Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

SEHEMU YA 21

Mwanamke ambae alikuwa amepambwa na tabasamu mbele ya  Amosi alikuwa  ni Tresha , pengine  Hamza angekuwepo ndani ya hilo eneo angemfahamu mara moja , ndio mrembo ambae  alimpagawisha katika  Apartment za Dosam Homes , mwanamke ambae kwa maelezo ya Amiri  uzuri wake ni wa kutengeneza  na inasemekana ni mfanyakazi wa Binamu Island.

Amosi alimwangalia Tresha kwa dakika kadhaa na kisha akayainua macho yake na kumwangalia  mwanaume aliemnyooshea Bastora.

Upande wa Tresha   hakuonyesha ishara yoyote  ya furaha , ilionekana alikuwa akifahamiana na Amosi lakini  muda huo alikuwa siriasi.

“Tresha nini  hiki, kwanini upo hapa na  nini  kinaendelea?”Aliuliza  Amosi.

“Nikuulize wewe Amosi unafanya nini hapa?”Aliongea Tresha  na alimsogelea Amosi  na kisha alichukua ile bahasha.

Amosi alikuwa na wasiwasi mno na  kwa haraka haraka alijua kabisa yupo ndani ya mtego.

“Tresha   najua unachomaanisha , lakini swala hili  linahusiana vipi  na wewe?”.

“Swali hilo  ulitakiwa kumuuliza aliekupa kazi , nilishakuonya  siku nyingi ikitokea umeingilia njia zangu tutakuwa maadui wakubwa na leo tupo hapa”Aliongea  na hapo sasa  hisia mbaya  zilianza kumvaa Amosi  na kitu kilichomjia akilini kwake mara moja ni  kujiokoa.

Alimjua mwanamke huyo fika , licha ya kuonekana mwanamke mrembo lakini ni kibaraka  wa watu wa  Binamu Island ambae hana huruma hata kidogo.

“Usije kufikiria kufanya chochote cha kijinga , sekunde ambayo utasogea hata nchi moja  ndio utakuwa mwisho wa uhai wako  Amosi”

“Unataka  nini kutoka kwangu Tresha , kama Binamu  wameagiza  kifo changu haikuwa na haja ya  kuniwekea mtego  kama huu”

“Haha.. hubadiliki  hata kidogo , siku zote  akili yako inafanya kazi  kwa haraka ukiwa  katika hatari , ungekuwa sawasawa kiakili ungejiuliza maswali mengi kabla ya  kuwa mtumwa wa pesa, niambie Amosi umeahidiwa kiasi gani cha malipo kwa ajili ya kufanya kazi  ya hatari namna  hii , unaniuliza nini   nataka kutoka kwako? , hakuna  chochote ninachotaka kutoka kwako , Curiosity killed  the cat “

Mara baada ya kumalizia  msemo ule wa  shauku ilimuua paka  alimpa ishara yule bwana kumpiga Amosi risasi.

“Wait!!”Amosi alizuia   kifo chake na kumfanya  Tresha  kumpa ishara  yule bwana asiruhusu risasi.

“Unataka kusema nini Amosi , kitakachokufanya uendelee kuishi”

“Naomba niulize swali?”

“Kwasababu ya  historia yako  unaweza kuuliza  kabla ya kupoteza uhai”

“Kanali Dastani  ndio aliekupatia taarifa juu ya ninachofuatilia?”Aliuliza Amosi akiwa na macho yaliojaa uchungu.

“Ukishajua ni Dastani  utafanya nini , unadhani  kuna  uwezekano wa kulipiza kisasi hata baada ya kufa”

“Kwasababu jibu  lako linaweza kunifanya nikupatie kitu cha thamani zaidi kuliko kifo changu”

“Amosi  nipo  hapa kwa maamgizo ya  Binamu , unadhani ni kipi unaweza kuniambia nikaenda kinyume, una kitu gani cha thamani zaidi ya kifo

chako?”Aliongea  Tresha huku muonekano wake

ukiwa siriasi lakini  swali lile lilimfanya Amosi aone bado  hawezi kufa kizembe.

