Reader Settings

Kwa zaidi ya dakika ishirini au therathini hivi  hakuna aliemuongelesha mwenzake , Regina  alidhania  Hamza angempa sababu japo kidogo tu ya  kutuliza  shauku  yake , alitamani kusikia  hata kisingizio  tu pengine angeelewa  lakini licha ya hivyo Hamza alikuwa akiendesha huku akipiga  ukimya.

“Huna kitu chochote cha kuniambia?”Aliuliza  Regina   baada ya kukosa uvumilivu  na kumfanya  Hamza kuangalia  kioo cha nyuma.

“Ni kweli asubuhi nilikuwa na dharula  muhimu , ningechelewa  kidogo kungekuwa na tatizo , alikuwa ni  mteja wangu  alienipigia , sikutaka kumpotezea”Aliongea Hamza lakini Regina hakuwa hata na  haja ya kusikiliza hizo porojo.

“Sitaki kusikia   kuhusu hilo , kwanini hukuniambia unafahamiana na huyo Master Alec?”

“Ah.. Unamzungumzia mzee Roboti , kwanini nimzungumzie sasa bila sababu?”

“Wakati ule nilikuambia ukatupe mavazi yako  lakini ukang’anania kubaki nayo , kwahio ulikuwa ukinikejeli kisirisiri kwa kuwa mshamba sio , unaonekana kabisa umeisubiria kwa hamu hii siku kwa ajili ya kuniumbua mbele za watu, sasa hiivi nadhani unajichekea mwenyewe  moyoni  kwa raha zako”Aliongea huku akionyesha kinyongo.

“Regina unaongea nini , sikufikiria sana wakati ule ni kwamba tu  nimezoea haya mavazi ndio maana,  ni zawadi kutoka kwa mzee , isingekuwa vizuri kuyatupa ilihali aliweka moyo wake wote kwenye kuyatengeneza”

“Basi niambie wewe na huyo Master Alec mnafahamina vipi?”

“Nilikutana nae Shardland Bar huko Uingereza  kipindi flani hivi  cha mwaka mpya na ndio tulianza kuongea kwa kubishana na urafiki wetu ukaanzia hapo”

“Unaniona mjinga , unadhani naweza kuamini huo uongo , mbona unapenda kuniona kama kichekesho?”

“Ananiona mjinga huyu sijui yukoje  ,  yaani mtu amemtisha  Fellini vile  lakini sasa hivi anasema  amekutana nae bar “Aliwaza Regina huku akiwa na hasira kali.

Muda uleule wakati washafika Kigamboni  Hamza alisimamisha gari pembeni  na kumshitua Regina aliekuwa kwenye mawazo.

“Wewe .. unafanya nini?”Aliuliza lakini  Hamza hakujibu zaidi ya kufungua mlango na kutoka nje na kutembea upande wa madukani, Regina na yeye hakutaka kukaa  ndani ya gari , alishuka na kumfuata huko huko na kufanya watu kumkodolea macho kutokana na urembo wake.

Baada ya kumfikia Hamza alimuona akiwa amesimama mbele ya Freezer akichagua Ice Cream za Bakhresa na alichukua yenye  Strawberry na kumpa Regina ambae aliipokea bila kupenda.

“Unafanya  nini sasa?”

“Mrembo  maswali mengi  ya nini , huoni hio ni Ice Cream”Aliongea na muda huo  Hamza alichukua na ya kwake ya ukwaju  na kisha akaenda kulipa  na sasa hapo ndio  Regina alijua kumbe huyu mwehu kaja kununua Ice Cream.

“Acha kusimama hapo twende , tumeegesha gari sehemu mbaya , hata kama una hela huwezi vunja sheria za barabarani”Aliongea Hamza na  kumshitua  Regina ambae alikuwa  kwenye mshangao.

“Nani kakuambia nina shida ya Ice Cream , jali mambo yako”

“Kama hutaki ilete basi ninao uwezo wa kula zote mbili kwa  pamoja”Aliongea  Hamza akijaribu kumpokonya lakini  Regina alipindisha mkono mbali.

