Mkataba wa Mpenzi  wa Kukodi.

“Kifungu cha kwanza  cha  mkataba wa kukodisha mpenzi ,Mhusika A ana haki ya  kumtafuta  mhusika B wakati wowote  ndani ya masaa 24, Mhusika B  ana wajibu  wa kuhakikisha simu yake muda wote ipo wazi , pili muhusika B ana wajibu wa kushirikiana kikamilifu na maombi yote ya Mhusika  A maadamu  maombi hayo hayavunji    sheria za nchi  au mkataba , tatu Mguso wowote  wa kimwili lazima  uruhusiwe na Mhusika A  kabla ya  kufanyika… nne ,,, tano …”

Ndani ya  chumba  cha kifahari  cha hoteli ya Dosam V alionekana  mwanamke mrembo  akiwa  amekaa kwenye sofa upande wa dirishani . alikuwa mrembo  mno  na siku hio mavazi yake yalizidi kumfanya kuwa mrembo zaidi.

Alikuwa amevalia mwenyewe  gauni  la light blue  huku akiwa  nywele zake amezirudisha nyuma  mara baada ya kutoa ile kofia ya Hat na mkononi alikuwa ameshikilia karatasi ya mkataba akimsomea Hamza.

Macho ya mwanamke huyo yalikuwa  mazuri  na angavu kama vile  ni maji ya vuli , nyusi zilizopindwa , kope zake ndefu  na midomo yake myekundu  na minene vilimfanya kuvutia zaidi ,bila kusahau  uumbwaji wa uso wake  ulioendana na haiba yake , alikuwa kama vile ni mchoro  wa sanaa uliotoka  kwa  mchoraji maridadi.

Hamza alikuwa ameketi mbele ya mwanamke huyo  mrembo akimwangalia  na kumsikiliza kwa umakini mkubwa.

Ki  ufupi umakini wake haukuwa kwenye mkataba bali ulikuwa kwenye uzuri wa huyo mwanamke , kwake ni kama vile yupo ndotoni.

Kusomewa mkataba huo ilikuwa ikimaanisha  alikuwa amepita kwenye usaili na sasa alikuwa akipewa mashari ya kuanza kazi.

Ukweli ni kwamba huyo mwanamke  baada ya kumwangalia Hamza  kwa sekunde kadhaa  alionekana kuridhika nae  na alienda moja kwa moja kwenye mkataba.

Upande wa Hamza kwa namna ambavyo alikuwa akitingisha kichwa kila mara baada ya mwanamke huyo alipokuwa akisoma  ni kama vile  aliogopa mwanamke huyo angebadilisha mawazo na  kushindwa kusaini mkataba wa kazi.

Alijiambia ni kheri hata kuigiza kuwa  mpezi tu  wa kukodi  na hio yenyewe ingetosha kumletea heshima.

“Sahihi ya mkataba  kipengele A , Regina Wilson Dosam., kipengele B Hamza Mzee..  ni muda wa kusaini…”Aliongea mwanadada mrembo  ambae anafahamika kwa jina la Regina  na kuweka mkataba ule juu ya meza kwa ajili ya kusaini mara baada ya  kusoma vipengele.

Regina alijikuta akivuta pumzi ya ahueni  huku akimwangalia Hamza  ambaye ndio amekutana nae kwa mara ya kwanza siku hio na alionekana kuridhika nae.

Alikuwa na uhakika  kuhusu macho yake  kulingana na muonekano wa  Hamza  na  taarifa ambazo amempatia  alikuwa na uwezo wa  kuona kwamba alikuwa ni mtu  muamiifu na muwazi.

Zaidi ya yote mrembo Regina   aliona muonekano wa Hamza sio mbaya sana  , ijapokuwa mavazi yake  hayajamkaa vizuri  lakini kama atamvalisha na  kupata matunzo kidogo  atafanikisha kuwadanganya  watu  kuwa ni mpenzi wake halisi kumbe ni  feki.

