Reader Settings

“Kwa.. kwanini?”

Regina alitaka kujua sababu ya Hamza kumuua mtu , alitaka angalau kujua  sababu pengine anaweza kujishauri, tokea siku ambayo  aliweza kuona Hamza akiifahamu lugha ya kifaransa vizuri ,  siku ambayo alijua Hamza anafahamina na mshonaji nguo mkubwa alijua fika pengine  kuwa mwanachuo , fundi   na mwalimu ni namna ya kuficha ubini wake , lakini licha ya hivyo  ilikuwa ngumu kwake kumvumilia kama kweli amemuua mtu bila sababu  licha ya kwamba hakujua uhusika wake.

“Nimewaua kwasababu walistahili kufa”Aliongea Hamza 

“Kwahio unajiona Mungu?”Aliuliza  kwa hasira  Norbert.

“Wame… inamaana sio mmoja?”Aliuliza Regina kwa mshangao.

“Huna haja ya kuniangalia hivyo , nilichofanya  ni kama mwanajeshi kumuua adui , siwezi kuhesabika  muuaji  kwasababu nimemmaliza  adui na kurudisha ushindi nyumbani , siwezi kuua bila sababu  lakini ikitokea  nipo hatarinni na  watu wangu wa karibu kuwa hatarini ni sababu tosha”

“Unamaanisha nini?”

“Namaanisha  mbele ya adui yangu  ninachukua uhusika wa  mwanajeshi  na kazi ya mwanajeshi ni kuangamiza adui , hivyo sio  tu jana wala kesho  adui ambae ni  hatari kwa usalama  wangu  anastahili kifo”

“Unazunguka zunguka sana na maneno mengi , au ndio sababu inayokufanya unaficha ficha mambo yako mengi”Aliuliza Regina.

“Kuna zaidi ya sababu kwa kila ninachofanya”Aliongea  “Wewe ni  muongo..”Regina alitaka kuongea zaidi  kihasira lakini alishindwa, aliishia kuondoka mbele ya Hamza na kuingia ndani ya hospitali.

Muda uleule  mara baada ya Hamza  kuondoka   wale mapolisi  walimzingira , ni kama   hali yao ya kujiamini imerudi mara baada ya bosi Regina kuondoka.

“Mr Hamza  kwanza kabisa nijitambulishe vizuri ,naitwa Kapteni Norbert Geza  kutoka kitendo cha usalama wa nchi , lakini  vilevile nafahamika kama Jino la Fisi, matendo yako  yameweka usalama wa nchi katika sintofahamu  na  kwa kosa hilo  rasmi sasa tutakukamata”Aliongea Afande Norbert huku akijiambia potelea pote wamesema  waachane nae  ni wao  ila yeye anamkamata  akamhoji.

“Kwahio kweli unataka kunikamata?”

‘Unataka kukataa , hii ni Tanzania , hivi unajua  nini kitakupata ukitaka kushindana na sisi”Aliongea Afande  Gamale.

“Natamani kuona kipi kitanipata”Aliongea Hamza. “Afande Gamale  acha kujibishana na  huyo  mhalifu  mfunge pingu”Aliongea Afande Kyombo.

Gamale hakutaka kuchelewesha na alimsogelea Hamza  akitaka kumvisha pingu  lakini  wakati akitaka  kufanya vile ni kama macho yake yaliingiwa na ukungu na ashindwe kumuona  Hamza  mbele yake wakati akili yake inakuja kukaa sawa alishangaa  yeye ndio amefungwa pingu na alijikuta akibung’aa.

“F*ck you “

Kyombo  kitendo cha   Gamale kuvishwa pingu na Hamza aliona ni tusi kwa jeshi la polisi  na kwa hasira alifyatuka na teke  akidhamiria kumpiga Hamza , lakini kabla ya   kumkaribia  Hamza alibadilishana nafasi na Gamale kwa  kumvutia  aliposimama  na kutokana na  Kyombo kutumia nguvu  nyingi alishindwa kuzuia shambulizi lake mara baada ya kuona linaenda  kumpata Gamale. “Puuh!!

