Reader Settings

SEHEMU YA 50

Kitendo cha  Chekani kuletewa Yonesi kupigana nae aliona ni kama dharau.

“Kwahio mnadhani nimejifunza sanaa ya mapigano  kwajili ya  kushindana na kila mtu hata kama  hana vigezo?”

“Acha visingizio , tutaongea  hili baada ya kuweza kunishinda”Aliongea Yonesi  akiwa ameshakaa  pozi la kupigana.

Kechani aliishia kutingisha kichwa na kuingia ndani ya ulingo  huku akipiga hatua moja kumsogelea  Yonesi , wakati huo  kidole chake gumba kilinyooka na kisha kikajikunja  huku vile vinne  , viwili vilitokezea kwa mbele huku viwili  vikisambaa  na  kufanya mkono wale uonekane kama vile ni mguu wa Mwewe.

Baada ya kuona mbwebewe za adui yake, Yonesi hakutaka kuchelewa na alianzisha mashambulizi kwa  kumrushia  ngumi Chekani akimlenga kifuani, lakini  mara bada ya kurusha ngumi ile  Chekani  alisogeza mkono wake wa kushoto uliokuwa katika umbo la kucha za tai  akinuia kuikamata ile ngumi , lakini  upande wa Yonesi  aliinama kwa mbele na kisha kunyanyua mguu  kwa mzunguko , alionekana kumzubaisha adui yake kwa  kumuonyesha anataka kumpiga ngumi lakini shambulio halisi alikuwa amepanga  litokee katika mguu wake.

“Bamm!!

Chekani alijikuta akishituka  na alijitahidi kwa uwezo wake wote kuzia shambulizi  lile.

Upande wa Yonesi mara baada ya  kufyatua mguu na kwenda hewani alipiga sarakasi na kwenda kusimama tena  lakini hakuzubaa alirudi na teke staili ya roundhouse  ambayo ilimpiga  Chekani mgongoni na kumfanya  kujikota kwenda mbele.

Tukio lile la Yonesi kufanikiwa kumpiga  Chekani lilimfanya Mzee Konki na wenzake kushangazwa mno , maana  ni kitu ambacho hawakuwa wametegemea kabisa.

Chekani alijikuta akigusa eneo alilopokea shambulizi na  uso wake ulizidi kujaa usiriasi , ni kama ile dharau aliokuwa nayo juu ya Yonesi ilipotea.

“Mbona unashangaa , unadhani kujua kwako  sanaa za kimapiugano zilizopitwa na wakati unaweza kunipiga kirahisi?”AliongeaYonesi.

“Safiii,,, nimekudharau  ndio maana , hebu angalia hii kwanza”Aliongea Chekani kwa kingereza  na palepale alisogea  kwa haraka  kwa staili flani kama vile ni  Sungura anaekimbia na kisha kumrukia  Yonesi  huku  kucha zake zilikuwa zimeleekezewa upande wa  kiganja cha mkono cha Yonesi.

Lakini  Yonesi hakuwa na mpango wa kumshambulia na mara baada ya Chekani kumfikia alimkwepa  kwa kuinama  huku akiweka mikono yake  nyuma kujisapoti  vizuri na kisha palepale alifyatua mguu wake kumlenga Chekani usoni.

Chekani kwa wepesi aliweza kukwepa shambulizi lile  , alijua fika kama litampata usoni basi  litategua  taya lake.

Yonesi mara baada ya kuona amezimisha shambulizi la adui yake palepale hakutaka kuchelewa na aliannzisha shambulizi lingine  la  teke la mzinguko  na kumfanya  Chekani kuweka mikono yake  kifuani kwa ajili ya kupangua teke lile.

Yonesi  hakuonekana mzembe, stamina yake ya kurusha mateke  pamoja na nguvu  ya miguu ilionyesha ni kwa  kiasi gani alikuwa na mazoezi makali  na ujuzi wa kimapigano.

Upande wa Chekani ni kama alikuwa akisoma mashambulizi ya Yonesi kwa kujilinda asipatwe na pigo lingine.

Hamza mara baada ya kuona tukio lile  aliona kabisa  mambo hayo hakutagemea yangetoka kwa  Yonesi, alimuona ameimarika  mno.

Ijapokuwa mbinu ya  Kucha za tai  ilikuwa na nguvu zaidi katika  mbinu ya mapigano ya  ana kwa ana katika ulingo  lakini  bado  Yonesi aliweza kuonyesha wepesi  zaidi, lakini hata hivyo Hamza aliona kabisa  mbinu ya Yonesi katika kupambana na mtaalamu kama Chekani hawezi kumzidi zaidi ya kujichosha, isitoshe  Chekani alionekana kuwa mzoefu zaidi ya Mzee Konki.

