Reader Settings

Dina alipata ahueni mara baada ya kuona  Hamza hajakasirika , alifika hapo akiwa  na hofu mno, baada ya kushusha pumzi hatimae aliwageukia wale watu waliomchukua Hamza kwa kujifanyisha  ni  polisi.

“Nimewaambia nini  kuhusu kutojihusisha na maswala ya uhalifu  hasa kipindi hiki cha uchaguzi?”Dina alifoka kweli 

“Boss  sikujua  kama unafahamiana na huyu Hamza , kama ningejua ni Braza nisingeenda mbali  na kupokea  maagizo ya  Zefa haha..”

“Nani kasema  mimi  ni Braza kwako …”Aliongea  Hamza lakini  bwana aliefahamika kwa jina la Kidula hakutaka kujali kauli yake , bado alikuwa na chembe  za dharau kwa Hamza , ilikuwa ni kama anajiamini bosi wake hawezi kumfanya lolote.

“Boss ni kweli kabisa sikuwa  nikifahamu kama unamjua Hamza , tunaomba ututambulishe ili   swala kama hili lisije kujirudia?”Aliongea Kidula , wakati huo Zefa alikuwa kimya tu akiwa na wasiwasi.

“Hakuna hata mwenye thamani kati yenu  wa kumjua hapa”Aliongea Dina kwa dharau.

Ukweli ni kwamba huyo Dina mwenyewe hakuwa akimjua Hamza  ni hisia zake tu ndio zilikuwa zikimwambia  sio mtu wa kawaida ambae nchi ndogo   kama Tanzania inaweza kudili nae.

“Hamza , unataka tulimalize vipi hili swala ?”Aliuliza Dina.

“Hawa  watu wako sina shida  nao , hakikisha siku nyingine  hawajitokezi mbele yangu , kuhusu huyu nataka akiondoka hapa sio

mwanaume”AliongeaHamza akiwa  katika hali utulivu na kauli yake ilimshitua Zefa.,

“Mr Hama naomba tulimalize hili swala , kama ningejua  mapema nisingekuchokoza ,  nipo tayari kukupatia kiasi chochote cha pesa , naomba tusiende mbali”Aliongea Zefa.

“Sina shida  na hela zako , watu wa aina yenu  hamtakiwi kuwepo uraini kama sio kufa basi ni kifungo cha maisha,  lakini  hayo yote nimeyasamehe kwa kukupa adhabu ndogo”Aliongea aliongea na kumfanya Zefa kuzidi kuwa na wasiwasi.

“Dina.. Madam  boss , hebu fikiria mara mbilimbili, kundi  lenu hili ni la kihalifu  na mzee ni moja ya watu ambao wanafumbia  macho uhalifu uneondelea, ukinigusa mimi jua umeigusa serikali , najua jana nimekosea lakini  tunaweza kulimaiza kwa pande zote kutokuathirika”Aliongea Zefa.

“Haha.. haha….unasema  nikikugusa  nagusa serikali ..haha”

Dina alicheka  kicheko cha ajabu kweli na ilikuwa ni  ghafla tu  ashatoka aliposimama  na  kwa spidi kubwa alipiga hatua mbele  na kilichofuatia ilikuwa ni Kidula kushika shingo yake  huku akianza kutetemeka na ishara ya damu kumtoka eneo la shingonni zilionekana..

Ki ufupi ni kwamba alikuwa amekatwa eneo la shingoni  na hata haikueleweka mrembo huyo alitoa wapi kisu  lakini miondoko yake ilikuwa ni ya kuogofya mno.

“Nimerudia zaidi ya mara tatu sitaki kusikia swala la uhalifu  , hasa kipindi hiki cha uchaguzi lakini hakuna anaelewa ninachomaanisha kwa maneno , nadhani  hii ndio  itaonyesha ni kwa namna gani nipo siriasi”Aliongea Dina  na muda uleule Kidula aliondoka huku  akianza kuchezesha miguu  yake akipambania uhai.

Dina licha ya kuuwa hakuonyesha ishara ya hatia  hata kidogo , ilikuwa ni kama mtu alieua kuku.

Vijana wote waliokuwa ndani ya hilo eneo walirudi nyuma huku hofu  ikionekana katika macho yake.

“Hivi umesema  baba yako ni nani vile..?”Aliuliza Dina huku  akiangalia kisu  kilichokuwa mkononni kwake , ilikuwa ni kama anaangalia kuona kama  kuna damu yoyote imebakia  lakini hakukuwa hata na doa ikionyesha spidi yake ya kuua ilikuwa ya juu mno.

