Reader Settings

MASAA KADHAA NYUMA.

Jaususi Mstaafu Amosi hakutaka kuchelewa hata dakika moja  mbele ya  Kanali Dastani , alijua akifanya kosa tu  atawahiwa ndio maana usiku huo huo  mara baada ya kumuwekea kirusi  Kanali katika chumba  cha Pub ile  moja kwa moja alianza kufanya uchunguzi  juu ya   wapi ataweza kumpata Mchuku, mkuu wa Gereza.

Katika ujasusi wake kuna mambo makuu mawili  ambayo alipata , kwanza  alijua kuna mfungwa ambae amehusika  na kesi ya Sedekia ambae yupo gerezani , jambo hili hakuwahi kulisikia hapo kabla licha ya kwamba  ni swala ambalo lilitokea wakati yeye akiwa kitengoni , hakujua kwanini  swala hili lilifichwa sana.

Swala la pili  nin mahusiano ya  Tresha Noah na  Kanali , alikuwa akijua fika Mheshimiwa Raisi ambae anakwenda kumaliza muda wake alikuwa  ni raisi ambae anapenda warembo , hili lilikuwa swala la wazi  mpaka kwa watanzania ,  licha ya kwamba  Raisi Elias alifanya makubwa katika uongozi wake lakini udhaifu wake ilikuwa ni wanawake ,  tokea siku ambayo alifiwa na mke wake akiwa madarakani  ndio aliongeza moto.

Ukweli ni kwamba  wakati wa  kifo cha First Lady kinatokea  sekeseke liibuka huku  ikiaminika ni  raisi huyo kumuua mke wake  baada ya kumsaliti   na moja ya tajiri Mkubwa aliekimbia nchi na kuishi uhamishoni kwa muda mrefu.

Wengi wanaamini kutokea kwa kifo cha First lady kulimfanya  azidi kubadilika tabia  na kuendekeza ngono, lakini kwanzia hapo Raisi Mbilu alikuwa makini sana na wanawake ambao anatembea nao , hata kama hakuwa akiwapenda lakini hakutaka wamsaliti , pengine ilikuwa ni Trauma aliopata  kutoka kwa mke wake ambae inasemekana alimpenda sana.

Sasa  Amosi kujua swala la  mwanamitandao ya kijamii maarufu Tresha Noah kuwa na mapenzi ya siri  na Kanali ilikuwa ni kete ambayo  kwake aliona itafikia  muda atatakiwa kuicheza vizuri na sio kwa kurupuka.

Kutokana na swala la mfungwa  huyo kuwa siri , hakujua moja kwa moja atakuwa  yupo gereza gani  na njia pekee ambayo  aliona inaweza kumpa majawabu ya haraka haraka ni kupitia kitengo cha TISA(Tanzania inteligence service Agency).

Lakini hata hivyo  asingeweza kupata taarifa hio ya siri  kwa uharaka bila ya kutumia mtu mwenye madaraka  na pia katika mazungumzo ya Kanali Dastani  alisikia  Waziri akihusishwa hivyo moja kwa moja aliona sio  jambo jepesi.

“Shit.. nimesahau kitu muhimu Mchuku  ni mkuu wa Gereza  hivyo ni rahisi kufuatilia anahudumu katika gereza lipi  kupitia Mkuu wa Magereza”Aliwaza Amosi huku akijiona  mjinga,kwanini hakufikiria njia nyepesi hio.

Dakika ileile baada ya wazo hilo kumwingia  alisimamisha IST yake pembeni na kulitafuta jina la  moja ya Askari polisi ambae aliamini  lazima atakuwa na taarifa  ya wakuu wa  Magereza kwa upande wa jiji la Dar es salaam, alienda kwenye majina mpaka akalifikia jina la  Afande Chika  na kupiga simu  lakini jibu ambalo alipata lilimkatisha tamaa , simu yake haikuwa hewani , lakini hata hivyo aliona  haina haja ya  kukata tamaa , alitafuta namba nyingine , jina  lilikuwa ni Sajenti Ulimboka  na alipiga na simu  iliita dakika chache na kupokelewa na kuanza kusikia makelele.

“Amosi nipigie baadae  , nipo eneo la tukio’Sauti  upande wa pili  ilisikika  na kumfanya Amosi kukunja ndita.

“Ulimboka namuulizia Afande Chika, hapatikani hewani kupitia namba yake ya kawaida”Aliongea Amosi kwa haraka haraka.

