Reader Settings

SEHEMU YA 33.

Hamza aliona  hakuwa na uhusiano wowote na  Regina  zaidi ya mkataba tu hivyo hana kosa , mara baada ya kuwaza hilo moyo wake ulijaa amani tele , na alizipiga hatua kutoka  ndani ya nyumba hio  kwenda nje.

Japo Regina ana magari mengi lakini hakutaka kutumia  gari , isitoshe anapoishi  Eliza ni wilaya hio hio  na Eliza ana gari.

Baada  ya kutoka  mji huo wa kisasa wa Egret  alichukua boda ambayo ilienda kumuacha  nje ya jengo la Apartment za Lotus na  aliruhusiwa kuingia  moja kwa moja.

Alipishana na warembo kadhaa lakini hakuwa na habari nao na moja kwa moja alienda kusimama nje ya  mlango wa Apartment ya Eliza na kisha alibonyeza  Kengere.

Ilichukua dakika kama  moja na nusu hivi  mpaka kufunguliwa  na Hamza alishangaa kumkuta mrembo huyo akiwa katika nguo za kulalia tena na Mask  usoni, alishangaa maana sio  kitu alichotarajia , alijua muda huo pengine  Eliza atakuwa ashajipodoa na kupendeza tayari.

Eliza baada ya kuona aliekuwa mlangoni ni  Hamza  na alikuwa ametoka kulala  alitimua nduki kurudi ndani  na kuingia moja kwa moja  bafuni.

“Eliza  mbona unakimbia?”

“Mbona umekuja mapema  hata kuniambia kwa simu ,, bado sijajiandaa”Sauti ya Eliza ilisikika kutoka bafuni.

Hamza alisogelea mlango wa bafuni na kisha alianza kuinama kutafuta upenyo wa kupiga chabo. “Haina shida ,  ni mzuri hata wakati wa kuamka”

“Naonekana kama zombie , hebu kakae  sebuleni usinichungulie”Aliongea   huku akifunga mlango wa bafuni vizuri na Hamza alirudi zake sebuleni kukaa.

Baada ya kufika hapo ndio  aliweza kuona nyaraka kibao zimesambaa kwenye meza na  wazo  la Eliza kufanya kazi usiku kucha licha ya kuwa wikiendi lilimvaa, pengine ndio maana amechelewa kuamka, Hamza hakuona ni jambo baya , pengine  Eliza alifanya hivyo kwa ajili ya kumaliza viporo  vyote ili kupata  amani wakati wa kutoka out  pamoja, alijikuta akitoa tabasamu.

Baada  ya  nusu  saa  Eliza  alitoka bafuni , ule mpauko wa uso ulimfanya avutie mno.

“Endelea kunisubiri  nivae nguo haraka haraka”Aliongea huku akikimbilia chumbani  na kufanya Hamza kuishia kumeza mate na uvumilivu ulimshinda na kumfuata huko huko , alitaka  kuona urembo wa Eliza wakati akibadili mavazi.

Lakini sasa ile anafika  mlangoni  ni kama Eliza alishitukia  Hamza angemchungulia na  alirudi  mlangoni  kwa ajili ya kuuloki  na hapo ndio alipoiona sura ya Hamza  ikiwa imekodoa macho. “Wewe muhuni , ukiendelea hivi tutaachana  ujue”Aliongea  huku akimkodolea macho  na  Hamza alisimama vizuri na kuweka nguo sawa.

“Umenielewa vibaya  nilikuwa  nataka kwenda chooni ,nimekosea mlango ..”Hamza alijibaraguza lakini  Eliza hakuwa hata na muda wa kumsikiliza kilichosikika ni mlango kubamizwa kwa nguvu huku  ufunguo ukizungushwa kwa ndani na kumfanya  Hamza kwa masikitiko kurudi kwenye sofa.

Baada ya kukaa kwenye sofa kwa zaidi ya dakika ishirini  uvumilivu ulimshinda tena na kujiambia  au hizo nguo zinamshinda kuvaa  maana muda unaenda mno  , lakini dakika ambayo anataka kugonga  mlango hatimae ulifunguliwa.

Eliza  nywele zake zilikuwa zimechanwa vizuri huku eneo la mbele zikipindishwa kidogo  na ule weusi wake wa chocolate ulimfanya kuvutia mno ,  Hamza alikosa hiari na kuwaza  ndio maana mtu kama  Zefa  alitaka kumbaka, Eliza alikuwa  mrembo na urembo wake unahitaji ukaribu zaidi.

Alikuwa amevalia kitopu cha rangi ya  kijani isiokolea  cha maua maua, huku kikiwa na mistari flani hivi upande wa mabega , chini sketi ya  rangi ya Dark Bluu iliovuka magoti  lakini   yenye kuacha wazi miguu ya bia.

Utofauti wa Eliza na wanawake wa kileo ni muonekano wake wa kiutu uzima licha ya sura yake kumpunguzia hio sifa , licha ya kwamba alikuwa akivaa kama wale waimba kwaya  lakini  alivutia mno.

Eliza alijikuta akiwa na furaha  kwa namna ambavyo Hamza alikuwa akimwangalia kwa mshangao , hakuwahi kuweka juhudi kwenye kujivalisha kama hivyo kwa muda mrefu , alivyokuwa single hakujali sana.

“Hamza tuondoke sasa nishamaliza”Aliongea mara baada ya kukohoa kidogo kusafisha koo.

Hamza alijikuta akicheka kidogo  na kisha kumsogelea Eliza na kumshika mkono. “Tutaanza na chakula cha mchana kwanza , nimepata  eneo tulivu kwa ajili yetu”Aliongea Hamza.

