Reader Settings

SEHEMU YA 36. 

Wakati wa mchana wote  taarifa  ya  Regina   Afisa mtendaji  mkuu  kumpata  msaliti wa kampuni zilisambaa kwa kila mmoja , lakini haikuwa hivyo tu  pia  kwa kitendo cha Regina  kuwatumia wasaliti kuidanganya kampuni ya Zena ni moja ya habari hizo. 

Kulikuwa hata  na  baadhi ya waandishi wa habari waliokuwa   wakitaka  kuzijua habari hizo na kuzichapisha katika mitandao yao. 

Wiki iliopita , wafanyakazi wengi walikuwa  katika hali ya  mawazo   mara baada ya  kampuni yao kushindwa kuipata Omega , lakini kumbe haikuwa mpango wa Regina kuipata  Omega. 

Regina alikuwa amedanganya  kampuni nzima  kwa kuwaaminisha kwamba  alikuwa  akitaka kuinunua Omega na  kuikosa , hata kuigiza  kabisa  kuonekana kama vile alikuwa katika msongo wa mawazo. 

Ijapokuwa wengi walimpongeza  Regina kwa kumuua adui yake bila  ya kumwaga damu  lakini upande mwingine  walimuona Regina kama mwanamke mkatili sana, haikuwa swala la kudanganya  watu wa kampuni ya Zena tu  lakini vievile amefannikiwa  kuidanganya kampuni nzima kuamini alikuwa akitaka kuinunua  Omega. 

Baada ya kazi  kama kawaida  Hamza na Regina walishuka  chini  pamoja katika lift. 

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni  walikuwa pia ndani ya lift hio na walimsalimia Regina kwa heshima  , lakini kulikuwa na hali ya  kumuogopa katika macho yao , kitu ambacho kilionekana wazi  tofauti na mwanzo. 

Tukio la siku hio licha ya kwamba lilikuwa na faida  kwa kampuni , lakini lilifanya  wafanyakazi kuzidi kumhofia. 

Yaani  ni kama mwanzoni walikuwa wakiamini Regina sio kama wanavyomfikiria , lakini mara baada ya tukio hilo waliamini Regina ni kama wanavyomfikiria. 

Regina  alikuwa akiiona hofu yao  lakini  aliishia kukaa kimya kama kawaida yae , hakujali watu walivyokuwa wakimfikiria. 

Barabara kuelekea  wanakoishi ilikuwa na msongamano sio wa kawaida hivyo  gari ilikuwa ikisogea kidogo kidogo , Hamza hata yeye alionekana kuboreka kuendesha gari kwenye msongamano  kama huo na aliishia kuangalia kioo  cha nyuma kuona  Regina anafanya  nini. 

Lakini Regina muda huo alikuwa  akiangalia upande wa nje   ya barabara huku akiwa na hali flani ya wasiwasi. 

“Usiwe na mawazo hivyo , kwenye hii dunia  usitegemee kupendwa na watu wote”Aliongea Hamza  na kumfanya  Regina kushangaa. 

“Nani ana mawazo , hebu endesha gari huko”  

“Regina huoni tupo kwenye foleni , ila  kwa tukio la leo kama ungekuwa mwigizaji  ungekuwa maarufu 

mno ,  wiki iliopita  nilidhani ulikuwa  katika mawazo kwa kuikosa  Omega”  “Vipi … umekasirika kukuigizia?”  “Nikasirike , kwanini nikasirike?”Aliulia Hamza.  

“Si ninekundanganya na wewe?”  

“Kwannini  swala hili linikasirishe , hili sio swala la kisheria  kwamba lazima uniambie kila kitu , kucheza rafu sokoni ni swala la kawaida kwa wafanyabiashara, ijapokuwa watu wanaweza  kufikiria  una roho   ya kikatili , lakini yote umefanya kwa ajili ya kampuni , kama ningekuwa wewe  pengine ningefanya hivyo hivyo, kama nilivyosema , huwezi kupendwa na watu wote kumbuka pia siku zote unapopata kitu jua unapoteza kitu”  

“Na wewe unaamini hivyo?”Aliuliza na Hamza alitingisha kichwa. 

“Ijapokuwa nimekudanganya mara kadhaa lakini hili namaanisha , ila siku nyingine Regina tukio kama hili likitokea  ni kheri uniambie hata kwa siri sitowaambia watu,  yaani  nakuona una mawazo najaribu kukubembeleza kumbe  napoteza nguvu zangu bure tu,itakuwa ni kujitia aibu tu”  

“Sitaki unibembeleze , wewe ni  nani kwangu  mpaka unibembeleze , halafu kwanini nikuamini huwezi  kutoa siri?”Aliongea Regina  huku akikunja nne , lakini  Hamza aliishia kucheka. 

