Reader Settings

SEHEMU YA 40.

Masaa kadhaa nyuma Kanali Dastani alikuwa ashaachiwa huru na kitengo cha MALIBU na sasa alikuwa akiingia ndani  viunga vya  Ikulu.

Katika  kipindi chote akiwa amezuiwa hakuwa na wasiwasi  kabisa , kutokana na kwamba alikuwa na ukaribu   na Mheshimiwa Raisi  lilikuwa swala la muda  kutolewa  ndio maana hata wakati wa mahojiano hakutaka kuongea chochote akijaribu kupoteza muda.

Amosi  Undercover Agent wa kitengo cha MALIBU ambae  alipewa jukumu  la kumfanyia  mahojiano  Kanali Dastani alijikuta akiwa katika wakati mgumu.

Kosa kubwa ambalo lilimfanya Kanali Dastani kuwa kizuizini  ni mara baada  ya kumuingiza Amosi katika  hatari kwa kumpeleka katika mikono ya   Tresha  Noah ninja kutoka kisiwa cha Binamu.

Dastani  alimhadaa  Amosi  kwa kumwambia  taarifa  ambayo anaitaka juu ya  uchunguzi  wa  kifo cha mwanamke  aliehusishwa katika  kesi ya radi  atapata pa kuanzia kwa kupata faili kutoka   katika moja ya mtu ambae anaabudu uchawi yaani Wiccan.

Lakini ule ulikuwa mtego  ambao   Dastani alimwekea  Amosi  na kwa bahati  mbaya mtego  wake haukunasa kama ambavyo alikuwa ametarajia , yalikuwa ni makosa upande wa Tresha na mwenzake kwa kushindwa kumdhiibiti Amosi kikamilifu.

Moja ya  maagizo ambayo yalimfanya Amosi  kusaga meno kwa hasira ni mara baada ya  kuambiwa  amuachie  Kanali Dastani huru , na maagizo yametoka kwa mkuu wa nchi.

Amosi aliona kabisa  kuna kitu ambacho Dastani anajua kuhusu kesi  ya Radi  lakini hakuwa tayari kuweka wazi , kilichomchanganya zaidi Amosi alishindwa kujua  ni  upande gani ambao Dastani  yupo , hakuelewa kama Dastani alikuwa upande wa jamhuri au watu wa Binamu.

Ushahidi wa kumfungamanisha na upande wa

Binadamu pia  haukupatikana  na kwasababu  Afande Doswe  mkuu wake alimpa masaa ishirini na nne pekee ya kumhoji  Dastani, baada ya kupokea simu kumuachia huru , muda pia ulikuwa umeisha hivyo alijikuta akiwa  hana jinsi na kufanya wakubwa zake wanachotaka kufanya.

“Kanali  hili halijaisha , nilikuamini sana lakini   ukautumia uaminifu wangu kwako vibaya ,  iwe sasa hivi au muda wowote  nitakukamata na ushahidi  na ikifika  huo wakati  ama zako ama zangu”Aliongea Amosi  mara baada ya kuingia katika chumba cha mahojiano na kumruhusu Kanali kuondoka.

“Amosi najua wewe ni mtu ambae unafuata sheria , hili swala  tushindane sisi wenyewe bila ya kutumia  watu  wetu wa karibu ,  ukinishinda nitakubali kushindwa  nikikushinda  kubali  kushindwa  pia”Aliongea  Kanali Dastani   mara baada ya kuwa huru.

“Taarifa za kuipeleka familia yako  sehemu  salama  nimezisikia , lakini umenishusha hadhi yangu sana kudhania  nitatumia  familia yako ili  kukubana, Mimi Amosi , licha ya kuonekana  jambazi na mbwa wa vigogo, lakini mimi ni mzalendo wa kweli  na  mapemzi yangu kwa Taifa hili  ndio kitu kinachonipa  nguvu ya kushindana na watu   mafisadi kama wewe”Aliongea Amosi kwa hasira  na Dastanni  alitoa tabasamu.

