SEHEMU YA 41.
Regina alijikuta akishindwa kuamini Hamza amemkandamiza kifudifudi kwenye meza na kuanza kumpiga makofi ya makalio, alijitahidi kufurukuta lakini alishindwa kabisa na vibao viliendelea kumshukia , Hamza aliona huyu mwanamke hataki kupokea simu yangu huku akisema hana sababu sasa vibao hivyo vitampa sababu ya kutopokea simu yake.
“Ongea , siku nyigine utapokea simu yangu au hutopokea?”Aliongea Hamza lakini upande wa Regina aliishia kung’ata meno huku akivumilia maumivu.
“Pah!”
Kitendo cha kuendelea kuleta ujeuri na kutojibu ilimfanya Hamza kumuongezea vibao , lakini hata kama aliyasikia maumivu kiasi gani , hakuwa tayari kukubali kushindwa.
“Bora uniue hapa hapa , la sivyo nitakufanya ujutie maisha yako yote”Aliongea Regina.
Ni kweli hakupokea simu lakini hakuona hilo ni kosa la kumfanywa kutendewa huo ukatili na alijiambia hawezi kuliacha hilo lipite.
Upande wa Hamza aliamini kumshikisha adabu kwa vibao kadhaa ingemfanya Regina kutii lakini kadri alivyokuwa akiendelea ndivyo alivyokuwa akizidi kuwa kiburi.
“Unadhani ni swala la kupokea simu , unadhani nakulazimisha kupokea simu kama haina umuhimu?”Aliongea na kumuongezea viwili vya mwisho na kisha alimwachia.
“Muhuni , jambazi wewe , unaona raha kupiga wanawake?”Regina alitamani kutafuta neno baya zaidi la kumlaani lakini alikosa kabisa , alihisi maumivu makali wakati wa kusimama.
Muda huo akiwaza kumfukuza Hamza kazi simu yake ilianza kuita mfululizo., alitaka kuipotezea ili kudili kwanza na Hamza lakini mara baada ya kuona ni Eliza ambae anapiga alipokea.
“Sis Eliza , kuna tatizo?”Aliuliza Regina , mara nyingi wakiwa peke yao anapenda kumuita Eliza Sis yaani dada kama kumheshimu maana ni mkubwa kwake.
“Asante Mungu , Regina nimefurahi upo salama, vipi umeonana na Hamza?”
“Mbona uko hivyo , kuna kilichotokea?”Aliuliza huku akiwa na mshangao kidogo na alimwangalia Hamza.
“Nilikuwa nikiendesha gari wakati tukirudi nyumbani na Hamza na tulipata ajali baada ya gari kubwa ya mizigo kutugonga , ilikuwa ni makusudi kabisa na Hamza alipatwa na mshaka pengine ni familia ya James ndio wamepanga kutusababishia ajali ndio maana kakimbia kuja kukutafuta baada ya kuambiwa haupo nyumbani bado..
“Halafu Mkurugenzi kwanini hukupokea simu wakati Hamza anakupigia , umetufanya tuwe na wasiwasi mno”Aliongea Eliza na kumfanya Regina kujua kosa liko wapi na aliishia kumwangalia Hamza , ile hasira aliokuwa nayo ndani ya moyo wake kwa kitendo Hamza alichomfanyia ilipotea haraka na kumuacha na aibu pamoja hatia , lakini kwa wakati mmoja alijihisi furaha bila ya kuelewa sababu ni nini.
“Ndio maana alionekana kuwa na hasira , kumbe hili ndio sababu”Aliwaza Regina kwenye moyo wake.
“Sis .. uko sawa , hujaumia?”Aliuliza Regina.
“Gari limebaribika lakini namshukuru Mungu nipo sawa , kama sio Hamza kunitoa kwenye gari kwa haraka sijui ingekuwaje , dereva wa gari amekufa pia , niliogopa mpaka nikapoteza fahamu , sijui nini kinaendelea ila kama ni familia ya James ndio wametutengenezea hii ajali Mkurugenzi unapaswa kuwa makini”Aliongea Eliza na upande wa pili alikuwa akisikia makelele, ilionekana Eliza bado alikuwa eneo la tukio.
Upande wa Regina wazo palepale lilimwingia na alishindwa kuzuia shauku yake.
“Lakini Eliza imekuwaje mpaka mkawa na Hamza pamoja , mnafahamiana vizuri?”
