Reader Settings

SEHEMU YA 09.

Saa mbili za usiku Hamza alionekana  katika  pikipiki  ambayo ilienda kusimama  kando  kando ya barabara  ndani ya  Kijichi.

Hamza mara baada ya kushuka katika  bodaboda hio aliangaza kulia na kushoto  na kisha alianza kupiga hatua  kwa kuvuka barabara upande wa  pili  akiachana   na ile iliokuwa ikinyoosha moja kwa moja kuelekea uelekeo wa Vikunai kwenda Kibada.

Mtaa huo ulikuwa ndio  mtaa wa kifahari kwa  wilaya ya Temeke ndani ya jiji la Dar es salaam , kulikuwa na utulivu wa hali ya juu  na mazingira yake yalikuwa safi na hata  Hamza aliyapenda.

Baada ya kutembea umbali mfupi  alikuja  kukunja  kulia kwake na  kuingia  katika  moja ya mgahawa mkubwa uliokuwa ukipatikana  ndani ya eneo hilo , uliofahamika kwa jina la  Dina Tea House & Restaurant.

Ulikuwa ni mgahawa  wa kifahari mno  na wa kipekee ambao unapatikana ndani ya jiji la Dar e salaam , upekee wake ulitokana na kwamba ndio mgahawa pekee ambao umejipambanua kwa kuuza  vinywaji aina ya chai  pekee na chakula  cha aina zote ambacho kinaendana  na aina ya chai husika.

Kwa mfano chai   aina ya Kombucha  lazima iendane  na  chakula chake   na  aina hii ya huduma iliufanya mgahawa huo kuwa  maarufu kati ya watu matajiri..

Ndio ulikuwa ni mgahawa wa  kifahari kwani  unaambiwa kikombe kimoja cha chai kinaweza kuuzwa si chini ya thamani  za  shilingi elfu kumi za kitanzania na kuna zaidi ya hapo, kwa mfano chai ya Gisaeng kutoka Korea tu  ilikuwa ikiuzwa zaidi ya shilingi  laki moja.

Ndani ya maegesho  kulikuwa na magari mengi ya kifahari , hakukwa na gari la chini ya milioni  therathini ndani ya magahawa huo.

Hamza alishazoea  na alijua   aina ya wateja ambao  huhudumiwa na mgahawa huo  lakini siku hio  kidogo  magari yalikuwa mengi kuliko siku zote ambazo alikuwa amefika ndani ya eneo hilo.

Hamza alijiambia  pengine kutofika kwake hapo zaidi ya mwezi mmoja  kunamfanya kuona mabadiliko makubwa.

“Bro Hamza  leo  naona umefika , karibu sana  Madam  anakusubiria ndani”Aliongea kijana mmoja   huku akitoa tabasamu  akimkaribisha Hamza.

“Lau  nishakuambia mara nyingi haina haja ya kutoka kunipokea kama hivi”Aliongea Hamza akiwa na muonekano ambao haukuwa umebadilika sana.

“Bro unakuja mara chache sana   hili eneo , hivyo sidhani kama nitapata usumbufu wa kutoka mara kwa mara na kuja kukupokea kila ninapokuona”Aliongea na kumfanya  Hamza kuvuta  pumzi   nyingi na  kuzishusha.

“Naona hali ya hewa  siku hizi ni ya joto sana ndani ya hili  jiji , kazi zimekuwa nyingi kwangu na  kunifanya kuwa bize  ndio maana sikupata muda wa kufika kuwasalimia”

“Ndio ndio , nakujua wewe ni mtu ambae upo bize sana”.

“Naona baisikeli yangu hamjaitoa  bado ipo palepale”Aliongea Hamza huku  akishangaa kidogo na kutaka kucheka kwa wakati mmoja baada kati ya  usafiri wa hali ya chini uliokuwa ndani ya maegesho  hayo ilikuwa baiskeli yake ambayo mara ya mwisho alifika nayo hapo na  aliiacha kwasababu iliharibika mara ya mwisho.

“Nimeitoa  na kuirudisha , madam  alinipa kazi ya kuipeleka kwa fundi na imetengenezwa , si unaona sasa hivi inamuonekao mzuri”Aliongea  na kumfanya  Hamza kutingisha kichwa kidogo   kwa kukubali na kisha kuanza kuzipiga hatua kuelekea  mlango wa nyuma.

