Wasichana wawili ambao walikuwa eneo la mapokezi kidogo walionyesha kukosa utulivu mara baada ya kumuona mwanamke alievalia suti akisogea upande wao na walijua pengine alikuwa akiwasogelea lakini walijikuta wakishangaa mara baada ya kumuona mwanamke yule akisimama mbele ya Hamza na kunyoosha mkono.
“I Suppose wewe ndio Hamza right!!?”Aliuliza yule mwanamke akiwa na tabasamu usoni.
“Yes ndio mimi Hamza Mzee”Aliongea Hamza huku akionyesha kukosa utulivu kiasi na kunyoosha mkono wake kusalimiana nae.
Wakati wa kushikana mkono na yule mwanamke alihisi ni kama kuna shoti za umeme zinampiga kwani zilianzia mkononi na kwenda kichwani kutoa mawasiliano kama ameshikana na kitu kisichokuwa cha kawaida na baada ya pale taarifa zilitumwa kwenye moyo kwa ajili ya kuongeza msukumo wa damu kuelekea kiwiliwili cha chini na ghafla tu kiungo cha uzazi cha Hamza kilianza kusisimka.
Muunganiko wa mwili ulikuwa ni wa ajabu sana na pengine Mungu katika kazi aliopatia ni kuumba kiumbe binadamu.
Mwanamke aliekuwa mbele yake alikuwa ni mweupe wa wastani, mrefu kiasi mwenye mwili uliojipanga huku ngozi yake ikiwa ni kama vile imetengenezwa , itoshe kusema katika wanawake ambao Hamza alishawaona tokea afike jijini Dar es salaam huyo ndio mwanamke wa kwanza kwa uzuri , Melissa mpenzi wake Amiri alijiambia tupilia kule , Tresha Noah msichana alieambiwa alikuwa ametengenezwa muonekano wake tupilia kule , Anitha hakutaka hata kuongea zaidi ya kutamani kusonya.
“Mr Hamza!, naitwa Prisila Singano Afisa mkuu wa idara ya Rasilimali watu kampuni ya Dosam, mimi ndio niliekupigia simu nadhani sauti yangu hujaisahau”Aliongea kwa mapozi na kumfanya Hamza kuzidi kupagawa , hakuamini huyu ndio mwanamke ambaye alikuwa akitafuta mchumba wa maigizo.
‘Nimefurahi kukufahamu mrembo Prisila Singano , lakini naomba kuuliza una undugu na Profesa Stephano Singano?”Alongea Hamza huku akiwa anajiamini kiasi kwamba kama unamjua ungesema hio hali ya kujiamini kaitolea wapi, maana Hamza tunaemjua sisi ni yule Mzembe aliepigwa cha mbavu na mrembo Anitha.
Wale wafanyakazi wa mapokezi walikuwa na maswali kibao , walikuwa wakimfahamu Prisila sio mtu wa mchezo mchezo ijapokuwa alikuwa mdogo ki umri lakini alikuwa ni mkali mno kazini na hakupenda uzembe lakini sio hivyo cheo chake kilikuwa kikubwa mno ndio aliekuwa ni CHRO wa kampuni ya Dosam Global.
Kila mwanadada ndani ya jiji la Dar es salaam ambaye alikuwa ni mtaaluma alikuwa akimchukulia Prisila kama ‘role model’ wao kutokana na mafanikio yake ya haraka haraka na kuongoza kampuni kubwa Afrika na duniani.
Yaani kwa maneno marahisi yeye ndio alikuwa mwajiri mkuu wa kampuni ya Dosam hivyo watu wengi wanaotafuta ajira walikuwa lazima wapitie kwa huyu mwanamke, kutokana na watu wengi kutaka kufanyia kazi katika kampuni ya Dosam wale ambao walipata nafasi hawakutaka kuzembea kazini na kutolewa , kwani kudumu ndani ya kampuni ya Dosam ilihitajika zaidi utendaji mzuri na ujuzi na sio maswala ya GPA au ufaulu mkubwa unaonekana katika cheti chako.
Hivyo ilimfanya Prisila kuogopeka sana kwani alikuwa ni mwanamke aliekuwa akienda na falsafa yake ya 4E katika eneo la kazi ambayo ilisimama kama mbadala wa Effort(juhudi), Excellence(Ubora), Embodiment(Mfano halisi) na Environment(Mazingira).
