amani sawa, lakini hapo angekuja kujikuta anaangukia kubaya zaidi ya kule alikodondokea kipindi cha nyuma kutokana na kusukumwa na huyo huyo kaka yake. Najua nisingeweza kuwa sehemu zote kwa wakati wote kuhakikisha ulinzi kwa Mariam, ndiyo sababu ningepaswa kumpa mwanga dada yake kwa yale niliyofahamu kabla mambo hayajaharibika.
Nikiwa bado natafakari vitu vya kufanya, Adelina akawa ametoka chumbani kwa Ankia na kuja upande wangu. Nilipomtazama, nikajikuta nimezubaa kiasi baada ya kumwona akiwa amejifunga khanga moja kutokea kifuani, iliyofikia mwanzo wa magoti yake hasa kutokana na yeye kuwa mrefu.
Alikuwa anaenda kuoga bila shaka, naye akanipita huku akisema macho yangu yamelegezwa kweli kwa wine niliyokuwa nimekunywa, nami nikatabasamu tu na kumsindikiza kwa jicho la chini mpaka alipokwenda nje. Hilo limlima huko nyuma! Siyo poa.
Nikageukia upande aliotokea pale chumbani na kukuta Ankia akiwa amesimama huku akinitazama, tabasamu la kuhukumu likionekana midomoni kwake, nami nikamuuliza 'nini?' lakini akacheka kwa mguno na kupiga kofi viganjani kuthibitisha kwamba kweli alikuwa ananihukumu kutokana na jinsi nilivyomwangalia Adelina akiwa ndani ya khanga.
Nikamnyooshea kidole na kumwambia 'wewe!' kisha nikanyanyuka na kuelekea chumbani kwangu; nikimwacha hapo anacheka baada ya yeye kunisukuma kidogo mgongoni. Najua na wine pia ilikuwa imemchangamsha kwa hiyo hata sikumkazia fikira. Nilikuwa tu nahisi uchovu wa mwili kiasi kutokana na mizunguko ya leo, nami nikashusha neti na kutulia tu kusikilizia Adelina atoke bafuni ili nami nikajimwagie.
Baada ya kusikia amerudi ndani, nikaenda zangu bafuni pia na kujimwagia maji, kisha nikaingia kujipumzisha. Ningeweza kuwasikia wanawake wakizungumza mambo yao yenye kufurahisha huko chumbani mpaka kufikia mida ya saa saba, ndiyo wakatulia baada ya hapo. Kwa sababu fulani, usingizi ulikuwa unanipinga mpaka kufikia saa nane kabisa, ndiyo hatimaye nikaingia ndotoni.
★★★
Nimekuja kushtuka kutoka usingizini pakiwa pameshakucha zamani sana, nami nikavuta simu yangu kuangalia muda. Ilikuwa ni saa nne asubuhi sasa, na kiukweli nilikuwa nimelala. Ile kulala ya moja kwa moja bila kushtuka hata mara moja usiku yaani. Nikakuta jumbe kadhaa kutoka kwa marafiki zangu, na namba ngeni.
Hiyo namba ngeni ilikuwa ni namba mpya ya Tesha. Alikuwa ameniambia kwamba alilala pale pale kwa Dina jana na sasa ndiyo alikuwa njiani kurejea huku, na ni mwanadada huyo ndiye aliyekuwa amempatia simu yake ya ziada ili jamaa atumie mpaka akinunua nyingine. Soraya pia alikuwa ametuma ujumbe wa salamu, Latifah aliuliza ningerudisha vile vifaa vya hospitali lini, na Adelina aliacha jumbe ya kuniaga, kwamba tayari aliondoka na alitarajia tungeonana Ijumaa.
Nikawajibu wote chap chap; Tesha nikimwambia sawa, Soraya nikimwambia ningemtafuta baadaye, Latifah nikimwamdikia tu "Jumamosi," na Adelina nikamtakia safari njema na kuomba radhi kuchelewa kuamka maana hata sikumsindikiza mpaka hapo Mzinga, kisha ndiyo nikatoka kitandani ili niianze siku kwa kawaida yangu ya kufanya usafi wa mwili.
Kama kawaida ya mwenye nyumba wangu, alikuwa ameshaamka na kufanya usafi wa ndani, na chai ilikuwa tayari. Nilipomaliza kuoga na kuvaa, akaniwekea chai na maandazi ya nguvu, nami nikanywa na kushiba. Akawa ameniambia kwamba leo alitamani sana kutengeneza pilau na nyama ya kuku yeye mwenyewe hapo nyumbani, nami nikampatia hela ya kumchangia kununua vyote alivyohitaji. Akafurahi sana!
