Reader Settings

SEHEMU  YA 17.

“Mwenzetu , unalalaje usingizi mzito hivyo?”Aliongea  Eliza mara  baada  ya Hamza kuamka.

Hamza bado akili yake ni kama ilikuwa imetawaliwa na ndoto aliokuwa ameota na aliishia kumwangalia tu  Eliza.

Akili yake ilianza kukusanya matukio na alikumbuka  jana alilala kwenye sofa na sio kitandani  na hio ni mara baada ya kukisi na mrembo huyo na akakimbilia  chooni.

“Mbona huongei chochote Hamza , umeniogopesha ujue kwa namna nilivopata shida ya kukuamsha”

“Babe , unajua wewe ni mrembo mno”Aliongea Hamza akijitahidi kurudi katika hali ya kawaida na kupotezea  kile alichoota, kauli ile ilimfanya  Eliza kusahau hata  namna alivyopata shida ya kumuamsha Hamza na alishikwa na viabu vya kike.

“Umeniitaje?”Aliuliza na kumfanya Hamza kutoa tabasamu.

“Tumeshakiss tayari  na kugusana , sidhani kama ni  kosa kukuita mpenzi”

Eliza hakujua hata namna ya kujibu kwani hakuwa  akichukia pia kuitwa mpenzi , ukweli alijisikia vizuri.

“Muda umeenda , nenda kaoge na kusafisha kinywa   upate kifungua , kinywa”Aliongea  kupotezea ile hali.

Hamza mara baada ya kufika chooni hatimae alivuta pumzi nyingi na kuzishusha , alikuwa akijitahidi kuwa sawa mbele ya   Eliza lakini bado ni kama  akili yake imetawaliwa na kile alichoota.

“Bwana eh ,  ni ndoto tu kama ndoto

nyingine”Aliongea  na kisha aliangalia mazingira  ya choo hicho na aliweza kuona taulo  pamoja na mswaki na  dawa ya meno  vikiwa vimewekwa , ilionekana Eliza alishaandaa kwa ajili yake.

Alijisikia viuri kwa kuona  E.liza ni mwanamke anaejua kujali mwanaume, kwa muda mrefu hajahudumiwa na mwanamke mrembo.

Mara baada ya kuoga  na  kujifuta  alirudi na  kuungana na Eliza kwenye meza kwa ajili ya kifungua kinywa , kulikuwa na   mayai ya kukaanga ,  chapati na supu ya kuku.

“Hizi chapati umepika?”Aliuliza.

“Hapana nimenunua kwa jirani hapo anatembeza , huwa mimi sio mtu wa kukaa  sana nyumbani , sio

kwamba sijui kupika chapati ila mahitaji sina”Aliongea akionekana kama vile anajitetea.

“Sijamaanisha hivyo?”

“Kwanini sasa  na muonekano huo?”

“Ni kwamba sijapata kifungua kinywa  nje na ninapoishi kwa muda mrefu sana”

“Oh , kama  ni hivyo unaweza kuja mara kwa mara nitakupikia”

“Kwahio unamaanisha unataka  tuishi pamoja”Aliuliza Hamza huku akicheka. “Wewe , sijamaanisha hivyo”Aliongea huku akiona  aibu na kujiambia   ni mjinga kwanini kuongea kauli ya aina hio   yenye  utata.

Hamza alipiga supu hio  nzito na  kupotezea kabisa swala la ndoto , hakutaka kujihangaisha nalo kwanza alikuwa na mambo mengi kichwani ikiwemo swala  la kumtafuta Mzee.

Baada ya kumaliza kifungua kinywa  Eliza alipaswa kuelekea kazini  na  Hamza mara baada ya kuangalia ratiba  chuo aligundua alikuwa  na kipindi saa nne, hivyo aliona huo ni muda wa kuondoka kwenda chuo akapoteze poteze muda.

Eliza alitumia gari la kampuni na alimpa Lift Hamza mpaka Tazara na kisha alichukua dalalada kuelekea chuo.

Licha ya kwamba hakuwa na mudi  alienda kwasababu kipindi cha saa nne ni cha  Profesa Singano mzee wa bonus point.

Hakukuwa na foleni kubwa sana na alitumia kama dakika ishirini hivi mpaka kufika chuo na mara baada ya kushuka alianza kutembea  taratibu taratibu kusogelea geti la chuo.

Lakini kabla hata hajalifikia Toyota Corola ilifika na kusimaa pembeni yake na kioo cha mbele kikashushwa na dakika ile wanaume watatu walitoka katika gari ile.

“Hamza Mzee , ndio wewe”Aliongea mmoja ya wale  watu  mwenye mwili mkubwa kidogo  na Hamza aliitikia kwa kutingisha kichwa.

“Sisi ni polisi kituo cha mjini kati , upo chini  ya ulinzi kwa kosa la uhalifu”Aliongea mmoja ya wale polisi na kisha alimsogelea Hamza kwa nia ya kumshikilia.