Kisu hicho kilikuwa kidogo mno kama vile vya  kufanyia  upasuaji , pengine ndio maana hakikuonekana  mkononi kwake  mpaka pale alipoua  mtu.

Zefa alianza kutetemeka huku akirudi nyuma kwa hofu, ule ujasiri wake wote ulimpotea  mara baada ya kuona namna ambavyo Kidula alikuwa akitapatapa kupambania uhai wake.

Dina hakuwa mwanamke mrembo  tena , alikuwa  ni muuaji  mwenye sura ya kirembo  ambae  huficha matendo yake  kupitia  biashara ya kuuza chai , sasa  Zefa  anajua kwanini mrembo huyo alikuwa akiogopeka  na kufanya kundi la chatu liwe na nguvu.

“Rudia kauli yako , umesema nikikugusa nimegusa nini…?”Aliuliza Dina mara baada ya Zefa kushikiliwa na moja ya   mwanaume  aliekuwa nyuma yake asizidi kurudi  nyuma.

“Naomba  unisamehe ,nitafanya chochote kile , naomba usiniue…”Zefa mara baada ya kuona hakuna dalili ya huruma kwenye macho ya mwanamke Dina aliamua kupiga magoti na kupasha viganja.

“Hamza  naomba unisamehe , sitomsumbua tena  Eliza , mkiniachia nitaenda kujisalimisha polisi kwa nilichomsababisia mama yake…”Mwanaume alipasha viganja na muonekano wa Zefa ni kama sasa ulimridhisha  Dina.

“Naweza kuonekana mwanamke mrembo na mlaini laini,  lakini hiko ndio ninachowapa walimwengu kuona ,  huku uhalisia wangu ukibakia siri, unadhani baba yako ana nguvu  ya  kuizima nguvu yangu  hapa nchini, kama ni hivyo  tutaona hilo kuanzia leo”Aliongea  Dina  na kisha alisimama.

“Kama hamtaki   yawakute kama yaliomkuta mwenzenu kiukeni maagizo yangu tena, hakikisheni  haondoki na korodani  hata moja na mtupeni barabarani  kisha nisiwaone hapa  wote muwe chimbo mpaka nitakapotoa maagizo mengine”

“Sawa Madam boss”

Vijana wale angalau hali ya ahueni iliwapata mara baada ya kuona wamesamehewa  na hawakutana na kifo kama ilivyokuwa  kwa  Kidula.

“Nadhani mnajua cha kufanya juu ya huu mwili , hakikisheni mnasafisha  kwa kufuata itifaki”Aliongea na  kisha  aligeuka na kumwangalia Hamza.

Upande wa Hamza hakuonyesha mshituko wowote , ilikuwa ni kama anaangalia kitu cha kawaida , pengine watu kwake kushuhudia kifo ni swala la kawaida ndio maana muonekano wake haukua na mabadiliko.

“Kwahio  hili ni kwasababu ya yule mwanamke tena…?”Aliongea  na swali hilo lilimfanya  Hamza kushangaa  na hakuelewa muda huo  Dina alikuwa na hasira au na furaha ilikuwa ngumu kuelezea muonekano wake.

“Ni bahati mbaya tu ilionifanya kukutana nae , ndio maana…”

“Huna  haja ya kujielezea  naelewa”Aliongea  huku  awamu hio akiwa na sura ya huzuni na kisha alimpita Hamza  na kuliendea gari  lake.

Hamza alikosa neno  lakini hata hivyo aliona anapaswa kumpeti peti mrembo huyo,  hivyo alimfuata haraka haraka  katika gari yake ya  Mercedenz  Benz  S600

Gari hio ilikuwa  ya thamani , japo sio sana lakini kwa mazingira ya Tanzania ni moja ya gari za bei ghali ,  uzuri wake zaidi ni kwamba hio gari vioo vyake havikuwa vya kawaida , ilikuwa kama gari  za mercedenz zinazoingia nchini lakini ilikuwa imetengenezwa kwa mfumo wa ki usalama  wa hali ya juu.

“Dina  usiwe hivi , mimi na Eliza sio kama unavyofikiria”Aliongea Hamza, alishajua  mrembo huyo ana taarifa zote  kuhusu Eliza ndio maana hakutaka kujizuia kumtaja jina  lake.

