Reader Settings

“Acha makusudi ya kujikweza , sheria  namba moja katika ulimwengu  wa mapigano  ni kujitambulisha wewe na shirka lako  , mimi  ni mwanafunzi kutoka Shirka ya Tai Mweusi, jitambulishe  Shirka  lako na wewe  kama ujasiri huo unao , udhalilishaji wa leo utalipwa mara mia zaidi”

“Nimefundishwa na Master Kato Hawk ushawahi kumsikia?”Aliuliza Hamza

“Kato Hawk , mbona sijawahi kumsikia  ni raia wa wapi?”Aliuliza  Mzee Konki akionyesha kutomjua.

James mara baada ya kuona Mzee Konki anaanza kuuliza maswali ya kipuuzi alitamani kwenda na kumpiga , ila uwezo huo hakuwa nao.

James alikuwa akimjua  Kato Hawk, mtu yote mpenda filamu za  angemfahamu Kato Hawk.

“Ushawahi kumsikia mtu anaeitwa Kato Hawk huko jeshini?.”Aliuliza Regina ki udadisi swali hilo likienda kwa  Yonesi.

Yonesi na wenzake walikuwa wakimjua ndio lakini hawakutaka kumwelezea  Regina na walishangaa kwanini hamjui.

“Taja jina la Shirka  ulilojifunzia, sijawahi kusikia jina la  mtu uliemtaja?”

“Kama hujawahi kumsikia  mtu maarufu kama huyo , basi  sioni haja ya kukuambia  nenda kaulize”Aliongea Hamza akiwa na muonekano wa kejeli.

Mzee Konki alikuwa na hasira mno , kama sio kuumia mkono wake angejaribu kuzipiga tena na  Hamza , alijua kuvunjika kwa vidole vyake  hawezi kupona ndani ya siku kadhaa.

“James , turudi kwa leo ila naahidi , nisipokuja kulipiza hili labda sio mimi Konki  Master”Aliongea Konki  kwa hasira , hakuamini miaka yake yote ya kujifunza mapigano na kutia mguu  Tanzania anakuja kukutana na udhalilishaji.

James mara baada ya kusikia hivyo alifurahi , alijua  lazima mzee huyo atakuja tu kulipiza kisasi.

James ashaona  kabisa  Hamza sio saizi yake  hivyo aliondoka  kimya kimya

Regina alimwangalia Hamza kwa macho ya  kiulizo na alijiambia ndio maana aliweza kumuokoa kiwepesi tu, hali hio  ilimfanya kukosa hiari ya moyo wake  na kujisikia hali isioelezeka.

Wakati wa kurudi nyumbani kulikuwa na foleni kubwa mno hivyo gari ilisogea taratibu taratibu. “Kwahio Master wako ndio anafahamika kwa jina la Kato  Hawk ,  umefahamiana nae nje ya nchi nini?”Aliuliza Regina.

Swali lile lilimfanya Roma  kushituka na kidogo tu  akanyage  kwenye  pedeli tofauti na breki kugonga magari ya mbele yake.

“Regina inamaana hujawahi kusikia hilo jina?”

“Ningekuuliza kama najua ,  hata Yonesi nimemuuliza ameonekana hajui”

Hamza alijifikiria na kujiambia inakuwaje hawamjui , lakini hata hivyo aliona  kwa  mwanamke  kama Regina ni haki kutokumjua.

“Nilikuwa nikiongea ujinga tu pale , usichukulie siriasi”Aliongea Hamza.

“Kwanini unakuwa hivyo ,unaona aibu kuwa na Master  eh?”

“Haha.. nimeongea kumugopesha tu yule  usichukulie siriasi”

“Usiponiambia nitatafuta mtandaoni  na lazima nitajua tu”Baada ya kuongea hivyo alichukua simu yake na kuingia kwenye mtandao wa google na kuandika  jina la Kato Hawk.

Hamza aliishia kutingisha kichwa tu na kujiuliza kwanini huyu mwanamke  ana shauku ya kujua siri zake namna hio.

