Reader Settings

SEHEMU YA 08.

Hamza alihisi siku hio ni kama  vile muda wowote ataamka kutoka ndondoni , ndoto ambayo ilianzia tokea siku ambayo aliweza kusoma Tangazo la ajira ya  mchumba feki  katika mtandao wa JamiiForum mpaka siku hio ambayo ameweza kupata kazi hio.

Wakati anatoka  katika hoteli ya Dosam V alitamani kuonana na  mrembo  Prisca lakini kwa bahati mbaya hakumuona na  alijua pengine amekwisha kuondoka hivyo hakutaka hata kujisumbua kumtafuta   na kutoka zake katika hio hoteli na kuelekea nje.

Alikuja kwa  usafiri wa  mwendokasi hivyo kama ni kurudi nyumbani alipaswa kuondoka kwa mwendokasi.

Wakati akiwa  anapita eneo la  Posta ya Zamani akitembea huku kichwa chake kikiwa katika mawazo mbalimbali  alijikuta akisimama kwa muda na palepale ilionekan kuna wazo lilimuingia ,  wazo hilo lilimwambia huo sio wakati wa kurudi moja kwa moja geto kwake  bali anapaswa kutafuta mahali kukaa na kupunga upepo  na mahali alipoona panamfaa ni  maeneo  ya Kivukoni.

Ukweli ni kwamba wazo hilo lilimjia kutokana na kutaka kukaa chini na kuanza kutafakari mambo ya kimaajabu ambayo yamemtokea siku hio ndio maana.

Hamza maisha yake  yalikuwa  ni yenye maajabu tokea  alivyokuwa mdogo mpaka kufikia wakati huo  na  msururu wa maajabu huo ulionekana kutokukoma katika maisha yake.

Maisha  ni msururu wa  mshangao ,  mzuri na mbaya  na hatujui ni kipi  kipo  katika  dakika nne zinazofuatia  na hichi ndio kinafanya maisha  yawe  ni  yenye msisimko mkubwa   na muda ambao  maisha  yanapokutupia mshangao chukua  muda  wako kutathimini yale ambayo  hayakuwa  ndani  ya matarajo na hicho ndio ambacho aliona.

Hamza alitumia zaidi ya lisaa kufikiria kile ambacho kimetokea siku hio , licha ya kwamba alikuwa na mambo mengi ya kuwazia lakini  ambalo  limetokea siku hio alilipa kipaumbele.

Ukweli ni kwamba hakujua kitakacho kwenda kutokea kwanzia siku zitakazofuatia lakini aliamini chochote kile ambacho kitamtokea kitakuwa ni jambo lenye msisimko  mkubwa.

Alikuja kushitushwa na simu  yake ambayo ilianza kuita mfululizo na mara baada ya kuotoa  na kuangalia aliekuwa akimpigia  ni Mama mmoja  ambaye alishawahi kwenda kufanya kazi kwake kwa kutengeneza AC(Air Conditioner)  yake ilipoharibika na alishangaa mama huyo kumpigia lakini moja kwa moja alijua lazima atakuwa na kazi  hivyo alipokea kwa furaha zote.

Ijapokuwa alikuwa na pesa nyingi mfukoni   ambazo zingemtosha katika matumizi ya  takribani mwezi mmoja kabla ya kupokea mshahara wake wa kwanza  lakini bado hakutaka kudharau kazi ambazo zimemsukuma na kumfikisha leo  hio.

“Kijana habari yako?”

Sauti ya mwanamama mtu mzima iliweza kusikika upande wa pili ya  simu.

“Salama  mama  habari za masiku?”

“Ni  nzuri tu , bado unapatikana hapa Dar sik hizi?”

“Ndio  Mama  nipo”

“Oh! basi vizuri, kuna jirani yangu nae  kapatwa na shida kama  ileile  ya kwangu , je unaweza kufiika  kumsaidia kumtengenezea?”

“Mama mimi kama malipo  yapo  ninaweza kuja  hata muda huu?”

“Asante sana baba yangu , mimi nipo kazini  kwasasa lakini  yeye pia atakuwa ndio anatoka kazini  nitakupatia  namba yake uwasiliane nae ukifika”

“Sawa mama Asante kwa kuniunganisha  na hii kazi?”Aliongea Hamza na mara baada ya   simu kukatwa alitoa tabasamu na kuangalia saa yake na kuona ilikuwa imetimu saa tisa  hivi.

Ukweli muda huo alikuwa akijichukulia kama mwajiriwa  lakini  kwasababu  kwake pesa ilikuwa kipaumbele hakuona  haja ya kukataa kazi ,  hata hivyo licha ya kwamba chuoni alikuwa akisomea maswala ya uhumi  na  uhasibu lakini ukweli alikuwa akipendasana kazi ya ufundi , ni kama alikuwa na kipaji  hicho kwani kazi ambazo nyingi alikuwa akifanya zilikuwa  ni za  ufundi, kusoma uhasibu ilikuwa ni sehemu ya maagizo ya Mzee.

Shukrani kwa mtandao wa  The Job  uliweza kumuunganisha na  watu wengi ndani ya jiji la Dar es salaam ambao wana  shida   na maswala ya ufundi na ndio  katika mtandao huo ambapo aliweza kupata kazi kwa mama huyo.

Eneo  la kazi ilikuwa ni Kigamboni  na kwasababu alikuwa  kivukoni ilikuwa rahisi kusafiri kutoka hapo kuelekea huko  lakini alikuja kugundua kwamba hakuwa na vitu muhimu vya kumsaidia kutengeneza lakini  kutokana na kuwa na hela kidogo mfukoni aliona atapitia dukani na kununua vifaa.

Kazi  yenyewe ilikuwa ni kurekebisha  AC hivyo  licha ya kwamba mama huyo kamwambia tatizo lilikuwa kama la kwake matatizo ya AC hayafanani  hivyo kwanza alipaswa kuona tatizo na hapo ndio atajua namna ya kudili na tatizo.

Dakika chache Hamza alikuwa ashafika katika Apartment za Lotus , jambo moja ambalo  Hamza alipenda kwenye hizo Apartment  ni kwamba  zilikuwa zikikaa wanawake tupu tena wale ambao hawajaolewa.

Unaweza ukashangaa lakini inasemekeana ndio utaratibu uliowekwa na mmiliki wa Apartment hizo ambazo  asilimia kubwa ya  wanaoshi hapo ni wafanyakazi a kampuni ya Dosam Global.

Sio kwamba kampuni hio ilikuwa ikipendelea wanawake, hapana bali  ukweli ni kwamba  ilikuwa imejenga  majengo hayo kwa kulingana na  stutus,  yaani kama mwanamke ameolewa basi  haruhusiwi kukaa ndani ya Apartment hizo.

Ni sehemu maarufu sana ndani ya jiji la Dar es salaam kwa kuwa na warembo wa viwango , yaani hakuna pisi mbovu ambazo zilikuwa zikishi ndani ya jengo hilo na hio yote ni kutokana na aina  yao ya kazi , asilimia kubwa ya wafanyakazi wa Dosam wa kike aidha ni  wafanyakazi ndani ya hoteli, Shopping Mall,  Wahudumu wa ndege  na  Benki.