Wasiwasi wake kwa muda huo ni ugonjwa wake  tu, lakini  kulingana na vipengele vya  mkataba huo aliamini  Hamza kila atakachokiona kwake kwa bahati mbaya  basi   itakuwa ni siri.

“The contract is roughly  like this , first  I’ll rent  it for three months, then  we‘ll see  how  it goes , do you  have any objections?”Aliongea kwa kingereza kitamu makusudi kabisa akitaka kumpima  Hamza uwezo wake wa kuongea kingereza.

Hamza alitoa tabasamu , kadri mrembo huyo anavyoongea ndio alivyokuwa  akipata hali  ya kujiamini na kumzoea na palepale alishika mkataba ule na kupitia kwa haraka haraka kabla ya kusaini.

“Miss Regina  , I have a few questions  that  I need to confirm first”Aliongea akimaanisha kwamba anayo maswali kadhaa ya kuuliza kujihakikishia  kwanza.

“Unaweza kuuliza?”

“Vipi kama  itatokea  nipo  kwenye kipindi  na  siwezi kuja  kwako mara   baada ya kunipigia simu  na  nikapoteza muda?”

“Upo makini , inaonekana  pia  ni mwanafunzi  mtiifu”

“Nishatoa ada hivyo nataka  kuitumia vizuri”Aliongea  na kumfanya Regina  kuonyesha ishara ya kuridhika, hakujali kuhusu  Hamza bado  kuendelea na masomo , alichojali   alionekana kuwa siriasi, na yeye alikuwa akitafuta mtu siriasi.

“Usijali  siwezi kukusumbua wakati wa masomo  yako , utanipa ratiba ya vipindi na kama kuna dharula  utaniambia”

“Hapo  vizuri , naona  na wewe pia ni mtu muwajibikaji” Aliongea huku akiwa  na tabasamu  na  muda uleule  simu yake ilianza kuita  na kujikuta akilaani kimoyo moyo , Regina s alimpa ishara ya kuipokea   na  Hamza mara baada ya kuangalia jina la mtu anaepiga ni  Iryn.

“Huyu ni mwanafunzi wangu namfundisha masomo ya  jioni  twisheni , yupo form six anapiga  maana jioni ya leo  nina kipindi nae”aliongea Hamza.

“Hakuna shida unaweza kupokea na kumsikiliza sina haraka” Aliongea Regina  na palepale Hamza alipokea.

“Ticha  nadhani hujasahau leo   tuna kipindi?”

“Najua lakini  si niliwasiliana na mama yako na kumwambia  tutaanza wiki ijayo?, kwasasa nina kazi nyingine hivyo nitakuwa   bize   tutaanza wiki  inayokuja kulingana na nilivyokubaliana na mzazi  wako”

“Oh! , Mama hajaniambia kuhusu hili”Sauti nzuri ya kike ilisikika.

“Unaweza kumuuliza tu “

“Basi sawa nadhani  tutaonana wiki  ijayo”Aliongea  huyo mwanamke na palepale simu ilikatwa na kwa sauti ya  Iryn alijua tu lazima amekasirika.

Ukweli ni kwamba  Hamza katika kujitafutia kipato  alikuwa akifanya kazi za aina mbalimbali ,miezi kadhaa iliopita  wakati akifanya kazi  ya kibarua chini ya  kampuni ya mazingira  ya Tata  ndio aliweza kukutana na  Mama Iryn  nyumbani kwake kwa mara ya kwanza na hapo ndio mwanamama huyo alimfahamu Hamza ni mwanachuo kutoka  FEMU ,

Sasa katika kuongea ndio mama huyo alisema ana binti yake kutoka shule ya  sekondari ya Alpha na anachukua masomo ya EGM na  alimuomba kama  ingewezekana kwa Hamza  kumfundisha  twisheni  kwa malipo na Hamza alikuwa na uhitaji wa pesa hivyo hakukataa.

