SEHEMU YA 23.
Yonesi aliishia kuinua kichwa na kumwangalia Hamza kwa sekunde kadhaa na kisha akampotezea na kuendelea na chakula chake , kitendo kile kiliwashangaza wengi na kuona au Hamza ameshamuweza Yonesi.
Muda huo Hamza aliweza kuona Yonesi alikuwa amejisevia Sausage kwenye sahani yake lakini hata yeye pia ni moja ya chakula alichochukuwa , ki ufupi ni kwamba hakubakisha.
Mgahawa huo wa kampuni chakula kilikuwa bure na kulikuwa na msururu wa mapot makubwa ambayo yanachakula , ni kazi yako kupita na kujisevia tu.
“Kapteni , kumbe na wewe unapenda kula Soseji , unaonaje nikikupatia na yangu?”
Maneno hayo yalisikika kikarimu lakini kadri alivyoyafikiria ndio aliona ni kama kuna zaidi ya maana na mwili wake ulianza kubadilika rangi na kujihisi kupatwa na joto licha ya eneo hilo kuwa na AC, aliona kabisa Hamza alikuwa akimfanyia hivyo makusudi kabisa.
“Usije ukanidhania vibaya , naamanisha soseji ya kwenye sahani yangu…”Aliongea Hamza huku akijifanyisha ni mwenye aibu.
Kadri alivyokuwa akiongea ndio ambavyo maneno yake yalivyoonekana ya kihuni , wafanyakazi waliokuwa karibu wakitega masikio yako kama antena baada ya kusikia kauli ya Hamza waliishia kucheka.
“Hakuna ambae atasema wewe ni bubu ukikaa kimya.”Aliongea Yonesi huku akijitahidi kuzuia hasira zake.
Watu mpaka hapo waliona kitendo cha Yonesi kuweza kuvumilia utani wa Hamza inamaanisha alikuwa hamuwezi na sifa zote walimpatia Hamza.
Hamza aliishia kushindwa kuongea na kumwangalia Yonesi namna ambavyo amevaa , lakini ilionekana kutokana na tukio la jana alikuwa amefunga shati lake mpaka kifungo cha mwisho.
Hamza aliona ngoja anyamaze adili na chakula chake , lakini Yonesi mara baada ya kuona ametulia yeye ndio aliongea.
“Wapi umejifunzia mapigano?”
Hamza alisikia hilo swali , lakini alijifanyisha hajasikia na aliendelea kuwa bize na chakula chake, lakini kitendo kile cha kupotezewa kilimuudhi Yonesi na kumfanya apige meza kofi.
“Wewe , nakuuliza swali , hujanisikia au?”
“Kapteni si umeniambia nikae kimya , kwanini unataka niongee tena , unajua unanitesa”
“Wewe..”Yonesi aliishia kusaga meno kwa hasira, alijua fika mwanaume huyo alikuwa akikwepa kujibu swali lake na kutokana na hasira zake aliishia kuinua sahani yake ya chakula na kisha akaondoka akimuacha Hamza mwenyewe.
Hamza aliishia kutoa tabasamu la kichokozi tu , huku akiangalia mandhari ya jiji , aliona inafurahisha sana kutania wafanyakazi wenzake.
Wakati akirudi kwenda juu kuendelea na kazi Hamza hakusahau kubeba tena matunda kwa ajili ya Regina , siku hio hakuchukua ma apple tu bali alibeba na zabibu.
Mara baada ya kufika katika mlango wa ofisi ya mkurugenzi , wakati akitaka kuingia aliweza kusikia majibishano kutoka ndani na kumfanya asimame.
“Mzee Sebastian, Mzee Willium , kama wakurugenzi wasaidizi , hebu niambieni sababu ya kwanini mpo kidedea kupinga hili , naona mnafanya makusudi kabisa kunipinga bila sababu”Aliongea Regina na sauti yake ilionekana imejaa hasira.
“Mkurugenzi wewe ni binti mdogo sana bado , maji unayotaka kujaribu kukanyaga yana kina kirefu ,
ununuzi wako wa awamu hii ni wa kukurupuka”Aliongea Mzee Willium.
“Kukurupuka?, mimi ninachoona hapa ni kwasababu hamtaki kuona kampuni inakuwa kutoka levo iliopo kwenda nyingine na wasiwasi wenu ni kuogopa kupoteza nafasi zenu , mnaonaje mkiniambia ni hisa kiasi gani mnahitaji ili muwe hiari na msishindane na mimi?”Aliuliza Regina.