Yaani kwa  haraka sana ni kwamba kampuni ya Dosam inajihusisha na biashara za miamala(Dosam Bank ) , Usafiri wa Anga (Dosam Air) ,Mahoteli(Dosam hotels and hospitality) na maduka(Dosam Distributions&Department store).

Sasa aina ya  kampuni hizo  ni kwamba  zinahitaji  sana wafanyakazi  ambao wana mvuto wa kipekee kimuonekano iwe ni mwaname au mwanamke , kwa mfano  mhudumu wa Hoteli hawezi kuwa na  sura ngumu lazima awe na  sura ambayo akitabasamu mgeni palepale anavutik, bila shaka hicho sio kigezo pekee cha kuajiriwa ndani ya kampuni hio  kikubwa  ni ujuzi  na taaluma, moenekano ni sifa ya ziada tu.

Sasa  asilimia kubwa ya  wafanyakazi wa Dosam walikuwa  wakiishi katika Apartment  za kampuni kwa wale ambao hawana makazi ,sio sheria kuishi katika Apartment  hizo lakini  asilimia kubwa ya wafanyakazi walikuwa wakiishi katika Apartment hizo kutokana na kwamba  walikuwa wakilipia gharama nusu halafu mazingira ni Premium.

Yaani kama nyumba kwa mwezi ni  milioni moja basi  mfanyakazi hulipia  laki tano, huo ni mfano tu na sio  gharama  husika..

Sasa nyumba hizo  mara nyingi  ni kama  zimetengwa japo si sheria, kuna Apartment ambayo inachukua tu wanaume  ambao ni mabachela na kuna Apartment ambayo ilikuwa ikichukua wanawake ambao ni mabachela na  kuna nyingine ambayo ilikuwa ikipangisha   wale ambao  wameoa au kuolewa , yaani familia.

Sasa katika Apartment zote ambazo zinakaliwa na wafanyakazi wa kampuni ni hio ya   Lotus Flower Apartment,  hio Apartent ilikuwa  na warembo sio mchezo , ilikwa ikiendana na jina lake, wanaume wengi mabachela  walikuwa wakitembelea hapo kujaribu bahati zao.

Ukitaka kuthibitisha hilo ni  nje ya  eneo la apartment hio kulikuwa na Dustibin kubwa  ambayo ilikuwa  na  maua mengi sana pamoja na kadi , yote hayo  ni  wanaume ambao walikuwa wakitembelea mji huo  kwa ajili ya kujaribu bahati zao na pale ambapo wanakataliwa wanaishia kutupa maua yao pamoja na kadi zao kwenye  Dustibin hizo na kuondoka.

Hamza  alikuwa akisikia habari za  Apartment hii lakini ukweli ni kwamba siku ambayo alikuja kufanya kazi  ilikuwa ni muda wa mchana  muda wa kazi hivyo hakukutana na warembo wengi.

Ilikuwa ni muda ambao Hamza anakaribia kufika ndani ya  Aparttn hizo , mita kadhaa kabla ya lilipo geti aliweza kuona gari mbili zilikiwa zimesimama, moja ilikuwa ni gari aina ya Aud na  nyingine ilikuwa  ni  gari aina ya Noah.

Kwa macho yake ambayo  yanaona  mbali aliweza  kushuhudia mwanamke ambaye  alikuwa amezingirwa na wanaume  na ilionekana ni kama vile   wanaume wale walikuwa wakibishana  hivi na yule msichana kwa kumzonga zonga.

Hamza  jambo lile lilimtia shauku na kuongeza mwendo ili kujua kililichokuwa kikiendelea , ukweli ni kwamba hata kama  asingetaka kujua angejua tu kwani  watu hao walikuwa wamesimama njiani kuingia katika Apartment hizo.

“Eliza  nimechoshwa  na majibu yako  ya kis**nge , ninachotaka leo hii ni pesa zangu   na si vinginevyo”Mzee mmoja mwenye mwili ambao ulikuwa umetuna kidogo aliongea.

“Mzee Amosi  nilishakuambia nivumilie , hela unayonidai ni nyingi na sasa hivi sina uwezo wa kupata mkopo tena, unafikiri kiasi chote hicho nitatoa wapi , isitoshe hela ambazo nimekupatia  ni kiasi kikubwa  mno  kuliko hata ulichonikopesha,  unachonidai hapa ni riba”

“Sitaki maelezo yako  Eliza yashanichosha na kila siku unatoa kauli zinazofanana , hivyo leo  una chaguzi mbili aidha ukubaliane na sharti ambalo nakuambia kila siku  na tuondoke pamoja  urudi kesho au  unipate pesa yangu leo  hii, kama hela huna na  sharti langu hukubaliani nalo basi vijana niliokuja nao  watafanya kazi yao”Aliongea kwa kufoka.

Hamza ambaye ndio  sasa amekaribia karibu alikuwa akisikia   kila kitu na kwa haraka haraka aliweza kuelewa kinachoendelea, kwanza ilionekana watu hao walimkinga mwanadada huyo kupitisha gari  kuingia ndani   na ilionekana  walikuwa wakimdai pesa.

Kadri mzozo huo ulivyokuwa ukiongezeka  wanawake baadhi ambao walikuwa wakiishi ndani ya hilo eneo walikuwa wanajikusanya huku wakionyesha hofu ya kuamulia ule ugomvi , ni  kama walikuwa wakimjua huyo mzee ambaye anaonyesha yupo kifujo fujo hata kama anadai pesa yake.

“Mzee Amosi naomba usinifanyie hivyo , kwanini unakosa utu?”

“Haha,… leo ndio unasema sina utu , wakati nakupatia pesa yangu nani alimbembeleza mwenzake,  kama nisingekuwa na utu  nisingekupatia kiasi chote kile cha pesa , sasa mama yako amekwisha kupona lakini  unashindwa  kulipa pesa yangu , kingine  unasema unalipa riba   kwani makubaliano yetu yapoje  wakati unachukua mkopo?, hebu acha kupoteza muda , nimekupa njia nyepesi kabisa lakini unaleta maringo , kwani mimi ni mbaya sana mpaka ushindwe kutii sharti langu dogo namna hio?”

Hamza ambaye  mara baada ya kusikia kauli hio alijua kabisa hapo  huyo mwanaume  sio kama alikuwa na shida sana ya pesa au huyo mwanadada mrembo alikuwa ameshindwa kulipa ila ilionekana  analazimisha kulipwa pesa yake hapo hapo  akijua  huyo mwanadada   atashindwa kuitoa ili akubaliane na sharti  lingine ambalo kwa haraka haraka alijua ni ngono.

Hamza  alifikiria kidogo  mwanamke aliekuwa akizongwa alionekana kuwa mrembo  mno, lakini kwasababu watu walikuwa wakiongezeka kukusanyika ndani ya eneo hilo hakuona haja ya kuendelea kusimama kwani muda ulikuwa ukisogea kwa kasi hivyo palepale alitoa simu yake na kutafuta  namba ambayo alitumiwa  na kisha akaipiga.

