Reader Settings

SEHEMU YA 47.

Regina pia alishangaa na  kumwangalia  Frank kwa ukauzu.

“Frank unachotaka ni nini?”

“Sister hakuna  ninachotaka , nataka kuongea na

shemeji yangu sidhani ni tatizo , isitoshe  siku zote

kuna mazungumzo ya kiume  huwa  yanafanyika”Aliongea  huku akicheka 

“Hamza unaweza kuondoka  , Frandk anataka kuongea na wewe  sio mbaya , isitoshe Dokta Ronica hajafika bado”Aliongea  Bibi  huku akijilaza vizuri kwenye kitanda.

“Wapi tunaenda kuongea?”Aliuliza Hamza. “Wewe nifuate  tu”Aliongea na kisha alianza kuongoza njia.

Regina alikuwa na wasiwasi , baada ya wote wawili kutoka alimsogelea bibi yake na kumuongelesha kwa sauti ya chini 

“Bibi umemuona  Frank alivyo katika macho yake anachokiwazia ni hisa zako , haonekani kujali  afya yako kabisa”

“Najua.. lakini vyovyote vile ni mdogo wako na  ni mjukuu wangu”Aliongea  na kumfanya Regina kujawa na hisia zisizoeleweka  na aliishia kugeuka na kunyamaza.

Upande  mwingine  Frank  alimchukuaHamza mpaka eneo la kuegeshea magari .

“Shem  vipi  tena , kwanini umenileta kote huku?”Aliuliza Hamza  akiwa na tabasamu.

“F*ck you , nani  shemeji yako?”Aliongea kwa hasira huku akimtolea Hamza macho.

“Wewe ndio ulieniita Shemeji  wala sijakulazimisha?”

“Unakichaa , unadhani mpuuzi kama wewe masikini masikini unaweza kuwa  shemeji yangu?”Aliongea  huku akiingiza mkono wake mfukoni.

Hamza aliishia kumwemwesa midomo huku akijiwazia huyu  Frank anaonekana kuwa  na akili ndogo mno , licha ya kwamba alikuwa na undugu na Regina alijiuliza imekuwaje kuna utofauti mkubwa wa akili baina yao.

“Kwahio umeniita hapa kwa ajili ya kuongea huu upuuzi?”

“Nimekuja kukuambia Dada yagu ataolewa na 

James na si vinginevyo , lazima aolewe na familia ya Mzee Benjamini , hivyo kama unajielewa  ni bora ukaondoka ndani ya hili jiji mapema  na kupotea  nisikuone tena”

“Kama niliependana nae ni dada yako wewe   kinachokuuma nini , unadhani naweza kusikiliza pumba zako?”

“Wewe  huwezi kunielewa kabla  ya kufanywa kiwete”Aliongea na muda  uleule alipiga simu na kwa sauti kubwa alionekana kuita watu.

Ilionekana kuna watu ambao alikuwa tayari ashawaandaaa kwani ndani ya nusu dakika  wanaume wawili warefu na waliojazia waliingia  huku wakiwa na  vifaa flani vya   mawasiliano  kwenye masikio yao , walionekana kama wanausalama .

“Hawa wote ni mabodigadi wangu , wamepitia jeshi kabisa , nikitaka kukupiga ni swala la dakika tu , vipi ushaanza kuogopa?”Aliongea  na ilionekana alitegemea mabodigadi hao kumuogopesha Hamza.

“Yaani unataka mabodigadi wanipige , huogopi  nikikusemea kwa  dada na bibi yako?”

“Hio ni baada ya kukugeuza kiwete , unadhani najali  ukiwaambia wala kunishitaki , hawawezi kunifanya chochote kwa ajili ya mtu usie na undugu kama wewe”Aliongea huku akicheka.

“Naamini hujawa mjinga kiasi cha kufanya haya maamuzi?”

“Mpuuzi  wewe yaani mtu huna mbele wala nyuma lakini unataka kuvunja undugu  tunaotaka kutengeneza kati ya familia yetu na ya Mzee James , mimi mrithi wa  mali za familia siwezi kuona hili likitokea  kwasababu ya wewe na mjinga mwenzako  Regina , hivyo nakupa onyo mara ya mwisho  unaondoka au huondoki?”