“Huna haja ya kuongea , kunikataa kwako kote kule  kumbe kuna mtu ambae  ushampenda tayari , haishangazi , moyo wako umejaa ndio maana nimekosa nafasi”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.

“Dina sababu ya wewe  kukosa nafasi ni kwasababu  tayari ushaujaza moyo wangu  muda mrefu tu”Kauli ile ilimshangaza sana  Dina.

“Kweli!!?”Aliuliza akiwa kama hajategemea kauli hio.

“Ni kweli , kama isingekuwa hivyo  unadhani kwanini asubuhi nilikutumia ujumbe  wa maandishi juu  ya kufuatiliwa na watu wako, ningekuwa sikujali  nisingehangaika ningewaua wote , lakini nikafikiria na kuona vipi kama nitawaua wote  utajielezea vipi mbele ya Umoja , ki ufupi ningekuingiza matatizoni na ungepokonywa uongozi”.Aliongea na kumfanya  Dina kufikiria hilo  na kuona inaleta maana na alijikuta akitabasamu.

“Mimi na yeye nani mzuri zaidi?”Ilikuwa zamu ya  Hamza kushangazwa na swali hilo.

“Bila shaka wewe ndio mrembo  zaidi”Aliongea

Hamza huku akimkonyeza  kichokozi lakini ilimfanya  Dina kucheka  vizuri na kwa jinsi alivyokuwa akionekana  utadhani sio yeye alieua mtu dakika  chache zilizopita.

“Unachojua ni kunichokoza tu muone, kama kweli unanipenda kama unavyyosema , kwanini hutaki hata kulala usiku mmoja kwangu  kama ulivyofanya kwake?, Au mimi sikuvutii kama yeye?”

“Naona  umefanya uchunguzi wa kutosha mpaka ukajua nimelala kwake”

“Nani kakuambia unipotezee , unadhani nitakaa chini 

tu bila kufanya chochote , nilitaka kujua  ni mwanamke wa aina gani huyo amekuteka”

“Sijakupotezea Dina unajua  nikwasababu…”Alisita.

“Sababu gani?”

“Ni kwasababu sina malengo makubwa ya kimaisha , nilichotaka ni maisha ya amani kuishi maisha ya kawaida , kuwa na  wewe moja kwa moja maisha yangu yatabadilika”Aliongea  lakini kauli ile palepale ilimfanya  mrembo huyo kubadilika.

“Ondoka mbele yagu”Aliongea  kwa kufoka

“Nimekosea nini?”

“Nimesema ondoka mbele yangu, sitaki kukuona tena”

“Dina kama nimekosea sema , acha kukasirika basi”

“Achana na mimi , kwahio  kwa macho yako  unaona kuwa na mimi kutakufanya ukose  amani kiasi cha kuyabadilisha maisha yako,Hamza umeniangusha sana leo”Baada ya kauli hio  palepale  mlango ulifungwa  kwa nguvu  na gari iligeuzwa na ikatolewa nduki.

Hamza aliishia  kuvuta pumzi  na kuzishusha huku akiwa ameshika kiuno, hakujua  kauli yake ingemkasirisha mno  Dina , eneo hilo lilikuwa mbali na muda umeenda na aliona hata  kipindi kishampita.

Aligeuka na kuangalia namna ya kuondoka hapo ndani lakini ile gari  ya Corolla iliokuwepo hapo ndani ilikuwa imepakia ile  maiti kwenye buti pamoja na  Zefa  aliekuwa amepoteza fahamu.

Hakutaka kuingia ndani ya gari hio ,  hivyo alitoka na kuanza kutembea wa mguu akiamini angepata usafiri  wa  daladala kurudi.

Kitendo cha kufika  kuipita  Bar iliofahamika kwa jina la  Jiteketeze  tu  gari aina ya subaru  nyeusi ilisimama pembeni yake  na kioo kilishushwa na  bwana mmoja mweye muonekano wa kihindi.

“Wapi Braza nikupe  lift?”Aliuliza yule bwana na kumfahya Hamza kutabasamu.

“Haina haja ya kujifanyisha wakarimu , wakati  ni wiki nzima sasa tokea muanze kunifuatilia, hamchoki tu?”Aliongea  na kauli ile ilimfanya  yule Mhindi kutoa tabasamu  na aligeuza uso wake nyuma  kana kwamba kuna mtu anamwangalia ndani ya gari hio.

“Uko vizuri , hatukujua kama ushatufahamu , unaonaje ukiingia ndani ya gari tukiongea kidogo?”