“Bro  naomba usitumie mlango wa nyuma , Madam akijua  hili  ataniletea shida”Aliongea  kwa kubembeleza   bwana aliefahamika kwa jina la Lawrence  au Lau  wengi wanavyomuita.

 “Hebu kwanza angalia nguo zangu namna zilivyochafuka , sidhani hao  mabosi waliopo  hapa ndani wataniangalia vizuri nikipita mlango wa mbele,  nashusha hadhi ya   huu mgahawa pia”

“Braza haina haja ya kuongea hivyo , Madam sio mtu wa namna hio , hawezi kujali na ititoshe  unadhani kuna yoyote  ndani ya hili eneo mwenye  kutosha  umuhimu wako kwa Madam?”

Hamza mara baada ya kuona Lau  yupo  ni mwenye kubembeleza sana aliona asikatae ukarimu huo hivyo aliamua kupita mlango wa mbele  na kwa bahati nzuri  katika Korido ya  mgahawa huo hakukuwa na watu wengi , staili ya mgahawa huo ilijengwa  kwa  namna ya  vyumba kama Kabini  tokea mwanzo , ijapokuwa kulikuwa na sehemu ambayo ni kama watu wote waliweza kukaa lakini kwa wale ambao walikuwa wakihitaji kufanya maongezi ya muhimu  walikuwa wakitumia vyumba hivyo kukutania , hii ni moja wapo ya faida ya mgahawa huo.,

Hamza alinyoosha mpaka  katika moja ya chumba cha mwisho kabisa binafsi ambacho  aliekuja kumsalimia ilikuwa ni kama ofisi yake na kisha alishika komeo  na kusukuma mlango.

Sekunde ambayo  mlango   alifungua  visu vitatu  vilirushwa kuelekea alipo  vikilenga eneo la moyo na tumbo kwa spidi ya mwanga.

“Damn!!”

Hamza alijikuta akimaka kwa mshangao lakini   wepesi wake  ulimfanya  kusogea pembeni  na  visu hivyo  vilipita  inchi chache sana kutoka kwenye mwili wake .

“Tuk ! , Tuk , tuk!!!”

Vile visu vitatu vilikuwa  vimefungwa na  vishada(Tassels)  vya rangi ya Violet , vilikuwa vyembamba mno  na vyenye makali kama viwembe  na viligonga katika ukuta na kudondoka chini.

Hamza mwanzoni  alidhani huo ndio mwisho lakini dakika ileile  ilitokea mianga kama  flash  aina tatu  na kumsogelea kwa kasi kubwa.

Lakini Hamza alionekana kuwa   mwepesi  na shambulizi hilo lingine na palepale  aliinua mkono wake  juu  na vile visu vyote vitatu vilinasa katiki ya vidole vyake, ilikuwa ni utaalamu wa hali ya juu mno.

“Dina , kuna haja ya  haya mambo , kwani lazima uone utumbo wangu ndio uridhike?”Aliongea Hamza huku akitoa kicheko.

“Nilitaka  kuona   kama uwezo wako umeusahau kama ulivyonisahau na mimi, miezi miwili inapita bila ya kunitembelea”Aliongea  mwanamke mrembo .

Alikuwa ni mrembo  haswa , akiwa amevalia  gauni  jeupe lenye maua maua ya rangi nyekundu  ambalo limefungwa na mkanda kiunoni na kuufanya mwili wake kugawanyika vizuri kati ya  kiuno na juu , alikuwa na sura ya kuchongoka kama  yai  na lips pana ambazo zimepakwa rangi  nyekundu.

Muonekano  wake ulikuwa sio wa kawaida   kabisa , pengine  licha ya kwamba   alikuwa akivutia sana lakini ni ngumu sana kwa mwanamke wa  kawaida  kuwa na mapozi ya aina hio.

“Sio muda mrefu sana tokea nifike ,  mimi naona ni  juzi tu”Aliongea Hamza huku akiokota vile visu vilivyokuwa vimedondoka chini na kuweka mezani.

