SEHEMU YA 10.
Hamza mara baada ya kurudi katika chumba chake alichopangisha maeneo ya uswahilini Gongo la mboto alikimbilia bafuni kuoga , maana muda huo wapangaji wote walikuwa washalala na kumaliza kuoga hivyo alikuwa huru kutumia bafu na choo.
Mara baada ya kumaliza kuoga moja kwa moja alijitupa kwenye godoro lake huku akiangalia juu kwenye ceiling board akionekana kuwaza kitu lakini ni dakika ileile alikumbuka alikuwa na karatasi ya kusoma ili kufanya vizuri katika ajira yake mpya.
Lakini kabla ya hapo aliingia katika mtandao na kutafuta jina lake na ndani ya sekunde lilionekana.
“Regina Wilson, Eldest daughter of the prestigious Dosam family in Tanzania , CEO of Dosam Group , intelligent and talented enterprenuer , the most beutifull businesswoman of the year ….”
“Kwahio kumbe huyu ndio mrembo ambae ni CEO wa makampuni ya Dosam, naona hata hii picha ni kama sio yake”Aliongea mwenyewe Hamza wakati akipitia taarifa hizo.
Ukweli ni kwamba kampuni ya Dosam ilikuwa ni maarufu sana nchini , na umaarufu wake unatokana na Brand yake , kila mahali ilikuwa ipo sio kwenye usafiri wa anga, maduka na mahoteli , hata Hamza jana yake aliweza kupendeza kutoka katika moja ya duka la Dosam.
Sasa ilimshangaza mwanamke mrembo namna ile ndio ambae alikuwa akivuma sana kwa kuwa mrembo asietaka kujionyesha lakini ambae alikuwa na akili nyingi kiasi kwamba ameiwezesha kampuni ya Dosam kutambulika kimataifa.
Hamza aliishia kupitia nyaraka ambayo alikuwa amepewa na mrembo huyo na kuanza kuisoma kwa umakini lakini ndani ya dakika tano tu alikuwa tayari ashapitiwa na usingizi.
Siku iliofuata Hamza alionekana katika moja ya mgahawa ambao alipendelea kula na alijipatia chapati zake tatu , maharage pamoja na juisi na mara baada ya kumaliza alianza safari ya kuelekea kwenye ajira yake kwa mara ya kwanza.
Hakuwa na mavazi yale ya jana , jana aliyachafua na hakufua hivyo hakujisumbua kubadilisha , mavazi yake ambayo yamemkaa vizuri lakini yamechakaa ndio aliamua kuvaa.
Kwa kutumia mwendokasi aliweza kufanikiwa kufika kituo kilichokuwa kikipakana na jengo la Dosam Tower sehemu ambayo alikuwa na miadi na mrembo Regina.
Katika jengo hilo ukiachana na kuwa na makao makuu ya baadhi ya kampuni katika floor za chini lakini chini kulikuwa na maduka makubwa ya luxury brand kama vile Chanell , Luis Vuiton na zaidi, juu kabisa kulikuwa na migahawa ya kimataifa kama vile Italian Restaurant , French Restaurant na Chiniese , ni sehemu ambazo Hamza asingeweza kutia mguu.
Saa nne kamili juu ya alama simu ya Hamza iliita na aliekuwa akipiga ni Regina na mara baada ya kumsikia Hamza amefika tayari alijikuta akipata ahueni.
Katika maegesho ya magari B2 , Hamza hakuweza kuona ile gari ya Maserati ambayo mrembo Regina alitumia jana bali kulikuwa na gari aina ya Lexus SUV.
Kama bosi wa kampuni hio kubwa sio swala la kushangaa kubadilisha badilisha magari hivyo haikumfanya Hamza kushangaa.
Mara baada ya kukaribia gari ile , kioo cha mbele kilishushwa na mwanamke mrembo sana alievalia gauni lenye kola ya bluu alionekana , gauni lililoacha mikono yake milaini wazi, huku akizidi kupendeza kwa mkufu wa madini ya dhahabu uliokuwa shingoni kwake., muonekano wake ulikuwa ni wa kitulivu mno kuliko ule wa jana.
