SEHEMU YA 50
Kitendo cha Chekani kuletewa Yonesi kupigana nae aliona ni kama dharau.
“Kwahio mnadhani nimejifunza sanaa ya mapigano kwajili ya kushindana na kila mtu hata kama hana vigezo?”
“Acha visingizio , tutaongea hili baada ya kuweza kunishinda”Aliongea Yonesi akiwa ameshakaa pozi la kupigana.
Kechani aliishia kutingisha kichwa na kuingia ndani ya ulingo huku akipiga hatua moja kumsogelea Yonesi , wakati huo kidole chake gumba kilinyooka na kisha kikajikunja huku vile vinne , viwili vilitokezea kwa mbele huku viwili vikisambaa na kufanya mkono wale uonekane kama vile ni mguu wa Mwewe.
Baada ya kuona mbwebewe za adui yake, Yonesi hakutaka kuchelewa na alianzisha mashambulizi kwa kumrushia ngumi Chekani akimlenga kifuani, lakini mara bada ya kurusha ngumi ile Chekani alisogeza mkono wake wa kushoto uliokuwa katika umbo la kucha za tai akinuia kuikamata ile ngumi , lakini upande wa Yonesi aliinama kwa mbele na kisha kunyanyua mguu kwa mzunguko , alionekana kumzubaisha adui yake kwa kumuonyesha anataka kumpiga ngumi lakini shambulio halisi alikuwa amepanga litokee katika mguu wake.
“Bamm!!
Chekani alijikuta akishituka na alijitahidi kwa uwezo wake wote kuzia shambulizi lile.
Upande wa Yonesi mara baada ya kufyatua mguu na kwenda hewani alipiga sarakasi na kwenda kusimama tena lakini hakuzubaa alirudi na teke staili ya roundhouse ambayo ilimpiga Chekani mgongoni na kumfanya kujikota kwenda mbele.
Tukio lile la Yonesi kufanikiwa kumpiga Chekani lilimfanya Mzee Konki na wenzake kushangazwa mno , maana ni kitu ambacho hawakuwa wametegemea kabisa.
Chekani alijikuta akigusa eneo alilopokea shambulizi na uso wake ulizidi kujaa usiriasi , ni kama ile dharau aliokuwa nayo juu ya Yonesi ilipotea.
“Mbona unashangaa , unadhani kujua kwako sanaa za kimapiugano zilizopitwa na wakati unaweza kunipiga kirahisi?”AliongeaYonesi.
“Safiii,,, nimekudharau ndio maana , hebu angalia hii kwanza”Aliongea Chekani kwa kingereza na palepale alisogea kwa haraka kwa staili flani kama vile ni Sungura anaekimbia na kisha kumrukia Yonesi huku kucha zake zilikuwa zimeleekezewa upande wa kiganja cha mkono cha Yonesi.
Lakini Yonesi hakuwa na mpango wa kumshambulia na mara baada ya Chekani kumfikia alimkwepa kwa kuinama huku akiweka mikono yake nyuma kujisapoti vizuri na kisha palepale alifyatua mguu wake kumlenga Chekani usoni.
Chekani kwa wepesi aliweza kukwepa shambulizi lile , alijua fika kama litampata usoni basi litategua taya lake.
Yonesi mara baada ya kuona amezimisha shambulizi la adui yake palepale hakutaka kuchelewa na aliannzisha shambulizi lingine la teke la mzinguko na kumfanya Chekani kuweka mikono yake kifuani kwa ajili ya kupangua teke lile.
Yonesi hakuonekana mzembe, stamina yake ya kurusha mateke pamoja na nguvu ya miguu ilionyesha ni kwa kiasi gani alikuwa na mazoezi makali na ujuzi wa kimapigano.
Upande wa Chekani ni kama alikuwa akisoma mashambulizi ya Yonesi kwa kujilinda asipatwe na pigo lingine.
Hamza mara baada ya kuona tukio lile aliona kabisa mambo hayo hakutagemea yangetoka kwa Yonesi, alimuona ameimarika mno.
Ijapokuwa mbinu ya Kucha za tai ilikuwa na nguvu zaidi katika mbinu ya mapigano ya ana kwa ana katika ulingo lakini bado Yonesi aliweza kuonyesha wepesi zaidi, lakini hata hivyo Hamza aliona kabisa mbinu ya Yonesi katika kupambana na mtaalamu kama Chekani hawezi kumzidi zaidi ya kujichosha, isitoshe Chekani alionekana kuwa mzoefu zaidi ya Mzee Konki.