“Miezi miwili  bado tu unasema sio muda mrefu ,  wanaume wengi wenye pesa zao na maarufu  hufika hapa kila siku kwa ajili ya kuniona mimi  Dina , kiasi cha kunifanya  kushindwa kutoka  lakini wewe  mkorofi  umekosa hata   nafasi moja katika mwezi kuja kunitembelea?”

“Distance makes the heart grow fonder , Kama tukionana kila siku   haitaleta raha  tena ,  kwangu mimi naona ni vizuri  zaidi kukuona mara moja   kwa uda mrefu , inannifanya nikuone kama malaika alieshushwa  kutokana na urembo wako”Aliongea Hamza.

Kwa namna ambavyo alikuwa akiongea ni kama vile amebadilika mbele ya mwanamke huyo , hakuwa na muonekano wa kipole bali  ulikuwa ni muonekano wa kicheshi uliojaa utu uzima.

“Eti  malaika alieshushwa , kwaho mimi ni mzuri sana mpaka  kuitwa malaika?”

“Nadhani unanijua vizuri mimi ni msema kweli “Aliongea  Hamza , lakini  ukweli ni kwamba katika moyo wake mwanamke ambae amekutana nae   muda  wa mchana hakuwa wa kawaida  kabisa ,  mrembo Regina kwake alikuwa mzuri zaidi ya Dina ,  faida kubwa ya Dina ni  mvuto  aliokuwa nao  kutokana na mapozi yake ya kike na mazoezi.

Upande wa mrembo huyo aliefahamika kwa jina la Dina , ambae hatujui wanafahamiana vipi na Hamza mpaka kuanza kurushiana visu alionyesha  tabasamu katika   uso  wake lililomfanya kuvutia zaidi na yote hayo ni ile raha ya kusifiwa kama mwanamke mzuri.

“Nimekusamehe siku ya leo ,  nina njaa  ya usiku ,  hebu kaa  na wewe ule , vyakula vyote unavyopenda vipo hapa”Aliongea.

Hamza  alikuwa na njaa mno na harufu ya chakula hicho tokea anaingia ilimfanya  njaa izidi kuuma , alisogea na kisha alivuta kiti na kukaa na  mara baada ya kufunua  chakula ambacho kilikuwa kimefunikwa  alijikuta akivuta pumzi nyingi.

“Unasemaje hiki ni chakula  ninachokipenda ilihali  siwezi kabisa kukilipia .. ugali wa hizi Abaloni za  ki’Australia   nadhani nikianza kula  nitatokwa na damu puani”Aliongea Hamza na kisha alisogelea bakuli ambao lilikuwa na pilau ndani yake na kisha alijisevia kwenye sahani  na akachukua na  nyama wa kukaanga  pamoja na mchuzi wa samaki na kuweka  kwenye sahani yake na kuanza kula chapu chapu , ndani ya dakika chache tu  asilimia sabini ya  pilau yote ilikuwa imeisha.

“Dina  dada yangu  mbona   umeacha kula?”Aliuliza Hamza  mara baada ya kuona  Dina hakuwa akifanya chochote zaidi ya kumwangalia  tu .

“Nishamaliza kula tayari  , pili   nnimeanza diet hivi karibuni,nakula  kidogo sana”

“Kuna haja  gani ya kufanya diet  ilihali  mwili wako  huo huo unakupendeza?”

“Wewe ni mwanaume na  huwezi kuelewa , ‘diet’  ni ‘life carear’ ya mwanamke , sitaki kuongeza uzito mimi .. kwanza hebu niambie, unapendelea mwanamke wa aina gani , mwembamba mwenye nyama  au mnene?”

“Napenda wale wanawake ambao  ni wembamba   na wana kalio lainiii ukiliminya”Aiongea  Hamza huku akitabasamu kifedhuli , alikuwa mtu mwingine kabisa kwa kile alichokuwa akikifanya.

“Wewe muhuni , yaani huna hata aibu nitakukata mimi?”Aliongea Dina  na palepale kutaka kumrushia tena  Hamza vile visu.

“Dina inatosha bwana , haina haja ya kutaka kunitumia kama   kifaa cha majaribio ya mbinu zako  za kininja””Aliongea na kumfanya  Dina kutulia.

