Reader Settings

SEHEMU YA  25.

“Ni rahisi sana kitabu  au tuambie  wapi  alipo Tembo wa Trishaza  na ndio tutamuachia  huyu mwanamke haraka iwezekanavyo”Aliongea Mendoza

“Mabadilishano  yatafanyikia wapi?”Aliuliza  Hamza , hakutaka kupoteza muda.

“Kama tulivyotarajia , kumbe kitabu unacho?”Aliongea na muda ulule alimtajia eneo ambalo anapaswa kwenda.

“Mr Hamza  tunakupatia masaa matatu kamili , ukipitisha  hayo masaa  usije kutulaumu  huyu mwanamke akipotea na sisi”Aliongea na Hamza hakutaka kuendelea kusikiliza porojo zao kwani alikata simu.

“Kuna nini?”Aliuliza Frida.

“Nadhani  nitakutafuta siku nyingine”Aliongea Hamza na mara moja alimuacha Frida akimwagalia kwa wasiwasi.

Hamza mara baada ya kutoka nje  kabisa alimpigia Shangazi simu na kumwambia  ashampata Regina na  watarudi muda si mrefu ila asiwahesabu kwenye chakula cha usiku , alifanya hivyo kwa ajili ya kumtoa wasiwasi.

Sehemu ambayo Mendoza aliokuwa amemtajia

ilikuwa  ni Zinga  ya Bagamoyo  kijiji cha wavuvi.

Eneo hilo lilikuwa tulivu mno, pengine ni kwasababu wavuvi walikuwa washaondoka kuelekea  baharini kuvua.

Nje kabisa ya moja ya Ghala  la kampuni ya uvuvi   Gari ya Regina ile Lexus ilikuwa imeegeshwa  karibu kabisa na sehemu  nyavu za kuvulia zinapohifadhiwa.

Ndani ya Ghala hilo kulikuwa na harufu nzito  mno ya samaki , Regina alikuwa amefungwa kwenye kiti na hakuwa na uwezo wa kusogea hata kidogo, nywele zake zilikuwa zimechanguka pia kutokana na  kibanio kumtoka  na vile alivyokuwa akitingisha kichwa ndio  alivyozidi kuchanguka.

Hakuwa akipiga kelele hata kidogo zaidi ya kuangalia  wanaume  wawili waliokuwa mbele yake na muonekano uliojaa sumu.

Regina alikuwa akikumbuka wakati alipokuwa akikaribia nyumbani  ni mwanamke wa kizungu ambae alionekana kama mgeni ndio  aliesimamisha gari yake akionekana kutaka kuuliza swali.

Matokeo yake kitendo cha kushusha kioo tu alijikuta akinusa marashi ambayo yalimpelekea  kupoteza fahamu  na mara baada ya kushituka  alikuwa tayari ndani ya eneo lenye harufu kali  katika ghala hilo akiwa amefungwa ,  mwanzoni alidhani   yupo feri lakini mara baada ya kuangalia  taa hafifu ndani ya  ghala hilo na maboksi ya kutunza baridi alijikuta akiaini hakuwa   karibu na jiji la Dar.

Akili yake ilimwambia kabisa watu wale hawakuwa watanzania hata kidogo  na hio ni kutokana na namna walivyokuwa wakiongea.

“What is your goal , if  you want money , then you should ask  me to call  home”Aliongea  Regina  kwa kingereza akimaanisha nini lengo lao, kama ni hela basi wamuache apige simu nyumbani.

“Madam , My Companion Huda  is only joking , she has no ill intentions , we just want to know  what kind of relationship  you have with that Mr  Hamza , who  is he and where he’s from”Aliongea  akimaanisha yeye na mwenzake Huda  wanatania tu , na hawana nia mbaya , wanachotaka kujua ni uhusiano wake na Hamza , ni nani na anatokea wapi.

“Mr Hamza.. Mnamaanisha Hamza!!”Aliongea 

Regina akionekana kushangaa  na palepale alijiuliza au hili kundi la watu lililomteka  hawakuwa wakimlenga yeye bali ni Hamza.

Kitu kingine ni kwamba walikuwa wakiuliza kuhusu   uhusiano wake na Hamza , sasa alijiuliza kwanini waulize swali hilo.

Regina  alishindwa kujizuia kimawazo na kuamini pengine ni James ndio  ametuma watekaji  kwa ajili ya  kuupata ukweli  juu ya uhusiano wake  na  Hamza , lakini alijiuliza kwanini  raia wa kigeni.?.

