Reader Settings

SEHEMU YA 45

ILIPOISHIA 

“Yulia ninachomaanisha  usije ukaruhusu mawazo yako yakaenda mbali ,  nipo ndani ya kampuni ya Dosam kwa ajili ya kutengeneza pesa kama  watu wa kawaida , mimi sio mtu ambae umekutana nae miaka saba iliopita”

“Kama huo ndio mpango wako , kwanini usijiunge  na kampuni yetu ya PRIMA? Nitakupa nafasi ya kuwa bodigadi wangu, haijalishi Regina anakulipa kiasi gani  nipo tayari kulipa zaidi yake”

“Hapana haiwezekani , nimeshasaini nae mkataba  , isitoshe kwa ulichosema  nadhani anahitaji ulinzi zaidi kuliko wewe”

“Unanionaje , nipo tayari kukuliipa milioni ishirini kwa mwezi , kama haitoshi nitajie  kwa ajili yako nipo tayari kulipa kiasi chochote”Aliongea  na kumfanya Hamza kuona Yulia anachagua cha kujibu maneno yake  na kumfanya acheke.

“Yulia  tulikutana kwa muda mchache sana Zurich , hivi unadhani  kuniona vile ndio kunijua , ukweli ni kwamba  hujui chochote kuhusu mimi  halafu unataka  niwe bodigadi wako?, mbona kama unaniamini sana kupitiliza”

“Mimi  ninachojua wewe sio mtu mbaya , kama kweli  ungekuwa ni mtu mbaya  usingeniokoa  katika  dakika zangu za mwisho za uhai”Aliognea huku awamu hio akilegeza sauti na  mikono yake kuiweka katika mabega ya Hamza.

“Au upande wako  mwingine unakufanya kuwa mbaya , kama ni hivyo  nakufaa zaidi ya Regina”Aliongea huku aking’ata lipsi zake kwa namna ya kukonyeza  na pumzi yake kuizuia na kufanya jicho kulegea.

Matendo yote ya Yulia yalimfanya Hamza mwili wake kuwaka moto, Yulia alikuwa akijua  anachokifanya katika kumpagawisha.

Hamza mara baada ya kuona  yanakwenda kumshinda alimshika kwenye shingo  kwa  spidi ya hali ya juu na kwenda kumbana kwenye ukuta na kusogeza mdomo wake karibu zaidi huku Yulia akiendelea kumwangalia kwa macho ya kumruhusu lakini yaliojaa waswasi kwa wakati mmoja.

ENDELEA 

Yulia alikuwa  amekabwa kisawa sawa  ukutani , umbali kati yao ilikuwa ni sentimita tatu tu.

Muonekano wa Hamza ulikuwa ni ule wa usiriasi , hakukuwa na ishara  yoyote ya uzembe , alionekana kama vile ni mtu wa karne nyingi zilizopita  na aliinua mkono wake wa  kushoto  na kukiinua kidevu cha Yulia  kwa kukibetua kwa  juu.

“Niachie bwana, unaniumiza ujue?”Aliongea  akilalamika  na hio yote ni mara baada ya kuona  macho ya Hamza yalivyokuwa na usiriasi usiokuwa wa kawaida hata kidogo , ule ujasiri wake mbele ya Hamza ulimpotea na sasa alikuwa ni kama Panya mbele ya  paka.

Muda huo  alikuwa ashapoteza ule muonekano wake wa hadhi ya ubosi , aligeuzwa ghafla tu  na kuonekana kama msichana mdogo ambae amekosa msaada. 

“Unaonaje ukiondoka hapa Tanzania?”Aliongea  Hamza huku akiwa na tabasamu lililojaa uovu na kumfanya  Yulia uso wake  kuwa wa moto  huku  mboni za macho yake zikicheza cheza.

“Usije kujaribu kunichezea na kujaribu kuniwekewa mtego  , maana nikigundua sina uhakika kama utaendelea kuwa salama”Aliongea Hamza.

“Hmmm..”Yulia aliishia kutingisha kichwa akikubali.

Alikuwa akiamini,  kuwa kwake ndani ya jiji la Dar es salaam sehemu aliozaliwa na kuijua vizuri basi angeweza kuwa  na uwezo wowote mbele ya wanaume  na kuwasumbua , lakini hakuamini  Hamza alishajua alichokuwa akiwaza tokea muda mrefu.

Yulia alikuwa akisita  kukubali lakini kutokana na muonekano wa  kutisha wa Hamza alijikuta akikubali kishingo upande , kwasababu Hamza hakuwa na dalili  yoyote ya kutania.

Hamza mara baada ya kuona mwanamke huyo  ameshika adabu yake na ameogopa alimwachia.

“Usije kuthubutu kuongea chochote kilichotokea baina yetu  jijini Zurich , sitotaka  kujiingiza kwenye matatizo kwasababu yako”

“Nimekuelewa , lakini je naweza  kukutana na wewe?”Aliuliza Yulia, hakuwa mwanamke mpumbavu  asielewe nia ya Hamza.

“Kwanini unataka kukutana na mimi?”Aliuliza .

“Mbona nahisi kama unanichukia?”

“Haipo hivyo , lakini  hakuna chochote kati yetu , nilifika Zurich  kwa  misheni maalumu ya kukuua  na nikakuta umeshatekwa tayari  nikakuokoa , kama  nilichofanya kinachukuliwa kama kuokoa uhai  wa mtu  basi  nitakuwa nimeokoa  maelfu ya watu , itakuwa ni kujichosha kuanza kukutana na kila mmoja kwasababu hio tu”Aliongea.

“Sio  kweli , hukuniokoa tu , lakini vilevile umenisaidia kulipiza kisasi kwa kundi lote  la watu waliomuua mama yangu  na  mdogo wangu , ni wewe ulienisaidia kulipiza kisasi na ukaenda mbali  kunipa nauli ya  ndege kurudi nyumbani  kwa kunitoa katika  lile giza  licha ya mbinu yako  kuwa rafu”Aliongea  huku muda uleule akiinamisha macho yake chini.