“Ni kama  nilivyokuwazia  Amosi ,  umeweza kuishi  undercover  kwa muda mrefu bila  kugundulika , inaonyesha ni kwa kiasi  gani  una uwezo wa juu , lakini  uwezo wako umeshindwa kuelewa kitu kimoja , mimi pia naipenda nchi yangu  na kila ninachofanya ni kwa maslahi ya nchi hii , hakuna kingine njia zetu tu ndio zinatofautiana”Aliongea  na baada ya hapo alitoka katika  chumba hicho.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa   baina ya Amosi Jasusi  wa siri wa serikali  na Kanali Dastani  mfanyakazi  wa upelelezi kitengo cha MALIBU.

Siku chache zilizopita Amosi alikuwa akiripoti operesheni zake zote za kiuchunguzi kwa Dastani , lakini baada ya Dastani kumuingiza katika  mtego  waligeuka kuwa mtu na bosi wake na sasa ni mahasamu ambao walikuwa wakijivunia  kwa kuipenda nchi yao.

Ukweli ni kwamba  haijalishi kati yao nani mkweli , Amosi  alionekana kuipenda hela , huku  Dastani akiwa  na matendo ambayo  yalimfanya kutokueleweka yupo upande gani.

Kwa  muda mrefu sana  iliaminika  serikali ya Tanzania  ilikuwa ikiongozwa  kwa mkono wa   watu wa kisiwa cha Binamu , licha ya kwamba ushahidi  huo  hakuwa wazi , lakini  ni jambo la  kuwezekana  kwa taifa dogo kutawaliwa na  watu wenye  nguvu ya hali ya juu  kutoka kisiwa cha Binamu.

Kanali Dastani hakujali  ahadi ya  Amosi  zidi yake

, kitendo cha kuiwa ikulu , ilimaanisha

Mheshimiwa alikuwa na  swala nyeti la kuzungumza nae  na yeye kama  jasusi mpelelezi alipenda changamoto.

Baada ya kukaguliwa na kutii itifaki zote za  awali kabla ya kuingia katika ofisi ya Raisi , hatimae alipokewa na katibu Muhtasi Maulidi Bakari.

“Mheshimiwa anakusubiri  Kanali”Aliongea  Maulidi  mara baada ya kutoa taarifa ujio wa  Kanali.

Dastani hakuwa na mshangao sana , alikuwa amefika Ikulu mara nyingi  mno na kama ni kuonana na raisi  ameonana nae sana tu katika kazi mbalimbali ambazo aliaminiwa na mheshimiwa  Samweli Eliasi Mbilu.

“Haina haja ya kukaa chini Kanali”Aliongea Mheshimiwa  akimzuia   Dastani  asikae kwenye kiti.

“Nimeitikia wito mheshimiwa”Aliongea Dastani, kitendo cha kukatazwa  kukaa chini moja kwa moja alijua Mheshimiwa  hajaridhika na matokeo yake.

“Dastani kwanini umekosa umakini mpaka unaingia  katika  Rada za TISA?”Aliuliza .

“Mheshimiwa sikutegemea kama   mpango wa kumuondoa  Amosi  kwenye kufatilia  ungefeli?” “Hata  kama mpango wa kwanza ulifeli , ulipaswa kuwa na mpango B , kwanini  umekuwa mzembe kwenye  kitu kidogo  namna hii , kitendo  cha kufeli   kumuua Amosi  moja kwa moja mmempatia kinga”Aliongea na kumfanya Kanali kushangaa kidogo.

“Mheshimiwa unamaanisha nini kuhusu Kinga?”

“Huna clearence ya kujua kinachoendelea , ila  kwanzia sasa Amosi  hapaswi  kuguswa tena , kuna watu wapo nyuma yake  na sio  Wabrazili wanaotaka uchunguzi  wa  kesi ya radi uendelee, kuna wenye nguvu zaidi , Wabrazili walikuwa ni kivuli  tu”Aliongea na kauli hio ilimfanya  Kanali paji lake   la uso  kutoa jasho.

