Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

SEHEMU YA 24.

Swali lile ilikuwa ni kama Trigger  ya bunduki , Hamza alibadilika palepale , zile nywele zake za kizungu zilisimama na kuanza  kuchemka  kama singa singa huku sura yake ikitisha.

Ilikuwa  ni kufumba  na kufumbua Miwani ya Frida ilishadondoka chini  huku yeye mwenyewe  akielea hewani  akiwa amezingirwa na kitu kama  kizimba  cha Dimension’tatu  chenye kufika mwanga flani mweupe na kufifia kwa wakati mmoja.

Hamza hakuwa na huruma hata kidogo , muda huo alionekana sio  Hamza tena , ni kama shetani.

“Wewe ni nani?”Sauti hio ndio iliomtoka Hamza  huku Frida  akiendelea kufurukuta.

“Naitwa… naitwa  Frida Franklin Genesha , Agent Two F”Aliongea  na mara baada ya kuongea vile usinga wa nywele za Hamza ulirudi katika hali yake ya kawaida  na Frida alidondokea katika  sofa.

Hamza alisogea mpaka katika Sofa la mbele na kukaa chini huku akikunja  nne na tabasamu la uovu usoni .

“Haina  haja ya  kuendelea kuwa  katika muonekano feki ,  unaonaje ukiondoa hio Mask ya kichawi tuone sura yako halisi”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu na kauli ile ilimfanya Frida  aliekuwa akihema kama mbwa aliekimbia maili nyingi kutoa mshangao.

“Ulinifahamu  tokea  siku ya kwanza!!?”Aliuliza akiwa katika hali ya mshangao  na  Hamza  aliishia kutoa tabasamu.

“Nilipokuja hapa siku ya kwanza sikukufahamu  moja kwa moja , lakini kuna  kitu kilinifanya nikushuku  mara moja”Aliongea Hamza na kumfanya  Frida kuongeza umakini.

“Inawezekana  ikawa kawaida  katika jamii , lakini  ni  mara chache sana  kushuhudia mwanamke anaogelea akiwa  na pete ya thamani kubwa kidoleni’Aliongea na  palepale alinyooshea mkono wa Frida aliovaa  pete.

Frida mara baada ya kusikia  kauli ile sasa alielewa  , ni kweli tokea avae hio pete hakujua ni lini aliivua na anasababu  za kufanya hivyo.

“In the Knows kati ya mwanachama na mwanachama wa Wiccan  katika kutambuana  mara nyingi  huhusisha  alama ya vito , japo zipo njia nyingi,mimi nilikufahamu  na nilijua  kuna uwezekano na  wewe umenifahamu , nimekuja leo hii nikitarajia swali lako”Aliongea Hamza.

“Haiwezekani ,  ni kweli pete yangu  ipo katika  orodha ya  In  the Knows  lakini  hii pete  aina ya Pentacle iliotumika  ni siri ya dunia, alama yake  inaingia katika orodha ya The lost symbols  , mpaka

kuifahamu  inamaanisha  na wewe ni mwanachama,  tena katika digrii ya juu”

“Mimi sio mwanachama wa Wiccan”Aliongea Hamza kivivu  huku akitoa tabasamu la kizembe.

“Kama wewe sio mwanachama wa Wiccan  ni nani , wewe ni  Muislamu , Mkristo au Mbuddha?”

“Unaniuliza swali la namna hio  inanifanya nishangae , umejitambulisha kwangu kama   Agent  Two F , hii ni  neno la kodi ambalo  Dokta Genesha alinitajia , ulivyotaja  jina hilo nikakuacha mara moja , nadhani unalifahamu hivyo ,  kama  ndio  haina haja ya kuniuliza mimi nipo upande upi  wa kiimani katika ulimwengu huu , hayo ni maswali ambayo wewe  unatakiwa kunijibu , Vinginevyo  nitaamini  hujatoka katika kivuli cha Dokta Genesha , ushajua siri yangu  napaswa kukuua kama huna majibu”Aliongea na   Frida alionekana kufikiria kidogo.

“Nimechukua  tahadhari tokea unakaribia kufika hapa , lakini tahadhari haitoshi ,  umenifahamu kama mfuasi wa Wiccan  na siwezi kukupa majibu nikiwa  katika vifungo vya kiroho vya Wiccan”.

“Njia gani  unaweza kujifungua katika vifungo na kujibu maswali yangu yote , nakupa heshima hii kwasababu ya Dokta  Genesha  hivyo unapaswa  kuwa mkweli”Aliongea  Hamza.

