Reader Settings

SEHEMU YA 16.

Ilikuwa  ni kama kila kitu kilikuwa chekundu mbele yake  kama moto, mbingu na ardhi  vyote vilikuwa ni rangi  ya moto , lakini ilikuwa ni ghafla tu mwanga ule mwekundu ulififia na sasa alichoweza kuona  ni giza totoro, ilikuwa  ni kama vile  anazama baharini na hakuwa tena na msaada.

Lakini akiwa  katika hali ya kukata tamaa , ghafla tu ni kama vile  ni kuchomoza kwa jua hatimae mwanga  ulijitokeza mbele yake , kupitia mwanga ule alijihisi  ni kama vile nguvu zake sasa zimemrudia kiasi   na alihangaika kwa kusogea mbele ili aufikie ule mwanga.

Mara baada ya kupiga hatua  aliweza kuona ule  mwanga ukizidi kuwa mweupe  huku giza ambalo lilikuwa nyuma yake  likizidi kumezwa na mwanga ule  na ndani ya sekunde kadhaa  giza lote lilipotea. “Ah…!!!”

Ghafla tu alikaa kitako  na sasa alikuwa akihema kwa nguvu kama mtu alietoka ndotoni , na katika ndoto alioota alijihisi ni kama vile alikuwa akiunguzwa na

moto  wa jehanamu ambayo ulimfanya kutokufurukuta hata kidogo na kujihisi kuwa katika mateso makali.

Ndoto ilikuwa  ni ya uhalisia mkubwa  mno kiasi kwamba ilimfanya kutaharuki  na mapigo yake ya moyo kwenda mbio.

Mara baada ya kuhema  kwa dakika kadhaa , alijikuta akitulia  na sasa aliruhusu  macho   yake na akili yake kufanya kazi katika uhalisia , hivyo kuanza  kuangalia mazingira.

Lakini  sasa mara baada ya kuangalia mazingira aliokuwepo , alizidi kutaharuki , alikuwa kwenye mazingira ambayo  hakuelewa yupo wapi  , kitanda alichokuwa  amelalia hakikuwa cha kawaida,kwanza kilikuwa chembamba sana.

“Nipo wapi?”

Aliuliza swali hilo ,  katika hali kama hio alijua kabisa  hakuwa katika mazingira ya kawaida , hata kama  pengine  alipata ajali  na sasa yupo hospitalini , hilo eneo halikuwa hospitalini kabisa.

Mapigo  yake ya moyo ambayo yalikuwa yametulia  yalianza kwenda kasi tena , aliangaza kulia na kushoto , mbele  na  nyuma lakini hakukuwa na mabadiliko ,

alijitahidi kusimama  lakini alihisi  hali ya kizunguzungu ikimvaa  na kidogo tu  aanguke chini.

Alijitahidi kushikilia ukingo wa kitanda ili kujiegamiza asidondoke chini , alikusanya nguvu zake zote ili aweze kutoka nje , akili yake ilikuwa ikimwambia kabisa hakuwa katika mazingira ya kawaida , alitaka kujua alikuwa wapi   na shauku yake ilimpa nguvu ya kujikongoja ili kutoka nje.

Mlango  ndani ya chumba alichokuwemo ulikuwa umechoka sana , ulionekana ni ule wa zamani  mno , pembeni ya  kona hio  kulikuwa na chungu kikubwa mno  kilichowekwa kwenye kijisturi., haikuwa hivyo tu kulikuwa na  jiko  lililochakaa  na   kuni ambazo zilionekana kuchomwa zilikuwa zimekwisha zima na kufanya eneo hilo kuwa la baridi mno.

Kila kitu kilikuwa kigeni kwake ,hakuwa na uelewa alikuwa wapi , udhaifu  na hali ya  kizunguzungu aliokuwa akisikia ilimletea shida sana.