Ndani ya nusu dakika tu ,  Regina  mashavu yake yalikuwa mekundu  na aliishia kung’ata lips zake na  kuweka simu chini bila kuongea chochote.

Hamza mara baada ya kuona  muonekano wa Regina alijua tayari ashaujua ukweli kuhusu Katona alitamani kucheka kicheko kikubwa.

“Hehe, nilikuambia mimi  usitafute  haya ona sasa?”Aliongea Hamza huku akicheka.

“Muhuni sana wewe..”Aliongea  Regina akiwa na hasira , hakuaminni  alikuwa ameuliza swali hilo kwa Yonesi na wenzake , alijihisi kuona aibu

“Nilishakuambia  nilikuwa nikiongea ujinga, halafu kingine  Kato Hawk hawezi  kuwa na vigezo vya kuwa master wangu , uwezo wangu  wa mapigano  kwa kutumia vidole  ni wa juu mno”

“Kimya , endesha gari”  Regina hakutaka kumsikiliza tena , alitamani kumsogelea na kumpiga kibao.

“Basi ngoja  nikuambie ukweli , kama usiponiamini unaweza kujaribu kutafuta tena”

“Ukiongea ujinga tena  nitakata mshahara wako”

“Sawa Madam , kama hutaki kusikia  basi nitakaa kimya”Aliongea Hamza huku akitamani kucheka.

****

Upande mwingine wa jiji kulikuwa na kikao kilichojumuisha  kundi la watu wenye mafunzo ya  kimapigano  lifahamikalo kwa jina la Tanzania Martial  Art Association.

Kundi hili  halikuwa la kihalifu lakini kwa namna moja lilitafsirika kama la kihalifu kutokana na usiri mkubwa  wa  ajenda zao , unaweza kusikia kuna kundi hili lakini huwezi kujua  ni kitu gani wanachokifanhya wakikutana.

Kuna wanaosema kundi hilo   hufadhiliwa na Binamu  , hakukuwa  na ushahidi wa moja kwa moja wa madai hayo., lakini  taarifa  ya kuaminika  hata baadhi ya wanajeshi wenye vyeo vya ukomandoo jeshini  walikuwa  ni wanachama  na hawakujiunga kwasababu walitaka bali  walipambanishwa na wenzao na kukidhi vigezo na kuingia katika umoja huo na kulikuwa na faida kubwa sana ya kimaslahi kwa kila mwanachama wa kundi hilo.

Sasa katika moja  ya jumba la kifahari  lililopo  Tegeta 

kulikuwa na kundi la watu ambao walikuwa wamevalia  mavazi ya suti na walikuwa wamekaa eneo la sebule yenye masofa mengi ya  thamani  ya juu.

Kwa muonekano wao ilionyesha   kabisa hawakuwa watu wadogo katika jamii , mmoja ambae alikuwa katikati ndio  kiongozi  alifahamika kwa  jina la

Fanueli Yowe  au unaweza muita Kanali Yowe.

Ndio alikuwa ni Komandoo  wa jeshi  la taifa  lakini pia mwanachama wa  umoja huo wa  sanaa ya mapigano.

Ukiziangalia sura zote zilizokuwa ndani ya eneo hilo  usingeamini kama  walikuwa na uwezo wa kupigana  wa hali ya juu na baadhi yao ni makomandoo wa jeshi.

“Nadhani kila mmoja wenu  amesikia , mwanachama wetu mpya Mzee Konki  amekutana  na mtaalamu  wa hali ya juu  wakati alipokodiwa  na Mzee Benjamini  wa kampuni ya Zena?”

“Hii maana yake ni kwamba mpaka sasa  hakuna mmoja wetu hapa anaemuweza mtu huyu , maana tunajua fika  Mzee Konki ndio mwanachama wetu mpya ambae ametushinda wote kimapigano, hii  ni taswira mbaya  kwa umoja wetu na maslahi yetu kwa ujumla  katika nchi hii, kwa kusema hayo nimeitisha kikao hiki ili kuwauliza mnaonaje  hili swala?”