Akiwa  amesogea pembeni ya barabara  aliweza kusikia simu ile ilikuwa ikiita  pasipo ya kupokelewa  na iliita mpaka ikakatika , akarudia kupiga na ikaita mpaka ikakatika mara baada ya kurudia mara ya nne akijiambia isipopokelewa anaondoka palepale simu ilipokelewa.

“Sikia Eliza  sitaki kukudhalilisha  na isitoshe  mimi na wewe tumetoka mbali , kama huna hela kwanini tusiwe wote wastaarabu,ongozana na mimi na kuondoka mbele ya macho haya ya watu?”

“Helloo..!!!”

Hamza alianza kuongea lakini  sauti ambayo ameweza kusikia ni ya mwanaume ambae anamdai  Eliza , palepale aligeuza sura yake na kuangalia upande wa  ugomvi unapoendelea na  alikuwa haoni vizuri  kutokana na kuzibiwa na watu na ilimfanya kusogea karibu zaidi.

“Boss amepokea simu..?”

“Kijana ambaye alikuwa  karibu na yule  mzee alieitwa Amosi aliongea  na kauli ile ilimfanya Amosi kumwangalia  Eliza  mkononni mwake na  palepale alimpokonya ile simu.

“Umetutegeshea simu sio , Eliza kwanini unaenda mbali hivi?”Aliongea huku hasira zikionekana zaidi na zaidi katika macho yake huku akiwa tayari ashakata ile simu.

 Upande wa Hamza mara baada ya  simu ile kukatwa palepale alijua mtu ambaye anapaswa kuja kumfanyia kazi ni huyo  mrembo ambaye anadhalilishwa na wadeni wake.

“Nakuuliza ulikuwa ukiongea na  nani?”Amosi alipatwa na mashaka na palepale alimshikilia mkono   na kummnya  Eliza kwenye gari.

“Puuh!!!”

Haikueleweka imekuwaje lakini Amosi alijikuta akidondoka  kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu  kama vile amevutwa.

Kitendo kile kilishangaza waliokuwa wakiangaliana na hapo hapo ndipo sasa waligundua  Amosi alikuwa amevutwa kurudi nyuma na kijana ambaye alikuwa amefika hapo muda huo.

Hata Eliza hakujua namna ambavyo  Amosi alitoka mbele yake  na alijikuta akiinua uso  wake  ambao  alikuwa amefumba macho kwa kile ambacho alitegemea kufanyiwa na hapo  ndipo  alipoweza kushuhudia sura ya kijana  ambaye amesimama mbele yake.

“Dogo  unakitafuta kifo sio?”Mzee  Amosi mara baada ya akili yake kufanya kazi  alionyesha kukasirika mno  kwa kile alichofanyiwa.

“Mzee hebu tuliza kwanza   jazba  najua una shida  na huyu  mwanadada lakini vilevile na mimi nina shida nae”Aliongea Hamza  kwa sauti iliojaa upole , ni kama alikuwa akitania hivi na kufanya watu kumshangaa  , hata Eliza mwenyewe alionekana kushangaa na kujiuliza huyo  kijana ni  nani kwanini anajiingiza kwenye mgogoro wake na kusababisha matatizo zaidi.

“Chongolo  mnashangaa nini , hebu  mshikisheni kwanza adabu ndio  tuongee nae vizuri na kumjua ni  nani”Aliongea Amosi kwa hasira , hakutaka kusikia  ngonjera za kijana huyo.

Chongolo mara baada ya akili yake kurudishwa kwenye   uhalisia  ni kama alishituka na palepale pamoja na wenzake wawili walimsogelea Hamza kwa  ajili  ya kumdhibiti.

“Mamaa…!!!”

Kijana mmoja ambae alikuwa kimbelembele mara baada ya kumsogelea Hamza alijikuta akipigwa teke la   kigoti  na kumfanya atoe  ukulele huku akichuchumaa chini  kutokana  na  maumivu.

Kitendo kile kilishangazwa wengi kwani kilitokea  kwa spidi ya hali ya juu sana kutoka kwa Hamza , ilikuwa ni kama vile  alikuwa na uzoefu wa hali ya juu  kwenye kudili na watu wa namna hio.

Wale wengine mara baada ya kuona  kiilichomtokea wenzao  ni kama hawakuaini amini kama shamblizi hilo lilitoka kwa  kijana wasiemjua na moja kwa moja  hasira zao ziliongezeka mara mbili na kusogelea  Hamza kwa kasi.

Puuh! , Bam!!!”

Chongolo  mara baada ya kumsogelea Hamza kwa ajili ya kurusha ngumi  mkono wake ulidakwa ukiwa hewani na kuvutwa mbele , wakati huo huo yule mwenzake aliekuwa nyuma akipigwa teke  la makagari   na kumfanya adondoke  kama furushi huku Chongolo  akisukumiziwa kwenye kiooo cha mbele cha  gari  ya Noah  kiasi cha kutengeneza  ufa.

“Sikutaka kwenda mbali  hivi  ila nachukia kupotezewa  muda, Mzee  unaonaje ukirudi siku  nyingine   kudai pesa yako, nahitaji kumalizana  na huyu mrembo   mapema  nirudi kwenye shughuli zangu  nyingine”Aliongea  Hamza huku akimwangalia Mzee  Amosi ambae alionekana kuwa katika kiwewe asiamini  vijana wake watatu  aliokuwa akiwaamini   kupambana na watu    ndani ya  dakika moja tu wamedhibitiwa  na wote wanaugulia maumivu.

Alimwangalia Hamza kwa macho yasiokuwa ya kawaida kama kwamba alikuwa akimtathimini.

Mzee Amosi alionekana  kutafakari  kwa muda , kwa jinsi alivyomuona Hamza akifanya mashambulizi  na  kupitia uzoefu wake wa  miaka mingi  kuna kitu alikiona haraka haraka  na hakutaka  kuendelea  kuuliza ni nani.

“Chongolo tuondokeni  tutarudi , Eliza   jiandae siku nitakayorudi sitokuwa na huruma  tena , ni kheri  upige simu mapema kabla ya kukutafuta”Aliongea Mzee yule huku  akimwangalia Eliza kwa macho makali  na kisha  alipangua watu na kuingia  ndani ya gari.

Hamza mara baada ya kuona  mzee huyo amekuwa mtiifu  kwake  alijikuta akivuta pumzi za  ahueni maana hakutaka kwenda mbali  sana.

Wakati akiona amefanya  jambo la kawaida upande wa watu waliokuwa ndani ya eneo hilo  walionekana kuwa katika mshangao, kila mtu alikuwa na lake kichwani  na kuna wale walioamini  huenda Hamza ni mwanajeshi  licha  ya kwamba muonekano wake haukuwa ukisanifu  kile alichokifanya.