“Mheshimiwa  kipi ambacho natakiwa kufanya ,  sijawhai kudhania  kuna watu wenye nguvu zaidi ya  watu wa Binamu?”

“Binamu ni sehemu ya wavamizi tu na  wanachojivunia ni teknolojia, unadhani  wanaweza kuwa  na nguvu kushinda   nchi kubwa duniani, wao ili waendelee  kuwepo wanahitaji  sapoti kutoka kwao hivyo  wakipewa oda wanatii mara moja  bila ya maswali”

“Mheshimiwa napaswa kufanya nini juu ya hili?”

“Hutakiwi kufanya kitu Kanali , nimekuita kwa kazi nyingine kabisa, sijaridhika na matokeo yaliopita , ila kwenye  hili  la  pili sitaki  uzembe”Aliongea na kisha alitoa faili  na kumpatia Amosi.

Amosi mara baada ya kushika faili hilo na kufungua ndani alikuta  ni ripoti ambayo  aliwasilisha kwa Brigedia Doswe kabla  ya kuingia kizuizini kwa ajili ya mahojiano.

“Hio ripoti  nadhani wewe ndio umeifanyia kazi , inakosa baadhi ya vitu  lakini haihitaji kuongezewa  kitu , unachopaswa ni kuondoka na jina moja tu  la huyo Hamza Mzee  na kish….”Aliongea  Mheshimiwa na  alimalizia kwa kuweka vidole shingoni akimaanisha  Hamza auwawe na jambo lile lilimpa  mushikeli  Kanali.

“Mheshimiwa  lakini uchunguzi haujakamilika  na hakuna uhakika  wa  Hamza kuhusika” “Unadhani  nimekuagiza hivyo kwasababu ya  watu waliokufa Zinga, sihitaji  hata kujua  kwanini walikufa , Hivi Dastani unanichukuliaje , unadhani kwasababu  nastaaafu  na akili imestaafu”

“Hapana mheshimiwa  najaribu kuwa makini ,  ana uhusiano  na  bosi wa kampuni ya Dosam , ikitokea amekufa  swala hili haliwezi kuwa rahisi kupita”

“Ndio maana  unachotakiwa  ni kuhakikisha kifo chake kinakuwa  cha kawaida  kabisa, ikishindikana  kumuua kwa kifo cha   kawaida ,  tumia mbinu yoyote  ili mradi nisikie  habari za msiba”Aliongea Mheshimiwa, kanali alitaka  kupinga lakini mheshimiwa alimpa ishara ya kutoka  ofisini kwake.

Baada  ya  Kanali Dastani kutoka palepale mheshimiwa alinyanyua simu yake  na kuitafuta namba na kupiga.

“Gabusha , huna haja ya kuwa na wasiwasi tena , kazi nimempatia kijana ninaemuamini  , amefanya kazi  za namna hii kwa  muda  mrefu”Aliongea Mheshimiwa.

“Hahaha… Mbilu  wewe ni rafiki yangu ,sikudhania  ungenizingatia  kwa muda mchache hivi”

“Huna haja ya kunishukuru  katika hili  Gabusha, wewe na Benjamini wote mnataka   matokeo ya aina moja  na  natumia  shida zenu kama matofali ya kujenga  ngome  yangu kabla ya kutoka Ikulu”Aliongea huku akiwa na tabasamu lililojaa kejeli usoni.

“Haha…  kama unatumia shida zetu kama matofali ya  kujenga ngome yako  , vipi  upande wako , mpango wako wa kuumiliki mtandao wa Chatu umekwama?”

“Hakuna utofauti kati yetu  , nilichofanya ni kuazima kibiriti kuuwasha moto , huyu kijana anaonekana kuwa na maadui wengi  na hakuna namna  akipoteza maisha  tukio lake linaweza kuunganishwa kwangu”Aliongea.

