Reader Settings

SEHEMU YA 49.

“Namaanisha tumeanza pamoja hivyo tutamaliza pamoja”Aliongea Hamza akiwa  na  tabasamu  la kawaida lakini macho yake yalionyesha namna gani alikuwa siariasi.

Refa  hakufikiria  sana na aliishia kumuuliza Regina kama anakubaliana na wazo la Hamza na  Regina  upande wake aliishia kukubali na mechi ikaanza  lakini kwa sura tofauti.

Wachezaji  wanne upande wa  Dosam huku  Aroni akiwa amekaa pembeni  kana kwamba anasubiria kuangalia kinachokwenda kutokea.

“Sikia nipasieni mpira mimi , hakikiisheni mnaeupka kufanyiwa  rafu”Aliongea Hamza na wachezaji watatu wote walitingisha kichwa kukubaliana nae.

Upande wa wachezaji wa  Zena waliamua kutumia uwezo wao wote wakiwa wengi uwanjani , isitoshe waliona ingekuwa ni  aibu kama watapoteza shindano kwa timu iliopo na wachezaji pungufu.

Lakini mwishowe mara baada ya mpira kumfikia Hamza walijikuta wakitamani kuzimia , Hamza alikuwa katikati  kabisa ya court  na bila kusema  chochote alirusha mpira mpaka kwenye  kikapu na ukaingia  na kuwapatia pointi tatu.

Kitendo hicho cha ushindi wa Hamza kutokea mbali uliamsha hata  mashabiki wa kampuni ambazo zimekwisha kutolewa na kuanza kuishangilia kampuni  ya Dosam.

“Mungu wangu , Jamani Hamza  weweee..!!”

“Wewe kaka jamani..!!”

“Kama angekuwa na urefu  hata sentimita kadhaa nadhani  anavigezo vya kushiriki NBA”

“Haha.. umeenda mbali sana lakini ni kweli yupo vizuri”

Watu walianza kuongea wao kwa wao huku kelele

zikiwa zimejaa , katika kipindi chote cha mashindano pengine siku hio ndio  mchezo huo umekuwa na hisia kubwa kwa wanaoangalia.

Wachezaji wa Zena waliona ni ngumu kumzuia Hamza kutoshinda hivyo walitumia mbinu ya kumzunguka kuhakikisha hapati mpira.

Lakini sasa Hamza ni kama anawapotea kimazingara na wanapotaka kumzunguka ashapotea  na kuwa sehemu nyingine  na kukamata mpira  na hakujali eneo alilosimama  akiupata hakufanya mbwembwe na kuutupia golini huku akijikosesha mara kadhaa huku mara nyingi akipatia.

Hamza hakutaka kuonyesha vitendo ambavo sio vya kawaida , alihakikisha mbinu zake zote zinaonekana katika  macho ya wanaomwangalia  kwa kuhakikisha  namna ambavyo anakwepa  wapinzani wake.

Ndani ya muda chache   ubao ulisoma  hamsini na moja kwa ishirini na tatu na Hamza pekee alishinda  pointi arobani, hivyo matokeo ya mchezo yalionekana wazi.

Mpira wa mwisho mara baada ya  kumfikia  Hamza aliamua kuonyesha ujuzi sasa alikimbia na mpira kwa kuudunda dunda mpaka  pembeni ya  uwanja  na kisha kwa  umakini mkubwa sana alirudi  kati  na kugonganisha  katika  ubao  wa gori  na kisha kwa  uwezo wa juu ali’dunk’  na kwenda kuujanza mpira  kwenye kikapu na mkono mmoj. “Damn!  anajua  hata Ku’slum dunk?”

“Nilijua anachojua ni kulenga  kikapu  tu”

“Hii inakwenda kuwa aibu kwa  upande wa itmu ya Zena  kushindwa na wachezaji wanne”

Watu walikuwa wakiongea kila walichowaza huku wengine wakishangalia  kwa  ujuzi  wa ku’dunk’ alioonyesha Hamza.

