Hamza kadri alivyokuwa akisikiliza ndio uso wake ulionyesha mabadiliko , hayakuwa mabadiliko ya mshangao bali ya kuchanyikiwa pia.
“Mbona nasikia lugha ambayo sijawahi kuisikia popote ni lugha gani hii?”Aliongea Hamza na kumfanya Amiri na yeye kuonyesha ishara ya kutokujua.
“Hapo ndio pamenichanganya sana , hio sauti ni ya Mellisa wangu , siwezi kosea Bro , lakini anaongea lugha ambayo siijui”Aliongea Amiri na Hamza aliongeza umakini katika kusikiliza ili ajaribu kutafsiri nini kinaongelewa , alikuwa akisikia sauti ndio lakini lugha hajawahi kuisikia.
“Hii lugha sijawahi kuisikia popote , au ni lugha sizizo rasmi za kimakabila, wanaongea nini”Hamza alionekana kujiuliza.
“Baada ya hapo watabadili lugha , sikiliza kwa umakini bro”Aliongea Amiri na Hamza alitingisha kichwa na kusikiliza.
“Silvia kadri tunavyochelewa ndio uwezekano wa kurudi kuwa mdogo , tunatakiwa kumpata Princess Natasha mapema kabla ya Profesa”
“Rosaron hatujui mpaka sasa roho ya Natasha inaishi katika mwili wa nani , sio rahisi kumpata”
“Atatutafuta yeye mwenyewe baada ya teknolojia ya
Somnus kufanikiwa , tunatakiwa kusubiri lakini kuwa tayari vilevile, kosa kidogo tu litamuamsha na Profesa , wakiungana itakuwa ngumu kwetu”
“Rosaron unadhani tupo sahihi , namaanisha Pincess Natasha kuwepo hapa Tanzania!!?”
“Tumefika hatua hii kutokana na imani tulioaminishwa , njia pekee ya sisi kuonekana ni kurudi, Silvia wewe ndio uliekuwa mpenzi wake , mapenzi yana nguvu akiamka atakutafuta wewe, ndio maana upo hapa”
Hio ndio namna ambavyo sauti zilisikika , lakini katika maongezi hayo Hamza na Amiri wote hakuna ambae alisikia neno Mellisa , kwa maana kwamba maongezi hayo hayakumhusu Mellisa.
“Sijasikia jina la Mellisa”Aliongea Hamza
“Sijasikia jina lake pia , lakini sauti ni yake”
“Una uhakika hio ni sauti ya Mellisa?”
“Ndio , siwezi kusahau sauti ya Mellisa hata niwe nimelewa pombe”Aliongea na kumfanya Hamza kufikiria kidogo.
“Vipi sauti ya pili unaitambua , namaanisha hio ya mwanaume?”
“Sijawahi kuisikia , lakini kwa rafudhi yake
anaonekana sio mbongo”Aliongea na Hamza pia alikubaliana na Amiri sauti ya pili ilikuwa sio mtu mwenye rafudhi ya kiswahili.
“Hebu subiri”Aliongea Hamza na kisha alichukua Earpord zote mbili na kuzitumbukiza kwenye masikio na kupelekea mbele ile rekodi ya sauti, Amiri alibakia kimya asijue nini ambayo Hamza anajaribu kufanya.
Hamza alikuwa akisikiliza ka kurudisha nyuma sauti na kwenda mbele na ndani ya dakika tano alitoa Eapord zile masikioni.
“Umegundua nini?”
“Najiuliza kwanini hawakuendelea kuongea kwa ile lugha na kubadilisha katika lugha ya kiswahili , pia sauti ya mwanaume tuliokuwa tukisikia ni ya Mzungu rafudhi yake , tena mzungu wa Ulaya kila kitu kinaonyesha alikuwa akiongea na Mellisa kutumia kifaa maalumu au simu”
“Unamaanisha hakuwa ndani kwa Mellisa?” Aliuliza Amiri na Hamza alitingisha kichwa.
“Kama hakuwepo unazungumzia nini kuhusu jina la
Silvia , kwanini huyo mzungu kamtambua kama Silvia mpenzi wangu?”
“Hapa siwezi kukupa jibu la moja kwa moja , kuna mawili ambayo yote yanawezekana , kuna uwezekano ni kweli Mellisa ni Silvia au huenda ana multiple Personality, kuhusu kuwa Silvia hilo halina maelezo mengi lakini kama kweli ana ugonjwa wa nafsi mbili ni ngumu kufanya mawasiliano na mtu au mtu kupigia akitarajia Mellisa kuwa Silvia au Silvia kuwa Mellisa”
“Kaka sijakuelewa kabisa ,
umenichanganya?”Aliongea Amiri na kumfanya Hamza amwangalie machoni , ni kweli bwana huyu alionekana kuchanganyikiwa.
