SEHEMU YA 53
Tuliishia Bibi yake Regina ametembelea makao makuu ya kampuni na kuzidiwa Ghafla.
Endelea sasa.
Licha ya kwamba Mirium kuonekana amepoteza fahamu lakini ilionyesha ni kiasi gani alikuwa katika maumivu makali , uso ulipoteza nuru kabisa na ulikuwa umejikunja kana kwamba alikuwa akisikia maumivu makali.
Hamza mara baada ya kumuona mzee huyo alijua moja kwa moja ni vipindi vya mwisho mwisho vya ugonjwa huo na muda wowote anaweza kuondoka.
Lakini namna ambavo Regina alikuwa akilia na alivyowekewana ahadi na bibi yake kwa ajili ya kutoka nae Out , aliona kama akifa mapema Regina atakumbwa na majuto na huzuni kubwa , hivyo mara baada ya kuingia garini aliliendesha kama kichaa na ilimchukua dakika ishirini kufika hospitalini.
Mara baada ya Manesi kumchukua upande wa Regina alikuwa ni kama mpira ulioisha upepo wakati akikaa kwenye benchi.
Hamza alijua hata aongee neno la kumfariji halitokuwa na maana kwa muda huo hivyo na yeye alikaa pembeni yake kimya akimpa kampani.
Muda nao haukusimama,sekunde baada ya sekunde dakika zilisogea na hatimae usiku ukaingia.
Regina aliejichokea aliinua uso wake na kuangalia saa na hakuweza hata kujua muda umesogea vipi kwa kasi namna hio , kwani ilikuwa imetimia saa mbili kamili za usiku tayari.
Aligeuza uso wake na kumwangalia Hamza na alimuona kuwa na utulivu huku mikono akiwa ameikunja kifuani.
Hamza muda huo alikuwa ni kama sanamu kutokana na mkao wake , ilikuwa ni kama anaogopa kupiga kelele.
“Unaweza kutangulia ili uwahi chakula cha usiku kabla ya muda haujapitiliza”Aliongea Regina kwa upole huku macho yake yakiwa na majimaji kama mtu anaetaka kutoa machozi.
“Hata wewe hujakula chakula cha usiku bado”
“Sijisikii kula , huna haja ya kuendelea kubaki na mimi hapa , ninaweza kubakia mwenyewe tu”
Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha na kisha alishika bega lake.
“Kama umechoka unaweza kuegamia hapa , niwe feki au halisi bado cheo changu ni mpenzi wako”
“Haina haja , sijachoka hata hivyo”Aliongea huku akigeuka na kuangalia pembeni na kumfanya Hamza kuishia kutoa tabasamu kuonyesha kumwelewa na kisha aliegamia ukuta.
“Japo sina kumbukumbu za kutosha wakati nikiwa mtoto , lakini napata nusu nusu ya kumbukumbu za maisha yangu nikiwa mdogo , nakumbuka nikimuona mama yangu akiwa katika hali ya maumivu makali.. natamani kukumbuka kila kitu lakini bado nashindwa kuona kila kitu lakini licha ya kumbukumbu kidogo nilizokuwa nazo nahisi maumivu makali ambayo hayavumiliki kila dakika na saa ninapojiwa na kumbukumbu kuhusu mama yangu”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kumwangalia Hamza kwa shauku.
“Huna kumbukumbu zote za utoto wako?”Aliuliza Regina na Hamza alitingisha kichwa kukubali.
“Mama yako amekufaje , pia hukumbuki?”
“Sikumbuki kabisa ninachokumbuka ni hisia nilizopata na kumbukumbu chache za mama yangu kuwa katika maumivu makali mpaka kukata roho, sikumbuki zaidi”.
