Reader Settings

SEHEMU YA 14.

Roma alikuwa ameshikilia Screwdriver na ni kweli alikuwa ameifungua Tv na alikuwa bize kuitengeneza ndio maana hata wakati ambapo  Regina anaingia hakuweza kumuona kwasababu alikuwa ameinama akiwa bize.

“Oh … nilikuwa nikiangalia Tv muda si mrefu lakini niligundua ilikuwa na ukungu hivyo picha kutoonekana vizuri ndio maana nimeifungua  kuitengennea , subiri kidogo na  maliza  muda si mrefu”

Regina  pumzi ni kama zilitaka kumkata  na alijitahidi kujituliza kwa kuvuta hewa nyingi na kuishusha.

“Hivi unajua  imenigharimu kiasi gani kununu hio Tv?”

“Milioni moja nahisi”

“Ongeza nane”

“Milioni  moja  na  nane”

“Wewe mjinga , ni milioni  nane”

“Duuh  kumbe ghali hivi , ndio maana  inaonekana kuwa ya teknolojia ya juu”

“Sasa wewe kuona ukungu kidogo tu ndio ukaifungua , unajua kuirudisha kama ilivyokuwa , unajua Tv zinavyofanya kazi?”

“Ngoja tuone kama nitaweza kuitengeneza”

“Uone kama unaweza , seriously?”

“Regina   kwanini unagombana na Hamza , yaani ndio umerudi unachoanza ni kufoka?”Aliongea  Shangazi Mariposa ambae alitoka jikoni mara baada ya kusikia makelele ya Regina kufoka.

“Shangazi kwanini umemruhusu  afanye hivi ,ameharibu Tv”

“Kumbe ndio kilichokukasirisha ,  hebu muache aitengeneze akishindwa tunaweza kununua nyingine tu au kumwita fundi”Aliongea akiwa na tabasamu na kisha alimgeukia  Hamza.

“Hamza harakisha , muda wa chakula unakaribia” “Sawa , ndani ya dakika  tano nitakuwa nishamaliza”

Regina aliishia kumwangalia shangazi yake na  Hamza wanavyoongeleshana  na aliona  kuna kitu hakipo sawa , imekuwaje wamekutana leo lakini wanaonekana kuzoeana kama wameishi pamoja muda mrefu.

Regina  wakati akimwangalia Hamza akizungusha nati  na kukunja kunja alitamani kumtupia rimoti.

“Acha kuzidi kuiharibu , utailipia  ikiharibika kabisa”

“Haiharibiki , you must trust  your man”Aliongea Hamza akiwa anajiamini

“Huna aibu kabisa”Aliongea.

Regina hakuwa na uwezo wa kufanya chochote kwa wakati huo na wakati alipogeuka aliweza kumuona  Shangazi  Mariposa akimwangalia huku akitabasamu , alionekana kufurahi namna ambavyo  Regina alikuwa amekasirika na kufoka , ilikuwa ni mara ya kwanza.

“Shangazi , ongea chochote , huyu  mtu kaja  kusababisha matatizo tu hapa”

“Mimi ni mzee , unaniambia vipi niingilie  mahusiano yenu  changa, ngoja nijipikie zangu  , mnaweza kufanya mnachotaka”Aliongea  

“Nini , mahusiano changa..”Regina ni kama hakuwa amesikia kauli ile vizuri lakini  Shangazi alikuwa tayari ashakimbilia jikoni, hata hivyo alikuwa akijua Hamza na Regina ni wapenzi  kweli maana hakumwambia kama ni feki.

Aliishia kuondoa kibanio  cha nywele zake  kama kwamba kufanya hivyo kichwa chake kitakuwa chepesi  kutokana na hisia hasi alizokuwa nazo.

Muda ambao chakula kishaiva  Hamza na yeye alikuwa ashamaliza  na kuirudisha  sehemu yake.

Regina kwa   haraka haraka alichukua Rimoti  na kuwasha  lakini  mara baada ya kubonyea mara kadhaa   Tv  haikuwezekana kuwaka.

“Angalia ulichofanya sasa”

Alilalamika kwa hasira , sio  kwasababu alikuwa akijali sana kuhusu Tv kuharibika maana hela za kununulia mpya anazo  lakini alikuwa na hasira kwa kitendo cha  Hamza kujimilikisha nyumba yake na kuanza kuharibu vitu.

