Reader Settings

Ilikuwa ni dhahiri  kwa mwanaume aliefahamika kwa jina la Mr Alfonso kutokutarajia mtu ambae alipaswa kuonana nae kwa kufanya safari ya kufika Israeli   kuwa  Frida, kwa muonekano wake wa haraka haraka ilionyesha alikuwa akimfahamu fika Frida  na macho yake yalionyesha hofu  na wasiwasi  kiasi cha kurudi nyuma na kurudia mlango akitaka kutoka.

Mara baada ya kupalamia mlango akihitaji kuufungua haukufunguka na alijikuta akigonga kwa nguvu lakini bado   hakuweza kusikia  watu kutoka  nje na akili yake ilimwambia  walinzi wake na wasaidizi wapo chini ya ulinzi wa  Frida.

“Mr Alfonso  sifa zako haziendani  na kile ambacho   watu wengi wanaongea kuhusu wewe , sidhani ni sahihi kumuogopa  mwanamke ambae  hana siraha yoyote”Aliongea  Frida   huku akitoa  sura ile ya usiriasi na kuuvaa ukarimu huku akipiga hatua  kumsogelea.

“Wewe ni shetani .. usinisogele?”

“Mimi  ni nani?!. Kama kweli mimi ni shetani sidhani  unapaswa kuogopa, kwa sifa za cheo chako wanaokufuata wakisikia kiongozi wa Sinagogu anamuogopa mwanamke aliemwita Shetani  ni dhahiri haitokuwa taswira nzuri kwako?”Aliongea  Frida  na kumnyooshea mkono Mr Alfonso.

“Unataka nnini kutoka kwangu , mpaka  kuniwekea

mtego kwa kujitambulisha wewe ni Prince?”Aliuliza.

“Sina chochote ninachotaka kutoka  kwako , bali sisi ni watu wenye malengo sawa ndio maana umefika kwa haraka bila ya kufanya  uhakiki wa ki usalama?, sipo hapa  kama adui  bali  kwa  niaba ya Maadam”Aliongea  na kumfanya  Mr Alfonso   kuvuta pumzi   nyingi huku bado  akimwangalia Frida  kwa wasiwasi.

“Historia na kanuni za imani yangu  zinanikataza kufanya hivyo, kwanini nikuamini wewe uliekengeuka , haijalishi nini unachohitaji kwangu , kutumia hila kunisafirisha mpaka  hapa ni kosa kwa upande wako  na sio kwa upande wangu?”Aliongea.

“Kama ni hivyo basi malengo yenu  hayawezi kufanikiwa  na hili unalijua  ndio maana taasisi yako ikanichomesha kwa  viongozi wangu , ili nichukuliwe hatua , lakini  ajabu malengo yenu hayakutimia   na  sasa nipo hapa kwa niaba  ya jumuiya”.

“Tulichofanya sio  kukuchomesha , huwezi kusema hivyo ilihali umeingia katika dhehebu letu  kama Double  agent na haukuwahi kuwa mmoja wetu, wewe ni msaliti na doa kwa imani yetu na  hatuwezi kukaribisha tena”Aliongea  na kumfanya  Frida kutabasamu.

“Basi nadhani ni muda sahihi  wa sisi kukaa chini  na kuongea, kama nilivyosema nipo hapa kama muwakilishi wa Wiccan , siku zote hii ndio njia yetu ya kuwasiliana ili kuficha mienendo yetu  , hivyo  huna haja ya kukasirika na unapaswa kuuliza kwanini  umeletwa  Israeli kutokea 

Brazili”Aliongea Frida na muda  ule hakutaka kuongea nae  tena akiwa amesimama kwani alirudi katikati ya chumba hicho  chenye  samani  za gharama  na kisha akakaaa kwenye sofa.

Mr Alfonso  licha ya kuwa na wasiwasi alijikuta akivuta pumzi na kisha  kusogea taratibu na kwenda kukaa  kwenye masofa mbele  ya Frida.

“Utapendelea kinywaji?”Aliuliza Frida huku akimimina mvinyo kwenye glasi.

“Hapana  nashukuru , nadhani ni vyema ukienda moja kwa moja  kwenye dhumuni lako”Aliongea na kumfanya Frida kutabasamu ki uchokozi.

“Nahitaji  nafasi yangu ndani ya taasisi” Aliongea Frida.

“Hilo haliwezekani  hatuajiri panya”Aliongea kwa kingereza.

“Taasisi yenu inanihitaji zaidi ya ninavyowahitaji ,sina haja ya kuelezea  hili zaidi , isitoshe  misheni  zenu zote zinategemeana  na  tafiti zangu”Aliongea Frida.

“Unamaanisha hatuwezi kuishi bila wewe , Miss Frida kama hicho ndio unachowaza umoja wetu  haupo tayari kukupokea , wewe  ni dosari  kwa misheni zetu na hatuwezi kuruhusu makosa kwa mara  nyingine”Aliongea Mr Alfonso.

“Vipi kama nikikuambia siri  ambayo  ni watu wachache mpaka sasa wanaijua , siri ambayo  umoja wangu haujawahi kuifahamu?”Aliongea Frida.

“Una siri ya namna hio , najua kila binadamu ana siri lakini  kuwa na siri  kama gia ya mazungumzo sidhani inaweza kuwa  na ushawishi wa kutosha wa  kukurudisha kwenye  taasisi”Aliongea  Mr Alfonso  huku  akijitahidi kuonekana  ni mwenye kujiamini. “Umeshawahi kusikia Agent  mwenye jina la msimbo(Codename) 2FcommaG?”

“Unataka kusema nini , hilo  ni jina la Ajenti ambae  umoja wetu  umekuwa ukimfatilia kwa muda mrefu  na  ni taarifa nyeti zaidi  ya daraja la juu, unafahamu vipi hii taarifa?”Aliuliza Mzee Alfonso huku akionekana ishara ya kuchangayikiwa.

“Kwasababu  mimi ndio Ajenti  2FcommaG  maana ya jina hili ni Frida Franklin Genesha”

“Quee!!!”(What!)

Mzee Alfonso alijikuta akimaka  huku akisahau kutumia lugha ya kingereza na kuongea  kireno, macho yake yalianza kumwangalia  Frida kama  kwamba kaona mzimu.

“Vipi?, siri yangu  imeweza  kukupagawisha kiasi hicho?”

“Najua vipi wewe  ni kweli ni  Ajent 2F tumeweza kukufuatilia kwa muda wa miaka saba mpaka sasa  bila ya kukufahamu , umewezaje kujificha kwa muda wote huo  mbali na teknolojia yetu?” “Sikujificha , miaka saba iliopita niliachana  moja kwa moja  na  jina hilo , mlikuwa mkitafuta mtu ambae amekufa  na hayupo kwenye ramani hivyo ni sahihi kwenu kushindwa kumpata licha ya kutumia  rasilimali nyingi na wanachama wote wa Wiccan tunaishi kwa sura nyingi”Aliongea na muda uileule alichukua  kishikwambi kilichokuwa kwenye mkoba wake   na kukiweka mezani huku picha ikionekana.

“Najua  malengo  yenu ya kufungua  taasisi  ya Haliz foundation nchini Tanzania , pamoja na Dhehebu  la kidini , ni kwa ajili ya kutafuta hii  alama iliowahi kuwepo  miaka mingi  na ikapotea..”Aliongea Frida  na kumfanya  Mzee Alfonso paji la uso wake kutoa jasho.

“Who are you!?”Aliuliza akimaanisha  yeye ni nani.

“Wewe ni nani , kwanini unajua siri  za juu  za dhehebu letu?”Aliuliza  na Frida muda huo alikuwa na tabasamu pana.