“Mkurugenzi sisi ni wazee ambao tulikuwa nyuma ya mwenyekiti wa kampuni aliepita mpaka kuifikisha kampuni ilipo sasa hivi hatua kwa hatua , tunaipenda sana hii kampuni ndio maisha yetu , hivyo usiongee ujinga”
“Sitaki kusikia maneno yenu yasio na msingi , nitawapa siku tatu , kama hamtokubali kubadilisha mawazo yenu , kuweni makini maana kuna uwezekano mkaondolewa kwenye nafasi zenu, nishamaliza , mnaweza kuondoka”Aliongea kibabe.
“Wewe mtoto , kwanini unatufanyia hivi , sisi ndio wazee, msingi wa kampuni”
“In this company , only the subordinates of the superior have seniority”Aliongea Regina kikauzu kwa kutumia kingereza akimaanisha wafanyakazi waliopo chini ya uongozi ndio wenye uzoefu zaidi.
“Hakuna shida Mkukufu Mkurugenzi , Willium tuondoke zetu , haina haja ya kuongea tena”Aliongea Mzee Sebastian mara baada ya kupiga kofi kwenye sofa.
Dakika hio hio Mzee Sebastian na Mzee Willium waliweza kutoka na mara baada ya kumuona Hamza ambae amesimama mlangoni , wakurugenzi hao wasaidizi nyuso zao zilizidi kuwa ngumu na kumwangalia Hamza kwa ukali.
Hamza aliishia kupumua tu kwa ahueni huku akijiambia mambo hayo hayamhusu hata wamwangalie vibaya, hivyo aliingia zake kwa CEO.
“Unafanya nini hapa na wewe?”Aliuliza Regina mara baada ya Hamza kuingia , alikuwa amesimama kwenye sofa akiwa na ukauzu.
“Kula matunda kidogo , punguza presha na acha kujisababishia matatizo ya mwili kwa ajili ya kazi”Aliongea Hamza baada ya kumkabidhi boksi lile lenye matunda akiwa na tabasamu.
“Sina hamu ya kula chochote muda huu , unaweza kuondoka nayo tu”
“Nishakula share yangu na yaliobaki ndio nimekuletea”
“Nimesema siyataki ,unaweza kuondoka nayo tu”
“Mbona matunda mazuri haya , unataka yaharibike”Aliongea Hamza.
“Sikia , nina kazi nyingi za kufanya sasa hivi , kula mwenyewe”Aliongea na kisha alirudi kwenye kiti chake .
“Usiniambie unapanga kujipigia zako kile kinywaji tena , ukifanya hivyo nampigia sasa hivi Shangazi simu”
Regina mara baada ya kusikia hivyo aliishia kugeuza kichwa chake huku akiwa amefura.
“Kinachokuuma ni nini?, inakuhusu nini mimi kula au kutokula , sisi sio wapenzi bali tupo katika maigizo tu ya kimkataba , kwanini unanijali sana?”
“Halafu wewe ni mwanaume , kuna haja gani ya kumhusisha shangazi kila kitu , Jiamini”
Hamza mara baada ya kusikia maneno hayo aliishia kutoa tabasamu hafifu na kisha aliweka matunda yale kwenye meza.
“Upo sahihi mimi ni mfanyakazi wa mkataba tu hapa , sio jukumu langu la kujali unachokula wala afya yako , hata upatwe na vidonda vya tumbo ukweli ni kwamba halinihusu , lakini ni juu yangu kumpa mtu yoyote chakula kama hajala , unaweza kula nimeyaweka hapa au ukiona vipi yatupe tu” “Wewe..”
“Kitu kingine , Shangazi yule kwako ni kama mzazi ambae amekulelea mpaka leo hii , kuhusu mimi sina hata wiki tokea tufahamiane , baada ya miezi mitatu kuisha iwe ni wewe au Shangazi sitokuwa na uhusiano wowote na nyie, hivyo sio kwamba najaribu
kukutishia na yeye , sio swala langu hili , ninachokukumbusha ni kwamba ni sawa tu kujifanya mbishi na mwenye hasira za karibu lakini siku zote jaribu kujali na watu wanaokujali”
“Sitaki unifundishe ..”Aliongea Regina mara baada ya kusikia maneno hayo , ni kama yalimgusa kidogo.