“Ushawahi kuagalia filamu ya Split?”
“Bro mimi sio mpenzi wa Filamu kabisa”Aliongea Amiri na kumfanya Hamza kufikiria kidogo.
“Okey , ipo hivi ninachomaanisha mpenzi wako Mellisa kuna uwezekano akawa mgonjwa wa akili wa kuwa na nafsi mbili , yaanni nafsi ya Mellisa na muda mwingine anakuwa Silvia kama ulivyosikia, ila kwa hapa nashindwa kuamini moja kwa moja , kwasababu kama kweli ni Silvia kwanini akaongea lugha ambayo haieleweki na baadae akahamia katika lugha ya kiswahili kama kawaida, vipi kuhusu alichokuwa akiongea ni kitu cha uhalisia?”
“Kwahio unamaanisha anaweza asiwe mgonjwa wa akili au vipi , mpaka kuweka hayo maswali?” “Ndio anaweza asiwe na shida hio?”
“Kama sio hivyo atakuwa na shida gani?”
“Kuna kitu nakiwaza lakini sina uhakika nacho , hata kama nikikuambia nitazidi kukuchanganya , kitu kimoja ambacho nina uhakika nacho Mellisa hakusaliti kama ulivyomdhannia, sauti ya mwanaume ukisikiliza kwa umakini sio katika ile nyumba”
“Bro unaonekana kujua vitu vingi na ndio sababu ya mimi kukushughulish, awali nilitaka kuona kama kweli Mellisa ananisaliti lakini hisia zako na zangu sasa hivi zimefanana , lakini hilo sina shida nalo , Mellisa ana tatizo na mimi kama mpenzi wake napaswa kumsaidia , Bro yule mwanamke nampenda na napanga kumuoa kabisa , hili swala lazima nilipatie ufumbuzi”Aiongea Amiri akiwa siriasi. “Hili swala nitakusaidia lakini utahitaji kuwa mvumilivu , kitu ninachotaka kujua kutoka kwako je kuna chochote kitu ambacho sio cha kawaida ushawahi kuona pale anapoishi na kwanini ulidhania anakusaliti?”
“Alianza kubadilika , nilikuwa na tabia ya kwenda kwake usiku , lakini siku moja nakumbuka ilikuwa Jumaane miezi minne iliopita , nilikuwa nimelewa siku ile nilipofika kwa Mellisa alikataa kabisa nikiingia ndani na alipogundua ni mimi hakufungua kabisa, kutokana na pombe sikujua kilichotokea , lakini asubuhi nilikuwa ndani kwake , mwanzoni nilidhani baada ya kulewa nilikuja kwake akanifungulia kawaida nikaingia , lakini mara baada ya tukio la pili ndio kumbukumbu za siku hio zikajirudia na kukumbuka alikataa kunifungulia”
“Tukio la pili likoje”
“Hii siku hakunikatalia kuingia ndani , ila alinisubirisha kwenye mlango , jambo hili halikuwa la kawaida , baada ya dakika kama tano niliingia ndani lakini kuna harufu kama marashi hivi ambayo Mellisa hatumii , nilitafuta haya marashi wakati akiwa amelala lakini sikuyaona , haikuwa hivyo tu usiku alikataa kunipa kabisa, haikuwa mara ya kwanza au mbili tu Bro , imekuwa kama ratiba , kila nikienda kwa Mellisa siku ya Jumanne lazima anifanyie janja janja nisile mzigo”Aliongea na kumfanya Hamza kumwangalia Amiri.
“Umesema kila Jumanne , inamaana hata siku ulioenda kwake amelewa na mara ya pili kunusa harufu ambayo sio ya kawaida , ilikuwa Jumanne?”
“Ndio nakumbuka siku niliolewa ilikuwa jumanne , ki ufupi Mellisa kila ikifika Jumanne hataki tuonane kabisa , hii ndio sababu ya kumuwekea kinasa sauti , zile kamera zilikuwa zikileta picha tu ila sauti hakuna , nikaenda kuweka kinasa sauti na jana ndio nimesikia hiki ulichosikia”
Muda uleule simu ya Amiri ilianza kuita na mara baada ya kuangalia jina alimpa ishara Hamza kwamba ni Mellisa ndio anapiga.