Gamale alijikuta akichwapwa teke na   mwenzake na kwenda chini huku akigulia maumivu. “Kyombo umekuwa kichaa , mbona unanipiga mimi”

“Unauliza ujinga ,kwani  nimekupiga makusudi?”Aliongea  Kyombo  huku akiwa na hasira nyingi.

“Nitalipiza , huwezi kunipiga teke kubwa hivi, umefanya makusudi”Aliongea Gamale kwa hasira huku akijaribu kusimama lakini kutokana na  pingu alijikuta akirudi ardhini.

“Afande Kizito mfungue Gamale  hizo pingu”Aliongea  Norbert mara baada ya kuona timu yake inapaluana wakiwa wamesahau adui yao ni Hamza. “Sawa kapteni”

Niobert alikuwa akiongoza vichaa wenzake , ni kama wote walikuwa wakifanana tabia , mara baada ya Gamale kuondolewa zile pingu walimzingira  Hamza na kuanza kumshambulia 

Lakini mbele ya  Hamza  aliona ni kama ngumi za wanawake wanaojaribu kuwa na hasira mbele ya mwanaume wanaempenda  hivyo alizikwepa  kama anacheza Amapiano.

“Wewe mpuuzi  hebu acha kutukimbia , ni mwanaume kweli wewe?”.

“Kama unadhani mimi sio  mwanaume kamuulize  mpenzi wangu”Aliongea Hamza.

“Niachieni huyu mimi namwendea na pigo za kijetilii , tuone kama atakwepa kwepa kama anacheza rede”Aliongea Kyombo  na kuanza kurusha miguu  , japo alionekana kuwa na stamina na mafunzo kiasi lakini kwa Hamza ilikuwa kichekesho maana alimuacha amsogele na kisha  aliudaka mguu wake  na kuusukuma na kumfanya adondokee makalio yake kwa nguvu.

Baada ya kuona Kyombo  ameshindwa waliobaki wote walimsogelea Hamza na kuishika mikono yake wakitaka kuikutanisha kwa ajili ya kuifunga pingu  lakini licha ya wote wawili kutumia nguvu kubwa  walishindwa kuikutanisha kadri walivyokuwa wakiisukuma., walihihisi ni kama wanasukuma  chuma kizito.

Upande wa Kapteni Norbert alikuwa pembeni akiangalia vijana wake wanachokifanya.

Baada ya kuona  wameshindwa kuuipindishahata kidogo mikono ya Hamza alijikuta akishangaa.

“Hamza kama sikosei hio ndio mbinuu maarufu inayofahamika  kama Joho la Chuma”Aliongea Norbert 

“Kama unaijua basi utakuwa unajua pia  namna ya kuishinda , acha kutegea wenzako fanya na wewe shambulizi”Aliongea Hamza.

“Nilikuwa najiandaa”Aliongea Norbert  na muda ule alianza kuizungusha mikono yake hewani kana kwamba anajaribu kukusanya nguvu ya kiroho.

Upande wa Hamza alikuwa ameshikiliwa  na polisi wawili , kama vile walikuwa wakitaka  bosi wao ampige  Hamza shambulizi  la kifuani.

Norbet mara baada ya kujikusanya kwa  sekunde kadhaa alifyatuka kwa spidi kiasi kwamba alisababisha  hadi upepo kama vile  ni gari  ambayo ilikuwa kwenye spidi kubwa na kumsogelea Hamza kwa kasi , lilikuwa ni teke la  tiktaka  ambalo lilienda kutua katika kifua cha Hamza.

“Bam!!

Sauti iliosikika ni kama  vile mtu anafungua mlango kwa teke  na mlango ukagoma kufunguka

Polisi wale walijikuta wakipatwa na wasiwasi  kutokana na ukubwa wa teke lile na  kuona   limemsababishia Hamza matatizo.