Hamza hakuongea lolote zaidi na alitoka katika ofisi hio na kufunga mlango na kufanya hali kutulia.
Mara baada ya kuona ameondoka , Regina alisita kidogo mara baada ya kukaa katika meza yake na kuvuta droo , sasa ile alivyokuwa akitaka kuchukua kile kinywaji cha virutubisho aliishia kukirudisha chini.
Maneno ya Hamza ni kama yalikuwa yakijirudia rudia katika akili yake , alikuwa akimpenda mno Shangazi yake kwani ndio kama mzazi pekee ambae alikuwa akimwelewa , Regina alivuta pumzi na kisha alifunga ile droo na kuchukua lile boksi la matunda na kuangalia ndani , lakini mara baada ya kuona ni zabibu alielewa kwanini Hamza kafanya hivyo na aliishia kuona aibu za kike.
“Muhuni sana huyu..”Aliongea na palepale alichukua Zabibbu zile nyingi katika mkono na kuzisindilia zote mdomoni , zilikuwa na ukakasi , utamu wa aina yake na sukari.
Alitaka kumaliza haraka hivyo alikuwa akila kifujo fujo ili arudi kwenye kuendelea na kazi ,kulikuwa na vipande vya matikiti pia na alivichukua na kuvisindilia vyote na kumfanya hadi mchuzi kumtoka mdomoni.
Kitendo kile kilimfanya mashavu kuvimba mnno kama vile ni mtoto mdokozi anaejaribu kula haraka haraka asishutukiwe.
Muda uleule ndio Hamza alifungua mlango na kuchungulia ndani na aliishia kucheka namna ambavyo mashavu ya Regina yalituna.
Regina alijikuta akitoa mguno mara baada ya kugundulika alichokuwa akifanya huku akiziba mdomo na mikono yake miwili.
Mdomo wake ulikuwa umejaa , alitamani kufoka lakini haikuwezekana na vilevile alishindwa kumeza kwa haraka na aliishia kujionea aibu yeye mwenyewe , kwa mkurugenzi mwenye heshima zake na mwanamke ambae anajali taswira yake kuonekana akiwa ametuna mashavu namna hio wakati wa kula ilikuwa aibu.
“Haha.. nilijua tu , umependezaje , kula taratibu usije ukapaliwa, hebu tukupige na kapicha”Aliongea Hamza.
Regina aliishia kukasirika ndani kwa ndani na kujiuliza kwahio alikuwa amesimama muda wote mlangoni , inamaana aliotea nitakula matunda kivurugu vurugu.
Aliona kama kweli picha itachukuliwa taswira yake ya mwanamke aliestaarabika itaharibika kabisa na kwa haraka haraka aliinua karatasi na kuficha uso wake. Huku akijitahidi kutafuna na kumeza kwa haraka.
“Unataka kufanya nini , ondoka ofisini kwangu la sivyo mshahara wako utakuwa nusu”
“Ah , Boss usifanye hivyo , hii simu kimeo hata Kamera haifanyi kazi, nilikuwa natania tu”
Mara baada ya kusikia jibu hilo kidogo alijituliza lakini alivyowaza namna ambavyo ameonekana alivyotuna mashavu kwa ajili ya chakula masikio yalishika moto.
Ukweli hakujua nini kinaendelea lakini alijishangaa tu kupotezea msimamo wake mbele ya Hamza.
Alijiweka sawa na kisha akajifuta midomo na tishu na akaurudia ukauzu wake kama vile hakuna kilichotokea na kisha akaguna kidogo.
“Ukirudia tena ninakuhakikisha mshahara wako utapata nusu”Aliongea huku akionyesha hadhi yake ya ubosi.
“Sawa bosi , nitaenda kuendelea na kazi”Aliongea Hamza akiwa katika muonekano wa kizembe huku akitingisha kichwa na kuondoka.
Regina mara baada ya Hamza kuondoka alijikuta akijibwaga kwenye kiti chake kama mtu ambae ametua mzigo mzito kichwani.
Mara baada ya kuanza kufikiria kilichomtokea sekunde kadhaa zilizopita alijikuta akicheka mwenyewe na kujiambia hili ni tukio lake la ajabu kumtokea akiwa kazini.
