Reader Settings

Regina alienda mbali na kukumbuka aligombana na Hamza kwa kutotaka kutupa mavazi yake , alishindwa kuzuia  hisia mbaya zilizoanza kumvaa na kujiambia kama kweli anachosema Fellini ni kweli basi mavazi hayo ya thamani si yatamfanya aonekane mjinga  na mshamba.

“Mr Fellini macho yako yatakuwa yanakudanganya , haya mavazi aliovaa unaweza kuyakuta kila mkoa ndani ya Tanzania yanauzwa”Aliongea Regina kuepusha kuabika.

“Msiniambie hakuna  ambae anaona  uzuri wa mavazi  aliovaa Mr Hamza pamoja na pensi yake?”Aliongea  huku akiwaangalia mmoja mmoja kana kwamba anaomba kuungwa mkono.

Lakini wote walitingisha  vichwa vyao kukataa , hakuna cha maana  kwenye hayo mavazi zaidi ya uchakavu tu”

“Nyie watu hamjui  kabisa , nadhani kwasababu sio mafundi,  katika ulimwengu wa kifundi   utaalamu wa juu zaidi ni  kutengeneza vazi ambalo unao uwezo wa kulirudisha  upya kwa mchakato mwepesi sana na ukauza sokoni kwa bei ileile”Aliongea   mzungu huyo lakini hakuna hata mmoja ambae alielewa anachomaanisha, hata  Salma aliesomea Person chuo  namba moja cha mitindo kutoka Marekani hakuelewa.

SEHEMU YA 31.

Regina mara baada ya kuona haelewi alichomaanisha  Fellini aliomba  aeleze kwa lugha  nyepesi, bado hakuwa amekubali nguo alizovaa Hamza ni za bei ya juu.

“Mr Fellini unaonaje ukituelezea  kwa  urahisi tupate kuelewa?”Aliongea na  Fellini alimwangalia Hamza.

“Mr Hamza naomba ruhusa yako kushika nguo zako”

“Hakuna shida , ungeniambia  vizuri ningekuelewa tokea mwanzo”Aliongea Hamza huku akicheka.

“Salma  nadhani utakuwa  unajua  ni malighafi  za nguo za namna gani zimetumika”Aliongea akimpa ishara  Salma kusogea karibu na  yeye pia  alishika lakini dakika ileile muonekano wake ulibadiika.

“Noble family material!!?”Aliongea  Salma  huku akishangaa.

“Correct, hii  ni aina ya kitambaa cha SCUBA  ambacho kiliongezewa ubora kwa mara ya kwanza nchini Ubelgiji na baadae kikawa kitambaa namba mmoja kinachotumiwa  ndani ya Savile , ni aina ya kitambaa ambacho mchakato wa kukitengeza  kuwa mgumu na ndio maana sio swala la hela tu kununua kitambaa hiki, sasa unadhani nguo yoyote ambayo imetengenezwa na aina hii ya kitambaa inaweza kuwa ya kawaida?”

Regina mara baada ya kusikia kauli hio  alishindwa kujizuia na kusogea na yeye ili kugusa kitambaa hicho  kwa umakini , ijapokuwa alishawahi kugusa nguo za Hamza mwanzo  lakini ile kejeli  juu ya nguo hizo  hakuweza kuona kitu special.

Lakini muda huo  alivyogusa  nguo hio  ki uchunguzi   ndio sasa anagundua ni kweli kitambaa chake hakikuwa cha kawaida kabisa.

“Mnajua nini kimeongezewa  upande wa hio michirizi ya pensi kushoto na kulia?,  angalia kwa pembeni utaona  ni kama inabadilika rangi  kutokana  na mwanga?”Aliuliza  Fellini na  wanawake  wote waliangalia kwa kutumia angle ya macho na kuona ni kweli rangi  ya nguo  inabadilika,  lakini hakuna ambae alikuwa na majibu.

