Regina alijikuta akivuta pumzi ya ahueni mara baada ya kuona Hamza alikuwa muoga ndio maana kasogea mbali , alijiambia kama atashindwa kumkontrol huyo mwanaume basi ataingia kwenye kazi nyingine ya kutafuta boyfriend feki mpya.
Lift ile iliwapeleka mpaka juu kabisa kwenye moja wapo ya mgahawa uliokuwa ukipatikana floor ya mwisho , sehemu ambayo ukikaa unaona karibia jiji lote la Dar na maeneo ya mbali.
Meneja wa mgahawa huo alikuwa ni mwanaume wa makamo Mfaransa, alikuwa amevaa akapendeza na mara baada ya kumuona Regina alimtambua haraka na kumsogelea huku akiongea kwa kuchapia chapia kiswahili.
“Karibu sana Madam Regina CEO”Aliongea akiweka tabasamu lakini kwa wakati mmoja akionyesha namna ya kushangaa namna ambavyo Hamza ameshikana mkono na Regina.
Licha ya kwamba alikuwa Mfaransa ila kuishi kwake Tanzania kwa muda mrefu kumemfanya kujua vitu vingi na kati ya vitu hivyo ni urembo na ukauzu wa mwanamke Regina, CEO wa makampuni makubwa ya Dosam.
Sasa baada ya kuona mrembo huyo akiwa ameshikiliwa mkono na mwanaume aliona ni swala zito ambalo mashilawadu kama watalifahamu itakuwa habari kubwa, isitoshe Regina alikuwa ni kama kioo cha jamii ndani ya taifa .
“Wazazi wangu washafika?”Aliuliza.
“Ndio wameshafika tayari , nitawapeleka moja kwa moja walipo sasa hivi”Aliongea na kisha aliongoza njia.
Wakati wakitembea katika mgahawa huo mkubwa na wa kuvutia , Regina alijikuta bila ya kupenda akimwangalia Hamza, ni kama alikuwa na wasiwasi kwani alijua fika watu wa daraja la chini kama watafika katika eneo hilo ambalo hutembelewa na watu wa vipato vya juu watakuwa na wasiwasi.
Lakini alionekana kuridhika mara baada ya kumuona Hamza hakuwa na wasiwasi wowote na kuona hapo kweli ameajiri mtu sahihi.
Mara baada ya kuingia katika chumba binafsi kulikuwa tayari kuna watu watatu waliokuwa wamekaa kuzunguka meza.
Mmoja wapo alikuwa ni mwanaume wa hadhi wa makamo na mwingine alikuwa ni mwanamke ambae alikuwa amevalia mavazi ya thamani pamoja na mkufu wa thamani kubwa shingoni , kwa umri wake wa miaka arobaini ilionekana alikuwa akijitahidi sana kuhakikisha anaonekana kijana bado.
Kulikuwa na mwanaume pia kijana alievalia shati la kola, brand ya Ermenegildo Zegna , alikuwa ni mtanashati mno lakini pia alionyesha ni aina ya wanaume ambao wanadharau kiana hivi kutokana tu na wajihi wake.
Wote watatu walizidi kuonyesha hali ya dharau mara baada ya macho yao kutua katika sura ya Hamza akiingia hapo ameongozana na Regina.
“Regina kwanini umekuja na Bodigadi mpaka hapa ndani , huu ni mkumsanyiko wa kifamilia hatuihitaji mtu wa nje”Aliongea mwanaume yule kijana huku akimwangalia Hamza kwa kumnyali.
“James kama unalijua hilo basi na wewe hupaswi kuwepo hapa , kuhusu mwanaume niliekuja nae naomba nikutambulishe leo hii , huyu ndio Boyfriend wangu”Aliongea huku akimsogelea Hamza karibu.
Mara baada ya James macho yake kuona tukio hio alijikuta akishikwa na wovu mkali na sura yake kukunjamana..
“Acha kuongea ujinga Regina , tangu lini ukawa na boyfriend ghafla tu”
“Tumekutana kupitia njia ya mtandao zaidi ya mwaka moja uliopita , ni juzi tu hapa nilijua yupo Dar na tukaamua kuanzisha mahusiano”Aliongea Ragina, kwa namna ambavyo alikuwa amejiandaa kumtambulisha Hamza, alikuwa akijiamini na maneno yake.
Upande wa Hamza aliweza kuona hali hio ambayo haikuwa tulivu na ni mwenye kuangaliwa kwa dharau lakini hata hivyo hakujali.
“Mjomba hapo , Shangazi pale na Braza mbele hapo, salamu kwenu ….”
“Nyamaza wewe mjinga , mimi ndio mchumba halali wa Regina sio wewe bidhaa ya kuokotwa dakika za mwisho kwa ajili ya maigizo”Aliongea James kwa hasira.
“Braza .. unamaanisha mimi au , haha.. unachekesha mno”Aliongea Hamza na baada ya pale alimpotezea na kisha akamvutia kiti Regina na kisha cha kwake na kuketi chini.