“Haina tatizo , nilikuwa nikitafuta lift hata hivyo?”Aliongea Hamza  na bila  ya kujiuliza mara mbilimbili alifungua mlango na kuingia ndani  na hapo ndipo alipoweza kuona watu wengine wawili wakiwa siti za nyuma , mmoja  alikuwa ni shombeshombe(Colored)  mwenye  nywele ndefu  kama rastafarians  na  mwingine alikuwa  ni mzungu.

“How did you discover us?”Aliongea kwa kingereza yule mweusi  mwenye rasta.

“Kuna hata haja ya kuuliza , mlilipa hadi vijana  waanze kunifuatilia  huku wakijifanyisha kucheza pooltable karibu  na ninapoishi , hii gari ndio iliokuwa ikinifuatilia juzi  nilipokuwa Morogoro road, kwa  rafudhi yako   inaonekana  umeishi sana visiwa vya Samar, kama sikosei kwa Tattoo  hio kwenye mkono wako mnatokea   katika kundi la wawindaji la Waray  kutoka mji usionekana wa Biringan”

Kauli ile ilimfanya  yule bwana aliesuka rasta kushangaa kidogo  na kuonyesha kuridhishwa na Hamza..

“Ni kama  tulivyosikia  sifa zako  za kutokuwa  binadamu wa kawaida,  haishangazi  ndio maana una urafiki na mtu mkubwa  kama Dokta Genesha” Hamza mara baada ya kusikia neno Dokta Genesha ni kama sasa ashajua nini kilichowaleta  Tanzania  kutoka  Ufilipino.

“Sijali mnachotafuta  wala mnachopanga , lakini  hamtakiwi kuwepo Tanzania”

“Umoja wetu wa wasionekana  unamtafuta  Dokta Genesha dunia nzima , ndani ya maabara ya Trishaza  tulikuta taarifa  zako  zote ikiwemo sehemu unayoishi  kwasasa , kitendo cha Trishaza wa Tembo  kuwa na taarifa yako inaonyesha ni kwa namna gani mna

ukaribu , swali letu  ni wapi  alipo  Trishaza  wa

Tembo?”

“Nadhani  kila mmoja anajua Dr Genesha alishafariki , hii sio siri  na hata kwenye vyombo vya habari  ililiripotiwa”

“Unachosema ni kweli , lakini hapa tunamzungumzia  Dr Genesha ambae ni Trishaza Wa Tembo , lolote linawezekana”

“Narudia tena mnaemtafuta alishakufa tena sio  kufa ameuliwa”Aliongea Hamza na wakati huo  sauti yake ilionekana kuwa siriasi.

Jamaa aliefamika kwa jiina la Mendoza , huyo  mwenye marasta  alimeza mate  na palepale  ni kama mwili wake ulianza kutuna  na nguvu isioonekana  ambayo haikuwa ya kawaida  iliongezeka.

“Kama  kweli amekufa , tunataka kujua kitabu  cha ufunuo wa Njiwa Juu Ya Mti Wa Uzima  kipo wapi .

je unajua alipokificha kabla  hajafariki au  kama  alikuambia itakuwa vizuri ukituambia?”Aliuliza  bwana mwingine  ambae alikuwa mzungu , huyo aliitwa Dodo.

“Mnachotafuta ni hadithi ya kufikirika tu  na hakuna ukweli wowote kuhusu uwepo wa hicho kitabu na sidhani kama kweli  kuna huo ufunuo wa Njiwa  juu ya mti wa Uzima”

“Acha porojo , taarifa tulizopata ni kwamba kabla ya  kufariki  kwa Dokta Genesha alitoa kauli kwamba   ya ‘wanachokitafuta hawawezi kukipata’ , unadhani alikuwa akimaanisha nini? ,  moja  kwa moja tunaamini  kuna mtu aliemuachia urithi na urithi huo ni juu ya kitabu hiko cha Ufunuo”

“Nadhani  hamuelewi na mnataka kulazimisha vitu ambavyo havipo , kwa hiari yenu  niachieni hii gari, nitahesabu mpaka tatu , sitaki kuona mtu ndani ya gari”Aliongea Hamza kwa sauti ya kibabe.

“Moja…, Mbili..”

“Tunaondoka”Aliongea  Mendoza Rastamani na aliwapa ishara wenzake  na kushuka katika gari.

Mara baada ya  wote kuondoka Hamza hakuchelewa  aliushika  usukani na kuondosha  gari hio kwa spidi.