“Kwa mtazamo wangu  lazima  mtu huyo atakuwa  si wa hapa Tanzania na hata kama ni wa Tanzania  basi

amerudi hivi karibuni  na pengine ameajiriwa  kulinda kampuni ya Dosam”

“Mimi pia nadhani huyu  ndio mtu alieripotiwa kwetu na   Amosi , unajua Amosi licha ya kutokuwa na uwezo wa hali ya juu lakini ana macho ya kuona  mtu ambae ana uwezo mkubwa , nasikia  baada ya hapo  Amosi alipokea vitisho kutoka kundi la Chatu aache kabisa kumchokoza  yule mwanamke mfadhili wetu  anaemtaka”

“Unamaanisha Dina ndio aliingilia , nadhani kadri siku zinavyoenda ndio anasababisha matatizo  zaidi”Aliongea  mwanaume mwingine  aliefahamika  kwa jina la Gosu  au Mzee Gosu  ni mstaafu  kutoka polisi.

“Kwanini  mnampa bichwa yule msichana ,tunajua  wote hapa hatumuwezi lakini hatuwezi kumsujudia pia”

“Mimi nadhani tuachane na swala la Dina ,  na Mzee  Konki mwenyewe atuelezee  ni kwa namna gani tutarudisha heshima yetu , wenzetu kutoka nje ya nchi wakisikia  kuhusu hili watadharau na hawatukubali kufanya biashara na sisi”

“Nadhani kwanza tumfahamu  ki undani ni nani ,  alitaja Master jina la Master  aliemfundisha  lakini sikuweza kumfahamu , nadhani  kati yetu  hapa kwenye huu umoja lazima atakuwa amesikia jina hilo , amesema anaitwa Kato Hawk na ni maarufu sana” “Eeh!!

“Watu  wote walikaa kimya  na kufanya hali itulie  na  kitendo kile kilimfanya  Mzee Konki kushangaa.

“Mbona kila mtu amekaa kimya?, au inamaana mnamjua tayari?”

“Mzee Konki nadhani  ni kweli umechoka  mno , unaonaje ukiingia chumbani kupumzika kwanza”

“Mkuu  kwanini nipumzike , hiki kikao si kinanihusu mimi na yule mpuuzi?”

“Mzee Konki acha kututania , yaani unatuambia mcheza filamu za ngono anaejitamba mtandaoni kuwa ni Bruce lee  ndio  mtaalamu  wa mbinu ya  kucha  za tai.”

“Nini !!, Mcheza filamu za ngono , mnamaanisha nini?”

“Mzee Konki hatukulaumu ,  wewe ndio mzee hapa hivyo  hutumii  sana mtandao wa  internet   hivyo ni rahisi kutomfahamu  Kato Hawk, huyo mtoto inaonekana alikudanganya makusudi , haina haja ya kuwa siriasi hivyo”Aliongea  Mzee Fanueli Yowe.

Mzee Konki mara baada ya kuagalia sura ya kila mmoja  alijikuta akishindwa kuzuia kicheko na muda huo huo  watu wote walimuunga mkono na kuanza kucheka na ghafla tu akaacha na wote wakaacha.

“Mpuuzi sana yule mtoto , nitamchuna ngozi”Aliongea kwa hasira , hakuamini  haikuwa swala la kupigwa tu lakini vilevile ametajiwa  mcheza  filamu za utupu kama Master.

Kato Hawk  kabla ya  kuwa  muigizaji wa filamu za kimapigano alifahamika kama Gerald Lupe   alikuwa ni mcheza filamu za  ngono maarufu sana , kitendo cha kubadilika kutoka ugiizaji wa filamu hizo na kuingia katika sanaa ya mapigano  huku akijifananisha na  Bruce lee ndio alijibatiza jina la Kato, uhusika wa Bruce lee katika  filamu ya Green Hornet(1966)

,hakuna  mtu ambae  alikuwa akiamini kama  Gerarld Lupe au Kato  alikuwa  akijua mapigano , kilichomfanya kuwa maarufu sana hadi Tanzania ni wakati alipofika nchini  katika uigizaji wa filamu huko Ngorongoro  na  kupewa  mapokezi makubwa kwa kigezo cha kutangaza utalii, kilichomfanya pia kuwa maarufu dunia nzima ni namna ambavyo alikuwa akijibrand kwa kutengeneza vidio fupi fupi katika mtandao wa Tiktok  na Reel Instagram akionyesha staili mbalimbali  za mapigano kama Bruce Lee  lakini   ikaja kujulikana anafanya Editing huku kile watu walichokuwa wakiona sio uhalisia.