“Regii , anza kukaaa”Aliongea Hamza akimpa ishara Regina kukaa na James mara baada ya kuona namna Hamza anavyomwita Regina kwa nickname uso wake ulikunjamana.
Hamza hakuona kabisa shida juu ya macho mabaya yaliokuwa yakimwangalia na alikaa mara baada ya Regina kukaa na kisha akatoa tabasamu akiulizia msosi.
“Mshaagiza tayari , nilipata chai asubuhi lakini bado najihisi njaa”Aliongea lakini kwa bahati mbaya ni kwamba hakuna ambae alimjibu.
“Regina nini unajaribu kufanya? , hivi unachukulia ndoa kama mchezo sio, James ni mwaminifu sana na amekuwa akikusubiria ufanye maamuzi zaidi ya miaka sasa , uwe na ukomo basi wa ubishi wako”Aliongea mwanamke ambae alionekana kuwa mrembo licha ya umri kuenda.
“Nyie ndio ambao mnalazimisha juu ya hii ndoa tokea mwanzo na wala sijakubali , kwasasa nishapata mwanaume ambae nataka awe mpenzi wangu , kwanini ionekane ni kama naleta ukiburi”
“Hey! Leta walinzi mara moja wamfukuze huyu mtu”Aliongea mwanaume wa makamo akiwa siriasi.
“Hakuna wa kumuondoa hapa , huyu ni mpenzi wangu , kwanini hakuna ambae anaonekana kunielewa hapa?”Aliongea Regina huku akijaribu kuonyesha ukiburi.
“Ni kweli kabisa mimi na Regi ni wapenzi na sio kuwa wapenzi tu tunapendana sana”Hamza alijitahidi kuongea huku akijiambia hii familia haipo vizuri kimahusiano na malumbano yao yatafikia hatua hawezi kupata chakula tena.
“Sijategemea hii kazi kuwa ngumu hivi , mbona hakusema kama tayari alikuwa na mchumba , kuja kwangu hapa ni kama kuibua ugomvi tu , hebu kwanza muangalie huyu anaeitwa mchumba wake , anaonekana ni mtu tajiri lakini kwa namna anavyoniangalia kwa chuki nadhani nimejipalia makaa”
Ningejua tokea mwanzo mambo yanakwenda kuwa magumu hivi juu ya hii kazi,bora hata ningeomba malipo makubwa zaidi”
Hamza alikuwa akijiwazia yeye mwenyewe , alikuwa akijitahidi kuendana na mazingira lakini kwa namna mazingira yenyewe yalivyo ilionekana ni kazi kubwa sana ambayo kwa mshahara aliokuwa akipewa katika ajira yake hio ulionekana mdogo.
“Regina hebu nisikilize mimi baba yako , kutaka uolewe na James ni kwa ajili ya faida yako mwenyewe , hebu acha ukiburi basi”
“Ni kwa faida yangu au ya kwenu , nadhani majibu kila mmoja anayo katika moyo wake”Aliongea Regina na kisha alimwangalia yule mwanamke, ambae jina lake anaitwa Lamla.
“Regina unaongea nini , usione unaweza kuongea chochote mbele angu kwasababu tu ni CEO wa Dosam , ijapokuwa sijakuzaa lakini mimi ndio nimekulea kwa miaka kumi , kwanini unaniona kama mtu mbaya?”Aliongea Lamla na palepale macho yake yalianza kuwa mekundu akionyesha anataka kulia.
Mzee Wilsoni mara baada ya kuona mke wake anataka kulia , haraka sana aliweka mkono wake begani na kuanza kumbembeleza.
“Aiya , Darling usikasirike , Regina hajamaanisha hivyo , usimuelewe vibaya..”
“Ni kweli hajamaanisha hivyo , Regina ni mtiifu sana na mkarimu na hiki ndio ninachokipendea kutoka kwake ndio maana nataka aje kuwa mke wangu kwa namna yoyote ile , anaweza asipende kwasababu nimewatumia nyie kumfikishia nia yangu ndio maana anagoma kufanya maamuzi”Aliongea James.
“James wewe ni kijana muelewa ambae una mfahamu vyema Regina , wewe umemsikia mwenzako namna anavyojitahidi kukuelewa , kwanini usimuombe radhi kwa kitendo chako cha kumleta mwanaume wa maigizo hapa”
“Daddy , haina haja ya kunilazimisha na kunisihi , sina mpango wa kuolewa na James mimi”Aliongea na kisha akamgeukia James .
“Jikatie tamaa tu , Dosam ni kampuni niliopewa na babu yangu kuiendesha na sipo tayari kuona inaangukia katika mikono ya mtu wa nje ya familia , huwezi kunipata na pia huwezi kuipata kampuni yangu”
“Regina , unaongea nini , sina matamanio yoyote na kampuni yako , isitoshe sina akili ya kibiashara kama wewe, macho yangu na moyo wangu unakuelekewa wewe tu siku zote , kwanini unashindwa kuona ni jinsi gani nakupenda Regina,”
“Haijalishi unaongea ukweli au uongo wewe ndio unaejua .. halafu usifikiri sijui wewe ndio unaehusika kunyanyasa wafanyakazi wa kampuni yangu”
“Regina unaongea nini , nani ananyanyasa wafanyakazi , mbona sijawahi kusikia juu ya hili?”Aliuliza mzee Wilsoni.