“Ah..!,Sisi.. ni marafiki tulikuwa tukirudi nyumbani baada ya kupata chakula pamoja”
“Oh..kumbe..”
Regina alishindwa kuendelea kuuliza zaidi , kwa akili yake ya haraka ilimfahamisha baadhi ya vitu na kumfanya kuwa na hali ya mshangao.
Upande wa Hamza aliweza pia kusikia mazungumzo yao na alijiambia inaonekana Eliza mbele ya Regina hana kifua kabisa cha kuficha siri.
Regina mara baada ya kukata simu alimwangalia Hamza , hali ya hewa kidogo ilikuwa na ukakasi flani hivi kutokana na kilichotokea.
“Mkurugenzi nini maamuzi yako, unanifukuza kazi?”
Regina aliishia kukohoa kidogo huku akiangalia pembeni kupoteza ishara za aibu zilizomvaa .
“Sikia .. kutokana na kilichotokea na uadilifu wako kwangu,nitakusamehe”Aliongea.
Maneno hayo kwake alijihisi ni kama anaisaliti nafsi yake ambayo ilikuwa ni ya kikauzu na kujikuta akijiona ni kama anakuwa mdhaifu mbele ya Hamza na ilimfanya kushindwa kabisa kukutanisha macho, huku akijihisi ofisi ikiwa na joto mno licha ya AC kuwa wazi.
Mwanamke kuwa na aibu mbele ya mwanaume anageuka kuwa kama ua linalochanua kwa namna ambavyo anapendeza , Hamza alijiambia kama huyu mwanamke angekuwa hivyo muda wote angekidhi vigezo vyote vya kuwa mke wake.
Alijiambia kwa muonekano huo basi kila siku angekuwa akimuangalia ingemfanya kuishi maisha marefu zaidi.
Lakini hio kwake ilikuwa ni ndoto , Regina alikuwa na ugonjwa wa kitabia wa mabiti wengi wa watoto wa kifalme maarufu kama Princess Syndrome.
Hamza hata hivyo hakuamini alikuwa amechukua maamuzi ya kumpiga Regina , ni kama amefanya kitendo ambacho hakutarajia na mara baada ya kukumbuka mabao alivyokuwa akimshushia na kisha kusamehewa alijikjuta akishindwa kujizuia na kucheka.
“Wewe unacheka nini , unafikiria upuuzi wako ulionifanyia?”Aliuliza Regina kwa hasira huku akijiambia kwanini amesamehe kiwepesi hivyo. “Hamna , nilikuwa nikiwaza ni kweli muuaji ametumwa na familia ya James au kuna kitu kinachoendelea sikijui”
“Haijalishi nani kakutengenezea ajali , tunapaswa kuwa makini kwanzia sasa hivi , kama wamefeli kwenye jaribio la kwanza lazima watarudia tena”Aliongea Regina.
“Usiwe na wasiwasi , ili mradi utaendelea kunifanya kuwa karibu yako nitahakikisha nakulinda”
“Nani akuamini , ukinilinda mimi wewe utashindwa kujilinda mwenyewe”
“Unanichukulia poa , mimi ni mwanaume ambae kumlinda mpenzi wangu ni kazi rahisi tu kama kutafuna keki”Aliongea Hamza akicheka na kumfanya Regina kuona aibu kidogo.
“Unaongea ujinga gani , bado nina kazi za kufanya hivyo kaa na mimi mbali”
“Unajua sasa hivi ni saa ngapi , na bado unataka kuendelea kufanya kazi?, hata chakula cha usiku una mpango wa kula kweli?”
“Sina mpango wa kula , nimemaliza na sitokula”Aliongea kijeuri.
“Hizo kazi zinaweza kufanyika hata baadae , lakini kula ni muhimu , ukiendelea hivi utashikwa na vidonda vya tumbo ushindwe kabisa kufanya kazi” “Inakuhusu nini . nimesema sitakula”
“Usipokula , nitakushushia kipigo tena”Aliongea Hamza huku akionyesha mkono wake.
“Wewe , thubutu, jaribu uone”Aliongea huku akirudi nyuma kwa woga , aliona ni kama Hamza angempiga tena ilihali bado alikuwa akiyasikia maumivu.
“Unadhani nashindwa?”Aliongea Hamza huku akimsogelea Regina taratibu taratibu huku akiwa na tabasamu la kifedhuli.
