SEHEMU YA 05.
Muda wa jioni Hamza akiwa chuoni aliweza kupokea simu kutoka kwa mtu aliejitambulisha ni mfanyakazi wa Alex na Hamza mara baada ya kusikia utambulisho wake aliweza kumjua mara moja na palepale alipewa maagizo ambayo Hamza alionekana kuyaelewa na kisha simu ilikatwa.
Dakika chache tu alikuwa tayari ashapata daladala ambayo ilimpeleka moja kwa moja mpaka Mwenge mahali ambapo ndio alielekezwa kushuka.
Kutokana na kuwa mzoefu aliweza kutoka kituoni na kuchukua upande wa kulia kwake na kueleka moja kwa moja mpaka eneo husika.
Hamza alijikuta akishangaa mara baada ya kugundua kazi ya Alex haikuwa kazi ndogo , kwani ilikuwa ni kama Kiwanda.
Jambo hilo lilimshangaza , watu walikuwa wakimchukulia Alex wa kawaida kutokana na kazi yake , lakini Hamza mara baada ya kupita getini na kuingia ndani aligundua ilikuwa ni zaidi ya alivyofikiria , kwani kulikuwepo wafanyakazi wengi.
“Wewe ndio Hamza?”Aliuliza jamaa mmoja mwenye nywele ndeefu mara baada ya kumuona Hamza ana shangaa shangaa”
“Ndio Bro”
“Umefanya la maana kuja haraka maana kidogo tu usingenikuta hapa , nina oda ya kupeleka , njoo nikuonyeshe Mzigo chapu”Aliongea yule bwana huku wakipita wamama ambao walikuwa bize kutengeneza vyungu.
Kulikuwa na utengenezaji wa aina tofauti tofauti , kulikuwa na vyungu ambavyo vilikuwa maalumu kwa ajili ya kuwekea maua na urembo mwingine , kitu kingine ambacho Hamza alikuja kugundua ni kwamba kilichokuwa kikitengenezwa hapo sio vyungu tu.
“Bosi mzigo huu hapa utaupeleka kwenye hii Anuani”Aliongea yule bwana huku akimpatia Hamza boksi ambalo juu lilikuwa na Sticker ambayo mzigo ulipaswa kupelekwa.
“Malipo yanakuwaje baada ya hapa?”Aliuliza.
“Bosi hajakuambia?”
“Hamna tumekubaliana ni 20k ila hajaniambia utaratibu wa kunilipa upoje?”
“Samahani mkuu, iko hivi huu mzigo bado haujalipiwa ukishafikisha utakaguliwa na baada ya hapo utalipiwa bei yake ni laki moja na nusu na gharama ya usafirishaji utapewa hapo hapo”
“Laki moja na nusu!!?”Hamza alijikuta jicho likitoka na kujiuliza ni chungu cha aina gani ambacho kinauzwa laki moja na nusu
Yule bwana alijua mshangao wa Hamza lakini hakutaka kumtolea maelezo yoyote na alionekana kuwa na haraka kwani aliingia kwenye gari na kisha akaondoka.
Hamza alitaka kuuliza kuhusu nauli vipi , lakini alikuwa amechelewa na kuishia kuangalia boksi ambalo lipo chini limefungwa kwa namna ya kipekee..
Alikuwa na shauku ya kujua ni chungu cha aina gani ambayo kinaweza kuwa na bei ghali namna hio lakini asingeweza kufungua.
Baada ya kusoma Anuani ya mzigo unapopaswa kueleka aligundua ni Madale .
Hamza alijaribu kuchunguza mazingira yaliokuwepo hapo ndani na aliweza kugundua hakuna ambaye alikuwa akimwangalia , kulikuwa na vijana wengi pamoja na wamama waliokuwa bize kuteneneza vyungu lakini hawakumwangalia usoni , ni kama hawakujali uwepo wake.
Hamza alinyanyanyua lile boksi na aliona halikuwa zito sana , alitamani kutafuta mfuko kulifunga lakini ilikuwa ngumu kuingia kwenye mfuko wa kawaida labda kwenye kiroba lingefiti lakini kiroba chenyewe hakuwa nacho hivyo aliamua kubeba hivyohivyo na kutoka ndani ya eneo hilo na kwenda kusimama kituoni.
Kama kawaida watu wa jiji la Dar hawakuwa na habari na mtu kila mtu alikuwa bize na mambo yake na Hamza na yeye hakujali watu na kuendelea kusubiri usafiri.
Hamza wakati akiwa kituoni hapo aliona ndio maana Alex alimtajia pesa kubwa kwa ajili ya kusafirisha kwa awamu moja kumbe gharama ya chungu kimoja ilikuwa kubwa hivyo.
Dakika kadhaa tu akiwa amesimama kituoni gari iliweza kusimama na Hamza licha ya kuona gari hio ilikuwa imejaa sana aliingia moja kwa moja na kisha akaweka mzigo wake sehemu husika na kisha akasimama na safari ikaanza.
Muda wa saa kumi foleni ilikuwa kubwa mno kutokana na watu wengi ndio kwanza wanatoka kazini , hivyo ilimchukua dakika nyingi sana kusimama mpaka kufika eneo husika.
Jiji la Dar lilikuwa limeboresheka sana katika maswala ya anuani za nyumba , ilikuwa ukiingia mtandao kwenye ramani unaweza kuona kila nyumba hivyo haikumpa Hamza shida kutafuta nyumba ya mzigo unapopaswa kufikishiwa.
