Reader Settings

Regina mara baada ya kusikia kauli hio  mikono yake iliokuwa imeshikilia usukani wa gari  ilianza kutetemeka , isitoshe  alikuwa msichana  na  ni ngumu kwake kuhimili mshituko wa namna hio 

“Kwahio tunafanya nini , gari halipunguzi mwendo  na tunakaribia mataa  mbele yetu?”

Hamza alijikuta akiinua macho mbele na kugundua kweli  mbele yao wanazikaribia Traffic light  na magari ambayo yalikuwa yakitoka  Kariako kwenda Mbagala yalikuwa mengi mno na pili katika lane yao  kulikuwa na magari mbele yao ambayo pia yanapunguza mwendo , kama wakiendelea hivyo hivyo basi ni  hakika  watayagonga magari yaliokuwa   mbele yao.

“Achia usukani , nitaendesha mimi  rudi nyuma”

“Lakini  siwezi kutoka hapa kirahisi”Aliongea

Regina lakini Hamza  bila ya kuchelewa kwa

mkono mmoja alimnyanyua  kutoka katika siti ya udereva na kumrushia   katika viti vya nyuma ya gari , bahati nzuri gari yao iliikuwa SUV hivyo Regina hakujigonga na Hamza  alimshika Regina makalio na kumsukumizia  mpaka kwenye siti. “Aiyaaa… umenigusa wapi!!?”

Regina licha ya kujua yupo hatarini  alishindwa kujizuia kwa namna  Hamza alivyomsukumiza kwa kumshika kalio.

Hamza hakutaka kujali  zaidi  na  alishika sterling kwa mikono yake miwili  na kuweka umakini kwenye kuendesha.

Gari ilikuwa ikiserereka kwa spidi  kubwa mno na Hamza alijitahidi kadri ya uwezo  wake kuyakwepa magari na kwenda mbele zaidi kiasi ambacho  alifanya  madereva kuanza kupaniki, ilikuwa ni upepo tu  aliokuwa akiacha kila alivyopokuwa akipita gari.

Jambo zuri aliweza kulikunja gari vizuri na kuingia katika barabara ya dharula  na  bahati ilikuwa yake maana aliweza kupita mataa bila  ya kugongana na gari.

Kitendo cha kupita  tu Hamza aling’ata meno kwa hasira na kisha alikanyaqga pedeli na kuongeza mwendo zaidi.

“Wewe umekuwa kichaa , kwanini unakanyaga mafuta?”Aliuliza Regina kwa kupaniki asijue  Hamza anafanya nini

“Wale watu  kwenye pikipiki wameshikilia  rimoti na inafanya kazi  kwa umbali wa mita ishirini mpaka arobaini  hivi,  hivyo najaribu kuwaacha kwa zaidi ya huo umbali ili isifanye kazi  ndio maana  nimeongeza spidi zaidi” “Kumbe! , wewe umejuaje sasa?”

“Wewe unadhani kama sina uwezo kwanini  bibi yako analazimisha nikuoe?”Aliuliza Hamza na kumfanya  Regina kugeuka yai.

“Ongeza umakini  barabarani”

Kitendo cha kumaliza sentensi hio  alichoweza kusikia  ni sauti ya Ziii.. ziii..Ziii , gari ilikuwa imebadilika mngurumo wake na sasa ni kama   ni mnyama aliekuwa akinguruma huku  tairi  zikisuguana na barabara.

“Argghh..!!”

Regina katika maisha yake hakuwahi kuwa  katika hali kama hio , gari kwenda katika spidi ya hali ya juu  mno  na hakutaka kuangalia mbele zaidi ya kukizika kichwa chake 

Uwezo wa Hamza wa kuendesha ulikuwa ni wa viwango va juu, baada ya kuingia katika daraja la  Kigamboni  aliongeza spidi zaidi  kwa nguvu kabisa  na gari ilichomoka kama  mshale, mara baada ya kuangalia kwenye kioo alitoa tabasamu na palepale kwa  nguvu alikanyaga breki na zilikubali.

“Creeek!!!”

Mataili ya magari yaliishia kuacha  michirizi katika barabara  ilioambatana na moshi , ilikuwa ni kama vile ndege  inatua  na hatimae aliweza kwenda kupaki  gari pembeni mita kadhaa  na daraja hilo  katika  stairi ya mshazari.