Regina aliishia kurudi nyuma huku akishindwa kujua afanye nini , ukweli ni kwamba alikuwa akimuogopa Hamza atampiga tena.
“Naomba utulie, kwasababu unadhamira safi ya kunijali nitaenda kula”Aliongea akimzuia na kumfanya Hamza kutabasamu na kuona kumbe muda mwingine kumtishia kunafanya kazi.
Baada ya Regina kukusanya kila kilichokuwa chake waliongozana mpaka kwenye maegesho ya magari na kwenda mpaka Mlimani City.
“Unataka kula nini?”Aliuliza Hamza mara baada ya kuingia ndani.
“Mmekula nini na Eliza?”Aliuliza Regina na swali lake lilimshitua Hamza.
“Linahusiana vipi na swala la wewe kuchagua chakula”
“Siruhusiwi kuuliza?”
“Kwannini unataka kujua , Regina unaona wivu?”Aliuliza Hamza huku akiwa na tabasamu.
“Wivu!,sh*nzi , nimeghaili sitaki kula chochote”Aliongea Regina huku akijifanyisha kununa.
“Kama hutaki kula chochote unaonaje Doghnut , hapa wanauza kila kitu”Aliongea na kumfanya Regina kutoa macho na mara baada ya kugeuza macho ni kweli aliweza kuona kabati la kioo lililojaa Doughnut.
Dakika ile anataka kukubali , alijihisi kuna tatizo , alijiuliza kama akila Doughnut si atamkubusha Hamza lile tukio la kula kiroho roho na kumfanya amcheke.
“Kula Doughnut muda huu kama chakula cha usiku sio vizuri”
“Wewe unajali nini kama sio vizuri , ili mradi ni kitu unachopenda haina haja ya kuwazia wengine wanavyokuona”
“Kama ni hivyo basi wewe ndio umenilazimisha na sina jinsi zaidi ya kula”Aliongea Regina akitafuta kisingizio .
“Hakuna shida chukulia kama vile
nimekulazimisha”Aliongea Hamza ambae muda huo hakujua acheke ama alie, mhudumu aliwasogelea na kuwauliza wanachotaka kupatiwa.
“Nataka Doghnut nne zilizochanganywa na Strawberry na juisi ya nanasi”Aliongea Regina na mhudumu alishangaa kidogo lakini alichukua oda yake.
“Na wewe kaka vipi , unaagiza nini?”
“Mimi nipe doughnut nane, nne ziwe za kawaida na nne nyingine zikiwa na Strawberry itafaa, nipatie na chai ya maziwa”Aliongea Hamza akiagiza na yeye Doughnut.
“Zote niweke kwenye sahani au niwafungie?”Aliuliza.
“Tunakula hapa hapa zote”Aliongea Hamza na kumfanya mhudumu kushangaa kidogo na alitingisha kichwa kwenda kutimiza oda ya wateja., hakushangaa sana kwani kuna wanaume wanakula sana , alishangaa kwasababu mara nyingi wanaofika katika mgahawa huo walikuwa wakila kidogo sana. “Na wewe unapenda Doughnut?”
“Nitakula nne za kawaida , zilizobakia zenye strawberry ni za kwako”
“Mimi nataka kula nne tu”Aliongea lakini alisikika kutokujiamini alikuwa nataka sitaki.
“Kama hutokula nitazimaliza tu hakuna shida”
“Mhmh..”Regina aliishia kuguna huku akitingisha kichwa.
Mara baada ya kupashwa kidogo hatimae ziliwekwa kwenye meza yao , muda huo Regina mara baada ya kunusa harufu nzuri inayotoka kwenye donati hizo , tumbo lake lilianza kunguruma kwa njaa na kwa haraka haraka alishika moja na kung’ata kidogo.
Hamza aliishia kumwangalia Regina na tabasamu tu kwa namna ambavyo alionekana kuridhika kula kitu kama hicho na alijiuliza kwanini Regina anapenda vitu yva aina hio , maana kwa mwanamke mwenye hela kama yeye angeagiza cha maana.
“Hivi kwako ni tamu sana?, mimi huwa naziona ni kama andazi lenye sukari nyingi”Aliongea Hamza na kauli ile ili mfanya Regina kumwangalia kwa usiriasi.
“Unaingea ujinga , hivi unajua namna zinavyotengenezwa?”
“Unakasirika nini sasa , kwani kuna nilipokosea?”Aliongea huku akicheka.
