Reader Settings

SEHEMU YA 29.

“Kuna ulazima wa kubadilisha na wikiend yote hii , nguo zangu nishazifua   ni safi na  hazina tatizo , kuna haja gani ya kuvaa nguo mpya?”Aliongea Hamza huku akiangalia  Tshirt yake ya rangi ya bluu  aliovaa na pensi yake.

“Kwahio zikiwa safi  ndio  nini, ni brand gani na umenunua shilingi  ngapi?”Aliuliza Regina akiwa na muonekano wa kukereka.

“Kuhusu  hilo ,.. sijui pia”Aliongea Hamza akigoma kujibu amenunua nguo zake shilingi ngapi.

“Mgeni tunae enda kukutana nae  ni Mr Felini , mkurugenzi  wa kitengo cha ubunifu kutoka Zara  Group , sio mtu wa kawaida ni mbunifu namba moja duniani  likija swala la mavazi, sasa akikuona na hayo mavazi yako unadhani atatuchukuliaje , anaweza asikubali kuongea biashara kabisa na sisi”Aliongea Regina.

Hamza alifikiri kidogo   lakini aliona  hakuna haja ya kujibishana na Regina  hivyo alitingisha kichwa kukubali.

“Kama ni hivyo nitaenda kubadilisha”

Lakini sasa  kabla hata hajasimama kutoka  kwenda juu kubadili mavazi yake simu yake ilianza kuita na jina lilitokea  Frida  na palepale bila ya kujiuliza mara mbilimbili alipokea.

“Hello ,  Dr habari za asubuhi?”Alisalimia Hamza.

“Hamza  haraka sana fika nyumbani kwangu , haraka sana  ni dharula”Aliongea  Frida na sauti yake ilikuwa na kitetemeshi na hilo Hamza alihisi.

“Kuna nini Dokta Frida?”Aliuliza Hamza huku akikunja sura  na  alihisi lazima kutakuwa na shida imempata lakini hakusikia sauti tena kwani simu ilishakatwa, Hamza alijifikiria kwa dakika kadhaa  na aligeuka  na kumwangalia Regina.

“Regina  kuna dharula kuna sehemu naenda , hivyo nitatangulia”

“Dharula gani?” Aliuliza Regina lakini  Hamza alikuwa ashatoka kwenye meza  na alikuwa akitokomea nje

“Wewe , unaenda wapi  , tuna kazi  ya kufanya leo , rudiii”Aliongea Regina akimwangalia  Hamza kwa mbali na Hamza alimuonesha ishara tu ya  simu akimaanisha atapiga.

“Nimekufukuza kazi kwanzia leo, usije ukarudi hapa”Aliongea Regina kwa  hasira  lakini hakujua kama Hamza alikuwa amemsikia.

Shangazi mara baada ya kuona tukio hili aliishia kutingisha kichwa chake tu huku akuonyesha wasiwasi   wa mahusiano ya  Regina  na  Hamza.

Hamza alitumia dakika  therathini  hivi kutoka anapoishi mpaka Madale , alitumia   taksi hivyo njia za mikato  zilikuwa nyingi ili kuepuka foleni barabarani.

Kitendo cha  taksi kusimama katika geti ya  nyumba hio , Frida alikuwa tayari yupo nje  na  mara baada ya Hamza  kufungua mlango kutoka, Frida alimpa ishara ya kurudi ndani ya gari na Frida na yeye aliingia.

“Tupeleke Asante Restaurant”Aliongea Regina.

“Malipo yataongezeka boss wangu”

“Just drive”Aliongea  Regina  na palepale dereva aligeuza  gari na kurudi alikotoka.

Hamza alimwangalia Frida , alionekana kuwa na wasiwasi mno kana kwamba ni mwizi anaefukuzwa.

“Kuna nini Frida?”

“Tutaongea”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa , alijua Frida hakutaka kuongea mbele  ya dereva.

Mgahawa wa Asante haukuwa mbali sana ni mita kadhaa kutoka anapoishi  Frida mkabala na kanisa la wakatoliki  na walishuka hapo huku Frida akitoa  elfu therattini  na kumkabidhi yule dereva n baada ya kupokea hela hio  alionekana kuridhika.

 Tuingie mgahawani sasa?”Aliongea Hamza mara baada ya kuona mwanamke huyo  ana sita  sita. “Hapana tunatembea taratibu taratibu  nitakuelezea kadri  tunavyotembea”Aliongea na  Hamza alishukuru jua sio kali sana.

“Kuna nini?”Hamza alivunja ukimya.

“Wiccan wameanza kunifuatilia , leo nachukuliwa kwenda kuhojiwa”

“Kuhojiwa , unamaanisha nini?”