Yaani kama mfanyakazi akikosa vigezo katika hio falsafa ya 4E basi kama ni mfanyakazi atafukuzwa au kama ndio anaomba hawezi kupatiwa kazi, ukikidhi vigezo hivyo hata kama cheti chako hakina maksi kubwa basi jihesabie unafanya kazi katika kampuni kubwa Afrika ya Dosam Global.
Prisila alicheka kwanza , hakuamini Hamza angekuwa ni mwanaume wa kujiamini namna hio tena na kwenda mbali na kumtania kama mrembo , asilimia kubwa ya wanaume wa rika la Hamza aliokutana nao wengi walionekana ni wenye kukosa hali ya kujiamini.
“Mzee Stephano ni baba yangu, sijui umefahamiana nae vipi lakini sina muda wa kuukuliza sasa hivi kwani unapaswa kukutana na bosi mwenyewe ambaye anataka kukuajiri , naomba nifuate Hamza”Aliongea na kauli yake ilimfanya Hamza kutoa macho.
Inamaana huyu mwanamke sio ambaye alikuwa akihitaji mtu wa kufanya nae maigizo ya boyfriend, alijiuliza Hamza na aliona ilikuwa ikileta maana , mwanamke mrembo kama huyo anahitaji vipi boyfriend wa maigizo kwa mfano , ilikuwa kichekesho.
Hamza alijiambia alikuwa akijidanganya tu , pengine matumaini yake ya kukutana na mwanamke mrembo yalikuwa yakienda kusambaratikika kabisa..
“Kwanini isingekuwa ni wewe , pumbavu kabisa yaani nimejitutumua vyote hivi kupendeza na kuwa jasiri mbele yako…”
“Mr Hamza come on,.. muda unaenda?”Aliongea Prisila mara baada ya kumuona Hamza amesimama tu na kumfanya bwana huyo kushitika kutoka kwenye mawazo na kuanza kutembea.
Wale wafanyakazi wa mapokezi waliishia kuangaliana kwa ishara kama vile wanajiuliza huyo mtu ni nani , kwanini bosi Prisila ndio kaja mpaka hapo kumchuka.
Asilimia kubwa ya watu ambao aliweza kuwaona ndani ya jengo hilo ni wazungu na wahindi na waliochanganya rangi kama yeye , watu weusi walikuwa ni wa kuhesabu sana , pengine ni kutokana na eneo lenyewe kuwa ghali sana , hii ilimfanya Hamza kujiambia kwamba hata kama mtu anaekutana nae kuwa mbaya lakin angalau anaonekana kuwa na pesa na kama angepita katika usaili huo ilimaanisha kwamba moja kwa moja angepata Exposire ya maeneo ya watu wazito wazito.
“Hata kama ni mbaya nnitaenda nae hivyo hivyo kibishi, pengine inaweza kuniweka na watu wazito wazito na ikawa safari ya kumjua Mzee”Aliwaza Hamza wakati akiwa kwenye lift.
Ijapokuwa alikuwa katika hali ya mawazo lakini bado hakuchoka kutazama umbo la mwanamke mrembo Prisila, alitamani kuuliza swali lakini alishindwa mara baada ya lift kufunguka na kuruhusu mtu mwingine kuingia.
Dakika chache tu walienda kutokezea katika floor ya juu kabisa na mara baada ya Hamza kutoka kwenye lift hiyo alijikuta akishangaa baada ya kuona uzuri wake lakini macho yake yalichanua mara baada ya kugundua eneo hilo lilikuwa likihudumia watu wa hadhi ya juu yaani VVIP.
Ijapokuwa alikuwa akijiamini kama vile amekunywa kiroba lakini bado mapigo yake ya moyo hayakuacha kudunda kwa kasi na kujiuliza ni mtu gani ambaye anaenda kufanya nae usaili tena eneo la VVIP katika hoteli kubwa ya hadhi kama hio.
Prisila alionyesha kutembea kama vile anafanya makusudi , pengine amevutiwa na sura ya Hamza maana bwana huyo alikuwa amependeza kweli ukijumlisha na muonekano wake wa ngozi ilimfanya kuwa wa kuvutia kwa kila mwanamke yoyote yule , lakini licha ya hivyo hali ya kimasikini ya Hamza haikujificha kwenye uso wake.
