Reader Settings

SEHEMU YA 51.

Sister Maya mara baada ya kuulizwa swali lile alionekana kuwaza  kidogo na kisha akamwangalia  Frida.

“Hakuna sababu   yoyote , wote tunaamini  katika siri ambazo hatujaambiwa”Aliongea Sister.

“Siri ambazo hamjaambiwa!, unamaanisha nini kusema hivyo?”

“Ndio, licha ya kwamba  umekuwa chini ya Sinagogu kwa muda mrefu lakini je imani yako inakuambia nini kuhusu siri , je unaamini  kuna uwezekano wa  uwepo wa siri kubwa sana  ambayo hujaambiwa  katika  maisha yako kuhusu ulimwengu ulivyo?”Aliuliza na kumfanya Frida kutingisha kichwa.

“Naamini zipo siri nyingi ambazo sijaambiwa  mpaka sasa”

“Hio ndio sababu yetu binafsi  , kila mwanasinagogi anaamini   katika siri ambazo hajaambiwa  na sio  ukweli  ambao tunaaminishwa, wala sababu ambazo tunapewa  ili kuamini”Aliongea na kumfanya Frida kufikiria sentensi yake.

“Kama ni hivyo basi kila mtu anaweza kuwa Mwanasinagogi , siamini katika ulimwengu huu hakuna  asieamini uwepo wa siri  juu ya vitu mbalimbali”

“Huo sio msingi pekee wa imani yetu , tunachoamini zaidi ni ile siri ambayo  tuna malengo nayo, unaweza kuamini  kuwepo kwa siri lakini huna juhudi yoyote ya kuzitambua hizo siri  basi wewe sio Mwanasigiogi, kwa lugha nyepesi Sinagogi ni  jamii ya watu wanaoamini katika kweli ambayo haijasemwa lakini inaonyesha dalili”

“Dalili!, naweza kufahamu zaidi?”Aliuliza Frida kwake ndio mara ya kwanza  kufahau kuhusu kauli hio , isitoshe  katika jamii ya wanasinagogu kuna  madaraja ya uanachama ndio unaweza kujua baadhi ya vitu.

“Kuhusu hili  nadhani  una majibu tayari , kama sio hivyo usingerudi katika  taasisi ya  Feliz na usingefanikiwa kumshawishi Askofu Alfonso kukurudisha  licha ya kwamba kwake unaonekana mtu hatari”Aliongea Sister na kumfanya  Frida kutulia na kuanza kutafakari maneno ya Sister.

“Unamaanisha  kuhusu wimbi la watu wenye zaidi ya nafsi moja!!?”Aliongea na kumfanya Sister Maya kutingisha kichwa.

****

Huna haja ya kuwa na wasiwasi , ni  nesi ndio kakubadilisha”Aliongea Hamza  mara baada ya kuona Yonesi alikuwa na wasiwasi  kama yeye ndio amembadilisha.

“Nimeuliza nguo zangu ziko wapi na sio nani  kanibadilisha”Aliongea Yonesi huku kidogo akihisi ahueni.

Hamza hakutaka kubishana nae hivyo alimpatia bakuli lile la uji  lakini sasa kitendo cha Yonesi  kuchota kwenye kijiko na kupeleka mdomoni alijikuta akishindwa baada ya kuhisi maumivu makali  ya viungo vya ndani.

“Ngoja  nikusaidie  acha ubishi   unakuwa mjinga sasa kuzidi kujiumiza kwa ujeuri wako”Aliongea Hamza  na kumfanya Yonesi kukosa sababu ya kukataa. 

Hamza alianza kumlisha Yonesi  taratibu lakini kitendo hicho ni kama kimempa nafasi ya kumwangalia zaidi usoni kwa ukaribu zaidi , sasa harufu ya  kimwili ya Yonesi pamoja na ya hospitalini  ilimfanya pua zake kuburudika.

Kitendo cha  Hamza kumlisha  akiwa kimya ilimfanya Yonesi kujihisi  hali isio ya kawaida.

“Mbona  huongei?”

“Kapteni leo Nimegundua ngozi yako ni laini mno  bila hata ya kuigusa”Aliongea Hamza.