“Mimi ni mtu pekee ambae  nahitajika katika taasisi yenu kukamilisha tafiti  zangu , najua mpaka sasa mpo njia panda  kuthibtishia waumini wenu  juu ya ushahidi wa kiimani wa  kuzaliwa upya  ili kujipatia  wafuasi wapya  na kuwa na msingi wa  kiimani baada ya kujitoa katika Kanisa kuu huku mkijua  muda ukiwa si rafiki kwenu  , lakini haya yote  hayawezi kufanikiwa bila mimi , mimi ndio ufunguo  aliouacha Dokta Genesha , ufunguo wa

kuthibitisha  nguvu  ya kiroho inaweza  kuthibitishwa kisayansi, mimi ndio ufunguo  wa kuwaonyesha  ni nani haswa katika maisha  haya anabeba alama yenu iliopotea  katika unabii”Aliongea Frida huku wakati huo akiwa amesimama na alionekana kuwa siriasi.

“Umejielezea kuhusu wewe  , juu ya kitu unachohitaji , vipi kuhusu Wiccan , wanataka nini kutoka kwetu  , sidhani kama ulikuwa na ushahidi wa kutosha  wa kujitoa katika adhabu ya kukiuka sheria za umoja wenu wa kipagani?”Aliongea Mr Alfonso na kumfanya Frida kutabasamu na alirudi kwenye sofa na kukaa chini  na kumwangalia  usoni.

“Hilo ni swali  zuri  kwa upande wako Mr Alfonso , kama nilivyosema sisi wote tunatafuta kitu kimoja?”

“Unamaanisha hata nyie  wapagani mnahitaji  kujua nani amebeba  alama iliopotea katika maisha haya? , mnataka kujiaminisha nini kupitia alama hio?”

“Mr Alfonso unajua  ni kitu gani ambacho dunia 

inashindwa kutafsiri  maana halisi ya  neno Wiccan?”

“Ni rahisi , kwasababu  hamuamini  uwepo wa   Mungu zaidi ya nguvu za giza?”

“Hilo  ndio kosa kubwa ,  sisi sio Wapagani kama 

watu wanavyojaribu kututafsiri , sisi pia tunaamini uwepo wa  Mungu”

“Hilo ni jipya kwangu kusikia  kutoka  kwa mpagani?”

“Tunaamini Mungu ni nguvu iliopo katika umoja  wakati wa kujitetea na udhihirisho  ila sisi  tunasimama kwa kuamini katika  vitu vingi ambavyo  hutengeneza kila kitu kinachoonekana na  kisichoonekana ikiwemo Mungu”Aliongea Frida na kumfanya Mr Alfonso macho kuwaka.

“Unaonekana  kuwa muumini mtiifu  wa Wiccan  kwa namna unavyoilezea imani yako , sio  jambo baya kwangu kuona unaitetea imani yako , lakini swali langu linasimama  palepale  mnataka  nini  kutoka kwetu na  ili mdhihirishe nini?”

“Kuijua lugha ambayo imewashinda  binadamu  wote  kuitafsiri  mpaka leo ili tuweze kupata vitabu vyote vilivyoelezea uchawi kutoka kanisa kuu”Aliongea  na kumfanya  Mzee Alfonso  macho yake kuchanua.

“Wakati nikihudumu kama Kardinali  niliwahi kusikia uzushi  mwingi juu ya  uwepo wa Manucript  za kale zilizohifadhiwa  katika maktaba za siri ndani ya makao makuu ya kanisa kuu ,nyaraka ambazo lugha yake haijaweza kutafsiriwa na kujulisha watu zinahusiana na nini , isitoshe sijawahi kuona huo ushahidi wa uwepo wa hizi nyaraka , unachosema  wewe  kinanifanya niamini  pengine ilikuwa kosa upande wangu kupotezea uzushi ule”Aliiongea  “Yapo maandiko  mengi sana ambayo  yametumia  lugha ambayo haijawezekana kutafisirika mpaka leo , kutokana na kanisa kuepusha hatari  waliamua kuzificha  wakati huo wakizifanyia utafiti, moja ya  maprofesa wa kiimani waliopewa kazi hio mmoja wapo ni Dokta Genesha  na ndio mtu pekee ambae alipata kufahamu uwepo wa  andiko lililojaa siri katika  simulizi fupi ya Njiwa juu ya mti wa uzima, tulipeleka mapendekezo kwa  kanisa kuu kutupatia hizi nyaraka lakini waligoma , Dokta Genesha alipendekeza njia  pia  ya kutafsiri nyaraka hizi lakini aligoma vilevile  na ndio kilichochangia mauaji yake”Aliongea.

“Dokta Genesha alipendekeza kitu gani kwenda kanisa kuu  kilichompelekea kupoteza maisha  na

vipi kuhusu hii simulizi ya Njiwa juu ya Mti wa Uzima?”

“Askofu sidhani ni sahihi  kujua kila kitu , isitoshe  kuna kichwa cha habari juu ya simulizi hio lakini kilichoandikwa  ndani yake hakifahamiki kwani lugha yake haitafsiriki , lakini kwa mtazamo wa Dokta Genesha ni  siri kubwa ambayo  inaweza kuhatarisha usalama wa binadamu”

Aliongea na kumfanya kuanza  kuonekana kama mwenye  kutafakari , hakueleweka alikuwa akifikiria nini.

“Wiccan wanataka kusaidiwa vipi katika hili ,  hili likifahamika kwa waumini   tutapoteza  msingi wetu wote wa kiimani na nguvu tuliotumia kupigania uhuru wetu  kwa miaka mingi ili kusimama kama kanisa itakuwa ni bure , siwezi kushirikiana na wapagani  kirahisi  , hata kukutana na wewe hapa ni kosa?”Aliongea Mr Alfonso.

“Ndio maana  tumechukua  kila tahadhari , tumemtumia mtu ambae unatamani sana kukutana nae , mtu anaefahamika kwa jina  la Prince , Mr Alfonso  nadhani huwezi kutuchukia katika hili , ilikuwa ni mbinu ya kuweza kufunika mienendo yetu, kuhusu  namna ya kutusaidia sisi  ni rahisi sana , napaswa kurudi   na kuendelea na  tafiti zangu ndani ya Haliz foundation  siku yoyote nitakayotia mguu nchini Tanzania , sisi kama Wiccan tumetoka mbali  shabaha yenu ni shabaha yetu, nataka kuendelea na misheni na wewe kama Askofu mkuu wa Sinagogi B unapaswa kunirudisha  kazini”

“Bado sijashawishika kukubali ombi  lako , isitoshe wewe ni muumini tu wa  chama cha wapagani  wanaoamini katika uchawi , wa kuzungumza hili  kiitifaki  ni mkuu wako na si vinginevyo”

“Nadhani unapaswa kuniambia unachohitaji , huwezi kuonana na mkuu wangu , kama nilivyosema mimi ni mwakilishi , kama una nia ya kuonana na mkuu wetu  ni lazima ukubali kutii mila na desturi za Kiwiccan ili kupata jicho la ziada la kuonana nae”Aliongea na kumfanya Mzee Alfonso sura kujikunja.

“Unamaanisha nini?”

“Namaanisha  ili uweze  kuwa na uwezo wa kuonana nae , unapaswa kuwa  na uwezo wa tofauti kidogo na binadamu wa kawaida , na ili kupata hio

nafasi lazima  upitie ibada ya  kuondoa ukungu wa macho”

“She is Shadow who speaks to me through you?”Aliongea akimaanisha kwamba  Frida anatumika na Kivuli  kuongea nae. “Unaamini uwepo wetu!!?”Aliuliza Frida.

“The abundunce  of informations relating  to the existence  of so called Night Shadows  has been a long-standing topic , we conducted  our  research to validate the truth”Aliongea akimaanisha kwamba kuna taarifa nyingi zinazozungumzia kuhusu  uwepo wa Night Shadows kwa muda mrefu  na walifanya  utafiti kuujua ukweli” “Na kipi  mlipata kupitia utafiti wenu?”