Kitendo cha Yonesi kupambana  mara ya kwanza na Mzee Konki ni kama ilimpa nafasi ya kwenda kufanya utafiti ya udhaifu  wa mbinu ya kucha za  Tai ndio maana alitumia nguvu ya miguu zaidi kushambulia maeneo ambayo yataifanya mbinu hio ya kimapigano kukosa nguvu.

Kwa wasiomjua Yonesi wanaweza kumuona ni msichana wa kawaida lakini ni  mwanamke ambae  ameanza jeshi akiwa  na umri mdogo  na alikuwa katika kitengo cha  makomandoo na likija swala la mapigano  alikuwa na uzoefu  pengine zaidi ya Chekani.

Walinzi wa kampuni ya Dosam walijikuta wakifurahi  mara baada ya kuona Chekani alikuwa  akishindwa kumshambulia  Yonesi.

Lakini upande wa Hamza aliona sio muda wa kushangilia  bado  ni ngumu sana  kwa  Chekani kushindwa bila ya kushambulia  kisawa sawa  la sivyo Mzee Konki asingemsafirisha kutoka   Thailland mpaka  Tanzania.

Sasa  upande wa Chekani alionekana  kushindwa kuvumilia  zaidi na alianza kuonyesha uwezo wake  wote.

Ghafla tu alipiga kelele kama vile  ni chui  na  misuli ya mwili wake ilianza kutuna  na akawa mgumu kama chuma.

Miondoko ya miguu yake ilibadilika ghafla na kuanza kucheza kwa kasi mno , licha Hamza kuwa mita kadhaa mbali lakini aliweza kuhisi kuna kitu kimebadilika kuhusu Chekani.

“Inner force!!!”

Yonesi alijikuta akipagwa , mwanzoni alijua ataweza kumdhibiti  Chekani kwa  kumshambulia  kwa haraka haraka lakini hakutegemea  Chekani  amejifunza mbinu  ya ajabu kuamsha nguvu  kutoka ndani  ya mwili.

Yonesi palepale alijikuta akikumbuka mafunzo ya  mkufunzi wake wakati akiwa nchini China chini ya usimamizi wa serikali.

“Wanajeshi wanatofautiana katika  madaraja mengi , mnaweza kuwa na mafunzo sawa na kutii kila maelekezo  mnayopatiwa  lakini haimaanishi kama wewe unaweza kuwa mwanajeshi bora , kwasababu mafunzo haya  haya hata adui yako anaweza kufunzwa na akayamudu kwa asilimia kubwa, kinachomtofautisha mwanajeshi na mwanajeshi licha ya kuwa na uwezo sawa ni namna ambavyo anauwezo wa kuvuna nguvu za asili ambazo zimejificha katika mwili wake ,  mwingine  ataweza kuwa imara  kwa kuweza kuamsha uwezo wake wa  kumuotea adui , mwingine  anaweza  kuamsha uwezo wake wa asili kutokana na  namna ubongo wake unavyofanya kazi kwa haraka , katika mbinu hizi zote  ni wanajeshi wachache sana ambao wamefanikiwa kujifunza  mbinu ya  kuamsha nguvu yao  ya ndani , ukifanikiwa kutumia  viungo vyako vya ndani kama  chanzo cha nguvu zako za mikono na miguu  basi  utahesabika kuwa mwanajeshi  mwenye nguvu  sana katika sanaa ya mapigano, Nguvu ya ndani  ni kama chanzo cha umeme  wakati wa kupigana, mbinu hii inakuwa bora kwasababu  msingi wake ni kuzungusha  nishati ya mwili  katika kila kiungo cha  mwili na kufanya uwezo wako wa kufanya maamuzi kuwa mkubwa sana na spidi yako  ya kivitendo kuongezeka , unaweza kupata majeraha ya nje  ambayo kiuhalisia  huwezi kuendelea kupigana lakini ukafanikiwa kushindana nae”Yonesi  alikuwa akikumbuka  mafunzo hayo  vyema  alikumbuka na  mkufunzi wao aliwapa mfano  wa mtu ambae hana uwezo wowote wa kuruka  ukuta na mara  hatari  ikawa mbele yake na kutokana na njia pekee ya kujiokoa ni kuruka ukuta akafanikiwa kruuka ule ukuta licha  ya kwamba ukimrudisha akiwa katika hali ya kawaida ukimwambia aruke hata ajitahidi vipi  hatoweza kabisa , huo ndio mfano wa nguvu ya ndani iliojificha.