“Ni Boyfriend wangu , pia ni mwanachuo  na fundi  wa vifaa vya kieletroniksi”Aliongea  Regina kwa kingereza.

“Boyfriend!!, Ndio maana  anakujali mno  mpaka kuwa tayari kutupatia Ankh, inaonekana anakupenda sana”

“Anka!! Unamaanisha nini?”Aliuliza  Regina  mara baada ya kusikia sauti hio  lakini hakuelewa maneno hayo yalikuwa yakimaanisha nini.

Upande mwingine kati ya wanawake wawili waliokuwa katika kundi hilo , yule aliefahamika kwa jina la Corrella uso  wake ulionyesha kutoridhika.

“Umesema ni fundi  na mwanafunzi , mtu ambae ameweza kujua uwepo  wetu  hawezi kuwa mwanafunzi  na fundi , acha kututania wewe mwanamke”Aliongea na dakika ileile alitoa kisu cha  kung’aa sana  na kumsogelea Regina na kukiweka karibu na uso wake , ilikuwa ni kama vile anataka kukata pua ya Regina.

Regina macho yake yalianza kuonyesha kupaniki  , ijapokuwa  siku zote hakujali sana kuupamba uso wake lakini  yeye ni mwanamke na  siku zote alikuwa akijivunia kuwa mzuri , ni mwanamke hata hivyo  , aliona kama akipotezewa urembo wake itakuwa   ni kheri ya kifo.

“Nilichosema ni kweli , kama huamini  muulizeni mwenyewe”Aliongea na Mendoza alimsogelea  Huda  na kumzuia kwa kumshika mkono.

“Huda muache , pengine  Hamza siku hizi kaamua kuwa mwanafunzi na fundi , ni jambo  la kawaida kwa ninja  kama yeye kuwa  na utambulisho feki”

Regina mara baada ya kusikia utambulisho feki ,Ninja  Regina mara baada ya kusikia maneno hayo ni  sasa ni kama akili yake inafanya kazi na kuona  ni kweli  Hamza alionekana sio wa kawaida.

“Madam , ushawahi kusikia kitabu chochote chenye alama ya Ankh  kutoka kwa  Mr Hamza , au Kitabu cha Riwaya  ya  ndege juu ya mti wa uzima?”

“Mnasema  sijui anka gani , ni kitabu cha namna gani hicho?”

“Inaonekana kweli huelewi tunachozungumzia , ni kitu muhimu hivyo   uwezekano ni mkubwa  hawezi kukiweka holelaholela mtu yoyote kuona , Sio rahisi kumuonyesha mpenzi wake”

Yule mwanamke  aliefahamika kwa  jina la Huda alichora chini  alama  flani  hivi ,haikuwa  kama msalaba bali ilikaa  kama  rungu yenye mkato katikati. “Hujawahi kuona kitabu chenye alama ya namna hii?”Aliuliza yule mwanamke  na  Regina aliishia kutingisha kichwa kwamba hajawahi kuona , ukweli ilikuwa ni mara yake  ya kwanza kuona alama hio.

“Hajui chochote , inaonekana Mr Hamza  alikuwa makini kuficha”Aliongea Correla.

Regina aliishia kusikiliza mazungumzo yao  na yalionekana sio kati yake na Hamza  kabisa  na  alianza kuwa na wasiwasi  zaidi.

“Sio James aliewatuma?”Aliuliza Regina , ijapokuwa aliona kabisa swali hilo  ni la kijinga lakini aliona aulize.

“James , ni nani huyo na anakaa wapi?, sisi ni  wawindaji wa binadamu kutoka Samar , unaweza

kutuita  Tumbili  Wenye mbawa za  Mwewe”Aliongea  kwa  majisifu.

Regina  japo hakuelewa walichokuwa wakimaanisha lakini alishaamini sio watu waliotumwa na James , maana ndio adui yake ambae alidhani anaweza kumteka.

“Nadhani  tukamfunge ndani ya boti yetu moja kwa moja , tusipopata kitabu tunaondoka nae , ndio  namna pekee ambayo  hatutaweza kupambana  nae  ana kwa ana”Aliongea bwana mwingine , huyu hakuwepo katika kundi  ambalo lilimsimamisha  Hamza kule Kongowe.

