Reader Settings

SEHEMU YA 37.

Upande wa pili ilikuwa ni kama vile  Lau hakutaka kusikika alikuwa akiongea na simu , licha ya kuwa na wasiwasi lakini sauti yake ilikuwa ya chini sana.

“Lau niambie ni nini kinachoendelea vizuri nikuelewe”Aliongea Hamza.

“Bro  hii simu nimekupigia kwa siri mno , naomba usimwambie  Madam mimi ndio  nimekupigia”

“Ongea bwana kama una cha kuongea , nini kimempata Dina?”Aliuliza  Hamza kwa usiriasi kidogo.

“Kamisheni tatu za mtandao wa  Chatu kutoka  Uganda , Kenya, Rwanda na Tanzania  wanaenda kinyume na  Madam ,  nadhani kuna mtu yupo nyuma yao , Madam ameamua  kudhibiti hili yeye mwenyewe , ni aidha augawanye mtandao wote wa Chatu   au kuzima wale wanaoenda kinyume, lakini  kwa chaguo lolote lile naona kabisa ni hatari kwake, hao watu wamekuja leo na walichosema wanataka kuonana na Madam kwa ajli ya mazugumzo pekee”.

‘Kama ni hatari kwanini Dina kaenda?”Aliuliza Hamza.

“Nilijaribu kumbembeleza asiende , lakini hakutaka kunisikiliza,ameondoka akidhamiria kutumia

vitisho ili  kutuliza hali”

“Alichofanya ni sahihi, kama   ni kiongozi alipaswa aende , ukiwa muoga watu watakudharau”Aliongea Hamza.

“Ndio bro , lakini wasiwasi wangu watu hawa wanaonekana kuwa na njama”

“Hili limetokea kwasababu ya  kilichomtokea  Zefa  na kufanya watu wasiridhike?”Aliuliza  Hamza.

“Nadhani ni kuhusu hilo pia, lakini  ukiachana na hilo  tokea muda mrefu wazee hawakuridhika kuongozwa na  mwanamke”

“Huna haja ya kuzunguka  katika hili ,  mimi ndio nimeuwasha moto hivyo ni sawa kuuzima mwenyewe”Aliongea Hamza , alijua swala la kumsaidia Eliza kwa kumpatia Zefa adhabu lilikuwa swala kubwa na lazima kungetokea migongano katika mtandao wote wa  Chatu.

Hamza aliomba  Lau amwambie eneo husika kikao kinapofanyikia  na alitumiwa.

“Kuna sehemu naenda mara moja , mnaweza kuendelea kula tu msinisubiri”Aliongea Hamza mara baada ya kurudi ndani na kabla hata hajaulizwa swali alikuwa ashakimbilia nje tayari.

“Hamza , kula kwanza ndio uende..”Shangazi  aliongea kwa nguvu  lakini  Hamza alikuwa ashaingia  kwenye gari tayari.

“Shangazi achana nae  ngoja afe na njaa”Aliongea Regina  kwa hasira , ijapokuwa ameongea hivyo lakini katika macho yake alikuwa na wasiwasi.

Upande  mwingine Hamza alikuwa akiiendesha Lexus ya Regina  kama hana akili nzuri.

Muda mrefu tu hakutaka kujiingiza kabisa katika biashara za Dina , lakini kwa muda huo aliona hakuwa na  jinsi zaidi   ya kuingilia  kwani Dina yupo  hatarini.,

Mwisho  wa siku  Dina na yeye ni kama alikuwa na sehemu yake katika moyo wake hivyo alikosa utulivu , wasiwasi ulimjaa.

Hamza aliishia kushika        tumbo lake       huku akiendesha gari kwa mkono mmoja na aliishia kutabasamu akikumbuka alikuwa na  njaa.

“Sijui kutakuwa na msosi?”Alijiuliza.

*******

Ilikuwa ni zaidi ya miezi mitatu tokea kiwanda cha  magodoro kufungwa na yote hio ni mara baada ya mmiliki huyo kufirisika ,  hakujali tena kiwanda hicho tokea itangazwe amefirisika.

Usiku huu   hata hivyo   magari zaidi ya kumi  na mbili yalikuwa  yameegeshwa nje ya kiwanda hicho , mengi  yakiwa ni  Noah  na yale ya  ki ofisi.

Katika kiwanda hicho kulikuwa na harufu nzito kweli ya  oil, ki ufupi hali ya hewa ilikuwa nzito.

Kulikuwa na  makundi mawili ya watu waliosimama upande upande ,  huku makundi yote yakiwa na watu wasiopungua mia  moja . upande wa kulia  alikuwa ni Dina , upande wa kushoto alikuwa ni  kundi la watu wengine.

Kwa jinsi hali ilivyo haikuhitaji elimu ya darasa la saba  kujua   kinachoendelea, kulionekana kulikuwa na uhasama kati ya kundi la  kwanza na  na la pili.

Baadhi ya watu katika kila kundi  walikuwa na Zana za kushambulia ikiwemo mapanga , visu  aina ya Jambia  na virungu.

Sura zote zilionekana katika hali ya utayari wa  kufanyiana fujo muda wowote   na ilionekana  ni  maagizo tu yaliokuwa yakisubiriwa kutoka  pande zote.

Kundi la upande wa kulia lilikuwa likionzowa na Dina mwenyewe  na alikuwa na vijana wake waliomzunguka ikiwemo Lau na kundi la pili liliongozwa na  mama mmoja , kama  ni mfuatiliaji wa wafanyabiashara maarufu kutoka  Kenya  basi ni dhahiri ungemfahamu,  mtu mwingine alikuwa ni mwanaume  hakuwa maarufu sana katika jamii lakini kwa wale wanaomfahamu  ni balozi kutoka Rwanda, kulikuwa na Mzee Mwingine aliekuwa na Mvi , alionekana kuwa mkubwa kuliko wote waliokuwepo hapo  huyu alifahamika kama Mzee  Dembe alikuwa ni raia wa Uganda.

Mrembo Dina ambae alikuwa amevalia   kitop cha mikono mifupi na jeans nyeusi aliwaangalia  watu wale waliomzidi umri yaani kwa macho yaliojaa hisia mchanganyiko.

“Mzee Dembe , Mzee Khu  na Madam Debo  nyie wote ni  wa kuheshimika katika  umoja wetu , Madam Debo  umekuwa ndani ya umoja kwa miaka ishirini  hadi sasa hivi kama sikosei ,lakini kwanini mkaamua kuongoza  kundi  la wasaliti , au ni kwasababu ya mimi kupewa uraisi  ndio maana hamjaridhika, ni lini nimewafanyia ubaya?”