“Goodmorning Madam, wapi tunaelekea?”Alisalimia Hamza huku akiwa na muonekano wa kizembe lakini hata hivyo hakuacha kutoa tabasamu.
“Ingia kwenye gari kwanza”Aliongea.
“Oh! , sawa boss”
Mara baada ya Hamza kuingia, Regina alimchunguza kwa dakika kadhaa , huku akijiambia huyu jana alifika akiwa amependeza lakini leo anaonekana wa kawaida , kuizoea kazi kabla hata ya kuanza.
“Vua nguo zako”
Kauli ile ilimshitua Hamza na kumwangalia mwanamke huyo kama anamaanisha , lakini hakukuonekana na utani.
“Madam!, ijapokuwa urembo wako ni wa viwango vya juu na pia tuna mahusiano ya kikazi , siwezi kuwa mrahisi namna hio , naomba ufikirie mara mbili , siamini kama wewe ni mtu mwepesi hivyo pia”Aliongea Hamza.
“Unaongea ujinga gani?” Mwanamke huyo alionekana kukunja sura na kujiambia mbona anakuwa na mawazo ya aina hio , lakini hata hivyo hakujali na alipitisha mkono nyuma ya gari na kutoa mfuko na kumpatia Hamza.
“Ninachomaanisha ni wewe kubadilisha , ndani ya hili jengo huwezi kuingia ukiwa na hayo mavazi”
“Ah , sasa si ungeongea hivyo mapema , angalau nimepata ahueni …”Aliongea Hamza huku akijifanyisha kupumua kwa nguvu , alijua sasa ndio maana alikuwa amebadilisha gari na kuja na kubwa kumbe malengo ilikuwa ni kumpa nafasi ya kubadili mavazi yake.
“Unamaanisha nini kuongea hivyo?”Aliuliza Regina huku akionekana kukosa utulivu , hata kama kitu kitatokea ndani ya hilo gari yeye ndio ambae atapata zaidi hasara kuliko Hamza , maana alijua kama mwanamke mrembo hakuna wa kumkataa , lakini ajabu yake Hamza ndio anajiona atapata hasara.
“Hamna tu , nilikuwa natania, nitabadilisha”Aliongea Hamza huku akicheka.
Hamza sio kama hakuwa akielewa ni kwamba tu alikuwa akitafuta nafasi ya kumfanya bosi wake amzoee haraka ili asiwe na wasiwasi na maigizo yao yasigundulike , hivyo kuwa mcheshi kama hivyo ilikuwa ni mbinu ya kuweka sawa mazingira yake ya kazi.
Sasa cha ajabu Hamza alivua shati lake palepale na mara baada ya Regina kuona tukio hilo aligeuka haraka kuangalia pembeni huku wakati huo akipata hisia mbaya kwa kujiambia mbona ni kama huyu mwanaume sio muwazi kama ilivyokuwa jana kwenye usaili.
Yaani Hamza wa jana alikuwa mpole na muwazi na ndio kilichomvutia , lakini wa muda huo aliionekana kama muhini fani hivi.
Lakini hata hivyo asingeweza kubadilisha mawazo , kwani kama ni mkataba umekwisha kusaini na pili hata kama atafute mtu wa kufanya maigizo asingepata mtu mwenye muonekano kama wa Hamza , muonekano wa kitanashati , alipenda sana namna ambavyo Hamza alichanganya rangi na kuona ingefaa sana kufanya maigizo.
Ndani ya dakika chache tu Hamza aliweza kumaliza kubadili mavazi yake yote ikiwemo shati na suruali , alikuwa amevalia shati la brand ya Givenchy na suruali yake , Mkanda wa ngozi brand ya Mont Blanc ulioendana na viatu vya ngozi ya Brown brand ya Ferragamo.
Mavazi yote kuanzia viatu mpaka juu iligharimu zaidi ya milioni therathini na kwa jinsi alivyokuwa amependeza iliendana vyema na ule msemo wa kizungu wa ‘Clothes make the man’ maana ndani ya dakika chache tu Hamza alikuwa ni mtu mwingine kabisa.
“Looks fine”Aliongea Regina kwa kingereza huku akijivunia kwa namna anavyojua kuchagua.