“Unasema huitaki , nataka kuichukua unaktaa , nyie wanawake ni viumbe wa ajabu sana”

“Unasemaje wewe…”Aliuliza Regina lakini Hamza

alijifanyisha mjinga  na kumuacha Regina akiwa amesimama

Wateja baadhi na watu  wauza maduka waliishia kutabasamu , kwani walionekana kama wapenzi.

Hamza mara baada ya kuingia garini  aliliwasha na kupiga honi na kumfanya Regina kwa hasira kukimbilia na kuingia.

Baada ya wote kuingia kwenye gari na Hamza kulirudisha  kwenye barabara aliendesha kwa mkono  mmoja huku mwingine ukishikilia Ice Cream , Regina hakuuliza tena swali , aliona hata akiuliza kusingekuwa na majibu hivyo alijikaliza zake kimya , huku akila Ice Cream kwa kutumia kijiko

Kama alivyosema Hamza wanawake hawaeleweki , Kwa Regina ilikuwa hivyo hivyo kulikuwa na wanaume kibao ambao washawahi kumtongoza kwa kumpatia zawadi kama vile magari , vito vya thamani na ahadi kibao , lakini  kitendo cha  Kununuliwa Ice Cream ndio zawadi ya thamani ya juu iligusa moyo wake.

Wakati wanafika  nyumbani Shangazi alikuwa sebuleni akiangalia TV, na hata walivyoingia  hakuweza kuwaona.

“Shangazi unaangalia nini , mpaka kuwa siriasi hivyo?”Aliuliza  Regina.

“Taarifa ya  habari , wanasema  kumekuwa na  mauaji mfululizo ya wanawake ndani ya jiji la Dar es saalam  na muuaji hafahamiki hivyo  wanaasa raia kuwa makini, Regina uwe makini , ukitoka kazini  hakikisha uwe na Hamza pembeni yako , wakati wa mchana usitoke peke yako pia”

Hamza aliangalia  taarifa hio ya  habari na alishangaa  na kuona namna muuaji alichokuwa akifanya , tofauti na kuua  tu alikuwa pia akikata maeneo  nyeti ya wanawake kama vile manyonyo na ngozi, yalikuwa mauaji ya kikatili mno.

“Muuaji wa namna hii muda  si mrefu atakamatwa , shangazi huna haja ya kuwa na wasiwasi sana”

“Natamani wakimuona wampige risasi wamuue kabisa , jamani mtu anaua watu wasio na hatia kikatili namna hio  , tena wasichana wadogo”Aliongea Shangazi na muda huo huo  kengele  iligonga  ikionyesha kuna  mgeni.

Shangazi alienda kufungua  mlango wa geti na alishangaa baada ya kuona ni Polisi.

“Ndugu polisi  kwanini…”

Walikuwa ni  Polisi wanne  wote wakiwa katika  sare zao  za kipolisi , aliekuwa mbele  alikuwa na uso ulichongoka na  mweusi Tii.

“Mama  hapa ni nyumbani kwa  Regina Wilson?”

“Ndio , upo sahihi , mnamtafuta?”

“Naitwa Afande Mlonga kutoka  kituo cha polisi  mjini kati idara ya uchunguzi , kuna kesi inayomhusu  Regina Wilsoni na tupo hapa kwa  uchunguzi”

Muda uleule  Regina  alikuwa ashatoka nje baada ya kuona  Shangazi  harudi na  mara baada ya kuona ni polisi  alimwambia shangazi awaruhusu.

Polisi wale walikaribishwa mpaka ndani  sebuleni huku  wakiangaza angaza kulia na kushoto kwa namna ya kuchunguza uzuri wa jumba hilo  kabla ya kukaa kwenye sofa.

Shangazi kwa haraka hraka alikimbilia friji na kuwaletea  maji  kama walivyoomba  , lakini alikuwa na wasiwasi mno kiasi cha mikono yake kutetemeka.

Afande Mlonga macho yake yalikuwa kwa Hamza tu , ni kama alikuwa akimchhunguza , upande wa  Hamza alikuwa zake bize akitafuna ma’apple’.

“Miss Regina naomba kuuliza  huyu Mr hapo  ni nani kwako?”Aliongea Mlonga na swali lile lilimfanya Regina kusita lakini kutokana na uwepo wa Shangazi aliamua kuongea.