“Regina , umeshikwa na homa?”Aliongea Hamza na kutaka kumuwekea Regina  kiganja cha mkono wake kwenye paji la uso  lakini mkono wake ulibetuliwa.

“Homa gani ,acha kubadilisha topiki , si ulikuwa ukionekana  kama vile fundi  mjuzi tu  , sasa umeharibu Tv na unatakiwa kunilipa”

“Hey  mrembo , hivi Tv inawaka bila ya  waya wake wa umeme kuchomekwa kwenye kebo?”Aliongea  Hamza huku akiwa ameshika kiuno

Shangazi wakati akitoka  jikoni  na kusikia kauli ya Hamza aliishia kugugumia kwa kuzuia kicheko.

Regina  alishangaa kidogo lakini alificha mshangao wake  kama kwamba anapotezea.

“Kutokuchomekwa haimaanishi imefaa”Aliongea na kisha akachomeka kebo kwenye umeme na baada ya hapo alibonyeza  na chombo kiliwaka na kuanza  kuonyesha picha  katika ubora wa hali ya juu.

“Aiyaa ,, naona kweli  kale kajiukungu kamepotea , Hamza  unaonekana kuwa fundi mzuri”

“Fundi wapi  shangazi , kabahatisha  tu   haina  haja  ya kumsifia , isitoshe kutengeneza sio jambo kuubwa ki hivyo”Aliongea  huku akimwangalia  Hamza kwa kutompa sifa zake.

“Mbona kama unajaribu kunitengenezea cha kuongea , sijasema  kutengeneza Tv ni jambo kubwa , mimi nimesema nitaitengeneza na imefaa”Aliongea lakini  Regina alijifanya hajasikia na alizipiga hatua mpaka kwenye  meza  kwa ajili ya chakula  na macho yake  mazuri yalichanua  mara baada ya kuona chakula kingi kikiwa mezani.

“Shangazi , mbona chakula ni kingi hivi?”

“Umemleta Boyfriend wako  nyumban ndio maana nimepika kingi kumkaribisha”

“Kuna haja gani ya kumkaribisha , kama ningejua   ni  mtu wa aina hii nisingechukua hata uamuzi wa kumfanya kuja kuishi hapa”

“Hakuna tiba ya majuto kwenye ulimwengu  huu , mimi namuona  Hamza  mtu mzuri tu, naona unajua kuchagua”Aliongea  

“Shangazi , wewe hujui tu   alivyo , halafu chakula ni kingi na hatuwezi kumaliza , naona upike  kama kawaida  tu  na usiongeze sana kwa ajili yake” Hamza hakujali  Regina alichokuwa akiongea  na alichukua sahani  na kisha akapakua wali kiasi  na kisha akampatia Shangazi.

“Shangazi  asante kwa juhudi zako”Aliongea.

Shangazi hakujua hata aseme nini , tokea aanze kushi na Regina haikuwahi kutokea mtu akampakulia chakula , siku zote aliwapakulia wengine chakula. “Jipakulie  tu Hamza , nitapakua mwenyewe”

“Sio sawa , wewe ndio  mkubwa hapa , ni sahihi kwa sisi wadogo kukupakulia , usiniambie  Regina hajawahi kukupakulia chakula?”

Mara baada ya kuuliza swali  hilo lilimgusa  Regina na sasa  ndio alikuwa akifikiria   na kuona Shangazi yake alikuwa akimhudumia kwa zaidi ya miaka kumi sasa  lakini hakuwa hata akikumbuka kama kuna siku ambayo ashawahi hata kumpakulia chakula.

Sio kwamba yalikuwa maringo bali ni kwasababu siku zote anakuta  tayari  kila kitu kishaandaliwa  na yeye ni kukaa tu na kula , hivyo hakuwahi hata kufikiria kufanya kama alichofanya Hamza.

“Regina , ijapokuwa  Shangazi ni kama mlezi tu kwako , lakini utatakiwa  kuonyesha unamjali pia , Shangazi anatumia daladala kwenda  sokoni  lakini una magari zaidi ya kumi  hapa ndani , weka ratiba rudi nyumbani na mchukue muende wote kwa pamoja sokoni”Aliongea Hamza.

