Reader Settings

Hamza mara baada ya kumaliza  kudili na nguo zake  moja kwa moja alienda katika  chumba  cha  kusomea cha Regina.

Chumba  hicho kilikuwa kidogo  sio kikubwa sana na  kulikuwa  na shelfu  mbili tu za vitabu  ambazo zimejaa  na   vyote vilikuwa vimepangiliwa kulingana na Genre zao.

Alikuwa mwanamke msafi mno , hakukuwa   hata  na ishara  ya vumbi na mpangiio wa kila kitu ulikuwa ni wa kuvutia .

Mtu yoyote akiambiwa amwelezee Regina moja kwa moja angekuambia ni mwanamke ambae  anajitahidi kuwa perfect katika maeneo mengi na vilevile alionekana alikuwa akipenda kile alichokuwa akifanya.

Katika meza alikuwa amekaa  huku  akisoma nyaraka iliokuwa mikononi  mwake kwa usiriasi wa hali ya juu mno.

Hamza  mara baada ya kuingia ndani ya chumba hicho , mwanamke huyo hakuongea chochote kabisa ni kama alitaka kumalizia alichokuwa akifanya kwanza ndio aanze maongezi.

Hamza alichukua kitabu kioja kutoka kwenye shelf na aliweza kuona  vyote vilikuwa vikihusiana na maswala ya management  na finance na kuendelea  hivyo havikumvutia licha  ya kwamba na yeye pia alikuwa mwanachuo.

“Unapenda aina hio ya vitabu?”

“Japo naenda  chuo na kusomea maswala ya uchumi lakini sio mpenzi wa kusoma sana  vitabu  vya aina hii , anyway nimekuja kuitikia wito”Aliongea kisha  akarudisha kile kitabu.

Regina hakuwa na mabadiliko ya muoekano  lakini kuna ishara za usiriasi katika macho yake , ilikuwa ni kama vile yupo ofisini na   mfanyakazi yupo  mbele yake, ki ufupi  kwa mtu ambae hajiamini  mbele ya Regina  angeomba muda wowote  maongezi yaishe  aondoke.

“Mr Hamza kuna kitu  natumaini  unapaswa kuzingatia…”

“Eh , nini hiko?”

Aliongea  lakini Hamza muda huo aliweza kuhisi namna ambavyo  kuna umbali kati ya Regina na yeye , licha ya kwamba umbali wao ulikuwa kama futi mbili tu lakini ni kama vile mmoja alikuwa ncha ya kaskazini mwingine akiwa ncha ya kusini.

“Kwanza kabisa sisi hatuna mahusiano  yoyote wewe ni  mwajiriwa  wangu wa mkataba , hivyo  ikiwa hakuna mtu yoyote   usiniite  Regi , Unaweza kuniita Boss au  CEO , lakini sio  kufupisha fupisha kama Regi  ,liweke  hilo kichwani maana  hatuna undugu wowote  na  hakuna anaemjua mwenzake.

Pili , unaishi hapa kwangu kwasababu za ki usalama peke lakini vile  kuendelea kuigiza  kama  mkataba unnavyokutaka ufanye , sijakuleta hapa kwasababu  labda unadhani  nataka kuwa  na mahusiano na wewe , lazima uheshimu  utofauti wa  jinsia  kati ya mwanaume na mwanamke , huwezi  kukaa  au  kuvua nguo unavyojisikia kama ulivyofanya leo

Tatu , mkataba wetu utaisha ndani ya miezi mitatu tu pengine   hata hivo  miezi mitatu isifike , usidhani labda nitabadilisha mawazo kwa namna unavyokuza mazoea yako na shangazi   na kumfanya awe na furaha kwa kumpeti peti , tabia yako katika nyumba  yangu leo hii  tayari imevuka  mpaka , matumaini yangu   utajua nafasi yako..”

Hamza mara baada ya kusikia hayo alishangaa mno  lakini  kwa wakati mmoja  alijisikia vibaya.

“Kwahio  unadhani  nilikuwa nikimfanya Shangazi kunizoea kwa haraka , kama ndio unachowaza usiwe na wasiwasi , mimi sipo   hivyo,  sijawaza kama ulivyonidhania , najua vizuri kabisa mimi na wewe  haiwezekani kabisa , sisi ni watu wa ulimwengu tofuati”

Regina alikunja ndita kidogo mara baada ya kusikia kauli hivo ya  neno haiwezekani kati yao  ni kama kuna kitu alijisikia.