“Siwezi kusema sana , ila nimevunja  kanuni  za ki uanachama na  baada ya mahojiano  pengine  nitaingia kwenye adhabu ya siku  arobaini”Aliongea Frida akiwa na wasiwasi mno na swala hilo lilimshangaza  Hamza.

Frida alikuwa akiangalia nyuma  na mbele , ni kama alikuwa akiangalia kama  kuna anaemchunguza.

“Kabla ya kuja kuchukuliwa  nilihitaji tuonane, maana kuna uwezekano  tusiweze kuonana tena  kwa muda mrefu kidogo”Aliongea na kumfanya Hamza kumwagalia mrembo huyo machoni.

“Kosa  ulilofanya linahusiana  na mimi?”Aliuliza Hamza na   Frida alitingisha kichwa kukataa. “Sijui nani  ananiandama , lakini  taarifa zimefikia umoja  mimi ni shushu wa Sinagogi , napaswa kupinga vikali shutuma hizi katika mahojiano  lakini sina uhakika”Aliongea Frida  huku akishika mkoba wake vizuri.

“Mbinu zinazotumika kutuhoji  sio za kawaida , kuna uwezekano nitaelezea kila kitu  hata zile siri ambazo zipaswi kusema , sina muda mrefu  wa kuongea na wewe , nataka kukuuliza swali moja tu?”

“Uliza?”Aliongea Hamza huku ndita zikijikunja kiasi.

“Baada ya kupata  taarifa  ya vifo vya  kundi la wawindaji kutoka Samar , moja  kwa moja nilijua  kuna uwezekano umehusika na vifo vyao,  kweli si kweli?”Aliuliza Frida na Hamza hakujua mwanamke huyo alijuaje lakini alitingisha kichwa  kuashiria ndio na  Regina alivuta pumzi nyingi na wote walikuwa wamesimama.

Kwa jjinsi walivyokuwa wakionekana ni kama  Frida na Hamza ni wapenzi  na hata baadhi ya watu waliokuwa wakiwaangalia  walikuwa wakiwaonea wivu , isitoshe Frida alikuwa mwanamke mrembo  na  watu wengi  katika mitaa hio walikuwa wakimjua kama mwanamke mgumu na wa hadhi ya juu.

“Naamini walichokifuata ni kitabu  alichokuachia Dokta Genesha, huwa inanishangaza  kuona watu wanawinda  hiki  kitabu ilihali hakuna  katika dunia hii mtu anaeweza kutafsiri lugha yake”Aliongea  Frida na kumfanya  Hamza midomo kucheza.

“Unaonekana  kujua mambo mengi mno , sishangai kwa  jasusi kama wewe , ila niambie  unadhani  ni kweli hakuna mtu wa kuweza kutafsiri maandishi ya  hiko kitabu?”

“Tofauti  na wewe sidhani kama kuna mtu anaweza kukitafsiri , hata Dokta Genesha mwenyewe uwezo huo hana  ndio maana alikupatia , haikuwa kwa bahati mbaya , wewe ndio mtu  pekee ambae utaweza kutafsiri lugha yake, swala ambalo linaweza kuwa hatari  zaidi”

“Kila mtu ananiambia ninaweza kutafsiri  lakini bado  nashindwa kuelewa  natafsiri vipi lugha ambayo  hakuna ambae anaijua?”Aliongea  Hamza huku akikuna nywele zake.

“Hamza njia pekee ya kumjua Mzee ni kukitafsiri , hakuna namna nyingine , kwa maelezo ya dokta Genesha  wewe pekee utaweza kukitafsiri  baada ya kuujua uhalisia wako , namaanisha kumbukumbu  za maisha yako ya nyumba ambazo umesahau?”

“Hey! Unaongea nini , kumbukumbu gani ambazo nimesahau , nina kumbukumbu  zangu zote  kasoro za wazazi wangu tu?”Aliongea Hamza  na muda huo walikuwa washaanza kutembea , Frida alikuwa akiangalia saa yake.

“Kiihusu swala  la kumbukumbu zako siwezi kusema sana , ila ni swala  la  ndoto ulioanza kuota, muda wangu umeisha , nilichokuitia ni kukukabidhi Mshumaa alioniachia Dokta  Genesha”Aliongea  Frida  na palepale  aliingiza  mkono  kwenye mkoba wake na kumpatia Hamza kiboksi.

“Mshumaa!!?”