“Kwa kipindi chote tokea nirudi nyumbani , nimetumia kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya kutuma watu kukutafuta , lakini ilikuwa ngumu kwangu kwani sikuwa nikilifahamu jina lako na unapoishi”

“Ulikuwa ukituma watu kuja kunitafuta?”Aliuliza  Hamza huku akicheka.

“Ulitaka kufanya nini baada ya kunipata , usiniambie mpango wako ni kunilipa kupitia mwili wako?”Aliuliza Hamza  na kumfanya Yulia kumwemwesa lipsi zake , macho yake yalikuwa yamejaa matarajio.

“Kama nipo tayari utaniruhusu?”Aliongea na kumfanya  Hamza kumwangalia huyo mrembo na kisha akavuta pumzi na kuzishusha.

“Ijapokuwa  ombi lako linavutia sana , nataka kuendelea kuishi maisha ya amani , nikijihusisha kwa namna yoyote na wewe nina uhakika  nitajipalia tu  makaa na kuingia matatizoni, isitoshe

mimi siwezi kurudi na  kuwa wa zamani tena”Aliongea.

“Inaonekana mpango wako ni kukaa Tanzaniwa kwa muda mrefu , kama ni hivyo je naweza kukutafuta  japo mara moja moja?”

“Yulia kwa hadhi yako  na nguvu ya familia yako  , hata kama unataka kupata bodigadi mwenye uwezo wa juu  ni  kitu chepesi sana , kwanini iwe mimi?”

“Umejuaje ukubwa wa hadhi ya familia yangu ,  au ulinifanyia uchunguzi kabla?”

“Haina haja ya kuigiza  najua mambo mengi kuliko unavyofikiria , katika   bango linalotambulisha  hoteli yenu , ile Logo inayotambulisha  kampuni yenu  ni  maalumu ambazo  zinatolewa kwa  familia  zenye hadhi  na kufanya  isitumike  kutambulisha biashara za watu wengine  duniani , kampuni yako ni kubwa   hivyo  ni rahisi kukutambulika kimataifa , huwezi kutumia Logo ile bila ya kujua  nguvu yake, hivyo moja kwa moja inaniambia familia  yako imesajiliwa  GREL  na kupewa hadhi ambayo inatambulishwa na ile Logo, familia zote ambazo zina usajili wa hadhi ndani ya  GREL hupewa alama zinazofanana lakini tofautishi kama ile”Aliongea Hamza.

GREL kirefu chake ni Global Registry of extraordinary lineages. Sio sahihi kuiita  GREl kama umoja hadharani kwani haijawahi kutangazwa hivyo  bali  kwa  nje ni kama  jarida tu  au kitabu cha kutambua hizo familia , lakini  kwa siri ni  umoja tena wenye nguvu.

Familia  ambazo zipo katika  orodha ya GREL ni kama vile  familia ya Rockfellers , familia ya Rothchild , familia ya Al Saudi kutoka Saudi Arabia, familia ya  Fujiwara kutokea Japani  na kuendelea.

Kwa lugha nyepesi  unaweza kusema familia hizi ndio  zenye mizizi ya kihistoria ,  kiuchumi na ushawishi ndani ya taifa husika au kwa bara zima, yaani  ndio sehemu ya familia ambazo zipo ndani ya Deepstate.

Sasa  inasemekana   wazo  la kupatia kila familia yenye nguvu  nembo(Logo)  lilitoholewa kutoka katika  utaratibu wa kifamilia  wa  familia za damu ya kifalme  hususani katika mataifa mengi ya  bara la Asia , mfano China na Japani ambapo  familia  kama vile Tang ina  alama yao  ya upekee kabisa ambayo haitumiwi  katika  biashara yoyote ndani ya taifa hilo.

“Wewe ni nani , kwanini unayajua haya yote , umejuaje ile logo ipo  katika GREL?”Aliuliza Yulia kwa mshangao.

“Napenda kujifunza vitu  vingi nisivyovijua , hivyo niliweza kujua mara moja”Aliongea Hamza.

“Ni kweli familia  ninayotokea ipo katika  GREL  lakini hili linahusiana vipi na wewe kuwa  bodigadi wangu?, wewe ndio muokozi wangu  nakuamini ndio maana, nimekusubiria kwa muda wote huo , kwanini hunionei huruma?”Aliongea na kumfanya Hamza kumwangalia kwa macho ya kichokozi.

“Haya yameisha , naonekana kuchoka wakati wewe   hujachoka  , nakubali  uwezo wako wa kuigiza ni mkubwa , kwanza umeuchukua  uhusika wa mwanamke anaeongojea mwanaume wake kwa muda mrefu kukutana nae  na kumlipa  kwa kutumia mwili wake  , tena sasa hivi umetoka katika uhusika huo na unaigiza kuwa mwanamke  kama bikra ambae anaogopa na anahitaji  mwanaume wa kumlinda , ki ufupi   hakuna ukweli wowote  kuhusu wewe , hebu niambie umeweza vipi kunitafuta  na  ni kipi unataka kutoka kwangu?”Aliuliza Hamza na kumfanya Yulia muonekano wake kubadilika  na kuwa wa kikauzu.

Mwishowe Yulia alitoka katika ule  muonekano wake wa  mapozi na kuwa mwanamke mrembo kauzu ambae amesimama kama roboti. “Umejuaje nakugizia tokea mwanzo , nadhani  nilipaswa kuwa makini zaidi”Aliongea  

“Uwezo wako wa kuigiza  ni mkubwa mno , miaka saba iliopita wakati nakuokoa nilikuwa nishajua  muonekano  uliokuwa nao  ni wa kimaigizo tu”

“Kwanini?”Aliuliza  huku akiwa na mshangao , hakuamini  Hamza wa miaka  saba iliopita aliweza kumtambua  mara moja  undani wake ukoje.

“Wazazi wako wote  na wadogo zako waliuliwa na wale  maninja , nilikuokoa na kisha nikakurudisha hotelini , unakumbuka ni kitu gani uliniambia cha kwanza?”

“Nimesahau , nilisema nini?”

