Reader Settings

DOSARI 

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Uhalifu, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

 SEHEMU YA NNE

★★★★★★★★★★★★★

Ikiwa ni kwenye mida hiyo hiyo ya saa tano usiku ndani ya kumbi moja kubwa ya starehe jijini, mwanaume fulani mtu mzima anaingia hapo akiwa anatembea taratibu na kwa kujiamini kuelekea ngazi zinazopanda hadi ghorofa ya kwanza ya jengo. Kuna umati wa watu wenye kujifurahisha, muziki mnene, pombe, wanawake wazuri wenye kuvaa kwa njia ya kujiachia kuvutia wanaume, na taa zinazobadilika rangi kwa mizunguko zinafanya kuwe na mwonekano bomba sana. Siyo sehemu wanayoingia watoto, na mwanaume huyo akiwa tu ndiyo amezifikia ngazi tayari ameshaanza kushikwa-shikwa na wanawake baadhi wanaouza miili yao, kujaribu kumvutia kwao, lakini anawapuuzia na kuendeleza hatua zake. 

Anapanda ngazi hizo kwa mzunguko hadi kufikia juu, ambapo napo pana mwonekano wa aina ile ile isipokuwa tu viti na meza; hapo juu ni masofa zaidi ndiyo yamezunguka meza fupi za kioo. Kwa hakika ndiyo sehemu ambayo wanakaa wale waonwao kuwa na pesa nyingi, hata gharama za vinywaji na wanawake hapo ni ghali, hivyo hakuna mtu anayesogea kizembe. Kuna baunsa maalumu anayelinda mwingilio, na baada ya mwanaume huyu kumfikia, anaunganisha naye kiganja kwa njia ya kirafiki tu, kisha baunsa anamwachia njia asonge mbele zaidi. 

Kuzungukia sehemu yote ya ghorofa hiyo walikaa wanaume wenye kuponda raha na wanawake walioenda shule, yaani wazuri, viuno na makalio vikitikiswa kwa waliosimamia wanaume zao, pombe za maana zikiwekwa hapo, na mwanaume huyu aliyefika sasa alikuwa akiwapita tu na kuelekea kwenye kona mwishoni zaidi ambapo mwanaume mwingine aliketi sofani kwa utulivu. Huyo aliyekaa alikuwa mtu mzima pia, akivalia koti gumu jeusi na kofia iliyopindia upande mmoja wa kichwa chake, akinywa kileo kikali kutoka kwenye glasi, huku chupa ya kileo hicho ikiwa mezani. 

Mwanaume huyu aliyefika hapo akasimama kwanza, na huyo aliyekaa akamwangalia na kusema, "Vipi?" 

"Safi boss. Nakuona," aliyesimama akamwambia hivyo huku akitabasamu kiasi.

Huyo "boss," akaangalia saa yake mkononi na kusema, "Kaa sasa. Muda ninao kidogo leo, nataka niwahi."

Akiwa anasogea kuketi, aliyeingia hapo akasema, "Ningefikiri unapanga kulala kabisa hapa, chupa nzima!"

"Ah, inaisha sa'hivi tu. Karibia pia," bosi akasema hivyo.

"Asante, kwa leo nimefunga," mwenziye akamwambia.

"Au siyo? Unaweka kichwa straight kwa ajili ya nini?" 

"Ukiwa kwenye line ya kazi kama yangu mkuu, kuangalia nyuma ya mgongo wako kila mara inakuwa jambo must, kwa hiyo... lazima kujiweka makini muda wote."

"Acha mambo yako wewe! Unataka kusema hujanywa kabisa tokea jana... kama siyo leo leo? Wewe Chomoka?" bosi akauliza hivyo.

Mwanaume huyu aitwaye Chomoka, akacheka kidogo.

"Mimina bana, acha bangi," bosi wake akamwambia hivyo.

Kweli, Chomoka akavuta glasi iliyokuwa pembeni na kuanza kuimiminia kinywaji.

"Uwe care kama we' ni mchanganyaji, haina urafiki na koo hiyo," bosi akamwambia.

"Ah, bado sana. Hakuna inayonisumbua kihivyo, sijaona," Chomoka akasema na kisha kunywa kileo kavu kavu.

Bosi wake akanywa pia.

Chomoka akaangalia upande uliokuwa na wanawake wazuri, ambao waliangalia upande huu pia, naye akauliza, "Mbona hujaita mtoto hata mmoja?"

"Time. Leo siyo siku yao," bosi wake akamwambia.

Chomoka akatabasamu na kusema, "Safi sana. Ukiwa makini na muda huwa hutikiswi, hata na kalio yaani..."

"Hahah... hao wapo tu, kama unataka kuita ni wewe. Ila sasa tufanye kilichotuleta hapa kwanza, mengine baadaye" bosi akasema.

Chomoka akatikisa kichwa kukubaliana na hilo.

"Vipi kazi?" bosi akauliza.

"Fresh," Chomoka akajibu.

"Vijana?"

"Wako good. Kila mmoja ashalipwa."

"Na umeshawapanga kuhusu...."