“Acha kuongea”

“Unatakiwa kuniacha nimalize kwanza kuongea na kisha ndio uniambie ninyamaze”

“Sitaki kusikia ujinga wako”

“Nimekusifia unaita ujinga”

“Haina haja ya kunisifia hivyo kwangu ni ujinga”Aliongea Yonesi lakini mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda kasi mno na kuanza kujiuliza nini kinaendelea kwanini anakosa utulivu mbele ya  Hamza.

“Labda  ni kwasababu tupo  katika  chumba kimoja wenyewe”Aliwaza Yonesi  akijaribu  kujipa sababu.

Upande wa Hamza wakati akiendelea kumlishaYonesi macho yake yalikuwa yamegota  katika kifua cha mrembo huyo , ilionekana nesi ambae alimvalisha  hakufanya kazi nzuri kiasi kwamba  kwa juu  kila kitu kilionekana  kwa ndani.

Yonesi  mara baada ya kumwangalia Hamza usoni aligundua ni wapi  alipokuwa akiangalia na alitamani kumpiga lakini kwasababu hakuwa na uwezo  huo  kutokana  na maumivu  aliishia kung’ata macho kwa hasira.

“Endelea kuangalia tu kama sijayatoboa hayo macho yako”

“Umenidhania vibaya Kapteni , nilikuwa  nikijiuliza nikusaidie kukufunga hicho kifungo vizuri , naona nesi hajafanya kazi nzuri kwenye kukuvalisha”

“Haina shida wewe jua mambo yako tu “Aliongea Yonesi  huku akivumilia maumivu na kujiweka vizuri.,

Mara baada ya kushiba Hamza alimsaidia kuegamia kwenye kitanda  lakini ni muda ule Yonesi alianza kukunja sura.

“Naomba uniitie nesi”Aliongea.

“Nesi wa nini , kuna shida yoyote?”

“Nenda  niitie nesi maswali mengi ya nini?”Aliongea  na kumfanya Hamza  kutoka nje  kwenda kumuita  nesi.

“Mgonjwa kuna chochote unachohitaji  nikusaidie?”Aliuliza Yule nesi.

“Nataka kwenda bafuni”Aliongea Yonesi na sasa kumfanya Hamza  ajue shida ya Yonesi ni nini na kutamani kucheka.

Ilikuwa ni sahihi kuhisi mkojo maana   tokea asubuhi   alikuwa amelala na muda huo amepewa madawa  pamoja na  kunywa uji.

Yule nesi alimwangalia Hamza kwa  maswali kadhaa ,  ni kama  alimuona Yonesi  na Hamza ni wapenzi lakini hata hivyo alikubali.

“Sawa ngoja nikusaidie , shuka  taratibu  taratibu ukiona unahisi maumivu  niambie”Aliongea  yule nesi hakuwa mrefu sana alikuwa na mita kama moja na nusu lakini Yonesi alikuwa na zaidi ya mita moja  nukta saba.

Yonesi alipiga hatua kuelekea  chooni lakini  mwili  wake wote ulikuwa umemlemea yule Nesi na kuonesha ni kwa namna gani alikuwa akipata shida kwani alianza kutetemeka.

“Arggh,,!”

Yonesi alijikuta akihisi maumivu   na kuguna  na yule  nesi kutokana na kuchoka alijikuta akishindwa kumsaidia zaidi Yonesi na kumuombaHamza amsaidie.

“Kaka itakuwa  vizuri ukimsaidia wewe , sina nguvu  za kutosha na itakuwa hatari kama nikidondoka” “Haina  shida nitaweza mwenyewe”

“Dada huna  haja ya kujilazimisha sana ni hatari kwako , ngoja mpenzi wako akusaidie ,  mtu yoyote anaweza kuwa mgonjwa na kuhitaji mtu wa kumsaidia , haina haja ya kuona aibu”

Upande wa nesi  aliamini  kama Hamza sio mpenzi wa Yonesi basi ni mume wake maana  ndio amemleta hospitalini na hata chakula ndio amemsaidia kumlisha na amekaa wodini tokea asubuhi.