Skendo  hio ya kufanya editing   ilimfanya  kuzomewa na watu wengi mtandaoni huku  wakimuonya

asitumie utambulisho wa  kusema  yeye ni Bruce lee aliezaliwa(Recarnated) katika mwili wa Gerald Lupe kwani ni kuchafua hadhi  ya kumbukumbu za kishujaa za Bruce lee.

Hivyo ukiingia mtandaoni ukiandika  jina la Kato Hawk  ni  Gerald Lupe mcheza filamu za ngono maarufu  anaedai  ni Bruce lee  aliezaliwa katika mwili wa Gerald Lupe.

“Mzee Konki  haina haja ya kuwa na hasira , tunachopaswa kuamini kwasasa  ni kwamba huyu mtoto sio wa kawaida , kama ni hivyo unadhani kwanini hajatoa jina la Shirka  analotokea.

“Kesho  mapema narudi  Thailland kwenye Shirka langu , nipo tayari  kualika  hata  wataalamu wa hali ya juu wa kimapigano kwa ajili ya kumshikisha yule mtoto adabu”Aliongea kwa hasira.

Kauli ile iliwafnaya  wote waliokuwa hapo ndani kufurahi , walijua fika Mzee Konki  kama ninja wa daraja la juu lazima atakuwa anafahamiana na maninja wengine  wa uwezo wa juu.

“Mzee  Konki tutasubiria kurudi kwako  kama ndio hivyo , ruhusa unayo kutoka kwetu”Aliongea Mzee Yowe.

******

Siku iliofuata ilikuwa ni jumamosi , Kwasababu ilikuwa wikiend haikuwa lazima kwenda kazini mapema , hivyo Hamza  alitoka nje kwenye uwanja wa bustani ya nyumba na kuanza kuchukua mazoezi.

Mazoezi yake Hamza hayakuwa ya kawaida  hata kidogo , hayakuwa  ya kukimbia wala ya kuruka ruka.

Ilikuwa ni kama vile anakata mauno kwa jinsi alivyokuwa akifanya , lakini utofauti ulikuwa kwenye viungio vya miguu yake  vilikuwa vikipinda katika  mjongeo  wa aina yake.

Kwa lugha nyepesi ni kama vile  anajaribu kucheza cheza tu kupoteza muda , hakukuwa na kitu cha  kushangaza sana kwa kile anachokifanya na mtu asiejua anachokifanya angeishia kucheka , kilichokosekana ni mziki  wa saida Karoli  wa  Maria Salome tu. 

Lakini Hamza alikuwa siriasi mno , alikuwa tena amefumba macho kabisa huku akiendelea kukata mauno.

“Wewe, wewe umekuwa chizi , kwanini unakata mauno asubuhi asubuhi  yote hii ?”Ilikuwa ni sauti  tamu ya Regina na ilimfanya Hamza afumbue macho yake.

Regina alikuwa amevalia tisheti ya rangi ya pink  iliomfanya chuchu zake kuchomoza kama miiba , kikaptura cha rangi nyeupe  na raba aina ya Converse , alionekana kama vile  ni mwanafunzi wa chuo anaejiaandaa kwenda Jogging.

“Mbona unanikodolea na macho yako?”Aliuliza  Regina huku akiona aibu za kike.