“Umesema   huwezi kuruhusu mtu kama mimi lakini kwanini unamwingiza na dada yako?”

“Kwahio nini sasa  au ndio unategemea mwanamke kuja kukusaidia hapa, wewe ni..”Kabla hata  hajamaliza sentensi yake alijikuta macho yake yakiingiwa na ukungu.

Frank alijikuta akipiga  ukulele huku mikono yake ikiwa mdomoni kwake kutokana na maumivu makali ambayo alikuwa akiyasikia.

Ilikuwa ni pigo kutoka kwa Hamza alilomlenga usoni , ijapokuwa hakutumia nguvu lakini  ngumi yake ilitosha  kumletea maumivu  makali mtoto wa kudekezwa kama huyo.

“Takataka kama wewe unajilinganisha vipi na mimi

, ushukuru tu sina mpango wa kukuua”Aliongea Hamza  huku akimwangalia  Frank ambae ashaanza kulia.

“Mpigeni huyu mshenzi , mpigeni mpaka afe”Aliamrisha mabodigadi wake.

Mabodigadi wale walijikuta  wakianza kumshambulia Hamza kulia na kushoto lakini  Hamza hakuongea chochote ilikuwa ni teke lake moja na ngumi yake moja  aliwafurusha wale mabodigadi kama vifurushi na kwenda kujigonga kwenye  magari.

Kitendo kile kiliwafanya waanze kumwangalia Hamza kwa hofu , ukweli ni kwamba hawakujua hata wamepigwa vipi  kwani walijikuta  tu wakiogelea hewani.

Hamza  baada ya kuwapatia kipigo cha kushitukiza  wale mabodigadi alimsogelea  Frank na kisha alimshika kola na  kumning’iniza hewani  na kuanza kumwangalia na macho yasiokuwa ya kawaida , kitendo kile  kilimfanya Frank kuanza kushikwa na ubaridi wa hali ya juu mno kiasi kwamba kidogo  tu angejikojolea.

“Bro.. hapana shemeji naomba unisamehe sitorudia tena , nimekosea usinipige”Aliongea huku akilia kama litoto jinga.

“Kumbuka hakuna dawa ya majuto  kwenye maisha , ukichagua kufanya  jambo baya basi   ni kosa lako  la maisha, lakini hata hivyo mimi ni mvumilivu sana , hivyo leo  nakupa onyo  lakini kumbuka kwenye maisha yangu sijawahi kumpatia mtu  nafasi mara mbili”

Frank  alikuwa ni kama amechanganyikiwa , hakuweza hata kumsikia Hamza vizuri  kwani alikuwa akiogopa mno.

Hamza aliishia  kumtupa Frank kama furushi kwenye lami na kisha  alitoa gomba mfukoni na kuitoa karatasi na  kuanza kuitafuna  bila ya wasiwasi huku akirudi  alikotoka.

Mara baada ya kufika katika wodi , kulikuwa na watu wengi wamesimama mlangoni  na  karibia wote walikuwa ni viongozi wa hospitali.

“Ilikuwa ni dhahiri  Ronica ashafika na kuanza matibabu , Hamza hata hakujali watu hao na alijiminya minya na kuingia ndani  na hatimae aliweza kumuona Regina akiongea na Dokta Ronica na Flora mara baada ya kumuona Hamza alimkonyeza huku akitabasamu.

“Well , do you want a CT?”Aliuliza Hamza akimaanisha je anahitaji  vipimo vya CT scan.

“No need , I‘ve already seen  them all , there are migratory  thrombophlebitis  and arterial thrombosis..”Aliongea 

“Duuh , ndio ipo hivyo…”Aliongea Hamza huku akionyesha kukunja sura.

Mara baada ya Regina kuona  Flora na  Hamza wanaongea kingereza huku wakitumia maneno ya kitabibu alijikuta akizidi kujiambia  Hamza anazidi  kutokuwa mtu wa kawaida.

Isitoshe mtu wa kawaida asingelewa maneno ya kitabibu lakini  Flora aliongea kama vile Hamza  anamuelewa.