“Tulipata ushahidi wa uwepo wa nguvu ya ziada  kwa  watu wote waliosema walitawaliwa na kivuli kisichokuwa cha kwao lakini  utafiti wetu ulikuwa wa kiroho  zaidi ,  jamii za wanasayansi duniani  wamekataa uwepo wenu kutokana na kukosa ushahidi unaonekana”

“Basi wewe ni   kiongozi wa kwanza mkubwa kuongea na sisi , muda wangu wa kutawala kivuli  cha Frida umekaribia mwisho ,  kama tulivyoongea unapaswa  kukubali  kila nilichoongea  kama unataka kufanikiwa na sisi kufanikiwa, ili  uwepo wetu kuwa wazi  tunahitaji kuwafundisha  lugha  yetu  na matumaini  yetu yapo  katika tafiti  ya Frida”Aliongea  Frida   na muda uleule mlango wa kuingilia katika chumba hiko  ulifunguliwa na mtu wa kwanza kuingia ni msaidizi wa Mr Alfonso na alionekana kuwa na ahueni mara baada ya kumuona bosi wake akiwa mzima.

“Mr Alfonso upo sawa?”

“Niko sawa Pretta”Aliongea huku akimwangalia Frida usoni.

“Umeondoka?!”Aliuliza Mr Alfonso  alionekana kuwa na swali lingine.

“Unamaanisha mimi au Madam?”Aliongea Frida  huku akiwa  na tabasamu na  kumfanya mzee huyo kushngaa.

“Ulikuwa ukijua anakutumia?”

“Ndio, lakini  ndani ya   Israeli pekee”Aliongea  Frida huku akitabasamu.

“Unamaanisha nini?”Aliongea na kumfanya Frida kumwangalia  Pretta msaidizi wa Mr Alfonso.

“Pretta subiri nje  kwanza ,  namalizia maongezi”Aliongea na Pretta alikubali na kutoka nje.

“Shadows wapo kila mahali  ni viumbe wasionekana lakini wenye ufahamu , udhaifu wao  mkubwa  hawawezi  kusafiri  kuvuka bahari  hata kwa vifaa , hivyo Shadows waliopo bara la Afrika  hawawezi kuwa  bara la Australia au Amerika  lakini haimaanishi hakuna mawasiliano  baina yao”Aliongea na kumfanya  Mr Alfonso  kushangaa.

“Kwanini wapo katika hali ya kivuli  na  malengo yao  ya mwisho ni nini , sidhani swala la  Lugha  linaweza kuwa mwisho?”

“Kuhusu malengo yao ya mwisho sina uhakika , lakini  nina hisia  juu ya kile ambacho wanahitaji, naamini  wanataka kuonekana  kama sisi tunavyoonekana”Aliongea na kumfanya  kukunja ndita.

“Hilo haliwezi kuwezekana”

“Kama nakumbuka vizuri  ni wewe  ambae ulipinga vikali  juu ya imani ya kuzaliwa upya”Aliongea Frida huku akitoa tabasamu.

*******

Lawrence  alionekana kuwa na wasiwasi  akiwa ameketi katika eneo la kusubiri , wasiwasi wake ni kile ambacho kinaendelea  ndani alikoingia bosi wake , hakujua kama  Dina anaweza kuwa salama  na alitamani kumpigia Hamza kumjulisha kile kinachoendelea lakini aliona akifanya hivyo angemkasirisha bosi wake , isitoshe  alimwambia amuamini katika hilo.

“Madam hili eneo ni miliki ya mheshimiwa na lolote linaweza kutokea , kwasasa una maadui wengi kwanini nisiongee na Bro kwanza tumfahamishe kinachoendelea?”Aliuliza  Lau  dakika kadhaa kabla ya kuingiza  gari katika makao makuu ya mheshimiwa mstaafu.

“Wewe ndio ulieniletea  taarifa  yupo bize na CEO wa Dosam  lakini  unataka kumsumbua , Lau najua unawasiwasi juu yangu lakini  Hamza amekwisha kutusiadia vya kutosha  na alisema nidili  na hili mwenyewe , niamini  nitalimaliza , siwezi kuruhusu  juhudi za babu  kupotea”Aliongea.

“Wasiwasi wangu ni  huyu mzee , alikuwa ni moja ya  adui mkubwa  kwa bosi wetu aliepita , ni ngumu sana kumuamini”

“Hata mimi  nimekuja hapa  sio kwasababu namuamini , nimekuja kwasababu nina kete ya kucheza na kwa vyovyote vile hawezi fanya chochote”Aliongea na  Lau kishingo  upande aliingiza gari  katika makazi hayo ya kifahari.

Makazi ya mstaafu Mgweno kwa  barabarani unaweza kudhani ni ya kawaida , lakini ndani yake  ilikuwa ni hekalu la kifalme  ambalo limejengwa kwa mtindo wa  kitamaduni  wa nyumba za kirumi.

Lau mara baada ya kuegesha gari alipokewa na moja ya mtumishi wa nyumba hio  na  kupitia maelekezo  Lau aliambiwa asubiri katika eneo maalumu la wageni huku  Dina akipelekwa moja kwa moja katika chumba cha  mikutano.

Sasa  nusu saa zilikuwa zimepita bila ya Dina kutoka na jambo hilo ndio  lilimfanya   Lau kuzidi kuwa na wasiwasi , alitamani  kuingia  alipoingia bosi wake lakini walinzi walionekana wapo tayari kumfanyia chochote  akifanya fujo.

Hatimae mara baada ya kujishauri kusubiri dakika   kumi na tano nyingine  bosi wake alitoka na kujikuta akihema kwa ahueni.

Upande wa Dina hakukuwa na ishara ya utani katika macho yake  na mara baada ya kumfikia Lau alimpa ishara ya kuondoka na alitii  haraka haraka na kuingia ndani ya gari.

“Tukitoka hapa  fanya utaratibu wa kuaachilia huru  Balozi , Debora na yule mzee”Aliongea Dina.

“Madam kwanini umefikia haya maamuzi?”

“Nimempa alichokitaka  na  nikapata nilichokitaka  lakini mzani  umelemea kwangu  hivyo  naweza kusema kilichonileta kimefanikiwa”Aliongea Frida huku akionyesha tabasamu hafifu  na  Lau alitabasamu na kisha akaliondoa gari.

“Katika kipindi hiki chote  nitahitaji utulivu  ndani ya  mtandao wetu , hakikisha vijana wetu hawatumiki  bila  ruhusa yangu , dawa ya msema kweli imeshapatikana lakini kosa kidogo linaweza kuifanya  ikose nguvu , umenielewa ninachomaanisha?”

“Ndio Madam”Aliongea Lau huku muda huo akiitoa  gari katika makazi hayo ya mheshimiwa.

*******

Licha ya  Kanali  Dastani kuwa katika uchunguzi ndani ya kitengo kwa muda haikumaanisha  alikuwa ametolewa katika  kitengo cha MALIBU , nafasi yake ndani ya kitengo hicho  ilikuwepo na alikuwa akifika kazini , isitoshe  hakukuwa na ushahidi wa kutosha wa  kumthibitisha alikuwa msaliti wa taifa.

Saa saba na nusu mchana alikuwa katika ofisi  yake na alionekana kuegamia kiti chake  kama kawaida  huku akiwaza hili na lile.

Moja ya kitu ambacho kilikuwa kikimfanya kuwaza ni juu  ya Afande Mchuku na  Amosi, alimuwaza Afande Mchuku kwa kuamini kitendo chake cha kuwasiliana nae kupitia simu kimemponza na kumfanya kukumbwa na umauti.

