Regina mara baada ya kusikia kauli hio mikono yake iliokuwa imeshikilia usukani wa gari ilianza kutetemeka , isitoshe alikuwa msichana na ni ngumu kwake kuhimili mshituko wa namna hio
“Kwahio tunafanya nini , gari halipunguzi mwendo na tunakaribia mataa mbele yetu?”
Hamza alijikuta akiinua macho mbele na kugundua kweli mbele yao wanazikaribia Traffic light na magari ambayo yalikuwa yakitoka Kariako kwenda Mbagala yalikuwa mengi mno na pili katika lane yao kulikuwa na magari mbele yao ambayo pia yanapunguza mwendo , kama wakiendelea hivyo hivyo basi ni hakika watayagonga magari yaliokuwa mbele yao.
“Achia usukani , nitaendesha mimi rudi nyuma”
“Lakini siwezi kutoka hapa kirahisi”Aliongea
Regina lakini Hamza bila ya kuchelewa kwa
mkono mmoja alimnyanyua kutoka katika siti ya udereva na kumrushia katika viti vya nyuma ya gari , bahati nzuri gari yao iliikuwa SUV hivyo Regina hakujigonga na Hamza alimshika Regina makalio na kumsukumizia mpaka kwenye siti. “Aiyaaa… umenigusa wapi!!?”
Regina licha ya kujua yupo hatarini alishindwa kujizuia kwa namna Hamza alivyomsukumiza kwa kumshika kalio.
Hamza hakutaka kujali zaidi na alishika sterling kwa mikono yake miwili na kuweka umakini kwenye kuendesha.
Gari ilikuwa ikiserereka kwa spidi kubwa mno na Hamza alijitahidi kadri ya uwezo wake kuyakwepa magari na kwenda mbele zaidi kiasi ambacho alifanya madereva kuanza kupaniki, ilikuwa ni upepo tu aliokuwa akiacha kila alivyopokuwa akipita gari.
Jambo zuri aliweza kulikunja gari vizuri na kuingia katika barabara ya dharula na bahati ilikuwa yake maana aliweza kupita mataa bila ya kugongana na gari.
Kitendo cha kupita tu Hamza aling’ata meno kwa hasira na kisha alikanyaqga pedeli na kuongeza mwendo zaidi.
“Wewe umekuwa kichaa , kwanini unakanyaga mafuta?”Aliuliza Regina kwa kupaniki asijue Hamza anafanya nini
“Wale watu kwenye pikipiki wameshikilia rimoti na inafanya kazi kwa umbali wa mita ishirini mpaka arobaini hivi, hivyo najaribu kuwaacha kwa zaidi ya huo umbali ili isifanye kazi ndio maana nimeongeza spidi zaidi” “Kumbe! , wewe umejuaje sasa?”
“Wewe unadhani kama sina uwezo kwanini bibi yako analazimisha nikuoe?”Aliuliza Hamza na kumfanya Regina kugeuka yai.
“Ongeza umakini barabarani”
Kitendo cha kumaliza sentensi hio alichoweza kusikia ni sauti ya Ziii.. ziii..Ziii , gari ilikuwa imebadilika mngurumo wake na sasa ni kama ni mnyama aliekuwa akinguruma huku tairi zikisuguana na barabara.
“Argghh..!!”
Regina katika maisha yake hakuwahi kuwa katika hali kama hio , gari kwenda katika spidi ya hali ya juu mno na hakutaka kuangalia mbele zaidi ya kukizika kichwa chake
Uwezo wa Hamza wa kuendesha ulikuwa ni wa viwango va juu, baada ya kuingia katika daraja la Kigamboni aliongeza spidi zaidi kwa nguvu kabisa na gari ilichomoka kama mshale, mara baada ya kuangalia kwenye kioo alitoa tabasamu na palepale kwa nguvu alikanyaga breki na zilikubali.
“Creeek!!!”
Mataili ya magari yaliishia kuacha michirizi katika barabara ilioambatana na moshi , ilikuwa ni kama vile ndege inatua na hatimae aliweza kwenda kupaki gari pembeni mita kadhaa na daraja hilo katika stairi ya mshazari.