“Ndio , Mshumaa huo ndio kitu ambacho  Dokta Genesha ameniachia nikupatie ,  ni Mshumaa wa  Nuru wa kuamsha  ndoto , ukifika  sehemu tulivu utaona  vifaa vyake vyote vipo , hakikisha ikifika saa tano usiku unautumia ,ila ni hiari yako  kuutumia katika huo muda , ndio njia ya wewe  kutafsiri kitabu alichokuachia Dokta Genesha  na ndio  njia pekee  ya kuujua uhalisia wako  na kumfahamu Mzee, maelekezo yote  namna ya kutumia yapo ndani”Aliongea  na kumkabidhi Hamza  ambae bado alikuwa na  mshangao.

“Nilidhani ulisema mpaka tuingie kwenye chumba cha Nuru?”

“Maelezo ya Dokta  Genesha wewe ndio mtu pekee unaejua chumba cha Nuru kilipo , lakini umesema hujui , njia pekee  kwasasa nikutumia huo Mshumaa”Aliongea Frida.

“Umeongea sana Frida ,  lakini mpaka leo hii ni siku ya  tatu tunaonana , sijui historia yako licha ya  mambo ulionielezea ,  nakuamini vipi katika hili?”

“Huna haja ya kuniamini, Amini nafsi yako na kila unalopanga litafanikiwa , muda wangu ushaisha , endelea kutembea  bila kuangalia nyuma”Aliongea  na Hamza alikifiria kidogo na kisha aliendelea kutembea kama alivyosema na  baada ya  hatua kama isihirini na nane aliishia  kukunja sura.

“Mateso mema Frida” Aliwaza Hamza peke yake.

Nyuma Frida hakuonekana tena , haikueleweka alipotelea  wapi lakini  watu  walikuwa wakiendelea na shughuli zao na hawakuwa kabisa na habari na Hamza.

Kwa lugha nyepesi  tukio ambalo sio la kawaida lilitokea nyuma ya Hamza lakini watu  hawakuweza kuona  kabisa wala kuhisi.

Hamza  hakuona haja ya kupoteza muda , alijua ashamkasirisha  Regina tayari kwa kuondoka bila ya kumpa maelekezo ya kutosha , hivyo aliona awahi  kuelekea  huko hata kama  ni kwa kuchelewa.

Alipiga mahesabu kutoka Umoja Road mpaka Tegeta Kibaoni ingemchukua dakika nyingi kutembea wa mguu hivyo alihitaji usafiri , wakati akijishauri ni usafiri wa aina gani aliweza kusikia honi ya gari ambayo ilimpita na kwenda kusimama  mbele yake.

Ilikuwa ni gari aina ya  BMW X7 rangi  nyekundu ,  kwa uelewa wa haraka wa Hamza  aliona gari hio ni ya thamani na hakujua ni  nani anapigiwa honi lakini mara baada ya kuchunguza  aliona alikuwa peke yake.

Dakika ileile akijiuliza kama yeye ndio anaepigiwa honi , mlango wa gari ulifunguliwa  na alitoka mwanamke mrembo katika ile gari alievalia suruali ya suti rangi ya ugoro hivi na viatu vya High  Heels.

Alikuwa mrembo haswa na kumfanya   hata Hamza mwili wake kumsisimka.

Mwanamke yule mrembo alionyesha ishara ya kuinua mkono  akimwita Hamza  na kitendo kile kilimfanya Hamza amkazie macho na  palepale aliikumbuka sura hio ya kirembo , alikuwa ni Prisila Singano, Mrembo aliekutaa nae  katika hoteli ya  Dosam V   wakati alivyofika kufanya usaili..

Hamza alitoa tabasamu , ukweli ni kwamba alikuwa akijiuliza mrembo huyo yupo wapi , kuna siku alitamani hata kumuuliza  Regina lakini alihofia  Regina anaweza kumfikiria vibaya.

Ila Hamza alijiuliza ilikuwaje mwanamke huyo alimuona maana walionana siku moja tu  na pili   yeye alikuwa amempa  mgongo, inamaana hakuona sura yake kwani uelekeo aliokuwa akielekea na  gari hio ndio  ilipokuwa ikielekea.

Upande  wa Prisila licha ya kusimamisha gari lakini  alionekana kidogo kuwa na uso uliokuwa siriasi na aliingia  ndani ya gari  kabla hata Hamza hajamfikia.

Hamza  alijiongeza  na kuzuguka upande mwingine na kufungua mlango na kuingia ndani.

Gari ya mwanamke ni ya mwanamke  tu , ilikuwa na harufu nzuri mno na ubaridi  usiokera.

“Asante sana kwa  Lift Prisila,  habari za toka siku ile?”Aliongea Hamza huku akiweka muonekano wake wa kizembe.

“Unakumbuka  jina langu?”Aliuliza  Prisila huku  akirudisha gari barabarani na muonekano wake uliimarika zaidi mara baada ya Hamza kutaja jina lake.