Mrembo Eliza alikuwa ni kama haamini  alikuwa amesalimika na  aliemsaidia  ni kijana  aliekuwa mbele yake ambaye ndio mara yake ya kwanza kukutana nae, maswali kibao yalichipua katika  akili yake  lakini alishindwa kuuliza zaidi ya kumwangalia Hamza bila ya neno.

Hamza ni kama sasa alikuwa akimthaminisha  mrembo huyo ,  wakati anafanya maamuzi ya kumsaidia mwanamke huyo  hakufikiria   sana  kwa sababau aliamini akifukuza watu wale  kazi yake iliomleta hapo itaisha  haraka na kupata ujira wake , lakini  mara baada ya kukutanisha macho na msichana huyo aliekuwa katika  hali ya mshangao  ni kama  sasa alikuwa akipata wazo la pili.

“Kwanini ndani ya hizi  siku   chache  nimekuwa nikikutana na wanawake warembo  namna hii , hii ni ishara nzuri kwangu au mbaya?”Hamza alijiuliza swali hilo.

Alikumbuka  wakati alipokuwa katika Apartment  za Dosam Homes alikutana na mwanamke aliefahamika kwa jina la Tresha Noah, akaja kukutana na mrembo aliempelekea chungu ,  hatimae Prisca , Mrembo Regita  ambae ndio  alimshangaza zaidi   na hatimae  leo hio anakutana na msichana aliefahamika kwa jina la  Eliza.

Kama angewapangilia warembo hao   kulingana na uzuri wao   basi Regina angeshika namba moja , Prisca  namba mbili , huyo Eliza  namba tatu , Anitha  namba nne na kisha Tresha Noah  namba  tano.

Ukweli Tresha Noah alikuwa akifikiana uzuri na  huyo Eliza lakini  alikosa vigezo  katika macho ya Hamza mara baada ya  Amiri kumwambia uzuri wake ni wa kutengeneza.

“Kaka upo vizuri kwa kweli , ni mara ya kwanza kuona mtu mwenye uwezo wa kuwashinda  wale Vibaka ,Wewe ni mwanajeshi au polisi , Vipi Eliza ni mpenzi wako?”Kundi lile la wanawake waliokuwa wakiangalia  tukio hilo walimzunguka Hamza wakitaka kusikia neno kutoka kwake.

“Eliza  kumbe una mpenzi mwanajeshi  na husemi  jirani?”Aliongea wanamama mwingine  na kumfanya Eliza  kushangazwa na swali hilo na kuishia kumwangalia Hamza.

“Jamani mimi sina mahusiano na huyu dada , mimi ni fundi  na nimekuja kutengeneza AC , kama kuna yoyote mwenye shida inayohitaji fundi nipo  hapa natengeneza kila kitu”

Kauli ya Hamza iliwashangaza  wanawake waliokuwa wamemsikia , ila  kauli ile ni kama  haijamfurahisha  Eliza ni kama vile alitamani Hamza akubali na aseme  niwapenzi hata yeye mwenyewe alijishangaa kuwa na mawazo ya namna hio , pengine ni kutokana na kuwa single kwa muda mrefu..

“Handsome , upo siriasi unatengeneza kila kitu?, unaonaje ukatengeneza na moyo wangu ulioumizwa”Aliongea mrembo mmoja ambae alikuwa ametumia Make up nyingi mno huku akiwa na kikuku mguuni.

“Recho..!!!”Aliongea Eliza ambae ni kama vile ameamka sasa  kutoka kwenye mshangao  na kumsogelea Hamza.

“Kaka tunaweza kwenda  ukaanganlie shida ya Ac yangu”Aliongea  Eliza  na kwasababu alikuwa na aibu za kutosha kuendelea kukaa katika eneo hilo kwa yale yaliomsibu alimchukua Hamza na wakaingia ndani  huku wakimwacha mwanadada aliefahamika kwa jina la Recho akivuta mdomo.

Hamza  alikuwa kimya kimya na mwanamke huyo mpaka wanaingia kwenye lift,   ilikuwa ni kama vile amerudi kwenye upole wake.

Ukweli ni kwamba Hamza kimuonekano alikuwa mpole sana lakini matendo yake yalikuwa tofauti  na   yeye alivyo , haikueleweka ana historia gani ya maisha yake ya yuma lakini ni rahisi kuotea  maisha yake hayakuwa ya kawaida.

Eliza na yeye ilikuwa mara yake ya kwanza  kusaidiwa  na mwanaume , tena mbele ya wale waliokuwa wakimdai.

“Asante kaka kwa kunisaidia”Aliongea  Eliza kwa kukosa kujiamini na kumshitua  Hamza aliekuwa akijiwazia mambo ya ajabu na yote hayo ni kutokana na kumtamani mrembo huyo Eliza.

“Hii tabia ya kuwazia kile mwanamke  inatokana na kukosa  mchezo muda mrefu  nini?”Alijiwazia Hamza.

“Hakuna shida ya kunishukuru Eliza , kama nilivyosema  nimekusaidia ili kumaliza kazi yangu kwa haraka”Aliongea Hamza huku akijiona kidume na kauli ile ilimfanya  Eliza kumwangalia  Hamza kwa macho ya kidadisi, ni kama vile alikuwa amejawa na hamu ya kumjua vizuri Hamza.

Kwa mtu yoyote pengine siku hio  angevutiwa na Hamza  hususani kwa muonekao wake na kwa kile abacho amefanya dakika  chache zilizopita.

Hamza hakuwa amebadili mavazi yake  ambayo yalikuwa mapya na mtindo wa nywele ulikuwa umempendeza sasa ukijumlisha na ngozi yake  yenye mchanganyo wa  kizungu  ilimfanya kuwa mtanashati kupindukia na hakika mwanamke yoyote angempenda na kuvutiwa nae , siku hio hakuwa akionekana kama fundi kabisa , kwa kumlinganisha na mrembo Eliza moja kwa moja kwa tu asie na uelewa atasema  wawili hao ni wapenzi kwa namna wanavyoendana.

“Ding..!!!”

Lift  ilifunguka katika Ghorofa ya  kumi na tano ambayo ndio mwisho  kabisa , mazingira ya  Jengo hilo yalikuwa yakvutia mno , yamejaa ufahari wa macho , Ijapokuwa haikuwa kama apartment za Dosam Homes lakini   ni mazingira ambayo yanatosha kuhifadhi watu wa vipato vya  kati   na juu.

“Karibu kaka”

“Asante , unaweza kuniita Hamza”Aliongea Hamza huku akijitahidi kuonekana mpole mbele ya mwanamke huyo , ni kama alikuwa akijitahidi kumpangawisha Eliza.

“Oh karibu sana Hamza  fundi”Aliongea na kumfanya  Hamza kutabasamu, alitamani  aendelee kuisikia sauti  ya Eliza kwani ni kama ilikuwa ikibembeleza.

Kama  alivyotegemea  nyumba hio  ilikuwa  safi  mno na mpangilio wake ulikuwa ni  wa kiwango cha juu , kulingana na uzoefu wa Hamza  hata  apartment ya Mellisa  mwanamke wa Amiri haikuwa na mpangilio safi kama huo , ijapokuwa hakuona  chumbani kulivyo lakini eneo la sebuleni lilimpa picha.