Baada ya kushuka katika kituo husika alianza kutembea kwa kufuatisha Ramani na alitembea kwa dakika kama kumi tu alikuja kusimama kwenye nyumba kubwa iliokuwa na geti rangi nyeusi ambalo lilikuwa limenakshiwa na madini ya shaba.
Hamza aliangalia kulia na kushoto katika maeneo hayo na alionyesha kuridhika , ijapokuwa kulikuwa na nyumba za kawaida ndani ya hilo eneo lakini nyumba nyingi zilionekana ni zile za kifahari na zenye bustani za kuvutia nje.
“Ngoo… ngooo , ngooo!!!”
Hamza aligonga mara tatu na kisha akasubiria kwa dakika nzima lakini hakukuwa na dalili yoyote ya kufunguliwa, na alijikuta akigonga tena kwa dakika nyingine lakini bado mlango haujafunguliwa na aliamua awamu hio kugonga kwa nguvu lakini kabla hata mkono wake haujagusana na geti kijimlango kidogo cha nyumba hio kilifunguliwa.
“Una shida gani?”
Sauti iliokuwa ya kibabe iliweza kusikika na Hamza kwa ufahamu wake wa haraka haraka alijua mtu huyo atakuwa mlinzi kwani hata rafudhi yake haikuwa ile ilionyooka katika kiswahili chake.
“Nimeleta Mzigo”Aliongea Hamza.
“Mzigo gani?”
“Chungu”
“Hapo pembeni yako unaona nini?”
“Pembeni wapi tena?”
“Kushoto kwako?”
“Sioni kitu?”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba wakati alipofika hapo aliweza kuona kitufe cha kengele lakini hakutaka kukigusa na aliamua kugonga geti na mlinzi huyo alivyokuwa akimuuliza alikuwa akijua alichokuwa akimaanisha.
“Acha ushamba basi , angalia pembeni yako hapo kuna kengele na Camera , bonyeza hiyo na kisha utasema shida yako”Aliongea kwa hasira na kisha alifunga kijidilisha na kumuacha Hamza kutoa tabasamu la uchungu
Hamza alijiamulia kubonyeza ile kengele mara mbili na palepale aliweza kusikia sauti kutoa ndani”
“Delivery!!”Aliongea
“Ok”
Sauti ya kike iliweza kusikika kutoka ndani na mara baada ya kusubiria kwa dakika kama mbili hivi mlango wa geti ulifunguliwa.
“Kijana unaweza kuingia”Aliongea Mlinzi na sasa Hamza aliweza kumuona yule mlinzi.
Ijapokuwa sauti yake haikuwa imekaa vizuri lakini kimuonekano alikuwa vizuri sana kuliko hata yeye kwa upande wa mavazi.
Hamza mara baada ya kuingia ndani alijikuta akishangazwa na mandhari nzuri pamoja na ufahari wa jengo ambalo lilikuwa mbele yake.
Mlinzi alimuonyeshea ishara Hamza kutembea kueleka upande wa kushoto na Hamza mara baada ya kuangalia upande ambao anaelekezwa ni kando ya bwana la kuogelea sehemu ambayo imejengwa kwa ajili ya mapumziko.
Hamza kila hatua aliokuwa akipiga kueleka hilo eneo mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda mno mpaka mwenyewe kujishangaa , ijapokuwa kiumbe alichokuwa akikiangalia mbele yake kilikuwa kimempa mgongo lakini utashi wake ulimwambia huyo mwanamke alikuwa mzuri sio kawaida.
Hamza alijiambia pengine anachanganyikiwa sana kila anapowaona wanawake warembo kwasababu ni muda mrefu hajakutana na mwanamke kimwili.
Ilikuwa ni kama akili yake ilivyomwambia kwani mara baada ya kufika katika hilo eneo aliweza kukutana na mwanamke ambaye alikuwa nusu uchi , ilionekana kabisa alikuwa akiogelea kwenye hilo bwawa na muda huo alikuwa amepumzika kwani hata mwili wake haukuwa umekauka maji.
Hamza kwa akili yae palepale alijua huyo sio mtu ambaye alimwitikia baada ya kubonyeza kitufe.
Hamza mara baada ya kufika mbele ya mwanamke yule akiwa ameshikilia boksi lake mapigo yake ya moyo yalionekana kudunda sana.
Alikuwa ni msichana mweupe mwembamba kiasi ambaye alikuwa na ngozi laini mno na nywele zake ndefu, alikuwa na macho madogo ambayo yaliendana na namna uso wake ulivyoumbwa.
Ijapokuwa mrembo huyo hakuwa akimfikia yule msichana aliefahamika kwa jina la Tresha Noah ambaye alikutana nae kule kwenye jengo la Apartment la Dosam Homes lakini itoshe kusema huyo alikuwa mrembo na wakuvutia zaidi.
Katika maisha ya Hamza alishakutana na wanawake wa aina nyingi , kuna wanawake ambao alikutana nao licha ya kwamba walikuwa na uzuri wa aina yake lakini hawakuwa wakivutia kingono , kuna wanawake wengine ambao alikutana nao licha ya kwamba hawakuwa na muonekanno wa kirembo lakini walikuwa wakivutia mno kingono(Sexy), hizo ni aina mbili ambazo alikutana nazo Hamza , ijapokuwa mrembo huyo hakuwa mzuri sana lakini alikuwa na umbo ambalo linavutia kingono sana, yaani ni aina ya wanawake ambao ukimuona tu unawaza kufanya mapenzi.