“Ni  kweli na sidhani  ana famili ya kuweza kutusumbua , hata mahusiano yake na Regina yanaonekana kutokuwa siriasi ,  kama ni hivyo asingejichanganya na  kuingia kwa   Eliza”Aliongea. “Ukimzungumzia Eliza , najua kabisa  hili swala linahusiana na maswala yako ya utajiri wa majini , Gabusha ninaemjua  hawezi kuhangaikia mwanamke muda mrefu”

“Mbilu tusiende mbali, usiku ndio umeingia , nataka kuimaliza siku vizuri”Aliongea upande wa pili na  kumfanya  Raisi Mbilu kutoa tabasamu la kejeli.

“Wapuuzi  nyie ,mpango wangu ukifanikiwa na ikatokea kuna makosa kila kitu nitawaangushia na baada ya hapa nitadili  na Mstaafu lazima nimtoe kwenye ramani , anajikuta wa mjini  ila hana lolote, Bilioni  tisini kwa mwezi kila kitu kitakuwa changu  haha..”Hayo ndio yalikuwa mawazo yake, alikuwa na miezi michache sana ya kumaliza muda wake , hakuwaza tena raia alikuwa akiwaza maisha baada ya kustaafu.

*******

Ilikuwa  ni wakati  ambao wanaingia  katika  makutano ya barabara inayoingia bandarini  , licha ya kwamba magari ya upande wa kulia kwao yalikuwa yamesimamishwa  kwa taa nyekundu ya kuongozea magari , lakini gari la mizigo lilikuwa katika spidi , ilikuwa ni kama vile gari yao   ndio ilikuwa ikisubiriwa ingie katika makutano yale.

Hamza akili yake ilikuwa  imecheza haraka na aliweza kujua  sio kama dereva amekosea bali ni kitendo cha kukusudiwa.

“Eliza simamisha gari”Aliongea Hamza  kwa nguvu na kumfanya Eliza ashituke.

“Simamisha gari pembeni usipite”Aliongea  Hamza  na  sasa mara baada ya Eliza kuelewa alichokuwa akimaanisha   Hamza alikuwa amechelewa kwani  alikuwa  tayari katika usawa wa  gari lile kubwa  na  lilikuwa likisogea kwa spidi kubwa mno na kosa ni kwamba Eliza alisimamisha  gari akiwa katikati ya barabara.

“Ahhhhh…!!”

Elliza alijikuta akifumba macho mara baada ya kukishuhudia kifo chake mwenyewe , lakini   ndani ya sekunde tatu tu kabla ya gari ile ya Toyota hajafikiwa Hamza alikuwa ashamfungua Eliza mkanda  tayari  na kufungua mlango upande mwingine,  kutokana  Eliza alikuwa amekanyaga breki  tayari Hamza alifanikiwa kuchoropoka akiwa amemshikilia Eliza na kwenda kutua  pembeni ya barabara.

Dereva wa gari lile kubwa la mizigo mara baada ya  kuona  waliokuwa ndani ya gari  wametoka  upande mwingine  haraka sana alizungusha usukani  na kulikwepa  na aliishia  kuharibu mlango wa kulia wa gari.s

Licha ya kwamba eneo lile ilikuwa ni sehemu ya kuelekea upande wa bandarini  na kulikuwa na giza lakini  daladala ambayo ilikuwa ikishusha  abiria pembeni yao  waliweza kushuhudia lile tukio na wanawake walipiga makelele wakiamini  vifo vya ajali vinakwenda kutokea..

Hamza mpaka anakwenda kumshusha Eliza chini , alikuwa ashapoteza fahamu tayari, ni kama alipoteza fahamu kabla hata ya kugongwa.

Upande wa Hamza hakuwa na hofu kabisa kwenye macho yake , na aliishia kumshikilia vizuri  Eliza ambae alikuwa ni kama mtoto aliepakatwa.