Kitendo cha gari kukanyaga breki na Hamza alivyoisimamisha gari katika mzunguko ilimfanya Regina kushikwa na kichefuchefu kikali , ijapokuwa mchakato wote ulifanyika kwa sekunde tu lakini ulikuwa sio wa kawaida kwake.
Wale watu kwenye pikipiki waliona hali sio nzuri na mpango wao ni kama umefeli hivyo kwa haraka waligeuza pikipiki wakidhamiria kukimbia.
Lakini Hamza hakuwa na mpango wa kuwaacha kabisa na alifungua mlango haraka na kutoka na kisha alianza kuikimbiza ile pikipiki na kadri alivyokuwa akikimbia mwili wake ulianza kubadilika.
Dereva wa ile pilipiki haikueeweka alikumbwa na nini lakini alijikuta akiyumba na kuisababisha pikipiki ile kuteleza na ikamshinda uzito na wote pamoja na aliempakia walidondoka chini na kabla hata hawajanyanyuka Hamza alikuwa ashawafikia tayari.
Muda huo hata Regina aliweza kutoka nje ya gari na kumkimbilia Hamza na kwenda kujificha nyuma yake.
“Nani kawatuma?”Aliuliza Hamza akiwa siriasi lakini yule dereva kwa utalamu alipiga sarakasi na kusimama na muda huo huo alichomoa Bunduki zile za kuwachomea sindano wanyama(Trangulizer gun) na kutaka kumfyatulia Hamza lakini Hamza alikuwa mwepesi mno kwani aliruka na teke na kumpiga kwenye mikono yake na kuifanya idondokee pembeni.
“Kama hamtaki kuongea nitawafanya muongee wenyewe”Aliongea.
Yule mwingine alionekana kuumia na alishindwa kusimama na Hamza aliamua kudili na yule aliesimama na kwa haraka alimsogelea na kumshika na kisha aliondoa ile helmeti na sasa aliweza kuona sura yake,alikuwa ni muafrika mwenye asili ya kisomali na alikuwa amevalia Heleni nyeusi.
Hamza alishangazwa na kitendo kile na kwa haraka haraka alimsogelea na yule mwingine aliekuwa akigulia maumivu na kutoa helmeti yake na wote kwa pamoja walikuwa wamevalia heleni japo yule mwingine alikuwa ni Mwafrika asilia.
“Nyie ni maninja kutoka kundi la Black Eared Snake!, inaonekana kuna watu kweli wamedhamiria kutuua”Aliongea Hamza akimaanisha watu hao ni kundi la maninja la Nyoka mwenye masikio meusi.
Kitendo cha Hamza kuongea neno hilo wale watu walijikuta wakishituka na kushangaa hawakuamini Hamza angeweza kuwatambua.
“Black Eared Snake ndio nini?”Aliuliza Regina.
“Ni kundi la maninja kutoka nchi ya CAR , ni kundi daraja C , ijapokuwa uwezo wa maninja wao hauwezi kuhesabika wa juu lakini wana mbinu nyingi za kusababisha mauaji , ndio kundi la kininja namba moja Afrika”Aliongea Hamza akimwelezea Regina kwa lugha nyepesi kwamba kundi hilo linatokea Afrika ya Kati.
Japo Regina hakuelewa maana ya kundi daraja C lakini alichojua muda huo hali ilikuwa ni ya hatari mno.
“Mmetumwa na familia ya Mzee Benjamini?”Aliuliza Regina.
“Usiulize maswali , ijapokuwa ni kundi daraja C lakini wanaongozwa na sheria kali za kininja , sheria kubwa ya ninja yoyote ni kutomtaja mwajiri wake”
“Kwahio tunafanyaje, tunawaacha waende?”
Hamza alifikiria kidogo na aliona asingeweza kuwaua wakati huo ambao Regina alikuwa mbele yake , alikuwa na uwezo wa kuwaua na kupoteza miili yao kimazingara lakini hakutaka maswali kutoka kwa Regina.
“Pigia simu polisi watakuja kudili nao”Aliongea Hamza na Regina alikubali lakini kabla simu haijapokelewa wale manijja walionekana kutafuna vitu huku wakiwa wamekaza sura.
Hamza hakutaka hata kuwazuia kwani aliona pia ni moja ya njia ya kutatua tatizo.