“Noni, ulichoongea kinaleta maana , nitaliacha hili mikononi   mwako”Aliongea Mendoza

Regina mara baada ya kuona kile kinachoenda kutokea alizidi kuwa na wasiwasi na alijiuliza au  alikuwa akishikiliwa kwa kudhaniwa ni  mpenzi kweli wa  Hamza.

Aliona woga kwani mmoja wapo alikuwa kabisa na bastora kiunoni  na moja kwa moja  akili yake ilijua watu waliokuwa mbele yake wanazidi kuwa hatari kila alivyokuwa akiwafikiria na kuwachunguzana, hisia zake zilimwambia kama ni hivyo basi na Hamza atakuwa hatarini.

Alikumbuka namna ambavyo  Hamza alivyokuwa akimkwepa  Yonesi wakati wakipigana  na kutofanya mashambulizi , aliona kabisa kitendo kile ilikuwa ni Hamza kuwa muoga.

“Subirini kwanza,mmekosea jambo moja  , kunikamata kwenu hakutowapatia hicho kitabu”Aliongea Regina.

“Oh , kwanini unasema hivyo?”Aliuliza  aliekuwa mlangoni.

“Mimi nimefahamiana na Hamza juzi tu hapa  ni mtu muoga mno , nina uhakika anawaogopa mno  na hawezi kuhatarisha maisha yake kuja kuniokoa , huu mpango wenu  ushafeli tayari”

Mara baada ya kumsikia akiongea hivyo  watekaji wote waliangua kicheko  kana kwamba alichoongea ni ujinga wa karne.

“Unadhani tunaweza kukuamini?, Yaani  Hamza atuogope sisi  haha…hiki ni kichekesho cha mwaka”

“Kwanini  asiwaogope? , nyie  hamumjui yule vizuri , ni muoga kweli”Aliongea Regina huku akiona yeye mwenyewe   maneno yake ni ya ajabu.

“Wewe mwanamke unadhani sisi ni wajinga , tulishampigia tayari wakati ukiwa hujitambui na ametuambia anakuja , nadhani muda si mrefu atafika  hapa , anaonekana kujali kweli usalama wako” “Nini!?Anakuja? , kwa uoga ule inawezekana vipi?”

Regina  alionyesha kushangaa  na kudhani  alikuwa amemdhania Hamza vibaya lakini mara baada ya kufikiria  anakuja kukutana na hawa wahalifu  alianza kushikwa na wasiwasi  na aliona kama Hamza ana akili  ni bora asije kabisa , Hamza anaemjua  yeye ni mtu ambae anaogopa mshahara wake kukatwa na amekaa kizembe zembe.

Hamza hakuwa hata mwanaume kwa kitendo chake cha kushindwa kujizuia na kumchungulia  kupitia kioo , alijiambia  hio sio tabia  ambayo mwanaume jasiri  anaweza kufanya, sasa mtu yule aliempiga chabo ndio aje kumuokoa  , aliona haiwezekani lakini hata hivyo aliona atulie aone mwisho wake.

Alijikuta akifikiria na upande  wa pili wa Hamza na aliona kuna muda mwingine anaonekana kuwa siriasi hivi na kuwa na akili nyingi  lakini pia ni mkarimu mpaka kumletea  matunda kwa ajili ya kupoza njaa , Regina hakukataa na kuona inawezekana  roho yake nzuri ikamtuma kuja kumuokoa.

Wakati  Regina akijiuliza maswali mengi  Hamza ni nani  mpaka kuwa na ujaisri wa kuja kumuokoa dio muda  mlango wa ghala hilo uligongwa.

“Noni  mlete huyo mwanamke  kuelekea  kwenye boti , nitadili nae mimi”Aliongea Mendoza mara baada  ya kuona  Hamza amefika.

“Hey , usiniguse”Aliongea Regina mara baada ya kuona yule mwanaume bonge  wa kifilipino aliefahamika kwa jina la Noni akitaka kumgusa.

“Stupid Woman , try this”

Aliongea Corrella  aliekuwa amesimama mbele ya Regina  na alitoa kichupa kama cha spray   na kumpulizia usoni  na palepale  mara baada ya kuvuta  yale marashi  alipoteza fahamu palepale.

Dakika hio hio kabla hata hawajamfungua kutoka kwenye kiti  mlango wa mbele wa ghala ulipigwa teke na kufunguka  mara moja licha ya loki zake kuwa za chuma, pengine ni kutokana na kutu ndio  maana imekuwa rahisi.