Alikuwa akimuwaza  Amosi  kwa kuwahi eneo la tukio  sehemu ambayo  ndio kifo cha Afande Mchuku  kimetokea.

Swali lilikuwa ni moja tu , imekuwaje  Amosi akawahi eneo la tukio  kabla yake , maana kwa mahesabu ya muda aliona kabisa  Amosi sio muhusika wa kifo cha Mchuku bali ni mtu mwingine  ila kuna hisia zilimwambia  Amosi alikuwa akijua kitu ambacho  Mchuku alikuwa  amebeba.

“Au Mchuku aliwasiliana na Amosi pia?”Aliwaza

Kanali lakini  swali hilo pia liligoma , alimjua Mchuku kwa  muda mrefu  isingekuwa rahisi  kuwasiliana na Amosi.

“Kesho  napaswa kwenda kuhudhuria mazishi Ikwiriri  ninaamini nitapata pakuanzia”Aliwaza kanali , ukweli  licha ya kwamba kifo cha  Afande Mchuku kimetoka  bado aliamini  rekodi  ya sauti ambayo alikuwa nayo Mchuku  mpaka kuuwawa  bado haijaingia katika mikono  ya mtu mwingine.

Wakati akiwaza simu yake ilimtoa katika mawazo  kwa kuanza kuita,   baada ya kuangalia jina la anaepiga ni katibu wa mheshimiwa raisi na hapo hapo tumbo lilianza kumchemka , alikumbuka misheni ambayo mheshimiwa alimpatia  kuikamilisha  na akashindwa , misheni ya kumuua Hamza.

“Habari za saa hizi  Mr Dastani?”Sauti upande wa pili ilisalimia mara baada tu ya  Kanali kupokea simu.

“Salama katibu  habari za mchana”

“Ni njema Kanali , mheshimiwa anakuhitaji ofisini saa nane kamili”Aliongea  Katibu na kumfanya Kanali kuangalia saa ya ukutani na sura yake ilijikunja mara moja.

“Sawa katibu nitakuwa hapo ndani ya muda”Alijibu huku simu ikikatwa upande wa pili , alikuwa na dakika kumi na tano kutoka hapo mpaka kufika Ikulu  ,  uzuri ni kwamba  kitengo chao hakikuwa mbali sana na  ilipo ikulu.

Kwa cheo chake hakuhitaji kuomba ruhusa zaidi ya kutoa taarifa hio kwa  Sekretari  na moja kwa moja aliingia katika gari lake na kuelekea  Ikulu.

Baada ya kupitia itifaki zote za ki usalama   hatimae aliweza kuongozwa na katibu moja kwa moja mpaka ndani ya ofisi ya Mheshimiwa.

Katika kipindi hicho ambacho Raisi Eliasi Mbilu alikuwa akimalizia muda wake kichwa chake hakikuwa kikiwaza kuwatumikia wananchi kabisa , alikuwa akiwaza maisha yake baada ya  kutoka  Ikulu , sio kama kiinua mgongo kulingana na katiba hakikuwa kikimtosha , ukweli ni kwamba  hata baada ya kustaafu serikali inamlipa lakini  pesa hizo aliona hazikumtosha , hivyo  mikataba  mbalimbali ya kumnufaisha ambayo hakuikamilisha ndio ulikuwa wakati wake  na kumfanya kuwa bize sana na wageni wengi waliingia na kutoka Ikulu.

“Dastani sitaki hata kuanza  kuongea  kilichotokea juu  ya kazi niliokupatia , naelekea  Nchini Malaysia masaa mawili  yajayo hivyo nipo bize ,  kuna swala  moja nataka  ulifanyie kazi na  nahitaji majibu ya haraka”Aliongea Mheshimiwa huku  akivuka hatua ya salamu. “Nipo tayari mheshimiwa”

“Sio tu upo tayari  Dastani , kwa miezi hii miwili sijaona matokeo ya kuridhisha  kutoka kwako , naweza kustaafu  hata kesho lakini kumbuka nguvu yangu serikalini  haiwezi kuisha mara moja, kama unataka kuendelea   kupata kinga kutoka kwangu  unapaswa kunifurahisha, una maadui wengi wanaosubiria nikupe mkono wa kwaheri”Aliongea  na kumfanya  Kanali kutingisha kichwa.

“Nadhani umezisikia habari za kifo cha mkuu wa Gereza  la Silo  na sababu ya kifo chake unazijua , sitaki kujua umeanza lini biashara  na Afande Mchuku  hayo  ni makandokando yako  na ni sehemu ya  ubinadamu , ninachotaka  ufanyie kazi ni kupata rekodi   alioacha  Afande Mchuku mara moja , fanya juu chini uipate,  ina taarifa ambayo haipaswi kumfikia mtu yoyote ni swala la kidiplomasia, umeleewa Afande?”

“Mheshimiwa unamaanisha  Afande Mchuku….”

“Unataka kuuliza  kilichomkuta Afande Mchuku kinahusiana na mimi? , sidhani ni swala la kushangaza , Mchuku alikiuka miiko yake ya kazi  na kilichompata kastahili, baada ya tukio  Mchuku alikuwa na USB drive na tuliamini  ndio yenye maongezi  ya wageni  waliofika kuonana na mfungwa  lakini  kwa hila za  Mchuku  kilichokuwa kwenye USB drive  ni picha za  nyumba yake anayojenga”Aliongea Mheshimiwa na kumfanya Kanali kushangaa  lakini  kutabasamu  ndani kwa ndani  baada ya kujua  wazo lake lilikuwa sahihi  Mchuku  hakupoteza  kitu muhimu.

“Mheshimiwa nitalifanyia kazi hili  ndani ya muda mchache nitapata majibu  na kukupatia taarifa?”

“Ukishapata faili haina haja ya kuja moja kwa moja kwangu  wasiliana  na wasaidizi wa Mgweno na ukabidhi”Aliongea na kumfanya  Dastani kushangaa kidogo.

“Sawa mheshimiwa?”Aliongea  

“Sikia Dastani  nakupa onyo, hakikisha  ukipata hio flashi  hufanyi  kitu kingine tofauti na kukabidhi , sitokuwa  na namna yoyote ya kukulinda ukienda kinyume na  maagizo yangu”Aliongea Mheshimiwa huku akimkazia  Dastani macho.

“Mheshimiwa kama hutaki nikisikiliza kilichomo kwanini unanipatia hii kazi mimi?”Aliuliza na kumfanya  mheshimiwa kumwangalia kwa sura iliojaa uchunguzi.

“Naitambua  tabia yako  Dastani  ndio maana unafaa katika hii kazi , kumbuka  maelekezo  yangu  pekee , watu wanaohitaji  hii kazi kumalizika wana nguvu kuliko unavyodhani, hawapo kama sisi, wanachotaka ni kuficha kile walichoongea na mfungwa basi”Aliongea  na Kanali aliishia kutingisha kichwa  kukubali.

Dakika chache mbele Kanali Dastani alikuwa  ndani ya gari lake , ukweli bwana huyo alianza kujifikiria na kuona kazi nyingi ambazo anafanya sio za kitengo cha MALIBU bali  ni za  kitengo cha TISA.

“Mheshimiwa anajua kuongea kwa lugha mbili kwa wakati mmoja , anachotaka   ni kujua kilichopo  katika rekodi alioacha Afande Mchuku , hii inaniambia  moja kwa moja  sio yeye alietoa ruhusa  ya hao wazungu  kuonana  na mfungwa , lazima  kuna  mkono wa mheshimiwa Mgweno , lakini kama ni hivyo  wameongea nini? , kwanini hawakuchukua tahadhari mpaka wakaruhusu  Mchuku kuweza kuwarekodi, hii kesi ya  huyu mwanamke ina  siri gani kubwa  mpaka  watu kuwa makini namna hii??”