"Ndiyo, kazi nyingine ikitokea wako tayari kukutana. Ni suala la lini na wapi, tunajua jinsi gani ya ku-handle, kwa hiyo hamna shida hapo," Chomoka akasema.

"Sawa. Kwa hiyo mambo yako poa, na yameenda vizuri so far. Ulitaka tuzungumzie nini sasa?" bosi wake akauliza.

Chomoka akaweka glasi ya kileo mezani, kisha akasema, "Morgan."

Bosi wake akatulia na kuendelea kumwangalia.

"Morgan anazingua boss. Haniheshimu, na hii siyo mara ya kwanza nakwambia hivi..."

"Najua."

"... yaani, concept yote ya mimi kuwapa amri vijana inamkera. Yeye anafikiri ukimpa order sijui unakuwa unam...."

"Amefanya nini? Usizunguke sana, shida nini?" bosi wake akamkatisha.

Chomoka akasema, "Ile ishu ya dukani ingekwenda mrama kwa upande wetu boss kwa sababu ya ujeuri wa Morgan. Kama ulivyoagiza, tulitakiwa kubeba vile vitu, tulichome duka, wale security tuachane nao. Lakini jamaa alitaka tuwaue, oh hapana... alikuwa anataka kuwaua yeye mwenyewe. Na akafanya hivyo ili ajiridhishe tu."

Bosi wake akatafakari kidogo, kisha akavuta glasi yake na kusema, "Sawa. Ndiyo kilichokukasirisha hicho, au kuna kingine?"

Chomoka akamwangalia kwa njia ya kushangaa kiasi.

Bosi wake akanywa kileo na kusema, "Unajua hiyo ni nature ya Morgan, wala hata sishangai. Hakuna shida kama alifanya hivyo ili kusiwe na... loose ends... inaweza ikasaidia..."

"Hapana, boss... tulikuwa tunaenda na muda. Kila kitu kilikuwa kimekamilika, tulitakiwa kuondoka, yeye akataka kuburudika eti... awaue, ajifurahishe, halafu mbaya zaidi... nilipomsisitizia kwamba hakuna sababu ya kuwaua, ili tu kuni-provoke mimi, akaamua kuvua mask makusudi ili atokeze sababu ya kuwaua. Halafu akawaua vibaya, yaani kama mnyama mkati... me mpaka nashindwa kuelewa ulimtoa wapi huyo mtu!" Chomoka akaongea kwa mkazo lakini kwa sauti ya chini.

Bosi wake akatabasamu kiasi na kunywa kidogo, naye akasema, "Damu bado inachemka baina yenu eti? Na yeye alivyo mbabe basi inakukera..."

"Please chukulia hili seriously..."

"Chomoka, achana na Morgan. Ndivyo alivyo. Anafanya hivyo makusudi tu... kama ulivyosema, kuku-provoke, maana nimemweka chini yako... lakini anajua hatakiwi kufanya lolote kulitia tumbua letu mchanga..." bosi wake akamwambia.

Chomoka akaangalia pembeni kwa kuudhika.

"Hakuna chochote kilichofanyika kitakachoharibu lolote. Kama ishu ni kuwaua hao security, haina umuhimu bro. Wameshakufa. Imepita. Mali tumechukua. Tupo secure. Naona kilichopo hapa ni tension mliyonayo nyie wawili tu ndo' inasumbua nerve zako, lakini Morgan yuko vizuri sana. Hata we' unajua hilo," bosi wake akamwambia.

Chomoka akatikisa kichwa kwa kukerwa.

"Kama kazi ilikuwa imeshakamilika na mkatoka fresh... fresh. Akitaka kuwaua hao wapumbavu, mwache awaue. Sikusema ni lazima muwaache hai. Na ndiyo, Morgan siyo wa nchi hii. Nimemtoa Jamaica huyo, kwa hiyo angalia usije kumpandishia bangi siku moja akakugeuza kama hao security... hahahah..." bosi wake akaongea kwa njia ya utani.

"Na wewe utakuwa sawa na hilo kwa sababu tu 'Morgan yuko vizuri?'" Chomoka akamuuliza.

"Punguza hasira Chomo, haina maana. Potezea," bosi wake akamwambia hivyo na kuvuta glasi yake ya kileo.

Chomoka akamwangalia kwa njia makini, kisha akasema, "Kulikuwa na jengo lenye ATM kuvuka barabara kutokea pale tulipokuwa."

Bosi wake akashusha glasi na kumtazama kwa umakini.

"Unajua hiyo inamaanisha nini?" Chomoka akauliza.

"Camera," bosi wake akajibu.

"Ndiyo. Wakati tunaondoka Limbe ndo' akaiona hiyo ATM, ikabidi baadaye kwenda kuzivuruga camera za pale maana zilikuwa zinaangazia mpaka ule upande tuliokuwa," Chomoka akamwambia.

"Mlizivuruga camera wakati tayari zilikuwa zimesharekodi...."

"Simaanishi muda huo huo, ila... sikukwambia, yaani... ilibidi siku iliyofuata niende pale kumlipa msimamizi wao mmoja afute footage za usiku uliotangulia. Nimetoa pesa yangu mwenyewe ili kumziba mdomo na kuziondoa hizo tape boss, la sivyo ingekuwa story nyingine hapa sasa hivi," Chomoka akamwambia.

