Reader Settings

SEHEMU YA 04

Mwaka 2020 ni mwaka ambao   ni  wa kukumbukwa dunia nzima, ni mwaka ambao uliandika historia ya aina yake  tokea  binadamu kuanza kuishi maisha  katika dunia  akitegemea nishati ya  joto na mwanga  kutoka  kwenye jua.

Kwanini mwaka  2022 ni mwaka wa kihistoria?

Ni kwasababu ya tukio  la ajabu sana ambalo  liliwahi kutokea , tukio ambalo mpaka leo hii halikutolewa ufumbuzi   wa kueleweka kwa wakazi wote wa dunia hii.

Kwa maneno marahisi ni kwamba ni tukio ambalo  tumefichwa  ukweli wake na watu wanaojiita serikali.

Mwaka huu ndio mwaka ambao kwa mara ya kwanza ndani ya bara la Afrika kupata majira ya theluji(snow).

Linaweza kuwa jambo la kushangaza lakini   ni kwa maeneo machache sana  pengine hakuna kabisa ndani ya bara la Afrika kihistoria  joto  kushuka  mpaka kufikia hatua ya unyevu nyevu uliopo angani kuganda na kupelekea Theluji.

Kushuka kwa baridi  kwa kiwango  cha kushangaza  haikuwa kwa Afrika tu , tukio hilo linakumbukwa kutokana na kwamba  maeneo ambayo yalikuwa yakipata  Theluji katika vipindi vya majira,  joto lake lilishuka  sana kiasi kwamba kuyafanya mazingira hayo kutoweza kusapoti maisha ya binadamu, mimea na wanyama kiasi cha kukimbilia   katika bara la Afrika ili kuweza kupata hifadhi ya muda kwa matarajio ya kipindi cha baridi kitakapo pita wangerejea katika makazi  yao.

Hili ndio tukio   la kwanza kuikumba dunia kiasi cha kufanya Afrika  kuonekana mahali salama  kwa makazi ya muda ndani ya dunia kwa ajili ya kujikinga na baridi iliokumba mabara mengi..

Ijapokuwa sio watu wote waliokimbia makazi yao na kuja kuishi   katika  bara la Afrika lakini  idadi kubwa ya watu waliokuja kuomba  makazi ya muda katika  bara la Afrika ilikuwa kubwa mno.

Wanasayansi mbalimbali walishindwa kutolea  maelezo mabadiliko ya ghafla ya hali ya hewa  hio  na kuishia kusema ni tukio la kustaajabisha.

Wapo waumini ambao waliweza kuamini  ni siku za mwisho za dunia zilizotabiliwa zimewadia.

Ajabu ni  kwamba tukio hilo halikudumu muda mrefu sana mpaka hali ya hewa kurudi katika   hali yake  ya kawaida na maisha kuendelea,

Baada ya tukio hilo ambalo lilikosa  maelezo  yakinifu, nadharia za kizushi za aina nyingi ziliibuka na kusema  pengine ni onyo kutoka kwa  Mungu kwa binadamu kwa  matendo yao  wanayoyafanya  kutokana na   anasa mbalimbali zilizokuwa zikifanyika , anasa ambazo zilikuwa zikienda kinyume na  mapenzi ya Mungu.

Ukweli ni kwamba kila mtu aliibua kauli yake na wale watu wenye wafuasi wengi kwenye mitandao waliweza  kuvumisha   kila uzushi uliosemwa na watu wengi kuamini,.(Wakuu nyie ni mashahidi  wa tukio hili)

Lakini watu wanasema sikio la kufa halisikii dawa , baada  ya  tukio hilo la ajabu kuikumba  kupita  kila mtu alisahau  na maisha kuendelea na wale ambao  ni watu wa  dini walizidi kujikita zaidi  na sala  wengine wakisema wanaisubiria siku ya kiama na wengine walisema wanasubiria siku ya unyakuzi.

Mara baada ya tukio  hilo kupita kulitokea Uzushi maarufu wa kinadharia(Consipiracy theory) iliohusisha uwepo wa  watu  vivuli(Night Shadows) ambao hutembea  usiku.