“Kwasababu mimi ni mpenzi wako , hivyo lazima unizingatie”  

“Wewe sio mpenzi wangu  , wewe ni mpenzi wangu wa maigizo tu , mpenzi wako  ni huyo ulietoka  nae out jana”Aliongea Regina  kwa hasira.  

“Kwahio  vipi , nisipokuwa  na mpenzi wewe utakubali  kuwa mpenzi wangu , sidhani kama utakubali kutoka na mimi kimapenzi?”  

“Nani kasema sitokubali”Aliongea  lakini dakika hio hio alijua maneno yake   hayakukaa sawa na kuulaumu mdomo wake kwa uropokaji , lakini jibu lile lilimshangaza  Hamza. 

“Regina kwahio unamaanisha unataka ku’date’ na mimi?”Aliuliza  na kumfanya  Regina kuona aibu kidogo. 

“Kwannini unajiaminisha sana , ushawahi kuniuliza hilo swali?”  

“Basi ngoja nikuulize sasa hivi , Regina  je unataka tuwe wapenzi ki ukweli ukweli?”  

“Mjinga wewe , Sitaki na sitotaka”Aliongea  huku akimkodolea macho bila ya hisia. 

Hamza alijikuta akikosa   neno ,alijiambia ni kheri asingeuliza tu , maana jibu  lilikuwa wazi. 

“Hata mimi sitaki pia , kwanza nina mpenzi tayari na  ni mpole  na  mchangafu  kuliko wewe”Aliongea Hamza huku akionyesha furaha kabisa  mara baada ya wazo la Eliza kumjia akilini . 

Upande wa Regina  ukauzu ulizidi kuonekana katika macho yake  na aliishia kushika sketi yake kwa mikono yote miwili. 

“Naona unamsifia sana huyo mpenzi wako , inaonyesha  kabisa nimemzidi vitu vingi ndio maana unanilinganisha nae”  

“Regina usiniambie unaona wivu ,  kwanini tokea  jana nilipoanza kumzungumzia mpenzi wangu  naona kuna kitu hakipo sawa kwako?”  

“Nini, yaani mimi niwe na wivu na wewe , nimekuwa chizi , halafu ukiendelea kuongea ujinga wako sitokupa  hata shilingi ya mshahara wako”  “Bosi usifanye  hivyo , najua hunipendi lakini usinikate mshahara”Aliongea Hamza akijitetea.  

Regina alikuwa na hasira sio  ya kawaida kiasi kwamba kifua kilikuwa kikimpanda na kushuka , aliishia kuvuta mdomo na kisha akageuza kichwa chake na kuangalia nje. 

Haikueleweka foleni ilisababishwa na nini , lakini muda ambao walifika nyumbani giza lishaingia tayari. 

“Umeongea pumba zako kwenye gari mpaka umesababisha nimechelewa kufika nyumbani”Alilalamika Regina.  

“Nunua gari lenye mabawa siku nyingine nitalipaisha ,  yaani unanilaumu kwa msongamano wa magari ambao sijausababisha”  

“Ni  makosa yako , ungetafuta njia  nyingine, halafu  usibishane bishane na mimi”  

“Okey , samahani bosi kwa kukuchelewesha nyumbani na kukukwaza”Aliongea Hamza , hakuaka kuendelea kubishana na Regina juu ya swala hilo maana hata kosa lake hakuwa akilijua.  “Shangazi ni bora uwe unapika moja kwa moja  na  

kuendelea kula tu , usitusubiri ukiona tumechelewa”Aliongea Hamza. 

“Nilijua  mtachelewa  sana , chakula cha kupasha sio kizuri  ndio maana nachelewesha kupika , hii AC inapoozesha chakula kwa haraka, subirini kidogo nimalizie”Aliongea Shangazi huku akielekea jikoni. 

Hamza  hakutaka kusubiria chakula   sebuleni na alienda jikoni pia . 

“Shangazi unaonaje  tukigawana upishi  ili tumalize haraka, mimi nitatumia jiko la umeme”Aliongea  Hamza na  Regina aliekuwa amekaa  kivivu sebuleni alishangaa   baada ya kusikia kauli hio. 

“Wewe unajua kupika?”  

“Najua ndio , kwani kuna ugumu gani  kupika?”  