Yonesi alitamani kumwelezea  yule nesi kwamba  sio vizuri kwasababu  ni  jinsia tofauti na hana mahusiano yoyote na Hamza lakini Hamza alikubali haraka.

“Ngoja nitamsaidia  mimi”Aliongea Hamza na kumpokea yule nesi  na  ni kama alipata nafuu , alionekana kuwa bize hivyo aliondoka mara moja.

“Kapteni usiwe na wasiwasi naahidi sitokuchungulia kabisa “Aliongea Hamza akiwa siriasi.

Yonesi kwasababu mkojo  ulikuwa umembana sana hakutaka kujizuia tena hivyo alikubali kusaidiwa.

“Sijasema chochote , nisaidie niingie”Aliongea na Hamza alikubali na alimsaidia mpaka ndani  lakini mara baada ya kuingia ndani kulikuwa na tatizo lingine , alishindwa kuinama ili kushusha suruali chini  kwani angejisababishia maumivu.

Alijikuta akikakamaa akishindwa kujua  afanye nini , aliogopa kujikojolea pia kwa kuogopa  aibu atakayoipata.

“Kapteni nitageuka nyuma halafu nitakusaidia kushusha suruali, nadhani hapo  hutojisikia vibaya” “Sawa”Aliongea Yonesi maana hakuwa na jinsi.

Hamza alijikuta akigeuka nyuma huku  mkono  ukiendelea taratibu kushusha  suruali ya Yonesi pamoja na nguo yake ya ndani kwa wakait mmoja.

“Taratibu usiniguse”

“Sawa”

“Huko unakogusa ni wapi wewe?”

“Sioni vizuri sasa , basi ngoja niangalie tu”

“Unajitakia kifo sio , ole wako ugeuke”

Mara baada ya kuteseka kwa sekunde kadhaa hatimae alifanikisha misheni ya kuishusha.

Yonesi alijiegamiza  katika mwili wa Hamza huku akijitahidi kukaa  katika choo ,  lakini bado alikuwa na wasiwasi Hamza atageuka na kumwangalia 

“Usiwe na wasiwasi ,  kama nilivyosema siwezi  kufanya chochote ni bora ujiachie hayo maji yakutoke haraka haraka kuliko kujikaza usitoe sauti”Aliongea

Hamza na kumfanya Yonesi kumwemwesa lips zake alitamani kumwambia  Hamza atoke.

Halafu Kapteni ushawahi kuwa mwanajeshi  inakuwaje unapata  wasiwasi na jambo la kawaida kama hili”

“Kwahio kuwa mwanajeshi ndio nini?”

Aliuliza Yonesi huku akiona asijikaze tena na kuachia kojo  limtoke , lilikuwa na presha kama vile  bomba  la maji limepasuka, isitoshe wote walikuwa kimya hakukua na alieongea.

Yonesi alikuwa na  aibu mno ilikuwa afadhali  Hamza hakuongea chochote mpaka anamaliza.

“Unaweza kuondoka tu”Aliongea Yonesi mara baada ya kufanikiwa kurudi  kitandani.

“Usiwe na wasiwasi , isitoshe bado ni muda wa kazi na hata nirudi  kwenye kampuni sitokuwa na chakufanya, kwa maelekezo ya Dokta unapaswa kupumzika kwa siku mbili”

“Siku mbili?”

“Umejiumiza sana  na  hutakiwi kujiingiza katika matatizo tena , halafu tena umenikumbusha imekuwaje mpaka ukajiumiza  ni mbinu gani ambayo umeitumia?”Aliuliza Hamza.

Ukweli ni kwamba alikuwa ashashuhudia mbinu  nyingi za mapigano lakini hakuwahi kuona  mbinu ambayo mtu  anajiumiza mwenyewe kiasi cha kutema damu , alijua lazima mbinu ya  Yonesi sio ya kawaida, lakini  licha ya kuuliza   Yonesi aliendelea kubakia kimya.

“Niwie radhi  , huna haja ya kujibu kama ni siri yako?”

“Ukweli ni kwamba hata sijui ni mbinu gani, siwezi pia kusema ni mbinu ya kuamsha  nguvu ya ndani?”

“Kwanini unasema hivyo?”