“Hamza hebu niambie  kwanza  ukweli , unadhani nitachukua miaka mingapi  ya mazoezi mpaka kufanikiwa kukupiga na  mashambulizi yangu?”

“Miaka..!, hehe ,  labda arobaini au hamsini hivi”

“Kwanini usiseme tu maisha yangu yote”Aliongea  huku akiwa siriasi.

“Haha.,. haina haja ya kuwa siriasi hivyo , ukiachana na mbinu za mafunzo ya nishati za  mbingu na ardhi,  siku zote mtu anapaswa kuangalia  kipaji chake kwanza kabla ya  bidii,  ule msemo wa kusema Bidii hushinda kipaji ni uongo, ni msemo ambao watu hutumia kujifariji tu”Aliongea Hamza.

“Halafu Dina hii supu   ya kuku ina radha flani hivi, ni  kama kuna  chembe chembe za  vinyama nyama ,umeweka Sea Cucumber nini?”

“Oh! , kumbe umeona,  kuhusu   hilo  ni nyama ya kusaga ya  mkia  wa  Kangaruu , nimenunua bei sana na  ni kwa ajili yako   kukupa virutubisho”Aliongea Dina huku akiwa na tabasamu flani la kichokozi.

“Mkia wa Kangaruu!!!”

“Unaonaje? , imekuwaje kwanza ukagundua utofauti wa harufu maana  unasagwa na kuwa kama vumbi la nyama na kisha  huweka kama viungo kwenye supu na harufu yake hupotea kabisa, inafanyika hivyo ili iwe rahisi  kufanya kazi mwilini”Aliongea.

Mkia wa  Kangaruu ni sawa na  mtu anapotumia Viagra au Mkongo , mara nyingi hutumiwa sana  na matajiri  tena kwa siri kuwekwa kwenye vinywaji  kama Mvinyo  na baadhi ya  dawa za kuongeza hamu ya tendo.

“Dah , sasa kwanini ukanifanya ninywe  supu  yenye huu mchanganyiko ,unataka nitokwe na damu  puani?”Aliongea Hamza  mara baada ya kuhisi presha ya damu kuongezeka kwa kasi.

Unaambiwa  vumbi  la  vinyama vya  mkia wa Kangaruu  kidogo tu  inaweza kumfanya  mwanaume kupatwa na uchizi na ni  ngumu sana kuepuka  mtego wa mwanamke ukiwa  katika   athari ya dawa hio.,

“Unadhani kwanini nimefanya hivi?” Aliongea Dina na alisimama kutoka alipokuwa amekaa na kumsogelea Hamza na kisha alimwinamia shingoni na kufanya marashi yake   yaliochanganyika na pumzi kumsisimua Hamza shingoni.

Kutokana na Athari ya dawa  hio , mwanamke ambae alikuwa mbele yake  urembo wake ni kama umeongezeka mara kumi , lakini kwa uwezo wake wote alijizuia kutoruhusu akili  kumpotea na kumgusa kwa namna  yoyote ile.

Alikuwa akijua kabisa  kufanya mapenzi na Dina  kila kitu kisingekuwa sawa tena , tokea arudi nchini  Tanzania na kuanza chuo  huku akiishi maisha ya kawaida   ni kama  ilimfanya kupata amani  ambayo alikuwa akiiota hivyo hakutaka  hali hio kubadilika.

Dakika ileile muonekano wa Hamza ulianza kubadilika na chumba  kilizidi kuwa cha baridi huku msisimko ndani ya eneo hilo ukiwa  ni ule wa kuogofya,Hamza  alikuwa ni mtu mwingine kabisa  na hakuwa na ishara yoyote ya utani katika macho yake.

“Dina usiendelee..!”Aliongea Hamza kwa sauti iliokuwa   na mikwaruzo lakini kwa namna flani ya kuhamasisha.

Mabadiliko ya Hamza yalimfanya mwanamke huyo   kushikwa na hali ya uchungu mno kwenye macho yake  na  ishara  za hasira  lakini  dakika hio hio alibadilisha muonekano wake na tabasamu bandia  na kujiondoa kwake.