“Dina  hatuwezi kusaliti Umoja wetu  ndio umetufikisha tulipo leo  hii , lakini kwanini  wewe ambae umekuja juzi tu  na  kulelewa  na kiongozi wetu aliepita upewe uongozi , mapenzi yetu kwa  huu umoja  ni zaidi ya  wewe , huu umoja  ni wa kwetu na sio wa kifamilia”

“Mlikuwa wapi kipindi cha machafuko, wakati  vijana wa umoja wetu wakiua watu  Kibiti na kulipwa na watu wenye  uroho wa madaraka mlikuwa wapi , wakati vijana wetu walivyoibuka na kujiita  Panyaroad na kuvamia watu hovyo, ni Babu ambae alituliza hii hali kwa kujitoa muhanga,  ni babu pekee ambae  aliona  hakuna mwenye uwezo wa kuongoza   umoja wetu  zaidi yangu”Aliongea Dina.

“Sikuwa hata na  tamaa ya kuwa kiongozi wa  Umoja  lakini  kutokana na  babu  kunibembeleza  niliishia kukubali  na tokea niingie kwenye uongozi sikuwahi  kujinufaisha mimi mwenyewe, zaidi ya kujitoa kuulinda umoja wetu ili usigawanyike”

“Haina haja ya kuongea   sasa hivi , tunajuaje  kama kweli maneno yako  ni ya kwei?”Aliongea Mzee Khu.

“Mmekuja Tanzania kufanya nini , kwanini sio kwenye kamisheni zenu  au mpango wenu ni kuigawanya Chatu?”

“Hatuna nia hio  Dina , tunachotaka kufanya ni kuhakikisha mtandao wa Chatu unarudi  kama mwanzo  na  ili hili kutimia  ni lazima  uondoke kwenye uongozi”

“Madam Debo  hebu  fikiria  kwanza mafanikio ya  raisi wetu tokea alivyoanza kuongoza  umoja, ni majuzi  tu  watu wasiokuwa na nia nzuri na umoja  wetu waliwalipa vijana  kujifanyisha ni Panyaroad  kwa kuwasambaza Tanzania nzima   na kuibua  taharuki ili kupata  sababu ya kuizima Chatu , lakini  Madam Dina kwa ujasiri wa hali ya juu aliweza  kusimama imara  na leo hii Umoja  umerudi katika  ubora wake , ni  maslahi kiasi gani ambayo unapata kupitia  mtandao wa chatu katika biashara zako, kwanini haya yote huyaoni   na unakubali kutumika?”Aiongea Lau.

“Lawrence wewe ni mtumwa wa Dina , una  hadhi gani ya kuongea  na sisi”Aliongea Debora  na Lawrence alitaka kuongea tena lakini alizuiwa na Dina.

“Nataka kujua  nini kimewafanya kuwa hivi , kwanini mnaona sifai  au ni kwasababu ya kumuadhibu  Zefa ambae alikuwa akienda kinyume na kanuni za umoja?”

“Huo ni mfano tu wa matumizi mabaya ya madaraka yako , kwanini  umemkatili vile mtoto  wa Chika  ambae  hana uhusiano wa moja kwa moja na umoja wetu?”

“Mzee Chika alimpa bichwa mtoto wake kutumia  nguvu yetu  kuleta madhara kwa watu wasiokuwa na hatia , jambo ambalo ni kinyume na  umoja wetu , Chatu ndio imemfikisha  Mzee Chika kushika  cheo alichokuwa nacho  polisi ,  lakini tofauti na kutoa mchango wa umoja  ana haribu taswira yake”

“Huna lolote Dina yule kakijana shombeshombe unaemlelea  ndio sababu  ya kumuua mtoto wa Afande Chika”

“Huyo mwanaume sio kakijana , unapaswa kumuonyeshea heshima la sivyo usinilaumu   kwa kitakachokutokea”

“Hahaha.. hatimae umeionyesha  rangi yako halisi , kwa mtu kama wewe kutojali kwanza familia yetu ya Chatu na kujali watu wa nje , tusipokuondoa katika uongozi  itafikia mahali hatutoishi kwa amani kwa kuhofia ndugu zetu”Aliongea  Mzee Milanzi.

“Kama  nia yenu ni kunitoa katika uongozi , basi jaribuni  kufanya hivyo”Aliongea Dina na palepale alipelekea mkono kiunoni , kundi lile mara baada ya kuona kitendo kile  walichukua tahadhari maana walikuwa wakijua uwezo wa  Dina kwenye kutumia visu.

“Dina usiwe  na  haraka , bado kuna  mtu muhimu hajafika “Aliongea Debora huku akiwa na  tabasamu  lililojaa ukejeli ndani yake.

Muda huo huo  baada ya kumaliza sentensi  mlango wa kuingilia ulifunguliwa na kuwafanya wote wageuze macho lakini walishangaa kuona mtu ambae walikuwa wakimtarajia sie..

“Hamza?”

“Bro!!”

Dina alimwangalia Hamza  kwa macho ya mshituko  wakati huo  Lau akimwangalia  Hamza kwa furaha , wengine wote ni kama vile walikuwa wakimjua Hamza hivyo kuwa na nyuso zilizojaa furaha.

Hamza alishika nywele zake za kizungu  kana kwamba  anakuna kichwa huu akizungusha macho kuangalia hali  halisi ilivyo.

“Imekuwa bahati nzuri  sikupata shida ya msongamano  wa magari na nimewahi kufika , Dina  vipi uko  sawa?”Aliuliza Hamza lakini  Dina alionekana bado alikuwa na hasira  na Hamza hivyo hakuendelea kumwangalia na aligeuza macho yake na kumwangalia  Lau.

“Lau  nilikwambia usimpigie , kwanini huelewi?”

“Madam , unaweza  kuniadhibu  utakavyo  tukisharudi , lakini mimi na  Bro  hofu yetu ni usalama wako tu”Aliongea Lau.

“Wewe si umesema hutaki kujiingiza katika maswala yangu , ondoka tu nitadili na hili mwenyewe”Aliongea Dina  akimwangalia Hamza.

“Dina  nimezoea kuja kwako kunywa chai  na chakula unachoniandalia , bila wewe unadhani nitakunywa wapi chai, siwezi kupotezea kama upo hatarini”

“Kwaho unataka kuja kwangu na kunywa na kula  bure tu maisha yako yote?”

“Ndio maana yake ,  kama hotonifukuza  nitaendelea kukutegemea   maisha        yagu yote”Alliongea Hamza akiwa na tabasamu na kumfanya  Dina kutabasamu.

“Alichoongea  Debora ni sahihi kabisa , hawa wanaonekana kuwa wapenzi, yaani wapo  hatarini lakini bado wanaongeleshana bila ya wasiwasi”

Sauti ilisikika ikitokea nje  huku ikifuatiwa na hatua za vishindo za viatu  na  hazikuwa  chache zilikuwa ni nyingi.

Mwanaume mwemmbaba  na mwenye macho 

yaliosinyaa  aliingia , alikuwa amevaa shati  la rangi ya maua maua  na koti la suti pamoja an jeans , nyuma yake  kulikuwa na  mabaunsa  zaidi ya kumi na mbili  na kila mmoja  alikuwa ameshikilia bastora.

Mara baada ya kuona kundi hilo la watu wakiwa na siraha ,  watu wa Dina walijikuta wakipauka kwa hofu.