Baada ya mlango kufunguka , mtu alieonekana mlangoni alikuwa  ni Hamza akitafuna bublish  huku mguu mmoja ukiwa hewani  , akionyesha kwamba mlango huo aliupiga na teke  moja tu mpaka kufunguka.

Mendoza , Huda na Noni  wote walikuwa kwenye mshituko kutokana na nguvu za Hamza, kwani teke  moja tu mlango ulikuwa umefunguka.

Hamza  hakuwa na wasiwasi kabisa ni kama amekuja kutalii , alikuwa akitafuna bablish  huku akipiga hatua za taratibu kuingia ndani kama bosi wa watekaji hao.

Lakini  kadri ambavyo alikuwa akipiga hatua  walijihisi miili yao kuwasisimka , ilikuwa ni kama vile  ghala lote limefunikwa na nguvu isio kuwa ya kawaida, dakika ileile  Vivuli  vitano viliweza kuonekana katika kila  upande wa ghala hilo  na ilikuwa ni kama  vile vivuli viilikuwa vikiwaangalia  wale watekaji jambo ambalo liliwashangaza.

Walianza kushikwa na hofu  na  waliweza kuona ni namna gani  Hamza alikuwa akitisha kama vile ni jini.

“Nadhani niliiwaambia hampaswi kuwepo Tanzania  na kunifuatilia , ila naona hamkunielewa”Aliongea na palepale alimsogelea Correla ambae alikuwa karibu na Regina akiwa ameshikilia kisu.

“Usisogee  kama hutaki huyu mwanamke  kufa mbele yako”Aliongea kwa kuamrisha.

Hamza  alionekana ni kama vile hajamsikia  na aliendelea kusogea mbele,muonekano wake haukubadilika hata kidogo, alikuwa akitembea kana kwamba anapita  kwenye  kiambaza cha nyumba.

Lakini sasa  kadri dakika  zilivyokuwa zikiongezeka  hali  ilizidi kuwa ya baridi ndani ya eneo hilo huku  Hamza akizidi kutisha  na nywele zake zilianza kucheza cheza 

Nori kuona vile palepale alichomoa bastora kutoka kiunoni na kumnyooshea.

“Simama hapo hapo, ukisogea tu nitakulipua”Aliongea  

“Lipua tu,  ila unatakiwa kwanza kuitoa katika safety deposit”Aliongea na palepale ndio aligundua hakuwa amepandisha risasi kwenye chemba kutokana na kuwa na woga., kosa la namna hilo  kwa  uzeofu wake halijawahi kumtokea.

Ijapokuwa kwa haraka sana aliitoa katika  hali ya usalama   lakini mikono yake ilianza kutetemeka. “Mr Hamza  tunachotaka ni  kitabu cha Ankh, ukitupatia  tunakuhakikisha  huyu mwanamke atakuwa salama”Aliongea Marasta.

“Si nilishawaambia sina  kitabu cha Ankh tokea muda mrefu tu”

“Nini?”

Wote waliangaliana   kwa mshangao  kana kwamba walikuwa hawajamsikia vizuri.

“Kama  ni  hivyo , tuambie alipo Dokta Genesha”

Hamza wala hakujali , ki ufupi  hakuongea lolotte tena na sasa alikuwa mita  kama kumi kutoka kwa watekaji watatu , mara baada ya kusikia lile swali aliishia kutingisha kichwa chake.

“Mr Hamza usitukuchukulie wepesi , au unadhani hatuwezi kumdhuru huyu mwanamke?”Mara baada ya kuongea Huda kisu chake kilikuwa kishafikia shingo ya Regina  huku  Nori akiwa amemlenga Hamza na bunduki.

Hamza alisimama  akiwa katika umbali wa mita kama sita hivi  na kuwaangalia wote  wanne bila ya  kupepesa macho 

“Kwasababu mmeweza kuteka  basi naamini mnaweza kuua pia”

“Kama unalijua hivyo unapaswa kutoa

ushirikiano”Aliongea Huda  na kufanya  midomo ya  Hamza kucheza.