“Ulisema una kiu mno ya maji , yaani mtoto ambae mama yake , baba yake na mdogo wake   ndio wametoka kufariki  unarudi hotelini na kitu cha kwanza  baada ya kulia kwa lisaa limoja ni kumuomba mtu usiemjua maji?,watu wengine wanaweza kuona ni kawaida , lakini kwa upande wangu sikuona kitu kile ni cha kawaida, katika moyo wako hukuwa na machungu kabisa ya 

familia yako kupoteza maisha , uliweza kupotezea kwa muda mfupi sana hisia za huzuni ulizokuwa nazo na kuanza kufikira hatua inayofuata”Aliongea na kauli ile ilimfanya Yulia kushangaa.

“Inaonekana  sikuwa msiri vya kutosha mbele yako”Aliongea Yulia.

“Makisio yangu  ni kwamba na wewe pia una ugonjwa wa akili  wa Protesting personality Disorder , nakosea?”Aliuliza Hamza akiwa na tabasamu.

“Hakika una uelewa mkubwa sana , tofauti na mama yangu  wewe ni mtu  wa pili kuijua siri yangu , ningekuwa na uwezo wa kukuua basi ungekufa leo hii”Aliongea akiwa siriasi.

“Duhh!, ili kutimiza malengo yako unataka kumuua kwanza aliekuokoa , yoyote yule anapaswa kufa hata kama ni kwa kumtishia , hizo ndio dalili za ugonjwa  wako”Aliongea Hamza  kwa upole.

“Huu  sio ugonjwa , ni Mungu  ambae  ameniumba kwa kutoniwekea  uwezo wa kuwa na hisia , ili nisisumbuke  na  hisia ambazo hazina maana”Aliongea.

Unachopaswa kuelewa  ugonjwa ambao anauzungumzia Hamza ni aina ya ugonjwa wa akili  ambao mtu anazaliwa nao na tabia yake  kubwa ni kwamba  mtu akiwa na ugonjwa huu  huwezi kumkuta akiishi katika uhalisia wake , maisha yake mwanzo mwisho ni maigizo tu  pili  hata kama anahitaji msaada na akaupokea kamwe hawezi kukubali alisaidiwa na njia pekee ni kumuua aliemsaidia ili kulinda siri  ya kusaidiwa  , dalili nyingine  ni kwamba watu wa aina hii hawana hisia  kabisa, yaani  wapo kama  maroboti yalivyo , yaani hawahisi maumivu wala furaha tofauti ni kwamba utawakuta wanaigiza kuhisi maumivu  au furaha , au kupenda, ndio walivyo, haijawahi kufahamika unasababishwa  na nini  lakini kitaalamu unaendana na ugonjwa wa akili  unaofanana na  Munchausen Syndrome.

“Kama hivyo ndio unavyowaza  , basi hakuna tatizo , ila usijali  siwezi kuwaambia watu kuhusu tatizo lako”Aliongea na kumfanya Yulia aliekuwa  kama roboti kupiga hatua moja mbele na kumwangalia  Hamza usoni.

“Kama ulijua tokea mwanzo kuhusu tatizo langu  kwanini bado ukaendelea kutoa ushirikiano  kwangu?”

“Kama ilivyokuwa miaka saba iliopita , tulikutana kwa bahati mbaya , hivyo haina haja ya kuongea  chochote kuhusu mimi  ili mradi  hatutokutana tena , sitaki kujua wewe ni mtu wa  aina gani na kipi

unafanya, ki ufupi  sitaki kujua chochote kuhusu wewe?”

“Kwanini bado  naona  unaonekana kujali maisha yangu , mpaka kuijua siri yangu?”

“Hapana , ninachomaanisha ni kwamba  sitaki  kupitia maigizo yako unitumie na mimi kama kete yako kwenye mipango yako ,  kwa kusema hayo siwezi kuwa bodigadi wako  au mtu yoyote kwako”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Yulia midomo yake kupinda kwa tabasamu lililojaa uovu.

“Ijapokuwa sijui  ni hisia gani ambazo wanawake wanapata wakimpenda mwanaume  lakini mimi nahisi nakupenda”Aliongea  na kumfanya Hamza kutoa tabasamu  huku akijihisi huu upendo utaanza kumbadilisha muda si mrefu.

“Lakini hata hivyo , kuna kitu kimoja ambacho  hujapatia”Aliendelea kuongea

“Oh! , ni kitu gani hicho?”

“ Sijakutana na wewe kwa kukutafuta , ni kwa bahati tu  tumeonana ndio maana natafsiri kama majaliwa”

“Kama ni hivyo  nadhani nilipangiwa kupatwa na hili  janga?”

“Ndio ,  hili ni janga kwako, lakini kwasababu unajua siri yangu  basi kwanzia leo  hatutojihusisha kwa lolote kati yetu , vinginevyo wewe ufe au mimi nife”Aliongea  Yulia na kumfanya Hamza kugeuka na kuzipiga hatua kurudi alikotoka.

“Nadhani pia unapaswa kuomba sana   isije ikatokea siku moja nikaliharibu ua kwa ukatili”Aliongea Hamza  na  kutokomea  Kitendo cha Hamza kupotea katika macho yake , Y ulia alitoa simu yake katika mfuko na kubonyeza namba.

“It’s me .. Go find someone Called Hamza , I want all his information..”Aliongea kwa lugha ya kingereza 

Baada ya kumaliza kutoa maelekezo aliweka nywele zake sawa pamoja na nguo zake na kurudia muonekano wake  na kutoa tabasamu la kimaringo  na mapozi  na kwa madaha alizipiga hatua kurudi  ndani.

Hamza na Yulia walitumia zaidi ya dakika kumi kwenye kuongea tu , lakini kwa watu ambao walikuwa ndani ya chumba  binafsi , walikuwa na hisia mchanganyiko  kana kwamba ni muda mrefu sana umepita tokea watoke , ikiwemo kwa  Prisila ambae ni kama alianza kushikwa na wivu.

Lidya  na Bahati  walikuwa wakijutia maneno yao kiasi kwamba utumbo wao ulikuwa ukijinyongorota  na kufanya nyuso zao kuonekana mbaya.

“Prisila hivi  ni kweli Hamza ni  fundi wa kawaida tu?”Aliuliza Saidi na kwa upande wa  Prisila ukweli ni kwamba alimjua Hamza juzi  tu hivyo hakuwa na taarifa za kutosha.