Kitendo cha Yonesi kupambana mara ya kwanza na Mzee Konki ni kama ilimpa nafasi ya kwenda kufanya utafiti ya udhaifu wa mbinu ya kucha za Tai ndio maana alitumia nguvu ya miguu zaidi kushambulia maeneo ambayo yataifanya mbinu hio ya kimapigano kukosa nguvu.
Kwa wasiomjua Yonesi wanaweza kumuona ni msichana wa kawaida lakini ni mwanamke ambae ameanza jeshi akiwa na umri mdogo na alikuwa katika kitengo cha makomandoo na likija swala la mapigano alikuwa na uzoefu pengine zaidi ya Chekani.
Walinzi wa kampuni ya Dosam walijikuta wakifurahi mara baada ya kuona Chekani alikuwa akishindwa kumshambulia Yonesi.
Lakini upande wa Hamza aliona sio muda wa kushangilia bado ni ngumu sana kwa Chekani kushindwa bila ya kushambulia kisawa sawa la sivyo Mzee Konki asingemsafirisha kutoka Thailland mpaka Tanzania.
Sasa upande wa Chekani alionekana kushindwa kuvumilia zaidi na alianza kuonyesha uwezo wake wote.
Ghafla tu alipiga kelele kama vile ni chui na misuli ya mwili wake ilianza kutuna na akawa mgumu kama chuma.
Miondoko ya miguu yake ilibadilika ghafla na kuanza kucheza kwa kasi mno , licha Hamza kuwa mita kadhaa mbali lakini aliweza kuhisi kuna kitu kimebadilika kuhusu Chekani.
“Inner force!!!”
Yonesi alijikuta akipagwa , mwanzoni alijua ataweza kumdhibiti Chekani kwa kumshambulia kwa haraka haraka lakini hakutegemea Chekani amejifunza mbinu ya ajabu kuamsha nguvu kutoka ndani ya mwili.
Yonesi palepale alijikuta akikumbuka mafunzo ya mkufunzi wake wakati akiwa nchini China chini ya usimamizi wa serikali.
“Wanajeshi wanatofautiana katika madaraja mengi , mnaweza kuwa na mafunzo sawa na kutii kila maelekezo mnayopatiwa lakini haimaanishi kama wewe unaweza kuwa mwanajeshi bora , kwasababu mafunzo haya haya hata adui yako anaweza kufunzwa na akayamudu kwa asilimia kubwa, kinachomtofautisha mwanajeshi na mwanajeshi licha ya kuwa na uwezo sawa ni namna ambavyo anauwezo wa kuvuna nguvu za asili ambazo zimejificha katika mwili wake , mwingine ataweza kuwa imara kwa kuweza kuamsha uwezo wake wa kumuotea adui , mwingine anaweza kuamsha uwezo wake wa asili kutokana na namna ubongo wake unavyofanya kazi kwa haraka , katika mbinu hizi zote ni wanajeshi wachache sana ambao wamefanikiwa kujifunza mbinu ya kuamsha nguvu yao ya ndani , ukifanikiwa kutumia viungo vyako vya ndani kama chanzo cha nguvu zako za mikono na miguu basi utahesabika kuwa mwanajeshi mwenye nguvu sana katika sanaa ya mapigano, Nguvu ya ndani ni kama chanzo cha umeme wakati wa kupigana, mbinu hii inakuwa bora kwasababu msingi wake ni kuzungusha nishati ya mwili katika kila kiungo cha mwili na kufanya uwezo wako wa kufanya maamuzi kuwa mkubwa sana na spidi yako ya kivitendo kuongezeka , unaweza kupata majeraha ya nje ambayo kiuhalisia huwezi kuendelea kupigana lakini ukafanikiwa kushindana nae”Yonesi alikuwa akikumbuka mafunzo hayo vyema alikumbuka na mkufunzi wao aliwapa mfano wa mtu ambae hana uwezo wowote wa kuruka ukuta na mara hatari ikawa mbele yake na kutokana na njia pekee ya kujiokoa ni kuruka ukuta akafanikiwa kruuka ule ukuta licha ya kwamba ukimrudisha akiwa katika hali ya kawaida ukimwambia aruke hata ajitahidi vipi hatoweza kabisa , huo ndio mfano wa nguvu ya ndani iliojificha.