“Hii sehemu  ni wapi?!, najihisi ni kama vile nimeamka kutoka kwenye  ugonjwa wa ajabu…”

Mawazo mbalimbali yalipita  lakini  hakuwahi katika maisha yake  kuwa katika hali ya ajabu kama hio, hali ya kupaniki ilimvaa pia   na kitu pekee ambacho aliona pengine ni  bahati hakukuwa na  kitu cha kutisha wala  kuhatarisha usalama wak. 

Mara baada ya kuvuta pumzi nyingi hatimae alijikakamua na kisha alijongea kutoka nje kwa kusukuma mlango.

“Burn the witch !Aderon  is going to burn a witch”

“Choma mchawi huyo , Aderon  anaenda kuchoma mchawi”

“Kila mtu”

“Burn that damn witch  to ashes!!”(Choma huyo mchawi  mpuuzi  mpaka awe majivu)…..

“Puuuh!!!”

Hamza alijikuta akiamka  huku akihema mno , hakuamini kile alichokuwa akiona  sio uhalisia bali ni ndoto.

Kilichomfanya kuamkaa ni kumwagiwa maji  ya  baridi  kabisa na hapo ndipo aliposhituka akihema.

Alijikuta akiangaza macho yake kulia na kushoto , kama mtu ambae ana hakiki mazingira, mara baada ya kuona mwanamke aliekuwa mbele yake , alijikuta akipata ahueni  na kuvuta pumzi.

Eliza ndio mwanamke ambae alimuamsha  Hamza , alijitahidi sana kumuasha kwa  kumtingisha , lakini alishindwa kabisa na hapo ndipo alipochukua jukumu la kumuamsha kwa maji ya baridi , na hatimae aliweza kuamka , mwanzoni alihofia mara  baada ya  kuona haamki, sasa kitendo cha kushituka kwa Hamza kilimfanya  kupatwa na ahueni na sasa anaona alikuwa katika eneo la sebuleni ndani ya  nyumba ya mrembo huyo na alianza kuvuta kumbukumbu za jana yake.

******

Hamza mara baada ya kuingia katika Bar ya muembeni mwanamke ambae alimwita   alikuwa ni Eliza  , mwanadada mrembo ambae alimsaidia kutoka katika mikono ya  Amisi na  genge lake.

“Hamza ni wewe”

“Eliza ?”

Hamza mara baada ya kugeuka  ndio aliweza kumuona  Eliza akiwa  katika meza na kundi  la wanawake wengine warembo  na wote walikuwa  wamevaa mavazi  ya kufanana.

“Kwa muonekano wako nilidhani hufikagi kwenye mazingira kama haya”Aliongea Eliza na  muda huo alionekana pia  alikuwa ameanza kulewa.

Kitendo cha Hamza kumuona mwanamke huyo mrembo ambae alikuwa akimfahamu mudi yake kidogo ilirudi  na alisogea katika meza  yao.

“Hii ni mara yangu ya kwanza hapa”Aliongea Hamza.

“Eliza mbona hututambulishi , huyu  ni  boyfriend wako?”Mmoja ya  mrembo aliekuwa katika  meza  moja na Eliza aliongea , alikuwa amevalia suti.

“Una mwanaume  mtanashati kweli na  mwenye kuchukua mazoezi , kumbe hii ndio aina ya wanaume unaopendelea Eliza …”Mwanamke  yule hakuacha kumsifia  Hamza.

“Asha , unaongea nini , huyu ni kaka  yangu”Aliongea Eliza akimtambulisha Hamza kama kaka yake.

“Acha  aibu Eliza , wewe tuambie huyu ni nani , nadhani wale wanaume wanaokufukuzia watakufa kwa wivu wakijua  una bwana”Mwingine aliongea akitania.

Ilionekana wanawake hao wote walikuwa wakifanya kazi pamoja  kutokana na mazoea yao.

“Endeleeni  tu kunitania na mtaona namna nitakavyokazia   tukiwa kazini..”Aliongea na muda huo huo alimwangalia Hamza.

“Hamza unaweza kuungana na sisi kama upo mwenyewe”Aliongea Eliza , hakuwa na aibu kama  mara ya kwanza alivyokutana na Hamza.