Kitendo cha gari kukanyaga breki na  Hamza  alivyoisimamisha gari  katika mzunguko ilimfanya  Regina  kushikwa na kichefuchefu kikali , ijapokuwa mchakato wote ulifanyika kwa sekunde tu lakini  ulikuwa sio wa kawaida kwake.

Wale watu kwenye pikipiki waliona hali sio nzuri na mpango wao ni kama umefeli hivyo kwa haraka waligeuza pikipiki   wakidhamiria kukimbia.

Lakini Hamza hakuwa  na mpango wa kuwaacha kabisa na alifungua mlango  haraka na kutoka na kisha alianza kuikimbiza ile pikipiki  na kadri alivyokuwa akikimbia mwili wake ulianza kubadilika.

Dereva wa ile pilipiki haikueeweka alikumbwa na nini lakini alijikuta  akiyumba na  kuisababisha pikipiki ile kuteleza  na ikamshinda uzito na wote pamoja  na aliempakia  walidondoka chini  na kabla hata hawajanyanyuka Hamza alikuwa ashawafikia tayari.

Muda huo  hata Regina aliweza kutoka nje ya   gari na kumkimbilia Hamza na kwenda kujificha nyuma yake.

“Nani kawatuma?”Aliuliza Hamza akiwa siriasi lakini yule dereva kwa utalamu alipiga sarakasi na kusimama na muda huo huo alichomoa  Bunduki  zile za kuwachomea sindano wanyama(Trangulizer gun) na kutaka kumfyatulia Hamza lakini  Hamza alikuwa mwepesi mno kwani  aliruka na teke na  kumpiga kwenye mikono yake na kuifanya idondokee pembeni.

“Kama hamtaki  kuongea  nitawafanya muongee wenyewe”Aliongea.

Yule mwingine alionekana kuumia na alishindwa kusimama  na Hamza aliamua kudili na yule aliesimama na kwa  haraka alimsogelea na kumshika na kisha aliondoa  ile helmeti  na  sasa  aliweza kuona sura yake,alikuwa ni muafrika mwenye asili ya kisomali  na alikuwa amevalia  Heleni nyeusi.

Hamza  alishangazwa na kitendo kile na kwa haraka haraka alimsogelea  na yule mwingine aliekuwa akigulia maumivu na kutoa helmeti yake na  wote kwa pamoja walikuwa wamevalia heleni japo yule mwingine alikuwa ni Mwafrika asilia.

“Nyie ni maninja kutoka  kundi la Black Eared Snake!, inaonekana  kuna watu  kweli wamedhamiria kutuua”Aliongea Hamza   akimaanisha  watu hao ni kundi la  maninja  la Nyoka  mwenye masikio meusi.

Kitendo cha Hamza kuongea neno hilo  wale watu walijikuta wakishituka na kushangaa hawakuamini Hamza angeweza kuwatambua.

“Black Eared Snake ndio  nini?”Aliuliza Regina.

“Ni kundi  la  maninja   kutoka  nchi ya CAR , ni kundi daraja C , ijapokuwa uwezo  wa  maninja wao hauwezi kuhesabika wa juu  lakini  wana mbinu nyingi za kusababisha mauaji , ndio kundi  la kininja namba moja Afrika”Aliongea  Hamza akimwelezea Regina  kwa lugha nyepesi kwamba kundi hilo linatokea Afrika ya Kati.

Japo  Regina hakuelewa  maana ya kundi  daraja  C lakini alichojua muda huo hali ilikuwa ni ya hatari mno.

“Mmetumwa na familia ya Mzee Benjamini?”Aliuliza Regina.

“Usiulize maswali , ijapokuwa ni kundi daraja C lakini   wanaongozwa na sheria kali  za kininja , sheria  kubwa ya ninja yoyote ni kutomtaja mwajiri wake”

“Kwahio tunafanyaje, tunawaacha waende?”

Hamza alifikiria kidogo na aliona asingeweza kuwaua  wakati huo ambao  Regina alikuwa mbele yake , alikuwa  na uwezo wa kuwaua na kupoteza miili yao kimazingara lakini hakutaka  maswali kutoka kwa Regina.

“Pigia simu polisi watakuja kudili nao”Aliongea Hamza na Regina  alikubali  lakini kabla simu  haijapokelewa wale  manijja walionekana kutafuna vitu  huku wakiwa wamekaza sura.