Upande wa timu ya Zena  sura zilikuwa nyeusi  tii , moja ya  mfanyakazi wa kampuni hio alikuwa ni mchezaji mkubwa sana wa  mpira huo ndani ya jiji la Dar  na alishangazwa na uwezo wa Hamza.

Aroni aliishia hata kusahau maumivu yake na alijikuta akiungana na wengine kushangailia 

Baada ya kuona  hamasa hio ya mashabiki  wapya kila mfanyakazi wa kampiuni ya Dosam alijawa na  furaha.

Eliza  aliishia kuruka ruka kwa furaha  , alitamani kutoka alipo  na kwenda kumbusu Hamza lakini kariba yake haikumuwezesha kufanya hivyo.

Regina aliishia kumwangalia  Hamza na macho yaliojaa hisia  ,  kwa jinsi Hamza alivyokuwa akijiamini na mwili wake wa mazoezi ulivyo mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi mno.

Linda ambae hajawahi kumkubali Hamza alijikuta akionyesha  ishara ya kumheshimu.

Viongozi  waliohudhuria walijikuta wakisimama na kuanza kupiga makofi , walikuwa pia na furaha  japo  wengi wao walijilazimisha kuja kutokana na mashindano hayo kukosa msisimko lakini kwa kilichotokea kiliwafurahisha.

Chriss  alikuwa na wasiwasi kwenye  macho yake , ukweli ni kwamba  licha ya kampuni yake kushindana hakuwahi kuitilia mkazo kushinda , kilichompa wasiwasi  ni kwamba  licha ya  Prisila kujitetea asubuhi  lakini bado alikuwa na wasiwasi , aliona kuna kila dalili ya Prisila kumpenda mwanaume kama Hamza ambae ana uwezo mkubwa.

Katika macho yake  hakumuona  Hamza  kama mwanaume mwenye pesa bali  mwenye  uwezo  na  kunasababu iliomwambia  ndio maana  Prisila alimchagua  ku’fake’ nae kuwa boyfriend wake , isitoshe habari za Hamza kufahamiana na Yulia alizisikia pia.

James yeye  alijikuta akibadilika sura kutokana na hasira , aliishia kuinamisha kichwa   chake chini na taratibu alitoka kwenye jukwaa na kuelekea upande wa parking na kisha kuondoka.

Hakuaka kuendelea kukaa hapo , alikuwa amemsahau hata rafiki yake  Chriss aliekuja nae.

Kutokana na  uwezo wa Hamza timu nyingine  ilikataa kuingia uwanjani hivyo   timu ya Dosam ilipewa ushindi moja kwa moja na kuwa mabingwa.

Hakuna  timu ambayo ilipenda kudharirishwa na Hamza  maana ni kama alikuwa akicheza peke yake uwanjani.

Hamza alikabidhiwa cheki ya pesa  kiasi cha  shilingi milioni  mia  na mara baada ya  kuona tarakimu hizo alijikuta akijawa na majuto na kujiambia kwanini hakufikiria  hili kabla , pengine mara baada ya kuja bongo angejiingiza kwenye  mchezo wa basketball na ingekuwa rahisi mno kwake kujipatia pesa za haraka.

Mara baada ya kupokea kitita hicho kama  mchezaji bora  hakuwaza kuzitumia yeye , alijua fika ni wapi  anapaswa kuzipeleka . sehemu  ambayo anakumbukumbu nayo  wakati wa utoto wake.

Jioni mara baada ya  mashindano kuisha  Regina aliandaa tafrija  ndogo katika  hoteli ya Dosam V kwa ajili  ya kuwazawadia  timu yote ilioshiriki katika mashindano hayo.

Tokea  aanze kufanya kazi kama kiongozi wa kampiuni hajawahi kuona morali ya wafanyakazi  wake kuwa juu namna hio  na aliona ni swala la kusherehekea.