Upande wa Regina kadri alivyokuwa akisikia kauli hio ndio ambavyo alijisikia ni mwenye hatia , lakini kitendo cha  Hamza kumfundisha cha kufanya hakutaka kukubaliana nacho.

“Jali mambo yako , nimeishi na shangazi kwa miaka ningi , sitaki unifundishe , kumpakulia tu shangazi chakula ndio sasa unajiona umemfanyia jambo la maana sana”

“Regina  haina haja ya kuwa na hasira , Hamza alikuwa akijaribu kuonngea  kile anachoona ni sahihi , nimekuona ukikuwa hivyo nakujua ni kwa namna gani unavyonijali”

“Shangazi  kama ukitaka kwenda sokoni  niambie twende pamoja , nilishindwa kung’amua hili”

“Hakutakuwa na muda wa kukusbiria mpaka urudi  kazini ndio twende sokoni na kisha tuandae chakula , huna haja ya kuwa na wasiwasi , isitoshe sijazeeka sana”

“Wasiwasi wangu  huyu mtu ataendelea kukufanyia maigizo ya kukujali .. anajua kujifanyisha mtu mwema  kweli usimuone hivyo  lakini ni mtu mbaya  mwenye ajenda nyingi”

“Regina acha kuongea upuuzi, ni saa ngapi nilijifanyisha?”

“Kila unachofanya ni maigizo”Aliongea  Regina.

Kuona namna   nyumba ilivyokuwa imejaa makelele ya Regina na Hamza , Shangazi  alijikuta akijisikia furaha , zamani nyumba ilikuwa kimya sana , lakini ujio wa Hamza ni kama uliifanya ichangamke na ionekane kweli ni nyumbani.

“Hamza ujio wako umeichangamsha sana  nyumba sio kama zamani”

Regina alitaka kuongea  lakini alikosa kujiamini , hakuwa akijua ni kwanini alikuwa akipandwa na hasira kwa kumuona Hamza tu. 

“Yameisha sasa , na tule  maana chakula kinapoa”Aliongea Shangazi  na wote walianza  kula.

Regina  bado hatia  ilikuwa ikimtafuna kutokana na maneno  ya Hamza , lakini hata hivyo alikula bila ya kuongea chochote.

Regina alikuwa akila kistaarabu mno , alitafuna bila  ya kuonesha   meno yake  nje 

Upande wa  Hamza   ni kama mbwa  anaetafuna mfupa , meno yote  yalikuwa nje  kutokana na spidi yake  ya kutafuna na alimaliza akaongeza , akamaliza na akaongeza tena.

Kwa mshangao wa Regina chakula chote kilikuwa kimeisha .

“Unakula kama Mzimu uliofufuka”Aliongea Regina maana kwenye maisha yake hakuwahi kuona mtu anakula namna hio , lakini Hamza hakujali kejeli zake , aliondoa vyombo na kisha alimshukuru  Shangazi kwa chakula kitamu.

“Ngoja  kwanza nikapigwe na upepo”Aliongea  Hamza na kisha alitembea  kutoka nje.

Dakika kadhaa za kujivuta ili chakula kimkae vizuri tumboni  Maybach nyeusi ilisimama nje ya uzio.

Mwanaume na mwanamke walishuka kutoka kwenye ile gari  na  mara baada ya kuwaangalia aliweza kuwajua ni Mzee Wilsoni  na mke wake Lamla.

Kulikuwa na dereva ambae alifuatishana nao  , alikuwa mrefu wa mita kama  1.7  akiwa na mwili uliojazia kimazoezi ,uso uliokomaa  na wenye  kovu  karibu na  na eneo la  nyusi, alionekana kuwa mwenye ari kubwa  na ilionekana kabisa hakuwa dereva wa  kawaida.

Mara baada ya kumuona Hamza Lamla na  Mzee Wilsoni nyuso zao zilijikunja.

“Karibuni nyumbani wakwe,  ila mmechelewa  kidogo ndio tumemaliza kula”Aliongea  Hamza.

“Unafanya nini hapa?”Aliuliza mzee Wilsoni akiwa  na sura  kauzu.