“Mh , chakula cha mchana mapema  yote hii?”Aliuliza na kumfanya Hamza kukuna kichwa.

“Sasa Babe   ni wapi unataka  twende kwanza ?”

“Nataka kwenda kumsalimia mama kwanza , Daktari anaesimamia  wodi ya Sanatorium alinipigia jana , amesema kuna  kitu anataka tuzungumze , pili  nataka  mtu wa kwanza kuniona nikitoka  out  na mpenzi wangu ni Mama , nataka aone  nimeshatoka kivulini na sasa nipo   tayari  kuyakaribisha maisha mapya”Aliongea   na Hamza upande wake aliona sio wazo baya , ijapokuwa  mama yake alikuwa katika hali ya kutoweza hata kuongea  lakini  alikuwa ni mama yake na lazima angefurahi  kuona  binti yake hapotezi maisha yake kumhudumia yeye tu  na ana mpenzi sasa.

“Hakuna shida , tukishamaliza kumsalimia mama yetu  tutaenda kula  chakula cha mchana”

“Mama yetu?!”Aliongea  Eliza huku akiona aibu  za kike.

“Ndio  ni mama  mkwe , kuna tatizo?”

“Unajiaminisha sana , unadhani nimekukubalia moja kwa moja  wakati ndio tunaanza  kuwa wapenzi”

“Sawa bibie , vyovyote vile nitahakikisha anakuwa mama yetu”Aliongea Hamza kwa kujivunia  na wakati huo walishatoka tayari na E.liza kufunga mlango  na kuingia kwenye lift.

Baada ya kufika maegeshoni  ya magari,  Eliza alikuwa na gari nzuri sana , ilikuwa  ni mali ya kampuni lakini kwa wakati huo ni ya kwake  kwani sio kwamba angeacha kufanya kazi ndani ya Dosam leo au kesho, isitoshe cheo chake kinapanda siku hadi siku na ni mchapakazi mzuri , ilikuwa ni Sedan, Toyota Crown Camry  Silver Mettallic.

Hamza ndio aliekuwa dereva , isitoshe  Eliza alikuwa amevalia High heels  hivyo ingekuwa ngumu kuendesha, uzuri ilikuwa ni upande huo huo wa Kigamboni  na kadri walivyokuwa wakienda mbele ndio  walivyoingia kwenye  eneo  lenye miti mingi ikiwemo Miarobaini(Neem tree).

Jua lilikuwa la saa tano lakini ni kama la saa saba na kufanya  eneo kuwa na harufu ya  kuungua kwa majani ya  miti.

Baada ya  Eliza kumuonyesha  sehemu ya kuegesha gari , hatimae  wote walitoka.

“Mazingira ya hapa naona sio mabaya  na hili eneo naona   ni  jipya  kabisa,si utakuwa unalipa kiasi kikubwa cha pesa kumuweka mama yako hapa?”

“Hii ndio sehemu  nzuri zaidi  Dar nzima kwa  huduma ya watu wasiojiweza, nalipia jumla ya milioni sitini kwa mwaka”

“Milioni  sitini , hizo zote ni hela zako tu?”Aliuliza Hamza kwa mshangao.

“Baba  ni mstaafu  na yupo kijijini kwa sasa akiendeleza maisha na kiinua mgongo chake cha ualimu , sikuona haja ya kumpa mzigo kumuuguza mama ,  usiwe na wasiwasi  nimemhamishia mama hapa mara baada ya kupanda cheo na kuwa meneja wa idara ya mauzo, mshahara wangu  sio mdogo , ukijumlisha na posho ninazopata”

Aliongea na  Hamza aliona  huyo  mrembo alikuwa na majukumu makubwa mno  ya kifedha, kwa haraka haraka aliamini lazima  mshahara wake wote anatumia kumuuguza mama yake , jambo ambalo sio baya lakini  yeye kama mwanaume alimuonea huruma.

Wote waliingia kwenye jengo hilo la ghorofa ,  kulikuwa na lift pana mno  ya kutosha kitanda cha

mgonjwa , baada ya kufika floor  ya nne  walitoka  na kwenda moja kwa moja kwenye chumba alichokuwepo mama yake Eliza.

Baada ya kuingia  ndani ya chumba hicho kulikuwa na vitanda viwili , vyote vilikuwa na wagonjwa ambao walikuwa katika  hali ya Vegetative, walimkuta nesi pia ambae mara baada ya  kumuona  Eliza alitoa tabasamu na aliandika vitu flani kwenye Cardboard yake na kisha  akaondoka kuwaacha.

Hamza  aliweza kumuona mama ambae sio mtu mzima sana , aliekonda upande wa  kushoto na alijua  bila ya kuambiwa ni mama yake  Eliza maana walionekana kufanana rangi.

“Mama, mwanao nimekuja kukuona”Aliongea  Eliza  akiwa amekaa  kwenye kitanda akishika kwa namna ya kupangusa  paji la uso wa mama yake.

“Naomba unisamehe mama yangu , nimekuwa bize wiki hii  kazini ndio maana sikupata muda wa kuja kukuona , usikasirike mama…”Aliongea huku macho yake yakianza kugeuka  mekundu , mama huyo hakuwa amefumba  macho alikuwa akiona  lakini hakuwa na uwezo wa kuongea.

Hamza aliamua kukaa kwenye sofa la mtu mmoja huku  akimwangalia  Eliza  na mama yake , hakutaka kwenda moja kwa moja alitaka  Eliza yeye ndio amtambulishe.