Jambo lile lilimshangaza Hamza maana hakujua hata ni uhalifu upi ambao amefanya mpaka kuja  kukamatwa na polisi asubuhi yote hio.

Hamza hakutaka kuvuta attention  ya watu na   alikubali kistaarabbu na kisha  aliingizwa kwenye  ile gari  na ikaondoshwa kwa haraka.

Dakika chache mbele gari ile ilipita Gerezani  na kusonga mbele , jambo ambalo lilimshangaza  Hamza.

“Afande si mmesema  mmetokea  kituo cha mjini kati?”Aliuliza Hamza.

“Acha uboya dogo , kituo cha mjini kati umekisikia wapi, tunakupeleka chimbo kukushikisha adabu”Aliongea moja ya  bwana mwenye sura ngumu na kumfanya  Hamza sasa kuelewa  kinachoendelea.

Hakutaka hata hivyo kuleta vurugu kwenye gari hio na aliacha kuona mwisho wake.

Foleni ilikuwa hakuna kabisa hivyo gari hio ilitembea kwa spidi kubwa na ndani ya dakika kadhaa waliipita Mbagala  na kufuata njia ya kwenda Kongowe na kisha gari ile ikakunja kushoto na kuingia katika barabara ya Vumbi na kusonga mbele na ilikuja  kupita Bar moja ambayo Hamza hata hakusoma jina lake ila ilienda kusimama  nje ya moja ya jengo ambalo lilikuwa limezungushiwa ukuta na kisha ikaingia ndani.

Kitendo cha gari ile  kusimama tu  na mlango kufunguliwa hatimae Hamza alijua  nani amekuja kumkamata,ilionekana  bwana aliemshikisha adabu  jana yake  ndio ametafuta tena  ugomvi.

Zefa ndio aliekuwa mbele yake , akiwa amezungukwa na vijana wengine , haikueleweka eneo hilo lilikuwa  ni kwa ajili ya  nini lakini Hamza alijua tu hio ni ngome ya kihalifu.

“Wewe boya , nadhani jana maneno yangu uliyasikia vizuri , nilisema lazima nikushikishe adabu , sasa leo utapata kipigo mara  mia ya kile ulichonifanyia jana”Aliongea  Zefa kwa hasira.

“Unajifanya  kidume sana , mwanamke niliemhangaikia kumpata kwa muda mrefu wewe   hujafanya juhudi yoyote unalala nae kizembe , leo  utanitambua, Vijana mpigisheni magoti”Aliongea kwa hasira mno  na sasa Hamza aliona hasira yake  bwana huyo ilionekana imechanganika na  wivu.

Lakini kaba hata ya vijana wale hajaanza kumshugulikia Hamza  honi ya gari ilisikika nje  na ndani ya sekunde kadhaa tu geti lilifunguliwa na gari aina ya Mercedenz iliingia ndani.

Vijana waliokuwa wapo tayari kwa ajili ya kumshughulikia Hamza walikakamaa na nyuso zao   kuwa na wasiwasi.

“Madam!!”

Moja  ya bwana  ambae ndio alifika na kumkamata  Hamza  akijifanyisha polisi aliongea  na kusogelea ile gari.

Muda uleule  mlango wa gari ile  ulifunguliwa na  viatu vyenye visigino virefu  vilianza kuonekana kabla ya mwili wote.

Mrembo Dina  ndio ambae alitoka kwenye gari hio  na kufanya vijana wote wamwangalie  kwa heshima , hakuna kijana ambae alikuwa jasiri  wa kwenda kinyume na Dina , walikuwa wakimjua vizuri ukatili wake licha ya kwamba alionekana mpole na mrembo kupindukia.

“Madam  kwanini umekuja mpaka huku,  hakuna taarifa kwamba leo utatutembelea”Aliongea yule bwana  kwa heshima  huku akifosi tabasamu , lakini alionekana kuwa  na wasiwasi .

Zefa hata yeye alikuwa akimjua  Dina  na siku zote  licha ya ubabe wake na kupenda kwake wanawake kwa Dina hakuwahi hata kuwaza kumtongoza.

Dina  alionekana alikuwa na haraka sana  na aliangalia mazingira kwa sekunde kadhaa na kisha alipotezea swali lile na  alimsogelea Hamza na kusimama mbele yake na kuinamisha kichwa.

“Samahani , sijatarajia swala kama hili litatokea”Aliongea Dina kwa heshima mbele ya Hamza.

Genge lile  ikiwemo  Zefa mwenyewe walishikwa na butwaa  kwani hawakuelewa ni  kipi kinatokea  mbele ya macho yao.

Dina malkia  na mmiliki wa kundi la Chatu alikuwa akionyesha heshima mbele ya Hamza?, mwanamke mrembo ambae  viongozi wa  kisiasa na wa jeshi  walikuwa nyuma yake, lakini leo  hii  anaomba msamaha mbele ya  mtu kama  Hamza.

