Reader Settings

SEHEMU YA 13.

Upande  mwingine  katika mtaa wa kitajiri wa Masaki ndani ya  moja ya kasri la kifahari  walionekana wanaume watatu wakiwa wamefura kwa hasira.

Wawili  kati  ya wanaume hao  walikuwa ni vijana na mmoja   alikuwa ni mzee wa makamo hivi.

“Alex mpango wako umeendaje , vijana wamefanikiwa?”Aliuliza mara baada ya Alex  kushusha simu chini  akionekana kumaliza maongezi.

“Wamepigwa wote mpaka wakazimia”Aliongea Alex kinyonge huku akikaa chini  kwenye sofa.

“Nini!!?”

“Chriss  sijui mpaka sasa nadili na mtu wa namna gani , lakini  huyu Hamza  ni mtu wa ajabu  kabisa, vijana  walioenda kufanya kazi ni wa kuaminika , lakini wanasema eti Hamza alifika na mwanamke na ndie aliewashambulia”Aliongea.

“Alex huna haja ya kunyongea hivyo ,  si umesema huyu  Hamza ni  mzembe mzembe ambae hana  mbele wala nyuma kwanini unamkuza , kufeli kwa  plan A haimaanishi Plan B imefeli pia”

“Mjomba sio kwamba  nanyongea  wala kumkuza , ila  kama sio wa kawaida kwanini mwanamke mrembo kama  Frida  anamuhitaji ,  anaonekana kabisa kutaka kumuweka karibu”

“Upo sahihi Alex , inaonekana huyo  kijana  sio wa kawaida  na haupaswi kumdharau , lakini   kutokuwa wa kawaida haimaanishi  umeshindwa vilevile , changa karata zako vizuri”

“Mjomba kwanini usiniunganishe  na  Chatu , wale ni wabobezi katika kazi   na hawana historia ya kushindwa”Chriss mara baada ya kusikia kauli ile  alimwangalia baba yake kwa umakini.

“Hawa  Chatu kwanzia sasa ni maadui zangu , wameniharibia  mpango wangu  na Eliza   na Amosi amekataa kabisa kufanya kazi ile tena”

“Baba unamzungumzia Eliza yupi?”Aiongea Chriss

“Kuna mrembo mmoja wa kampuni ya  Dosam , nilikuwa nikimfatilia  kwa muda mrefu sana, Chriss  nadhani unakummbuka  skendo ya Dokta Bensoni  wa Mayaya Clinic?”

“Unamaanisha ile ya kuomba rushwa ya ngono?”

“Naona unakumbuka vizuri , sasa mwanamke ambae  amemfukuzisha kazi Dokta Bensoni ni huyu mrembo Eliza , alikuwa na mama yake pale hospitalini aliekuwa akihitaji matibabu  , kutokana na  Eliza kukosa pesa za kulipia ndipo Dokta Bensoni  aliruhusu tabia yake kumvaa na kumuomba mrembo huyo  ngono, siku ambayo anadhalilishwa pale Serena  nilikuwepo na  ndio mara yangu ya kwanza kumuona huyu mrembo Eliza , namna alivyomkataa Dokta Bensoni licha ya shida  zake ilinifanya nimuone wa

kipekee  na kuanzia hapo nilitaka kumfanya awe mama yako mdogo”

“Haha.. Mzee kwahio  kitendo cha  Dokta Bensoni kukataliwa ukaona  huyo mwanamke anafaa kuwa mama yangu?”

“Bensoni   yule alikuwa rafiki yangu  wa kitambo  namjua nje ndani , wanawake wote ambao amepita nawajua , hawa wanawake  ni wa heshima zao  na amepita nao  kwa kutumia mbinu ya aina moja , lakini  kwa msichana masikini asie na kitu kama Eliza alimkataa , unadhani huyo ni mwanamke wa kawaida?”

“Mjomba naunga hoja , huyo Eliza sio mwanamke wa kawaida , lakini vipi  mpaka  sasa ukashindwa kumpata?”