Dakika mbili tu wale manijja walitema damu nyeusi na kufariki palepale mbele ya Regina.
“Mamaaaa..!!!”
Regina alijikuta akipiga ukulele na pasipo ya kujua upande wa pili polisi alikuwa ashapokea simu yake.
“Hello , nini tatizo!!?”Hamza mara baada ya kuona Regina ameshikwa na mshituko alichukua simu na kutoa maelekezo kwa poilisi, upande wa pili wa polisi walionekana kushangaa maana ni kama hawakuwa wakiamini walichoambiwa , lakini hata hivyo walisema wanafika muda si mrefu.
Regina aijikuta akichuchumaa pembeni ya barabara huku akionekana ni kama ameshikwa na kichefu chefu.
Ilibidi Hamza kumsogelea na kisha alimshika bega kwa namna ya kumtuliza , mwanamke huyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuona mtu akijiua kwa staili hio hivyo ilikuwa haki yake kushituka.
Dakika chache baadae Polisi waliweza kufika eneo la tukio na kutokana na muda ulikuwa umeenda sana Hamza alimchukua Regina na kuingia ndani ya gari na kuanza safari ya kuelekea nyumbani .
Lakini sasa kitendo cha dakika chache tu za kuendesha sikio la tatu la Hamza liliweza kunasa sauti ya kitu kubip ndani ya gari , kama hakuwa mtu mzoefu asingeweza kugundua kitu hicho.
Ilikuwa ni bomu , ilionekana ndani ya gari lao kulikuwa kumetegwa bomu kama mpango B.
Hamza hakuwa hata na muda wa kumwambia Regina nini kinachoendelea na haraka sana alijifyatua kutoka katika siti yake na kuelekea upande wa Regina alipo na kumbeba juu juu akimtanguliza mbele yake , kitengo cha kufyatuka kwenye gari walisukumizwa na presha ya msukumo wa bomu na kwenda kutua kwenye majani upande wa pili wa barabara huku gari yao ikiteketea kwa moto mkubwa.
Kiikuwa kitendo cha sekunde chache mno kufanyika kuanzia kufunguliwa mkanda mpaka kutolewa nje ya gari na mlipuko kutokea na kuja kutua chini akiwa hajaumia.
Mlipuko ule uliyafanya masikio ya Regina kupatwa na ukiziwi wa ghafla na kengele za masikio kugonga , ilimchukua dakika kadhaa mpaka akili yake kurudi katika uhalisia.
Regina hakuamini alikuwa ameokoka katika mlipuko huo wa gari , Hamza angechelewa kidogo tu wangekuwa tayari ni maiti.
“Hamza… Hamza..!!”
Regina alijikuta akiita kwa nguvu mara baada ya kuzidi kulemewa na uzito wa mwili wa Hamza uliomlalia kwa juu , lakini licha ya kuita hakukuwa na majibu na alijikuta akimeza mate mengi na kujitoa katika mwili wake kwa kumsukuma pembeni..
Mara baada ya kuona mgongo wa Hamza machozi yalianza kumtoka bila ya kujua , aliweza kujua Hamza alitumia mwili wake kumkinga na presha ya mlipuko.
Regina alikuwa ameshikwa naBumbuwazi na maswali mengi yalipita katika kichwa chake na kujiuliza inamaana yeye ni wa muhimu mno kwa Hamza mpaka kujitoa kwa namna hio kumlinda.
Alijikuta akipotezea mawazo yale na kwa haraka sana alimtingisha Hamza kuamka.
“Hamza amka , nakuomba usife , fungua macho yako..”Regina alijikuta akipaliwa mpaka na mate na alijikuta akianza kutafuta simu yake ili kupiga simu lakini simu hakuwa nayo na alijikuta ni kama kuchanganyikiwa kumemvaa.
Dakika hio hio watu ni kama walisikia mlipuko huo na walianza kusogelea eneo hilo kwa kasi na Regina alianza kupiga kelele kuomba msaada.
“Regina..!!”
Alijikuta mwili wake ukimtetemeka mara baada ya kushikiliwa mkono wakati akitaka kuamka kwenda kuomba msaada lakini Hamza alionekana kuamka. “Nipo hapa , unaendelea , hali yako ikoje?”