Upande wa Hamza aliona  ni sahihi kabisa  na  ukweli ni kwamba hakushangaa  kumuona  Chekani kuwa na uwezo wa kuamsha nguvu yake  ya ndani  , kama  ndio makamu wa Shirka yote ya Mwewe mweusi  lazima awe na kitu kinachomtofautisha na wenzake wote na ndio mbinu hio  ya ndani.

Kwa lugha nyepesi nguvu ya ndani ni  uwezo ambao  binadamua anakuwa nao  lakini umejificha na uwezo huu hudhihirika mara moja moja  wakati  mtu akiwa katika hatari , sasa  kuna  mafunzo maalumu ambayo hufanyika  ili  kuweza kuuamsha huu uwezo muda wowote unaotaka hata kama haupo kwenye hatari.

“Mwanamke mjinga sana wewe , kwasababu unaonekana kupenda sana kupiga mateke  ninakwenda kukuvunja miguu yako”Aliongea Chekani ambae alimwangalia  Yonesi kama kiumbe cha hatari.

Alikuwa amekasirika mno , aliona ni dharau kwake  kuona  mwanajeshi kama yeye anweza kupigwa mateke na mwanamke mara nyingi kiasi hicho. 

Muda huo   hasira zilikuwa zimemvaa na hakujali  ni  nguvu kiasi gani  atatumia kumshambulia Yonesi  lakini mpango wake ni kumvunja vunja na kidole kimoja tu cha Tai.

Ilikuwa ni kwa uwezo mkubwa Chekani alikuwa ashamfikia   Yonesi  na kutokana na kujua kabisa  Chekani sio saizi yake tena  Yonesi alijikuta akirudi  nyuma na kusababisha mpaka kiatu kumtoka mguuni  lakini  Chekani alimshika bega la mkono wa kulia  kwa spidi kubwa ambayo ilikuwa ngumu kwa Yonesi  kumkwepa, kitu cha pakee alichoweza kufanya  ni  kusogea kidogo ili kuepuka kuguswa maeneo ambayo  yanaweza kumsababishi kifo.

“Arhhhhhhhhhhhh..!!”

Yonesi alijikuta akipiga yowe la maumivu,  eneo la bega  nguo  yake ilichanika palepale  huku   matobo ya  midole ya  Chekani ikionekana 

“Yonesi!!!”

Regina alijikuta akishindwa kujiuzia na kuomba waache kupigana mara moja.

Hamza hata yeye aliona  hana muda wa kupoteza kwani Yonesi anaweza kufanywa kiwete na aliruka na kuingia  kwenye ulingo mara moja, hakujali   swala hilo  litamfanya  Yonesi kujihisi mnyonge au nini.

“Mtu uliemfuata kupigana nae ni mimi”Aliongea Hamza.

“Subiri kwanza!!”

Yonesi aliongea huku akionekana kuvumilia maumivu eneo la bega lake  na alitembea  mpaka mbele  ya Hamza.

“Bado sijashindwa”Aliiongea Yonesi kibabe  huku aking’ata meno kwa nguvu , kitendo cha  ukiburi na  hasira alizokuwa nazo Yonesi  na hali ya kutokata tamaa ilimfanya Hamza kumkubali  kutoka ndani ya moyo wake, aliona ni wanawake wachache sana ambao wanaweza kuwa kama Yonesi.

“Kapteni  nadhani  mwili wako ni muhimu zaidi”Aliongea Hamza , alijua hata kama  Yonesi ana nia ya namna gani ya kupigana na Chekani haiwezi kutosha kushinda.

“Unanidharau  sio?”

“Sijamaanisha hivyo”

“Yonesi  nakuagiza  mara moja acha na uende ukatibiwe”Aliongea Regina  kibabe lakini licha ya hivyo Yonesi bado hakutaka kukubali na aligeuka na kumwangalia Chekani.

“Ukiendelea kushindana na mini  nitahakikisha unabakia uchi kwa kuchana chana nguo zako zote , bado  tu unataka kuendelea?”Aliongea Chekani kwa dharau.

Yonesi alishindwa kusema lolote huku jasho jingi likimtoka  kiasi cha  kudondoka chini, aliishia kukunja ngumi yake kwa nguvu  huku mwili wake ukianza kumtetemeka na kitendo kile kilimfanya Hamza kuhisi nguvu  kubwa ambayo  inamtoka Yonesi , ilikuwa ni kubwa mno kuliko hata ya  Chekani.

Sasa  muda ule Hamza aliona   pengine amemdhania vibaya Yonesi na  kuna uwezo ambao ameuficha alijikuta akishangazwa na kilichotokea. Yonesi alijikuta akitapika damu  na dakika ileile mwili wake ulilegea na  alidongoka chini.