“Regina ameniambia nihamie , nadhani hataki kukaa mbali  na mim”

“Oneni jamani , huyu mtoto  amerukwa na akili  kabisa , ni mwanamke gani wa kuruhusu mwanaume kuishi nae kabla ya ndoa ,  hili swala likifahamika  ataiweka wapi sura yake”Aliongea Lamla lakini muda uleule mlango wa kutokea ulifunguliwa. “Nimemkaribisha mpenzi wangu nyumbani kuishi na mimi na  sio mtu wa kufanywa siri  na kwanini nione aibu  kwa walimwengu”

“Wewe  mtukutu ,  kwanini unajibishana  na wazazi wako?”Alifoka Lamla  mama wa kambo wa Regina.

Regina alikuwa kauzu mno na hakusogea hata nchi wakati akimkodolea macho mwanamke huyo , ilionyesha ni  dhahiri  kiasi gani hawakuwa wakipatana.

Kitendo cha Regina kusimama mlangoni  kilimfanya  Shangazi aliekuwa akisafisha meza kutoka haraka na

kutaka kumuondoa Regina mlangoni na kuwakaribisha ndani.

“Ingieni ndani jamani , karibuni”

“Tuingie ndani , na tukaongee vizuri na Regina juu ya hili”Aliongea Wilsoni na Lamla alimwangalia kwa  jicho la dharau Hamza.

“Sawa tunaingia lakini hili ni swala la kifamilia , mtu wa nje kama huyu hapaswi kuwepo”

“Huyu ni mpenzi wangu sio mtu wa  nje , mwanaume ambae  nitaolewa nae”

“Wewe.. unaruhusu vipi  mdomo wako  kuongea hayo maneno”

“Nimeongea ukweli”

Lamla mama wa kambo wa Regina alikuwa na hasira mno kiasi kwamba macho yake yalikuwa yakianza kuwa mekundu 

“Mnaona  wenyewe , ananidharau sana kwasababu mimi ni mama yake wa kambo tu”

“Hebu acheni malumbano nyie  wawili , Regina  tunakujali sana ndio maana  tumekuja usiku usiku hapa   kwa ajili yako , kuna mambo hatukukuelezea vizuri wakati wa mchana , sio vizuri kuzuia wazazi wako kuingia  ndani”

“Regina , waache wazee waingie ndani”Aliongea

Shangazi na Regina kwasababu alikuwa akimheshimu Shangazi aliondoka mlangoni na kuingia ndani.

Upande wa Hamza hakutaka hata kuingia ndani , alipendelea kukaa hapo kuendelea kupigwa na upepo.

“Zaka   baki mlangoni  na muangalie huyo mtu kwa umakini mkubwa , usimruhusu  alete fujo wakati wa  mazungumzo ya kifamilia  ndani”

“Sawa Madam”Zaka  aliitingia kwa heshima.

Mara baada ya kila mmoja kuingia ndani ,  Zaka na  Hamza ndio watu pekee waliobakia  nje na Hamza

“Kiti hicho  hapo bosi  , unaweza kukaa”

“Asante mkuu , lakini bosi haruhusu sisi walinzi kukaa chini wakati wa kazi”

“Iko hivyo  kumbe , mbona  inasikitisha”

“Mr Hamza , naona inaboa kuendelea kusimama tu hivi , kwanini tusifanye kitu cha  kutuchangamsha kidogo?”

“Oh ,  unadhani tunaweza kufanya nini?”

“Unaonekana ni mtu wa mazoezi makali , itakuwa unapiga tizi mara kwa mara , sina hobi nyingi sana tofauti na  kushindana nguvu kwa mikono”Aliongea.

“Unamaanisha Arm Wrestling , mbona wazo baya sana hili , mimi  mdogo  kwako”

“Usiwe na wasiwasi ,  kuwa mkubwa haimaanishi kuwa na nguvu nyingi , kinachoangaliwa ni kama wewe ni mwanaume halisi , nina uhakika  kwa mtu kama wewe mpenda  mazoezi huwezi kuogopeshwa na kitu kidogo kama hiki , kwanza unamiliki mtoto mkali kama Regina  halafu muoga?”

“Ah , kwasababu   unaongea kwa staili hio  basi sina jinsi ya kukubaliana na  wazo kao , tutashindana mara moja tu , wasiwasi wangu nitakuumiza”

“Haha… nasubiri kwa hamu uniumize”

Baada ya kukubaliana wote kwa pamoja walisogea mpaka kwenye meza ya  mawe  ya kupumzikia  na kisha wakachuchumaa  na kushikana mikono yao  “Utaniambia  ukitaka tuanze?”Aliongea Hamza.

