Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

SEHEMU YA 20.

Yonesi kama bodigadi alikuwa na taarifa zote za

Regina kuajili msaidizi wake mwingine  na mara baada ya kufahamu ni  Hamza  aliishia kushangaa na kujiuliza nini kinachoendelea , hakuwa na taarifa zote, alihisi  kuna kitu kinaendelea kati  yao lakini  aliona ni kheri ajirushe baharini aliwe na mamba kuliko kuamini  Regina anaweza kutoka kimapenzi na mwanaume kama Hamza.

Kingine ambacho kilimfanya  Yonesi kumdharau Hamza ni tabia yake  ya kukosa aibu  na uwoga woga  usio na maana , yeye alipenda wanaume ngangari lakini kitendo cha siku ile kumuachia msaala kule gongo la mboto  alimuondolea nyota ya  heshima  kama mwanaume.

“Kapteni, unapaswa kuwa na sababu ya msingi kunifukuza kwenye hii meza, hakuna sheria inayonizuia kukaa kwenye hii meza si ndio?”

“Nenda kakae meza inayofuatia haina mtu , kwani lazima ukae hapa”

“Siendi popote”Aliongea Hamza.

“Kwanini?”Aliuliza  huku akiwa amekunja ndita.

“Kwasababu nataka kuona   namna mwanamke mrembo kama wewe unavyokula”

Yonesi alikuwa ni mweupe kabisa , kauli ile japo haijamshangaza sana lakini  kulikuwa na viashiria vyote, sura yake ilianza kubadilika rangi na kuwa nyekundu.

Ni kweli   anatongozwa  sana , lakini haijawahi kutokea mwanaume kuongea kuhusu muonekano wake bila  wasiwasi kama  Hamza, lakini ilikuwa ni dakika ile aling’ata meno yake kwa hasira 

“Wewe mpuuzi , rudia kauli yako tena uone”

“Kapteni nimesema wewe ndio mrembo kuliko wote hapa , lakini ajabu umekaa mwenyewe”

“Ukiendelea kuongea  ujinga wako , nitakushushia kipigo hapa hapa  bila kujali watu”

“Ah!, basi yaishe  Kapteni , nimeacha  usije kunipig”Aliongea Hamza akijifanyisha kuwa mzembe huku akinywa juisi yake kwenye glasi.

Yonesi alikosa hata nguvu ya kumfukuza  Hamza tena na aliamua kujiweka bize   na chakula chake , lakini kadri alivyokuwa akila ndio alivyokosa  ule uhuru aliokuwa nao na aliinua macho yae na kumwangalia Hamza , lakini ndio anaona Hamza alikuwa akimkodolea macho eneo la kifuani.

Hamza alikuwa akifurahia chakua chake , kilichomfanya kumkodolea Yonesi macho ni  aneo la kifuani  tu , alikuwa akiona  namna manyonyo yake yalivyokuwa yakivutia.

“Mh , juzi nadhani sijamwangalia vizuri , anaita sio poa”Aliwaza Hamza ndani kwa ndani  

“Unaangalia  nini?”Aliuliza Yonesi kibabe.

“Unataka  kujua kweli wa ninachoangalia?”

“Jibu swali?”

“Naangalia hayo mayai  kwenye sahani yako”

“Kuna mayai gani kwenye sahani yangu!!?”Yonesi aliongea kwa hasira mno huku akipiga kofi meza na kufanya watu kugeuka na kuangalia kinachoendelea, lakini Hamza  alijifanyisha  kuwa bize  kula chakula chake.

“Kapteni   ni kweli nimekuona  na mayai  kabisa , tena mawili ..”Hamza aliendelea kumchokoza Yonesi.

“Mbwa wewe ,nani ana mayai , sema ulichokuwa ukiangalia lasivyo nitakufanya kipofu”Aliongea huku akimnyooshea  Hamza na uma.

“Kama unabisha , wewe unadhani nilikuwa nikiangalia nini?”

“Kwahio unabishana na mimi , unadhani  maneno yangu ni ya bure siwezi kukufanya chochote”

Yonesi  kwenye maisha yake hakutaka kuonewa kizembe  na kwasababu hasira zishamvaa aliona amshikishe adabu  Hamza hapo hapo , hivyo alichukua  uma na kumlenga nayo  uelekeo wa macho.