Inaeleweka wazi kabisa  nchi ya Tanzania uhalifu  upo chini sana  tofautii na nchi kubwa kama  Italia , Japani na  China  na likija swala la umiliki wa siraha  kuna sheria ngumu mno  hivyo kufanya watu wachache  mno kuwa nazo.

Hivyo ni  ngumu kuona kundi la watu wakiwa wamebeba siraha  za moto kama hvyo , tena watu ambao sio watu wa usalama.

“Chika   hatimae umeweza  kufika ndani ya  muda , tulichokuwa tukisubiri ni  ujio wako tu wewe na Nasri”

“Haha.. Debora  umekuwa na jeuri sana , tokea uuokote utajiri hujawahi kuniita  kaka tena, saivi kwenye macho yako unaniona  mimi ni mdogo wako”Aliongea Afande   Chika, alikuwa ndio baba  yake Zefa.

Mwanamama Debora  na Afande  Chika walikuwa  ni ndugu wa damu. Miaka kadhaa nyuma mara baada ya Debora kuolewa na   mfanyabiashara wa  kutengeneza Bia kutoka Kenya aliukana  Uraia na rasmi akawa Raia  wa Kenya, baada ya  kifo cha mume wake  ndio alirithi kila  kitu chake na hatimae kuwa  moja ya wanawake  matajiri ndani ya  jiji la Nairobi.

Wakati wa kifo cha Tajiri Barasa kinatokea ,  ulitokea  uvumi  kwamba  tajiri huyo ameuliwa na  Debora kwa kushirikiana na  Samweli Mbilu  raisi  wa Tanzania anaemaliza muda wake,lakini uvumi huo haukuwa na ushahidi na ndani ya  miezi kadhaa ya  kuzikwa kwa Barasa  ulizima  wenyewe.

Nguvu ya Debora   ndani ya  mtandao wa Chatu  ilimuwezesha kumfanya  Afande Chika  kuwa  DCP(Deputy Commisioner of police).

Upande wa  Dina mara baada ya kuangalia watu waliongozana na  Mzee Chika  sura yake ilijikunja mno.

“Binamu  huna  haja ya kuniangalia kwa macho ya chuki hivyo , nimerudi nyumbani”Aliongea  bwana mmoja wa makamo mwenye umri  makadirio ya miaka kama  therathini na sita hivi kauli yake ikimlenga Dina.

“Nasri  nimekupeleka  Australia na  kila mwezi nakutumia  hela ya matumizi  ya kukutosha kufanya kila aina ya starehe , lakini  bado umepata ujasiri   na kuungana na maadui zangu na kujionyesha hapa?”Aliongea Dina  kwa hasira.

“Kwahio  utanifanya nini kama nimerudi , unadhani  naweza kuridhika kwa vichenchi ambavyo ulikuwa ukinitumia , huna undugu wowote na babu lakini akakupatia urithi na uongozi  usiostahili  , nimerudi  rasmi kupata haki yangu ya urithi”Aliongea  Nasri.

Hamza hakuelewa chochote kinachoendelea na alimwangalia Dina kwa kuhitaji maelezo. “Unakumbuka nishawahi  kukuambia  Chatu  ilikuwa ikifahamika kama Panyaroad  na  kwanini tuliamua kubadilisha jina?”Aliuliza  Dina na Hamza alikumbuka.

Kwa  maelezo ya Dina  ni kwamba  Panyaroad ulikuwa ni mtandao wa kimaslahi  ulioanzishwa chini  Tanzania  ,  mtandao huu ulianzishwa kwa lengo la  kufanya biashara  haramu ikiwemo  madawa ya kulevya ,  kuuza pembe za ndovu   na biashara nyingine ambazo sio halali.

Njia  ambazo zilikuwa zikitumika katika  kufanya biashara hii ziliitwa njia za Panya,  zilikuwa ni  njia za siri mno ambazo serikali  ilishindwa kudhibiti  njia hizi  katika kuingiza  na kusafirisha  bidhaa haramu.

Kutokana na biashara zisizohalali kupamba  moto  hatimae wafanyabiasha wengi waliongezeka  na

walihitaji kutumia  njia ya usafirishaji ya  Panyaroad  kuingiza  na kusafirisha biashara zao na hapa sasa Mzee Mninga  tajiri  mkubwa  ndani ya Tanzania na mwanzilishi wa Panyaroad alivyoona kutumia njia za Panyaroad kama fursa ya kujitengenezea pesa zaidi , alichokifanya  ilikuwa ni kutumia mdandao wake wa ki usafirishaji na  kuingiza na kutoa bidhaa nyingi za kimagendo na zile ambazo si halali  ikiwemo  madawa ya kulevya, vitu hivyo ambavyo alisafirisha vilikuwa vya   wafanyabiashara wengine yeye alikuwa akikusanya ada ya usafirishaji pekee  na  fursa hio ilimpatia hela nyingi mno kwa Tanzania , lakini hata hivyo hakutosheka ,  wahenga wanasema pesa mwanaharamu , hivyo alitengeneza mtandao mwingine wa usafirishaji katika mataifa  mengi ambayo  yanapakana  na Tanzania.

Ki ufupi ni kwamba matajiri wengi ndani ya nchi za  jumuia  ya  Afrika Mashariki na kati walinufaika na kutajirika sana  kupitia  mtandao wa usafirishaji huu uliopewa jina la Panyaroad.

Kwa lugha nyepesi Panyaroad ilikuwa ni kama kampuni ya kusafirisha bidhaa haramu  hilo ndio lilikuwa chimbuko lake.

Wahenga wanasema penye riziki hapakosi fitina  ndio kilichotokea miaka kadhaa  nyuma  kipindi cha uongozi  wa serikali  iliojaa  neema,  kulitokea tukio la vijana  wahalifu waliojiita Panyaroad na kuanza kushambulia  watu mitaani na kuwapora  mali.

Ukweli wa tukio hili ulitokea mara baada ya Tajiri Mninga  kukataa  kutoa sehemu ya umiliki  wa mtandao wa Panyaroad kwenda kwa  kiongozi mkubwa wa kisiasa ambae alikuwa akitumia  njia ya Panyaroad kwa muda mrefu kufanyabiashara hizo  haramu  na kutokana na hilo kiongozi huyo  akaanza kutumia nguvu yake ya kimadaraka kutoka kumiliki mtandao wote wa  Panyaroad kwa nguvu, kete ambayo  aliamua kucheza  ilikuwa ni  kutengeneza   Panyaroad watu ambao   ndio hao wahalifu walioanza kukata watu na mapanga na kupora.