“Regina labda utakuwa umekosea , James hawezi kuhusika”Aliongea Lamla.
Upande wa Hamza mara baada ya kusikia kauli hio alijua pengine tukio la Eliza kunyanyaswa na wale wadeni wake lilikuwa likihusiana na swala analoongelea Regina , ila hakuwa na uhakika.
Regina hakuwa hata na mpango wa kuendelea kuzungumzia swala hilo , maana hata kama aseme hakuwa na ushahidi wa moja kwa moja.
“Kama nilivyosema , nishapata mpenzi tayari hivyo kwanzia sasa sitaki kusikia maswala ya ndoa”Aliongea
James licha ya kwamba alikuwa na tabasamu lakini uso wake ulikuwa wa kikauzu mno , ilionekana alikuwa akilazimisha furaha.
“Haha…haina shida Regina , mimi ni mtu mvumilivu, nani anajua , pengine mnaweza kuachana kesho au kesho kutwa , nadhani wakati huo utanifikiria”Aliongea James huku akitoa kicheko, na maneno yake yalionekana kuwa na zaidi ya maana.
“Wilson sitaki kumuona huyu masikini mbele yangu , hebu ita watu waje wamtoe kama unataka niendelee kubakia hapa”Aliongea Lamla.
“Akiondoka na mimi naondoka”Aliongea Regina.
“Wewe..”
“Madam usiwe na hasira , haijalishi akikaa hapa na kula chakula tulichoandaa , iwe ni familia yenu au yetu pesa sio tatizo , chukulia tu kama msaada kwa mpitaji, sidhani kama ni tatizo”
“Mh! , Kwasababu wewe ndio umeongea James basi sina jinsi na kumuacha”Alijibu Lamla..
Upande wa Regina alikuwa na wasiwasi , aliogopa James anaweza akawa na mpango kichwani usio mzuri anapanga kuufanya
Muda uleule alimwita mhudumu wa mgahawa huo wa kifaransa na kisha alibadili kutoka lugha ya kiswahili na kuongea kifaransa.
“Prenez la commande de ce monsieur , soyez pls professionel..”Aliongea akimwamlisha muhudumu kuchukua oda kutoka kwa Hamza lakini awe profesheno zaidi huku wakati uleule akimkonyeza.
Muhudumu yule wa kike ambae alikuwa akifanya kazi katika mgahawa wa matawi ya juu kama huo alikuwa akijua kuongea kifaransa na alielewa kauli ya James kwa haraka sana .
“Mmonsieur , Que desirez-vous?”.
Mhudumu huyo alikuwa ni mbongo tena mrembo aliejazia kifua , lakini licha ya hivyo aliweza kuajiriwa katika mgahawa huo wa hadhi ya juu utokana na elimu yake na Exposure , ilikuwa hivyo kwa wahudumu wote.
Upande wa Regina alikuwa ashausoma mchezo tayari , alichokuwa akitaka kufanya James ni kumuaibisha Hamza na kumchezesha shere kama mjinga.
Ni kama alikuwa akitaka kumwonyesha yeye ni wa daraja la chini , mtu ambae hakuwa akistahili kuingia katika mgahawa wa hadhi ya juu kama huo.
Regina mwenyewe hakuwa vizuri kwenye lugha ya kifaransa hivyo alitaka kuingilia kwa lugha ya kingereza akimtaka yule mhudumu kuongea kingereza.
“Waitress please speak ..”
“Le-menu s’il-vous -platue me consillez Vous?”(“Niletee menu ya mapendekezo ya vyakula nichague”)
Wakati Regina anataka kuongea , palepale alijikuta akisikia sentensi ambayo hata yeye hakuielewa ikimtoka Hamza.
Hali ya ukimya ilivaa watu wote waliouwa ndani ya chumba hich cha hoteli , Mzee Wilsoni , Lamla na James wote walikuwa katika hali ya mshituko.
Aliekuwa katika hali ya kushangaaa zaidi alikuwa ni Regina , macho yake mazuri yaliongezeka ukubwa huku akimwangalia Hamza.
Upande wa muhudumu mara baada ya kuona amejibiwa alijikuta akishangaa kidogo lakini akaupotezea mshangao wake kwa haraka.
“Sir , nitaenda kukuletea Menu haraka , nisamehe kama nimekuwa mkorofi”Aliongea yule mhudumu , alikuwa amesikia vizuri Hamza na kumuelewa kwani alikuwa ameongea kifaransa kilichonyooka , na matamshi ya Hamza kwa uzoefu wake aliona hata yeye hakuwa vizuri , hivyo hakutaka kuleta ujanja tena wa kuongea kifaransa mbele ya mtaalamu wa lugha hio.