Upande wa Hamza aliona ni sahihi kabisa na ukweli ni kwamba hakushangaa kumuona Chekani kuwa na uwezo wa kuamsha nguvu yake ya ndani , kama ndio makamu wa Shirka yote ya Mwewe mweusi lazima awe na kitu kinachomtofautisha na wenzake wote na ndio mbinu hio ya ndani.
Kwa lugha nyepesi nguvu ya ndani ni uwezo ambao binadamua anakuwa nao lakini umejificha na uwezo huu hudhihirika mara moja moja wakati mtu akiwa katika hatari , sasa kuna mafunzo maalumu ambayo hufanyika ili kuweza kuuamsha huu uwezo muda wowote unaotaka hata kama haupo kwenye hatari.
“Mwanamke mjinga sana wewe , kwasababu unaonekana kupenda sana kupiga mateke ninakwenda kukuvunja miguu yako”Aliongea Chekani ambae alimwangalia Yonesi kama kiumbe cha hatari.
Alikuwa amekasirika mno , aliona ni dharau kwake kuona mwanajeshi kama yeye anweza kupigwa mateke na mwanamke mara nyingi kiasi hicho.
Muda huo hasira zilikuwa zimemvaa na hakujali ni nguvu kiasi gani atatumia kumshambulia Yonesi lakini mpango wake ni kumvunja vunja na kidole kimoja tu cha Tai.
Ilikuwa ni kwa uwezo mkubwa Chekani alikuwa ashamfikia Yonesi na kutokana na kujua kabisa Chekani sio saizi yake tena Yonesi alijikuta akirudi nyuma na kusababisha mpaka kiatu kumtoka mguuni lakini Chekani alimshika bega la mkono wa kulia kwa spidi kubwa ambayo ilikuwa ngumu kwa Yonesi kumkwepa, kitu cha pakee alichoweza kufanya ni kusogea kidogo ili kuepuka kuguswa maeneo ambayo yanaweza kumsababishi kifo.
“Arhhhhhhhhhhhh..!!”
Yonesi alijikuta akipiga yowe la maumivu, eneo la bega nguo yake ilichanika palepale huku matobo ya midole ya Chekani ikionekana
“Yonesi!!!”
Regina alijikuta akishindwa kujiuzia na kuomba waache kupigana mara moja.
Hamza hata yeye aliona hana muda wa kupoteza kwani Yonesi anaweza kufanywa kiwete na aliruka na kuingia kwenye ulingo mara moja, hakujali swala hilo litamfanya Yonesi kujihisi mnyonge au nini.
“Mtu uliemfuata kupigana nae ni mimi”Aliongea Hamza.
“Subiri kwanza!!”
Yonesi aliongea huku akionekana kuvumilia maumivu eneo la bega lake na alitembea mpaka mbele ya Hamza.
“Bado sijashindwa”Aliiongea Yonesi kibabe huku aking’ata meno kwa nguvu , kitendo cha ukiburi na hasira alizokuwa nazo Yonesi na hali ya kutokata tamaa ilimfanya Hamza kumkubali kutoka ndani ya moyo wake, aliona ni wanawake wachache sana ambao wanaweza kuwa kama Yonesi.
“Kapteni nadhani mwili wako ni muhimu zaidi”Aliongea Hamza , alijua hata kama Yonesi ana nia ya namna gani ya kupigana na Chekani haiwezi kutosha kushinda.
“Unanidharau sio?”
“Sijamaanisha hivyo”
“Yonesi nakuagiza mara moja acha na uende ukatibiwe”Aliongea Regina kibabe lakini licha ya hivyo Yonesi bado hakutaka kukubali na aligeuka na kumwangalia Chekani.
“Ukiendelea kushindana na mini nitahakikisha unabakia uchi kwa kuchana chana nguo zako zote , bado tu unataka kuendelea?”Aliongea Chekani kwa dharau.
Yonesi alishindwa kusema lolote huku jasho jingi likimtoka kiasi cha kudondoka chini, aliishia kukunja ngumi yake kwa nguvu huku mwili wake ukianza kumtetemeka na kitendo kile kilimfanya Hamza kuhisi nguvu kubwa ambayo inamtoka Yonesi , ilikuwa ni kubwa mno kuliko hata ya Chekani.
Sasa muda ule Hamza aliona pengine amemdhania vibaya Yonesi na kuna uwezo ambao ameuficha alijikuta akishangazwa na kilichotokea. Yonesi alijikuta akitapika damu na dakika ileile mwili wake ulilegea na alidongoka chini.