“Muda mzee , nilioahidiana nae”Aliongea Amiri na Hamza alimpa ishara apokee simu kwanza.
“Babe uko wapi , mbona hutokei?”
“Nakuja dakika chache , nipo maeneo haya haya” “Sawa , wahi njaa inaniuma”
“Sawa love , nakuja”
“Kwahio unasemaje Mzee?”Aliuliza Amiri mara baada ya kumaliza kuongea na simu.
“Kuwa nae karibu kwanza , angalia kama kuna kitu kisicho kawaida , au matumizi ya dawa yoyote, kwasasa nina shauku na hii lugha waliokuwa wakiongea mwanzo, naweza kuchukua sauti zao nikaitafutie ufumbuzi?”
“Nakuachia kila kitu mtaalamu , mwenyewe nina shauku ya kutaka kujua Mellisa anaongea lugha gani , mwanzoni nilijua labda ni roho mtakatifu , yule ni mkristo na wakristo kuna muda wanaongea lugha zisizoeleweka”
“Kunena kwa lugha wanaita , inawezekana mpenzi wako alikuwa akinena kwa Lugha wakati akiongea na Rosaroni”Aliongea Hamza na kumfanya Amiri kutabasamu.
“Unazingua kaka”
“Sijazingua , naamaanisha ni kitu ambacho hakiwezekani kunena kwa ligha huku unaongea na mtu , tena mzungu”
Amiri alichomoa flash na kuunganisha na OTG kisha akakopi faili lile la sauti na kumpa Hamza.
“Ukipata chochote nishitue nakuaminia sana mtaalamu”
“Nikifanikiwa nitakuambia , ila kuhusu hii lugha…anyway nitakushitua”Aliongea Hamza na kisha alishuka kwenye gari.
“Sema mzee hatujaonana kama wiki na nusu hivi ila muonekano wako umebadilika sana, umekuwa bomba”Aliongea Amiri akiwa ameshusha kioo , ni kama sasa anamuona Hamza akia na mavazi ya bei ghali.
“Nimeangukiwa na bahati , pengine ninaweza kubadilika zaidi ya hivi”Aliongea Hamza huku akitabasamu.
“Haha.. hapo kidogo mrembo Anitha anaweza kukusikiliza , halafu umekuja na usafiri gani , ulipokuwa ukiongea ni kama ulikuwa ukiendesha?” “Nilikuwa nikiendesha ndio , kuna mtu niliomba niendeshe gari yake”Aliongea Hamza hakutaka kumuonyesha Amiri kama alikuja na ile Lexus , maswali yangekuwa mengi .
Hamza mara baada ya kuachana na Amiri alifikiria kidogo , aliwaza kurudi nyumbani lakini wazo hilo ni kama halikuwa kipaumbele kwenye halmashauri yake ya kichwa, lakini mara baada ya kukumbuka alimwahidi Shangazi angekula akirudi aliona arudi nyumbani tu moja kwa moja.
****
Upande wa Regina hakupata hata hamu ya kula mara baada ya kuongea na simu, baba yake alimpigia akimlaumu kwanini anataka kuunua kampuni ya Omega inayojihusha na uhandisi wa Programu endeshi za tarakishi.
Baba yake alimwambia sio vizuri lakini pia ingemgharimu hela nyingi kununua kampuni hio kwani hisa zake zimepanda.
“Regina kwanini unafanya maamuzi bila ya kushirikisha wajomba zako na wakurugenzi wa bodi?”
“Huu ni mpango ambao ulishapitishwa tayari katika kikao kilichofanyika mwezi uliopita”Aliongea Regina.
“Unadhani walichopitisha ndio wanachotaka , wamefanya yote kukusikiliza kwasababu wanakuamini sana lakini vilevile hawana uelewa na maswala ya komputa , Tanzania kwa mara ya kwanza tunaingia katika biashara ya uhandishi wa Programu endeshi , kwanini unataka kujiingiza katika vitu ambavyo huna uzoefu navyo , isitoshe ni mpaka wakurugenzi wote wa bodi wakubali”Aliongea Mzee Wilsoni.
“Kwanini hawakujitokeza kwenye kikao na kunipinga waziwazi?”