“Ngoja niwaambie , ni nyuzi  nyuzi za madini ya 

Platinum kutoka Afrika ya kusini, hii inafanya kitambaa chake  kuwa  cha thamani ya juu   mno  na adimu dunia nzima,  gharama  ya uzalishaji wa kutengeneza  suruali ni Euro  laki moja”Aliongea  

Euro laki moja inamaana  Hamza amevaa nguo  ya thamani ya  milioni mia tatu  za kitanzania , Regina , Linda na  Salma mara baada ya kusikia kauli hio  walishindwa hata kupumua vizuri.

“Hey usiongee kwa nguvu , unataka  watu wasikie  na kuniwinda wanivue nguo nitembee uchi”Aliongea Hamza  akimwambia Fellini.

Fellini alijikuta akigundua alikuwa na mzuka  kiasi kwamba alikuwa akiongea kwa sauti na aliinamisha kichwa kuonyesha  ishara ya kuomba radhi.

“Hilo ni la kwanza , kinachofuata  na kutofautisha hizi nguo ni aina yake ya ushonaji”Aliongea na  kisha alishika  kola  ya tisheti ya Hamza na kuinyanyua kwa juu.

“Nadhani  mshawahi kusikia teknolojia  ya Hermes  ya ushonaji wa nguo  za leather  wanatuia  SDD-

stilt method ,  hii njia ya ushonaji  mara nyingi inatumia sindano mbili kwa wakati mmoja na kufanya bidhaa yoyote ya kampuni ya Hermes  ya Leather kuwa   imara sana  na kupendeza kwa wakati mmoja 

Ukweli ni kwamba  kati ya washonaji wengi  , kuna mbinu ya kale  ambayyo  ipo karibu kupotea , inaitwa Concealment Saddle needle techinique, hii ndio mbinu ambayo Master George anatumia , lakini mpaka leo hii  hata yeye mwenyewe hajabobea  kuitumia kwa asilimia mia moja , mbinu hii  inakupa nafasi ya kutumia  nyuzi tatu  katika uzi mmoja, hivyo kufanya nguo kuwa imara  na kudumu kwa muda mrefu”Aliongea  na  Regina  na Salma walisogea karibu kuangalia namna ya ushonaji ulivyokaa na kwa kuangalia tu  waligundua mashine ya cherehani ni ngumu sana kufanikisha ushonaji huo.

“Hakuna ushonaji wa aina yoyote  duniani unaoifikia hii mbinu , cha kufurahisha zaidi  ukitaka kuifumua nguo yote kwa urahisi unagusa sehemu moja  na unatoa nyuzi zote na  nguo inarudi katika kitambaa na baada ya hapo inaweza kufanyiwa maboresho  na kisha kurudishwa  katika muonekano wake mpya”

Regina aliishia  kukosa hiari  na kuamini kabisa maamuzi yake  ya wakati ule  hayakuwa sahihi , lakini aliona pia  Hamza alikuwa ni mshenzi sana , yaani mtu anavaa  nguo  ya thamani kubwa namna hio  lakini anajifanyisha   ni masikini  tena mbaya zaidi anajifanyisha  mtu anaependa sana hela.

“Hamza kwahio ni kweli unafahamiana na huyo Master Alec , kwanini hukusema?”Aliuliza Regina.

“Umesahau nilikuambia nguo hizi nilipewa na rafiki yangu , halafu sio kama uliniuliza ni rafiki  gani?”Aliongea na kumfanya Regina kumwemwesa midomo , ilikuwa ni kweli hakuuliza ni rafiki gani.

“Wewe ni dereva tu , kwanini  nguo zako zitengenezwe na mafundi wanaoshonea nguo wafalme , au umeziiba  ndio maana umeshindwa kujua thamani yake?”Aliongea Salma.

Fellini mara baada ya kusikia kauli  hio ni kama hata yeye wazo hilo lilimwingia  , kwani ni ngumu mtanzania  kama Hamza  kuwa na nguo ambayo imetengenezwa na  Alec , hata kama Hamza alionekana kuchanganya damu  ya kizungu lakini bado ilikuwa ni ngumu kuamini, isitoshe swala la  kuchanganya damu halikuwa la kushangaza sana ,  Waafrika wengi walikuwa  wanaanza kupoteza rangi yao halisi kutokana na kuzaa na  watu weupe, hivyo kumuona mtu mwenye muonekano wa Hamza sio swaa la kushangaza.