“Amosi  unaemtafuta jeshi  la polisi pia linamtafuta ,  sijui kwanini unamtafuta ila  kwasasa nipo  kwenye majukumu ya kazi,  nipigie

asubuhi”Aliongea Ulimboka na kabla hata hajampa maelezo  Amosi ya kueleweka simu ilikatwa palepale  na kumfanya Amosi kutamani kutoa tusi.

Mpaka hapo koneksheni yake polisi ilikuwa ishafika mwisho , Amosi licha ya  maisha yake  mtaani kuonekana kama vile ni ya kihalifu hakuhitaji kujuana na  askari wengi  polisi , alihitaji  afande mmoja tu mwenye nguvu  na  ambae anaishi kifisadi na huyu alikuwa ni Afande Chika.

Asichokijua Amosi ni kwamba Afande Chika aliingia katika  mikono ya Chatu na haieleweki alifichwa wapi mpaka kutokuonekana  kwake au  amekufa au lah.

Baada ya kukosa jibu la haraka haraka aliona  amuhusishe bosi wake wa kazi ,yaani Brigedia Doswe , ilikuwa ndio njia yake ya mwisho  kutaka kupata  kile anachohitaji tena mapema mno.

Hakujali muda ni saa ngapi na ingeonekana  ni ukorofi wa  namna gani kumpigia Brigeida muda huo lakini kwasababu jeshi  ni  kazi ya wito pia,  hakujifikiria mara mbilimbili na kupiga simu na iliita kwa muda mrefu bila ya kupokelewa , alipiga mara nyingine na haikupokelewa na aliamini moja kwa moja  Brigedia huenda amelala hivyo  aliona labda afanye asubuhi asubuhi ,  jambo la uhakika tu  ni kwamba  Brigedia  angeona  missed call zake angempigia.

Amosi kinyonge  alirudi garini na kuliwasha  kisha taratibu aliliingiza  barabarani huku mpango wake  ni kurudi nyumbani kwa ajili ya  kupumzika, akiwa njiani alikuwa akifikiria kauli ya Ulimboka juu ya DCP Chika kutafutwa na polisi, ilikuwa kichekesho kwake , yaani polisi anatafutwa na polisi wenzake, alijua lazima kuna kitu kinachoendelea.

Wakati akiwa katika  mataa ya  Mwenge   ili aelekee Mikocheni  kwenye apartment yake simu yake ilianza kuita na alipoangalia anaepiga  ni Brigedia , palepale alipunguza mwendo  wa gari  na kupokea simu. “Jambo  Afande “

“Jambo ,Amosi habari za usiku , kuna taarifa yoyote?”Aliongea Brigedia na sauti yake iliashiria haraka  na Amosi alilitambua hilo.

“Nimepata uelekeo wa  ile  kazi ya Wabrazili , nilimfuatilia  Kanali  na nimemsikia akiwa katika mazungumzo na moja ya wakuu wa Magereza wakizungumzia juu ya Mfungwa  aliehusika na kifo cha Sedekia…”

“Amosi hebu acha kuendelea kuongea kwanza , Umesikia wapi hio  taarifa nyeti hivyo  ya daraja la kwanza kitengoni?”

“Mkuu ni kama nilivyosema nilisikia mazungumzo  kutoka kwa Kanali Dastani..”Aliongea Amosi huku akijiuliza mbona amekasirika  baada ya kusikia  hilo swala  , inamaana hata yeye alikuwa akijua na ameupiga kimya.

“Amosi kuhusu swala hilo ni sehemu ya siri za taifa kwa kushirikiana na  washirika  wetu wa nje , ni swala linalogusa diplomasia ya nchi , niambie unachotaka nikusaidie ni nini  kwenye uchunguzi  wako , ila achana na swala  kabisa la mfungwa , sitoweza kukuepusha  tena na kifo uking’ata zaidi ya  usichoweza kumeza”

“Nataka kujua Afande Mchuku ni Mkuu wa gereza lipi Afande , nimejaribu kuwasiliana na Afande Chika  lakini hapatikani hewani…”Aliongea  na upande wa pili  ulikuwa kimya na kumfanya   Amosi kusimamisha gari  mkabala na  hoteli ya Krebyss.