Eliza alitumia muda  mwingi kumwambia mama yake kila stori iliomjia akilini na mambo yanayoendelea nyumbani na baadae  alimgeukia Roma.

“Mama nimekuja leo na  mpenzi  wangu , nimepata mpenzi  mama  anaitwa Hamza , ni mhuni kidogo lakini anajua kunilinda , kwanzia sasa mama usiwe na wasiwasi , nina mwanajeshi pembeni yangu…”

Baada ya kumtambulisha  Hamza  hatimae alirudi katika  hali yake ya kawaida akizima majonzi yake.

“Naenda kuonana na daktari , vipi  

nisindikize?”Aliuliza na Hamza alitingisha kichwa bila hiyana , hata yeye alikuwa na  shauku ya kutaka kujua kwanini dokta anamtafuta Eliza , alitaka  kujua kama kuna  tatizo  ili aweze kusaidia.

Walitoka kabisa  nje ya jengo hilo na kwasababu ilikuwa jumapili , wafanyakazi wengi hawakuwepo na  kufanya eneo kuwa kimya mno.

Jengo la madaktari  lilikuwa upande wa pili na walitembea katikati ya barabara hio yenye maua

mpaka katika  jengo hilo na kusimama katika mlango uliokuwa na bango CHIEF PHYSICIAN OFFICE na Eliza aligonga.

“Dokta Maonga..”Aliongea  Eliza kiheshima akimsalimia mwanaume aliekuwa na umri wa makadirio ya miaka  theratini na tano kwenda arobaini hivi , alikuwa amevaa  miwani  ya macho  na alikuwa na uwalalaza , ila alipendeza kwa namna alivyozichana nywele zake , alionyesha kujipenda.

“Eliza umefika, karibu”Aliongea  na muda huo mara baada ya kuiona sura ya   Hamza uso wake ulijikunja.

“Huyu ni…”

“Ni rafiki yangu , nimekuja nae”Aliongea Eliza , alitaka kusema ni mpenzi wake   lakini aliamua  kuwa makini.

Upande wa Dokta Maonga aliweza kuona kuna kitu hakipo sawa , lakini alijitahidi kuweka muonekano wake wa kitaaluma.

“Kumbe ni rafiki yako , lakini  maongezi  ya leo ni ya siri , hivyo itakuwa vizuri huyu bwana akitembea tembea kuona  mazingira ya hospitali yetu”Aliongea  na mara baada ya kusikia hivyo  Eliza  alijisiikia vibaya  kidogo.

“Hamza nisame..”

“Usijali  Eliza , ngoja  ninyooshe nyooshe miguu , nipigie simu ukishamaliza”Aliongea na Eliza aliishia kutingisha kichwa tu.

Mara baada ya Hamza kuondoka Maonga  alimkaribisha  Eliza na baada ya hapo alifunga mlango kwa ndani.

“Dokta  nini kimekufanya kuwa makini sana kuhusu afya ya mama?”Aliuliza Eliza  lakini Dokta Maonga alisogelea kwanza  Dispenser na kumimina maji kwenye glasi.

“Usiwe  na wasiwasi Eliza , nitakuelezea taratibu taratibu , kunywa kwanza maji”

“Asante Dokta”Eliza alikuwa na kiu , kutokana na haraka   alishindwa hata kukumbuka  kunywa maji.

“Kiua tatizo  juu ya afya ya mama yangu?”Aliuliza  mara bada ya kumaliza kunywa maji yote.

“Mgonjwa Ratifa Mlowe amekuwa katika hali  ya kutojitambua  kwa zaidi ya  miaka miwili sasa , uwezekano wa  yeye kupona  ni chini ya asilimia tano , nafikiri..”

“Dokta hata kama  ni asilimia  moja , siwezi kumkatia tamaaa mama , kama unataka hela zaidi nipo tayari kulipa  lakini naomba usiache kumtibu”Aliongea Eliza kwa kubembeleza.

“Bila shaka tupo tayari  kutumia fursa hii   lakini kama ujuavyo  kuna hospitali chache sana  ndani ya taifa hili ambazo zimejikita katika kuhudumia wagonjwa wasiojiweza , kikawaida kutokana na asilimia chache za  Ratifa kuamka   ilitakiwa  ndani ya mwaka mmoja awe amesharudishwa na kuugulia nyumbani na kusubiria wakati wa Mungu kumchukua”

“Lakini  Dokta wakati namleta mama hapa ulinihakikisha kutakuwa na matibabu ya hali ya juu ambayo yatamuwezesha mama kuamka , inamaana hukumaanisha”

“Usinielewe vibaya , uwezekano huo upo lakini mpaka sasa tunapokea wagonjwa wengi sana na wengi wameomba nafasi katika wodi zetu , tukisema tukuruhusu  mama yako aendelee

kutibiwa hapa , itahitajika malipo makubwa zaidi ya mwanzo”

“Hayo malipo yatakuwa ni kiasi gani?”Aliuliza Eliza, hakuwa tayari kuona mama yake anarudishwa nyumbani  kwenda kusubiria kifo chake , hata kama kulikuwa na asilimia  moja ya matumaini alitaka kuishikiria hio hio.

Dokta Maonga aliishia   kunyanya kidole hewani na kuchora  namba na Eliza macho yalimtoka.

“Milioni saba kwa mwezi!!?”

Eliza alijikuta akipagawa , kiasi hicho kilikuwa sawa na mshahara wake wote ukiondoa  posho , ijapokuwa alikuwa  katika nafasi ya juu ya kampuni  lakini  hakuwa kama Regina  ambae ni Mkurugenzi  maana yeye hakuwa na hisa kama  wafanyakazi wenzake , wakati wenzake wakinunua hisa za  kampuni kama njia ya uwekezaji yeye alikuwa akimuuguza mama.