Baada ya hayo ndiyo nikamuaga sasa ili niende kumwona Mariam. Nilikuwa na mwonekano wangu safi kabisa na niliwapita wakina Fatuma na mashosti zake hapo nje wakiwa wamekaa kwa kutulia tu, nami nikaingia moja kwa moja getini kwao Tesha na kuelekea mlango wa kuingilia ndani ya nyumba. Niliweza kuona viatu vya kike vilivyokuwa vigeni machoni kwangu, na kwa sababu gari la Miryam halikuwepo hapo, hiyo ilimaanisha kwamba bila shaka kulikuwa na mgeni.
Nikafungua mlango huku nikisema "Hodi, hodii," na sauti ya Bi Zawadi ikajibu, "Karibu, karibuu."
Nikaingia huku nikitabasamu kiasi, lakini nilipomwona mgeni aliyekuwa amekaa sofani pamoja na Mariam, tabasamu langu likatoweka.
Ilikuwa ni mke wake Joshua, mwanamke mwenye kiuno na miguu mirefu pia. Alikuwa amevaa kijora chenye rangi kama vile moto unawaka nguoni, na alizificha nywele zake kwa kilemba cha hiyo nguo. Alikuwa akinitazama kwa macho yenye utulivu tu, naye binti Mariam, akiwa ndani ya dera pia, akatoka sofani na kunifuata huku akitabasamu kwa hisia sana.
"Mamu huyoo... hi-five," nikasema hivyo nikiwa nimenyanyua kiganja changu juu.
Mariam akagongesha kiganja chake hapo na kusema, "Shikamoo?"
"Marahabaa. Umeisema kwa wepesi hiyo, safi sana," nikamwambia hivyo.
"Asante. Karibu," Mariam akaniambia hivyo.
"Wacha!" nikamwambia hivyo, naye akacheka kidogo.
Ingawa wakati huu Mariam alikuwa akizungumza, hiyo haikumaanisha kwamba alikuwa amepona kabisa, kwa sababu tabia za kitoto kwenye utu wake bado zilikuwepo, na ndiyo mazoezi ya juu zaidi yalitakiwa kufata ili ziondolewe. Lakini hawa wakina Joshua walikuwa wameanza kuleta tena michezo yao ya kijinga ambayo ingepaswa kukoma haraka kabla hawajamvurugia mtoto maendeleo yake.
"Shikamoo cheupe wangu?" nikamwamkia Bi Zawadi.
"Marahaba baba, karibu ukae," akaniambia hivyo.
Mariam alikuwa ameshanizoea vya kutosha kunishika mkononi na kunivuta ili nikakae, lakini sikutaka kukaa pale alipozoea mimi kupenda kukaa kwa sababu huyo mke wake Joshua alikuwa amekaa hapo wakati huu. Lakini sikuwa na jinsi kwa kuwa binti mwenyewe alinivuta kwa raha zote, nami nikasogea mpaka hapo kwa kumfuata.
Huyo mwanamke akasogea pembeni kiasi ili nafasi iwe ya kutosha, na Mariam akakaa mwishoni mwa sofa ili mimi nikae katikati. Yaani mimi ningekaa katikati ya Mariam na mke wake Joshua, na ile nimeketi tu, katika kujisawazisha vizuri, nikawa nimemkanyaga kiasi mwanamke huyo mguuni kwake. Ha, makosa! Sijui tu akawa amefikiria nini.
"Bi Jamila hajaamka bado?" nikamuuliza hivyo Bi Zawadi.
"Mh? Mpaka sa'hivi? Hamna ametoka na Mimi. Ameamka hajisikii vizuri kwa hiyo Miryam kampeleka apigwe check-up kabisa," akanifahamisha hilo.
"Ahaa, sawa. Kwa hiyo watarudi pamoja?" nikauliza tena.
"Hamna, Shadya ndiyo anampitia wanakuja naye. Miryam yeye anapitilizia kazini," Bi Zawadi akasema hivyo.
"Sawa. Bora kupima kabisa, wamefanya la maana," nikamwambia.
Bi Zawadi akasema, "Eeh ni kweli. JC baba... huyu ni mke wa Joshua, anaitwa Khadija."
Nikamwangalia huyo mwanamke pembeni yangu na kusema, "Sawa sawa. Nimefurahi kukujua."
Bila kuniangalia, huyu Khadija akasema, "Asante," lakini nikahisi namna ambavyo alinikanyaga mguuni kwa njia ya kukonyeza. Dah!
Nikajikausha na kumwangalia Mariam.
"Huyu ndiyo daktari wetu mahiri. Yaani unavyomwona Mamu sasa hivi ujue ni yeye ndiye kasaidia," Bi Zawadi akamwambia hivyo mkwe wake.
"Aaa... hongera sana kaka. Umemsaidia sana Mamu mpaka amepona," Khadija akaniambia hivyo.