“You are Hamza right?”Aliuliza yule mwanamke na sauti yake ilimuacha Hamza hoi.
“Yes.,.. yess”Alijibu kwa kubabaika.
“Okey nimepewa taarifa zako na Alex ,unaweza kufungua nithibitishe mzigo”Aliongea yule mwanamke , hakuwa na sura ya dharau wala ya ukarimu yaani alikuwa katikati huku akionekana kumkagua Hamza.
Hamza hicho ndio kitu pekee ambacho alikuwa akitaka kufanya , alikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini chungu hicho kilikuwa kikiuzwa pesa nyingi sana kuliko uhalisia.
Ilimchukua dakika chache sana kwa Hamza kufungua ndani , ijapokuwa kwa mtu wa kawaida angehitaji kisu kukata hizo gundi lakini Hamza hakuhitaji kisu na namna ambavyo alifungua ilimshangaza kudogo yule mwanadada lakini hakuongea chochote zaidi ya kubakia kimya.
Hamza mara baada ya kufungua lile boksi macho yake ni kama yamesaliti matarajio yake , ukiachana na namna ufungashaji wa chungu hicho ulivyo lakini hakikuwa na muonekano ule wa kimaajabu , kilikuwa chungu kama chungu ambacho muonekano wake ulikuwa wa kawaida sana , vilikuwa vyungu kama vile vya kitamaduni ambavyo wamama wengi hupikia.
Jambo hili lilimfanya Hamza kushangaa na kujiuliza nini kinaendelea , alijaribu kuangalia ndani yake kwani mwanzo alijua pengine kuna madawa ya kulevya kwenye hilo boksi lakini hakukuwa na kitu chochote cha kushangaza zaidi ya chungu.
“Kaka , inaonekana hii ni mara yako ya kwanza kufanya Delivery”
“Kwanini?”
“Unashangaa sana”Aliongea yule msichana huku akisimama na kumpokea Hamza kile chungu na kuanza kukichunguza kwa dakika kadhaa na mara baada ya kuridhika alitoa tabasamu na kumpatia Hamza kukirudisha kwenye boksi.
“Wait here”
Aliongea huku akibeba kile chungu na kutembea kuelekea upande mbele wa jengo hilo sehemu ambayo kuna mlango wa kuingilia ndani.
Hamza macho yake yalikuwa yakiangalia mpwito wa makalio ya mrembo huyo ambaye hakuwa akijali kama amevalia kijichupi tu na kuingia hadi ndani.
“Kuna watu wanafaidi aisee”Alijiwazia Hamza mara baada ya mrembo yule kutokomea kwenye jumba hilo ambalo lilikuwa na ghorofa mbili kwenda juu.
Hamza alitumia dakika hio kujaribu kukagua mazingira kwa haraka haraka na ile anagueza sura yake macho yake yalikutana na mlinzi aliekuwa akimwangalia na baada ya kukutanisha nae macho alionekana kama mtu ambaye alikuwa akimwangalia kwa macho yasiokuwa ya kawaida na Hamza alishindwa kuelewa lakini aliamua kupotezea na kugeuza macho yake sehemu nyingine.
Baada ya dakika kama sita hivi mwanamke yule alirudi huku awamu hio akiwa tofauti na alivyokuwa , alikuwa amejisitiri kwa kuvalia vazi refu la kitambaa cha hariri(Silk Duster) ambalo lilikuwa na vishikizo huku kichwani akiwa amevaa Bonnet.
Alikuwa hajalifunga vishikizo vyake na kumfanya bado nguo yake ya ndani kuonekana.
“Hesabu hizi?”Aliongea yule mwanamke huku awamu hii akiweka tabasamu na kumfanya Hamza kushangaa kidogo na kujiuliza mwanzoni hakuwa na mwonekano wa kusomeka lakini sasa hivi alikuwa akitabasamu.
Hamza alihesabu kwa haraka sana zile hela na baada ya kumaliza aligundua ni Shilingi laki moja na tisini.
“Hela iliozidi ni kama ofa Hamza , naamini utakuwa mwaminifu kuniletea mzigo wangu mwingine kila nitakapohitaji”Aliongea huku akiweka tabasamu na kuufanya uzuri wake kuzidi kuongezeka.
“Asante sana”Aliongea Hamza , ijapokua hakuelewa mwanamke huyo anamaanisha nini kumwambia anategemea kuletewa mzigo mwingine na yeye lakini hakutaka kuuliza.
Hamza mara baada ya kuaga aliweza kutoka nje ya geti huku bado akiwa na maswali mengi sana , swali lake kubwa ni kwanini chungu cha kawaida kama kile mwanamke huyo akakinunua kwa bei ghali,
Ilikuwa ni ajabu ambayo chungu cha kawaida ambacho kilikuwa kikiuzwa sokoni kwa shilingi elfu tatu kununuliwa kwa zaidi ya laki mbili.
Hamza alijiambia hata kama watu hao ni matajiri lakini bei hio ni kubwa sana kiasi kwamba haina uhalisia , akili yake palepale ilimwambia pengine kuna kitu cha ziada kwenye kile chungu lakini hakujua, kwani kila kitu hakikumwingia akilini.
Ijapokuwa alikuwa akijua madawa ya kulevya yalikuwa yakisafirishwa kwa mbinu nyingi lakini ilikuwa ngumu madawa kusafirishwa kwenye kile chungu, lakini hata hivyo hivyo hakutaka kufikiria zaidi.