“Nawajua nje ndani Night Shadows na namna ya kuwasiliana nao!!!”Aliongea Amosi na kauli ile ilimfanya  yule bwana ambae  alikuwa ameshikilia bastora kupepesa  macho  kwa kumwangalia  Tresha na hio ndio nafasi adhimu ambayo Amosi alikuwa akiitafuta.

“Clang!!!”

Ilikuwa ni wepesi wa hali ya juu mno , kitendo cha  yule mtu alieshikilia siraha kupepesa macho pembeni  baada ya kutaja Night Shadows  Amosi alikuwa ashahama aliposimama  na kumtupia Bedlamp iliopasuka kwenye mikono yake na bastora kwenda pembeni.

Tresha  ambae alikuwa mita kadhaa kutoka alipo Amosi hakuweza kufanya chochote kwani hakuwa na siraha.

Amosi hakuzubaa , mpango wake ilikuwa ni kukimbia  na sio kushindana na Tresha , alijua mwanamke huyo likija swala la map[igano hamuwezi maana ni  Ninja aliepitia mafunzo na mafunzo yakamzoea.

“Bang!!!”

Bahati mbaya  spidi yake  haikutosha  na  bastora iliofungwa kiwambo cha kuzuia sauti   ilikohoa , kama sio  kupinda kidogo tu pengine ingekuwa  mwisho wake palepale.

Amosi  licha ya kupigwa risasi hakutaka  kusikilizia maumivu ,  bahati nzuri  alikuwa hajauloki mlango  , hivyo spidi yake  ya kutoka ndani ya chumba hicho ilimfanya kukoswa koswa na risasi nyingine.

“Fuckk!!!”

Tresha alitoa tusi  huku yule bwana  alieshikilia  bastora  kutaka kukimbilia nje lakini alizuia.

“Carlos Stop!!!”Aliongea Tresha kwa nguvu na mwanaume mweusi ambae sasa tunafahamu jina lake ni Carlos aliishia mlangoni.

“Tresha  tunapaswa kumuua kama oda yetu ilivyo”Aliongea Carlos.

“Umefeli kumuua akiwa mbele yako  unadhani  unaweza kumuua akiwa kwenye korido , unataka kuibua taharuki , unataka kuonekana  katika  Kamera”Aliongea  Tresha huku  akionyesha hali ya kukasirika.

“Wewe ndio  umesababisha misheni imefeli , nilikuambia tokea mwanzo hili nitalimaliza mwenyewe , kulikuwa na haja gani  ya kutaka kushiriki?”Aliongea  Carlos na kauli ile ilimfanya  Tresha  kutoa  tabasamu.

“Ndio tulipaswa kumuua , lakini  ni mpaka  atupe taarifa  tuliohitaji , likija swala la kuua Carlos unatoka nje  ya malengo ya misheni”Aliongea  na kumfanya Carlos kuvuta pumzi na kuzishusha.

“Ninachojua mimi ni kuua, nimefundishwa hivyo?” “Ndio maana  ya uwepo wangu  hapa Carlos, tunapaswa kupata taarifa tunayotaka kutoka kwake , ndio tumuue sio vinginevyo?”

“Ameshakimbia  , unadhani itakuwa rahisi?”

“Hilo niachie mimi , namjua Amosi nje ndani , nimefanya nae kazi kwa muda mrefu”Aliongea  na  kisha mwanamke huyo aliangalia mazingira ya chumba  na kisha  alichukua bahasha ambayo Amosi alionekana kuifuata na kutoa makaratasi  na kuyakagua kwa muda.

“Unapaswa kuondoka”Aliongea  Tresha   ambae alipanda juu ya kitanda na kujiachia na kumfanya Carlos kumwangalia mrembo huyo kwa macho ya kimatamanio  lakini Tresha hakujali macho yake  na palepale aliweka  bastora yake kwenye kiuno na kutoka nje huku  akidhibiti hasira zake.