Kuonekana tajiri ni tofauti na uvaaji wa mavazi , unaweza kuwa tajiri lakini ukaamua kuishi maisha ya kawaida lakini siku zote huwezi kuonekana masikini , masikini siku zote ataonekana kwa umasikini wake na tajiri ataonekana kwa utajiri wake, kuna vitu vingi sana vya kumtofautisha tajiri na masikini au mtu aliefanikiwa na ambaye hajafanikiwa na hio inaenda kabisa kwanzia katika namna mtu unavyoongea ,wajihi , namna unavyotembea na ujengaji wa hoja wakati wa kuchangia mambo.
Tajiri anaweza akajificha katika kundi la watu masikini lakini siku zote hawezi kufanana na masikini.
Masikini na tajiri wote wanaweza kuwa na njaa kutokana na kutokula lakini kama utaamua kuwatofautisha na njaa zao utagundua masikini ndio anaeteseka zaidi na njaa kuliko yule tajiri, maana njaa ya tajiri ni ya kuchelewa kula wakati njaa ya masikini ni ya kukosa chakula.
Kwa upande wa Hamza ukweli ni kwamba ilikuwa ngumu kumtofautisha na masikini , kwa haraka haraka unaweza kusema kwamba Hamza ni mtoto wa tajiri ambaye ameamua kuishi maisha ya kimasikini.
Prisila alienda kusimama katika mlango namba 402 na kisha aligonga mlango kwa dakika kadhaa na palepale mlango ulifunguliwa na mwanadada mwenye sura iliokakamaa alievalia suti kama vile ni afisa usalama au bodigadi.
Mwanamke yule alimruhusu Prisila kuingia lakini alimwashiria Hamza kusimama nje kabla ya kuingia.
“Kijaji mruhusu, ndio mgeni anaepaswa kuonana na bosi”Aliongea Prisila lakini mtu alieitwa Kijaji bado alimwangalia Hamza kwa macho ya tahadhari na palepale alimsogelea na kuanza kumpapasa kama hana siraha ya aina yoyote na aliporidhika alimpiga jicho kali la tahadhari na kisha akamruhusu kuingia.
Hamza alijiambia huyu mwanamke ni mrembo sana lakini tabia yake ya ukakamavu inamfanya kuwa na sura ngumu.
Hata hivyo hakutaka kumfikiria sana , yeye hofu yake ni mtu ambaye anakwenda kuonana nae.
Hamza alikaribishwa na mandhari ya kuvutia ya chumba cha hadhi ya raisi(Presidential suite), haikuwa chumba cha kawaida kwa mtu wa kawaida kuingia na ilimfanya Hamza macho yake kuangalia vitu vilivyokuwemo pamoja na uzuri wake kwa haraka haraka.
Mbele yake kabisa upande wa dirisha kubwa ambalo linaangaliana na bahari ya Hindi kulikuwa na eneo la sebuleni na sofa kubwa ambalo lilikuwa imekaliwa na mtu alievalia kofia ya hat kichwani.,
“Huyo ndio bosi , nadhani mawazo yangu yapo sahihi nakwenda kukutana na mtu mbaya ambaye amekataliwa na wanaume mpaka kuamua kutafuta boyfriend feki , aisee hata hivyo maji nimeyavulia nguo sharti ni yaoge”Alijiongelesha katika mawazo yake akimwangalia yule mwanamke aliempa mgongo akisubiria surprise ya kuona sura ya mwanamke mbaya,
“Bosi , Mr Hamza kashafika kwa ajili ya usaili?”Aliongea Prisila huku akionyesha hali ya heshima.
“Okey mnaweza kuondoka , nitawaita baada ya usaili”
“Boss!!’Aliongea Kijaji kwa tahadhari.
“Hakuna kibaya kinachoweza kunitokea , mnaweza kuondoka”Aliongea bila ya kugeuka .
Upande wa Hamza sauti hio ilimsababishia mshituko wa aina yake , ilikuwa ni sauti nyororo lakini yenye madaraka ndani yake, ilikuwa ni kama wimbo wa kubembeleza unaozigonga ngoma za masikio yake.