“Hapo tu haitoshi  kwani lazima  nikaombe   kwa wakubwa kumuacha mama yako aendelee na matibabu , wanataka wagojywa wanaobaki wawe angalau na asilimia ishirini na tano za kuamka” Eliza hakujua kwanini lakini mara baada ya kusikia hio  namba saba , kichwa chake kilikuwa kikimzunguka,  lakini baada  ya kufikiria kidogo  alipata wazo.

“Hata kama ni hio hela  nitalipa tu  ili kumuacha  Mama aendelee na matibabu”Aliongea lakini  kwa Dokta Maonga  alionyesha ishara  ya ajabu.

“Ukweli ni kwamba kuna namna  ya kuokoa kiasi hicho cha pesa  na  utaendelea kulipia milioni  nne kwa mwezi  kama kawaida”Aliongea na  Eliza  aliona sio wazo baya.

“Ni njia gani hio?”Aliuliza na Maonga palepale alinyanyua mdomo wake na kutoa tabasamu  la ajabu  , alisimama kutoka kwenye kiti chake na kumsogelea Eliza

“Eliza unajua tokea mara ya kwanza na kutia machoni nilikuona mwanamke  mrembo sana , tena unaendana na mimi vizuri”Aliongea  huku akinyoosha mkono wake kutaka  kumshika Eliza lakini mwanamke huyo aliwahi kushituka na kusimama.

“Dokta naomba usifanye hivi … nipo tayari kulipia kiasi ulichonitajia lakini sio hili”

“Eliza kama unataka  mama yako kuendelea kutibiwa hapa ni kheri utulie  na kukubali  ombi langu”

“Wewe… kwahio unamtumia mama kuni…”Eliza alijihisi kichwa chake kikianza kuwa kizito mno  huku kizunguzungu kikimvaa  na macho yalianza kujfiumba yenyewe bila ridhaa yake.

“Haha.. vipi  tena , naona unataka kusinzia?”Muda uleule ndio sasa  Eliza aliangalia kikombe alichotumia kunywa  maji na kuhisi  tatizo.

“Umeniwekea dawa kwenye maji?”

“Hehe.. ndio  ili usishituke niliweka dawa nyingi  maji yote , lakini dozi yake inatosha kukufanya usinzie , usiwe na wasiwasi kabisa , mpaka muda utakaoshituka kila  kitu kitakuwa kimemalizika”

Eliza moyo wake ulianza kujawa na majonzi huku  akijihisi kuwa dhaifu kutokana na ukali wa dawa aliowekewa ,hakuamini dokta kama huyo anaweza kufanya kitendo cha namna hio, lakini  hata hivyo aliona sio wa kumlaumu Dokta Bensoni pia alionekana kama mtu wa heshima kwake lakini mwisho wa siku alimuomba rushwa ya ngono.

Eliza alijiona kama mwanamke mwenye mikosi na hapo hapo  machozi yalianza kumbubujika , katika maisha yake alipona chupuchupu kubakwa mara nying , pengine jaribio la  siku hio linakwenda kuwa mara ya tano katika maisha yake.

Alijikuta akilegea na  kwenda kukalia sofa bila  ya kupenda , muda huo  Dokta Maonga alikuwa  na tabasamu la ushindi na aliingiza mkono kwenye koti lake la kidaktari kutoa simu.

“Ni muda wa mzee Gabusha kutimiza  ahadi ya upande wake”Aliongea huku akiwa haamini anakwenda kupokea hela  nyingi.

Lakini sasa kabla hajafanya chochote mlango wa  chumba hiko ulipigwa teke na kufunguka kwa nguvu, japo ulikuwa umefungwa kwa ndani lakini loki zake zilipinda na ukafunguka.

Kitendo kile kilimshitua  Dokta Maonga kiasi cha kudondosha simu chini na mara baada ya kuona  ni Hamza alijikuta akipandwa na hasira.

“Wewe..  unathubutu..”

“Dakika ambayo umeniona nikifika  hapa ulionekana  kutoridhika na ujio wangu kana kwamba  nimeingilia mpango wako , kila  ulichokuwa unakiwaza kilikuwa kimejiandika kwenye uso wako , unadhani ingekuwa  ngumu kwangu kutokukushitukia”Aliongea Hamza.

“Hamza… naomba unisaidie…”Eliza alikuwa ndio anasinzia , alimuona Hamza lakini alidhani ni kama anaota.

“Lala tu usiwe na wasiwasi , nitakulinda”Aliongea Hamza huku  akiwa na uchungu moyoni, ukweli hakuwa hata na haja ya kumruhusu  alale maana  ilikuwa ndio sauti yake ya mwisho kabla ya kupotelea usingizini.

Dokta Maonga baada ya kuona kitumbua kimeingia mchanga aliangalia mlango na  kitendo cha Hamza kuangalia pembeni aliusogelea kwa spidi , lakini Hamza anamwachaje akimbie kwa mfano.

Ile anapiga  tu hatua alikuwa ashainua mguu na kumpiga eneo la kigoti cha mguu  na kilichosikika  ni’ kacha’.

“Arghhh…!!”

Maonga alijikuta akipiga ukulele huku akikaa chini  na kidogo tu apoteze fahamu maana maumivu hayakuwa ya kawaida.