Lakini  mara baada ya kumwangalia Hamza walishangaa akiwa amesimama na hakuwa na mabadiliko yoyote hata kidogo.

“Unaonekana umejifunza funza, Precelestial Kick  sio mbaya ,  ila umetumia hisia  nyingi sana kwenye hili teke”Aliongea Hamza  

Afande Norbert  alijikuta akibung’aa mara baada ya kukaa sawa na kumuona Hamza  yupo vilevile kama jiwe , sio kwake tu hata kwa wenzake pia.

“Vipi kuna mwingine  ana shambulizi ambalo anataka kunionyesha?”Aliuliza Hamza akiwaangalia  kwa zamu.

Wale polisi waliokuwa wamemshikilia Hamza walijikuta wakianza kushikwa na woga na walimuachia  na kurudi nyuma.

“Hamna uwezo hata wa kunipiga halafu mnataka kunikamata , sidhani hata mna vigezo vya kuongea na mimi , poteeni wakati  nikiwa  na roho ya kistaarabu”Aliongea Hamza huku  akianza  kutoa msisimko ulioanza kumtisha  Norbert kiasi kwamba mapigo yake ya moyo  yalikuwa yakienda   mbio mno.

“Hii ni  Tanzania nchi ya amani  huwezi…”Alitaka aendelee kujibishana lakini Hamza alimsogelea na kumpiga kofi  la kifuani na kumfanya  adondoke chini  kama  mzigo .

“Kapteni!!”

Wale polisi walijikuta wakimkimbilia mwenzao  wakidhani amekufa maana sio kwa uzito wa bao lile.

Walijikuta wakipatwa na ahueni  kapteni wao alikuwa hai licha ya kutema damu , lakini upande wa  Norbert aliona  kama   Hamza angetumia   nguvu kidogo kwenye mkono wake  basi   kifo kingemkuta palepale.

Wale polisi mara baada   ya kuona  Kapteni wao hali yake si nzuri  walimbeba na kumrudisha kwenye gari na safari ya hospitalini ilianza mara moja. *****

Hamza mara baada ya kuingia ndani aliweza kumuona Regina  akiwa ameshika kile cheti cha  ndoa mbele ya bibi yake , alikuwa na furaha , ule muonekano wake wa nje ulikuwa umepotea  na ilimfanya Hamza kuvuta pumzi ya ahueni.

Bibi Mirium mara baada ya kumuona  Hamza alitoa tabasamu hafifu  huku akimpa  Hamza ishara ya kumsogelea.

“Safi sana .. wewe ni mtoto mzuri”Aliongea Bibi Mirium.

“Bibi kuna kitu unataka tena?, niambie nitakamilisha”Aliongea Hamza. “Haraka iwezekanavyo  mfanye Regina apate mtoto

, ndio  njia ya kuifanya nyumba yako kuchangamka”

“Bibiii!!!” Regina  aliongea , aligeuka mwekundu kwa aibu kiasi kwamba hakutamani kuendelea kubakia ndani ya wodi.

“Nimekuelewa bibi nitalifanyia kazi”Aliongea Hamza akitingisha kichwa kukubaliana nae 

Bibi Marium  alitoa tabasamu hafifu na kisha alifunika macho  yake kana kwamba amekwisha kushoshwa na dunia na yupo tayari kuondoka.

“Regina unaonaje tukitoka nje kidogo , kuna vitu nataka kukuambia”Aliongea Hamza na Regina alisita kidogo  lakini aliishia kugeuka  na kutangulia nje.

Mara baada ya kufika mwishonni mwa korido haikuwa na mtu yoyote hivyo ilikuwa sehemu nzuri kwao kuongea.

“Vipi kuhusu wale polisi?”

“Wameondoka”

“Kwanini hawajakuchukua?”

“Mbona kama unataka  nikamatwe ?”