Tajiri Mninga alikuwa ni moja ya watu ambao wana akili sana ukiachana na uwezo wake wa kifedha , asingekuwa na akili asingeweza kumiliki mtandao wa  usafirishaji katika mataifa  yote  yaliopo ndani ya ukanda wa Afrika mashariki nzima,  hivyo  ili kumshinda mwenye nchi  akaingia dili na moja ya kiongozi mkubwa kutoka  nchi jirani  na   mpango wa kuzuia mtandao wa Panyaroad usimilikiwe kimabavu ukasukwa, wakati huo huo Mninga  akamwahidi   kiongozi wa nchi ya jirani  kusafirisha  zana zote kwenda kwa Wazalendo waliokuwa wakipambania  maslahi ya  asili katika nchi ya jirani.

Kiongozi  wa nchi ya Jirani  ni mwenye uwezo mkubwa wa akili   na uwezo wake umeonekana kwa namna ambavyo aliitoa nchi yake katika umasikini  wa harufu ya damu mpaka  kuwa  moja ya nchi  yenye uchumi unaokuwa kwa kasi,  tena  nchi ikiwa  ina rasilimali  kidogo mno za  asili.

Tajiri Mninga  ili kuepuka makucha ya  mwenye  madaraka akahamisha makazi yake kwa muda na kwenda kuishi  nchini Denmark huku akilindwa na ulinzi mkali sana katika makazi yake , aliamua kujihamisha kutoka  Tanzania  kusubiria mpango wa  rafiki yake kutoka nchi ya jirani kukamilika  na kweli kila kitu kilienda sawa ,  akiwa nchini  Denmark alizipokea  taarifa za kukamatwa kwa  mtoto wa  adui yake  katika nchi ya Kimagnesiamu  akiwa na furushi la madawa ya kulevya  na kupelekwa jela.

Siku chache mbele Mninga alikabidhiwa   ushahidi uliokuwa  ukionyesha adui yake  kuuza rasilimali  za nchi kwenda  nchi ya Kimagnesiamu  kwa ajili ya kumuokoa mtoto wake  kuachiwa huru,  rafiki yake kutoka nchi ya jirani alimwambia autumie ushahidi huo  kurudisha  mtandao wake wa Panyaroad katika mstari na kuendeleza dili lao  la kusafirisha Zana kwenda nchi ya  Madini..

Mheshimiwa  mara baada ya kukaa kikao  na Mninga  hakutaka mambo yaende mbali alikubali masharti yote ya Mninga   ili siri yake kuendelea kubakia siri.

Mninga  mara baada ya  kurudisha  nguvu yake ndani ya mtandao  hakutaka kuzembea tena , aliamua kuweka mipango ambayo itaifanya mandao wake wa Panyaroad kujilinda  wenyewe  na katika mpango huo ndipo alipoamua kuitoa Panyaroad kutoka kuwa  kampuni ya usafirisjai wa bidhaa  haramu   na kuitengeneza  kuwa  Umoja  wa siri wa kimaslahi kwa kila mwanachama na alifanikiwa hilo kwa kuhusisha  watu wengi  serikalini  katika mataifa yote ambayo mtandao wake ulikuwa ukifanya  kazi.

Awamu ya uongozi wa neema nchini Tanzania ulipita na  ikaingia  awamu nyingine na hii ilimpa changamoto  kweli Mninga  kuendelea kuimarisha umoja wake   ndani ya Tanzania  kiasi ambacho  ilimfanya kuamua kupeana mkono na aliekuwa  adui  yake..

Tajiri Mninga katika kipindi hicho  alikuwa haamini

mtu kabisa , alikuwa na marafiki lakini  hakuwaamini  kwa asilimia  mia moja , wakati  anarudi  Tanzania kutokea Ulaya alirudi akiwa  na msichana mdogo ambae alimtambulisha  kama mjukuu wake , Msichana ambae alifahamika kwa jina la Dina.

Ukweli ni kwamba licha ya Dina kuwa kufahamika kama  mjukuu wa  tajiri Mninga lakini  pia alikuwa ni  mlinzi wake wa siri  na kupitia Dina majaribio mengi ambayo yalikusudiwa kumuua Tajjiri Mninga yalifeli kwani msichana huyo ukiachana na urembo wake alikuwa ni hatari mno likija swala zima la  mapigano   na kufanya watu kuwa na maswali ni wapi Mzee Mninga alikomtoa msichana huyo , lakini hata familia yake  hakuiweka wazi juu ya   wapi alikomtoa  Dina zaidi ya kusema kwamba  Dina ni mjukuu wake hivyo ni mwanafamilia ambae anapaswa kupata haki zote.

Jambo hilo  lilimfanya  Nasri  mjukuu wa tajiri Mninga kumchukia mno Dina  lakini licha ya chuki zake  hakuweza kumfanya chochote.

Licha ya tajiri Mninga kupeana mkono na adui wake wa Zamani lakini adui yake  alikuwa  akimchukia  kwa moyo wa dhati kabisa  na alijaribu kufanya mpango mwingine  wa kujimilikisha  mtandao wa Panyaroad  kwa kutaka kumtumia  mtangulizi wake , na ili kufanikisha hilo  akatumia  mbinu  nyingine katika moja ya  wilaya ndani ya pwani  , mbinu ambayo ilimwaga damu  lakini kwa bahati mbaya mpango ukafeli  lakini licha ya kufeli kwa mpango huo ilikuja kugundulika Nasri mjukuu wa Mzee Mninga alihusika  katika hilo  na hata majaribio ya mara kadhaa ya Tajiri Mninga kutaka kupoteza maisha ni Nasri  mjukuu wake ambae alihusika.

Mzee Mninga  baada ya  kuona familia yake ilikuwa haimtakii mema na hakuna ambae alikuwa na uwezo wa kuongoza mtandao mkubwa kama wa Chatu  ndipo alipompatia Dina mlinzi wake ambae aliamua kumfanya mjukuu kuwa kiongozi , jambo hilo lilikuwa  ni la kushangaza  kwa msichana mdogo kama Dina  kuwa  kiongozi na iliibuwa  migongano ndani ya umoja lakini  baadae  lilikuja  kukubalika na  Dina akawa kiongozi  rasmi.

Moja ya mfanikio makubwa ambayo Dina aliyapata tokea kufariki kwa babu yake  ni kudhibiti  tukio la mara ya pili  ambalo  lilifanywa na adui  wa babu yake  kwa  kutumia mbinu ileile ya Panyaroad , ilitumika miaka kadhaa nyuma , tukio hilo lilitikisa sana nchi ya Tanzania kiasi kwamba  mara baada ya Dina kufanikiwa kulizimisha aliamua kubadili   jina la mtandao wa Panyaroad  na kuubatiza jina la Chatu.

Maswala hayo yote tokea kuanzishwa  kwake kwa mtandao huu wa kimaslahi  mpaka kubadilika jina lake  ilikuwa ni siri  kabisa , ni swala ambalo lilikuwa likifanyika katika ulimwengu wa underwold.

Dina mara baada ya  Nasri ambae ni binadamu yake sasa  kuasi kundi kwa kumuua   tajiri  Mninga aliamua kumtoa nchini  kwenda kuishi nchini Australia huku akimtumia hela  ya matumizi  hakutaka  kumpa adhabu  kutokana na kwamba bado alikuwa  ni familia ya tajiri Mninga.