“Mwanaume yoyote ambae  anaweza kusahau jina la mwanamke mrembo kama wewe atakuwa  na matatizo”

“Kwa jinsi ulivyokuwa ukiniangalia  nilijua umenisahau , ila nimeshangaa uko peke yako , yule mrembo yupo wapi?”Aliuliza  Prisila  huku akikaza macho barabarani.

“Mrembo gani?”

“Ulieshuka nae pale Asante Restaurant, nilikuwa ndani , nilitegemea mtaingia ila niliona  mkiondoka , unadhani ningekufahamu kwa kuangalia mgongo  wako tu?”Aliongea na kumfanya Hamza sasa kuelewa.

Prisila alikuwa na sauti nzuri  mno na kila dakika ambayo mwanamke huyo alivyokuwa akiongea ndio mwili wake ulivyokuwa ukisisimka.

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio sasa ndio  alijua kumbe Prisila  alimuona wakati akishuka na Frida pale mgahawani , ilileta maana kwani kulikuwa na watu wengi ndani ya mgahawa huo ndio maana  Frida akasema watembee.

“Ni heshima kubwa kukumbukwa na mwanamke mrembo kama wewe?”

“Hakuna cha kushangaza kukumbuka , mimi ndio nilikukutanisha na Regina ,  si rahisi kusahau mpenzi feki wa bosi wangu , anyway  hadhi yako imepanda  pia , Dokta Frida sio mwanamke anaeweza kutangulizana na yoyote”

“Unamjua Dokta Frida?”Aliuliza Hamza  na Prisila  alitingisha kichwa.

“Baadhi ya watu wa kawaida  wanaweza wasimfahamu

Frida , lakini  katika  ulimwengu wa   wanataaluma   wengi  tunamfahamu ,  ndio maana nimeshangaa kukuona  ukiwa na Frida  ,Dokta namba moja wa taasisi ya Haliz, una siri gani ambayo hatuijui?”

“Siri gani tena?”Aliuliza Hamza  na kuna kitu alishajua kuhusu Prisila ni mwanamke ambae yupo siriasi sana , ijapokuwa alionekana kama maneno yake  yapo  na viashiria vya urafiki lakini alionekana ni mwanamke anaehitaji majibu ya haraka.

“Kwa mtu yoyote aliewaona  atasema  mna ukaribu , kama sio wa kimapenzi, ni wa kindugu  na kama sio wa kindugu basi pengine  ni wa kikazi , lakini  kwenye uhusiano wa kikazi  ni asilimia chache  sana  uwezekano huo kuwepo , Frida ni mwanasayansi  wewe ni  mwanafunzi wa chuo taaluma  mbili tofauti?”Aliongea na  Hamza alitingisha kichwa.

“Uliosema yote hayawezekani , mimi na Frida ni mtu na  mfayakazi wake, ulivyotuaona nilikuwa nikipokea maagizo pale”Aliongea Hamza huku akicheka.

Prisila  aliongeza umakini  barabarani baada ya kufika  makutano ya barabara ya  Tegeta.

“Nimekupa  lift  ila hujanniambia unaelekea wapi?”Aliuliza  na kumfanya  Hamza kukuna kichwa. “Nilipaswa kwenda  na bosi wangu kwenye kikao na mgeni wake  ila nilipata dharula , sijui ni hoteli gani?”.

“Nini!, Dharula  hio ni  kukutana na  Frida?, Regina akijua anakufukuza kazi?”

“Dharula ni dharula kwanini anifukuze kazi?”

“Sikulaumu , hujakaa muda mrefu na  Regina , kama mpenzi feki kazi unayo?”Aliongea huku akicheka.

Prisila ndio mtu pekee ambae alikuwa akijua mahusiao  yake na Regina  ni feki , pengine ni kwasababu  Prisila ndio aliweka tangazo mtandaoni na  hata kumpokea Hamza katika usaili , kufikiria hilo  Hamza shauku ilimjaa,haikuwa rahisi kwa  Regina kumpatia kazi  nyeti kama hio  Prisila , ilimaanisha wawili hao lazima watakuwa na ukaribu.

Prisila kwa kutumia gari  yake hio ya kisasa alipangusa katika  kioo na kisha akapiga namba ya Linda  na Hamza alitoa tabasamu na kuona  huyu mwanamke ni jiniasi , amefanya kile ambacho alikuwa akiwazia amuombe afanye.

Hamza alikuwa ashapiga namba ya Regina kabla hata

hajaingia kwenye gari ya   Priisila  lakini haikupokelewa  tena ilikatwa baada ya kuita  kidogo,alijaribu na ya Linda hivyo hivyo lakini pia ilikatwa.