Lakini hata hivyo  jina la Hamza halikusahauliwa maana ndio liliipatia heshima kampuni.

*****

Upande mwingaine  wakati  wafanyakazi wa kampuni ya Dosam wakisherehekea ushindi kwa furaha kubwa , nyumbani  kwa mzee Benjamini  wingu   zito lilikuwa limetanda kuzunguka  nyumba yao tu.

Ndani ya jumba la kifahari la Mzee Benjamini  katika eneo la sebuleni  Mzee Benjamini  na James walikuwa wamekaa kwenye masofa  huku chupa kadhaa za whiskey zikiwa zimeenea.

Walionekana walikuwa wamekunywa mno , macho yao yalikuwa mekundu na yamevimba kama ya nguruwe.

“Kulingana na   uchambuzi .. taarifa ya habari ikitoka  hisa za kampuni ya  Dosam zitapanda  kwa asilimia tatu  na hisa zetu zitazidi kuporomoka  kwa asilimia mbili”Aliongea Mzee Benjamini.

“Kushuka tena , nimeweka juhudi kubwa kuzipandisha  na  zinakwenda kushuka tena?, F*ck him,  haya yote ni kwasababu ya huyu mpuuzi Hamza , huu ndio ulikuwa mpango pekee wa kuirudisha  taswira ya kampuni yetu lakini  tumeshindwa tena”Aliongea James kwa hasira huku akipasua glasi ukutani.

“James usiwe na wasiwasi  tulikuwa kwenye kikao kizito na mstaafu  Mgweno  na ajenda kubwa ilikuwa ni namna ya kumuondoa  Hamza  hapa Tanzania , mheshimiwa kupitia  umoja wa Makomandoo  ametoa agizo Master Konki kufika mara moja  nchini na watalaamu wa mapigano, mawasiliano yashafanyika na  muda si mrefu atafika  na kumshikisha adabu”

“Baba  hata  kama   hao watu kutoka  kundi la Mwewe mweusi wakifika  sidhani kama   wanaweza kumjeruhi  Hamza  na hata kama wafanye hivyo hawawezi kubadilisha chochote  ndani ya kampuni

yetu  ni  raia wa kigeni  sidhani watakuwa na ujasiri wa kumuua  Hamza”Aliongea James na kumfanya Mzee Benjamini kuwa kimya , hata yeye pia alikuwa akifikiria juu ya swala hilo.

“Baba si ulisema  mara ya mwisho  kama hatuwezi kumpata Regina kwa njjia za kawaida tutatumia njia nyingine , huoni huu ni muda sahihi wa  kutafuta maninja hatari  ili kumuua Hamza na Regina”

“Kuwaua wote kutarahisisha changamoto zetu nyingi , lakini  kwa maelekezo ya mstaafu   huu ni mpango wa mwisho kabisa kama mbinu zote zikishindikana, isitoshe pia  tuna  watu wetu ndani ya  familia ya  Regina”Aliongea  na dakika hio hio anamaliza  aliweza kusikia kelele za mwanamke kutoka nje.

“Waueni , kama msipo waua sasa hivi  tunaweza kuchelewa kabisa”

Baada ya kauli hio  kusikika iliwafanya James na baba yake kugeuza vichwa.

Alikuwa ni Lamla mke wa mzee Wilsoni na  Regina mama yake wa kambo. 

“Rebe nini tatizo , kwanini umekuja   ghafla ghafla?”Aliuliza mzee Benjamini.

“Madam  , nini  kimetokea?”Aliuliza James 

Lamla ambae aliitwa  Rebeka na Mzee Benjamini kama vile yupo kwake alitupa  mkoba wake kwenye sofa na kisha alijimiminia kilevi kwenye glasi na kupiga mkupuo mmoja.

“Kama nisingekuja kukuelezea kinachoendelea  pengine ningechelewa”

“Nini kimetokea?”