“Kuna kipindi  wakati nikiwa chini ya kitengo  kama mwanajeshi katika misheni maalumu  katika Jangwa la  Sahara  niliweza kupata hii mbinu  imeandikwa katika Notebook , mtu ambae  aliandika nilimkuta akikaribia kupoteza maisha na alinikabidhi , nilimpatia  Kapteni hio notebook lakini alisema haina maana yoyote , wakati nikiwa mafunzoni  China  nilimpa mkufunzi  hio notebook na alitafsiri maandishi yale na  kusema ni mbinu ya mafunzo ya kichawi ya kuamsha  nguvu ya asili ya mwili  lakini haijakamilika”

Kwahio uliamua kujifunza  bila ya kukamilika kwake?”

“Mwanzoni sikupanga kujifunza  ila niliamua kuhifadhi tafsiri yake kama ilivyo , lakini kutokana na  maelezo yake  yalivyo  yalinipa shauku  na kuanza kuitumia na wakati nikifanya hivo  mwili wangu huwa najihisi ni kama vile unaungua  na presha kupanda  juu mno  huku nikijihisi mwenye nguvu lakini viungo vya mwili huwa  ndio vinauma mno, nilikuwa na wasiwasi  ni  mbinu ya  nguvu za giza  hivyo sikuendelea nayo sana , lakini mara baada ya kumuona  yule Chekani na kutamani kumshinda kwa mbinu  yoyote ile  nilianza kufuata maelekezo  ya  hio mbinu na  matokeo yake  ndio  kama ulivyoona”

“Yaani kitu hakikukamilika lakini ukaamua kujifunza?”

“Ndio, mwanzoni nilifanya  kutokana na shauku lakini mara baada ya kujaribu yale mabadiliko yalinijengea shauku ya kutaka kujua zaidi , Master alikuwa sahihi kabisa  hii mbinu sio nzuri”Aliongea na kumfanya Hamza kumwangalia  kwa mshangao kidogo.

Kwanini unaniangalia hivyo?”

“Kapteni  nimekusaidia kwenda chooni  , vipi  mimi unaweza kunisaidia kitu?”

“Niondokee hapa , kuna haja gani ya kurudish kumbukumbu za matikio yaliopita”

“Kukusaidia kwenda chooni inamaanisha wewe ni rafiki yangu mpaka hatua hii  ndio maana naomba msaada kama rafiki pia”

“Kama unataka kujamba wewe jamba , huna haja ya kuongea sana”Aliongea  Yonesi lakini  Hamza  alibadilika na kuwa siriasi zaidi.

“Unaweza kuniambia hio mbinu ilivyo?”

“Unataka kujaribu pia , inaweza kukusabishia matatizo?”

“Nataka kuijua tu , usiwe na wasiwasi siwezi kwenda mbali zaidi”

“Basi nitakuambia maana sio kama ni  hazina ya maana mpaka nikufiche”

Yonesi mara baada ya kuona  namna ambavyo Hamza alikuwa siriasi  aliona amwelekeze tu maana ni kama ndio mara ya kwanza anamuona akiwa siriasi.

Fumba  macho   kisha  tengeneza  hisia za kusikiliza mapigo ya moyo wako yanavyodunda , iliruhusu nafsi yako kuitawala akili yako , endelea hivo hivyo  mpaka uone giza katika macho yako linapotea , litafute jua katika nafsi yako  mpaka liwe katika uhalisia  wa macho yako kisha lipotezee ,  utafute mwezi katika nafsi yako na kisha upotezee  na kwanzia hapo kila kitu kitajielezea  chenyewe kwa kadri unavyoona ….”Yonesi aliendelea kuongea   lakini baadhi ya maneno yake hayakueleweka kwani yalikuwa na rahaja ya  mafunzo ya kimapigano ambayo mtu wa kawaida hawezi kuelewa.

Hamza aliendelea kuwekeza akili yake  katika  kile alichoona lakini  ghafla alijihisi mapigo  yake ya moyo yakizidi kwenda mbio  kwa kile alichoona  na alijikuta akitoka  mara moja  katika  mawazo yale  na kufumbua macho.