Wakati akianza kutembea kukisogelea kituo cha daladala simu yake ilianza kuita na alipoangalia jina la mpigaji alikuwa ni Alex na palepale alipokea.
“Hahaha.. Bro kazi nzuri”Sauti ya Alex ilisikika bila hata ya salamu.
“Nimeleta mzigo tu sehemu husika , ni swala ambalo mtu yoyote anaweza kufanya”
“Hapana Bro , ni kweli linaweza kuonekana swala la kawaida lakini sio la kawaida kama unavyoona wewe”
“Unamaanisha nini?”
“Tutaongea usijali , ila nikuambie mwanangu sijui niseme una bahati au kuna siri kuhusu inayoendelea ,ila kwanzia sasa hivi utahusika na kumpelekea huyo demu kila atakapohitaji mzigo , amenipigia simu na kusema lazima iwe wewe”Aliongea Alex na kumfanya Hamza kusimama kwanza.
“Alex unajua mambo mengi umeniacha hewani , nina maswali mengi sana , itoshe kusema leo ni siku ambayo imenifanya kushangaa sana”
“Najua bro lazima utakuwa na maswali ila utajua , kwasasa elewa kwamba utakuwa unampelekea huyo manzi mzigo wake na malipo yatakuwa mazuri”Aliongea Alex na kumfanya Hamza kufikiria kidogo.
“Tunakutana wapi nikupe hela ya mzigo”
“Haina haja mzee unaweza kwenda nayo, hio chukulia kama pesa ya kujikimu kwa mwanzo wa kazi yako”Aliongea na palepale simu ilikatwa na kumfanya Hamza kuzidi kuchanganyikiwa
Kitu kingine kilichomfanya kuchanganyikiwa ni kama Alex alikuwa akiongea kinafiki ila hakutaka kuwaza sana kuhusu Alex bali aliwazia vyungu.
“Kuna siri gani juu ya hivi vyungu..?”
Ndio swali ambalo liliibuka kwenye kichwa chake na hali ya kutaka kuanza udadisi ilimvaa palepale , Hamza alijikuta akitengeneza Scenerio mbalimbali kwenye kichwa chake kuhusu vyungu ambavyo anatengeneza Alex.
Ukweli ni kwamba hata yeye aliona kuna kitu ambacho sio cha kawaida tokea dakika ambayo aliingiza mguu katika kiwanda cha Alex cha utengenezaji vyungu.
Hamza alianza kufikiria mbali zaidi na kujiambia hili swala halikuwa la kawaida tokea siku ambayo anaisikia Alex alikuwa muuza vyungu , kulikuwa na wafanyabiashara wengi nchini ambao wanatengeneza vyungu iweje Alex biashara hio imtoe na kuwa na maisha mazuri namna hio.
Safari yake ya kupata majibu ni kama ndio imeanza rasmi , kwanza kabisa alishajua aina ya vyungu ambavyo vilikuwa vikitengenezwa lakini pia alijua uthamani wa vyungu vingine , kilichokuwa kimebakia ni kujua nini siri iliokuwemo kwenye vyungu hivyo.
Swali tu la kumshangaza Hamza ni kwamba kwanini maisha yake yamejaa mshangao tokea siku anajitambua.
******
Saa kumi na mbili kamili za jioni Hamza alikuwa eneo la Mwenge , ijapokuwa haikuwa mwisho wa safari yake lakini aliamua kushukia hapo huku akiwa na wazo moja akilini na hio yote ni kutokana na kuwa na pesa nyingi mfukoni.
Hamza mara baada ya kushuka kituoni alivuka barabara upande mwingine na kisha akaingia kwenye maduka ya nguo, alikuwa na wazo la kununua nguo kwa ajili ya kwenda kwenye usaili siku ya kesho.
Ijapokuwa kwake ilikuwa kichekesho kwenda kwenye usaili huo kutokana na aina ya kazi yenyewe lakini hakutaka kudharau hata kidogo , kitendo cha kupigiwa simu asubuhi kilimwaminisha yoyote ambaye alituma lile tangazo alikuwa siriasi , lakini shauku yake nyingine ni kwamba kama mtu huyo alikuwa siriasi na kuamua kumlipa mtu zaidi ya laki saba wa ajili ya magizo tu basi ilimaanisha kwamba ni mwanamke mwenye pesa , lakini vilevile huenda kuna sababu ya ziada.
Hamza moja kwa moja aliingia kwenye jengo la Dosam Shopping Mall . hili ni jengo ambalo alikuwa akitamani sana kuingia siku moja kwa ajili ya kununua nguo , lakini kutokana na kukosa pesa kila siku alikuwa akiliogopa kama ukoma,lakini siku hio alikuwa na zaidi ya laki na nusu mfukoni hivyo aliamua kuzitumia katika manunuzi ya nguo kadhaa na kisha baada ya hapo angeenda saluni kuweka muonekano wake vizuri.
Sifa kubwa ya maduka ya Dosam ambayo yametapakaa nchi nzima ni nguo zake kuwa bora lakini kwa bei nafuu kabisa , ilikuwa ni tofati kabisa na madumka ambayo yalikuuwa yakipantikana mlimani City na kwingineko.
Kwa mfano Mlimani unaweza kukuta nguo inauzwa bei lakini ubora wake ukafanana na nguo ambayo inauzwa katika maduka ya Dosam, na inasemekana tokea kampuni ya Dosam kufungua maduka ya nguo biashara nyingi zimefirisika sana kutokana na mauzo kupungua.