“Wewe mtoto , hawakujitokeza mbele yako kwasababu wanaheshimu mawazo ya babu yako , ndio watu waliokuwa wakifanya kazi na babu yako kwa miaka na miaka , wanachokifanya ni kutotaka kuona unafanya maamuzi ambayo yapo nje ya sera ya kampuni”
“Baba , ijapokuwa wewe ni moja ya mmiliki mkubwa wa hisa lakini huna nafasi yoyote ya uongozi , hivyo siwezi kuzungumza hili swala na wewe , kama wao ndio wanataka kuongea basi waache waongee na mimi mwenyewe , sio wewe kuwa msemaji wao”
“Hakuna shida , bodi ya wakurugenzi kesho itakaa kikao na unapaswa kutushawishi kwa fact , ukishindwa kutushawishi usije kutulaumu tukipiga kura ya kutokuwa na imani na wewe kuendelea kuwa katika nafasi ya ukurugenzi wa kampuni, na ikitokea hivyo utapoteza kila kitu”
Wajomba ambao walikuwa wakizungumziwa hapo mmoja wapo alikuwa ni Mzee Willium , huyu alikuwa makamu raisi wa kampuni na mwingine alikuwa ni Mzee Sebastian ambae pia alikuwa Mkurugenzi msaidizi., wote hao walishikiria nafasi hizo kutokana na hisa walizokuwa wakimiliki ndani ya kampuni ya Dosam.
Regina hakutaka kuendelea kujibishana na baba yake na alimwambia kesho ahudhurie kikao cha bodi kama kweli anataka kupinga mpango wa kununua kampuni mpya ambayo imeanza kustawi inayojihusiaha na uhandisi wa programu endeshi, pamoja na akili mnemba.
Ijapokuwa Regina alikuwa ashaweka mizizi yake kama kiongozi wa kampuni lakini bado kuna waliokuwa na nguvu ya ushawishi na haikuwa rahisi ya kuwaondoa.
Wafanyakazi kama Eliza , Prisila na wengineo ambao wananafasi za juu na wanamuamini Regina katika maamuzi ukweli ni kwamba ushaiwhi wao unahesabika kama mdogo mno , kwao walikuwa kama wafanyakazi tu.
Hivyo hata kama viongozi hao wakae kikao na kutaka kufanya maamuzi makubwa yasingepita moja kwa moja , lazima yangepita katika bodi ya wakurugenzi na kisha wao ndio wanapiga kura ya kupitisha maamuzi hayo , huo ndio utaratibu kwasababu kampuni ya Dosam haikuwa ya Regina peke yake.
Kilichokuwa kikimuuzi Regina zaidi ni pale ambapo baba yake alikuwa akitumiwa na watu wa nje kujaribu kumbadilisha mawazo , haikuwahi kutokea Mzee Wilsoni kukubaliana na mawazo ya binti yake , siku zote ni mwenye kumpinga,sio kwamba hakuwa akikubaliana nae bali ni kwasababu alikuwa akijaribu kumlinda kwa staili yake , alijua akimfanya Regina kupunguza kujiamini ndio anamlinda.
Sasa wakati Hamza akiwa SamakiSamaki kama angeingia katika mgahawa huo angeweza kumuona James na baba yake wakiwa pamoja na wazee wawili ambao wana miaka makadirio kama ya miaka hamsini hivi wakiwa wamezungukwa na wahudumu ambao walikuwa wamevalia kimitego.
“Mzee Willium kwahio ni kweli Regina anataka kuinunua Omega?”Aliuliza baba yake James.
Mzee Willium alikuwa na nywele rangi nyeupe tupu, wakati huo walikuwa ameshikilia mrembo mmoja mkono huku akijaribu kuthaminisha maumbile yake.
“Ni kweli kikao cha wahisani kilishapita mbona”Aliongea huku akicheka.
“Mzee Willium nina marafiki zangu kadhaa na tumefanikiwa kumshawishi Wilsoni , tunapanga kupinga kila ambacho Regina ataongea kesho”Aliongea Mzee Sebastiani na kauli ile ilimshangaza kidogo baba James.
“Mzee Wilsoni amekubali?”Aliuliza.
“Wilsoni bado ni mtoto na hajui mambo mengi , tulichofanya ni kusema maneno machache ya hapa na pale na akatuamini , nadhani mpaka sasa amempigia simu binti yake na kumlalamikia lakini ninavyojua mimi Regina hawezi kumchukulia siriasi”
“Kesho katika kikao lazima Regina atakuja na mbinu za kutaka kuwashawishi ili kuinunua Omega , muda huo nitahitaji mnitumie taarifa hio”Aliongea Baba James.
“Usiwe na wasiwasi huna hata haja ya kuomba , tumekuwa tukifanya kazi pamoja kwa muda mrefu , hatuwezi kumruhusu Regina kufanikiwa kuinunua”Aliongea Mzee Willium.