“Mbaya sama nadhani siwezi kuishi tena”Aliongea kinyonge.
“Uisongee hivyo huwezi kufa , ngoja niombe msaada tukupeleke hospitalini”Aliongea huku akisimama.
“Haina haja , mpaka nikifika hospitalini nitakuwa nishakufa”
“Acha kuongea kuniogopesha, huwezi kufa”
“Namuona Israeli mtoa roho mbele yangu , Regina nisamehe siwezi kukuoa kama bibi yako alivyosema”Aliongea Hamza
“Hapana usife , umesema mwenyewe unataka unioe, huwezi kufa leo, kesho tunatakkiwa kwenda kusajili ndoa yetu , naomba usife jamani”
Regina hakujua hata maneno yanatokea wapi lakini aliona ndio mbinu ya kumbembeleza Hamza asipoteze uha.
“Upo tayari tuandikishe ndoa yetu?”
“Ndio nipo tayari .. please Hamza naomba usiniache..”Aliongea na alijikuta akianza kulia kwa kwikwi.
“Kwakuwa umekubali mwenyewe , basi nimeghairi kufa mpaka siku nyingine”Aliongea Hamza huku akimwangalia Regina na tabasamu la uchokozi.
Regina mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akimwangalia Hamza na kumkuta hakuwa na dalili yoyote ya kuonyesha yupo kwenye maumivu.
Hamza alikaa kitako huku akipangusa mikono yake na kumwangalia Regina huku akimcheka.
“Kwahio Regina kesho ndio siku yetu ya kuuaga ubachela sio?”
Regina alijikuta akiwa haamini alikuwa akichezewa akili na Hamza muda wote , kadri alivyokuwa akimwangalia ile huzuni aliokuwa nayo ilianza kubadilika na kuwa na hasira kali, alijikuta akiona kipande cha zege pembeni na bila ya kujiuliza mara mbilimbili alikichukua na kumlenga nacho Hamza kichwani.
“Holly shit!!!”
Hamza alijikuta akifyatuka kama mshale akikwepa kipande kile ambacho kilienda kutua mtaroni. “Hamza nitakuua …!!!”Aliongea huku akirusha ngumi za kike kwa hasira lakini Hamza aliishia kuidaka mikono yake na kumkumbatia kwa nyuma.
Shida halikuwa kumbatio tatizo ni mikono ya Hamza iliposhikilia katika eneo la kifua la mrembo huyo.
Hamza aliweza kuhisi kitu kilaini katika mikono yake na hakuweza kujizuia na kuuliza.
“Regina kumbe upo vizuri kiasi hichi”
“Wewe mpuuzi niachie”
Regina uso wake ulikuwa umeshika moto alitamani kujirusha kwenye mtaro.
“Sawa ila sijafanya makusudi”Aliongea Hamza huku akimuachia.
“Halafu kingine kwanzia kesho unakwenda kuwa mke wangu hivyo haijalishi wapi nina gusa” “Kafie mbali huko , siwezi kuwa mke wako”
“Umeahidi mwenyewe zaidi ya mara mbili kama nikiendelea kuishi tutaenda kujiandikisha , kama bosi wa kampuni kubwa sidhani ni vizuri kwenda kinyume na ahadi yako unatoa mfano mbaya kwa wafanyakazi wako”
“Umenitega kwa kunidanganya , niliongea vile nikajua unakufa kweli”
“Kama upo tayari kuoana na mimi wakati nakaribia kufa si vizuri zaidi nikiwa hai maana utafurahia zaidi matunda ya ndoa , hata hivyo tuachane na hayo kwanza hata nikikuelezea huwezi kuelewa nini maana ya Matunda ya ndoa”
“Wewe..!!”
Regina alijikuta akipiga miguu chini kwa hasira na kuanza kupiga hatua kurudi barabarani.
Ukweli ni kwamba alishasahau kabisa kama
walipata ajali ya gari lao kulipuka , ilionekana makusudi ya Hamza kumchezea akili yamemshushia presha kabisa ya swala zima la ajali.
“Mke unaenda wapi tena?”