“Dokta Genesha sikutaka kukuamini tokea mwanzo juu ya ulichoniambia, ila  kama sio shida yangu ya kutaka kumfahamu Mzee  nisingeendelea  kubaki na kitu ambacho kinanifanya niwe shabaha ya watu wengi.

Kazi imeanza , maisha ya utulivu  nishayaishi  ni muda sahihi wa  kuanza kumtafuta Mzee , nitafuata ushauri wako , kama  kuna ukweli wa  simulizi ya Njiwa juu ya Mti  wa Uzima  basi  malengo yangu yatafanikiwa”Aliwaza na muda huo  alifanikiwa kumkwepa mtoto aliekuwa akiendesha  gurudumu barabarani  na kumfanya mawazo yake yarudi katika uhalisia.

Dokta Raphaeli Genesha ndio jina lake, ni raia wa Ureno  ambae amechanganya rangi kwa kuzaliwa na baba wa kijapani na mama wa kireno.

Kabla ya  kutambulika  kwake kama mwanasayansi aliewaacha wanasayansi wenzake mdomo wazi  alikuwa  ni muumini mtiifu sana wa kanisa la kikatoliki.

Mara baada ya  kuishi katika misingi ya kiimani  kwa miaka mingi  ndipo  aliposhikwa na shauku  na shauku yake ndio ambayo ilimtambulisha  leo hii na pengine  kumsababishia kifo chake.

Huyu  ndio  mwanasayansi ambae alitoka hadharani na kusema kwamba  Spirituality is real  na anao uwezo wa kuthibitisha hilo.

Kauli yake  hio iliinua  mijadala mingi sana  kwa wanasayansi wengi duniani huku wengi wakienda mbali kwa kusema hilo ni swala ambalo haliwezekani kwani sayansi msingi wake ni majaribio na majaribio hayo sio juu ya namna  kitu kinavyofanya kazi bali ni sababu ya  kitu  hicho kufanya kazi  kwa kufuata mchoro wa tabia husika.

Ukweli ni kwamba  hata huo uthibitisho hakuwahi kuuweka wazi  lakini baadhi ya watu walianza kumuunga mkono  bila ya kuona ukweli husika , huku wale waliokuwa wakimuunga mkono ni kulingana na hisia zao  tu juu ya matukio yaliowapata yasioelezeka.

Miaka miwili mbele baada ya Dokta Genesha kutangaza  msimamo wake kama mwanasayansi ambae anaamini uwepo wa nguvu za kiroho  hatimae alikutwa na umauti na  ushahidi wa juu  ya  ukweli aliokuwa akizungumzia hakuweka wazi na stori yake ikaishia hivyo.

Ni sawa leo hii atokee mtu aseme anao ushahidi wa  kisayansi wa kuthibitisha  uwepo wa Mungu, ndio iliyokuwa kwa  Dokta Genesha.

Sasa kuhusu kuwa na ukaribu na Hamza haikueleweka ilikuwa vipi na historia yao ipoje  mpaka kuja kufatiliwa na  kundi la wawindaji kutoka visiwa vya Samar.

******

Dakika kadhaa mara baada ya Hamza kuondoka , wale watu  wote watatu walisogea upande wa barabarani na kuingia katika gari aina ya Toyota Crown nyeupe  , ndani ya gari hio kulikuwa tayari na mtu mwingine na ilionekana walikuwa wakimwambia kilichotkea.

“Umesemaje ,unamaanisha alikuwa akijua uwepo wetu tokea muda mrefu?”Aliuliza , alikuwa na sauti ya kike  hivyo ikiashiria ni mwanamke na mkononi alikuwa ameshikilia picha.

“Mbona anaonekana wa kawaida  sana ,  inawezekana amewapiga mikwara kuwaogopesha tu”

“Haiwezekani, anaonekana sio wa kawaida kabisa na ni mtaalamu, nilikuwa  karibu yake  lakini kila nilipo jaribu kuamsha uwezo wangu  wa kichawi  pumzi zilikuwa zikiniishia, anaonekana kuwa na mwili  dhaifu mno lakini sio wa kawaida, hisia zangu zimeniambia kama nitamshambulia kuna uwezekano wa kutopona”

“Uwezo wako  unachukuliwa kama wa juu ndani ya umoja , haiwezekani awe amekuzidi?”Aliongea  yule mwanamke.