“Dokta Ronica unaweza kuelezea shida yake , sijaelewa kitu”

“Wewe niite tu  Flora , ni mpenzi wa Hamza  hivyo haina haja ya kuonyesha heshima kiasi hicho mbele yangu”Aliongea  na kumfanya Regina kuona aibu huku akitaka kuelezea yeye sio kama anavyofikiria lakini alishindwa kutokana na uwepo wa bibi yake.

“Miss Regina , ijapokuwa naweza kuonekana mkatili   kwa kauli yangu , lakini naomba niseme tu kwamba  huna haja tena ya kupoteza nguvu na pesa zako kutafuta madaktari , kitu pekee unachoweza kufanya  ni kumuandaa mgonjwa kwa ajili ya saa yake ya mwisho”Aliongea na kauli ile ilimfanya  Regina sura yake kujikunja.

“Dokta  hata wewe huwezi kufanya chochote?”

“I am so sorry , I am a doctor not a God”Aliongea  kwa  sauti ya radhi huku akimwambia kwamba yeye ni daktari na sio  Mungu.

“Ukweli ni kwamba  mara nyingi  nakutana na wagonjwa ambao  kesi zao zinakuwa ni ngumu sana kimatibabu  na   katika utaalamu wangu  ni asilimia therathini tu ya wagonjwa waliopona , asilimia sabini  wengi  wao hawatibiki”Aliongea.

Ijapokuwa Regina alikuwa amejiandaa kwa  taarifa hio lakini  ilikuwa ni huzuni kwake  kusikia  hakuna tumaini  lolote kabisa na alijikuta machozi yakimtoka.

Bibi  nae alikuwa akisikia kila kitu  juu ya afya yake na  mara baada ya kuona namna  mjukuu wake alivyokuwa na  huzuni aliishia kumwambia asogee karibu yake.

Ukweli ni kwamba tokea  jana  mara baada ya

Ronica kupokea  taarifa ya kimatibabu ya  Bibi Mirium alishajua   anakufa na ni swala la muda tu  ila kufika kwake ni kwa ajili ya kumheshimisha  Hamza  pekee.

Lakini yeye kama dokta alishakutana na hali kama hizo mara nyingi na huwa hampi mgonjwa matumaini hewa.

Baada ya hapo  Dokta aliaga  na kisha alimpa ishara Hamza kuongozana nae nje na waienda kusimama kwenye balkoni.

“Unaondoka leo?”

“Ndio , nitaondoka mchana  lakini kabla  ya kuondoka nimesikia taarifa inayokuhusu”Aliongea.

“Nini?”

“Kuna mtu alivunja  katika maabara ya Profesa  na aliweza kupata  anuani ya mahali unapoishi kwa sasa , hivyo  ni sawa na kusema inajulikana unaishi  Dar es salaam”

“Umeshachelewa kuniambia mbona , watu tayari walishatumwa na kuanza kuniletea matatizo”Aliongea na kumfanya  Flora kushangaa.

“Mapema hivyo?”

“Doctor Genesha amejua kuniletea matatizo mno , nataka ukifika  ukusanye kila  kinachomuhusu  na uchome moto , ndio namna pekee ya kuniepushia na matatizo”

“Vipi kuhusu tafiti ya Mti Wa uzima , unataka na zenyewe zichomwe moto?”

“Bado tu unazo hizo tafiti , zitakuletea mtatizo  mno , ijapokuwa hatujapiga hatua  yoyote kwenye  kutafsiri  lakini huwezi zuia shauku na matamanio ya watu wenye tamaa”

“Lakini  tafiti ile ndio maisha ya  Mwalimu na alikufa kwa ajili  ya kuilinda”Aliongea Flora kwa kusita.

“Utafiti  wake haujakamilika na Tembo wa Trishaza ameshakufa , chukulia tu kama ndoto  nzuri na  baada ya kuamka sio uhalisia”Aliongea Hamza akiwa siriasi.

“Sidhani kama ni kweli , taarifa za siri nilizosikia ni kwamba kabla ya Profesa kupoteza maisha alishafanikiwa na matokeo ya  tafiti yake  alimpatia rafiki yake wa karibu , kwa  ninavyojua Profesa hajawahi kuwa na rafiki  wa karibu tofauti yako”Aliongea na kumfanya Hamza kumwangalia  Flora na macho yaliojaa usiriasi.