Sifa nyingine katika maduka haya ni huduma ya viwango vya juu sana , yaani hawakujali muonekano wa mteja ambaye alikuwa akifika kufanya manunuzi katika maduka yao, wao walimjali kila aina ya mteja na kuwakwa daraja sawa na muda wote walikuwa ni watu wenye tabasamu usoni na wangekusaidia katika machaguzi ya nguo mpaka pale utakaporidhika.
Jambo hili lilimfanya Hamza kukubali sana mmiliki wa kampuni ya Dosam Global,
Ukweli ni kwamba inasemekana kampuni ya Dosam mmiliki wake ni mwanamke tena pengine ni kosa kusema mwanamke bali ikawa sahihi kusema ni Msichana ndio mmiliki.
Mwanzoni kampuni hii ilimilikiwa na Mzee Lasuli Dosam mwenywe na mara baada ya kufariki inasemekana usimamizi na urithi wa makampuni yote ulienda kwa mjukuu wake kike.
Uzushi unaenda mbali zaidi na kusema kwamba msichana huyo ambaye ni mmiliki alikuwa ni mrembo haswa , pengine zaidi ya neno lenyewe la Urembo lakini pia kwa wakati mmoja alionekana kuwa ni mwenye akili nyingi , baadhi ya watu walikuwa wakimtaja kama kiumbe kutoka sayari nyingine.
Jina hilo liliibka kutokana na kwamba aliweza kufanya biashara nyingi katika mataifa mbalimbali kupata hasara kubwa kutokana na mbinu zake za kibiashara tokea kupewa uongozi wa kampuni , vyombo mbalimbali vya habari vishawahi kumwandika kuhusu mwanamke huyo.
Hamza yote hayo alikuwa akiyajua , isitoshe alikuwa ni mtu mpenda mitandao ya kijamii hivyo ilikuwa ni rahisi kwake kukutana na taarifa ambazo zinamzungumzia , ukweli ni kwamba kukutana na taarifa hizo kwenye mitandao sio jambo la bahati mbaya , ukweli ni kwamba kuna taarufa zake nyingi , kwa mfano tu katika mtandao wa kijamii wa JamiiForum umejaa mada zinazomzunguzia mmiliki wa kampuni ya Dosam Global mara mia nne tokea kupewa uongozi , sio hivyo tu majarida makubwa duniani na yenywe yamemzungumzia mara nyingi sana na kufanya mahojiano nae.
Ajabu ni kwamba katika kila mahojiano ambayo yalifanyika inasemekana mwanamke huyo alikataa kupigwa picha.
Kuna wengine wanasema mrembo huyo alikuwa mbaya wa sura ndio maana hakutaka kuonekana lakini wale ambao wameenda kumfanyia mahojiano walisema alikuwa mrembo wa sura na hata wale ambao walikuwa wakifanya kazi katika kampuni hio walikuwa wakisema ni mrembo wa sura.
Hamza alijikuta akiwaza kila aina ya mada ambazo alizisoma mtandaoni kuhusu mmiliki wa kampuni ya Dosam na kilichomfanya kukumbuka taarifa hizo ni siku hio mara baada ya kuingia kwenye duka hilo.
“Kaka hii itakufaa sana , kwanza kabisa inaendana na mwonekano wako wa mwili kwanzia rangi yako mpaka urefu na unene wako , kitu kimoja ambacho kitakufanya upendeze zaidi ni kunyoa nwele kwa mtindo huu”Aliongea mwanamke mrembo sana huku akimuonyesha Hamza vazi maalumu ambalo amechagua.
Hamza aliweza kushika kishikwambi huku akiangalia mtindo wa nywele ambao mfanyakazi wa eneo hilo amependekeza na aliishia kutoa tabasamu.
“Sijazoea kunyoa hivi dada”AliuongeaHamza.
Mtindo wa nywele ambao aliokuwa akiangalia kwake ni kama haukukaa kimaadili, pengine sio kwamba mtindo wenyewe haukukaa kimadili lakini kutokana na sheria zake au pengine aina ya maisha aliokulia ndio maana aliona ni mtindo ambao haukukaa kimaadili.
Ilikuwa ni kama vile wale wazee waliozaliwa miaka ya sitini na sabini uwaambie wanyoe kiduku ukweli ni kwamba hawatokuelewa, lakini sasa kidogo ilishangaza kwa Hamza kwani alionekana ni kijana kabisa ambaye hata miaka therathini hajafikisha.
Yule mfanyakazi wa kike mrembo aliishia kushangaa kidogo lakini aliubadilisha mshangao wake na tabasamu.
“Kaka niamini , huu ni mtindo ambao utamfanya mwanamke yoyote yule kukupenda , kwanza wewe ni handsome na kwa muonekano wako ni kama vile Justin Timberlake, hivyo staili yako ya nwele inakupasa kufanana…..”