“Yonesi!”

“Kaptenni!”

Kila mtu ambae alikuwa akimjua  Yonesi alijikuta akipiga kelele  za kuogopa maana ilikuwa ni damu nyingi aliotapika.

Hamza dakika ileile alichuchumaa na kushika mkono  wa  Yonesi ili kupima mzunguko wake wa damu.

“Huyu mwanamke ni mkurupukaji sana , angalia sasa   alichojisababishia”Aliwaza Hamza  

"Hahaha.,.. ndio  umeamua kujitapisha damu , kama umekubali kushindwa sema  acha maigizo”Aliongea Chekani lakini Hamza alipotezea kauli yake. “Mkurugenzi nampeleka  Yonesi

hospitalini”Aliongea Hamza  mara baada ya kuona  akichelewa kidogo  tu  Yonesi anaweza kupatwa na shida kubwa.

Regina alitaka kuita gari ya wagonjwa lakini aliona itakuwa rahisi zaidi kama Hamza atamuwahisha   kwa  gari.

Hamza muda uleule alimpakata Yonesi  na kuanza kuondoka na kitendo kile kilimfanya  Chekani kukasirika.

“Wewe mwanaharamu nani kasema unaweza kuondoka , isije ukawa unadharau uwezo  wangu?”

Mzee Konki pia  hakutaka  Hamza kuondoka kabla ya pambano hivyo wale watu aliokuja nao walimzuia kwa mbele.

“Muweke huyo mwanamke chini na uonje  kipigo cha mkuu wetu”Aliongea.

“Unataka kufa?”Aliuliza Hamza akiwa amemgeukia  Chekani.

“Wewe ndio unakimbia halafu  unaniuliza  nataka kufa?”

“Kupigana na wewe  sihitaji hata kutumia  mikono yangu”Aliongea Hamza kwa hasira  

“Unaongea sana ,  kama  unajiamini njoo ujaribu  nikuonjeshe nini maana ya  nguvu ya ndani  yenye muunganiko na kucha za Tai”Aliongea Chekani huku akiwa na hasira zaidi mara baada ya kuona ni kama anadharauliwa na Hamza  na  alitooka alipokuwa amesimama  na kumsogelea Hamza kwa nguvu akidhamiria kumshambulia.

“Hamza kuwa makini”Aliongea Regina mara baada ya kuona kitendo kile  cha  Chekani kutaka kumshambulia Hamza.

Kwasababu Hamza alikuwa amempakata  Yonesi hakuna aliejua  kama ataweza kufanya chochote.  

Kutokana na spidi aliokuwa nayo  Chekani aliweza kumfikia Hamza  na kilichosikika ni  sehemu ya nguo  mgongoni kuchanika  lakini ilikuwa ni  mchanikoo huo  mdogo tu , lwani wakati kila mmoja akijua Hamza anakwenda kuumizwa na shambulizi lile upande wake   Hamza alikuwa amesimama katika eneo moja bila ya kusogea huku akimwangalia  Chekanni kwa macho yaliojaa ukauzu.

Macho ya Hamza yalikuwa ya  hatari kama vile ni  ya  mnyama Chui.

Chekani alijikuta akiwa mjinga mbele ya Hamza ,  shambulizi lake ambalo alimfanyia Hamza aliliunganisha na  nguvu  yake yote ya ndani  lakini ajabu hakumletea  madhara yoyote Hamza  hata kumsukuma tu.

Kwa jinsi Hamza alivyokuwa amesimama ni kama vile hakuwa amemshambulia kabisa.

“Hili limeweekana vipi..”

Muda huo  Hamza aligeuka  na kuinua nguu wake wa kulia   na kumpiga  Chekani teke  kwenye paja lake la mguu wa kushoto kama vile anapiga mpira.

“Crack!!!”

Watu walichoweza kusikia ni  kama mshindo wa  kitu kudondoka , upande wa Chekani hakuwa hata na muda wa kukwepa teke lile na  alichoweza kusikia ni mvunjiko wa ndani kwa ndani wa mfupa wa paja lake.

“Arghhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh!!!, Mguu wanguuuuu!”

Lilikuwa teke la kawaida tu lakini kwa Chekani ni kama  paja ake limepigwa na bomu.

Aliishia kupiga magoti  na  mkuu mmoja huku machozi ya maumivu  yakimtoka  na ilionekana  anaweza kuzimia , ukulele wake ulifanwa watu wote waliokuwa wakiangalia   ikiwemo Regina kushikwa na butwaa. 