“Alikuwa fundi  ndio , lakini sasa hivi  ana kazi yake nzuri tu”Aliongea  Prisila akilenga Hamza  kuwa boyfriend feki wa Regina na pia msaidizi wake.

Ijapokuwa Prisila aliongea hivyo lakini hakuna ambae aliweza kuelewa kile alichomaanisha haswa , ilikuwa ni kama kauli yake ni nyepesi sana kwa swali gumu ambalo ameulizwa.

Muda huo wakitaka kumchimba zaidi ndio muda ambao Hamza  alirudi  na mara baada ya kundi lote kuona hakuna anaekula  zaidi ya kuonekana kama watu wanaesubiria mtu alijikuta akishindwa kujizuia na kutoa tabasamu.

“Nyie mnafanya nini , mbona kama mpo kwenye kikao?”Aliuliza. lakini ilikuwa ndio nafasi ya kila mmoja kuanza kumuuliza maswali Hamza. “Hamza kwanini hukutuambia unafahamiania  na  bosi Yulia?”

“Hamza umefahamiana vipi na bosi Yulia?”

“Bro Hamza , Kaka  mkubwa , hebu kwanza kunywa hii Wine nadhani itakidhi  radha ya  ulimi wako?”

Yaani ki ufupi bila aibu kila mtu alianza kuwa chawa   kwa kujipendekeza kwa Hamza 

Lakini Hamza  hakuwa na mudi ya kuendelea kula tena  na alichotaka  ni kuedelea kumpa kampani Prisila  hivyo aliwapotezea kabisa , isitoshe  alijua kabisa  taifa hili lazima lipo chini ya Yulia , hivyo chochote atakachofanya kinaweza kumletea shida.

“Prisila vipi  chakula  ni kitamu?”Aliuliza Hamza  na Prisila kwa kumwangalia tu Hamza ni kama kuna kitu amekisoma.

“Ni kitamu ila nimeshiba , unaonaje tukitangulia kuondoka , nahitaji kwenda kupumzika”

“Hakuna shida  nitakusindikiza”Aliongea  na muda huo huo wote walisimama  ili kuondoka na watu  hao waliona aibu kwa kuona kwamba Hamza amechoshwa na kujipendekeza kwao.

Muda huo ambao Hamza anataka kuondoka  Yulia alirudi na kuingia  na mara baada ya kuona  Hamza anaondoka alitoa tabasamu  la kumuaga.

“Hamza , siku nyingine  ukiwa na muda  jaribu kuja hata mara moja moja basi , haina haja ya  kuwa mpole mbele yangu”Aliongea na Hamza alitoa tabasamu hafifu.

Muda uleule  Yulia alichukua kadi ya madini ya dhababu kutoka kwa msaidizi wake.

“Hii ni kadi ya daraja la  juu kabisa ya uanachama wa hoteli zetu, ndani ya jiji hili wanazo watu wasiopungua kumi , ichukue  na unaweza kuja hapa muda wowote ndani ya masaa ishirini na nne na hutoweza kulipia hata shilingi”Aliongea  

Lidya, Bahati na tajiri Saidi mara baada ya kuona hio kadi  macho yao yaliwatoka kwa matamanio na wivu , hata kadi ya unachama  ya  Bosi Side haikuwa   ya daraja la juu kama hio, kadi hio ilimaanisha unaweza kuingia  ndani ya hoteli hio na kupata huduma bila ya kulipia  hata shilingi.

Sasa walijiuliza kadi ya  hali ya juu ya namna hio inakuwaje  Yulia anampatia  Hamza, lakini sasa  wakati kila mtu akiitamani  upande wa Hamza aliikataa.

“Nashukuru sana , lakini haina haja”

Lidya na wenzake  kichaa kilitaka kuwapnda , ni kama walikuwa wamesikia tofauti  hata kwa bosi Side alijikuta akikunja ndita bila ya  kupenda.

Ukweli ni kwamba  maana halisi ya kadi hio sio  kwa ajili tu ya kupata huduma  bure katika mahoteli yote ya Prima , bali ilikuwa ikiashiria hadh, sasa inakuwaje Hamza  hataki kadi kama hio  tena kwa kumkatalia mtu mwenye nguvu  kama  Yulia.

Upande wa  Yulia licha ya kukataliwa  waziwazi hakujali sana , alijua Hamza alikuwa akifanya hivyo ili kumuepuka , lakini sasa kadri ambavyo  Hamza alijifanya kumkataa ndio alivyozidi kumtaka.

“Upo sahihi , kwasababu tunafahamina huitaji uthibitisho , unaweza kuja hapa muda wowote , au kuja makao makuu ya kampuni yangu  au nyumbani  , wewe nipigie tu simu”Aliongea huku akiwa na tabasamu.

Na watu nyuma ya  Yulia walijikuta wakishindwa kupumua vizuri , ukweli ni kwamba Yulia  hakuwahi  hata kumjali raisi wa Jamhuri iweje leo aoneshe udhaifu mbele ya Hamza.

Hamza alijua  kabisa huyo mwanamke hakuwa na mpango wa kumuacha kirahisi , lakini alijiambia ili mradi havuki mpaka basi atamuacha aendelee kuongea anavyotaka.

Wakati Hamza akiingia katika gari na kuliondoa ndani ya hoteli hio  watu wale wote walijipanga mstari  kwa ishara ya kumsindikiza,pengine walifanya hivyo kwasababu  Yulia alikuwepo  pia akisindikiza gari ya Hamza kwa macho.

Hamza mara baada ya kufika  barabara ya kuingia

Salasala aliingiza gari katika moja ya mgahawa, alifanya hivyo kwani alijua kabisa Prisila alikuwa na njaa na pia muda ulikuwa umeenda.

Prisila alijikuta akifurahi kuona Hamza alikuwa na uwezo wa kuona ishara ndogo ndogo na kuzifanyia kazi , mfano kujua alikuwa na njaa na kumleta mgahawani.

Muda huo ndio sasa Prisila alipata ujasiri wa kumuuliza Hamza kuhusu  Yulia , imekuwaje kuwaje  amefahamiana nae , maana njia nzima alikuwa kimya.

“Umefahamiana vipi na  Yulia ?”