“Ndio, umeua  na  unapaswa kuadhibiwa kisheria”

“Regina mrembo , mambo hayapo ‘simple’ namna hio, haiwezekani kufupisha maisha yangu yaliopita na neno  kuua”

“Basi elezea vizuri nikujue wewe ni nani  na  ndio nifanye maauzi kama naweza kukuamini”Aliongea Regina na kumfanya Hamza kukosa neno , aliona  si vyema  kumwambia chochote Regina , sio kwasababu anataka kumficha ila ni kwasababu akishamjua  atakuwa hatarini.

“Ninachoweza kukuambia  ni kwamba , unaweza kunijua ila sio sasa?”

“Mhh,  kama hutaki kusema , vipi hiki nisichokijua kuhusu wewe, je kinahusiana na maswala ya kihalifu  , kama kuua na  kuteka nyara?, Aiu polisi walikuwa sahihi  wewe ndio muuaji  ulietangazwa kwenye vyombo vya habari?”

“Regina!!”

Hamza sauti yake ilianza kuwa siriasi  kidogo.

“Unaweza kusema ndio nimemuua mtu  lakini mimi sio mhalifu  wala huyo muuaji muhuni muhuni . sijawahi kujihusisha  hata na makundi ya kigaidi sio hivyo tu  sijawahi kufanya  kitu ambacho kinaifunga dhamiri yangu”

“Kwanini  nikuamini  kama huwezi kusema chochote?”

“Siwezi kukuambia kwasababu siri ninayoficha hapa , kama nikisema nikuambie utakuwa hatarini  , nafanya haya kukulinda”

“Haina haja, hatujafahamiana muda mrefu hivyo    huna haja ya kunilinda kwa staili hiii”

“Sekunde ambayo ulitia saini hiko cheti   umebeba cheo cha mke wangu ,  unaweza  usikubali lakini ni jambo siriasi  kwa watu wengine”

“Unamaanisha hili karatasi , hivi unadhani kuna mwanamke duniani anaweza kukubali kuolewa na mtu asiemjua?”

Hamza alitamani kusema  ndio ,isitoshe katika uzoefu wake ameshuhudia  ndoa ningi zikifanyiika kwa ajili ya manufaa mbalimbali , wengine walifanya hivyo kupata uraia , wengine mali  na kadhalika lakini hata hivyo aliona  haitokuwa  na maana mbele ya Regina.

“Hatutaachana  mpaka niweze kuishikilia kampuni kwa asilimia kubwa , hivyo naomba  usiambie watu chochote kuhusu ndoa yetu,  una uhuru  asilimia  mia moja  ya kutafuta mwanamke unaempenda  na hata kuanza taratibu za ndoa , ikifikia  muda  wa ndoa  nipo tayari kwenda kubatilisha hiki cheti”Aliongea Regina huku akitingisha cheti kilichokuwa kwenye mikono yake. “Regina unamaanisha nini kuongea hivyo?”

“Kipi ambacho huelewi , sina mpango wa kuwa mke wako  kabisa ,haiwezi kutokea kihisia nikakubali kuwa mkeo , kitu kingine unaweza kutangulia nyumbani au kazini  , nitakaa kidogo na bibi  usinisubiri”

Mara baada ya kuongea hivyo aligeuka  kikauzu na kisha aliingia ndani  akimwacha Hamza akimwangalia kwa nyuma.

“Ningeililia ndoa kama kweli naitaka , lakini nipo  kazini  Regina”Aliwaza Hamza huku  akitingisha kichwa , katika maisha yake pengine Regina ndio mwanamke wa kwanza kumuongelesha kwa tabia hio.

********

Upande mwingine katika moja ya hospitali ya jeshi alionekana  Afande Norbert akiwa amelala kitandani  huku uso wake ukiwa  umepauka.

Timu yake ilikuwepo ndani ya chumba alicholazwa  na walimwangalia  kwa hali ya  huzuni.