Dakika chache tu Menu ililetwa na Hamza alitoa oda yake kwa kutumia lugha ya kifaransa na kisha akamgeukia na Regina.
“Regi, una agiza nini , nadhani uonje Oulesarinires , desert , Clafautis …. na kuhusu kinywaji nadhani itakuwa vyema kama ukitumia mvinyo wa Ubelgiji usio na kilevi , lakini nadhani hawauzi hapa , unaweza kutumia tu mvinyo mweupe..”Aliongea Hamza kama vile yeye ndio aliekuwa mwenyewe na aliowakuta ni wageni.
“Sir unao uelewa mkubwa na vyakula vya kifaransa, unapendelea kula mara kwa mara nini?”Aliuliza yule mhudumu akishangaa kidogo kwnai muonekano wa Hamza ulikuwa tofauti na matamshi yake.
“Haha.. nakuaje mara kwa mara wakati mimi masikini tu , ni kwamba tu nina mazoea ya kusoma soma vitu ndio maana..”
Baada ya kuongea hivyo ilimfanya kila mmoja sasa angalau kuelewa , huku wakijiambia hakuna uwezekano masikini kama Hamza kuwa na uelewa wa vyakula vya kifaransa.
lakini upande wa Regina yeye alikuwa tofauti , hakushawishika kabisa na maneno ya Hamza , alijiambia hata kama ni kweli anaweza kusoma kuhusu vyakula vya kifaransa katika vitabu , vipi kuhusu rafudhi yake namna anavyoongea kifaransa , swala la mtu kujifunza lugha nyingine halikuwa jepesi mno na lilihitaji muda tena wa kuishinda ni ya mazingira ya wazungumzaji wa kifaransa.
Kitu kingine ambacho kilimfanya Regine asiamini ni namna ambavyo Hamza hakuwa na wasiwasi wakati wakuingia ndani ya mgahawa huo , ilionekana ni kama vile maeneo hayo hayakuwa mageni kwake.
Kwa namna moja Regina aliona mwanaume ambae ni boyfriend wa maigizo alikuwa ni mwenye kushangaza kiana.
Baada ya kaupepo kale kupita , hatimae chakula kiliwekwa mezani na kila mtu kuanza kudili na sahani yake , lakini kwa Mzee Wilsoni alionekaa bado dukuduku lake juu ya Hamza haikuisha.
“Mr Hamza umejifunzia wapi kuongea kifaransa?”
“Ah , mimi ni mwanachuo mwaka wa mwisho , na wakati wa masomo yangu A-Level niliongeza somo la kifaransa kama la ziada , tokea hapo nimekuwa nikipendelea kuongea kifaransa”
“Kwahio kumbe wewe bado ni mwanafunzi , nilijua pengine ushahitimu kutoka vyuo vya ufaransa ndio maana rafudhi yako kuwa nzuri kumbe bado unasoma , ngoja nikuambie ukitoka hapa achana kabisa na Regina , naweza kukupatia hata kiasi kikubwa cha pesa”Aliongea Lamla.
“Mama .. sihitaji kabisa pesa zako , najua kwasasa mimi ni masikini lakini nina nguvu ya upambanaji , nitahakikisha natafuta pesa ya kumtunza Regina kwa mahitaji yake yote atakayotaka”Aliongea Hamza.
Upande wa Regina licha ya kujua Hamza alikuwa akiongea hivyo kimaigizo , lakini hakuacha kuona aibu kidogo kwani ni kama vile kauli ile ilikuwa ikimaanisha ukweli.
“Unadhani ni kiasi gani unachoweza kupata kumhudumia Regina , hivi unajua ni bilioni ngapi kampuni ya Dosam inatengeneza kwa mwaka , unamiliki nini mpaka sasa , hata ufanye kazi kwa miaka mingapi sio rahisi kufika katika daraja ambao tumefikia…”Aliongea Lamla kwa dharau.
Hamza mara baada ya kauli ile alilipiza kwa kumvuta Regina kwake na kisha akambusu kwenye shavu kwa sauti ‘Pop’.
Regina aliekuwa bize akijipatia chakula chake alishindwa kuelewa hata tukio lilivyotokea , kwani kitendo chake cha kuzubaa tayari alikuwa amepigwa busu.
“Kila kitu sio pesa , Regina ni zaidi ya pesa”Aliongea Hamza huku akicheka.
Regina alitaka kumpiga ngumi Hamza , lakini mara baada ya kukumbuka alikuwa kwenye maigizo alijikuta akivumilia kwa kile alichofanyiwa, ijapokuwa alikuwa na hasira lakini uzuri wake ulimfanya aonekane kama mwanamke ambae anaona aibu kwa kubusiwa mbele ya wazazi wake.
“Paah!!”
James aligonganisha glasi ya mvinyo kwenye meza na kisha akasimama.
“Vizuri , vizuri sana ..”Jamaa huyo mara baada ya kuona mrembo Regina akibusiwa mbele yake alikosa kabisa uvumilivu , aishindwa kumuaibisha Hamza kupitia mhudumu lakini vilevile alikuwa amesababisha mchumba wake mwenyewe kubusiwa , hivyo alishindwa kabisa kuendelea kuvumilia.