Watu waligeuka  mara baada ya kuona tukio hilo  wakitaka kujua mwisho wake 

Lakini  Hamza  hakukwepa wala kufanya chochote , alikuwa akiendelea kutafuna  huku  Uma ile ikimkaribia machonni .

Yonesi  asingeweza kumchoma nayo kweli  machoni   na baada ya kufika nchi kadhaa  karibu na jicho la Hamza aliishia  njiani , upande wa Hamza hakupepesa macho hata kidogo.

Kitendo kile kiliwashangaza watu , maana mtu yoyote angeogopa kwa kulengwa na ncha  machoni  , lakini Hamza hakuonyesha hofu.

“Kapteni  unajua kila mtu anatuangalia , huoni sio vizuri kunichokoza mchana  yote hii”Aliongea Hamza akitabasamu , alijiambia Yonesi hata amshikilie bunduki hawezi kuogopa.

Yonesi aliishia kushusha uma chini  huku akijiuliza imekuwaje  huyo mpuuzi leo kujiaminni hivyo.

“Leo  nitakusamehe , ukinichungulia siku nyingine hutoamini  nitakachokufanyia” Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu tu.

“Kapteni , naomba kuuliza?”

“Nini?”

“Wewe ni D au F?”

“”…”

Yonesi alishindwa hata kuongea  kutokana na namna alivyokuwa amekasirika kwa mara nyingine na Swali lile.

“Mpuuzi wewe , ulikuwa kweli ukinichungul..”

Kabla hata hajamaliza sentensi yake alijizuia mara baada ya kuona ameongea kwa sauti kubwa  na kufanya watu kumwangalia , uso wake ulikuwa umebadilika mno kutokana na hasira , hakuwahi kudhalilishwa kiasi hicho  ndani ya kampuni.

“Hamza nifuate”Aliongea  kwa kuamrisha , hakutaka kuleta fujo ndani ya mgahawa , aliona ni bora amtoe hapo akampe kibano  pembeni.

“Sijamaliza kula”Hamza alikataa.

“Wew..”

Kitendo kile kilifanya Yonesi agundue watu walikuwa wakicheka  kwa siri  na aliishia kusugua  meno yake  kwa hasira  na alifyatua mkono wake wa kulia kijeshi kwa ajili ya kumshika  Hamza tai , lakini   Hamza  alirudi nyuma na kufanya mkono wake kupita.

Yonesi aliona Hamza aliotea hivyo alizunguka upande wa pili kwa ajili ya  kumshika , Hamza hakuwa na haraka mara baada ya kuona  Yonesi anamkaribia alipiga  kiti teke ambacho kilienda kumvaa   afande Yonesi  na kumfanya akose mhilimili na kuelekea chini akitanguliza uso.

“Ahh..”

Yonesi alijua alikuwa akidondoka vibaya , kitendo cha

Hamza kupiga kiti teke hakukiotea kabisa ,sekunde  hio  akiona anakwenda kudondoka vibaya  Hamza alikuwa ashamzuia  kwa   mkono mmoja na  kumshikilia kifuani sehemu ileile  ambayo  ilimfanya kukasirika kwa kuchunguliwa.

Yonesi  ni kama alikuwa amepigwa na shoti  , alijikuta akitetemeka mara baada ya kuona namna mkono wa Hamza ulivyoyashikilia manyonyo yake

 “Wewe muhuni umenigusa..”

“Kapteni , unamaanisha  nini kugusa wakati nakuzuia usidondoke”Aliongea Hamza na muda uleule Yonesi alisimama vizuri, mara baada ya kuona macho ya wafanyakazi  yamezidi kuongezeka  , alimwangalia Hamza kwa macho makali.

“Subiri uone , inaweza isiwe sasa hivi ila nitakufanya ujutie kwa ulichonifanyia leo”Aliongea Yonesi kwa hasira na kisha aligeuka zake na kuondoka  huku kichwa kikiwa chini , kwa mara ya kwanza mbabe wake ndani ya kampuni  alipatikana.