Hamza hakutaka hata  kuwazuia  kwani aliona pia ni moja ya njia ya kutatua tatizo.

Dakika  mbili tu wale  manijja walitema damu nyeusi  na  kufariki  palepale mbele ya Regina.

“Mamaaaa..!!!”

Regina alijikuta akipiga ukulele  na pasipo ya kujua  upande wa pili  polisi alikuwa ashapokea simu yake.

“Hello , nini tatizo!!?”Hamza  mara baada ya  kuona  Regina ameshikwa na mshituko alichukua simu  na  kutoa maelekezo  kwa poilisi, upande wa pili wa polisi walionekana kushangaa maana ni kama hawakuwa wakiamini walichoambiwa , lakini hata hivyo walisema wanafika muda si mrefu.

Regina aijikuta akichuchumaa  pembeni ya  barabara huku akionekana ni kama ameshikwa na kichefu chefu.

Ilibidi  Hamza kumsogelea na kisha alimshika  bega kwa namna ya kumtuliza , mwanamke huyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuona mtu akijiua kwa staili hio  hivyo ilikuwa haki yake kushituka.

Dakika chache baadae Polisi waliweza kufika eneo la tukio  na kutokana na muda ulikuwa umeenda sana  Hamza alimchukua Regina na kuingia ndani ya gari  na kuanza safari ya  kuelekea nyumbani .

Lakini sasa  kitendo  cha dakika chache tu  za kuendesha sikio la tatu la Hamza liliweza kunasa sauti  ya kitu  kubip ndani ya  gari , kama   hakuwa mtu mzoefu asingeweza kugundua kitu  hicho.

Ilikuwa ni bomu , ilionekana ndani ya gari lao kulikuwa kumetegwa bomu kama mpango  B.

Hamza hakuwa hata na muda wa kumwambia  Regina nini kinachoendelea  na haraka sana  alijifyatua kutoka katika siti yake  na kuelekea upande wa  Regina alipo na kumbeba juu juu  akimtanguliza mbele yake , kitengo cha kufyatuka  kwenye  gari walisukumizwa na presha ya msukumo  wa bomu na kwenda kutua kwenye  majani upande wa pili wa barabara huku gari yao ikiteketea kwa moto mkubwa.

Kiikuwa kitendo cha  sekunde chache mno kufanyika  kuanzia  kufunguliwa mkanda mpaka kutolewa nje ya gari na mlipuko  kutokea  na kuja kutua chini akiwa hajaumia.

Mlipuko ule uliyafanya masikio ya Regina kupatwa na ukiziwi wa ghafla  na kengele za masikio   kugonga , ilimchukua dakika  kadhaa mpaka akili yake kurudi katika  uhalisia.

Regina hakuamini  alikuwa ameokoka katika  mlipuko huo wa gari , Hamza angechelewa kidogo tu wangekuwa  tayari ni  maiti.

“Hamza… Hamza..!!”

Regina alijikuta akiita kwa nguvu   mara baada ya kuzidi kulemewa na uzito wa mwili wa Hamza uliomlalia kwa juu , lakini licha ya kuita hakukuwa na majibu na alijikuta akimeza mate mengi  na kujitoa katika mwili wake kwa kumsukuma pembeni..

Mara baada ya kuona mgongo wa Hamza machozi yalianza kumtoka bila ya kujua ,  aliweza kujua Hamza alitumia mwili wake kumkinga  na   presha ya mlipuko.

Regina alikuwa ameshikwa naBumbuwazi na maswali  mengi yalipita katika kichwa chake na kujiuliza inamaana yeye ni wa muhimu  mno kwa Hamza mpaka kujitoa kwa namna hio kumlinda.

Alijikuta akipotezea  mawazo yale na kwa haraka sana alimtingisha Hamza kuamka.

“Hamza amka ,  nakuomba usife , fungua macho  yako..”Regina alijikuta akipaliwa mpaka na mate  na alijikuta akianza kutafuta simu  yake  ili kupiga simu lakini simu  hakuwa nayo na alijikuta ni kama  kuchanganyikiwa kumemvaa.

Dakika hio hio watu  ni kama walisikia  mlipuko huo na walianza kusogelea eneo hilo kwa kasi na  Regina alianza kupiga kelele kuomba msaada.

“Regina..!!”