“Donati sio kama andazi la kawaida, andazi likishaumuka moja kwa moja unalikaanga na mafuta , lakini Donati ni tofauti , mfano hilo tundu katikati linapimwa kuendana na ukubwa wa mviringo wa nje lakini pia na radha yake na ulaini , mfano ukiona yenye tundu dogo mara nyingi inakuwa ni laini kutafuna , lakini ikiwa na tundu kubwa ukitafuna ni kama biscuit , sukari yake pia inakuwa ni ya kiwango sahihi , mara nyingi huwa ni kati ya gramu tano au sita”
“Aisee inaonekana kweli unazipenda mpaka kuwa mtaalamu”Aliongea Hamza huku akishangaa, lakini Regina hakujali na kuendelea kula donati nyingine na ndani ya dakika chache nane zote zilikuwa zimeisha.
Muda wa kuondoka Regina alionekana kuwa na uso unaong’aa kwa furaha , ilionyesha ni dhahiri akili yake imemkaa sawa mara baada ya kula Donati.
“Twende moja kwa moja nyumbani au tuzunguke zunguke?”Aliuliza Hamza.
“Vyovyote vile”Aliongea na Hamza aliona wazunguke zunguke , isitoshe ni mara chache kwa Regina kuwa na mudi ya kuzunguka zunguka nae kama hivyo.
“Basi tuzunguke zunguke tuone kama kuna kitu tunaweza nunua”
“Sitaki kununua chochote”
“Sio kwa ajili yako , tunamnunulia shangazi”Aliongea Hamza.
“Ah ..Shangazi anapenda sana Korosho , tununue hizo”
“Kama ni hivyo basi tupitie upande ule wa supermarket”Aliongea Hamza na Regina alitingisha kichwa huku akitoa tabasamu.
Tabasamu lile ilimfanya Hamza kumwangalia Regina kwa umakini maana ni kama ameona kitu cha ajabu.
“Mbona unaniangalia sana?”
“Nimejikuta nikiwaza, nakuona itakuwa vizuri ukiwa unacheka mara kwa mara , unaonekana kupendeza zaidi”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kushangaa huku akiganda.
“Kwanini nicheke?”
“Unazidi kuwa mrembo ukicheka?”Alijibu Hamza huku akimkazia macho na kumfanya Regina uso wake kuwa laini kutokana na kupata joto.
“Ukiendelea kuongea ujinga nitakupotezea mazima na kurudi zangu nyumbani”Aliongea akiwa siriasi na kumfanya Hamza kuchezesha ulimi na kufunga mdomo wake na kuanza kutembea huku wakipita kila maduka.
“Regina kwanini unapenda sana kula Donati?, au ni kwasababu zina sukari maana wanawake wengi mnapenda vitu vitamu?”
“Kwasababu mama ndio chakula kikubwa ambacho alikuwa akipenda wakati akiwa ni mjamzito wa mimi?”Aliongea.
“Mama yako akiwa mjanzito , wewe umejuaje?”
“Niliambiwa na watu waliokuwa karibu na mama , inasemekana mama alikuwa ni masikini mno na mimba ilimpelekesha hivyo hakupenda kula chochote zaidi ya Donut, kutokana na habari hizo nilijikuta nikijaribu kula mara kwa mara nikiwa kituoni na nilijikuta nikizipenda mno, sina uhakika kama ninachopenda ni radha au ni kwasababu ya kutamani mama yangu angekuwa hai”Aliongea Regina kwa huzuni na kumfanya Hamza kumuonea huruma kidogo.
“Nisamehe kwa kukuuliza swali ambalo limekutia huzuni”
“Huna haja ya kuomba msahama , ni mambo yaliopita isitoshe namjua mama kwenye picha pekee , nilichosikia mama alininyoshesha kwa wiki mbili tu ndio akapoteza maisha, kwangu hizi Doughnut ndio kitu pekee kinachoniweka karibu na marehemu mama yangu”
Hamza alijikuta akiona ni haki yake kuzipenda , ilionekana hata hivyo ndio kitu pekee ambacho alishirikiana na mama yake kula.
Asilimia kubwa ya ulaji wa mtoto baada ya kuzaliwa huathiriwa na mama,ikitokea mama wakati akiwa mjamzito anapenda kula kitu flani mara kwa mara kwasababu ya kukipenda inatengeneza radha ya kitu kile katika majimaji yaliopo ndani ya mfuko wa uzazi hivyo kadri mtoto anavyokuwa ndio ambavyo radha ya kitu kile inapozoeleka katika ulimii wake , akija kuzaliwa akionja kitu hicho ulimi wake utatambua na kukikubali moja kwa moja na kuona ndio kitu kitamu zaidi, kitaalamu inaitwa Amniotic
fluid flavor effect.