Upande mwingine  Amosi alikuwa amesambaza matone ya damu kila mahali ndani ya hoteli hio lakini hakujali , hata watu aliopishana nao wakati akiwa ameshikilia  ubavu wake wa kushoto  hakutaka kuwapa hata nafasi ya kuona sura yake , ki ufupi akili yake ilikuwa katika tahadhari ya kujiokoa na alikimbia kweli.

Hoteli hio ilisifika kwa ulinzi  mkali na usalama  lakini kilichotokea kiliwashangaza watu.

Dakika chache alikuwa  ashatokezea barabarani  na kuanza kujikongoja kusogelea  gari lake.

“Amosi!!”

Sauti ilimwita, ilitokea katika gari nyeupe RAV4 iliosimama kando ya barabara , Amosi aliangalia gari hio na kuonekana kuitambua na   bila ya kujiuliza mara mbilimbili aliisogelea, mlango wa gari  hio ulifunguliwa na aliingia ndani  na hapo hapo ikaondoshwa.

*****

Hamza mara baada ya kumaliza kuongea na simu  iliotoka kwa  Amiri  alikaa kwenye tarakishi na kisha  alianza kufanya utundu wake , alishajua  tarakishi za wafanyakazi zinafuatiliwa hivyo alitaka kuifunga  tarakishi yake ki ujanja aendelee na mambo yake bila kushitukiwa.

Dakika ambayo ndio anamaliza kuseti mitambo , Linda aliingia  akiwa  na rundo la  makaratasi mkononi , zilikuwa nyingi kiasi kwamba hata kubeba alionekana kupata shida.

“Hizi nyaraka  unatakiwa kuzitafsiri  kutoka  kingereza kwenda lugha ya kiswahili , ziishe zote leo hii”Aliongea  kikauzu na kauli ile ilimshangaza  Hamza.

“Linda haiwezekanni  ni nyingi mno kumalizika kwa siku moja “

“Bosi ndio  kasema , eti kwasababu uwezo huo unao  hataki kuona ukipotea bure”Linda aliweka  nyaraka zile mezani na kisha kwa maringo alitoka.

Alikuwa akijua kabisa  Hamza amemchokoza bosi , kwani alisikia akipiga makelele kutoka ndani ya ofisi yake ndio maana akapewa adhabu hio.

Ki ufupi  kwa Regina ilikuwa ni kisasi  mwanzo mwisho ili kumkomesha.

Hamza  aliishia kujisikia uchungu lakini hata hivyo alikuwa akiupenda mshara wake hivyo  aliishia kukubali kufanya kazi.

“Bora ningejifanyisha tu sijaona kitu ,  angalia sasa  msala niliojitengenezea”Aliwaza Hamza.

Mpaka inafika  jioni  Hamza aliweza kutafsiri  nusu tu ya kazi yote aliopewa na aliona hakuna uwezekano wa kumaliza yote na aliona atafute namna yoyote ya kuongezewa siku.

Lakini kabla hata hajajua  cha kufanya mlango  wa ofisi yake ulifunguliwa na Linda.

“Ni muda wa kuondoka kazini sasa , nenda maegeshoni  na  washa gari , washa AC  na kisha msubiri bosi”Aliongea  na  Hamza alivuta pumzi ya ahueni , alikuwa amechoshwa kweli kuendelea kukaa hio  sehemu.

Aliingia  zake kwenye lift  ambayo ilimpeleka moja kwa moja mpaka  maegesho ya chini kabisa ya jengo hilo na kutoka ,  lakini wakati akitaka kusogelea gari ya  Regina  aliweza kumuona  Kapteni Yonesi akiwa amesimama pembeni  huku akimwangalia   kwa macho yaliojaa sumu.

Ilionyesha ni dhahiri alikuwa amejitega hapo ili kumpata Hamza  amshikishe adabu.

“Wewe mhuni  hatimae umejitokeza”Aliongea  kikauzu.

“Kapteni   ndio  unajiandaa kutoka  kazini na wewe , hehe kwaheri  tutaonana kesho”Aliongea Hamza akijifanyisha  mjinga.