“Hivi unajua  kazi yangu ya  mwanzo ilikuwa ni ipi?”Aliuliza Zaka.

“Si udeteva , au una kazi nyingine”

“Upo sahihi , kwasasa mimi ni dereva lakini  zamani nilikuwa  katika kikosi cha  makomandoo mikoa ya kaskazini huko , usije kunilaumu kama  nitakuumiza ,, jilaumu wewe mwenyewe kwa kumchokoza Madam”Baada ya kuongea kauli  hio palepale   aliongea kwa sauti waanze.

Dakika ileile  misuli ya mkono wa Zaka ilituna kwa nguvu  ikilazimisha mkono wa  Hamza kushuka chini.

Mkono wa Hamza ulianza kushuka chini na kidogo  tu uguse sakafu  na kwa  nguvu alizotumia Zaka  ilionekana  angeumia kama angegusana na pembe ya ile meza  kama sio kuvunjika kabisa.

Lakini sasa wakati  Zaka akijua ashamaliza kazi   ya kumshikisha Adabu Hamza kwa kumchokoza bosi wake , alikuja kugundua  Hamza hakuwa na mabadiliko yoyote , ijapokuwa  mkono wa Hamza ulikuwa umeelemea chini lakini alishindwa kuendelea kuusukuma uguse sakafu ya  meza ile ya jiwe.

Haikujalisha ni nguvu kiasi gani alitumia, Zaka alishindwa kusukuma  mkono wa Hamza na  mbaya zaidi haukutikisika hata kidogo.

“Unaonekana kuwa vizuri kwenye  nguvu za mikono kwa mtu kama wewe ambae kazi yako ni udereva”Aliongea Hamza huku akiwa na tabasamu la kichokozi. Na ghafla tu mkono wa Zaka ulinyanyuliwa kwa nguvu kubwa  kwenda upande mwingine  na ile  unafika kwenye kingo ya  meza ile ya jiwe kilichosikikika   ni sauti ya mvunjiko wa mfupa.

“Arghhh , mkono wangu..”

Hamza muda uleule alimuachia Zaka  ambae mkono wake ulikuwa ukimtetemeka  kwa  maumivu makali 

“Nilikuambia  wasiwasi wangu ni kukuumiza tokea mwanzo , kama maumivu yamezidi tuite  gari la wagonjwa”

Zaka jasho lilimtoka , kwa mtu kama yeye aliepitia  jeshi  alipatwa na wasiwasi palepale.

“Wewe ni mtu wa aina gani , kwanini mikono yako ina nguvu namna hio?”

“Sina nguvu , wewe ndio ambae ni dhaifu , unaonekana  kuwa na utapia mlo  wa madini ya Kalsiamu”Aliongea Hamza  na kutoa tabasamu la kifedhuli na kisha alipiga  raba kurudi ndani.

Upande wa ndani  majadiliano yalikuwa yamepamba moto ,  Mzee Wilsoni na mke wake walikuwa wakimsihi sana Regina kubadili maamuzi yake na kukubali kuolewa  na James

“Regina , mimi baba yako na shindwa kukuelewa kabisa , kuna kitu gani Hamza anacho ambacho mtoto wa Mzee Benjamini anakosa , hebu fikiria  kuhusu James , kuanzia taswira  ya familia ake  , monekano , elimu , uchumi  na mengineyo mengi James anayo na huyu Hamza hana , ukiachana na hayo   ni mtu ambae anakupenda  na hajaanza leo kukufuatilia , kwanini unaendelea kumuona kama mtu mbaya?”

“Kuna haja hata  ya kuuliza , anachofanya ni kwenda kinyume na mtazamo wetu  kwa makusudi kabisa ,  anataka kupigana na kila kitu tunachoongea ili aonekane  ni  mwenye uwezo wa juu kiakili kwasababu ni CEO”Aliongea Lamla.