“Si yule Ajuza  amekuja Dar  jana kwa ajili ya matibabu na inaonekana  hana muda   wa kutosha kuendelea kuishi  na mpango wake ni kumrithisha  Regina hisa zake zote”Aliongea kwa hasira

“Nini!!?, Amekuwa kichaa , kwahio anaacha kumpaitia  mtoto wake  Wilsoni na  kumpatia mjukuu wake?”

“Kinachokasirisha zaidi , Benjamini yule kizee hana mpango kabisa wa kumpatia mtoto wetu Frank  hata  hisa moja  na ameenda mbali kumwambia aende eti akafanye kazi  katika nafasi ya chini, yaani nimeitumikia ile familia kwa muda mrefu  na bado wananidharau”Aliongea Lamla huku aking’ata meno kwa hasira lakini upande wa James alikuwa na mshituko.

“Baba.. madam ,  mnaongea nini, Frank ni mtoto wenu?”Aliuliza kwa hamaki na kumfanya Mzee  Benjamini  kunywea.

“Benjamini inamaana hujamwambia  James bado?”Aliuliza na kumfanya Mzee Benjamini kumwangalia mtoto wake.

“Sikia James  ukweli ni kwamba  Frank  ni damu yangu ..  hivyo ni  mdogo wako”Aliongea

MzeeBenjamini na kauli ile ilimwamsha James 

“Nini!!, nyie watu  mekuwa vichaa ?”

“Wewe mtoto hebu kaa chini , cha kushangaza nini hapo , unadhani  ningejisumbua vyote hivyo  kupambania ndoa  yako na Regina  na kushirikiana  na baba yako  ili tuichukue kampuni ya Dosam, unadhani nimefanya bure, ni kwasababu mimi na baba yako tunahistoria”

James alikuwa ameshikwa  na bumbuwazi bado hakuwa  ameamini kinachoendelea.

“James  sisi ni familia”Aliongea Lamla.

“Wilsoni ni   mwanaume mpuuzi puuzi , kwa miaka yote hio ameshindwa hata kujua  Frank sio mtoto wake ,  ni hivyo tu  Mzee Dosam aliwahi kumleta Regina  kipindi kile  na kumfanya kuwa sehemu  ya familia na  mpango kuvurugika … kama sio Regina tungeweza kuichukua kampuni ya Dosam muda mrefu sana”

“Mzee Dosamu yule hakuwajhi kuwa mtu mwepesi  na hata kwa  mke wake ni hivyo hivyo , sina  uhakika kama  yule kikongwe hajui  Frank sio  damu ya  mtoto wake , mimi nadhani anajua ndio maana yupo tayari kumpatia  Regina hisa zake zote”

“Tunapaswa  kuhakiksiha  Frank anaendelea na  mafunzo ya  kivitendo ndani ya  kampuni ili  kuonyesha uwezo wake , ninaamini yule kikongwe anaweza kuishi  kwa muda mrefu kidogo kabla ya  kutoa hisa zake  na Frank atakuwa  na  uwezo wa kuthibitisha uwezo wake”

“Unadhani  atabadilika , ana hisa asilimia 32 yule na yupo tayari kumpatia Regina zote?”

“Nimeulizia  idara  ya sheria  na nilichoambiwa  wosia wa Mzee Dosam utafuatwa  kama kawaida ,  Kama Regina ataoana  na Hamza ndio atawapaitia hisa zake”Aliongea Lamla.

“Huu ni upuuzi yaani kumpa mtu hisa kwasababu

kaolewa , yaani sijawahi kuona sababu kichaa kama hii”

“Hata mimi  nimewaza hivyo hivyo , ninachoona yule kikongwe anachotaka kuona ni Regina kuolewa kabla ya kufa  , lakini maamuzi ya  kumpatia hisa Regina yashafanyika muda mrefu na anafanya maigizo tu”Aliongea Lamla kwa chuki.