“Mzee , Madam kuna kitu napaswa kwenda kushughulikia , hivyo nitatangulia , tutaonana siku nyingine”Aliongea na baada ya hapo alizipiga hatua lakini kabla ya kutoka nje kabisa alimwangalia Hamza kwa chuki kali mno.
Regina alikuwa na hasira na Hamza lakini mara baada ya kuona sura ya hasira ya James alianza kuona wasiwasi juu ya usalama wa Hamza
Waziwazi wa Regina mara baada ya kuona kitendo cha Regina , mtoto ambae hajawahi kuwa na boyfriend maisha yake yote kukubali kubusiwa mbele yao walijua lazima ni kweli atakuwa kwenye mahusiano hivyo hakuwataka kuendelea kuongea na mara baada ya chakula waliondoka wakiwa hawana furaha.
Upande wa Hamza alimshika mkono mrembo Regina na kwa kujiamini kabisa waliingia katika lift.
Kitendo cha kuingia kwene lift tu Regina alitaka kumchapa Hamza kibao lakini Hamza alimuwahi na kuudaka mkono wake.
“Regina , unataka kufanya nini?”
“Nani kakuambia unibusu?”Aliuliza mwanamke huyo huku akionekana kama mbogo, katika maisha yake hakuwahi kufanyiwa kitendo cha namna hio na mwanaume bila ya ridhaa yake.
“Sijakubusu , nilichofanya ni kuigiza kukubusu shavuni , kuna haja gani ya kuonyesha hasira , isitoshe hii ni kazi yangu , unadhani ningewaaminisha vipi wazazi wako waliokuwa wakiniita mtu wa maigizo?”
“Mkataba unaeleza wazi kabisa , kama kuna haja ya sisi kufanya migusano ni mpaka nitoe ridhaa , kwani hukusoma vipengele?”Aliongea kwa hasira ,Ukwei Regina alikuwa akijiuliza vipi kama pela angegeuka bahati mbaya , pengine wangeishia kugusanisha lipsi na alizidi kukasirika.
“Hukuelezea kwenye mkataba wa kazi kama unamchumba tayari , umenileta hapa na kufanya watu waanze kuwa na chuki na mimi , hivi unadhani walivyokuwa wakinifanyia ni vizuri?, nilikubusu kuwakomoa pia”Aliongea.
“Wewe..”Regina aliishia kutoweza kuongea zaidi , aliona ni kama kweli lilikuwa kosa lake.
Lakini yote hayo alifanya kwasababu ya usumbufu wa James kwake kutumia wazazi wake kutaka afungishwe ndoa , ndio maana akafikia uamuzi mgumu , lakini haikuwa hivyo tu ili kutii masharti ya urithi alioachiwa na kutunza siri ya ugonjwa wake.
Moja ya sharti la urithi wa kampuni alilopewa Regina katika wosia wa babu yake ni kuolewa ndio atakuwa mrithi kamili wa kampuni ya Dosam , na kama hatokidhi kigezo hicho ndani ya miaka kumi basi baba yake angekuwa mrithi wa mali za familia.
“Unaongeaka hata wewe unamjua yule James sio mtu mzuri , nilitaka kumuaminisha wewe ni mpenzi angu , ili akuache , mtu kama yule huwezi kumkataa kwa maneno tu , kwa urembo wako kama huu hawezi kukata tamaa kirahisi labda tu umwaminishe umeolewa na si vinginevyo”
“Sidhani kama ni kweli , kuna wanawake warembo sana , anachotaka yeye ni mimi tu kwasababu kampuni yake haifanyi vizuri kwa miaka mitatu mfululizo na anashindwa kushindana na mimi likija swala la mauzo , anachotaka ni mimi niolewe nae ili kuimeza Dosam”
“Wazazi wako hawajuia juu ya hilo?”
“Sio swala jepesi kukuelezea na hupaswi kujisumbua pia juu ya hili”Aliongea na kisha alirudia ukauzu wake na ndani ya dakika chache tu walitokea katika maegesho ya magari.
“Unajua kuendesha gari?”Aliuliza Regina na kumfanya Hamza kushangaa maana alikuwa ashajidaa kuondoka zake lakini ilionekana bosi wake alikuwa na mipango mingine na yeye.
“Najua ndio ila sina leseni”
“Kuna taarifa ya kikao nataka kuindaa na nimechelewa , nisaidie kuendesha mpaka ofisini kwangu”Aliongea.
Hamza hakuwa na hiyana , hata hivyo ni kama ashajiuza kwa pesa taslimi kwa mkataba hivyo hakuona haja ya kukataa.
Hamza alitoa gari hio kwenye maegesho huku akipewa onyo asiendeshe kwa spidi kubwa na alitii , safari nzima mrembo huyo alikuwa bize na Ipad yake akionekana kufanya kazi akiwa hana habari kabisa.