Wazungu wanasema ‘A house  is a mirror to its owner’ hivyo mazingira ya  eneo hilo yalimpa picha kamili  Eliza ni mwanamke wa namna gani.

“Hamza sijui nikukaribishe  kwanza kinywaji au uanze kazi  moja kwa moja nikikuandalia chochote”Aliongea Eliza ambae alionekana kukosa  kujiamini  kwa namna flani hivi , pengine  ilikuwa ni kwasababu ya kile kilichomtokea dakika kadhaa ilizopita mpaka Hamza kuingilia kati.

“Kwa leo  naomba niende moja kwa moja kwenye ufundi , itakuwa vizuri   baada  ya ufundi kupata  hata juisi tu itatosha kutia baraka”Aliongea  Hamza  akijiamini .

*****

Upande mwingine ikiwa ni dakika kadhaa tokea kuondoka kwa  Amosi na kundi lake , ikiwa ni kilomita kadhaa  kutoka  eneo hilo  la Apartment walienda kusimamisha  gari  katika  moja ya mgahawa na kabla ya Amosi  kushuka aliwaangalia vijana wake waliokuwa  hawajiamini kwa kile kilichotokea na kisha akavuta pumzi.

“Chongolo nadhani unajua  hii  kazi  hainihusu mimi moja kwa  moja  bali  ni bosi, kama atasikie kile ambacho  kimetokea leo  hii nadhani kuna  swala lolote ambalo litatokea ,  nani anajua   anachokiwaza bosi sasa hivi?”Aliongea Amosi.

“Mkuu tunapaswa  kufanya nini?”

“Inamaana bado tu hamjaelewa  ninachomaanisha , mbona mnakuwa na vichwa  vidogo namna hii”Aliongea Amosi huku  akionyesha kukasirika , ni kama aliongea kauli tatanishi ili mradi  wasielewe ili tu awafokee kupunguza hasira zake.

“Sikieni  kuhusu Eliza hili swala  nitaongea na bosi mwenyewe , ninachotaka ni kumfatilia yule mpuuzi alievuruga  mipango yetu, kazi hii inaanza sasa hivi mtaondoka na gari”Aliongea Amosi  na palepale  akashuka  kwenye gari  na kisha akaingia  katika Mgahawa huo.

Hazikupita dakika kadhaa Chongolo na wenzake waliondosha  gari hio ya Noah na kutokomea upande waliotokea.

Amosi alitembea kiwasiwasi kuingia ndani ya Mgahawa   huo wa kisasa , kulikuwa na  watu wachache sana lakini  hao wachache walionyesha  ni  wale wenye uwezo mkubwa wa  kifedha.

“Unavyonifanyia sio vizuri , unajua kabisa nakupenda lakini  kwanini  leo unataka kukatisha mahusiano yetu , kwanini unanifanyia hivi  Chriss”

“Anitha unaenda mbali  na nadhani akili yako haifanyi  kazi vizuri , mimi na wewe nani alitaka mahusiano ,  ulinifuata mwenyewe ukitaka  niwe Boyfriend wako  kwa muda kuwaringishia wenzako  lakini  kwa huruma zangu tumefikisha  mwezi huu , unataka nini kutoka kwangu , leo ndio mwisho  maana nina mtu tayari ninaempenda , naomba uondoke  nina mazungumzo  muhimu  na Amosi”Aliongea  mwanaume mmoja   mtanashati sana aliekuwa amekaa kwenye Kona ya mgahawa huo huku  mbele yake akiwa ni msichana mrembo  ambae alionyesha hali ya kutaka kulia katika macho yake,

 

Kwa kauli mbili tu ambazo  Amosi aliweza kusikia alijua fika kile kinachoendelea , ila hakutaka  kuongea neno kwanza bosi wake amalizane na mlimbwende huyo.

Mwanamke  huyo aliefahamika kwa jina la Anitha alionekana kuwa na hasira mno na mwanaume  aliefahamika kwa jina la Chriss , kwa kile kilichokuwa kikionekana hapo ni kama msichana huyo anafosi penzi  kwa kijana  huyo.

“Anitha  nimesema naomba uondoke , mkataba wangu   na wewe umeisha leo hii”Alirudia Chriss kuongea na  msichana mrembo wa haja alimwangalia mwanaume huyo kwa macho yaliojaa hasira na kisha akasimama na kuchukua mkoba wake.

“Siku moja utakuja  kujua mimi ndio mtu ninaekupenda kwa dhati na sio pesa zako  Chriss  na  utakuwa umechelewa”Aliongea  na kisha palepale akageuka na kuondoka.

Amosi ambae alikuwa amesimama pembeni ya  meza hio aliishia kugeuza shingo kumtathimini  mwanamke ambae analilia penzi , na aliishia kuona wivu kwani msichana huyo alikuwa amebarikiwa kila kitu , alikuwa ni mrembo haswa kuliko  maelezo , pengine katika maisha yake na uzee huo hajawahi kuwa na mwanamke wa urembo huo , hata kuota kuwa na mwanamke wa namna hio hajawahi , sasa kijana aliekuwa mbele yake alikuwa na uwezo wa kuacha  mwanamke mrembo huyo ambae analilia penzi , aliona wivu  na kujiambia   katika maisha pengine sio pesa tu na muonekano pia  huvutia zaidi wanawake.

“Chriss  huyu  binti   ni mrembo sana , lakini kuna haja gani  ya kumuacha namna hii ni bora ungemdanganya  na kuendelea nae pale unapomhitaji”AliongeaAmosi huku akikaa kwenye kile kiti.

“Nina sababu za kuachana  nae  ambazo hata wewe ukizijua hutonilaumu”Aliongea  na kumfanya  Amosi kutabasamu..

“Wewe  na mzee wako mna   tabia  zinazofanana , tatizo  mnapenda  sana wanawake lakini kudumu nao hamuwezi”

“Haha .. Siwezi kufanana na  yule mzee mimi , ni muhuni kupindukia, sidhani kuna mwanamke mrembo ambae ashawahi kumvutia akashindwa kumpata”Aliongea Chriss na kumfanya Amosi kutabasamu  na kujiambia kwa wakati mmoja  Chriss hakuwa akimfahammu baba yake vizuri , sio kila mwanamke anaemtaka ashawahi kumpata, kwani ni mwaka wa pili huo  alikuwa akihaha kutaka kumuweka Eliza kwenye himaya yake lakini imeshindikana.

“Nimeitikia wito  bosi wangu ,  simu kama hizi  hunipa hamasa  kwani naamini kuna malipo”Aliongea Amosi huku akiweka tabasamu.

