SEHEMU YA 40.
Masaa kadhaa nyuma Kanali Dastani alikuwa ashaachiwa huru na kitengo cha MALIBU na sasa alikuwa akiingia ndani viunga vya Ikulu.
Katika kipindi chote akiwa amezuiwa hakuwa na wasiwasi kabisa , kutokana na kwamba alikuwa na ukaribu na Mheshimiwa Raisi lilikuwa swala la muda kutolewa ndio maana hata wakati wa mahojiano hakutaka kuongea chochote akijaribu kupoteza muda.
Amosi Undercover Agent wa kitengo cha MALIBU ambae alipewa jukumu la kumfanyia mahojiano Kanali Dastani alijikuta akiwa katika wakati mgumu.
Kosa kubwa ambalo lilimfanya Kanali Dastani kuwa kizuizini ni mara baada ya kumuingiza Amosi katika hatari kwa kumpeleka katika mikono ya Tresha Noah ninja kutoka kisiwa cha Binamu.
Dastani alimhadaa Amosi kwa kumwambia taarifa ambayo anaitaka juu ya uchunguzi wa kifo cha mwanamke aliehusishwa katika kesi ya radi atapata pa kuanzia kwa kupata faili kutoka katika moja ya mtu ambae anaabudu uchawi yaani Wiccan.
Lakini ule ulikuwa mtego ambao Dastani alimwekea Amosi na kwa bahati mbaya mtego wake haukunasa kama ambavyo alikuwa ametarajia , yalikuwa ni makosa upande wa Tresha na mwenzake kwa kushindwa kumdhiibiti Amosi kikamilifu.
Moja ya maagizo ambayo yalimfanya Amosi kusaga meno kwa hasira ni mara baada ya kuambiwa amuachie Kanali Dastani huru , na maagizo yametoka kwa mkuu wa nchi.
Amosi aliona kabisa kuna kitu ambacho Dastani anajua kuhusu kesi ya Radi lakini hakuwa tayari kuweka wazi , kilichomchanganya zaidi Amosi alishindwa kujua ni upande gani ambao Dastani yupo , hakuelewa kama Dastani alikuwa upande wa jamhuri au watu wa Binamu.
Ushahidi wa kumfungamanisha na upande wa
Binadamu pia haukupatikana na kwasababu Afande Doswe mkuu wake alimpa masaa ishirini na nne pekee ya kumhoji Dastani, baada ya kupokea simu kumuachia huru , muda pia ulikuwa umeisha hivyo alijikuta akiwa hana jinsi na kufanya wakubwa zake wanachotaka kufanya.
“Kanali hili halijaisha , nilikuamini sana lakini ukautumia uaminifu wangu kwako vibaya , iwe sasa hivi au muda wowote nitakukamata na ushahidi na ikifika huo wakati ama zako ama zangu”Aliongea Amosi mara baada ya kuingia katika chumba cha mahojiano na kumruhusu Kanali kuondoka.
“Amosi najua wewe ni mtu ambae unafuata sheria , hili swala tushindane sisi wenyewe bila ya kutumia watu wetu wa karibu , ukinishinda nitakubali kushindwa nikikushinda kubali kushindwa pia”Aliongea Kanali Dastani mara baada ya kuwa huru.
“Taarifa za kuipeleka familia yako sehemu salama nimezisikia , lakini umenishusha hadhi yangu sana kudhania nitatumia familia yako ili kukubana, Mimi Amosi , licha ya kuonekana jambazi na mbwa wa vigogo, lakini mimi ni mzalendo wa kweli na mapemzi yangu kwa Taifa hili ndio kitu kinachonipa nguvu ya kushindana na watu mafisadi kama wewe”Aliongea Amosi kwa hasira na Dastanni alitoa tabasamu.
“Ni kama nilivyokuwazia Amosi , umeweza kuishi undercover kwa muda mrefu bila kugundulika , inaonyesha ni kwa kiasi gani una uwezo wa juu , lakini uwezo wako umeshindwa kuelewa kitu kimoja , mimi pia naipenda nchi yangu na kila ninachofanya ni kwa maslahi ya nchi hii , hakuna kingine njia zetu tu ndio zinatofautiana”Aliongea na baada ya hapo alitoka katika chumba hicho.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa baina ya Amosi Jasusi wa siri wa serikali na Kanali Dastani mfanyakazi wa upelelezi kitengo cha MALIBU.