“Kapteni  inamaana ndio tunakwenda kuachana na hii misheni?”

“Mnapaswa kuelewa  sisi  ni wanajeshi kabla ya kuwa polisi  na  yote ni kwa ajili ya kuikamilisha hii misheni , acheni kuwa  kama walinzi , kuna watu wanamfatilia Hamza kwa ukaribu”Aliongea Kapteni.

“Norbert  haina haja ya kuendelea kumfatilia  Hamza tena”Sauti iliweza kusikika kutoka  mlangoni  na wote walijikuta wakikakamaa kwa mshangao wakimwangalia mwanaume aievalia gwanda   za jeshi la ulinzi akiingia,alikuwa na vyeo vilivyochafuka  begani mwake.

Hakuwa peke yake alikuwa ameongozana na wanajeshi wengine  wawili .

“Kapteni Mdudu!!,”Aliongea  Norbert kwa mshangao  ni kama hakutegemea  kumuona Mdudu ndani ya hilo eneo.

Afande Mdudu alikuwa ni  Kapteni wa kikosi namba mbili  kutoka  kitengo cha  uchunguzi cha

MALIBU.

Moja ya sababu kubwa  ambayo ilimfanya Mdudu kuheshimika jeshini  mpaka kupewa nafasi ya kukaa pamoja na wakubwa ni kutokana na kwamba ndio mwanajeshi  ambae amepanda vyeo  akiwa na elimu kidogo, kwa lugha nyepesi ndio mwanajeshi aliepanda vyeo bila ya kutegemea  elimu zaidi ya  mafanikio yake ya kijeshi.

Alionyesha uhodari wa  namna yake  kipindi  alipokuwa katika mpango wa Umoja wa  Taifa wa kulinda Amani nchini Sudani na  Congo.

Mara nyingi MALIBU  wanafanya uchunguzi wao kupitia  jeshi la polisi , Norbert alikuwa ni mwanajeshi wa kitengo cha MALIBU  ambae  anaongoza timu namba moja  aliepandikizwa ndani ya  jeshi la polisi , hivyo alikuwa akipokea  maagizo kutoka  kwa mkuu wa polisi  na  pia vilevile alikuwa akipokea maagizo kutoka kwa  mkuu wa kitengo cha MALIBU.

‘”Tumepewa  maagizo  ya kuja hapa , kwanzia sasa kikosi namba mbili ndio kitaongoza  misheni ya kumchunguza Hamza, operesheni  mlizofanya  nyie kama kikosi cha kwanza hazijawaridhisha viongozi , mnaweza kuendeea na taratibu za kawaida kama polisi”

“Nini!, mbona niliwasiliana na mkuu mwenyewe  na hajaniambia kuhusu hili”

“Kwahio Norbert nini ambacho huamini , angalia

hio  karatasi kuna sahihi ya mkuu  wa kitengo”Aliongea akimrushia karatasi kwenye kitanda na kweli kulikuwa na sahihi.

“Kwanini  mnataka tuiachie hii kesi kwenu , bado hatujakamilisha kumkamata Hamza  lakini vilevile hatujafanya kosa lolote”

“Norbert licha ya kwamba wakuu wanasifia uwezo wako lakini kwangu nakuona kama mjinga , kwanini hukujiuliza  licha ya Afande mwenye  cheo kikubwa  kama Afande Yowe kuuwawa lakini bado viongozi wakakuambia uachane  na Hamza , lakini angalia  ulichokifanya ukajaribu kumkamata na sasa upo hapa hospitalini , viongozi hawakuridhishwa na  namna  yako ya kukosa utiifu  na wamesikitishwa sana na hili ndio maana  tumepewa jukumu la  kumchunguza Hamza na kumjua kwa undani”

“Nimefanya vile kama polisi , sikuona haja ya

kumwangalia mhalifu anafanya  anavyotaka”Aliongea Norbert  na kumfanya Mdudu kutoa tabasamu la dharau.