“Ni mpenzi wangu”

Baada ya kujibu hivyo  Afande Mlonga na wenzake ni kama hawajatarajia jambo hilo.

“Tulisikia habari  nyingi  unaenda kuolewa na mtoto wa Mzee Benjamini , hatukutarajia  kuona tayari  una Boyfriend”

“Naona  taarifa  zangu zinazagaa sana  lakini hili linanihusu mimi na yeye , sikuona haja ya kuliweka wazi, sidhani kama ni kosa?”

“Hakuna mgongano  wowote baada ya hili na familia ya Mzee Benjamini?”Aliuliza Mlonga huku wakionyesha kunakiri majibu.

“Nyie wote ni polisi , sidhani ni vizuri kuuliza maisha yangu binafsi”

“Usituelewe vibaya Madam , ni kwasababu kilichotuleta hapa kina uhusiano na maisha yako binafsi”Aliongea na muda uleule  Afande Mlonga aliweka picha chini , zilikuwa ni za gari ya Regina.

“Hili gari  limesajiliwa kwa  majina ya Regina

Wilsoni ambapo tunaamini wewe ndio mmiliki  halali , juzi  limeonekana katika  kijini cha Wavuvi Zinga bagamoyo  na Dereva aliekuwa akiendesha gari  hio ni moja ya mhangwa wa mauaji.. wakati wa kurudi gari ilikuwa ikiendeshwa na huyu mwanaume ambae umesema  ni Boyfriend wako”Aliongea  huku akiweka picha ya Hamza akiendesha gari  hio hio na gari ikiendeshwa  na mwanamke, alikuwa ni Corresa.

Regina  mikono yake ilicheza na bila hata kujijua alihikilia sketi yake , akiwa na wasiwasi, mwanamke aliekuwa kwenye picha  alimfahamu ni moja ya watekaji.

“Kwahio amekufa?”

“Kwanini unauliza , inamaana hujui kama amekufa,  tunaamini watu wote waliokufa walikuwa ndani ya gari lako”

Regina  aliishia kugeuza kichwa chake na kumwangalia  Hamza  lakini  upande wa Hamza hakuonyesha wasiwasi kabisa , lakini kwake aliona  hio kesi sio nyepesi, baada ya kufikiria kwa muda Regina aliona aeleze moja kwa moja kilichotokea.

“Nilitekwa siku hio , lakini sikujua watu wale walikuwa ni wakina nani  maana walikuwa ni  raia wa kigeni , nilikuwa sina fahamu na  pale niliposhituka  nilikuwa nishaokolewa tayari na Hamza , kuhusu  watu hao kufa sikuwa  nikijua chochote”

“Kwahio unamaanisha huyu Mr Hamza ndio aliekuokoa na baada ya hapo akawaua hawa wahalifu?”

“Ma afande mnakosea , sijaua mtu , mimi nilienda nikawapa kichapo  tu , sidhani kama mnaweza kunilaumu kwa hilo”Aliongea Hamza lakini Regina aliona  hali inazidi kuwa  mbaya na alitaka kutumia nguvu yake hivyo alisimama.

“Afisa  mna ushahidi wowote wa kuonyesha Hamza ndio aliewaua?”

“Usipaniki Madam ,  hata kama  Mr Hamza ndio aliehusika  sio  kosa , kwasababu  hawa wahalifu ni kama Mr  Hamza tu , lakini tunahitaji kuchunguza hili swala, tunataka kujua  imekuwaje Mr Hamza akawa na uwezo wa kuua hawa wahalifu wa daraja la juu , wanaosakwa dunia nzima”

“Mimi ni mwanafunzi wa chuo  na fundi , nina nguvu nyingi  hivyo mapigano yalikuwa makali sana , lakini sijua mtu”Aliongea Hamza.

“Mr Hamza tunakuahidi hatutokutia hatiani kwa kuuwa hawa watu , tunachotaka kujua ni kilichotokea katika mazingira ya kirafiki tu”AliongeaMlonga huku  akiwa na tabasamu bandia.