“Vipi kuhusu Mzee Wilsoni, hana pingamizi lolote katika hilo?”

“Pingamizi alitoe wapi , mwenyewe bado anamuogopa mama yake na hataki kumpinga kwa kuogopa atapokonywa asilimia saba anayomiliki, yaani hana analojua kichwa maji kabisa ,  nachukia kipindi kile kukubali kuolewa nae”

“Lamla  ni makosa yangu kipindi kile , kama sio wazazi wangu usingekuwa katika hali hii”Aliongea 

MzeeBenjamini huku akimpeti peti na kumfanya  Lamla kulegea 

“Baba unamaanisha nini , usiniambie ulilazimishwa kuoana na mama yangu?”Aliuliza James.

“Ah, sijamanaisha hivyo  ni kwamba  baba alichanganya mambo , ni makosa  ya baba”Aliongea Benjamini  huku akijitetea.

“Sitaku kuhusika   kwenye maswala  yako mzee , nimezdhalilishwa vya kutosha na Regina na yule

mwanaharamu Hamza , ninachotaka ni wao kufa sio  kingine”

“James  yupo sahihi , hatuna muda wa kupoteza , ikitokea  Bi Mirium kumpatia  Regina hisa zake  moja kwa moja hatuna cha kufanya tena , tunapaswa kuchukua hatua sasa hivi”

“Huna haja ya kuongea sana , ninajua mtu ambae anaweza kuniunganisha na muuaji  mbobevu  hapa Dar , awamu hii  nitatumia pesa yoyote kuhakiksiha  namuua Regina na Hamza”Aliongea James  na kwa hasira aliondoka.

Kitendo cha  James kuondoka  ni kama wamepewa uhuru kwani  Lamla alimbusu  mdomoni  Mzee Benjamini na kisha kuegamia kifua chake.

“Benja .. unadhani  James hatonichukia?”

“Huna haja ya kuwa na wasiwasi , umekuwa    msaada mkubwa kwake kwa muda mrefu , nina uhakika mambo yakienda sawa  ataelewa tunachokifanya sio kwa ajili ya Frank pekee”

“Upo sahihi kwa ajili ya Frank  na James tumeshirikiana kwa muda mrefu  kwa siri sana kukamilisha mipango yetu , hatuwezi kuruhusu tulichopanga miaka  kumi na tano  nyuma kupotea hivi hivi na  kampuni kuchukuliwa na

Regina”Aliongea  Lamla na kumfanya  Mzee Benjamini kugida kilevi chote kilichobakia na kisha alisimama na kumshika Lamla kiuno.

“Leo hakuna kurudi , nimekumisi kwa muda mrefu , hebu twende chumbani kwanza”Aliongea na kumfanya  Lamla uso wake aliojichubua kuwa mwekundu.

“Yaani wewe , kila ukiniona unachowaza ni ngono 

tu , miaka yote hio ni kazi ya kukupa tu huchoki wewe mwanaume “

“Hehe , kama umechoka wewe sema , mimi naiweza shoo kuliko yule goigoi wako, au nasema uongo?”

“Tena hata usimtaje huyo  mjinga , hebu twende zetu tukaliamshe”

******

Siku iliofuata  katika bahari za michezo  ni juu ya ushindi waliopata kampuni ya Dosam na namna ambavyo Hamza alionyesha uwezo wake.

Ilikuwa ni habari ambayo ina  taswira chanya kwa kampuni hivyo hisa zake zilipanda kama ilivyotabiriwa 

Wakati wa  chai ya asubuhi  Regina aliona habari hio  na alijikuta akifurahi mno.

Baada ya kumaliza kula walipokea Delivery  kutoka kampuni ya usafirishaji wa mizigo  ya kimataifa na mzigo  huo ulikuwa ni wa Hamza.