“Nisamehe , Bwana mdogo naomba  usiniue nina familia”Maonga alijikuta akibembeleza ili kujiokoa katika hali hio , lakini Hamza hakutaka kumuacha alimpiga teke lingine na kumvunja  mguu mwingine na alipotaka kuzimia  Hamza alimshika shingo kwa nguvu.

“Umeweka nini katika maji uliompatia mpenzi wangu?”

“Hapana … ni vidonge vya usingizi .. uwiii miguu yangu , naomba usinipige tena”Aliongea huku mwanaume akitokwa na machozi mfufulizo.

Hamza alijikuta akivuta pumzi ya ahueni , aliona angalau huyu mhuni hajatumia dawa ambayo haieleweki la sivyo mambo yangekuwa magumu.

Hamza alichukua simu ya Maonga iliodondoka chini  na kisha aliitoa  nywira na kwenda moja kwa moja upande wa Vidio rekodi.

“Nataka  ujirekodi kila kitu ulichofanya kupitia hii

simu , vipi unajiona upo tayari au niongeze kidogo maumivu?”

Hamza hakutaka kumuua  , wala  pia hakutaka  itokee Maonga kuja kumshitaki hivyo aliona   atengeneze ushahidi kabla  ya kuondoka hapo.

“Una chaguzi mbili tu , ya kwanza ni kuongea kila kitu ulichofanya na   pili nipigie simu polisi  na

nikufungulie kesi ya ubakaji, hivyo fikiria kipi ni nafuu kwako”

Maonga alijua  chochote atakachochagua hakuna namna anaweza kulipiza kisasi , lakini vilevile  alitamani  kumtaja Mzee Gabusha kama ndio alimpa kazi hio lakini hakuwa tayari kwa hilo , alijua nguvu ya Gabusha  anaweza akawa hai ndio lakini ni  rahisi kupotezwa na Gabusha  muda wowote, hivyo aliona  bora achague  chaguo la kwanza pengine akipona anaweza kuendelea kuwa daktari huku   akipata fidia kutoka kwa Gabusha.

Alikuwa na akili mno , alikuwa na familia hivyo akili yake ilikuwa ikicheza, hakuwa na jinsi  na alielezea  mwanzo mwisho  mpango wake wa kutaka kumbaka  Eliza  kupitia  matatizo ya mama yake.

Hamza mara baada ya kuridhika alituma ushahidi huo katika Email yake na  akamchukua  Eliza kimyakimya na kumuingiza katika  gari.

Bila ya watu kushitukia kinachoendelea  aliweza kutoka ndani ya gari na kuingia ndani ya jengo la hospitali , akiwa na mpango wa kutafuta dawa ya kumumsha  Eliza  haraka iwezekanavyo ili  waendelee na mtoko wao.

Bahati ilikuwa kwake baada ya kufika katika chumba cha dawa mlango ulikuwa umerudishiwa tu na aliingia  haraka haraka na kutafuta baadhi ya dawa na pamoja na sindano na kutoka nazo.

Alirudi kwenye gari na kisha  alifyonza maji katika kijichupa na kuchanganya  na unga unga kisha alivuta  na kumwingizia  Eliza kwenye mshipa wa damu kutumia sindano.

Kwa  jinsi alivyokuwa akifanya Hamza utadhani ni daktari mzoefu wa miaka mingi , alionekana kujua kile alichokuwa akifanya.

Eliza  alikuwa  amelala  mpaka anatoa sauti  lakini alionyesha dalili ya jasho hivyo Hamza alimwegamiza vizuri kwenye siti na kumtoa  kibanio cha nywele na baada ya hapo alirekebisha  ubaridi wa gari, nusu saa kupita  hatimae  Eliza alifumbua macho kivivu.

Bado dawa ya usingizi ilikuwa  kali hivyo  alikuwa akiona ukungu tu , kwa dakika  tano hatimae akili yake ilirudi  katika hali ya kawaida na kukumbuka kilichomtokea na alikaa  kitako kwa mshituko na kuangalia pembeni.

“Hamza  imekuwaje nikafika kwenye gari , kidogo tu ni…”

“Usiwe na wasiwasi  tena , yule mpuuzi nimempa kibano  lakini sijamuua”Aliongea Hamza na  mara  baada ya Eliza kusikia hivyo alijikuta akihema kwa nguvu akionyesha ahueni.

Lakini mara baada ya kuwaza kilichotaka kumtokea  hali ya woga iliamza kumvaa  na kadri alivyokuwa akifikiria ndio macho yake yalivyoanza kuwa mekundu  na  ghafla tu alianza kulia kwa kwikwi.

“Eliza usilie sasa ,  hili limeisha”Aliongea  Hamza akijaribu kumfariji.

“Asante ,  asante sana kwa kuniokoa mara nyingine , lakini vipi kuhusu mama yangu mimi , nini kitampata mama kwa staili hii”

Wazo la kuona  mama yake  akikosa matibabu  sahihi  moyo ulizidi kumuuma.

Hamza hata yeye hakufikiria hilo  lakini alijikuta akiwaza kwa mdua namna ya kufanya.

“Eliza usiwe na  wasiwasi , kuna daktari namfahamu na uwezo wake sio mbaya sana , unaonaje tukimchukua  mama na kumrudisha nyumbani kwanza na kumtafutia mtu wa kumhudimia  na  nitawasiliana na huyo dokta , akifika  atamwangalia  au ikishindikana tutamsafirisha moja kwa moja nje  ya nchi”

“Una rafiki ktuoka nje ya nchi  ambae ni dokta, na yeye anahusika na   ugonjwa kama wa mama?”