“Kwahio vipi kama akiwa na uwezo wa juu , ijapokuwa  umoja wetu unachokuliwa kama daraja  B  lakini  kazi hii sisi ndio tumepewa  kwasababu  ilionekana tunao uwezo wa kuikamilisha , Tanzania inaonekana kama nchi tulivu sana ila kuna  mambo mengi yasioyakawaida  yanaendelea , tunapaswa kuwa makini  hasa nyakati za usiku”Aliongea Mendoza.

“Ila sidhani kama itakuwa rahisi  kupata uelekeo juu ya kitabu  hiki kilipo, mtu ambae ana urafiki na Dokta Genesha hawezi kuwa wa kawaida”

“Mbona kama tunaogopeshana , sisi ni  wawindaji   na sifa ya muwindaji hawezi kuacha kitoweo kupita mbele yake kirahisi , Tumekuja  mpaka Tanzania kwasababu ya kazi na  tunapaswa kuimaliza ili kuwa na maelezo ya kutosha mbele ya wakuu wetu”Aliongea Dodo.

“Kwahio   ni hatua gani  tuendelee nayo , ashatuona tayari hivyo atakuwa  ni mwenye tahadhari”

“Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi , kwasasa  kitu pekee  tunachoweza kufanya ili kupata taarifa kutoka kwake ni  kupitia watu wake wa karibu”

“Unamaanisha nini  Huda?”Aliuliza Mendoza  akimwangalia mwanamke aliekuwa mbele yake , alifahamika kwa jina la Huda.

“Mendoza umeshanielewa ninachomaanisha”

“Sidhani kama ni  wazo zuri  ila  kwasababu hatuna namna  na tunahitaji matokeo  tuendelee kumfuatilai kwa ukaribu , Udhaifu wake utaonekana na tutautumia vizuri”Aliongea  yule Mhindi na kauli yake iliungwa mkono.

***

Hamza  mara baada ya kutoka hapo  aliona haina haja ya kwenda chuo   na kwasababu  alikummbuka Regina alimpigia simu alijua kabisa alikuwa  akihitaji arudi  nyumbani hivyo moja kwa moja aliona aelekee huko  lakini kabla ya  hapo aliona kwanza arudishe gari aliokuwa akiendesha.

Gari hio ilikuwa na nembo ya kampuni ya  kukodisha magari  ya  DriveUs  na Hamza aliijua fika kwani ashawahi kukodi gari katika kampuni hio ,ilikuwa na makao yake Posta  lakini Hamza hakuona haja ya kupeleka gari hio Posta kwani  wenyewe walikuwa na mfumo wa kufatilia magari yao pale  aliekodishwa asiporudisha.

Dakika kadhaa  tu alikuwa ashafika Kigamboni na alitafuta eneo  na kuegesha gari hio katika megesho ya moja ya supermakert,  alitembea mpaka zilipo bodaboda na kisha alitoa maelekezo ya eneo analoelekea  na  alichukuliwa kuelekea huko.

Alikuwa na uhakika wa kumkuta  Shangazi nyumbani hivyo hakuwa na wasiwasi.

Dakika kumi  na tano zilimtosha  kufika kabisa , ukweli ni kwamba hakuwa hata na haja ya kupanda pikipiki  kutokana na ukaribu  wa mji wa Egret lakini kwasababu kulikiuwa na jua  kali  hakutaka kutembea.

Baada ya kushuka tu kwenye pikipiki na kubonyeza kitufe cha kengele  hatimae aliweza kusikia sauti ya furaha  ya shangazi kutoka ndani.

Mfumo wa nyumba wa kengele ulikuwa umeunganishwa na kamera  na  kifaa cha kusafirishia sauti na muda uleule mlango wa geti la kuingilia ulijifungua na akazama ndani.

“Hatimae  umerudi nyumbani , nilikuwa na wasiwasi mno “Aliongea Shangazi ambae alionekana kuwa na furaha  kabisa kumuona Hamza amerudi na mapokezi hayo yalimfanya kujihisi kuwa mwenye hatia ,  kwani   Shangazi alimchukulia Hamza kama mwanafamilia  ilihali alikuwa akiujua ukweli yupo hapo kwa muda tu .

Lakini sasa  wakati   Hamza  anataka kuingia ndani   sauti ya mwanamke anayoifahamu ilimwita.

“Hamza!,Unafanya nini hapa?”

Hamza alishangaa  maana hakutegemea , aliinua kichwa chake  na mara baada ya kuangalia eneo la sebuleni ndio sasa aliweza kumuona  Eliza akiwa amekaa kwenye sofa.

 

 

 

Previoua Next