“Inamaana hata wewe  huniamini?”

“I am Sorry my Prince , I‘m just curios”

“Curiosity is sometimes not a  good thing”Aliongea akimaanisha kwamba shauku  muda mwingine sio nzuri na Flora alitingisha kichwa kumwelewa.

“Nitaondoka  kwanza , napaswa kwenda kuangalia kinachoendelea”Aliongea Hamza na Flora alitingisha kichwa.

Wakati  Hamza anakaribia mlango ulifunguliwa na Regina alitoka , ukiachana na macho yake kuwa mekundu lakini alikuwa amerudi katika hali yake ya kikauzu.

“Nipeleke kazini”Aliongea.

“Hutaki kuongozana na bibi kurudi nyumbani?”

“Nitaongozana na wewe, isitoshe napaswa  kukujua  kidogo  kwa muda  haina haja ya kuwa na haraka sana , vipi au huoni unapaswa kujiandaa?”

“Kujiandaa na nini?”Aliuliza  Hamza akimwangalia Regina  kwa mshangao,

*******

TEL AVIV- ISRAEL, 13;25.

Ni saa  saba dakika ishirini na tano  katika uwanja wa ndege wa kimataifa  wa Tel Aviv Israeli  , katika eneo la maegesho ya magari ziliingia gari tatu  mbili zikiwa gari ndogo za kifahari  na  moja ilikuwa ni gari   ndefu ya kifahari  aina ya Cadillac escalade ESV isiopitisha risasi.

Baada ya gari zile kusimama gari iliokuwa mbele  kabisa  walishuka vijana wakiyahudi waliovalia suti na miwani pamoja na vifaa vya mawasiliano.

Haikuhitaji akili  kujua kuna mtu  mzito ambae anapokewa ndani ya eneo hilo   na ilikuwa kweli kwani ndani ya dakika chache baada  ya ndege ya kifahari  kutua , alitoka mwanaume  katika mlango wa  watu mashuhuri mzee wa makamo ambae ameongozana  na watu wanne  kati yao mmoja alikuwa mwanamke na kwa tembea yake ilipaswa kuonekana  wale wote walikuwa ni wasaidizi wa yule mzee aliekuwa  na  mvi wa umri kama wa miaka  sabini hivi.

Dakika ileile mara baada ya  mzee yule kutoka nje  kabisa wale watu ambao walikuja na  gari la kifahari walimsogelea yule mzee na kumzingira huku kiongozi wa msafara akijitambulisha kwa dakika chache na  baada ya pale walioekana kuelewana na kusogelea lile gari la milango  mingi na bwana yule aliingia pamoja na yule mwanamke na  bwana  mwingine  na kisha waliobakia  mmoja aliingia katika gari ya nyuma huku mwingine akiingia  katika gari ya mbele.

Ilichukua dakika chache  tu   gari zile zilikwenda

kusimama    katika jengo la hoteli ya David Kempisky na kupokelewa na  wahudumu waliokuwa nadhifu na kumuelekeza  moja kwa moja kuingia ndani.

Lakini  Mzee  yule mwenye nywele zake nyeupe kadri alivyokuwa  akipiga hatua  ni kama kuna hali ya wasiwasi iliokuwa ikionekana katika  macho yake, mara nyingi  kwa kufika hotelini alipaswa kuwa na hali ya utulivu  kwa kuelekea sehemu ya kupumzikia lakini kulikuwa na wasiwasi.

Yule  mwanamke  wa  makadirio ya miaka kama  therathini hivi  mwenye nywele zake nyeusi ni kama aliona  hali aliokuwa nayo bosi wake na alitoa kitu  kama bublish kutoka kwenye mkoba na kumpatia na kisha akampatia na maji na mara baada ya dakika  moja tu alijikuta akivuta pumzi na kutulia  na hatimae lift  ilifunguka  na safari ya kuingi katika korido  ilisonga huku wakipokelewa na Maneja na walienda kusimama katika  mlango  uliokuwa  na maandishi  makubwa ya VVIP na kwa nje alionekana  kuwepo mwanamke  mlinzi ambae alikuwa amekakamaa mwili na baada ya kupewa kadi na  yule mwanamke, alionekana kuelewa na kisha  aliongea  kupitia kifaa cha mawasiliano na mlango uifunguka palepale.