“Sijui ila anaonekana kama Dokta wa magonjwa yote , ni MD hata kama  hajui jinsi ya kutibu lazima atakuwa anafahamu madokta wenye uwezo”Eliza alitaka kuongea neno lakini alisita mara baada  ya kuona sindano na mabomba ndani ya gari.

“Hizi sindano ndio ulinichoma nazo ,  sio kama umenitingisha nikaamka?”

“Ndio nimekuchoma , wewe unadhani ungemka mapema hivi?”

“Kwahio unajua kumchoma mtu sindano?”

“Mimi ni dokta  ndio  tena wa moyo , mambo ya kushika kisu na  kumchana mgonjwa kwangu rahisi sana ,  nikishamaliza kumpima kama hivi  kazi inaanza taratibu , shwa , shwaa!!”Hamza alikuwa akifanya utani  huku akijifanyisha anampima Eliza mapigo ya moyo kumbe anashika nyonyo, ila kitendo  kile kilimfanya  Eliza kuficha kifua chake.

“Unamdanganya nani  hapa , eti daktari,  mateja tu wanajua kujichoma sindano , unadhani nadanganyika kirahisi” “Sawa bwana kama huniamini”

“Kwahio umenichoma dawa gani na umezitoa wapi?”Aliongea huku akinyanyua vijichupa vya dawa vilivyokuwa kwenye siti.

“Nizitoe wapi tena wakati mimi sio Dokta , niliziiba wakati wakiwa bize  na simu zao , hii hapa  sijui wanaiita Benzo nini huko ila  kazi yake ni kupoza nguvu ya vidonge vya usingizi “ “Vipi kuhusu hii nyingine?”Aliuliza

“Hio ni Mannitol “

“Kazi yake?”Aliuliza na kumfanya Hamza kusugua pua yake.

“Eliza unaonaje tukienda kula  kwanza , unaonekana   una njaa”

“Acha kubadilisha topiki , niambie kwanza hii dawa kazi yake?”

“Ni nzuri kwa afya  yako , kwanini unauliza sana?”

“Kama ni nzuri kwangu niambie kazi yake nini?”

“Kuhusu hio.. basi ngoja nikuambie , vipi kwanza hujisikii  mkojo kukubana”

“Labda wewe ndio  mkojo umekubana , niambie kazi ya hii dawa acha kuzunguka zunguka”

“Hio ni dawa ya kukufanya ukojoe  ili kupunguza  sumu mwilini”

“Kwanini umenipa dawa ya kunitoa mkojo  wakati  tupo date”Aliongea Eliza huku akimpiga  piga Hamza   na kumfanya acheke.

“Usinipige bwana , nilikuwa na wasiwasi  ,  kama usingemka mapema kuna uwezekano ungejikojolea , bahati  nzuri umewahi kuamka”Eliza alitaka  kumpiga lakini  alihisi mafuriko  yakijikusanya  na aliishia kusugua meno kwa hasira.

“Nitakushikisha adabu nikirudi, ngoja uone”Aliongea  na kisha alifungua mlango na kutimua nduki kwenda chooni kama mwanariadha.

Wakati wa kurudi   alishindwa kuzuia aibu aliokuwa nayo.

“Babe naona sasa umekaa sawa , haha ..tuendelee zetu na mtoko sasa , tunaanza kula kwanza”

“Nitakusamehe leo kwasababu umeniokoa , ila siku nyigine ukinichoma sindano zisizoeleweka , sikuongeleshi tena”Aliongea na  Hamza hakutaka  kurefusha hilo jambo hivyo alikubali kwa kutingisha kichwa.

Kabla  hajawasha gari  wazo lilimjia palepale na aliinama kuelekea upande wa Eliza   na kisha alichomoa mkanda wa siti.

Eliza alijua kuna kitu  Hamza  anataka kumfanyia , lakini mara baada ya kuona ni mkanda wa gari alijikuta akipumua kwa ahueni.

“Nitafunga mwenyewe”

“Tulia hivi hivi , jana  nimekula shule ya mapenzi mtandaoni  na wamesema ukimsaidia mpenzi wako kufunga mkanda  unajinyakulia  pointi za mapema sana , ni namna ya kuonyesha unajali”

Kauli ile ilimfanya Eliza kujikuta akicheka mpaka basi.

“Vipi kama mpenzi wako  hataki kufungwa mkanda?”

“Hapo ndio pagumu sasa maana  walinihakikishia

kabisa nitajinyakulia pointi , vipi  wewe hupendi kufungwa mkanda?” 

“Haha..hebu endesha huko , siku nyingine nitafunga mwenyewe .. unalishwa matangopori  unayabeba kama yalivyo”

Hamza alijikuta akijifanyisha kuona aibu  na mara baada ya kumwangalia Eliza walijikuta wakicheka wote.

****

Muda wa saa  sita Mchana Mzee Gabusha aliingia nyumbani kwake na wala hakumjali hata  Chriss aliekuwa bize na simu bali alivua koti la suti pamoja na tai na kisha  alikimbilia friji na kuibuka na Vodka pamoja na glasi.

Kwa haraka haraka alimimina kinywaji kile katika  ile glasi  na kupiga pafu kwa nguvu kana  kwamba anakunywa maji.

Kitendo kile cha baba yake kurudi akiwa katika hali hio alijua lazima kuna swala ambalo limetokea  na hio ilimpa shauku Chriss.

“Mzee  nini tatizo?”Aliuliza Chriss.

“Hakuna tatizo”Aliongea  huku kifua kikipanda na kushuka.