“Amosi  nipo na Afande Mafulu  hapa CP wa mkoa , kama unaemzungumzia  ni Afande Kigo

Mchuku taarifa za kifo chake zimeripotiwa sasa hivi  kwa wakati mmoja na za DCP Chika , kuna uwezekano  unachotaka  kufuatilia kwa Mchuku ndio kimemuua akiwa  chooni  huko Fulu Dozi 

Bar Segerea , alikuwa  kaimu mkuu wa gereza la

Segerea baada ya Afande  Simba kupalalaizi , Amosi kesho fika ofisini kwangu  nadhani tuna la kuongea, kwasasa nakata simu nipo kwenye kikao”Aliongea  na  simu ilikatwa palepale  

Amosi alijikuta akitoa macho , yaani ndani ya dakika  kumi  tu mtu ashapoteza maisha , akili  ilijaribu kumwambia pengine ni Dastani  lakini iligoma kabisa, Japo Kanali Dastani aliaminiwa kwa uwezo wake wa akili na  ushapu lakini  sio kwa namna  hio ,kuna kitu tayari alikihisi pengine  kuna muhusika mwingine , lakini  swali liliibuka palepale , kwanini Mchuku afariki  ndani ya dakika chache baada ya kuwasiliana na Dastani , akili yake ilimjibu lazima alichorekodi kina taarifa ya kutosha , swali lingine  kama ameuwawa  je  alichorekodi kimechukuliwa  na muuaji  jibu  hakupata  na kwa haraka haraka aling’ata meno kwa hasira na kujiambia anapaswa kuwahi Fuludozi Bar eneo la tukio kabla ya  taarifa hazijamfikia  Kanali Dastani , aliamini lazima angepata kitu.

*******

Upande mwingine  nusu saa mbele  lango la nyumba ya mapumziko ya Mheshimiwa raisi 

lilifunguliwa  na gari aina ya V8 iliingia  na palepale alitoka  mwanaume mwenye muonekano mgumu kidogo mwenye masharubu.

Kama  Amosi angekuwepo  angemfahamu mara moja , ndio mwanaume ambae alimpiga risasi ya ubavuni mpaka kumpelekea kulazwa siku  kadhaa  katika hospitali ya jeshi.

“Nipo kwa ajili ya  kuonana na

mheshimiwa”Aliongea  bwana huyo mara baada ya kuzuiwa na bodigadi namba  moja wa  raisi.

“Mheshimiwa ametoa taarifa hataki usumbufu”Aliongea  bodigadi yule akiwa na sura isiokuwa na utani , hakuwa  na dalili yoyote ya kumpisha, sio kama hamjui  alikuwa akimjua lakini  alizingatia itifaki za ki usalama kwa mheshimiwa, hususani muda huo wa usiku.

“Ni swala muhimu  Afande , napaswa kuripoti  mara moja kwa mheshimiwa na kupotea” “Kama nilivyosema Mheshimiwa  kapumzika, hakuna namna  ya kuonana nae sasa hivi, kama una maagizo yoyote  yaache hapa 

nitayafikisha”Aliongea  na kumfanya  bwana yule kumwangalia   kwa macho makali kidogo na alionekana kutulia kidogo  na aliingiza mkono mfukoni lakini kitendo chake kilifanya  walinzi wote kukoki bastora  na kumnyooshea wakidhani anatoa siraha licha ya kumkagua getini, lakini bwana yule   alinyoosha mkono juu kwa ishara ya kujisalimisha huku mkononi akionekana ameshika kitu.

Afisa  huyu  mkuu wa  kitengo cha Itifaki mara baada ya kuona kitu kilichokuwa kwenye mikono ya  yule bwana alinyoosha mkono na kuchukua.

“Ni taarifa ambayo nilipaswa kumpatia mheshimiwa moja kwa moja , kazi alioniagiza nimemaliza”Aliongea na  Kanali Ashrak alimwangalia bwana huyo kwa macho ya umakini na kisha aliwapa ishara wenzake kushusha siraha chini.

Unajua nyumbani kwa raisi unaweza ukaruhusiwa kuingia getini  lakini ukashindwa  kupita  mbele ya  kitengo cha itifaki ya  kumuona Raisi ambacho   huongozwa na  ADC mwenyewe , hiki ndio kilichomkuta.

“Bundi najua ukaribu  wako na mheshimiwa  na naheshimu hilo lakini  kwasasa  hali ya usalama  kwa mheshimiwa  imeimarishwa ni vizuri ukipotea mpaka pale mheshimiwa atakapokuhitaji  yeye mwenyewe. This isn’t personal” Aliongea ADC  na Bundi alitingisha kichwa kuelewa na kisha  alisindikizwa   na kutoka nje kabisa.