“Linda  mpo hoteli gani?”

“Madam Prisila kwanini unauliza?”Sauti upande wa pili ilisikika . ilikuwa ya  Linda na ilionyesha heshima.

“Nataka kujua kikao kinafanyikia wapi?” “Tupo Seaview  hoteli”Aliongea.

“Okey!!”

Prisila palepale alikata simu na kumwangalia   Hamza na  Hamza alitabasamu.

“Uwezo wako wa kumsoma mtu  ni wa juu , upo kama baba yako”

“Usifurahi sana ,  nimekusaidia  hii  inamaanisha una deni kwangu”

“Nipo tayari kulipa muda wowote Madam”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu  la kizembe  na  Prisila  alitoa kicheko hafifu.

“Nitakuacha  Jogoo , nadhani itakuwa  rahisi kupata usafiri wa kukufikisha   Serena”

“Nitashukuru sana”

“Kama unanishukuru niambie ukweli  mahusiano yako na  Frida?”

“Ah..!” Hamza aliishia kushika pua yake na kujiambia  inamaana bado swala la Frida linamsumbua huyu mwanamke , lakini  hayo ni mambo yake binafsi kwanini anauliza sana.

“Ni kama nilivyosema”

“Okey!”Aliongea Prisila  na muda huo walikuwa washafika tayari  kituo cha  Jogoo na  Regina alisimamisha gari.

“Prisila asante sana kwa lift , nadhani tutaonana kazini?”Aliongea  Hamza na Prisila alitingisha kichwa. 

Hamza alitoka na kufunga kioo na Prisila   aliondoa gari tataribu huku wengi wakiikodolea macho gari ile na ilipokumja kushoto  waligeuza macho na kumwangalia  Hamza.

Hamza kwa jinsi alivyoshushwa alijisikia vibaya kupanda daladala , lakini aliona  pia daladala sio chaguo sahihi kama anataka awahi hivyo aliiita boda na kupanda , ili mbele kwa mbele achukue  taksi itakayomfikisha Seaview.

Baada ya kupata pikipiki huku akihakikisha mzigo wake aliopewa na  Frida upo salama  aliondoka.

Nusu saa mbele wakati  akiingia ndani ya hoteli ya Serena aliweza kuiona  ile Lexus lx 600 ni alijua mara moja ni ya Regina  maana ndio moja  ya  gari la kifahari  ambalo lipo katika maegesho ya muda  mfupi.

Hamza alijua kabisa Regina atakuwa aliendesha gari yake  mwenyewe mpaka kuja hapo.

Hamza  mara baada ya kufika alijipiga kichwani , hakujua   Regina atakuwa katika floor ipi wala anakutana  nae vipi  na  Hamza alisita huku akijiuliza au aende  front desk kuuliza  lakini kabla hata hajaamua cha kufanya aliweza kumuona Linda  na hatimae Regina katika floor ya kwanza upande wa mhagawa na alijikuta akivuta pumzi ya ahueni na kisha alizipiga hatua kuwasogelea.

“Mkurugenzi , Linda , mbona mmekaa hapa , ndio manisubiri au?”Aliuliza Hamza.

Regina mara baada ya kumuona Hamza  hakuweza kujizuia  kukunja ndita  na alimwangalia mara moja tu na kisha akashusha kichwa chake chini akijiweka bize na juisi yake  huku akimpotezea, ilionekana alikuwa amekasirishwa  na kitendo cha   Hamza kuondoka bila kupata ruhusa yake kumuwahi mwanamke aliemsikia akiitwa Dokta Frida.

“Mkurugenzi alihitaji  uwe  mkalimani katika kikao chetu lakini ukaamua kuondoka kana kwamba   jambo hili sio la muhimu , huhitajiki tena kwa  kazi  ya ukalimani hivyo unaweza kuondoka”Aliongea Linda.

“Kwanini niondoke, naamini  hata  bado hamjakutana na  Mr Felini”Aliongea Hamza  huku akiondoa wasiwasi wake na tabasamu.

“Tunaweza kuongea na Mr Felin kwa kingereza tu  hata  bila ya uwepo wako , na isitoshe kwa mavazi uliovaa  ukikutana na mgeni wa heshima  huyo ni kuleta matatizo tu”Aliongea  Linda na kumfanya Hamza kuangalia mavazi yake.

“Kwanini unasema hivyo , sioni tatizo juu ya mavazi yangu”

“Mavazi gani hayo ambayo  yashaanza kufubaa kwa kufuliwa  mara nyingi, halafu staili yake ni ya kizamani kama vile upo karne ya ishirini”

“Hii ni Retro style, ina radha ya kifasheni ya upekee”Aliongea na  Linda wakati alipokuwa akitaka kuendelea kujibishana nae aliacha mara baada  ya kuona watu wakitokea upande wa lift.