“Haha.. Amosi mimi napenda watu wanaopenda pesa kama wewe , ndio maana kila  inapokuja swala   linalohitaji juhudi  na uharaka wa utimilifu  jina lako hujitokeza”

“Hii ndio kazi inayoniweka mjini , ijapokuwa pesa ni kipaumbele  lakini  matokeo  mazuri nazingatia  sana , kuna wanaopenda pesa zaidi kiasi cha kutumbukia kwenye utapeli, matokeo ndio kila kitu baada ya malipo”

“Haha.. Ijapokuwa  unaniita bosi  lakini wewe ni mtu  mzima sana kwangu , si shaka kuwa na busara  na nidhamu katika kazi yako , anyway  tokea nikujue kupitia  baba  nimekuwa na shauku sana kuyajua maisha yako lakini   maswali hayo nitayaweka kapuni kwa leo  na niende moja kwa moja kwa kilichonifanya nikutafute”Aliongea  lakini kwa sauti yake ilimfanya Amosi kuona  hali ya kusita sita katika macho ya Chriss.

“Kuna mwanamke  nataka unisaidie kumtafuta”Hatimae Chriss aliongea  na kumfanya   Amosi kushangaa kidogo.

“Mwanamke!!!?”

“Ndio  mwanamke ,  kuhusu taarifa zake faili lake utaletewa kesho ofisini  kwako, Mzee Amosi  nimekuita tuongee swala hili  ili kuonyesha  ni kwa namna gani   ni swala muhimu,  hii inaweza kuwa kazi kubwa kuwahi kuipata  tokea kuanza kwako  kazi ya maswala ya kijasusi..”Alisita kidogo na kisha akaendelea kuongea.

“Kuna watu nyuma yangu juu ya hii kazi , mimi ni kama Freelancer , ijapokuwa sitowataja  ni wakina nani kwa ajili ya usalama wako na wangu lakini wapo tayari kulipa kiasi chochote cha pesa , cha msingi ni matokeo ya kuridhisha”Aliongea  na kwa  namna Amosi alivyokuwa akimuona Chriss  alihisi uzito wa kazi yenyewe   maana bwana huyo  mara nyingi  alionekana kutokuwa siriasi lakini kwa namna flani ni kama hofu ilianza kumvaa.

“Kwa  muonekano  inaonekana sio kazi ya kawaida  na  inahitaji  rasilimali za ki uwezeshaji?”

“Haha.. Amosi unaonekana kuwa na uelewa wa haraka ,  ndio maana Mzee anakuita jasusi nje ya mfumo,, kama ulivyosema  mimi ni kama Freelancer katika hii kazi hivyo nipo tayari kuwekeza kiasi cha pesa kwako kwa ajili ya uwezeshaji wa ukamilishaji  wa hii kazi, tutaanza na  milioni  mia moja”Aliongea Chriss.

“Milioni  mia moja!!?”Amosi alishangaa mno.

“Kama ni  milioni mia moja kama rasilimali uwezeshaji  inamaana…..”

“Ndio Amosi ,  kazi hii ni ya mabilioni ya pesa , wenye  uhitaji wa kukamilisha kazi hii wanataka ifanikiwe kwa haraka  na kwa ufanisi lakini wapo Desparate, ukubwa wa pesa unaendana na ukubwa wa kazi  yenyewe  hivyo usishangae”Aliongea Chirss na kumfanya  Amosi kumeza mate mengi.

“Nipo tayari  juu ya kazi hii”Aliongea Amosi bila ya kufikiria , ukweli  kilichomfanya kutoa jibu la haraka haraka sio ukubwa wa kiasi cha pesa bali ni  shauku juu ya kazi yenyewe , kama   anataka matokeo ya kazi hio anataka kutoa mapesa mengi kiasi hicho basi jambo hilo linaweza kumshangaza.

“Safi Amosi, unaonekana kuwa na shauku , hata mimi nilipokea kazi hii kutokana na shauku, nadhani tutazungumza  zaidi baada ya kupokea faili, kumbuka usiri  mkubwa unahitajika katika kazi hii  na  tahadhari zote zimechukuliwa, katika faili   kutaambatana na  fomu ya  makubalianao ya kufanya jambo hili kuwa siri”Aliongea  na Amosi alitingisha kichwa.

****

Dakika  chache mbele mara baada ya Hamza kuelezewa tatizo la  AC aliweza  kuijua shida yake  kabla hata hajafanya uchunguzi ,  ilionekana kulikuwa na  shida ya  kipima joto cha AC hivyo kufanya  Ac kushindwa kukadiria  kiwango flani cha  ubaridi  ndani ya nyumba hio.

Hamza hilo halikuwa tatizo kubwa kwake  na aliweza kurekebisha  haraka haraka na kumaliza lakini hakuishia hapo tu alijaribbu kuagalia na shida  nyingine  na aligundua kulikuwa na vumbi  jingi upande wa Evaporator Coill hivyo alijaribub kurekebisha, mpaka anakuja kumaliza kazi yake ni kama nusu saa imepita na alijihisi njaa.

Kilichomfanya kuhisi  njaa ni harufu ya chakula  iliokuwa ikisambaa ndani ya nyumba hio ikimaanisha mrembo Eliza alikuwa jikoni.

“Inaonekana huyu mwanamke amekamilika kila idara , sio kwa kunukiza huku”Alijiwazia Hamza huku  akijifuta vumbi kwenye mikono yake na Hangerchief , shati ambalo alikuwa amevaa lilikuwa limechafuka kutokana na kuparamia ukuta  wakati wakusafisha  Ac hio.

Inaweza  ikawa kazi nyepesi kwa Hamza kutokana na uzoefu lakini kwa mtu mwingine ingekuwa kazi ngumu mno , kwani kwanza ilimhitaji kuchungulia  upande wa nje wa jengo hilo , jambo ambalo lilikuwa likiogopesha kutokana na urefu wa jengo.

“Nishamaliza kazi yako , kulikuwa na shida ya setting tu  na nimerekebisha”Aliogea  Hamza  huku akimwangalia Eliza ambae alionekana kutokea upande wa jikoni kuja eneo la sebulenni, alikuwa amependeza kwa mavazi ya kinyumbani zaidi na kumfanya kuonekana wife material.

“Oh!, Asante kaka yangu , naona  pia namna ulivyochafuka”

“Yeah, wakati  mama ananipigia kuja nnilikuwa nimetoka mahali na kuona nisiende nyumbani moja kwa moja”

“Na maamuzi yako yemeishia kuniokoa siku ya  leo , nashindwa hata kuelezea  tukio  hili , linanifanya niwe na aibu mbele yako”Aliongea Eliza huku sauti yake ikionekana ni ya kusita sita na hakukutanisha macho   kumwangalia Hamza .

“Ni swala la kawaida  ambalo linaweza kumtokea yoyote , watu wa aina  ile hawana  mipaka  na  ni vizuri  kutojihusisha nao”

“Asante sana , Hamza sijui nakushukuru vipi  lakini naamini kile ulichokifanya ni kwa ajili ya kuninsaidia , kila mtu alikuwa akifurahia  kudhalilika kwangu, ni swala la kawaida kwa binadamu , nadhani dunia sio mbaya kama  nilivokuwa nikifiiria , umekuwa mtu wa kwanza kusimama upande wangu..”Aliongea  Eliza huku  hali yake ya kihisia ilionekana kubadilika mara moja jambo ambalo lilimshangaza  Hamza , ilikuwa ni kama ashasoma Eliza ni mwanamke ambae alikuwa amepitia changamoto  za kimaisha  na kutokana hali ile ya kubadilika alishindwa kujua ni hatua gani  achukue.