“Vipi kuhusu wewe?”Aliuliza Regina mara baada ya kumaliza kuongea.
“Mimi nini!?”
“Nimekuambia kuhusu mama yangu , vipi kuhusu wewe wazazi wako,kwa mfano mimi namuwaza sana mama wakati nikila Donati , vipi wewe ni kipi ukifanya unamkumbuka sana mama yako?”
Swali lile lilimfanya Hamza kujawa na mawazo na alijikuta akipiga hatua mbele akimuacha Regina.
“Kama hutaki kusema acha..”Aliongea Regina.
“Sina kumbukumbu nyingi kuhusu mama , ila namkumbuka wakati wote , kila saa kila dakika na natamani kukumbuka kila kitu kuhusu mama lakini siwezi”Aliongea na kumfanya Regina kumuonea huruma.
“Usitie huruma sana , sina mpango wa kukufariji mimi”
“Hehe.. ni mambo yaliopita hata hivyo sihitaji faraja” Aliongea Hamza na kumfanya Regina kuwa na ahueni.
Baada ya kuzunguka zunguka walinunua Korosho nyingi tu pamoja na baadhi ya vitu na kurudi garini kuanza safari ya kurudi nyumbani.
Regina kama kawaida alipendelea kukaa nyuma na wakati akiwa anasinzia sinzia kwa kushiba simu yake ilimshitua na alipoangalia anaepiga ni Linda msaidizi wake.
“Linda vipi uchunguzi wako umefikia wapi?, Dokta Ronicas yupo Tanzania kwa ajili ya nani?”
“Mkurugenzi , unaweza usiamini , hata mimi mwenyewe bado nimeshindwa kuamini”
“Kwanini hebu niambie vizuri”
“Ilikuwa ni ngumu kuipata ratiba yake , kwa nilichopata kesho anaelekea Mbutu nyumbani kwao Eliza”Aliongea Linda.
“Nini.. nyumbani kwa Eliza?”
“Ndio , ineonakana yupo Tanzania kwa ajili ya mama yake Eliza meneja wa idara ya mauzo , wiki iliopita Eliza amemtoa mama yake kwenye hospitali aliokuwa akipatiwa matibabu na kumpeleka kwenye nyumba yao, hili limenifanya kushangaa ndio maana mpaka sasa nimeshindwa kuamini”
“Hebu ngoja niwasiliane na Eliza kwanza kuhakikisha , umefanya kazi kubwa pumzika sasa”Aliongea Regina na kukata simu na mara moja alimpigia Eliza.
“Mkurugenzi habari za usiku , kuna tatizo?”Aliongea Eliza mara tu baada ya kupokea simu.
“Eliza hivi unamfahamu Dokta Ronicas?”Aliuliza Regina kwa sauti ya chini.
“Ndio ,kwani Hamza hajakuambia , namjua ni Dokta ambae anakuja kesho kumwangalia mama”Alijibu
Eliza na kumfanya Regina mikono yake kutetemeka.
“Kwahio unamaanisha unafahamiana nae ?”
“Ndio namjua , nimekutana nae leo kwa mara ya
kwanza , ni rafiki yake Hamza na ndio aliniombea aje kumwangalia mama”
“Nini Hamza ndio kamuomba..!!?”Aliongea Regina kwa mshituko huku akimwangaliaHamza ambae alikuwa bize kuangalia barabarani.
Hamza alitamani kucheka tokea dakika ambayo Linda anapiga simu , alikuwa na mpango wa kumwambia licha ya kwamba alionekana kumltea jeuri wakati wa mchana, lakini staili hio ya Regina kuujua ukweli ilimfanya kufurahi.
Regina aliishia kumwangalia Hamza kwa macho yasio ya kawaida na kujiambia huyu Hamza ni nani mbona anamchanganya akili yake , ilitosha kufahamiana na fundi cherehani wa kushonea nguo wafalme , lakini sasa hivi alikuwa na uwezo wa kumuita dokta maaurufu duniani kuja kumtibia mama yake Eliza , kitu ambacho licha ya kuwa na pesa nyingi alishindwa kuweka miadi na dokta huyo kuonana nchini kwake sembuse kumuita Tanzania.