“Nani kakuambia naondoka?, unadhani naweza kusahau  kirahisi   kilichotokea  mchana”

“Mchana kumetokea kitu  gani?, mbona hata sina kumbukumbu”

“Wewe mpuuzi usie na aibu ,  kwahio unakataa  kosa lako  sio , umenidhalilisha   mbele ya watu na  sijakufanya chochote , huu ndio muda , nisipokushikisha adabu siwezi  kuendelea kuitwa Kapteni”Aliongea  na sekunde ileile alifyatuka  kama mshale akitanguliza mguu  akilenga maeneo nyeti ya Hamza.

Hamza  aliishia kukwepa pigo lile na kumfanya  Yonesi kupita.

“Kapteni  ukiendelea hivi utanikasirisha ujue , mimi ni mwanaume na sio vizuri kupigana na mwanamke” “Unajiita mwanaume , kwangu wewe ni mwanaume ulievaa suruali tu, kama unajiamini pigana na mimi tuone”Baada ya kuongea hivyo alijiandaa kumshambulia tena Hamza lakini aliishia njiani mara baada ya mlango wa lift  kufunguka na Regina kutoka.

Regina mara baada ya kuona tukio lile alijikuta akishangaa huku akikunja sura.

“Yonesi , nini kimetokea?”

“Boss  nina mashaka na tabia ya huyu mtu …”Aliongea Yonesi na kuanza kuelezea kilichotokea mchana juu ya Hamza kumchungulia  manyonyo yake na kisha kumdhalilisha mbele ya wafanyakazi.

“Boss tusipomshikisha adabu mapema , hii tabia itafanya wafanyakazi kunidharau”Aiongea  Yonesi  akipigilia msumari.

“Mkurugenzi , usimsikilize Yonesi na porojo zake , mimi hio tabia  ya kuchungulia watu sina kabisa , mimi nilikuwa nimekaa zangu kwenye meza tukiwa tunaangalia na nilimsifia kidogo tu  kama ni mrembo  na ndio  akakasirika”Hamza alijitetea , lakini kwa bahati nzuri  au mbaya  Regina  na Yonesi wote ni wahanga wa tabia ya Hamza na kwa muda huo alikuwa akimchukia mno  Hamza kiasi kwamba mpaka  meno yake yalikuwa yakimuwasha., Alidhani swala lile lilimtokea yeye tu kumbe  alikuwa  amemfanyia  uhuni na Mlinzi wa kampuni .

Dakika hio hio  Regina aliona aungane na Yonesi  kumshikisha Hamza  adabu l akini hakutaka kuonyesha kama alikuwa na yeye ni mhanga wa kupigwa chabo.

“Kama  ni hivyo  basi unaruhusa yangu ya kumshikisha adabu , angalia tu usije kumuua  au akalazwa, anapaswa kuja kazini”Aliongea  Regina  na kumfanya  Hamza amwangalie  na kuona namna  ambavyo Regina alikuwa amejaa sumu juu yake.

“Usijali mkurugenzi , najua ninachokifanya”Aliongea  Yonesi  na palepale muonekano wa kishujaa ulimjaa, alikuwa kama komandoo anaejiandaa kwa misheni  ‘shikisha adabu’.

Subiri kwanza  , twendeni  mpaka floor ya pili  katika chumba cha mazoezi”Aliongea  Regina , alijua  ikitokea mfanyakazi wa kampuni kushuhudia tukio  la 

Yonesi kumpigwa Hamza inaweza kuleta  shida

“Kuna haja  ya  hili , mkurugenzi au unakinyongo na mimi?”Aliuliza Hamza.

“Eliza alisema  wewe ndio uliemsaidia  kumuokoa katika udhalilishaji , naamini unao uwezo wa kushindana na  Yonesi japo kidogo, chukulia kama mazoezi ya kukuweka fiti kidogo uonekane mwanaume”Aliongea Regina.

Hamza hakuwa na jinsi zaidi ya kutii maagizo ya Mkurugenzi na  kwenda katika floor ya  pili kwa ajili ya kushikishwa  adabu.