Hamza aliweka nguo zake alizokuja nazo kwenye ule mfuko na kisha akatupia nyuma.
“Miss wapi tunaelekea sasa?”
“Kukutana na wazazi wangu”Aliongea kikawaida kabisa lakini kwa Hamza alibung’aa akiwa ni kama hajasikia vizuri.
“Aisee naona mambo yanaenda haraka haraka sana , vipi napaswa kubeba zawadi au kitu chochote , naona sio vizuri kwenda kukutana na wazazi wako mikono mitupu”
“Haina haja ,,, hata hivyo unakutana nao leo tu na haijalishi kama utakutana nao siku za mbeleni , ninachotaka ni wao kujua nimepata boyfriend basi”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kumuelewa.
“Halafu usiniite madam , unaweza kuniita kivingine”
“Kama ni hivyo unaonaje nikikuita , Babe Regi , au Darling Regina , Mrs Hamza, Sweatheart..”Aliongea Hamza huku akicheka.
“Hey! Inatosha”Alibweka huku mrembo huyo akizidi kuona Hamza jana alikuwa akijifanyisha muigizaji na sio kama alivyokuwa akimdhania.
“Huyu mtu huu ni ucheshi au ni kukosa aibu , mbona jana hakuwa hivi?”Aliwaza Regina.
“Niite Regina tu inatosha”Aliongea na kisha palepale akatoka nje ya gari na kuongoza njia kuzielekea lift.
Mara baada ya kuingia kwenye lift Hamza palepale alimshika mkono Regina.
“Unafanya nini?”
Regina alionekana kutetemeka ni kama vile amepigwa na shoti , alitaka kuvuta mkono wake lakini Hamza alionekana kuushika vizuri.
“Regi nipo kazini , unadhani tutaweza kuwadanganya wazazi wako kama tusipoonyesha vitendo”
“Sawa lakini , Mkataba unakutaka kuomba ruhusa kwanza”Aliongea huku akizidi kuwa kauzu.
“Kama ni hivyo unadhani ni sawa tukiachiana?”Swali hilo lilimfanya Regina kukosa neno , alijua fika kama kweli kusipokuwa na kitendo hata cha kushikana mikono mbele ya wazazi wake itaibua wasiwasi.
“Okey , tunaweza kushikana mikono lakini…”
“Haha… Regii unaona sasa … hii ni kama unavyoingia kwenye basi kwanza na baada ya hapo ndio unapewa tiketi ..”
“Nimekuambia uniite Regina , acha kufupisha”
“Oh sawa Regi”Aliongea Hamza na dakika ambayo mrembo huyo alitaka kuongea alikosa neno.
Ndani ya lift hio walikuwa wawili tu na kumfanya Hamza kuweza kunusa harufu nzuri ya marashi.
Katika kazi ambazo amefanya hio ni moja ya Ajira ambayo aliona ni nzuri na ya kuburudisha.
“Endelea kusogeza pua zako karibu , utashitukia ngumi”Aliongea Regina mara baada ya kuona Hamza ni kama anasogeza uso wake karibu zaidi na alikosa uvumilivu.
“Regi , haina haja ya kukasirika , hii ni kazi kama kazi zingine na ili ifanyike kitaalamu unapaswa kutoa ushirikiano , hivyo kukusogelea karibu ni sehemu ya kazi , wewe unaonaje?”Aliongea Hamza , ule muonekano wa kizembe hakuwa nao tena.
“Niseme kweli tu , jana nadhani sikuwa na umakini , sikuwaza kama utaweza kubadilika ndani ya muda mfupi na kuwa mwanaume mwenye aina hii ya tabia , nikutahadharishe tu usije ukaona una uwezo wa kufanya chochote ukisingizia kazi , leo sijaja tu na bodigadi wangu la sivyo ungejutia”Mara baada ya kauli Hamza alisogea mbali kidogo.
******
Jasusi mstaafu Amosi Masekela aliingia ofisini saa nne na nusu huku akionekana ni mwenye uchomvu mkubwa huku usoni akiwa na viashiria vya michubuko na kuvimba uso.