Hamza alikiri mwanamke huyo alikuwa na ukauzu sio wa kawaida , pengine ndio maana hakuwa na boyfriend mpaka akatangaza ajira.
Wakati Hamza akiingia Morogoro Road macho yake yalicheza mara baada ya kugundua gari alioona wakati wakitoka kule hotelini ikiwa ipo nyuma ya na aliishia kutoa tabasamu hafifu na kujiambia tayari ashayakoroga lakini hata hivyo ni kama hakuwa na uhakika kama alikuwa akifatiliwa yeye au alikuwa akifatiliwa Regina.
Hakutaka kujali wala kuwapoteza , aliendesha gari polepole mpaka maeneo ya mawasiliano sehemu ambayo makao makuu ya kampuni ya Dosam hupatikana.
Jengo la makao makuu ya Dosam lilikuwa likivutia mno , lilijengwa kwa usanifu wa hali ya uu na ilikuwa ni fahari ya macho kwa eneo hilo, ilikuwa refu kwenda juu kwa ghorofa arobaini. Hivi na lote lilitumika kwa kampuni , ilikuwa ni kama ishara ya jinsi kampuni ya Dosam ilivyokuwa kubwa.
Hamza mara baada ya kuingiza gari hio katika maegesho kwa maelekezo ya Regina mbele yake aliona mwanamke ambae alikuwa amesimama kikakamavu katika eneo la maegesho , ilikuwa ni kama vile alikuwa akiwasubiria na huyo alikuwa tofauti na aliekutana nae kule hotelini wakati wa usaili.
Kwa macho ya haraka haraka tu , Hamza aliamini mwanamke huyo atakuwa ni bodigadi kama ambavyo Regina alisema alikuwa na bodigadi.
Mara baada ya kusimamaisha gari mwanamke yule kikakamavu kabisa alisogelea gari hio na kisha akafungua mlango wa abiria akimpa nafasi Regina kutoka.
Hamza alijikuta akiangaliwa kwa macho ya kikauzu na mwanamke yule mara baada ya kushuka kwenye gari hio , ilikuwa ni kama vile mwanamke yule anataka kummeza na hata pale alipotaka kumsogelea karibu Regina alizuiwa kwa mbele jambo ambalo lilimfanya Regina kutabasamu na kujiambia huyu mtukutu mbele ya bodigadi wake hawezi kumchukulia faida.
Kwa kumwangalia mwanamke huyo licha ya kwamba alikuwa na sura ya kirembo iliofichwa na ukakamavu wake , lakini ilioneysha alikuwa na mazoezi makali ya kijeshi.
Hamza alikuwa na uwezo wa kuona namna muunganiko wa mwili wa mwanamke huyo ulivyokuwa sahihi.
‘Yonesi Dustani’ Secirity team leader’ ndio jina ambalo lilisomeka kwenye kitambulisho chake.
“Yones hali ya Eliza ikoje?”Aliuliza Regina.
“Madam CEO , sijui nini kimetokea lakini leo amefika Amosi na kuomba msamaha kwa Eliza na kuahidi deni lake kwanzia muda huo limeisha”Aliongea Yonesi na kumfanya Regina kushangaa.
“Kwanini wabadilike wakati katika ile vidio walionyesha kumdhalilisha Eliza kiasi kile?”Aliongea Regina na kauli yake ile ni kama sasa ilimfanya Hamza kujua kinachoendelea.
“Hata mimi nimeshindwa kuelewa ,vipi tuendelee kuwachukulia hatua kama ulivyotoa maagizo?”
“Kama wameahidi kutokumsumbua tena , haina haja ya kwenda mbali , isitoshe wanaonekana kuwa na mtu nyuma yao, nitaongea na Eliza”Aliongea Regina na Yonesi alitingisha kichwa na muda uleule Regina alimgeukia Hamza.
“Utaishi nyumbani kwangu kwanzia leo hii na kuendelea , kama una mizigo nitamwagiza Yonesi kukusindikiza”Aliongea.
“Nini , unataka tuishi pamoja?”Aliuliza Hamza kwa mshangao.
Hata yule mwanamke aliefahamika kwa jina la Yonesi alikuwa katika mshangao pia, hakutaka sana kujali maisha binafsi ya bosi wake lakini ilikuwa ngumu kwa mwanamke wa hadhi ya juu kama Regina anaweza kukubali kuishi na mwanaume wa kawaida kama huyo na alijiuliza ni nani.
Mara baada ya Regina kusikia neno kuishi pamoja muonekano wake ulibadilika na akavuta pumzi nyingi za masikitiko.
“Ulinzi nyumbani kwangu ni mzuri , hivyo angalau kwa muda hamia , unachokifikiria hakipo”Aliongea
Hamza mara baada ya kusikia kauli hio kavu kiasi flani alijisikia vizuri na kuona kwamba mwanamke huyo alikuwa akijali usalama wake, isitoshe alikuwa tayari ashatengeneza maadui kwa kutangazwa kama boyfriend , ijapokuwa aikuwa feki lakini watu wale walimchukulia siriasi.