Alijikuta mwili wake ukimtetemeka mara baada ya kushikiliwa mkono wakati akitaka kuamka kwenda kuomba msaada lakini Hamza alionekana kuamka. “Nipo  hapa , unaendelea , hali yako ikoje?”

“Mbaya sama  nadhani siwezi kuishi tena”Aliongea  kinyonge.

“Uisongee hivyo huwezi kufa , ngoja niombe msaada  tukupeleke hospitalini”Aliongea huku akisimama.

“Haina haja , mpaka nikifika hospitalini nitakuwa nishakufa”

“Acha kuongea kuniogopesha,  huwezi kufa”

“Namuona Israeli mtoa roho mbele yangu , Regina nisamehe siwezi kukuoa kama bibi yako alivyosema”Aliongea  Hamza  

“Hapana usife , umesema mwenyewe unataka unioe, huwezi kufa leo, kesho tunatakkiwa kwenda kusajili ndoa yetu , naomba usife jamani”

Regina  hakujua hata maneno yanatokea wapi lakini  aliona ndio mbinu ya kumbembeleza Hamza asipoteze uha.

“Upo tayari  tuandikishe ndoa yetu?”

“Ndio nipo tayari .. please Hamza naomba usiniache..”Aliongea na  alijikuta akianza kulia kwa kwikwi.

“Kwakuwa umekubali mwenyewe  ,  basi nimeghairi kufa mpaka siku nyingine”Aliongea Hamza huku akimwangalia  Regina na tabasamu  la uchokozi.

Regina mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akimwangalia Hamza  na kumkuta hakuwa na dalili yoyote ya kuonyesha yupo kwenye maumivu.

Hamza  alikaa kitako huku akipangusa mikono yake na kumwangalia Regina huku akimcheka.

“Kwahio Regina kesho ndio siku yetu ya kuuaga  ubachela sio?”

Regina  alijikuta akiwa haamini  alikuwa akichezewa akili na Hamza muda wote  , kadri alivyokuwa  akimwangalia ile huzuni aliokuwa nayo ilianza kubadilika na kuwa na hasira kali, alijikuta akiona kipande cha zege pembeni na  bila ya  kujiuliza mara mbilimbili alikichukua na  kumlenga nacho Hamza kichwani.

“Holly shit!!!”

Hamza alijikuta akifyatuka kama mshale akikwepa  kipande kile ambacho kilienda kutua mtaroni. “Hamza nitakuua …!!!”Aliongea huku akirusha ngumi  za kike kwa hasira lakini Hamza aliishia kuidaka mikono yake na  kumkumbatia kwa nyuma.

Shida halikuwa kumbatio tatizo ni mikono ya Hamza iliposhikilia katika eneo la kifua la mrembo huyo.

Hamza aliweza kuhisi kitu  kilaini  katika mikono yake  na hakuweza kujizuia na kuuliza.

“Regina kumbe  upo vizuri kiasi hichi”

“Wewe mpuuzi niachie”

Regina uso wake ulikuwa umeshika moto  alitamani  kujirusha kwenye mtaro.

“Sawa ila sijafanya makusudi”Aliongea Hamza huku akimuachia. 

“Halafu  kingine kwanzia kesho unakwenda kuwa mke wangu hivyo  haijalishi wapi nina gusa” “Kafie mbali huko , siwezi kuwa mke wako”

“Umeahidi  mwenyewe zaidi ya mara mbili kama nikiendelea kuishi  tutaenda kujiandikisha , kama bosi wa kampuni kubwa   sidhani ni vizuri  kwenda kinyume na ahadi yako unatoa mfano mbaya kwa wafanyakazi  wako”

“Umenitega kwa kunidanganya , niliongea vile nikajua unakufa kweli”

“Kama upo tayari  kuoana na mimi wakati nakaribia kufa  si vizuri zaidi nikiwa hai maana utafurahia zaidi matunda ya ndoa , hata hivyo tuachane na hayo kwanza hata nikikuelezea huwezi kuelewa nini maana ya Matunda ya ndoa”

“Wewe..!!”

Regina alijikuta akipiga miguu chini kwa hasira na kuanza kupiga hatua kurudi barabarani.

Ukweli ni kwamba  alishasahau kabisa  kama

walipata ajali ya gari lao kulipuka , ilionekana makusudi ya Hamza  kumchezea akili  yamemshushia  presha   kabisa ya swala zima la ajali.

“Mke  unaenda wapi tena?”