Regina alijikuta akishindwa kujizuia na kushikilia sketi yake , ijapokuwa alimuona Hamza akiongea katika hali ya utulivu lakini alijisikia vibaya katika moyo wake kusikia maneno hayo. “Ninachomaanisha ni kwamba najua ni hisia gani unazopita muda huu na nataka kukupunguzia mzigo”
Regina aliishia kuinamisha kichwa chake tu na hakuongea neno , upande wa Hamza pia hakuongea neno zaidi na alifunika macho yake akiwa ameegamia ukutani akisubiri.
Dakika kumi mbele aliweza kuhisi kitu kikiyagusa mabega yake na kumfanya afungue macho na kuangalia na hakuweza kujizuia kutabasamu mara baada ya kuona ni Regina aliejiegamiza kwake.
Regina alionekana kuwa na waswasi kana kwamba hakutaka Hamza kumwelewa vibaya.
“Usinifikirie vibaya , nimechoka kidogo tu”
“Ndio najua”
Baada ya hapo hakuna alieongea na walisubiria kwa namna hio mpaka lisaa lingine likapita na hatimae mlango wa cha ICU ulifunguliwa na bibi yake Regina alitolewa
“Dokta vipi hali ya bibi?”Aliuliza Regina mara baada ya kumkimbilia dokta na manesi waliokuwa wakimtoa bibi yake.
“Tumejitahidi kadri ya uwezo wetu lakini niseme tu hali yake ya inazidi kudhoofu kadri dakika zinavyosogea na muda wowote anaweza kuondoka, mnapaswa kujiandaa”Aliongea Dokta huyo wa kike wa makamo na kisha aliungana na kundi lake na kuendelea na safari
Regina aliishia kumwangalia bibi yake kwa huzuni wakati akitolewa ICU kwenda wodi za VIP.
Haikuchukua dakika nyingi na Shangazi alifika kutokea nyumbani na mara baada ya kusikia Mirium hana muda mrefu alijikuta akishikwa na huzuni.
“Baba bado tu hajafika?”Aliuliza Regina.
“Yupo mkoani kwa wakwe zake”Aliongea Shangazi akiwa katika hali ya huzuni kidogo.
“Oh..!
Regina alijikuta akikosa neno , ni kama alitegemea kitu kama hicho hivyo hakutaka kuwaza zaidi na kujipa matumaini hewa.
“Regina nitakaa hapa hospitalini kwa siku kadhaa na madam , inabidi mteseka kwa siku kadhaa wenyewe nyumbani”Aliongea.
Regina hakuwa na pingamizi , isitoshe alikuwa na majukumu makubwa sana ya kuendesha kampuni hivyo muda wa kukaa hospitalini ulikuwa ni mdogo mno.
Wakati huo Bibi Mirium ambae amewekewa Oksijeni aliweza kufumbua macho yake taratibu kivivu na kwa ukungu wa macho aliweza kuwaangalia watu hao watatu waliokuwa mbele yake.
“Regina …!”Aliita.
“Bibii!!”
Regina mara baada ya kusikia jina lake linaitwa alikimbilia kitandani kwa haraka na kwenda kushikilia mikono ya bibi yake huku akiwa ameinama.
“Bibi mimi hapa”Aliongea Regina huku akitabasamu.
“Mjukuu wangu nataka uniahidi kitu kimmoja…”Aliongea huku mikono yake ikionekana kumtetemeka na kauli yake ilimfanya Shangazi na Hamza kukunja sura kiasi maana ilionekana kabisa ni maneno ya mwisho mwisho.
“Bibi nakusikiliza , niambie tu.”
“Niahidi kwanza utafanya ninachokuambia”
“Bibi sijawahi kwenda kinyume na ahadi , bibi usiwe na wasiwasi nakuahidi”
“Hapo sawa .. nataka ufunge ndoa na Hamza hata kama ni ya serikali”Aliongea hatimae.
Dakika ambayo Regina aliyasikia maneno hayo macho yake yalichanua kwa mshagao huku uso wake ukiwa katika hali ya kutokuamini , ilikuwa ni kama vile nafsi imeuacha mwili wake.