“Kama   mnao ushahidi wa kutthibitisha niliwaua basi nitawaelezea kilichotokea , lakini ushahidi hamna na mpo hapa mnanijaribu siwezi kuwaambia chochote”

Polisi hao walijikuta wakiwa  kimya , alichoongea Hamza kilikuwa na ukweli ,hata hivyo kesi haikuwa chini yao , baada ya kesi hio kutolewa ktuoka kitengo cha MALIBU na kuhamishiwa idara  ya polisi Afande  Mlonga ndio alipewa kazi ya kuongoza uchunguzi , lakini licha ya kupata picha hakukuwa na alama za vidole zinazomlenga moja kwa moja Hamza ndio alifanya  mauaji.

“Afande Mlonga  kama hakuna ushahidi siwezi kukubali  mpenzi wangu  kusingiziwa , kama kuna ambacho nitaweza kufanya kwasasa ni kumshirikisha mwanasheria wangu  ili muongee nae yeye , hivyo naomba muondoke  nyumbani kwangu na mkatafute Warantt  kwanza”

“Madam , mpaka sasa nadhani umeona taarifa ya habari inayohusisha muuaji anaeua wasichana wadogo  kwa kuwakata viungo vya siri , unadhani 

ni salama kwako kukaa na mtu ambae humjui vizuri”

“Chunga maneno yako afande , chochote utakachoongea  bila ushahidi nitakushtaki nacho”Polisi wengine walitaka kuongea  lakini Afande Mlonga aliwazuia.

“Kama ni hivyo basi hatuna haja ya kukaa zaidi na tutaondoka , ila kama kuna  ushahidi tutarudi”Aliongea  na kisha wote kwa  pamoja walitoka nje.

“Regina nini hiki kinaendelea , ulitekwa?”Shangazi  ndio aliekuwa akiuliza huku akionekana kuwa na maumivu  ya moyo.

“Shangazi sikufanya makusuti kutokukuambia , sikutaka kukufanya kuwa na wasiwasi , lakini  lishaisha”Aliongea na Shangazi aliishia kuvuta pumzi huku akijikalia kwenye sofa.

“Asante Mungu  angalau amekukutanisha na Hamza  angalau anaweza kukulinda, ningefanya nini mimi kama ningekuwa peke yangu”Aliongea  Shangazi akijituliza lakini wakati huo Regina alimwangalia Hamza kwa macho ya  kuchukia.

“Sijui  kama umeua au hujaua , lakini hili swala linapaswa kuisha ukiwa hujaua”Aliongea. “Haha.. Regina asante sana kwa kunijali”

“Eti kukujali , sitaki  kuhusika katika hili ndio maana , nina kazi nyingi za kufanya”Mara baada ya kuongea hivyo kwa hasira alipandisha juu  huku akifunga mlango kwa nguvu.

Upande wa Shangazi alimwangalia  Hamza  kwa macho yenye umakini mkali , ni kama kuna kitu anakitafuta.

“Hamza hukupata tatizo?”Aliuliza.

“Shangazi usiwe na wasiwasi  ni swala dogo na lishaisha”Aliongea na Shangazi alitingisha kichwa kuelewa.

“Naona unatafuna sana matunda , kama  hamjala mchana niwaandalie chochote”

“Hakuna shida shangazi”

*****

Upande mwignine  mara baada ya mafande wale kutoka walisogelea gari  ya Land Cruiser na kuingia ndani , kulikuwa na watu wawili ndani ya gari hio tayari , mmoja akiwa dereva na mwingine akiwa ni mwanaume mnene hivi mwenye kitambi aliekaaa nyuma.

“Kanali , tumemaliza  mahojiano nae , lakini mambo yamekuwa magumu kuliko tulivyotarajia”Aliongea Mlonga  akimwambia yule mzee aliekuwa kwenye gari.

“Nini kimetokea?”

“Amekataa yeye kutohusika  kabisa , cha kushangaza sio dereva wala mlinzi tu  ni Mpenzi wa bosi  Regina”

“Nini , mpenzi!!, Sio James tena”

“Hata sisi tumeshangaa , inaonekana kuna kinachoendelea , lakini sidhani kama kinahusiana na hii kesi”Aliongea Mlonga na kumfanya  mwanaume alieitwa Kanali  kufikiria kidogo.