“Mkurugenzi mbona umekaa kimya?”Upande wa pili sauti ya Eliza ilisikika.
“Eliza hivi unaijua hadhi ya Dokta Ronicas katika fani ya matibabu?”
“Kutokna na ajali ilionitokea leo nimejikuta na mawazo mengi , na ndio nimemaliza kuoga hapa , bado hata sijamfuatilia”
“Kama ni hivyo hebu ingia mtandaoni na utafuje jina lake kwanza, mimi nakata simu”Aliongea na Regina alikata simu muda uleule.
Baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha alimwangalia Hamza kwa macho ya maswali. “Kwanini hukuniambia unafahamina nae ?” “Nadhani ushasahau , hukumbuki nilipoingia kwenye ofisi yako na kuulizia hali ya bibi yako ukaishia kufukuza , unadhani ningeanza vipi kukuambia”
“Sikujua , ungeniambia kama unafahamiana nae?”Aliongea Regina kwa sauti ya chini.
“Ulisema hutojutia , vipi sasa hivi unajjisikiaje?, nikwambie tabia yako ya kukasirika bila sababu kwa kutolea watu hasira zako inafanya watu wakuogope na pengine kukuchukia kabisa”
Regina alitaka kupanda juu lakini mara baada ya kufikiria hali aliokuwa nayo alijikuta akiwa mpole.
“Naomba unisaidie kumuomba basi Dokta Ronica kuangalia shida ya bibi yangu”
“Kama bibi yako atakubali mimi sina shida, nitamuambia”
“Usiwe na wasiwasi , ili mradi Dokta Ronica akikubali nitahakikisha na bibi anakubali kufanyiwa uchunguzi”Aliongea Regina akiwa siriasi
“Nilivyokuona namna ambavyo hampatani na baba yako nikajua ni hivyo hivyo kwa bibi yako pia , ila kumbe unamjali?”
“Wakati babu alivyonileta katika familia nilikuwa na miaka kumi na mtu pekee ambae alinikaribisha kwa ukarimu ni bibi , Namheshimu babu kwasababu alinifundisha nini maana ya biashara lakini bibi ndio aliekuwa mtu wa karibu na mimi zaidi , ukiachana na Shangazi ambae alikuwa mlezi wangu, familia nzima ambae alikuwa akinipenda ni bibi pekee , wakati ambapo Lamla mke wa baba akinifokea ni bibi ambae alinikingia kifua, baada ya babu kufariki ni bibi ambae alihakikisha nakuwa CEO wa kampuni, hivyo naweza kutumia kiasi chochote cha pesa kuhakikisha bibi anapona”Aliongea na Hamza alimwelewa.
“Nitaongea na Flora , nadhani hawezi kunikatalia”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kufurahi na alipumua kwa nguvu kuonyesha amepata ahueni.
“Lakini imekuwaje ukafahamiana na mtu mkubwa kama Dokta Ronicas?”
“Sisi ni…”
“Unataka kusema tena umekutana nae Bar sio?”Aliingilia Regina mara bada ya kuhisi uongo wa Hamza.
“Ndio , umejuaje?”Aliongea Hamza huku akicheka.
“Unadhani mimi ni mjinga , kama unataka kuniongopea angalau tunga uongo mzuri”Aliongea .
“Kwasababu unaonekana kunijua vizuri unaonaje tukiachana na hilo , si kikubwa ni bibi yetu kutibiwa”
“Ni bibi yangu sio wetu”
“Haha.. haijalishi ni kweli au hapana , lakini mbele ya macho ya watu sisi ni wapenzi hivyo ni bibi yetu”Aliongea na kumfanya Regina kuvuta mdomo.
******
Upande mwingine usiku huo huo katika moja ya Club maarufu iliokuwa kipatikana Mbezi mwisho , ifahamikayo kwa jina la Nipe tano pub alionekana Kanali Dastani akiwa katika chumba binafsi amekaa kivivu kwenye masofa , mbele yake kulikuwa na chumba za Whiskey mbili moja ikiwa imeisha nyingine ikiwa nusu , ikionyesha alikuwa hapo muda mrefu kidogo.
Alionekana kuwa siriasi kidogo na alikuwa akiangalia saa yake mara kwa mara kana kwamba kuna mtu aliekuwa akimsubiria.