Lakini  cha ajabu ni kwamba  mkono wake  wa kushoto  ulikuwa ukicheza kwa kulenga  lile gari  na ilikuwa ni kitendo cha haraka sana baada ya dereva kukwepesha  kugongana na gari yao ,  lilipinduka lile gari  na kulitokea  mshindo mkubwa mno  ambao ulimtoa  Eliza katika usingizi.

Eliza alijikuta akishituka kwa nguvu na woga ulimvaa lakini Hamza alimtuliza.

“Usiwe na wasiwasi , hujaumia”Aliongea Hamza kumtuliza ,

Eliza alitamani kutoa kilio kwa  nguvu , mwili wake ulianza kumtetemeka , lakini alishindwa kabisa kulia zaidi ya macho kuwa mekundu.

Sekunde chache zilizopita aliamini anakwenda kupoteza uhai  moja kwa moja , lakini miujiza imetokea na amepona.

Muda uleule watu walikuwa washajazana kuzunguka  eneo la tukio  na walijikuta wakiwa  katika bumbuwazi  baada ya kugundua  waliokuwa ndani ya gari washatoka nje , kila mtu alihisi ni kama  anaona picha isio na uhalisia  na kujiuliza wametokaje.

Hamza hakujali watu waliokuwa wakimuuliza maswali  na alitembea mpaka kwenye gari lile kubwa na kisha alifungua mlango  uliopondeka kwa juu na kutaka  kumchoropoa  yule dereva lakini mara baada ya kuangalia kwa umakini aligundua dereva yule hana uhai na  cha kushangaza zaidi alikuwa ameshikilia bastora iliofungwa kiwambo cha kuzuia sauti , alionekana kujiua mwenyewe   na palepale akili ya Hamza ilicheza , tukio hilo alithibitisha  lilikuwa ni la kupangwa.

“Assassin…”Hamza alijikuta  akimwemwesa midomo yake  huku akijiuliza nani ambae alitaka kumuua.

Aliamini   tukio hilo alilengwa yeye , kama ingekuwa Eliza  basi  angesubiriwa akiwa peke yake na  ingekuwa rahisi zaidi.

“Bro upo sawa , huyu dereva  anapaswa kunyongwa , anaendeshaje gari  kwa ukichaa namna hii”

“Pigieni simu polisi, aisee  hawa watu wanabahati mno , nilijua  tunaokota maiti”Watu waliokuwa wamezunguka walianza kuongea wao kwa wao huku wakimwangalia Hamza  na Eliza kwa macho  ya  mshangao , hawakuamini kama wamepona katika tukio  hilo.

Upande wa Hamza hakujali swala la polisi kufika hapo, kwasababu hisia mbaya zilishamvaa , aliwaza kama   mpango huo wa kuuwawa umepangwa na  familia ya James basi  Regina na yeye atakuwa kwenye matatizo.

Alikumbuka tukio la   James kufika kwenye kampuni akiwa na yule mzee anaejua  mapigano kwa kutumia vidole  na  kengele ya hatari ilizidi kugonga.

Haraka sana alichukua simu yake na kumpigia  Regina lakini  simu iliishia kuita  bila kupokelewa , alijaribu mara ya pili  ilikuwa vilevile simu haipokelewi.

Hamza hakuamini  kama kumuacha  Regina peke yake kwa siku moja tayari ashapatwa na matatizo , hakutaka kuchelewa aliamua kumpigia shangazi simu na hakuwa  hata na salamu.

“Shangazi , Regina amerudi?”

“Alipiga simu  muda wa saa kumi na moja na kusema  atachelewa kurudi  mpaka sasa hivi hajarudi bado”Aliongea shangazi na Hamza palepale  alihisi hatari na alikata simu  na kumsogelea  Eliza  ambae amezungukwa na watu.

“Eliza panda daladala urudi nyumbani kwanza ,   naenda  makao  makuu  mara moja”Aliongea Hamza 

Gari ya   Eliza licha ya kwamba haikuharibika sana  , lakini haikuwa ikiendesheka tena.