“Naenda nyumbani”Aliongea Regina  alijua hawezi kumfanya chochote Hamza hivyo hakuona haja ya kuendelea kujibishana nae , kuhusu  maswala ya gari yao kulipuka aliona awaachie polisi wafanye kazi yao.

Dakika  kadhaa  tu wote waliweza kufika nyumbani  na Regina mara  baada ya kuingia ndani na kukumbuka  Shangazi hayupo aliona  ni kama kuna hali ambayo sio ya kawaida na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza lakini alishangaa kumuona   amekaa kwenye  ngazi akionekana kufikiria.

“Wewe unafikiria nini?”

“Nawaza namna ya kudili na hawa watu ambao wanatusababishia ajali kila siku , sidhani kama nisiposhughulika nao mapema wanaweza kuacha”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kumshangaa , dakika kadhaa zilizopita  mwanaume huyo alionekana  kuwa  kama kichaa lakini sasa hivi amegeuka na kuwa siriasi.

“Kama  unatengeneza hela nyingi jua kuna ambao hawana uwezo wa kutengeneza hizo hela , hivyo ni kawaida kuwa na  maadui, nimejiandaa kwa  vitu kama hivi ndio maana sipati shida  hata vikitokea”

“Wewe unapaswa kuzingatia kufanya biashara na mimi nitazingatia namna ya kukulinda”

“Kwahio unapanga kufanya nini?”

“Regina hivi unadhani   wale wajinga  wametumwa na familia ya Mzee Benjamini  au kuna maadui wengine ambao hatuwajui, sidhani ni swala la kawaida  kukodi maninja hatari kama wale nje  ya nchi kwa ajili yetu”

“Siwezi kujua ila familia ya James ndio maadui zangu wakubwa”

“Mpaka wameenda mbali kukodi  majina kutoka  Afrika ya kati!!?”

“Siwezi kujua  kama kuna adui mwingine au  lah”Aliongea  Regina na kumfanya Hamza kutingisha kichwa.

“Usikurupuke  kutaka kulipa kisasi , haijalishi una nguvu kiasi gani  ni ngumu kushinda watu wengi”

Regina  aliona swala la kuweza kuokoka katika ule mlipuko ilikuwa bahati  lakini upande wa Hamza haikuwa swala la bahati.

“Naona ushaanza  kuchukua cheo cha  mke  kwa namna unavyotoa ushauri”Aliongea Hamza akitabasamu kizembe na kumfanya Regina kugeuka  na  kuelekea juu chumbani kwake 

Hamza mara baada ya kukaa sebuleni kwa dakika kadhaa   hakuelekea tena ndani bali alitoka  nje na kufunga mlango na kisha kuondoka

*******

UHALISIA NDANI YA NDOTO 04:30am

Licha ya mwanamke yule kuungua na ule moto wa maajabu  na kufariki lakini  kicheko chake na  laana  alizokuwa akiongea wakati wa kuungua zilikuwa bado zikisikika  kama vile ni mwangwi unaojirudia rudia  katika masikio ya watu.

Watu wale  waliokuwa  wakishangilia yule  mwanamke mchawi kuchomwa moto walijikuta wakipatwa na woga kutokana  na kitendo kile cha kuendelea kuzisikia zile sauti licha ya kwamba  tayari amekwisha kuungua na  kufariki.

Kusanyiko lile baada ya yule  Askofu aliehusika  kumuunguza yule  mwanamke na moto wa nuru kuondoka  walimfuata nyuma na kuingia katika kanisa  kubwa  na kuanza kusali kwa kutubu.

Licha ya kila mtu kutawanyika  Hamza alijikuta akiwa amesimama katika eneo lilelile  bila ya  kupiga hatua , kilichokuwa kikimshangaza ni kwamba  bado akili yake ni kama ilikuwa ikiyaona macho ya yule mwanamke yakimwangalia , haikuwa hivyo tu ule moto ambao ulimuunguza  yule mwanamke bado alikuwa akihisi nguvu yake.

Alikuwa katika mshituko mkubwa mno  kwa kile kilichotokea ,  kiasi cha kusahau kabisa  nafsi  yake na akili yake ipo katika mwili ambao  sio wake

“Hii nguvu ni ya  kimaajabu mno”Aliwaza Hamza.

Tofauti na kuogopa  kama ilivyokuwa kwa watu wale  ambao hakuwa akiwajua lakini yeye alikuwa ameshikwa na tamaa kubwa ya nguvu ile alioweza kuiona  na kujiuliza anawezaje kujifunza uwezo  ule.