Hamza  mpango wake ni kutafuta  mtoto wa kike yoyote yule kupitisha nae usiku  lakini  baada ya kukutana na wanawake warembo kama hao  aliona akubali na kukaa nao.

Muda huo alikuwa tayari ashaagiza  bia yake na aliendelea kunywa huku stori mbalimbali zikiendelea  na aliweza kugundua  wanawake wote waliokuwa  hapo walikuwa chini ya idara ya  Eliza kazini na ilionekana  Eliza ndio aliewatoa out mara baada ya kupandishwa cheo kazini kwake.

“Eliza  vipi wale  watu , hawajakusumbua tena?”Aliuliza Hamza kimitego.

“Huwezi kuamini kilichotokea , hivi  unajua  kiongozi wao alikuja kwenye kampuni  ninayofanyia kazi  kwa ajili ya kuomba msamaha , mimi mwenyewe sijui nni ni kilichotokea , lakini  vyovyote vile  yaliopita yashapita.. sitaki hata kukumbuka namna nilivyodhalilika mtandaoni”Aliongea  “Ni vizuri kama hatokusumbua tena”

“Eliza  lazima kuna mtu amekusaidia kwa siri , kwa taarifa tulizopata  nasikia Amosi amekuja akiwa  na  nundu usoni  ikionekana kama  vile kuna mtu kampiga”Aliongea.

Hakuna kilichojificha ndani ya kampuni, mrembo aliekuwa  pale mapokezi ndio aliesambaza umbea juu ya  Amosi kuonekana kuumia usoni.

“Acha kuota , unadhani  mambo ni kama kwenye filamu..”Eliza aliongea  huku akikataa ile kauli.

Ukweli nin kwamba mrembo huyo  alikuwa na wasiwasi pia juu ya kile kilichotokea , lakini kadri ambavyo alifikiria siku hio hakuweza kupata jibu , isitoshe kwenye maisha yake hakuwa na marafiki ambao wanaweza kumsaidia.

“Vyovyote vile , Naomba leo nilipie kila utakachonunua hapa  kama asante ya kile ulichonifanyia  juzi na kuniokoa kutoka kwa wale mabaradhuli”Aliongea  na aliinua glasi yake akigongesehana cheers na Hamza.

Hamza alifurahi kuona mrembo huyo alivyokuwa amechangamka,ukweli hakujua kama  mrembo huyo alikuwa akitumia kilevi.

“Kwahio Eliza  usiniambie huyu ndio babe aliekuokoa  jana”Aliongea.

“Mimi siamini kama huyu  kaka yako  kweli,  Eliza acha kuficha  bwana”Waliongea kumtania na ilimfanya Eliza kuwa mwekundu  mno  lakini muda uleule Eliza aliweza kuona kundi  la watu wakisogelea  na palepale uso wake ulibadilika.

Mabadiliko yake yalionekana kwa kila mtu aliekuwa hapo ndani na kufanya wote wageuke.

Mwanaume  wa maji  ya kunde ambae alikuwa mrefu na amevalia  t-shrt ya Ginvenchi na saa  ya Rolex alionekana , alikuwa na  wajihi  wa uchangamfu, akiwa ametangulizana na wanaume  wanne pia ambao  walikuwa wamevaa mavazi ya bei ghali.

“Aiyaa… nikadhani nilikuwa nikikufananisha , kumbe ni wewe mrembo wetu Eliza”Aliongea  yule mwanaume.

Eliza  alionekana kujizuia na alijifanya kama vile hajasikia  na aliendelea kudili na kinywaji chake.

Asha  na wale wanawake wengine  walikuwa katika hali  ya chuki mara baada ya kuona ni kama wanataka kuvurugiwa.

Upande wa Hamza wakati akiwa hajui kinachoendelea , tayari yule mwanaume alionekana kumwangalia kwa kejeli.

“Hey! Mzee potea  na umwachie  bosi  nafasi yako”:Aliongea moja ya vijana  waliokuwa wametangulizana nae.