Na muda huo huo mlango wa wodi uifunguliwa na  msichana mdogo  ambae Hamza alimfahamu ni moja ya mlinzi katika idara ya  Yonesi aliefahamika kwa jina la Joyce.

“Kapteni vipi hali yako , unaendeleaje?”

Joy unafanya nini  hapa muda wa kazi?”Aliuliza  Yonesi.

“Mkurugenzi kaniambia  nije kumpokea  Hamza ,  maana mimi ni mwanamke mwenzako hivyo ni rahisi kukusaidia”

Yonesi alijikuta akiona aibu  kidogo lakini kwa wakati mmoja alijikuta akikasirika alitamani  Joy angekuja  mapema kabla ya kuaibika mbele ya Hamza.

“Mr Hamza Mkurugenzi anasema urudi  makao makuu  haraka haraka kuna vitu anataka kukuuliza”Aliongea Joyce na kumfanya  Hamza kushangaa kidogo maana aliona kama ni kuuliza si angepiga tu simu, lakini hata hivyo hakuuliza zaidi na  aliaga na kuondoka.

Hamza mara baada  ya kuingia kwenye gari  alijikuta  akifikiria kile alichoona wakati wa kujaribu kufuatisha ile mbinu , alijiuliza kwanini aliona sura ya  yule mwanamke  aliekuwa akichomwa moto  kwenye  ile ndoto na ni kama alikuwa akimsubiria.

Hamza aliamua kupotezea kwanza  swala hilo na  palepale  aliondoa gari mpaka katika makao makuu ya kampuni   na mara baada ya kuegesha gari na

kwenda moja kwa moja katika ofisi ya Regina , alishangaa kumkuta Bibi Mirium  akiwa ndani ya  ofisi katika kiti chake cha Magurudumu.

Pembeni yake alikuwepo Regina alieismama  kiadabu kabisa , hakuwa kabisa na ile hali ya kuwa bosi wa kampuni.

“Kwanini bibi amekuja mpaka huku , shangazi  hayupo nyumbani?”Aliuliza Hamza mara baada tu ya kuingia  ndani ya ofisi hio na kumfanya  Bibi yake  Regina kugeuka na kumwangalia Hamza.

“Nasikia umevunja  mtu mguu  alietumwa na familia ya Benjamini kwa teke moja tu licha ya kuwa na mafunzo ya hali ya juu ,  nikama nilivyoambiwa unaonekana sio  mwepesi mwepesi  nadhani ndio maana Regina anakupenda”Aliongea.

“Bibi, Simpendi mimi”Aliongea Regina kwa haraka  akikataa. 

“Bibi  ngoja nikuambie ukweli , yaani  tokea nijiunge na hii kampuni nimekuwa na  mchango mkubwa sana

, siku nyingine ukija  utazisikia sifa zangu tu”Aliongea Hamza 

“Hehe,, nimekuja angalau kwa mara ya mwisho 

katika hii ofisi ili niweze kuliangalia jiji la Dar kupitia hili dirisha , sidhani kama nitaweza kuja tena kwenye maisha haya. Ila uzee una mambo mengi sana  nakumbuka kipindi  na babu yako wakati  tunasimama hii sehemu  baada ya jengo kukamilika mandhari hayakuwa ni  ya kuvutia  kama ninavyoyaona leo,  naona kama uzuri wake umezidi kuongezeka mara  tatu zaidi”Aliongea huku akionekana kama vile ni mwenye kujutia.

“Bibi kwanini kila saa unapenda kuongea maneno ya kujikatia tamaa”

“Wewe mtoto sisi wote ni wafanyabiashara  na ili ufanikiwe kama mfanyabiashara unapaswa kujifunza namna ya kuukabili uhalisia , haina  haja ya kufikiria mambo  yasiowezekana  kwasababu tu uhalisia ni mgumu , mimi bibi yako siku zangu  zinahesabika  na  nashukuru hata kuweza kufika hapa juu nikiwa katika kiti cha magurudumu , pengie inaweza hata kunisahaulisha kile ambacho nataka kuona kikitokea kabla ya kuondoka”Aliongea na kumfanya Hamza kumkubali huyo bibi  aliona ni kama umri wake umemfanya kuzidi kuwa na busara.