“Nyie mnaigopa familia ya mzee Benjamini  na sio

mimi ,  kabla  ya kifo cha babu alinisihi sana  niwe msimamizi wa kampuni zote za Dosam  na nihakikishe  hakuna mtu wa nje wa kuikwapua, mkiendelea  na maswala ya kuongea kuhusu  James , basi sina  chochote cha kuongea na nyiwe , Shangazi wageni wanaondoka”Aliongea Regina  na kusimama kutoka kwenye sofa.

Dakika ambayo Hamza aliingia ndani  ndio alikuwa akimsikia  Regina akisema wgeni wanaondoka na  aliona maongezi hayo yamedumu kwa muda mfupi sana.

Lamla mara baada ya kumuona Hamza akiingia sura yake ilijikunja palepale.

“Zaka yuko wapi , kwanini  upo mwenyewe?”

“Ah , yule dereva wenu , alikuwa ameboreka na aliomba  tucheze  kamchezo kakushindana nguvu ya mikono , lakini kwa bahati mbaya amevunjika mkono”Aliongea Hamza huku akiwa na sura ya kizembe.

“Nini!, inawezekana vipi ?”Aliuliza  Lamla akiwa katika mkanganyiko.

Regina hata yeye sura yake ilibadilika  pia , kwa kile alichokuwa akijua Zaka alikuwa  ni moja ya  madereva waliokuwa wakiaminiwa mno  na  Lamla  lakini wakati huo huo akiwa bodigadi , hakuwa mtu wa kawaida wa kuvunjika mkono kirahisi.

“Zaka  ni kichwa maji , kwanini  kushidana   nguvu kimikono kwa ghalfa tu , alisema  kabisa  ni veterani wa  jeshi  kitengo cha komandoo ,  nilishakuambia usitafute  mlinzi mwenye mdomo sana, turudi  tutapata mlinzi mwingine”Aliongea Mzee Wilson akiwa  na hasira.

Lamla alikuwa  ameshikwa na  aibu mno  na aliishia kumtukana Zaka kimoyo moyo  na kupigisha miguu chini na kisha akatoka nje  kuondoka.

Mzee Wilsoni mara baada ya kuona mke wake akikimbia kutoka njce  alionekana kama vile hakutaka  kumuona   binti yake kuendelea na msimamo wake.

“Tena nimekumbuka  Regina , ulisema  familia ya  Benjamini  wananyanyasa wafanyakazi , nini  hasa kilichotokea?”

“Mdhibiti  mkeo na mtoto wako  kwanza , huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu  maswala ya kampuni”

“Wewe.. yaani mimi baba yako naonyesha wasiwasi kwa ajili yako unaniongelesha hivyo , wewe  pia ni binti yangu  ukumbuke”

“Sitaki uwe na wasiwasi , nachukia kuona namna unavyoruhusu watu kukutumia kwa manufaa yao” “Kwahio kwenye  macho yako naonekana kama  baba nisiejielewa si ndio?”

“Wilsoni inatosha sasa , Regina anaongea kwasababu ya hasira , usiwe hivyo”Aliingilia  Shangazi.

Mzee Wilsoni alikuwa na hasira mno na aliishia kuvuta pumzi nyingi huku akimwangalia Regina na kisha alipiga hatua kutoka ndani ya nyumba hio.

Kutokana na kuvunjika mkoo kwa  Zaka yeye mwenyewe ndio alishika usukani lakini alikuwa amefura mno , ni kama vile hakutaka kuendesha.

Baada  ya wazazi  hao  kuondoka , hatimae amani ya nyumba ilirudi , Regina hakubakia sebuleni  na alipandisha juu   na waliobakia  ni  Hamza ni  Shangazi.

“Shangazi  Regina ana  mdogo wake?”

“Ndio, ana mdogo wake wa kiume ,  wamepishana miaka  mitatu , anaitwa Frank  , bado yupo chuo ,  mama zao ni tofauti  na hawana ukaribu  sana  tokea  wakiwa watoto, Baada ya babu yake  Regina kufariki aligawa hisa zake zote za kampuni kwa Regina  na kumfanya awe mkurugenzi , ndio maana unaona  mdogo wake  hampendi kabisa”

Hamza aliishia kutingisha kichwa  na aliona kuna kitu sio cha kawaida , katika familia nyingi   za kitajiri watoto wa kiume ndio hurithishwa mali na sio wanawake.

“Shangazi  vipi  Regina  ana ndugu yake anaefanana nae?”Aliuliza Hamza na kauli ile ilimshitua kidogo   Shangazi.