“Ni vizuri umelitambua hilo , natumaiini utaijua nafasi yako  na usiende mbali na kumfanya  Shangazi kuwa na huzuni siku utakayo ondoka hapa”

Hamza alitingisha kichwa  na kisha aliweka mikono yake mfukoni , alionekana kusita kidogo  lakini akaamua kuongea.

“Regin.. Bosi  sijui navuka mpaka ila nadhani kuna kitu unapaswa uzingatie”

“Nini?”

“Naona kabisa ni  namna  gani baba yako  anavyokujali , ila inaonekana mambo mengi hayajui  badala..”

“Shut up!!”Aliongea kwa nguvu kumzuia Hamza asiendelee na palepale alibadilika  na kuwa mtu mwingine kabisa na kumwangalia  Hamza kwa chuki kubwa.

“Wewe ni nani unaetaka kuongelea maswala yangu binafsi , sitaki mtu wa nje  kutoa maoni  yoyote kuhusu familia yangu, ondoka nyumbani kwangu  sitaki kukuona”Aliongea huku akinyoosha mkono  kama ishara ya kumfukuza Hamza.

Muda huo huo ndio Shangazi alionekana kufika na alishangaa mara baada ya kuona namna ambavyo  Regina alibadilika  na wasiwasi ulionekana  katika macho yake.

“Nata.. Regina  nini kinaendelea , mbona mnagombana”Aliuliza lakini kuchanganya kwake jina kulimfanya  kidogo Hamza kushangaa.

“Shangazi  usiwe na wasiwasi  kuhusu huyu  mtu , mpe mizigo yake aondoke nyumbani kwangu” Hamza  hakutegmeea  Regina kuwa hivyo mara baada ya kutaka kuongea kuhusu baba yake  lakini hata hivyo hakutaka kuendelea kubakia hapo na kugombana na mwanake  aliona ni kama  kujidhalilisha.

Alishia kutoka   huku akitoa tabasamu la aibu mbele ya shangazi na dakika chache aliweza kutoka kabisa nje ya nyumba hio na kuondoka.

Asingeweza kubeba chochote kwani nguo zilikuwa  zimeloa baada ya kuzifua  na nyingine zilikuwa kwenye mashine.

Kwake hakujali sana , hakutaka kujishusha mbele ya mwanamke huyo  na kuomba msamaha , alijiambia tena ana bahati sana siku hizi ni mwenye kujizuia la sivyo angemshikisha adabu palepale na kisha kuondoka.

Hamza mara baada ya kutoka  alitembea mpaka nje  ya geti la mji huo na kisha alipanda daladala , hakuwa na pakuelekea  na alitafuta eneo lililochangamka  ili kupoteza muda na sehemu pekee ni Bar.

Hakuwahi kwenda kumbi za starehe muda mrefu  ili kuokoa hela  na kilichomfanya kuwa bize ni kufaya kazi za kifundi.

Lakini  siku hio  alijiambia anapaswa kunywa japo kidogo , kama angepata na mtoto mzuri usiku huo ingefaa kabisa.

Mwembeni  Bar  ndio  sehemu ambayo  aliona itamfaa , ni  moja ya Bar ambayo ina utulivu sana na ambayo ni ya viwango  ki huduma.

Mara baada ya Hamza kuingia ndani ya Bar hio  alienda moja kwa moja mpaka Counter  na kisha aliomba  apewe Whiskey.

Kwa namna ambavyo aliagiza usingedhania ni yule

Hamza mzembe , hapo alikuwa  mzoefu lakini kabla hata hajapewa kinywaji chake  alisikia jina lake likiitwa na sauti ya kike kutoka nyuma.

******

Saa nne kamili Amosi alionekana  akitembea  katika   mtaa wa Sinza, muda huo alikuwa amevalia  shati la mikono  mifupi , alionekana  katika mavazi  ya ujana  zaidi.

Baada ya kutembea  kwa miguu kwa dakika kadhaa aliweza kusimama katika moja ya mgahawa  maarufu unaosifika kwa nyama choma, mgahawa huo ulikuwa umegawanyika mara mbili  kulikuwa na Bar na upande mwingine ulikuwa ni mgahawa bila  Bar.

Amosi aliingia moja kwa moja upande wa Bar na aliagiza  nyama choma nusu  na kisha alisogea na kisha akaenda  kukaa katika  kitu ambacho kilikuwa na mtu mmoja aliekuwa bize kula  nyama na bia, kulikuwa na chupa kadhaa za Windhoek  ikionyesha  amefika muda mrefu.

Amosi alianza kueletewa chupa yake ya bia K- vant  na kumimina kiasi kwenye glasi.