“Mara baada ya  tukio lile  nikaona  nimsaidie kwa njia za siri na baada ya hapo ndio nimtokee, hivyo nikampa kazi hio  Amosi  na alifanya vizuri kwani alimkopesha kiasi cha pesa  ambacho alitumia kumtibu mama yake, kama kawaida yangu baada  ya hapo nikajitokeza  sasa kunadi sera zangu lakini  yule msichana hakutaka kunielewa  kabisa , nadhani kitendo cha kuonekana na Dokta Bensoni ndio  kilinitia nuksi , Chriss mama  yako mtarajiwa alinikataa  katakata na mbaya zaidi alilipa mkopo wote  na nusu riba , tukio lile lilinipandisha hasira  na nadhani unajua tabia yangu , sijawahi kukataliwa na mwanamke hivyo nilitaka kumnyanyasa kidogo kumshikisha adabu  ili  kuulegeza msimamo wake”

“Nadhani sasa naelewa kwanini Jasusi  amesema sikufahamu vizuri , nilijua hakuna mwanamke wa kukutataa , kumbe  umeshapigwa cha mbavu mzee , hahaha”Aliongea Chriss.

“Nyamaza mpuuzi wewe , unamcheka vipi mwanaume mwenzo kisa kakataliwa , hii ndio maana halisi ya  kukua , umri umeenda  ndio maana nimepata uzoefu mpya , tokea nipate hela hakuna mwanamke ambae ashawani kunikataa  na niliamini hivyo  lakini  Eliza alibadilisha mtazamo  wangu na hii imenifanya nimpende zaidi na zaidi”Aliongea lakini Chriss aliendelea kucheka.

“Kwahio Mjomba baada ya hapo nini kikaendelea?”

“Unajua wakati  namwambia Amosi ampe mkopo , nilikuwa na uhakika   asingeweza kulipa maana  ni kiasi kikubwa mno  na hakuwa na kazi  lakini  mipango yote ilivurugika mara baada ya Regina kuingilia kati”

“Regina! , Unamaanisha  mkurugenzi wa makampuni ya Dosam?”Aliuliza Chriss. “Ndio  huyo”

“Ilikuwaje akaingilia?”

“Sijajua , ila  kwa taarifa nilizopata   Regina ndio kalipa kiasi chote  na  kisha akamfanya  kuwa msaidizi wake na sekretari”

“Duh!,Mjomba  sijawahi kuwaza kwa pesa zako kuna mwanamke ambae  atakukataa ,  imani yako ilikuwa kama imani yangu , mara baada ya kukumbana na kizingiti kwa Frida nadhani najua unachojisikia”

“Mjomba umekuwa ndio maana , achana na Chriss , anadhanau sana , huu muonekano aliokuwa nao ambao unatokana na juhudi zangu  ndio unamfanya kupendwa na kila  mwanamke”

“Baba kila siku  unajigamba kwamba muonekano wangu umetokana na juhudi  , utaacha lini?”Aliongea Chirss  hakupenda sana hio kauli kutoka kwa baba yake.

“Haha.. sema kweli  Chriss , unajua  Mjomba amehangaika  kwa kiasi gani kipindi hicho mpaka akampata shangazi  mhindi”Aliongea Chriss na alitaka kuongea lakini alikatishwa na simu yake mara baada ya kuangalia anaepiga aligundua ni  James.

“James huyu  anapiga”Aliongea  na kisha akapokea.

“Uko wapi Chriss?”

“Nyumbani , vipi  mbona  haraka hivyo hata salamu hakuna?”

“Kuna ms**nge kanitibulia kwa Regina, niambie uko wapi nije tuone unanisaidia vipi”

“Niko nyumbani kwa  mzee”

“Poa”

Simu ilikatwa palepale na  kumfanya Chriss kuanza kutoa kicheko cha nguvu, hakucheka kwasababu rafiki yake ana matatizo , ila alicheka kwasababu watu wake wote wa  karibu walikuwa na matatizo sawa.

“Anasemaje , mbona unacheka  Chriss?”Aliuliza Alex.

“Anasema mpango wake  na  Regina umebuma”

“Nilijua tokea siku nyingi  hawezi kufanikiwa”Aliongea  Mzee  Gabusha.

“Unamaanisha nini  baba?”