Zilipita dakika kama tano hivi simu yake ilianza kuita na alichukua haraka na kupokea. “Niambie taarifa nzuri Afande?”
“Dastani mpango umekwama , sijui nini kilichotokea lakini hakuna madhara yaliowapata walengwa , Bunji amekutwa eneo la tukio akiwa hana uhai”Sauti iliongea na jibu lile lilimfanya Kanali uso wake kujikunja na alimimina Whiskey kwenye glasi na kupeleka yote mdomoni.
“Sagenti , nilikuambia unitafutie kijana anaejiua kazi , ila umetafuta mtu wa kujitoa muhanga?”
“Tajiri, Bunji ndio mfungwa ambae alikidhi vigezo vyote ulivyohitaji na nimeshangaa kusikia amepoteza uhai kwa kujimaliza , hii sio kazi yake ya kwanza kufanya”Sauti upande wa pili ilijitetea na kumfanya Kanali kufikiria kidogo.
“Hakikisha swala la Bunji linabakia kuwa siri , isitokee minong’ono kwa wafungwa wengine na ikaleta ukakasi”
“Tahadhari nimezichukua , kuhusu hilo usiwaze kabisa..”Sauti ilisikika na kumfanya Kanali kupumua.
“Malipo yako yataingizwa kama kawaida”
“Bosi kuna taarifa nyingine nadhani napaswa kuiripoti kwako nadhani ni taarifa ya kukufanya uniongezee ongezee , uchumi mgumu bila kujiongeza mambo hayaendi”
“Mchuku huwezi kunipatia hio ripoti mpaka uhusishe hela?”
“Sio kama napenda kuhusisha fedha Bosi , unajua kabisa mjengo wangu upo hatua za mwisho na mama watoto amechoka kukaa Kota za Magereza” Sauti iliongea na kumfanya Kanali kutoa tabasamu la kejeli.
“Nipe hint , nikiona inanifaaa nitakuongezea kitu”
“Ni kuhusu yule Mfungwa wa Kimexico , Ninja wa kundi la Dragon tooth, nadhani bosi unajua hii kesi ilivyokuwa siri, kukuambia hivi nahatarisha kibarua changu cha ukuu wa gereza”
Kanali mara baada ya kusikia sauti hio palepale akili yake ilicheza mfungwa , kesi ya mfungwa hio ilikuwa siri, ndio mtu ambae alihusika katika mauaji ya jasusi wa kitengo cha usalama wa taifa , jasusi muadilifu Sedekia Kunembe ambae alipewa misheni ya kufuatilia tukio la radi mkoani Rukwa miaka kadhaa iliopita.
“Ngapi unataka niongeze?”Aliongea Kanali huku aking’ata meno kwa hasira, maada Afande Mchuku alikuwa akijua kumtoa hela sana , ni hivyo tu alikuwa ni wa faida ndio maana alimpatia.
“Milioni sita tu bosi wangu , kama nilivyosema hii ripoti inakufikia wewe kabla ya kitengo cha TISA walioniambia nitoe ripoti kwa kila kinachoendelea kwa yule mfungwa”
“Nitaongeza nne kamili nielezee”Aliongea Kanali na upande wa pili ulinyamaza kidogo.
“Kuna wazungu wanne wamefika leo kumtembelea”Aliongea na kumfanya Kanali macho yake kuchanua kidogo.
“Wazungu , nilidhani ni mfungwa ambae hapaswi kuruhusiwa kuonana na mtu yoyote wa nje?”
“Ilikuwa ngumu kuwakatalia , walikuwa na kibali kutoka kwa Lughalila”
“Unamaanisha Waziri ndio ambae ameruhusu?!”
“Ndio maana nikaona hii ni habari ambayo inaweza kunipa posho ikianza kukufikia wewe?”
“Kitu gani wameongea , umeweza kujua walichoongea”
“Kuhusu hilo Kanali sijajua , ila wametumia ofisi yangu kufanyia maongezi yao”Aliongea Mchuku na kumfanya Kanali kutamani kutoa tusi kwa mtego wa Mchuku.