Upande waShangazi alionekana kuwa katika tafakari ya kina huku akimwangalia Hamza.
Ijapokuwa Hamza aliikuwa ametegemea hilo lakini hakuamini bibi huyo atatumia dakika zake za mwisho kumtaka Regina kufanya jambo hilo.
Ukweli ni kwamba katika hali aliokuwa nao ilikuwa ni jambo lisilokuwa la kawaida kuongea , lakini ilionekana kutokana na uzoefu na ugumu mzee huyo aliopitia ndio maana akaongea hivyo.
Alionekana akijua hakuwa na muda wa kusubiri Regina aamue mwenyewe kuolewa na Hamza ndio maana alitaka kitendo hiko kifanyike kabla hajakata roho.
Upande wa Hamza na yeye alikuwa akimwangalia Shangazi na kwa jinsi alivyokuwa akimuona alijiambia tu lazima kuna maneno ambayo Shangazi ameongea kwenda kwa Bibi Mirium, isitoshe licha ya kumuonaShangazi kuwa kama mama wa nyumbani lakini siku ya kwanza tu kumuona alijua sio mtu wa kawaida.
“Bibi unapaswa kupumzika , unajichosha zaidi ukiongea”Aliongea Regina akitaka kuingilia anachotaka kusema bibi yake kwa mara ya pii.
Lakini Mzee huyo alimshikilia Regina kwa nguvu zake zote huku akijitahidi kumkazia macho, alionekana kuwa siriasi mno kile ambacho anataka Regina kufanya.
“Niahidi hapa hapa kama utakubali ninachokuambia”
Regina alijikuta akiingiwa na hisia mchanganyiko , ilikuwa ni hisia za maumivu , majonzi , kuchanganyikiwa, aibu na uoga.
Baada ya dakika moja ya ukimya aliishia kutoa tabasamu la kukubal.
“Nakuahidi nitafanya hivyo lakini swala la ndoa ni la makubalianyo ya watu wawili , Hamza anaweza asikubali”Aliongea Regina na kisha alimgeukia Hamza na kumpa ishara ya kukataa.
Hamza alimwangalia Regina namna alivyokuwa siriasi akimpa ishara za kukataa na alijikuta akisita kidogo.
“Mimi sina tatizo , nakubali ndoas”Aliongea
“Wewe..!!”
Regina alijikuta akifoka katika hali ya aibu na hasira kwa wakati mmoja huku akijimbia Hamza anawaza nini.
Bibi Mirium mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Hamza alijikuta akipandisha kifua na kukishusha kwa nguvu na kumwachia Regina, ilikuwa ni kama kila anavyovuta pumzi na kupumua ameongeza mwaka mmoja wa kupumua.
“Vizuri …nyie wote ni watoto wazuri na nataka kuwaona mkiwa pamoja kwa kifungo cha ndoa”
Hamza aliishia kuvuta pumzi huku akimwangalia Regina kwa kumuonea huruma , kumbukumbu za kile ambacho Yulia alimwambia kilimjia na aliona pengine ndio maana bibi yake Regina anafosi wafunge ndoa.
“Naenda kupunga kidogo upepo hapo nje , kama unataka tuongee utanikuta”Aliongea Hamza na kisha bila ya kujali alitoka nje mpaka eneo la maegesho ya magari na kwenda kuegamia kwenye mtende na kukodolea macho mwezi huku akionekana kuwa katika mawazo.
Alijikuta akiingiza mkono kwenye mfuko na kutoa simu yake na alienda upande wa namba za simu na alijikuta akiiangalia namba ya Eliza kwa muda na kisha alienda katika namba ya Dina na kuiangalia na alijikuta akirudisha simu mfukoni.
Swali lilikuwa moja tu , vipi kama kweli atafunga ndoa na Regina , Eliza atachukuliaje swala hilo? , si ataumia mno , vipi atakubali kuendelea nae , vipi kuhusu Dina.