“Mlonga nakuamini uwezo wako   wa kumjua mtu kwa kumwangalia tu , wewe unamuonaje , unadhani ndio aliehusika kuua watu hatari kama wale?”

“Dastani sijui hata namna ya kumuelezea , ukiachana na ushombeshombe  wake  nimemuona kama mtu wa kawaida sana… lakini  kuna kitu sio cha kawaida  nimekiona”Aliongea.

“Kitu gani mmekiona?”

“Hakupaniki kabisa , ni  kama vile alitarajia ujio wetu  na wala hakuonyesha kukasirika hata tulivyomwambia  ameuwa watu wale , ki ufupi hakuonyesha kuwa na wasiwasi  wakati tunamuuliza maswali, lakini ukiachana na hilo sioni kama  ni mtaalamu , anaonekana kama vile ni mfanyakazi  wa kawaida tu wa kwenda kazini na kurudi nyumbanni  kuangalia TV”Aliongea na  Kanali Dastani alionekana kuwaza.

“Kanali  hii kazi haiwezi kuwa rahisi kama ikiendelea kuwa chini ya Idara ya polisi , Kitengo cha MALIBU  kina kila rasilimali  ya kufanikisha  hili”Aliongea Mlonga.

“Unadhani  hatujui kuhusu hilo , unadhani kwanini sikutaka kuambatana na nyie moja kwa moja kwenda kufanya mahojiano nae , hizi ni taratibu  za kitengo pia  katika hatua za ki uchunguzi”

“Mkuu unamaanisha  na nyie mnaendelea na uchunguzi kimya kimya?”

“Mlonga licha ya kwamba upo vizuri kwenye  mahojiano  lakini  kuna baadhi ya sehemu haupo  vizuri , Ni  lini  ushawahi kuona MALIBU wakimhoji raia moja kwa moja , tunatumia idara ya  polisi kufanya kazi hii , hivyo  mlichofanya ni kutimiza wajibu  wenu  na sisi tutatimiza wajibu  wetu”Aliongea na  Mlonga alitingisha kichwa kukubali 

“Ila Kanali kama kweli ndio amehusika na mauaji  ya maninja kutoka  Ufilipino  basi  ni mtaaamu wa hali ya juu  na atakuwa ameficha ushahidi wa sisi kumfikia , hivyo uchunguzi chini ya idara yetu utakuwa mgumu kweli”

“Kama unahisi hivyo , basi  atakuwa haogopi  hata tukiwa na ushahidi  kuna kinachoniambia sio  wa kawaida”Aliongea moja ya polisi akitoa mchango wake.

“Kama ulivyosema ni sahihi  , unadhani kwanini hakukuwa na alama yoyote  hata ya vidole tu kuonyesha yeye ndio muuaji , alionekana kuwa makini , hata kama  ameonekana kwenye gari ashajiandaa namna ya kujitetea”

“Kanali kwanini  tusimkamate moja kwa moja , kuna uwezekano akawa  na uhusiano  na mauaji ya  wanawake yanayoendelea”

“Hatuwezi  kwenda moja kwa moja kwenye hitimisho  , iwe yeye ndio muuaji au sie kama polisi mnapaswa kuendeleza uchunguzi wetu na kuwe na ushahidi , muuaji  lazima akamatwe na haya ni maagizo  kutoka  juu , mkitimiza wajibu wenu na sisi wa kwetu kazi itakuwa rahisi , Mlonga hili lipo juu  yako na timu yako, Ondoa gari napaswa kwenda kuripoti makao makuu”Aliongea Kanali na gari iliendeshwa muda uleule.

Nusu saa tu  Kanali  Dastani alikuwa akiingia katika kitengo cha MALIBU makao makuu , na alipiga hatua zake  kana kwamba hataki kufanya watu wajue  amefika. 

Hakuelekea moja kwa moja  katika ofisi ya mkuu wake bali alienda moja kwa moja  katika ofisi yake , alitaka kukusanya ripoti kamili kabla ya kuiwasilisha.

Siku kadhaa nyuma alipewa  kazi ya kuhakikisha  anajua ni  nani aliehusika katika kuuwa wale raia wa kigeni  na kazi hio alikuwa ameifanya kwa uadilifu mkubwa mpaka kumpatia majibu aliokuwa akitaka.