“Mchuku acha kuzunguka zunguka , najua ofisi yako haijawahi kuwa sehemu salama ya kufanyia maongezi”
“Hehe… Kanali nilichofanya ni kukupa taarifa tu , kuhusu walichoongea sidhani napaswa kukwambia kila kitu , kama nilivyosema hili swala linaweza kuniingiza kwenye matatizo”
Kanali Dastani aliishia kugugumia Whiskey , katika maisha yake hajawahi kukutana na mtu ambae anajua kufanya biashara kihuni kama Mchuku , wakati wakiwa katika mafunzo ya upolisi hakuelewa kwanini Mchuku alichagua uelekeo wa Magereza na kukataa kuwa polisi wa kawaida, kumbe kwake aliona fursa gerezani na kweli fursa alikuwa akiitumia vizuri.
“Mchuku nataka kujua kila kitu walichoongea, ni muhimu kwangu, nitalipa kiasi chochote unachotaka”
“Kanali kama nilivyosema ilikuwa ngumu kwangu kusikia wanachoongea , isitoshe walikuwa wakitumia Lugha nisioijua?”
“Umeweza kujua walikuwa wakitumia lugha usioijuas , halafu unasema ilikuwa ngumu kujua wanachoongea , unaonaje nikikupatia pesa ya kumaliza nyumba yako moja kwa moja na kumaliza mkopo wako wa benki?”
“Tajiri tutaongea kesho, nikishafikiria vizuri”
“Nyumba , mkopo benki na lile gari la ndoto zako, unaonaje?”Aliongea Kanali , alijua kabisa Mchuku sio mtu wa kufikiria fikiria , akikwambia ngoja afikirie ujue hajaridhika na malipo.
“Hela ya malipo ya Bunji na ripoti ya kukuelezea hii issue yanajitegemea”
“Sawa , niambie sasa, je umeweza kujua wanachoongea?”
“Kama nilivyosema walikuwa wakitumia ligha nisioijua , ila nimerekodi maongezi yao yote”Aliongea Mchuku na kumfanya Afande kutoa tabasamu, japo alikuwa na wasiwasi maongezi hayo yanaweza yasmpe anachokitaka , lakini alikuwa tayari kulipa , isitoshe hela hizo hazikuwa zikitoka kwenye mifuko yake.
Baada ya kukubaliana na Mchuku siku inayofuata waonane kwa ajili ya makabidhiano , Kanali aliitafuta namba ambayo alikuwa ameisave kama Tajiri na kisha akaipiga.
“Madam!!,”Aliongea Kanali mara tu baada ya simu kupokelewa.
“Salama Madam , nimepata dalili ya muongozo , ila upande wa pili unahitaji motisha….”
“Oh sawa , Madam namba ni ileile , ndio, kesho nikipata lolote nitakurudia, Asante sana nahakikisha hili swala tunalijua ki undani kabisa”Aliongea Kanali na muda uleule simu ilikatwa, haikueleweka aliekuwa akiongea ni nani.
Muda huo huo mara baada ya simu kukatwa mlango wa chumba hiko ulifunguliwa na mara baada ya Kanali kugeuka alijikuta akitabasamu , alikuwa ni mrembo Tresha Noah ambae alikuwa amevaa akapendeza , alikuwa amevaa kimtego na kumfanya Kanali kumeza mate mengi.
Kitendo cha Tresha kuingia moja kwa moja alimvamia Kanali na busu zito la mdomoni , haikuhitaji kuambiwa kinachoendelea , ilionekana wawili hao walikuwa wapenzi wa siri.
Chumba kinachofuata alikuwepo Jausi Mstaafu mzee
Amosi akiwa amekaa huku akiwa amevaa
Headphone, alikuwa ameshikilia simu janja mkononi na alikuwa ameikazia macho na kumfanya kutabasamu.
“Hii kitaalamu inaitwa kupiga ndege wawili kwa jiwe moja , Dastani mwisho wa siku na wewe ni binadamu tu ambae unafanya makosa”Aliongea na bila ya kuchelewa alitoa maburungutu mawili ya hela na kuyeka juu ya meza na kisha alitoka ndani ya chumba hicho na kutokomea akiwa na tabasamu usoni.
“Kazi yangu ya kwanza ni kumuwahi Mchuku kabla ya Dastani , lazima ni swala linalohusiana na hii misheni ya mwanamke”Aliwaza Amosi na alijikuta akiona mpango wake wa kuja katika Pub hio haukuwa mbaya kabisa.
Amosi alikubali Dastani amemzidi vitu vingi likija swala la ujaususi wa ki uchunguzi na kuliona hilo , siku nzima alikuwa akimfuatilia nyuma nyuma ili kujua kila ambacho anafanya na mazungumzo yake yalivyo na mpango wake ulimlipa.
Comments