“Yonesi!”
“Kaptenni!”
Kila mtu ambae alikuwa akimjua Yonesi alijikuta akipiga kelele za kuogopa maana ilikuwa ni damu nyingi aliotapika.
Hamza dakika ileile alichuchumaa na kushika mkono wa Yonesi ili kupima mzunguko wake wa damu.
“Huyu mwanamke ni mkurupukaji sana , angalia sasa alichojisababishia”Aliwaza Hamza
"Hahaha.,.. ndio umeamua kujitapisha damu , kama umekubali kushindwa sema acha maigizo”Aliongea Chekani lakini Hamza alipotezea kauli yake. “Mkurugenzi nampeleka Yonesi
hospitalini”Aliongea Hamza mara baada ya kuona akichelewa kidogo tu Yonesi anaweza kupatwa na shida kubwa.
Regina alitaka kuita gari ya wagonjwa lakini aliona itakuwa rahisi zaidi kama Hamza atamuwahisha kwa gari.
Hamza muda uleule alimpakata Yonesi na kuanza kuondoka na kitendo kile kilimfanya Chekani kukasirika.
“Wewe mwanaharamu nani kasema unaweza kuondoka , isije ukawa unadharau uwezo wangu?”
Mzee Konki pia hakutaka Hamza kuondoka kabla ya pambano hivyo wale watu aliokuja nao walimzuia kwa mbele.
“Muweke huyo mwanamke chini na uonje kipigo cha mkuu wetu”Aliongea.
“Unataka kufa?”Aliuliza Hamza akiwa amemgeukia Chekani.
“Wewe ndio unakimbia halafu unaniuliza nataka kufa?”
“Kupigana na wewe sihitaji hata kutumia mikono yangu”Aliongea Hamza kwa hasira
“Unaongea sana , kama unajiamini njoo ujaribu nikuonjeshe nini maana ya nguvu ya ndani yenye muunganiko na kucha za Tai”Aliongea Chekani huku akiwa na hasira zaidi mara baada ya kuona ni kama anadharauliwa na Hamza na alitooka alipokuwa amesimama na kumsogelea Hamza kwa nguvu akidhamiria kumshambulia.
“Hamza kuwa makini”Aliongea Regina mara baada ya kuona kitendo kile cha Chekani kutaka kumshambulia Hamza.
Kwasababu Hamza alikuwa amempakata Yonesi hakuna aliejua kama ataweza kufanya chochote.
Kutokana na spidi aliokuwa nayo Chekani aliweza kumfikia Hamza na kilichosikika ni sehemu ya nguo mgongoni kuchanika lakini ilikuwa ni mchanikoo huo mdogo tu , lwani wakati kila mmoja akijua Hamza anakwenda kuumizwa na shambulizi lile upande wake Hamza alikuwa amesimama katika eneo moja bila ya kusogea huku akimwangalia Chekanni kwa macho yaliojaa ukauzu.
Macho ya Hamza yalikuwa ya hatari kama vile ni ya mnyama Chui.
Chekani alijikuta akiwa mjinga mbele ya Hamza , shambulizi lake ambalo alimfanyia Hamza aliliunganisha na nguvu yake yote ya ndani lakini ajabu hakumletea madhara yoyote Hamza hata kumsukuma tu.
Kwa jinsi Hamza alivyokuwa amesimama ni kama vile hakuwa amemshambulia kabisa.
“Hili limeweekana vipi..”
Muda huo Hamza aligeuka na kuinua nguu wake wa kulia na kumpiga Chekani teke kwenye paja lake la mguu wa kushoto kama vile anapiga mpira.
“Crack!!!”
Watu walichoweza kusikia ni kama mshindo wa kitu kudondoka , upande wa Chekani hakuwa hata na muda wa kukwepa teke lile na alichoweza kusikia ni mvunjiko wa ndani kwa ndani wa mfupa wa paja lake.
“Arghhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh!!!, Mguu wanguuuuu!”
Lilikuwa teke la kawaida tu lakini kwa Chekani ni kama paja ake limepigwa na bomu.
Aliishia kupiga magoti na mkuu mmoja huku machozi ya maumivu yakimtoka na ilionekana anaweza kuzimia , ukulele wake ulifanwa watu wote waliokuwa wakiangalia ikiwemo Regina kushikwa na butwaa.