“Naenda nyumbani”Aliongea Regina alijua hawezi kumfanya chochote Hamza hivyo hakuona haja ya kuendelea kujibishana nae , kuhusu maswala ya gari yao kulipuka aliona awaachie polisi wafanye kazi yao.
Dakika kadhaa tu wote waliweza kufika nyumbani na Regina mara baada ya kuingia ndani na kukumbuka Shangazi hayupo aliona ni kama kuna hali ambayo sio ya kawaida na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza lakini alishangaa kumuona amekaa kwenye ngazi akionekana kufikiria.
“Wewe unafikiria nini?”
“Nawaza namna ya kudili na hawa watu ambao wanatusababishia ajali kila siku , sidhani kama nisiposhughulika nao mapema wanaweza kuacha”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kumshangaa , dakika kadhaa zilizopita mwanaume huyo alionekana kuwa kama kichaa lakini sasa hivi amegeuka na kuwa siriasi.
“Kama unatengeneza hela nyingi jua kuna ambao hawana uwezo wa kutengeneza hizo hela , hivyo ni kawaida kuwa na maadui, nimejiandaa kwa vitu kama hivi ndio maana sipati shida hata vikitokea”
“Wewe unapaswa kuzingatia kufanya biashara na mimi nitazingatia namna ya kukulinda”
“Kwahio unapanga kufanya nini?”
“Regina hivi unadhani wale wajinga wametumwa na familia ya Mzee Benjamini au kuna maadui wengine ambao hatuwajui, sidhani ni swala la kawaida kukodi maninja hatari kama wale nje ya nchi kwa ajili yetu”
“Siwezi kujua ila familia ya James ndio maadui zangu wakubwa”
“Mpaka wameenda mbali kukodi majina kutoka Afrika ya kati!!?”
“Siwezi kujua kama kuna adui mwingine au lah”Aliongea Regina na kumfanya Hamza kutingisha kichwa.
“Usikurupuke kutaka kulipa kisasi , haijalishi una nguvu kiasi gani ni ngumu kushinda watu wengi”
Regina aliona swala la kuweza kuokoka katika ule mlipuko ilikuwa bahati lakini upande wa Hamza haikuwa swala la bahati.
“Naona ushaanza kuchukua cheo cha mke kwa namna unavyotoa ushauri”Aliongea Hamza akitabasamu kizembe na kumfanya Regina kugeuka na kuelekea juu chumbani kwake
Hamza mara baada ya kukaa sebuleni kwa dakika kadhaa hakuelekea tena ndani bali alitoka nje na kufunga mlango na kisha kuondoka
*******
UHALISIA NDANI YA NDOTO 04:30am
Licha ya mwanamke yule kuungua na ule moto wa maajabu na kufariki lakini kicheko chake na laana alizokuwa akiongea wakati wa kuungua zilikuwa bado zikisikika kama vile ni mwangwi unaojirudia rudia katika masikio ya watu.
Watu wale waliokuwa wakishangilia yule mwanamke mchawi kuchomwa moto walijikuta wakipatwa na woga kutokana na kitendo kile cha kuendelea kuzisikia zile sauti licha ya kwamba tayari amekwisha kuungua na kufariki.
Kusanyiko lile baada ya yule Askofu aliehusika kumuunguza yule mwanamke na moto wa nuru kuondoka walimfuata nyuma na kuingia katika kanisa kubwa na kuanza kusali kwa kutubu.
Licha ya kila mtu kutawanyika Hamza alijikuta akiwa amesimama katika eneo lilelile bila ya kupiga hatua , kilichokuwa kikimshangaza ni kwamba bado akili yake ni kama ilikuwa ikiyaona macho ya yule mwanamke yakimwangalia , haikuwa hivyo tu ule moto ambao ulimuunguza yule mwanamke bado alikuwa akihisi nguvu yake.
Alikuwa katika mshituko mkubwa mno kwa kile kilichotokea , kiasi cha kusahau kabisa nafsi yake na akili yake ipo katika mwili ambao sio wake
“Hii nguvu ni ya kimaajabu mno”Aliwaza Hamza.