Hamza alisaini  na kisha akapoktea  mzigo wake , ulikuwa ukitokea London Uingereza na ilionekana  Master Alex  alikuwa ashamaliza kazi yake ya kuandaa  mavazi ya Hamza ya kuvaa.

“Aiii.. huyu mzee inaonekana ametumia juhudi kubwa sana kukamilisha kazi sio kwa uzito huu”Aliongea Hamza na  kisha alilitupia  boksi lile kwenye ngazi akiwa hana haraka ya kulipeleka juu kwake.

Regina aliishia kuangalia lile boksi  na macho yake yalionekana alikuwa na shauku ya kutaka kuona nguo alizoletewa Hamza.

“Vipi Regina unataka  na wewe kuona nguo zangu za ndani?”Aliuliza  Hamza na kumfanya Regina  uso kuanza kupata joto kutokana na kauli ya Hamza , maana ni kama  anamwambia baada ya kuona nguo yake ya ndani  siku ile basi ni zamu yake na  yeye kuona zake.

“Sina shida , hebu fanya  haraka

tuondoke”Aliongea Regina huku akinywa juisi yote kwa mkupuo mmoja.

“Nimeheshimisha kampuni kwa kushinda ,  hujaniambia ni zawadi gani unanipatia?”

“Nitakupa muda wowote , haraka ya nini , kwani huna kitu kingine cha kuongea   kisichohusisha hela?”

“Kama ni hivyo   basi nitaongea kitu kingine  kisichohusisha hela , eti Regi  ni lini tunafunga ndoa kama bibi alivyosema?”Aliuliza Hamza na kumfanya Regina  kuzidi kubadilika na uso wake wa kirembo kuwa mwekundu.

“Sifungi ndoa  halafu nani anataka kufunga ndoa na wewe?”Aliuliza na kumfanya Hamza kucheka ,  hata hivyo  alikuwa akitania  tu.

Tokea   bibi yake Regina ataje swala la ndoa  , Regina alikuwa  sensitive sana na neno ndoa , ukimtajia  ni kama  Simba aliekanyagwa mkia.

“Nimeuliza tu , hasira za nini sasa?”

“Ukiniuliza hilo swali  la kipuuzi tena  nitahakikisha sio zawadi tu ambayo utakosa  bali ni mpaka mshahara wako”Aliongea kwa hasira  na alitamani kumwagia Hamza maji ya uso.

Shangazi ambae alikuwa bize jikoni  aliishia kusikiliza mtafaruku huo na kujikuta akitingisha kichwa chake kwa masikitiko.

Ilikuwa ni bahati tu bibi  yake Regina alikuwa hospitalini bado la sivyo  angecharuka kusikia makelele hayo.

Muda huo huo simu  ya Regina ilianza kuita na Regina alimwangalia  Hamza kwa  sekunde  na kisha kuipokea. “Linda  kuna nini?”

“Bosi mambo sio mazuri huku , yule mtu  aliekuja mara ya mwisho anaejiita Konki amerudi tena akiwa na kundi  la  wathailland  na wameingia mpaka floor ya  pili  idara ya  walinzi na Gym, inaonekana wamekuja kulipa  kisasi”Aliongea  Linda.

“Nini!!?”

“Kapteni  Yonesi anajaribu kuwazuia  lakini sina uhakika kama ataweza , vipi nipigie simu polisi?”Aliuliza na kumfanya  Regina kufikiria kwa muda , alijua fika mpaka  wakafika  katika kampuni yake kuna mkono kutoka  kwenye  jeshi la polisi hivyo haiwezi kuwa na maana.

“Mwambie Yonesi asifanye kitu chochote , tunakuja muda si mrefu”

“Sawa bosi”

Regina mara baada ya kukata simu hakuweza kumuona Hamza mbele yake  tofauti na ngurumo ya gari  na  hakutarajia Hamza angekuwa mshapu kiasi hicho , alitoka haraka haraka na kuingia kwenye gari 

“Tunaelekea…”

Regina kabla hata ya kuongea  gari ilinguruma kama simba na kupiga msele  huku ikiacha moshi kana kwamba inataka kupaa.