Ilikuwa ni sauti nzuri mno na Hamza alijiuliza au mawazo yake ni tofauti na uhalisia , kwanini mwanamke anaemdhania kuwa ni mbaya wa sura kuwa na sauti nyororo hivyo , alijiambia pengine sio mbaya kila kitu , isitoshe kuna msemo wa kwamba Mungu hakupi vyote , anaweza akakupa sauti nzuri lakini akakupa sura mbovu, anaweza akakupa mguu ila akakupa Komwe kubwa.
Licha ya Prisila Singano kusita sita pamoja na mlinzi wa bosi huyo lakini waliishia kutii maagizo yake.
“Ukifanya chochote kibaya kitakachomdhuru bosi basi jua ndio kifo chako”Aliongea Kijaji kwa tahadhari na kumfanya Hamza kutoa tabasamu na kuzidi kumkera mlinzi wa watu,
Baada ya kila mtu kuondoka ndani ya hiko chumba yule mwanamke palepale aliinua mkono wake na kuitoa ile Hat.
Ilikuwa ni hat aina ya Beekeeping Veil, yaani hat ambazo huunganishwa na kitambaa cheusi ili kuzuia sura ya mtu kutokuoenekana
Hamza mara baada ya kuona mkono wa yule mwanamke ukiondoa ile hat taratibu mapigo yake yalianza kuongezeka spidi spidi , ilikuwa ni hisia ambazo kwenye maisha yake hakuwahi kuzisikia hata siku moja, kadri ile Veil ilivyokuwa ikiiacha sura wazi alizidi kujawa na hofu pamoja na mshituko wa aina yake,
Mwanamke yule baada ya kuivua alisimama na sasa namna ambavyo alikuwa akisimama ni kama vile yupo kwenye mwendo wa slow motion , ni kama vile malaika anaibukia kutoka ardhini.
Yalikuwa ni matarajio tofauti kabisa na kile alichokuwa akikiwazia Hamza , mwanamke aliekuwa mbele yake akili yake ilimwambia kabisa ni mwanamke ambaye anapaswa kusujudiwa kwa kupaza sauti.
******
MIEZI KADHAA ILIOPITA.
Ni miezi kadhaa iliopita ndani ya eneo la maegesho ya magari katika hospitali ya chuo ya Mayaya Clinic iliingia gari ya kifahari aina ya Porsche Gayenne G Coupe .
Baada ya gari hii kusimama palepale mlango wa dereva ulifunguliwa na mwanaume mtanashati alievalia suti na kwa haraka haraka alizunguka upande wa kushoto na kisha akafungua mlango wa abiria.
Mwanamke mrembo sana alievalia gauni lenye mkanda kiunoni na Blazer ya rangi ya ugoro alishuka kwenye gari lile huku yule mwanaume akionyesha heshima mbele yake.
Kwa haraka haraka anaeangalia tukio lile angeelewa kwamba yule mwanaume ni dereva wa yule mwanamke.
“Utanisubiria hapa mpaka nitakapomaliza”.
“Sawa madam”
Alijibu yule bwana kwa heshima kubwa tu mbele ya yule mwanamke , alikuwa ni msichana mrembo haswa pengine zaidi ya neno urembo , alikuwa ni msichana mdogo pia kimuonekano makadirio ya miaka kama ishirini na nne hivi , alikuwa ni mweupe wa wastani mrefu na aliejaaliwa umbo zuri.
Kitu kimoja tu ambacho pengine ambacho kinapunguza asilimia mbili ya uzuri wake ni muonekano wa yule mrembo , alikuwa ni kauzu mnno lakini hata hivo bado alikuwa amependeza.
Aliweza mkoba wake kwapani vizuri na kisha alizipiga hatua kuingia ndani ya hospitali hio kubwa.
Mayaya Clinic ni moja ya hospitali kubwa sana ndani ya ukanda wa Afrika mashariki na kati yote , ilikuwa ni hospitali ya binafsi ambayo ipo chini ya kampuni ya Vexto Group kampuni namba moja kwa ukubwa Afrika na namba kumi kwa Dunia nzima.
Yule mwanamke mrembo alitembea kwa mwendo wa kujiamini mpaka kwenye lift huku akionyesha sio mwenye kujali macho ya wanaume na wanawake wanaomwangalia.