“Yule mwanamke sio wa kawaida ,  hivi unadhani  Mzee Dosam  kwanini  kamrithisha  mjukuu wake kampuni tofauti na  baba yake ,  vipi kilichotokea mara baada ya kurithishwa? , IQ  ya yule mwanamke  inasemekana ni kubwa mno  tokea akiwa  mtoto na inasemekana  akiwa  na miaka  mitano  aliendwa kutengenezwa”Aliongea na kumfanya  Alex  na Chriss wote  kushikwa na  shauku.

“Mjomba unamaanisha nini kutengenezwa?”

“Hata mimi  sijui kwasababu   ni swala ambalo hata  raisi wa nchi hii hawezi kujua, ila  tetesi nilizosikia  ni kwamba sio binadamu wa kawaida, hili ni swala nyeti sana  msije kulisambaza ,  mimi mwenyewe siamini  ila mtu alieongea kauli hio  ni mtu anaejua siri nyingi”

“Dunia ina siri nyingi sana hii baba , hasa baada ya wazungu kuishi  nchiin kwetu   kwa muda , lakini kauli yako  inaniogopesha na kuona mshikaji wangu  James  anajiingiza kwenye matatizo”

“Haha…James ukweli ni kwamba hana uwezo wa kumpata Regina  sio  yeye tu hata mimi na wewe , ijapokuwa yule mwanamke ni mrembo  na ananivutia lakini  najua  ukomo wangu,, Mzee Wilsoni na Lamla wanafosi tu kumsapoti James  kwasababu ya uhusiano wa familia zao , ila sidhai malengo yao kama yatatimia”

“Tena nimekumbuka , una dili gani  na  Jasusi?”Aliuliza Mzee Gabusha akimlenga  Chriss alikuwa na dili gani na Amosi.

“Hakuna dili la siriasi  kihivyo , kuna  mipango  yangu ya kibiashara niliomba anisaidie?”

“Chriss hakikisha  hujiingizi katika maswala ya hatari ,  taarifa zimenifikia  ni wiki ya pili sasa  unajihusisha na wale wachawi  kutoka Brazil”

“Baba umejuaje?”

“Nina njia nyingi za kujua kila kitu , Lile kanisa  la 

Wabrazil  lipo  chini ya Rada za  jeshi kitengo cha MALIBU , Sijui nini kinachoendelea lakini  kuwa makini , fanya ufanyavyo hakikisha hufi kabla  ya kuniletea mrithi”

“Kama MALIBU kweli  wanalifuatilia lile kanisa , Chriss zingatia ushauri wa mjomba , nimesikia   licha ya mafundisho yao kuendana na ya kikristo lakini pia  wanasisitiza mambo ya spiritism”Aliongea Alex.

“Kuna kitu kilichonipeleka pale  na sio swala la ibada  Alex ,  ni swala la kibiashara , ukiwa  mfanya  biashara  hutakiwi kifungwa na imani za watu”Aliongea  Chriss na muda uleule mlango  wa sebuleni ulifunguliwa  na James aliingia.

Alikuwa akijulikana hapo ndio maana hakuwa na  haja hata ya kugonga  mlango , James , Chriss , Alex walikuwa ni marafiki  tena waliosoma shule  moja , Alex na Chriss walikuwa ndugu   huku  James  yeye akiwa rafiki  yao , wote hao walikuwa wakisifika  kama wazee wa makoloni, yaani mwanawake wao  walikuwa  wakimwita  Koloni na  wakimpata wanasemea wana’colonize’,  wakimuacha aidha ni kwa uhuru wa bendera  au  kwa kumwaga damu , zilikuwa ndio lugha zao za ujana.

Mzee Gabusha  hakuwa amepishana  sana   umri  na mtoto wake Chriss na ndio maana muda mwingi walikuwa  wakionekana kama   marafiki , inasemekana  Mzee Gabusha akiwa na  miaka  kumi na sita  tu ndio Chriss alizaliwa  mara baada ya kutoka kimapenzi na mwanamke wa kihindi ambae  mara baada ya kujifungua alitoweka.

“Aisee kwa sura hio ,  kweli   inaonekana sio kwema”Aliongea  Alex.

“Mjomba  habari  za  saa hizi?”Alisalimia  James huku akijitahidi kujituliza.