Hamza kwa namna ambavyo mwanamke huyu alivyokuwa akiongea ungeweza kuamini na kujisikia vizuri lakini kilichomfanya kutokuamini maneno yake ni kwamba pembeni yake kulikuwa na bwana ambaye alikuwa ni mweusi sana na kichwa kama kibuyu aliekuwa pia akihudumiwa , ukweli katika maisha yake hakupenda kujifanananisha lakini alisema ijapokuwa yeye hakuwa akijiona Handsome lakini huyo bwana aliekuwa pembeni yake alikuwa na sura ngumu mno, ndio mwanaume hasifiwi kuwa na sura nzuri lakini kilichompa mshangao ni namna ambavyo mfanyakazi alivyokuwa akimpamba kwa kumwambia alikuwa na sura nzuri na kichwa kizuri, hivyo ilikuwa ni ‘redflag’ ya kuona hata yeye alikuwa akipambwa tu kinafiki nje ya uhalisia wa muonekano wake.
Iliimchukua kama nusu saa kuhudumiwa na kisha alipewa nguo zake na kutoka, alikuwa amenunua suruali mpya , Jeans pamoja na viatu na ajabu ni kwamba hakuwa amelipa pesa nyingi, kilichokuwa kimebakia ni kwenda Saluni na kuweka nywele zake sawa kwa ajili ya maandalizi ya kesho.
Hamza wakati akitoka kwenye Lift alijikuta akijichekea , yaani kwa namna ambavyo alikuwa akijiandaa ni kama vile anakwenda kukutana na mchumba au anaenda kwenye ‘Blind date’, alicheka kutokana na kwamba siku kadhaa zilizopita wakati wa kumtongoza mwanamke mrembo kama Anitha hakujali kabisa muonekano wake zaidi ya hisia zake, tena anakumbuka ile siku shati lake lilikuwa limechafuliwa na juisi ya matunda wakati akiwa kwenye daladala na kutengeneza doa..
Hamza alitamani kughairisha kwenda saluni lakini kuna roho ilikuwa ikimwambia ‘ingia saluni bro upendeze acha uchafu’, pengine mwanamke unaekwenda kukutana nae ni zaidi ya Anitha.
Hamza mwenyewe alishangaa na kujiuliza hio sauti inatoka wapi , lakini aliamua kuitii na kujiambia pengine ni roho mtakatifu , lakini mara baada ya kuingiwa na neno Roho mtakafitu alipotezea na kujiambia kwanza hakuelewa yeye ni dini gani hivyo aliamua kupotezea kile anachofikiria na kuamua kufuata utashi wake unakomwelekeza.
“Bro unanyoa staili gani?”Aliuliza kinyozi mara baada ya Hamza kukalishwa kwenye kiti na kinyozi kumaliza maandalizi yake.
Hamza alifikiria ni staili gani anyoe , au apige para..”Alijikuta akikosa majibu na palepale macho yake yalitua kwenye picha ambazo zilikuwa na vichwa ambavyo vimenyolewa kwa staili tofauti tofauti.
Baada ya kuangalia ni staili gani ingemfaaa palepale alijikuta akiishia kwenye staili ambayo alionyeshwa muda mchache uliopita na yule muuza nguo,.
“Bro hio staili ni nzuri na inaendana na nywele zako lakini kidogo itakugharimu, kwani ili upendeze utahitajika na kuosha pia na kupakwa dawa”Aliongea kinyozi akiwa na wasiwasi Hamza asingeweza kumdumu bei.
“Ni shilingi ngapi jumla?”
“Kwa kila kitu nilichokutajia jumla yake ni elfu kumi na tano tu?”Aliongea .
“Ni bei kubwa ndio ila nitalipia”Aliongea Hamza na yule bwana alimwangalia kidogo na kisha akaanza kupiga kazi,
Hamza hakuwa mwafrika orijinal bali alikuwa ni chotara , mchanganyiko wa Mwafrika na mzungu hivyo nywele zake zilikuwa zimekaa kizungu pia japo rangi yake ilikuwa imefubaa kidogo kupoteza ile hali ya uzungu yaani kwa maneno marahisi ni kwamba uzungu wake umeathiriwa na rangi ya kiafrika.
Zilipita dakika chache tu kama nusu saa hivi kinyozi alikuwa ashamaliza kumuweka Hamza sawa upande wa nwele na alitakiwa kuweka dawa pamoja na kuoshwa na kukaushwa na hakuwa na hiyana kufuata maelekezo kutokana na kwamba ndio mwenyewe aliamua kuyavulia maji nguo hivyo hakuwa na budi kuyaoga.
Baada ya lisaa lizima aliweza kusafishwa vizuri na alipewa na ofa ya kusafishewa uso na Scrub .
“Edmund naelekea nyumbani , bado hujamaliza tu?”Sauti ya kike iliweza kusikika katika Saluni ambayo Hamza anapunguza nywele.
“Leila nisuburi kuna bwana anamalizia kukaushwa nataka nione kama hana kasoro tuondoke”Aliongea kijana huyo na kumfanya Leila kuvuta pumzi na kisha kwenda kukaa kwenye sofa.
“Zamu yako ishaisha , leo mapema sana mpenzi”Aliongea Edmund.
“Bosi katoa maagizo kila mfanyakazi anaefikia malengo ya mauzo kwa siku anaweza kuondoka hata kama ni mchana”Alijibu na kumfanya Edmund kutingisha kichwa huku akichomoa simu yake chaji.
Dakika ileile mlango wa chumba cha wanaooshwa kwenye saluni hio kilifunguliwa na Hamza aliweza kutoka akiwa anawaka hatari na kumfanya yule mdada aliekuwa ameketi kwenye Sofa kupigwa na mshangao.
“Kaka nilikuambia hio staili ya nywele itakufaa , jamani hebu muone alivyopendeza”
Msichana Leila alikuwa ndio aliemhudumia Hamza katika kununua mavazi na aliweza kumtambua Hamza mara baada ya kumuona.