“Hana , mama yake  Regina alikuwa ni mfanyakazi wa ndani  na alipopata ujauzito  alifanya siri na akaacha kazi akarudi kwao , baada ya hapo akaja kujifungua na akapoteza maisha  punde tu baada ya kujifungua, Regina aliishi  kituo cha kulelea Yatima mpaka alipofikisha miaka kumi   na ndio hapo  babu yake alivyomchukua na kumleta nyumbani, ilikuwa ni swala la kushangaza kabisa kwani hata Wilsoni hakuwa akijua hilo”.Aliongea na kumfanya  Hamza kumuonea  huruma kidogo Regina.

“Vipi kuhusu baba yake   na wewe ni ndugu kabisa?”

“Mimi na Wilsoni sio ndugu kabisa , alienileta  katika familia  ya Regina ni babu yake , historia yangu kidogo inaweza kufanana na yako”Aliongea na kumfanya  Hamza kushindwa kuuliza sana maana alijua angekumbusha kumbukumbu za nyuma.

Upande wa Hamza kuna kitu kilichokuwa kikimsumbua akili  tokea siku  ya kwanza aliokutana na Regina , haelewi ni  nini lakini kuna hisia zinamwambia  ashawahi kukutana  na Regina,kwa jinsi alivyokuwa akikumbuka ni kama vile  mtu aliekuwa amepoteza kumbukumbu.

“Hamza , nini hiki  kinachotoa   harufu kwenye chumba chako?”Sauti  ilisikika kutoka juu  , alikuwa ni Regina , Hamza palepale alipandisha haraka haraka kwenda juu  na alimkuta Regina akiwa amesimama kwenye  mlango wa chumba chake , ambacho mlango ulikuwa wazi.

“Regina unamaanisha nguo zangu ?”Aliuliza kama vile haelewi huku akinyooshea mkono  nguo ambazo zilikuwa zimesambaa chumba kizima.

“Niliona   ni usumbufu kuzifungia kwenye kabati hivyo nikazicha nje , naonaga ndio njia nyepesi  ya kuzivaa”

“Husikii harufu yoyote?”

“Nasikia ,  hio ni harufu yangu ya uanaume , huwa inakuwa nzito”

Kauli  hio ilimfanya Regina kuwa  kauzu zaidi na alitamani kumpiga Hamza teke  na kudondokea chini huko  sebuleni.

“Kuna baadhi ya nguo  nimesahau kuzifua  ndio maana zinatoa harufu , sorry kwa hilo”Aliongea Hamza mara baada   ya kuona  dalili za mrembo  huyo kukasirika.

“Zitupe  zote  , nitakupa hela ukanunue mpya”

“Kwanini nifanye hivyo , hizo nguo  zikifuliwa vizuri tu zinakuwa sawa ,  ni hasara kutupa nguo , kama unaona zinakusumbua sana na harufu nitaenda kuziosha sasa hivi”

“Nimesema nitakupa hela , hutolipia hata senti moja”

“Sio swala la  pesa , hizi  ni nguo ambazo  nimezizoea  na  nina mazoea nazo  kabisa  na baadhi nimepewa kama zawadi  na marafiki zangu siwezi tupa kirahisi”

Baada ya kuongea hivyo , haraka haraka aliingia katika chumba chake na kukusanya zote  na kuziweka katika begi na  kushuka nazo chini.

“Shangazi , naweza kwenda kufulia wapi , au mna mashine ?”Aliuliza  na alielekezwa.

Regina alijikuta akikosa cha kusema , ashawahi kukutana na  masikini  pia pengine ikiwa hata yeye wakati akiwa  kituo cha  watoto Yatima  lakini hajawahi kukutana na mtu  kama  Hamza  wa kung’ang’ania nguo chakavu.

“Regina , hapa umepata bwana , yaani  anajali mpaka nguo  zake chakavu , naamini huyu hawezi kubadilika  haraka  ukiolewa nae”

Upande wa Regina haikueleweka alikuwa akifikiria nini  na  alionekana kuwa na  hisia mchanganyiko.

“Shangazi ,  mwambie  anifuate kwenye chumba changu akishamaliza kuosha nguo zake”Aliongea na kisha aliondoka.

 

 

 

 

Previoua Next