Chekani ambae alionekana mbabe dakika chache zilizopita na kumfanya Yonesi kutapika damu alikuwa ameshikishwa ardhi na kupiga mayowe kwa teke moja tu kutoka kwa Hamza.
Hamza alijifanya ni kama hakuna kilichotokea na hakurudia hata kumwangalia aligeuka na kisha akiwa amempakata Yonesi aliondoka, Mzee Konki na wale watu wake aliokuja nao walimpisha njia huku wakimwangalia kwa maswali mengi , kama isingekuwa eneo hilo ni la kazi Hamza alijiambia angewageuza viwete kila mmoja.
Mzee Konki alikuwa katika majuto , kama angejua hilo litatokea asingemsafirisha mtoto wa mkuu wake kuja nchini Tanzania , hakujua Shirka yao itaonekana vipi kwa mtu ambae ametumia maisha yake kufunzwa kupigana kushindwa kwa pigo moja tu , ki ufupi aliona ni fedheha kwa wakufunzi wake.
Regina aliishia kumwangalia Hamza akiondoka na Yonesi bila kuongea neno loloe lakini wakati huo kichwa chake hakikuwa sawa kwa kile alichokuwa akiwaza.
Hamza mara baada ya kumwingiza Yonesi kwenye gari alimpeleka moja kwa moja moja katika hospitali binafsi iliokuwa mita kadhaa kutoka yalipo makao makuu ya kampuni yao.
Mara baada ya kumtambulisha Yonesi kama mfanyakazi wa Dosam haraka sana alipokelewa na kuanza kufanyiwa tiba ya kiuchunguzi.
Baada ya vipimo kutoka ilionekana Yonesi hakuwa ameumia sana na ni kwamba alikuwa katika hali ya uchomvu sana
Hamza mara baada ya kupewa majibu hayo moja kwa moja alimpeleka Yonesi mpaka wodini na baada ya hapo alimtaarifu Regina hali ya Yonesi.
“Vipi Yonesi anaendeleaje , imeonekana hajaumia?, kwanini ametapika damu?”Aliuliza Regina akiwa na shauku mara baada ya Hamza kumwambia kuwa hakuwa na shida kubwa , lakini upande wa Regina hakukubali maana aliona kabisa Yonesi akitapika damu.
“Yonesi alipata majeraha ya viungo vya ndani lakini kwa vifaa vya kawaida haviwezi kuona hili tatizo , wanachoweza kuona ni uchomvu tu, ki ufupi ni kwamba damu aliotema ilivuja kidogo tu na kuacha na ndio aliitapika yote”
“Kwahio unamaanisha ni kitu cha kweli hicho kinachoitwa inner force?”Aliuliza Regina na
kumfanya Hamza kufikiria huku akijiambia kitendo cha Yonesi kutema damu sio kutokana na shambulio la Chekani bali alijisababishia mwenyewe, lakini Hamza hakutaka kuongea sana hivyo alilipotezea swali la Regina , isitoshe hata yeye alikuwa na maswali kwa Yonesi imekuwaje akajitapisha damu.
“Kwanza nini kinaendelea huko kwenye kampuni?”Aliuliza Hamza.
“Umemvunja yule mbaba wa watu mguu unadhani wangeendelea kukaa?, halafu familia ya James imepiga simu na kusema kwamba hawahusiki na Mzee Konk tena na alichokifanya ni kisasi chake mwenyewe”Aliongea Regina.
“Wamekupigia simu na kuongea hivyo?”
“Ndio walivyosema hawahusiki na ni maamuzi ya
Mzee Konki pekee”Aliongea Regina na kumfanya Hamza kuhisi kuna kitu hakipo sawa lakini hata hivyo hakutaka kuuliza zaidi.
“Hebbu tuachane na hayo kwasasa , kwasababu wamekupigia na kusema hawahusiki nadhani hawatoleta matatizo ndani ya kampuni tena”
“Sawa , huna haja ya kuja kazini unaweza kuendelea kukaa hospitalini mpaka hali ya Yonesi ikiwa sawa”Aliongea Regina na Hamza alikubali. ******
Upande mwingine alionekana James akiwa nyumbani kwao sebuleni mbele yake kulikuwa na mwanaume alievalia suruali ya Jeans na tishirt iliombana mikono , alikuwa na miwani ya juu alioitundika kwenye kifua chake huku mkononi akiwa ameshikilia sigara.
“Nadhani kwa staili hii itakuwa ni rahisi kudili na Regina , ataona kabisa kumwambia hatuhusiki na swala la Mzee Konki lazima ataanza kuishi bila tahadhari na ndio itakuwa rahisi kumuua”Aliongea yule bwana huku akitoa moshi.