Leo hii unaweza kukuta watoto wa mtaani wenye  muonekano wa  kizungu na kiafrika au  waarabu na  waafrika.

“Sidhani ni sahihi kusema hivyo , maana ninazo nguo nyingine nyingi tu ambazo ametengeneza Alec?”

“Nani anajua , pengine uliiba furushi la nguo , kama  una urafiki na mtu mkubwa kama huyo inakuwaje leo hii upo hapa Tanzanina , tena  Dereva , si ulitakiwa uwe Ulaya huko?”Aliuliza  Salma , hakutaka kukubali kabisa.

“Kwahio  vipi  msaidizi wangu kuwa dereva , kwahio siku hizi tunabaguana  kwasababu ya mavazi?”Aliongea Regina , hakutaka kuona  Salma anapandisha mdomo mbele  ya Hamza.

“Regina  haijalishi unachoongea , tena nimezidi kuwa na mashaka , kuna namna  mmepanga bada ya kuhisi hamuwezi kushidana na kampuni yetu , hivyo mnacheza kamchezo  ka kumfanya  Fellini kukubaliana na nyie”

“Unaumiza kichwa chako bure kwa kufikiria sana , kama nilivyosema , sina mpango wa  kushirikiana tena na Zara, tuondokeni”Aliongea Regina lakini muda ambao  Regina alianza kupiga hatua kuondoka hapo alizuiwa na Hamza.

“Hamza , unafanya nini?”

“Msaidizi wako nimeitwa mwizi , unadhani tunaweza kuondoka hivi hivi?”Aliongea. “Kwahio wewe sio mwizi?”Aliuliza Salma.

“Mr Hamza , je una ushahidi wowote wa kutuonyesha  hizi nguo ni za kwako  au unafahamiana na Master Goerge?”Aliuliza Fellini. “Sasa hivi ni saa saba kasoro  hivyo  itakuwa ni Asubuhi London , nadhani Mzee Roboti muda huu atakuwa macho , ninaweza kumpigia simu”Aliongea

“Nini , unasema una namba ya Master?, wakati hata mimi sina”Aliongea  Fellini kwa mshituko.

“Unaongea ujinga , kama  hakutengenezei  nguo , kwanini uwe na namba yake”Aliongea  na kumfanya Fellini kukakamaa mwili , alikuwa akijisikia  vibaya kana kwamba  ameona mende.

Regina  na Linda wote walikuwa na hali ya shauku  na matarajio kwa wakati mmoja , upande wa Salma alikuwa  na wasiwasi mno.

Hamza alitaka kutumia simu yake kupiga lakini alisahau  kwamba ni kimeo hivyo alimwangalia Regina.

“Mkurugenzi niazime simu yako , siwezi kupiga kimataifa  kupitia simu yangu”Aliongea na Regina alitoa Iphone yake na kumkabidhi  Hamza  na palepale aliingiza namba alizokariri  na kupiga na ndani ya dakika chache tu  simu ilipokelewa baada ya kuita.

“Who is it …”Sauti ya  kingereza ya kizee upande wa pili ilisikika , ilikuwa nzito mno na  lafudhi ya London na Hamza alitoa tabasamu mara baada ya  kutambua sauti hio ambayo  hajaisikia muda mrefu.

“Elmo , its me..”Aliongea Hamza  upande wa pili kulikuwa na kimya kama cha sekude arobaini hivi.

“Do you finally rembember this lowly person!?”Sauti upande wa pili  ilijibu na ndio dakika ileile  Hamza  aliweka simu aweze kusikia yeye tu ili wasije kusikia jina ambalo  Alec anaweza kumuita.

Hamza asingejua namna ya kujieleza kama  wangesikia  Alec anamwita  kwa cheo chake cha heshima.