“Dad tunaishi wote na nakujua ukiwa katika mudi tofauti tofauti , ukiwa na kitu kinachokusumbua  lazima utumie Vodka”

Kabla hata hajajibu swali la   Chriss simu yake ilinguruma na aliitoa haraka haraka na kuangalia jina la anaepiga  na alipokea palepale.

“Boss ashaanza matibabu, amevunjika miguu yote miwili”

“Vipi kuhusu  Eliza  hajaongea chochote , hakunitaja  wala kutoa ushahidi wowote?”

“Imekuwa ngumu kumhoji kwasasa  maana ndio amerejewa na fahamu , bosi  nitachukua maelezo kutoka kwake”

“Sawa nitaarifu ukifanikiwa”Aliongea na kisha akakata simu na Chriss shauku ilizidi kumjaa.

“Mzee nini kinaendelea”

“Yule boya kamvunja  Maonga miguu yote”Aliongea na kauli ile ilimfanya  Chriss kuwa na hali ya kuchanganyikiwa. “Baba unamaanisha boya yupi?”

“Alievuruga mpango wangu na Eliza  na kumfanya Amosi  kujitoa kabisa  baada ya Chatu kumtishia maisha yake”Aliongea  huku akichukua kinywaji kingine na ukigida na kufanya jicho kuwa jekundu.

“Imekuwaje  Maonga  akaingia katika hili sakata Mzee ..usiniambie?”Aliongea Chriss na wazo lilimjia palepale  na kujikuta akikaa kwenye sofa  huku akimwangalia mzee  wake kwa mshangao.

Mzee Gabusha  hakujali muonekano wa  chirss na alichukua koti lake  pamoja na tai  na kisha aligeuza  akitoka nje , haikueleweka alikuwa akienda wapi maana ndio amefika nyumbani.

Chriss  aliishia kutingisha kichwa  tu, huku akijiambia mzee ni mkatili sana na hakutarajia kama angekamilisha mpango wake muovu.

Dakika chache kupita mlango wa kuingilia ulifunguliwa  na Alex ambae alikuwa na yeye mbiombio na kumfanya Chriss ajiulize leo hawa ndugu zake wana matatizo gani.

“Hey! Chriss , mjomba amekuwaje mbona mbiombio hata namsalimia haitikii?”

“Mpango wake  na Eliza unaonekana kubuma , ndio maana yupo hivyo?”Aliongea Chriss kivivu  na  Alex mara baada ya kusikia kauli ile alienda kukaa haraka haraka kwenye  sofa na kumkazia Chriss macho.

“Kulikuwa na mpango  ambao siujui?”

“Unajuaje wakati siku sita zote  huonekani na hata  taarifa  hujatoa , unazingua?”Aliongea na kumfanya  Alex kunywea kidogo.

“Niliitwa na Madame , yule mwanamke akisema njoo hata  upo chooni unaacha  unaenda , sikupata

muda wa kukutaarifu. Niambie ni mpango ngani  uliofeli?”

“Unajua Mzee na mambo yake , juzi ananiambia ana mpango wa kumtia  Eliza mimba , hivyo ameanza kufatilia mzunguko wake  wa hedhi?”

“Nini , Mjomba anajua mzunguko wa hedhi wa

Eliza , kivipi?”

“Mzee   juhudi anazowekwa kwa huyu mwanamke ingekuwa ni kwenye biashara zetu tungeipita hata  Dosam   muda mrefu ,  lakini ndio hivyo juhudi  anazoweka hazimpi majibu, Inaonekana huyu Eliza  anapata  maumivu wakati  wa hedhi  na kutumia vidonge flani hivi vya kuyapunguza, duka analopenda kununulia Vidonge hivyo ni lile la Mzee Benjamini  kule Kigamboni , nadhani ndio   alijua hapo  kwa kupiga mahesabu ya siku ambayo  anaingia kwenye mzunguko”Aliongea  Chriss na kumfanya  Alex kutoa macho.

“Aisee Mjomba kafanya yote haya kwa ajili  ya  huyo mwanamke , mbona shauku inanijaa , nataka kumuona huyo mrembo”

“Hata mimi nimejikuta nikipatwa na shauku ya kutaka kumuona , nilitaka kutumia kisingizio cha kwenda kumuona Prisila  kazini kwake  ili anikutanishe na huyo Eliza  ila  kwasasa  yupo likizo”

“Sasa imekuwaje mpango ukafeli?”

“Wewe mpaka hapo ulitakiwa uwe ushaelewa nini mzee angefanya , mpango wake ulikuwa ni  kumbaka  Eliza akiwa katika siku za hatari ili amtie mimba ,  juzi wakati ananiuliza  maswala ya mzunguko wa hedhi yanavyokuwa  nilimdadisi  

lakini hakufunguka sana , ila leo baada ya kurudi   akiwa amefura nishausoma mchezo mzima, Dokta Maonga  ni Mkuu wa Vizda Sanatorium  na  huyo  Eliza   mzazi wake ni mgonjwa ambae  hajitambui  hivyo ni lazima  atakuwa  yupo  huko Vizda na Mzee Kamtumia  Maonga kufanikisha mpango  matokeo yake  Maonga kavunjwa miguu”Aliongea  huku akicheka.

“Maonga kavunjwa miguu?”

“Ndio  na Mzee  kwa ninavyoona wasiwasi wake ni  kama Maonga amemtaja  katika tukio hilo, nadhani ndio kinachomsumbua zaidi akili  kwa sasa”

“Huyo  jamaa aliefanikisha kitendo cha kumvunja  miguu Dokta Maonga  ni nani  huyo, au ndio yule  yule  aliemfanya Jasusi kukimbbia”

“Ndio huyo , kasema  tu yule boya kaharibu mpango wangu”Alex  alijikuta  akifikiria.