“Unadhani ni sawa kumuua sasa hivi , nazungumzia ushirikiano wa baba yako zidi ya mgombea wa uraisi?”Aliuliza yule bwana.
“Kuhusu hili baba pia alinipa msisitizo , lakini tusipomuua sasa hivi na Hamza wake tutajikuta tunachelewa”
“Ninachomaanisha kumuua kwa staili ya wazi wazi kama hivi , kwa mfano leo imeonekana Mzee Konki akiingia ndani ya kampuni ya Dosam na kuleta vurugu kama ikitokea Regina akikumbwa na kitu kikubwa zaidi basi moja kwa moja tukio hili litaunganishwa na familia yenu , isitoshe ndio wanufaika wakubwa”Aliongea Yule bwana.
“Kwahio Gonji unamaanisha kipi kifanyike?,”
“Kuna njia nyingi za kumuua mtu bila ya kifo chake kuonekana cha kupangwa”Aliiongea na kumfanya James macho kuchanua.
“Unadhani inaweza kuwa rahisi , MzeeKonki na kundi lake wameenda kumshambulia Hamza lakini wameambulia maumivu , hawa vijana wako ambao unawasifia unadhani wanaweza kuwa na uwezo wa juu kumzidi Hamza?”
“Kama nilivyosema kuna njia nyingi za kumuua mtu lakini njia hizo sio lazima ziwe kupigana ana kwa ana , kama huwezi kumuua mtu kwa kushindana nae ulingoni basi unatumia mtego, mfano kusababisha
ajali , kutega bomu katika gari yake na kadhalika”Aliongea Gonji na kumfanya James sasa kuelewa.
“Hapo kwenye ajali nakubaliana na wewe lakini vipi kuhusu bomu , sio rahisi kupata bomu”
“Hilo lisikupe shida , kwasasa vigogo wengi wanahitaji kuona Hamza akifariki kutokana na kuzuia mipango yao, ni rahisi kushawishi makomandoo kutupa siraha yoyote ile”
“Kama hili unadhani linawezekana basi naliacha katika mikono yako , lakini nikukumbushe linapaswa kufanyika kwa haraka maana hatuna muda wa kupoteza”Aliongea James na kumfanya Gonji kutoa tabasamu.
“Ili mradi malipo ni ya kueleweka nitahakikisha wiki mbili hazipiti unaipata taarinfa nzuri”Aliongea kwa kujiamini huku akizima ile sigara kwa kuiminya katika kisahani cha majivu.
********
Yonesi alijikuta akifumbua macho yake taratibu na kitu cha kwanza alichoweza kuhisia ni radha ya damu iliokuwa kwenye midomo yake.
Baada ya akili kumkaa sawa ndio sasa aliweza kujua alikuwa hospitalini katika wodi na hio ni mara baada ya kupatwa na harufu ya dawa za kuzuia maambukizi ya vinyemelea.
“Fyaaaa…Fyaaa…sio mbaya , sio mbaya hii juisi ni tamu”
Ilikuwa ni sauti ya mwanaume iliomfanya kugeuza shingo yake na aliweza kumuona Hamza akifyonza juisi kwa kutumia mrija na kufanya chupa ile itoe sauti kwa ndani ikionyesha imeishiwa na juisi na anavuta hewa.
Hamza alikuwa amemaliza chakula chote ambacho kililetwa kwa ajili ya mgonjwa na muda huo alikuwa akimalizia juisi.
Upande wa Yonesi ilikuwa mara ya kwanza kuona mtu akifurahia chakula namna hio mpaka kujilamba midomo akiwa katika mazingira ya hospitalini.
“Ah! Kapteni umeamka sasa?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona Yonesi anamwangalia.
“Kwanini upo hapa?”
“Mkurugenzi kaniambia nibaki na wewe , kazi yangu leo ni kukaa na wewe na kukuhudumia kwa kila unachotaka”
“Mkurugenzi… nini kiliendelea kwenye kampuni?”
“Yashaisha yale , wale watu wote wamekwisha ondoka”Aliongea Hamza na kumfanya Yonesi kuvuta pumzi ya ahueni.,
“Vipi ulifanikiwa kumshinda yule Kechani?”Aliuliza na kumfanya Hamza kutingisha kichwa huku akicheka.