Bosi wake akatulia kwanza kutafakari hayo.

"Umeona nilivyokuwa nakwambia? Huyu mtu wako atakuja kutu-cost boss. Usinione mjinga mimi kuja kusema haya. Nikimwambia afanye au asifanye hivi ananiona me bwege-fala sijui, ile kujipa ukubwa fulani hivi, basi hasikilizi order. Kwa nini, kwa sababu anatokea kwa wajamaica? Anataka wengine wamwogope yeye zaidi kwa kujifanya anajua sana ukatili. Yuko vizuri, lakini anajiamini kupita kiasi, na tusipoangalia... atakuja kutuangusha. Na nimeshamwona kuwa mtu ambaye akianguka, atakuangusha na wewe boss..." Chomoka akasema hayo.

Bosi wake akabaki kukunja uso tu.

"Nakwambia. Hafai," Chomoka akasisitiza.

Bosi wake akatulia kidogo, kisha akauliza, "Kwa nini hukuniambia hayo mapema?"

"Nilikuwa nangoja hali zitulie. Wewe ndo' umenipa niwasimamie hawa, siyo rahisi maana kila mmoja wao ana akili ya kivyake. Lakini wenziye huwa wanafata order tukiwa kwenye mission, yeye ndo' ana kichwa kigumu. Kama hiyo tumbua ingeingia mchanga, wewe ndiyo ungekula hasara, na mimi najua ningeumia. Nilitaka kuhakikisha hiyo haitokei ndiyo sababu nikai-handle kimya kimya," Chomoka akasema.

"Una uhakika hakutakuwa na shida kwa huo upande wa ATM?"

"Hamna, hapo hamna shida tena..."

"Tunapaswa kuangalia possibility kwamba huyo uliyemlipa anaweza kuja kufungua mdomo wake baadaye... hata akawaambia mapolisi kuhusu wewe. Hilo utali-handle vipi?" bosi wake akamuuliza.

Chomoka akatulia kidogo, kisha akasema, "Umeona?"

Bosi wake akabaki kumwangalia kwa umakini.

"Bado tunakaa kusumbua akili, tena kusumbua akili yako kwa sababu ya upuuzi alioufanya huyo jamaa. Usingekuwa hata unawaza hivyo kama asingefanya ule ujinga, hapa tatizo siyo ATM wala msimamizi... shida unajua ni kwamba kama akifikiwa, yeye ndiyo ataweza kusema sisi ni nani," Chomoka akasema hivyo.

Bosi wake akatazama pembeni kwa umakini.

"Hii imetokea kama bahati tu sa'hivi hatusakwi moja kwa moja, lakini inaweza kuja kuwa mbaya tena muda mwingine ukituleta pamoja kwa ajili ya kazi. Itabidi udili nalo hili vizuri," Chomoka akamwambia.

Bosi wake akashusha pumzi na kusema, "Unanishaurije?"

"Me siwezi kukupangia. Chochote unachoamua me nafata," Chomoka akamwambia.

Bosi wake akasema, "Namjua Morgan vizuri. Na ni wa muhimu kwetu, kwa hiyo... siwezi kufikiria kufanya jambo kama kumwondoa asiwe nasi kwenye kazi tena..." 

"Ukimwondoa kwa namna hiyo kuna chance anaweza kutusaliti boss, siyo wazo zuri. Ukifanya kumwondoa... inabidi iwe kumwondoa kumwondoa," Chomoka akasema hivyo.

"Nini? Kwamba tumuue?" bosi akauliza.

Chomoka akapandisha mabega yake tu.

"Unafikiri ni jambo rahisi tu kufanya hivyo? Yule jamaa ni mta...."

"Najua," Chomoka akamkatisha.

"Kwanza kwa nini mpaka uwaze hivyo? Usisahau tuna mengi ya kufanya, ni mwenzetu, na..."

"Boss, Morgan ni tatizo. Najua unajua Morgan ni tatizo, achana na fikira za tunamhitaji sijui, sikuzote wapo watu wengine walio makini tunaoweza kuongeza. Huyu jamaa atakuja kutuharibia, I swear. Me ndo' namwona, namjua zaidi maana nipo kwenye field pamoja naye. Sisemi ni lazima mpaka.... kumuua... najua siyo rahisi, ila kama ni kumwondoa, inabidi tu tumwondoe boss. Kwa njia moja ama nyingine," Chomoka akasema.

"Kwa nini unasisitizia hilo?" bosi wake akamuuliza.

"Kwa sababu sitaki uanguke. Nakuita boss, lakini wewe ni rafiki yangu, Francis. Najua unapotoka, na najua unapotaka kwenda. Yeye hajui mengi, anajali tu anachopokea mradi anafanya kazi yake. Kitendo alichofanya juzi hapo... inapaswa iwe mwisho. Ni uamuzi wako tu iweje lakini," Chomoka akamwambia hivyo na kuvuta kinywaji chake.