“Leila unamjua?”
“Yeah mimi ndio nilimuelekeza kuja hapa”Aliongea huku akimwangalia Hamza kwa macho ya kurembua na kumfanya Edmund kuona wivu.
Ukweli hata Hamza mara baada ya kujiangalia kwenye kioo alijiona kabisa amebadilika , ijapokuwa bado alikuwa na mavazi yake yaleyale lakini aliamini kama atavaa alionunua basi atakuwa ni mtu mwingine kabisa, aliishia kutoa tabasamu kwa kujikubali na kujiambia yeye kumbe ni Hamdsome aliekosea matunzo.
“Bro naona umekaa sawa sasa , unaweza kulipa sasa , nilikuwa nikikusubiria wewe tu”Aliongea Edmund huku akimkatisha Hamza ambaye alikuwa akijiangalia kwenye kioo pasipo ya kuridhika.
“Okey ngoja nilipe”Aliongea na palepale aliingiza mkono mfukoni na kutoa pesa nyekundu mbili na kisha kumpatia”
“Sister asante kwa kupendekeza hii staili ya kunyoa , chenchi inayobakia ni shukrani yangu kwako”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu na palepale alimkonyeza Leila na kuchukua mifuko yake na kutoka.
“Broo….!!”Edmund alitaka kuongea neno lakini palepale Leila aliekuwa akimwangalia Hamza kwa macho ya kurembua alimpa ishara ya kufunga mdomo wake.
Siku iliofuata Hamza hakuwa na ratiba za chuo kabisa mpaka jumatatu, yaani siku hio ilikuwa ni Ijumaa na kwa kozi aliokuwa akisomea ni kama wikiendi ndio imeanza rasmi.
Usiku hakuwa amelala kabisa , alikuwa na mawazo mengii, kwanza aliwaza sana kuhusu mtu anaefahamika kwa jina la Mzee mtu ambaye hakuwa akimjua licha ya kwamba amehusika katika maisha yake kwa kiasi kikubwa , aliwaza namna ya kumfahamu Mzee ni nani na kwanini alikuwa akimtafuta nyakati za usiku , aliwaza mambo mengi kuhusu mzee na kujijengea picha katika akili yake na kujiambia pengine Mzee ni mtu mzito serikalini .
Mawazo ya namna hio yalimjia kutokana na maisha ambayo amekulia kulingana na maagizo ambayo Mzee alitaka awe.
Yaani kwa maneno marahisi ni kwamba mpaka wakati huo Hamza hakuwa ameyaishi maisha yake , ni kama maisha aliokuwa akiishi ni kwa ajili ya Mzee kwani ndio aliekuwa akimwambia afanye hivi na vile na yeye kutii.
Alikumbuka siku ambayo hakutii maagizo ya Mzee na kilichomkuta mpaka siku hio na umri wake huo hajawahi kusahau , sasa kutokana na tukio hilo ambalo lilimtokea ilimfanya kuamini pengine mzee ni mtu mkubwa sana serikalini , ukweli ni kwamba alikuwa na mawazo mengi kuhusu Mzee.
“Kama mzee hataki kujitokeza kwangu mimi nitajitokeza mbele yake uwezo huo ninao”
Aliongea Hamza baada ya kuwaza , alionekana ameamua mwenyewe katika kichwa chake na kujiambia kama mtu huyo anaemtambua kwa jina moja tu la Mzee asipojitokeza kwake basi yeye atajitokeza kwake ,. Hakujua ni kwa namna gani ambavyo angemfahamu Mzee lakini alijiambia kutokana na uwezo wake basi lazima amfahamu mzee .
Hamza hakuwaza tu kuhusu Mzee pia aliwaza kazi ya Alex ya utengenezaji vyungu namna ambavyo ilionekana kumtajirisha nje ya uhalisia wa biashara wenyewe , alikuwa na shauku ya kutaka kujua kilichopo nyuma ya vyungu vile ni nini, kuna hali ilikuwa ikimwambia pengine ni njia nyingine ya usafirishaji madawa lakini alipingana na mawazo yake na akili yake ilimwambia kabisa pengine ni kitu kingine kabisa ambacho hajawahi kukifikiria kwenye maisha yake, kutokana na mawazo mengi alijiambia pia hilo ni swala ambalo atalitafutia ukweli.
Baada ya kuoga vizuri na kujiandaa kwa kuvaa mavazi yake mapya na viatu, licha ya kwamba hakuwa na kioo lakini aliamini alikuwa amependeza haswa.
Usaili kwa maelekezo ya mwanamke kwenye simu alimwambia ni saa nne asubuhi katika hoteli ya Dosam V
Hamza alikuwa akijua hoteli hio vizuri kwani ilikuwa ni hoteli maarufu na yenye jengo refu kwenda juu ndani ya jiji lote la Dar es salaam , pengine asilimia hamsini ya watanzania wote walikuwa wakiijua hoteli hio kwani matamasha mengi hufanyikia hapo, hata vikao vya waandishi wa habari hufanyikia ndani ya hoteli hio.
Siku hio pengine ndio inakuwa mara yake ya kwanza kuingia katika hio hoteli,lakini licha ya hivyo hakuonekana na wasiwasi kabisa.
Hakutaka hata kujihangaisha na maswala ya nchi asubuhi hio na alijiambia atajua mbele kwa mbele.