Kwa namna alivyocheka alipendeza mno , kana kwamba ni mmea uliochanua wakati wa ukame mwingi, lakini kwa bahati mbaya tukio hilo hakuna ambae aliweza kuona.
Hamza hakuwa na chakufanya, kazi alikuwa amemaliza na alijikuta akiingiza gemu katika tarakishi na kuanza kucheza kupoteza muda lakini alikuja kusitishwa mara baada ya simu yake kuita , alipoangalia namba ilikuwa ngeni kwa maana hakuwa ameisevu.
Bila kujiuliza mara mbilimbili aliamua kuipokea ili kusikiliza ni nani anampigia , sauti iliosikika ilikuwa ya mwanamke.
“Hello , Mr Delivery”
Ilikuwa ni sauti tamu kweli , pengine aliekuwa akiongea hivyo alikuwa ameilegeza.
“Naongea na nani?”Hamza alikuwa akihisi aliekuwa akiongea nae lakini alitaka kuthibitisha.
“Mteja wa vvungu , Hamza nahitaji mzigo unifikie leo hii , nadhani Alex alikuambia”Hamza mara baada ya kuthibitisha mwili wake ulimsisimka.
Ukweli ni kwamba ni kama ana katabia ka kusahau baadhi ya vitu , ijapokuwa alikuwa na shauku ya kutaka kujua vyungu vile vilikuwa na siri gani mpaka kununuliwa kwa kiasi kikubwa cha pesa , lakini mara baada ya kujiunga na famiia ya Regina ni kama alisahau kwa muda.
“Nakumbuka ndio , nitakuletea mzigo, ngoja niwasiliane na Alex kabisa, saa ngapi nifike?”
“Muda ni uleule Mr Hamza”Aliongea mwanadada Frida upande wa pili na sauti yake ilionekana kuwa na ucheshi.
“Leo lazima nijue vungu hivi vina siri gani?”Aliwaza Hamza na kisha paleale alitoa jibu kwamba muda tajwa lazima awe hapo akiwa na chungu.
Hamza hakuwa akijua kwamba swala la Frida kumchagua yeye kama mleta vyungu lilimfanya Alex kumchukia kwa kudhania mrembo huyo ana hisia za kimapenzi na Hamza.
Muda husika mara baada ya kuwadia Hamza ilibidi kwanza akamuage Regina ili afahamu kwamba hawezi kwenda nae nyumbani , alitaka kuunganisha moja kwa moja.
Mara baada ya kumwambia kwamba kuna sehemu anapitia Regina hakuwa hata na haja ya kuuliza ni wapi , aliishia kuitikia tu.
Kwasababu hio Hamza hakuacha kujisikia vibaya , kwa namna ambavyo Regina alimchukulia , ni kama vile alikuwa na nafasi ndogo sana kwenye maisha yake , hakujua ni kwanini lakini aliona yeye na Regina hawawezi kuwa wapenzi na ndani ya miezi mitatu kila mtu atashika lake.
Kwasababu hakuwa na usafiri ilibidi achukue mwendokasi kwa mara nyingine , muda ulikuwa umeenda na kwa kuminyana sana aliweza kufika Mwenge ndani ya dakika ishirini pekee , kutoka Mlimani city yalipo makao maku ya kampuni mpaka Mwenge hapakuwa mbali.
Hamza mara baada ya kufika katika kiwanda hicho bado hakuacha kushangaa , kitu kingine siku hiio kulikuwa na mabadiliko kidogo , wale wanawake ambao walikuwa bize kutengeneza vyungu hawakuwepo ni kama vile kiwanda kimesitisha utengenezaji kwa muda.
Hamza hakujali sana , mara baada ya kujitambulisha hakukuwa na maswali mengi , alipewa mzigo na utaratibu ulikuwa ni uleule kama wa mwanzo.
Hamza alidhani angemuona Alex ndani ya hilo eneo , lakini hakuwepo hivyo pia hakujishughulisha kumpigia simu.
Muonekano wake ulikuwa mzuri zaidi kuliko wiki aliofika hapo kuchukua mzigo , alikuwwa amevaa suti ya bei ghali na viatu vya bei ghali , hivyo ilifanya watu kumwangalia kwa namna flani ya kumshangaa , wengi wao ikiwemo wadada.