Ukweli ni kwamba ilionekana ni kawaida kwake kuangaliwa hivyo kutokana na yeye mwenyewe alivyo , alikuwa mzuri hivyo ilileta maana kuangaliwa na kila mtu , wengine walimwangalia kwa matamanio na wengine walimwangalia kwa maswali kwa Mungu kwa kuweza kuumba mwanamke wa aina hio.
Wahenga wanasema Mungu hakupi vyote na kauli hii ilithibitishika kwa mrembo huyu ndio maana siku hio ya asubuhi alikuwa ndani ya hospitali hio
Dakika chache mbele mwanamke yule alikuja kutokezea katika floor namba saba ambayo ni idara ya Saikolojia(Psychiatric Department).
Idara ya saikolojia mara nyingi huhusiika na tiba ya magonjwa mbalimbali ya yanahusiana na akili.
“Miss Regina karibu sana , Dr Shukuru anakusubiria”Aliongea mwanadada wa mapokezi.
Kwa haraka haraka ilionekana mrembo huyu ambaye sasa anafamamika kwa jina la Regina alikuwa ni mgonjwa wa mara kwa mara kufika ndani ya hospitali hio kutokana na nesi wa mapokezi alivyompokea.
Mrembo Regina aliishia kutingisha kichwa na kisha alitembea kuelekea upande wa kulia akipita mapokezi na alisimama mbele ya mlango uliokuwa na kibao juu ofisi ya daktari au chumba cha daktari namba 01.
Mazingira ya hospitali katika idara hio ya magonjwa ya akili ilikuwa tulivu mno, pengine unaweza kusema wagonjwa wanaofika katika hospitali hio ni wachache lakini huo sio ukweli hospitali hio ina floor mbili ambazo zote hutumika kama idara ya magonjwa ya akili lakini floor ya sita ni yale magonjwa ya akili ambayo ni very comnon yaani yanayoeleweka na floor namba sita ni ya magonjwa ya akili ambayo ni special zaidi.
Unaweza ukashangaa mgawanyo huu lakini ukweli ni kwamba zama za miaka ilipita na zama za wakati huo zilikuwa zimebadilika sana tena sana , ni miaka ya hivi karibuni kulibuka wimbi la magonywa ya akili ya kipekee ambayo yamekuwa ni magumu sana kueleweka wa wataaluma na mpaka wakati huo chanzo cha magonjwa hayo hakijafahamika bado na wanasayansi wanapambana kujua chanzo chake.
Hii yote inasemekana ni mara baada ya tukio la mwaka 2020 , tukio la mwaka 2020 halikuwa na athari moja tu bali lilikuwa ni tukio ambalo lilibeba athari nyingi na moja ambazo ya athari ambazo zinahusishwa ni kuibuka kwa magonjwa ya akili ambayo sio ya kawaida.
Sasa ukiona mtu ambaye sio mfanyakazi wa hospitali ya Mayaya anaingia floor namba saba basi jua ni mwasilika wa tukio la mwaka 2020.
“Miss Regina karibu sana”
Mwanaume mmoja mtanashati wa makamo alievalia koti la udaktari alisimama mara baada ya mango kufunguliwa na mrembo Reginai.
Kwa muonekano wa daktari huyo ilionekana Regina ukiachana na uzuri wake ambao sio wa kawaida lakini kuna sababu nyingine ambayo inambeba kwani daktari aliefahamika kwa jina la Shukuru alionyesha unyenyekevu mkubwa.
“Thanks , I can see that you’re still a little nervous around me , please relax , I am regular patient remember”Aliongea yule mwanamke akitoa tabasamu hafifu kidogo akimwambia yule daktari kuacha wasiwasi akiwa nae na atulie kwani yeye ni mgonjwa wa mara kwa mara.
“Bila shaka .. ni kwamba tu wewe ni mgonjwa wangu muhimu”Aliongea Dr Shukuru huku akikaa kwenye kiti chake”
“Najua lakini mimi ni kama wagonjwa wengine tu na isitoshe bado natakiwa kuonana na daktari wakati kwa wakati”
“Ni kweli kabisa Ms Regina , umuhimu wako katika jamii unanifanya niwe makini na kutotaka kufanya makosa”
“Oh.. nashukuru naamini utafanya vizuri , isitoshe wewe ndio daktari bingwa ninaekuamini na tatizo langu , ni miaka mingi sana tokea nianze kupata matibabu kutoka kwako, ni mwaka wa tatu huu unaingia kama sikosei”
“Upo sahihi na imekuwa heshima kwangu muda wote kukusaidia kwa kila namna kuweza kupona ..”Aliongea na kisha palepale aliwasha tarakishi yake na kuandika jina la Regina kutafuta taarifa zake.