“Welcome Mr Alfonso!!”

Sauti ya kike iliongea na kumfanya yule mzee kupagawa na mara baada ya  kuangalia mtu aliekuwa mbele yake sura yake ilianza kujikunja na hata ule wasiwasi kupotea.

“Frida kwanini ni wewe hapa?, yupo wapi Prince?”Aliuliza  na  swali lake lilimfanya Frida  kutoka katika tabasamu  na kuwa na uso uliojaa usiriasi na kuanza kupiga hatua kiasi cha  kufanya  bwana alieitwa Alfonso kurudi nyuma kwa hofu. ******

Upande  mwingine  katika makazi ya  Raisi Mstaafu Mzee Mgweno  Mandia  kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea , kikao hiki  kilikuwa kikihusisha  kamati ya  kampeni ya Mheshimiwa Jongwe  pamoja na wadhamini wake wakuu.

Moja ya watu ambao walikuwa wakitambulika kwa sura alikuwa ni  MzeeBenjamini mmiliki  wa kampuni ya Zena.

Watu wote walikuwa wamekaa kwenye masofa ya  gharama na  mtu ambae alionekana kukosekana ni Mzee Mgweno mwenyewe , ilikuwa ikionyesha ni yeye  pekee ambae  alikuwa akisubriwa.

“Mzee Benjamini   misheni yako naona  inazidi kuchukua muda , imekuwaje ukashindwa kuimeza  kampuni  ya Dosam , unarudisha  nyuma juhudi za mheshimiwa  katika ujenzi wa ngome yake ,  umeshakuwa ufa  tofauti ya gundi”Aliongea.

“Kwavava  unaongea nini? , kitu pekee ambacho  una mchango  katika  ujenzi wa ngome ya mheshimiwa ni cheo chako cha umakamu ndani ya  kitengo cha MALIBU , ukivuliwa hicho cheo  wewe sio tofali tena unabakia kuwa tope”Aliongea Mzee Benjamini na kauli ile ilifanya baadhi ya watu kutabasamu na baadhi ya watu  kuingiwa na wasiwasi.

“Acha kujipa umuhimu ambao hujapewa , mtu mwepesi kama wewe huwezi hata kutofautisha kati ya seruji  na tope  ndio  maana huwezi  kuona umuhimu wangu ,  Shame on you”Aliongea na kumfanya  Benjamini kutaka kupandisha lakini alizuiwa na bwana aliekuwa karibu yake.

“Kwavava  hivi ni lini  mtakuja kukaa meza moja bila ya kugombana , sisi wote ni familia moja maswala yenu  binafsi hapa  hayana nafasi , kwa  nje Afande Kwavava unaaminiwa kuwa na busara lakini  mbele ya Benjamini unashindwa kujizuia  ni kipi kinaendelea kati yenu?”Aliongea na kuwafanya wote wawili kunywea.

“Mzee Jongwe kama kawaida yako , nadhani mheshimiwa hakukosea kukupigia chapuo mpaka sasa  unapeperusha bendera ya chama , neno lako moja tu  kelele  kwisha”Aliongea  na kauli yake ilimfanya Mzee Jongwe kutoa tabasamu hafifu.

“Mheshimiwa Lughalila  huna haja ya kwenda mbali kwenye kunisifia , kama nilivyosema  nafasi yako baada ya kushinda  ipo wazi”Aliongea Jongwe na kumfanya  jamaa alieitwa  Lughalila  kutoa  tabasamu.

Dakika ileile mlango  ulifunguliwa na  msaidizi wa Mheshimiwa mstaafu na aliingia kana kwamba yeye ndio anaeongoza nchi , maana watu waliokuwa hapo ndani kila mmoja alikuwa na cheo , kama sio mwanajeshi basi ni mwanasiasa.

Mheshimiwa Jongwe licha ya kwamba ni mstaafu lakini bado afya yake ni imara kabisa , ndio  mstaafu pekee  ambae alikuwa hai mara baada ya  watangulizi  wake wote kutangulia mbele za haki.

“Nafasi ya Gabusha  mbona ipo wapi?”Aliuliza mara baada ya kusalimiana  na viongozi hao na kauli ile ilimfanya kila mtu kumwangalia Mzee Benjamini.