“Kaa kwanza chini James”Aliongea Mzee Gabusha  akiwa na shauku ya kutaka kujua nini kimetokea , ijapokuwa alijua Regina   hakuwa  mwanamke wa kawaida lakini alikuwa na shauku.

James mara baada ya kukaa chini alichukua glasi iliokuwa  na  kilevi  , hakujali nani alikuwa akitumia hio  glasi na alishusha pombe yote.

“Nini kimetokea  James?”

“Leo Regina kamtambulisha  boyfriend wake mbele yangu na  mbele ya wazazi wake”Aliongea.

“Nini!!?”

“Ndio hivyo  na huwezi kuamini huyo  fala ni choko tu  hana mbele wala nyuma , lakini   namna alivyokuwa akijiamini mbele ya Regina  ndio inanitia hasira zaidi na zaidi”Aliongea na kumfanya  Alex  na Chriss kuangaliana na kisha wakamgeukia Mzee Gabusha.

“Sasa hivi nimepokea taarifa   huyo fala  kahamia kabisa  nyumbani kwa Regina”

“Unatania James ,  mwanaume gani wa kumfanya Regina  alegee mpaka kwenda kuishi kwake, sidhani  kama ni kweli?”Aliongea  Chriss.

“Hata wewe umeona  eh ,  kuna hisia zinaniambia yule choko yupo kwenye maigizo  na Regina kwasababu ya mimi  kulazimisha ndoa”

“James punguza jazba , ushasema huyo mtu ni choko  halafu  amekukasirisha hivyo ,basi anaonekana sio  mtu wa kawaida”

“Mjomba sio  kama namkuza . lakini  kama hili likiendelea mipango yangu mingi inafeli , napaswa kumuoa Regina kwa haraka la sivyo dili  na wale wachina litakuwa limekufa rasmi, baba  nae kanikaa kooni”

“Bora wewe  unamtaka Regina kukamilisha mipango  yako , lakini  James  ni biashara gani hio ambayo inakutaka  umuoe  Regina kwanza ndio dili liendelee?”Aliuliza  Alex.

“Alex magizo yako  unayoyafanya pale  FEMU  ndio yanakupotezea muda  na mambo mengi  huyajui”Aliongea Chriss.

“Nina sababu za kuwa pale  FEMU Chriss, mambo sio  rahisi kama unavyodhani”

“Tuachane na hayo , Alex  kuhusu wachina ni siku nyingine , nataka kujua namna ya kudili na hili swala haraka , mjomba  naomba umsaidie kumpoza baba ni rafiki yako na anakusikiliza”Aliongea.

“James  haina haja ya kuwa na wasiwasi, mimi na baba yako  ni wafadhili wa  wakuu wa Mheshimiwa Jongwe  , kama  ataingia madarakani kitu ambacho nina uhakika nacho asilimia mia  fursa  zitakuwa nyingi za kuirudisha ampuni yako katika mstari , kama unamtaka huyu Regina kwa ajili ya kampuni yako nadhani unapaswa kuachana  nae , nitaongea a baba yako na  atanielewa”

“Mjomba  ukweli  nampenda  sana  Regina , ijapokuwa ni kweli kwa namna nyingine  nataka kukamilisha mipango yangu kupitia yeye ,  lakini  moyo  wangu unampenda sana na sipo tayari kuona mtu yoyote anamchukua”Aliongea na kumfana Chriss na Alex kuangaliana.

“Kwahio unataka tukusaidie nini  James ?”Aliuliza Alex.

“Hisia zangu zinaniambia  kabisa  yule mpuuzi anatumiwa  na Regina ili kuzuia   mchakato wa ndoa usiendelee , ninachotaka  ni vijana waingie kazini , atekwe  na baada ya hapo apewe kibano  nijue ukweli kwanza na kisha  tumpe onyo la kukaa mbali na Regina”Aliongea James  huku akionekena alikuwa akimaanisha  kwa namna  ya kauli aliokuwa akiongea.