Kwa haraka haraka ilionekana mrembo huyo anaefahamika kwa jina la Regina sio mara yake ya kwanza kufika ndani ya hospitali hio.
“Awamu hii umechukua muda mfupi sana tokea appointment ya mwisho , nilikutegemea mwezi ujao , vipi kuna mabadiliko yoyote?”Aliuliza Dokta na kumfanya Regina uso wake kidogo kukosa utulivu.
“Siwezi kusema kuna mabadiliko makubwa na leo nilitaka kuonana na wewe kwa ajili ya ushauri zaidi”
“Ushauri , unaweza kuendelea nipo tayari kukupatia ushauri wowote kama ni swala linalogusa shida yako maana ndio taaluma yangu”
“Dr kwa miezi kadhaa mpaka sasa familia yangu wanalazimisha niolewe na mwanaume ambaye wamemchagua , nilikataa pendekezo lao lakini wameenda mbali na kuanza kufanya vikao kushawishi Shareholders wa kampuni ili kunilazimisha , wanasema nisipokidhi vigezo basi natakuwa kuachia nafasi yangu kwenye kampuni kama CEO na mwenyekiti wa bodi”Aliongea na kumfanya Dr kuwaza kidogo.
“Nadhani nimekuelewa unachotaka kumaanisha .. lakini ili niwe more specific kwenye ushauri wangu , hebu elezea unachukuliaje swala hili?”
“Dokta ninachofuata ni ushauri wako wa kitabibu kuhusiana na ugonjwa wangu wa ukichaa…”
“Miss Reginai naomba nikurekebishe, wewe huna tatizo la ukichaa bali una shida ya ugonjwa wa DID, nadhani nimekuambia ili matibabu yako kufanya kazi vizuri lazima utambue ugonjwa wako kwa jina hilo na sio ukichaa”
“Nimezoea kwa muda kuiita ugonjwa wa ukichaa, tukiachana na hilo nadhani katika ushauri wako wa kitabibu ulisema ugonjwa wangu unaweza kumalizwa na mapenzi?”
“Ndio nilimaanisha kutokana na shida yako kuwa ya kisaikolojia zaidi itakuhitaji kuwa na high self willing ya kuchagua ni namna gani unataka kuishi na kuishinda nafsi yako nyingine na hili litawezekana ukiwa na msaada wa nje wa kisaikolojia , kama vile kushare hisia zinazofanana na mtu mwingine , hii ni moja wapi ya njia ambazo nilipendekeza lakini haikuwa lazima sana lakini kwa wagonjwa wengi ambao nimekutana nao njia hio imeonyesha mafanikio , njia ya pili ni kuzipatanisha nafsi zako zote mbili tofauti na kuzikataa na njia hii ili kuweza kufanikiwa nilikuelezea kwamba unatakiwa ujue chanzo cha kila nafsi na pengine kujua kumbukumbu za maisha ya nyuma ambazo umepoteza”Alielezea Dokta Shukuru kwa kirefu.
DID ni kifupi cha neno la Kingereza yaani Dissociative identity Disorder ni ugonjwa wa akili ambao ulikuwa ukifahamika kwa jina la Multiple personality disorder , ugonjwa ambao unamfanya mtu kuwa na Utu wa aina mbili au nafsi mbili ambapo humvaa mtu kwa nyakati tofauti tofauti na kudhibiti tabia.
Yaani kwa mfano unaweza ukajitambbua kama John na watu pia wakakutambua kama John na tabia zako lakini muda mwingine unabadilika na kuwa Ayubu na tabia zako zinakuwa ni kama Ayubu bila ya kufanana kabisa na John.
Huo ndio ugonjwa ambao mrembo Regina alikuwa nao , yaani anatawaliwa na ugonjwa wa akili ambao unamfanya kuwa na nafsi mbili zenye tabia tofauti tofauti.