Dosam ilikuwa ni kampuni yenye wafanyakazi  wengi na biashara zao zilihusisha  bidhaa  za thamani , hivyo walikuwa na kitengo cha ulinzi ambacho  ikitokea mzigo unasafirishwa basi ndio huhusika kuimarisha ulinzi , hivyo  kwa ajili ya  idara ya ulinzi  ilitengwa floor nzima ya pili kwa ajili ya mazoezi , kulikuwa na kila aina ya vifaa ikiwemo  Gym  na hata eneo  la kupimana  nguvu.

Ilikuwa ni muda  wa kuondoka kazini , hivyo hakukuwa na watu ndani ya eneo hilo.

Yonesi alimchukua Hamza na kumpeleka katika

Arena , alifanya hivyo ili isitokee Hamza  akakimbia wakati wa kumpiga.

“Ni kweli unataka kupigana  na mimi?”Aliuliza Hamza.

“Usiwe na wasiwasi , ngoja nikunyooshe nyooshe viungo  , lakini sitokuua”

“Basi hakuna shida , ila kumbuka  miguu na mikono haina macho hivyo kuwa makini”

“Acha woga , jali usalama wako  kwanza”

Mara baada ya kumaliza sentesi hio  Yonesi alimsogelea  Hamza kwa spidi huku akinuia kumchapa ngumi ya bega.

Lakini alichokifanya  Hamza ni kuwa na spidi kidogo  tu  kwani  mara baada ya ngumi ile kumfikia aliinama  ikapita lakini  muda huo huo bila ya  Regina kuona

Hamza alishainua mkono  na kugusa msambwanda.

“Ahhhhhh…”

Yonesi alijikuta akipiga  makelele mara baada ya kuhisi mkono ukimgusa upande wa kushoto.

“Mshenzi wewe” Ishara ya mauaji ilimvaa  Yonesi. “Kapteni vipi tena  , mbona unafoka  wakati tunapigana?”Aliongea Hamza ambae alikuwa  amejificha kwenye kona ya steji.

“Umenigusa tena”,

“Unamaanisha nini nimekugusa , kwahio  wewe unaweza kunipiga lakini mimi siruhusiwi kukugusa, kama ni hivyo  unaweza kuniua hapa hapa”.

“Mhenzi wewe , hujui kupigana kazi yako ni kugusa  tu”

“Nimegusa wapi?”Hamza  alikuwa akijua fika ni wapi amegusa  lakini alijifanyisha hajui ,  alijisikai vizuri, alitaka kumshikisha adabu  mjeda huyu  bila hata ya kumpiga.

Regina alikuwa akiangalia pambano  na hakuwa akielewa kinachotokea , kutokana na spidi ya  Hamza.

Yonesi hakujua namna ya kuongea tena hivyo alijiamulia kupambana tu , awamu hio alikuwa amedhamiiria kumpiga  Hamza kwa kutumia mguu  na sio ngumi tena 

Hamza aliishia kuvuta pumzi  na  dakika ambayo shambulizi linamfikia  alishafanikiwa kusogea   kushoto.

Yonesi alijikuta akipandwa na hasira mara mbili mara baada ya kuona amepiga hewa , lakini hakutaka kujiuliza Hamza kaweza vipi kukwepa shambulizi lake hivyo  aligeuka na kumsogelea tena  na kuanza kurusha ngumi mfululizo.

Hamza alikuwa akijifanyisha kuwa muoga wa ngumi zile na kurudi nyuma  kila mara  Yonesi alipokuwa akishambulia , alionekana kama amezidiwa lakini ukweli ni kwamba   yeye ndio aliekuwa  na maamuzi ya kumaliza pambano hilo au kulirefusha 

Yonesi aliishia kumkimbiza Hamza kila mahali alipohama lakini mwisho wa siku yeye ndio  aliekuwa wa kwanza kuchoka.

“Kwanini unakuwa  muoga na kukimbia kimbia kama panya , kama kweli wewe ni mwanaume  usikimbie  na tupigane ana kwa ana”

“Kapteni unachofanya ni kulazimisha nifanye kitu ambacho sitaki  na kwasababu sitaki nitaendelea kukimbhia”

“Kuwa mwanaume basi”Aliongea kwa kufoka.