“Gabusha  yupo mkoani Kigoma  kujiimarisha?”Aliongea Benjamini na kumfanya  Mstaafu  kukunja  sura.

“Ina maana mambo yake na yule mwanamke  hayajakaa sawa mpaka  kwenda kujitoa  fidia?”

“Mheshimiwa  mambo hayakuwa mepesi , kizingiti kilichomkuta  Gabusha  kimenikuta na mimi?”Aliongea.

“Benjamini  unamaanisha nini , usiniambie umeshindwa  kutimiza  kazi yako mpaka sasa?”Aliuliza  na kumfanya  Mzee Benjamini kukunja sura.

“Mheshimiwa   mpango ulikuwa ukienda vizuri  , lakini mara baada ya huyu  bwana anaeitwa Hamza kujitokeza kila kitu kimeenda ndivyo sivyo , kila tunalopanga  linaenda Kombo”Aliongea  kwa namna ya kujitetea huku akisimama na kumfanya Mheshimiwa kumwangalia kwa kutoridhika.

“Unaweza kukaa  chini  tuanze  kikao chetu , isitoshe Ajenda  yetu  pia inahusiana na huyu anaeitwa Hamza , nilimpotezea mwanzo ila naona anaanza  kuwa tatizo”Aliongea  na kumfanya Mzee Benjamini kupata ahueni na baada ya hapo alianza

kupitia sura ya kila mmoja aliehudhuria na  alikuja kusimamisha macho yake kwa Mheshimiwa Jongwe.

“Jongwe hali  ya mwitikio   katika kampeni zako kwa wananchi  zinaendaje?”

“Mheshimiwa  kampeni zinaendelea vizuri sana  na nimerudi Dar es salaam kwa ajili ya  kufunga  kampeni  , kwani mwezi ujao tunaingia moja kwa moja katika upigaji  kura”

“Una uhakika wa kushinda, vipi kuhusu mpinzani wako?”Aliuliza na kumfanya  Mzee Jongwe kusita kidogo  lakini  alianza kuongea.

“Kuhusu Msemakweli  amekuwa tatizo  na hivi baada ya tukio la kupotea kwa  Tajiri wa Kenya na Balozi  wa Rwanda  na jambo hili kulihusisha  na mtandao wa Panyaroad  ameanza kuteka fikra za wananchi, mheshimiwa kwannini nisitangaze  moja ya  nia yangu ni kuitokomeza Chatu?”Aliongea  na kumfanya Mheshimiwa kukunja ndita kidogo. “Uko juu juu sana  Jongwe kimawazo , ndio kitu ninachokupendea na kutokukupenda  kwa wakati mmoja kwani inakufanya kuwa dhaifu, mpaka sasa kushinda kwako kwa  uchaguzi kupo katika mikono ya  mtu mmoja , inategemea na namna utakavyomshawishi katika kikao hichi , la sivyo  tutatumia nguvu nyingi sana kukuweka  Ikulu au Waangalizi  watushitukie kuiba  kura  na kuhatarisha  amani ya nchi”Aliongea na kufanya watu wote hapo ndani kutoelewa kauli yake inamaanisha nini , lakini dakika ileile  walielewa alichomaanisha kwani mlango  ulifunguliwa  na hapo ndipo  walipojua Mheshimiwa alikuwa akimaanisha nini.

“Nadhani wote mnajua huyu , sina haja ya kuwatambulisha , lakini kabla hajaenda kuongea  na kuanza kikao nataka kutoa  maelekezo kwamba tukio  la  kupotea kwa balozi , kifo cha Kamishina msaidizi na  wengine  linahusiana na yeye”Aliongea na kisha alilazimisha tabasamu na kumwangalia  Dina  kwa namna ya kumkaribisha.

“Siwezi kuhatarisha mtandao wa Chatu kuteteleka  , ndio msingi  wa ngome yangu , nitakutumia kuimarisha na kuvuta kipindi hiki cha  mpito na baada ya hapo nitakutoa kwa ulazima”Aliwaza mheshimiwa huku akimwangalia mrembo huyo kwa macho yaliojaa ufeki na matamanio.

Previoua Next