“Tulichokifanya ni kujaribu uwezo wake  kwa kumtishia kumkamata , timu namba mbili mnataka kuchukua  crediti zetu  wakati misheni inaendelea vizuri”Aliongea Kyombo.

“Norbert wewe ndio uongee , unadhani tunakuibia sifa zako?”Aliuliza Mdudu.

“Kyombo kaa kimya”  Aliongea Kapteni  Norbert na kumfanya Kyombo kunywea.

“Norbet una timu ina  watu vilaza kweli…”Aliongea  mwanajeshi aliekuwa nyuma ya Afande Mdudu lakini  alizuiwa asiendelee maana angeibua ugomvi.

“Norbert  uliwaambiwa viongozi kwamba hisia zako   zinakuaminisha Hamza ndio muuaji  anaeua wanawake ndani ya jiji la Dar es salaam , lakini kwanini umeshindwa kujiuliza swali jepesi , kwanini   Bounty  hunters kutoka Samar wamesafiri kutoka 

Ufilipino  mpaka Tanzania  kwa ajili ya kumtafuta Hamza , nadhani unawajua vizuri hawa wawindaji hawatumiki sehemu ambayo haina hazina”Aliongea Mdudu.

“Ni hazina gani ambayo Hamza

anashikilia?”Aliuliza Norbert  huku  kidogo akiona ni kweli kuna mahali amekosea.

“Huna  haja ya kuuliza maswali , tokea mwanzo ulikuwa ukitafuta kitu sehemu ambayo sio sahihi  , lakini usijali mimi na  timu yangu mapema tu tutaweza kujua ni kitu gani  wale wawindaji wamekijia Tanzania na  ndio namna tutakavyomjua Hamza kwa undani zaidi na hakuna atakaepata majeraha kama yako”

Mara baada ya Mdudu kuongea hivyo aliwapa ishara wenzake na kisha waliondoka .

******

Saa mbili kamili za usiku Hamza alikuwa  ndani ya  eneo la kijichi akilisogelea lango la kuingia  katika mgahawa wa Dina.

Mara baada ya kuingia aliweza kuona Mercedenz  s Class ikiwa imeegeshwa  na  Lau  alionekana kuilinda  gari ile.

Hamza alikuwa hapo kwa ajili ya kutii wito wa mrembo Dina mara baada ya kumpa  agizo  la kufika hapo bila ya kukosa.

“Bro  umewahi mno , ungenipigia simu nije kukuchukua  kabisa”Aliongea Lau kwa bashasha. “Mbona hii gari ipo hapa,Dina anapanga kutoka?”Aliuliza Hamza.

“Ndio , anaelekea Club”

“Club!!”

“Ndio  kila mwisho wa  mwezi  vigogo  na watu wazito wazito hukusanyika katika  club  moja , ni kama tukio maalumu  , sio lazima kwenda lakini kutokana na kwamba wengi ya  wanaohudhuria ndio  wateja wetu wakubwa  haina jinsi kwenda”Aliongea Lau.

Muda huo  wakati wakiongea  Dina aliweza kutoka  akiwa amevalia amependeza.

“Nilijua utachelewa”

“Siku kwenye  mudi nzuri ndio maana nimekuja, nimeambiwa unaenda Club, nitakusubiri mpaka utakaporudi”

“Nilikuambia  uje leo  kwasababu nataka unisindikize”Aliongea Dina.

“Lakini hujaniambia  ni club  ya aina gani” “Nitakuambia tukwia tunaeekea huko , ingia kwanza kwenye gari, umesema huna mudi  club ndio sehemu inayokufaa”Aliongea  huku akitangulia  kuingia  ndani.

Hamza aliishia kutingisha kichwa  na paepale aliona sio mbaya kutokana na mudi yake kuwa  mbaya  ni  kheri  kidogo akapunguze mawazo huko Club.

Previoua Next