Kila mtu alimwangalia Hamza kwa mshangao na kumkubali , hio ilikuwa mara yao ya kwanza  kuona  Yonesi akitawaliwa na mwanaume na ashindwe kufanya chochote, wanaume wengi walionekana dhaifu mbele ya Yonesi.

Hamza wala hakujali vile  vitisho  na baada ya kumaliza kula alichukua matunda ya apple kwenye friji na kisha akaweka kwenye mfuko na kuondoka

nayo , alijua  Regina hajala hivyo  alijihisi sio vizuri kutopeleka chochote  hata kama ataonekana anajipendekeza.

Mara baada ya  kutoka kwenye lift moja kwa moja alienda mpaka kwenye  mlango wa  mkurugenzi na kugonga.

“Come in”

Hamza alisukuma mlango  na kisha akaingia , aliweza kumuona  Regina akiwa bize amekodolea tarakishi yake huku akionekana kuandika vitu kwa karamu  kwenye  notebook.

Mbele yake kulikuwa na  nyaraka nyingi ambazo  ilionekana alikuwa akizifanyia kazi pia , ki ufupi alikuwa bize.

“Weka   ripoti hio  juu ya meza  na unaweza kuondoka”Aliongea Regina bila ya kuangalia aliengia , alijua ni  Linda sekretari wake.

Mara baada ya Hamza kuweka matunda yale juu ya meza ndio sasa  Regina aliinua macho  na kumwangalia.

“Kwanini ni wewe?”

“Sekretari wako kasema hupendelei kula chakula cha mchana na nimeona sio vizuri ,  kula hata matunda nimekuletea”

“Nishakula na haikuhusu kama nimekula au sijala”Aliongea bila ya ishara ya furaha yoyote.

“Kwahio umekula?”Aliongea Hamza huku akizungusha macho yake na ndio alipoweza kuona mfuko uliojaa makopo , yalikua kama kumi na mbili hivi.

“Gum- syrup!!”Hamza alionekana kushangaa ,

“Hiki kinywaji ndio unachotumia kama chakula cha mchana ?”Aliongea Hamza  na  kumfanya Regina kumwangalia.

“Kumbe unajua  hata jina lake kwa kingereza ni Gum syrup?, kweli wewe ni mwanachuo una exposure ya kujua vitu vingi”Aliongea Regina lakini  Hamza hakujali. 

“Hata kama unataka kuzuia njaa hutakiwi  kutumia  aina hii ya kinywaji  cha virutubisho , unatakiwa kula chakula?”

“Chakula kinaathiri mzunguko wa damu na oxygen  kwenye ubongo  na muda wangu wa kufanya kazi  ni muhimu sana, sitaki kusinzia, kitu kingine  huna kigezo  hata kimoja cha  kunijali”Aliongea kikauzu.

“Kula angalau  hata hayo matunda , kuliko kushinda na tumbo ambalo halina kitu”

Licha ya kwamba Hamza alikuwa akionyesha kumjali , lakini kwake alimuona kama mtu asiemfahamu tu.

“Ondoka nayo , sitokula”Aliongea lakini  Hamza alitoa kicheko na kisha akashika simu  yake.

“Ngoja nimpigie shangazi  na kumwambia unashindia vinywaji vya virutubisho mchana na huna ratiba ya  chakula cha mchana”

Regina mara baada ya kuona  anachotaka kufanya 

Hamza alijua maana yake ni nini ,  kama kweli Shangazi angelifahamu hilo angekuwa na wasiwasi mno  maana  kwake ni kama mama. “Weka simu chini , acha kupiga”

“Nitafanya hivyo kama utakula  matunda yote

nilioleta  la sivyo  hili swala nitalifikisha kama lilivyo kwa Shangazi”

“Mbona unapenda kunisumbua  na mitunda yako mibaya mibaya”Aliongea  huku akionyesha hasira za wazi.

“Nakusumbua sio,ngoja tuone kama nakusumbua , mimi nampigia”

“Wewe inakuhusu ni nini kwanza kula kwangu , unanijali kama nani?”

“Nimeshiba  tayari  ila kuona  hujala chochote nimejikuta na shikwa na huzuni”

“”..”

Regina  aliishia kuegamia kiti chake huku akimwangalia  Hamza , ni kama hakuwa ametegemea angetoa jibu  la aina hio.