Utata ndiyo ulikuwa penyewe hapo, na hizi ndizo zilizokuwa siri za mitungini! Kiongozi mkuu wa kundi lile la majambazi hakuwa mwingine ila Francis mwenyewe, rafiki yake Reuben. Aliachana na masuala ya msiba wa mke wa mwanaume yule ili abaki kushughulika na mambo yake haramu ambayo, kama Josephina tu, hakuna watu wengi waliofahamu kuyahusu. Alilimiliki kundi hilo la majambazi kutokana na kuwa na pesa nyingi kutonana na mishe nyingi haramu, na walifanya kazi alizowatuma kufanya ili wapate faida kwa hasara za wengine, aidha kwa kuiba, ama kwa kuua watu ili wapate pesa. Na sasa akawa amebaki kutafakari maneno ya "rafiki" yake huyo, Chomoka, yakiwa yamemwingizia mambo mengi ya kufikiria ili afikie uamuzi sahihi wa jinsi ya kushughulika na jambo hili alilomletea. 

Chomoka akaendelea tu kutulia na kumsikilizia. Huyu ndiye yule mwanaume aliyewaongoza wale majambazi usiku ule kufanya wizi na kulichoma duka la Stanslaus Mwita, na hapa sasa baada ya tukio hilo kuwa limepita ndiyo alikuwa akizungumza na bosi wao kuhusiana na vitendo vya mwenzake mwenye jeuri ya kinyama. Yule mwanaume mwenye rasi. Morgan. Chomoka alikasirishwa sana na matendo ya mwanaume yule, na akiwa anataka kumkomesha baada ya siku ile Morgan kumwonyesha hakujali kuhusu uongozi wake, Chomoka sasa akawa amemchongea kwa bosi wao. 

Na ilikuwa ni kuchongea kwa hila kabisa kwa sababu alipoona Francis hachukulii kwa uzito tabia za Morgan na hata kumtetea, Chomoka akatia uwongo huo wa jengo la ATM ili kumfanya bosi wake afikiri kuwa kweli Morgan aliwatia ndani ya hatari ya kufichuliwa; na angeweza kufanya hivyo hata wakati mwingine. Hivyo sasa Chomoka akatulia ili kuona ni hatua gani ambayo Francis angetaka ichukuliwe dhidi ya huyo Morgan wa Jamaica, akibaki na matumaini kwamba ataondolewa kabisa-kabisa kundini mwao na yeye ndiyo abaki kuwa sauti kuu kwa majambazi wenziye. 

Huyo ndiyo alikuwa Francis!


★★★


Upande wa jumba la starehe lililomilikiwa na Josephina, au kama alivyopenda aitwe na waliomfanyia kazi, madam Phina. Ikiwa ni muda mfupi tu baada ya Paulina na wanawake wengine kuletwa kwenye jengo hilo, walitambulishwa kwa mwanamke huyo ambaye ndiye aliyetakiwa kuwa mheshimiwa kwao. Josephina aliachana na msiba wa Reuben ili kuendelea na mambo yake haya, kama tu Francis kule, akija huku mida ya usiku wa mapema baada ya kumwacha mwanaye nyumbani, na sasa ndiyo akawa ameupokea mzigo wake huo wa wanawake walioletwa ili aanze kuutumia kujiingizia faida.

Baada ya kuweka msingi wa utambulisho wake kwa wanawake hao wapya, sasa ingekuwa ni kuwapatia maelekezo ya namna ambavyo biashara hapa zilikuwa, kisha awapitishe kwenye "madarasa" muhimu kuwawezesha kuzoea mazingira ya hapo upesi ili fursa ziwachangamkie haraka. Yaani wateja. Wanaume. Isaya alikuwa pamoja nao bado ndani ya ofisi hiyo Josephina alipomaliza utambulisho wake kwa madaha, na sasa kazi ingeanza. Akawaangalia mmoja baada ya mwingine, akiwa anawapima kwa macho yake, na yalipotua kwa Paulina, Josephina akamkazia uangalifu kwa kumshusha na kumpandisha huku akiguna mara kadhaa kama kuonyesha mshangao.

"Eh! Wewe... huyu mtoto mmemtoa wapi?" Josephina akamuuliza Isaya hivyo kwa njia ya kustaajabu.

Paulina akabaki kumwangalia kwa ugeni sana.

Isaya akamwambia, "Ndo' aliyemtuma Rozalia. Amefika leo."

Josephina akamwangalia Paulina na kusema, "Ah! Aisee, nyama nzuri hii! Baby, utanibariki sana. Ulikuwa wapi huo muda wote wa maisha yangu?"

Isaya akatabasamu.

"Huyu tunamweka level 5, unanielewa? Ni wa pochi nene tu," Josephina akamwambia Isaya.

"Hiyo ni uhakika madam. Hawaonji wengine hapo," Isaya akasema.

"Kweli. Roza amefanya kweli. Licheki kwanza. Hebu nipe 360 baby..." Josephina akamsemesha Paulina hivyo na kumsogelea.

Paulina akabaki tu kumwangalia.

Josephina akamwangalia pia na kusema, "Mtoto changamka basi!"

Bado, Paulina akatulia tu.

"Vipi, ni bubu?" Josephina akamuuliza Isaya.

"Hamna, anaongea. Ni ugeni tu madam... anakuogopa," Isaya akasema hivyo kumpamba Josephina.