Mara baada ya kutoka nje ya eneo hilo la uswahilini wanawake na wanaume walikuwa wakimkodolea macho kwa mshangao mkubwa.
Ukweli ni kwamba muoenknao wa Hamza ulikuwa hauendani kabisa na maeneo hayo ya uswahilini , kitendo cha kuchanganya rangi ya mzungu na mwafrika ilikua ni kama sababu kubwa ya kumuona Hamza sio wa kawaida.
Hata asubuhi hio watu wengi sio kama walikuwa wakimwangalia kutokana na kupendeza kwake bali ni kwamba walikuwa wakimwangalia huku wakijiambia moyoni Hamza amerudi katika uhalisia wake na maisha ambayo alikuwa akiyaishi hapo na familia hizo ni ya magizo tu.
“Niliwaambia mimi , hakuna mtu mzungu akawa masikini hivi”Aliongea mmoja ya viijana walioamkia kucheza pooltable.
“Juma uko sahihi , hata mimi kwasasa nakuunga mkono , jamaa hakuwa mwenzetu kabisa, ule upole wake ulikuwa ukificha mambo mengi”Alichangia mwingine. Na stori juu ya Hamza hazikuishia kwa wacheza pooltable tu hata wanawake waliokuwa wakiuza vitafunwa nje ya vibaraza vya nyumba zao walikuwa wakimzungumzia Hamza.
Hamza kutokana na watu wengi kumshangaa kwake ilitosha kumwambia kwamba alikuwa amependeza.
Naam ni saa tatu na nusu Hamza aliweza kufika kandokando ya bahari ya Hindi nje ya geti la kuingilia katika hoteli ya Dosam.
Tofauti ya Hamza na wageni ambao walikuwa wakiingia ndani ya hoteli hio ni kwamba yeye alishuka na basi la mwendokasi lakini wageni wengine wote aidha walifika wakiwa kwenye gari binafsi au waliletwa hapo na Uber , Bolt na magari mengine yanayofanya huduma ya Taxing,
Licha ya hivyo swala hilo halikumpa unyonge sana Hamza , pengine kwa watu waliokuwa wakimwangalia wangesema labda Hamza alikuwa amejipa uzoefu mwingine wa kupanda magari ya abiria.
Mwonekano wake ulimbeba,alikuwa ni mtanashati mno, Hamza alikuwa ni mwanaume mrefu kwenda hewani , mwenye mwili ambao umejengeka kimazoezi akiwa na weupe wa kuchanganya rangi na macho yake ambayo yana kiini ambacho hakikuwa cheusi sana kama waafrika wengi , pengine uzungu wake ulionekana zaidi machoni kuliko sehemu yoyote ya mwili lakini hata hivyo ilikuwa kosa kumuita Mzungu.
Katika mavazi yake aliovaa kitu pekee alichokosa ilikuwa ni saa tu mkononi , pengine ingemfanya kuonekana Handsome zaidi lakini hata hivyo bado alionekana kupendeza.
Hamza alitembea kwa kujiamini kana kwamba alikuwa ni mzoefu kabisa wa eneo hilo.
“Ni muda mrefu sana nimejitenga na maeneo ya namna hii , nadhani ni mwanzo wa mimi kurudi kwenye maisha yangu”Alijiwazia Hamza huku akiongea kauli ambayo kidogo inachanganya.
“Hello!, nina miadi na mtu ndani ya hii hoteli?”Aliongea Hamza mara baada ya kufika katika Front desk.
“Karibu sana kaka , nitajie jina la mgeni unaetaka kukutana katika hoteli yetu tafadhari”Aliongea yule mwanadada na kumfanya Hamza kuwaza kidogo , ukweli ni kwamba hakuwa akijua jina lake kamili na aliambiwa tu kufika ndani ya hoteli hio muda wa saa nne.
Wakati akijiuliza ni jina gani anapaswa kutaja palepale simu yake ilianza kuita na aliitoa haraka haraka na kuangalia jina la mpigaji na alitoa tabasmau na kumwangalia yule mrembo wa mapokezi akimpa ishara kwamba anapiga.
Hamza aligeukia upande mwingine ili kuongea na simu lakini macho yake yalitua kwa mwanamke mrembo sana ambaye alikuwa akisogea katika dawati la eneo la mapokezi.
“Hello Mr , uko wapi unakumbuka miadi ni saa nne kamili?”Sauti ilisikika upande wa pili lakini wakati huo macho ya Hamza yalikuwa kwa mwanamke aliekuwa akitembea kimadaha kusogelea upande wake.
“Nipo eneo la mapokezi ndani ya hoteli ya Dosam”Aliongea Hamza na palepale yule mwanamke alisimama huku akitoa simu yake sikioni na kuangalia mbele yake na palepale alionekana kugundua kitu na haikuwa kwake tu hata kwa Hamza mwenyewe alionekana kugundua mtu aliekuwa akiongea nae kwa simu ni mwanamke aliekuwa mbele yake.
Sasa tofatui ni kwamba Hamza mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda mno kutokana na kushangaa urembo wa mwanamke ambaye alikuwa akimsogelea huku akiwa na uso uliopambwa tabasamu.
Hamza ni kama hakuamini kama huyo ndio mwanamke ambaye alikuwa akienda kuonana nae.
Kuhusu yule mwanamke hakuonyesha mshangao wowote wa Hamza , yaani ni kama Hamza alionekana wa kawaida sana na mara baada ya kumfikia alinyoosha mkono kwa ishara ya kusalimia.
Comments