Kwa jinsi ambavyo alikuwa akijisikia asingeweza kufika ofisini kwa namna yoyote ile , ila ilimradhimu kufika kutokana na Chriss kumsisitizia kuwepo ofisini saa tano kamili wakati bahasha ikiletwa ofisini kwake , nguvu ya pesa na shauku ya kazi ambayo anakwenda kufanya ndio ilimpa hamasa ya kujitahidi kuamka.
Wakati anaingia vijana wake walikuwa tayari wapo ndani ya eneo la kazi na hata wao pia walishangaa kumuona bosi wao akiwa na michubuko pamoja na nundu usoni.
Amosi baada ya kupita mapokezi aliwapa ishara wale vijana kumfuata kwenye ofisi yake na kisha akapita.
Amosi Masekela alikuwa akifanya kazi kama mkopeshaji , alikuwa akikopesha watu kiasi flani cha pesa na kisha kurudisha kwa riba flani ndani ya muda anaokubaliana na wateja wake , ofisi yake ilikuwa ni kama benki isio rasmi lakini iliosajiliwa kufanya biashara hio.
Alikuwa na uwezo wa kukopesha mpaka bilioni moja ndani ya ofisi hio kwa masharti nafuu kabisa.
Lakini yote hayo yanawezekana kwa kuaminika kwamba alikuwa akifanya kazi chini ya bosi mwingine , yaani ofisi hio haikuwa ya kwake kabisa bali yeye ni kama msimamizi mkuu.
Sasa aina yake ya ukopeshaji kwasababu ilikuwa ikitofautiana na wakopeshaji wengine kwa mfano kuweka dhamana ya kitu fulani alijikuta akifanya kazi ya ziada kudai pesa kwa nguvu kwa wale ambao hawakuwa wakilipa ndio maana akaajili watu wa kumsaidia kazi hio na sasa ndio vijana kama Chongolo na wenzake.
Kabla ya Masekela kuanza kazi hio iliaminika alikuwa ni mwana kitengo ambae aliachana na kazi hio na kuamua kujitegemea ndio maana alivuma sana kwa jina la Jasusi mstaafu.
Sasa iwe kweli alikuwa ni mstaafu au kuna kilichotokea mpaka kuamka kwa uvumi huo lakini ukweli ambao upo ni kwamba Amosi alikuwa akiaminiwa na watu wazito wazito serikalini katika kazi ambazo zilihitaji akili ya utafiti na ujasusi zaidi na ndio kazi ambayo ilikuwa ikimlipa kwa kiasi kikubwa na angalau kuwa na maisha mazuri,vigogo wengi walikuwa wakimwita Hunting dog.
“Bosi nini kimetokea , kwanini una michubuko na nundu usoni , tuambie ni fala gani kakufanyia hivyo tutaenda kumshikisha adabu”Aliongea Chongolo.
“Bosi tupo tayari kwenda kupambana wewe tutajie jina , ni radhi tufe tukipambana kuliko bosi wetu kuumia”Aliongea mwingine.
“Bosii…”Kijana wa tatu wa kundi hilo alitaka kuongea lakini Amosi aliinua mkono kumzuia na kisha aliangalia saa ukutani.
“Kazi niliowapa jana mmeishia wapi Chongolo?”Aliuliza huku akiwa ameegeamia kiti chake lakini swali lake ni kama liliwafanya Chongolo kuanza kukosa kujiamini.
“Bosi yule mtu ni jini , sio wa kawaida mbele ya macho yetu alitoweka”Aliongea na kumfanya Amosi kukunja sura.
“Ndio maana mshaanza kuwa chawa asubuhi asubuhi , kumbe kazi hamkumfanya inavyostahili?”
“Bosi sio hivyo , alikaa sana ndani kwa yule demu lakini wakati wa kutoka tulimuona na tulianza kumfuatilia , wakati tunafika kwa Mzee Mashimo hatukuweza kumuona tena mbele yetu”Aliongea Chongolo.
“Alikuwa akitembea?”
“Ndio bosi , alikuwa akitembea na hiki ndio kilitufanya tuchanganyikiwe na kuona ni jini , anapotea vipi mbele yetu?”Aliongea Kihedu na kumfanya Amosi kutafakari.