Josephina akamwangalia Paulina tena.

"Zunguka madam akuone, hiyo ndiyo 360," Isaya akamwambia Paulina hivyo.

Paulina akaonekana kubabaika kiasi na kuendelea tu kumtazama Josephina usoni.

Josephina akamwangalia Paulina kwa uvutio, naye akamshika mabegani na kusema, "Oh... usiogope baby. Hapa jijini, umefika. Mali kama wewe ya uhakika, yaani unawaona hawa wote... hawajafika kwako. Kwa hiyo jiachie kabisa mpenzi, hii ndiyo himaya yako, kuua utaua yeyote unayetaka, sijui unanielewa?"

Paulina, akiwa hajaelewa, akauliza, "Kuua?"

Josephina na Isaya wakacheka kidogo, na mwanamke huyu akasema, "Ulivyo huna clue... safi sana. Nisikilizeni nyote..."

Wanawake waliokuwa hapo wakamkazia uangalifu.

"Hakuna kigeni kwa mwanamke yeyote anayefika hapa jijini hata kama ndiyo mara ya kwanza, mbele ya mwanaume wewe tayari unajua kila kitu. Mazingira mtayazoea haraka, tuna makocha wa kutosha. Kikubwa ni nyie kuwa tayari kufanya kila kitu kuingiza wateja na kuhakikisha wanarudi kwa raundi saba zaidi. Sijui mnanipata?" Josephina akaongea, ki-madam zaidi.

"Ndiyo..." wachache wakajibu.

"Ndiyo nini?" Josephina akauliza.

"Ndiyo madam," Paulina akawa wa kwanza kujibu.

Josephina akamwangalia na kusema, "Namna hiyo."

Paulina akatazama chini tena.

Josephina akasema, "Mnajua mnachopaswa kufanya, mmeshafanya sana toka zamani, ila hapa mtatakiwa kuwa ma-professional. Tuna utaratibu wa kufata, kila mmoja wenu anapaswa kuufata. Mtakula na kulala hapa lakini mnajua mjini hakuna cha bure. Wanaume wanakuja, hata wakiwa na wake zao, mnapaswa kuhakikisha hawaondoki bila kuwachomolea mtonyo. Huo mtonyo mnapaswa kuufikisha kwangu, na nyie mnalipwa kwa asilimia kuendana na kila kitu mnachopata hapa; kuanzia make-up, nguo, viatu, chakula, mpaka toilet paper mtazotumia chooni..."

Loh! Wanawake wapya wakaendelea tu kutulia, wakiona ukali wa aina yake ndani ya bosi wao huyo mpya.

"Malipo kwa bajeti. Sijui mnanielewa? Uwe na sura mbaya au nzuri, tako kubwa ama dogo, hakikisha... agh, mnaelewa. Sidhani kuna mengi zaidi ya kueleza. Sipendi mambo ya kujivuta-vuta, mkiona mtu ni msumbufu, mnaachana naye. Akisumbua zaidi, mnamjua Isaya. Kazi, matokeo. Sijui mnanielewa?" Josephina akaongea kwa uthabiti.

Wanawake wakatikisa vichwa kukubali na kuendelea tu kumtazama kwa umakini.

"Secy yuko wapi?" Josephina akamuuliza Isaya.

Isaya akaangalia saa mkononi na kusema, "Atakuwa ashafika. Nikamwite?"

"Hamna. Wapeleke hawa kwake aanze kuwapanga. Me kichwa kinauma sa'hivi," Josephina akasema.

"Sawa," Isaya akajibu.

Akawaonyesha wanawake ishara kwa kichwa kuwa wamfuate. Walipoanza kutoka ndani ya ofisi hiyo kumpita mwanaume, Josephina akamshika Paulina mkononi kumzuia kwanza, na mwanamke huyu akamwangalia.

"We' ni keki, binti. Utakuwa na wenzio naowapendelea huko juu, achana na hayo majinga. Fanya kazi ya maana kweli, utatoka na pesa nyingi sana," Josephina akamwambia kwa njia yenye ushawishi.

Paulina alikuwa akihangaishwa sana na haya yote moyoni, lakini akajikaza na kutikisa kichwa kukubali. Josephina akamwachia, na mwanamke huyo akampita Isaya kuelekea nje.

Isaya alikuwa akiangalia umbile zuri la Paulina kwa nyuma, kisha akamtazama Josephina na kusema, "La moto!"

Josephina akazungusha macho na kuangalia pembeni, naye Isaya akatabasamu kiasi na kuanza kutoka pia. Ila kabla hajaufunga mlango, mtu mwingine akawa amefika hapo, na jamaa alipomwona akauachia mlango na kumtikisia kichwa kisalamu, lakini mwanaume huyo akampita tu na kuingia kwenye hiyo ofisi ya Josephina. Mlango ukafungwa. Josephina alikuwa tayari kukaa kwenye kiti chake, ila alipogeuka kukuta mja mpya ameingia, akaghairi kukaa na kuendelea kumwangalia kwa njia ya kawaida. Ilikuwa ni Francis. Kaka mtu. Kuu la majambazi. Alimalizana na Chomoka kule walipokuwa muda mfupi nyuma na moja kwa moja akaja mpaka hapa. Alikuja na jambo lake moyoni, na ni Josephina pekee ndiye ambaye angeweza kulipatia suluhu.