“Mzee Roboti sio kama nimekusahau , mpaka sasa  kila nilipokuwa ikivaa mavazi ulionipa kama zawadi  nakukumbuka ,  ni miaka mingi lakini nguo zako  bado   nazivaa”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu.

“Niheshima kwangu kufanya kazi na wewe na nilikuwa nikitegemea tuendelee kufanya kazi pamoja  ila umepotea , nakumbuka wakati nakutengenezea hizo nguo ilikuwa ni miaka mitatu iliopita”Aliongea mzee huyo  akionekana kama vile analalamika.

“Okey , Okey mzee nilikupa likizo kwanza ili ujali afya yako , lakini kwasababu unaonekana kuwa tayari kunitengenezea tena nguo basi  nakupa ruhusa , nitakutumia  anuani ya ninapoishi kwasasa , nadhani unajua  ninachopendelea”

“Kweli !,  nipo  tayari kufahamu sehemu unayoishi kwasasa , najua umeondoka bila kuaga   hivyo  itakuwa siri yetu kama tunawasiliana”

“Mzee japo umezeeka lakini akili yako inafanya kazi  vizuri , ninakuamini ndio maana nimeamua kukupigia”Aliongea Hamza huku akicheka, alikuwa akiongea kingereza na lafudhi yake ni kama vile amekulia jijini London.

“Mimi kama kijakazi wako   lazima niwe na akili japo kidogo , vinginevyo  nitaweza vipi kutimiza wajibu wangu wa kukuhudumia?”Aliongea.

“Sawa sawa , tuachane na hayo kwanza , nimekupigia  leo  kwasababu kuna baadhi ya mambo nataka unisaidie kuyaweka sawa”Aliongea Hamza.

“Usisite kabisa kuniambia , nipo tayari  kufanya chochote , hata  kama nikuhatarisha maisha yangu”

“Sio swala kubwa sana , usiwe na wasiwasi ,  je kuna mwanaume anaefahaika kwa jina la Fellini  kati ya wanafunzi wako ?"Aliuliza Hamza na wakati huo alikuwa akimwangalia Fellini.

Muda huo Fellini uso wake wa kizungu ulikuwa umepauka na kulikuwa na viashiria vya jasho katika paji la uso wake , alikuwa  akijiuliza kama  kweli

Hamza aliekuwa akiongea nae ni  Master Alec , Hamza mwenyewe atakuwa  ni nani 

Salma  na yeye alikuwa  aking’ata lipsi zake huku  akiwa amekunja ngumi , alionekana kuwa na wasiwasi mno.

“Mkurugenzi ni kweli  anafahamiana na huyo mtu  mzito , mbona  naona kama  anatufanyia magizo?”Aliuliza Linda.

Upande wa Regina yeye alikuwa  katika  kuwaza   na aliishia kutingisha kichwa ,huku akishindwa kuongea neno, alijiambia atajua baada ya matokeo.

Lakini muda huo mapigo ya moyo wake yalikuwa yakienda kasi  mno , alijiambia kama ni kweli basi koneksheni ya Hamza  ni kubwa mno  kama vile yupo ndotoni.

“Felini!?, Oh nimemkumbuka  sasa , Fellini ni mwanafunzi aliekuja akiwa mdogo  katika duka langu kwa ajili ya kujifunza kushona, lakini hakuweza kudumu sana  maana moyo wake ulikuwa haujatulia sehemu moja , ijapokuwa alikuwa na kipaji lakini hakuwa  na  Ari ya kuja kuwa mshonaji  mkubwa hivyo aliondoka , kwanini unamuulizia , Mshonaji  kama Fellini ni  wa daraja la pili na  hana hadhi ya kuandaa  nguo zako”Aliongea.

“Hamna mzee, sijakutana nae kwa ajili ya kunitegneenea nguo , nimekutana nae kwa bahati mbaya na ameweza kugundua maazi yangu wewe ndio umeyatengeneza, ila haamini  amesema mimi mwizi”

“Nini!!, anakitafuta kifo , tafadhari bwana  wangu naomba  usiwe  na  hasira juu ya tabia ya Fellini , nitamwambia Eric amfukuze , mtu kama  yeye hawezi kutuingiza kwenye mgogoro na wewe , kama  bado  hutoridhika unaweza kumfanya  chochote nitaandaa maelezo”Aliongea na kumfanya Hamza kutamani kucheka kutokana na namna Alec alivyopaniki.