“Eh! , jamani naunguza..!!!”Aliongea Eliza akiwa kama ameshituka na kukimbilia jikoni na kumfanya Hamza atabasamu na kukaa kwenye sofa akimsubiria achukue pesa yake  na aondoke maana muda ulikuwa umeenda.

“Samahani  kwa kukuchelewesha mwaya ,  naandaa chakula cha kupeleka  hospitalini , muda naona umeenda , unaonaje ukipata kabisa chakula   cha usiku?”Aliongea Eliza huku akionekana kutokujiamini.

“Pole kwa kuuguza”

“Asante , nimeshapoa”Aliongea.

“Sasa mimi nisikucheleweshe , kwasababu kazi ilionileta ni ufundi  na nishaimaliza  ngoja nikuache  uendelee na ratiba zingine”

“Malipo yatakuwa kiasi gani?”

“Nipatie  elfu kumi tu inatosha “Aliongea Hamza , ijapokuwa mwanamke huyo alikuwa akimfanya amwambe nimetengeneza bure lakini aliona ni  udhaifu hivyo anapaswa kuchukua chake.

Eliza palepale aliingia chumbani na kutoka na noti mbili za elfu kumi  na kisha kumpatia  Hamza.

“Sidhani  ni sawa nikikuita fundi  au Hamza wewe  ni mwokozi wangu leo hii na  angalau nilipaswa kukupa chochote kuweka baraka zaidi ya hii  juisi,  hii ya ufundi na hii naomba utumie  kama nauli”

“Wewe unaweza kuniita fundi , namba yangu inayo ukiwa na tatizo unaweza kuniambia muda wowote nitafika”Aliongea Hamza  na kupokea ile hela , hakutaka kukataa malipo ya elfu ishirini , ijapokuwa alijua mwanamke huyo alikuwa na matatizo lakini  kama atakataa angeonekana kama  alikuwa na ajenda  zaidi  ya moja.

Baada ya  hela kama  kawaida alipewa  juisi na Korosho   lakini Hamza kutokana na haraka na kutomfanya mwanamke huyo kuwa na wasiwasi ,korosho aliweka kwenye koti  na juisi akainywa kama maji  na kisha akaaga na kuondoka.

*******

Saa  mbili kamili  za usiku ndani ya  mgahawa  wa Golden Fork mbezi Beach ilisimama gari  nzuri ya thamani aina ya BMW 14Oi   ya rangi ya blue metallic.

Ilikuwa gari nzuri kweli  iliofanya  watu baadhi waliokwa wamekaa   upande wa   madirisha yanayoangaliana na  maegesho kukaza macho  kwa mtu anaeshuka katika gari  hio.

Dakika  kama moja kupita aliweza kutoka  mtu katika gari hio ,ijapokuwa ilikuwa usiku na taa hazikuwa kali sana lakini ilitosha  kuwafanya watu kukaza macho zaidi, kwani mwanamke alietoka katika gari hio hakuwa wa kawaida,alikuwa mrembo haswa japo  kwa macho ya  Hamza  ambae ameshakutana na mrembo Regina angemuweka pengine nafasi  ya  tatu au ya pili mwanamke huyo.

Akiwa si mwenye kujali macho yanayomwangalia  alizipiga hatua kuingia ndani ya mgahawa huo huku waliokuwa wakimtathimini wakitaka kujua  yupo peke  yake au kuna mtu amefika hapo kwa ajili ya kukutana nae.

Mwanamke   huyo alievalia suruali ya rangi nyeupe na blazia ya rangi ya bluu alitembea kwa kuchezesha miguu yake na viatu vyake vya high heels mpaka  upande wa kulia  wa  mgahawa huo  huku  nyuma akiacha usumbufu wa marashi yake.

“Alex!, umefika muda mrefu sana?”Aliongea  yule mwanamke  baada ya kumfikia mwanaume aliekuwa ameketi  kwenye meza peke yake upande wa kulia  wa mgahawa huo ,sehemu ambayo ni kama imejitenga.

“Wakati na kutumia meseji ndio nilikuwa nikikaribia , ni kama dakika  ishirini zilizopita, kwanza sijategemea kama ungewahi maana najua wanawake  na tabia zenu”Aliongea Alex  kwa  namna flani hivi ya kukosa amani  kutokana na uzuri wa  mwanamke huyo.

“Wewe mwenyewe ndio ulitaka usumbufu wa kukutana , malipo yangeweza kufanyika kwa njia ya mtandao  kwanini unataka  Cash?”

“Nadhani ushajua sababu ya mimi kutaka Cash Frida , nataka kuongea na wewe maana kuna mambo mengi bado sijayaelewa , mimi ndio  ambae nilikuwa nikikuletea mzigo  na hakuna kosa  la aina yoyote limetokea , Frida kama ni  lile swala la kuzielezea hisia zangu kwako  naomba usahau , chukulia kama  halijatokea  na kazi iendelee”Aliongea Alex akiwa katika hali ya kulalamika hivi  mbele ya mwanamke huyo , kwa macho ya haraka ilikuwa ni sawa na kusema alikuwa akimpenda huyo mwanamke  lakini ilionekana  mwanamke alikuwa  amemkataa.

Mwanamke aliefahamika kwa jina la Frida alitoa tabasamu   huku akimwangalia  Hamza bila ya kujibu akimpa nafasi muhudumu kuweka juisi alioagiza  kisha aendelee kuongea.

“Tatizo lako Alex unakosa focus, wewe ni mfanyabiashara  lakini  unakuwa kama vile ni mwajiriwa”

“Unamaanisha nini kusema hivyo??”

“Namaanisha  utaendelea  kutii  kile ambacho ninahitaji kama mteja wako  na si vingineyvyo,kuhusu  sababu ulizoelezea  kwangu  huwa sizipi kipaummbele sana, wewe sio wa kwanza hata hivyo,anyway nimekuja hapa  kwa maswala mawili  tu, la kwanza ni kukupatia mzigo wako  na hii ni mara ya mwisho  sisi kuonana moja kwa moja , malipo yote yatafanyika kwa njia  za kawaida , pili  Alex acha kuuliza maswali mengi , wewe fanya biashara na kidhi mahitaji ya mteja wako , maswali mengi  huua uaminifu, Nadhani  kuna sheria  na vigezo umepatiwa na Binamu  mpaka kukidhi  kuendesha biashara zao”Aliongea Frida huku akinywa juisi ile kimapozi.

“Lazima  awe Hamza , Frida kuna ajenda gani, yeye ana nini mpaka ndio awe mwenye kukuletea mzigo?”