Ni ugonjwa ambao huwapa changamoto sana madaktari kuutibu lakini unatibika kupitia njia za kiushauri zaidi.
“Kwahio kulingana na tatizo langu na mipango ya familia yangu , unanipa ushauri gani?”
“Njia ambayo ni rahisi zaidi ambayo tokea mwanzo nilisisitiza ni kuishirkisha familia yako juu ya tatizo uliokuwa nalo ,lakini sio wewe tu ambaye ulikataa juu ya hili lakini babu yako pia alikataa swala ambalo naelewa kulingana na haki za mgonjwa wangu, nasema hivi kwasababu pengine kama mama yako wa kambo anajua una tatizo la namna hii asingefanya maamuzi ya kutaka kukutafutia mume wa kuolewa nae kwani haitokusaidia kupona tatizo lako , nikizingatia msingi wa matibabu nikiri kwamba familia yako maamuzi ambayo imeamua ni hatari kwa maendeleo ya shida yako, lakini naelewa pengine ni kutokana na kutokuwa na uelewa, pia najua kwa upande wako unachukua tahadhari”
“Asante Dokta kwa kuwa muwazi , ukweli tokea nafike hapa nishafanya maamuzi na nilitaka kusikia maoni yako juu ya hili”
“Ndio nipo tayari kusikia maamuzi yako”
“Napanga kuajiri mwanaume yoyote aigize kuwa boyfriend wangu ili kuzuia mpango wa wazazi wangu zidi ya kampuni”Aliongea na kumfanya Dokta Shukuru kushangaa kidogo lakini alipotezea mshangao wake.
“Kuna haja ya kwenda mbali hivyo , Ms Regina najua unalichukulia tatizo lako kwa ukubwa lakini ni tatizo la kawaida na kwa muonekano wako na mafanikio yako sidhani kama kuna haja ya kuwa na mwanaume wa maigizo , wapo wanaume wengi ambao wanaweza kukupenda na wewe kuwapenda ni swala la kutoa nafasi tu”
“Dokta kwa maelezo yako unahisi ni rahisi kupata mtu kunipenda , ushasema kwa muonekano wangu na mafanikio hivyo sidhani kuna mwanaume ambaye anaweza kunipenda kwa dhati tofauti na kutanguliza nilichokuwa nacho , nimeona wakati nikiendelea kumtafauta huyo mwanaume nitakaempenda na ambaye atanipenda kwa dhati nitafute mbadala maana mapenzi pia ni swala la mchakato na kama hili swala likishindikana nitaenda na plan B kupatanisha nafsi zangu”
“Unafikiri unaweza kupata mwanaume ambaye anaweza kukubali kuajiriwa kuigiza kuwa mchumba?”
“Naamini nguvu ya pesa ndio itafanya kazi, itakuwa ni kama ajira tu na ni swala ambalo nataka kulifanya ili kujipatia muda nikiendelea kufuatlia namna ya kumaliza tatizo langu , huenda pengine ni kapata mwanaume ninaempenda na ikawa rahisi tatizo langu kumalizika”Aliongea na kumfanya Dokra Shukuru kuwaza kwa muda.
“Nadhani sio wazo baya kulingana na hali yako , umesema pengine unaweza kupata mwanaume unaempenda wakati ukiwa na mchumba wa maigizo , hoja yangu ni kwamba pengine mchumba wa maigizo akawa ndio mtu uliepangiwa kuwa nae na mkapendana hivyo nipo tayari pia kubeti , nilisha fikiria kwa kina nitakuja kufanya chochote kwa ajili ya kuhakikisha hali ya mgonjwa wangu inaisha , kwasasa tujaribu na hiki ulichoamua” Aliongea Dr Shukuru na kumfanya Regina kutoa tabasamu.
Ugonjwa wa DID ulikuwa mgumu kudili nao ndio maana inashauriwa na daktari kuwa flexible wakati wa kushughulika na mgonjwa na hicho ndio ambacho alikifanya Dr Shukuru.
Dr Shukuru Omari ni daktari mbobezi ambaye amepitia mafunzo makubwa ya kudili na wagonjwa wa akili na haikuwa mara yake ya kwanza kudili na mgonjwa mwenye nafsi mbili.
Comments