Siku chache zilizopita Amosi alikuwa akiripoti operesheni zake zote za kiuchunguzi kwa Dastani , lakini baada ya Dastani kumuingiza katika mtego waligeuka kuwa mtu na bosi wake na sasa ni mahasamu ambao walikuwa wakijivunia kwa kuipenda nchi yao.
Ukweli ni kwamba haijalishi kati yao nani mkweli , Amosi alionekana kuipenda hela , huku Dastani akiwa na matendo ambayo yalimfanya kutokueleweka yupo upande gani.
Kwa muda mrefu sana iliaminika serikali ya Tanzania ilikuwa ikiongozwa kwa mkono wa watu wa kisiwa cha Binamu , licha ya kwamba ushahidi huo hakuwa wazi , lakini ni jambo la kuwezekana kwa taifa dogo kutawaliwa na watu wenye nguvu ya hali ya juu kutoka kisiwa cha Binamu.
Kanali Dastani hakujali ahadi ya Amosi zidi yake
, kitendo cha kuiwa ikulu , ilimaanisha
Mheshimiwa alikuwa na swala nyeti la kuzungumza nae na yeye kama jasusi mpelelezi alipenda changamoto.
Baada ya kukaguliwa na kutii itifaki zote za awali kabla ya kuingia katika ofisi ya Raisi , hatimae alipokewa na katibu Muhtasi Maulidi Bakari.
“Mheshimiwa anakusubiri Kanali”Aliongea Maulidi mara baada ya kutoa taarifa ujio wa Kanali.
Dastani hakuwa na mshangao sana , alikuwa amefika Ikulu mara nyingi mno na kama ni kuonana na raisi ameonana nae sana tu katika kazi mbalimbali ambazo aliaminiwa na mheshimiwa Samweli Eliasi Mbilu.
“Haina haja ya kukaa chini Kanali”Aliongea Mheshimiwa akimzuia Dastani asikae kwenye kiti.
“Nimeitikia wito mheshimiwa”Aliongea Dastani, kitendo cha kukatazwa kukaa chini moja kwa moja alijua Mheshimiwa hajaridhika na matokeo yake.
“Dastani kwanini umekosa umakini mpaka unaingia katika Rada za TISA?”Aliuliza .
“Mheshimiwa sikutegemea kama mpango wa kumuondoa Amosi kwenye kufatilia ungefeli?” “Hata kama mpango wa kwanza ulifeli , ulipaswa kuwa na mpango B , kwanini umekuwa mzembe kwenye kitu kidogo namna hii , kitendo cha kufeli kumuua Amosi moja kwa moja mmempatia kinga”Aliongea na kumfanya Kanali kushangaa kidogo.
“Mheshimiwa unamaanisha nini kuhusu Kinga?”
“Huna clearence ya kujua kinachoendelea , ila kwanzia sasa Amosi hapaswi kuguswa tena , kuna watu wapo nyuma yake na sio Wabrazili wanaotaka uchunguzi wa kesi ya radi uendelee, kuna wenye nguvu zaidi , Wabrazili walikuwa ni kivuli tu”Aliongea na kauli hio ilimfanya Kanali paji lake la uso kutoa jasho.
“Mheshimiwa kipi ambacho natakiwa kufanya , sijawhai kudhania kuna watu wenye nguvu zaidi ya watu wa Binamu?”
“Binamu ni sehemu ya wavamizi tu na wanachojivunia ni teknolojia, unadhani wanaweza kuwa na nguvu kushinda nchi kubwa duniani, wao ili waendelee kuwepo wanahitaji sapoti kutoka kwao hivyo wakipewa oda wanatii mara moja bila ya maswali”
“Mheshimiwa napaswa kufanya nini juu ya hili?”
“Hutakiwi kufanya kitu Kanali , nimekuita kwa kazi nyingine kabisa, sijaridhika na matokeo yaliopita , ila kwenye hili la pili sitaki uzembe”Aliongea na kisha alitoa faili na kumpatia Amosi.
Amosi mara baada ya kushika faili hilo na kufungua ndani alikuta ni ripoti ambayo aliwasilisha kwa Brigedia Doswe kabla ya kuingia kizuizini kwa ajili ya mahojiano.
“Hio ripoti nadhani wewe ndio umeifanyia kazi , inakosa baadhi ya vitu lakini haihitaji kuongezewa kitu , unachopaswa ni kuondoka na jina moja tu la huyo Hamza Mzee na kish….”Aliongea Mheshimiwa na alimalizia kwa kuweka vidole shingoni akimaanisha Hamza auwawe na jambo lile lilimpa mushikeli Kanali.