“Mkurugenzi , Mr Felini na timu yake wale wanakuja”Aliongea Linda na mara baada ya Regina kusikia kauli hio  aliweka   glasi yake chini na kisha akasimama  ili kwenda kuwapokea  lakini kabla hata hajaanza kupiga hatua alimgeukia Hamza.

“Usinifuate unaweza kubakia hapa au ukiona hapakufai ondoka”

Hamza mara baada ya kusikia kauli ile alijihisi kama vile amekosewa  na alijiambia inamaana mavazi yake  yanaonekana sio ya thamani kiasi kwamba wanamnyanyapaa, Hamza aliangalia mavazi yake na aliona ya kawaida , isitoshe ni mavazi ambayo anahistoria nayo kubwa  tu.

Lakini Hamza hakutaka kumuudhi Regina , ilionekana kabisa mwanamke huyo alikuwa akikipa  kikao hicho thamani kubwa hivyo aliamua kukaa kusubiri.

Muda uleule Regina na Linda waliweza kuwafikia  wazungu wale  na kuwasalimia.

Felini alikuwa mrefu mwenye kifua kipana  akiwa na nywele alizofunga kwa nyuma kama Halaand, alikuwa amevalia  suti ya rangi ya  bluu na nyekundu , shati jeupe  ambalo  lina kola ilionakshiwa kwa mua maua ,  jeans  na  sendo za ngozi.

Mtu  wa aina hio na mavazi yake ilikuwa rahisi  kumtofautisha na yule mzungu mwingine moja kwa moja hasa  kwenye saa yake ya Patek Phillipe.

“Oh, you must be Miss Regina , I’ m really sorry , I took  a break  at the hotel  and made you visit  for  a long time”Aliongea  bwana huyu mzungu akiomba radhi kwa  kumsubirisha Regina kwa muda mrefu wakati akiwa amepumzika, alionekana kuwa mkarimu.

Regina upande  wake  aliishia kutoa  tabasamu  hafifu , ijapokuwa lilioneksha hali ya ukaribisho lakini kwa ukauzu wake  ni mara chache sana kumuona akitoa tabasamu la aina hio.

“Umekuwa kwenye ndege kwa  masaa mengi hivyo ni  haki yako kupata muda kidogo wa kupumzisha mwili

,  nimekuwa na matarajjio makubwa juu ya kikao hiki ,  sasa hivi tayari ni  saa sita muda wa chakula cha

mchana , mnaonaje tukipata chakula pamoja?”Aliongea Regina kwa kingereza 

“Nimeshapata chakula tayari nilipokuwa kwenye ndege  hivyo sitopata muda wa chakula cha mchana , napaswa kwenda Dubai baada  ya hapa  kutembelea matawi yetu  na baada ya hapo nitaelekea Paris, ratiba yangu imebanana sana”Aliongea na jambo lile lilimshangaza  Linda na Regina kwani

hawakutegemea kama Fellin  angekaa  Tanzania kwa muda mfupi sana.

Lakini ilikuwa sawa kwa mtu  mbunifu maarufu kama huyo  muda ulikuwa ni kitu cha thamani sana , maana ukiachana na kubuni mavazi ya  kampuni lakini vilevile alikuwa akibuni mavazi yake mwenyewe kwa ajili ya maonyesho.

Kitendo cha  mfanyabishara kama yeye kumualika  mtu bize kama huyo kuja mpaka Tanzania ilikuwa ni heshima kubwa.

“Kama  ni hivyo  kwanini tusitafute sehemu  na kukaa kwenda moja kwa moja kwenye  maongezi?”Aliongea Linda.

“Yes”Aliongea na muda ule aligeuka  nyuma  kama kwamba kuna mtu mwingine alikuwa akimsubiria na kweli alinyanyua mkono mara baada ya kumuona mwanamke.

“Hey!, Salma ,  I am here..”

Mara baada ya kuona  Fellin kuna mtu anamwita iliwafanya Linda na Regina kugeuka pia kuangalia  mtu alieitwa Salma.

Alikuwa ni mwanamke mrembo haswa alievalia   gauni  lenye kola nyeusi la  chui chui ambalo limebana sana , alikuwa amependeza mno kwa jinsi vazi hilo lilivyomkaa huku akivalia  viatu vya skuna , alitembea kwa kujiamini   mno.

Kwa jinsi alivyovalia unaweza kusema anaenda  kwenye date  lakini muonekano wake pamoja na 

makeup ilimfanya kuwa na muonekano wa 

kimaringo  na kumfanya  watu wengi wamwangalie.