Tatizo  lilianza mara baada ya kufanya vipindi kadhaa na Iryn  alianza kumtega  Hamza na kumtaka kimapenzi,, Hamza alikuwa hana mwanamke ndio lakini hakuwa tayari kutoka na mwanafunzi na hio yote ni kutokana    na mama yake Iryn kuweka imani kubwa kwake  hivyo kutokana na dalili hizo Hamza alikuwa akimkwepa Iryn kiaina.

Ki ufupi Hamza ni mtu wa  harakati  na aliishi   kwa kuchakalika , hakuchagua kazi ili mradi ilikuwa na pesa, lakini   kwa Iryn ilikuwa ngumu  licha  ya kazi hio ilikuwa na malipo mazuri  kutokana na mama yake Iryn kutokea kumpenda Hamza.

Kitu kingine sio kwamba Hamza  alishindwa kumuonya lakini ukweli ni kwamba  Iryn alikuwa binti mrembo  sana ambaye kwa mwanaume rijali  yoyote yule ni rahisi kuingia kwenye mtego wake  ndio maana alikuwa akiona ugumu.

“Samahani Miss Regina  kwa kukuchelewesha  wakati naongea na simu”Aliijibu Hamza.

“Hakuna shida , kama huna pingamizi lolote unaweza kusaini  mkataba”Aliongea.

Ijapokuwa sauti yake ilikuwa ya kirafiki lakini  alionekana kuwa kauzu mno na hata Hamza mwenyewe alijiambia hajawahi kuona mwanamke Kauzu kama huyo halafu mrembo , lakini alichopenda ni kwamba hakuona  aina yoyote ya Dharau,

Hamza alitia sahihi yake kama vile  ana saini mkataba wa   mabilioni kwa niaba ya nchi , sahihi yake ilikuwa  nzuri mno na kumfanya hata Regina  kushangaa kidogo,  ilionekana  Hamza alikuwa na mwandiko mzuri  sana kwa kuangalia sahihi yake tu.

Baada ya  kutia sahihi yake na Reginai kutia sahihi yake  palepale alifungua mkoba wake na kutoa bahasha na kumpatia.

“Haya ni malipo ya utangulizi kama mkataba unavyosema ni milioni tano ,  unaweza kuhesabu kujihakikishia, lakini  hela zipo katika mfumo wa dollar hivyo  utazibadili”Aliongea na  Hamza alipokea ile bahasha .

“Haina haja ya kuhesabu  uzito wa bill ya  dollar mia ni sawa na  gramu 1.51 na humu ndani kuna dollar elfu mbili hivyo uzito wake ni sawa na  gramu 30.2, hivyo  kwa kuzingatia uzito huu  basi   hesabu zipo sawa”

Reginai macho yake  mazuri yalichanua , hakuamini kama mtu anaweza kuhesabu  hela kwa kuzingatia uzito  wake tu ,  moja kwa moja  ilimwambia mtu ambaye  yupo  mbele yake  anapenda sana hela na hilo lilimuongezea pointi.

Upande wa Hamza  alifanya makusudi tokea jana yake alikuwa akipanga namna ya kukubalika  na kushinda usaili  na alikuwa na mbinu nyingi lakini hata hivyo mbinu zake hakuwa ameziandaa na kutokana na kuamini kichwa chake kilivyo chepesi basi  angetunga hapo hapo.

Sasa mara baada ya kupewa kibunda alitaka kumhakikishia  Regina kwamba yeye  anajali sana  pesa  kuliko  kitu chochote kile.

Unajua bwana watu wanaopenda hela ni rahisi kuwakontrol na kuwaambia hiki na kile na wakatii kuliko watu ambao hawapendi sana hela  mara nyingi  wanakuwa sio watiifu  hio ni kanuni ambayo  Hamza aliizingatia.