Chekani ambae alionekana mbabe dakika chache zilizopita  na kumfanya  Yonesi kutapika damu  alikuwa ameshikishwa ardhi na  kupiga mayowe kwa teke moja tu kutoka kwa Hamza.

Hamza alijifanya ni kama hakuna kilichotokea  na hakurudia hata kumwangalia aligeuka na kisha akiwa amempakata  Yonesi aliondoka, Mzee Konki na wale  watu wake aliokuja nao walimpisha njia huku wakimwangalia kwa maswali  mengi , kama isingekuwa eneo hilo ni  la kazi Hamza   alijiambia angewageuza viwete  kila mmoja.

Mzee Konki  alikuwa katika  majuto , kama angejua hilo litatokea asingemsafirisha  mtoto wa mkuu wake kuja  nchini  Tanzania , hakujua  Shirka yao itaonekana vipi  kwa  mtu ambae ametumia maisha yake kufunzwa kupigana   kushindwa  kwa pigo moja tu , ki ufupi aliona ni fedheha kwa wakufunzi wake.

Regina aliishia  kumwangalia Hamza akiondoka na  Yonesi bila  kuongea neno loloe lakini wakati huo kichwa chake hakikuwa sawa kwa kile alichokuwa akiwaza.

Hamza mara baada ya kumwingiza  Yonesi  kwenye gari alimpeleka moja kwa moja moja katika hospitali binafsi iliokuwa  mita kadhaa kutoka  yalipo makao makuu  ya kampuni yao.

Mara baada ya kumtambulisha  Yonesi kama mfanyakazi wa  Dosam  haraka sana alipokelewa  na kuanza kufanyiwa tiba ya  kiuchunguzi.

Baada ya vipimo kutoka ilionekana  Yonesi hakuwa ameumia sana  na  ni kwamba alikuwa katika hali ya uchomvu sana 

Hamza mara baada ya kupewa majibu hayo moja kwa moja alimpeleka Yonesi mpaka wodini na baada ya hapo alimtaarifu Regina hali ya  Yonesi.

“Vipi Yonesi  anaendeleaje , imeonekana hajaumia?,  kwanini ametapika damu?”Aliuliza Regina akiwa na shauku mara baada ya Hamza kumwambia kuwa hakuwa na shida kubwa , lakini upande wa Regina hakukubali maana aliona  kabisa  Yonesi akitapika damu.

“Yonesi alipata majeraha ya viungo vya ndani  lakini  kwa vifaa vya kawaida haviwezi kuona  hili tatizo , wanachoweza kuona ni  uchomvu tu,  ki ufupi ni kwamba damu aliotema ilivuja kidogo tu na kuacha na ndio aliitapika  yote”

“Kwahio unamaanisha ni kitu cha kweli  hicho kinachoitwa inner force?”Aliuliza Regina na

kumfanya Hamza kufikiria   huku akijiambia kitendo cha Yonesi kutema damu sio kutokana na shambulio la Chekani bali alijisababishia mwenyewe, lakini  Hamza hakutaka kuongea sana hivyo alilipotezea swali la Regina , isitoshe  hata yeye alikuwa na maswali kwa Yonesi imekuwaje  akajitapisha damu.

“Kwanza   nini kinaendelea huko  kwenye kampuni?”Aliuliza Hamza.

“Umemvunja yule mbaba wa watu mguu unadhani wangeendelea kukaa?, halafu familia  ya James imepiga simu  na kusema kwamba hawahusiki na  Mzee Konk tena na alichokifanya ni kisasi chake mwenyewe”Aliongea Regina.

“Wamekupigia simu na kuongea hivyo?”

“Ndio  walivyosema  hawahusiki  na  ni maamuzi ya

Mzee Konki pekee”Aliongea Regina na kumfanya Hamza kuhisi kuna kitu hakipo sawa lakini hata hivyo hakutaka kuuliza zaidi.

“Hebbu tuachane na hayo  kwasasa , kwasababu wamekupigia  na kusema hawahusiki  nadhani hawatoleta  matatizo ndani ya kampuni tena”

“Sawa , huna haja ya kuja kazini  unaweza kuendelea kukaa  hospitalini mpaka hali ya Yonesi ikiwa sawa”Aliongea Regina  na Hamza alikubali. ******

Upande mwingine  alionekana James akiwa nyumbani kwao sebuleni  mbele yake kulikuwa na mwanaume alievalia suruali ya Jeans  na tishirt iliombana mikono , alikuwa na miwani ya juu alioitundika kwenye kifua chake huku mkononi akiwa ameshikilia sigara.