“Endeleeni kumfatilia Eliza kwa siri kama kawaida , picha za kila siku zinahitajika juu ya kila kitu anachokifanya”
“Lakini bosi vipi kuhusu yule jamaa?”.
“Chongolo una akili kweli wewe , kama mtu amewapotea mbele yenu mtaanzia wapi kumtafuta , kama atakuwa na mahusiano na Eliza ndio namna nyepesi ya kumuona ,hakikisheni mnafanya hili kwa siri, hakikisheni hamjitokezi mbele ya Eliza , sitaki kilichonitokea jana kijirudie sawa?”
“Ah!, Nimekuelewa bosi , lakini unamaanisha nini kilichokutokea jana?”
“Kafanyeni kazi, muda wa kuongea na nyie umeisha”Aliongea na kisha palepale alitoa bahasha kwenye mfuko wa koti lake na kurushia mezani.
Chongolo alitabasamu na kisha kwa heshima aliinua bahasha ile na kisha akaaga na wenzake wakaondoka.
Hio ndio kazi ya vijana hao, hawakuwa waajiriwa wa Masekela Credit and Loans bali walikuwa na kazi moja tu kudili na watu ambao walikuwa wagumu kulipa pamoja na baadhi ya kazi chafu ambazo Amosi hakutaka kujihusisha yeye mwenyewe kama bosi, ki ufupi Amosi kwa namna nyingine unaweza kumchukulia kama Loan Shark.
Baada ya Vijana hao kutoka , alionekana kukosa utulivu mno na kila saa alikuwa akisubiria muda ufike ili kupokea bahasha alioahidiwa na Chriss.
“Bosi kuna mzigo umefika?”
“Ulete ofisini kwangu Bertha”
“Anasema anataka upokee mwenyewe na kutia saini”Aliongea mwanamke wa mapokezi kupitia simu ya meza.
Amosi mara baada ya kuambiwa hivyo hakutaka kuchelewa , kwa taratibi hizo alijua ni kile ambacho alikuwa akisubiria hivyo kwa haraka haraka aliienda mapekezi kupokea mzigo wake.
Aliekuwa ameleta mzigo huo alikuwa ni kijana mdogo wa miaka kama ishirini na nne hivi ambae ni mfanyakazi wa Swift Courier , kampuni ambayo ilikuwa chini ya Chriss.
“Bosi nimepewa maelekezo kukufikishia huu mzigo wewe mwenyewe na kuupokea, niwe radhi kama nimekusumbua”
“Unatii maagizo , haina haja ya kukakamaa hivyo”Aliongea Amosi huku akilazimisha tabasamu na kupokea mzigo ule na kisha akasaini.
“Chriss anaonekana kuwa makini mno , sio kwa ufungashaji huu”Aliwaza Amosi wakati akiondoka mapokezi akiwa na mzigo wake.
Mara baada ya kukaa kwenye kiti , ujumbe wa meseji uliingia na aliona ni kutoka kwa Chriss na kumfanya aufungue haraka.
“Napiga baada ya dakika kumi”Meseji iliingia na Amosi alielewa alichokuwa akimaanisha Chriss.
Mzigo uliofika ulikuwa ni Limu A4 na mara baada ya kuuweka mezani alitoa ile katarasi ya juu na kisha akaanza kuchangua karatasi moja baada ya nyingine na ile anafika katikati aliweza kukutana na karatasi ambayo imechapishwa.
Amosi alikuwa na shauku , usiri wa kazi hio ulimfanya kuzidi kujawa na shauku ya kutaka kujua ni kipi ambacho Chriss anahitaji kifanyiwe kazi ambacho kina malipo makubwa hivyo.
Kabla ya kusoma karatasi ile aliendelea kuangalia vitu vingine na aliweza kuona picha ya mwanamke mrembo , ijapokuwa picha hio ilionekana kuchakaa lakini bado mwanamke aliekuwa katika picha hio alikuwa akionekana vizuri.
Picha hio ilimfanya Amosi kuiangalia kwa muda mrefu , ni kama alikuwa akijaribu kukumbuka ni mahali gani aliweza kuiona lakini licha ya kusumbua akili yake hakuweza kukumbuka mara moja.