Zimekuwepo shuhuda  mbalimbali  kuhusu matukio ya watu kadha wa kadha ambao wameweza kukutana na hawa watu wanaosemekama kuwa ni vivuli  na kuwahusisha  na viumbe kutoka sayari nyingine(Aliens).

Wakuu  mnachokiona chini  ni baadhi ya picha za ushahidi ambazo zimepigwa kuhusisha   hawa watu wanaojiita Night Shadows.

Je hawa watu   ni kweli ni Alien kama watu wanavyosema, je  tukio la  mwaka 2020 December  lilikuwa na uhusiano  na   hawa watu vivuli , je  ni kweli  ujenzi wa kisiwa  cha Binamu  kuna uhusiano  na hawa watu.

Kabla ya kuendelea  wanabodi  nataka kwanza mjiulize kwanini  kisiwa cha  Binamu kimekuwa maarufu?, kwanini kisiwa hichi  ni ghali sana kutembelea  lakini  bado watu wanaenda.?

Itaendelea hivi punde

********

à                 

Down here  in the rain fields

Outside  of the Glow

My world is getting Smaller

Oh , oh , oh no

………………..

à                 

Mwito wa simu wa wimbo wa Low Tides kutoka kwa msanii Tom Rhodes ndio uliomuamsha Hamza ambaye hakujua hata  amelala saa ngapi na alichokumbuka tu ni kwamba  alikuwa akisoma mada ya kizushi kwenye mtandao wa JamiiForums mpaka kupitiwa na usingizi , baada ya kufumbua macho  kivivu akiwa bado na usingizi alianza kuitafuta simu yake kwa kupapasa godoro lake lakini hakuiona na iliita mpaka ikakatika na hapo hapo aliendelea kujilaza kivivu, asiangalie hata muda huo ni saa ngapi.

Wakati  akibadilisha staili ya kulala  palepale simu ilianza kuita tena  na awamu hii ilimuamsha kwa kusogea  kidogo mpaka kwenye  kingo ya Godoro na kuichukua simu hio ikiwa imedondoka chini Sakafuni.

Hakushangaa kwani  hata hivyo   haikuwa mara yake ya kwanza  kupotelea usingizi usiku akiwa anaitumia  na  kudondokea chini.

“Hello!!”

Hamza  hakujisumbua kabisa hata kuangalia aliekuwa akipiga ni nani na yote hio ni kutokana na macho yake kuogopa  mwanga wa simu kwani ndio kwanza alikuwa akiamka.

“”Naongea  na Ndugu  Hamza Mzee?”

Sauti  ya kike  nzuri iliweza kusikika kwenye ngoma za masikio yake na kumfanya  Hamza kushituka  na kutoa simu sikioni na kuangalia namba ambayo ameipokea bila ya kuangalia jina la mpigaji lakini alishangaa mara baada ya kugundua  ni  namba mpya.

“Hello.. Mbona kimya!!”Sauti upande wa pili iliweza kusikika  mara ya pili mara baada ya kimya cha  Hamza kuwa kirefu.

“Ndio mimi ni Hamza , naongea na nani tafadhari?”

“Unaongea na mwanachama wa JamiiForuma mwenye  ID  ya Ngwena”Sauti  ilisikika na kumfanya  Hamza akili yake kufanya kazi kwa haraka na mara baada ya kukumbuka alijikuta akijikalisha kwenye   godoro lake.

“Oh! .. wewe ndio   ulieotoa tangazo la Ajira  la  kutafuta  boyfriend feki  eh?”Aliongea Hamza akiwa  sio mwenye kuamini.

“Upo sahihi , je utapenda tuchati kwa meseji  au tuongee  kwa simu?”Sauti  ile nyororo ilianza kumsisimua  Hamza.

Katika maisha yake hio ilikuwa ndio mara ya kwanza kuamshwa na simu asubuhi  na  sauti ya mwanamke mwenye sauti nyororo  namna hio , ilikuwa ni kama  anaota  na muda wowote angeshituka  kutoka usingizini.

Ukweli ni kwamba  licha ya jana kujaribu kuingia katika PM ya  mwanachama huyo wa mtandao wa Jamii Forum hakuwa na uhakika kama anaweza kutafutwa yote hayo ni kutokana na kwamba hakuchukulia swala lenyewe kuwa siriasi kutokana na maoni ya watu , lakini pia  asili ya Tangazo lenyewe kwani halikukaa  sawa.