“Nadhani kwa staili hii itakuwa ni rahisi kudili  na Regina , ataona kabisa kumwambia hatuhusiki na  swala la Mzee Konki lazima ataanza kuishi bila tahadhari  na ndio itakuwa  rahisi kumuua”Aliongea yule bwana huku akitoa moshi.

“Unadhani ni sawa kumuua sasa hivi , nazungumzia ushirikiano  wa baba yako zidi ya  mgombea wa  uraisi?”Aliuliza yule bwana.

“Kuhusu hili  baba pia  alinipa  msisitizo , lakini  tusipomuua sasa hivi na Hamza  wake tutajikuta tunachelewa”

“Ninachomaanisha kumuua kwa staili ya wazi wazi kama hivi , kwa mfano leo imeonekana  Mzee Konki akiingia ndani ya kampuni ya Dosam na kuleta vurugu  kama ikitokea  Regina akikumbwa na kitu kikubwa zaidi basi moja kwa moja tukio hili litaunganishwa na  familia yenu , isitoshe ndio wanufaika  wakubwa”Aliongea  Yule bwana.

“Kwahio Gonji unamaanisha kipi kifanyike?,”

“Kuna  njia nyingi za kumuua mtu bila ya  kifo chake kuonekana cha kupangwa”Aliiongea na kumfanya James macho kuchanua.

“Unadhani inaweza kuwa  rahisi , MzeeKonki na kundi lake wameenda kumshambulia Hamza lakini wameambulia maumivu , hawa vijana wako ambao  unawasifia unadhani wanaweza kuwa na uwezo wa juu kumzidi Hamza?”

“Kama nilivyosema kuna njia nyingi za kumuua mtu lakini njia hizo sio lazima ziwe kupigana ana kwa ana , kama  huwezi kumuua mtu kwa kushindana nae ulingoni basi unatumia mtego, mfano  kusababisha

ajali , kutega bomu katika gari yake na kadhalika”Aliongea Gonji  na kumfanya James sasa kuelewa.

“Hapo kwenye ajali nakubaliana na wewe lakini vipi kuhusu bomu   , sio rahisi kupata bomu”

“Hilo lisikupe shida , kwasasa vigogo wengi  wanahitaji kuona Hamza akifariki kutokana na kuzuia mipango yao, ni rahisi kushawishi  makomandoo kutupa  siraha yoyote ile”

“Kama hili unadhani linawezekana basi naliacha katika mikono yako , lakini nikukumbushe linapaswa kufanyika kwa haraka maana  hatuna muda wa kupoteza”Aliongea James na kumfanya Gonji  kutoa tabasamu.

“Ili mradi malipo ni ya kueleweka nitahakikisha  wiki mbili hazipiti unaipata taarinfa  nzuri”Aliongea kwa kujiamini huku akizima ile sigara kwa kuiminya katika  kisahani cha majivu.

********

Yonesi alijikuta akifumbua macho yake taratibu  na kitu cha kwanza alichoweza kuhisia ni radha ya damu iliokuwa kwenye midomo yake.

Baada ya akili kumkaa sawa ndio sasa aliweza kujua alikuwa  hospitalini katika wodi  na hio  ni mara baada ya kupatwa na harufu ya  dawa za  kuzuia  maambukizi ya  vinyemelea.

“Fyaaaa…Fyaaa…sio mbaya , sio mbaya hii juisi ni tamu”

Ilikuwa ni sauti ya mwanaume iliomfanya kugeuza  shingo yake na aliweza kumuona Hamza  akifyonza juisi kwa kutumia  mrija na kufanya  chupa ile itoe sauti  kwa ndani ikionyesha imeishiwa na juisi na anavuta hewa.

Hamza alikuwa amemaliza chakula chote ambacho  kililetwa kwa ajili ya mgonjwa na   muda huo alikuwa akimalizia juisi.

Upande wa Yonesi  ilikuwa mara ya kwanza kuona mtu akifurahia chakula namna hio mpaka kujilamba midomo akiwa katika mazingira ya hospitalini.

“Ah! Kapteni  umeamka  sasa?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona Yonesi anamwangalia.

“Kwanini upo hapa?”

“Mkurugenzi kaniambia nibaki na wewe , kazi yangu leo ni  kukaa na wewe na kukuhudumia  kwa kila unachotaka”

“Mkurugenzi… nini kiliendelea  kwenye kampuni?”

“Yashaisha  yale  , wale watu wote wamekwisha ondoka”Aliongea Hamza na kumfanya  Yonesi kuvuta pumzi ya ahueni.,

“Vipi ulifanikiwa kumshinda yule Kechani?”Aliuliza na kumfanya Hamza kutingisha kichwa huku  akicheka.