Regina  aliona na hicho ni kigezo pia ambacho alikuwa akitafuta , alitaka pia mtu ambaye anakwenda kuigiza kama mpenzi wake awe anapenda pesa ili iwe  rahisi  kumuendesha.

Regina mara baada  ya kuzuia mshangao wake aliingiza mkono wake kwenye mkoba na kisha akaibuka na  bahasha  nyingine na kumpatia  Hamza.

“Katika hii nyaraka kuna taarifa ambazo zinahusiana kuhusu wewe na mimi namna ambavyo  tumekutana  na  tulivyoanza kuwa pamoja , nenda nayo na  ukaisome uilewe lakini hakikisha  hakuna mtu ambaye ataiona.”

Hamza hakuamini mwanamke huyo kuwa  profesheno kwenye kazi yake namna hio na alitoa tabasamu  na kuchukua ile bahasha.

“Nitaisoma kwa umakini  nikisharudi”

“Kesho asubuhi  saa nne kamili  tukutane Dosam Tower  kwenye parking B2, hakikisha  hauchelewi”Baada ya kuongea kauli hio alisimama akitaka kuondoka.

“Ms Regina    usiwe na wasiwasi , mimi najali sana muda”

“That is for the best”Aliongea  na  Hamza aliangalia  glasi ya juisi ambayo  ilikuwa mbele ya mwanamke huyo , alichukua ya kwake kwanza na kuinywa  na kisha akamwangalia.

“Ms Regina   bado  umebakisha  nusu ya juisi yako”

“Siitaki tena”Aliongea.

“Utakuwa ni  uharibifu sana kwa alieitengeneza”Aliongea Hamza na palepale aliinua ile glasi na kisha  akainywa yote  kwa mkupuo mmoja.

Mrembo Regina  alitaka kumzuia  lakini  aliona aibu kwa kitendo chake na  mawazo yake ya kijinga yalimwambia anachokifanya Hamza ni  kubusiana nae kwa njia isio  ya moja kwa moja.

Hamza na Regina walitoka pamoja na sasa  rasmi  Hamza alikuwa ni mpenzi feki wa  mrembo Regina  , Hamza ijapokuwa alikuwa hapo kwa kazi lakini alijiambia atahakikisha huyo mrembo anampenda mwenyewe.

Baada ya kutoka nje   ya mlango alimwambia  mlinzi wake  kwenda nyumbani na kuanzia hapo ataendesha gari yake mwenyewe   , mwanadada yule mlinzi alitaka kugoma lakini alikubali na aliishia kumwangalia bosi wake  na  Hamza wakitokomea kwenye lift akiwa katika hali ya wasiwasi.

Haikueleweka  Prisila alikuwa ameenda wapi na Hamza alitamani kumuona mara ya mwisho , kwake  ni kama alikuwa ameokota   embe kwenye mnazi.

Baada ya  kutoka kwenye lift  watu waliokuwa eneo la mapokezi walikuwa wakimwangalia  mrembo  Regina  kwa macho ya mshangao na matamanio  lakini  alionyesha kutojali  na moja kwa moja alitoka nje na kwenda  upande wa  magari yalipoegeshwa na kusogelea  gari moja ya kifaharai aina ya  Maserati  Gran Gabrio.

Uzuri wa lile gari ulimfanya Hamza kumwangalia kwa macho  yaliokuwa na  matamanio  ilikuwa ni  gari ambayo inaendana na muonekano wake,

“Hivi ulisema  upo mwaka wa ingapi chuo?”

“Nipo  mwaka wa tatu , kuna tatizo?”Aliuliza   Hamza kiwasiwasi.

“Hakuna”

Aliongea   na palepale kimadaha aliingia upande wa mbele  ya gari  na kuliwasha.

Regina alijihisi kujiamini  na kuona  sio mbaya mwanafunzi wa digrii ya uchumi  mwaka wa tatu anamfaa sana.

 

 

Previoua Next