“Mheshimiwa lakini uchunguzi haujakamilika na hakuna uhakika wa Hamza kuhusika” “Unadhani nimekuagiza hivyo kwasababu ya watu waliokufa Zinga, sihitaji hata kujua kwanini walikufa , Hivi Dastani unanichukuliaje , unadhani kwasababu nastaaafu na akili imestaafu”
“Hapana mheshimiwa najaribu kuwa makini , ana uhusiano na bosi wa kampuni ya Dosam , ikitokea amekufa swala hili haliwezi kuwa rahisi kupita”
“Ndio maana unachotakiwa ni kuhakikisha kifo chake kinakuwa cha kawaida kabisa, ikishindikana kumuua kwa kifo cha kawaida , tumia mbinu yoyote ili mradi nisikie habari za msiba”Aliongea Mheshimiwa, kanali alitaka kupinga lakini mheshimiwa alimpa ishara ya kutoka ofisini kwake.
Baada ya Kanali Dastani kutoka palepale mheshimiwa alinyanyua simu yake na kuitafuta namba na kupiga.
“Gabusha , huna haja ya kuwa na wasiwasi tena , kazi nimempatia kijana ninaemuamini , amefanya kazi za namna hii kwa muda mrefu”Aliongea Mheshimiwa.
“Hahaha… Mbilu wewe ni rafiki yangu ,sikudhania ungenizingatia kwa muda mchache hivi”
“Huna haja ya kunishukuru katika hili Gabusha, wewe na Benjamini wote mnataka matokeo ya aina moja na natumia shida zenu kama matofali ya kujenga ngome yangu kabla ya kutoka Ikulu”Aliongea huku akiwa na tabasamu lililojaa kejeli usoni.
“Haha… kama unatumia shida zetu kama matofali ya kujenga ngome yako , vipi upande wako , mpango wako wa kuumiliki mtandao wa Chatu umekwama?”
“Hakuna utofauti kati yetu , nilichofanya ni kuazima kibiriti kuuwasha moto , huyu kijana anaonekana kuwa na maadui wengi na hakuna namna akipoteza maisha tukio lake linaweza kuunganishwa kwangu”Aliongea.
“Ni kweli na sidhani ana famili ya kuweza kutusumbua , hata mahusiano yake na Regina yanaonekana kutokuwa siriasi , kama ni hivyo asingejichanganya na kuingia kwa Eliza”Aliongea. “Ukimzungumzia Eliza , najua kabisa hili swala linahusiana na maswala yako ya utajiri wa majini , Gabusha ninaemjua hawezi kuhangaikia mwanamke muda mrefu”
“Mbilu tusiende mbali, usiku ndio umeingia , nataka kuimaliza siku vizuri”Aliongea upande wa pili na kumfanya Raisi Mbilu kutoa tabasamu la kejeli.
“Wapuuzi nyie ,mpango wangu ukifanikiwa na ikatokea kuna makosa kila kitu nitawaangushia na baada ya hapa nitadili na Mstaafu lazima nimtoe kwenye ramani , anajikuta wa mjini ila hana lolote, Bilioni tisini kwa mwezi kila kitu kitakuwa changu haha..”Hayo ndio yalikuwa mawazo yake, alikuwa na miezi michache sana ya kumaliza muda wake , hakuwaza tena raia alikuwa akiwaza maisha baada ya kustaafu.
*******
Ilikuwa ni wakati ambao wanaingia katika makutano ya barabara inayoingia bandarini , licha ya kwamba magari ya upande wa kulia kwao yalikuwa yamesimamishwa kwa taa nyekundu ya kuongozea magari , lakini gari la mizigo lilikuwa katika spidi , ilikuwa ni kama vile gari yao ndio ilikuwa ikisubiriwa ingie katika makutano yale.
Hamza akili yake ilikuwa imecheza haraka na aliweza kujua sio kama dereva amekosea bali ni kitendo cha kukusudiwa.
“Eliza simamisha gari”Aliongea Hamza kwa nguvu na kumfanya Eliza ashituke.
“Simamisha gari pembeni usipite”Aliongea Hamza na sasa mara baada ya Eliza kuelewa alichokuwa akimaanisha Hamza alikuwa amechelewa kwani alikuwa tayari katika usawa wa gari lile kubwa na lilikuwa likisogea kwa spidi kubwa mno na kosa ni kwamba Eliza alisimamisha gari akiwa katikati ya barabara.
“Ahhhhh…!!”