Alihamia kwenye ile karatasi na kuanza kusoma na sasa anafahamu mtu aliekuwa kwenye picha jina lake ni Naomi Lindsey mmarekani mweusi, mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili ambae alifariki dunia mwaka 1999 kwa mshituko wa Moyo wakati akiwa katika tamasha huko jijini Milani Italia.
Mwanzo mwa taarifa hio inamshangaza Amosi na kumfanya azidi kusoma mbele , lakini anajikuta akipagawa zaidi mara baada ya kugundua ambae yupo kwenye picha anafahamika kwa majina mawili , anafahamika kwa jina la Naomi Lindsey kutoka Marekani lakini vilevile anafahamika kwa jina la Rosemary Macha raia wa Tanzania.
Amosi kabla ya kuendelea kusoma anajiuliza inamaana Rosemary na Naomi ni watu wawili wanaofanana au ni mtu mmoja mwenye majina mawili tofauti.
Amosi aliendelea kusoma karatasi ile kwa umakini mkubwa ili kujua ni kipi ambacho anapaswa kufanya na anakuja kugundua kazi iliokuwa ikihitajika ni kuunganisha historia ya Rosemary Macha na Naomi Lindsey.
“Krii.. Krii..!!”
Simu yake iliita na kwa namna ambavyo alikuwa ameweka mwito wenye nguvu ni kama alikuwa na ugonjwa wa masikio , ila mwenyewe ukimuuliza kwanini mwito wa simu wa namna hio atakwambia mwito wa simu yake ni wa fursa na kwasababu hataki kukosa fursa anakaa kimachale.
“Jasusi nadhani umesoma bahasha?”
“Ndio lakini mbona kuna mkanganyiko wa hii kazi?”
“Ndio maana nimepiga simu Jasusi , siwezi kuweka wazi kwa kila kitu lakini kazi unayotakiwa kufanya ni kumtafuta huyo Mtanzania kwanza na baada ya hapo tafuta uhusiano na Mmarekani”
“Hii taarifa haina mwelekeo wowote , kama nitaanza kutafuta tanzania nzima itachukua muda , nahitaji angalu mwanga wa uelekeo kuanza kazi yangu”Aliongea Amosi.
“Jasusi kazi hio umepewa wewe kwasababu ndio mtu pekee ambae unajua pa kuanzia , ‘hebu angalia hio picha vizuri na vuta kumbukumbu’ hio ndio kauli ambayo nimeambiwa nikufikishie kama ilivyo”
“Kwahio kazi yangu ni kumtafuta tu huyu mwannamke?”Aliongea Amosi ambae kwa namna moja hata yeye mwenyewe ni kama alikuwa katika hali ya kujiuliza , kuna kitu kilikuwa kikimwambia kabisa picha hio alishawahi kuiona mahali kama sio mtu kabisa wa kwenye picha.
Lakini kwa wakati mmoja anashanga kuona kwamba waliompatia kazi Chriss ni kama pia wanamfahamu na yeye , hali ya shauku ilizidi kuongezeka.
“Jasusi najua una maswali mengi , mimi pia nina maswali mengi lakini kwasasa ninachojali ni pesa itakayopatikana juu ya kukamilika kwa kazi hio, Narudia ninachojali ni pesa, hivyo maswali uliokuwa nayo mimi sijauliza”Aliongea Chriss na kisha simu ikakatwa.
Amosi alifikiria kidogo akiwa amekaa kwenye meza na kisha aliinua ile picha kwa mara nyingine na kuiangalia.
“Huyu mwanamke kwenye picha nishawahi kumuona , lakini ni wapi na lini?”Aliendelea kujiuliza swali hilo na kuendelea kutafakari lakini kumbukumbu zake hazikumps bahati..
Dakika chache mbele Amosi alikata shauri , hakutaka tena kuendeea kukaa ofisini na alitoka isieleweke anaelekea wapi lakini kwa muonekano wake ni lazima hakuwa akielekea nyumbani, alikuwa na karatasi zile mkononi lakini zikiwa zimehifadhiwa katika bahasha ya kaki.
Comments