“Siwezi kumcheka Mjomba wakati na mambo yangu hayajakaa sawa  kabisa , Frida  katoweka   na sijui  kaelekea wapi?”

“Katoweka au kasafiri?”Aliuliza

“Kusafiri unajua mtu kaenda wapi , ila huyo katoweka , sijui hata kama amesafiri” “Amesafiri huyo na atarudi ,unadhani mfanyakazi wa taasisi kubwa kama Haliz anaweza kupotea tu hivi hivi , tumia akili bro”

“Nimefikira hivyo pia , lakini hata akirudi sidhani kama pale nitang’oa , itafikia  hatua naweza kutumia hata njia  ya mjomba”

“Wewe na Mjomba mnafanana sana tabia , nimehangaika na Prisila mwaka wa ngapi huu lakini  sijaambulia  chochote zaiti ya mate tu , lakini sijawahi kufiikiria kumfanyia  hila , nitaenda nae

taratibu  mpaka ajae kwenye himaya yangu”Aliongea.

“Wewe Chriss unachofanya ni uboya , endelea na ubaba paroko ,utakuja kushitukia  demu sio wako tena , unaweza ambulia  mate kuna mwenzako anapewa zaidi ya hivyo”

“Acha uboya  Alex ,  namjua Prisila vizuri, unadhani  mpaka muhuni kama mimi ku fall in

love ni rahisi hivyo”Aliongea .

“Simu yako inaita”Aliongea  Alex  akinyooshea simu iliokuwa  juu ya meza ya kioo,

Chriss aliichukua haraka haraka   na  mara baada ya kuangalia jina la mpigaji  mapigo yake yalienda mbio.

“Huyu Jasusi baada ya wiki kupita ndio  ananipigia sasa hivi  simu, nimemtafuta sana”Aliongea  kwa hasira mara baada ya kuona jina la Mzee Amosi kwenye kioo cha simu yake.

******

Hali ya  Eliza iliimarika mara moja na hio ilimpa  

amani ya kuendelea na siku yao kama walivyopanga.

Walitoka hospitalini na moja kwa moja walienda kwenye mgahawa  ambao  Hamza aliuchagua , wakiwa njiani  Hamza alimwelezea Eliza namna  alivyodili na Dokta Maonga.

Eliza hata yeye baada ya kusikia kibano alichokutana nacho aliona haina haja ya kwenda  kushitaki , kwani ingempotezea muda tu , isitoshe vitendo vya namna hio vilikuwa vikikemewa kila siku lakini havikuwahi kukoma.

Kwa mara ya  kwanza  mrembo huyo alijisikia vizuri sana  ana mwanaume ambae anaweza kumlinda wakati wote , siku zote alikuwa peke yake akihangaika  huku na huko na hata kuombwa rushwa ya ngono , lakini  malaika Hamza kujitokeza  ni kitu kilichomfanya ampende zaidi.

Siku nzima hakuacha kumwangalia  Hamza   huku akiwa na tabasamu 

Upande wa  Hamza na yeye alifurahi  kuwa karibu na mrembo huyo  na  ni mwanamke wake wa kwanza kuingia nae katika mahusiano kwa kipindi kirefu.

Aliweza kumjua  kiundani   zaidi  Eliza  na alijua  ashawahi kuwa katika mahusiano huko nyuma , hakushangaa , kwa uzuri wa  Eliza lazima wanaume wengi walijaribu bahati zao na ni ngumu  kuwakatalia wanaume wote, ki ufupi hakuona tatizo Eliza kuwa na Ex.

Saa tatu kamili za usiku ndio  Hamza alimaliza mtoko wake na mtoto  mzuri Eliza , ijapokuwa ilikuwa mapema lakini kwasababu  siku iliofuatia ni Jumatatu hivyo Eliza alitaka kuwahi kupumzika.

Hamza wakati anafika nyumbani  aliweza kumkuta Shangazi akiwa bado macho , akiwa bize na kuandaa  vifungua kinywa kwa ajili ya  siku inayofuara asubuhi.

“Hamza bora umewahi kurudi , hebu  chukua hizi doghnut  na hio chai ya maziwa umpelekee Regina , hajakula chochote tokea mchana”

“Regina hajala chochote tokea mchana?”Aliuliza Hamza kwa mshangao.

“Ndio , nadhani ni maswala ya kampuni ndio yanamuumiza kichwa , nashindwa hata kumuelewa ila  anaonekana kutokuwa na raha kabisa , nimeenda hapo   supemarket na kununua hizi Doghnut”

Hamza  alishangaa  kuona Shangazi na giza lote ameenda kutafuta Doghnut kwa ajili ya Regina , kwenye mfuko zilikuwa nane na zilikuwa zikinukia harufu flani hivi nzuri  ya Strawberry, Hamza aliishia kujiuliza Regina  atamaliza zote hizo.

Ukweli ni kwamba  mwenyewe  alikuwa aksihangaa yaani mtu aache kula chakula cha usiku  na ale doghnut saa nne kasoto ya usiku.

“Usiwe na wasiwasi kabisa , Regina huwa anazipenda sana hizo , huwa akiwa hana hamu ya kula ndio naendaga kuzinunua na kumpa , hizo nane  ni chache sana mbona”Aliongea  Shangazi  lakini  Hamza hakuamini, aliishia kuchukua maziwa yaliochanganywa na majani  na kisha kupandisha juu.

“Regina upo ndani?”Aligonga  lakini  hakuna suati iliosikika kutoka ndani.

Previoua Next