“Hio kazi ni ngumu kukusaidia James , hiki kipindi  ni cha uchaguzi  na mimii ni mdhamini  namba  moja wa mgombea wa uraisi, kosa kidogo  tu wapinzani watatumia kama siraha ya kujinadi, James  mimi kama mjomba wako na rafiki  wa baba yako  swala la Regina achana nalo kwasasa , najua kampuni yako  ipo  karibu kufirisika lakini uchaguzi ukipita tenda zote za kiserikali zitakuja kwetu  , hii ndio maana ya

mimi na baba yako  kuwa kidedea kuhakikishaJongwe anaingia ikulu, wewe  ni  mwanaume  zipo njia nyingi za kumpata  Regina 

kama kweli una nia  basi sio lazima kutumia fujo, labda kama  wewe mwenyewe huamini uwezo wako wa kutongoza mwanamke”

“Mzee unaongea sana ki utu uzima , katika hali  hii ya James wote tupo katika ‘ground’  moja , wewe mwenyewe  njia zako za  kawaida  zimekushinda zidi   ya…”

“Chirss usivuke mpaka…”Alionya Mzee  Gabusha  na palepale alisimama  na kuondoka.

“James   mimi pia nipo kwenye tatizo kama lako , hapa Chriss ndio anajiona mshindi  tu lakini hana ushindi wowote,  ni mwezi wa ngapi huu tokea aanze kumfatilia  Prisila lakini anatolewa nje”

“Alex unataka kusema  nini…”Aliongea  Chriss huku  macho yake yakibadilika na kuwa ya usiriasi.

“Ninachomaanisha  ni kwamba  sisi kama marafiki  hili ni swala la kusaidiana, njia zipo nyingi sana”

“Njia  hazipo nyingi sana , njia ambayo   mnataka kufanya ni kama ambayo umeifanya  muda uliopita na haijakupa majibu”

“Njia gani ulifanya Alex?”Aliuliza James,.

“Kuna choko  mmoja   ametengeneza ukuta kati yangu na Frida , leo  niliwapa kazi vijana kwenda kupekuwa anapoishi kutafuta ni kitu gani anaficha mpaka  Frida kumuhitaji , lakini wapuuzi wale wameambulia kipigo  mpaka kuzimia”

“Haha.. Alex wewe umafia huujui , kama umetuma vibaka ulitegemea nini , tena wanaenda mchana kweupe”Aliongea  James.

“Huna unachokijua James nyie wote wawili  hamjui  ni hustle ngapi nimepitia mpaka leo hii  ni meneja  wa  usambazaji wa viungo vya akili  na sasa pesa ninayo na tunazungumza lugha moja , mimi sio kama nyie  utajiri mmeukuta , mimi nimeanzia chini  na huko chini mambo mengi yametokea, umafia  naujua sana tu”

“Huu sio muda  wa kujisifia , nina miadi na Prisila  leo hivyo kwasasa nashauri James usikilize ushauri wa   mshua  na wewe  Alex … tafuta sababu kwanza kwanini hilo koloni linamtaka   mwanaume mwingine na sio wewe , pengine unachokiwaza sicho kabisa” “Unamaannisha nini  ninachokiwaza sicho?”

“Wewe  unamjua  Frida vizuri  nje ndani , yule mwanamke umesema kakulia nje ya nchi na  ni juzi tu hapa  karudi , unadhani  unamjua  vizuri  nje ndani, Vipi kuhusu  viungo vya akili , kwanini anatumia? , wewe unawatafuta wateja ?, si Binamu ndio wanatafuta wateja na wewe ndio unafanya  usambazaji tu?”

“Upo sahihi Chriss , kitendo cha  Frida kuwa mteja  wangu  ni ishara  namba moja sio wa kawaida , lakini sheria  ya kazi yangu inanizuia kumfuatilia”

“Ndio ujiulize unaitaka kazi  au unamtaka  Frida”Aliongea na kisha aliondoka.

“Chriss unaenda wapi sasa , hatujamaliza swala langu” “Nimemuacha Anitha tayari kwasababu ya Prisila ,  lazima nimkomalie la sivyo nitaishia  kuita ya Delivery”Aliongea  na kutokomea nje.

“Unapanga kufanya nini  James?”