“Taarifa!!”

Sauti ya chini ilimtoka yule mwanaume wa makamo aliekuwa bize  kutafuna na kushushia na  kinywaji, kwa kumwangalia tu alikuwa na kitambi, lakini vilevile alikuwa mtu mzima kuliko hata Amosi.

“Nimepata dili jipya”Aliongea Amosi huku akipeleka Glasi  mdomoni na kupiga pafu.

“Dili gani?”

“Kuna mwanamke  nimepewa kazi ya kumtafuta , malipo  ni makubwa sana ,   ndio kazi yangu ya kwanza  kupata malipo makubwa hivi”

“Kuna muunganiko wowote  na kazi  yako?, Mwanamke huyo ni nani? Na vipi  kuhusu waliokupatia  kazi”

“Sijaweza kufanya  muunganiko bado , lakini mwanamke ni kama sura yake nishawahi kuiona , lakini nimeshindwa pa kuanzia , waliotoa kazi sijawajua bado ,Chriss ndio mtu wa kati alienikonekti na hili dili”

Kwa jinsi walivyokuwa wakiongea usingeweza kusikia , lakini vilevile usingejua kama wanaongeleshana.

“Chriss ameingia kwenye rada  za MALIBU  tokea mwezi uliopita , ukaribu wake na  wabrazili  umeongezeka na kuibua wasiwasi  kwa kitengo , kuna uwezekano kazi hio  ikawa  ni kutoka kwa Wabrazili ,

kama ni kweli muunganiko   na kazi yako  utakuwa mkubwa”

“Nahisi hivyo pia ,  kwa maelezo ya  Chriss wanasema   ni kazi ambayo najua pa kuanzia , inaonekana wananijua vizuri , nadhai hatua yangu ya kwanza ni kujua  nilimuona wapi  mwanamke  katika picha  alionipa.

“Una hio picha”

“Ndio”Aliongea na palepale alipitisha picha ile kwa chini na bwana yule asiefahamika jina alipokea.

Baada  ya kutumia mwanga hafifu aliweza kuangalia  picha ile na palepale sura yake ilionekana kujikunja.

“Unamjua?”Aliuliza  lakini kabla ya kupokea jibu  lake  mhudumu alifika  alipo Hamza na kupokea alichoagiza hivyo ukimya ulitawala.

“Ndio maana wamekupatia hii kesi , inaonekana waliokupatia wapo ndani ya mfumo  wa  intelijensia yetu”

“Nini!!?”

“Rejea kesi ya radi ya mwaka 2002, iliomfanya  Kanali Sedekia  kupotea”Aliongea na hapo hapo  sasa akili ya  Amosi ilipata network.

“Nilidhani nilikutana nae ana kwa ana huyu mwanamke , lakini kumbe niliona picha yake pia”Aliongea huku akiwa ni mwenye wasiwasi kwenye macho yake.

“Kama  ni hivi kwanini  Wabrazili kumtafuta  huyu mwanamke , si faili  la kesi lilishafungwa mara  kuthibitishwa  yule mama alifariki?”Aliongea  Amosi.

“Sidhani  kama ipo hivyo ,   uchunguzi wa  kesi ile  walipewa  wanausalama wa serikali wafanye kazi , lakini yalikuwa maagizo kutoka Jesuit , mpaka sasa  kuna uwezekano  Sedekia  kuna kitu alichofahamu  ndio maana akapotea”

Jasho lilimtoka Amosi na sasa alijua ni kwanini  kazi hio ilikuwa na   malipo makubwa sana , inaonekana ni  kazi ya hatari mno.

“Kwahio  ni dhahiri  uchunguzi unaendelea  nje ya kitengo cha usalama wa taifa”

“Hilo linawezekana , ni swala ambalo hata mimi mpaka leo hii  linanifikirisha , nani  aliondoka  na   maiti ya mtoto mmoja?, shauku yangu  imeongezeka  baada ya kuona kuna siri kubwa  iliojificha kama si hivyo kwanini  kanisa la Wabrazili wamekupa kazi umtafute mwanamke ambae amekwisha kufariki , nadhani  kuna kitu wanataka kujua”Aliongea yule bwana na kisha alisimama akionyesha ishara anataka kuondoka.

“Kuwa makini na hii kazi ,  la  sivyo kilichomtokea Sedekia kinaweza kutokea kwako pia, ukifanikiwa  umepata taarifa  muhimu kwa kitengo chetu pia, fanya hii kazi ukiwa na uzalendo kwenye moyo wako”Aliongea na kisha aliondoka.

Previoua Next