“Mmethuburu kufanya utekaji lakini haimaanishi mnaweza  kuua mbele yangu”

Mara baada ya kusikia kauli hio  walijikuta wakiwa katika hali ya kuchanganyikiwa  lakini ndani ya sekunde iliofuata  nguvu kubwa ya ajabu  ilitokea   na kuwababishia wahisi kama vile  pumzi zinawaishia  huku wakati mmoja ni kama vile wameshikwa na jinamizi na washindwe hataakupiga hatua , Hamza muda huo alikuwa ashawasogelea tayari.

Wakati   sasa wakijua  Hamza hakuja kutii maagizo yao bali kupigana , waliishia kujitahidi kurudi nyuma , na ghafla tu  Nori alivuta Triga na kumlenga  Hamza na bunduki.

“Bang , Bang, Bang!!”

Risasi zilifyatuka  huku zikibeba  joto kali  lakini ajabu   risasi zile  ni kama vile  zimetoboa karatasi  na kupita,

Hamza alikuwa ni kama vile amefifia katika ile

sehemu aiokuwa amesimama na ni mwanga flani wa sura yake  tu ndio uliokuwa ukicheza cheza, ilikuwa ajabu kweli.

Huda mara baada ya kuona hakukuwa na madhara juu ya risasi  zile kwenda kwa Hamza aliamua kudili na  Regina  lakini  alikuwa amechelewa  kwani  mkono wake ulioshikilia kisu  ulikuwa umeshikwa na kivuli na ushindwe kuusogeza kabisa, hakujua hata ni kitu gani kimemshika na wakati akijaribu kufurukuta  Hamza alikuwa  ashamsogelea tayari.

Wawindaji wale wote walijikuta wakishangazwa na tukio  hilo na walimwangalia  Hamza kwa woga mno.

Walijiuliza nini kimetokea , mbona alikuwa mbali mno na alipo Huda lakini ameshindwa hata kumchinja  yule mwanamke , ni nguvu gani iliokuwa ikimsaidia.

“Crack , Crack!!!”

Huda hakuwa hata na muda wa kujibu shambulizi , mikono yake yote ilikuwa imevunjwa vunjwa.

“Arghhhhhh…”

Hamza  hakujali hata ukulele wake alimuondoa Huda mbele ya Regina kwa teke na kwenda kudondokea kwenye  kingo ya kimbweta cha  kuhifadhia maboksi ya kuhifadhia samaki,kutokana na nguvu iliotumika kumrusha kuwa kubwa alijikuta akivunjika uti wa mgongo na maisha yake yalikoma palepale huku damu nyingi  zikimtoka.

“Huda!!”

Walijikuta wakiita wakiwa hawaamini mwenzao alikuwa ameshapoteza maisha , kila mmoja alishikilia siraha yake  , wengie wakiwa na visu na wengine wakiwa na  vifaa kama misumari mirefu na kutaka kumlenga Hamza  lakini  Hamza alikuwa mwepesi mno kwani sarakasi   alizoruka hazikuwa za kawaida  na kisha kuwapiga na Roundhouse kick.

“Arghhh!!”

Mara baada ya kuwapiga na mateke  kifuani  watekaji  wale walijikuta wakipiga   ukulele  mkali na kwenda kudondokea kwenye ukuta huku wakitema damu nyingi chini, ilionekana eneo walilopigwa kifuani  nguvu yake ilibomoa mpaka  mapafu kwani walionekana wakishidwa kuvuta hewa na waliishia kutapatapa na kupoteza uhai  kwa teke moja tu la kifua.

Ndani ya  sekunde kumi tu  Huda , Nori  na Dodo walikuwa wameshapoteza maisha 

Aliebakia alikuwa ni Mendoza na Mhindi  na ilionekana ndio waliokuwa na nguvu kuliko wenzao wote.Walikuwa ni maninja   daraja  B,ni kosa kuwafananisha na  wanajeshi  au makomandoo, walikuwa zaidi ya makomandoo.

Katika mapigano ogopa   yule mwanafunzi ambae anafundishwa kuua na si vinginevyo , uwezo wake unakuwa sio wa kawaida kabisa  na ndio kilichokuwa kwa  Mendoza.

Lakini  mbele ya Hamza  ni kama walikuwa watoto  wa darasa la tatu ambao hawakuwa na  mahali pakukimbilia.

Ijapokuwa alikuwa   na hofu lakini  utashi wa kutaka kuishi ulimfanya kutoa kisu  kutoka katika kiuno chake na kutaka kumkata nacho shingoni Hamza, alikuwa ametumia uwezo wake wote  wa  kininja ili kuhakikisha shambulizi lake linafanikiwa.