Elliza alijikuta akifumba macho mara baada ya kukishuhudia kifo chake mwenyewe , lakini ndani ya sekunde tatu tu kabla ya gari ile ya Toyota hajafikiwa Hamza alikuwa ashamfungua Eliza mkanda tayari na kufungua mlango upande mwingine, kutokana Eliza alikuwa amekanyaga breki tayari Hamza alifanikiwa kuchoropoka akiwa amemshikilia Eliza na kwenda kutua pembeni ya barabara.
Dereva wa gari lile kubwa la mizigo mara baada ya kuona waliokuwa ndani ya gari wametoka upande mwingine haraka sana alizungusha usukani na kulikwepa na aliishia kuharibu mlango wa kulia wa gari.s
Licha ya kwamba eneo lile ilikuwa ni sehemu ya kuelekea upande wa bandarini na kulikuwa na giza lakini daladala ambayo ilikuwa ikishusha abiria pembeni yao waliweza kushuhudia lile tukio na wanawake walipiga makelele wakiamini vifo vya ajali vinakwenda kutokea..
Hamza mpaka anakwenda kumshusha Eliza chini , alikuwa ashapoteza fahamu tayari, ni kama alipoteza fahamu kabla hata ya kugongwa.
Upande wa Hamza hakuwa na hofu kabisa kwenye macho yake , na aliishia kumshikilia vizuri Eliza ambae alikuwa ni kama mtoto aliepakatwa.
Lakini cha ajabu ni kwamba mkono wake wa kushoto ulikuwa ukicheza kwa kulenga lile gari na ilikuwa ni kitendo cha haraka sana baada ya dereva kukwepesha kugongana na gari yao , lilipinduka lile gari na kulitokea mshindo mkubwa mno ambao ulimtoa Eliza katika usingizi.
Eliza alijikuta akishituka kwa nguvu na woga ulimvaa lakini Hamza alimtuliza.
“Usiwe na wasiwasi , hujaumia”Aliongea Hamza kumtuliza ,
Eliza alitamani kutoa kilio kwa nguvu , mwili wake ulianza kumtetemeka , lakini alishindwa kabisa kulia zaidi ya macho kuwa mekundu.
Sekunde chache zilizopita aliamini anakwenda kupoteza uhai moja kwa moja , lakini miujiza imetokea na amepona.
Muda uleule watu walikuwa washajazana kuzunguka eneo la tukio na walijikuta wakiwa katika bumbuwazi baada ya kugundua waliokuwa ndani ya gari washatoka nje , kila mtu alihisi ni kama anaona picha isio na uhalisia na kujiuliza wametokaje.
Hamza hakujali watu waliokuwa wakimuuliza maswali na alitembea mpaka kwenye gari lile kubwa na kisha alifungua mlango uliopondeka kwa juu na kutaka kumchoropoa yule dereva lakini mara baada ya kuangalia kwa umakini aligundua dereva yule hana uhai na cha kushangaza zaidi alikuwa ameshikilia bastora iliofungwa kiwambo cha kuzuia sauti , alionekana kujiua mwenyewe na palepale akili ya Hamza ilicheza , tukio hilo alithibitisha lilikuwa ni la kupangwa.
“Assassin…”Hamza alijikuta akimwemwesa midomo yake huku akijiuliza nani ambae alitaka kumuua.
Aliamini tukio hilo alilengwa yeye , kama ingekuwa Eliza basi angesubiriwa akiwa peke yake na ingekuwa rahisi zaidi.
“Bro upo sawa , huyu dereva anapaswa kunyongwa , anaendeshaje gari kwa ukichaa namna hii”
“Pigieni simu polisi, aisee hawa watu wanabahati mno , nilijua tunaokota maiti”Watu waliokuwa wamezunguka walianza kuongea wao kwa wao huku wakimwangalia Hamza na Eliza kwa macho ya mshangao , hawakuamini kama wamepona katika tukio hilo.
Upande wa Hamza hakujali swala la polisi kufika hapo, kwasababu hisia mbaya zilishamvaa , aliwaza kama mpango huo wa kuuwawa umepangwa na familia ya James basi Regina na yeye atakuwa kwenye matatizo.
Alikumbuka tukio la James kufika kwenye kampuni akiwa na yule mzee anaejua mapigano kwa kutumia vidole na kengele ya hatari ilizidi kugonga.
Haraka sana alichukua simu yake na kumpigia Regina lakini simu iliishia kuita bila kupokelewa , alijaribu mara ya pili ilikuwa vilevile simu haipokelewi.