“Unacheka nini sasa , kama unasema sema tu, usinidharau ukidhani mimi dhaifu kiasi hicho”

“Lakini sijasema nakudharau”

“Lazima  utakuwa unajiambia kwenye moyo wako   nina kiburi na sijui  kukubali kushindwa  na najikweza sana hata kwa watu ambao sina uwezo wa kupambana nao  na mwisho wa siku nikaishia kujiumiza mwenyewe”Aiongea  Yonesi kwa sauti ya kulalamika na kumshangaza kiasi Hamza.

“Kapteni nikupe maji kidogo?”

“Sitaki maji , unaweza kwenda huna haja ya kunisaidia”Aliongea Yonesi huku akijitahidi kusimama lakini alijikuta akigugumia maumivu makali ya tumbo.

“Majeraha uliopata kwa ndani hayajapona bado , hivyo kuwa makini usijilazimishe  la sivyo utajiumiza zaidi”

“Sihitaji ushauri wako”Aliongea Yonesi huku akionyesha  hasira waziwazi.

“Sikia Yonesi sio kwamba  nakudharau , unaweza kuniamini au  usiniamini hio  ni juu yako lakini ukweli  sijawahi kudharau uwezo wako”

“Huna  haja ya kunifariji kwa kujitia upole”

“Ninachomaanisha sio kwamba huna uwezo wa kupigana na  yyule Kechani , kama umeweza hadi kufanya utafiti  wa namna ya kudili na mbinu za  Kucha za tai  basi unaonyesha ni kwa kiasi  gani una juhudi ya kujifunza  na kuhusu hili nimekukubali na  kama ni ushindi pale ulishinda , kosa lako ni kwamba hukujua mwenzako ana  mafunzo ya kuamsha  nguvu za ndani  hivyo ni halali kukuzidi”Aliongea Hamza na maneno yale kidogo yalionesha kumlainisha Yonesi.

“Ndio uivyoona  pia?”

“Kapteni kwanini nikudanganye , umeonyesha ni kiasi gani una  nia ya  kutimiza wajibu wako , nadhani kupitia hili Mkurugenzi anapaswa kukuongeea mshahara”Aliongea na kumfanya Yonesi  bado kutoyaamini maneno ya Hamza.

“Unaongea maneno ya kijinga ili kunifariji tu ila ndani kwa ndani utakuwa unachekelea”Aliongea lakini Hamza alipotezea alijua asingeweza kushinda mbele ya ukiburi wa Yonesi.

“Vipi  una njaa?, Dokta amesema unapaswa kula vyakula vya ujiuji  kwa siku tatu , ngoja nikuagizie uji”

“Sina nja… “Kabla hata hajamaliza sentensi yake tumbo  lake lilianza kunguruma kama jenereta.

Muda ulikuwa umeenda tokea aletwe hapo  na pia alitoka kwenye pambano kali hivyo ilikuwa ni halali kushikwa na  njaa.

Hamza   aliishia kutoa tabasamu na alipiga simu  uji uletwe mpaka kwenye wodi yao ,  Hospitali hio ilikuwa ni binafsi  na  ilikuwa   na huduma ya  mgonjwa kuagiza chakula kabisa na kuletewa kutoka jikoni.

Dakika chache mbele  uji uliletwa  na  Hamza aliumimina kwenye bakuli na kuchukua kijiko kwa ajili ya kumlisha Yonesi , lakini alikataa.

“Nina mikono nitakunywa mwenyewe”Aliongea na Hamza hakutaka kulazimisha na kumpatia Yonesi lile bakuli.

Muda huo  Yonesi  aliweza kugundua sasa   mavazi yake yote  mwililini yalikuwa yamebadilishwa  na amevaa  mavazi maalumu ya hospitalini.

“Nguo zangu ziko wapi?”.

*******

Saa nane za mchana alionekana  Frida akiingia ndani  ya majengo ya taasisi  ya Haliz, mwendo wake siku hio ulionekana kuwa ni ule wa kujiamini zaidi kuliko siku nyingine zote.

Baadhi ya wafanyakazi  aliopishana nao baadhi yao walimkaribisha kazini kwa mara nyingine huku wengine wakimpa ishara  ya salamu tu ambapo  Frida alizipokea kwa kutabasamu.

Mara baada ya kuzikaribia Lift alibonyeza kitufe  na  dakika chache Lift ilifunguka  na akaingia ndani na alibonyeza kitufe cha  floor ya 24   juu kabisa ya jengo hilo.

Na ilimchukua dakika  tu   lift ilimfikisha  katika floor ya uongozi wa taasisi hio  na alitembea kwa kujiamini katika Koridio hio    huku akipokewa na marashi mazuri yaliotokana na  AC.