Hamza hakutaka kuonewa na wale watu kizembe  na alikaa vilevile bila kuonyesha wasiwasi.

“Kama una uwezo  jaribu kuniondoa na akae bosi wako”

“Wewe boya , unajua mimi ni nani ,  uliza uambiwe , mtu yoyote ambae anajifanya kutaka kupandishiana na mimi  lazima avunjike mkono au mguu”

“Kumbe ndio ulivyo, nimekuelewa?”Aliongea  Hamza huku akiendelea kupiga kinywaji chake.

Mara baada ya kuona  Hamza hakutaka kuondoka , bwana yule alipiga meza kwa mkono wake.

“Hili  ni onyo la mwisho  ,  ondoka kwa hiari yako”

“Zefa naomba uondoke , acha kutuharibia mudi , ondoka na genge lako tuna mambo yetu”Eliza  alikosa uvumilivu.

“Haha.. Eliza naona sasa  kwa hiari yako umelitaja jina langu ,  acha kuwa mkali hivyo , nilikuwa na wasiwasi tu na rafiki yangu wa kitambo ndio maana nimekuja kukujulia  hali”

“Haina haja  na hatujawahi kuwa marafiki”

“Roho mbaya hio , nilitaka nikutoe angalau hela kidogo  ufanyie matumizi, nimesikia  gharama za  hospitali ni kubwa  mnno  kwa matibabu ya mama yako asiejiweza kitandani”

Mara baada ya Eliza kusikia habari za mama yake zikiingizwa hasira zilimpanda mno na hakuweza kuvumilia tena na palepale alichukua glasi iliokuwa na mvinyo na kumwagia Zefa.

“Mnyama mkubwa wewe , unatoa wapi  ukijogoo wa kumuingiza mama yangu hapa”

“Wewe malaya , nadhani umekuwa kichaa”Aliongea Zefa kwa hasira na palepale alitaka kumchapa  Eliza kibao lakini mkono wake uliishia hewani mara baada ya kudakwa.

Eliza alijua angepigwa na kile kibao  na alifumba macho kukisikilizia  lakini hakikumpata .

Hamza alitumia mkono wa kushoto kuudaka mkono wa Zefa  wa kulia.

“Ni udada   huu kutaka kumpiga mtoto wa kike”Aliongea Hamza akiwa katika sura ya upole. “Niachie wewe boya , unakitafuta kifo sio”Aliongea na palepale alijaribu kutumia mkono  wake mwingine wa kushoto kujaribu   kumpiga Hamza usoni, lakini kabla hata ngumi ile hajamfikia  Hamza kwa mkono wake wa kulia alikuwa tayari ashamsukuma  Zefa na kudondoka chini.

Hata Zefa mwenyewe hakuelewa kilichotokea , kwani nguvu kubwa isiokuwa ya kawaida ilimsukuma ghafla tu na alidondoka kama vile   alikuwa hajasukumwa bali amedondoka kutoka umbali wa juu , alisikia maumivu makali mno  kutokana na kuteguka mkono.

“Boss, uko ssawa”

Lile genge  lake la watu  lilimsogelea bosi wao  na kumsaidia kusimama.

Eliza na wenzake walishangaa  hata baadhi ya wateja waliokuwa ndani ya bar hio waliosikia mzozo huo  walishangazwa na kitendo cha  Zefa kudondoka chini baada ya  kusukumwa.

“Hamza , unapaswa kuondoka haraka , sidhani kama utawaweza kwa ulichomfanyia  mwenzao”Aliongea  Eliza akimsihi  Hamza kukimbia lakini Hamza hakuwa  hata na ishara ya kutaka kuondoka , alikuwa katika hali ya utulivu kabisa.

“Niondoke , halafu wewe  nakuacha na nani?”Aliongea na  kauli ile ilimfanya  Eliza kujishangaa lakini kwa wakati mmoja alijisikia vizuri  mara baada ya kuona  Hamza anajaribu  kumlinda.