Bibi unaonaje tukienda kupata chakula cha usiku katika hoteli kubwa ya kifahari , inaweza kuwa sehemu ya matamanio yako ya mwisho mwisho kutaka kufanya”

“Kuhusu hilo .. nadhani sio mbaya  chagua hoteli nzuri kabisa  tutaagiza mvinyo wa bei ghali kuliko yote inayopatikana nchini  na kusherehekea”Aliongea kinyonge na kumfanya Regina macho yake kuanza kuwa mekundu.

“Nitamwambia   Linda aweke utaratibu , vipi nialike na wazee wa kampuni”

“Washaondoka kuna haja gani ya kuonana nao , malizana nao kabisa ndio nitapata nafasi ya kwenda kuwaona , kwasasa sitaki kuwaona maana sidhani kama  wana  maana yoyote kwangu”Aliongea kikauzu na kumfanya  Hamza kuishia kupumua  tu kwa masikito  aliona  kabisa  kuna uwezekano  Regina karithi kila kitu kwa huyo  mzee.

Muda huo huo mwanaume mzee  wa miaka kama sabini na kitu hivi  mwenye dalili ya mvi aliweza kuingia katika ofisi hio  na kumfanya Regina kushangaa.

“Mzee Kibatala  kwanini upo hapa?”Aliuliza Regina , Mzee Kibatala ndio aliekuwa mwanasheria mwenye umri  mkubwa sana ndani ya  kampuni yao na alisimamia maswala mengi tokea kipindi cha babu yake.

Ni moja ya  wanasheria ambao walikuwa wakiheshimika mno ndani ya Tanzania nzima.

Kutokana na umri mkubwa aliokuwa nao alijichukulia kama vile amestaafu hivyo kazi nyingi za kampuni zilikuwa zikiwakilishwa na  vijana  waliokuwa katika ulingo wa sheria na yeye alionekana mara chache sana kwenye  maswala ya kisheria  ya kampuni.

“Mkurugenzi nipo hapa  kwa  maombi ya Madam ,

nimeleta wosia  na nyaraka nyingine  za kisheria”Aliongea.

“Wosia!!”

“Ndio”Aliongea na muda uleule  alianza kutoa nyaraka  katika mkoba wake wa Briefcase aliokuja nao , ilikuwa ni ile mikoba ya zamani kabisa na ilionekana ulitumika kwa  kipindi kirefu mno.

Kwasababu  Madam hawezi kusaini na karamu basi tutatumia alama ya vidole  vyake , pia nitarekodi  tukio zima  kwa ajili ya ushahidi”Aliongea.

“Mzee Kibatala amefikiria vya kutosha na  ameona huu ndio muda”Aliongea Bibi Mirium.

Muda uleule yule mzee alianza kusambaza nyaraka katika  meza ya kioo iliokuwepo  katika ofisi hio na kumpa nafasi ya  Mirium kuweka kidole gumba katika kila nyaraka 

Regina ambae alikuwa pembeni aliweza kuona kila kitu  na mara baada ya kuona mwisho wa nyaraka hio alijikuta akishangaa.

“Bibi , unataka kunipa hisa zote?”

“Ndio lakini kama nilivyosema  kuna

masharti”Aliongea huku akinyooshea mkono karatasi ya mwisho.

“Sharti langu ni  wewe kuolewa , nikifariki bila  ya kuona  hujaolewa basi hisa zote   kisheria zitaenda kwa baba yako”Aliongea na kumfanya Hamza kukunja sura na kujiambia huyu mzee ni mkatili mno kwa kutumia sababu hio kumfosi Regina kuolewa.

Lakini kwa upande mwingine aliona  kama hisa hizo zitaenda kwa baba yake Regina basi kampuni inaweza kuwa ndio mwisho wake maana moja kwa moja  hisa zote zitakuwa zinamilikiwa na Lamla.

Sasa kama Regina amefanya kazi kwa  juhudi kubwa kuifikisha kampuni ilipo ataweza kuruhusu kuona kampuni inaangukia katika mikono ya watu wenye nia ovu.

Upande wa Regina aliona ni kama bibi yake anamuonea  na  kabla hajaweka kidole gumba katika karatasi yenye masharti alianza kulalamika.