Kanai Ashrak aliishia kuangalia ile flashdrive  na kisha alitoa  tabasamu na kuiweka mfukoni na baada ya pale alitoa ishara kadhaa  kwa wenzake  na kuingia ndani, pengine  alikuwa akipeleka ujumbe ule kwa mheshimiwa lakini mara baada ya kuingia ndani haikuwa hivyo , mmoja kwa moja alielekea  katika chumba kingine ambacho ndani yake kilikuwa na tarakishi.

****

Kilichowaacha midomo wazi  zaidi ni kwamba Yulia  hakuleta ukinzani na zaidi sana alionyesha kufurahi kushikwa mkono na kutolewa nje, lakini kitendo cha  Hamza kumtoa Yulia mpaka kwenye Korido mabodigadi waliingilia  kati  na kumzuia.

“Mkuu muachie bosi wetu , vinginevyo  usitulaumu tukichukua hatua”Aliongea mmoja wapo  lakini kauli yao ilimfanya  Yulia uso wake kujikunja  na kuwafokea.

“Ondokeni  njiani ,  yoyote atakaemchokoza huyu mwanaume  awe makini maana nitamtimua , kingine  msinifuate”Aliongea  na kufanya  wafuasi wake kuangaliana  kwa mshangao , hawakuwahi kumuona bosi wao kuwa legelege mbele ya mwanaume kama hivyo.

Hamza alimpeleka Yulia mpaka floor inayofuata  upande wa balkoni  sehemu ambayo aliona  ni tulivu.

Mara baada ya kusimama  alijikuta akivuta pumzi nyingi  na kumwangalia mwanamke huyo , upepo wa bahari  ndio uliowapuliza na kufanya nywele za kizungu za Hamza kupepesuka.

Hamza alikuwa akimchunguza mrembo huyo na kitu pekee alichoona ni kwamba hakuwa amebadilika kabisa , alikuwa mrembo  vilevile kama alivyomuacha.

“Unaniumiza   bwana mkono wangu”Aliongea  na palepale alimfanya Hamza kukumbuka kumbe amemshikilia mkono huyo  mrembo. “Sorry”Aliongea Hamza na kumuachia.

“Usiwaze unaweza kuendelea kunishika mpaka uchoke , kwasababu miaka saba iliopita ulikuwa muhuni zaidi ya hivi , kunishika mkono tu kuna tatizo gani?”

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akimeza mate mengi  na kutoa tabasamu.

“Hehe ,, mpaka leo unakumbuka”Aliongea Hamza lakini  mrembo huyo ambae macho yake ni kama yamejaa maji aliendelea kumwangalia Hamza huku akionekana  kuwa mbali kihisia.

“Imekuwaje  upo hapa Tanzania, sehemu ambayo sijawahi kuiwazia  utakuwepo hata  mara moja?”

“Kuna mambo yalitokea  na kunifanya kuchoka  maisha  niliokuwa nayo, nikaona nibadilishe mazingira  na kwasababu ya kuijua lugha ya kiswahili vizuri  Tanzania ndio niliona  mahala sahihi”

“Unajua kiswahili?”Aliongea , ukumbuke hapa muda wote walikuwa wakitumia kingereza.

“Najua ndio”Aliongea  Hamza kwa kiswahili na kumfanya  Yulia kushangaa.

“Sikutegemea kama ungejifunza kiswahili na kuongea kama mzawa”Aliongea.

“Mimi ni Mzawa hivyo najua kiswahili vizuri tu siwezi kukuambia chochote lakini jua hivyo”Aliongea  Hamza.

“Mwisho wa siku licha ya kuwa hapa nchini hujajua kilichotokea  na kukutana kwetu ni kwa bahati mbaya tena,  wakati ule hukutaka kunipatia hata mawasiliano yako  na sasa unaanza kunificha pia” “Ni kwasababu mambo yangu   hayahusiani kabisa na wewe , Madam unapaswa kujua sasa  hivi mimi ni  mfanyakazi na mwanachuo  tu , hivyo yaliopita  tuyaache yapite”

“Mwanachuo?, Mfanyakazi?”Aliuliza kwa mshangao  , ilikuwa ni kama vile amegundua  uwepo wa sayari nyingine katika mfumo wa jua  kwa mshangao wake.