Hamza mara baada ya kuona kisu kinakaribia kuikata shingo yake,alikuwa ashanyoosha mkono wake  kwa chini na kuwekza kukikamata  kwa vidole viwili  tu tena kule kwenye makali.

Mtekaji alijaribu kusukuma mbele lakini alishindwa kabisa , ilikuwa ni vidole viwili tu  vilivyoshikilia kile kisu  lakini ni kama vile ni chuma ndio kimeshikilia.

Hamza aligeuza macho yake na kumwangalia , alikuwa na macho  sio ya kawaida , ijapokuwa hayakutoka katika ubinadamu wake lakini ilidhihirisha hakuwa mtu mwenye huruma hata kidogo kwa namna ambavyo  kiini cheusi kilivyokuwa kikipotea , Mhindi  mara baada ya ya kuona  namna ambavyo Hamza amebadilika  kwa woga aliichia kile kisu na kukaa chini.

Hamza alikuwa na macho ya kichawi ,  macho yake ni kama yamepoteza kiini na hicho ndio kilimuogopesha Mhindi mtekaji na kuishia kukaa chini kwa hofu huku akijuliza ni macho ya namna gani.

“Wewe ni nani?”

Mendoza aliishia kuuliza  kwa hofu  akimwangalia Hamza kwa mshangao lakini Hamza hakujibu zaidi ya kutoa tabasamu la  kikatili.

“Haiwezekani .. au wewe ni..?”

Mendoza aliekuwa na ujasiri wote  alikuwa akimwemwesa midomo kwa woga  kana kwamba ukichaa umemvaa , kutokana na msukumo wa nguvu  kubwa  isiokuwa ya kawaida  alihisi mkojo ukimtoka palepale ,  wazo  baya lilimwingia na kujiuliza inamaana  kundi lao litakwenda kufutwa kama anachohisi ni  cha kweli.

Mara baada ya  kuona  Hamza anaweza kuwa yule anaemdhania palepale alishuka  chini na kupiga magoti.

“Sikujua  wala kutegemea  anuani ilioachwa katika maabara ya Dokta  Genesha ni kuja kukutana na wewe , kama ningejua  wewe ndio rafiki yake  aliemzungumzia , sisi  pamoja na kundi letu tusingekubali kuibeba kazi hii , naomba kwa  gharama ambayo tumekwisha kulipa kwa vifo  vyetu usije kuadhibu na  umoja wetu wote”Aliongea Mendoza.

Hakujali tena kama  atapoteza maisha hapo hapo , alichojali  ni  kuokoa umoja wao tu kwa muda huo  maana  kitendo cha kuja kumchokoza mtu aliekuwa mbele yake inamaanisha  moja kwa moja umoja wao umeingia katika  vita  nae.

Muda uleule  Hamza alikuwa ashatoka kwenye ule muonekano wake wa kishetani na kurudi kawaida 

“Mimi sijali , mnaweza kuja kunitafuta lakini  nitaendelea kuwapoteza mmoja baada ya mwingine, sina mudi  ya kwenda kupambana na genge lenu lote la wachawi mimi”Aliongea Hamza.

“Ni kweli kabisa , sisi kwako ni kama kunguni tu , naomba kifo changu  kiondoe kinyongo  baina yako na kundi letu”Aliongea na palepale  aliinnua  kisu  kilichokuwa chini na kujichoma eneo la moyo  mwenyewe na kudondoka chini.

Kilikuwa ni kitendo cha kushangaza , alijichoma yeye mwenyewe kwa ajili ya kumzuia  Hamza asiweke kinyongo na kundi lao.

Mhindi  mara baada ya kuona mkuu wake  kashajiua  hakutaka kujiua   kama ilivyokuwa kwake na mara baada ya kuona Hamza ameangalia pembeni palepale alisimama na kutimua mbio lakini  jambo lile lilimfanya  Hamza kutoa tabasamu na kurusha kile kisu  kilichokuwa mkononi  mwake  na  ile Mhindi anaukaribia mlango  kisu kiliingia kutoka  kwenye  kisogo  na kutokezea kwa mbele  kwenye koromeo na akadondoka chini akitapatapa.

Hamza hakujali kabisa hata kitendo kile na aligeuza macho yake  na kumwangalia Regina aliekuwa kwenye usingizi mzito  na kuishia kutabasamu.

Previoua Next