Wanaume hao watukutu walikuwa wakitamani hata kumwangalia mrembo Dina kwa ukaribu , walikuwa wakimhusudu mno lakini licha ya kuwa na utofauti mkubwa kati yao na Hamza  lakini  aliekuwa akipewa heshima ndio yeye.

Sasa tukio lililofuatia ndio liliwashangaza zaidi kwani  Hamza alimshika Dina kidevu na kukiinua juu , kama vile  ni mfalme mbele  ya masuria wake.

“Dina  kwanini unaomba msamaha , mimi ndio nilifanya fujo na kumpiga mtu na hata sasa hawajanifanya chochote”Aliongea Hamza.

“Kwahio  huna hasira yoyote  na mimi?”

“Haha.. kwanini niwe na hasira , kama ningekuwa na hasira  nisingekutumia ujumbe  wa maandishi”Alionngea na Dina alionekana kuvuta pumzi ya ahueni.

******

Regina hakuwa na kikao asubuhi hivyo  hakuharakisha  kwenda kazini  na saa nne ndio muda alioshuka  chini  kwa ajili ya kupata kifungua kinywa , hakuwa na wasiwasi wowote  na baada ya kifungua kinywa alikaa kwenye sofa na kuangalia habari za kimataifa huku akila tunda la shufaa kimapozi.

Shangazi alionekana kuwa  bize na alionekana akitoka nje akiwa ameshikilia nguo ambazo zimekwisha kukauka , zilikuwa ni nguo za Hamza alizofua jana na kuziacha.

“Regina, jana umemfukuza Hamza  na hakurudi kabisa na nguo zake pia hajachukua , ukute amelala mtaani huko”Aliongea  na sasa ni kama vile  Regina  anamkumbuka Hamza kwani alishikwa na mshangao. “Hivi kumbe  jana aliondoka kabisa na hakurudi?”

“Ndio , chumba chake kipo wazi usiku mzima ,  sijui hakuna kilichomtokea , kwanini usijaribu kumpigia simu  na kumuuliza yupo wapi?”Aliongea.

“Mtu mzima kabisa yule  , hakuna chochote cha kumtokea , pengine ukute amelala alikokuwa akiishi”Aliongea Regina akiwa sio mwenye ishara ya kujali kabisa lakini ilikuwa tofauti kwa  Shangazi.

“Nadhani hutonichukia  kwa kuongea kwangu sana ,  lakini jana  Hamza aliongea  vile mpaka ukakasirika kwasababu ya maisha aliopitia”Aliongea na kumfanya Regina kumwangalia Shangazi kwa shauku kidogo.

“Unamaanisha nini Shangazi?”

“Hebu fikiria hata wewe , hana wazazi na tokea akiwa mdogo amekuwa peke yake, pengine ana hamu  kubwa  kutaka kuwa  hata na wazazi kama ilivyokuwa kwako , pengine  kwa kukosa  wazazi ameshikwa na uchungu kwa namna wewe na baba yako mlivyokuwa  mkijibishana jana , sidhani  hata kama akitaka baba wa kubishana nae anaweza kupata”

“Shangazi kwahio unamaanisha ni Yatima?”Aliuliza  Regina huku akishangaa  na kumfanya kuwa mzuri zaidi lakini kauli yake ilimshangaza  Shangazi.

“Inamaana  wewe hukuwa ukijua?”

Regina  aliishia kumumusa lipsi zake na alikumbuka namna alivyomfukuza   jana  Hamza,  alionekana kuelewa kwanini Hamza alitaka kuzungumzia swala la baba yake.

“Ngoja nijaribu kumpigia”Aliongea  na kisha akachukua simu yake.

“Shangazi  wewe ndio unataka  nifanye hivyo , ila sio mimi ninaetaka kumpigia”Aliongea Regina kama vile ni mtu ambae anajihami  lakini kauli yake ilimfanya Shangazi kutabasamu na kutingisha kichwa.

Baada ya kuipiga namba ya Hamza  hatimae iliita  na kumfanya akohoe kidogo kusaficha koo na kweli muda uleule simu ilipokelewa.

“Uko wapi?”Aliuliza  Regina kistaarabu.

“Nipo kitaa” Sauti  ya kikauzu ilisikika.

“Najua upo kitaa , nauliza upo kitaa gani?”

“Kuna shida?”

Kauli ile  ilimfanya Regina kukunja sura , alitaka kujali kuuliza amelala wapi usiku  lakini  sauti ya Hamza ilimfanya kupotezea wazo hilo.

“Hakuna shida.. nauliza tu”

“Kama huna cha kuongea  nakata simu”

Bila hata  ya kuongea simu pale ilikatwa 

Mrembo huyo sura yake ilibadilika na kwa hasira aliweka simu chini kwa nguvu  na kisha aling’ata pande la Apple  kwa hasira kama kwamba tunda hilo limemkosea.

“Shangazi , haina   haja ya kumjali , muache na maisha yake”Aliongea  

Shangazi Mariposa  alijikuta akitingisha kichwa , aliona ni bora  asingependekeza wazo la  Regina kumpigia simu.

Previoua Next