“Naima nipo hapa kwa ajili ya kuonana na Mkurugenzi”Aliongea Frida mara baada ya kufika katika dawati la  mapokezi na kukutana na mwanadada alievalia  sare  za rangi ya  bluu iliokolea pamoja na  Hijab   huku akiwa na tabasamu.

“Karibu sana Dokta , Mkurugenzi anakusubiri”Aliongea yule mwanadada  kwa tabasamu  kwa kingereza na  Frida alimrudishia tabasamu  la ukarimu na  kupiga hatua kuingia katika ofisi ya Mkurugenzi.

Frida hakusumbuka hata kugonga kutokana na kuona taarifa za ujio wake zishamfikia bosi wake , hivyo aligonga kidogo na kisha akasukuma mlango na kuingia ndani.

“Karibu  tena  kazini  Dokta Frida”

Sauti ya mwanamama iliweza kusikika na kumfanya  Frida kutoa  tabasamu  huku akimwangalia mwanamke ambae amevalia Hijab.

Alikuwa ni Dokta Maya  Thema na ndio mkurugenzi mkuu wa taasisi ya maswala ya  fahamu ya  Haliz Foundation.

“Asante sana Dokta Maya”Alijibu  Frida na  Sister   yule alitoka katika  meza yake ya kufanyia kazi na kuja kuketi katika   masofa.

Ilikuwa ni ofisi  kubwa mno , ilikuwa  na kila sifa ya kuitwa Ofisi ya Mkurugenzi mkuu wa  taasisi hio kubwa , licha ya kwamba vitu vingi vilionekana kawaida lakini kwa  macho ya  tathimini lazima ujue samani  na mapambo ni ya bei ghali , ki ufupi kila kitu kiliendana na hadhi  ya mtu wa dini. “Inaonekana taarifa za kurudi kwangu zimefika mapema kuliko nilivyotarajia”Aliongea Frida akiwa na tabasamu.

“Ndio, Frida wewe ni mwanasayansi mkubwa  sana ndani ya taasis ya  Haliz na viongozi wanajua hilo , licha ya kwamba nimekutangulia ki uzoefu lakini umenizidi vitu vingi, Askofu alinipigia simu juu ya  kurudi  kwako tena , Karibu sana”

“Unaonekana kuwa na furaha sana juu ya ujio wangu  pia Professor , licha ya kujua kilichotokea”Aliongea  na kumfanya Sister kutabasamu na alisimama kutoka kwenye sofa na kumimina maji kwenye glasi kutoka kwenye  Dispenser 

“Utapendelea  maji?”Aliuliza.

“Asante sister , ila sina kitu”Aliongea  na kumfanya  Sister  Maya kutingisha kichwa na  kurudi  kwenye sofa  na kukaa.

“ Faiths!,  to me all faiths  are admonitions  that there is something we cannot understand , something  to which  we are accountable. It doesn’t matter what we believe personally , as long as there is sometting that we cannot understand about someone’s faith , then we have no reason to judge”Aliongea Sister akimaanisha kwamba  hatuna uwezo wa kumhukumu mtu kutokana na dini yake kwasababu katika hio imani mtu anayokuwa nayo lazima kuna kitu ambacho  mtu mwingine huwezi kuelewa.

Kauli ile ilimfanya  Frida kutoa tabasamu  hafifu  akionekana kukubaliana na Profesa wake.

“Frida  unajua  sababu kubwa  ya kuanzishwa kwa  kanisa la Wasinagogi?”Aliuliza na kumfanya Nadia kutingisha kichwa kwamba haelewi.

“Mwasisi wa  kanisa la Sinagogu  alikuwa ni muumini mkubwa  kutoka  kanisa  kuu  mpaka siku ambayo Dokta  Genesha alitoka hadharani  na kusema kwamba  ana uwezo wa kuthibitisha  uwepo wa nguvu ya kiroho kwa kutumia  sayansi, mpaka leo hatukujua ni ushahidi gani ambayo Dokta Genesha  alimuonyesha mwasisi wetu  lakini ni kitu ambacho kilimbadilisha mawazo  mno na kugeuka mara moja kutoka Kanisa kuu na kuanza kufikiria kama mtu ambae hajawahi kusoma biblia”

“Kama wanasinagogu hawakuona ushahidi ambao

Dokta Genesha aliongelea na mwasisi hakuwaambia   kwanini alipata  wafuasi , lazima kuna sababu ambayo iliwashawishi  wengine  kumfuata na kuja kuwa jumuia tishio na yenye ushawishi mkubwa duniani?”

Previoua Next