Hata Regina ambae alikuwa akiangalia  alishindwa kuvumilia  mara baada ya kuona Hamza anachofanya ni kukwepa tu na hashambulii.

“Hamza jikaze  basi hata kidogo?”Aliongea.

“Nijikaze  niumie , naogopa  nisije kupoteza  taifa la kesho hapa hapa”

“Huna lolote , pigana  na mimi acha

kukimbia”Aliongea Yonesi  na palepale alimsogelea Hamza kwa mara nyingine , uwezo wa  Yonesi kuanzisha mashambulizi haukuwa wa kawaida , alikuwa akijua kujipima  wakati wa kushambulia mno   alichokosa ni spidi tu basi na ndio maana kila shambulizi alilorusha  Hamza alikuwa na uwezo wa kulikwepa bila shida yoyote 

Mwishowe Yonesi aliona kabisa Hamza pengine kuna kitu anaficha , inawezekana vipi mtu wa kawaida kuweza  kuwa na stamina ya aina hio , maana  yeye alikuwa amechoka  lakini Hamza ni kama bado ndio anaanza na anahema kawaida tu.

Kilichomkasirisha zaidi ni kwamba mpuuzi huyo alikuwa akimwigizia  na hakuwa akionyesha uwezo wake kabisa ,  kitendo hicho   kilimfanya  Yonesi aone ni udhalilishaji.

Mara baada ya kufeli zaidi ya mara tano , hatimae alipata wazo  ambalo lilimfanya  adondoke chini  kwa kupiga magoti  na kufunika  uso wake na viganja  na kuanza kulia kwa kwikwi.

Kwa namna ambavyo  Yonesi alikuwa akilia  ilikuwa ni kama  mke aliefiwa na mume wake , mtu yoyote angemuona  mjeda huyo mrembo  angemuonea huruma.

Hamza alijikuta akiingiwa  na  aibu baada ya kuona   Yonesi analia   hata kwa  Regina hivyo hivyo  alishangaa kuona Yonesi analia, maana ilikuwa mara yake ya kwanza  kumuona afande akilia   baada ya kupigwa.

Ukweli ni kwamba Regina hakuona  Hamza akimpiga  Yonesi  na upande mwingine alimjua Yonesi kama mwanamke  jasiri  na mkali.

“Hamza muombe msamaha Yonesi , kama mwanaume unatakiwa kujua wakati wa kuacha”Aliongea Regina lakini Hamza alijihisi  ni kama anaonewa , maana hakumpiga hata kidogo Yonesi.

Hamza hakutaka kuona Yonesi akiendelea kulia na alimsogelea kwa ajili ya kumbembeleza 

“Kapteni  usiendelee kulia , nimekosa mimi nisamehe sa…”

Kabla hata  Hamza hajamaliza kuongea  Yonesi aliibuka na kibao na kumchapa nacho Hamza upande wa kushoto, baada ya kibao aliunganisha na ngumi  kwenye tumbo na kumfanya  Hamza kutoa mguno.

“Naomba  unisamehe Kapteni ,  vinauma , vinauma”Hamza  alibembeleza asemehewe huku akifanya kuugulia  maumivu  chini sakafuni.

“Wewe mpuuzi  nitahakikisha  kila siku utakayoniona unanikimbia”Aliongea Yonesi  huku akisimama  na kupumua kwa ahueni.

Regina  aliekuwa chini ya steji alishia kushangaa  mara baada ya kugundua kumbe  Yonesi alikuwa akijifanyisha mdhaifu kutafuta nafasi ya kumshitukiza  Hamza.

Mashambulizi  yale yalionekana kumuumiza Hamza na  Regina alijiuliza  atakuwa katika hali gani. 

Mara baada ya  kilichotokea  Regina aliishia kumlaani Hamza ndani kwa ndani kwa kujifanyisha kijeba  na kuchungulia chungulia wanawake na kujiambia  anastahili  kweli kipigo.

Mara baada ya  kumshinda Hamza , Kapteni Yonesi  hakuhisi hata kidogo  furaha  wala mafanikio , alikuwa akijua   kabisa yeye ndio ambae ameshindwa.