“Huzuni utoe wapi , umekaa kiuongo uongo tu”

“Acha maswali mengi , unakula au huli”

“Nitakula , acha kuendelea kunichukiza”

“Hilo ndio jibu sasa , nitakaa  hapa hapa mpaka nione umemaliza ndio naondoka”Aliongea   lakini  Hamza alimwangalia mara baada ya kuona  Regina amekunja sura huku ameshikilia mkononi  apple.

“Sipendi kula  na maganda yake na mimi mvivu wa kumenya”

“Ukila  na maganda yake ndio vizuri , yamebeba

Asidi ya kutosha inayosaidia kuondoa uchomvu”

“Ndio hivyo sipendi sasa , unalazimisha”

“Uvivu tu ndio unasumbua “

Aliongea Hamza na kwasababu hakuwa na chaguo lingine ilibidi atafute kisu na kuanza kuyamenya moja moja na kuyaweka kwenye sahanni.

Spidi yake ya kumenya ilikuwa kubwa  mno  na ndani ya dakika chache tu alikuwa ashamaliza yote.

Regina alianza kuyatafuna haraka haraka , alitaka kumaliza  ili aendeee na kazi yake.

“Halafu una malengo gani , kwanini unalazimisha nile haya  matunda?”

“Sina malengo  yoyote , ninachotaka ni ujaze hilo tumbo lako , kwanini una mawazo mabaya kila ninachofanya”

“Umekaa kimashaka mashaka  ndio maana”Aliongea huku akiendelea kula  kama abiria anaetaka kumaliza haraka apande basi.

Baada ya Regina kumaliza kula  alionekana kukumbuka kitu  na kumwangalia Hamza.

“Zile nyaraka  ulizotafsiri nimeziona , umetafsiri vizuri sana kuliko  hata Freelancer tuliemwajiri  kututafsiria mara ya mwisho, nadhani  uwezo wako wa  kuongea kifaransa na kingereza ni C2?”

“C2 maana yake ndio nini?”

“Hujui?, Inamaana  hujawahi kufanya DEF test?, C2 maana yake  ni kiwango  cha juu cha kuongea lugha ambayo sio uliozaliwa nayo”

“Sijajifunza kifaransa na kingereza kwa njia rasmi, wakati  nilipokuwa nje ya nchi  nilikuwa nikiongea na watu mara kwa mara ndio maana nilizidi kuzoea”

“Ushawahi kuwa nje ya  nchi, masomoni au?”Aliuliza Regina kwa mshangao  , alihisi ni vizuri kumjua  Hamza angalau kidogo.

“Ndio nilipofikisha miaka kumi  nilidhamia  nje ya nchi, kutokana na maisha kuwa magumu nilijikuta nikifanya kila aina ya kazi, bahati nzuri kutokana na muonekano wangu wa kuchanganya rangi  nikapata  familia”

“Sasa ilikuwaje ukarudi?!!”

“Kuna mambo yalitokea  ,nilishindwa kuendelea kuishi katika familia yangu mpya mara baada ya kugundulika kama mtanzania”Aliongea Hamza , Regina  japo alikuwa na maswali mengi aliona aishie hapo  kuuliza , alitamani kujua ilikuwaje mpaka akafika chuo.

Mara baada ya kumaliza kutafuta yale matunda alihisi ukakasi kwenye midomo na alihitaji maji ya moto  kwa ajili ya kusukutua.

“Nitakusaidia kumimina maji?”Aliongea Hamza mara baada ya kumuona Regina akisogelea  Dispenser ya maji ya moto.

“Nishafika tayari , haina haja”Aliongea na kumfanya Hamza arudi kukaa kwenye sofa.

Lakini sasa kitendo cha  Regina kuinama  ili achukue Glasi  ilifanya gauni lake kupanda juu kutokana na kuwa na shepu kubwa , alikuwa amechukua tahadhari ya kugeukia  upande wa nyuma lakini akasahau  kuna kioo ambacho kina akisi mwanga.

Hamza  alikaza macho , alikuwa na shauku ya kutaka kuona mwanamke kauzu kama Regina huko ndani  atakuwa anavaaje.