Mara baada ya kufika katika ofisi yake aliingiza nywira katika tarakishi yake  na  palepale ilionekana Vidio ambayo ilionekana ilikuwa ikicheza lakini  ikasitishwa kwa muda.

Kanali mara baada ya kukaa kwenye kiti aligusa batani na palepale Vidio ile ilianza kuonyesha Kapteni  Yonesi  akipigana na Master Konki na kudhibitiwa na ghafla tu  Hamza anaingilia na kumuadhibu Master Konk.

Aliichezesha kwa kuirudisha mbele na nyuma  kwa zaidi ya mara tano  na alionekana kufikiria kitu.

Baada ya kukaa kwa muda katika ofisi yake , ujumbe wa meseji uliingia kupitia watsapp na alipoona jina  lililomtumia ujumbe huo alifungua haraharaka na alikuta  kuna kiambatanisho cha nyaraka iliokuwa katika mfumo wa PDF.

Kwa haraka haraka aliihamishia kwenye tarakishi yake   na kisha akaigeuza nyaraka ile kwa kuiprint, kadri alivyokuwa akiisoma ndio jinsi uso wake ulivyojikunja.

“Hamza ndio muhusika , nina uhakika asilimia mia  moja , kabla ya ripoti ngoja nikutane na Yonesi kwa siri kwanza”Aliongea  na kisha palepale alizima  tarakishi yake  na kuchukua karatasi alioprinti  na kujiandaa kutoka lakini muda uleule simu yake iliiita na alipoangalia  jina  lilisomeka Dokta Bensoni.

“Bensoni’Aliongea  mara baada ya  kupokea.

“Amosi amerudiwa na fahamu nusu saa iliopita” sauti ilisikika  na kufanya moyo wa  Kanali Dastani kudunda.

“Nakuja sasa hivi  Dokta , mdunge kwanza sindano ya usingizi?” “Kuna tatizo Dastani”

“Tatizo gani?”

“Nimefanya kupigiwa simu baada ya kurudiwa na fahamu , lakini nafika hospitalini Amosi hayupo”Aliongea na Kanali Dastani palepale uso wake ulikunjamana. “Unamaanisha nini  Bensoni”

“Ametolewa hospitalini  na haieleweki amepelekwa wapi ,  ki ufupi  Amosi ametoweka”

“Fu**ck , unanitania Bensoni , Amosi anatoweka vipi ndani ya hospitali  ya jeshi”

Kanali Dastani hakuwa hata na muda wa kumfikiria tena Yonesi , aliona analo swala muhimu zaidi la kushughulika , hofu ilimvaa , kama  Amosi ametoweka  bila ya kupata maelekezo yake kuna hatihati familia yake inaweza ikawa mashakani , lazima  Amosi  atakuwa anafikiria  kulipa kisasi kwa kumsaliti.

****

 Hamza  hakuwa hata na wasiwasi juu ya polisi waliofika hapo ,  mawazo yake yalikuwa siku ya kesho  wapi anamtoa out mpenzi wake  Eliza, ki ufupi hata swala la  Frida hakulitilia maanani kabisa.

Sio kama hakuwa na uzoefu , ukweli ni kwamba pengine Eliza anaenda kuwa mwanamke wake wa kwanza kuwa nae katika mahusiano yenye  usiriasi.

Hamza  aliona   kabisa amekuwa mzembe , kitendo cha  mrembo Anitha wa chuo kumkataa ilithibitisha kabisa alikuwa mzembe na mvuto wake umeshuka , hivyo alitaka  kujua namna ya kumpagawisha  Eliza.

Baada ya kuwaza kwa muda alienda mpaka chumba cha kujisomea cha Regina na aligonga mlango na kuambiwa aingie na mara baada ya kuingia  Hamza alianza kuangalia  vitabu vilivyokuwa kwenye Shelf bila ya kuongea.

“Wewe unafanya nini?”Aliuliza  Regina , wakati huo aliwaza Hamza alifika kwa ajili ya kuelezea kwanini wale watekaji walikuwa wamekufa lakini anaanza kuchunguza vitabu vyake.