Aliishia kujiwazia  huyu  Hamza  kila  dakika anazidi kuonekana sio wa kawaida na pengine  hata kufanywa  kuwa msaidizi  ni kutokana na  Regina kufahamu hilo.

“Mkurugenzi , nitaondoka sasa , kwaheri”Aliongea  Yonesi.

“Ni kweli unapaswa kwenda kupumzika , siku imekuwa kubwa kwako”Aliongea.

Hamza alikuwa bado amelala kwenye steji licha ya  Yonesi kuondoka  na Regina alimwangalia kikauzu.

“Uko sawa wewe? , kama bado hujafa amka tuondoke”

“Regi nimeumia  kwa ndani”Aliongea Hamza.

“Acha maigizo , kama huamki naondoka zangu”

“Nataka  busu ili niamke”Aliong ea  na kauli ile ilimshangaza  Regina na kumfanya kuona aibu za kike , lakini tofauti na kuwa na hasira  alimuuliza.

“Wapi unataka upigwe busu?”

Hamza mara baada ya kusikia swali lile alijikuta akifurahi  na kujiambia kumbe kupigwa nako  kuna faida na kwa haraka haraka  alitumia kidole chake kuonyesha eneo la mdomoni.

Regina alivuta pumzi  nyingi   huku  ukauzu ukizidi kumvaa , aliangalia pembeni  na   kuona kifaa cha kuchukulia mazoezi ya mkono   na  mara baada ya kukiokota alimlenga nacho Hamza mdomoni.

“Kiss your ass!!”

Hamza  aliweza kukwepa haraka  kifaa kile   kabla hakijampata  na kusimama na  kumwangalia mwanamke huyo alivyokuwa amefura kwa hasira. “Hey! Nilikuwa nakutaia tu usikasirike hivyo”

“Ukiendelea kuongea ujjinga nitahakikisha unapata  mshahara nusu”

“Ah , boss basi yaishe, nimekosa mimi naomba usinikate mshahara , nitaenda kuwasha gari tuondoke sasa”

Hamza hakutaka kukosa pesa kwa tukio  dogo kama hilo , isitoshe kutafsiri makatarasi yote yale haikuwa kazi ndogo ambayo anaweza kukubali kukatwa mshahara kizembe.

Lisaa limoja baadae  wote waliweza kufika nyumbani  na  Shangazi alikuwa bize kuandaa chakula cha usiku.

“Hamza  vipi siku yako ya kwanza kazini?”Aliuliza na Hamza alitaka kusema   amenyanyaswa siku  nzima  lakini Regina alimpiga  jicho  asije kuongea ujinga  na akaacha  na kuanza kucheka.

“Haha.. Shangazi  siku yangu ilikuwa nzuri sana , sitaki tu kuongelea ilivyokuwa  lakini ,itoshe kusema nimepata  Vitamini ya macho”

Kauli yake ilikuwa na zaidi ya maana  na kumfanya   Regina aliekuwa  pembeni yake kupandwa na hasira na kutaka kumpiga na rimoti palepale.

Hamza alikuwa na miadi yake hivyo hakutaka kukaa sana nyumbani , ijapokuwa chakula ndani ya nyumba hio kinawahishwa  hakutaka kula kwanza mpaka amalizane na Amiri., hivyo alipandisha juu kujiandaa kuondoka lakini wakati anashuka  aliweza kumsikia   Regina akiongea na simu na moja kwa moja aliweza kujua ni baba yake aliekuwa akiongea nae lakini aliishia kukaa kimya , ilionekana kuna jambo ambalo liliwafanya kujibishana  tena.

“Shangazi natoka  kidogo , kuna rafiki yangu nataka  kuonana nae”Aliongea  Hamza.

“Lakini chakula  cha usiku kinakaribia kuiva utawahi kurudi?”

“Sijajua Shangazi , kama nitachelewa naomba uniwekee tu  nitakula nikirudi , anaonekana kuwa na matatizo”Aliongea Hamza na  Shangazi alionekana kumuelewa , ukweli alifurahi kuona Hamza alikuwa angalau na rafiki.