“Tuliwahi kukutana mara moja  na  nilimsaidia , sio kama nafahamiana nae sana ile  tu kwasababu ya

msaada wangu ndio maana kanichangamkia”Aliongea.

“Kumbe..”Aliongea  Prisila huku akiona kabisa Hamza kuna  vitu anaficha , mwanamke huyu kuna muda alikuwa akiwaza imekuwaje  Hamza ndio ambae alikubali malipo   kwa kuwa boyfriend feki , maana   yeye ndio alibandika lile Tangazo. “Imekuwaje  mara baada ya kuona tangazo  kule kwenye mtandao ukaamua   kutuma ujumbe wa kuwa tayari?”Aliuliza Prisila na kumfanya Hamza kucheka.

“Kama nitakuwa na jibu  basi naweza kusema baba yako alichangia kwa kiasi kikubwa”

“Nini, Baba yangu, kivipi?”Aliuliza  Prisila kwa mshangao , alikuwa akijua Hamza  alikuwa chini ya profesa Singano  ambae ni baba yake chuoni.

“Unajua tokea niujue mtandao wa JamiiFroum , nimekuwa  nikipenda sana kusoma maoni  ya hapa na pale wakati ambao nakuwa sina kazi , sasa siku naona lile Tangazo  siku iliofuata  baba yako ndio alifundisha  kuhusu shauku”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu.

“Kwahio   ulikuja PM kwasababu  ulikuwa na shauku ya kujua kama aliebandika tangazo yupo siriasi?”Aliuliza a Hamza alitingisha kichwa na kumfanya Prisila  kutabasamu.

“Mimi sio mtumiaji sana wa mtandao wa JF ,  ila  baba  ni mtumiaji mkubwa na ameanza kuutumia muda mrefu tu”

“Unaonekana kabisa , mtandao wako pendwa utakuwa ni Insta  na Tiktok?”

“Mimi napendelea Insta na Linkedin , sina akaunti Tiktok ila  muda mwingine natumia”Aliongea  na kumfanya Hamza kuelewa.

“Ila mpaka  Regina kukupa kazi ya  kumtafutia mchumba feki , inaonekana anakuamini sana?”Aliuliza Hamza.

“Sio kuniamini tu namwamini pia , Regina sijafahamiana nae kazini , tulicheza wote tukiwa wadogo?, nimeweza kumfanya rafiki licha ya  tabia yake yake ya kupenda kuwa peke yake , nakumbuka  hakuna ambae  aliweza kufanya nae urafiki kati yangu  wakati analetwa na babu yake,  alikuwa mpole mno na Bibi  Mirium ndio alikuja kwetu kuniomba nicheze na Regina kumchangamsha”Aliongea Prisila akiwa katika tabasamu kana kwamba anakumbuka matukio ya utoto.

“Ulifanya kazi kubwa kwelikwel?”Aliongea  Hamza na kumfanya Prisila kucheka  sana kana kwamba anajua anachomaanisha.

“Ndio maana siwezi kuondoka  katika kampuni ya Dosam , kwasababu ni mimi pekee ambae anaweza kunifungukia  kuhusu anachojisikia”.

“Namini nikuulize swali , ilikuwaje katika wote waliotuma maombi ukachagua  jina langu?”Aliuliza  Hamza.

“Niseme tu licha ya  watu kutoa lugha chafu  katika  maoni yao lakini kulikuwa na maombi zaidi ya mia tano?”Aliongea

“Zaidi ya Mia tano!?”Aliuliza Hamza na  palepale alijikuta akicheka.

“Ndio , hata mimi nilishangaa na nilikesha sana kupitia”

‘Sasa ilikuwaje ukanichagua mimi?”

“Regina ndio alikuchagua , ukweli ni kwamba  aliangalia  nani aliandika  ujumbe mfupi zaidi  na unaoeleweka  na  ulikuwa ni wa kwako na akaniambia niwasiliane na wewe  niweke miadi, alionekana kuwa na uhakika utamfaa, nadhani  ilipangwa  lakini kila nikifikiria  ni uchizi unajua siku  Regina alivyoniambia  nimtafutie boyfriend feki”Aliongea huku akianza kucheka na kumfanya kupendeza mno, Prisila alionekana kujiachia mno mbele ya Hamza kiasi kwamba alijishangaa.

Mpaka wanakuja kutoka walitumia  saa moja kamili na Hamza kwasababu hakuwa na usafiri ilibidi  aite Uber mpaka mawasiliano  ili achukue gari yake  hivyo  aliagana  na Prisila ambae  anaishi Makongo juu.

****

Upande  mwingine  ndani ya gari aina ya Porche Cayenne, Bahati  na Lidya walikuwa  ndani .

Ukweli ni kwamba kitendo cha  Hamza na  Prisila  kuondoka ni kama ile vibe ilipotea na kufanya  hata bosi Side kukosa mudi ya kuendelea hivyo kila mtu alitawanyika.

Sasa wawili hao walikuwa wakirudi nyumbani  na  walikumbana na foleni ya magari mengi barabarani kuliko isivyokawaida na kufanya waonyeshe  kukosa uvumilivu.

“Hivi nini kinaendelea kuhusu yule

Hamza?”Aliuliza Lidya  huku akiwa amekunja  uso

.

“Haijalishi  kilichotokea , ilikuwa ni makosa yako kuanza kumdharau tokea mwanzo  na kuniweka katika  hali tatanishi namna ile , ki ufupi leo tumedhalilika sana”Aliongea Bahati  

“Kwa misingi gani unanibebesha lawama zote mimi , usijione mtakatifu sana  wakati  muda wote ulikuwa ukimkodolea macho  Prisila unadhani sijaona , kama umempenda si useme tu?”Aliongea Lidya kwa hasira.

“Unaongea  upuuzi gani  hebu acha kubadili topiki”Aliongea Bahati  

“Sikia bahati  usije  ukanionyeshea  dharau ukidhani nimekosa soko , naweza kuolewa  muda wowote , wapo wanaume  kibao  wanaonitaka , halafu kama sio mimi usingeweza hata kukaa meza moja na Side”Aliongea  Lidya huku akionyesha maringo.