Kilichombeba Hamza licha ya kuonekana muda mwingine kama Mzembe ni muonekano wake wa kuchanganya rangi , kitendo cha kuingia katika daladala na muonekano wake ni kama vile hakuwa na hadhi hio , watu walimpa hadhi ya kuwa na usafiri binafsi.
Mambo yalienda haraka haraka kuliko siku ile kwani alikuwa ashajua anuani ya nyumba mzigo ulipokuwa unaelekea.
Baada ya kufika Madale kwenye geti alibonyeza kitufe na aliitikiwa kwa ndani na mlango ukafunguliwa , lakini siku hio mlinzi alikuwa tofauti , hakuwa yule wa siku ile ambae aliikuwa akimwangalia kwa macho ya dharau dharau , aliekuwepo alikuwa ni kijana mdogo sana.
“Karibu Bro”Aliongea yule kijana , alikuwa humble kuliko ilivyokuwa kawaida, pengine ni kutokana na muonekano wa Hamza.
Hamza mara baada ya kupita getini alielekezwa aende moja kwa moja ndani , ilikuwa ni tofauti na siku ile alipofika mrembo yule alikuwa kwenye bwawa la kuongelea.
“Welcome!!”
Sauti tamu ya mrembo Frida ilimkaribisha, siku hio mwanadada huyo alikuwa na muonekano wa tofauti kabisa , alikuwa amevalia suti ya rangi nyeupe na miwani ya macho , alionekana kuwa katika mavazi ya kikazi zaidi tofauti na ya nyumbani.
Alimkaribisha Hamza kwa tabasamu , ilikuwa ni kama vile anamjua na jabo hilo Hamza aliliona pia , lakini hakufikiria sana.
“Nimeleta mzigo boss wangu , sijui utaratibu ni uleule naufungua kwanza?”Aliuliza Hamza.
“Haina haja , naamini hakuna makosa”Aliongea na Frida hakumpokea Hamza bali aligeuka na kurudi ndani na Hamza alielewa , alipaswa kuingia ndani ya jumba hilo la kifahari.
Nyumba hio kwa nje ilionekana nzuri , japo haikuwa kubwa sana kama ile ya Regina lakini ilikuwa nzuri ya kupendeza ambayo ilitosha kuitwa Mansion.
Hamza mara baada ya kuingia ndani aliweza kuona uzuri halisi sasa , staili ya upambaji ilikuwa ni ile ‘go
all out’or maximalist yaani juhudi kubwa zilitumika
kuhakikisha mapambo mengi kama hayo yanaendana na muonekano wa sebule na kufanya ipendeze , ilikuwa tofatui na nyumba ya Regina ambayo samani za ndani zilikuwa chache huku upambaji ukiwa ni ule mwepesi, Hamza alijiambia iwe upambaji ni vitu vichache au vingi kilicholeta maana eneo hilo linapendeza na linaendana na tabia ya mtu.
Regina alikuwa kauzu ndio maana hata mazingira yake yalikuwa mepesi , hakupenda kuzungukwa na mapambo mengi ya thamani ya juu , Frida alionekana kama mwanamke mcheshi na anaependa kujiachia na ndio maana alipenda kuzungukwa na mapambo ya kifahari.
Hamza alizungusha macho kwa haraka na aliweza kuona tarakishi ikiwa juu ya meza na baadhi ya makaratasi yalionekana , ilionekana alikuwa akifanya kazi na hivyo ilimpa ishara ya kwamba hakukuwa na chumba cha ofisi kama nyumbani kwa Regina.
“Siku ile nilidhani kwa urembo wako utakuwa celebrity , lakini napata hisia kazi yako itakuwa ni ya
kutaaluma zaidi”Aliongea Hamza na kumfanya Frida kucheka kidogo, alikuwa mrembo na alipendeza alivyocheka.
“Nikajua mpole , ila unaonekana ni muongeaji”
“Mimi sio mpole , kuna muda nakuwa mkimya tu , ila nachangamka sana mbele ya wanawake warembo” “Haha..weka kwanza mzigo chini”Aliongea na kumfanya Hamza kukumbuka kumbe alikuwa amebeba boksi.
Frida alimwangalia Hamza kwa umakini , ni kama kuna kitu alichokuwa akikitafuta.
“Nilijua pia wewe ni mtu wa Delivery , ila unaonekana sio wa kawaida?”Aliongea.
“Unamaanisha nini mimi kutokuwa wa kawaida?”