“Nipo Dosam pale  msaidizi wa karibu kabisa na CEO?”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu la kejeli ni kama vile nafasi hio haikuwa ikimtosha, Regina na hasira zake za karibu  angekuwepo pengine angemtukana.        “Nini..isijekuwa  umempenda  bosi wa kampuni ya Dosam , Regina Wilsoni namfahamu vizuri alivyo mrembo”

“Hehe… najua CEO wetu ni mrembo   lakini 

haimaanishi kwamba nimempenda nipo kikazi zaidi”

“Siwezi kuamini , kwa uwezo wako  si ni rahisi sana kupata pesa , isitoshe  sidhani kama  Regina anakufaa  inasemekana ni mgonjwa wa aki…”Alitaka kuongea lakini  alisita.

“Ni mgonjwa wa nini..??”Aliuliza Hamza akiwa siriasi  na kumfanya  Yulia  kuonyesha  kujutia  palepale mdomo wake , lakini  alijua ni kwasababu ya furaha kubwa aliokuwa nayo.

“Sina maelezo ya kutosha , taarifa hizi ni za siri pia , nimesikia  ni mgonjwa  wa akili wa nafsi mbili , itakuwa vizuri zaidi ukifuatilia kwa upande wako”Aliongea Yulia  na kumfanya Hamza kushangazwa na jambo lile mno. “Kuna mwingine anaejua kuhusu hili?”

“Sidhani  kama kuna anaefahamu , lakini niamini mimi taarifa hii  ni ya siri mno  hata familia  yake hakuna anaejua kasoro bibi yake pekee, ninachomaanisha ugonjwa wake  ukimpata  hata kama anaweza kukupenda akiwa na nafsi ya Regina  akibadilika  anaweza akakupotezea moja kwa moja”Aliongea  na kumfanya Hamza kuwaza lakini muda huo  Yulia alitumia  kumsoma Hamza kimawazo  na kuna kitu alichogundua lakini hakutaka kukiweka wazi.

“Kuhusu hili nitafuatilia , kama umesema ni la siri naomba liendelee kuwa siri , mimi kama msaidizi wake wa karibu  chochote kikimpata  nitawajibika”Aliongea  Hamza na kauli yake ilimfanya  Yulia  kuwa na wivu wa wazi.

“Yulia ninachomaanisha  usije ukaruhusu mawazo yako yakaenda mbali ,  nipo ndani ya kampuni ya Dosam kwa ajili ya kutengeneza pesa kama  watu wa kawaida , mimi sio mtu ambae umekutana nae miaka saba iliopita”

“Kama huo ndio mpango wako , kwanini usijiunge  na kampuni yetu ya PRIMA? Nitakupa nafasi ya kuwa bodigadi wangu, haijalishi Regina anakulipa kiasi gani  nipo tayari kulipa zaidi yake”

“Hapana haiwezekani , nimeshasaini nae mkataba  , isitoshe kwa ulichosema  nadhani anahitaji ulinzi zaidi kuliko wewe”

“Unanionaje , nipo tayari kukuliipa milioni ishirini kwa mwezi , kama haitoshi nitajie  kwa ajili yako nipo tayari kulipa kiasi chochote”Aliongea  na kumfanya Hamza kuona Yulia anachagua cha kujibu maneno yake  na kumfanya acheke.

“Yulia  tulikutana kwa muda mchache sana Zurich , hivi unadhani  kuniona vile ndio kunijua , ukweli ni kwamba  hujui chochote kuhusu mimi  halafu unataka  niwe bodigadi wako?, mbona kama unaniamini sana kupitiliza”

“Mimi  ninachojua wewe sio mtu mbaya , kama kweli  ungekuwa ni mtu mbaya  usingeniokoa  katika  dakika zangu za mwisho za uhai”Aliognea huku awamu hio akilegeza sauti na  mikono yake kuiweka katika mabega ya Hamza.

“Au upande wako  mwingine unakufanya kuwa mbaya , kama ni hivyo  nakufaa zaidi ya Regina”Aliongea huku aking’ata lipsi zake kwa namna ya kukonyeza  na pumzi yake kuizuia na kufanya jicho kulegea.

Matendo yote ya Yulia yalimfanya Hamza mwili wake kuwaka moto, Yulia alikuwa akijua  anachokifanya katika kumpagawisha.

Hamza mara baada ya kuona  yanakwenda kumshinda alimshika kwenye shingo  kwa  spidi ya hali ya juu na kwenda kumbana kwenye ukuta na kusogeza mdomo wake karibu zaidi huku Yulia akiendelea kumwangalia kwa macho ya kumruhusu lakini yaliojaa waswasi kwa wakati mmoja.

Previoua Next