“Salma  Mohamed Salah!!”

Wasiwasi ulionekana katia macho ya Regina huku akimwemwesa midomo kwa kutaja jina hilo.

Hata kwa yule mwanamke mrembo mwenye kuchanganya rangi ya kiarabu na kiafrika alionekana kumfahamu  Edna na alionyesha tabasamu lenye viashiria vya dharau.

“Regina  na wewe upo hapa kwa  ajili ya  ushirikiano wa kibiashara na  Fellini?, Nadhani nikuambie tu  kwamba  umechelewa na utaishia kukata tamaa”Aliongea.

“Salma unafahamiana na   Miss Regina?”

“Ndio ,  tumesoma  shule moja High school , baada ya kumaliza kila mtu alichukua uelekeo wake , hatujawahi  kuonana kuanzia hapo mpaka wote tulipokuja kuwa wafanyabiashara na kuingia kwenye ushindani”Aliongea Salma.

“Basi  vizuri , kama mnafahamina nadhani ni vizuri tukianza kuongea  kuhusu  ushirikiano , kuna mgahawa hapa hivyo haina haja ya kutafuta eneo lingine”Aliongea na  palepale mzungu yule pamoja na msaidizi wake walisogea upande wa mgahawa.

Hamza mara baada ya kuona kundi hilo la  watu limesogea  karibu  na yeye hakutaka kumkasirisha  Regia hivyo hakuwasalimia kabisa  na kula buyu.

Ukweli ni kwamba  Linda na Regina hawakuwa na time nae kabisa  na Regina muda huo mara baada ya kuona  Salma  alikuwa na mawasiliano na  Fellini   alijua kabisa mazungumzo yashaingia doa , mshindani wake mkubwa wa kibiashara kwa ukanda  Afrika mashariki  na kati  ni kampuni ya  Salah,  lakini hata hivyo  hakuwa na jinsi na kukubali kupitia changamoto hio,  angejua  kampuni ya Salah ilikuwa 

ikitaka pia  ushirikiano na  Fellini pengine angejiandaa zaidi, kingine ambacho kilimshangaza  Regina ni kwamba  Salma alikuwa akisimamia kampuni ya mitindo  upande wa China  lakini ghafla  anaonekana mbele yake, moja kwa moja alijua  lazima kampuni imempa kazi ya kuhakikisha dili  la ushirikano na Zara  liafanikiwa kwa namna yoyote.

Wote kwa pamoja walitafuta  siti zao  na sasa kukawa na makundi matatu yanayowakilisha kampuni  tatu tofauti , Regina  akiwakilisha Dosam , Salma akiwakilisha  Salah  na  Fellini akiwakilisha  Zara. “Mr Fellini , we have an appointment  to meet privately , joining of Salah  family’s representative , I’ m  afraid, is not appropriate”Aliongea Regina akimaanisha kwamba walikuwa na ahadi ya kukutana lakini kuunganisha na familia ya  Salah , sio  sawa.  

Upande wa Felini alipewa Kiko  ya kuvutia sigara na kuwasha na kisha akavuta moshi  huku akiwa na tabasamu lenye utulivu.

“Usiwe na wasiwasi  Miss Regina , nilikutana na 

Salma  kwenye maonyesho ya wiki ya Fasheni jijini New York  na kugusia  swala  la kibiashara , najua  familia yake ndio wamiliki wa kampuni  kubwa ya mavazi ya Salah kutoka Uturuki  , lakini sina mahusiano  yoyote na yeye zaidi ya  maswala ya kibiashara, yoyote kati yenu ambae atakuja na vipengele  pamoja na ofa nzuri  ya ushirikiano wa kibiashara sitokuwa na upendeleo wa  kuchagua , kwa haki  na uwazi nitachagua  upande sahihi”

“Hehe..  Regina unaogopa nini, nakukumbusha tu  familia yetu ndio  wa kwanza kabisa  kuwa wakala wa bidhaa za kifahari kutoka makampuni  makubwa kabla yenu, Vigezo vyake  ni vingi sana , sisi ni tofauti na kampuni yeu ambayo  ipo  kila sekta”Aliongea Salma.

“Kuwa na vigezo vingi haimaanishi  chochote , nakubali nyie ndio mlianza  kuleta mavazi ya kimitndo Tanzania lakini  baada ya  kampuni yetu kuingia katika biashara hio tuliwapita miaka mingi  tu , Zara ni kampuni ambayo malengo yao  ni

kuendeleza utawala wao wa  kimavazi katika kila soko , unadhani ni rahisi kuingia mkataba na kampuni ambayo  inalega lega sokoni”Aliongea Regina.