Tofauti na kuogopa kama ilivyokuwa kwa watu wale ambao hakuwa akiwajua lakini yeye alikuwa ameshikwa na tamaa kubwa ya nguvu ile alioweza kuiona na kujiuliza anawezaje kujifunza uwezo ule.
Muda huo alijikuta akishikwa mkono kitendo kilichomshitua na kumwangalia aliemshika.
“Jamani Luther , Asante Mungu wa nuru , Asante Mungu wa nuru kwa kumuokoa na mateso kama ya baba yake , kijana mdogo kama huyu anastahili rehema za Mungu”
Hamza alijikuta akivutwa kutolewa katika eneo lile na yule mwanamke huku akiongea kila aina ya maneno ya shukrani kwa Mungu wa Nuru.
Alikuwa Mzungu , ukweli ni kwamba kila mtu aliekuwa akimuona kwake alikuwa ni Mzungu.
Hamza alijaribu kunyanyua mdomo ili kuongea lakini mdomo ulikuwa mzito mno na bado alikuwa katika mshangao wa kuitwa Luther, alitaka kuuliza yeye ni nani na kwanini ana mwili wa kizungu.
Hamza aliendelea kushangaa zaidi mara baada ya kuingizwa katika nyumba ndogo na mwanamke wa makamo wa kizungu ambae alikuwa akitaja kila aina ya shukrani kwenda kwa Mungu.
Kitendo cha kushangaa na kujishangaa kilimfanya yule mwanamke kumwangalia Hamza na kuendelea kutokwa na machozi.
“Luther ugonjwa wa akili umekutesa mno , hebu jiangalie ulivyokonda..”Aliongea yule mwanamke huku akimwangalia Hamza.
Hamza bado alikuwa na maswali , hakujua kilichokuwa kikiendelea ni nini lakini alijua kitu kimoja hakuwa ni Hamza bali alikuwa ni Luther, aliogopa pia kuongea kwa kuonekana labda watamjua yeye ni Hamza katika mwili wa Luther.
“Alisa usiongee sana na Luther, ndio kwanza amepona na lazima atakuwa na uchomvu , Ivani msaidie mama yako twende nyumbani”
Hamza aligeuza macho yake na kumwangalia mwanaume wa kizungu mwenye nywele nyeupe akiongea , alikuwa na kama miaka hamsini hivi kwenda sitini hivi , licha ya kuwa na ndevu nyingi lakini ilionyesha katika ujana wake alikuwa na mwonekano mzuri.
“Asante Shangazi , nipo sawa bado tu najihisi kizunguzungu”Hamza aliongea lakini aliongea nje ya hiari yake , ilikuwa ni kama kuna kitu ambacho kilikuwa kikimsukuma kuongea hivyo.
Yule kijana ambae alikuwa amemleta Hamza kuangalia mchawi akichomwa moto alikuwa amemshikilia mwanamke huyo wa kizungu aliefahamika kwa jina la Alisa.
“Luther nimefurahi sana kukuona hali yako inatengemaa yule mchawi amestahili , amekutesa sana”
“Wakati ule anahamia na kuwa jirani yako alionekana kama mwanamke mrembo sana mstaarabu mpaka nilipatwa hadi na wazo la kuhakikisha John anakuwa mke wake lakini alikuwa ni mchawi, tulimshuhudia mara kadhaa akifukua miili ya watu kutoka makaburini ili kufanyia majaribio ya kichawi , Asante sana Mungu kwa kumfanya akamatawe na ushahidi wakati akifukua mwili kaburini , nashindwa hata kufikiria kama angefanikiwa katika uchawi wake ni watu wangapi wangeathirika”
Hamza aliendelea kusikiliza yale maneno ya Alisa kwa umakini na sasa ni kama anapata mwanga , yule mwanamke alikuwa mchawi na alikamatwa na ushahidi akiroga kwa kufukua maiti makaburini ndio maana akachomwa moto.
Kutokana na mwanamke yule kuwa jirani yake na yeye pia alichukuliwa kama mshirika wa uchawi na yule mwanamke na kuanza kuhojiwa na ilionekana mahojiano hayakuwa ya kawada , kuna nguvu za ziada ambazo zilikuwa zikitumika na ndio kilichomfanya Luther kupoteza fahamu, ilimfanya Hamza kudhania pengine Luther alikuwa akishirikiana katika maswala ya ulozi na yule mwanamke ndio maana alikuwa akimwangalia sana.