Upande wa Bahati  aliishia kumdharau  kimoyomoyo  Lidya  na alikuwa akijiuliza  kama kuna uwezekano  wa wao kuendelea na swala lao la ndoa au ndio  mahusiano yao yamefika mwisho , ukweli hakuona  uwezekano wa kuweza kuishi na mwanamke  kama Lidya,  mwanzoni  alimtongoza kwasababu aliona kuna ukaribu kati ya Lidya na Side lakini  baada ya kilichotokea leo  kwa  Side kumpotezea  alimdharau zaidi  Lidya na  moyo wake ulizidi kubadilika mara baada ya kumuona Prisila, akili zake zilimwambbia kabisa anahitaji mwanamke kariba ya Prisila, mstaarabu ambae hababaishwi na vitu  vya kupita.

Wakati akiendelea kuwaza namna  ya kumalizana na  Lidya , kioo cha gari kiligongwa kwa nje na kufanya Lidya na Bahati wote kugeuka na kuangalia na walishangaa mara baada ya kuona sura ya polisi

“Ndugu afande kuna tatizo gani?”Aliuliza Bahati.

“Simamisheni gari pembeni ,  nahitaji kuwahoji”

“Kutuhoji! , kuna kosa lolote ambalo tumefanya?”Aliuliza  Bahati kwa mshangao.

“Sio kuhusu nyie ,  tunafanya uchunguzi juu ya mwanaume anaefahamika kwa jina la Hamza  Mzee,  nadhani mnaweza kutusaidia kwa kujibu maswali yetu mawili matatu”Aliongea  Polisi yule na kumfanya Lidya na Bahati kuangaliana na mwishowe walikubaliana.

Kitu ambacho  hawakujua ni kwamba kila mtu ambae alifika katika hoteli ile ukimtoa Prisila alihojiwa na polisi hao , lakini ukweli ni kwamba sio polisi bali ni watu waliovalia mavazi ya kipolisi.

Kitendo cha polisi kuwahoji kiliwafanya waone kabisa kuna kitu ambacho kinaendelea  katika maisha ya Hamza na jambo hilo liliwafanya kuwa na waswasi nae.

******

Upande mwingine  katika  moja  ya  Bar iliokuwa ikipatikana  ndani ya eneo la Masaki alionekana  Chriss  akibugia bia mfululizo  kama hana akili nzuri huku  macho y ake yakiwa mekundu.

Pembeni yake  alikuwepo  Amosi  Jasusi mstaafu ambae alikuwa akimwangalia  Chriss  kwa macho yaliokuwa na mashaka.

“Bwana Chriss nadhani kwa hali hii hatuwezi kuendelea na  maongezi yetu”Aliongea Amosi.

“Sikia Jasusi bado sijalewa tunaweza kuongea , niambie uchunguzi wako umefikia wapi?”Aliongea  Chriss huku akiongea kwa sauti  ya juu kiasi cha kumfanya Amosi kugeuka na kuangalia nyuma  kama  kuna watu wamesikia kauli yake.

“Nimepoteza muda wangu kuja  hapa , ukiwa sawa kiakili tutaongea”Aliongea Amosi huku akisimama kuondoka.

“Sikia Mzee Amosi nishasema sijalewa bado , akili yangu inafanya kazi , au na wewe pia unanidharau , mimi sijalewa kaa chini tuongeee”Aliongea  kwa nguvu  lakini Amosi alijua kama akiendelea kubakia katika eneo hilo basi siri ya uchunguzi anaofanya  itabumbuluka hivyo  maamuzi ni kumuacha.

“Prisila  nitamfanya mbaya huyo boya uliemtambulisha leo , Mimi ndio  Chriss Gabusha,  uwezo ninao na nia ninayo , Ma**na zako  Prisila unaniumizaje kiasi hichi , ni mwaka wa ngapi  huu nimekufuatilia  na kutaka uwe wangu….”Chriss aliendelea kuongea kwa hasira  kiasi kwamba watu walishaelewsa bwana huyo alikuwa  ametoswa , wanawake waliokuwa hapo ndani ambao walikuwa wkaimfahamu Chriss walishangaa na kujiuliza ni mwanamke gani anaweza kumuumiza  mwanaume

mtanashati na tajiri kama Chriss , lakini   licha ya maswali yao  huo ndio ukweli  kwamba ametoswa , Prisila hakuwa akimpenda  na hicho ndio kilichomuumiza maana alikuwa amemfuatilia msichana huo kwa miaka miwili mfululizo bila ya mafanikio.

Sasa habari za Prisila kumtambulisha  mpenzi  wake katika  kusanyiko  lao zilimfikia  kutoka kwa Saidi huku akienda mbali   kumwambia  mtu ambae  ametambulishwa anaonekana kuwa na ukaribu na Yulia, huku akimbeza  kwa kumtania kwamba maneno yake yote yalikuwa ni bure , Side alifanya hivyo kwasababu alikuwa akimpenda pia Prisila na  alikuwa na kinyongo na Chriss ambae alimuona  kama mwanakauzibe.

Muda huo wakati  bwana huyo akiendelea  kufakamia kilevi  Alex na James waliweza kuingia  na kusogea katika meza aliokaa Chriss huku wakimwangalia kwa mshangao na kisha waliangaliana.

“Chriss hebu punguza kunywa  bwana , unajiabisha ujue”Aliongea Alex huku akimpokonya  Chriss chupa ya Whiskey.

“James , yule boya wako  aliekuchukulia  mwanamke  wako amemchukua na wangu”Aliongea  Chriss na kumfanya James kushangaa.

“Chriss  unamaanisha nini , ongea vizuri nikuelewe?”

“Nimesema boya wako kamchukua na demu

wangu  fullsto…p”Aliongea  na dakika ileile alijilaza kwenye meza   na haikueleweka alikuwa usingizini au pombe zimemzidia na kupoteza fahamu.

“Anamaanisha nini  huyu mpuuzi?”Aliuliza  James na kumfanya  Alex kutingisha mabega.

“Mimi najuaje , hebu tumbebe tumrudishe home”Aliongea Alex na  James alikubali na  walianza kumkokota Chriss na kumtoa  ndani ya Bar hio.