Muda huo  alijikuta akishikwa mkono  kitendo kilichomshitua na kumwangalia aliemshika.

“Jamani Luther , Asante Mungu wa nuru , Asante Mungu wa nuru  kwa kumuokoa  na mateso  kama ya baba yake ,  kijana mdogo kama huyu anastahili  rehema za Mungu”

Hamza  alijikuta akivutwa kutolewa  katika eneo lile na yule mwanamke huku akiongea kila aina ya maneno ya shukrani kwa Mungu wa Nuru.

Alikuwa Mzungu ,  ukweli  ni kwamba kila mtu aliekuwa akimuona kwake alikuwa ni Mzungu.

Hamza alijaribu kunyanyua mdomo ili kuongea lakini mdomo ulikuwa mzito mno   na bado alikuwa katika mshangao wa kuitwa  Luther, alitaka kuuliza  yeye ni nani na kwanini  ana mwili wa kizungu.

Hamza aliendelea kushangaa zaidi mara baada ya kuingizwa  katika  nyumba ndogo na mwanamke wa makamo wa kizungu ambae alikuwa akitaja kila aina ya shukrani kwenda kwa Mungu.

Kitendo cha kushangaa na kujishangaa kilimfanya yule mwanamke kumwangalia Hamza na kuendelea kutokwa na machozi.

“Luther ugonjwa wa akili  umekutesa mno , hebu jiangalie  ulivyokonda..”Aliongea  yule mwanamke  huku akimwangalia  Hamza.

Hamza bado alikuwa na maswali , hakujua kilichokuwa kikiendelea ni nini lakini alijua kitu kimoja  hakuwa ni Hamza bali alikuwa ni Luther, aliogopa pia kuongea kwa kuonekana  labda watamjua yeye ni  Hamza katika mwili wa Luther.

“Alisa  usiongee sana na  Luther, ndio kwanza amepona  na lazima atakuwa na uchomvu , Ivani  msaidie mama yako  twende nyumbani”

Hamza aligeuza macho yake na kumwangalia mwanaume wa kizungu mwenye nywele nyeupe akiongea , alikuwa na kama miaka hamsini hivi  kwenda sitini hivi , licha ya kuwa na ndevu nyingi  lakini ilionyesha katika ujana wake alikuwa na mwonekano mzuri.

“Asante Shangazi , nipo sawa  bado tu najihisi kizunguzungu”Hamza aliongea lakini  aliongea nje ya  hiari yake , ilikuwa ni kama kuna kitu ambacho kilikuwa  kikimsukuma kuongea hivyo.

Yule kijana ambae alikuwa amemleta Hamza kuangalia  mchawi akichomwa moto alikuwa amemshikilia mwanamke   huyo wa kizungu aliefahamika kwa jina la Alisa.

“Luther nimefurahi sana kukuona hali yako inatengemaa  yule mchawi amestahili , amekutesa sana”

“Wakati ule anahamia  na kuwa jirani yako alionekana kama mwanamke mrembo sana   mstaarabu  mpaka nilipatwa hadi na wazo la kuhakikisha  John anakuwa mke wake  lakini  alikuwa ni mchawi, tulimshuhudia mara kadhaa akifukua miili ya watu kutoka makaburini  ili kufanyia majaribio ya kichawi , Asante sana Mungu  kwa kumfanya  akamatawe na ushahidi  wakati akifukua  mwili kaburini , nashindwa hata kufikiria kama angefanikiwa katika uchawi wake ni watu wangapi wangeathirika”

Hamza aliendelea kusikiliza yale maneno ya Alisa kwa umakini  na  sasa ni kama anapata mwanga , yule mwanamke alikuwa mchawi  na alikamatwa  na ushahidi akiroga kwa kufukua maiti makaburini ndio maana akachomwa moto.

Kutokana na mwanamke yule kuwa jirani yake na  yeye  pia alichukuliwa  kama mshirika wa uchawi na yule mwanamke  na kuanza kuhojiwa  na ilionekana  mahojiano hayakuwa ya kawada , kuna nguvu  za ziada ambazo zilikuwa zikitumika  na ndio kilichomfanya  Luther kupoteza fahamu, ilimfanya  Hamza kudhania pengine  Luther alikuwa akishirikiana katika maswala ya ulozi na yule mwanamke ndio maana alikuwa akimwangalia  sana.