Maisha ya watanzania wengi yalikuwa ni ya kimasikini sana na uchumi ulikuwa  ni mgumu  mno   na hata waajiri   hawakuajili tena zaidi ya kupunguza wafanyakazi.

Hali hii  haikuwa ya kawaida kwa  mtu kuweka tangazo mtandaoni la kutafuta mchumba   wa maigizo  halafu kumlipa , ilikuwa ni swala la kichekesho  na ambalo haliwezekani.

“Kwahio  unasema kwamba tangazo lile lilikuwa siriasi na umeridhishwa na mimi ndio  maana ukanipigia?”Aliuliza Hamza akiwa  bado haamini huku akiangalia saa ya simu yake na kulaani  kimoyo moyo kwani alikuwa  amechelewa kuamka sana, ilikuwa ikikaribia saa moja na nusu na muda huo pengine angetakiwa kuwa kwenye gari kuelekea chuoni.

“Ndio maana nimekupigia Hamza , lakini  ili kujua kama  unafaa lazima nikuulize maswali kadhaa ndio  nikupe muongozo wa kinachofuata”

“Unaweza kuendelea tafadhari?”Aliongea.

“Una ishi mkoa gani Hamza?”

“Naishi  hapahapa Dar es salaam  kama nilivyoelezea kwenye ujumbe wangu”Alijibu Hamza huku akitoa tabasamu , alijiambia  lazima mwanamke huyo  atakuwa   ni mrembo  kutokana na sauti  yake.

“Vizuri , je  una miaka mingapi?”

“Nina  miaka ishirini na saba?”

“Okey! Hamza asante kwa kujibu maswali   yote ,  hatua ya pili inayofuatia kama upo siriasi  kufanya kazi ya  kuwa boyfriend feki  unapaswa kufika katika  Dosam V hotel muda ni  kesho  saa nne asubuhi kwa ajili ya Usaili na kama utafanikiwa  kupita basi  utasaini mkataba wa ajira”

“Usaili!!, ?Unamaanisha nini kuhusu Usaili  , kuna haja juu  ya hilo?””

“Hamza  nadhani ni utaratibu wa kawaida kufanyiwa Usaili na kama utafaa kivigezo  basi  utaweza kupewa ajira  rasmi kama ilivyotangazwa”

“Aaa..!”

“Kumbuka Hamza ni siku ya kesho saa nne kamili asubuhi heshimu muda”Baada ya mwanamke huyo kuongea maneno hayo palepale simu ilikatwa na kumfanya Hamza kushikwa  na bumbuwazi akisahau kwamba anachelewa kwenda chuoni.

******

Maisha ya ajabu ni nini na tunawezaje kuyatumia  kufanikiwa?

Maisha  ya ajabu ni neno ambalo lina urejeo wa mambo mengi , lakini kwa ujumla  linamaanisha mambo ya kuvutia  na kushangaza ambayo tunakutana nayo maishani,  mambo ya ajabu  kama hayo ni kama vile  kuangalia maporomoko ya maji  ya  umbali mrefu ,  uzuri wa mtoto  anapotabasamu na mengine  mengi.

Maisha  ya   ajabu  yanaweza kutusaidia  kufanikiwa kwa njia nyingi ikiwemo  , kutupatia  hali ya mshangao na udadisi , kutusaidia  kuthamini  mambo madogo madogo , kutuhamasisha kuwa wabunifu , kutuunganisha na wengine  pamoja na kutupa matumaini mapya.

Zipo  njia kadha  wa kadha ambazo zinaweza kutusaidia   kutumia maisha yetu ambayo yamejazwa na uajabu  ili kufanikiwa   ikiwemo: kutengeneza  orodha ya mambo  ya ajabu  ambayo ni ya kukushangaza na kukuvutia , jaribu kutafuta uzoefu  mpya  nje  na eneo  la faraja(Comfort Zone),Kuwa na shukrani  na  shirikisha   uzoefu  wako kwa wengine.