Ni maswali ambayo  Kanali alikuwa akijiuliza lakini kadri ambavyo aliona anazidi kupiga hatua kuisogelea kesi hio kwa ukaribu ndio  usalama wake unavyopungua.

Wakati   akiwa ashatoka nje kabisa ya geti  la  ikulu simu yake ilianza kuita na mara baada ya kuangalia anaepiga alijikuta akitabasamu kijeuri na kuipokea.

“Kuna nini Tresha!!?”

“Uko  wapi?”Sura ya  Kanali ilijikunja.

“Kwanini haraka hivyo? , kuna kilichotokea?”

“Nadhani Amosi   kafanya kile tulichokuwa tukijilinda nacho muda  mrefu, nimeangalia  Kamera za  ulinzi na kumhoji Mwanaidi  amekubali Amosi alikuwa  ndani ya pub  na vifaa vya kusikilizia sauti na Kamera..!!”Kanali mara baada ya kusikia taarifa hio alifunga  breki mara moja huku kichwa kikianza kuwaka moto.

“Sikia Dastani  huna haja ya kufikiria  sana , nadhani  ameamua kutumia nyendo  zako kufanya uchunguzi wake kwa hilo nampa credit, lakini  haipaswi hii kuendelea , Amosi  atavuruga  mipango yetu yote , hebu fikiria  picha zikifika kwa Eliasi atachukua maamuzi gani?”

“Tresha unazunguka zunguka, unataka  nitafanye nini?”

“Kwahili  hata  mimi nimechangia , lakini ukweli  hauwezi kupingika  haukuwa makini  Dastani , tabia yako ya kumdharau  Amosi itakuletea matatizo , nimempa kazi mtu kumtafuta Amosi popote pale na kumuua, hili  swala lishakuwa binafsi tayari”

“Tresha  hebu subiri….”Kanali  alijikuta akipiga usukani wa gari mara baada ya simu kukatwa , dakika ileile alipiga tena  simu kwenda kwa Tresha lakini simu ilikuwa haipatikani hewani.

“Tresha ataniingiza kwenye matatizo huyu Ma*ya kwa kukurupuka, nakiri nilikosea  kumdharau  Amosi lakini  namjua Amosi nje ndani sio mtu wa kukurupuka na hachukulii vitu  kuwa binafsi, sio mwepesi kuvujisha picha”Aliongea chini chini huku akikanyaga pedeli na kusogeza gari lake  makao makuu ya  kitengo  huku wazo  namba moja ni kumtafuta alipo Amosi kabla hajafikiwa na Tresha.

********

“Hukujumuishwa?”Aliuliza Regina  huku akimwangalia Hamza kwa macho makavu.

“Mbona unauliza kimkato mkato sio tabia yako hii?”Aliongea Hamza akilalamika.

“Ninachomaanisha leo  kuna  mashindano ya

Basketball , mbona katika taarifa ilionifikia wewe pia umejumuishwa kama mchezaji?”Aliongea Regina na sasa kumfanya Hamza kukumbuka.

Siku kadhaa nyuma  anakumbuka alifuatwa  na moja ya  wafanyakazi  aliefahamika kwa jina  la

Aroni wa kampuni na kumuomba kujiunga na timu yao ya  kampuni kwa ajili ya mchezo wa  basketball,

kilichomfunga Hamza ni mara baada ya wafanyakazi hao kumuuliza kama anaujua mchezo huo na aliitikia kama anaujua na  moja kwa moja wafanyakazi wale walimwambia  ashiriki  kama mchezaji lakini kwake Hamza alisema anaujua na sio kujua kucheza.

Ukweli katika mambo ambayo hayakuwa na umuhimu katika kichwa cha Hamza  hilo lilikuwa namba moja  ndio maana alisahau kabisa na hata  kwenda kwenye mazoezi  hakukumbuka.

“Waliniandika kama mchezaji bila ridhaa yangu, waliniuliza kama naujua mchezo wa Basketiball nikawaambia naujua   nadhani  wamenielewa vibaya nani asieujua mchezo wa Basketball  , halafu  kwani kuna  umuhimu wa kushiriki?”Aliuliza Hamza huku akikuna kichwa.

“Kwako wewe inaweza isiwe na umuhimu  kwasababu umejiunga na kampuni juzi , lakini huu umekuwa utaratibu  wa muda mrefu wa  wafanyakazi  wa kampuni mbalimbali  kushindana katika michezo mbalimbali ikiwemo  mpita wa miguu, Marathon  na Basketball, nikuambie tu  leo Mkuu wa Mkoa na viongozi wengine   wamealikwa

hivyyo wewe kama mchezaji nahitaji ushindi”Aliongea Regina.

“Lakini sijasema mimi ni mchezaji kwanini unaniamrisha nikupe ushindi?”

“Iwe jina lako limeandikwa bila ridhaa yako au kwa hiari wewe ni mchezaji na majina yashatolewa tayari , unapaswa kuelewa  kampuni yetu haina wafanyakazi wa kiume wengi hivyo endesha gari  kurudi  kazini , mchezo unaanza mchana”Hamza alijikuta   akishindwa kujua alie au acheke , licha ya kwamba ni kweli anajua mchezo huo lakini hakuwa na mpango wa kucheza kabisa na alitamani kumpigia simu Aroni msimamizi wa mchezo huo na kumwambia  hakuwa tayari kuhusika.

“Regina  hebu subiri kwanza ,  kwahio haya mashindano mshindi  anazawadiwa nini   au ndio mnacheza kujifurahisha?”

“Hujakubali hata kuwa mchezaji unaanza  kuuliza  zawadi utakayopewa , hebu tuondoke muda unaenda”Aliongea Regina  huku kwa wakati mmoja akitamani kumpiga Hamza teke, alishindwa kujielewa kwanini  muda wote anahisi   kukerwa na Hamza  lakini kwa wakati mmoja akiifurahia kampani yake, kilichokuwa kikimuuzi zaidi  Regina ni maigizo ya Hamza alijua sio mtu masikini lakini muda wote anawaza pesa.

Lisaa limoja mbele  Hamza  na  Regina  waliwasili katika  uwanja  wa Basketi wa chuo  kikuu cha  Dar es salaam.

Sehemu hio ilikuwa imezingirwa na  polisi waliokuwa wameshikilia siraha  na hio yote ni kutokana na uwepo wa viongozi wa kiserikali ambao walialikwa kushuhudia mchezo huo.

Ijapokuwa ni mashindano   ambayo yalihusisha  wafanyakazi wa jiji lote lakini  yalifanyika siku moja tu.

Mpira huo wa kikapu  sheria zake sio kama za mpira wa miguu , raundi zilikuwa ni kila dakika ishirini ishitini.

Kulikuwa na  timu jumla kumi na sita  ambazo zinashiriki , kimsingi mashindano hayo huanza mchana mpaka  usiku  na ndio hufikia mwisho , ilikuwa hivyo kwasababu viongozi ambao wamealikwa hawawezi kuhudhuria kila siku kwa ajili ya mechi kadhaa  , kingine  wachezaji  karibia wote ni wafanyakazi wa makampuni hivyo muda wao wa kucheza mechi hizo kila siku ni mdogo.

Moja ya sababu kubwa kwa mashindano hayo na kwa timu ambayo inaweza kushinda ni  kujitangaza  bila  ya kutumia pesa kwa kupiga picha pamoja na  viongozi  wa kiserikali , ukweli ni kwamba  tuzo ya mshindi sio kitu kinachotafutwa sana hapo.

Hamza mara baada ya kufika tu alisogelewa na 

Aronni ambae alionyesha furaha kumuona , Hamza alilalamika kama sio mchezaji lakini Aroni alimwambia anapaswa kushiriki kwani idadi yao ni  ndogo na kutokana na  macho ya Regina yalivyokuwa siriasi  ilimfanya Hamza kutingisha kichwa  kukubali.