Akawa amesimama hapo mbele huku akimwamgalia Josephina kwa umakini, na mwanamke akauliza, "Nini?"

Francis akasema, "Sikukuona tena. Ulienda wapi?"

Josephina akabaki kumwangalia kama vile hamwelewi. Aliweza kuona ni kama Francis alikuwa amekunywa, na aliudhika.

"Nakuuliza," Francis akasema.

"Unaniona niko wapi sa'hivi?" Josephina akauliza pia.

"Usinijibu hivyo Phina," Francis akamwambia huku akimnyooshea kidole.

Josephina akavuta ulimi kwa kukerwa na kukaa kitini, akikiegamia na kufumba macho kabisa kuonyesha hamjali.

"Hivi saa zile ni nini kile ulichokuwa unafanya pale msibani? Mm?" Francis akamuuliza huku akianza kusogea.

"Frans, naomba usinisumbue. Kichwa kinaniuma, hayo ma-stress yako naomba usiyalete kwangu mie..."

"Ulikuwa unamwambia nini Reuben?"

"Ahah... ss.. you're pathetic..."

"Sitauliza tena, naomba jibu," Francis akaongea bila utani.

"Ama utafanya nini? Kama umekosa kazi, hata kuuliza mtoto yuko vipi haimo kichwani kwako, basi naomba usini...."

Josephina akiwa anaongea hivyo huku amefumba macho, tayari Francis akawa ameanza kumwelekea na kufika karibu naye, na ile mwanamke anafumbua macho, mwanaume akamshika mkononi na kumvuta kwa nguvu ili amsimamishe. Josephina akashtuka kiasi, na baada ya kunyanyuliwa hivyo kwa lazima, akakunja uso kwa njia yenye hasira na kumtazama Francis usoni.

"Sipendi dharau Phina!" Francis akamsemesha kiukali.

"We' vipi? Hebu niachie..." Josephina akalalamika.

"Niambie ulikuwa unafanya nini yale..." Francis akafoka. 

Josephina akamsogelea karibu usoni na kusema, "We' una shida gani? Mimi huwa nakuuliza kila kitu unachoongea na watu wako, au?"

"Ndo' mpaka uanze kumshika mikono? Umsemeshee sikioni... kila mtu alikuwa anakuangalia, halafu pale ni msibani, unafikiri ilijenga picha gani?"

Josephina akamwangalia kwa njia yenye mshangao na kucheka kidogo kwa dharau.

"Unacheka nini?" Francis akamuuliza.

Josephina akasema, "Kinachokusumbua ni mimi kuongea naye msibani, au wivu tu?"

Francis akabaki kumtazama kwa hisia makini.

"Nini... ulikuwa unafikiri najitongozesha kwake? Kama watu wote wamefikiri hivyo, basi labda ni kweli. Msiba, msiba kitu gani? Cha ajabu ni nini Frans? Hata mabusu tungepiga pale pale..." Josephina akaongea kwa kejeli ya makusudi.

Francis akapandwa na hasira na kumsukumia hadi ukutani huku akimkandamiza, na Josephina akakunja uso kwa kuudhika na kujaribu kujinasua.

"We' ni mshenzi sana!" Francis akamwambia kwa sauti ya chini.

"Ndo' unajua hilo leo?" Josephina akasema huku akijaribu kujitoa kwa nguvu.

Wakaanza kuvutana, Josephina akijaribu kujitoa na Francis akiendelea kumkandamiza ilhali mwanamke mpaka kuanza kumpiga na makofi usoni, ndipo Francis akamkandamiza zaidi na kuirarua nguo yake Josephina kwa juu. Hiyo ikamwacha mwanamke akiwa amefunuka upande mmoja wa titi lake ambalo hakulisitiri kwa sidiria, na Francis akaanza tu kuvuta gauni hilo kutokea chini kwa kulazimisha na kuyafunua mapaja ya mwanamke huyo.

"Frans, hebu niachie! Ach..."

Francis akafanikiwa kuingiza mkono wake kwa ndani kupita mapaja ya Josephina, naye akaishika tight kwa humo na kuingiza kiganja chake katikati kuushika uanamke wa mwanamke huyo.

"Sitaki Frans, nimesema niache..."

Josephina akaendelea kulalamika, mwanaume sasa akiwa ameanza kuukuna uanamke wake na hata kumwingizia vidole, halafu akaanza kumsugua kwa nguvu huku akimkandamiza zaidi ukutani na kuukaribia uso wake. Josephina akalaza kichwa chake ukutani kwa upande na kuanza kutoa miguno ya kimahaba, akiwa bado anampiga-piga jamaa kwa mkono mmoja, mwingine akiukandamiza mgongoni kwake kwa kuufinya. Francis hadi akaanza kumnyonya shingoni mwanamke huyo, akiendelea kumsugua na vidole kwa jeuri sana, na Josephina akaachama na kuanza kuhangaika kwa kuhisi raha. 