“Kwasasa nitatafuta namna  yoyote ile ya kumlazimisha  Regina akubali ombi langu la ndoa , kwa hizi dharau ambazo amenionyeshea leo   lazima nimfanye alie kilio cha  mtoto  akiwa kitandani ,  tuone kama ataendeleza maringo yake”Aliongea James kwa hasira  na  kisha alisimama na kuondoka.

Alex mara baada ya kuona ameachwa peke yake alijiambia na yeye lazima Frida  awe wake kwa namna yoyote ile,. Hata kama itakuwa ni kumuua Hamza ikitokea  wana mahusiano.

*****

“Shangazi , nimerudi”

Ilikuwa ni  saa kumi na mbili kamili wakati  Regina  akisukuma mlango  wa kuingilia nyumbani kwake na mara baada ya kufika  katika sofa alijirusha  kwa kujiachia  kiasi kwamba  nguo aliovaa iliyaacha mapaja  yake wazi huko koti la suti akitupa kule.

Baada ya kujinyoosha  kidogo  hatimae aligeuka akiitafuta rimoti ilipo ili awashe TV  lakini  hapo ndipo alipokumbana na  sura chafuchafu iliokuwa ikimwangalia kwa tabasamu kutoka nyuma ya sofa.

“Regi naona ndio unarudi”

Hamza alikuwa ameshikilia Screwdriver  kwenye  mikono yake , alikuwa  hajavaa hata shati zaidi  ya libukta kubwa kubwa  hivyo kuacha  wazi mwili wake uliojengeka kimazoezi.

Ni muda huo huo  Regina alikumbuka kuna mtu ambae  ameongezeka nyumbani kwake  na kwa namna ambavyo amejiachia alijikuta  akiwa mwekundu kama nyanya na haraka sana alisimama na kujiweka sawa 

“Muhuni sana  wewe , unaangalia nini!!?”Alibweka huku akimsukuma  Hamza ambae alikuwa nyuma ya sofa akimchungulia.

“Regina unafanya nini , kwahio siruhusiwi kukaribisha  nyumbani”Hamza alijitetea mara baada ya kupigwa.

“Kwanini unaangalia kifua changu ..”Aliongea  huku akiziba kifua na mikono yake miwili.

“Halafu kwanini huna nguo?”

“Naongea   na wewe ndio maana  nakuangalia  na siangalii kifua , ni kama ishara ya heshima tu , kuhusu nguo zangu   ni kama tabia ambayo na wewe unayo ukifika nyumbanni  na kuvua nguo zako na kujiachia”

“Hii ni nyumba yangu na sio yako , huruhusiwi kutembea kifua wazi “Regina alikuwa  na tabia ya  ukimya sana na hio ni mara yake ya kwanza kuongea kwa sauti hivyo  hasa kwa  maeneo ya nyumbani,alikuwa na hasira kweli.

Aliishia kujilaumu yeye mwenyewe kwa  kuona kwamba hakuchagua mtu sahihi  kwa kuamini mwanzo  ni mtu mzuri  kumbe sivyo.

Hamza mara baada ya kuona mrembo huyo alivyokasirika aliamua kuvaa shati lake  haraka haraka.

Regina aligeuza shingo yake mbali  asimwangalie Hamza lakini alikuwa ashaona kifua chake na mgongo wake  na mapigo ya moyo yalisimama.

Ilikuwa mara yake ya  kwanza  kuona mwanaume kuwa na mwili mzuri hivyo , ijapokuwa Hamza mwili wake haukuwa umetuna sana kimisuli lakini ulikuwa umebalansi vyema.

“So this chap  actually do Gyms?”Ndio yalikuwa mawazo yake muda huo  na  haraka sana alitingisha kichwa chake na kujiambia  anafikiria ujinga gani.

Mara baada ya kuona  tayari  Hamza ashabadili mavazi  alisimama na kwenda kuchukua rimoti kwa ajili ya kuwasha TV,   mara baada ya kuipata  na akiwa anataka sasa kuwasha aliweza kugundua kuna kitu hakipo sawa  na mdomo wake  mzuri ulipanuka kwa mshangao 

“Wewe.. wewe ,, umeifanyia nini TV yangu ?”

Regina hakuamini TV yake  ya kisasa na ya bei ghali  hivyo ilikuwa imetolewa ukutani na kufunguliwa  funguliwa.

 

Previoua Next