Sasa kitendo cha kuona Nasri akiwa ametangulizan ana Afande  Chika basi alijua  kuna  mpango unaendelea chini kwa chini na swala la Zefa  kupewa adhabu  sio sehemu bali ni  kisingizio  tu cha  kuficha mpango wa muda mrefu.

Hamza  na yeye sasa aliweza kuelewa, Hamza alikuwa akiujua ukubwa wa kundi hilo la Chatu  ndio maana hakutaka kujiingiza tokea muda mrefu , ki ufupi alijua Dina alikuwa na majukumu makubwa mno kuhakikisha operesheni za mtandao huo zinafanya kazi.

“Kwahio huyu ndio Nasri ambae alimuua  babu yake kwa kumtumia Daktari , ili  aweze kuwa kiongozi .. sasa  kama mtu unaweza kumuua babu yako wa damu,  unaweza vipi kuongoza   umoja wa mtandao wa  Chatu..”Aliongea Hamza.

“Acha kuongea ujinga , sikumuua babu mimi , huyo m*laya ametunga uongo  ili watu kumuamini , babu aliamua kumfanya kuwa mjukuu wake  akiwa hana hata familia  lakini akaamua kuulipa ukarimu wake na chuki ,  ndio ambae amenipokonya  urithi wangu kwa kusambaza uongo”

“Kama unachosema ni kweli kwanini  babu yako akaamua kumpatia Dina uongozi na sio wewe?”

“Kwasababu  alikuwa mzee  na  tayari uzee ulimfanya kuwa mjinga”

“Duuh ,  unadhani ni sahihi kumuita  marehemu babu yako mjinga?”Aliuliza Hamza na palepale  Nasri alijua ameongea ujinga na alibadilisha topiki haraka.

“Wewe shombeshombe , siku ya leo nimeisubiri kwa muda mrefu , tunakwenda kusafisha 

wasiohusika na umoja wetu moja kwa moja”Kauli ile ilimfanya Dina kutoa tabasamu na alipiga hatua mbili mbele.

“Kwahio  mmeamua kulea fujo kwasababu mmeshamrudisha  Nasri  kutoka Australia ,  hivi mnadhani kinachoufanya mtandao wa Chatu  kuendelea kuimarika  ni kwa kumrudisha Nasri?”

“Mnadhani huu umoja unaendeshwa kwa sheria za kifalme sio , kwamba kwasababu Nasri  anadamu ya Mzee Mninga anaweza  kuwa kiongozi , mnapaswa kujua  Nasri anatumika  tu na wanasiasa ambao wanataka kujimilikisha  mtandao  huu , mimi Dina  ikitokea  mmeleta  mtu ambae hana makando kando na wanasiasa  nipo tayari kuachia ngazi, lakini kama mnaleta hili shushu lenu ndio  liwe kiongozi  , hata mnikamue damu yangu mpaka tone la mwisho sipo tayari kukabidhi  uongozi”

“Dina  sio juu yako kuamua kuhusu hili , Nasri  ana sapoti  ya wazee kutoka  Congo , Rwanda, Kenya  na Uganda , na  tunaamini anaweza kurithi mikoba ya babu yake , usidhani  kwasababu ya kutaka kuleta fujo zako hapa unaweza  kufanikiwa”Aliongea Debora.

“Dina umesikia , mimi ni Nasri Mninga mtoto wa Mzee Rama Mninga nina damu ya Mzee  na babu  yangu , hivyo  mimi ndio mrithi halali , wewe ni  yatima  tu”

“Huna unachokijua  Nasri , babu hakuniachia uongozi kwasababu  ya damu yake , aliniachia  kuongoza kwasababu aliona ni mimi pekee ambae naweza kuendeleza alichokianzisha”Aliongea Dina na kisha alimgeukia Afande Chika”

“Afande Chika  naona umeamua kuungana na kundi  na kundi la kihalifu  na kuwakabidhi siraha za moto , huoni hili  likitoka nje ya hapa itakuwa skendo kwako?”

“Nyamaza wewe (tusi), unadhani  nimeaacha mlumbane kwasababu  sina cha kuongea , ulichomfanyia  kijana wangu leo nalipiza kisasi kwa kuondoa kiungo kimoja kimoja katika mwili wako”Aliongea Afande Chika ka hasira mno.

“Nilichokifanya  ni kumuadabisha  kijana wako kwa tabia zake   chafu baada ya wewe kutumia cheo chako kumkingia kifua, na siogipi vitisho vyako maana hutonifanya chochote , halafu wewe Nasri  muda mwingine  tumia hata akili za kuzaliwa , umakuja  na watu wamepewa siraha za moto  , hujui hili hata lina maana ngani ndani ya nchi kama Tanzania , huoni kwamba inatafutwa sababu ya  kuugawanya umoja wetu?”aliongea Dina kwa hasira.

“Dina  kama unaona woga wewe sema naona woga , acha  visingizio , maamuzi yashafanyika , tunajua uwezo wako wa kininja lakini mbele ya  chuma cha  moto  uwezo wako unafikia mwisho…haha”Aliongea  Nasri.

“Sikuwa na mpango wa kukuua kwasababu   ya uhusiano wako na babu lakini  naona   sina jinsi ,  ili

kufanikiwa kuendeleza alichokianzisha babu  inabidi niwaue wote na kurudisha amani katika  mtandao wetu”

“Sogea  utuue kama huo  uwezo unao , agizo langu  moja tu  hakuna ambae atabakia hai kwenye kundi lako”Baada  ya kuongea hivyo  Debora  na wenzake wote walisogea  nyuma ya wale  mabaunsa wenye siraha wakihofia  watapigwa risasi.

Dina upande wake aligeukia wale  watu wake aliokuja nao  waliokuwa na sura za kijeshi lakini  hawana siraha   kwa kuwathaminisha.

“Ndugu zangu leo  tunavita ya damu  na jasho  na adui yetu ana bunduki , kama mnaogopa kufa bila sababu mnaweza kuondoka ,  mkibaki  piganeni na mimi, naahidi  nitaenzi  utiifu  na uaminifu wenu maisha yangu yu yote”Aliongea Dina kwa nguvu. “Tupo tayari  kwa ajili yako  Raisi wetu”Aliongea Mmoja  wapo  wa  vijana wale na wengine wakafuatia.

“Utiiifu kwa raisi wetu Dina , vifo kwa wasaliti”Waliongea kwa nguvu   huku  wakionekana kuchangamka.

Dina mara baada ya kuona tukio hilo alijikuta akipatwa na hali ya msisimko , hakuamini  watu wake walikuwa wakimwamini hivyo.

Hamza upande  wake mara baada ya  kuona hali ilivyo alijikuta akivuta pumzi , ilikuwa ni kama  anakummbuka  matukio ya  nyuma ambayo

alishawahi kufanya  na muda ule alitoa tabasamu  lililojaa uovu ndani yake.