“Yonesi naomba umsaidie kumpa ulinzi huyu mtu , yupo kwenye matatizo , nenda nae anapoishi na mchukue mzigo yake na kisha umpeleke nyumbani kwangu , Aunt Maliposa atajua cha kufanya”Aliongea Regine asitake kumpa nafasi Hamza kuropoka tena.
“Sawa, Madam”
Licha ya kwamba alikuwa na wasiwasi pamoja na kusita lakini alitii maagizo ya bosi wake.
Hamza aliona namna ambavyo Regina aliongea kibosi , lakini kwasababu ilikuwa ni kwa ajili yake aliona haina mbaya kuishi kwake licha yeye kama mwanaume hakutaka kuishi kwenye nyummba ya mwanamke.
“Hey ,Acha ndoto za mchana , ingia garini”Yonesi aliongea kwa kufoka.
“”Hey Mjeda , niite Hamza tu inatosha , siitwi Hey”
“Unaishi wapi ?”Aliuliza hata asimjai Hamza.
“Gongo la mboto Kivule”Aliongea Hamza na kumfanya Yonesi kumwangalia Hamza na mavazi yake ya kisasa kabisa ya bei ghali na alijikuta akikunja ndita.
“Mh , unaishi huko uswahilini kweli?”
“Yeah kunaweza kuwa uswahilini , lakini ndio ambako kodi ipo chini, nilipanga nikitoboa kimaisha naja kwenye maeneo ya kifahari, usiangalie sana mavazi yangu , Regi ndio ambae ameninunulia , sio za kwangu”AliongeaHamza akijihami.
******
Saa saba mchana Frida alionekana akiingiza gari ndani ya hospitali na taasisi ya kitafiti ya Neuroscience inayopatikana Kibaha , kilomita kadhaa kutoka ilipo hospitali ya Tumbi.
Ilikuwa ni hospitali kubwa mno na ya kisasa yenye jengo moja lililoenda hewani kwa ghorofa kumi kumi na nane hivi na kufanya kuwa jengo refu zaidi ndani ya mkoa wote wa Pwani.
Hospitali hio ilijengwa kwa msaada wa watu wa Marekani kupitia shirika na taasisi isiokuwa ya kiserikali ifahamikayo kama Haliz Neuroscience Foundation(HNF).
Taasisi ya Haliz ilisifika dunia nzima kwa kujikita zaidi katika kuutafiti ubongo na maswala ya neva kwa ujumla wake , sera ya taasisi hio ilikuwa ni kuwezesha mataifa mengi kujifunza namna mfumo wa ubongo na neva unavyofanya kazi na hii imechangia sana kufungua matawi yake mengi karibia nchi nyingi duniani.
Mashirika ya Afya ya umoja wa kimataifa yalikuwa yakiunga mkono kazi kubwa ambayo ilikuwa ikifanywa na taasisi hii kubwa ya kimarekanni isiokuwa ya faida(Non-profit organisation).
Katika miaka ya hivi karibuni maendeleo ya sayansi ya neva na ubongo yalikuwa yamepiga hatua kubwa sana , wale wagonjwa ambao walikuwa wamepoteza kumbukumbu ilikuwa rahisi kurejeshewa kumbukummbu zao ndani ya muda mfupi tu chini ya taasisi hii ya Haliz.
Haikuwa wagonjwa waliopoteza kumbukummbu tu , watu wengi ambao walionekana kusahau mambo muhimu katika maisha yao , iwe ni kubukumbu za utotini au za ukubwani taasisi ya Haliz ilikuwa na teknolojia ya tiba ya kurahisisha hayo yote.
Licha ya taasisi hio kufanikiwa lakini bado utafiti wa kuujua ubongo wa binadamu ulikuwa ukiendelea zaidi , kwani wanasayansi wanaamini ubongo uwezo wake ni mkubwa kuliko ile ambavyo inadhaniwa , hivyo wanaamini kuuwezesha ubongo kufikia uwezo wake kamili kimatumizi italeta maendeleo makubwa.
Frida alitembea kwa kujiamini kabisa ndani ya hospitali hio huku akipokelewa na harufu ya taasisi hio yenye kuzoeleka katika pua zake, kwa namna baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hio walivyokuwa wakimsalimia kwa kutingisha vichwa ilionekana alikuwa ni mfanyakazi mwenye cheo.
Aliishia kutoa tabasamu huku akitingisha kichwa kwa kuonyesha tabasamu kwa baadhi ya watu aliopishana nao ndani na ndani ya dakika kadhaa aliweza kuzifikia lift na kuingia ndani, lakini kabla hata ya mlango wa lift haujajifunga mwanaume mzungu wa makamo alievalia koti la kimaabara aliweza kuzuia lift hio na kuingia ndani.
Alikuwa ni mtanashati kweli aliependezeshwa na miwani ya macho , huku akiwa amepambwa na tabasamu.
“Well!. Fancy meeting you here, Frida”Aliongea yule mzungu na kumfanya Frida kutoa tabasamu.