“Lakini bibi mimi sitaki kuolewa nae”Aliongea na kumfanya Hamza  midomo yake kucheza na kujiambia kwani amemkosea nini huyo mwanamke mpaka kumkataa waziwazi.

“Mimi sina shida , sio lazima uolewe na Hamza  , mimi ninachotaka ni ndoa hivyo sijali nani  unaoana nae”Aliongea na kumfanya Regina  kuona  wazo hilo ni baya zaidi.

“Bibi kwani lazima niolewe , ninao uwezo wa  kuendesha kampuni  bila ya kuolewa , sitaki mwanaume  kabisa”

Huu ni wosia wa baba yako na wa kwangu pia  na   sifanyi hivi kwasababu  sina sababu haya yote ni kwa ajili yako , na nishaweka alama  tayari  hivyo kama unataka kuilinda kampuni isiende kwa mwingine hakikisha unaolewa  haraka iwezekanavyo”Aliongea na kisha alimwangalia Hamza.

“Ila  kwa upande wangu nimetokea kumkubali  Hamza zaidi  kama utaolewa nae  una baraka zangu zote”Aliongea na kumfanya   mzee Kibatala kutabasamu.

“Madam mimi ninawaacha kazi yangu ishamalizika hapa”

“Asante sana  na  pole kwa usumfufu  matumaini yangu hili swala utalifanya kuwa siri kwa  muda”

“Usiwe na wasiwasi Madam”Aliongea na Bibi Mirium alitingisha kichwa kumuaga.

Muda ule hali ya  Bibi  ilianza kubadilika na kumfanya  Regina kumpeleka mpaka chumba cha  kupumzikia , ofisi ya Regina  ilikuwa  na chumba cha kulala na sebule  kabisa , ilikuwa ni kama ofisi ndani ya Apartment.

Upande wa Hamza  wakati akiwa akimsubiria Regina kutoka  ujumbe kwenye simu yake  uliingia na alipoangalia namba  ni mpya  na aliufungua ule ujumbe  na alikuta sentensi  ya neno’   I  am  Back – From  2F .

Hamza palepale  alijua aliekuwa  ametuma ujumbe huo ni Frida na alijikuta akishangaa kidogo  na  alitaka kuipiga ile namba palepale lakini simu yake ilianza kuita  na aliekuwa akipiga ni Eliza.

“Babe naona unanipigia muda wa kazi , utakuwa umenimisi sana nini?”

“Hata sijakumisi , nimesikia Yonesi kalazwa ndio maana nimepiga kujua maendeleo  yake”

“Kwahio unachojali ni Kapteni Yonesi tu na sio mimi?”

“Hamna  bwana..  ukweli nimepiga kwa ajili yako  , nataka kujua kama una ratiba usiku , kama huna unaonaje ukija nyumbani  nikupikie chakula kitamu 

kama ishara ya shukrani  kwa  ajili ya matibabu ya mama yangu?”

“Kwa leo  haiwezekani , nishakubali kwenda kupata chakula cha usiku na bibi yake Regina”

“Oh… basi  hata siku nyingine tu”Aliongea Eliza kinyonge.

“Babe ila usiwe na wasiwasi naweza kuja hata baada ya chakula”

“Sikufungulii mlango”

“Napitia dirishani”

“Halafu wewe .. sitaki kuongea na wewe”Aliongea na muda uleule simu ilikatwa.

Hamza mara baada ya kusikia sauti tamu ya Eliza moyo wake ulianza kuhisi majuto ,  na kuanza kujiuliza au baada ya chakula aende  kwake kumfanyia surprise , pengine anaweza kupewa tunda.

Hamza mara baada ya kurudi katika ofisi yake ili kupoteza poteza muda  ghafla tu mlango wa ofisi yake ulifunguliwa bila hodi na aliengia alikuwa ni Linda.

“Hamza”

“Kuna nini?”

“Bibi kazidiwa , wahi ukawashe gari

tunamshusha”Aliongea Linda  na kumfanya Hamza muonekano wake kubadilika mara moja na kitendo cha kutoka aliweza kusikia sauti ya kilio cha Regina  akimwita bibi yake aamke.

Previoua Next