“Ni kweli kabisa alichoongea Willium , tunachosubiri hapa ni James kufunga ndoa na Regina na mpango wetu kuanza , pumbavu kabisa tunaruhusu vipi undugu wa kitajiri tuliojenga kwa miaka kuishia katika mikono ya msichana mdogo kama Regina”
James mara baada ya kusikia kauli ile alitoa cheko na kisha aliinua chupa ya wine akiwa amesimama. “Asanteni sana wazee wangu , ili kuonyesha ni namna gani ninashukuru nitawamiminia kinywaji,
Baadae kama nikifanikiwa katika mpango wangu Dosam tutaiunganisha na kampuni yetu , nawahakikishia sitowaangusha , mtapata hisa za kutosha katika kampuni yetu”Aliongea James na mabwana wale matabasamu yalikuwa nje nje.
“Usiongee sana unamaliza mate tu bwana mdogo , tunajua ukubwa wa familia yenu , hatuwezi kuishi kwa kujibana bana chini ya utawala wa yule msichana mkatili”Waliongea huku wakicheka na kwa pamoja waliinua glasi zao na kugongesheana.
Baba yake na James alimwangalia mrembo aliekuwa nyuma yake na kisha alimpa ishara, mwanamke yule alielewa somo na kimapozi kabisa alizungusha mkono katika shingo ya mzee Willium huku akilegeza jicho.
“Pedeshee Willium muda umeenda na naogopa mwenzio , unaonaje ukinipa lift kwenda nyumbani”Aliongea huku akiwa amerembua , alikuwa mweupe na mapaja yake makubwa yalivutia kwa mwanaume yoyote rijali.
“Hakuna tatizo mrembo , wewe niambie unaishi wapi , halafu kama ni mbali kwanini hukuongea mapema , pengine tungeanza safari mapema”Aliongea huku akimkonyeza.
“Aiyaa, Mzee Willium unajua hadi unaboa … mimi sitaki bwana….”Aliongea yule mwanamke lakini wakati huo akihakikisha manyonyo yake kumsugua vilivyo Mzee Willium.
Upande wa Mzee Sebastian hakutaka kulembesha na alikuwa akichimba mgodi hapohapo mezani kwa mrembo mwenye umbo matata rangi ya kunde, wote walionekana vilevi vimewakolea.
James na baba yake waliangaliana na wote kwa pamoja walitoa tabasamu lenye uovu ndani yake.
****
Siku iliofuata Hamza alienda kazini kama kawaida na alihakiksiha tarakishi yake haifuatiliwi ili afanye mambo yake.
Hamza alijua alikuwa na kazi kubwa hivyo alihakikisha kwanza kiporo cha jana anakimaliza ili awe na muda wa kutosha wa kufanya mambo yake bila wasiwasi ikiwemo swala la kufatilia ile lugha aliokuwa akiongea Mellisa.
Mpaka inafika mchana alikuwa ashamaliza kazi yote na alijisifia kwa kuwa na uwezo mkubwa wa akili wa kufanya vitu haraka haraka.
Baada ya kuona njaa inauma moja kwa moja alitoka na kuelekea mpaka chini kwenye mgahawa.
Kitendo cha kuingia katika mgahawa huo wa kampuni macho yalikuwa yakimwangalia , ukweli ni kwamba tukio la jana ni kama limempa umaarufu na kufanya watu wengi wamfatilie na walifahamu alikuwa msaidizi wa bosi.
Ukiachana na alichokifanya jana siku hio wafanyakazi wa kike ikiwemo Asha na Mirium hamu yao ilikuwa ni kuona namna Yonesi na Hamza wataendeleza pale walipoishia jana, hawakuwa na uelewa kilichotokea jana kwa Yonesi kupigana na Hamza.
Wafanyakazi wengi walikuwa wakiamini lazima Yonesi na Hamza wataishia kuwa wapenzi na hicho ndio ambacho walikuwa wakitamani kuona, waliamini Yonesi hakuwa akinyanduliwa na ikitokea pengine ukauzu wake utapungua na kufanya maisha yawe marahisi hivyo kete zao ilikuwa ni Hamza.
Hamza marra baada ya kuchukua chakula chake hakuhaingika kutafuta sehemu ya kukaa kama jana , aliangalia tu kushoto na alimuona Yonesi akiwa peke yake na alipiga hatua na kwenda kukaa pembeni yake.
“Habari za mchana Kapteni?”Aliongea Hamza
Comments