“Ndio maana nakuita Mzee Roboti unaishi kikanuni sana , haina haja ya kupaniki , sina mpango wa kumfanya chochote , nitampatia simu uongee nae , ninachotaka ni  wewe kumthibitishia  tunafahamiana , usiongee zaidi kuhusu mimi , nadhani umenielewa”Upande wa pili kimya  kilitawala.

“Sawa sawa , najua nini chakufanya”Alijibu na  Hamza alimpatia  Fellini simu.

Upande wa Fellini mikono ilikuwa ikimtetemeka , ilimchukua  sekunde kadhaa mpaka kupokea simu hio kutoka kwenye mikono ya  Hamza.

Hakuwahi kuongea na mwalimu wake huyo kwa zaidi ya  muongo mmoja,sasa wazo la kuona kwamba  anakwenda kuongea na mwalimu wake huyo mtu mzito  sana ndio maana alikuwa na hofu.

“Nice  to talk to you , Master Alec”Aliongea  Fellini kwa kitetemeshi  lakini upande wa pili hakukuwa na jibu.

“I heard from Eric  that you’re now quite famous  outside ?”Sauti upande wa pili iliongea na palepale  Fellini ni kama  vigoti vinamlainika 

“Hapana Master ,Mimi ni kivuli cha Sir Eric tu , nimekosea Master naomba radhi”Aliongea na upande wa pili ilionyesha ni kiasi gani Alec alikuwa amekasirika.

Muonekano aliokuwa nao  Fellini ulimfanya  Salma  ambae alikuwa pembeni kushangaa mo , Mbobezi  maarufu wa  ulimwengu wa fasheni  amebadilika 

na kuwa kama piritoni hivyo kwa kuongea  na mtu kwenye simu

Regina na Linda  na wao walikuwa sasa washaamini mtu ambae anaongea na Fellini ni kweli ni huyo  Alec  mweye hadhi ya juu.

“Sikiliza  wewe mtoto , mtu uliekutaa nae  huwezi kumwita mwizi , ukimfaya akasirike basi hutonilaumu  tukikutoa kwenye circle yetu na umaarufu wako kupotea , nadhani unajua ninachomaanisha”

Fellini alikuwa na hofu mno , alikuwa akijua maneno ya Alec sio ya kumuogopesha tu , ukweli ni kwamba kauli yake moja tu hawezi kuwa na umaarufu aliokuwa nao , alijua nguvu  iliokuwa nyuma katika fasheni ya mavazi  ilitawaliwa na watu kama  Alec.

“Master usiwe na wasiwasi , najua nini napaswa kufanya”Aliongea.

“Mrudishie simu”

Fellini alimwangalia  Hamza kama vile ni kiongozi wa heshima na jambo hilo liliwashangaza zaidi  Regina , Linda na  msaidizi wa Alec, upande wa Salma  muonekano wake ulikuwa mbaya mno ,

maana  kile kinachoendelea ni kama matusi kwake

.

Hamza aliongea na Alec kwa dakika kama mbili hivi na kisha alikata simu na kumrudishia Regina.

“Sasa  nadhani kila mtu amethibitisha nguo hizi ni zangu , Mkurugenzi , tunaweza kuondoka sasa”Aliongea Hamza.

Regina  alijihisi ni kama yupo ndotoni  na aliishia kutingisha kichwa huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi.

Upande wa Fellini  aliona haiwezi kuwa nzuri  kama atamuacha Hamza aondoke akiwa na kinyongo.