Yule mwanamke Alisa alionekana kuongea mfululizo kana kwamba alikuwa akisimulia tukio zima la namna mwanamke yule alivyokamatwa na namna ambavyo pia Luther alihusishwa katika swala hilo mpaka kuachiliwa.
Yule mwanaume mwenye nywele nyeupe alimwangalia Hamza na muda uleule alionekana kutabasamu na kumshika bega.
“Yupo hivyo , unapaswa kumzoea”Aliongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa.
“Alisa alikuwa mwanamke mrembo sana wakati wa ujana wake lakini mara baada ya kumzaa John alibadilika sana na kuwa kama hivi , mpaka sasa naweza kusema amekuwa sio mshindani wangu tena likija swala la kuongea”Aliongea yule mzee kwa kingereza.
Upande wa Hamza bado hakuzingatia mazungumzo yao ni kama alikuwa akiwaza kutaka kujua alikuwa wapi na kwanini nafsi yake ipo katika mwili ambao sio wake.
“Joeli mwanaume aliekuwa na nguvu na hamasa ya juu ya kutimiza ndoto zake za kuwa msanii mkubwa sasa hivi amegeuka na kuwa mlevi”Aliongea Alisa
“Aalto ni jiji ndani ya nchi ya Zaburi , watu wasiohesabika wanafika kwa ajili ya kutimiza ndoto zao lakini je ni wangapi ambao wamefanikiwa , isitoshe Alisa nimeacha kuwa mlevi tokea siku John aliopata kazi”
“Asante Mungu , nadhani unajua namna tulivyoweka matumaini yetu kwa John na Ivan , John amekuwa mtoto mzuri kwetu ameweka juhudi kubwa na sasa ameweza kuchaguliwa na kujiunga na jeshi , kama ataweza kuamsha karama ya damu yake na kutambulika ataweza kupewa cheo cha Ubwana na wengi watamheshimu”Hamza alimsikia yule mwanake Alisa akiongea na upande wa yule mwanaume aliefahamika kwa jina la Joeli alitingisha mabega na yule mwanamke aliefahamika kwa jina la Alisa alionekana kujishtukia na kumwangalia Hamza.
“Luther nisamehe , sijamaanisha kwamba wewe huna uwezo , ulitakiwa kupitia mafunzo kidogo wakati ulipokuwa mdogo”Aliongea yule Alisa lakini ni kama radhi yake haikuwafanya kazi. “Luther hana shida na naamini ataweza kuibeba ndoto yangu na kuwa msanii mkubwa”Aliongea yule Joeli.
“Ndio nataka kuwa msanii mwanamuziki mkubwa”
Hamza alijikuta akisema bila ya kufikiria huku akicheka na kumfanya yule mwanamke kuvuta pumzi ya ahueni na kuanza kuongea tena kila neno ambalo lilimjia mdomoni na ilimfanya Hamza kuelewa mji huo na ulimwengu huo kitu alichojua ni kwamba yupo katika jiji lililofahamika kwa jina la Aalto ndani ya nchi ya Zaburi.
Hamza muda huo licha ya kujua nafsi yake ipo katika mwili ambao sio wa kwake lakini ukweli alijikuta ni kama alikuwa akiangalia TV kwa kupitia VR na kumfanya awe katika mazingira yale matukio yanapotokea.
Nafsi yake muda huo ilikuwa ikimwambia lazima afahamu yupo wapi , kama yupo kwenye ulimwengu mwingine lazima ajue yupo ulimwengu gani , kama ni kumbukumbu za maisha lazima azifahamu ni kumbukummbu gani ambazo zimemleta katika mazingira ya namna hio , mazingira ambayo ni ya kale kabisa lakini yenye kujaa maajabu na hata kama ni ndoto lazima ajue kwanini anaota ndoto ya namna hio.
Hamza alijikuta akishituka mara baada ya kutingishwa kwa nguvu na akiwa katika hali ya kuhema alijikuta akifumbua macho yake na pembeni yake alikuwa amesimama Regina.