Lakini sasa kabla ya mtifuanno huo haujaanza simu ya Hamza   ya kichina ilianza kuita  kwa nguvu ,  mwito ulikuwa wa juu kiasi kwamba ulisababisha  watu wote kumwangalia.

Wale  maadui walimwangalia kwa waswwasi wakidhania pengine Hamza kuna kitu ambacho anapanga , kwanini simu kuia katika muda kama huo.

Hamza hakujali macho yao , aliingiza mkono mfukoni na kutoa simu na  kisha akaanza kuongea.

“Ndio , nimekuambia ni   kwenye kiwanda mwisho kabisa huku , ukikaribia utaona kuna magari mengi yameegeshwa nje , ukikaribia wewe  gonga  nitapokea”Aliongea Hamza na kisha akakata simu.

“Ulikuwa ukiongea na nani?”Aliuliza Dina.

“Niliagiza chakula  kwenye Bar moja hapo ,  nina njaa  sio  ya kawaida , hawa watu ambao  wanataka kukuua  wasubiri kwanza nishibe, ni kheri kufa ukiwa umeshiba kuliko kufa na njaa”Aliongea  Hamza.

Kauli yake iliwaacha mdomo wazi kila mtu aliekuwa hapo ndani na hata wale wa upande wa  uadui.

“Haha… Dina  umewakataa vibopa wengii  lakini leo hii umekuja kupenda  mpuuzi kama huyo, ambae anataka kushiba kwanza ndio ashuhudie kifo chako”Aliongea  Nasri kwa kejeli.

Upande wa Dina alikuwa kwenye mawazo , ijapokuwa matendo ya Hamza yalichekesha  lakini upande mwingine ilionyesha  kwa kiasi gani hakuwa na wasiwasi juu ya hatari iliokuwa mbele yake.

Dakika chache tu  mtu wa  delivery alifika na Hamza mara baada ya kusikia mlango ukigonghwa alikimbilia  na kwenda kuufungua.

“Bro  mbona magari mengi hivi hili eneo ,  kazi zinafanyika hadi usiku??”Aiongea yule kijana  mara baada ya kumkabidhi  Hamza parcel  ya chakula na baada ya pale  kwa umbea  aliingiza kichwa ndani na kupiga chabo na alijikuka akikamaa mwili mara baada ya kuona watu wakiwa na  bunduki na alimwangalia Hamza kwa hofu.

“Dogo usiwe na wasiwasi  tunashoot  filamu ya kimapigano ,  hizo bunduki ni za  risasi za plastiki”Aliongea Hamza,

“Kumbe ,  aisee  kwa hizo bunduki zinavyoonekana kama za ukweli naamini   litakuwa bonge la muvi, lakini kwanini wengine hawana bundiki wamebeba  mapanga na virungu?”Aliuliza   bwana huyo  ambae alikuwa na rafudhi  yake  ya watu wa kanda ya ziwa. “Dogo  inamaana kwenye  muvi hujawahi kuona  watu wanapambana na mapanga?”

“Nimeona bro”

“Nadhani sasa umeelewa , hii ni pesa yako  chenchi utakunywa soda”Aliongea Hamza akimkabidhi  na bwana yule alipokea  na badala ya kuondoka alisogea pembeni akitaka kuangalia.

“Dogo  wewe  nenda kaendelee na mishe zako , hii filamu utaoiona wakati wa kutoka “

“Nitajie basi hata jina  ili  ikitoka niwe wa kwanza  kuicheki?”

“Itakuwa inaitwa Ngumi ya uzalendo”

“Poa Bro nasubiria kwa hamu zote”Aliongea na kisha  aliruhusiwa kuondoka na Hamza alifunga mlango wa geti kwa ndani.

Hamza mara  baada ya mtu wa delivery kuondoka alitembea mpaka kwenye  bodi ya trella la gari   na kukaa chini.

“Dina  nimeagiza   nyama ya mbuzi ya kukaanga na ndizi , njoo tule , usafi  umezingatiwa”Aliongea Hamza huku akishika  toothpick vizuri akibeba vipande vya ndizi.

“Wewe endelea tu , sina njaa”

“Kama wew huna njaa basi  sina haja ya kuwakaribisha wengine , nisubirini  dakika  chache nimalize kula haraka mambo mengine yaendelee”

Nyama zile zilikuwa nyingi mno  na zililikuwa zikitoa harufu nzuri mno kiasi kwamba  watu  walikuwa washasahau      kilichokuwa kikiendelea               na kumkodolea Hamza kwa macho ya uroho.

“Bro wewe malizia chapu tuwashughulikie hawa  wasaliti”Aliongea Lau mara baada ya  Hamza kumpa ishara ya kusogea kujiunga nae lakini  akakataa huku akivaa gloves zake  nyeusi vizuri.

“Lau  ijapokuwa  umekunywa sana damu ya  mbwa mwitu  lakini  huwezi kushindana na risasi”Aliongea Nasri.

“Achana na mimi Nasri”Aliongea Lau kwa hasira , walikuwa  marafiki  hapo mwanzo kabla ya kuhitalafiana.

“Alichosema Nasri ni sahihi , Lau tunaujua uwezo wako , kama upo tayari kujisalimisha  tutakuacha uendelee kuwa  na  sehemu yako ndani ya umoja”Aliongea Debora lakini Lau alimpotezea.

“Afande Chika kama unataka kuendelea kuwa   na cheo ndani ya jeshi la polisi  ondoka na watu wako  na washauri na wengine waache uhasama tutahakikisha mnaendelea kupata maslahi  ndani ya mtandao”

“Acha kuongea ujinga , sisi ndio wenye siraha  za moto na unaongea ujinga , Lau  nakushauti umshauri  bosi wako Dina   akubali kujisalimisha  kuliko  kumwaga damu zenu ambazo hazina hatia”

“Hayo ni mawazo yako , nipo tayari kwa ajili ya  Madam muda wowote ,  kama sio yeye  ningekuwa gerezani sasa hivi , kwangu  tokea siku ile  ni Madam alienipatia nafasi ya  mara ya pili ya kuishi . sio mimi tu kila mmoja upande wetu amepitia  changamoto nyingi ambazo  Madam amesaidia sana kuzitatua , kwetu sisi  Madam  ni wa kwanza kabla ya nafsi zetu” “Master Lau  tupo tayari kukufauta  na kumlinda Madam”Wengine wote walimuunga mkono   kwa sauti  na  muda uleule   wale wanaume  mabaunsa waliokuwa   na  bunduki walisogea mbele na kukoki  siraha zao kuelekea  kundi  la Dina huku wakiwa wamezifunga  viwambo vya kuzuia sauti.

“Bro’s  kwa ajili ya umoja wetu  ni muda wa kupambana kwa ajili ya kiongozi wetu”Aliongea  Lau kwa nguvu  akisogea   mbele bila hofu.

Lakini muda huo huo kivuli kilisogea  mbele kwa spidi ya ajabu , alikuwa ni Dina  mwendo wake ulikuwa sio wa kawaida hata kidogo  na alikuwa  akijongea kama vile ni  nyoka aina ya Cobra aliekuwa ameinua shingo yake juu.