Lakini jibu lilikuwa ni ndio, akimuoa Regina atamuumiza mno mpenzi wake Eliza , ni kweli hakuwa akimpenda Regina kiviile na pengine ni kutokana na kutokumjua kwake kwa muda mrefu , lakini mahesabu yake ni kama yalikuwa yakimwambia alimuona Regina kwanza kabla ya kumuona Eliza , pili Regina alionekana kuhitaji ulinzi mno kulingana na maadui zake pamoja na kile alichokifahamu kuhusu Regina kuwa na ugonjwa wa akili , haya yote ndio yaliomsababishia kusema ndio , lakini bado moyo wake ulikuwa mzito mno kila alipokuwa akimfikiria mpenzi wake Eliza.
Hamza alionekana kuwa na wasiwasi pia kwa wakati mmoja , hakufika Tanzania kwa ajili ya kufunga ndoa bali alifika Tanzania kwa ajili ya kumfahamu Mzee ni nani, wasiwasi wake hakujua katika misheni yake hio ni hatari za aina ngapi ataweza kupitia maana Mzee hakuonekana kuwa mtu wa kawaida.
“Kwanini umekubaliana na alichosema bibi?”Aliuliza Regina ambae alionekana kuwa katika hasira na kumfanya Hamza kumwangalia Regina kwa muda bila ya kutoa jibu , ni kama aikuwa akimchunguza lakini upande wa Regina alionekana alikuwa akitaka majibu.
“Kuna sababu gani ipi nyingine , nimeamua kujipandisha cheo kutoka kuwa Boyfriend mpaka kuwa Mume , naamini mshahara wangu utaongezeka mara mbili”Aliongea Hamza.
“Hebu geukia huko kwanza , sipo hapa kutaniana na wewe”Aliongea Regina huku akiona aibu kidogo.
“Hebu ingia kwenye gari tutafute eneo lolote tule chakula , hata kama njaa huna mimi njaa ninayo , tutaongea huku tunakula, sitanii”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfahya Regina kuingia ndani ya gari kihasira hasira .
Hamza hakujali ubora wa Mgahawa kwa muda huo alijali kushibisha tumbo lake tu hivyo aliendesha gari na kwenda kupaki katika Mgahawa mdogo tu lakini ulionekana kuwa na mazingira safi na ilikuwa bahati Regina hakuwa na pingamizi.
Mmiliki wa mgahawa huo pamoja na wafanyakazi wake mara baada ya kuona gari hio ya Lexus ambayo imekaa kama zile zinazoendeshwa na wanasiasia waliishia kumkazia macho Regina na mmoja ya wafanyakazi hao ni kama alimfahamu Regina.
Walishangaa maana mgahawa wao ulikuwa ni wa hadhi ya wateja wa kawaida na sio matajiri, isitoshe hawakuwa na vyakula vya aina nyingi.
Hamza mara baada ya kukaa aliuliza ni chakula gani kinapatikana na mhudumu alimwambia. “Vipi unaonaje tukiagiza Tambi na rosti ya mainu , unapenda?”
“Kwanini sipendi , dada niwekee hizo tambi na maini tu ila usiweke mchuzi mchuzi wenye vitunguu naomba na pilipili, pia utaniletea juisi ya embe ya Cereals”Aliongea Regina na kumfanya bosi wa mgahawa huo kutingisha kichwa huku akitoa tabasamu ni kama vile anaifurahia sauti ya Regina kama sio kumuonea wivu kutokana na uzuri wake.
Hamza alijikuta akinyamaza kimya, kwa jinsi Regina alivyochangamka ni kama alikuwa mzoefu wa migahawa ya namna hio na ilimfanya kumwangalia kwa tabasamu.
“Unaniangalia nini?”
“Sijakuangalia , ila kuna muda nakuona kama malaika uliemuasi Mungu”
“Unaongea upuuzi”Aliongea Regina huku akiona uvivu wa kujibishana na Hamza.