Kisha Francis akavitoa vidole vyake kwa mwanamke huyo, naye Josephina akampiga kofi usoni kwa nguvu, lakini mwanaume akaendelea kumkandamiza na sasa kuikaba shingo yake kwa mkono mmoja. Akatumia mwingine kuishusha tight aliyovaa Josephina, halafu akajaribu kufungua zipu ya suruali yake mwenyewe lakini ikawa inamshinda. Josephina akapitisha mikono yake kwa chini na kuanza kumfungulia suruali mwanaume, yeye mwenyewe, huku bado akiwa amekabwa, na baada ya kuuweka huru mtambo wa jamaa akaanza kuusugua kwa kiganja chake, naye Francis akalamba kiganja chake mwenyewe na kuipakaa mashine yake. Josephina akatanua mguu mmoja hapo ukutani kwa kuupandisha usawa wa paja la mwanaume, na Francis akamwingia hatimaye. 

Mapigo ya utamu yakaanza baina ya wawili hawa, Francis akitumia nguvu kumpa mahaba mwanamke, na Josephina akiyapokea kwa kupenda huku anamtazama kijeuri. Hapo hapo ukutani, jamaa akaendelea kumpa na kumpa mpaka hatimaye akajiachia ndani yake, naye akailalia shingo yake huku kwa pamoja wakipumua kwa uzito. Ilikuwa ni hali yenye kusisimua kwa wote, na haikuwa ajabu hata kidogo. Francis akajiondosha taratibu kwa mwanamke huyo, naye Josephina akajirekebisha huku akivuta tight yake na kuliweka gauni lake vizuri. 

"Ahh... umenichania nguo! Nitaondokaje hivi?" Josephina akasema hivyo na kupiga ulimi.

Francis akafunga zipu ya suruali baada ya kurudisha silaha mahali pake, naye akasema, "Nitamwambia Secy akuletee."

Josephina akawa anajaribu kulirudishia titi lake kwa ndani lakini likawa likitoka tu nje, naye akasonya kwa hasira na kumpita Francis kwa kumpamia, akienda upande wa pili wa meza.

Francis akamgeukia na kumwambia, "Phina... usiwe hivyo. Sometimes vitu vingine unavyofanya siyo..."

"Siyo nini? Kuongea na mtu ni vibaya? Mbona unakuwa una-panic sana?" Josephina akaongea kwa kuudhika.

Francis akajitahidi kuzuia hisia zake, naye akamfuata mpaka hapo na kujaribu kumshika, lakini Josephina akaupiga mkono wake kwa kutotaka aguswe. Akamwambia, "I'm sorry basi. Nili... nilihisi wivu tu, ndiyo... nilipatwa na wivu nilipoona umemshika namna ile, halafu ukawa unaongea naye kama yaani..."

"Kwani hujui mipango yetu sisi ni nini?" Josephina akamkatisha.

Francis akatulia.

"Faida ni nini sasa ya kumdanganya kwamba mimi na wewe ni kaka na dada kama utashindwa kuji-control kila utakaponiona niko karibu naye?" Josephina akamuuliza.

"Najua...."

"No, hujui. Unaruhusu ma-stress yako hayo huko yaje kunivurugia mimi mipango yangu..."

"Ni mipango yetu..."

"... wakati unajua siyo rahisi kufanya hizi ishu namna hii. Sasa hivi mke wake amekufa, yuko weak, naweza nika-exploit hiyo, nimvute, tupate faida. Sasa wewe ukikaa kuonyesha-onyesha wivu wako unafikiri itakuwaje?" Josephina akaongea kwa hisia kali.

Francis akashusha pumzi na kusema, "Okay, sawa. Naelewa. Usipandishe sana sauti, sipendi."

"Si ni wewe ndiyo ulikuwa unanipandishia mimi?"

"Basi, yaishe. Nimekuelewa," Francis akamwambia.

Josephina akaangalia mbele kwa kukerwa.

Francis akasema, "Ulikuwa na mipango ndiyo, sikujua tu kama ungeanza mapema, tena kama hivyo leo msibani. Kama kweli utaweza kujiingiza kwenye maisha ya Reuben, tu...."

"Ninaweza! Siyo kama nitaweza," Josephina akamkatisha.

"Sawa, Phina..."

"Tatizo we' unanidharau. Hii biashara ingesimama hivi bila me kuwepo hapa kuiendesha?" 

"Ndiyo, najua, sijakataa. Ila ukumbuke bila mimi hii biashara isingekuwepo hata kidogo. Kwa hiyo nikiongea naomba unisikilize," Francis akaongea kwa uthabiti.

Josephina akatazama pembeni.

Francis akasema, "Mambo tunayofanya yanaweza kuvuta attention, tuko hapa muda tunalijua hilo. Reuben ni territory mpya Phina. Ninataka uwe mwangalifu, usije kuchukulia kwamba yuko soft sana kwa hiyo utaweza kila kitu. Hiyo ikikukaa kichwani namna hiyo utapuuzia kwamba makosa yanaweza kujitokeza kwa kujiona uko sahihi kwenye kila kitu, na hiyo ni hatari. Nimeshakufundisha. Kuna mahali na wakati wa kila jambo, na leo we' kufanya vile msibani... siyo kuongea, ila kumkumbatia namna ile... haikuwa sawa. Unapaswa uwe care. Sipendi attention..." 