“Lazima  awe Hamza  ndio na si vingineyo ,  nadhani  unashindwa kuelewa nilichokuambia , hizi ni hela zako  natumaini   mahitaji yangu   katika mtazamo wa kibiashara yatashughulikiwa ipasavyo , Alex  nakuambia mara nyingine acha kuuliza  sana maswali , fanya biashara”Aliongea Frida na kisha alitoa  bahasha na kuiweka mezani  na kisha akamwinamia Alex na kumbusu shavuni la kwaheri ya kuoanana.

Busu lile  lilimfanya   Alex mwili wake wote kusisimka lakini kwa  Frida ilionekana ni  kitendo cha kuficha kile kilichokuwa kikiendele kati yao , ijapokuwa walikuwa wamejitenga lakini eneo hilo  lilikuwa wazi kufanya watu wawaone.

Alex aliishia  kumwangalia mrembo Frida akitokomea kwenye macho yake , hata ile hamu ya kuendelea kukaa hapo  ilikuwa imempotea , mwanamke huyo alikuwa akimvutia kimapenzi  mno.

Alex kama mfanyabiashara maarufu wa vyungu jijini Dar es salaam alikuwa akifanya biashara na wateja wengi ambao sio wa kutafuta bali ni wale wa oda , yaani ki ufupi ni kwamba biashara yake haikuwa ya kujitangaza kama zilivyo biashara nyingi , alikuwa kama mfanyabiashara ambae ameridhika  na wateja aliokuwa nao lakni ukweli ni kwamba sio kama kile kilichokuwa kikionekana , wateja wake alikuwa akiwatafuta kwa namna  za  upekee sana   na mathalani sio yeye ambae anawatafuta , wapo watu wa  kazi hio.

Sasa kati ya wateja ambao  anafanya nao kazi  ni  mwanamke mrembo , Frida , ijapokuwa mwanamke huyu hakuwa  mrembo sana kuliko wanawake wote aliokuwa akifanya nao biashara lakini  Frida ni aina  ya wanawake ambao  walianza kumvutia kingono  kwa mara ya kwanza tu kuonana nae ,  pengine ni ile tabia ya mwanamke huyo ya kizungu ndio iliomfanya kumvutia   kingono , mwanzoni ulikuwa ni mvuto wa kupenda kufanya nae ngono na  Alex aliamini kwa namna yoyote ile lazima mwanamke huyo angeingia  kwenye kumi na nane zake kama wanawake wengi ambao amepita nao ,  ‘hakuna mkate mgumu mbele ya chai’ ndio   falsafa yake ya siku zote kila anapomtongoza mwanamke , hivyo aliamini falsafa hio hio ingefanya kazi  kwa Frida lakini kinyume chake mwanamke huyo mlimbwende wa haja hakuwa na haraka  nae , ki ufupi licha ya kwamba alikuwa mwanamke wa kujiachia achia lakini alionekana  ni  wanawake ambao si rahisi kumvua  nguo moja tu ambayo mara nyingi  Alex ndio humkuta nayo kila alipokuwa akipeleka mzigo wa chungu.

Mara nyingi mwanamke huyo angemkuta akiwa na nguo   za kuogelea tu akipunga upepo  na kusitiri manyonyo na kitumbua  pekee huku akiacha kila kitu wazi ,  tabia ambayo ilizidi kumpagawisha mno  Alex , ule ugumu wa mwanamke huyo ulimfanya kuanza kutengeneza chembechembe za kihisia  na  hapo ndipo  ambao alipojihisi kupenda.

Kitu pekee ambacho kilianza kumchanganya Alex ni siku kadhaa  nyuma mara baada ya Frida kumwambia anahitaji  mwanaume aliefahamika kwa jina la Hamza Mzee kumletea mzigo  wake kila siku.

Alex alishangaa , ndio alishangaa kwani   Hamza alikuwa ni mtu wa kawaida mno  kufahamika kwa  Frida  na  hata  yeye aliona pengine   Frida anamaanisha Hamza mwingine , lakini kwa msisitizo  Frida alimwambia  ni Hamza huyo huyo anaemfikiria.

Japo swala hili lilimshangaza lakini lilimpa shauku na maswali mengi kichwani, akijiuliza inakuwaje Frida mwanamke mrembo anaemsumbua kumfahamu Hamza  na kwanini  anataka yeye ndio amletee delivery.

Kama kawaida  ya Frida alikuwa ni mtu wa kuongea mara moja na  atakachotaka   ni vitendo ndio  ambavyo alimpa  Alex namna ya kupinga  maamuzi yake.

Alex alikuwa na maswali , lakini biashara yake ilipaswa  kuendelea na  tokea amekabidhiwa biashara hio kulikuwa na misingi ya sheria  ambayo  alitakiwa kuifuata , kwanza hakupaswa kuwa na maswali mengi kwa wateja na anapaswa kuwasikiliza kwa chochote wanachohitaji na ikitokea amevunja kanuni hizo basi  ilitosha  kuhamishwa kikazi au kuachishwa kabisa.

Hivyo akiwa na  wasiwasi wake na shauku aliamua kutii takwa la mteja wake na kumfuata  Hamza kwa ajili ya kazi hio , bila shaka alikuwa na matumaini makubwa Hamza hawezi kukataa kazi ya donge nono hilo ,alijiambia   ni rahisi kumchimba Hamza zaidi kuliko  ilivyo kwa Frida ambae alionekana kama mwanamke msiri.

Dakika chache mara baada ya kupokea simu kutoka kwa Frida juu ya mzigo  kufika , huku mwanamke huyo akionyesha furaha yake  ya kuletewa na mzigo  na Hamza ilimfanya  Alex kutaka kumhoji  Frida ana kwa ana ndio maana akawekeana miadi nae kwa kisingizo kwamba anahitaji  pesa yake  cash, wazo zima ilikuwa ni kutaka kujua  au Frida alikuwa  na hisia za kimapenzi na  Hamza ,au Hamza alishawahi kufahamiana na Frida lakini kulingana na Hamza ilionekana ni kama wawili hao hawafahamiani kabisa.

Sasa anapata  nafasi ya kumhoji   Frida mrembo lakini  bado anashindwa kupata majibu anayotaka.

“Kuna kitu kinaendelea kuhusu  huyu  Frida , nina uhakika sio swala   la kimapenzi , Hamza  ni nani kwanini  mwanamke kama huyu mrembo mwenye pesa  anataka kuweka ukaribu na Hamza kupitia  delivery ya vyungu”Kichwa cha Alex kilicheza , alijua  lazima Frida alikuwa akilenga kujenga ukaribu na Hamza.

Zikiwa ni dakika chache baada ya Frida kutoa gari yake katika  mgahawa wa  Golden Fork  , akiwa anaendesha  katika barabara ya  Bagamoyo   uelekeo wa Jogoo, heads up display(HUD)  ya gari yake ilionyesha ujumbe  ambao ulikuwa kama vile ni  kodi.

“Board to Alamos!!

Ujumbe huo ulisomeka hivyo  na Frida bila ya  kubadili uelekeo alikanyaga pedeli zaidi akiongeza spidi.

Previoua Next