“Njia pekee ni kuuvua muonekano wangu  katika chumba cha nuru , ndio jia  pekee ambayo watu wa madhabahu hawatogundua , nikiwa katika  uhalisia  wangu  nitaweza kujibu maswali yako yote”Aliongea na kumfanya  Hamza kushangaa.

“Kwahio wewe ni Double Agent , unafanya kazi chini ya Sinagogi na Wiccan kwa wakati mmoja?”

“Wote tuliopo chini ya kivuli cha Genesha kiasili ni wanasinagogi , sidhani hili ni swala la kukushangaza , kabla sijaingia katika chumba cha nuru  unapaswa kujibu swali langu  kwa maelekezo ya  Dokta Genesha?”

“Uliza swali lako?, maana ikija  wakati wa maswali yangu  unapaswa kujibu yote”

“Ushawahi kuota ndoto  kama uhalisia , upo katika mazingira ambayo ni tofauti na ulimwengu wa kawaida?”Aliuliza  Frida huku wakiwa na muonekano wa siriasi.

“Umejuaje nimeota  ndoto ya namna hio?”Aliuliza Hamza akiwa ameshangaa , ilikuwa ni kweli kabisa  aliota  ndoto yupo katika mazingira ambayo  sio ya kawaida.

Hamza ni  kama sasa anaanza kuamini uwezo wa  Frida , ukweli ni kwamba  wakati anarudi Tanzania  alikuwa akisubiria mtu ambae anaweza kumwambia yeye ni nani , sio kama hakuwa akijua yeye ni nani  la hasa , alikuwa akijua yeye ni  Hamza  na historia yake kwa ufupi , lakini kuna swali kubwa ambalo linahusiana  na nguvu iliopo ndani ya mwili wake.

Kwa maelekezo ya Dokta Genesha ambae alikuwa mwalimu wake , alimwambia  amtafute Agent Two F na ndio maana  mara baada yya  Frida kutaja jina lake kamili  alimuacha  mara moja.

Frida alimwangalia  Hamza , licha ya kuonekana kuridhika lakini  alionekana akifikiria pia.

“Ulichoota sio ndoto , uhalisia wako ndio unakuita, ndio njia pekee ya kumfahamu mtu aliekuwa nyuma yako mpaka  kufikia  leo hii”

“Unamaanisha Mzee?”

“Hio si ndio misheni yako kwa sasa ya kumfahamu Mzee , huwezi kumfahamu kabla ya kuujua uhalisia wako , mimi sio mtu wa  kujibu maswali yako,  ni  wa kukuongoza tu kisayansi kupitia taaluma yangu, kufupisha tu majibu yapo ndani ya nafsi ambayo imelala ndani yako”

“Nafsi unataka kumaanisha kuna nafsi zaidi ya niliokuwa nayo?”Aliongea Hamza akiwa katika mshangao na Frida  tofauti na kujibu  alishika ile  tarakishi  na  kuchezesha vidole kwa dakika kadhaa na kumpatia  Hamza.

“Hizi  ni takwimu za wagonjwa wa  akili   kwa upande wa Afrika  tu katika kipindi cha   mwaka 2020 mpaka mwaka huu , ni idadi  mara kumi zaidi ya  miaka yote ya nyuma”Aliongea  na  Hamza alisoma takwimu ile , ilikuwa  ni kweli kuna idadi kubwa ya  wagonjwa  wa akili.

“Umegundua nini?”

“Wengi ya hawa wagonjwa  naona  wanafanana dalili na Diagnosis, Ugonjwa wa akili wa DID ndio umeshika kasi , Zamani ugonjwa huu wa akili ulikuwa adimu sana”

“Ndio ulikuwa adimu , hivyo inamaanisha kuongezeka kwa wagonjwa wa aina hii kuna sababu, hii  ni takwimu za wale tu ambao wameripoti  hospitalini , lakini wapo wengi  hawajui wanaugua  huu ugonjwa, japo  wanaonekana kuwa wa kawaida  kwa nje lakini  kwa ndani  kuna  kitu kikubwa kinachoendelea”Hamza mara baada  ya kusikia maelezo hayo  alijikua akimfikiria Mellisa mpenzi wake na Amiri , alijiuliza au Mellisa alikuwa  pia  mhanga wa ugonjwa huo , alifikiria lakini aliona  haiwezekani  iwe hivyo.

“Umeongea sana ,  nataka kujua  kinachofuata  ni  nini , umesea majibu ninayo mwenyewe lakini sina ninachoelewa,  halafu  kwanini hutaki kuwa katika uhalisia wako , hio mask unavua saa ngapi?”