“Hebu muone  sasa uoga ulivyokushika ,  unadhani  mimi Dina  nataka kukumeza mpaka kunibadilikia hivyo , haya  sitaki tena hata kuchokozana na wewe mimi”Aliongea akijitahidi kurudisha  hali ya utani ili kuonoa  hali  hio isiokuwa ya kawaida katika uso wa Hamza.

“Tena umekuja wakati muafaka ,  nimepokea mzigo wangu wa majani ya chai  kutoka nje ambayo  nahitaji ujuzi wako kuyachunguza, nione kama sijapigwa  maana ni hela nyingi nimetumia”Aliongea.

Dakika hio Hamza hatimae alikuwa amerudi katika ule muonekano wake wa kizembe na kuangalia  chai ambayo ilikuwa ikimiminwa  kutoka kwenye jagi.

“Hakuna shaka ,  ni wakati wa  kufurahia  chai ya kimatawi ya  mrembo Dina  kwamara nyingine”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu , spidi  yao ya kubadilika haikuwa ya kawaida kabisa , pengine watu wa kawaida kwa kile kilichotokea dakika chache zilizopita   wasingerudi katika hali hio.

Dina kama bosi wa mgahawa huo  ambao  umaarufu wake ni kutokana na  kuhudumia aina mbalimbali ya ‘premium tea’ alikuwa makini sana kwa kila mzigo ambao anaagiza.

Dina upande wake alionekana kuwa siriasi na  hakutaka kuendelea kuongea matani  na alianza kuonyesha  umahili wake katika kufanya mchanganyiko wa viungo  vya chai  , pamoja na kuweka  majani flani  katika kikombe  na kuyaloanisha na maji ya moto. Na baada  ya hapo ndipo alipompatia  kikombe  Hamza ajaribu.

“Hii  ni chai   ya mmea wa  jamii ya Camellia Sinensis , ambayo  hutengeneza chai maarufu ya Hui , majani haya yamefika jana kutoka China, hebu jaribu kuonja  na uniambie ni gredi ya ngapi?”Aliongea Dina  kwa kirefu  wakati wa kumpatia  kikombe Hamza.

Hamza kabla ya kunywa kwanza aliangalia majani  hayo ,  yalikuwa majaini kama majani ambayo  hayajasagwa na ilishangaza  kwa  namna ambavyo yalionekana mabichi licha ya kusafirishwa umbali mrefu.

“Hili  jani limenyooka  na  ni zito , ukiangalia veini zake  kidogo  ni nyeusi kuliko jani , hii  ni jamii  moja ya majani ya Camellia  kama ulivyosema , mmea wa  chai ya kijani , unaofahamika kwa jina maarufu la kichina, Taipeng”

“Sio mbaya  hebu jaribu  radha yake kwanza”Aliongea na  Hamza alionja  pamoja   na kunusa harufu ya chai ile.

“Mh! , hii ni chai nzuri sana , radha yake  unaipata   baada ya kumeza , sio chungu hata kidogo”

“Hio ndio maana yake ,  la sivyo isingenigharimu  zaidi ya   kiasi cha shilingi laki moja kwa kilo tu , ninachouliza ni gredi ya ngapi?”Aliongea na kumfanya Hamza kunywa tena  na   alionekana ni kama alikuwa akiichezesha kwenye ulimi na kisha akameza.

“Harufu na ‘Aftertaste’ inatosha kusema  imeingia gredi namba tatu , lakini  kuhusu utamu usioisha haraka  naweza kusema   hii ni Grade A”Aliongea  Hamza.

“Kwa maneno yako ,  ni sahihi kusema kwamba Lawrence bado hana uelewa wa kutosha kuhusu  sayansi ya chai, licha ya kusoma food science”Aliongea.

“Uzoefu  unahitajika sana likija swala la chai  za tamaduni mbalimbali , ni rahisi kufanya makosa kwa mtu ambae   hajatembea sana na kuonja  kila aina ya chai”Aliongea Hamza.

“Unaonaje ukifanya kazi hapa ,  utapata faida ya sehemu ya kuishi  na chakula, lakini pia malipo mazuri,  kuliko  kule uswahilii unakoiishi”Aliongea.

“Ah! Hapana,  napenda aina ya maisha yangu bwana ,  yananitosheleza”Aliongea  Hamza  huku akijiambia wakati huo hakuhitaji kazi  nyingine kabisa ya uboifried wa maigizo inamtosha.