"Sijakuwekea attention yoyote Frans, unajifikiria kupita kiasi. Usisahau mbele ya wengine me ni dada yako. Sa' sijui unaogopa nini. Huo ni wivu wako tu wa kijinga ndo' unakusumbua... tsk..." Josephina akasema hivyo na kusogea pembeni zaidi.

Francis akainamisha uso wake kwa kuhisi kuchoka, kisha akasema, "Okay. Tuachane na hayo. Niambie unahitaji nini sasa hivi. Michongo ilitiki ile juzi, nataka niku-bless kidogo baby."

Josephina akasema, "Wala usijisumbue. Acha nifanye tu makosa, atani-bless Reuben."

"Aaa Phina..." Francis akaongea kwa kukwazika.

Josephina akaendelea kununa. 

Francis akamsogelea na kumshika kiunoni, naye akasema, "Sawa. Haina shida basi. Kama unajiamini unaweza kum-handle Reuben wewe mwenyewe, basi sawa. Ukitaka usinihusishe."

Josephina akabaki kuangalia pembeni kwa kuudhika.

Francis akamshika mabegani na kumgeuza ili watazamane, naye akasema, "Ila usisahau kwamba hili game ni langu mimi na wewe. Nitaenda kule, utaenda huko... lakini sisi ni kitu kimoja bado. Sitaacha kuwa hapa kwa ajili yako baby. Kwa chochote. Nataka tu uwe makini. Always."

Josephina akaendelea kujinunisha.

Francis akamshika pajani na kusema, "Unakuwaga mtamu kweli ukikasirika."

Josephina hakutoa itikio lolote kwa kauli hiyo isipokuwa kumwangalia kwa kushusha na kupandisha.

Francis akacheka kidogo kwa pumzi na kumbana kwake kibembelezo, naye akasema, "Niambie. Juzi ulisema kuna vitu vinapungua, na nimeona wasichana wapya wameshakuja. Kuna kitu unahitaji?"

 Josephina akaibana midomo yake kama hataki vile, lakini akasema, "Milioni tano."

"Mhm... sawa. Nitaituma kwenye akaunti yako kabla sijaondoka. Hiyo... pamoja na matumizi yako na Hans," Francis akamwambia.

Josephina akamwangalia na kuuliza, "Unaenda wapi?"

Francis akatoa simu mfukoni huku akisema, "Kuna ishu tunaenda kumalizia majengoni. Midomo mingi inayotakiwa kunyamazishwa."

"Si uwatume wengine waende?" 

"Hamna, hii nahitaji kuwepo. Vipi, utani-miss?" 

Josephina akaangalia pembeni kwa nyodo.

Francis akatabasamu kiasi na kusema, "Hans?"

"Yuko na Linah nyumbani. Atakuwa ameshalala," Josephina akasema.

"Sawa. Acha kudeka sa,' kuna kazi za kufanya. Nenda ukawe bosi," Francis akamwambia na kumwachia.

"Kichwa kinauma," mwanamke akaongea kwa kudeka.

"Nikupe dozi ya pili? Kitaacha tu," Francis akamwambia kiutani.

Josephina akasonya na kumsukuma kidogo, kisha akazunguka kukiendea kiti, naye Francis akatabasamu na kuweka simu yake sikioni baada ya kumpigia mtu.

"Hey, Secy... Safi. Uje kwa Phina sa'hivi, anataka akuagize. Wahi..."

Kisha akakata na kumwangalia mwanamke "wake" tena.

"Me naenda," Francis akamwambia.

Josephina akatikisa tu kichwa kukubali bila kumtazama, naye Francis kweli akajigeuza na kuondoka kutoka hapo.

Kama ni siri ya wawili, hii ndiyo iliyokuwa nzito zaidi baina ya wawili hawa. Francis na Josephina hawakuwa ndugu wa kimwili hata kidogo, bali wapenzi wa muda mrefu walioshirikiana kufanya kazi na mambo haramu kuvuna pesa nyingi. Na Hans alikuwa mtoto wao. Walijitahidi sana kuficha ukweli kwa wengi kuhusu maisha yao isipokuwa wachache waliowafahamu vyema, na sasa kwa kipindi hiki baada ya kukutana na Reuben ile majuzi, kwa pamoja wakawa wameunda njama ya kutaka kumwingia ili awafaidishe kimaslahi kutokana na yeye kuwa mtu mwenye pesa. 

Josephina, baada ya mke wa Reuben kupoteza uhai, akawa amepata njia moja. Alikuwa akipanga kujiweka karibu na Reuben hasa kipindi hiki cha huzuni kwake kwa kumzuzua na njia zozote ili aanze kumnyonya pesa. Kwake yeye na Francis kupata pesa nyingi ndilo lililokuwa jambo muhimu zaidi, na Reuben angekuwa sehemu bora ya kujichumia matunda hayo mpaka wahakikishe wamemmaliza na kusonga mbele kwa wengine. Mambo yalikuwa hivyo.


★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

Previoua Next