“Kitendo cha kuvua hii Mask moja kwa moja  najitoa katika mtandao  wa Wiccan ,siwezi kufanya hivyo hapa  na  pia siwezi kukuingiza katika uhalisia wako nikiwa katika mtandao wa Wiccan , lazima  niingie katika Chumba cha nuru kwanza”

“Chumba cha Nuru, ndio kwamba  huwezi kushitukiwa unachofanya?”

“Ukishaingia katika chumba cha nuru ni kama unapotea katika mazingira ya kawaida , kwa maana   mtandao wa kimadhabahu wa Wiccan hauwezi kujua eneo ulipo na unachofanya ni nini?”Hamza alionekana kumwelewa  hata hivyo alikuwa na uzoefu wa aina hio.

“Tanzania kuna chumba cha Nuru?”

Hamza alikuwa akijua kuhusu chumba cha Nuru ,  

Dokta Genesha alikuwa ndio mgunduzi  mkuu wa

Nuru ndio ilikuwa uthibitisho  wa kisayansi aliokuwa nao wakati akitangazia ulimwengu  kwamba ulimwengu wa kiroho ni uhalisia na anaweza  kuthibitisha hilo, lakini ukweli  ni kwamba  alichogundua  Dokta Genesha kilikuwepo na kikafanywa siri  kama ililivyokuwa siri kwa dunia  na kwanzia hapo   Dokta Genesha  hakuwahi kuweka  wazi  ni ushahidi gani aliokuwa nao mpaka kuaminisha watu kwamba ulimwengu wa kiroho ni uhalisia.

“Swali hilo napaswa nikuulize wewe , kwa maelezo niliokuwa nayo wewe ndio mtu pekee unaejua wapi kilipo chumba cha Nuru”Aliongea na kauli ile ilimsahngaza Hamza.

“Unamaanisha nini mimi ndio ninajua , kama  ninajua ningeuliza?”Aliongea Hamza akiona kabisa ni kama Frida anamchezea akili.

“Mpaka sasa Wiccan  udhaifu wao mkubwa  ni  elementi zilizounda nguvu ya Nuru , licha ya ukweli kwamba Nuru ndio ugunduzi uliokuwepo tokea zama za kale lakini  hakuna  mwanachama  yoyote ambae alishawahi kushuhudia kwa macho ushahidi  huo  , imebakia kuwa katika makisio  ndani ya Wiccan , lakini haibadilishi ukweli kwamba kitu hicho hakipo  na wanaamini ni nguvu ambayo ni  mali yao?” “Wiccan ni wachawi kama wachawi wengine tu , kwanini wanahangaika na Nuru , kitu ambacho  kina madhara kwao?”

“Hawahaingiki na Nuru , Wanaamini  nguvu hio imetokana na  alementi zote nne za dunia  yaani  , Roho ,   hewa , maji , moto na Ardhi,mfano mwepesi  alitoa  mwanachama wa juu kabisa wa Wiccan Ann Marie Galagher , ili mmea  ustawi unahitaji  ardhi  , maji au unyevunyevu , moto au jua  na hewa ambayo ni  oksijeni kutoka Carbondioxide sasa katika hivi vitatu vinawezekana kufanya kazi pamoja  kwa kuunganishwa na roho , sasa unaona hapo hawahangaiki na Nuru kwani  tayari Nuru ipo  katika  elementi hizo  tano”

“Kwahio unachomaanisha ni kwamba  Nuru inayozungumziwa hapa  sio nuru kama nuru inayoonekana bali ni kitu  tofauti kabisa?”

“Ndio lakini  wanaamini msingi wake ni ndani ya elementi zote  za dunia na hakuna  sababu ya nje ya nuru , siri hii wamekuwa wakiiwinda kwa muda mrefu sana  na  wote wenye majibu  walishakufa , ambae alikuwa na siri hii ni Dokta  Genesha  na ndie ambae ametengeneza chumba cha Nuru  ambapo mpaka

sasa haieleweki  kipo sehemu gani lakini ndio udhaifu mkubwa  wa nguvu ya Wiccan”

“Sasa kwanini mimi niwe  ndio ambae najua chumba hiko , hapa mnanichanganya sijui chochote”

“Kitendo cha kuota tayari ndoto  hio inamaana unaukaribia ukweli , kazi ambayo  inatakiwa kukufanya kwasasa ni kuendelea pale ulipoishia?”