“Ahhhhhh.., wewe wewe unafanya nini?”

“Funga  mkanda vizuri , leo  barabara inaweza isiwe nzuri”Aliongea Hamza huku akikunja sura.

Regina alitaka Hamza kuendesha gari kwa haraka lakini  hakutaka Hamza kuchafua hali  ya  hewa kwa kuendesha gari kama kichaa , lakini mara baada ya kukumbuka  kinachoendelea kwenye kampuni hakutaka kumzuia.

Aliishia kufumba macho na mara baada ya Hamza kuliingiza  gari barabarani kama  mshale  alilitoa nduki  na walichukua  dakika  ishirini na tano mpaka kufika makao makuu , ilikuwa bahati kwao hakukuwa na msongano.

Mpaka  gari linakuja kusimama ndani ya  maegesho ya kampuni  Regina alijihisi tumbo la kuhara lakini aliamua kujikaza na kuvuta pumzi na kisha kushuka na kuingia ndani.

“Linda hali ipoje?”Aliuliza  Regina mara baada ya kupokelewa na  Linda.

“Mkurugenzi   wapo katika  floor ya mazoezi , Yonesi anabishana nao , anang’angania kushindana nao”Aliongea Linda na mara baada ya Regina kusikia hivyo  kwa haraka sana aliingia kwenye lift  pamoja na Hamza na kwenda juu.

Mara baada ya kuingia katika floor hio waliweza kumuona Master Konk na kundi  la wanaume  nane, watano wakiwa ni weusi huku  watatu wakiwa sio raia wa Tanzania na kulikuwa na wafanyakazi wengine wa kampuni ambao wamefika pia kuangalia.

“Hakikisha  wafanyakazi wote waliofika hapa kuangalia wanaondoka na kuendelea na  majukumu yao”Aliongea Regina  akimpatia Linda maagizo na ndio muda ambao  Linda anagundua wafanyakazi wengi walikuwa wamefika kuangalia kinachoendelea na kwa haraka aliwaambia waondoke wakaendelee na kazi.

“Yonesi hebu shuka  kwanza hapo?”Aliongea Regina akimtaka  Yonesi kutoka kwenye ulingo, hakutaka kukurupuka maana alikumbuka mara ya mwisho  alimshindwa  Master Konki na kama sio Hamza angeumizwa.

“Mkurugenzi wamekuja kutafuta tu matatizo  hapa , kama tusipowapa sababu ya kuondoka watarudi tena”

“Wewe msichana  hivi unadhani unaweza  kuwazidi hawa ,  yaani unishindwe mimi uweze kushindana na  hawa wataalamu wa sanaa  ya mapigano”Aliongea Master Konki alikuwa bado na  Bandeji kwenye mkono wake na alichukua nafasi ile kumtambulisha  Mthalland mmoja aliekuwa  mrefu wa mita kama moja na  nusu hivi , ambae amevalia mvazi ya kitamaduni ya Thailland ,ni kama amevaa shuka  halafu akalitengeneza suruali 

“Mimi  ni makamu  kiongozi mkuu wa dhehebu la Black Eagle nafahamika kwa jina la Chekani ,  mwanafunzi wetu mzee  Konk alitoa taarifa ya kukutana na mtu anaemzidi kwa kutumia msingi wa  sanaa ya kimapigano wa mbinu yetu ya vidole vya  Tai , hivyo kwa shauku   nimesafiri na  kaka zangu hawa wawili kujionea wenyewe, ni  maagizo pia  kutoka kwa  baba yangu”

“Mzee mara ya mwisho sikuwa makini na sikutarajia kama una mafunzo yale  lakini awamu hii hata tukutane sina uhakika  kama utaniweza”Aliongea Yonesi huku akimsogelea yule bwana aliejitambulisha lakini  bwana yule  aliefahamika kwa jina la Chakeni alimwangalia  Yonesi  kwa dharau.