“Umemuumiza bosi  halafu unataka kuondoka , hakuna kuondoka mpaka tukushikishe adabu boya wewe”Waliongea wale vijana , wote walionekana kulewa pia  akiwemo bosi wao na palepale walimsogea Hamza kutaka kumshambulia lakini  kilichowatokea ilikuwa ni  maumivu.

Hamza hakutaka tena  kuvumilia yale makelele  na alisimama na kilichoendelea ilikuwa ni vijana wale na bosi wao kuchezea kichapo cha kufa mtu.

Ki ufupi ni kwamba hali ya hewa ilibadilika kabisa  na hata wale wateja  waliokuwa ndani ya eneo hilo walishangazwa na uwezo wa Hamza wa kupigana , wahudumu walijitahidi kutuliza hali lakini ilishindikana.

“Wewe boya ,  nitakuonyesha , nitakutafuta kwa nama yoyote ile , lazima nilipe kwa leo hii”Aliongea Zefa kwa hasira na kisha alijikongoja na watu wake na kuondoka ndani ya eneo hilo mara baada ya watu kuingilia ugomvi huo.,

Wale wanawake ambao  Eliza alikuwa ameambatana nao na wenyewe waliondoka  na kumuacha Eliza akiwa na Hamza

Eliza alikuwa  kwenye mshangao , ukweli ni  kwamba licha ya  siku hio ni kama mara ya pili ya  Hamza kupambana na watu lakini   wale wa siku ile na wa wakati huo walikuwa na utofauti , hao walikuwa  na uwezo  mkubwa wa kupambana , lakini Hamza kiwepesi kabisa aliwadhibiti.

Kwasababu  bili haikuwa imelipwa  , Eliza alilipa bili na kisha  Hamza  aliondoka na mrembo huyo  mpaka nje.

“Hamza   huna woga kabisa

“Kwanini?”

“Zefa baba yake  ni  mkuu wa  polisi kanda ya Dar es salaam , watu wengi walipelekwa polisi kwasababu  ya kugombana na Zefa , anatumia hadi magenge ya wahuni kuadhibu  watu  ambao ana kisasi nao na hakuna wa kumfanya lolote”

“Hata kama , kwanza simjui na nilichofanya ni kutotaka wewe kuchokozwa”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Eliza  kuonyesha hali kidogo ya kuchanyikiwa na kusita  na alimwangalia Hamza machoni  na kushindwa kuongea neno.

“Mbona unaniangalia hivyo?”Aliuliza  Hamza mara baada ya kuona  mwanamke huyu kasimama.

“Tunaweza kwenda kutembea tembea kule beach, japo ni usiku lakini watu wapo”Aliongea Eliza kwa kusita sita.

Hamza japo alishangaa ombi  hilo ila hakukataa, walitoka katika Bar hio ya Mwembeni na kisha walisogea upande wa Beach , kulikuwa na  Bar nyingine  katika beach hio  na mziki ulikuwa ukisikika , baada ya kufika    wote walinunua vinywaji  va baridi na kisha walishikilia mkononi  na kutembea  katika fukwe hio , Eliza alikuwa na kibegi chake huku Hamza akiwa mikono   mitupu.

“Zefa alikuwa akinifuatilia kwa muda mrefu , kwa zaidi ya miaka miwili  , lakini nilimjua sio mtu mzuri hivyo nilikuwa nikimkataa kila  alipokuwa akinitongoza , siku moja  akiwa amelewa  alifika nyumbani kwetu  na alianza kunilazimisha  tufanye mapenzi , wakati nikiendelea kufurukuta  mama aliweza kufika na mara baada ya kuona  kitendo kile alipatwa na mshituko  uliompelekea kupooza kiwiliwili cha chin…”Aliongea Eliza huku machozi yakianza kujilenga lenga katika mboni za macho yake.

“Lakini kwasababu ya baba yake kuwa  mkuu wa kituo cha polisi na vilevile kuwa na konekshini alikamatwa  kwa siku chache tu na kisha akaachiwa huru , ilikuwa ni siku kadhaa tu mara  baada ya mama kupona kutoka hospitalini  lakini alipatwa na kiharusi  na sasa amekuwa ni  wa kulala tu hospitalini kwa zaidi ya miaka miwil, kutokana na tukio hili ndugu zangu walianza kunisema vibaya  na kunifanya nisipate msaada wowote wa kumuuguza mama..”