Dakika kadhaa waliletewa chakula na kutokana na njaa kila mtu alijikuta akiwa bize na chakula , muda huo Regina aliona midomo yake ilikuwa imejaa mafuta na kabla hata hajatafuta namna ya kujifuta Hamza alikuwa ashamchomolea tishu na kumpatia.
Regina aliishia kumwangalia Hamza kwa macho makavu kwa sekunde na kisha aliichukua ile tishu na kujifuta midomo.
“Ongea sasa kwanini umemkubalia bibi ilihali mimi sitaki”Aliongea Regina.
“Niongee nini tena , wakati kama huu bibi akiwa katika hali nzuri kidogo tunapaswa kwenda kujisajili na kupata cheti cha ndoa , isitoshe babe siwezi kubadili dini kwa ajili yako hehe”
“Acha kujipelekesha kimawazo , siwezi kuolewa na wewe”
“Lakini ushamuahidi bibi yako tayari na nimekubali mbele yake”
“Lakini wewe si una mpenzi wako?”
“Upo sahihi nina mpenzi na tupo hatua nzuri lakini hili lisikupe shida nitadili nalo mwenyewe”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha na muonekano wake ulizidi kuwa wa kikauzu.
“Ngoja nikuambie tu , mimi sijawahi kuamini maswala ya ndoa kabisa na tokea nikiwa mdogo nilijiapiza sitokuja kuolewa”
“Kwanini unasema hivyo , usiniambie ni kwasabqabu ya baba yako?”Aliuliza Hamza na Regina aliishia kuwa kimya kuonyesha ndio sababu.
Hamza alihisi kumwelewa Regina , isitoshe alikuwa ni mtoto wa nje ya ndoa.
“Sio kwasababu ya baba tu , ila nyie wanaume hamuaminiki kabisa , angalia kama wewe sasa hivi una mpenzi tayari na anaonekana kukupenda lakini bado unataka tufunge ndoa , unadhani ni kitu kizuri kwa mpenzi wako?”Aliongea Regina na kauli ile ilimfanya Hamza kutingisha kichwa kukubaliana nae.
“Nadhani sasa ushanielewa ninachomaanisha , hivyo achana na hayo mawazo kabisa , sina mpango wa kuolewa, kwangu mimi kuzikamilisha ndoto zangu naona kuna maana zaidi kuliko kuingia katika ndoa zilizojaa mateso” “Unadanganya?”Aliongea Hamza.
“Kwanini nikudanganye?”
“Namaanisha hunidanganyi mimi ila unajidanganya mwenyewe”Aliongea na kumfanya Regina kukosa neno lakini kushangaa zaidi kutaka kujua Hamza anachomaanisha.
“Kama kweli huamini swala la ndoa basi unao uwezo wa kuolewa na yoyote yule, sio mimi tu hata awe James , kuna msemo wa kingereza wanasema ‘The more you care the more you will
resist’ , kwa lugha nyepesi kama kweli ungekubali
kuolewa na mtu yoyote ili kumridhisha bibi yako basi ni kweli hujali na huamini swala la ndoa”
“Sio kweli”Regina alikataa na kumfanya Hamza kumwangalia Regina na macho ya ki uchunguzi kana kwamba anajairbu kuangalia kilichopo ndani ya moyo wake.
“Basi ngoja nikuulize swali?, kwanini siku hizi umeanza kujilemba , kwanini umekuwa makini sana na mavazi yako na kwanini muda mwingine unakua mchangamfu na muda mwingine unakuwa kauzu mbele yangu?”Aliuliza Hamza na kumfanya Regina uso wake kuwa mwekundu.
“Unadhani nafanya hayo yote kwa ajili yako?, nafanya kila ninachotaka”
“Kama ni hivyo kwanini ulikasirika mimi kutokurudi nyumbani usiku na ukakasirika zaidi kutokana na kutorudi na nguo ulizonipa , kwanini umenisamehe kirahisi vile baada ya kukupiga vibao , kwanini unaonyesha hali ya kunitegemea katika baadhi ya vitu?”