Yule mwanamke Alisa alionekana kuongea mfululizo  kana kwamba alikuwa akisimulia tukio zima la namna mwanamke yule alivyokamatwa na  namna ambavyo pia  Luther alihusishwa katika  swala hilo  mpaka kuachiliwa.

Yule mwanaume  mwenye  nywele nyeupe alimwangalia Hamza  na muda  uleule alionekana kutabasamu na kumshika bega.

“Yupo hivyo , unapaswa kumzoea”Aliongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa.

“Alisa alikuwa mwanamke mrembo sana wakati wa ujana wake  lakini mara baada ya kumzaa John alibadilika sana na kuwa kama hivi , mpaka sasa naweza kusema  amekuwa sio mshindani wangu tena likija swala la kuongea”Aliongea yule mzee  kwa kingereza.

Upande wa Hamza  bado hakuzingatia mazungumzo yao ni kama  alikuwa akiwaza  kutaka kujua alikuwa wapi  na kwanini nafsi yake  ipo katika mwili ambao sio wake.

“Joeli mwanaume aliekuwa na nguvu  na hamasa ya juu ya kutimiza ndoto zake za  kuwa msanii mkubwa   sasa hivi amegeuka na kuwa  mlevi”Aliongea Alisa  

“Aalto  ni  jiji ndani ya nchi ya Zaburi , watu wasiohesabika  wanafika  kwa ajili ya kutimiza ndoto zao  lakini je ni wangapi ambao wamefanikiwa , isitoshe Alisa nimeacha kuwa mlevi  tokea siku  John aliopata kazi”

“Asante  Mungu , nadhani unajua namna tulivyoweka matumaini yetu kwa John na Ivan ,  John amekuwa mtoto mzuri  kwetu  ameweka juhudi kubwa  na sasa ameweza kuchaguliwa na kujiunga   na jeshi , kama ataweza kuamsha  karama  ya damu yake  na kutambulika ataweza kupewa cheo cha Ubwana na wengi watamheshimu”Hamza alimsikia yule mwanake  Alisa akiongea  na upande wa yule mwanaume aliefahamika kwa jina la Joeli alitingisha mabega na  yule  mwanamke aliefahamika kwa jina la Alisa alionekana kujishtukia na kumwangalia Hamza.

“Luther nisamehe , sijamaanisha kwamba wewe huna uwezo , ulitakiwa kupitia mafunzo kidogo wakati ulipokuwa mdogo”Aliongea yule  Alisa lakini ni kama  radhi yake haikuwafanya kazi.  “Luther hana shida  na naamini ataweza kuibeba ndoto yangu na kuwa msanii mkubwa”Aliongea yule Joeli.

“Ndio nataka kuwa msanii  mwanamuziki mkubwa”

Hamza alijikuta  akisema bila ya kufikiria  huku akicheka na kumfanya yule mwanamke kuvuta pumzi ya ahueni na kuanza kuongea  tena kila neno ambalo lilimjia mdomoni  na ilimfanya Hamza kuelewa  mji huo na ulimwengu huo kitu alichojua ni kwamba yupo katika  jiji lililofahamika kwa jina la Aalto  ndani ya nchi ya Zaburi.

Hamza muda huo  licha ya  kujua nafsi yake ipo katika mwili ambao  sio wa kwake  lakini ukweli alijikuta ni kama alikuwa akiangalia  TV  kwa kupitia VR  na kumfanya  awe katika  mazingira yale matukio yanapotokea.

Nafsi yake muda huo ilikuwa ikimwambia  lazima afahamu yupo wapi , kama yupo kwenye ulimwengu mwingine lazima ajue  yupo ulimwengu gani , kama ni kumbukumbu  za maisha lazima azifahamu  ni kumbukummbu gani ambazo zimemleta katika mazingira ya namna hio , mazingira ambayo ni ya kale kabisa lakini yenye  kujaa  maajabu na hata kama ni ndoto  lazima ajue kwanini anaota ndoto ya namna hio.

Hamza alijikuta akishituka mara baada ya kutingishwa kwa nguvu  na akiwa  katika hali ya kuhema alijikuta akifumbua macho yake na pembeni yake alikuwa amesimama Regina.