Upande mwingine  mara baada ya Amosi kutoka  ndani ya Bar ile  akiwa ameshindwa kuongea na Chriss  aliingia kwenye gari lake kama kawaida , lakini sasa  kitendo cha kuvuta pumzi  alijikuta akinasa harufu  ya marashi ambayo imeongezeka  ndani ya  gari yake na palepale alihisi hatari lakini hata hivyo alichelewa kwani kabla hata ya kugeuka  alijikuta akifunikwa na Helmet zito kichwani  na kumfanya  kukosa pumzi na  kupoteza fahamu.  

******

Hamza akiwa njiani  kuelekea nyumbani aliweza kupokea simu kutoka  Amiri rafiki yake akimuulizia juu ya  lile swala  la lugha  na Hamza ukweli ni kwamba hakuweza kulipatia ufumbuzi kabisa.

Amiri upande wake anasema Mellisa anazidi kubadilika  kitu ambacho kinampa mawazo , ijapokuwa  hakuongea anabadilika kivipi lakini Hamza alielewa na kuona  ngoja  alifanyie kazi.

Baada ya kufika  nyumbani  aliweza kugundua  nyumba yote ilikuwa  kimya ikiashiria hakukuwa na mtu nyumbani , ilikuwa ni bahati tu  Hamza alikuwa  na kadi pamoja na  nywira za kufungulia mlango hivyo  hakupta shida ya kuingia ndani.

Mara baada ya kuingia katika chumba chake tu , jambo la kwanza  alilofanya ni  kuwasha laptop  aliopewa na Regina  na kisha alihamisha lile faili la  Amiri  kutoka kwenye simu yake  na kulituma kwa njia ya Email  kwenda kwa barua pepe ambayo aliijua yeye.

Baada ya kufanya hivyo alijiunga kifurushi cha  kimataifa na kuingiza namba  ya nje ya nchi na kupiga simu na hazikuchukuwa  dakika nyingi sauti ya mwanamke aliekuwa akitumia lugha ya Kiswedish  ilisikika.

“My Prince  hatimae umenitafuta baada ya kimya cha  muda mrefu”Sauti ilisikika hivyo   huku  ikionekana upande wa pili alikuwa akijaribu kuzuia  hisia zake.

“Niwie radhi sana  Sally sio makusudi”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu kana kwamba alifurahia kusikia sauti hio.

“Haina haja ya kuomba radhi  najua umechoka na ulihitaji kupumzika”

“Naomba radhi kwa kukuachia matatizo na kufanya uyafanyie kazi  , utakuwa umechoka sana kurekebisha makosa yangu”

“Sio kweli ,  kuniamini kwako  na kuniachia  familia yako niiangalie  ni heshima kubwa  kwangu,  kwanini nichoke?”

“Huwa navutiwa sana na ukamilifu wako , ni wewe pekee ambae  najua unaweza kunisaidia mambo mengi , vipi  hali ya ndugu zangu?”Aliuliza Hamza.

“Kila mtu yupo bize na mambo yake , wewe ndio uliwaambia wasikutafute  na wamejitahidi kupotezea mawazo ya kukumbuka kwa kujiweka bize , kila mtu  yuko  sawa..”Aliongea na kumfanya Hamza kucheka kidogo 

“Ungenifuata  pengine sasa hivi ungekuwa na maisha magumu sana ,  angalau  kuwa nao karibu  kunakufanya upumue”

“Ukiongea hivyo unakosea , maisha yangu  yote  natamani kuwa karibu yako katika mazingira  yoyote yale”Sauti ilisikika na kumfanya Hamza kutoa tabasamu la uchungu.

“Anyway , nimekutafuta   kwasababu  kuna kitu nataka  ujaribu kukifanyia uchunguzi?”

“Nielekeze tafadhari”

“Nimetuma faili la sauti kupitia  barua pepe yako , hebu sikiliza lugha iliotumika  nataka kujua ni sehemu gani duniani  wanazungumza lugha hio , nitafute ukiwa na majibu ya uhakika”Aliongea 

“Hakuna shaka  nitampa kazi  mtu wa lugha  kufanyia kazi  , naamini  mpaka wewe kushindwa kuijua  hio lugha basi itakuwa ni ngeni  kwenye masikio yako”

“Nadhani umenielewa , Sally  nashukuru kwa kila unachofanya kwa ajili yangu..”Aliongea Hamza na hakusbiri  jibu upande wa pili na hio ni mara baada ya kusikia sauti za  viatu kutoka  chini.

Hamza mara baada ya kushusha  pumzi  na kujituliza  alitoka kwenye chumba chake na kushuka chini sebuleni , ilikuwa ni kama alivyohisi Shangazi na Regina walikuwa wamerudi.

Kilichomshangaza  Hamza ni kwamba  baba yake Regina  na mke wake walikuwepo pia  na  walikuwa wakisukuma kiti cha magurudumu   ambacho kimekaliwa  na mwanamke mzee.

Bibi huyo licha ya kuonekana kuwa mzee lakini alikuwa  na muoekano wa hadhi. Licha ya sura yake kujikunja  lakini   mpangilio wa uso wake ilionyesha  alikuwa ni mwanamke mrembo wakati wa ujana wake.

Hamza hakuwa na haja ya kujua  bibi huyo ni nani , alijua fika atakuwa ndio  bibi yake Regina, hivyo alimsogelea na kumsalimia.

“Nimefurahi kukutana na wewe bibi , jina langu

naitwa  Hamza mzee , Mpenzi wa

Regina”Alisalimia bila ya kumjali mzee Wilsoni  na mke wake.

“Kwahio wewe ndio Hamza , sio mbaya , sio mbaya , unaonekana kuwa mtoto mzuri , ushakula chakula cha usiku?”Aliuliza. “Ndio bibi , vipi  wewe umeshakula?”

“Wote tumekula”Aliongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa na alisimama na kumwangalia Regina.

“Vipi hali ya bibi , mbona anaonekana kuchoka sana?”

“Sijachoka  kabisa , baada ya kuona ni kweli  Regina kapata mchumba  nimefurahi mno , sijachoka kabisa”Aliongea.

Upande  wa Regina alijikuta akizungusha macho yake  mara baada ya kuona namna Hamza alivyokuwa akiongea  na bibi yake  bila wasiwasi.