“Mr Hamza nakiri  ilikuwa ni ujinga  wangu , hivyo naomba msamaha wako , kama ningejua na wewe ni mmoja ya watu wa kampuni ya Dosam  nisingesita  kufanya nao ushirikiano, naomba unipe nafasi  ya kurekebisha makosa , nipo tayari kampuni  ya Zara kushirikiana  na Dosam Group” “Mr Fellini huwezi kufanya hivi , tushakubaliana kampiuni zetu zinaenda kushirikiana”Aliongea Salma kwa hasira.

“Miss Salma, hakuna mkataba wowote tuliosaini kati yetu , hivyo siwezi kusema  kuna makubaliano ya kufanya kazi pamoja , baada  ya kufikiria kwa kina nimeona kampuni ya  Dosam inaweza kukuza hadhi yetu”

“Kwanini unaenda kinyume na maneno yako?” Aliongea Salma huku akiona swala hilo ni kama udhalilishaji, lakini Fellini alimpotezea kabisa.

“Kama nilivyokwisha kujitambulisha, mimi ni msaidizi tu , unapaswa kuongea na Mkurugenzi akikubali sina neno”Aliongea Hamza.

“Miss Regina naomba mazungumzo yetu yaanze upya , naomba kuona mipango yenu”Aliongea  mara baada ya kupata ruhusa.

Upande wa Regina alikuwa asharudi katika hali ya kawaida akiuzima mshangao wake na alimwangalia

Salma kwa macho ya uchokozi na palepale alichukua mkataba ambao ulikuwa umeshikiliwa na Linda na kuuchana mbele yake.

“Cooperation is fine , but we need to redesign  the cooperation proposal”Aliongea  akimaanisha ushirikiano hakuna shida lakini wataenda kuandaa upya vipengele.

Fellini aliishia kuangalia chini , kwa wakati huo  Regina alikuwa na Upperhand , hivyo  ni kama yeye ndio anaomba ushirikiano na kampuni ya Dosam  na sio Regina kumuomba  yeye ushirikiano., Regina  alishaliona hilo hivyo alitaka kubadilisha vipengele ili kuinufaisha kampuni yake.

“Hakuna shida, nipo tayari kusubiri  kwa siku kadhaa”Aliongea Fellini , hakuwa yule mwenye ratiba iliobanana tena.

Hamza alimwangalia Regina kwa macho ya kuridhika , alimuona Regina kama mwanamke ambae akili yake inafanya kazi kuendana na hali kwa haraka , hali ya mazungumzo ya kibiashara imebadilika hivyo hakutaka kwenda na mkataba  uleule.alitaka kubadilisha mbinu ili kujinufaisha.kitaalamu alimuona Regina kama mwanamke ambae   sio mzembe kabisa likija swala la fursa.

Kwa vyovyote vile Kampuni ya Zara  lazima ishirikiane na  Dosam  kama  Fellini anataka kulinda hadhi yake katika ulimwengu wa fasheni.

Fellinni aliwasindikiza kabisa  Hamza na  Regina mpaka  kwenye gari yao na kuwafungulia mlango  huku akiwa na heshima  kubwa .

Upande wa Salma alimwangalia  Hamza kwa macho yenye ukali mno  na kisha aliondoka bila hata ya kuaga.

“Mr Fellini huna haja ya  kuwa hivi , ijapokuwa leo sijafurahishwa na namna tulivyoanza  lakini  nimeridhika na  matokeo”Aliongea Regina.

“Ili Mradi  Mkurugenzi  umeridhika , hakuna tatizo kabisa , natarajia  kufanya kazi na  Dosam kwa miaka mingi”

“Kama hakuna lingine  tunaondoka”Aliongea Hamza.

“Mr Hamza  tafadhari subiri kidogo , najua nimekukosea leo , naomba  uniwie radhi , kama kuna mahali ambapo  hujaridhika  tafadhari naomba uniambie nitarekebisha”

“Usiwe na wasiwasi , ili mradi kila kitu kitaenda sawa mimi sina shida , nitakusaidia pia  kukupigia chepuo  kwa Alec “

“Thank you so much, you are so magnanimous”Aliongea na muda huo  Hamza alikumbuka  aliachaga nguo kwenye hilo gari.

“Mkurugenzi , hivi zile nguo zangu bado zipo humu?”