“Sija.. umenielewa vibaya Hamza”
Regina alijikuta akishindwa kuwa na neno sahihi la kuongea na alijikuta akikwepesha macho yake na Hamza , mapigo ya moyo yalikuwa yakimwenda mbio mno na kauli za Hamza kusema ukweli zimemfanya kuhisi hali ya kupaniki. “Regina!”Aliita Hamza na kumfanya Regina kumwangalia.
“Sikia kama kweli hujali ndoa basi hupaswi kuweka matarajio yoyote yae katika ndoa , kwasababu ndoa ni neno tu na hata cheti cha ndoa siku zote ni ushahidi tu wa kimaandishi , usidhanie kwasababu watu wanatambulika kama mke na mume na wanatambulika furaha wanayo au wanapendana, chukulia mfano baba yako na mama yako wa kambo, hivi unadhani wanafuraha kwasababu ni wanandoa?”
“Mama yako hakuwa ameolewa lakini alikuwa tayari kukuzaa ikimaanisha hakujutia kuzaaa na baba yako licha ya kutokuwa ndani ya ndoa , unadhani kama angekuwepo hai sasa hivi akikuangalia angejiona ni mwanamke mwenye laana kukuzaa nje ya ndoa?”
Maneno ya Hamza yalimfanya Regina machozi kuanza kujitengeneza katika mboni za macho yake.
“Tokea dakika ambayo mtoto anaanza kulia baada ya kuzaliwa moyo wake hupevuka palepale na hauna tofauti yoyote na wa mtu mzima , ili mradi una moyo na ni binadamu basi uwe ndani ya ndoa au nje ya ndoa haimaanishi kwamba huwezi kupenda, ndoa kama ndoa sio tatizo , tatizo ni watu , au nasema uongo?”
“Kupenda… kupenda… kwahio kwa mawazo yako unadhani nakupenda, hebu acha ukichaa wako”Aliongea Regina kwa hasira.
“Sawa unaweza kuniona kama kichaa na kunichukulia kama kichaa lakini kwa niaba ya kile anachopenda kuona bibi yako katika nyakati za mwisho wa uhai wake na kwa ajili ya wafanyakazi wote wa kampuni ya Dosam , tunapaswa kujiandikisha ili kupata cheti cha ndoa , kulingana na mtazamo wako hujali kabisa maswala ya ndoa na kwa mantiki hio kujisajili kama wanandoa haiwezi kukuathiri isitoshe utakuwa umepiga ndege wawii kwa jiwe moja , utamfurahisha bibi yako na utaikoa kampuni isiende kwenye mikono ya watu wasio na nia nzuri”
“Sitaki maswala ya ndoa fullstop”Aliongea Regina huku akigonga meza kabisa kutilia mkazo na kufanya baadhi ya wateja kumwangalia mrembo huyo na kujiuliza kuna nini mpaka kuonekana kuwa na hasria.
Regina hakuendelea kubakia ndani ya mgahawa huo , aliichukua mkoba wake na kuondoka haraka haraka
Hamza hakujali gharama ya chakula alitoa noti tatu za elfu kumi na kuziweka mezani na kumkimbilia Regina ambae alikuwa akilisogelea gari.
“Regina nitaendesha mimi?”Aliongea Hamza lakini Regina alimsukuma na kisha alifungua mlango wa dereva na kuingia.
“Sitaki kukuona tena , ondoka”
Regina alijihisi kuchanganyikiwa sio kwasababu
Hamza alikosea ni kwasababu kila alichoongea Hamza ulikuwa ukweli ambao alikuwa katika vita nao.
“Bosi umesahau funguo za gari ninazo mimi?” “Nipe funguo”Aliongea Regina mara baada ya kugundua hakuwa na funguo na anataka kuwa dereva.