“Sawa, wahi ukamuone rafiki yako”

Hamza mara baada ya kuaga  alitaka amuage  Regina lakini   mwanamke huyo alionekana   bado alikuwa akiongea na simu , huku muonekano wake ukiwa umebadilika hivyo alijua maongezi hayo ni siriasi.

Alitoka nje  na  kuchukua ile Lexus  ya Regina  na kuondoka , akiwa njiani alimpigia  Amiri  lakini hakupokea , lakini hata hivyo hakutaka kughairi  , aliendelea kuendesha na wakati anakaribia  daraja  la kigamboni  simu iliita.

“Uko wapi bro , nilikuwa nimetingwa kidogo”

“Okey , ndio nimetoka  niambie tuonane wapi?”

“Samaki Samaki bro , ukikaribia nishitue”

“Poa”

Licha ya  kwamba anakoenda ni mbali , lakini  kutokana na kuwa na gari kali  hakuona shida , pili  hakuwa ametoka usiku muda  mrefu.

Ilikuwa ni saa moja  kwenda na nusu na foleni  hazikuwa kubwa  sana upande wa magari yanayorudi mjini , hivyo hakupata shida kubwa, dakika arobaini  tu aliweza kufika Samaki Samaki  na  alimpigia simu  Amiri.

“Bro umewahi mno , nikajua kwa foleni utachukua muda kidogo kufika”

“Nipo  na usafiri binafsi , tuonanae wapi”

“Ah kumbe , nisubiri hapo mgahawani nakuja   muda si mrefu”

Hamza aliangalia mazingira ya eneo hilo  na   palionekana kuchangamka, kulikuwa na magari mengi.

Kutokana na gari  yake  kuwa ya bei ghali  hakupata shida ya kuegesha , watu waliomuona akitoka kwenye gari  hio ya Lexus walimwangalia  kwa macho ya  maswali mengi.

“Bro!!!”

Hamza kabla  hata hajapiga hatua kuingia ndani ya mgahawa aliweza kuitwa kwa nyuma  na aligundua aliekuwa akimwita ni Amiri.

“Nilijua utachukua muda”Aliongea.

“Nilikuwa maeneo haya haya , njoo  tuongee kwenye gari”Aliongea  Amiri  huku akizungusha  macho.

Amiri  alikuwa ameegesha Aud yake   katika maegesho ya muda mfupi na waliingia ndani wote , jamaa huyo alionekana kuwa na haraka mno  na hilo Hamza aliliona.

“Unaonekana  akili haijatulia lakini kwa muonekano wako nadhani  hali sio mbaya kama nilivyofikiria”Aliongea Hamza.

“Nimechanganyikiwa kutokana na kuwa na maswali mengi , lakini  bado nina hofu ,  pengine  unaweza kunipa jibu ambalo linaweza kuifanya hali yangu kuwa mbaya zaidi”Aliongea.

“Huna haja ya kuwa na wasiwasi , wewe ndio ambae ulichukua hatua , inabidi  kuyakabili matokeo”

“Nadhani tuongelee  hapa hapa kwenye gari , nina miadi na Melisa , nimepata ahueni  tumeonana kabla ya kukutana nae”

“Unakutana nae  sasa hivi?”

“Ndio , nilimuahidi nitamtoa Out  leo , japo  nina wasiwasi na kinachoendelea lakini angalau nataka

kuondoa huu  mkanganyiko kabla hatujaonana”Aliongea na palepale alitoa  simu pamoja na Earpod na kumpa Hamza.

“Sikiliza hio  na unipe majibu”

“Nisikilize tena , nikajua ni Vidio”

“Bro , tuliweka kamera za vidio   ndio lakini sikuweza kuona cha maana,  mpaka siku moja nilipoona tukio  ambalo sio la kawaida , ndio ambalo lilinipelekea kuweka kinasa sauti”

“Tukio gani?”Hamza aliuliza kwa shauku.

“Sikiliza kwanza hio sauti niliosikia kutoka   ndani kwake”Aiongea na Hamza  alitingisha kichwa kukubali.

 

 

 

Previoua Next