Hamza hakuamini kama kumuacha Regina peke yake kwa siku moja tayari ashapatwa na matatizo , hakutaka kuchelewa aliamua kumpigia shangazi simu na hakuwa hata na salamu.
“Shangazi , Regina amerudi?”
“Alipiga simu muda wa saa kumi na moja na kusema atachelewa kurudi mpaka sasa hivi hajarudi bado”Aliongea shangazi na Hamza palepale alihisi hatari na alikata simu na kumsogelea Eliza ambae amezungukwa na watu.
“Eliza panda daladala urudi nyumbani kwanza , naenda makao makuu mara moja”Aliongea Hamza
Gari ya Eliza licha ya kwamba haikuharibika sana , lakini haikuwa ikiendesheka tena.
“Unamaanisha bosi…”Eliza alijikuta akipatwa na mshituko na Hamza alitingisha kichwa na bila ya kusema neno alitimua nduki kama kichaa na kufanya watu kumshangaa na wengine walihisi labda tukio limemchnganya.
Spidi ya Hamza kukimbia haikuwa ya kawaida kabisa , kilichoonekana ni kivuli, kwani alikuwa ni kama vile anaibukia sehemu na kupotea tena anaibukia sehemu nyingine na kupotea.
Ilimchukua dakika kumi tu kutoka makutano ya barabara ya kuingia bandarini mpaka mawasiliano yalipo makao makuu ya kampuni.
Mara baada ya kufika mbele ya geti la kampuni alikutana na mlinzi ambae alimzuia lakini mara baada ya kuona ni Hamza alishangaa kidogo.
“Mkurugenzi ashaondoka?”Aliuliza Hamza.
“Sidhani , sijamuona akitoka , wewe si msaidizi wake?”Aliuliza Jamali , alikuwa akimjua Hamza vizuri.
Hamza mara baada ya kusikia hakutaka kuhangaishana na maneno na mlinzi huyo na alifyatuka mbio kuingia ndani ya jengo hilo na mara baada ya kufika katika floor ya juu na kuingia kwenye korido aliweza kuona floor hio taa zilikuwa zikiwaka na alitembea kwa haraka na kuingia ndani na aliweza kumuona Regina.
Alikuwa ameshikilia karamu na alikuwa bize akifanya kazi , sasa mara baada ya kusikia mlango kufunguliwa kwa nguvu alijikuta akikunja ndita lakini mara baada ya kuona ni Hamza , ndita ziliongezeka zaidi.
“Umerudi kufanya nini tena?”
Hamza hakutaka hata kumsikiliza na alitembea mpaka kwenye meza yake na kuitafuta simu na mara baada ya kuangalia aliweza kuona Missed call zake.
“Kwanini hukupokea simu?”Aliuliza Hamza kibabe , sauti yake haikuwa ya kawaida kabisa , kwa Regina alihisi ni kama sio Hamza anaeongea na alikuwa akitoa msisimko ambao ulimuogopesha Regina.
“Sikuwa na sababu ya kupokea simu yako”Aliongea kwa jeuri.
“Kwahio unapokea simu ukiwa na sababu , kwanini unakuwa mjeuri hata kwenye mambo ya msingi?”
“Kama ulikuwa na cha kuongea ongea , kwani ni sheria kupokea simu yako kila ukinipigia?”
Kauli ile ilimkasirisha mno Hamza , kila akikumbuka alivyoruka viunzi mpaka kufika hapo ndio hasira zake zilimvaa na tabasamu la ajabu lilimvaa na kuanza kuzipiga hatua kuzunguka meza akimsogelea Regina.
Regina mara baada ya kuona namna ambavyo Hamza yupo siriasi alishindwa kujizuia na kuanza kujawa na hofu..
“Wewe unataka kufanya nini.. usinisogelee”Alipiga makelele lakini Hamza hakumjali tena na palepale alimbeba juu juu kumtoa kwenye kiti na kumlaza kifudifudi juu ya meza.
“Arghhh… wewe mshenzi niache , niache, mamaa..”Regina alikuwa akifurukuta kwa kurusha miguu lakini mbele ya Hamza hakuwa na nguvu za kumshinda.
“Pah!
Kilichosikika ni mtu kupigwa vibao vya makalio na jambo hilo lilimfanya Regina kujawa na hasira na aibu kwa wakati mmoja.
Kama Dokta Flora Ronicas ana miaka sitini na sita unadhani Hamza ana mingapi , kwanini tukio la radi liliuwa familia ya mwanamke kule Sumbawanga linafichwa sana , kuna siri gani.
Comments