"Bado hajapona kabisa. Tunatakiwa kuendelea na mazoezi yetu, au siyo Mamu?" nikasema hivyo.
"Ndiyo kaka. Leo tutacheza mchezo gani?" Mariam akaniuliza.
Huku nikimwona Bi Zawadi anatabasamu, nikamwambia binti, "Leo tutacheza mchezo wa kuchora. Inabidi ukamwibie dada Mimi kalamu na karatasi haraka ili tuje tumchore halafu uje kumwonyesha, sawa?"
Mariam akatikisa kichwa na kwenda upande wa chumba upesi, naye Bi Zawadi akacheka kidogo.
"Za jana? Huyu alitulia wakati mpo huko?" nikamuuliza hivyo Bi Zawadi.
"Ndiyo. Aa... ni mambo mengi sana... mazuri ya jana. Ahah... ngoja nikakuwekee chai kidogo baba," Bi Zawadi akasema hivyo na kunyanyuka.
Nilielewa upesi kwamba mwanamke huyo hakutaka tuzungumze mengi yaliyotokea jana nyumbani kwa Joshua huku mke wake akiwa hapa, yawe mazuri au mabaya, ili asitoe picha ya kwamba huwa wanawazungumzia wawili hao kwangu pia. Kwa hiyo kisingizio cha kuniletea chai kilifaa ili akate hiyo mada, lakini kuniacha hapo na huyo mwanamke likawa suala la utata.
Nafikiri alikuwa mwanamke jasiri kiasi, yaani hakuwa na aibu juu ya mambo aliyotaka, kwa sababu baada tu ya Bi Zawadi kuelekea jikoni papo hapo akaanza kutelezesha kidole chake cha mguuni kwenye mguu wangu bila kuniangalia, akijifanya ametazama mbele tu kwa utulivu. Haloo! Yaani kosa tu kidogo kumkanyaga likawa limeiingizia akili yake jambo ambalo hata halikuwa karibu na himaya ya fikira zangu.
Nikamwangalia usoni kwa umakini, naye akaibana midomo yake na kunitazama kwa macho yenye uvutio eti. Kwa hiyo sekunde mbili tu kukaa naye akawa amenitaka? Sikupendezwa na jambo hili, lakini uharaka wake ukawa umenipa wazo.
Ikiwa mwanamke huyu alikuwa akishirikiana na mume wake katika mipango yake mibaya ama tu kuijua, ningehitaji kupata jambo fulani hakika kutoka kwake ambalo lingesaidia kuthibitisha na kuitibua mipango hiyo. Mara nyingi ushahidi huwa ni muhimu sana kwenye visa vya namna hii, na sikujua kivipi tu lakini nikawaza kwamba kwa njia moja ama nyingine kuwa na ukaribu wa kisiri pamoja na mwanamke huyu kungesaidia kufanikisha wazo langu, kwa hiyo nikaamua kwenda na mchezo aliofikiri nilikuwa nimeanzisha. Si unajua kwa wanawake sinaga mbambamba?
Nikaangalia upande wa jikoni kupitia pale dining na kuona kwamba Bi Zawadi alikuwa anamimina chai kikombeni, nami nikarudia kumwangalia Khadija. Sijui alikuwa mwislamu aliyebadili dini? Maana Joshua ni mkristo bila shaka, lakini hayo nikayaweka pembeni kwanza.
Mwanamke huyu akawa ananiangalia kama vile anasubiria nifanye jambo fulani au kumpa ishara yoyote ile, kwa sababu sasa alikuwa ameacha kunisugua mguuni, nami nikaweka kiganja changu kwenye titi lake la kushoto lililofichwa kwa nguo yake na kulikamata. Hakuwa amevaa sidiria maana lilihisika vyema kiganjani kwangu. Na hakunizuia, bali akaweka kiganja chake kwenye paja langu na kuanza kulipa massage huku akielekea kati taratibu. Huyu alikuwa na ile akili sharp ya kimya kimya, asipindishe maana wala kujishaua, na hiyo ilikuwa nzuri.
Nikaifinya chukuchuku yake na kuivuta kwa nguvu, naye akaniangalia huku amekunja sura yake utadhani alikuwa anataka kuanza kulia, na kiganja chake kikaishika sehemu yangu ya siri iliyokuwa imeanza kuvimba ndani ya jeans. Huyu hakuwa mwoga yaani, na mimi nilikuwa makini kuhisi wakati ambao Bi Zawadi angeanza kurudi, ila likafuata jambo ambalo sikuwa nimetarajia.
Kutokea upande wa korido lililoelekea vyumbani, akatokea Joshua akiwa anakuja upande wetu kwa mwendo wa taratibu tu! Nikashtuka machoni kwa sababu ya ughafla wa jambo hilo ambalo sikutazamia kabisa. Alikuwa ametokea wapi?
★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★
Comments