“Swiii.. Swiii!!!”

Nyota mbili zenye makali kama ya kisu zilifyatuliwa na  Dina  na kabla ya  wale   mabaunsa wenye bunduki hawajainua siraha zao   walikuwa washatobolewa kwenye mapaji ya  nyuso zao na kudondoka chini.

Debora na wenzake waliofika   hapo  ambao hawakuwa wakijua nini maana ya   uninja walijikua wakitetemeka kwa hofu.

“Acheni kushangaa  mnasita nini mshambulieni asiwasogelee”Aliongea kwa nguvu  Chika maana wale mabaunsa  ni kama  wamezubaa na baada ya  kuambiwa hivyo walishituka.

“Tuutu , tuuu  , tuuu”

Kitendo cha   wale watu kuanza  kushambulia  Dina hakutaka kufanya  uzembe aliruka sarakasi na kwenda kutua  kwenye kabati la chuma kulia kwake. “Ding , Ding !!”

Sauti ya risasi kugongana na chuma ndio iliosikika , kilichowasaidia watu wa upande wa Dina ni kwamba walikuwa wamesimama upande wenye  magari na  mashine za vyuma.

Kitu kilichompa  ahueni  Dina ni mara baada ya kuona wale mabausa  licha ya  kuwa na bunduki lakini hawakuwa na uwezo wa kulenga ikimaanisha  walikosa mafunzo.

“Wasogeleeeni  kwa spidi , hawana  mafunzo ya kutumia bunduki”Aliuongea  Lawrence kwa nguvu lakinin kabla hata hawajachukua hatua  Hamza aliwazuia kwa mbele.

“Bro!!”Aliongea  Lau asijue   Hamza  anataka kufanya nini.

“Hamza acha kusimama mbele  utashambuliwa na risasi”Aliongea Dina ambae alikuwa amejificha nyuma ya chuma.

Kwasababu Hamza alikuwa mbele basi risasi yoyote ingeanza kumpata yeye kabla ya wengine.

“Huwa inaleta faraja ukipigana huku ukiwa umeshiba ..”Aliongea Hamza.

“Bro Hamza  najua uwezo wako ni mkubwa  lakini usiwe  na  haraka  watakupasua  na risasi , tushambulie kwa pamoja kuwapunguzia umakini” “Haina haja”Aliongea Hamza.

“Kwanini?”

Lakini Hamza alikuwa ashaondoka mbele yake na ile anakuja kurudi  alimuwekea  Hamza lile boksi ililokuwa na chakula ndani yake.

“Nishikie     chakula       changu sijashiba      vizuri bado”Aliongea  na kisha akasogea mbele , kila mtu alimshangaa hata Dina mwenyewe alikuwa  kwenye  mshangao na alitamani kwenda kumzuia  lakini aliogopa             akijitokeza bila plan             wataanza kushambulia.

Upande wa Nasri   na Afande Chika hawakuwa na wasiwasi kabisa , walishajua vita ni yao hivyo walikuwa wakisubiri wajitokeze washambulie  , sasa baada ya kuona Hamza anawasogelea bila ya wasiwasi   walijikuta wakimshangaa.

“Huyu mpuuzi kweli ni  kichaa”Aliongea Nasri akimwangalia Hamza.

“Mshambulieni kabla hajawafikia”sauti ilisikika kwa nguvu na muda huo sauti ya risasi kugongana na  vyuma zilianza kusikika  kama mvua nyingine zikimsogelea Hamza.

Lakini kitu cha ajabu ni kama Hamza alikuwa akiwasoma mawazo  na matendo  yao   ya mikono , kwani  alianza kukwepa kwa namna  flani hivi kama anacheza  mziki na kila risasi iliomfikia iliweza  kumpita , haikuwa spidi ya kawaida  kwa binadamu hata kidogo.

Wale mabaunsa walijikuta wakishikwa na mshangao wa  uwezo  usiokuwa wa kawaida wa Hamza na walipaniki na kuanza kurusha risasi haraka haraka.

Ilikuwa ni kufumba na kufumbua Hamza alikuwa mbele yao  huku  baadhi  risasi zikiwaishia  na walimwangalia kama vile wamekutana na  Israeli mtoa roho.

Hamza hakutaka hata kuwapa nafasi ya kufikiria  amewafikiajena kwa kutumia toothpick tatu

alizisukumizia zote  katika  koo la  moja ya baunsa  na  ni damu tu zilizoanza kutoka.

“Pumbavu ,muueni haraka”Alipiga kelele Nasri mara baada ya kuona moja ya watu wake ashadondoka na anatapatapa akitokwa na damu  eneo la shingoni.

Kitu cha ajabu  kilitokea muda uleule wale  mabaunsa walijikuta wakimwangalia Hamza bila ya kumfanya chochote , ilikuwa ni kama wanamshangaa  lakini haikuwa hivyo   viungo vyao vya  mwili ni kama vilikuwa vimeshikiliwa  na kitu   na kufanya  wasiweze kufanya chochote , Hamza kwa kutumia vidole viwili  aliwapitia kwa spidi na kuwaangusha mmoja baada ya mwingine na ndani ya  dakika moja  wote waliokuwa na bunduki walikuwa wamekufa wengine wakipoteza fahamu.

Mzee Dembe  alijikuta midomo yake ikicheza cheza kama anakifafa asiamini kile anachoona mbele yake.

Wale wa upande wa  Dina mara baada ya tukio  lile waliwahi bunduki na kuwasogelea wale wazee walioongoza usaliti  na  kuwalenga.

“Msije kufyatua, subiri kwanza”Debora alikuwa ndio  wa kwanza kujihami  huku Afande Chika  akiwa haeleweki alikuwa  katika hali ya namna gani zaidi ya kumwangalia Hamza tu kwa mshangao.

Hamza mpango wake ni kudhibiti waliokuwa na  bunduki pekee  na hilo lilifanikiwa ndani ya dakika moja tu.

Dina aliekuwa amejificha alijikuta akisimama kwa mshangao  usiokuwa na kifani , ilkuwa ni mara yake ya kwanza kuona tukio la namna hio.

“Dina nimekuondolea hatari tayari , ni juu yako kudhibiti waliobaki  , hakikisha huleti huruma”Aliongea Hamza na kisha alinawa mikono  kwa maji ya bomba  kwenye tanki  na kisha alimsogelea  Lau na kuchukua chakula chake na kuendelea  kula.

Dina  aliishia kumwangalia Hamza  tu   na haikueleweka mrembo huyo alikuwa akifikiria nini.

Mwanzoni alikuwa akijua  Hamza  ni mtu mwenye uwezo wa hali ya juu wa kimapigano lakini  hakujua kama  ni zaidi ya alichoweza kuona.

Yaani mtu ameweza kutoguswa  na risasi  nyingi namna hio   na kisha kuua  karibia  watu wote waliokuwa na  bunduki  tena kwa kutumia vidole  tu na toothpick.