“Naangalia kama nitaona kitabu cha kunifaa hapa” “Naona umekumbuka kuwa ni mwanachuo , kitabu gani unataka?”

“Hehe.. kinachohusiana na mapenzi”Aliongea na kauli ile ilimshangaza Regina.

“Yaani  hakuna kitabu cha maana unachotafuta zaidi ya vitabu vya kipuuzi  namna hio?”Aliongea kwa hasira.

“Nataka kujifunza namna mapenzi

yanavyoendeshwa , jinsi  vitu vya kumfanyia mpenzi wako akolee bila  ya  kumhonga , kuna haja gani ya kukasirika  hivyo bosi?”

Mapenzi!, Regina  hakujizuia na kuwaza au Hamza anataka  wawe wapenzi  kweli , baada ya wazo hilo aliona aibu za kike na kugeuka.

“Sina hivyo vitabu , unaweza kuondoka”Aliongea akiwa siriasi.

“Kama huna ngoja nikatafute mtandaoni, nilijua pengine na wewe una shauku ya mapenzi  yalivyo”Aliongea Hamza na kisha alitoka nje.

Regina  mara baada ya Hamza kutoka alijikuta akivuta pumzi nyingi , mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda kasi mno  kana kwamba  amekutana na  Simba  mkali , alijikuta akishika uso wake na kuona umepatwa na  joto.

“Mjinga huyu , kuna haja  hata ya kusoma kwenye kitabu..”Aliwaza.

Baada ya kukaa akifikiria kwa muda  alishika tarakishi yake na alisita kwa muda lakini alijikuta akiingia mtandao wa Google na kuandika ,  How to fall in love.

*****

Asubuhi kama kawaida Hamza aliamka mapema na kucheza mdundiko  nje katika mpangilio maalumu , na baada ya  kunywa chai  alibadili katika mavazi mapya kabisa  alionunuliwa na Regina.

Wakati akishuka kutoka chini Regina alikuwa sebuleni akiangalia  taarifa ya  habari kupitia CNN. “Regina  nadhani leo hakuna kazi yoyote , si ndio?” “Ndio huna kazi ya kufanya leo , vipi unatoka?”Aliuliza na kumwangalia Hamza namna alivyopendeza.

“Ndio , nitatoka leo siku nzima ,  msinihesabu chakula cha   mchana wala usiku”

“Unaenda wapi , kwenye kazi zako za ufundi  kama kawaida , kama  ni kazi ninazo nyingi tu unaweza kunisaidia”Aliongea Regina huku maneno yake akiwa hana uhakika nayo , alijua  Hamza alikuwa na koneksheni kubwa hivyo hata hela lazima alikuwa nazo  sasa alijiuliza kwanini anasoma chuo , kwanini aliishi maisha ya kimasikini kama vile hana hela.

“Wewe usinipe kazi ,nimepndeza vyote hivi niende  kufanya kazi tena za nini, nina mtoko  na mtoto mzuri leo , hivyo bosi leo ni siku yangu usinipigie simu”

Regina mara baada ya kusikia kauli hio , alijikuta akinywea lakini  alibadilika  dakika hio hio.

“Haina haja ya kuripoti una mtoko na mtoto  mzuri”

“Haja ipo , tunaishi ndani ya nyumba moja  na mimi ni mfanyakazi wako , sitaki itokee dharula nikiwa nakula bata  uniambie nirudi nitamkera mpenzi wangu , lakini hata hivyo usiwaze sana , mpango wangu ndani ya  miezi mitatu ikiisha sitotaka kuchelewa  kuondoka hapa hata kwa sekunde, ila kwasasa nitahakikisha  jambo letu linaendelea kuwa siri “

“Sina haja ya kujua  kama una mpenzi hayo ni maisha yako ungeondoka zako tu bila kuniaga , kuna haja gani ya kuniambia”Aliongea Regina kihasira na kutupa Rimoti kwenye sofa na kupandisha zake juu.

Hamza aliishia kukuna kichwa chake na kujiambia kwani kosa lake  ni lipi hapo , yeye kaomba ruhusa kwa bosi ni kufuata  itifaki,  hakutaka itokee anakula maisha na  mrembo  Eliza mara  Regina anapiga  wakutane.

Previoua Next