“Regina kumbe na wewe una  ratiba za kuchukua mazoezi”

“Wiki nzima kazini , siku mbili za mazoezi , unadhani  ukiwa na shida ya mwili unaweza kufanya vizuri kazini , halafu acha kubadilisha topiki , kwanini unacheza kibwebwe asubuhi asubuhi?”

“Kibwebwe ndio nini , hii sio mchezo ni mbinu yangu ya mazoezi , ina nguvu  ya ajabu  mno”

“Mh ,mbingu gani hio ya mazoezi ya kukata viuno , jina lake inaitwaje?”

“Jina lake .. dah  hata sijawahi kulifkiria.. kwa mtu wa kawaida anaweza kuona nacheza au kufanya maigizo  lakini usichokijua ni kwamba nisingeweza kuwa na uwezo  niliokuwa nao  leo hii kama sio hii  mbinu”

“Unajaribu kumdanganya nani , mimi nadhani ni kwasababu tayari  wewe ni kichaa  hivyo hata sikulaumu ukikata viuno asubuhi asubuhi”Aliongea  Regina na alijua kabisa  Hamza anaendelea na mchezo wake wa kumdanganya.

“Unadhani nadanganya , ijapokuwa kuna maelezo mengi ambayo  naweza kukuelezea  mpaka uelewe ila hii ni mbinu inayokuwezesha  kuwa na muunganiko wa kimapigano”

“Acha uongo wako , kama ukiona kichaa kishaamka  tafuta sehemu ya mbali ucheze midundiko yako , usije kumuua Shangazi kwa presha”Aliongea Regina  na hakutaka kuongea nae zaidi bali alitoka nje ya  geti na kuanza kukimbia  katika barabara ya ufukwe wa bahari kuchukua mazoezi.

Mara baada ya  Regina kutoka  Hamza hakujali kejeli za  Regina kabisa aliendelea kucheza kama vile  ni  mchawi , alikuwa akicheza anapanda juu anaenda mpaka chini  halafu  anarudi tena na kutingisha kiuno , kwa namna alivyokuwa akifanya ungeishia kucheka tu na kujisemea bangi ya asubuhi asubuhi sio nzuri.

Baada ya lisa kupita hatimae   Regina alirudi akiwa anakimbia  na kwa kuangalia mwili wake  tu alijua  Regina hakuwa mzembe kabisa na ilimshangaza na kujiuliza kwanini hakuona hilo mapema, au ni kwasababu ya  urembo wake ndio maana hakumchunguza, Hamza aliishia kuguna tu na kujiuliza Regina ana siri  gani na kuwa na mwili wa kijeshi.

Hamza mara baada ya mazoezi aliamua kuingia  ndani na kujisafisha na kisha  alikaa mezani kwa ajili ya Breakfast  ambayo ilikuwa imeandaliwa na shangazi.

Regina na yeye alikuwa ndio wa mwisho kukaa mezani , kama kawaida ya  tabia ya wanawake kujiremba ndio maana alichukua muda mrefu  na mara baada ya kukaa mezani  alikula kidogo tu  tena nusu kikombe cha maziwa.

Wakati  Hamza akiwa  bize aliweza kuona simu  ya Regina inaita kupitia kio chake  , ilikuwa ni ya Linda sekretari wa Regina.

“Linda Mr Frei amefika tayari?”Aliuliza  Regina mara baada ya kupokea.

“Ndio  Mkurugenzi , Mr Ferney  ndege yake imekwisha kutua, anajiandaa kuelekea  Hotelini , nasikiliza maelekezo yako?”

“Haina haja ya kumsumbua kwasasa , atakuwa amechoka sana , tukiongea nae sasa hivi  anaweza asitoe ushirikiano mzuri,tuma barua pepe kwa  msaidizi wake na muulize ni saa ngapi tunaweza kukutana”

“Sawa  madam”

Mara baada ya kukata simu Regina alimgeukia  Hamza aliekuwa bize kumalizia   vitafunwa vyote.

“Nimekuandalia nguo  kadhaa  na zimewekwa kabatini chumbani kwako , kazivae kama zilivyo  muda si mrefu tunaondoka”Aliongea Regina.

Previoua Next