Hamza mara baada ya kuona namna alivyokuwa siriasi aliishia kuzunguka upande mwingine na kuingia kwenye gari na kisha alimkabidhi ufunguo.
“Toka kwenye gari”
“Sitoki, kama nilivyosema kesho naenda kuaga ubachela”
“Wewe endelea tu kunichokoza”
“Nitakuchokoza mpaka uwe mke wangu”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba sio kama alikuwa akitaka sana kumuoa Regina bali aliona ndio njia pekee ya kumsaidia kwa wakati huo , ki ufupi hakuwa na jinsi na ili kufanya hivyo alitaka angalau kuonekana siriasi,ijapokuwa Regina anakataa lakini yeye ndio njia ya kutatua tatizo.
Regina aliishia kumwangalia Hamza kwa dakika kadhaa huku akijiuliza ni mkosi gani amejiingiza mpaka kukutana na Hamza, licha ya kwamba mwanzoni mpango wake ni kumridhisha bibi yake angalau kuwa na boyfriend feki lakini muda huo alijihisi kukosa amani kabisa, aliishia kuwasha gari na kulitoa ndani ya eneo hilo kurudi nyumbani.
“Regina mimi sio mtu mbaya ki hivyo , ukifikiria vizuri utaona nimekuokoa ulivyotekwa , hebu
fikiria stori inavyonoga mtu akisikia namna shujaa Hamza alivyomuokoa mwanamke mrembo katika mikono ya watekaji , hili kitalaamu tunasema ni Penzi la papo kwa papo”
“Tunalikaribia daraja la Kigamboni , unadhani nashindwa kulitumbukiza gari baharini na wote kupotea, wewe endelea kuongea”
“Damn .. acha kuniogopesha namna hio .. siongei tena”
Regina hakuwa mkataa ndoa bali alikuwa anaiogopa ndoa , ki ufupi wengi wanaosema ni wakataa ndoa mara nyingi wanaona aibu kusema wanaogopa ndoa.
“Usinikodolee macho angalia pembeni”Regina hakuweza kuhimili macho makali ya Hamza
Muda ambao Hamza anaangalia pembeni kama alivyoambiwa hisia mbaya zilimvaa muda uleule mara baada ya kuona pikipiki ambayo ilikuwa nyuma yao kwa muda mrefu.
Ilikuwa ni Ducat 1299 igales inayovuma kwa uwezo wake wa mbio na kusafiri kilomita nyingi, thamani yake ilikuwa sawa tu na BMW X3 au zaidi , sasa juu ya pikipiki hio kulikuwa na wanaume wawili ambao wamevalia helmeti nyeusi na kufanya sura zao zisionekane.
Kilichomfanya Hamza kuhisi hali isiokawaida ni kutokana na msisimko wa nia ovu ya kimauji iliowavaa watu wale ni hisia ambazo mtu wa kawaida hawezi kuzipata.
“Regina simamisha gari”Aliongea Hamza mara baada ya kuona usalama wao ndani ya gari ni mdogo.
“Unataka nini tena?”
“Kuna watu wanatufuatilia , haraka simamisha gari pembeni”Aliongea Hamza.
“Tunafuatiliwa…!”Regina palepale akili yake iliamka na kukanyaga breki lakini mara baada ya kuikanyaga uso wake ulifubaa.
Hamza palepale aligundua kuna kitu hakipo sawa na alimgeukia na kumwangalia.
“Nini tatizo?”
“Breki hazifanyi kazi”Aliongea Regina na kumfanya Hamza kukunja ndita na palepale alijua watu ambao wapo kwenye pikipiki mmoja wao ameshikilia kifaa kinachofanana na simu kwenye mkono wake.
“Wanatumia kifaa maalumu kudhibiti mfumo wa kielektroniki wa gari , naona wanatumia mbinu hii kutusababishia ajali ili ionekane ni ajali ya kawaida kabisa baada ya uchunguzi”
Comments