Regina mara baada ya kugeuza uso wake na kumuona Hamza anapoangalia  alishituka na kugeuka nyuma na hapo ndipo alipojua  alikuwa akionekana kwenye kioo kwa nyuma.

“Wewe…!!!”

Regina alijikuta akisimama wima huku akijiweka vizuri  na kisha akageuka  huku akimkazia macho 

Hamza , wazo la kumuua Hamza  lilimvaa palepale. 

Hamza alikuwa ashageuza  macho yake  na alijifanyisha kushangaa kwa mabadiliko ya Regina.

“Mkurugenzi  nini shida , kwanini unafoka?”

“Hujawahi kuona mwanamke , umekuwa chizi?”Aliongea  akiwa  amekasirika.

“Boss  kama unataka kunifokea ni bora ukaniambia sababu , sijafanya kosa lolote”

“Sijawahi ona mwanaume mshenzi kama wewe ambae huna aibu  na kuchungulia watu”

“Nini!, unamaanisha nini kukuchungulia , mimi muda wote  nilikuwa nikifurahia mandhari mazuri  ya jiji letu, Mkurugenzi utakuwa unanifikiria vibaya”

“Bado unabisha tu”Aliongea  na wakati huo alimimina maji ya moto kwenye kikombe na kumsogelea  Hamza.

“Boss unataka kufanya nini?”

“Kwanini?, unadhani  nataka kukumwagia maji  kama huna kosa?”

“Mkurugenzi , ni kweli umenifikiria vibaya . ila kama dhamira yako ni kunimwagia maji ya moto basi  ni  kheri nikimbie tu”Aliongea Hamza lakini muda ule mikono ya  Regina ilicheza na kufanya  maji  ya moto kutoka katika kile kikombe  na  kuelekea  katika miguu yake .

Lakini Hamza alikuwa na spidi kwani  aliyakinga yale maji kwa kupitia viganja vyake  ili yasimfikie  na kitendo kile kilimshitua Regina  na mara  baada ya akili yake kufanya kazi aliwahi kuweka kile kikombe chini 

“Hujaungua?”

“Mikono yangu inasugu na ngozi yake ni ngumu , maji kidogo hivi hayawezi niunguza”Aliongea na  Regina mara baada ya kuangalia mikono ya  Hamza haijaungua kidogo alijisikia amani.

“Sorry , sijamwaga makusudi”Aliongea Regina  bila ya kumwangalia Hamza machoni, hakutegemea kama  Hamza angechukua hatua ya kukinga maji na mikono yake yasimuunguze.

“Hakuna shida, ili mradi  tu Mkurugenzi hutoendelea kunifikiria vibaya, nitaacha hili lipite”

Mara baada ya kuona namna  Hamza alivyoongea kipole   aliona pengine ni kweli alimfikiria vibaya na hakuwa akimchungulia.

“Ni kweli   hujanichungulia?”Aliuliza kwa kusitasita.

“Kama huniamini basi siwezi kuendelea kujielezea , narudi ofisini kwangu”Mara baada ya kuongea hivyo  Hamza alisimama na kupiga hatua kuondoka ndani ya  ofisi  hio akimuacha  Regina  kwenye mawazo. “Mkurugenzi , kabla sijaondoka  naomba nikuulize swali?”Aliongea Hamza mara baada ya kufika mlangoni.

“Uliza?”

“Huwa unapendelea rangi ya pink  plain au pink  yenye maua maua?”Aliuliza na kabla hata hajajibiwa alishatoka na kufnga mlango.

Upande wa ndani  Regina alinyanyua kikombe  kile cha glasi na kurusha mlangoni , lakini ashachelewa  na kilichosikika ni sauti ya kuvunjika tu.

“Hamzaaa..!!!”

Regina  alitoa ukulele wa hasira huku sura yake yote ikiwa nyekundu.

Aliona mpango  wake wa mwanzo wa kumfundisha kazi kulingana na kozi yake anayosomea  ulikua ni wa

kijinga ,  dakika hio hio alishaona alikuwa  amemsingizia kumbe yote  hayo alikuwa akichezewa akili.

Upande mwingine  mara baada ya Hamza kuingia tu katika ofisi yake simu yake ilianza kuita na alipoangalia jina la anaepiga  alikuwa ni Amiri  rafiki yake.