“Unacheka nini sasa , kama unasema sema tu, usinidharau ukidhani mimi dhaifu kiasi hicho”
“Lakini sijasema nakudharau”
“Lazima utakuwa unajiambia kwenye moyo wako nina kiburi na sijui kukubali kushindwa na najikweza sana hata kwa watu ambao sina uwezo wa kupambana nao na mwisho wa siku nikaishia kujiumiza mwenyewe”Aiongea Yonesi kwa sauti ya kulalamika na kumshangaza kiasi Hamza.
“Kapteni nikupe maji kidogo?”
“Sitaki maji , unaweza kwenda huna haja ya kunisaidia”Aliongea Yonesi huku akijitahidi kusimama lakini alijikuta akigugumia maumivu makali ya tumbo.
“Majeraha uliopata kwa ndani hayajapona bado , hivyo kuwa makini usijilazimishe la sivyo utajiumiza zaidi”
“Sihitaji ushauri wako”Aliongea Yonesi huku akionyesha hasira waziwazi.
“Sikia Yonesi sio kwamba nakudharau , unaweza kuniamini au usiniamini hio ni juu yako lakini ukweli sijawahi kudharau uwezo wako”
“Huna haja ya kunifariji kwa kujitia upole”
“Ninachomaanisha sio kwamba huna uwezo wa kupigana na yyule Kechani , kama umeweza hadi kufanya utafiti wa namna ya kudili na mbinu za Kucha za tai basi unaonyesha ni kwa kiasi gani una juhudi ya kujifunza na kuhusu hili nimekukubali na kama ni ushindi pale ulishinda , kosa lako ni kwamba hukujua mwenzako ana mafunzo ya kuamsha nguvu za ndani hivyo ni halali kukuzidi”Aliongea Hamza na maneno yale kidogo yalionesha kumlainisha Yonesi.
“Ndio uivyoona pia?”
“Kapteni kwanini nikudanganye , umeonyesha ni kiasi gani una nia ya kutimiza wajibu wako , nadhani kupitia hili Mkurugenzi anapaswa kukuongeea mshahara”Aliongea na kumfanya Yonesi bado kutoyaamini maneno ya Hamza.
“Unaongea maneno ya kijinga ili kunifariji tu ila ndani kwa ndani utakuwa unachekelea”Aliongea lakini Hamza alipotezea alijua asingeweza kushinda mbele ya ukiburi wa Yonesi.
“Vipi una njaa?, Dokta amesema unapaswa kula vyakula vya ujiuji kwa siku tatu , ngoja nikuagizie uji”
“Sina nja… “Kabla hata hajamaliza sentensi yake tumbo lake lilianza kunguruma kama jenereta.
Muda ulikuwa umeenda tokea aletwe hapo na pia alitoka kwenye pambano kali hivyo ilikuwa ni halali kushikwa na njaa.
Hamza aliishia kutoa tabasamu na alipiga simu uji uletwe mpaka kwenye wodi yao , Hospitali hio ilikuwa ni binafsi na ilikuwa na huduma ya mgonjwa kuagiza chakula kabisa na kuletewa kutoka jikoni.
Dakika chache mbele uji uliletwa na Hamza aliumimina kwenye bakuli na kuchukua kijiko kwa ajili ya kumlisha Yonesi , lakini alikataa.
“Nina mikono nitakunywa mwenyewe”Aliongea na Hamza hakutaka kulazimisha na kumpatia Yonesi lile bakuli.
Muda huo Yonesi aliweza kugundua sasa mavazi yake yote mwililini yalikuwa yamebadilishwa na amevaa mavazi maalumu ya hospitalini.
“Nguo zangu ziko wapi?”.
*******
Saa nane za mchana alionekana Frida akiingia ndani ya majengo ya taasisi ya Haliz, mwendo wake siku hio ulionekana kuwa ni ule wa kujiamini zaidi kuliko siku nyingine zote.
Baadhi ya wafanyakazi aliopishana nao baadhi yao walimkaribisha kazini kwa mara nyingine huku wengine wakimpa ishara ya salamu tu ambapo Frida alizipokea kwa kutabasamu.
Mara baada ya kuzikaribia Lift alibonyeza kitufe na dakika chache Lift ilifunguka na akaingia ndani na alibonyeza kitufe cha floor ya 24 juu kabisa ya jengo hilo.
Na ilimchukua dakika tu lift ilimfikisha katika floor ya uongozi wa taasisi hio na alitembea kwa kujiamini katika Koridio hio huku akipokewa na marashi mazuri yaliotokana na AC.