Regina muonekano wake ulikuwa  na hali ya kukosa utulivu  na alinyoosha mkono nyuma na kutoa ule  mfuko , mwanzoni alitumia nguo hizo kumdharau Hamza lakini  dakika chache zilizopita zimegeuka kuwa hazina.

Hamza alichomoa shati kutoka kwenye  mfuko huo na alivyolinusa lilinuka jasho kali mpaka akakunja sura, lakini  katika macho ya Fellini alionekana  kuwa katika  mchangao.

“Unaweza kuchukua hizi nguo , chukulia kama zawadi kutoka kwangu  kwa kuingia makubaliano ya kibiashara”Aliongea Hamza na kumkabidhi mfuko wote  Fellini aliepokea kwa mikono miwili.

Hamza hakuwa na wasiwasi na nguo tena , alishaahidiana na  Alec angeletewa nguo nyingine mpya 

Mtu yoyote angeona shati ambalo Hamza amemkabidhi Mzungu Fellini  wangesema  huyo mzungu ni kichaa.

“Mr Hamza asante sana kwa ukarimu wako, nitaweka nguo hizi sehemu salama kabisa nikirudi” Aliongea Fellini, alipanga kuzifanya nguo hizo  kama sehemu ya maonyesho  ofisini kwake , ili kutukuza uwezo wa Master Alec katika swala zima  la ushonaji.

Isitoshe Master Alec alikuwa ametengeneza kwenye maisha yake nguo nyingi sana lakini sio watu wengi ambao washawahi kuona nguo yenye muonekano wa kawaida kama hio lakini ya thamani , Rare things are priceless.Aliwaza Alec.

Kwa furaha mazungumzo yao yaliisha hivyo na Hamza aliendesha gari kurudi nyumbani.

Linda ambae alifika na  gari yake  aliweza kuangalia gari ya Regina ikitokomea  huku akiwa na muonekano usioelezeka , katika macho yake kulikuwa na hali flani hivi ya  kukata tamaa.

******

Upande mwingine ndani ya jiji la  London  ilikuwa ni asubuhi  karibia maeneo  yote , Uingereza haikuwa kama nchi ya Marekani ambayo ina Time Zone  zaidi  ya nne, pengine ni kutokana na udogo wa kijiografia wa nchi hii  yenye maendeleo makubwa sana   katika nyanja zote.

Katika mtaa wa Savile Row mwanaume mzungu mzee hivi mwenye nywele nyeupe  pamoja na miwani  alionekana akishuka katika ngazi katika moja ya jengo kwa kukimbia, alikuwa amevalia  shati jeupe na Vest nyeusi.

“Erice, John”Mwanaume yule aliita kwa nguvu.

Dakika hio hio mwanaume bonge mzungu alijitokeza  akiwa ameambatana na mwanaume mwingine kimbau mbau ,wote walionekana katika

umri wa iaka hamsini hivi na  walikuwa wameshikilia vitambaa.

“Mwalimu , una maagizo yoyote”Yule bonge ndio aliitwa  Erice  na ndio alieuliza.

“Wote nyie acheni kazi zenu zote kwa sasa na mnifuate , nahitaji kutengeneza nguo nyingi  suti na suruali”

“Mwalimu ,  bado hatujamaliza kutengeneza nguo za Mfalme wa Hispania na  Prince  wa Wales, sidhani kama tunaweza kukusaidia”Aliongea John.

“King or Prince let them all wait, For the past week, we have served one lord” Aliongea akimaanisha Mfalme au mwana mfalme wote wasubiri. kwani kwa wiki za nyuma walikuwa wakihudumia bwana mmoja tu.

“Mwalimu unamzungumzia bwana gani?”Erice aliuliza.

“Seraph”Aliongea Alec huku akigusa gusa  kifua chake.

Erice na John mara baada ya kusikia jina hilo  moja kwa moja walielewa ni mtu gani anaelengwa  na wote kwa pamoja walikakamaa huku  wakitamka kwa juu “Divine Wrath”

Previoua Next