“Una ajenda gani kukimbilia lift Blake, huu si muda wako wa kufanya Demostrations na wanafunzi?”Aliuliza Frida na kumfana Blake kutoa kicheko kama anakohoa.
“Ndio nimemaliza, kulikuwa na mabadilishano na Dr John , Vipi wewe ndio umekuja kutubariki na utaalamu wako?,nilidhani upo likizo?”
“Nipo likizo ndio , lakini haimaanishi sipaswi kufika hapa , nina biashara katika floor ya kumi na saba”
“Wow!, Wow! , Floor ya wabobevu, sina neno la kuongezea, it’s nice to see you Frida”Aliongea Dr Blake na ni muda uleule Lift ilisimama katika floor ya kumi na bwana huyo mzungu alitoka akimuacha Frida kuendelea na safari yake.
Frida aliishia kutoa tabasamu tu huku akiangalia namna ambavyo Blake anapotelea kwenye macho yake wakati lift ikijifunga.
Haikuwa kama ambavyo amesema Frida kwani mara baada ya lift kufika katika foor ya kumi na saba alitoka katika lift na kuingia katika floor hio ambayo ilikuwa na utulivu wa hali ya juu , ilikuwa ni ubaridi tu na harufu ya kuvutia , huku rangi ya taa zisizokuwa na mwanga mkali zikipendezesha eneo hilo.
Frida hakuingia ndani ya Foor hio bali alizunguka upande wa kushoto kwake na kuanza kupandisha ngazi kuelekea juu na ndani ya dakika chache tu aliweza kutokezea juu kabisa ya jengo hilo.
Licha ya kwamba alionekana kutembea kwa haraka, lakini kwa namna ambavyo alikuwa na spidi hakuonyesha hata kuchoka, alionekana kama aina ya wanawake ambao walikuwa na mazoezi makali.
Baada ya kutoka katika paa kabisa ya jengo hilo refu na kumfanya kuona mazingira ya mji wa Kibaha na baadhi ya maeneo ya Dar es salaam na Bagamoyo alivuta pumzi na kisha aliendelea kupiga hatua kusogea mbele.
Hali ya hewa haikuwa ya jua kali ,ilikuwa ni kama vile mvua ingenyesha muda wowote.
Mbele yake Frida alikuwa amesimama mwanaume alievalia suti ya rangi ya bluu akiangalia upande wa maeneo ya Dar es salaam kwa umakini mkubwa kana kwamba kuna kitu alichokuwa akitafuta.
Alikuwa ni mzungu kwa muonekao wa nywele tu na kadri Frida ambavyo alikuwa akitembea hatua zake zilionyesha hali ya kuwa dhaifu kiasi.
Kama ilivyo mwanaume yule alivyosimama ndio namna ambavyo Frida alienda kusimama katika ukingo wa jengo hilo na kuendela kuangalia upande wa mbele yake, ilikuwa ni kama vile anamwigizia yule mtu , na upande wa yule mtu hakugeuka kabisa ni kama alijua nani amefika hapo na kusimama pembeni yake.
“Any progress on KF-Target?”Aliongea yule mzungu kwa sauti nzito.
“We are almost there ,I’ve initiated a plan to bring him closer to me, his curiosity will ensure our swift entry into the next phase”Aliongea akimaanisha kwamba anakaribia kumaliza , na ameanzisha mpango wa kumuweka karibu , anasema shauku yake itawafanya waingie hatua inayofuata kwa haraka”
“Elezea”Aliongea.
“Nimemfanya anifanyie Delivery ya Viungo vya akili kutoka Binamu , uhakika ni kwamba atauliza maswali juu ya malipo makubwa yanayolipwa kwa ajili ya chungu kimoja kama njia ya usafirishaji, kwa kile nilichoona amevutiwa”
“A risky move”
“Calculated Risky Sir”Aliongea Frida kwa kingereza na jibu lake lilimridhisha.
“Vipi kuhusu wale wengine , namaanisha wanaoangalia kutoka mafichoni?”
“We are keeping eye on them , once we have what we need, they ‘ll be nothing more than loose ends”
“Endelea na kazi kwa umakini , hatuwezi kuruhusu kosa lolote”
“Umeeleweka”
“Sinagogi wanataka hii misheni kumalizika kwa haraka , siku zijazo utashughulikia na zaidi ya mtu mmoja katika tafiti yako , mategemeo makubwa yamewekwa juu ya hii sayansi mpya Frida ,natumaini kila kitu kitaenda sawa,Hatuwezi kuruhusu washindani wetu kupiga hatua kablsa yetu”
“Ili mradi malengo yanakuwa wazi , kila kitu kitaenda sawa , natumaini utakuwa vizuri kwenye kuwatoa wasiwasi”
“Kama ni hivyo tutaonana tena katika hatua inayofuata kujua maendeleo”Aliongea yule mwanaume na ilitokea kitu kama upepo tu kwani alipotea palepale na wala hali ile isimuogofye Frida ikionyesha ni jambo ambalo amezoea.
Comments