Alishangaa kidogo kwani tokea siku ambayo alimsaidia kutega kamera  hawajaonana.

“Hello!!”

“Bro vipi?”Sauti ya Amiri ilisikika  na ilikosa utulivu  jambo ambalo Hamza alilijua haraka sana.

“Poa  kabisa , mambo vipi?”

“Mambo sio shwari kaka?” “Kwanini unasema hivyo?”

“Hata sijui nikuelezee vipi , ila nimechanganyikiwa  tokea jana”Aliongea  na Hamza aliamini lazima ni swala linalohusiana na Mellisa.

“Ni swala la Mellisa nini?”

“Ndio  kaka, sijui ni mauza uza gani yanaendelea kwa huyu mwanamke , ila naomba tuonane leo  hii , ikiwezekana hata sasa hivi , pengine unaweza kuwa na  majibu ya nilichokiona”

“Kwasasa kuna mishe  imenishika hapa ,  unaonaje  baadae saa kumi  na moja”

“Sina jinsi kaka nitasubiri , wewe ndio mtu wangu  wa karibu ninaeweza kukushirikisha hili , pengine unaweza kuwa na majibu , mimi nimekwama”

“Sawa nitakushitua”

Hamza  baada ya  simu ile alikaa kwenye  kiti , alikuwa na shauku pia ya kujua ni kitu gani ambacho  kimetokea , maana kwa  alichokuwa akiongea  Amiri alijua  kuna jambo kubwa ameona kupitia zile Kamera za siri.

******

Upande mwingine  Amosi  alionekana akiegesha gari yake katika kituo cha  kujazia mafuta cha Puma  kandokando ya barabara ya Haile Selasie  na mara baada ya kutoka  katika  gari  hio  nyeusi aina ya Mercedenz alipiga hatua na kuingia  uelekeo wa hoteli ya Peninsula.

Alikuwa  makini mno katika tembea yake , ni kama vile   mtu ambae anaogopa kufatiliwa, wakati huo simu ilikuwa sikioni na mara baada ya kuignia ndani kabisa ya hoteli hio eneo la mapokezi   aliongea maneno machache tu na kisha alisonga mbele na kuzisogelea ngazi.

Jengo la hoteli hio halikuwa refu  sana na mara baada ya kufika floor  ya tatu alisimama katika mlango wa chumba na  akagonga mlango  na hazikuchukua hata dakika  chache mlango wa chumba ulifunguliwa na ksiha akaingia ndani.

Chumba hakikuwa cha  ghali sana , kilikuwa cha kawaida tu  kitanda  kikubwa cha  sita kwa sita pamoja na  Tv.

Mtu aliemfungulia mlango alikuwa ni mwanaume wa makamo hivi mrefu  mweusi ambae ana nywele ndefu  na  masharubu.

“Mzigo vipi?”Aliongea Amosi mara baada ya kusalimiana kwa kugongesheana tano.

“Huu hapa  boss”Aliongea yule kijana na kuchukua  bahasha iliokuwa juu ya kitanda na kumpatia.

Amosi  alifungua bahasha ile  kwa kuihakiki  na kisha alitingisha kichwa kuonyesha  kuridhika.

“Kuna maagizo mengine?”

“Hamna , nimepatiwa hizo tu”Aliongea yule  bwana na kumfanya Amosi  kukagua chumba hicho kwa dakika kadhaa na kisha alitingisha kichwa na kugeuka kuondoka.

“Simama hapo hapo?”Sauti  kutoka nyuma ilisikika  ikimwamrisha  na kumfanya ageuke huku akiinua mikono yake juu mara baada ya kuona amenyooshewa Bastora, huku yule mtu akiwa  hana  utani hata kidogo kwenye macho  yake.

Ni dakika ileile  mlango wa  bafuni ulifunguliwa  na akatoka  mwanamke ambae ni kama alikuwa akitoka kuoga kutokana  na kwamba hakuwa na nguo zaidi ya Bathrobe ya rangi nyeupe, alikuwa mrembo haswa.

“Tresha!!”Aliongea Amosi kwa mshangao.

“Amosi!!”

Previoua Next