“Una mawazo ya kimasikini , hivi unadhani  kujipanua kwenu kusiko  na malengo  ndio uwezo wa kampuni , sisi  kama kampuni sio  fasheni tu tunayoheshimu bali na utamaduni pia  unaoendana na  mavazi, kampuni yetu inaendeshwa kwa misingi  ya kisera ilioweka tokea kuanzishwa kwake, hatuwezi kufanya kila biashara ambayo tunaona  tunaweza kupata faida , kwetu sisi  hela sio malengo  bali ni kukuza  utamaduni,  tunataka ushirikiano na  Fellini kwasababu malengo yetu ni kuhakikisha tunateka soko  la fasheni inayoendana na utamaduni wetu wa kiafrika”aliongea Salma  kwa kingereza akimjibu

Regina na  Felini aliweza kusikia  majibishano yao . “Salma yupo sahihi , kampuni ya Zara  haingii  katika ushirikano wa  kibiashara na kampuni ambayo  ina Asset nyingi  wala  thamani ya hisa sokoni, tunajua fika uchumi  wa kampuni ni   moja ya kigezo  lakini  kwa vyovyote vile  tunazingatia  kampuni ambayo ina sera zinazoendana na mazingira  ya jamii husika”Aliongea  Fellini.

“Mr Fellini nakiri kwamba   katika biashara ya mavazi , kampuni ya  Salah ina  uzoefu mkubwa na taaluma , lakini  tupo na nia ya dhati  pamoja  na  ari  ya kujiamini  katika kuifanya kampuni ya Zara  kuuza sana katika soko  la  Afrika”Aliongea lakini  kauli ile ilimfanya  Fellini kukunja ndita.

“Miss Regina , naomba uniwie radhi kama  nitatoka nje ya mpaka , ukweli ni kwamba nimejaribu kufanya uchunguzi  kiasi kuhusu wewe na nikiri nakuheshimu sana  kwasabau upo katika kundi adimu la watu wenye akili  nyingi duniani , lakini hata hivyo  nimefuatilia malengo ya kampuni yenu sera yenu kubwa ni kujipanua na kuhakikisha mnaingiza faida  kwa kiasi kikubwa , hivyo  mbinu zenu za kibiashara

zipo kwa ajili ya  kutengeneza hela..”

Regina  alishangazwa na kauli za Felllini na alianza kujisikia wasiwasi katika moyo wake.

“Kama nilivyosema   sera ya kampuni yetu ni  kutamfuta   mshirika ambae anatulewa  ili kusambaza tamaduni zetu, tunachouza sokoni sio bidhaa tu bali ni  wazo , huduma  na  ustaarabu  ulioendelea katika jamii”

“Mr Fellin naelewa unachosema , sitoingilia  mapendekzo ambayo mtakuwa mnatoa kama   kampuni , ninachotaka kusema ni kwamba  tunao uwezo wa kuwafikia wateja  kwa haraka na kwa wingi zaidi kuliko kampuni yoyote ndani ya  Afrika mashariki na kati”

“A nouveu riche is a nouveu riche , Regina huelewi tu , anachotafuta Mr Felleni ni mshirika wa kibiashara  na sio muuzaji, maana yake ni kwamba  lazima na wewe kama kampuni ushiriki katika mawazo ya  ubunifu wa bidhaa, michoro  , aina ya  kitambaa  na eneo la uzalishaji , ukishajua hatua zote hizo inamaana utaelewa na  kilichokusudiwa katika bidhaa  na itakuwa rahisi kumfikia  mteja  na kumfanya anunue .’listen up , its not the consumer its customer”  Kulikuwa na  kila ishara ya furaha katika uso  wa  Mr Fellini mara baada  ya kusikia msemo aliomalizia nao  Salma.

“Yes , Miss  Salma is right , As expected  of a talented  girl who graduated  from parsons  school of Design , My analysis is very thorough , that is what I mean”Aliongea  akimaanisha kama alivyotegemea kwa msichana mwenye kipaji aliemaliza  chuo  cha ubunifu cha Parson , uchambuzi wake ni yakinifu.

Salma mara baada ya kusifiwa alifurahi mno meno yote nje na alimwangalia Regina kwa  tabasamu la uchokozi.

“Regina  jikatie tu tamaa , wewe endelea na biashara  ya kununua ardhi , kujenga viwanda na kununua hisa , mambo ya  fasheni  hayakufiti kabisa”

Kwa jinsi alivyoongea ni kama vile alikuwa akishindana na  Regina  au alikuwa na kinyongo cha muda mrefu.

Regina aliishia kubaki kimya  na alimwemwesa lips zake , huku pembeni  Linda  akiwa na uso uliopauka kwa hasira.

Previoua Next