Hamza mara baada ya kusikia mrembo huyo akiongea kwa huzuni aliweza kuona ni hali gani alikuwa akipitia kwenye maisha yake.

Juzi alimkuta kwenye matatizo na leo pia alikuwa kwenye matatizo , ilioekana kulikuwa na watu wengi sana waliokuwa wakiyafanya maisha yake kuwa magumu.

“Baada ya tukio hilo ndio  nilitoka nyumbani na kuhamia kwenye Apartment  na  kitu kinachochukua muda wangu mwingi ni kazi na kwenda  hospitalini  tu”

Eliza alikuwa amejikunyata kwenye  miguu yake  kutokana na upepo mwingi uliokuwa ukivuma alihisi baridi na  baada ya  kuwa kimya kwa muda mrefu  aliinua macho  yake na kumwangalia Hamza.

“Hamza  najua hatufahamini  na leo ni mara ya pili umenisaidia , kwanini  umekuwa mtu mzuri kwangu ghafla tu?”Aliuliza.

“Nilifanya nilichopaswa kufanya , isitoshe mimi ni mwanaume  na  huwa  napenda kujichukulia pointi mbele ya mrembo kama wewe”Aliongea Hamza  huku akigida  pombe iliokuwa mkononi mpaka ikaisha na kutupa kopo ,kauli yake ilimfanya Eliza kucheka.

“Unaonekana kuwa mtu  muwazi sana , lakini napaswa kukushukuru kwa wema wako  licha ya kwamba hunifahamu”

Hamza hakuongea chochote na alichukua  bia nyingine ya kopo na kuifungua.

“Vipi  nikupe..”

“Hapana .. nitashikwa na haja ndogo muda si mrefu , nimekunywa sana leo”Aliongea na Hamza hakutaka kumpa  tena kilevi.

Baada ya kukaa kama nusu saa katika fukwe hio Hamza aliona muda umeenda.

“Eliza nitakusindikiza mpaka  unapoishi , muda umeenda, sawa”Aliongea  na kumfanya  Eliza aliekuwa amezika kichwa chake katika mapaja  kunyanyua kichwa chake na kumwangalia Hamza usoni.

“Utaweza  kweli kunifikisha mpaka ninapoishi..?”Aliuliza na swali lile lilikaa kimtego.

Upande wa Hamza alijiambia kwanini ashindwe kufika , isitoshe hana pa kwenda kama ni chumba alisharudisha na mpenzi wake feki kamfukuza.

Hamza alimchukua Eliza  na palepale walitoka  hapo  na kurudi barabarani na kisha walipanda bajajaji mpaka  anapoishi  Eliza.

Hamza hakuwa na mpango wa kusimama getini , aliingia kabisa hadi ndani  kwenye lift  na Eliza alikuwa kimya tu , baada ya kufika katika floor husika wote walitoka mpaka kwenye  mlango.

Eliza alionekana kuwa na wasiwasi mno  na alikuwa akijiuliza  na kujiambia imekuwaje leo kuja na mwanaume mpaka anapoishi  tena usiku huo, ijapokuwa alikuwa amelewa kiasu lakini fahamu zake zilifanya kazi vizuri kabisa.

Lakini hata hivyo  ashamruhusu mpaka kufika  hapo asingemwambia aondoke , kitendo cha kumfanya  Hamza kuja mpaka hapo ni kama  nia yake ilikuwa wazi kabisa

Alijiambia yeye ni mtu mzima  na  kama atamwambia  Hamza aondoke  ingeonekana kama anamchezea akili bila sababu ya msingi.

Alikumbuka tukio la juzi kusaidiwa na Hamza na leo pia  kusaidiwa na Hamza mbele ya   mwanaume anaemchukua, palepale alifanya maamuzi ya liwalo na liwe ,  hata kama simjui vizuri ngoja nimkaribishe.