“Kwahio kumbe kila binadamu siku hizi ni mpishi?”Aliongea Regina   na kumfanya  Hamza kutingisha kichwa kwa masikitiko. 

“Ni hivyo tu sina mpango wa kuonyesha uwezo wangu leo hii , nina nyota tano za Michellin , likija swala la upishi”  

“Michellin wanatoa nyota tatu tu  za upishi , wewe hizo tano umezitolea wapi ,  unadhani wote  sisi ni washamba?”Aliongea  Regina akimkosoa.  

“Natania tu , nilikuwa  namaanisha ninao uwezo wa kuharakisha mapishi na  yakawa ya kiwango”:Aliongea Hamza .  

Shangazi alifurahi kuona amepata mtu wa kumsaidia hivyo  alimwachia  Hamza samaki aziunge. 

Hamza mara baada ya kuanza kukatakata vitunguu  na nyanya kwa spidi kali  pamoja na mpangilio wake wa ki upishi   jambo hilo lilimsahngaza Shangazi. 

Ndani ya muda  mfupi tu mboga saba zote zilikuwa zimeiva  na  kila kitu kilikuwa kipo kwenye meza. 

Regina alijikuta akimeza mate kutokana na harufu nzuri ya chakula , mara baada ya kusogea mezani na kuangalia namna samaki alivyokatwa katwa katika vipande vya nyama , pamoja na  namna  ilivyopambwa na kachumbali kwa juu  ilipendeza kwa macho. 

“Regina , Hamza ni fundi mno kwenye upishi , mimi nashindwa kutumia jiko la umeme kukadiria  moto lakini  yeye  ameweza na hakuna kilichoungua na chakula chake kinapendeza”Aliongea  Shangazi kwa  kusifia. “Shangazi chakuka kuonekana vizuri haimaanishi ni kitamu”Aliongea Regina na alichukua uma na kisha kuchukua kipande cha samaki  na kupeleka mdomoni na kitendo cha kutafuta  mara kadhaa muonekano wake ulibadilika mara moja. 

“Haha ,, unaonaje , nishakuambia nina nyota tano”Aliongea Hamza  kwa majisifu.  

Regina aliishia kukosa neno la kuongea kwasababu radha ya hio samaki ilikuwa ni zaidi ya  radha ambayo alikuwa akiipata kutoka kwenye chakula kinachopikwa na Shangazi. 

Regina aliishia kujiambia kwanini huyu mwanaume kila kitu anajua , alijikuta akiishia kuchukia kwa  kitendo cha Hamza kujua kila kitu. 

“Regina kwa Hamza  hapa nadhani sina wasiwasi hata  nisipokuwepo baadae, hata kama usipojifunza kupika Hamza atakuwa yupo tayari kukusaidia”Aliongea Shangazi na mara baada ya  kusikia kauli ile Regina alijikuta akiwa mwekundu. 

“Shangazi kwanini unaongea hivyo”  

“Nini , inamaana   Regina hajui kupika , Shangazi huyu ukimuacha mwenyewe ataisha kula mayai ya kuchemsha au hotelini”  

“Regina  hata  mayai ya kuchemsha hajui  kabisa , anachojua ni kufanya biashara tu, nakumbuka  alishawahi kuchemsha mayai mpaka maji  yakakauka  huku  mayai yakipasuka na kubakia  makasha tu”Aliongea shangazi na kuanza kucheka.  

“Ili mradi hakuungua tu , inatosha”Aliongea Hamza. 

“Nyamaza  wewe , kwani kujua kupika ndio  nini , nikiamua kujifunza  nitaweza pia’”Aliongea  Regina huku akiona aibu , ni kama  anaona Hamza anamdharau  kwa kutokujua kupika na kuonekana amekuzwa kimayai mayai. 

“Regina usikasirike  ni utani tu , hebu kaeni tule kwanza”Aliongea Shangazi lakini Regina alikuwa na hasira mno na kadri alivyokuwa akimwangalia  Hamza ndio alivyokuwa akizidi kuchukia. 

Muda huo huo simu ya Hamza iliita na alipangalia jina la mtu anaepiga  ni  Lau  mfanyakazi wa Mgahawa wa Dina. 

Hamza hakutaka  Regina kusikia  anachoongea  hivyo alitoka nje  na  kupokea simu  

“Lau vipi  kuna tatizo?”  

“Madam ameniambie nisikueleze , ila yupo kwenye matatizo makubwa”Aliongea Lau upande wapili akioyesha kuwa na wasiwasi. 

Previoua Next