Kabla ya mashindano kuanza kulikuwa na  sherehe za ufunguzi  na kitu ambacho Hamza aliweza kusikia ni sauti za watu  asiowafahamu wakiuongea juu ya jukwaa.

Baada ya hotuba kutoka kwa viongozi na  wakuu wa kampuni husika  Hamza na wachezaji wengine waliokuwa wakishiriki walienda moja kwa moja mpaka kwenye vyumba vya kubadilishia 

Lakini  kitendo cha  kuingia ndani ya  korido ya vyumba hivyo aliweza kukutana na sura ya mtu ambae anamfahamu.

Aliekuwa mbele yake alikuwa ni James  na Chriss  wote wakionekana ni  mabosi  kutoka timu tofauti , Chriss akiwakilisha kampuni yao na upande wa  James  akiwakilisha  kampuni yao.

Chriss alikuwa na  kundi la wachezaji nyuma yake  huku  James pia hivyo hivyo,  licha ya timu kuwa tofauti lakini kulionekana  ukaribu kati yao.

“Hamza!!”Aliita James  huku akisogea kiswaga kumsogelea Hamza , mara baada ya Chriss kusikia jina la Hamza na yeye macho yake yalichanua na kusogea.

Ukweli ni kwamba Chriss hakuwa akimjua  Hamza vizuri zaidi ya kumsikia tu na alitamani kuonana nae , sasa ilikuwa ni kama bahati maana alikuwa na hasira sana   na bwana huyo kwa kujihusisha na Prisila.

Ki ufupi James alikuwa na hasira na Hamza kwasababu ya  Rregina , huku  Chriss akiwa na kisasi na Hamza kwasababu ya  Prisila.

Upande wa timu ya Hamza mara baada ya kuona kundi   la  James  walionekana kama vile walikuwa wameona   maadui wakubwa.

“Na nyie mpo hapa kwenye mashindano?”Aliuliza Hamza.

“Unauliza au umejijibu , unadhani  kampuni kubwa kama yetu inakosaje nafasi ya ushiriki ,sisi ndio waasisi wa mashindano haya”Alionge na kisha alimgeukia Chriss.

“Chriss huyu boya ndio Hamza ambae anatusumbua” Aliongea James huku akimwangalia Chriss.

Ukweli upande wa Chriss hakumwangalia Hamza kwa macho ya dharau alikuwa katika hali ya kumtathimini, kimwonekano hawakuwa wamezidiana sana   ni kwamba Hamza alikuwa na asili ya kizungu huku Chriss akiwa na asili ya kiarabu.

Kitu pekee kinachowatofautisha ni kwamba Hamza anaonekana kuwa mkakamavu zaidi kuliko Chriss wakati huo Chriss akionekana  aliestaarabika zaidi kuliko   Hamza.

“Chriss mbona huongei chochote? Huyu boya ndio alietambulishwa  na  Prisila?”Aliongea James na kumfanya Hamza kushangaa kidogo.

“Mimi kutambulishwa na Prisila  kuna tatizo gani mpaka kutaka mshikaji hapo aongee?”

“Mimi ndio mpenzi wa Prisila , naitwa Chriss Gabusha”Aliongea  Chriss akiwa katika hali ya  tabasamu.

Ukweli  ni kwammba  asubuhi mara baada ya Chriss kuamka  hasira yake zidi ya  Hamza ni kama ilishuka mara baada ya kuongea na  Prisila.

Upande wa Prisila hakujua kama Hamza  alikuwa akifahamika kwa  Chriss sasa ili kulinda  siri ya Regina ilibidi aseme  Hamza sio mpenzi wake bali   jana alimsindikiza tu  kama rafiki   wa rafiki yake  yaani Regina.

Upande wa  Hamza hakutaka  mambo kuwa mengi hivyo alipokea salamu  ya Chriss isitoshe  hakuwa na mahusiano na  Prisila hivyo hakutaka kuingilia sana maswala yake, maana  Regina alimpa

tahadhari kutofanya chochote ambacho kinaweza kumfanya James  kuona mahusiano yao ni feki.

“Hamza na wewe upo hapa kwa ajili ya mashindano?”Aliuliza Chirss.

“Ndio  na nyie vipi?”

“Unataka  kujilinganisha  na mimi , kwanini nishindane mwenyewe wakati wafanyakazi kama wewe wapo?”Aliongea James akiingilia maongezi.

“Upo sahihi , nadhani  kutokana hata kupigana hujui  mwili wako ni dhaifu hivyo  ni ngumu kwako kucheza  mpira wa kikapu?”Aliongea Hamza.

“Wewe mpuuzi  unajikuta nani  kuniita dhaifu , labda hujui ila mwaka jana  kampuni yetu ndio ilishinda  na tunataka na mwaka huu kushinda pia, tukikutana  kama timu  nitahakikisha nakuabisha mbele  ya Regina”Aliongea kijeuri , alikuwa akimchukia mno  Hamza kiasi kwamba alitamani kuongea kila neno  baya lakini muda  hakuwa nao.

Hamza na yeye alimpotezea na  kwenda kubadilisha mavazi , mwanzoni hakuwa na mudi kabida ya  kucheza mchezo huo lakini  uwepo wa James ni kama umempa motisha.

“Bro imekuwaje ukawa na uadui na  James , wale wachezaji wa kampuni yake licha ya kuwa wachezaji lakini pia ni  walinzi waliopitia mafunzo maalumu  na  wanajua mno kucheza rafu hivyo  uwe makini”Aliongea Aroni.

“Haina haja ya kuwa na wasiwasi tunaenda kushindana  kurusha mpira na sio 

kupigana”Aliongea Hamza na kumfanya Aroni   na wenzake kuwa na sura ziliozokunjamana.

Asilimia kubwa ya wachezaji  wenzake  Hamza hakuwa akiwajua vizuri kwasababu walikuwa wakifanyakazi nje na makao makuu .

Nusu saa mbele   mechi ilianza katika viwanja vyote vinne , Hamza mara baada ya kuingia katika Court  aligundua  wafanyakazi baadhi  kutoka makao makuu wamefika pia na walikuwa wakishangalia  kwa kutaja jina lake kitendo kilichomfanya kuhisi damu kuanza kumsisimka na kuona ni mahali pake pakujichukulia pointi kwa warembo hao.

Wafanyakazi hao walikuwa ni  kutoka idara ya mauzo  walioambatana na Eliza  na  mara baada ya mrembo huyo kukutanisha macho na Hamza aliishia kutoa tabasamu huku akimpungia mkono ,  alikuwa na macho yaliojaa matamanio kana kwamba anajaribu kuwaambia watu kupitia hisia yule ni mpenzi wangu.

Upande wa Regina kama bosi wa kampuni alikuwa ameungana na  mabosi wengine wa kampuni  na walikuwa wamekaa  kwenye jukwaa la VIP.

Sasa kitendo cha kumuona Hamza akipungiana mkono na Eliza na namna Eliza alivyokuwa akitabasamu  uso wake na macho yake yalijawa na hali ambayo haikutafsirika.

Muda huo James  akiwa na tabasamu zito alisogea na kwenda kukaa pembeni  ya Regina.

“Mrembo  , nadhani hutojali nikikaa pembeni yako?”Aliongea lakini upande wa Regina hakuwa na  hisia zozote  katika macho yake na hata hakujisumbua kumjibu.

James alijikuta akijisikia aibu kidogo  kutokana na macho ya  watu wengi yalikuwa yakimwangalia, alijikuta akijitafuta mwenyewe na kukaa chini  na   hazikupita  dakika  tano  lazima ageuze macho kumwangalia  mrembo Regina.