“Unamaanisha  nilipoishia kuota ama , inawezekana vipi  kumfanya mtu kuendelea kuota  kama unaangalia  filamu”

“Ni kitu ambacho hakikuwa kikiwezekana  lakini  teknolojia imekuwa, katika ulimwengu wa kiroho 

you’re more than yourself, wewe ni zaidi ya wewe mwenyewe”Aliongea na kumfanya  Hamza asimame.

“Kabla  sijaondoka nataka kwanza kujua vyungu  hivyo  kazi yake ni  nini , kwanini  gharama yake ni kubwa , tuanzie kwanza hapo na ndio tuendelee”

“Tunachonunua sio chungu , chnngu  ni njia ya usafirishaji tu , kinachonunuliwa  ni viungo  vya akili iliolala, unaweza kusema ni kama dawa inayomsaidia mtu kuota nje ya uzoefu wa kumbukumbu za maisha yake”

“Unamaanisha kuna  vitu vipo katika chungu  hiko?”

“Hilo ndio jibu , kinachofanyika  unapewa  kifaa maalumu ambacho kinapasha joto  chungu hicho  na hapo  hutoa  marashi  ya aina flani yanayokufanya mwili wako kuwa kama  umekufa  huku akili  yako

ikifanya kazi katika mazingira  ya nje ya kumbukumbu zako, sijui  ni siri gani  ilopo juu ya marashi hayo lakini nilikuwa nikifanya utafiti mwaka wa tatu huu sijaweza kuona chochote tofauti  kisayansi  nje ya udongo wa kawaida uliotengenezea”

“Kwahio  wewe unachukua hivi vyungu sio kwasababu  unataka kutumia kama viungo vya akili , bali ni kwasababu ya kufanyia utafiti?”

“Upo sahihi ,  kuna siri kubwa  ndani yake ,ambao ndio  na itafuta , wenye kujua siri hii ni  Binamu pekee na ndio wenye mtandao wa usambazaji dunia nzima , kwasasa imekuwa mbadala wa madawa ya kulevya, inaweza kuwa chanzo pia cha   ongezeko kubwa la ugonjwa wa akili”.

Hamza alijikuta akiangalia saa  na muda ulikuwa umeenda kweli , ilikuwa ni saa moja  kamili  tayari za usiku.

Alitamani kujua vitu vingi kutoka kwa Frida lakini simu yake ndio iliomshitua , alipoangalia  aliekuwa akipiga ni  Shangazi na alipokea haraka na baada ya kumsalimia swali lilofuatia ndio lilimshangaza Hamza.

“Hamza kuna sehemu  mmepitia , mtakula huko huko  au niwahesabu  kwenye chakua cha usiku?”Swali lile lilimshangaza Hamza.

“Shangazi  kwanini unauliza hivyo?”

“Nimeona hamjarudi wote ndio maana nauliza”

“Shangazi unamaanisha Regina hajarudi  bado?”

“Ndio , kwani hampo pamoja , nimeshindwa kumpata hewani ndio maana nimekupigia wewe , nini kinaendelea?”Shangazi alionekana kuwa na wasiwasi na  Hamza alisimama palepale.

“Basi sawa shangazi , usiwe na wasiwasi ngoja  nimtafute nitakupa jibu muda si mrefu”Hamza kengele ya hatari ilishagonga katika akili yake na kwa haraka sana alipiga  simu ya Regina  na  iliita  ndani ya sekunde chache tu na kupokelewa.

“Regina upo wapi ,  Shangazi anasema hakupati hewani”Sauti iliomjibu  Hamza  ilimfanya uso wake kujikunja palepale.

“Mr Hamza it seems  like this beautiful lady real does have a special relationship  with you…”

Hamza mara moja alishaijua sauti hio  kutokana na lafudhi yake , alikuwa ni Mendoza  jamaa mwenye Marasta aliekutana nae siku kadhaa nyuma.

“Hivi unajua unachokifanya kwanza?”Aliuliza Hamza huku akihisi miguu yake kuwa na ubaridi 

Upande mwingine licha ya  kwamba walikuwa mbali na Hamza  lakini walikuwa na hofu kubwa mno , kama sio kwa matamanio yao juu ya  kitabu walichokuwa wakifatilia  wasingeenda  mbali kumshika simba masharubu 

“Mr Hamza tunajua  kabisa  tunachokifanya kitakukasirisha , lakini kuna ule msemo  wa  ni kheri kufa ukiwa unajaribu kuliko kutojaribu kabisa.

“Ongea  unachotaka kutoka kwangu  ni nini?”Aliongea  Hamza.

Previoua Next