“Amka  wewe , nenda kaoge  na kisha  badilisha mavazi yako”Aliongea Regina aliekuwa amesimama akimwangalia  Hamza namna alivyojiachia bila ya  kujifunika shuka  kutoka kiunoni  na kufanya  kifua  chake kuwa wazi  pamoja  na mwili uliovimba kutokana na mazoezi , alijikuta akishindwa kujizuia na kuanza kuona aibu za kike.

Alijiambia ndio maana  Hamza anaonekana kuwa na maamuzi ya haraka  kutokana na kuwa na mwili  wenye mazoezi.

Aliona mwili wa Hamza haukuwa wa kawaida  kabisa na aliushangaa kana kwamba hakuwahi kuona mwili wa mwanaume.

Hamza upande wake ni kama  hakupenda kutoka ndotoni , ukweli ni kwamba  siku kadhaa nyuma alihofia ile ndoto lakini  mara baada ya kuota zaidi ya mara nne ni kama alianza kupata shauku  ya kuendelea kuota , kwake ni kama  alikuwa akiangalia tamthilia  akiwa ndotoni , kiichomfurahisha ni kwamba ndoto  hio ni kama ilikuwa ikijua wapi  aliishia kuota kwani ilianza palepale na kuendelea lakini sasa mara baada ya kuona  kumekucha ilimshangaza, aligeuza macho  upande wa  eneo la swichi kuangalia labda ule mshumaa wa nuru umechomekwa kwenye umeme lakini hakukuwa na mshumaa na  aliona kabisa ameota bila ya msaada wa kitu.

“Regina kwanini umeingia chumbani  kwangu bila ya kugonga?”Aliuliza Hamza.

“Nimegonga  mara kibao  hufungui ndio maana nikaingia , fanya haraka nataka tukachukue cheti cha ndoa”Aliongea Regina na  kumfanya Hamza   kufunua shuka bila ya kujali alikuwa amevalia boksa tu.

Regina  hakutegemea Hamza alikuwa na boksa tu na  baada ya shuka lile kumtoka mwilini  kilichoonekana ni eneo la mbele la Hamza kuwa na hamasa  kubwa ya mapambano.

“Ah!!.. unafanya nini ?”Regina alijikuta akigeuka na kuangalia pembeni  huku mapigo ya moyo wake yakienda kasi mno.

“Hii ni swala la kibaiolojia , kuna haya gani ya kushituka  wakati ni ishara  nzuri  kuonyesha  nina afya nzuri”Aliongea Hamza  

“Huoni aibu?”

“Nione aibu ya nini ndani ya chumba changu , Regina  unaonekana kuwa na mchecheto mno kwenda kuchukua cheti cha ndoa  asubiuhi asubuhi, hukulala nini?”

“Sitaki  bibi  kuwa na wasiwasi kabla ya kuondoka , usifikirie mbali ni cheti tu  ila  maisha yetu yatabakia vilevile, nimekaa chini na kufikiria na nimegundua bibi anachotaka ni  kuona cheti tu  na hajasema  hatuwezi  kuachana hapo baadae ,  baada  ya  mkataba wako wa kazi kuisha  tunaweza kuachana na kila mtu akaendelea na  mambo yake”

“Kuna haja ya kwenda mbali hivyo , kuna haja ya kuichukia ndoa kiasi hicho?”

“Sijasema naichukia ndoa  nachukia kufunga ndoa na mtu kama wewe”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi ya masikitiko huku akimwangalia mwanamke huyo akizipiga hatua kutoka chumbani kwake.

“Regina kwasababu umekuja kuniamsha chumbani kwangu , unaonaje na mimi nikiwa nakuja chumbani kwako kukuamsha , itakuwa  ni kuamshana kwa zamu”

“Ole wako uingie chumbani kwangu”Aliongea Regina na kutoka nje.

Upande wa Hamza wakati akijiandaa kwenda kuoga  simu ilimfanya aghairi kwa dakika kadhaa na kisha kuchukua kujua nani anampigia asubuhi asubuhi hio ,  baada ya kuangalia   na kuona jina  ni la Dina alijikuta  akitoa tabasamu la uovu  na moja kwa moja alikumbuka  ukatili aliofanya usiku.

“Mrembo   nini maana ya kupiga simu asubuhi yote hii”

“Unaniuliza nini , umefanya nini wakati nikiwa nimelala?”Sauti upande wa pili ilionekana kuwa na hasira mno.

Previoua Next