Hatimae kipenga kilipulizwa na mechi zote nne kwa wakati mmoja zilianza 

Upande wa Hamza timu waliokuwa wakishindana nayo ilikuwa imejaa wachina   na  baadhi ya  watanzania  wachache  na  kwa muonekano wao walionekana ni wataalamu   wa mchezo huo kwa namna miili yao ulivyojaa mazoezi.

Kwa macho yao   walionekana  kuwadharau wafanyakazi wa Dosam , licha ya kwamba ni kweli hata upande wa Hamza wachezaji wake walionekana kuwa na miili iliojengeka kimazoezi lakini  kutokana na uzoefu wao mchezo wa kikapu sio   swala la kuwa  na nguvu bali ni swala la nguvu , ujuzi na muunganiko  kitimu.

Lakini licha ya hivyo  walishangaa kukutana na ukinzani mkubwa wa kimashambulizi kutoka kwa timu ya Hamza.

Timu ya  Dosam haikuonyesha  kujali sana  kuonyesha mbwembwe  zaidi ya kurushiana mpira  mpaka  eneo la pointi tatu  na mtu wa mwisho kupata mpira   kama mwanariadha  aliruka  na kwenda kuutumbukiza mpira kwenye  kikapu

“Suui!!!

Mpira uliingia na kelele  kama zote na  hatimae  Dosam kujikuta wakianza na kupata  pointi  mbili.

Kampuni ya Dosam ilikuwa imebarikiwa  na wanawake  warembo na walikuwa wakishangilia kwa  shangwe na sauti tamu mara baada ya kuona timu yao imeshinda.

“Hamza tupo nyuma  yako , twende kazi, tuheshimishe baba!!!”Wakina Asha na  Mirium  walipiga kelele  na  wengine wote waliunga na kuanza kulitaja jina la Hamza.

Eliza  alikuwa na tabasamu kama lote ,  alijihisi kuwa na furaha kumuona mpenzi wake akicheza mpira wa kikapu kama hivyo. “Pumbavu wana bahati hawa”

Wapinzani wao walijikuta wakisemezana wao kwa wao wakiwa  na mshangao  na hatua iliofuata   waliingai katika pambano  la kuzuia  na kushambulia kwa wakati mmoja.

Upande wa Hamza ni kama alikuwa akitalii  , ukweli ni kwamba alikuwa akitembea  kurudi nyuma na kwenda mbele  na  hata uwezo wake wa kuzuia ulionekana mdogo.

Upande wa  Aroni  na wenzake mara baada ya kudaka mpira wa Rebounds palepale walimrushia   Hamza na  hakurembesha kwani kwa jicho lake la kichawi  alisogea mpaka eneo la pointi tatu  na kisha akarusha  mpira na uliingia bila  kugusa kigo za gori  na kilichosikika ni mkwaruzano tu wa  nyavu.

Mpaka dakika ishirini zinaisha Hamza alikuwa ameonyesha uwezo  wa  kurusha mpira  kwenye kikapu wa hali ya juu mno , hakuonekana kama mchezaji  wa basketbal ila alionekana kama  mtaalamu wa kulenga shabaha.

Matokeo ya mwisho  Dosam iliishinda  kampuni  ya kutengeneza rangi   kwa pointi 43 kwa 25.

Jambo hilo lilifanya wanawake  wa kampuni ya Dosam kumpigia kelele  Hamza huku  kila kilichowakalia mdomoni waliongea , ukweli ni kwamba hata  Aroni na wenzake walikuwa wakimshangaa Hamza kwa uwezo wake wa kulenga kikapu na mpira.

Na wakati wa kucheza kwao kote ni kama wameona namna ya kushinda hivyo  kila wakipata mpira walikuwa wakimpelekea Hamza ili kutupia.

Hakuna alietegemea kampuni ya Dosam inaweza kuvuka hata mechi ya kwanza na kwenda hatua inayofuata , maana siku zote Dosam ndio iliokuwa  ikiongoza kwa kuwa wa mwisho katika mchezo huo.

“Haha.. Bro aisee umenishangaza sana  , uwezo wako wa kulenga sio wa kawaida ni kama sio binadamu vile”Aliongea Aroni.

“Aroni  wakati unasema  huyu ni moja ya mchezaji nilijua umetupiga na kitu kizito  na tunaenda kuonyesha tu tumeshiriki, Bro una heshima  yangu katika mchezo wa Basktetball”

Wachezaji walianza kumsifia  Hamza  kutokana na uwezo wake , mpaka  hapo walijiona hawakuwa  na hofu tena ya kushinda mechi zinazofuatia.

Hamza  alienda mpaka pembeni ya uwanja na kisha akachukua chupa ya maji na kunywa kidogo huku akijiambia anapaswa kupunguza  namna anavyoshinda la sivyo watamuona sio wa kawaida , ili mradi timu ishinde basi  haina haja ya kuonyesha kupatia  kulenga kila  dakika anayopata mpira.

Upande wa Regina  alijikuta akipata ahueni na mara baada ya kusikia mabosi wenzake wanavyojadili namna  Hamza alivyokuwa na uwezo wa kulenga kikapu alijikuta akijihisi furaha  moyoni mwake.

“Regina  timu yako inacheza vizuri , lakini usiombee ikutane na timu yetu”Aliongea James

Regina  aliishia kumwangalia kwa ukauzu  tu huku akishikwa na wasiwasi , hofu yake ni  kwamba  James anaweza akawa na  kitu kibaya anapanga.

“Mr James nimesikia  kampuni yenu  imekuwa katika ushindani mkali na  Dosam hivi karibuni,  sidhani pia kama  mkikutana   utakuwa mchezo  rahisi, ninachoona hapa kila timu  inacheza kwa ajili ya kuheshimisha kampuni yake”Aliongea  Mkuu wa mkoa Mheshimiwa   Chamali  Ngala mara baada ya kusikia maneno  ya James kwenda kwa Regina

“Mheshimiwa kumbe na wewe una wasiwasi na  kampuni zetu pia , niwie radhi  kama  maneno yangu yameonekana sio mazuri kwa mpiuzani”Aliongea James huku upande wa Regina

pia akitingisha kichwa  kukubaliana  na Mheshimiwa.

“Zena na Dosam ni  moja ya kampuni kubwa zinazolipa kodi  kubwa  ndani ya Tanzania , mimi kama kiongozi ni swala la kawaida kujua kinachoendelea , matumaini yangu ni kuona  kampuni zote  zinakuwa na  kustawi  vizuri kwa manufaa ya  taifa zima , mashindano kama haya ni kawaida lakini  hata kama kampuni ni kubwa vipi haiwezi kuwa juu ya  sheria za nchi”Aliongea  Mheshimiwa.

“Ni kweli kabisa mheshimiwa , tutazingatia  maelekezo yako”Aliongea James huku akitabasamu  kinafiki ni kama  yeye ndio aliekuwa akisemwa.

Upande wa Regina hakuongea chochote  zaidi ya kutoa tabasamu hafifu.

Kwa bahati nzuri  Mheshiimiwa Chamali na  Jopo la Mameya wa jiji hilo walikuwa wakiijua fika tabia ya  Regina  na washamzoea sio mtu wa kuongea neno , hivyo ni kama walijua  kumvumilia.

Ilikuwa tabia ya Regina  hata mara baada ya kuombwa na  wagombea wa kiti cha uraisi  kufadhili  kampeni  lakini   Regina alikuwa na jibu moja tu kwamba  hatofadhili  upande wowote  maana hakutaka  kuiingiza  kampuni yake na maswala ya kisiasa.

Baada ya  kumpumzika kwa dakika kadhaa hatimae raundi ya pili ilianza na Hamza aliongea na wenzake na kuwaambia  wakipata mpira  wampasie, Hamza aliona  iwe hivyo kwasababu hakuwa na mbinu nyingine ya kuonyesha zaidi ya kuujaza mpira kwenye kikapu.