“Unaongea kama vile nitakuingilia kwenye mambo yako, nataka kukuona mara kwa mara ndio nia yangu”

Mara baada ya  mwanamke huyo kuongea kwa sauti hio ya  kubembeleza ilimfanya Hamza moyo wake kulainika  na  kwa  mvuto  wa huyo mwanamke alijiambia anapaswa kuondoka la sivyo  anaweza kushindwa kuvumilia.

“Dina  muda umeenda , ngoja niondoke”

“Mbona haraka , hivyo  kwanini usikae kidogo  tukipiga stori , inachosha sana  kukaa mwenyewe”

“Hahaha… kaa na Lawrence mpige  stori , kwaheri , haina haja ya kunisindikiza”Aliongea Hamza   na kisha alitoka.

“Mjinga sana wewe, mpuuzi sana wewe Hamza, unanuka, umeniona sivutii ndio maana unanikwepa kila siku?”Mrembo huyo alilaani  huku macho yake yakitawaliwa na upweke.

Upande wa Hamza mara baada ya kutoka nje ya mgahawa huo  alijikuta akipatwa na  ahueni kwa kupumua kwa nguvu ,  maana alikuwa akijitahidi kujizuia mno   na alikosa amani  kwa kuona kwamba ataishia kufanya kitu ambacho hakikuwa kwenye mpango wake , ukweli ni kwamba ijapokuwa alikuwa akimkwepa huyo mwanamke lakini  alifika hapo kutokana na kwamba alikuwa amemmisi.

“Bro vipi unaondoka na baiskeli yako?”Aliuliza  Lau.

“Nitaiacha usiku mkubwa huu nitaondoka na  pikipiki, ihifadhi vizuri”

“Sawa broo”

“Halafu hivi  unamjua  mtu mmoja anaefahamika kwa jina  la Amosi , mzee flani hivi  ambae ni kama mkopeshaji?”

“Unamzungumia Jasusi mstaafu , ni maarufu sana   katika maeneo haya  mpaka Kigamboni yote ,  yupo chini   ya tajiri Hamdu  mfadhili  mkuu  wa mgombea wa uraisi  kupitia chama tawala.. anajitapa sana kwa kuamini jeshi lote  la polisi lipo mikonoi  mwake , anaweza kufungwa leo kwa uhalifu na kesho asubuhi ashatoka … vipi  amekuletea tatizo lolote?, kwanini unamuulizia?, kama unataka nikamshikishe adabu  niambie , nitahakikisha asubuhi anaitwsa hayati”

“Ah! , sijamaanisha hivyo , huyo  bwana kuna  mwanamke anamdai  na anatumia deni kumtaka kingono , nataka  angalau apatiwe vitisho  ila usiende mbali”Aiongea Hamza.

“Nimekuelewa braza”Aliongea  na kisha  Hamza alimshika Lau Bega na kisha alizichapa raba kuelekea barabarani  kutafuta bajaji au boda  kwenda nyumbani , alitaka akakae chini kwanza asome karatasi ambayo alipewa na mrembo Regina kwa ajili ya  kujiandaa na ajira yake kuanzia siku  inayofuata.

“Madam !!”Aliita   Lau mara baada ya  kumuona bosi wake amesimama mlangoni akimwangalia  Hamza akitokomea.

“Alikuwa akikuambia nini?”

“Inaonekana  Braza Hamza amekosana na  Amosi , Jasusi mstaafu , vipi tumuue?”Aliuliza Lau huku akiwa na  muonekano tofauti na ambao alikuwa nao wakati wa kuongea na Hamza, alikuwa siriasi mno  kama vile ni ninja.

“Haina haja tutaamsha matatizo mengine  tu  , hakikisha mnampa  vitisho  na onyo , pia fuatilia umfahamu mwanamke ambae  Hamza  anajaribu kumlinda , nataka kuona picha yake”

“Sawa Madam ,  halafu  Zedi , Mbunge wa Ukonga  amepiga  simu ,anaulizia kama upo free kesho  kwa  ajili ya chakula cha usiku?”

“Mwambie siko free”Aliongea  Dina  kikauzu na Lau alitingisha kichwa na kutoka.

Previoua Next