“Unamaanisha bosi…”Eliza alijikuta akipatwa na mshituko na Hamza alitingisha kichwa   na bila ya kusema neno alitimua nduki kama kichaa  na kufanya watu kumshangaa na wengine walihisi labda  tukio limemchnganya.

Spidi ya Hamza kukimbia  haikuwa ya kawaida  kabisa ,  kilichoonekana ni kivuli, kwani alikuwa ni kama vile anaibukia sehemu na kupotea tena  anaibukia sehemu nyingine na kupotea.

Ilimchukua dakika kumi tu kutoka  makutano ya barabara ya kuingia bandarini  mpaka  mawasiliano yalipo makao makuu  ya kampuni.

Mara baada ya kufika  mbele ya geti la kampuni alikutana na mlinzi ambae alimzuia  lakini mara baada ya  kuona  ni Hamza alishangaa kidogo.

“Mkurugenzi ashaondoka?”Aliuliza Hamza.

“Sidhani , sijamuona akitoka , wewe si  msaidizi wake?”Aliuliza Jamali  , alikuwa akimjua Hamza vizuri.

Hamza mara baada ya kusikia hakutaka kuhangaishana na maneno na mlinzi huyo na alifyatuka mbio kuingia ndani ya jengo hilo  na mara baada ya kufika katika floor ya juu  na kuingia kwenye korido aliweza kuona floor hio taa zilikuwa zikiwaka na alitembea kwa haraka na kuingia ndani  na aliweza kumuona Regina.

Alikuwa ameshikilia  karamu na alikuwa bize akifanya  kazi , sasa mara baada ya kusikia mlango kufunguliwa kwa nguvu  alijikuta akikunja ndita  lakini mara baada ya  kuona ni Hamza , ndita ziliongezeka zaidi.

“Umerudi kufanya nini  tena?”

Hamza  hakutaka hata kumsikiliza na alitembea mpaka kwenye meza yake na  kuitafuta simu  na mara baada ya kuangalia   aliweza kuona Missed call zake.

“Kwanini hukupokea simu?”Aliuliza  Hamza kibabe , sauti yake haikuwa  ya kawaida kabisa ,  kwa Regina alihisi ni kama  sio Hamza anaeongea  na alikuwa akitoa  msisimko ambao ulimuogopesha Regina.

“Sikuwa na sababu ya kupokea simu yako”Aliongea   kwa jeuri.

“Kwahio unapokea simu ukiwa na sababu , kwanini unakuwa mjeuri   hata kwenye mambo ya msingi?”

“Kama ulikuwa na cha kuongea ongea ,  kwani  ni sheria kupokea simu yako kila ukinipigia?”

Kauli ile ilimkasirisha mno Hamza , kila akikumbuka alivyoruka viunzi mpaka kufika hapo ndio hasira zake zilimvaa  na tabasamu la ajabu lilimvaa  na kuanza kuzipiga hatua kuzunguka meza akimsogelea Regina.

Regina mara baada ya kuona  namna ambavyo Hamza yupo siriasi  alishindwa kujizuia na kuanza kujawa na hofu..

“Wewe unataka kufanya nini.. usinisogelee”Alipiga makelele  lakini  Hamza hakumjali tena  na palepale alimbeba  juu juu  kumtoa kwenye kiti na kumlaza kifudifudi juu ya meza.

“Arghhh… wewe mshenzi niache , niache, mamaa..”Regina alikuwa akifurukuta  kwa kurusha miguu lakini mbele ya Hamza hakuwa na nguvu za kumshinda.

“Pah!

Kilichosikika ni mtu kupigwa vibao  vya makalio  na  jambo hilo lilimfanya Regina  kujawa na hasira na aibu kwa wakati mmoja.

Kama  Dokta Flora Ronicas  ana miaka  sitini na sita unadhani Hamza ana mingapi , kwanini tukio la  radi liliuwa familia ya  mwanamke kule Sumbawanga linafichwa sana , kuna siri gani.

Previoua Next