“Naima nipo hapa kwa ajili ya kuonana na Mkurugenzi”Aliongea Frida mara baada ya kufika katika dawati la mapokezi na kukutana na mwanadada alievalia sare za rangi ya bluu iliokolea pamoja na Hijab huku akiwa na tabasamu.
“Karibu sana Dokta , Mkurugenzi anakusubiri”Aliongea yule mwanadada kwa tabasamu kwa kingereza na Frida alimrudishia tabasamu la ukarimu na kupiga hatua kuingia katika ofisi ya Mkurugenzi.
Frida hakusumbuka hata kugonga kutokana na kuona taarifa za ujio wake zishamfikia bosi wake , hivyo aligonga kidogo na kisha akasukuma mlango na kuingia ndani.
“Karibu tena kazini Dokta Frida”
Sauti ya mwanamama iliweza kusikika na kumfanya Frida kutoa tabasamu huku akimwangalia mwanamke ambae amevalia Hijab.
Alikuwa ni Dokta Maya Thema na ndio mkurugenzi mkuu wa taasisi ya maswala ya fahamu ya Haliz Foundation.
“Asante sana Dokta Maya”Alijibu Frida na Sister yule alitoka katika meza yake ya kufanyia kazi na kuja kuketi katika masofa.
Ilikuwa ni ofisi kubwa mno , ilikuwa na kila sifa ya kuitwa Ofisi ya Mkurugenzi mkuu wa taasisi hio kubwa , licha ya kwamba vitu vingi vilionekana kawaida lakini kwa macho ya tathimini lazima ujue samani na mapambo ni ya bei ghali , ki ufupi kila kitu kiliendana na hadhi ya mtu wa dini. “Inaonekana taarifa za kurudi kwangu zimefika mapema kuliko nilivyotarajia”Aliongea Frida akiwa na tabasamu.
“Ndio, Frida wewe ni mwanasayansi mkubwa sana ndani ya taasis ya Haliz na viongozi wanajua hilo , licha ya kwamba nimekutangulia ki uzoefu lakini umenizidi vitu vingi, Askofu alinipigia simu juu ya kurudi kwako tena , Karibu sana”
“Unaonekana kuwa na furaha sana juu ya ujio wangu pia Professor , licha ya kujua kilichotokea”Aliongea na kumfanya Sister kutabasamu na alisimama kutoka kwenye sofa na kumimina maji kwenye glasi kutoka kwenye Dispenser
“Utapendelea maji?”Aliuliza.
“Asante sister , ila sina kitu”Aliongea na kumfanya Sister Maya kutingisha kichwa na kurudi kwenye sofa na kukaa.
“ Faiths!, to me all faiths are admonitions that there is something we cannot understand , something to which we are accountable. It doesn’t matter what we believe personally , as long as there is sometting that we cannot understand about someone’s faith , then we have no reason to judge”Aliongea Sister akimaanisha kwamba hatuna uwezo wa kumhukumu mtu kutokana na dini yake kwasababu katika hio imani mtu anayokuwa nayo lazima kuna kitu ambacho mtu mwingine huwezi kuelewa.
Kauli ile ilimfanya Frida kutoa tabasamu hafifu akionekana kukubaliana na Profesa wake.
“Frida unajua sababu kubwa ya kuanzishwa kwa kanisa la Wasinagogi?”Aliuliza na kumfanya Nadia kutingisha kichwa kwamba haelewi.
“Mwasisi wa kanisa la Sinagogu alikuwa ni muumini mkubwa kutoka kanisa kuu mpaka siku ambayo Dokta Genesha alitoka hadharani na kusema kwamba ana uwezo wa kuthibitisha uwepo wa nguvu ya kiroho kwa kutumia sayansi, mpaka leo hatukujua ni ushahidi gani ambayo Dokta Genesha alimuonyesha mwasisi wetu lakini ni kitu ambacho kilimbadilisha mawazo mno na kugeuka mara moja kutoka Kanisa kuu na kuanza kufikiria kama mtu ambae hajawahi kusoma biblia”
“Kama wanasinagogu hawakuona ushahidi ambao
Dokta Genesha aliongelea na mwasisi hakuwaambia kwanini alipata wafuasi , lazima kuna sababu ambayo iliwashawishi wengine kumfuata na kuja kuwa jumuia tishio na yenye ushawishi mkubwa duniani?”
Comments