“Amka wewe , nenda kaoge na kisha badilisha mavazi yako”Aliongea Regina aliekuwa amesimama akimwangalia Hamza namna alivyojiachia bila ya kujifunika shuka kutoka kiunoni na kufanya kifua chake kuwa wazi pamoja na mwili uliovimba kutokana na mazoezi , alijikuta akishindwa kujizuia na kuanza kuona aibu za kike.
Alijiambia ndio maana Hamza anaonekana kuwa na maamuzi ya haraka kutokana na kuwa na mwili wenye mazoezi.
Aliona mwili wa Hamza haukuwa wa kawaida kabisa na aliushangaa kana kwamba hakuwahi kuona mwili wa mwanaume.
Hamza upande wake ni kama hakupenda kutoka ndotoni , ukweli ni kwamba siku kadhaa nyuma alihofia ile ndoto lakini mara baada ya kuota zaidi ya mara nne ni kama alianza kupata shauku ya kuendelea kuota , kwake ni kama alikuwa akiangalia tamthilia akiwa ndotoni , kiichomfurahisha ni kwamba ndoto hio ni kama ilikuwa ikijua wapi aliishia kuota kwani ilianza palepale na kuendelea lakini sasa mara baada ya kuona kumekucha ilimshangaza, aligeuza macho upande wa eneo la swichi kuangalia labda ule mshumaa wa nuru umechomekwa kwenye umeme lakini hakukuwa na mshumaa na aliona kabisa ameota bila ya msaada wa kitu.
“Regina kwanini umeingia chumbani kwangu bila ya kugonga?”Aliuliza Hamza.
“Nimegonga mara kibao hufungui ndio maana nikaingia , fanya haraka nataka tukachukue cheti cha ndoa”Aliongea Regina na kumfanya Hamza kufunua shuka bila ya kujali alikuwa amevalia boksa tu.
Regina hakutegemea Hamza alikuwa na boksa tu na baada ya shuka lile kumtoka mwilini kilichoonekana ni eneo la mbele la Hamza kuwa na hamasa kubwa ya mapambano.
“Ah!!.. unafanya nini ?”Regina alijikuta akigeuka na kuangalia pembeni huku mapigo ya moyo wake yakienda kasi mno.
“Hii ni swala la kibaiolojia , kuna haya gani ya kushituka wakati ni ishara nzuri kuonyesha nina afya nzuri”Aliongea Hamza
“Huoni aibu?”
“Nione aibu ya nini ndani ya chumba changu , Regina unaonekana kuwa na mchecheto mno kwenda kuchukua cheti cha ndoa asubiuhi asubuhi, hukulala nini?”
“Sitaki bibi kuwa na wasiwasi kabla ya kuondoka , usifikirie mbali ni cheti tu ila maisha yetu yatabakia vilevile, nimekaa chini na kufikiria na nimegundua bibi anachotaka ni kuona cheti tu na hajasema hatuwezi kuachana hapo baadae , baada ya mkataba wako wa kazi kuisha tunaweza kuachana na kila mtu akaendelea na mambo yake”
“Kuna haja ya kwenda mbali hivyo , kuna haja ya kuichukia ndoa kiasi hicho?”
“Sijasema naichukia ndoa nachukia kufunga ndoa na mtu kama wewe”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi ya masikitiko huku akimwangalia mwanamke huyo akizipiga hatua kutoka chumbani kwake.
“Regina kwasababu umekuja kuniamsha chumbani kwangu , unaonaje na mimi nikiwa nakuja chumbani kwako kukuamsha , itakuwa ni kuamshana kwa zamu”
“Ole wako uingie chumbani kwangu”Aliongea Regina na kutoka nje.
Upande wa Hamza wakati akijiandaa kwenda kuoga simu ilimfanya aghairi kwa dakika kadhaa na kisha kuchukua kujua nani anampigia asubuhi asubuhi hio , baada ya kuangalia na kuona jina ni la Dina alijikuta akitoa tabasamu la uovu na moja kwa moja alikumbuka ukatili aliofanya usiku.
“Mrembo nini maana ya kupiga simu asubuhi yote hii”
“Unaniuliza nini , umefanya nini wakati nikiwa nimelala?”Sauti upande wa pili ilionekana kuwa na hasira mno.
Comments