Unapaswa kuelewa mtu wa kawaida  akinyooshewa bunduki  atahisi  woga  wa hali ya juu  na ataishia kunyoosha mikono juu kujisalimisha  , lakini kwa mtu kama Hamza alikuwa na  uwezo wa kuona  risasi itapita wapi na  ni kipi afanye , mbinu hio ilihitaji kiwango kikubwa cha  kudhibiti saikolojia  na uwezo  wa  ajabu.

“Lau huyu  bwana  siku nyingi nilikuwa

nikikudharau kumpa heshima , lakini  inaonekana  ulikuwa ukimjua  nje ndani , huu uwezo alionyesha sio wa kawaida”

“Sijawahi kushuhudia  binadamu wa hivi, nadhani kuna siri , Lau hebu tuambie  unadhani huyu  jamaa ni wa kawaida?”

“Hebu acheni kuongea ujinga ,  Bro Hamza anaweza asifurahi  akisikia juu ya hili”

Hamza hakujali kama alikuwa ameua mtu , hamu yake ya kula haikumpotea kabisa ,  kwa namna moja ama nyingine  usingedhani huyu ni Hamza ambae   wiki kadhaa nyuma au mwezi alionekana kuwa mzembe , haikujulikana kulikuwa na siri gani anaficha , lakini ilikuwa ni dhahiri  hakuwa  kiumbe wa kawaida, alikuwa ni kama roboti.

Kulingana na sheria  za  umoja wa  Chatu wasaliti  walipaswa kuuliwa mara mmoja 

“Nasri  ulipanga  mauaji ya kumuua Babu  na nikakusamehe na leo tena ukakubali kutumiwa na kufanya usaliti , leo  hakuna msamaha zaidi ya kifo”Aliuongea Dina  mara baada ya kurudi katika hali yake ya kawaida.

Nasri aliwaangalia  mabaunsa waliobaki ambao walikuwa ni  sehemu ya mtandao wa Chatu.

“Okoteni bunduki mumshambulie”Aliongea  Nasri kwa nguvu lakini hata afande  Chika  hakuwa na nguvu ya kunyanyua bunduki ,  alikuwa akimwangalia Hamza kwa hofu kubwa mno   huku akifikiria namna  ya  kujiokoa.

Wale  mabodigadi tofauti na kumtii  Nasri wote walipiga magoti chini wakiomba kusamehewa , kitendo kile kilimfanya Hamza aliekuwa akitafuna nyama kutoa tabasamu.

Walitoa kila sababu ya kujitetea na kwa bahati nzuri  Dina hakutaka kuua watu wengi  usiku huo , isitoshe wengi wao walikuwa wakifuata maagizo, waliokuwa wamebakia ni  Mzee Dembe , Debora ,  Balozi Khumeriana  na Afande  Chika  pamoja na Nasri.

“Yoyote ambae  yupo tayari  kupiga magoti  na  kuahidi  utiifu na  uaminifu kwangu , nitamtoa katika kundi la  wanaokufa leo hii”Aliongea.

“Dina  hebu fikiria kwanza , unadhani  sisi  pekee ndio tumeamua kufanya usaliti , unadhani silaha kama hizi  katika  taifa  kama Tanzania tungezipata wapi?”Aliongea Debora kwa sauti na Dina aliendelea kuwasogelea taratibu taratibu.

“Hiuna haja ya kuongea chochote , najua  ambaye  yupo nyuma yenu  ni Samweli Mbilu hawala wako wa muda mrefu”Aliongea  Dina  na kumfanya  Debora kutoa macho.

“Wewe umejuaj….?”

“Unadhani  kwasababu nafanya kazi ya kuuza chai  sijui  nani ni adui yangu na nani ni rafiki yangu , unadhani  mtandao wa chatu ni  kuitwa kiongozi tu, Nasri  unadhani  kwanini  babu aliniamini na kunipatia uongozi , ni kwasababu  akili yangu ishatoka nje ya boksi muda mrefu , kukupeleka Australia  haikumaanisha sifuatiliii unachokifanya kila siku , vikao vako na balozi wa  Tanzania nchini   Australia  nilikuwa nikipata ripoti ya kila mnachozungumza”Aliongea  Dina.

“Sikutaka kukuchukulia hatua tu kwasababu ya  undugu wa damu na Mzee Mninga , lakini leo hii umevuka mpaka tena  ulichonikasirisha zaidi ni kukubali kutumiwa na Raisi Mbilu ili  ajimilikishe  mtandao wetu”Aliongea kwa hasira na  palepale Nasri mara baada a kusikia hivyo  alijikuta akilainika na alijikuta akipiga magoti  bila ya kupenda.

“Cousin ,  cousin  kwasababu mimi ni ndugu yako naomba  unisamehe , sito…”

Kabla hata hajamaliza sentensi yake kisu tayari kishatoboa paji la uso wake  na   kudondoka chini  akitoa  macho.

Tukio lile liliwafanya waliobaki kutetemeka mno na aliekuwa wa kwanza  kupiga magoti  alikuwa ni Afande Chika na wakafuatia wengine.

“Madam , mimi Chika   nimefanya  mengi  yasiostahili kwa kutumia madaraka ya cheo changu na kuumiza watu wengi , nakiri makosa yagu naomba  uyasamehe  maisha yangu , mimi na

Debora  tupo  kukupaia siri ili  utusamehe”

“Siri gani hio  ambayo  inaweza kulingana na  uhai wenu”Aliongea  Dina  huku akimkazia macho mwanamaa Debora.

Chika alimwangalia mdogo wake kwa kumpa ishara amwelezee   Dina lakini upande wa Debora alionekana kuwa na wasiwasi.

“Mpango   wa kuudhoofisha  mtandao wa  Chatu  haujasukwa na  Samweli”Aliongea  Debora huku akiwa na wasiwasi.

“Kama sio Samweli ni nani mwingine mwenye madaraka ya kuwapatia mpaka siraha kwa ajili ya kunishambulia?”

“Kuna watu wapo nyuma yake”Aliongea  Debora na kisha alimpa ishara Dina kusogea karibu  na palepale alimnong’oneza jambo, kitendo kile kilimfanhya  Hamza aliekuwa  mbali kuongeza umakini  kwa Debora asije kuwa na hila.

“Wahusika  wakuu  ni  watu kutoka  Binamu Island”Aliongea Debora na kauli ile ilimfanya  Dina kushangaa kidogo na palepale tabasamu la uovu lilimtoka  na kufumba na kufumbua  Debora aliguswa shingoni  na kudondoka chini kama furushi. “Debora..!!”

Afande Chika aliishia kushikwa na hofu   akidhania  mdogo wake Debora ashapoteza maisha.

“Sijamalizana na nyie bado”Aliongea na kisha aimgeukia Lau.

“Lau  wapelekwe Chimbo , Adhabu yao ya usaliti itafuatia baada ya kukutana na Mbilu”

Previoua Next