“Eliza vipi , umekosea ufunguo?”Aliuliza  Hamza mara baada ya kuona  namna ambavyo  mrembo huyo alikuwa na wasiwasi  akichangua kibegi chake  Muda  uleule  hatimae aliweza kupata kadi ya mlango  na kuweka sehemu husika na hatimae mlango kufunguka.

“Karibu ndani…”

Mara baada ya  Eliza kuingia ndani alitupia  mkoba wake kwenye sofa na kupunguza nguo  na kubakia na shati pekee  na kufanya chuchu zake zilizosimama kuonekana vizuri , ilikuwa ni jambo la kuvutia kwa Hamza kweli.

Eliza aligeuka nyuma na kupepesa macho yake  mazuri huku akimwangalia Hamza aliesimama mbele yake.

“Hamza .. umeoa  au una mpenzi?”Aliuliza huku akisita sita, hakuwa akimjua Hamza vizuri na kitu pekee ambacho aliona anapaswa kujua angalau ni kama mwanaume huyo ana mke au ameoa , hakutaka kujihusisha na waume za watu  na kujiingiza katika matatizo, aliokuwa nayo yalimtosha.

“Nina girlfriend lakini ni feki ,  vipi  unaweza kusema nipo kwenye  mahusianno?”

“Ndio inamanisha ndio , unamaana gani kusema ni feki?”

“Ukweli  ni kwamba sina mpenzi , bado nipo single”Aliongea maana hakutaka kuongea sana maswala ya Regina.

Eliza mara baada ya kusikia kauli ile alijikuta akipatwa na ahueni  na alimsogelea Hamza na kisha aliinua uso wake  na kumwangalia , alioekana kuwa na wasiwasi  na kusitasita kwa wakati mmoja.

Hamza mara baada ya kuona mrembo huyo anajilengesha  kwake  hakujua  acheke au aune.

“Eliza  unafanya nini?”Hamza alijifanya mzembe na swali lile lilimfanya Eliza kushikwa na aibu.

“Wewe , kwani hujui ninachofanya au unanichokoza”

“Sijui”

“Kama hujui basi”Aliongea  na kisha akageuka lakini dakika ambayo alitaka kuondoka Hamza alimshika mkono na kumvuta kwake na palepale alimpiga denda 

“Uh..”

Eliza hata  hakujua alivyofika kifuani kwaHamza lakini alishitukia tu akiwa  tayari ashabusiwa, kiini cha macho yake kilicheza cheza mno  na kabla hajaendelea alijitoa kwa Hamza.

“Subiri  kidog”Aliongea.

“Nini shida?”Aliuliza  Hamza  kwa sauti nzito  huku akipumua kwa nguvu maana hisia zishamvaa tayari.

“Naomba niende kwanza kujisaidia”Aliongea na hakusubiri hata jibu alikimbilia  chooni.

Eliza mara baada ya kukaa chooni na kushusha mkojo hatimae alipumua kwa nguvu  huku akiwa na wasiwasi , hakuwa mzoefu sana na wakati huo  alijiuliza akishatoka hapo nini kinaendelea, alikuwa akivutiwa  na Hamza lakini hakutaka  kufika hatua ya kufanya mapenzi kwa haraka sana.

Lakini  baada ya kukaa kwa muda wa dakika kumi na tano  alitoka  na hapo  ndipo aliposhangaa mara baada ya kumkuta Hamza ashajirusha kwenye sofa na anakoHamza , akiwa usingizini, alijikuta akipatwa na ahueni na alirekebisha AC na kisha akachukua blanketi na kumfunika na kuingia chumbani kwake.

Lakini  wakati huo sio kwamba Hamza alikuwa amelala , alijifanyisha  alikuwa  amelala tu ili  kutokumfanya  mrembo huyo kuwa na wasiwasi.

Baada  ya  nusu saa kupita ndio alipotelea usingizini na anajikuta anaota ndoto ya ajabu mno.

Previoua Next