Hatimae mara baada ya  dakika  kumalizika  upande wa Hamza ulishinda tena  kwa faida ya Hamza kurusha mpira kutoka mbali na kuujaza na  hatimae raudi tatu zilipita  na ikafikia hatua ya  nusu fainali.

Na sasa ilikuwa ni zamu ya kampuni ya Zena  kushindana na  kampuni ya Dosam.

Aroni na  wenzake alikuwa wameloa jasho  lakini  walikuwa na morali kubwa  mno ya kushinda mechi.

Hasa pale walipokuwa wakitajwa majina yao na warembo wa kampuni yao  hali ya kujiamini iliongezeka huku wakiamini wakishindwa itakuwa rahisi kuwaopoa  hao warembo.

“Bro Hamza kama tukifanikiwa kushinda hii timu nina uhakika tutaweza kuwa bingwa , hii ndio timu ngumu  pekee  hivyo tunakutegemea”Aliongea Aroni.

“Ndio Bro  tutahakikisha tunausaka mpira  kwa namna yoyote na wewe ndio utakuwa  kete yetu ya ushindi”

Walishauriana huku wakimuona Hamza kama shujaa wao wa mchezo  ambae amewatoa katika  mateso ya kuonewa kila  mashindano hayo yakianza.

Hamza  licha ya kwamba hakuwa amezoeana na watu wengi lakini kupitia mechi hio ni kama ameweza kupata marafiki ndani ya kampuni kwa haraka sana.

“Haina noma , nyie nipasieni mpira  nitatupia”Aliongea Hamza na kisha waliwekeana mikono ya kitimu  na kisha kujipanga  kusubiria kipenga cha refa.

Nadhani moja ya sababu ya  wachezaji wa  kampuni ya Zena kushinda ni urefu wao , walikuwa wameenda hewani mno, wote walikuwa katika makadirio ya  mita  moja  pointi  tisa ki urefu, hivyo iliwapa  faida ya kushambulia  na kushinda kwa uharaka.

Mara baada ya mchezaji wa Dosam kupata mpira  alimpasia Hamza  na lijamaa lirefu la upande wa Zena lilimsogelea haraka na kumzuia kwa mbele  akinyoosha mikono yake.

Lakini ajabu Hamza aliruka juu zaidi kwenda angani kiasi cha kumzidi kimo yule mwamba  na kuurusha mpira kirahisi.

Kadri mechi ilivyokuwa ikiendelea ilionyesha ni namna gani urefu wao na ukubwa wa miili haukuwa na athari zote mbele ya Hamza kwani  wakimzuia hivi Hamza anafanya hivi na kushinda.

Ijapokuwa hata wao walikuwa wakishinda lakini  ilikuwa ni pointi mbili kwa  tatu , yaani wakishinda mbili Hamza anashinda tatu.

“CEO Regina  yule  bwana wa pointi tatu  tatu  naona  sio wa kawaida kabisa”Aliongea  Mheshimiwa huku akipiga makofi.

Regina upande wake  mdomo wake ulicheza kwa tabasamu  na kujiambia asije akajitia aibu  kutokana na furaha yake hivyo alijitahidi kujizuia kutoamka kushangilia.

“Yupo vizuri”Aliongea .

‘Upande wa wafanyakazi wa Dosam walikuwa na furaha , kuishinda  kampuni ya Zena ilikuwa  na  msisimko mkubwa kuliko kushinda timu yoyote ile.

“Eliza  , Hamza  ameshinda tena”

“Jamani jamani na alivyo Handsome , lazima nijishobokeshe kwake , sijui  atanipenda”

“Hebu acheni kujishebedua , Hamza ni wa kwetu na haendi popote..”Aliongea Mirium  na  Aisha   wakishindana na wafanyakazi wa benki ya Dosam katika kundi hilo alikuwepo  Mellisa  mpenzi wake Amiri ambae  alionekana kuwa tofauti kidogo na wenzake  licha ya kuwa na furaha, alikuwa mrembo haswa , ilikuwa haki kwa  Amiri kulilia penzi.

Upande wa  Eliza alikuwa na furaha kwasababu ya uwezo wa Hamza , lakini mara baada ya kusikia kila  mwanamke alikuwa akimtaka Hamza  wasiwasi ulimvaa.

Alikuwa na wasiwasi  kutokana na umaarufu Hamza aliojipatia  ni lazima warembo wa kampuni watamshobokea. 

Kutokana na Hamza kushinda mara kwa mara James wasiwasi ulimvaa mara moja na aliangaliana na Chriss ambae alikuwa amekaa upande wa nyuma akimwangalia Hamza kwa mshangao  na palepale James alitoa simu na kuonekana akituma meseji na hali ya  uovu ilionekana kwenye macho yake.

Baada ya  awamu ya pili kuanza  wachezaji wa kampuni ya  Zena walikuwa na mwonekano wa kikatili  na ilionekana mpango wao ni kucheza rafu  na ndio kilichotokea ,   wakati wa kushindania

Rebounds  mchezaji wa kati  aliruka  na  ghafla tu alimpiga  Aroni  kwenye kifua kwa kiwiko cha mkono 

Kitendo cha  Aroni kupiga ukulele kwa rafu ile   yule mchezaji alishuka chini na kumkanyaga kwenye enka ya mguu.

“Arghhhh..!!!”

Ukulele wa Aroni ulishitua baadhi ya watu   na Refa aliwahi kupuliza filimbi  akionyesha  kuwa ni faulu.

“Aroni  vipi hali yako?”

“Refa hawachezi kushinda ila ni  rafu”Aliongea  Aroni akiwa na maumivu na wachezaji wenzake mara baada ya kuona hilo walianza kugombana na wachezaji wa upande wa Zena.

Lakini upande wa timu ya Zena walionyesha hali za upole wakiashiria kwamba  faulu hio haikufanyika makusudi.

Kitendo kile  Regina alishindwa kukivumilia na kumgeukia James akimwangalia kwa macho makali.

“James  wachezaji wako wanafanya makusudi kuumiza wachezaji wetu””

Ukweli ni kwamba  James alitoa maelekezo ya Hamza asiguwe maana atawadhalilisha kwa kujua mapigano hivyo  alitoa  maelekezo kwa wachezaji wenzake ndio waumie

“Regina  hatimae umeanza kuniongelesha mwenyewe , lakini mbona unanisingizia , tukio  kama lile ni la kawaida  kwenye mchezo wa  kikapu”

Regina alijikuta akisugua meno kwa hasira , alijitahidi kujizuia kwasababu alikuwa amezungukwa na watu wa heshima , hivyo aliachana na James  na  pamoja na  Linda walishuka mpaka chini kwenda kumwangalia  Aroni.

“Vipi  hali yako , umeumia sana?”Aliuliza Regina .

Aroni mara baada ya kumuona  bosi amekuja kumwangalia alijitahidi kusimama  ili aongee nae lakini alijikuta akidondoka bila ya kupenda chini  kutokana na maumivu makali 

“Bosi Regina una mchezaji mwingine wa hakiba kwenye timu yako?”Aliuliza Refarii huyo wa kike

“Mchezaji mwingine!?”

Regina alijikuta  akishindwa kuongea mara baada ya kujua hakuna mchezaji mwingine 

“Refa kwani kuna ulazima  wa kucheza   watu watano ili kuendelea na mechi?”

“Ndio , hatuwezi kupindisha sheria ya mchezo”Aliongea Refa na kumfanya Hamza kufikiria.

“Kama ni hivyo unaonaje  Aroni akiendelea kubakia uwanjani hata kwa kukaa?”Aliuliza na kufanya kila mtu kushangazwa na pendekezo lake.

“Unachomaanisha aendelee kubakia mchezoni?”

Previoua Next