“Bibi  unapaswa kupumzika mapema , kesho  utaendelea kufanyiwa uchunguzi wa afya yako”Aliongea Regina.

Kiasili familia ya  walikuwa wakiishi Mkoani Tanga Wilaya ya Bumbuli, ni umbali mrefu kidogo mpaka  mpaka kufika Dar es salaam , hivyo  kwa mzee  kama huyo atakuwa amechoka sana.

“Regina kwanini unataka kunipumzisha mapema

,bibi yako nataka  kuongea kidogo na Hamza”Aliongea 

“Mtoto masikini kama huyu utaongea nae nini?”Aliongea Lamla.

“Wewe Lamla unaongea nini , baba mkwe wako  alikuwa masikini pia  wakati  akianza kufanya biashara  kutoka chini , kwahio unanidharau na mimi kuolewa na mwanaume masikini?”Aliongea na kumfanya  Lamla uso kumuiva.

“Mama  sijamaanisha hivyo?”

“Miaka mingi imeenda lakini sioni mabadiliko yako , Vipi kwanza  Frank anafanya nini siku hizi?”

Alikuwa akiulizia mdogo wake Regina  yaani mtoto wa Lamla na Mzee Wilson, na swali lile  lilimfanya Lamla sura kuwa mbaya.

“Frank yupo bize siku hizi kufanya Research  yake , ndio maana hajaweza kufika   ndani ya muda”Aliongea 

“Mtu  sio kama anasomea nje ya nchi , yaani hapo UDSM   tu ameshindwa kuja kumsalimia  mtu alietoka Tanga?”Aliongea  huku akionyesha kutoridhika kabisa.

“Hapana mama , ni  kwamba tu yupo bize ,kila siku anasema atakuja kutembelea lakini imekuwa ngumu kutokana na ratiba za chuoni”

“Hebu  acha kumtetea , lini  alikuja kunisalimia, inamaana hata kupiga simu kumshinda?, kwanini anashindwa kuwa na tabia ya  Regina , licha ya umri mdogo lakini ameweza kuendeleza alipoishia babu yake na kuwa  bosi wa kampuni   lakini bado anapata muda wa  kunitafuta”

“Mama nitamrekebisha Frank , hajui  hata anachofanya kama anakosea”Aliongea Mzee Wilsoni.

“Mnaweza kuondoka sasa , nitalala hapa nyumbani kwa Regina”Aliongea

“Mama , hebu fikiria vizuri , tumeshakuandalia chumba chako  cha siku zote”Aliongea Mzee Wilsoni kwa uchungu.

“Nimekuja  Dar mwenyewe na nitaishi ninapotaka kuishi , rudini nyumbani mkamuadabishe  mtoto wenu”Aliongea akiwa siriasi na kwasababu walimjua  hakawii kukasirika , Mzee Wilsoni na  mke  wake walishia kumwangalia  Regina kwa dakika na kisha wakaondoka. 

“Mariposa  hebu nipeleke chumbani kwangu”

“Sawa Madam”Aliongea Shangazi na kumwendesha bibi kuelekea katika chumba chake  Kulikuwa na chumba kikubwa cha Master   floor ya kwanza , ni kwa ajili ya wageni lakini  kutokana na kwamba  ni ngumu kumpandisha juu hivyo  chumba hicho kilimfaa  bibi yake Regina.

“Dokta Ronicas hajakuambia ni wapi  tunapaswa kuonana nae kwa ajili ya kuonana na bibi?”Aliuliza Regina.

“Ni hospitali  ya Muhimbili ,  kaalikwa kutoa hotuba kwa wanafunzi  katika chuo cha MUHAS, baada ya hapo ataingia hospitalini”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kumwangalia kwa maswali.

“Asante kwa hili?”

“Huna haja ya kunishukuru , isitoshe  tunakaribia kuzeeka ndani ya ndoa yetu”Aliongea Hamza akijaribu kumtania.

“Unaongea upuuzi gani  , nani anakaribia kuzeeka?”Aliongea huku akimkodolea  Hamza na kujiambia kadri  wanavyozidi kuzoeana ndio ambavyo  Hamza  anazidi kushindikana.

Muda huo  Shangazi aliweza kutoka  na kuwaita Hamza na Regina.

“Regina  na Hamza mnaitwa , Bibi yenu  anataka kuongea na nyie”Aliongea na kufanya Hamza na Regina kushangaa ,  Regina alijiuliza ni kitu gani ambacho bibi  yake anataka kuongea maana  ni kama wameongea  kila kitu njia nzima.

Baada ya kuingia Bibi Mirium alikuwa  ameshalala tayari na alionekana kuchoka.

Kwa kuangalia tu Hamza aliweza kuona  bibi huyo yupo katika hatua za mwisho za ugonjwa  wake.

Ijapokuwa  hakuwa daktari  lakini alijua fika  kwa hali ambayo amefikia hakuna kitu ambacho  Flora anaweza kufanya kumtibia, labda kuwe na teknolojia mpya.

“Bibi kwanini usipumzike kwanza ni kitu gani unataka kuongea?”Aliuliza Regina  akikaa pembeni ya kichwa cha bibi yake.

“Sidhani kuna haja  ya mimi kupumzika haraka haraka , isitoshe  ninakwenda kupumzika  kwa muda mrefu siku chache zijazo”

“Bibi usiongeee hivyo  , hakuna kitakachokutokea , kesho  utakutana na Dokta Ronicas , ni dokta namba moja dunia nzima  anaeaminiwa hata kutibia wafalme , nina uhakika ataweza kukuponyesha”Aliongea Reigna  lakini Bi Mirium hakuona haja ya kuongea zaidi na alimshika mkono Regina.

“Kama kweli unataka niishi japo kwa siku chache , unapaswa kunipa tumaini…”

“Nipo tayari  Bibi , ni kipi nifanye?”

“Nataka muoane haraka  iwezekanavyo , nikishaona umebeba ujauzito sitotaka kuondoka kwa haraka mpaka nimuone mjukuu wangu ili

nikikutana na babu yako  niwe na stori nzuri ya kumwambia”Aliongea 

Previoua Next