“Haya ndio maneno yangu kwenu ambayo  ni kama Bonus Point kwenu , niwatakie siku njema , Mono  no aware.

“Paaa.. Paaah!!!

Ilikuwa kama kawaida  Hamza aliguswa sana na maneno ya  Profesa  Singano  ukiachana na  namna maneno hayo yalivyomwingia na kuyaelewa lakini kwa wakati mmoja  ni kama yaligusia kile ambacho amekutana nacho asubuhi ya leo.

Hamza tokea anatoka  mahali anapoishi kuja chuoni alikuwa akiikumbka mara mbilimbili  kauli ya kuhitajika kwenda kwenye usaili  kwa ajili ya kupewa kazi  ya kuwa Boyfriend feki.

“Hakika maisha  na maajabu yake , lakini  leo  Profesa  maneno yake yamenifanya nichukue maamuzi , lazima kesho niende  kwenye huo usaili nikajionee mwenyewe”Aliwaza Hamza.

“Oya Mzee unawaza nini? , huna mpango wa kuondoka  nini?”Sauti ilisikika nyuma ya Hamza na kumfanya ageuke na   kukutana uso kwa uso na Alex muuza vyungu.

“Hamna  ndio  najiandaa kutoka hivyo”

“Haha,, Hamza una mawazo mengi sana , kila   siku ambayo Profesa akimaliza kipindi chake wewe unaishia kushangaa”

“Mara nyingi namchukulia  Profesa kama mchungaji pale anapokuhubiria juu ya jambo la Dhambi ambalo unalifanya,  kwa  urahisi ni kama Profesa anayagusa sana maisha yangu kwa ujumla”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Alex kuangua kicheko.

“Unajua nini   braza ,Profesa Singano naona muda mwingi  anapoteza muda wake  tu  lakini hakuna cha maana anachoongea  na hilo sio kwangu tu   nakuhakikishia  ni wachache sana ambao  wanaguswa na maneno yake , wengine wote wanapenda  kumuona anavyoongea ili kucheka basi lakini sio ujumbe”Aliongea Alex  na kumfanya  Hamza  asiweze kuongeza neno.

“Sio kawida yako kunitafuta   wakati wa kumaliza kipindi kama huu  kwa ninavyokujua sasa hivi ungekuwa na kundi la warembo kwenye gari yako mnaondoka”Aliongea Hamza.

“Upo vizuri mtu wangu , nimekufuata   kwasababu   nina mishe  nataka  msaada wako”

“Mishe gani?”

“Ni kazi nyepesi  sana yenye  malipo mazuri”

“Okey , nipe mchongo”

“Iko hivi  leo  nina oda za kupeleka vyungu sehemu mbalimbali   na  wafanyakazi  niliokuwa nao ni wachache na hawawezi kumudu oda zote..”

“Nipo  tayari, nishakuelewa unachomaanisha , wewe zungumzia   kiasi cha pesa ambacho  utanilipa “

“Elfu ishirini unaonaje   kwa trip  moja”Aliongea Alex na  Hamza macho yalichanua , aliona   ni dili zuri.

“Kama upo siriasi mimi nipo tayari kwa ajili ya kazi”

“Ndio maana nakukubali  Mzee ,  huna   tabia za kulemba lemba kwa kuchagua kazi ,  sasa   sikia  muda wa jioni jioni saa kumi  ndio  utaanza  , kuna  mfanyakazi wangu nitampa namba yako atakupigia na utafika maeneo ya uzalishaji  na kisha utachukua mzigo na atakupa na  Anuani wapi unapaswa kupeleka”Aliongea na Hamza hakuona tatizo , alikuwa na uhitaji wa pesa na  kama  kuna mtu alikuwa tayari   kumlipa kiasi  kidogo cha pesa  kwa malipo ya kawaida aliona  hana haja  ya kukataa dili hilo.

Baada ya kuachana na  Alex  Hamza yeye hakuona haja ya kwenda nyumbani mapema hivyo , chuoni  kulikuwa na  Wife ya  bure hivyo kutokana na  mara nyingi kutokuwa na bando   la kuosha aliona atumie muda huo  kukaa chuoni hapo kupakua  muvi na kwenda kuangalia getoni kwake.

Previoua Next