“Mavazi yako , ineonekana umetokea ofisini na sio ofisi ya kawaida , mtu wa kawaida hawezi kumudu kuvaa Armani , Jimmy Choo , Audamars Piguet na Monte Blanc, sio mavazi ya mtu wa hadhi ya delivery haya”Aliongea Frida huku akiwa amemsogelea Hamza kwa ukaribu na kuchunguza mavazi yake.
Hamza alikuwa ashasahau kama amevaa mavazi ya bei ghali , ukweli ni kwamba asubuhi alivyorushiwa na Regina nguo hizo hakujiuliza uliza ni Brand gani, pengine labda ile staili ya Regina alivyomrushia kama vile ni nguo za mtumba, lakini sasa ni kama anaambiwa alikuwa amevaa suti ya Armani , Viatu Brand yya Jimmy Choo , Saa Brand ya Audamars Piguet na mkanda wa Monte Blanc, aliishia kumlaani Regina ndani kwa ndani kwa kumvalisha mavazi yasioendana na hadhi yake, alijiambia yaani anapokea mshahara wa milioni moja lakini amevalishwa mavazi ya milioni kumi , tena akapanda kabisa daladala.
Kwa mtu wa kawaida pengine ingeonekana mavazi hayo kuwa kitu cha ajabu lakini kwa mwanamke kama Regina ambae hela ni kitu cha kawaida, ukweli ni kwamba alifanya kuagiza tu kwa kutoa vipimo na alieleta mavazi ndio alichagua ya gharama ya juu, lakini hata kama angeenda mwenyewe kununua basi angechagua mavazi ya bei hio hio , labda brand tofauti tu.
Hata hivyo aliona mrembo huyu alikuwa na uwezo wa kuzifahamu Brand, maana ilikuwa ni kwa kuangalia tu ashajua.
“Usipagawe na haya mavazi ya kawaida sana , mimi ni wale wa nimevalishwa na .. ki ufupi ni kwamba kutokana na muonekano wangu nafanya matangazo ya nguo , nikirudi navua nawarudishia wenye mali yao, nimebadilika muonekano ila sio hadhi”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu lakini kauli ile ilimfurahisha Frida maana imekaa ki uongo sana.
“Anyway , niite Dr Frida Franklin, nadhani nimejibu swali lako , mimi sio celebrity mpaka kuvalishwa nguo kwa ajili ya kutangaza biashara”Aliongea kwa tabasamu na kisha alibeba boksi lile na kuondoka sebuleni.
Hamza aliishia kutoa tabasamu tu na sasa ndio anajua mrembo huyo ni Dokta , ndio maana alionekana kitaaluma taaluma.
“Hehe. napenda wanawake wasiotabirika kama hawa..”Aliwaza Hamza na palepale alikaa kwenye sofa.
Dakika chache tu Frida alirudi akiwa na kibunda cha hela na kumpatia Hamza jambo ambalo lilimfanya ashangae.
“Mbona nyingi tofauti na malipo yaliopita?”Aliuliza kwa shauku.
“Leo nakulipa kulingana na muonekano wako , hio ni hela ya delivery kuhusu malipo ya mzigo nishalipa kwa Alex moja kwa moja”Aliongea na kauli ile ilimpagawisha Hamza , alikuwa akipenda hela , lakini kulipwa kitita cha pesa halikuwa jambo la kawaida.
“Hivi vyungu kwanini thamani yake ni kubwa , kuna haja ya kutoa kiasi chote hiki cha pesa?”
“Unataka majibu?”Aliongea Frida akiwa na tabasamu huku akikaa kwenye sofa.
“Ukinijibu utaiondoa shauku yangu?”
“Kilichokufanya kuwa na hiari ya kuleta delivery licha ya kuwa na muonekano huo ni dhahiri shauku ndio inakusukuma , kama ilivyokwako , mimi pia kutoa kiasi kikubwa hivyo kwa ajili ya kuleta delivery shauku yangu imenisukuma pia”Aliongea
“Shauku gani?”
“I see you’re in the initial stage of sorcery,what led you to the choice of delving into the study of magic??
“Naona upo hatua za mwanzoni za kujifunza uchawi,nini kimekufanya kuchukua maamuzi ya kujifunza ulozi”Aliuliza kwa kingereza lakini swali lile lilimfanya Hamza kubadilika ghafla tu.
Comments