“Sina mpango wa kupigana na mwanamke , usiniambie wanaume  mliopo hapa hakuna mwenye uwezo  wa kupigana na mimi”Aliongea

Chekani huku macho yake yakitua kwa Hamza.

“Hili sio swala la  nani  kuwa mwanamke au mwanaume  bali ni swala la uvunjifu wa  sheria , kampuni ya Dosam ni kubwa na kuingia ndani   kuleta taharuki ni kuvunja sheria , serikali inatulinda pia, sijui  uhusiano wa   kundi lenu la mapigano na serikali ukoje  lakini usije kuona hatuwezi kufanya chochote”Aliongea Regina  kwa hasira na Mzee Konki  macho yake aliyageuzia kwa Hamza.

“Haina haja ya kutumia sheria  kutuogopesha na hatujaja hapa kuvunja sheria , sababu ya kuja ni kwa ajili ya kupambana na huyo  mtoto . hili swala halina uhusiano wowote na kampuni yako”Aliongea Mzee Konki.

“Yaani mmekuja ndani ya kampuni halafu mnasema hili swala halina  uhusiano wowote  na kampuni?”Aliuliza  Yonesi.

“Hakuna shida , kama    hamtaki tukitumia eneo hili basi   tunaweza kutafuta sehemu nzuri  ya kupigana ,sidhani  tukiondoka na Hamza hili litakuwa na uhusiano na kampuni”Aliongea Master Konki na  kumfanya Regina kumwangalia Hamza.

“Una maamuzi gani?”Aliuliza , Regina hakuwa na uelewa mkubwa sana kuhusu sanaa ya mapigano   hivyo alikuwa na wasiwasi  Hamza anaweza  kumshindwa  Kachani.

Upande wa Hamza wasiwasi wake   ni kuogopa walinzi wa kampuni  akiwemo Yonesi watapigwa lakini mara baada ya kukuta hakuna  kilichotokea  alijikuta akipumua.

“Sijachukua mazoezi ndani ya muda mrefu kidogo

, nadhani sio mbaya kama nikienda  nao”Aliongea Hamza

“Subiri kwanza , unamaanisha nini , unadhani   wanaweza kunishinda?”Aliuliza Yonesi  akizuia na hakuwa na furaha baada ya  Hamza kutokumuuliza  chochote.

“Kapteni Yonesi hawa wapo hapa kwa ajili yangu , sidhani  kuna haja ya wewe kujihusisha”

“Mimi ndio kapteni wa timu ya ulinzi  , nina kila sababu ya  kulinda usalama wa wafanyakazi wote , sitaki  kuonekana kama sina thamani na kazi yangu siiijui”Aliongea  Yonesi na kisha  akamwangalia  Regina.

“Mkurugenzi tafadhari naomba uniamini mimi , awamu hii siwezi kushindwa”Aliongea Yonesi kwa namna ya kubembeleza na  ilimfanya Regina na Hamza kushangaa kwani hawakuamini Yonesi  atakuwa siriasi mno kuhusu swala hilo, ilionekana ni dhaihiri kabisa  Yonesi hakukubali kushindwa kirahisi.

“Basi haina haja ya kuondoka mtapigana hapa hapa , Hamza muachie Yonesi pambano”Aliongea Regina.

“Asante sana Mkurugenzi  kwa kuniamini nakuahidi sitokuangusha”Aliongea huku akionyesha shukrani  za dhati kabisa kwa  Regina.

Muda huo Chekani hakuwa na jinsi  zaidi ya kuingia kwenye ulingo kwa ajili ya kupigana na Yonesi licha ya kuona   msichana huyo hana chochote cha  kumtishia”

Unadhani Yonesi atashinda au atadundwa mpaka  maji ayaite mma.

Previoua Next